MAKAMU WA RAIS AZUNGUMZA NA WATENDAJI WAKE WA MAZINGIRA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akizungumza wakati wa kuhitimisha kikao cha kazi kilichodumu kwa
siku mbili ambao alipokea na kujadili masuala mbali mbali yanayohusu
mazingira, kulia ni Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais
anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba.
Waziri
Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais
anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akichangia
jambo wakati wa kikao kazi cha Idara ya Mazingira kilichoongozwa na
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Watendaji wa Idara ya Mazingira
na Wakuu wa Vitengo, waliokaa pamoja na Makamu wa Rais kushoto ni
Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais
anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba na kulia ni
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Ndugu Mbaraka Abdulwakil.
.............................. .............
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka
watendaji wa Idara ya Mazingira katika ofisi yake wajipange vizuri kwa ajili ya
kufanya tathmini ya athari za kimazingira mjini Dodoma wakati serikali
ikijiandaa kuhamia kwenye mji huo.
Makamu
wa Rais ametoa kauli hiyo 21-Aug-16
alipokuwa akifunga mkutano wa kazi wa siku mbili na watendaji wa Idara ya
Mazingira ambapo walijadili namna ya kukabiliana na uharibifu wa mazingira
unaoendelea kote nchini.
Ameeleza
kuwa hatua hiyo itasaidia kuuweka mji wa Dodoma salama kimazingira ikiwemo
ubora wa miundombinu za maji taka.
Makamu
wa Rais amesema kutokana na idadi kubwa ya watu hasa watumishi ambao watahamia
Dodoma bila miundombinu imara hali ya uchafuzi wa mazingira itakuwa si nzuri
hivyo ni muhimu kwa watendaji hao kuweka mipango na mikakati madhubuti ya
kuhakikisha mji wa Dodoma hautaathirika kimazingira.
Kuhusu
utendaji kazi wa watumishi wa ofisi yake amewataka watumishi wote kufanya kazi
kwa ushirikiano na kwa uwazi katika matumizi ya fedha za miradi na hasa inayohusika na uhifadhi wa mazingira jambo
ambalo litaondoa manung'uniko miongoni mwa watumishi na wananchi kwa ujumla.
Amesema
ushirikiano huo miongoni mwa watumishi utasaidia kwa kiasi kikubwa ufanisi
katika kazi za kila siku ili kufikia malengo waliyojiwekea.
Makamu
wa Rais amesema ataendelea na utaratibu wa kukutana na watumishi kila baada ya
miezi 4 katika ngazi ya viongozi kama hatua ya kujitathmini katika mipango
ya kazi waliyojiwekea.
SERENGETI BOYS YAITANDIKA AFRIKA KUSINI MAGOLI 3-1 UWANJA WA AZAM CHAMAZI, NA KUIFURUSHA KWENYE MICHUANO
Mchezaji Asad Ali Juma wa timu ya
Taifa ya vijana Serengeti Boys akikokota mpira mbele ya wachezaji wa
timu ya Vijana ya Afrika Kusini katika mchezo wa kufuzu katika fainali
za Mataifa ya Afrika zitakayofanyika nchini Madagascar uliofanyika
kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi wilaya ya Temeke jijini Dar es
salaam.
Katika kipindi cha pili mchezaji
Ibrahim Abdallah ameifungia goli la pili timu ya Serengeti Boys ,
Wakati kipindi cha kwanza mchezaji wa Serengeti Boys Rashid Abdalla
alifunga goli la kwanza.
Kwa matokeo hayo Serengeti Boys
inasonga mbele katika michuano hiyo ya vijana baada ya kuitoa timu ya
Afrika Kusini kwa magoli 3-1 kufuatia sare ya magoli 1-1 nchini Afrika
Kusini, Ambapo inatarajiwa kukutana na timu kati ya Namibia au Congo
Brazaville.
Mchezaji Ibrahim Abdallah kushoto
akisahangilia na wenzake mara baada ya kuifungia goli la pili timu ya
Serengeti Boys kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi
Waziri wa Habari , Utamaduni ,
Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akizungumza kwa furaha mara baada ya
timu ya Serengeti Boys kuifunga timu ya Afrika Kusini kwenye uwanja wa
Azam Chamazi magoli 3-1
Vikosi vya timu hizo vikiingia uwanjani kabla ya kuanza kwa mchezo huo.
Kikosi cha timu ya vijana ya Afrika Kusini
Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania Serengeti Boys kikiwa katika picha ya pamoja.
Viongozi wa shirikisho la mpira wa
miguu Tanzania wakiwa katika jukwaa kuu kulia ni Celestin Mwesigwa
nakushoto ni Rais wa Shirikisho la Mpira Tanzania Jamal Malinzi pamoja
na viongozi wengine.
Benchi la Ufundi la Serengeti Boys.
Benchi la Ufundi la timu ya taifa ya Afrika Kusini.
Majaliwa awasili Mpanda
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akiwapungia wananchi wa Mkoa wa Katavi baada ya kuwasili kwenye uwanja
wa ndege wa Mpanda kuanza ziara ya kikazi mkoani humo Agosti 20, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akiongozwa na Vijana wa CCM baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa
Mpanda kuanza ziara ya kazi mkoani Katavi Agosti 20, 2016. (Picha na
Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisalimiana na baadhi ya wananchi wa mkoa wa Katavi baada ya kuwasili
kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda kuanza ziara ya kazi mkoani humo
Agosti 20, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisalimiana na baadhi ya wananchi wa mkoa wa Katavi baada ya kuwasili
kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda kuanza ziara ya kazi mkoani humo
Agosti 20, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
GHALA LA KAMPUNI YA BOSS SHOPPING CENTRE LTD LIKITEKETEA KWA MOTO JIJINI DAR ES SALAAM
Askari wa Kikosi cha Uokoaji cha Zimamoto wakizima moto uliokuwa ukiteketeza ghala la Kampuni ya Boss Shopping Centre Ltd zilimo kuwa zikihifadhiwa bidhaa mbalimbali eneo la Viwanda Chang'ombe jijini Dar es Salaam leo mchana.
wananchi wakijadiliana jambo eneo la tukio.
Kazi ya uokoaji ikiendelea.
Askari wa uokoaji wakiwa kazini.
Mmoja wa wamiliki wa ghala hilo akisaini fomu ya uzimaji wa moto huo.
Moto ukiendelea kuwaka
Wananchi wakiwa eneo la tukio.
Na Dotto Mwaibale
MOTO mkubwa umeteketeza ghala la Kampuni ya Boss Shopping Centre Ltd lililokuwa likitumika kuhifadhia bidhaa mbalimbali maeneo ya viwandani Chang'ombe jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio mmoja wa wamiliki wa ghala hilo ambaye hakupenda kutaja jina lake kwa kuwa hakuwa msemaji alisema moto huo ulianza saa 9 mchana.
"Tumepata hasara kubwa katika ghala hili tulikuwa tukihifadhi friji, TV, sabufa kwa ujumla ni Boss Bland Home" alisema.
Alisema chanzo cha moto huo bado hakijafahamika.
Baadhi ya waokoaji walikuwepo eneo la tukio walilalamikia Kikosi cha Uokoaji cha Zimamoto kwa kufika eneo la tukio bila ya kuwa na maji ya kutosha hivyo kushindwa kuhudhibiti moto huo kwa wakati ambapo ilizuka taharuki na kwa wamiliki wa viwanda vilivyokuwa jirani na ghala hilo.
Jitihada za gazeti hili kumpata Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro ili kuzungumzia tukio hilo hazikuzaa matunda baada ya kumpigia simu ambayo ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa.
TANAPA KUTUMIA TUKIO LA KUPATWA KWA JUA KUTANGAZA HIFADHI ZAKE.
Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog.
SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limesema litatumia fursa ya tukio la kupatwa kwa jua kama njia mojawapo ya kutangaza hifadhi za taifa hususani zinazopatikana katika mikoa ya nyanda za juu kusini na Magharibi mwa Tanzania.
Tukio la kupatwa kwa jua linataraji kuonekana vizuri ukilinganisha na maeneo mengine Duniani katika eneo la Rujewa wilayani Mbarali mkoani hapa,eneo ambalo liko jirani na Hifadhi za taifa za Ruaha,Kitulo na Katavi.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la
Hifadhi za Taifa (Tanapa) Pascal Shelutete
alisema maandalizi kwa ajili ya kupokea wageni wanao tarajia kufika
nchini kwa ajili ya tukio hilo ambalo limekuwa likitokea kwa nadra.
“ Wataaam na wanasayansi wa
kitaifa na kimataifa wathibitisha kuwa eneo pekee ambalo tukio hilo
litaonekana vizuri kuliko maeneo yote duniani ni Tanzania katika mikoa ya
nyanda za juu kusini,eneo ambalo lina vivutio utalii vinavyopatikana katika
hifadhi zetu za Katavi.Kitulo na Ruaha”alisema Shelutete .
“Shirika limejipanga kuhakikisha kuwa wageni wanoukuja kwa ajili ya tukio hilo pia wanapata fursa ya kuingia katika moja ya hifadhi zetu,niwaomba wadau wa sekta ya utalii nchini kutumia nafasi hii adhimu kukutana na wageni wanaokuja ili kuuza bidhaa zao za utalii”aliongeza Shelutete.
Naye mkuu wa hifadhi ya taifa ya
Ruaha Christopher Timbuka alisema kituo kikubwa ambacho kimethibitishwa
kutumika kwa ajili ya watu kujionea vizuri tukio hilo ni katika eneo la rujewa
wilaya ya mbarali ambako maandalizi yote muhimu yamefanyika.
Kwa upande wake mhifadhi wa idara
ya utalii Tutindaga Mdoe alisema baada ya tarifa za tukio hilo
kuthibitishwa idadi ya wageni imeanza kuongezeka na kwamba wameandaa mahema na
eneo la vyakula na vinywaji kwa wageni watakaofika kushuhudia tukio hilo katika
eneo la Bonde la Ihefu lililopo katika hifadhi ya taifa ya Ruaha.
Utafiti mdogo uliofanywa na gazeti
hili katika eneo hilo maarufu kwa kilimo cha mpunga umebaini asilimia kubwa ya
nyumba za kulala wageni tayari zimejaa kwa tarehe ya tukio hilo.
JK AONGOZA MAMIA MAZISHI YA BI SHAKILA MBAGALA CHARAMBE JIJINI DAR.
s
Mstaafu awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete akiweka udongo kwenye kaburi la
Bi Shakila Said,wakati wa maziko huko nyumbani kwake Mbagala
Charambe,jijini Dar .
Waziri
wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye akiweka udongo
kwenye kaburi la Bi Shakila Said,wakati wa maziko huko nyumbani kwake
Mbagala Charambe,jijini Dar.
Makamu
wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akiweka saini kitabu cha maombolezo
cha Bi Shakila Mbagala Charambe,jijini Dar,kushoto ni Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye.
Mke
wa Rais Mstaafu awamu ya nne,Mama Salma Kikwete akiweka saini kitabu
cha maombolezo cha Bi Shakila Said ,huko nyumbani kwake Mbagala
Charambe,jijini Dar.
Rais
Mstaafu awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete (wa pili kulia) na Waziri wa
Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye (pili kushoto)
wakishiriki maziko ya aliyekuwa Mkongwe,mwimbaji mahiri wa muziki wa
Taarabu hapa nchini,Bi Shakila Saidi ambaye mazishi yake yamefanyika leo
huko nyumbani kwake Mbagala Charambe,jijini Dar.
Makamu
wa Rais Mh,Samia Suluhu akijadiliana jambo na mmoja wa waombolezaji
nyumbani kwa marehemu,kabla ya maziko kufanyika.Bi Shakila,amefariki
ghafla nyumbani kwake,huko Mbagala Charambe.
Waziri
wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye akiwa na baadhi ya
waombolezaji wengine wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya na
wanamuziki wakongwe wakiwa kwenye mazishi ya Bi Shakila,hukko nyumbani
kwake Mbagala Charambe,jijini Dar.
Baadhi ya Waombolezaji wakiwa nyumbani kwenye mazishi ya Bi Shakila,aliyefariki ghafla nyumbani kwake,huko Mbagala Charambe.
Baadhi ya Waombolezaji wakiwa nyumbani kwenye mazishi ya Bi Shakila,aliyefariki ghafla nyumbani kwake,huko Mbagala Charambe.
Mwili wa marehemu Bi Shakila ukiswaliwa tayari kwa maziko
Waombelezaji
wakiwa wamebeba Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Bi Shakila
wakielekea mazikoni,jioni ya leo huko nyumbani kwake Mbagala
Charambe,jijini Dar.
Mwili ya Bi Shakila tayari umeishapumzishwa kwenye nyumba yake ya Milele
Safari ya mwisho ya Bi Shakila Said .
Rais
Mstaafu awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete (wa tatu kulia) akijalidiliana
jambo na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh.Nape Nnauye
(pili kushoto).
Baadhi
ya wanamuziki wakongwe na bongofleva wakiwa katika picha ya pamoja mara
baada ya kushiriki mazishi ya Bi Shakila huko nyumbani kwake Mbagala
Charambe jijini Dar
Rais Mstaafu awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete akizungumza na waombolezaji.
Katibu MKuu wa Shirikisho la Wanamuziki nchini,John Kitime akiweka saini kitabu cha maombolezo cha Bi Shakila Said ,huko nyumbani kwa marehemu Mbagala Charambe,jijini Dar.
Subscribe to:
Posts (Atom)