ROYAL TOUR YAPAISHA MAPATO YA TANAPA

March 21, 2024

 

Kamishina  wa  Uhifadhi wa Shirika la Taifa la Uhifadhi (TANAPA) Mussa Kuji akizungumza   Mafanikio ya TANAPA katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Mheshimwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kikao kazi na Wahariri wa vyombo vya Habari kilichofanyika chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa TEF Deodatus Balile akizungumza kuhusiana na umhimu wa waandishi kutumika kalamu katika kutangaza hifadhi zetu weledi.
Afisa Habari Mwandamizi wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Sabatho Kosuri, akizungumza kuhusiana na vikao kazi kati ya Taasisi zilizochini ya Msajili wa Hazina ,jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki katika mkutano wa TANAPA  na wahariri na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.

*Kamishina Kuji na timu yake aweka mikakati ya kung'arisha TANAPA

Na Chalila Kibuda,Michuzi Tv
SHIRIKA la Taifa la Uhifadhi (TANAPA) limesema kuwa limepata mafanikio hifadhi za Taifa kutembelewa kwa idadi kubwa ya watalii hadi kufikia2024 idadi ya watalii 1,514,726 kutokana na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuendelea kuliwezesha Shirika kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa

Hayo ameyasema Kamishina Mkuu wa Uhifadhi Mussa Kuji wakati akizungumza na wahariri na waandishi wa habari kuhusiana na mafanikio ya Shirika hilo kwa kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina jijini Dar es Salaam.

Kamishina Kuji amesema kuwa mafaniko hayo yameongeza mapato na hii inatokana na Filam ya Royal Tour aliyoifanya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuingia mwenyewe hifadhin hali inayoonesha kuwa kuna uongozi mahiri kuimarisha na kukuza sekta ya uhifadhi na utalii nchini katika kipindi chake cha uongozi wa nchi kwa miaka hii mitatu.

Amesema katika kipindi cha kuanzia Julai 2023 – Machi 19, 2024 idadi ya watalii 1,514,726 (wa ndani wakiwa 721,543 na wa nje wakiwa 793,183) wametembelea Hifadhi za Taifa sawa na ongezeko la asilimia 5

“Mafanikio haya yanayoendelea kufanywa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa ushiriki wake wa moja kwa moja kwenye kukuza sekta ya uhifadhi wa wanyamapori na utalii ikiwemo ushiriki wake kwenye filamu maarufu ijulikanayo kama “Tanzania: The Royal Tour”. Filamu hii imeleta chachu kubwa katika ukuaji wa utalii hapa nchini nchini pamoja na kuendelea kuelekeza fedha katika sekta ya uhifadhi na utalii”amesema Kuji .

Amesema Shirika linasimamia Hifadhi za Taifa 21 zenye eneo la ukubwa wa kilomita za mraba 96,908.88 ambalo ni sawa na 10.2% ya eneo lote la nchi.

Aidha amesema kuongezeka kwa idadi ya watalii katika Hifadhi za Taifa kumekuwa na ongezeko la watalii wanaotembelea Hifadhi za Taifa katika mwaka 2018/2019 jumla ya Watalii waliotembelea Hifadhi za Taifa walikuwa watalii 1,452,345 ikihusisha watalii wa ndani (719,172) na nje (733,173).

Hata hivyo amesema idadi ya watalii ilipungua hadi kufikia 485,827 mwaka 2020 ambayo ilitokana na UVIKO-19.

Mwaka 2021/2022 idadi ya watalii ilianza kupanda na kufikia watalii 997,87 nq 2 Hali ya kuimarika kwa utalii nchini iliendelea kupanda ambapo mwaka 2022/2023 idadi ya watalii waliongezeka na kufikia 1,670,437.

Aidha, kwa mwaka huu wa fedha 2023/2024 katika kipindi cha kuanzia Julai 2023 – Machi 19, 2024 idadi ya watalii 1,514,726 (wa ndani wakiwa 721,543 na wa nje wakiwa 793,183) wametembelea Hifadhi za Taifa sawa na ongezeko la asilimia 5 ikiwa ni zaidi ya lengo la kupokea watalii 1,387,987 (wa nje 827,713 na watalii wa ndani 726,676) katika kipindi husika.

Aidha, idadi ya watalii wanaotarajiwa kutembelea Hifadhi za Taifa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ni 1,830,081 (watalii wa nje 963,413 na watalii wa ndani 866,667).

Amesema katika kipindi cha miaka mitatu kumekuwepo na ongezeko la siku za kukaa wageni kutoka wastani wa siku 1,749,194 katika mwaka wa fedha 2021/2022 hadi kufikia wastani wa siku 2,669,586 kufikia Februari 2024 ambalo ongezeko hilo limechangia mapato.

Amesema Katika kipindi cha miaka mitatu, kumekuwepo na ongezeko la mapato ya zaidi ya shilingi bilioni 174 (2021/2022) hadi kufikia zaidi ya shilingi bilioni 337 kwa mwaka 2022/2023 sawa na ongezeko la shilingi zaidi ya bilioni 162 ambayo ni asilimia 94.

Aidha, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 (Julai 2023 hadi Machi 19, 2024) Shirika limekusanya zaidi shilingi Bilioni 340 ukilinganisha na matarajio ya kukusanya zaidi shilingi bilioni 295 mpaka Machi 2024. Kiasi hiki (Bilion 340) ni ongezeko la zaidi ya shilingi ya bilioni 44 ambayo ni sawa na asilimia 15 huku Shirika lina matarajio ya kukusanya kiasi cha zaidi shilingi bilioni 382 hadi Juni 2024.

Mapato haya ya sasa yanazidi mapato ya zaidi ya shilingi bilioni 282 yaliyokusanywa mwaka 2018/2019 kabla ya janga la UVIKO – 19 ambayo yalikuwa ndio kiwango cha juu cha mapato katika Shirika.

Kamishina Kuji amesema kuwa kumekuwepo na kuchipuka kwa masoko mapya ya utalii yenye idadi kubwa ya watalii ambapo inatoa uhakika wa kuendelea kupokea watalii wengi kuja kutembelea Hifadhi za Taifa.

Amesema TANAPA imefanikiwa kupata tuzo ijulikanayo kama “Best Practice Award” ambayo hutolewa kila mwaka na taasisi ya “European Society for Quality Research - ESQR”. Tuzo hii ya utoaji wa huduma bora kimataifa hutolewa na taasisi hiyo baada ya kutambua taasisi za Serikali na zisizo za Kiserikali pamoja na watu binafsi wanaotoa huduma za ubora wa viwango vya hali ya juu kimataifa.

TANAPA imeendelea kupata tuzo zinazotolewa na taasisi ya ESQR kwa kipindi cha miaka minne (4) mfululizo ambazo kati ya hizo tuzo za miaka mitatu (3) mfululizo zimepatikana katika kipindi cha uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kiwango cha “Platinum category” mwaka 2021, “Gold category” mwaka 2022 na “Diamond category” mwaka 2023.

Kamishina huyo amesema Hifadhi ya Taifa Serengeti imepata tuzo itolewayo na shirika la “World Travel Awards (WTA)” ya kuwa hifadhi bora barani Afrika kwa miaka mitano mfululizo (2019 hadi 2023). Tuzo tatu (3) kati ya hizo tano (5) zimepatikana chini ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita (tuzo za mwaka 2021 hadi 2023).

Hifadhi ya Taifa Tarangire na Kilimanjaro zilipata tuzo mara mbili mfululizo kwa mwaka 2021 na 2022 ya kuwa vituo vyenye mvuto katika utalii na Tuzo hizo hutolewa na jukwaa la kimataifa lijulikanalo kwa jina la “Trip Advisor”.

Pia, kampuni ya Explore Worldwide yenye makao yake makuu nchini Uingereza mwaka huu 2024 imeutambua Mlima Kilimanjaro kuwa namba moja ya Alama za Asili za kudumu na zinazokumbukwa zaidi ulimwenguni (World’s topmost unforgettable natural landmarks).

Amesema Tuzo hizo zimeliongezea Shirika kuaminiwa na wateja mbalimbali na kutoa uhakika kwao kuhusu aina ya huduma zitolewazo, kutambulika zaidi na kuongeza idadi ya watalii pamoja na kutoa uhakika kwa watalii na wadau wa utalii kuhusu ubora wa hifadhi.

Amesema katika mafanikio hayo ni pamoja na kuwepo na ongezeko la wawekezaji kwenye maeneo ambayo yaliyokuwa hayana mvuto kwa wawekezaji zikiwemo Hifadhi za Ruaha, Saadani na Mikumi ikiwa na Jumla ya maeneo mapya ya uwekezaji 176 (34 ni loji na 142 ni kambi) yameainishwa katika Hifadhi zote kwa kuzingatia mipango ya uendeshaji wa kila Hifadhi na yametangazwa kwenye tovuti ya Shirika.

Amesema kuongezeka kwa wigo wa shughuli za utalii wa puto (balloon) kutoka kufanyika katika Hifadhi ya Taifa Serengeti kwenda hifadhi za Tarangire, Ruaha na sasa maandalizi yanaendelea kwa hifadhi ya Mikumi; Utalii wa faru (Hifadhi ya Taifa Mkomazi), utalii wa baiskeli (Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro na Arusha.

Mwaka 2018 TANAPA iliingia katika mchakato wa kutambuliwa na Shirika la Viwango Duniani ili kujijengea kuaminiwa na wateja. Kutambuliwa kwa TANAPA mwaka 2021 na ISO kumepelekea wateja kuamini na kuchagua huduma zinazotolewa na TANAPA na hifadhi zake hivyo kuongeza idadi ya watalii na mapato. Katika miaka mitatu, Shirika limeendelea kutekeleza shughuli za utalii na uhifadhi kwa kuzingatia matakwa ya kiwango cha ubora cha ISO 9001:2015 kinachohusu utoaji wa huduma bora kwa wateja.

TANAPA imeendelea kuimarisha miundombinu ya ukusanyaji wa mapato ikiwemo kukamilisha ujenzi wa lango la kisasa la Naabi lenye uwezo wa kupokea zaidi ya magari 600 na wastani wa wageni zaidi ya 1,500 kwa siku. Katika kipindi cha miaka mitatu TANAPA pia imeweza kujenga malango mapya 10 na ya kisasa katika Hifadhi za Taifa Tarangire (2), Mkomazi (3), Serengeti (2) na Nyerere (3).

kutambua mienendo yao ili kurahisisha udhibiti wanapotoka nje ya maeneo ya hifadhi.

Hata hivyo amesema kupitia mradi wa REGROW, Shirika limewezesha mafunzo kwa askari wa vijiji (Village Game Scout – VGS) 354 kutoka vijiji 39 ili kuwezesha kukabili kwa wakati matukio ya wanyamapori wakali na waharibifu.

Aidha, Shirika linaendelea na ujenzi wa vituo 8 vya Askari Uhifadhi katika maeneo ya kimkakati yaliyopo katika vijiji vinavyoathirika zaidi katika wilaya za Mbarali, Kalambo, Kilwa, Namtumbo, Ruangwa, Serengeti, Bunda na Bariadi. Vituo hivi vitasaidia askari kudhibiti kwa wakati wanyamapori wakali na waharibifu.

Shirika limeendelea kufanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha kuwa linabuni vyanzo mbalimbali vya mapato ambavyo vitaliingizia Shirika fedha na kuongeza ukusanyaji wa mapato. Miongoni mwa vyanzo bunifu vya mapato ambavyo vimeendelea kuibuliwa na Shirika ni pamoja na kuanzishwa kwa Kampuni Tanzu ya Uwekezaji ya Shirika (TANAPA Investment Limited – TIL) inayolenga kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati na pia kuwa chanzo kikubwa cha mapato kwa Shirika kwa kutekeleza miradi mbalimbali Kuanzishwa kwa Kiwanda cha Ushonaji wa sare za watumishi na kupokea zabuni kutoka taasisi nyingi

Ujenzi wa Hoteli yenye hadhi ya nyota tatu katika eneo la Rubambagwe Wilaya ya Chato yenye vyumba 30 vya kulala; na Ujenzi wa Uwanja wa Gofu wa hadhi ya kimataifa wenye mashimo 18 uliopo eneo la Forti Ikoma - Hifadhi ya Taifa Serengeti.

Shirika limeendela kuimarisha uhifadhi wa wanyamapori walio katika hatari ya kutoweka na kuwezesha kuongezeka kwa idadi ya Wanyama hao wakiwemo faru, mbwa mwitu na sokwe.

Serikali ya awamu ya sita (6) imeweka mazingira wezeshi kwa Shirika kusimamia maliasili zilizopo katika Hifadhi za Taifa hapa nchini pamoja na upatikanaji wa rasimilimali fedha, rasilimali watu na vitendea kazi kama magari, mitambo ya kutengeneza barabara na mafunzo kwa watendaji.

Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na Kudhibiti uwindaji wa wanyama adimu ambapo hakukuwa na tukio la kuuawa kwa Faru, Sokwe au Mbwa mwitu.

Amesema kuwa wamekuwa na jitihada za kudhibiti uingizwaji wa mifugo hifadhini kwa kufanya doria na kutoa elimu ya uhifadhi kwa jamii zinazoishi jirani na hifadhi. Madhara ya uingizaji wa mifugo ni pamoja na uharibifu wa mazingira na vyanzo vya maji, maambukizi ya magonjwa kutoka kwa wanyama wafugwao kwenda kwa wanyamapori, kuendelea kushamiri na kusambaa kwa mimea vamizi na kuharibu shughuli za utalii.

Amesema Shirika linakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo Mabadiliko ya tabia nchi; (ukame, mafuriko, uwepo wa mimea vamizi inayoathiri upatikanaji wa chakula na mizinguko ya wanyamapori, uwepo wa ujangili ,Matukio ya uingizwaji wa mifugo ndani ya hifadhi,Matukio ya wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo ya jamii.

Shirika limeendelea kujiimarisha katika jitihada za utatuzi wa changamoto miongoni mwa mikakati inayoendelea kutekelezwa kama sehemu ya kukabiliana na baadhi changamoto zilizopo za uhifadhi na utalii ni pamoja Kutoa elimu ya uhifadhi kwa jamii

SHILINGI TRILIONI 1.4 KUTUMIKA KUKABILIANA NA MAGONJWA YA MALARIA, UKIMWI NA KIFUA KIKUU

March 21, 2024

 Na WAF- Dodoma

Serikali ya Tanzania imepokea jumla ya dola za kimarekani milioni 602 sawa na trilioni 1.4 za kitanzania kwa ajili ya kukabiliana na magonjwa ya Malaria, Kifua Kikuu na UKIMWI katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2024 hadi 2026.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. John Jingu leo Machi 21, 2024 jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano wa mkakati wa utekelezaji wa fedha hizo kupitia mradi mpya wa Mfuko wa Dunia mzunguko wa saba.

Dkt. Jingu amesema fedha zilizopokelewa zimetokana na jitihada za Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha huduma za afya ili ziweze kuwafikia wananchi katika maeneo yao bila kikwazo.

“Mkutano huu umeandaliwa kwa wakati muafaka ili uwe chachu ya kuhakikisha utekelezaji wa mradi huu unakua na ufanisi uliokusudiwa huku lengo letu ni kuangalia na kufanyia kazi mambo muhimu tuliyojiwekea kwenye mikakati itakayoongoza utekelezaji wa mradi huu katika kipindi chote cha utekelezaji”. Amesema Dkt. Jingu

Aidha, Dkt. Jingu amefafanua kuwa Serikali kwa kushirikiana na Wadau imeendelea kutenga rasilimali zinazotumika kugharamia utekelezaji wa afua mbalimbali za kudhibiti UKIMWI, Kifua Kikuu, Malaria na Uimarishaji wa Mifumo ya Afya hivyo ameushukuru mfuko wa dunia kuweza kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa afua zilizopangwa. 

“Tunatakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji na kuongeza uwajibikaji kwa lengo la kuboresha hali ya utoaji wa huduma za Afya nchini. Ili kufikia malengo haya, wote tunao wajibu wa kusimamia na kutekeleza ipasavyo mipango tuliyojiwekea na kuwezesha shughuli zote za mradi ambazo zimepangwa kutekelezwa kwa kipindi cha mwaka 2024-2026 zinakamilika kwa asilimia mia moja”. Amesisitiza Dkt. Jingu.

Akitoa salamu za Serikali ya Marekani, Mwakilishi wa Serikali ya Marekani Dkt. Etruda Temba, ameishukuru Serikali kwa kuandaa mkutano huo na kusema wadau wa Maendeleo wanatambua mchango wa Serikali  huku akitoa angalizo wakati wa utekelezaji kuepuka ubadhirifu wa fedha ili kupata matokeo yaliyokusudiwa.

Naye, Mwakilishi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Subisya Kabuje, amesema Wizara yao imekuwa mnufaika mkubwa wa fedha za Mfuko wa Dunia ambapo katika kipindi cha awamu ya sita TAMISEMI ilipokea shilingi Bilioni 39.9 zilizofanikisha ukamilishaji wa mfumo wa taarifa za afya wa GoTHOMIS ambao umekuwa kichocheo kikubwa katika kusimamia huduma za afya kwenye ngazi za Mikoa na Vituo vya afya.

Mapema akimkaribisha Katibu Mkuu kufungua Mkutano huo, Maganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu, amesema ni lazima nchi kujipanga kufikia malengo ya dunia namba tatu lakini pia kukamilisha lengo kwenye sekta ya Afya mkakati wa tano, ili ifikapo 2026 nchi iweze kujipima kikamilifu mafanikio iliyopata.






UJENZI WA KIWANJA CHA NDEGE CHA MSALATO SEHEMU YA KWANZA KUKAMILIKA DISEMBA, 2024

March 21, 2024

 Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato - Dodoma umefikia asilimia 54.1 kwa sehemu ya kwanza inayohusisha ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege, maegesho ya ndege, barabara za maungio na barabara za kuingia na kutoka kiwanjani ambapo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Disemba, 2024.


Bashungwa ameeleza hayo leo, Machi 21, 2024 wakati akiwasilisha Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2023/24 na Makadirio ya Mpango na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2024/25 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu.

"Nikuhakikishie Mwenyekiti kuwa ujenzi wa uwanja huu sehemu ya kwanza unaendelea vizuri na mkandarasi anaendelea na kazi, sehemu ya pili inayohusisha ujenzi wa jengo la abiria na majengo mengine nayo imefikia asilimia 17.1", amesema Bashungwa.

Aidha, Bashungwa amebainisha kuwa ukarabati, upanuzi na uboreshaji wa viwanja vya ndege vingine umefikia hatua mbalimbali ambapo Iringa (90%), Musoma (55%), Tabora (38%), Shinyanga (11%), Sumbawanga (6%) na Kiwanja cha Ndege cha Kigoma Mkandarasi yupo katika maandalizi ya kuanza ujenzi.

Bashungwa ameeleza kuwa Wakala wa Barabara (TANROADS) imefanikiwa kujenga barabara kwa kiwango cha lami zenye urefu wa kilometa 134.75 za barabara kuu, kilometa 23.11 za barabara za Mikoa na ukarabati kwa kiwango cha changarawe kilometa 253.67 katika kipindi cha utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2023/24.

Bashungwa ametaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa ikiwemo ujenzi wa Daraja la Kigongo-Busisi (km 3.2) na barabara unganishi (km 1.66) umefikia asilimia 85, ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Awamu ya Pili (km 20.3) umefikia asilimia 99.

Ameeleza miradi mingine ni ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje Dodoma (km 112.3) sehemu ya kwanza umefikia asilimia 68.3 na sehemu ya pili ya utekelezaji umefikia asilimia 56.32, upanuzi wa madaraja ya kibamba, kiluvya na mpiji yamekamilika pamoja na upanuzi wa barabara ya Kimara-Kibaha (km 19.2) njia nane.

Halikadhalika, Bashungwa amesema Wizara kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) imekamilisha ukarabati wa vivuko nane (8) ambavyo vinaendelea kutoa huduma maeneo mbalimbali, ukarabati wa vivuko vitatu (3) vipo katika hatua mbalimbali ya utekelezaji pamoja na ujenzi wa vivuko vipya sita vinaendelea.

Vilevile, Bashungwa amesema kuwa Wizara kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB) imesajili Mkandarasi 1,192 ambapo Mkandarasi wa ndani ni 1,155 na wa nje ni 37 sawa na asilimia 99.3 ya lengo kwa mwaka 2023/24.

Hata hivyo, Bashingwa ameeleza Wizara kupitia Wakala wa Majengo (TBA) inaendeleza ujenzi wa majengo yenye uwezo wa kuchukua familia nyingi kutoka familia 4 hadi 114 katika maeneo yaliyokuwa chini ya usimamizi wa TAMISEMI ikiwemo Temeke Kota, Magomeni Kota na Ghana Kota.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Selemani Kakoso ameitaka Wizara kuendelea kusimamia na kutekekeleza miradi yote iliyoahidiwa na Serikali ili wananchi kupata huduma stahiki zinazotarajiwa.

Kadhalika, Kakoso ameisitiza Wizara hiyo kuendelea kufuatilia mchakato wa upatikanaji wa fedha ili kulipa madeni ya Makandarasi na kusaidia miradi mingine kuweza kutekelezwa kwa wingi na kwa wakati.









TGNP-UWAKILISHI WA WANAWAKE NAFASI ZA UONGOZI BADO CHANGAMOTO

March 21, 2024

 NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV


TAKWIMU zinaonesha bado hakuna uwakilishi wa kutosha wa wanawake katika nafasi za uongozi, za kuchaguliwa au kuteuliwa katika ngazi mbalimbali za uongozi na hata hivyo ukilinganisha na tulipotoka, kuna mabadiliko chanya katika ushiriki wa wanawake na uongozi.

Lengo namba 5 la Malengo ya Maendeleo Endelevu linataka wanawake washiriki kikamilifu na kwa tija na fursa sawa katika uongozi na ngazi zote za maamuzi katika siasa, uchumi na Maisha kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa leo Machi 21, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa Mtandao wa Jinsia Tanzania- TGNP, Bi. Lilian Liundi wakati akifungua warsha ya waandishi wa habari ngazi ya jamii iliyofanyika katika Ofisi za TGNP Mabibo Jijini Dar es Salaam.

Amesema kutokana na mila na mitizamo kandamizi ambayo inadai kuwa wanawake hawana nafasi kwenye umma, madai yanayopewa nguvu na maarifa duni waliyonayo wanawake na uelewa mdogo wa haki zao,

"Kwa wale waliofanikiwa kuwa viongozi walau katika nafasi ndogo za maamuzi, wamekuwa wakiacha nafasi hizo kutokana na kukosekana kwa mfumo wa kuungwa mkono (supportive mechanism) kuanzia kwenye ngazi ya familia hadi jamii kwa ujumla". Amesema

Aidha amesema pamoja na kujivunia kuwa na wanawake viongozi katika nafazi za juu za maamuzi katika mihimili miwili ( Serikali na Bunge) pamoja na maeneo mengine, bado kuna changamoto kubwa katika kufikia 50/50.

Ameeleza kuwa bado hakuna mifumo rasmi na wezeshi ya kikatiba , kisheria na kisera, katika usawa katika nafasi za uongozi. Mila kandamizi, desturi na mitizamo hasi dhidi ya ushiriki wa wanawake katika maamuzi bado ni changamoto kubwa katika jamii yetu.

Kwa upande wake Mwandishi wa habari kutoka Rufiji FM, Bi. Kaundime Bakari amesema vyombo vya habari ni vyanzo vikubwa kupeleka taarifa eneo husika, hivyo atatumia chombo chake cha habari kuhakikisha wanatengeneza programu mbalimbali ambazo zinachochea wanawake kushiriki katika uongozi.

"Tunapoelekea kwenye kipindi cha uchaguzi, nitawashawishi wanawake wenzangu kuhakikisha wanashiriki katika kugombea nafasi ya uongozi mbalimbali na wasiweze kukaa nyuma". Amesema

Nae Mdau wa habari nchini, Bw. Meshack Michael amesema licha ya uwepo wa taasisi mbalimbali ambazo zinahimiza wanawake kushiriki katika uongozi, kuna jukumu la muhimu kwa waandishi wa habari nao wakatoa ushirikiano wa kutosha kwa taasisi hizo ili kundi kubwa la wanawake waweze kujitokeza katika kugombea nafasi za uongozi.












UCRT YAZINDUA MRADI WA UHIFADHI JUMUISHI WA MAZINGIRA NA KUBORESHA MAISHA YA JAMII YA MBULU

UCRT YAZINDUA MRADI WA UHIFADHI JUMUISHI WA MAZINGIRA NA KUBORESHA MAISHA YA JAMII YA MBULU

March 21, 2024

 

KATIBU Tawala wa Wilaya ya Mbulu, Paulo Bura ambaye amemwakilisha mkuu wa Wilaya ya Mbulu Veronica Kessy, amewataka watendaji wa vijiji, wenyeviti wa vijiji na watendaji wengine wa kata waweze kuwapa ushirikiano wa kila hali shirika la UCRT ili kile walichokuja nacho kiweze kuwanufaisha wananchi wa wilaya ya Mbulu na lengo lao la makusudi na nia yao njema iweze kutimia.

Hayo yalisemwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Mbulu, Paulo Bura, wakati akifungua kikao cha uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji sita, chini ya Ujamaa Community Resource Team (UCRT), uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Machi 19, 2024.

“Lakini sisi tulioingia kwenye awamu hii vijiji hivi sita, pia tujue sisi ni mfano wa vijiji vingine ambavyo vimeendelea kuombwa ili viingie kwenye mradi,wale wa awamu ya kwanza vijiji vitano hawajatuangusha,ndio maana maombi yalivyorudishwa kwa wahisani wa maendeleo wakaona vile vijiji vilifanya vizuri, kwahiyo hata hivi vijiji sita vikifanya vizuri vinaweza kuwa fursa na mlango kwa ajili ya vijiji vingine, kwa hiyo sisi ambao tuliopata fursa na bahati hiyo tuweze kuitumia vizuri ili basi tuweze kufungua milango kwa vijiji vingine kuweza kunufaika na mradi huu mzuri kwa ajili ya hifadhi ya mazingira lakini pia kwa ajili ya uchumi wa wananchi wetu.” Alisema Bura.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Hamashauri ya wilaya ya Mbulu Petro Tarmo aliwaomba wale wanufaika wa mradi wa zamani waendelee kutoa ushirikiano na hawa wapya waendelee pia kutoa ushirikiano kwa UCRT, waendelee kutoa elimu kwa wananchi na kuepuka migogoro ya mipaka ambayo inaweza kupelekea changamoto kwenye mradi. Waepukane na migogoro ili waende kwenye maslahi mapana ya wananchi.

Aidha mratibu wa Ujamaa Community Resource Team (UCRT), Dismas Meitaya ameushukuru uongozi wa wilaya Mbulu kwa ujumla kwa kuweza kuushirikiana nao vizuri kwa Zaidi ya miaka ishirini waliyokuwa wakitekeleza miradi yao. Ikiwemo ofisi ya mkuu wa Wilaya, ofisi ya Mkurugenzi, wataalam wa hamashauri na viongozi wa vijiji.

Alisema kuwa malengo makuu ya UCRT ni kuwezesha jamii ya asili kuweza kumiliki, kusimamia na kunufaika na ardhi. Na wamelenga Zaidi kwenye jamii ya wakusanya matunda, ambao ni wa hadzabe na waakie, wamaasai, wadatoga pamoja na wafugaji – wakulima wabatemi na wa iraqw.

“Huu mpango ni shirikishi sana, wakina mama wanapewa kipaumbele na washiriki kisawa sawa. Kwa hiyo nataka kuona jamii ya akina mama na vikundi vingine wakiwa mstari wa mbele kushirikishwa kwa kila hatua ambayo tunakuja kufanya.” Alisema Dismas.

Alibainisha vijiji lengwa sita vya mradi katika bonde la Yaeda na ziwa Eyasi ni Garbabi, Yaedakati, Dirim, Endalat, Murkuchida na Endamilay.      

MGODI WA BARRICK BULYANHULU WAONGEZEWA MUDA WA LESENI YA UCHIMBAJI

March 21, 2024

 

Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba (kushoto) akimkabidhi leseni ya kuongezewa muda wa uchimbaji wa mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido katika hafla hiyo , wanaoshuhudia nyuma (kushoto) ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha. Leseni hii mpya iliyotolewa ni ya kipindi cha miaka 27.
---
Serikali kupitia Wizara ya Madini imeongeza muda wa leseni ya uchimbaji wa dhahabu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, uliopo katika wilaya za Kahama na Nyang’hwale mkoani Shinyanga kwa kipindi cha miaka 27 kuanzia mwaka huu.

Hafla ya kukabidhi leseni hiyo ilifanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Maofisa waandamizi kutoka Wizara ya madini, Wakuu wa mikoa ya Tanga na Shinyanga na wadau mbalimbali kutoka sekta ya madini ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Waziri wa Madini, Mh.Antony Mavunde.
Aliyekabidhi leseni hiyo ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, na Mwakilishi wa Barrick, aliyepokea leseni hiyo kwa niaba ya kampuni ni Meneja wa Barrick Tanzania, Melkiory Ngido.

Mgodi wa Bulyanhulu tangu uanze kuendeshwa na kampuni ya Barrick kwa kushirikiana na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals, umefanikisha kuleta mafanikio chanya katika kukuza uchumi wa nchi ,kuongeza fursa za ajira sambamba na kutekeleza miradi mikubwa ya kijamii kupitia fedha za uwajibikaji wa jamii (CSR) ambayo inazidi kuboresha maisha ya wananchi katika maeneo yanayozunguka mgodi huo hususani katika sekta ya afya na elimu.
Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kushoto) katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa makampuni ya uchimbaji wa madini waliokabidhiwa leseni katika hafla hiyo.

Maofisa Waandamizi wa Barrick waliohudhuria hafla hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu.

Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (kulia) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita wakati wa hafla hiyo.
 Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Antony Mavunde katika hafla hiyo.