Waziri
Mkuu Mh. Mizengo Pinda akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja
wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo mara baada ya kuwasili akitokea
katika ziara yake ya Ulaya na Mashariki ya Kati Oman.
Baadhi ya viongozi alioongozana nao katika ziara hiyo wakiwa katika mkutano huo.
…………………………………………………………………..
Na Magreth Kinabo – MAELEZO
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema Serikali imeanza kulifanyia kazi
tatizo la wakulima kukosa mahali pa kuhifadhia ya mazao yao, hivyo
litapatiwa ufumbuzi katika kipindi cha miezi mitatu hadi minne ijayo
baada ya mpango wa kujenga maghala makubwa kuanza.
Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu, Pinda katika mkutano wake na
waandishi wa habari alioufanya mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K.Nyerere uliopo jijini Dares
Salaam kufuatia ya ziara yake ya kikazi katika nchi za Uingereza, Poland
na Oman. yenye lengo la kuhimarisha mahusiano.