SERIKALI YAAHIDI KUTAFUTA UFUMBUZI SUALA UHABA WA MAGHALA.

SERIKALI YAAHIDI KUTAFUTA UFUMBUZI SUALA UHABA WA MAGHALA.

October 30, 2014

Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere  leo mara baada ya kuwasili  akitokea katika ziara yake ya Ulaya  na Mashariki ya Kati Oman. 2 
Baadhi ya viongozi alioongozana nao katika ziara hiyo wakiwa katika mkutano huo.
…………………………………………………………………..
Na Magreth Kinabo – MAELEZO
Waziri Mkuu Mizengo  Pinda amesema  Serikali imeanza kulifanyia kazi tatizo la wakulima kukosa mahali pa kuhifadhia ya mazao yao, hivyo  litapatiwa  ufumbuzi katika kipindi cha miezi mitatu hadi minne ijayo baada ya mpango wa kujenga maghala makubwa kuanza.
Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu, Pinda  katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu  Julius  K.Nyerere  uliopo jijini Dares Salaam kufuatia ya ziara yake ya kikazi katika nchi za Uingereza, Poland na Oman. yenye lengo la kuhimarisha mahusiano.
Rais Kikwete afungua Maadhimisho ya miaka 10 ya Tume ya Utumishi wa Umma

Rais Kikwete afungua Maadhimisho ya miaka 10 ya Tume ya Utumishi wa Umma

October 30, 2014

 D92A1608 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano la Maadhimisho ya miaka 10 ya Tume ya tutmishi wa Umma lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam . D92A1654 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano la Maadhimisho ya miaka 10 ya Tume ya tutmishi wa Umma lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam . D92A1782 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Maadhimiso ya miaka 10 ya tume ya Umma lililofanyika jijini Dar es Salaam leo.D92A1837 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (wa tatu kushoto) pamoja na makatibu wakuu Kiongozi wastaafu Matern Lumbanga(kulia) na Philemon Luhanjo(kushoto)(picha na Freddy Maro)
Viongozi wa Msondo wamtembelea Rais Kikwete Ikulu

Viongozi wa Msondo wamtembelea Rais Kikwete Ikulu

October 30, 2014


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na viongozi wa Bendi ya Msondo ngoma ikulu jijini Dar es Salaam leo mchana.Viongozi hao walimtembelea Rais Kikwete ikulu leo na kufanya naye mazungumzo(picha na Freddy Maro). D92A1988 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha ya pamoja  na viongozi wa Bendi ya Msondo ngoma ikulu jijini Dar es Salaam leo mchana.Viongozi hao walimtembelea Rais Kikwete ikulu leo na kufanya naye mazungumzo(picha na Freddy Maro).

Spika Makinda apigiwa chapuo Urais Bunge la SADC

October 30, 2014

Na Owen Mwandumbya, Victoria Falls, Zimbabwe
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda ameendelea kuungwa mkono na wajumbe wa Mkutano wa 36 ambao ni Maspika na Wabunge kutoka Umoja wa Chama cha Mabunge ambao ni wanachama wa  nchi za kusini wa Jangwa la Sahara (SADC PF) kugombea nafasi ya Urais ya Umoja huo ili aweze kuongoza kwa kipindi cha miaka 2 ijayo katika chama hicho.
Jitihada hizo zimeendelea kujitokeza hapa Victoria Falls ambako mkutano huo unafanyika baada ya baadhi ya Maspika wa Nchi za SADC pamoja na wabunge wao kuomba miada ya kukutana naye na kumwambia dhahiri kuwa nchi zao wanamuunga mkono na wangependa aweze kushiriki uchaguzi huo ili waweze kumchagua awaongoze katika kipindi cha miaka miwili kutimiza malengo waliyojiwekea katika umoja huo.

WAZIRI WA FEDHA AZINDUZI WA CHAPISHO KUU LA UTAFITI WA MAPATO NA MATUMIZI YA KAYA BINAFSI 2011-2012-TANZANIA BARA

October 30, 2014


Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum (Katikati) akionyesha kitabu cha Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2011/12 wakati akikizindua katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam jana Oktoba 29, 2014. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Ofisa kutoka Shirika la Maendeleo la DPG, Sinikka Antila, Mwakilishi wa Benki ya Dunia, Philippe Dongier na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu.  Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.

Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kitabu cha Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2011/12 wakati akikizindua katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam jana Oktoba 29, 2014. Wanaoshuhudia ni Afisa Habari wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Veronika Kazimoto (kulia) na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu (katikati).

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dk. Albina Chuwa akimfafanulia jambo Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum mara baada ya kufanya uzinduzi.

Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum akimkabidhi chapisho Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu.

Wawakilishi toka Mashirika mbali mbali ya Kimataifa wakiwa katika picha ya pamoja.
   Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, akihutubia wageni waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa kitabu cha Ripoti ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi wa Mwaka 2011/12 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam jana Oktoba 29, 2014.

Wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini.
Waandishi wa habari nao hawakuwa mstari wa nyuma.
Meza kuu ikifuatilia kwa makini.
Wanafunzi wa Chuo cha Takwimu nao walifika.
Wawakilishi toka mashirika ya kimataifa nao walifika.

Furaha ya kukutana pamoja.
Picha ya Pamoja.

“RC GALLAWA AAMURU MKAGUZI WA NDANI WA HALMASHAURI AWEKWE NDANI”

October 30, 2014





MKUU wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu ChikU Gallawa amemuagiza Mkuu wa
Jeshi la Polisi wilaya ya Tanga(OCD)Omari Ntungu kumkamata Mkaguzi wa
ndani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Hassani Njama na kumuweka ndani
mpaka atakapomaliza ziara yake kwa kushindwa kuwepo eneo la usimamizi
wa mradi wa ujenzi wa maabara.