(Kikosi cha timu ya TA Veteran SC Kutoka kushoto ni David Stanlaus,Mohamed Kirua(Kazungu),Edgar Mdime,Daud Kabingwa,Iddy Bilal,Kilango Salum,Peter Kwingwa,Acheni Maulid na Dastan Charles)
Na Oscar Assenga,Tanga.
Na Oscar Assenga,Tanga.
TIMU ya Maveteran ya TA Veteran SC ambayo inaundwa na wachezaji
kutoka sekta mbalimbali mkoani hapa imeanza mazoezi yake mwishoni mwa wiki
kwenye uwanja wa shule ya Msingi Bombo ikijiandaa na bonanza la maveteran.
Akizungumza na blog hii,Katibu wa timu hiyo,Edgar Mdime
amesema uanzishwaji wa timu hiyo ni kuleta changamoto ya kisoka mkoani Tanga
pamoja na kutoa burudani kwa wapenda soka mkoani hapa hasa ukizingatia
maveteran wanapokutana hubadilishana mawazo na kukumbushana enzi zao.
(Mshambuliaji wa timu ya TA Veteran SC Edgar Mdime akiwa mazoezini mwishoni mwa wiki)
Mdime alisema wanatarajiwa kufanya ziara ya kimichezo katika
wilaya zote za mkoani wa Tanga kucheza mechi za kirafiki na maveteran za wilaya
hizo lengo likiwa kutoa burudani kuonyesha soka la kisasa.
Kikosi cha timu hiyo kinaundwa na David Stanlaus, Mohamed Kirua(Kizungu),Edgar Mdime, Daud Kubingwa,Iddy Bilal,Kilango Salum,Peter Kwingwa, Acheni Maulid na Dastan Charles .
Mwisho.
Mwisho.