Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy
Mwalimu akizungumza na wananchi wa Tarime mkoani Mara na kutoa miezi
sita kwa wakuu wa shule za Msingi na Sekondari kuanzisha madawati ya
ulinzi na usalama kwa mtoto kike katika Shule zao.
Mkuu
Wa mkoa wa Mara Mhe. Charles Mlingwa akihamasisha wananchi wa mkoa wa
Mara kuzingatia na kulinda haki za Mtoto katika Maadhimisho ya Siku ya
Kimataifa ya Mtoto wa Kike iliyofikia kilele chake 11/10/2017.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
akizindua kampeni ya kitaifa ya kutokomeza mimba za utotoni yenye kauli
mbiu isemayo:” "Najitambua Elimu ndio Mpango mzima".
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
akibonyeza kitufe kuzindua ujumbe wa radio wa kampeni ya kutokomeza
mimba za utotoni yenye kauli mbiu isemayo:” Najitambua Elimu ndio Mpango
Mzima”
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto, wadau na madereva
bodaboda wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara muda mfupi baada ya Maadhimisho
ya Siku ya Mtoto wa Kike yaliyofanyika kitaifa wilayani Tarime mkoani
Mara. Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW