WATANZANIA CALIFORNIA WAMUAGA BALOZI LIBERATA MULAMULA

August 01, 2015

 Watanzania California wakiongozwa na Balozi wa Heshima Mhe. Ahmed Issa walijumuika pamoja siku ya Ijumaa na kumuaga Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico na kurudi nyumbani kwenda kulitumikia taifa kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Watanzania wa California wakipiga picha ya pamoja na Mhe. Balozi Libarata Mulamula (wapili toka kushoto) siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomuaga rasmi.
 Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi yake Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme mara tu baada ya kukabidhiwa na Watanzania California siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomualika rasmi kwa ajili ya kumuaga.
 Balozi Liberata Mulamula akicheza na kuburudika kwenye moja ya nyimbo zilizopigwa kwenye tafrija hiyo.
 Balozi Liberata akipiga makofi
Moja wa kikundi maarufu cha ngoma ya asili kikitoa burudani

Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar akutana na ujumbe Taasisi ya Ushauri wa Uhandisi katika miundombinu ya ujenzi, usarifu wa Miji, Majengo ya Kisasa pamoja na Vituo vya Kimataifa vya Biashara { ECG } ya Nchini Misri

August 01, 2015

Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Ushauri wa Uhandisi katika miundombinu ya ujenzi, usarifu wa Miji, Majengo ya Kisasa pamoja na Vituo vya Kimataifa vya Biashara { ECG } ya Nchini Misri Mhandisi Amri Alouba akimuonyesha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar michoro iliyotengenezwa na Wataalamu wa ECG ya jinsi linavyoweza kujengwa eneo la Darajani na kuwa katika mazingira ya Biashara ya Kimataifa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Wafanyabiashara pamoja na wataalamu wa ushauri wa Uhandisi kutoka Nchini Misri waliopo Tanzania kuangalia maeneo ambayo wanaweza kuwekeza miradi ya Kiuchumi.
Meneja wa Biashara wa Kampuni ya Kimataifa ya AIKAN ya Nchini Misri Bwana Mohammed Alef Sherief wa kwanza kutoka kushoto akimfahamisha Balozi Seif hayupo pichani fursa zinazotolewa na Taasisi yake katika kuwajengea Vijana uwezo wa kufanya Biashara.
Balozi Seif katika Picha ya pamoja na Wafanyabiashara na wataalamu wa ushauri wa Uhandisi kutoka Nchini Misri mara baada ya kufanya mazungumzo nao Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar. Kushoto ya Balozi Seif ni Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Ushauri wa Uhandisi katika miundombinu ya ujenzi, usarifu wa Miji, Majengo ya Kisasa pamoja na Vituo vya Kimataifa vya Biashara { ECG } ya Nchini Misri Mhandisi Amri Alouba na Balozi wa Tanzania Nchini Misri Balozi Mohammed Hamza. Kulia ya Balozi Seif ni Mtaalamu wa Taasisi ya Ushauri wa Uhandisi katika miundombinu ya ujenzi, usarifu wa Miji ya ECG Mhandisi Sherif Meurad pamoja na Meneja wa Biashara wa Kampuni ya Kimataifa ya AIKAN ya Nchini Misri Bwana Mohammed Alef Sherief.
Balozi Mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Bwana Ali akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kabla ya kufanya mazungumzo yao ya Ushirikiano wa kuimarisha uhusiano wa Kihistoria wa muda mrefu wa kidugu uliopo baina ya Oman na Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na Balozi Mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Bwana Ali Abdullah Ofisini kwake Mtaa wa Vuga Mjini Zanzibar. Picha na – OMPR – ZNZ.

Taasisi ya Ushauri wa Uhandisi katika miundombinu ya ujenzi, usarifu wa Miji, Majengo ya Kisasa pamoja na Vituo vya Kimataifa vya Biashara { ECG } ya Nchini Misri imeamua kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika azma yake ya kusaidia Uchumi wa Zanzibar na ustawi wa Wananchi wake.

Kiongozi wa Ujumbe wa Wafanyabiashara wa Misri wanaotembelea Tanzania kuangalia maeneo wanayoweza kushirikiana na Serikali katika uwekezaji Mhandisi Amr Allouba alisema hayo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Ofisi kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Mhandisi Amri Allouba ambae pia ni Makamu  Mwenyekiti wa Taasisi hiyo ya  uhandisi ya { ECG } alisema Wataalamu wa Taasisi hizo wako tayari kuelekeza nguvu zao ndani ya ukanda wa Afrika ya Mashariki, Zanzibar ikiwa miongoni mwake kutokana na mazingira mazuri ya rasilmali pamoja na uwekezaji.

Makamu Mwenyekiti huyo wa Taasisi ya Uhandisi ya ECG alisema Wataalamu wa Taasisi hiyo tayari wameshaandaa michoro ya jinsi linavyoweza kujengwa eneo la Darajani na kubadilishwa kuwa katika mazingira ya kisasa ya Biashara  ya Kimataifa.

Mhandisi Amr alifahamisha kwamba eneo hilo la Darajani upande wa iliyokuwa kituo cha Dala dala pamoja na Makontena linaweza kujengwa Vituo vya Biashara bila ya kuathiri mipango Miji iliyowekwa katika Mji Mkongwe wa Zanzibar ambao umo katika urithi wa Kimataifa.

Wakati huo huo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikutana na Balozi Mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Bwana Ali Abdulla Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Katika mazungumzo yao Balozi Seif kupitia Balozi Mdogo huyo wa Oman aliishukuru Serikali ya Nchi hiyo kwa jitihada inazochukuwa katika kusaidia harakati za Maendeleo ya Wananchi wa Zanzibar.

Mapema Balozi Mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Bwana Ali Abdulla alimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Nchi yake itaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika harakati zake za kuelekea kwenye maendeleo.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
1/8/2015.

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MHIMBILI 1988 WAIKUMBUKA SHULE YAO.

August 01, 2015

Mgeni Rasmi Balozi Kassimu Mwawado, akikata utepe ili kufungua Ofisi ya walimu wa shule ya msingi Mhimbili, iliyokarabatiwa na kuweka viti 29 na meza 8 na wanafuzi waliohitimu darasa la saba katika shule hiyo Mwaka 1988, pamoja na kiti na meza ya kisasa katika ofisi ya Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo katika hafra fupi iliyoandaliwa na wanafunzi hao ikiwa imeudhuliwa na walimu wa shule hiyo wa tangu mwaka 1978.
 Walimu wa Shule ya Msingi Mhimbili wakifurahia kupewa viti vipya pamoja na meza na wanafunzi wao waliohitimu shule ya msingi mwaka 1988 katika shule hiyo, wamekabidhiwa Samani hizo leo katika shule hiyo jijini Dar es Salaam.
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mhimbili, Dafrosa Assenga akipeana mkono na Mgeni Rasmi Balozi Kassimu Mwawado, mara baada ya kukabidhiwa kiti na meza Mpya kutoka kwa wanafunzi walihitimu katika shul;e hiyo Mwaka 1988, ikiwa ni mchango wao katika kuendeleza elimu katika shule hiyo.Kutoka kulia ni Mhitimu wa shule ya msingi Mhimbili mwaka 1988 na Mkurugenzi wa Galaxy Cargo, Jonatha Kasesele, Mwenyekiti wa wahitimu 1988  shule ya msingi mhimbili,Usia Mkoma
Mwalimu mstaafu katika shule ya msingi Mhimbili wa mwaka 1972-2012, Amani Ndussy na  Mwenyekiti wa bodi shule ya msingi Mhimbili, George Ntevi.
Mwalimu mstaafu katika shule ya msingi Mhimbili wa mwaka 1972-2012, Amani Ndussy akizungumza mara baada ya wanafunzi wa hitimu wa sarasa la saba mwaka 1988 katika shule hiyo kukabidhi viti vya walimu pamoja na meza, katika hafra fupi iliyoandaliwa na wanafunzi hao katika shule hiyo jijini Dar es Salaam leo. 
Mwalimu wa shule ya msingi Mhimbili wa mwaka 1986 hadi sasa, Marry Massawe akiwashukuru wanafunzi waliosoma shule hiyo kwa kuikumbuka shule yao.
Wanafunzi wa shule ya msingi Mhummbili mwaka huu wakiwa wamehudhulia hafra fupi ya wahitimu wa shule hiyo mwaka 1988 leo jijini Dra es Salaam.
 Wanafunzi wa shule ya msingi Mhimbili wakiimba wimbo kuwashukuru wanafunzi wa zamani katika shule hiyo kwa kuwakumbuka waalimu wao pamoja na shule yao.
Baadhi ya wanafunzi waliomaliza katika shule ya Msingi Mhimbili wakiwa wamehudhuria hafra fupi pamoja na waalimu wao,katika shule hiyo jijini Dar es Salaam leo. 
 Kutoka kushoto ni Mhasibu wa wahitimu wa 1988 shule ya Msigi Mhimbili, Ernest Nyambo  katikati ni Makamu Mwenyekiti wa bodi shule ya msingi Mhimbili, Jacquline Kaluwa na Mwenyekiti wa wahitimu 1988  shule ya msingi mhimbili,Usia Mkoma wakiwa wameshiriki hafra iliyoandaliwa na wasnafunzi hao katika shule ya msingi Mhimbili jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii

LOWASSA ARUDISHA FOMU ZA KUWANIA URAIS KUPITIA CHADEMA, ADHAMINIWA NA ZAIDI YA WANANZANIA ZAIDI YA MIL. 1.6

August 01, 2015

 Mtangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akiwapungia maelfu ya wafuasi na wapenzi wa Chama hicho, wakati alipowasili kwenye Ofisi ya Makao Makuu ya Chama hicho, Kinondoni Jijini Dar es Salaam jioni ya leo. Mh. Lowassa alifika ofisini hapo kurudisha fomu za kuomba ridhaa ya Chama hicho, kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.Kulia kwake ni Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Mh. Godluck Ole Medeye alieambatana nae.
 Mtangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA - Zanzibar, Salum Mwalim wakati akilakiwa kwenye Makao Makuu ya Chama hicho, Kinondoni Jijini Dar es salaam leo.
 Mtangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akiwasalimia wafuasi wa Chama hiyo kwa ishara ya vidole viwili.
 Sehemu ya Viongozi wa CHADEMA waliokuwepo kwenye hafla hiyo.
 Baadhi ya Wadau walioambatana na Mh. Lowassa.
 Wakitambulishwa.
 Mkurugeni wa Oganaizesheni na Uratibu wa Kanda wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Benson Kigaila akionyesha fomu zenye idadi ya wananchi waliomdhani Mtangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama hicho, Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa. ambapo jumla ya wananchi 1,662,397 walijitokea katika maeneo mbali mbali kumdhamini Mgombea huyo.
 Mtangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa (wa pili kulia) akikabidhi fomu hizo kwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Prof. Abdalaah Safari wakati wa hafla fupi ya kurudisha fomu hizo, iliyofanyika jioni ya leo kwenye Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA, Kinondoni Jijini Dar es salaam. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Wadhamini wa CHADEMA, Mh. Arcado Ntagazwa na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA - Zanzibar, Salum Mwalim.
Mtangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Prof. Abdalaah Safari wakionyesha fomu hizo kwa wanahabari.Kushoto ni  Mwenyekiti wa Wadhamini wa CHADEMA, Mh. Arcado Ntagazwa.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Prof. Abdalaah Safari akizipitia fomu hizo.
Mwanasheria wa CHADEMA, Mh. Mabere Marando akizipitia fomu hizo kama zimejazwa sawa sawa.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Prof. Abdalaah Safari akizungumza machache baada ya kupokea fomu hizo.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Prof. Abdalaah Safari akipongezwa na Mtangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa.
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA - Zanzibar, Salum Mwalim akizungumza.
Sehemu ya Wabunge wa CHADEMA waliokuwepo.





Mchezo wa Kirafiki Kati ya Simba na Polisi Usiku Huu Uwanja wa Amaan Simba Ikiwa mbele kwa bao 2--0

August 01, 2015

Mgeni wa rasmin katika mchezo wa kirafiki kati ya Simba na Polisi Zanzibar Kamishna wa Polisi Zanzibar Ndg Hamdanmi kulia Mwenyekiti wa ZFA Wilaya ya Mjini Ndg Hassan Chura na kushoto Mjumbe wa Kamati Tendaji ya ZFA Taifa Hashim Salum na Kiongozi wa timu ya Polisi.wakisimama wakati ukipigwa wimbo wa Polisi na Usalama wa Raia kabla ya kuaza kwa mchezo huo wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan Simba imeshinda 2--0 
Wachezaji wa timu ya Polisi na Simba wakisimama wakati wa kupigwa kwa wimbo wa Usalama wa Raia kabla ya kuaza kwa mchezo wao wa kirafiki kujiandaa na michezo ya Ligi Kuu inayotarajiwa kuaza mwezi ujao.  
Makocha wa Simba wakifuatilia wimbo huo maalum uliopigwa wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan timu ya Simba imeshinda 2--0.
Kamishna wa Polisi Zanzibar Kamishna Hamdan akisalimiana na wachezaji wa Timu ya Polisi Zanzibar kabla ya kuaza kwa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan.
Kamishna wa Polisi Zanzibar Kamishna Hamdan akisalimiana na wachezaji wa Timu ya Polisi Zanzibar kabla ya kuaza kwa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan.
Kikosi cha timu ya Polisi Zanzibar kilichokubali kipigo cha bao 2--0 kutoka kwa timu ya Simba wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Kikosi cha timu ya Simba kilichotowa kipigo cha mabao 2--0 dhidi ya timu ya Polisi Zanzibar wakati wa mchezo wao wa kujipima nguvu wa tatu kisiwani Zanzibar ikiwa imeshinda michezo yake yote
Mchezaji wa timu ya Simba akimiliki mpira huku mchezaji wa timu ya Polisi akijiandaa kumzuiya wakati wa mchezo huo
Kazi hiyo kuwania mpira kati ya wachezaji hawa wakiwa wameinua madaruga yao juu bila ya mafanikio kuupata mpira.
Mshambuliaji wa timu ya Simba na kipa wa timu ya Polisi wakiwania mpira wakati wa mchezo wao huo wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan Simba imeshinda 2--0.
      Kipa wa timu ya Polisi akiokoa mpira golini kwake huku mchezaji wa Simba akiwa nyuma yake
Mchezaji wa timu ya Simba akimpita beki wa timu ya Polisi wakati wa mchezo wao wa kirafiki kujipima nguvu kujiandaa na Ligi Kuu zinazotarajiwa kuaza hivi karibuni Ligi ya Tanzania Bara na ya Zanzibar.
Mchezaji wa Simba akijiandaa kumpita beki wa timu ya Simba, wakati wa mchezo wao wa kirafiki katika mchezo huo timu ya Simba imeshinda 2--0
                       Wachezaji wa timu ya Simba na Polisi wakiwania mpira
Mshambuliaji wa timu ya Simba akiweka majaro golini kwa timu ya Polisi 
Picha na OthmanMapara.Blog Zanzinews.com