January 21, 2014

Kampuni ya Issere Sports yazawadiwa

DSC_0224
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Amos Makala ambaye kwa sasa amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri akimkabidhi vyeti vya utendaji bora wa huduma za michezo Mkurugenzi wa Masoko  Kampuni ya Issere Sports, Abbas Ally Issere katika kongamano la Wasanii lililoandaliwa na Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Makala kwa sasa amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri (Picha na Mpiga Picha Wetu).
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Issere Sports inayojishughulisha na uuzaji wa vifaa vya michezo nchini ni miongoni mwa wanamichezo, wasanii na awaandishi wa habari 1,000 waliotunukiwa vyeti vya utendaji bora katika fani za michezo kwa mwaka 2013 hadi 2014 katika kongamano lililofanyika ukumbi wa Lamada, Ilala Dar es Salaam.
Katika kongamano hilo ambalo kulitolewa mada mbili za kusaidia jamii ya wanamichezo kujiepuka na matumkizi ya dawa za kulevya, ya pili ikiwa ya maadili bora katika jamii, Kampuni ya Issere ni pekee iliyopata nafasi ya kuwakilisha nyingine zinazojihusisha na uuzaji wa vifaaq vya michezo.
January 21, 2014

Kampuni ya Issere Sports yazawadiwa

DSC_0224
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Amos Makala ambaye kwa sasa amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri akimkabidhi vyeti vya utendaji bora wa huduma za michezo Mkurugenzi wa Masoko  Kampuni ya Issere Sports, Abbas Ally Issere katika kongamano la Wasanii lililoandaliwa na Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Makala kwa sasa amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri (Picha na Mpiga Picha Wetu).
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Issere Sports inayojishughulisha na uuzaji wa vifaa vya michezo nchini ni miongoni mwa wanamichezo, wasanii na awaandishi wa habari 1,000 waliotunukiwa vyeti vya utendaji bora katika fani za michezo kwa mwaka 2013 hadi 2014 katika kongamano lililofanyika ukumbi wa Lamada, Ilala Dar es Salaam.
Katika kongamano hilo ambalo kulitolewa mada mbili za kusaidia jamii ya wanamichezo kujiepuka na matumkizi ya dawa za kulevya, ya pili ikiwa ya maadili bora katika jamii, Kampuni ya Issere ni pekee iliyopata nafasi ya kuwakilisha nyingine zinazojihusisha na uuzaji wa vifaaq vya michezo.
January 21, 2014

Kampuni ya Issere Sports yazawadiwa

DSC_0224
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Amos Makala ambaye kwa sasa amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri akimkabidhi vyeti vya utendaji bora wa huduma za michezo Mkurugenzi wa Masoko  Kampuni ya Issere Sports, Abbas Ally Issere katika kongamano la Wasanii lililoandaliwa na Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Makala kwa sasa amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri (Picha na Mpiga Picha Wetu).
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Issere Sports inayojishughulisha na uuzaji wa vifaa vya michezo nchini ni miongoni mwa wanamichezo, wasanii na awaandishi wa habari 1,000 waliotunukiwa vyeti vya utendaji bora katika fani za michezo kwa mwaka 2013 hadi 2014 katika kongamano lililofanyika ukumbi wa Lamada, Ilala Dar es Salaam.
Katika kongamano hilo ambalo kulitolewa mada mbili za kusaidia jamii ya wanamichezo kujiepuka na matumkizi ya dawa za kulevya, ya pili ikiwa ya maadili bora katika jamii, Kampuni ya Issere ni pekee iliyopata nafasi ya kuwakilisha nyingine zinazojihusisha na uuzaji wa vifaaq vya michezo.
January 21, 2014

Wasafirishaji wahimizwa kutii sheria bila shuruti

DSC05860
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, akifungua rasmi ofisi ya SUMATRA mkoa wa Singida.Kulia ni mstahiki meya wa manispaa ya Singida,Sheikh Salum Mahami na katikati ni kaimu mkurugenzi wa SUMATRA Ahmed Kilima.Picha na Nathaniel Limu.
DSC05857
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone,akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa ofisi ya SUMATRA ya mkoa wa Singida.Kulia ni Kaimu mkurugenzi mkuu wa SUMATRA Ahmed Kilima na kushoto ni meya mstahiki meya wa manispaa ya Singida,Sheikh Salum Mahami.
DSC05849
Baadhi ya wadau wa usafirishaji mkoa wa Singida,waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa ofisi ya SUMATRA mkoa wa Singida iliyofanyika mjini Singida.
Na Nathaniel Limu, Singida
MKUU  wa Mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone, amewahimiza wasafirishaji wa abiria na mizigo kujenga utamaduni wa kutii sheria na kanuni bila shuruti ili kujiepusha na faini mbali mali zinazopunguza mapato yao.
Dk. Kone ametoa wito huo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye ufunguzi wa ofisi ya SUMATRA mkoa wa Singida zilizoko kwenye majengo ya idara ya ujenzi mjini hapa.
Amesema baadhi ya wasafirishaji wamekuwa wakilalamikia faini na adhabu za SUMATRA kuwa ni kali sana.
January 21, 2014

NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA HABARI APOPOKELEWA KATIKA OFISI ZA WIZARA HIYO

IMG_9633Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Olegabriel akimkaribisha Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia katika tukio la kumkaribisha lililofanyika jijini Dar es Salaam jana IMG_9642  Mkurugenzi  Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania Bwana Clement Mshana (kushoto) akimpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia wakati wa mapokezi yake katika Ofisi za Wizara zilizopo jijini Dar es Salaam Leo  katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara Prof. Elisante Olegabriel IMG_9649Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA Bwana Kulwa Magingila wakati wa mapokezi yake yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara Prof Elisante Olegabriel
January 21, 2014

Tuesday, January 21, 2014

BAWAZIR AIPIGA JEKI UHURU SC


Mwenyekiti wa CCM kata ya Jangwani, Mohamed Bawazir akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mwenyekiti wa CCM kata ya Jangwani, Mohamed Bawazir (kulia) akikabidhi mpira kwa Katibu wa klabu ya michezo ya Uhuru, Rashid Zahor (kushoto), ikiwa ni sehemu ya vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. 450,000 alivyotoa msaada kwa timu hiyo juzi katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Uhuru Publications Ltd, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo la Burudani, zilizoko barabara ya Lumumba, Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Uhuru, Chamwingi Mpondachuma. (Picha na Yassin Kayombo).

Mwenyekiti wa CCM kata ya Jangwani, Mohamed Bawazir (kulia) akikabidhi jezi kwa Katibu wa klabu ya michezo ya Uhuru, Rashid Zahor (kushoto), ikiwa ni sehemu ya vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh. 450,000 alivyotoa msaada kwa timu hiyo juzi katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Uhuru Publications Ltd, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo la Burudani, zilizoko barabara ya Lumumba, Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Uhuru, Chamwingi
January 21, 2014

IGP MANGU AJITAMBULISHA KWA RAIS WA ZANZIBA DKT. SHEIN LEO

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na kumkaribisha Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Elnest Mangu,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Elnest Mangu,alipofik
January 21, 2014

*MAMA SALMA KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA MAJADILIANO YA WADAU KUHUSU KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VVU KTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO

 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akifungua rasmi mkutano wa siku moja wa majadiliano ya wadau kuhusu kutokomeza maambukizi ya virusi vya ukimwi toka kwa mama kwenda kwa mtoto uliofanyika kwenye hoteli ya Serena leo mchana.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akifungua rasmi mkutano wa siku moja wa majadiliano ya wadau kuhusu kutokomeza maambukizi ya virusi vya ukimwi toka kwa mama kwenda kwa mtoto uliofanyika kwenye hoteli ya Serena.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongozanan na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid (kulia) na Mheshimiwa Mama Zakhia Meghji, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya WAMA, (kushoto), wakielekea kwenye chumba cha mkutano.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano wa siku moja wa majadiliano ya wadau kuhusu kutokomeza maambukizi ya virusi vya ukimwi toka kwa mama kwenda kwa mtoto wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi Mama Salma Kikwete (hayupo pichani). Mkutano huo ulifanyika katika hoteli ya Serena hapa Dar es Salaam.

TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF LEO

January 21, 2014
Release No. 010
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Januari 21, 2014

MZUNGUKO WA VPL KUANZA JUMAMOSI
Mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara unaanza Jumamosi (Januari 26 mwaka huu) kwa mechi tano katika miji ya Bukoba, Dar es Salaam, Tanga wakati mechi ya Tanzania Prisons na Ruvu Shooting inahamishiwa uwanja mwingine.

Ashanti United itacheza na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Coastal Union itacheza na Oljoro JKT katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Azam na Mtibwa Sugar.

Jumapili (Januari 26 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya JKT Ruvu na Mgambo Shooting itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex wakati Simba na Rhino Rangers zitaumana kwenye Uwanja wa Taifa.

MREMA CUP 2014 YAZINDULIWA

January 21, 2014
Mbunge wa Jimbo la Vunjo, Dkt. Augustino Mrema akikagua wachezaji wa klabu ya Himo na Njia panda katika mechi ya uzinduzi wa Mrema Cup 2014, uliofanyika juzi katika viwanja vya Himo, wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro. Picha na Taifa Letu.com Blog
Mbunge wa Jimbo la Vunjo, Dkt. Augustino Mrema akikabidhi jezi kwa viongozi wa vilabu 15 vitakavyoshiriki mashindano ya Mrema Cup 2014, katika hafla ya uzinduzi uliofanyika juzi katika uwanja wa Himo. Picha na Taifa Letu.com Blog
Mbunge wa Jimbo la Vunjo, Dkt. Augustino Mrema akikabidhi jezi kwa viongozi wa vilabu 15 vitakavyoshiriki mashindano ya Mrema Cup 2014, katika hafla ya uzinduzi uliofanyika juzi katika uwanja wa Himo. Picha na Taifa Letu.com Blog

DKT MREMA AMKINGIA KIFUA KIKWETE

January 21, 2014

Na Mwandishi Wetu, Moshi
 MBUNGE wa jimbo la Vunjo, Dkt Agustino Lyatonga Mrema, amewaonya  baadhi ya wanasiasa ambao  wamekuwa wakieneza siasa chafu  za  kubeza shughuli zinazofanywa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete,  kwa kushirikiana na Mbungu huyo,  katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Kauli hiyo ameitoa  juzi  wakati alipokuwa akiongea katika mkutano wake na  wananchi wa kata ya Himo- Makuyuni, wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, ambapo alisema Rais Kikwete  ameweza kufanya mambo makubwa katika jimbo hilo.


Alisema kazi ya wapinzani si kila kitu kupinga kazi ambazo zimekuwa zikifanywa na Mbunge, wanachopaswa ni kupongeza na kutoa ushauri pale ambapo wanaona kuwa hapajatekelezwa.



Dkt Mrema alisema moja ya kazi kubwa aliyoifanya Kikwete ni pamoja na kuwajengea barabara ya lami kutoka Marangu  mtoni hadi kilema Kusini yenye kilometa 5, ujenzi wa barabara ya Kwawawa hadi Nduoni Kirua vunjo yenye kilometa 10.

Dkt.Mrema na JK katika moja ya shughuli zilizokutanisha viongozi hao

Dkt Merema alisema kuwa Rais Kikwete  ameweza kusaidia  kutoa kiasi cha Shilingi milioni 150 kwa lengo la upatikanaji wa maji Safi na Salama katika  Mji wa Himo.

Aidha aliongeza kusema kuwa katika kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo ya kiuchumi pia Kikwete amewezesha masoko mawili ya Kimataifa, ambapo  soko la Lokolova litakuwa la nafaka na viwanda huku soko la Njia panda litakuwa la ndizi na mbogamboga.

CHANETA TANGA YATOA SEMINA KWA WALIMU WA MCHEZO HUO.

January 21, 2014
Na Safari Chuwa,Tanga.
CHAMA cha Mpira wa Pete Mkoa wa Tanga,(Chaneta)kimeanza kutoa semina ya walimu wa mchezo toka wilaya zote za mkoa wa Tanga lengo likiwa ni kuwaanda walimu hao kwa ajili ya kufundisha kwenye michezo ya Umitashumta na Umiseta mkoani Tanga.

Akizungumza na TANGA RAHA BLOG,katibu wa chama hicho,Julieti Mndeme alisema semina hayo ina lengo ya kuwajengea uwezo washiriki na kuhamasisha mchezo huo ambayo yanaendeshwa na mkufunzi wa toka Chama hicho Taifa Anna Kibira.

Mndeme alisema semina hiyo itaendeshwa kwa muda wa siku kumi na moja  yalianza Januari 16 na  yanatarajiwa kuhitimishwa Januari 27 mwaka huu na yanashirikisha wanawake na wanaume yakifanyika kwenye viwanja vya bandari mkoani hapa.

VISIMA TISA VILIVYOCHIMBWA WILAYANI MUHEZA MAJI YAKE YANA UBORA MZURI KWA MATUMIZI YA BINADAMU.

January 21, 2014
Na Hadija Bagasha Muheza,
MAABARA  ya kupima ubora wa maji Mkoani Tanga imesema kuwa visima tisa vya maji vilivyochimbwa katika mji mdogo wa Muheza maji yake yameonekana kuwa na ubora mzuri na kubainika kuwa yanafaa kwa matumizi ya binadamu.

Taarifa hiyo ilitolewa na Kaimu Meneja wa Maabara ya Maji mkoa wa Tanga Rukia Tuwano na kupewa nakala Mbunge wa jimbo la Muheza Herbert Mntangi.

Alisema kuwa kazi hiyo ya vipimo vya maji imegharimu shilingi 1848000 na
  kueleza kuwa uchunguzi wa ubora wa maji umefanyika na kilichogundulika ni kwamba maji kutoka katika vyanzo vyote vya visima tisa yanafaa kwamatumizi ya nyumbani.