Kampuni ya Issere Sports yazawadiwa
Naibu
Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Amos Makala ambaye kwa sasa
amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri akimkabidhi vyeti vya
utendaji bora wa huduma za michezo Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya
Issere Sports, Abbas Ally Issere katika kongamano la Wasanii
lililoandaliwa na Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA),Makala kwa sasa
amehamishiwa Wizara ya Maji kama Naibu Waziri (Picha na Mpiga Picha
Wetu).
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI
ya Issere Sports inayojishughulisha na uuzaji wa vifaa vya michezo
nchini ni miongoni mwa wanamichezo, wasanii na awaandishi wa habari
1,000 waliotunukiwa vyeti vya utendaji bora katika fani za michezo kwa
mwaka 2013 hadi 2014 katika kongamano lililofanyika ukumbi wa Lamada,
Ilala Dar es Salaam.
Katika
kongamano hilo ambalo kulitolewa mada mbili za kusaidia jamii ya
wanamichezo kujiepuka na matumkizi ya dawa za kulevya, ya pili ikiwa ya
maadili bora katika jamii, Kampuni ya Issere ni pekee iliyopata nafasi
ya kuwakilisha nyingine zinazojihusisha na uuzaji wa vifaaq vya michezo.