ASA WATEKELEZA KWA VITENDO AGIZO LA WAZIRI MKUU

December 14, 2023


WAZIRI wa Kilimo Hussein Bashe kulia akimgaia mche wa Mbegu ya Mchikichi zinazozalishwa na Shamba la Wakala wa Mbegu Asa Mkinga Mkulima wakati wa halfa ya ugawaji miche hiyo shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga
WAZIRI wa Kilimo Husein Bashe katika akionyeshwa maeneo mbalimbali yeye miche ya Michikichi kwenye Shamba la Wakala wa Mbegu Asa lililopo wilayani Mkinga wakati wa ziara yake kulia ni Mtendaji Mkuu wa Asa Sophia Kashenge na kushoto ni mkulima aliyepewa miche shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga

Waziri wa Kilimo Husein Bashe katikati akitembelea Shamba la Wakala wa Mbegu ASA wilaya ya Mkinga wakati wa ziara yake shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga kulia ni Mtendaji Mkuu wa ASA Sophia Kashenge akisisitiza jambo

Mtendaji mkuu wa wakala wa Mbegu (ASA) Sophia Kashenge kushoto akimueleza jambo Waziri wa Kilimo Husein Bashe wakati alipotembelea wakati huo kugawa miche kwa wakulima

Mtendaji mkuu wa wakala wa Mbegu (ASA) Sophia Kashenge wa pili kutoka kulia akimuonyesha kitu Waziri wa Kilimo Husein Bashe wakati wa ziara yake kwenye Shamba hilo

Waziri wa Kilimo Husein Bashe akizungumza na wakulima wa wilaya ya Mkinga wakati wa ziara yake ya kutembelea Shamba la Mwele lililopo wilayani Mkinga

Mkurugenzi Mkuu Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona akiwa na viongozi wengine wakifuatilia kwa umakini maelekezo ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe

Watumishi wa Wakala wa mbegu za kilimo nchini (ASA) katika shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga wakiwa na viongozi wengine wakimsikiliza kwa umakini Waziri wa Kilimo Husein Bashe




Na Oscar Assenga,MKINGA

WAKALA wa mbegu za kilimo nchini (ASA) katika shamba la Mwele lililopo wilaya ya Mkinga mkoani Tanga wamezindua zoezi la ugawaji wa mbegu za michikichi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu la kutaka zao hilo litumike ipasavyo kuongeza uzalishaji wa mafuta hapa nchini.

Hatua ya utekelezaji huo imekuwa na mafanikio makubwa naa kwa sasa wana michikichi elfu 88 na lengo ni kutoa michikichi laki mbili kwa wakulima ambao wataipanda katika maeneo mbalimbali na hivyo kuwezesha kilimo cha zao kuwa na tija

Akizungumza wakati akikabidhi Miche ya Michikichi kwa Wakulima wwa zao hilo lengo likiwa ni kukabidhi michikichi laki mbili katika wilaya ya Mkinga mkoani Tanga,Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alisema wananchi wanaopewa miche hiyo lazima wajaze fomu na kusaini ikiwemo kubaki na kumbukumbu ambazo zitapelekewa Halmashauri.

Alisema zitapelekwa huko ili maafisa kilimo wapewe taarifa kwenye vijiji vyao ambavyo wananchi wamepewa miche ili wawafuatilie kwa ukaribu wanapopata matatizo waone namna ya kuyapatia ufumbuzi huko huko vijijini.

Waziri Bashe alisema kwa sababu wamekuwa bahati mbaya wakigawa miche lakini mingi inaishia njiani haikui na wananchi wanapoteza muda na kuweka nguvu zao hivyo ni muhimu uwepo wa ufuatiliaji huo

“Leo tunagawa miche ya Michikichi wilaya ya Mkinga na wananchi ambao wamepewa watajaza fomu kusaini na kubaki na kumbukumbu ambazo baadae zitapelekwa Halmashauri pia maafisa Kilimo wapewa Taarufa kwenye Vijiji vyao kwa lengo la kuwa na ufuatiliaji wa karibu watakakukumbana na matatizo waweze kuyapatia ufumbuzi”Alisema

Hata hivyo Waziri huyo alisema wataanzisha mashamba makubwa ya pamoja ambao amesema miongoni mwa wafaidika watakuwa wananchi wa maeneo husika huku akisisitiza umuhimu wa maafisa kilimo wakae vijijini.

“Kama walimu wanakaa vijijini na maafisa kilimo nao wakate vijiji lakini pia mikutano ya Serikali za vijiji ifanye kazi ya kujadili maafisa Kilimo maeneo hayo kama hawatimizi wajibu wao kama hawafanyi hivyo serikali za vijiji ziandike taarifa kwenye mustasari zipelekewe kwenye WDC halafu ziende Halmshauri”Alisema

Waziri huyo alisema kwamba katikaa taarifa hiyo waeleze Afisa kilimo walionae hajawahi kuwatembelea wakulima hata siku moja kwani Serikali imegawa pikipiki na sasa wanawapa vishkambie na wamepekea vipima afya vya udongo ili wanapopima shamba wawaambie kama shamba linafaa kulima mashina au na huduma hiyo ni bure.

Katika hatua nyengine Waziri Bashe amemuagiza Mkurugenzi wa Asa Sophia Kashenge waanze shughuli za kuzalisha miche ya minazi kwenye kituo hichgo kama wanavyozalisha mice ya mazao mengine ili wananchi waweze kupata m iche ya minazi kutoka kwenye kituo hicho,

Awali akizungumza katika Mtendaji mkuu wa wakala wa Mbegu (ASA) Sophia Kashenge alisema kwa sasa wana michikichi elfu 88 na lengo ni kutoa michikichi laki mbili kwa wakulima.

Sophia alisema kwamba wamefarijika sana kuona Waziri kufika katika shamba hilo ambalo kipindi cha nyuma lilikuwa limetekelezwa lakini nguvu ya Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu imeonekana na wameweza kulifufua.

Alisema kwamba huwezi kufanya uzalishaji bila kuwa na miuondombinu ya umwagiliaji na hivyo lengo lao wataendelea kuongeza uzalishaji wa mbegu jambo ambalo ni kipaumbele cha nchi.

“Suala la Uzalishaji wa Mbegu za Michikichi ni Agizo la Waziri Mkuu tokea 2018 na sisi tumeitika vizuri tuna mashamba matatu ya ASA na la Mkinga ni la pili kwa uzalishaji wa michikichi na tunaamini kazi tunayoifanya ni kumuongezea mwananchi kipato”Alisema

Naye kwa upande wake Mkulima wa zao la Michikichi Mtarajiwa wilayani Mkinga Maaono Mkangwa alisema serikasli imechukua uamuzi mzuri kuwaletea kilimo hicho ambacho wanaamani kitawainua kiuchumi.

Mpango wa serikali ni kupunguza kiwango kikubwa cha kuingiza mafuta kutoka nje ya nchi wakati mafuta hayo yanaweza kuzalishwa na wakulima hapa nchini.

Barrick Buzwagi yakabidhi vituo 2 vya Raslimali Kilimo kwa Serikali mkoani Shinyanga

December 14, 2023

 

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme (kulia) akipokea nyaraka za umiliki na funguo za trekta kutoka kwa meneja wa Mgodi wa Barrick Buzwagi,Rebecca Stephen katika hafla ya mgodi huo kukabidhi vituo viwili viwili vya raslimali kilimo (Agricultural Resources Centres) vya mwendakulima na Mondo kwa Serikali iliyofanyika wilayani Kahama.Katikati mwenye miwani ni Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme (kulia) akionyesha nyaraka za umiliki na funguo za trekta baada ya kukabidhiwa na Meneja wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Rebecca Stephen (kushoto) katika hafla ya mgodi huo kukabidhi vituo viwili viwili vya raslimali kilimo vya mwendakulima na Mondo kwa Serikali iliyofanyika wilayani Kahama.Katikati mwenye miwani ni Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme (kushoto) na ujumbe wake, wakipata maelezo kuhusu uendeshaji wa kituo cha Mwendakulima.
Wananchi waliohudhuria hafla hiyo wakifuatilia matukio mbalimbali.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme, na Meneja wa Barrick nchini, Melkiory Ngido (wa kwanza kushoto waliokaa) katika picha ya pamoja na Wafanyakazi waandamizi wa Barrick..
Moja ya nyumba kitalu katika vituo hivyo.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme, amewataka wakulima na wafugaji wilayani Kahama, kuchangamkia fursa ya kupata mafunzo ya kuendesha shughuli zao kwenye vituo vya mafunzo ya kilimo na ufugaji ((Agricultural Resources Centres) vilivyojengwa na Barrick Buzwagi, katika eneo lao ili waweze kujikwamua kimaisha.

Mndeme, alitoa wito huo jana wakati wa hafla ya kupokea vituo viwili vya uwezeshaji Wananchi katika sekta ya kilimo na ufugaji vilivyojengwa katika kata ya Mwendakulima na Mondo, kwa Ufadhili wa Mgodi wa Barrick –Buzwagi.

Alisema vituo hivi vitawawezesha wakulima kuachana na kilimo na ufugaji wa kujikimu na badala yake watalima kilimo cha kisasa na ufugaji wenye tija huku vituo hivyo vitakuwa kitovu cha upatikanaji wa maarifa kwaajili ya kilimo na ufugaji.

’’Napenda kuchukua fursa hii kutoa pongezi na shukrani kwa Mgodi wa Barrick Buzwagi, kwa kujenga vituo hivi ambavyo vikitumika ipasavyo vitaweza kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo na ufugaji ambapo Wananchi watapata maarifa ya kuendesha kilimo cha kisasa na ufugaji wenye tija huku vituo hivyo vitakuwa kitovu cha upatikanaji wa maarifa kwa ajili ya kilimo na ufugaji.

Awali akiongea katika hafla hiyo, Meneja wa Mgodi wa Buzwagi, Rebecca Stephen, alisema kazi zilizokamilika katika vituo hivyo ni ujenzi wa majengo ya darasa,majengo ya usindikaji ,kitalu kimoja kila kituo ,kaushio la mazao ,duka la pembejeo ,Ununuzi wa mashine za kusindikia Mpunga na Alizeti ,trekta moja kila kituo na zana rahisi kila kituo Ambapo kwa vituo vyote viwili vimegharimu shilingi milioni 976.5.

Aidha Amesema tangu vituo hivi vianze kufanya kazi mafanikio mbalimbali yamepatikana ikiwa ni kuongezeka kwa mavuno ya mahindi kutoka tani 1.5 hadi tani 3.0 ,mpunga kutoka tani 2.0 hadi tani 3.0 huku kaya 4,648 zimepatiwa mafunzo ya kilimo bora kupitia mashamba darasa ya mahindi, alizeti, mpunga na mbogamboga.

Baadhi ya wakulima waliohudhuria hafla hiyo walishukuru Mgodi wa Barrick Buzwagi kwa kufungua vituo hivyo vya kuwajengea uwezo kwa kupata maarifa ya kuendesha shughuli zao za kilimo ,samnamba na kuwakabidhi miradi ya kujikwamua kimaisha.

Mgodi wa Barrick Buzwagi, ambao uko katika mchakato wa kufungwa umebuni miradi mbalimbali endelevu ya kuwawezesha wananchi wanaoishi jirani na mgodi huo kuendelea kujipatia mapato kwa lengo la kujikwamua kimaisha na kuboresha maisha yao.