MADIWANI WA HALMASHAURI YA MJI WA MAFINGA WILAYANI MUFINDI WAPIGWA MSASA NA POLICY FORUM

December 04, 2016

 Mbunge wa jimbo la Mafinga mjini Cosato Chumi alikuwa mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo.

NA FREDY MGUNDA,IRINGA


Madiwani wa halmashauri ya mji wa mafinga wilayani mufindi wameongezewa makali ya kiutendaji  na uwajibikaji na shirika lisilo la kiserikali la policy forum kutoka jiji Dar es salaam.
Akizungumza na blog hii mbunge wa jimbo la Mafinga mjini Cosato Chumi alisema kuwa mafunzo wanayopewa madiwani yanalengo la kuwaongezea uwezo wa utendaji wa kazi katika kata zao.
Aidha Chumi alisema kuwa ili kupata maendeleo ya halmashauri ya mji wa Mafinga ni lazima madiwani wawe na uelewa wa kuzishughulikia kero za wanachi na kuwa wabunifu wa kupanga mipango ya kuleta maendeleo.
“Ukiangalia madiwani wengi bado hawavijui baadhi ya vitu na kuhoji kutokana na kanuni na sheria za halmashauri hivyo nimeleta semina hii kuwaongezea uwezo madiwani wa jimbo la mafinga”.alisema Chumi
Nao baadhi ya madiwani walimshukuru mbunge wa jimbo la mafinga Cosato Chumi kwa kuwatafutia watu wa kuwapa elimu ya kiutendaji na kujua majukumu ya madiwani katika kuisimamia miradi ya halmashauri.
“Angalia tulikuwa hatujui mambo mengi na ndio chanzo tulikuwa tunamuingilia majukumu mkurugenzi kama tulikuwa tunakagua barabara za mji wa mafinga kumbe tulikuwa kinyume na utaratibu”.walisema madiwani wa mafinga
Kwa upande wake meneja uwajibikaji wa shirika lisilo la kiserikali la policy forum Richard Angelo alisema kuwa madiwani wengi wanakumbana na changamoto za kuisimamia halmashauri hivyo wameamua kuwa elimu ya kujua wajibu wao.
Hata hivyo Angelo alisema kuwa wamekuwa wakitoa elimu kwa madiwani na wabunge karibia wote lengo likwa ni kukuza uelewa na uwezo wa kuongoza maeneo wanayowaongoza.
“Hivi karibu tumetoa elimu kwa wabunge mjini Dodoma na ndipo mbunge wa jimbo la Mafinga Cosato Chumi alituomba tuje kutoa elimu kwa madiwani wa jimbo lake na ndio maana ndio tupo hapa mjini Mafinga”.alisema Angelo

MFUKO WA LAPF KWA MARA NYINGINE WAIBUKA KIDEDEA KATIKA UTUNZANI WA MAHESABU NCHINI

December 04, 2016

 Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko wa LAPF, John Kida (katikati mwenye tuzo), akiwa na wafanyakazi wenzake baada ya kutunukiwa tuzo ya Utunzaji Bora wa Mahesabu Dar es Salaam juzi. Kushoto ni Meneja Masoko na Mawasiliano wa LAPF, James Mlowe.
 Mgeni rasmi katika hafla hiyo akisoma hutuba kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Uhasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), Profesa Isaya Jairo na katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa NBAA, Pius Maneno.
 Mkurugenzi Mkuu wa NBAA, Pius Maneno (kushoto), akimpongeza Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko wa LAPF, John Kida baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi NBAA. Profesa Isaya Jairo.
 Wapiga picha za habari wakiwa tayari kwa kazi.
 Wafanyakazi wa Mfuko wa LAPF wakipita meza kuu baada ya kutunukiwa tuzo hiyo.
Washindi wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi na viongozi wa NBAA.

Na Dotto Mwaibale

MFUKO wa Pensheni wa LAPF, umetunukiwa tuzo ya kuwa kinara katika utunzaji  wa mahesabu dhidi ya mifuko mingine ya hifadhi ya jamii nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam juzi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo, Elyudi Sanga baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkurugenzi wa Fedha wa mfuko huo, John Kida, alisema kwao ni mafanikio makubwa kwa kupata tuzo hiyo.

"Tunatumia njia za kisasa ya utunzaji wa mahesabu huku tukifunga mahesabu yetu kwa wakati jambo linalotupa fursa ya kuweka sawa mambo yetu ya mahesabu" alisema Kida.

Alisema wamekuwa wakifunga mahesabu yao kwa kiwango cha kimataifa ndio maana wamekuwa wakiibuka washindi mara nyingi.

Kida alisema kuwa ushindi huo ni wa mara ya nane tangu kuanzishwa kwa utoaji wa tuzo hizo mwaka 2008.

Meneja Masoko na Mawasiliano wa LAPF, James Mlowe, alisema kuwa wanachama wao wanatakiwa kuendelea kuwa na imani na mfuko wao na kuwa fedha zao zipo kwenye mikono salama.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), Pius Maneno, alisema makampuni na taasisi 56 zilishiriki katika mashindano hayo kwa  mwaka huu ambapo waligawanywa katika makundi 12 kulingana na huduma wanazozitoa.

Alisema tuzo hizo zina lengo la kuongeza uwazi na uwajibikaji katika suala zima la mahesabu na kuhakikisha viwanago vya kimataifa vinazingatiwa katika utunzaji wa mahesabu.

Aliwataka wahasibu nchini kuandaa taarifa bora za fedha ili kuboresha hesabu za mashirika na makampuni na kuongeza uwazi katika shughuli zao.

Tuzo hizo ziliandaliwa na Bodi ya Taifa ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu (NBAA) na zilitolewa juzi katika Kituo cha Taaluma ya Uhasibu (ACP) kilichopo Bunju nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

WANAWAKE WAJASIRIAMALI MASOKONI WAMETAKIWA KUWA NA MSHIKAMANO

December 04, 2016
 Mwakilishi Mkazi wa Taasisi ya Sura Mpya na Sauti Mpya Tanzania (NFNV), Emma Kawawa (kulia), akizungumza na wanawake wafanyabiashara katika masoko ya Ilala na Temeke wakati akifunga mkutano wa kupanga na kuweka mikakati ya vikundi vya umoja na umoja wa kitaifa wa wanawake (Uwawasota) kwa mwaka 2017 uliofanyika Hoteli ya  Dreamer Buguruni jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake katika Soko la Mchikichini, Betty Mtewele (kulia), akizungumza katika ufungaji wa mkutano huo.
Ofisa Mradi na Mwanasheria wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Mussa Mlawa (kushoto), akiteta jambo na Ofisa Uwezeshaji Jamii Kiuchumi wa Shirika hilo, Theresia Jeremia .
Wanawake wajasiriamali wakiwa kwenye mkutano huo.
Ofisa Mradi na Mwanasheria wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Mussa Mlawa (kulia), Mwezeshaji sheria masokoni, Consolatha Cleophas na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake katika Soko la Mchikichini, Betty Mtewele wakifuatia kwa karibu mafunzo hayo.
Mwezeshaji wa sheria katika Soko la Temeke Sterio, Batuli Mkumbukwa akiandika changamoto na  za uendeshaji na usimamizi wa umoja kwenye masoko.
Mkutano ukiendelea.

Mkutano ukiendelea.
Makofi yakipigwa baada ya hutuba ya mgeni rasmi Emma Kawawa.
Usikivu katika mkutano huo.
Mafunzo yakiendelea,
Mgeni rasmi Emma Kawawa akifunga mafunzo hayo.

Tabasamu wakati wa mafunzo hayo.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Picha  hiyo 
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na viongozi.


Na Dotto Mwaibale

WANAWAKE Wajasiriamali nchini wametakiwa kuwa na mshikamano, uthubutu, na upendo ili kusonga mbele katika shughuli zao za kiuchumi.

Mwito huo ulitolewa na Mwakilishi Mkazi wa Taasisi ya Sura Mpya na Sauti Mpya Tanzania (NFNV), Emma Kawawa ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati akifunga mkutano wa kupanga na kuweka mikakati ya vikundi vya umoja na umoja wa kitaifa wa wanawake (Uwawasota) kwa mwaka 2017 uliofanyika Hoteli ya Dreamer Buguruni jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

"Mkitaka kusonga mbele kiuchumi kupitia ujasiriamali wenu kama wanavyo fanya wanawake wenzetu katika nchi mbalimbali duniani mnapaswa kuwa na uthubutu, kupendana, kuacha majungu, kutunza muda  na kushirikiana" alisema Kawawa.

Ofisa Mradi na Mwanasheria wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Mussa Mlawa alisema lengo la mkutano huo ni kuwakutanisha viongozi wa vikundi vya umoja wa wanawake kwenye masoko ya Manispaa  ya Ilala na Temeke ili kuweza kujadili changamoto za uendeshaji na uimarishaji wa umoja masokoni kwa mwaka 2017.

"Malengo mengine ya mkutano huu ni kutengeneza mpango kazi wa kufufua na kuimarisha umoja masokoni kwa mwaka 2017, kupeana mrejesho wa usajili wa umoja wa kitaifa (Uwawasota) na kupokea taarifa ya kamati ya uhamasishaji wa umoja kwa mwaka 2016" alisema Mlawa.

Ofisa Uwezeshaji Jamii Kiuchumi wa Shirika hilo, Theresia Jeremia alisema mkutano huo uliwahusisha wanawake wajasiriamali kutoka masoko sita ya katika manispaa za Temeke na Ilala ambayo ni Gezaulole, Tabata Muslimu, Ferry, Temeke Sterio na Mchikichini.

SERIKALI YA AWAMU YA TANO INAONGOZWA KWA NGUVU ZA MUNGU

December 04, 2016
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira pamoja na wachungaji, wakiinua mikono wakati wa ibada ya Kuliombea Taifa Kinziga, Salasala Jijini Dar es Salaam.
 Mwimbaji Alfonsina Samweli wa kanisa la Assemblies of God la Kinziga Salasala Jijini Dar es Salaam akimpa Mkono Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina, baada ya kumkabidhi kablasha lenye DVDs zenye nyimbo za Injili wakati wa ibada ya Kuliombea Taifa.
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Mhe. Luhaga Mpina akikata Utepe katika CD kuashiria kuzinduliwa kwa Abum ya Nyimbo za Injili za mwimbaji Alfonsina Samweli.
Sehemu ya waumini wa kanisa la assemblies of God la Salasala. Wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muugano na Mazingira Mhe. Luhaga  Mpina Hayupo Pichani wakati wa ibada maalumu ya kuiombea Taifa iliyofanyika Jijini Dar es Salaam. (Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)

Na Evelyn Mkokoi – Salasala DSM
NAIBU  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina amesema Serikali ya awamu ya Tano inaongozwa na Nguvu za Mungu katika kuwatumikia wananchi wake na si vinginevyo.
Pia amesema  Serikali ya awamu ya Tano kamwe haitayumbishwa wala kuyumba katika kutenda yaliyomema kwa maendeleo ya nchi  kwa kuogopa maneno ya watu ya kuwakatisha tamaa.
Akizungumza Dar es Salaam jana wakati wa Uzinduzi wa Tamasha la Kusifu  na Kuabudu na kuliombea Taifa la Kanisa la Tanzania Assemblies of God lililopo katika eneo la Kinzugi Salasala, alisema  Serikali itaendelea kusimamia misingi yake bila kuogopa maneno ya watu wanaoyoikatisha tamaa kwani Sheria na Katiba za nchi zinatokana na maneno yaliyopo  katika vitabu vya Mungu.
Alisema watumishi wa Mungu wanatakiwa kuwaombea viongozi katika kutenda kazi zao kwani uongozi waliokuwa nao ni uchaguzi kutoka kwa Mungu na sio kwa nguvu za mtu yeyote.
" Uongozi unatokana na  Mungu,Mimi Mpina sikujua kama ningekuwa Waziri nilimaliza siku mbili sikujua kama niliteuliwa kuwa Naibu Waziri kipindi hicho  nilikuwa shambani nikafatwa na kuambia kuwa nimechaguliwa ,nikasema ni uweza wa Mungu,"alisema na kuongeza kuwa
"Utawala wa awamu ya tano tunemtanguliza mbele Mungu,tunaomba muendelee kutuombea tutekeleze majukumu yetu licha ya kuwepo kwa vikwazo mbalimbali katika kutekeleza majukumu yetu,"alisema Mpina
Aidha aliziomba familia za wakristo kuwa mfano wa kuigwa katika utunzaji wa mazingira kwani bila kuwepo kwa mazingira safi magonjwa yatapata nafasi katika jamii.
"Familia za Kikristo lazima  ziwe mfano wa kuigwa katika utunzaji wa mazingira, hizi faini tunazowapiga watu kutokana na ukiukwaji wa sheria za mazingira kwa uchafuzi  wa Mazingira, sio kama tunawaonea bali kuwakumbusha wajibu wao "alisema
Kwa Upande wake,Mchungaji wa Kanisa la Assembly of God , Deusi Sabuni alisema  watahakikisha wanaendele kufanya Maombi kuiombea serikali ya awamu ya tano na viongozi wake.
Alisema roho za uadui zilizopo na watu kusema vibaya na kuwakatisha tamaa kusiwavunje mioyo kwa kusikiliza  maneno ya watu katika kuleta maendeleo ya nchi kwa manufaa ya taifahili na watu wake.
"Makanisa na Misikiti tupo pamoja nanyi katika kuwaombea na kama serikali hii ikiendelea hivi ndani ya miaka mitatu nchi yetu itabadilika,"alisema Mch.Sabuni.
Ibada maalum ya Kuliombea Taifa, kusifu pamoja na kuimba, ilienda sambamba na uzinduzi wa Ablum ya nyimbo za injili za mwimbaji Alfonsina Samweli pamoja na mnadawa kuuza DVDs zenye nyimbo za injili.