BILIONI 3.5 ZA RAIS DKT SAMIA ZILIVYOBORESHA HUDUMA ZA AFYA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA –BOMBO

September 24, 2023

 

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Dkt Naima Yusuf



Na Oscar Assenga,Tanga.


Ni ukweli usiopingika kwamba huduma za Afya ni muhimu kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya jamii katika harakati za kujiletea maendeleo na kukuza uchumi wao na Taifa kwa ujumla.

Jamii isipopata huduma nzuri za afya inaweza kushindwa kutimiza ipasavyo majukumu yake hususani katika shughuli zake za kila siku za kujiletea maendeleo na hivyo kupelekea kuwa tegemezi.

Kwa kutambua umuhimu wa jambo hilo Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ilipoingia madarakani ilianza na kufanya uwekezaji na maboresho makubwa katika Hospitali mbalimbali za Rufaa,Kanda na Taifa hapa nchini.

Uwekezaji huo umekuwa ni chachu  katika kuboresha huduma kwa watanzania waliopo katika maeneo hayo na hivyo kuwapunguzia mzigo  wa gharama ambazo awali walikuwa wakizipata kufuata huduma hizo kwenye mikoa mengine.

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo ni miongoni mwa Hospitali za Rufaa hapa nchini ambazo zimenufaika na uwekezaji mkubwa wa Bilioni 3.5 ambao umefanya na Rais Dkt Samia Suluhu hapa nchini katika kuhakikisha huduma za afya zinaimarika.

Dkt Naima Yusuf ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo anasema wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kwa uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya Afya ikiwemo uboreshaji miundombinu katika Hospitali hiyo.

Anasema kwamba Serikali imewasaidia katika mambo tofauti tofauti ikiwemo ujenzi na upanuzi wa majengo mbapo awali walikuwa wanatoa huduma  muhimu nne ambazo ni pamoja  na ya upasuaji wa kawaida ya watoto,mama na magonjwa ya ndani.

Anaeleza Serikali imewasaidia kujenga jengo la wagonjwa mahututi ,magonjwa ya dharura pamoja na kutanua sehemu ya matibabu ikiwemo ya vijana wanaotumia dawa za kulevya (Methadone) huku miradi mingine ikitarajiwa kujengwa kwenye Hospitali hiyo.

Dkt Naima anaeleza kwamba pia kuna mradi wa damu salama ambapo watakuwa wanapataa huduma ya damu salama kwenye mkoa  na hospitali ya Rufaa ambao utakuwa ni mkombozi kwa wananchi.

Anaeleza kuhusu vifaa tiba anasema Serikali awamu ya sita imewasaidia kununua vifaa tiba vingi vya uchunguzi mpaka vya kutolea matibabu ambavyo ni CT Scan ambayo imeleta huduma ya uchunguzi,vifaa vya dharura pamoja na kuweka fedha kwenye mafunzo ,ujenzi kwa ajili ya watalaamu.

“Uwekezaji huo umegharimu sh Bilioni 3.5 kwa  ujumla ambao umefanywa chini ya mwaka mmoja na hivyo huduma zimepanuka Bombo wagonjwa wengi waliokuwa wakipata rufaa sasa hivi wanapata huduma hapa hapa  hayo ni mafanikio makubwa sana”Anasema Dkt Naima

 “Tulikuwa tunatoa rufaa wagonjwa 50 mpaka 60 kwa wiki mbili lakini kwa sasa  ni chini ya rufaa 25 kwa wiki mbili hayo ni mafanikio makubwa sana na wananchi wa Tanga wanamshukuru sana Rais Dkt Samia Suluhu kwa uwekezaji huo mkubwa”Anasema Dkt Naima

Anasema wameweza kupanua huduma za uchujaji wa damu  na  huduma za watoto njiti ambao wanahudumiwa hapo hapo kwa ajili ya vifaa na kupanua huduma za dharura ambazo kwa sasa zimeimarika.

Hata hivyo anasema wameweza pia kupanua huduma ya mkojo kutokana na kwamba unapofikia uzee wapo wanaopata shida ya tezi dume huduma sasa inapatikana ikiwemo zile za macho,pua koo na masikio na meno na huduma mahututi.

“Nikisema huduma za mahututi na dharura tumeweza kufufua wagonjwa waliokuja bila mapigo ya moyo kama watano ambayo hiyo ingekuwa haiwezekani bila kuwa na vifaa tiba msaada huo ambao tumesaidiwa na Serikali utusaidia kufanikisha hayo”anasema

Kuhusu Ajira. Dkt Naima anaendelea  kuishukuru Serikali ya awamu sita kwenye kuwasaidia kuwapelekea waajiriwa wapya 50  kutokana na kwamba hiyo imesaidia kuleta huduma kwenye maeneo walioyapanua kuwa na madaktari ,manesi pamojà na wataalumu katika kada mbalimbali.

“Nakumbuka nilivyoanza hapa Hospitali ya Rufaa ya Bombo mwaka 2008 Bombo kulikuwa na madaktari bingwa chini ya 11 na waliokuwa wanatoa huduma walikuwa wanne tu leo tuna madaktari bingwa 21 kwa kweli ni hii ni pongezi kubwa sana kwake Rais Dkt Samia Suluhu na Waziri wetu wa Afya Ummy Mwalumu”alisema Dkt Naima

Alisema leo wameona umuhimu wa kuwapeleka madaktari na wameweka bajeti ya kuwaongeze ujuzi  madaktari bingwa watano kufikia kwenye Ubingwa Bobezi wanasubiri bajeti ikipita waende kwenye mafunzo na warudi kutoa huduma hapo.

Kuhusu upatikanaji wa Dawa

Dkt Naima anasema kuhusu suala la upatikanaji wa dawa wameongezewa bajeti ya kununua dawa na mfumo wa upatikanaji wa dawa umekuwa mzuri mwanzoni walikuwa wanapata shida kutoka MSD .

Alisema kwa maana dawa nyingi zilikuwa hazipatikana lakini sasa hivi alikuwa amekaa na Meneja MSD  na wameona ongezeko lilivyokuwa sasa hivi imefikia asilimia 57 na dawa nyingi watapa MSD na mlolongo wa upatikjaji wa dawa utapungua.

Hata hivyo Dkt Naima anasema hospitali hiyo inatambua kuwa na madaktari bingwa 21 sio sahihi kubaki tu Hospitalini kuna wananchi wengi wanashindwa kuja hospitaklini Tanga kutokana na umbali wa maeneo ya wilayani hivyo kwakutambua hilo wanakwenda kutoa huduma kwenye hospitali hizo ikiwemo kuwafundisha wataalamu walipo kwa hiyo kwa mwaka wanafanya mara nne na wanajaribu kwenda wilaya zote za Tanga.

Anaeleza kwamba Bombo Hospitali ni miongoni mwa Hospitali za Rufaa 28 nchini ambapo kwa sasa wanajivunia kwenye umahiri wa Plastic Surgery mradi ambao ulianza 2011 kuna madatari wanatoka nchini Ujerumaani kwenye hospitali yao na kufika kwenye Hospitali hiyo ya Bombo wanafanya kliniki za ubobezi za Plastic Surgery.

Anasema hiyo imesaidia watu wengi hapa nchini ambao wakati wa kliniki hizo wamekwa wakijitokeza kupata huduma hiyo na  wamechukua hatua baada ya Waziri kuona kuna umihumu wa kuendelea nayo hapa  hivyo wameanzisha Programu ya  Plastic Surgery unaitwa Tazzy Plastic ambao utakuwa unatoa huduma ndani ya Hospitali.

Dkt Naima anasema huduma hiyo itakwenda sambamba na  kuanzisha program ya kufundisha madaktari ili kuweza kupata madaktari bobezi katika eneo hilo na madaktari wawili wanakwenda kusoma wapo na ushirikiana na Muhas na Muhimbili na watakachokifanya ni  kufanya eneo la Umahiri katika Urekebishaji Viungo(Plastic Surgery) hapa nchini .

Anasema unapoongelea urekebishaji wa viungo sio ya kufanya mtu awe mrembo ila ni watu waliozaliwa mfano mdomo au pua haijaka vizuri au walioungua na mikono yao haijakaa vizuri wanachofanya wanamuweka vizuri ili waweze kufanya kazi kama kawaida na kuirudisha ngozi na kufanya kidonda kukaa vizuri kwa hiyo ni huduma kama hizo.


DKT.BITEKO AANZA ZIARA YA KIKAZI BUKOMBE MKOANI GEITA

September 24, 2023

 --APATA MAPOKEZI MAKUBWA YA WANANCHI


---AAGIZA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA ZA SERIKALI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Dkt. Doto Biteko ameanza ziara ya kikazi katika jimbo hilo lililoko mkoani Geita ikiwa ni ziara ya kwanza kufanyika  kutoka ateuliwe na kuapishwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati.

Mara baada ya kuwasili katika Jimbo hilo tarehe 24 Septemba, 2023, Dkt.Biteko alipokelewa na wananchi wa Jimbo hilo pamoja na viongozi mbalimbali katika Wilaya Bukombe na Mkoa wa Geita.

Akizugumza  katika Mkutano wa hadhara, Dkt.Biteko amemshukuru Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kuona kuwa anaweza kumsaidia katika majukumu aliyokabidhiwa na kuahidi kuwa, atatekeleza majukumu yake kwa ufanisi katika kuwatumikia wananchi ili kuitendea haki imani iliyooneshwa kwake.

Amesema kuwa, chini ya uongozi wa Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan kila kitu kilichopangwa kufanyika  kinaendelea kufanyika kutokana fedha anazotoa katika  miradi ya sekta mbalimbali ikiwemo mradi wa umeme wa Julius Nyerere (MW 2115), ujenzi wa Daraja wa Busisi, ununuzi wa ndege, madarasa, vituo vya afya, utalii n.k.

Kutokana na hilo, Dkt. Biteko amewataka watendaji na watumishi nchini kusimamia matumizi sahihi ya fedha za Serikali kwani fedha hizo ndizo zinategemewa na watanzania katika kuwaletea maendeleo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, viongozi wa Mkoa wa Geita wamemshukuru Rais,  Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini Dkt.Doto Biteko katika nafasi hiyo kubwa na adhimu na kwamba wana imani kuwa ataitendea haki nafasi hiyo kutokana na historia yake ya uchapakazi na uadilifu.

Viongozi hao wakiwemo Wabunge na Wakuu wa Wilaya katika Mkoa wa Geita wamemshukuru Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara wilayani Chato, ujenzi wa Chuo cha VETA wilayani Nyang'hwale na upelekaji umeme vijijini katika vijiji vya Mkoa huo.

Kwa upande wake, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesifu juhudi zilizofanywa na Dkt.Biteko wakati akihudumu kama Waziri wa Madini  na kueleza kuwa amesaidia kuinua mchango sekta ya madini katika uchumi wa nchi na ameahidi kuwa ataendeleza misingi hiyo mizuri ikiwemo ya kufanya utafiti wa madini katika eneo lote la nchi ili wachimbaji wachimbe madini kwa uhakika na hivyo kuongeza mapato ya nchi.

Aidha, ameendelea kusisitiza kuwa, hatalifanyia mzaha suala la utoroshaji wa  madini nchini na kwamba wote watakaotorosha madini watachukuliwa hatua za kisheria kwani wanakosesha nchi mapato.

kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela amemshukuru Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo na huduma za kijamii ikiwemo shule, hospitali na umeme katika Mkoa Geita.