Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Dkt Naima Yusuf
Na Oscar Assenga,Tanga.
Jamii isipopata huduma nzuri za afya inaweza kushindwa kutimiza ipasavyo majukumu yake hususani katika shughuli zake za kila siku za kujiletea maendeleo na hivyo kupelekea kuwa tegemezi.
Kwa kutambua umuhimu wa jambo hilo Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ilipoingia madarakani ilianza na kufanya uwekezaji na maboresho makubwa katika Hospitali mbalimbali za Rufaa,Kanda na Taifa hapa nchini.
Uwekezaji huo umekuwa ni chachu katika kuboresha huduma kwa watanzania waliopo katika maeneo hayo na hivyo kuwapunguzia mzigo wa gharama ambazo awali walikuwa wakizipata kufuata huduma hizo kwenye mikoa mengine.
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo ni miongoni mwa Hospitali za Rufaa hapa nchini ambazo zimenufaika na uwekezaji mkubwa wa Bilioni 3.5 ambao umefanya na Rais Dkt Samia Suluhu hapa nchini katika kuhakikisha huduma za afya zinaimarika.
Anasema kwamba Serikali imewasaidia katika mambo tofauti tofauti ikiwemo ujenzi na upanuzi wa majengo mbapo awali walikuwa wanatoa huduma muhimu nne ambazo ni pamoja na ya upasuaji wa kawaida ya watoto,mama na magonjwa ya ndani.
Anaeleza Serikali imewasaidia kujenga jengo la wagonjwa mahututi ,magonjwa ya dharura pamoja na kutanua sehemu ya matibabu ikiwemo ya vijana wanaotumia dawa za kulevya (Methadone) huku miradi mingine ikitarajiwa kujengwa kwenye Hospitali hiyo.
“Nakumbuka nilivyoanza hapa Hospitali ya Rufaa ya Bombo mwaka 2008 Bombo kulikuwa na madaktari bingwa chini ya 11 na waliokuwa wanatoa huduma walikuwa wanne tu leo tuna madaktari bingwa 21 kwa kweli ni hii ni pongezi kubwa sana kwake Rais Dkt Samia Suluhu na Waziri wetu wa Afya Ummy Mwalumu”alisema Dkt Naima
Alisema leo wameona umuhimu wa kuwapeleka madaktari na wameweka bajeti ya kuwaongeze ujuzi madaktari bingwa watano kufikia kwenye Ubingwa Bobezi wanasubiri bajeti ikipita waende kwenye mafunzo na warudi kutoa huduma hapo.
Kuhusu upatikanaji wa Dawa
Dkt Naima anasema kuhusu suala la upatikanaji wa dawa wameongezewa bajeti ya kununua dawa na mfumo wa upatikanaji wa dawa umekuwa mzuri mwanzoni walikuwa wanapata shida kutoka MSD .
Alisema kwa maana dawa nyingi zilikuwa hazipatikana lakini sasa hivi alikuwa amekaa na Meneja MSD na wameona ongezeko lilivyokuwa sasa hivi imefikia asilimia 57 na dawa nyingi watapa MSD na mlolongo wa upatikjaji wa dawa utapungua.
Hata hivyo Dkt Naima anasema hospitali hiyo inatambua kuwa na madaktari bingwa 21 sio sahihi kubaki tu Hospitalini kuna wananchi wengi wanashindwa kuja hospitaklini Tanga kutokana na umbali wa maeneo ya wilayani hivyo kwakutambua hilo wanakwenda kutoa huduma kwenye hospitali hizo ikiwemo kuwafundisha wataalamu walipo kwa hiyo kwa mwaka wanafanya mara nne na wanajaribu kwenda wilaya zote za Tanga.
Anaeleza kwamba Bombo Hospitali ni miongoni mwa Hospitali za Rufaa 28 nchini ambapo kwa sasa wanajivunia kwenye umahiri wa Plastic Surgery mradi ambao ulianza 2011 kuna madatari wanatoka nchini Ujerumaani kwenye hospitali yao na kufika kwenye Hospitali hiyo ya Bombo wanafanya kliniki za ubobezi za Plastic Surgery.
Anasema hiyo imesaidia watu wengi hapa nchini ambao wakati wa kliniki hizo wamekwa wakijitokeza kupata huduma hiyo na wamechukua hatua baada ya Waziri kuona kuna umihumu wa kuendelea nayo hapa hivyo wameanzisha Programu ya Plastic Surgery unaitwa Tazzy Plastic ambao utakuwa unatoa huduma ndani ya Hospitali.
Dkt Naima anasema huduma hiyo itakwenda sambamba na kuanzisha program ya kufundisha madaktari ili kuweza kupata madaktari bobezi katika eneo hilo na madaktari wawili wanakwenda kusoma wapo na ushirikiana na Muhas na Muhimbili na watakachokifanya ni kufanya eneo la Umahiri katika Urekebishaji Viungo(Plastic Surgery) hapa nchini .
Anasema unapoongelea urekebishaji wa viungo sio ya kufanya mtu awe mrembo ila ni watu waliozaliwa mfano mdomo au pua haijaka vizuri au walioungua na mikono yao haijakaa vizuri wanachofanya wanamuweka vizuri ili waweze kufanya kazi kama kawaida na kuirudisha ngozi na kufanya kidonda kukaa vizuri kwa hiyo ni huduma kama hizo.