UBA TANZANIA STAFF STAYING HEALTHY

UBA TANZANIA STAFF STAYING HEALTHY

September 22, 2015
IMG-20150919-WA068
UBA Tanzania staff during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015.
IMG_0311
UBA Tanzania staffs participate in the aerobics session during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015
IMG_0330
UBA Tanzania staffs participate in the aerobics session during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015.
IMG_0358
A cross section of UBA Tanzania staff in a group photo after the exercises during the jogging to bond event which took place on Saturday September 19, 2015.

NJOO TUSHEHEREKEE PAMOJA KWENYE MKESHA WA EID NA SKYLIGHT BAND LEO NDANI YA KIOTA CHA ESCAPE ONE MIKOCHENI

September 22, 2015
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower( kushoto) akiendelea kutoa burudani ya nguvu huku msanii mwenzake Sony Masamba akiendelea kuzirundi ngoma ndani ya kiota cha Escape One, Mikocheni jijini Dar. Usikose leo siku ya Jumatano kwenye mkesha wa EID maana kuna vitu vingi vipya.
Mwimbaji wa Bendi ya Skylight, Natasha pamoja na mwenzake Kasongo Junior haya ni Majembe mapya ya bend ya Skylight yenye uwezo mkubwa wa katika uimbaji.
Sony Masamba ambaye ni mmoja wa waimbaji wa Skylight akiendelea kutoa burudani akisindikizwa na waimbaji wenzake.
Sam Mapenzi pamoja (kulia) akiimba pamoja na Ashura Kitenge wakiendelea kuwakonga nyoyo mashabiki wa Skylight Band waliofika siku ya Jumapili kwenye kiota cha Escape One Mikocheni na leo sio ya kukosa njoo tukeshe pamoja tukifurahi na mziki mzuri kutoka katika bendi hiyo.
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower  akiimba huku mashabiki wa bendi hiyo wakiserebuka kwa furaha na leo sio ya kukosa njoo na mwenzako uje kuona vitu vipya kutka kwenye bendi hiyo.
Mwimbaji wa Bendi ya Skylight, Natasha akiendelea kutuoa burudani kwa mashabiki wao waliofika kwenye kiwanja cha Escape One kujionea burudani ya nguvu kutoka katika bendi hiyo.
Msanii wa Bendi ya Skylight, Sony Masamba akiwafundisha mashabiki wao style mpya ya kucheza nyimbo za Bendi ya Skylight.
Rapa mkongwe kwenye muziki wa Live Joniko Flower akishusha mistari na kucheza huku waimbaji wenzake Sony Masamba (katikati) pamoja na Sam Mapenzi wakisebeneka Jumapili iliyopita katika kiota cha Escape One, Mikocheni jijini Dar.
Msanii wa Bendi ya Skylight  Ashura Kitenge akiimba kwa hisia kali mbele ya mashabiki i wa bendi hiyo(hawapo pichani) waliofika kwenye kiota cha Escape One, Mikocheni jijini Dar kwa kuburudika na band hii.
Ilifika time ya Nigeria Flavour Sam Mapenzi akitoa burudani huku akisindikizwa na wanamziki wenzake waliokuwa wakimpa support ya nguvu kwenye ngoma za Nigeria ambao ni Joniko Flower (wa kwanza kushoto), Ashura Kitenge(wa pili kutoka kushoto) pamoja na Sony Masamba.
Ilikuwa noma sana siku ya Jumapili iliyopita maana ilikuwa sio ya kupitwa basi mchuke na ndugu, jamaa au rafiki yako leo Jumatano kwenye mkesha wa EID uje kuona vitu vitamu kutoka kwenye Bendi ya Skylight ndani ya kiota cha Escape One, Mikocheni jijini Dar.
Waimbaji wa Skylight Band wakiendelea kutoa burudani ya kukata na shoka
Skylight Band ni mwendo wa kutoa raha sana tukutane jumatano hii ndani ya kiota cha Escape One, Mikocheni jijini Dar kwa kuburudika na band hii.
Mashabiki wa Bend ya Skylight wakiendelea kuserebuka na waimbaji wa bendi hiyo.
Sakata rhumba na Skylight band hapana chezea hatareee ukigusa lazima unase leo kwenye mkesha wa EID njoo wewe na rafiki yako
Mashabiki wakiendelea kuserebuka nyimbo za Skylight.

Bi. Samia Suluhu Amnadi Dk. Magufuli Wilaya za Korogwe na Lushoto

September 22, 2015

Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo mjini Korogwe, Mkoa wa Tanga.
Mgombea mwenza nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wasanii na wananchi wengine alipokuwa akiwasili katika viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi leo Mjini Korogwe ambapo alifanya mkutano wa kampeni.
Mgombea mwenza nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu Hassan (kulia) akiwapokea baadhi ya wanachama wapya waliojiunga na CCM katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo Korogwe. Jumla ya wanachama 25 walijiunga na CCM katika mkutano huo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo mjini Korogwe, Mkoa wa Tanga.
Baadhi ya wasanii waigizaji, Wema Sepetu (kulia) na Bibi Mwenda wakizungumza na WanaCCM na wananchi katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza kuwashawishi waichague CCM kutokana na mazuri mengi iliyowafanyia wasanii.
Mgombea mwenza nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu Hassan (kulia) akimtambulisha na kumuombea kura mgombea ubunge wa Jimbo la Bumbuli, January Makamba (katikati) katika mkutano wa hadhara wa kampeni wa mgombea mwenza uliofanyika Lushoto Jimbo la Mlalo. Kulia ni mgombea wa ubunge Jimbo la Lushoto, Shaban Shekilindi.
Mgombea Ubunge Jimbo la Korogwe Mjini, Mary Pius Chatanda akizungumza na wanaCCM na wananchi wa jimbo hilo walipojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza leo viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi.

Mgombea Ubunge Jimbo la Korogwe Mjini, Mary Pius Chatanda akizungumza na wanaCCM na wananchi wa jimbo hilo walipojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza leo viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi kunadi sera za CCM, huku mgongoni akiwa amebandika kipeperushi cha mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Profesa 'Maji Marefu' akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara wa kampeni za mgombea mwenza uliofanyika Korogwe Mjini leo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo mjini Korogwe, Mkoa wa Tanga.

Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya Kwagunda, Salehe Abdullah (kushoto) akizungumza mara baada ya kujiunga na CCM leo kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza na kukikimbia chama chake cha CHADEMA.
Mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wanaCCM na wananchi wa jimbo la Korongwe Mjini walipojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea huyo leo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi.
Baadhi ya wananchi wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Mombo ili asikilize kilio na changamoto zao kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Baadhi ya wananchi wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Mombo ili asikilize kilio na changamoto zao kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Sehemu ya wananchi  na wanaCCM wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Soko la Soni Lushoto ili asikilize kilio na changamoto zao hasa akinamama kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza mgombea mwenza huku wakiendelea na biashara zao sokoni hapo.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza mgombea mwenza huku wakiendelea na biashara zao sokoni hapo.
Sehemu ya wananchi  na wanaCCM wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Soko la Soni Lushoto ili asikilize kilio na changamoto zao hasa akinamama kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Mgombea ubunge wa Jimbo la Bumbuli, January Makamba (kushoto) akibadilishana jambo na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Lushoto, Balozi Abdul Mshangama leo katika Jimbo la Mlalo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo katika Jimbo la Mlalo, Lushoto.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mlalo, Shaban Omar Shekilindi akizungumza na wapiga kura wake jimboni Mlalo.
Mgombea ubunge Jimbo la Bumbuli, January Makamba akizungumza na umati katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza, Makamba akizungumza aliwaomba wananchi wasikipe kura chama cha Chadema na ushilika wao wa UKAWA kwani wapo kwa ajili ya mabadiliko ya nafsi zao na si vinginevyo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo katika Jimbo la Mlalo, Lushoto.
Mgombea mwenza, Bi. Samia Suluhu (katikati) akimtambulisha mgombea ubunge wa Jimbo la Lushoto, Shaban Shekilindi.
Mgombea mwenza, Bi. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akimtambulisha Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mlalo, Shaban Omar Shekilindi alipokuwa akizungumza na wapiga kura wake jimboni Mlalo.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com



___________________________________________________________________________________ Joachim Mushi, Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mhariri Mkuu wa Thehabari.com. Mail address:- mushi@thehabari.com/ jomushi79@yahoo.com/ info@thehabari.com Mobile:- 0717 030066 / 0756 469470 Web:- www.thehabari.com http://joemushi.blogspot.com

MAGUFULI AMALIZANA NA KAMPENI ZAKE KAGERA,KESHO KUUNGURUMA MKOANI GEITA.

September 22, 2015

 Wananchi wa mji wa Ngara na vitongoji vyake wakiwa wamefurika kwenye viwanja vya posta mjini humo,huku wakishangilia wakati Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi mbele yao na kuwaomba ridhaa ya kuwa Rais na kuiongoza nchi Tanzania katika awamu ya tano.Dkt Magufuli amekamilisha mikutano yake ya kampeni zake katika mkoa wa Kagera wenye jumla ya majimbo 9 ya Uchaguzi. PICHA NA MICHUZI JR-KAGERA
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika viwanja vya Posta,wilayani Ngara jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.Dkt Maguful kwa siku mbili mfululizo ameweza kukamilisha mikutano yake kwenye Wilaya  zote za Mkoa wa Kagera,ambapo kesho anaelekea mkoani Geita kwa ajili ya kujinadi kwa wananchi wa mkoa huo ili waweze kumpigia ya kuwa Rais wa awamu ya tano,katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwafafanulia kwa umakini mkubwa alipokuwa akiwahutubia wananchi katika uwanja wa shule ya sekondari Rumanyika,wilayani Kyerwa mapema leo mchana mkoani Kagera kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
 Sehemu ya umati wa watu ulikuwa umefika kwenye mkutano wa kampeni wa Dkt Magufuli uliofanyika mapema leo mchana kwenye uwanja wa shule ya sekondari Rumanyika,wilayani Kyera mkoani Kagera.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika uwanja wa shule ya sekondari Rumanyika,wilayani Kyerwa mapema leo mchana mkoani Kagera kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
 Wakazi wa Ngara na vitongoji vyale waliokusanyika kwenye viwanja vya Posta mjini Ngara jioni ya leo wakishangilia jambo,wakati Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi mbele yao kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
   Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika viwanja vya Posta,wilayani Ngara jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
 Wananchi wa Ngara wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano huo wa kampeni
  Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akisisitiza jambo alipokuwa akiwahutubia wananchi katika viwanja vya Posta,wilayani Ngara jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika viwanja vya Kayanga,Karagwe mjini asubuhi hii kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
   Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi katika viwanja vya Mashujaa mjini Misenyi asubuhi hi kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni
 wakazi wa mji wa Misenyi  katika viwanja vya mashujaa wakishangilia huku wakiendelea kumsikiliza mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,alipokuwa akijinadi kwa kumwaga sera zake na kuomba watanzania wamchague kwa ridhaa yao ili awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa awamu ya Tano