MAPOKEZI YA LOWASSA MJINI TARIME

October 11, 2015


Vijana wa Mjini Tarime wakiongoza mapokezi ya Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, alipowasili mjini Tarime kwa Mkutano wa Kampeni, leo Oktoba 10, 2015.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia
mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Tarime
katika Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime
Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015. 
Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye, akiwasalimia wananchi wa Mji wa Tarime waliokuwa wamefurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015. 
Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara, Mh. Vicent Nyerere, akizungumza wakati wa Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia
mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa
, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime
Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tarime Vijijini kupitia CHADEMA, Mh. John Heche, akihutubia wananchi wakati wa Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia
mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa
, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime
Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tarime Mjini kupitia CHADEMA, Mh. Ester Matiko akihutubia wananchi wakati wa Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia
mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa
, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime
Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015
Sehemu ya wananchi wa Mji wa Tarime, walioshiriki Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015.

Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akiwapungia wananchi wa Mji wa Tarime Mkoani Mara.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa na Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye, wakiwa pamoja na Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara, Mh. Vicent Nyerere, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Mh. Ester Matimo pamoja na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, Mh. John Heche, wakati wa Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, asikiliza jambo kutoka kwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Mh. Ester Matimo, wakati wa Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Tarime katika Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Sabasaba, Tarime Mjini, Mkoani Mara leo Oktoba 10, 2015.

KENYA-TANZANIA BUSINESS FORUM ON OCTOBER 6, 2015 IN NAIROBI, KENYA IN PICTURES

October 11, 2015

 Executive Director of Tanzania Investment Centre Ms. Juliet Kairuki welcomes the President of Republic of Kenya H.E. Uhuru Kenyatta to the Forum
 President of the Republic of Kenya  H.E. Uhuru Kenyatta arrives at the venue of the Kenya-Tanzania Business Forum. He is escorted by Kenyan Minister of Industrialization and Enterprise Development
 Kenyan Minister of Industrialization and Enterprise Development and Managing Director of Intercontinental Hotel, Nairobi welcome the President of the United Republic of Tanzania
 Ms Juliet Kairuki , CEO of Tanzania Investment Centre welcomes President of the United Republic of Tanzania HE. Dr Jakaya  Kikwete
 Their Excellencies Dr. Jakaya Kikwete and Uhuru Kenyatta enter the conference room
Permanent Secretary Ministry of Industry and Trade Mr Uledi Musa deliver his remarks
 The two Presidents stand at attention as Nationa Anthems are played
 President Jakaya Kikwete delivers his keynote address during the forum
 Godfrey Simbeye (CEO of the Tanzania Private Sector Foundation) extends a hand  to the Managing Director of Kenya Investment Authority Dr . Moses Ikiara
 From left, Juliet Kairuki CEO of Tanzania Investment Centre; Mr. Godfrey Simbeye (CEO of Tanzania Private Sector Foundation) and Dr Moses Ikiara (CEO of Kenya Investment Authority-Keninvest) take timr off for a souvenir photo during the forum
 CEO of Kenya Association of Manufacturers ( in red) Ms Phyllis Wakiaga and other delegates await the arrival of the Kenya and Tanzania Presidents at the forum. 


 Senior members of the Tanzanian delegation at the forum  
 Kenya Police Brass band play  the National Anthems during the business forum. They are also famous for playing Tanzanian top hits like Diamond's "You are my number one" to the surprise of many a Tanzanian listening to them
 Prominent Kenyan business moguls including  Great  Chris Kirubi the richest  business magnet in Kenya owning  virtually most of the companies in HACO industries, and Kenya Airways shareholder engage President Kikwete post delivery of his key note address
 Mr Geodfrey Simbeye Simbeye (CEO of TPSF) greets the President  of Kenya H.E. Uhuru Kenyatta in Nairobi
 Ms. Juliet Kairuki with the Permanent Secretary, Ministry of Trade and Industry from Tanzania Mr. Musa Uledi
 TIC’ EXD listens attentively to speech of the CEO of Kenya Investment Authority
 Kenyan investor seeks clarity on some issues from Executive Director of Tanzania Investment Centre.
Mrs Juliet Kairuki addressing the audience

BENKI YA DUNIA NA JAPAN (JICA) KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NCHINI TANZANIA

October 11, 2015

  Katibu Mkuu Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile katika majadiliano na Bw. Hiroshi Kato ambaye ni Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo ya Japan (JICA).
 Baadhi ya Ujumbe wa Tanzania na Ujumbe wa Japan wakiwa kwenye majadiliano. Katikati ni Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile, kushoto kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Zanzibar Bw. Khamis Mussa na Kamishna wa Fedha za Nje Bw. Said Magonya na kulia kwake ni Rais wa JICA Bw. Hiroshi Kato. Katibu Mkuu Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali.
 Katibu Mkuu Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile wa kwanza kulia akiendelea  kufanya majadiliano na ujumbe wa JICA ukiongozwa na Rais wa JICA Bw.  Hiroshi Kato wa pili kulia.
Ujumbe wa Tanzania na Ujumbe wa JICA wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile wakati wa majadiliano ya kuwekeza katika sekta ya umeme, utalii na kuboresha mazingira ya biashara.

JAPANI YAKUBALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KATIKA KUCHANGIA BAJETI YA MAENDELEO KATIKA MIKUTANO YA WB & IMF  HAPA NCHINI  PERU - LIMA

Serikali ya Jumhuri ya Muungano wa Tanzania yapata dola milioni 280 kutoka Benki ya Dunia na Japani, fedha hizo zitatumika kusaidia mipango mbalimbali nchini Tanzania. Akiongea  na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia ukanda wa Afrika Bw. Makhtar Diop na Rais wa Shirika la Maendeleo ya Japan-JICA Bw. Hiroshi Kuto, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius  Likwelile alisema dola milioni 230 zimetolewa na Benki ya Dunia. Kiasi cha  Dola milioni 100 ni kwa ajili ya kuhimiza mambo ya uwazi katika utawala, dola milioni 80 ni kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara na dola milioni 50 ni kwa ajili ya kuboresha sekta ya hifadhi ya jamii yaani  pensheni.

Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) wamethibitisha kuendelea kuunga  mkono Serikali ya Tanzania  katika mipango ya maendeleo. Wakiwa katika kikao na ujumbe kutoka Tanzania, Bw. Hiroshi Kato ambaye ni Makamu wa Rais wa shirika hilo alisema  kuwa , Serikali ya Japan kupitia shirika lao la maendeleo ( JICA) lina mipango ya kuunga mkono Tanzania   na Kenya watajenga barabara ambayo itaunganisha  Arusha na Mombasa kwa kiwango cha juu ili kuweza kurahisisha mazingira ya biashara na utalii. Bw. Kato katika mazungumzo yake aliongeza kuwa bado wao wako tayari kusaidia kupitia bajeti kuu ya Serikali kama vile ambavyo wamekuwa wakifanya  miaka ya  nyuma.

Akifafanua kuhusiana na sekta ya hifadhi ya jamii Dkt. Likwelile alisema kuwa uboreshaji wa pension umeahirishwa kwa sasa na wameomba Shirika la kazi la Kimataifa (ILO) wafanye mapitio ya sekta hiyo na baada ya mapitio hayo ndio tutajua ni masuala gani tunaweza kuyazingatia ili kuboresha sekta yetu ya hifadhi ya jamii.

Katika majadiliano na viongozi wa benki ya Dunia  Dkt. Lilkwelile aliwaeleza kuwa, Tanzania kuna changamoto kubwa kwasababu uzalishaji wa umeme kupitia maji umepungua kutokana na kina cha maji kupungua katika maeneo ya uzalishaji hivyo tunategemea gesi.

“Tunategemea gesi ya Kinyerezi One ambayo inatupatia megawatts 405-407, na vilevile tunapata umeme kutokana na matumizi ya mafuta ambapo ni gharama kubwa na uzalishaji haujafikia lengo ambalo ni mahitaji yetu ya siku ambayo tunapata. Tuna mapungufu ya megawatts160, suala hili limeleta shida sana  kwenye bajeti yetu”. Alisisitiza Likwelile

Benki ya Dunia watashirikiana na Idara ya Serikali ya Uingereza ya maendeleo ya Kimataifa (DFID) pamoja na Japan kuwekeza katika reli ya kati ili kuunga mkono jitihada zetu za kuboresha huduma ya reli nchini Tanzania, Likwelile aliendelea kufafanua.

Kwa upande wa maendeleo ya uchumi wa Tanzania ni kwamba uchumi bado unakuwa kati ya asilimia 6.5 mpaka 7, mfumuko wa bei umeshuka japokuwa unapanda kidogo kufikia asilimia 6.4, akiba ya fedha za kigeni bado inawezesha Tanzania kuingiza bidhaa za karibu miezi minne, aliongeza Dkt. Likwelile.

Katika majadiliano hayo Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Afrika Bw. Diop alisisitiza kuwa Tanzania iweke msisitizo mkubwa kwenye kilimo chenye tija na cha kibiashara pamoja  na kuwekeza kwenye miundombinu ambayo itasaidia uchumi kuimarika hasa kwenye nishati, reli, barabara, mawasiliano pamoja na kuwekeza kwa vijana  kwani ni wengi sana na  wanahitaji uhakika wa kupata ajira. Tukiweza kufanya kilimo kikawa cha tija na kuwekeza kwenye viwanda vidogovidogo na kuwapa vijana elimu ambayo itawasaidia kuweza kujitegemea, Tanzania itaweza kusonga mbela.

Akiendelea kufafanua Bw. Diop alisema, kutokana na uchumi wa Tanzania ulivyo hakuna sababu ya kukusanya mapato yetu ya kodi kwa kiwango cha sasa, tuna uwezo wa kwenda hadi asilimia 12 ya pato la Taifa. Naye Dkt. Likwelile alimuhakikishia Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Afrika Bw. Diop kuwa lengo la Tanzania ni hili ila tunahitaji uwekezaji ili tuweze kufikia lengo tuulilokusudia,  maana tumeweka ukomo wa fedha angalau tufikie mpaka asilimia14.5 lakini tunaweza kwenda mpaka asilimia 17 – 20 katika miaka mitatu ijayo.

Katika kuhitimisha majadiliano hayo Dkt. Likwelile alisema kwamba ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya Dunia ni mzuri na mkubwa sana. Kiwango cha fedha ambacho tunakipata kutoka kwao kinazidi kuongezeka na wameweza kuturuhusu kuwekeza kutumia mlango  mwingine mfano kwenye Chama cha Maendeleo ya Kimataifa(IDA) na pia kwa sasa tumeweza kupata fedha kupitia Benki ya Kimataifa ya ujenzi na maendeleo(IBRD) kwa ajili ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam.
Hali ya hewa mjini hapa ni baridi sana.
Imetolewa na: Bi. Ingiahedi Mduma
     Msemaji wa Wizara ya Fedha
                                                                    Peru – Lima

NSSF YASHIRIKI MAONYESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA ABITAT JIJINI DAR ES SALAAM

October 11, 2015

Ofisa Uwekezaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mselem Mwanamsoga akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, Edward Sungura (kulia), wakati wa Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa yaliyoandaliwa na Umoja wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki (Abitat), yanayoendelea katika Ukumbi wa Diamond Jubilee. (Picha na Francis Dande).
 Ofisa Masoko na Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Aisha Sango (wa pili kulia), na Ofisa Uwekezaji wa NSSF, Mselem Mwanamsoga wakitoa maelezo kuhusu huduma wanazotoa, ikiwemo uuzwaji wa viwanja vilivyopimwa katika eneo la Kiluvya, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, kwa watu waliofika katika Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa yaliyoandaliwa na Umoja wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki (Abitat), yanayoendelea katika Ukumbi wa Diamond Jubilee. 
 Baadhi ya watu wakipata huduma katika banda la NSSF.
 Ofisa Masoko na Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Aisha Sango (kulia), akigawa vipeperushi kwa watu waliotembelea banda la NSSF vyenye maelezo kuhusu huduma wanazotoa, ikiwemo uuzwaji wa viwanja vilivyopimwa katika eneo la Kiluvya, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, wakati wa Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa yaliyoandaliwa na Umoja wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki (Abitat), yanayoendelea katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.
Ofisa Masoko na Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Aisha Sango (kulia), akigawa vipeperushi kwa watu waliotembelea banda la NSSF vyenye maelezo kuhusu huduma wanazotoa, ikiwemo uuzwaji wa viwanja vilivyopimwa katika eneo la Kiluvya, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, wakati wa Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa yaliyoandaliwa na Umoja wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki (Abitat), yanayoendelea katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.