WATUMISHI wa serikali kutoka
idara mbalimbali mkoani hapa kesho jumamosi watachuana katika michezo
mbalimbali ikiwamo ya soka na netiboli katika bonanza litakalofanyika
uwanja wa shule ya Sekondari
LIGI YA MABINGWA WA MIKOA KUANZA MEI 12
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Ligi ya Mabingwa wa
Mikoa kutafuta timu tatu zitakazopanda kucheza Ligi Daraja la Kwanza(FDL) msimu
ujao chini ya usimamizi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itaanza
Mei 12 mwaka huu.
Mwisho wa mikoa kuwasilisha majina ya mabingwa wao ni
Mei 1 mwaka huu wakati ratiba ya ligi hiyo itapangwa mbele ya waandishi wa
habari Mei 3 mwaka huu kwenye ofisi za TFF.
Uwasilishaji wa jina la bingwa wa mkoa unatakiwa
kufanyika pamoja na ulipaji ada ya ushiriki ambayo ni sh. 100,000. Mfumo wa ligi
hiyo ni bingwa wa mkoa X kucheza na bingwa wa mkoa Y nyumbani na ugenini ambapo
mshindi ndiye anayesonga mbele katika hatua inayofuata.
Usajili wa wachezaji wa timu hizo ni uleule uliofanyika
katika hatua ya mkoa na unatakiwa kuwasilishwa TFF kwa ajili ya uthibitisho. TFF
inapenda kusisitiza kuwa hakuna usajili mpya wa wachezaji kwa ajili ya ligi
hiyo.
Mwisho.
KILA LA KHERI AZAM FC
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaitakia
kila la kheri timu ya Azam FC katika mechi yake ya kwanza ya raundi ya pili ya
Kombe la Shirikisho dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco itakayochezwa kesho (Aprili
20 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili
jioni.
Azam FC ina fursa nzuri ya kufanya vizuri kwenye mechi
hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Emile Fred kutoka Shelisheli kutokana na
maandalizi iliyofanya, lakini vilevile tunatoa mwito kwa Watanzania kujitokeza
kwa wingi uwanjani kuiunga mkono.
Makocha wasaidizi wa timu zote mbili, Kalimangonga Ongala wa Azam na Lahcen Ouadani wa AS FAR Rabat wamezungumza na waandishi wa habari kuhusu mechi hiyo, kuwa wamejiandaa kuibuka na ushindi.
Kocha Ongala amesema wamepata DVD za mechi tatu za
mwisho za AS FAR Rabat, moja ikiwa dhidi ya timu ya Al Nasir ya Libya ambayo
waliitoa katika raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho na nyingine mbili za
ligi ya Morocco ambazo wanazifanyia kazi kuhakikisha wanashinda
kesho.
Naye Ouadani amesema hawaifahamu vizuri Azam, lakini
wanaujua mpira wa Tanzania baada ya kuangalia mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia
kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Morocco (Lions of the Atlas) iliyochezwa
jijini Dar es Salaam Machi 24 mwaka huu na Stars kushinda mabao 3-1.
Baadhi ya wachezaji ambao Azam inatarajia kuwatumia
kwenye mechi ya kesho ni pamoja na Aishi Manula, Mwadini Ally, Khamis Mcha, John
Bocco na Salum Abubakar ambao pia wamo kwenye kikosi cha sasa cha Taifa Stars
kilicho chini ya kocha Kim Poulsen.
AS FAR Rabat ina wachezaji sita kwenye timu ya Taifa ya Morocco. Wachezaji hao ni mabeki Younes Bellakhdar, Abderrahim Achchakir, Younnes Hammal, na viungo Salaheddine Said, Salaheddine Aqqal na Youssef Kaddioui.
DC MGAZA aagiza viongozi wa vijiji na kata kuendelea kuhimiza upandaji miti kwenye maeneo yao.
Na Oscar Assenga,
Mkinga.
“Ni jukumu letu sisi wananchi wote kuona
kwamba haya ni matatizo makubwa yenye madhara na ni vyema kukemea visababishi
vya madhara haya na kuchukua tahadhari “Alisema DC Mgaza huku akisisitiza
umuhimu wa kutunza mazingira.
Alisema hata hiyo wanajukumu la kuongeza kasi ya upandaji miti ili kukabiliana na upungufu wa miti uliopo na mabadiliko ya tabia ya nchi vile vile kufikia lengo lililowekwa na Taifa la kila wilaya kupanda miti 1,000,000 kila mwaka.
MKUU wa wilaya ya
Mkinga, Mboni Mgazi amewaagiza viongozi wa vijiji na kata kuendelea kuwahimiza
wananchi kupanda miti kwenye maeneo yao na kuhakikisha wanaitunza ili iweze
kukua na kutumika kw
malengo yanayotarajiwa.
Agizo la Mkuu wa wilaya alilitoa
leo wakati wa uzinduzi wa wiki ya kupanda miti kiwilaya iliyofanyika kwenye
kata ya Duga Maforoni wilayani humo katika hotuba yake ambayo ilisomwa na Afisa
Tarafa ya Mkinga, Qegen Mkinga ambapo
amesema wiki hiyo ya kupanda miti ililengwa makusudi ya kuwahimiza wananchi
kushiriki katika mchakato huo wa upandaji na kutunza mazingira katika maeneo
yao.
Mgaza amesema mabadiliko
mbalimbali ya tabia ya nchini ambayo yanachangiwa na shughuli za kibinadamu
ikiwemo ukataji miti usiozingatiwa urushiaji huleta madhara mbalimbali ikiwemo
kupata mvua zisizo za uhakika, ongezeko la joto duniani na upungufu wa
rasilimali zinazotokana na miti pamoja na kukauka kwa vyanzo vya maji.
Amesema licha ya kuleta
madhara hayo huchangia pia ongezeko la magonjwa ya mlipuko pamoja na kuongezeka
kina cha bahari hivyo kuwataka wananchi kutoruhusu ukataji wa miti ovyo kwenye
maeneo yao kwani athari watakazo kumbana nazo ni kubwa kuliko wanavyodhani.
Aidha amesema kutokana
na upungufu wa miti ya asili jamii imehamishia matumizi kwenye miti ya matunda
kama vile mikorosho, miembe, minazi na mifenesi ambayo sasa inapasuliwa mabo
kwa matumizi mbalimbali ambapo aliwataka wananchi wafuate ushauri wa kitaalamu
na sio kujichukulia sheria mikononi za kuikata.
Mkuu huyo wa wilaya
amesema wilaya hiyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wilayani humo
wanajukumu la kutoa elimu ya upandaji wa miti kwa wananchi wa kuanzia ngazi za
vijiji na kata pamoja na kukemea uharibifu wa mazingira.
Pamoja na hayo alisema wilaya hiyo imepanga
kupanda miti 810,000 hasa katika maeneo yote yenye vyanzo vya maji ikiwemo
kuwahimiza wananchi kuisimamia na kuilanda ili iweza kukua na kutunza mazingira
yao siku zijazo.
Alisema hata hiyo wanajukumu la kuongeza kasi ya upandaji miti ili kukabiliana na upungufu wa miti uliopo na mabadiliko ya tabia ya nchi vile vile kufikia lengo lililowekwa na Taifa la kila wilaya kupanda miti 1,000,000 kila mwaka.
Katika uzinduzi huo
jumla ya miti 100 ilipandwa katika maeneo yaliyopo pembezoni mwa vyanzo vya
maji ambapo zoezi hilo linatarajiwa kuendelea wiki nzima.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)