ZIMBABWE YAPONGEZA MIFUMO YA UTUNZAJI TAARIFA ZA MADINI TANZANIA

December 06, 2023

 


Na. Wizara ya Madini , Dodoma.

Ujumbe wa Wataalam kutoka Wizara ya Madini na Maendeleo ya Migodi nchini Zimbabwe umeipongeza Wizara ya Madini kuwa na mfumo mzuri wa Usimamizi wa Leseni za Madini ujulikanao _Mining Cadastre Information Management System_ (MCIMS) unaotumia Teknolojia shirikishi katika utunzaji wa taarifa za madini.

Hayo yamebainishwa leo Desemba 5 , 2023 jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Uendeshaji Migodi Wizara ya Madini nchini Zimbabwe Charles Simbalache wakati mafunzo kuhusu mfumo wa MCIMS unaotumika Tanzania.


Ikiwa siku ya kwanza ya mafunzo maalum kwa ujumbe huo, Wataalam wa Wizara ya Madini Tanzania wakiongozwa na Kamishna Msaidizi Francis Mihayo wameeleza juu ya mfumo mzima wa MCIMS unavyofanyakazi kuanzia hatua ya awali za kujisajili huku akieleza faida zinazopatikana ndani ya mfumo huo.


Sambamba na hapo, ujumbe huo umejifunza kuhusu Sheria za Madini na Kanuni zake, Muongozo wa Sera ya Madini, mifumo ya utoaji leseni pamoja na aina zake .


Pia, ujumbe huo umeelezwa jinsi Wizara ya Madini inavyosimamia maendeleo ya migodi nchini na namna ya kujikinga na majanga katika migodi na jinsi inavyosimamia utunzaji wa mazingira maeneo yenye migodi.


Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Teknolojia ya Mawasiliano Wizara ya Madini Zimbabwe, Bi. Susane Kachote, amesema kuwa lengo la ziara hii ni kupata mafunzo kuhusu namna bora kuimarisha na kuweka teknolojia ya kuweza kusimamia mnyororo mzima wa sekta.


"Pamoja na usimamizi pia tukiwa na mifumo mizuri itasaidia kuzuia mianya ya utoroshaji madini nchini Zimbabwe" Kachote amesema


Awali, akifungua mafunzo hayo Kamishna Msaidizi kutoka Wizara ya Madini Francis Mihayo amesema kuwa Tanzania inatajwa kufanya vizuri katika sekta ya madini kutokana na kuwepo kwa mifumo mizuri ya usimamizi kuanzia ngazi ya uchimbaji mdogo mpaka mkubwa, jambo linalopelekea mataifa mengine kuja Tanzania kujifunza namna ya usimamizi wa mifumo hiyo.


Kutokana na kufanana kwa jiolojia nchi ya Tanzania na Zimbabwe zimekuwa zikishirikiana katika kubadilishana uzoefu katika sekta ya madini.

ZAIDI YA WAJASIRIAMALI 300 KUSHIRIKI MAONESHO YA NGUVU KAZI/ JUA KALI NCHINI BURUNDI

ZAIDI YA WAJASIRIAMALI 300 KUSHIRIKI MAONESHO YA NGUVU KAZI/ JUA KALI NCHINI BURUNDI

December 06, 2023

 


Baadhi ya Wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali nchini Tanzania wakiwa katika foleni ya mchakato wa taratibu za kuvuka mpaka wa Burundi walipowasilia katika mpaka wa Tanzania na Burundi.

Na; Mwandishi Wetu – Bujumbura, BURUNDI

WAJASIRIAMALI zaidi ya 300 kutoka maeneo mbalimbali nchini Tanzania kushiriki maonesho ya 23 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki maarufu Nguvu Kazi au Jua Kali yanayofanyika Bujumbura, Burundi kuanzia tarehe 5 hadi 15 Desemba, 2023.

Maonesho hayo yanafanyika katika Viwanja vya Cercle Hyppique (Golf Course), Bujumbura yakiongozwa na kauli mbiu isemayo ‘Kuunganisha Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Afrika Mashariki kufanya biashara katika eneo la Jumuiya ya Afrika Mashariki’.

  

Baadhi ya Wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali nchini Tanzania wakiwa katika foleni ya mchakato wa taratibu za kuvuka mpaka wa Burundi walipowasilia katika mpaka wa Tanzania na Burundi.


Baadhi ya Wajasiriamali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kupata vibali vya kuvuka mpaka wa Burundi.

PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)
WAJUMBE WA BODI YA JKCI WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM

WAJUMBE WA BODI YA JKCI WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM

December 06, 2023




Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Asha Izina ambaye pia ni Mratibu wa huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto Mkoa wa Rukwa akiongoza kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge.

Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge akiwaonesha mfano wa jengo litakalojengwa katika Hospitali ya JKCI Dar Group wajumbe wa bodi hiyo wakati wa kikao cha tano cha Bodi kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa akichangia mada wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kulia ni mjumbe wa Bodi hiyo CPA.Godfrey Kilenga ambaye pia ni Mtendaji Mkuu kutoka ofisi ya TAB Consult Audit Firm Partner.

Baadhi ya Viongozi wa Menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge wakati akitoa taarifa ya utendaji wa kazi zilizofanywa na taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba katika mwaka wa fedha wa 2023/24 wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
- Advertisement -


Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Harun Matagane kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali akichangia mada wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Katibu wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Peter Kisenge akitoa taarifa ya utendaji wa kazi zilizofanywa na taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Oktoba katika mwaka wa fedha wa 2023/24 wakati wa kikao cha tano cha Bodi hiyo kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Benki Ya NMB Yasaidia Waathirika Wa Mafuriko Hanang

December 06, 2023

 Waathirika wa mafuriko Wilayani Hanang, Mkoani Manyara, waliopoteza ndugu zao, makazi, pamoja na mali, wamepatiwa misaada ya kibinadamu na Benki ya NMB.


Misaada hiyo inajumuisha magodoro, vyakula na vifaa vingine, ikiwa lengo ni kutoa msaada muhimu baada ya janga hilo.

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus, akikabidhi misaada hiyo, amesema benki hiyo inaungana na familia za wahanga na kutoa misaada ya kibinadamu. Msaada huo unalenga kutoa faraja na msaada wa msingi ili kusaidia katika kurejesha hali ya kawaida kwa wahanga wa mafuriko.

Mbunge wa Viti Maalumu, Asia Halamga, ameipongeza benki hiyo kwa kuwa mstari wa mbele kusaidia jamii, hasa kwa wahanga wa mafuriko katika kipindi hiki.

Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Baraka Ladislaus (aliyevaa fulana nyeupe), akikabidhi misaada kwa waathirika wa mafuriko Hanang. Anamkabidhi Mbunge wa Vijana wa Hanang, Asia Halamga, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa.

 

MWENYEKITI WA BODI YA NSSF AFANYA ZIARA YA KIKAZI MAKAO MAKUU YA NSSF

December 06, 2023

 


*Aahidi ushirikiano wa kutosha kufanikisha utendaji wa Mfuko


*Mkurugenzi Mkuu aweka wazi mafanikio na mikakati ya uboreshaji huduma

Na MWANDISHI WETU


Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bi. Mwamini Malemi, amefanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) jijini Dar es Salaam, na kuahidi kufanya kazi kwa ushirikiano na Menejimenti pamoja na wafanyakazi wa Mfuko.


Katika ziara hiyo ya kikazi iliyofanyika tarehe 5 Desemba 2023, Bi. Malemi alikutana na kuzungumza na wajumbe wa Menejimenti ya NSSF, ambapo pamoja na mambo mengine alipokea taarifa ya utendaji kazi kutoka kwa Mkurugenzi wa Mkuu, Bw. Masha Mshomba.


Taarifa ya NSSF iliyowasilishwa na Bw. Mshomba ilionesha utendaji mzima wa Mfuko, ikigusia uandikishaji wanachama, uchangiaji, uwekezaji pamoja na ulipaji mafao. Aidha Bw. Mshomba alizungumzia kuhusu uboreshaji huduma kwa wanachama, uboreshaji mifumo na namna wafanyakazi wanavyoshirikiana katika kuhakikisha majukumu ya Mfuko yanakamilika.


Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuzungumza na Menejimenti ya NSSF, Bi. Mwamini alimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua kushika nafasi hiyo, ambapo aliahidi kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuweza kufikia malengo na matarajio ya Mfuko.


Awali, Bw. Mshomba alimueleza Mwenyekiti huyo matarajio ya Mfuko ikiwemo kuendelea kuboresha huduma kwa wanachama kupitia njia mbalimbali ikiwemo ya matumizi ya TEHAMA kwani hicho ndio kipaumbele muhimu cha NSSF.




Bw. Mshomba alisema matarajio ya Mfuko ni kuona mwanachama baada ya kustaafu na kuwasilisha taarifa zake zote zinazotakiwa kwa mujibu wa Sheria analipwa stahiki zake ndani ya muda mfupi.














MAJERUHI WA MAFURIKO YA HANANG WOTE WAMETIBIWA MANYARA BILA YA RUFAA.

MAJERUHI WA MAFURIKO YA HANANG WOTE WAMETIBIWA MANYARA BILA YA RUFAA.

December 06, 2023

 

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Tulia Ackson ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa uboreshaji wa huduma za afya nchini na kufanya majeruhi wote wa mafuriko ya Hanang kupata huduma Mkoani Manyara bila kupewa rufaa.

“Nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweka utaratibu mzuri wa kuhudumia vyema majeruhi wa mafuriko na kutibiwa bure bila gharama yeyote” amesema Dkt. Tulia.

Aidha ameipongeza Wizara ya Afya na wataalamu wote kwa kazi nzuri waliofanya katika kuwahudumia majeruhi hao na kuwataka wataalam kuendelea kutoa huduma bora za matibabu kwa wananchi.