MAHAKAMA KUANZISHA KITUO CHA MAFUNZO DAR ES SALAAM

August 26, 2017
 Mhandisi wa Mahakama ya Tanzania, Khamadu Kitunzi akielezea teknolojia inayotumika kujenga jengo la kituo cha mafunzo cha mahakama leo jijini dar es salaam.
 Kaimu jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akiwa na Mwakilishi wa Benki ya dunia nchini, Bella Bird (kulia) na kulia ni jaji kiongozi wa mahakama kuu ya Tanznaia Mhe. Ferdinand Wambali walipotembelea ujenzi wa kituo cha mafunzo cha Mahakama leo jijini Dar es salaam
Picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo.

Na Mohamed Ali-Mahakama.
MAHAKAMA ya Tanzania inakusudia kuanzisha kituo cha Mafunzo kwa ajili ya watumishi wake pamoja na wadau ili kuwaongezea ujuzi utakaosaidia kuboresha huduma zinazotolewa na Mahakama. 

Kituo hicho kinachojengwa katika eneo la Mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam kitawaunganisha watumishi wa Mahakama na wadau katika mafunzo kwa njia ya video (video conferencing).

Akizungumzia Kituo hicho, Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof Ibrahim Hamis Juma amesema ujenzi wa kituo hicho ni sehemu ya Maboresho ya huduma za Mahakama ambacho pia wadau wa Mahakama watakuwa ni sehemu ya mafunzo yatakayokuwa yakitolewa.

Amesema badala ya Majaji, Mahakimu, watumishi na wadau wa Mahakama kwenda kupata baadhi ya mafunzo kwenye chuo cha Uongozi wa Mahakama- Lushoto (IJA), baadhi ya mafunzo watakuwa wakiyapata katika kituo hicho.

Naye Mratibu wa Mpango Mkakati wa Mahakama pamoja na maboresho ya Huduma za Mahakama Mhe. Zahara Maruma alisema ujenzi wa kituo hicho ni utekelezaji wa nguzo ya tatu ya mpango Mkakati wa miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania ambapo kupitia nguzo ya pili ya Mpango huo, Majaji na Mahakimu hupatiwa mafunzo mbalimbali ili kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati.

Akizungumzia nguzo ya tatu ya Mpango huo, Mhe. Maruma alisema nguzo hiyo inahusiana na urejeshaji wa imani ya wananchi kwa Mahakama na ushirikishwaji wa wadau katika shughuli za Mahakama ambapo kupitia kituo hicho wadau wa Mahakama watahusishwa kwenye Mafunzo mbalimbali ili kurahisisha suala la upatikanaji wa Haki.
KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI YATEMBELEA KIWANDA CHA DANGOTE

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI YATEMBELEA KIWANDA CHA DANGOTE

August 26, 2017
Mtaalam kutoka Kampuni Tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) ya GASCO inayojihusisha na usambazaji wa gesi, Mhandisi Mwanaidi Rashid (kulia) akielezea hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa kituo Namba I cha gesi ambapo Kiwanda cha Saruji cha Dangote kitaunganishwa na huduma hiyo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwenye ziara hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa tatu kutoka kulia mbele) na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia ( wa nne kutoka kulia mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na kamati hiyo wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (kulia) akimpokea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto) aliyeambatana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti mara baada ya kuwasili katika kiwanda hicho.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (kulia) akielezea mafanikio na changamoto za kiwanda hicho kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti (hawapo pichani). Wengine kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Jaji Mstaafu Josephat Mackanja.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo, akifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (hayupo pichani ) katika kikao hicho.