February 04, 2014

BUMBULI WALIA NA UPUNGUFU WA WATUMISHI

{Beatrece  Msomisi  ambae  ni Mkurugenzi  wa  bumbuli   akipokea  zawadi} 
Raisa Said, Bumbuli
 Halmashauri  ya Bumbuli  mkoani  Tanga inakabiliwa na  tatizo kubwa la upungufu wa watumishi jambo ambalo linakwamisha utendaji wa kazi katika Halmashauri hiyo mpya.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo kilichofanyika Bumbuli mwishoni mwa wikli hii, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauiri hiyo,  Beatrice Msomisi alisema kuwa Halmshauri hiyo ina upungufu mkubwa wa  watumishi ambao alisema kuwa unaathiri shughuli za kazi.

KINGWENDU:NIMEJIPANGA VYA KUTOSHA KUINGIA BUNGENI 2015.

February 04, 2014

Mwigizaji wa Comedy (Futuhi) Anajulikana kwa Jina la kingwendu Amweka wazi Nia yake ya kuwania Ubunge katika kinyanganyiro cha 2015,
 
Amesema kwa sasa Amejipanga vya kutosha kuingia mjengoni , Kuhusu chama atakacho gombea kwa sasa ni siri yake ila atakitaja mambo yakikaribia....
UNAONAJE ATAWEZA AU NDIO ATAPELEKA BUNGENI VICHEKESHO? 
February 04, 2014

HANDENI KUTUMIA ZAIDI YA TSH BIL. 7 KWA MWAKA 2014/15

{Mkurugenzi  Mji wa  Handeni    Thomas Mzinga  pichani}
                                                                    Raisa  Said, Handeni


Baraza la Halmashauri Mji wa Handeni limepanga kutumia jumla ya Sh. Bilioni 7.92 kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo na utawala kwa mwaka wa fedha 2014/2015.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya bajeti yaliyopitishwa na kikao cha Baraza la Halmashauri hiyo, kati ya fedha hizo Sh. milioni.503.19 zimepangwa kutuimika kwa ajili kutekeleza miradi mbalimbali za maendeleo kwa mwaka huo wa fedha.

Akisoma mapendekezo hayo katika kikao hicho kilichofanyika makao makuu ya Halmashauri hiyo, Chanika, Handeni , Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri,Thomas Mzinga alisema vyanzo vikuu vya fedha za utekelezaji wa miradi ni ruzuku kutoka serikali kuu na wahisani.

February 04, 2014

MAKAMBA,KINANA NA WENGINE WACHANGIA

          
Raisa Said, lushoto
Zaidi ya Sh. Mil. 41 zimechangwa  kwa  ajili  ya  ujenzi  wa  kanisa katika Chuo  cha Kumbukumbu ya  Sebastian Kolowa (SEKOMU), wilayani Lushoto katika juhudi za kuwasogezea  huduma  karibu wanafunzi  na  jamii  inayozunguka  katika chuo  hicho.

Kwa  mujibu  wa  Makamu  Mkuu wa  Chuo hicho, Dk Aneth  Munga  kati  ya  fedha  hizo, Sh. mil.22  zilichangwa na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, January  Makamba  kwa  kushirikiana  na   baadhi  ya Mawaziri, wabunge  pamoja  na  Katibu  Mkuu wa  CCM, Abdulahman Kinana.
February 04, 2014

Kampuni ya Bia ya Serengeti Kuwapeleka Watanzania Brazil

Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Ephraim Mafuru (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Pamoja naye ni Meneja Masoko wa SBL, Allan Chonjo (wa pili kushoto).
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Ephraim Mafuru (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Pamoja naye ni Meneja Masoko wa SBL, Allan Chonjo (wa pili kushoto).
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Ephraim Mafuru (wa kwanza kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Pamoja naye ni Meneja Masoko wa SBL, Allan Chonjo (kushoto).
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Ephraim Mafuru (wa kwanza kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Pamoja naye ni Meneja Masoko wa SBL, Allan Chonjo (kushoto).

MWAKILISHI WA JIMBO LA KIEMBE SAMAKI AAPISHWA LEO ZENJI

February 04, 2014
 Msafara wa Mhe. Mwakilishi Mpya wa Jimbo la Kiembesamaki ukiingia katika viwanja Baraza la Wawakilishi kumshindikiza kwa ajili ya kuapishwa leo asubuhi. 
 Gari iliomchukuwa Mhe. Mahmoud Thabit Kombo likingia katika viwanja vya Baraza leo asubuhi kwa ajili kuhudhuria kuapishwa na kushiriki katika Kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea kujadili Ripoti za Kamati za Baraza Zinazowakilishwa na Wenywviti wa Kamati hizo.
 Mhe. Mwakilishi Mteule akiwasili katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi Chukwani tayari kwa kuapishwa Rasmin kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki  Zanzibar,akishindikizwa na Mwakilishi wa Jimbola Rahaleo Mhe Nassor Salim Jazira na katikati Mwakilishi wa Bububu Mhe Hussein Ibrahim Makungu (BHAA) wakimshindikiza katika ukumbi wa Mkutano kwa ajili kuapishwa
Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Yahya Khamis Hamad, akisalimiana na Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo alipowasili katika Ofisi ya Katibu wa Baraza kwa ajili kujitambulisha na kuhudhuria kuapishwa kwake kuingia katika Baraza la Wawakilishi baada ya kushinda kiti hicho katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki uliofanyika wiki iliopita.
Mhe. Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Pandu Ameir Kificho akiingia katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi kwa ajili ya kuaza kwa taratibu za shughuli za Kikao na kumapisha Mwakilishi Mpya wa Jimbo la Kiembesamaki Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo. wakati wa Kikao cha asubuhi leo. 
Mhe. Spika Pandu Ameir Kificho akisoma Dua kabla ya kuaza kwa Kikao cha Baraza cha Asubuhi leo. 
February 04, 2014

*KINANA AFIKA NYUMBANI KWA MAREHEMU DKT. MGIMWA

 Katibu Mkuuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsalimia Mama Mzazi wa aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa, Consolata Mgovano, alipokwenda nyumbani kwa marehemu Mgimwa, Kijiji cha Magunga, jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, leo jioni. Wengine ni watoto wa marehemu Mgimwa, Stanisla Mgimwa, na Rozalina Mgimwa.
 Kinana akizungumza na familia huyo ya marehemu Mgimwa. Wapili kushoto ni Johakim Mgimwa
February 04, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MKUU WA JESHI LA POLISI NCHINI IGP MANGU

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kumkaribisha Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Feb 4, 2014, kwa mazungumzo. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Feb 4, 2014, kwa mazungumzo. Picha na OMR
February 04, 2014

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE APOKEA HUNDI YA SHILINGI MILIONI 100 ILIYOTOLEWA NA BENKI YA CRDB KUSAIDIA WALIOATHIRIKA NA MAFURIKO MKOANI MOROGORO


  Rais Dkt  Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hundi ya Shilingi Milioni 100 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei, kusaidia waathirika  wa mafuriko yaliyozikumba wilaya tatu za Kilosa, Mvomero na Gairo katika Mkoa wa Morogoro, mwezi uliopita katika shughuli fupi iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam leo Februari 4, 2014 na kuhudhuriwa pia na Mhesimiwa William Lukuvi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia pia masuala ya maafa pamoja na maafisa wa CRDB.


 Rais Dkt  Jakaya Mrisho Kikwete Mhesimiwa akimkabidhi Mhe William Lukuvi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia pia masuala ya maafa pamoja na maafisa wa CRDB, hundi ya shilingi milioni 100 iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei, zikiwa ni msaada wa benki hiyo kwa waathirika wa mafuriko yaliyozikumba wilaya tatu za Kilosa, Mvomero na Gairo katika Mkoa wa Morogoro, mwezi uliopita katika shughuli fupi iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam leo Februari 4, 2014.

Rais Dkt  Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei, baada ya kukabidhiwa hundi ya shilingi milioni 100 kutoka benki hiyo kusaidia waathirika  wa mafuriko yaliyozikumba wilaya tatu za Kilosa, Mvomero na Gairo katika Mkoa wa Morogoro, mwezi uliopita katika shughuli fupi iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam leo Februari 4, 2014 na kuhudhuriwa pia na Mhesimiwa William Lukuvi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia pia masuala ya maafa pamoja na maafisa wa CRDB. 

  Rais Dkt  Jakaya Mrisho Kikwete akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei, baada ya kukabidhiwa hundi ya shilingi milioni 100  kutoka benki hiyo kusaidia waathirika  wa mafuriko yaliyozikumba wilaya tatu za Kilosa, Mvomero na Gairo katika Mkoa wa Morogoro, mwezi uliopita katika shughuli fupi iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam leo Februari 4, 2014 na kuhudhuriwa pia na Mhesimiwa William Lukuvi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia pia masuala ya maafa pamoja na maafisa wa CRDB. 

Picha na IKULU.
February 04, 2014

WEMA SEPETU AOMBA AKIFA AAGWE UWANJA WA TAIFA

Kazi ipo! Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ambaye huwa haishiwi habari, ameibuka na jipya akidai kuwa akifa leo au kesho basi aagwe Uwanja wa Taifa jijini Dar, Ijumaa Wikienda limemtegea sikio.
Wema Isaac Sepetu.

Miss Tanzania huyo wa 2006/07 ambaye anakimbiza kwenye sinema za Kibongo alifunguka hayo wikiendi iliyopita wakati akiwa safarini kuelekea jijini Arusha ambapo msanii anayemilikiwa na kampuni ya Wema ya Endless Fame Production aliyetajwa kwa jina moja la Mirrow alikwenda kuangusha shoo pande hizo.

Wema aliyasema hayo alipokuwa akichangia mada ya utabiri wa mtoto wa aliyekuwa mtabiri bingwa, marehemu Sheikh Yahya Hussein, Maalim Hassan Hussein aliyetabiri kwamba wasanii wengi wenye majina makubwa watakufa mwaka 2014.
February 04, 2014

HATIMAYE UVCCM MKOA WA MOROGORO WAMPA UVCCM FEKI ZA USO LEO LIVE!!

UVCCM Feki Apewa Za Uso!!

 Mwenyekiti wa umoja wa vijana mkoa wa Morogoro Harriet Sutta akiwa na katibu wake Nicodemas Tambo wakizungumiza juu matamko yanayotolewa na baadhi ya viongozi mkoani hapa kinyume na taratibu.
Mimi nazungumzia juu ya uchaguzi tulionao mbele yetu katika wilaya ya Gairo ludewa na Tungi Manispaa ya Morogoro, vijana washiriki kikamilifu kufanya kampeni za amani na utulivi na sio vurugu.
February 04, 2014

LIVEEE,MH:MWIGULU NCHEMBA ANASA WATOROSHAJI WA BIDHAA MPAKANI MWA -TANZANIA NA MALAWI

Naibu Waziri wa Fedha Mh;Mwigulu Nchemba akiwa ameongozana na Naibu Kamishina Idara ya Forodha na Ushuru wa Bidhaa Tanzania,Ndugu Patric Kisaka(kulia) na Mkurugenzi wa huduma za Ulipaji Kodi na Elimu Ndugu,Richard Kayombo pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kyela Bi.Magreth Kalenga(hayupo pichani) wakiondoka kwenye Ofisi za TRA Kuelekea kwenye eneo la Mpakani Mwa-Tanzania na Mawali wilayani Kyela hii leo.
 Kibao Kianachoonesha "KARIBU TANZANIA" kilichopo pembezoni mwa Mto Songwe unaotumiaka kama mpaka wa Tanzania na Malawi.

TFF YASITISHA MATUMIZI YA TIKETI ZA ELEKTRONIKI

February 04, 2014

Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesitisha matumizi ya tiketi za elektroniki kwenye viwanja vyote vyenye huduma hiyo ili kutoa fursa ya kufanyika tathmini ya kina kabla ya kuendelea tena.

Uamuzi huo umefikiwa kwa kuzingatia sababu mbalimbali baada ya kikao kati ya Sekretarieti ya TFF na maofisa wa benki ya CRDB kilichofanyika jana (Februari 3 mwaka huu) katika ofisi za Shirikisho.

MTIBWA SUGAR, SIMBA KUUMANA MOROGORO

February 04, 2014
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 16 kesho (Februari 5 mwaka huu) kwa mechi tano huku Mtibwa Sugar ikiikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Kiingilio katika mechi hiyo ambayo itakuwa ya kwanza kuchezwa kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000 tangu uanze mzunguko wa pili wa VPL kitakuwa sh. 5,000. Jonisia Rukyaa kutoka Bukoba ndiye atakayechezesha mechi hiyo.

Mechi nyingine za ligi hiyo ni Tanzania Prisons vs Coastal Union (Sokoine, Mbeya), Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting (Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers vs Oljoro JKT (Ali Hassan Mwinyi, Tabora) na JKT Ruvu vs Ashanti United (Chamazi, Dar es Salaam).

40 KUNG’AMUA VIPAJI UBORESHAJI TAIFA STARS

February 04, 2014
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeteua kikosi cha makocha 40 kutoka sehemu mbalimbali, Tanzania Bara na Zanzibar ili kung’amua vipaji katika mpango wa kuboresha timu ya Taifa (Taifa Stars).

Makocha hao ambao watafanya kazi hiyo katika michuano maalumu ya mikoa wanatakiwa kuripoti katika ofisi za TFF siku ya Jumamosi (Februari 8 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwa ajili ya kupewa maelekezo zaidi.

Walioteuliwa ni Abdallah Hussein (Kilimanjaro), Abdul Mingange (Dar es Salaam), Ali Bushiri (Zanzibar), Ali Mayay (Dar es Salaam), Ally Mtumwa (Arusha), Ayoub Selemani (Zanzibar), Boniface Pawasa (Dar es Salaam), Dan Korosso (Mbeya), Dk. Mshindo Msolla (Dar es Salaam) na Edward Hiza (Morogoro).

KARIBU SANA MKUU

February 04, 2014
MENEJA MKUU WA HOTEL YA TANGA BEACH RESOT JOSEPH NGOYO KUSHOTO AKITETA JAMBO NA MKURUGENZI MTENDAJI WA (TSN) GARIEL NDERUMAKI WAKATI WA UFUNGUZI WA KIKAO CHA KAZI CHA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO HAPA NCHINI AMBACHI KILIFUNGULIWA NA WAZIRI WA HABARI,VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO DR.FENELLA MUKANGARA JANA.

MCT WATEMBELEA TANGA PRESS CLUB.

February 04, 2014
MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA TANGA(TANGA PRESS CLUB)KUSHOTO AKIZUNGUMZA NA MAAFISA KUTOKA BARAZA LA HABARI TANZANIA (MCT) WA KWANZA KULIA NI THERESA CHILAMBO NA ANAYEFUATA NI ANITHA MENDOZA.





MRATIBU WA TANGA PRESS CLUB NEEMA KHATIBU KULIA AKIFURAHIA JAMBO NA OFISA WA MCT ANITHA MENDOZA MARA BAADA YA KUTEMBELEA KLABUNI HAPO LEO