Rais Magufuli awatembelea na kuwajulia hali Mzee Malecela na Mhe. Ndugai

August 16, 2016




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 16 Agosti, 2016 amewatembelea na kuwajulia hali Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. John Samuel Malecela Jijini Dar es Salaam.


Pamoja na kuwajulia hali, Rais Magufuli aliyeongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amewaombea kwa Mwenyezi Mungu wapone na kupata nguvu haraka ili waweze kuendelea na majukumu yao ya kawaida katika ujenzi wa Taifa.Akizungumza na Rais Magufuli nyumbani kwake Salasala Jijini Dar es Salaam spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai amemshukuru Rais Magufuli kwa kumtembelea, kumjulia hali na kufuatilia kwa ukaribu wakati wote alipokuwa akipata matibabu nchini India hadi aliporejea hapa nchini.

"Kwa kweli nimefarijika sana, kwanza naomba nimshukuru sana Mhe. Rais kwa sababu nilipopata matatizo haya ya maradhi alikuwa karibu sana na mimi nikiwa hapa nchini na hata nilipopelekwa nchini India alinipigia simu mara kwa mara na kunifariji sana, na hapa amekuja kuniona kwa niaba ya watanzania kwa kweli namshukuru sana na namuombea kwa Mwenyezi Mungu aendelee kumpa moyo huu wa kuwajulia hali wale wenye matatizo mbalimbali"Lakini niwahakikishie Watanzania, kwamba kwa sasa nina nafuu kubwa sana, naweza kufanya kazi nyingi tu sasa lakini tuendelee kuombeana" Ameeleza Mhe. Ndugai alipokuwa akizungumzia hali yake kwa sasa.

Kwa upande wake Makamu wa Rais Mstaafu na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. John Samuel Malecela pamoja na kumshukuru Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli kwa kumtembelea amesema afya yake inazidi kuimarika na pia amewashukuru Madaktari wanaompatia matibabu.

"Mheshimiwa Rais nakushukuru sana, namshukuru pia Mama Janeth Magufuli kwa kunitembelea na kunifariji, naendelea vizuri na matibabu na afya yangu imeimarika kwa kiasi kikubwa" Ameeleza Mhe. Malecela.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

Dar es Salaam

16 Agosti, 2016.

 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana kwa furaha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Sala sala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai nyumbani kwake Sala sala jijini Dar es Salaam alipokwenda kumjulia hali. 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli kushoto akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai nyumbani kwake Sala sala jijini Dar es Salaam walipokwenda kumjulia hali. Kulia ni mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai.

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili nyumbani kwa Spika Sala sala jijini Dar es Salaam. 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Waziri Mkuu mstaafu John Samuel Malecela ambaye anapata matibabu jijini Dar es Salaam. 

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimsalimia Waziri Mkuu mstaafu John Samuel Malecela ambaye anapata matibabu jijini Dar es Salaam. 
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa pamoja na Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Sala ya kumuombea Waziri Mkuu mstaafu John Samwel Malecela pamoja na mkewe Anne Kilango Malecela.

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akizungumza na Mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai wakati alipokwenda na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwajulia hali nyumbani kwao Sala sala jijini Dar es Salaam. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai huku Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiagana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwajulia hali nyumbani kwao Sala sala jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU 
BLACKFOX MODELS AFRICA WAFANIKISHA ZOEZI YA KUSAJILI VIJANA WA ARUSHA

BLACKFOX MODELS AFRICA WAFANIKISHA ZOEZI YA KUSAJILI VIJANA WA ARUSHA

August 16, 2016
Jumapili ilikuwa siku ya furaha kwa wanamitindo wa Arusha, kwani timu ya Blackfox Models ilitua jijini humo kusajili vijana wenye fani hiyo.

Zoezi hili lilifanyika katika hoteli ya Tulia Boutique Hotel and SPA iliyopo Sakina.
Miss Aj Mynah, alisema " nimefurahi sana kwa sisi kufanikisha jambo hili, kwani, lengo letu kubwa ni kuendeleza vipaji vya vijana hawa hasa kwenye uanamitindo na hata kwenye mambo ya Arts Vililevile.

Tumeona Arusha ina vipaji vingi sana, na tumekuta kijana mmoja utakuta ana kipaji cha kuimba, uanamitindo, acrobatics na hata kucheza. Kwakweli tumefurahishwa na tutafanya vilivyo kuhakikisha tunakuza vipaji hivi - alisema AJ.
Blackfox wamesajili vijana 12 kutoka Arusha, na wameahidi kutembea kwenye miji mingine kusajili.

Blackfox Models Africa, ni Agency ambayo inajihusisha kwenye kusajili vijana na kuwapa mazoezi kwenye uanamitindo, pia kuwatafutia kazi za kwenye uanamitindo nchini. Ofisi yao iko Karibu na ubalozi wa Marekani. Kwa wale vijana ambao wanataka kuingia Blackfox wanaweza kwenda kwenye tovuti yao www.blackfoxmodelsafrica.com
-- Zainul A. Mzige, Operation Manager, MO BLOG, www.modewjiblog.com +255714940992.

ULEGA AKABIDHI MADAWATI HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA.

August 16, 2016


Mbunge wa Jimbo mkuranga Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Njopeka mara baada ya kufanya ziara ya kuwashukuru wananchi hao baada ya kumchagua kuwa mbunge wa jimbo hilo ambapo pia mbali na kushukuru anatumia mikutano hiyo kuhamasisha maendeleo na kuwataka kufanya kazi kwa bidii leo mkoani Pwani.
Walimu wa shule ya msingi Misasa wakimsikiliza mbunge wa Jimbo la mkuranga Abdallah Ulega mara baada ya kuzuru shuleni hapo kwa lengo la kuwahamasisha kufanya kazi kwa bidii na kwamba yeye kama kiongozi wao yupo pamoja nao .
Akina mama wa kijiji cha Misasa kilichopo kata ya Likanga wakimsilikiliza mbunge wa Jimbo hilo Abdallah Ulega kwa makini wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru uliofanyika kijiji hapo ambapo pia walipata nafasi ya kuwasilisha changamoto zao hususani kukosekana kwa Zahanati na maji safi.
Watendaji wa halmashauri wakimsikiliza kwa makini mbunge wa jimbo hilo Abdallah Ulega,katika mkutano wake wa hadhara wa kushurukuru wananchi wa kijiji cha Njopeka ,kata ya Likanga ambapo katika ziara hizo amekuwa akitembea na watendaji hao ili kujibu hoja mbalimbali kutoka kwa wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akiwasili katika kijiji cha Misasa kilichopo kata ya Lukanga ,akiwa sambamba na baadhi ya viongozi wa kijiji waliokuja kumpokea,ulega yupo katika ziara ya kushukuru wananchi wake pamoja na kuhamasisha maendeleo ya watu.
Mbunge Abdallah Ulega akikabidhi madawati 537 kwa mkurugenzi wa halmashauri ya mkuranga Msham Munde ,madawati hayo yametokana na fedha zilizotolewa na bunge baada ya kubana matumizi na kukabidhiwa Rais Dkt John Magufuli ambaye naye aliagiza zitengeneze madawati.
Mdau wa maendeleo kutoka kampuni ya Hamisi Njomoke Limited akimkabidhi madawati 50 mbunge wa jimbo hilo Abdallah Ulega ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kauli mbiu ya rais ya kuwataka watanzania kujitokeza kuchangia ili kuondoa kero hiyo katika shule leo mokani Pwani.
Mbunge Abdallah Ulega (katika alie simama) akiwa katika picha ya pamoja na mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya mkuranga Msham Munde, mkuu wa wilaya hiyo Filberto Sanga, na mdau wa maendeleo Hamisi Njomoke mara baada ya kukabidhi madawati 537 ya mbunge wilayani humo.Sehemu ya madawati ya hayo. (Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)

AWATAKA VIONGOZI NA WALIMU KUTUZA MADAWATI HAYO

Mbunge wa jimbo la mkuranga Abdallah Ulega amekabidhi madawati 537 kwa halmashauri ya wilaya hiyo, huku akiwataka viongozi wakiwamo madiwani wa kata mbalimbali kusimamia vizuri madawati hayo ili kutambua mchango mkubwa wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi alisema kuwa madawati hayo yametokana na fedha zao ambazo zilibaki baada ya kubana matumizi katika ofisi ya bunge na kwa kauli moja walikubali kumkabidhi Rais Dkt. Magufuli, ambapo naye kwa kutambua changamoto ya madawati akaelekeza fedha hizo zipelekwe kutengeneza madawati hayo.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Msham Munde alimshukuru Mbunge huyo na kudai kuwa uchangiaji wa madawati hayo ni mchakato endelevu hivyo wadau waendelee kujitokeza kuchangia huku akisisitiza kwamba kwa asilimia kubwa yamekwenda kutatua kero hiyo.

Wakati huohuo mdau wa maendeleo Hamisi Njomoke alimkabidhi mbunge wa jimbo hilo Ulega Madawati 50 kama sehemu ya kumuunga mkono mbunge paoja na Rais Dkt Magufuli huku akiwataka wadau wengine kujitokeza kuchangia ili watoto wasome katika mazingira rafiki.
Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla afanya ukaguzi wa kushtukiza kituo cha CHESA

Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla afanya ukaguzi wa kushtukiza kituo cha CHESA

August 16, 2016


Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla amefanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY- (CHESA) kilichopo Upanga, Wilayani Ilala, jijini Dar es salaam.
Ziara hiyo ya kushtukiza inafuatia baada ya hatua ya Naibu Waziri huyo wa Afya Dk.Kigwangalla kuendelea kufanya ukaguzi wa Asasi mbalimbali zisizo za kiserikali zikiwemo NGO’s na CBO zenye makosa ya kiutendaji na kimfumo ambayo ni tofauti na taarifa zao katika usajili wa Serikalini na namna ya uendeshaji wa wao.
Mbali na hayo kituo hicho cha CHESA kinashukiwa kuhusika na vitendo vya uhamasishaji wa mahusiano ya mapenzi ya Jinsia moja (USHOGA), ambayo ni kinyume na mila na Desturi za kitanzania pamoja na Katiba na sharia za Nchi.
“Mahusiano ya jinsia moja si kinyume na mila na desturi zetu tu. Bali hata sheria na katiba ya nchi yetu haziruhusu mfumo huo wa kimahusiano” amesema Dk..Kigwangalla
Aliendelea kubainisha kuwa : “Sisi kama Serikali hatujawahi kusaini mikataba yoyote ya kimataifa inayoruhusu ushoga hivyo kwa taasisi yoyote hapa Nchini inayofanya hivyo ni kuvunja sheria za Nchi na inapaswa kuchukuliwa hatua kali za kisheria na hata kufutiwa usajili wake” aliongeza Dk. Kigwangalla.
Katika ukaguzi wa kituo hicho, Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla akiwa ameambatana na Kaimu Msajili wa Asasi zisizo za kiserikali kutoka Wizara anayoiongoza, Bw. Julius Mbilinyi pamoja na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Ilala, Hassan Selengu pia wamefanya ukaguzi katika kituo hicho ili kubaini kama kuna uwepo wa vilainishi vinavyotumiwa na watu wenye mahusiano ya jinsia moja ambavyo hivi karibuni Serikali ilipiga marufuku matumizi yake hapa nchini.
“Serikali ilikifuta kituo cha ‘SISI KWA SISI’ kwa sababu kilihusika na tuhuma za ushawishi wa mahusiano ya jinsia moja ambacho pia wewe ulikuwa Mkurugenzi wake. Sasa tumeamua kuchunguza na kituo hichi ili tujue kama mnahusika na vitendo hivyo ili tuchukue hatua endapo itabainika ama la” ameeleza Dk. Kigwangalla.
Aidha, Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla amemtaka Mkuu wa upepelezi Bwana Hassan Selengu afanye uchunguzi wa kina katika kituo hicho ili kubaini pesa za misaada katika kituo hicho zinatokea wapi lakini pia ni kubaini kama kituo hicho kinajihusisha na ushawishi wa watu kujiunga na mahusiano ya jinsia moja.
“Tunawasiwasi kuwa mnapokea pesa nyingi na misaada mingi kutoka katika Taasisi mbalimbali lakini pesa hizo zinatumika kuhamasisha mapenzi na mahusiano ya jinsia moja.
Mbali na hayo. taarifa za usajili wa kituo hichi zinakinzana na malengo na miradi inayofanyika hapa. Pia ipo miradi mbalimbali ambayo haijasajiliwa wala hujaitaja katika maelezo yako lakini inafanyika katika kituo hichi” alihoji Dk. Kigwangalla huku akimtajia baadhi ya miradi hiyo ambayo Serikali inaitambua.
Na Hashim Ibrahim (UDSM-SJMC).
Tazama hapa MO TV, kuona tukio hilo:
Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamis Kigwangalla akiwasili katika ofisi za kituo cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY- (CHESA) kilichopo Upanga, Wilayani Ilala, jijini Dar es salaam.
DSC_5718 DSC_5724Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akiandika maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa kituo cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY-(CHESA) Bw. John Kashiha wakati alipotembelea katika kituo hicho chenye maskani yake Upanga, Ilala, Jijini Dar es Salaam, leo Agosti 15.2016
DSC_5730Mkurugenzi wa kituo COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY-(CHESA) Bw. John Kashiha akielezea miradi mbalimbali ya kituo hicho kwa Naibu Waziri. (Hayupo pichani).
DSC_5744Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo kwa Mkuu wa upepelezi wa Mkoa wa Ilala, Bwana Hassan Selengu juu ya kukifanyia uchunguzi wa kina kituo cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY-(CHESA).
DSC_5764Mkuu wa upepelezi wa Mkoa wa Ilala, Bwana Hassan Selengu akiwa pamojana wasaidizi wake wakifanya upekuzi katika ofisi za kituo hicho cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY-(CHESA), Kulia ni Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla.
DSC_5774Upelelezi na Upekuzi ukiendelea ndani ya kituo hicho...
DSC_5796Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo na kuwaonyesha moja ya makablasha (file) zilizokutwa hapo ilikusadia uchunguzi kwa Mkuu wa upepelezi wa Mkoa wa Ilala, Bwana Hassan Selengu na Kaimu Msajili wa Asasi zisizo za kiserikali kutoka Wizara hiyo, Bw. Julius Mbilinyi juu ya kukifanyia uchunguzi wa kina kituo cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY-(CHESA).
DSC_5797Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo na kuwaonyesha moja ya makablasha (file) zilizokutwa hapo ilikusadia uchunguzi kwa Mkuu wa upepelezi wa Mkoa wa Ilala, Bwana Hassan Selengu na Kaimu Msajili wa Asasi zisizo za kiserikali kutoka Wizara hiyo, Bw. Julius Mbilinyi juu ya kukifanyia uchunguzi wa kina kituo cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY-(CHESA)
DSC_5818Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akimweleza jambo Bwana John Kashiha wakati wa tukio hilo..
DSC_5811Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia moja ya nyaraka za taasisi za kituo hicho
DSC_5828
Upekuzi ukiendelea..DSC_5834Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akionyesha moja ya kijarida kwa Mkuu wa upepelezi wa Mkoa wa Ilala, Bwana Hassan Selengu na Kaimu Msajili wa Asasi zisizo za kiserikali kutoka Wizara hiyo, Bw. Julius Mbilinyi juu ya kukifanyia uchunguzi wa kina kituo cha COMMUNITY HEALTH EDUCATION SERVICES AND ADVOCACY-(CHESA)
DSC_5842Upekuzi ukiendelea.. katika ofisi hizo.

WAKUU WA WILAYA WASTAAFU WAJIUNGA PSPF, RAIS MAGUFULI AWAPONGEZA KWA KUJIPANGA KIMAISHA

August 16, 2016


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (kulia),akimkabidhi kadi ya kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mwenyekiti wa Wakuu wa Wilaya Wastaafu, Ramadhan Maneno, mara baada ya kufungua mafunzo ya ujasiriamali kwa wakuu hao, iliyoandaliwa na PSPF jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2016. Waziri Simbachawene alimwakilisha Rais John Magufuli. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, George Yambesi
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (kulia),akimkabidhi kadi ya kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Jackline Liana, mara baada ya kufungua mafunzo ya ujasiriamali kwa wakuu hao, iliyoandaliwa na PSPF jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2016. Waziri Simbachawene alimwakilisha Rais John Magufuli. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, George Yambesi
 Waziri Simbachawene akitoa hotuba yake
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (kulia),akimkabidhi kadi ya kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Gerald Guninita, mara baada ya kufungua mafunzo ya ujasiriamali kwa wakuu hao, iliyoandaliwa na PSPF jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2016. Waziri Simbachawene alimwakilisha Rais John Magufuli. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, George Yambesi

 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, akitoa hotuba yake
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akitoa hotuba yake kuelezea huduma na fursa mbalimbali zilizopo kwenye Mfuko, wakati wa Mafunzo hayo
 Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, (TAKUKURU), Dkt. Edward Hosea, ambaye pia ni Mwanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mafunzo hayo kwa wakuu wa wilaya wastaafu
 Baadhi ya washiriki
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSPF, akimkabidhi kadi ya kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashantu Kijaji kupitia mpango wa PSS
 Maafisa wa PSPF, wakifuatilia mafunzo hayo
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashantu Kijaji, (kulia), akiongozana na Meneja Masoko, na Mawasiliano wa PSPF, Costantina Martin, wakati wa mapumziko
Waziri Simbachawene akitoa hotuba yake

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (katikati), akimkabidhi kadi ya kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Katibu wa Wakuu wa  Wilaya Mstaafu, Betty Mkwasa,  mara baada ya kufungua mafunzo ya ujasiriamali kwa wakuu hao, iliyoandaliwa na PSPF jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2016. Waziri Simbachawene alimwakilisha Rais John Magufuli. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, George Yambesi

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (kulia),akimkabidhi kadi ya kujiunga na uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mkuu wa Wilaya Mstaafu, Gerald Guninita, mara baada ya kufungua mafunzo ya ujasiriamali kwa wakuu hao, iliyoandaliwa na PSPF jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2016. Waziri Simbachawene alimwakilisha Rais John Magufuli. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, George Yambesi

 Mkuu wa wilaya mstaafu Manju Msambya, akitoa neno la shukrani
 Waziri Simbachawene, akkimsikiliza aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Omar Mangochie(kulia)
 Washiriki wakifuatilia kwa kusoma vipeperushi na kusikiliza


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (katikati), akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kufungua mafunzo ya siku mbili kwa wakuu wa wilaya wastaafu iliyoandaliwa na PSPF na kufanyika Agosti 15, 2016. Waziri Simbachawene alimwakilisha Rais John Magufuli. Wenine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt.Ashantu Kijaji,Mwenyekiti wa Wakuu haoi wa Wilaya wastaafu, Ramadhan Maneno, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSPF, George Yambesi, na Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (kulia), Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt.Ashantu Kijaji, (katikati), wakionyesha fomu za kujiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kupitia mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), mara baada ya waziri kufungua mafunzo ya siku mbili kwa Wakuu wa Wilaya wastaafu, na Wanachama wastaafu wa Mfuko jijin Dar es Salaam, jana Agosti 15, 2016. Wazuru alimwakilisha Rais John Magufuli kufungua mafunzo hayo. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu
Mtaalamu wa Saikolojia Dkt. Chris Mauki, akitoa mada juu ya kudhibiti Stress
 Picha ya pamoja na viongozi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF
 Picha ya pamoja ya mgeni rasmi, viongozi wa PSPF, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango na kamati tendaji ya wakuu wa wilaya wastaafu
 Wakurugeni wa PSPF
 Mkurugenzi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji, Beng' Issa, akitoa mada juu ya fursa zilizopo za uwezeshaji kwa watanzania
Dkt. Kijaji akiteta jambo na Mkuu wa wilaya mstaafu, Betty Mkwasa


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), George Simbachawene, (kulia), akifurahia jambo baada ya kukabidhiwa kadi ya uanachama wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, kupitia Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS), kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, George Yambesi. Waziri Simbachawene, alijiunga na Mfuko huo mara baada ya kufungua mafunzo ya siku mbili ya ujasiriamali kwa wakuu wa wilaya wastaafu na maafisa wastaafu wa serikali kwa niaba ya Rais John Magufuli jijini Dar es Salaam Agosti 15, 2016.