NEC: AJIRA ZA WATENDAJI WA UCHAGUZI ZIZINGATIE SIFA NA UWEZO

August 10, 2023

 

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Rufaa (Mstaafu) Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakati akifunga mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi, wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na maafisa uchaguzi mkoani Morogoro leo tarehe 10 Agosti, 2023.
Sehemu ya wasimamizi wa uchaguzi, wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na maafisa uchaguzi wakimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakati akifunga mafunzo hayo Mkoani Morogoro leo. 

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imewakumbusha Wasimamzi wa Uchaguzi kutekeleza wajibu wao kwa kuhakikisha kwamba ajira za watendaji wa uchaguzi zinazingatia sifa na uwezo.

Ukumbusho huo umefanywa na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Rufaa (Mstaafu) Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk mkoani Morogoro leo tarehe 10 Agosti, 2023 wakati akifunga mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi, wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi na maafisa uchaguzi.

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku tatu na kuhudhuriwa na washiriki 88 ni maandalizi ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbarali na kata sita za Tanzania Bara.

“Tunayo imani kuwa mtateua na kuajiri watendaji wenye sifa na uwezo wa kufanya kazi hii muhimu, jambo hili limekuwa likisisitizwa tokea siku ya kwanza ya mafunzo kwa kuwa hao ndio watakaosimamia zoezi la kupiga kura na kuhesabu kura vituoni. Kazi ambayo inahitaji umahiri, umakini na weledi katika kuitekeleza,” amesema Jaji Mbarouk.

Amesisitiza juu ya kuhakikisha kwamba mafunzo kwa watendaji wa vituo vya kupigia kura yanafanywa kwa ufanisi ili wawe na uelewa na kuweza kufanya kazi zao kwa usahihi na kujiamini.

 “Ni imani yetu kuwa mafunzo ya watendaji wa vituo yatafanyika kwa ufanisi na weledi katika tarehe zilizopangwa kwenye ratiba ya utekelezaji wa shughuli za uchaguzi. Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo ili waweze kufahamu majukumu yao na kuyatekeleza ipasavyo wakati wa uchaguzi,” amesema Jaji Mbarouk.

Aidha, amewahimiza watendaji wa uchaguzi kutenga muda kujisomea ili kupata ufahamu wa sheria, kanuni na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

“Natumia nafasi hii kuendelea kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kutenga sehemu ya muda wenu kusoma Katiba, Sheria na Maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume ili yawaongoze katika kusimamia uchaguzi utakaokuwa huru na wa haki,” amesema.

Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbarali na kata sita za Tanzania Bara utafanyika tarehe 19 Septemba, 2023, wagombea watachukua fomu kuanzia tarehe 13 hadi 19 Agosti, 2023, siku ya uteuzi itakuwa tarehe 19 Agosti, 2023 na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia tarehe 20 Agosti, 2023 hadi tarehe 18 Septemba, 2023.

Kata zitakazofanya uchaguzi mdogo ni; Nala iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, mkoani Dodoma, Mwaniko iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, mkoani Mwanza, Old Moshi Magharibi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi na Marangu Kitowo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro, Mtyangimbole iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba na Mfaranyaki iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma.

DC KAJI AWATAKA WALIMU KUTUMIA BENKI YA NMB KUWEZA KUJIKWAMUA KIUCHUMI

August 10, 2023

MKUU wa wilaya ya Tanga James Kaji akizungumza wakati alipomwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema  katika kongamano la siku ya  Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo.
MKUU wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
MKUU wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
MKUU wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Ladislaus Baraka akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji,ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Ladislaus Baraka akizungumza wakati wa kongamano la siku ya Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji,ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema
sehemu ya Walimu kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Tanga wakifuatilia kwa umakini Kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyemaha
sehemu ya Walimu kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Tanga wakifuatilia kwa umakini Kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema

sehemu ya Walimu kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Tanga wakifuatilia kwa umakini Kongamano la siku ya walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo na kufunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga James Kaji, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema


 Na Oscar Assenga, TANGA.


MKUU wa wilaya ya Tanga James Kaji amewataka walimu mkoani humo kuhakikisha wanaitumia benki ya NMB kutokana na bidhaa zao wanazotoa za mikopo ambazo zimeweza kuwainua kimapato na hatimaye kuwakwamua kiuchumi badala ya kujiingiza kwenye mikopo kandamizi.

Kaji aliyasema hayo  wakati alipomwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema  katika kongamano la siku ya  Walimu wa Mkoa wa Tanga lililoandaliwa na Benki ya NMB na kufanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Jijini humo.

Ambapo alisema kwamba hilo ni kutokana na kwamba benki hiyo kusheheni huduma mbalimbali ambazo wanaweza kuzitumia katikaa kujikwamua kiuchumi na kuondokana na mikopo kandamizi.

“Niwapongeza NMB kwa kuandaa Kongamano hili kwa walimu ni ya kipekee kwani nimetoa msisitizo kwa kutumia nguvu nyingi kuwezesha walimu kwenye shule za Msingi na Sekondari kwani wamekuwa wakiishi kwenye mazingira magumu  kutokana na kujiuingiza kwenye mikopo umiza”Alisema

Aidha alisema mikopo hiyo imekuwa ikiwaumiza na hivyo kupelekea kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kuweza kufundisha kutokana na kutumia muda mwingi kufikiria namna ya kuirejesha.

“Warsha hii imekuja wakati muafaka na niipongeza NMB nitoa wito kwa walimu kuweza kutumia NMB kutokana na bidhaa zao wanazotoa za mikopo ambapo lakini tumeshuhudia jinsi benki ilivyoweza kuwainua kimapato na kuweza kuboresha maisha yao hali inayoongeza uwezo kwenye utumishi wa kazi zao za kila siku”Alisema

Awali akizungumza Mkuu wa Kitengo cha Bima wa Benki ya NMB Makao Makuu Martin Massawe alisema kwamba wamezindua mpango maalumu kwa ajili ya walimu ambao waliuita “Specho” na wamekuja Tanga kutoa elimu zaidi na kusisitiza juu ya huo mpango unaomwezesha mwalimu kupata mikopo yenye riba nafuu ikiwemo ya kujiendeleza kielimu wao na watoto wao.

Alisema pia wanatoa mikipo ya biashara ndogo ndogo ,ujenzi,vyombo vya moto kama bodaboda na pikipiki za miguu mitatu ikiwemo kupata mkopo wa bima yaani Insurance Premium Finance (IPF) ambayo inawezesha walimu kulipa bima kujikinga na majanga mbalimbali.

“Lakini pia tunatoa mikopo ya pembejeo na mashine za kilimo fursa za kushiriki promosheni na kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo elimu ya kifedha kwa walimu na kadhalika”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Tafiti zinaonyesha kati ya watanzania milioni 60,ni asilimia 22 tu ndio wenye akaunti za benki pia zaidi ya asilimia 70 ya watanzania wanaamiliki simu za mkononi na wana uwezo wa kufanya malipo na miamala kupitia simu zao za mkononi.

“Kwa kulitambua hilo benki yenu ya NMB imeendelea kuja na masuhulisho mbalimbali yanayohusu makundi tofauti tofauti kama hili la walimu kama njia mojawapo ya kuleta watanzania zaidi kwenye mifumo rasmi ya kifedha na kuipatia Serikali mapato kupitia masuluhisho hayo pia benki imeweza kufikishja asilimia 94 ya miamala yake kupitia simu za mkononi”Alisema

Hata hivyo alisema hivi karibuni wamezindua huduma kubwa tatu ambazo zinaendelea kuleta mapinduzi makubwa katika sekta hya kibenki Tanzania ambazo ni mikopo kidigitali (MshikoFasta),NMB Pesa Wakala na NMB Lipa Mkononi.

Alisemna kupitia mifumo hiyo wameweza kuwafikia watanzania wengi zaidi na hivyo kuchangia kuongeza idadi ya watanzania wanaotumia huduma za kibenki na pia hata kuwasaidia walimu ambao wanaweza wakawa mbali na matawi ya benki.

Naye kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Ladislaus Baraka alisema siku ya mwalimu kwa benki ya  NMB ilianzia mkoa wa Tanga miaka ya nyuma wilaya ya Korogwe kwa zaidi ya miaka 7 iliyopita na wameendelea kuboresha huduma zao.

Alisema  kwa sababu walimu wameendelea nao wafanye nini na niwashukuru walimu mmekuwa wateja wote wa thamani sana kutokana na walimu kuwa chachu kubwa kwao kubioresha huduma zao wanazotoa kwa mikopo na hudumaza bidhaa mbalimbali na mwaka 2005 walikuwa wanaliopa mishaha kupitia madirisha yaliyokuwa halmshauri na baada kupitia benki .