KAYA 58 ZENYE WANANCHI 228 NA MIFUGO 350 ZAHAMA HIFADHI YA NGORONGORO

September 07, 2024

 

Na Mwandishi wetu, Ngorongoro.
Katika muendelezo wa hamasa ya wananchi wa Ngorongoro kujiandikisha kuhama kwa hiari, leo tarehe 7 Septemba, 2024 jumla ya kaya 58 zenye wananchi 228 na mifugo 350 wamehama katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Kijiji cha Msomera na maeneo mengine waliyochagua katika wilaya za Monduli, Meatu na Simanjiro.

Akitoa taarifa wakati wa kuaga kundi la 19 la awamu ya pili linalohama kutoka hifadhi ya Ngorongoro, Meneja mradi wa kuhamisha wananchi wa Ngorongoro Afisa Uhifadhi Mkuu Flora Assey ameeleza kuwa, kati ya kaya  58 zilizohama leo, kaya 30 zenye watu 151 na mifugo 235 zinahamia Kijiji cha Msomera,  Kaya 28 zenye watu 78 na mifugo 115 zinakwenda maeneo mengine waliyochagua katika wilaya za Monduli Mkoani Arusha,  Meatu mkoani Simiyu na Simanjiro katika mkoa wa Manyara.

Amebainisha kuwa tangu zoezi la kuhamisha wananchi kwa hiari lilivyoanza mwezi Juni 2022 hadi kufikia leo Septemba 7, 2024 Jumla ya kaya 1,627 zenye watu 9,778 na mifugo 40,051 zimeshahama ndani ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro
Akiaga kundi hilo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Katibu tawala wa Wilaya hiyo Bw. Hamza Hussen Hamza ameeleza kuwa, muitikio wa wananchi kuendelea kuhama ndani ya hifadhi hiyo unasaidia kupunguza shughuli za kibinadamu hifadhini, kupunguza changamoto kwa wananchi wanazokutana nazo kwa kuishi na wanyamapori wakali na hatarishi, kukosa uhuru wa kumiliki vyombo vya moto na kufanya shughuli za kiuchumi pamoja na  kukosa uhuru wa kutembea ndani ya hifadhi baada ya saa 12 jioni.

“Tunawapongeza sana kwa maamuzi ya kuhama hifadhini kwa ajili ya kupisha shughuli za uhifadhi, maeneo mnayohamia Serikali imeshawajengea huduma muhimu kama shule, zahanati, maji, majosho, mawasiliano, nishati ya umeme, makazi bora pamoja na mashamba ya kilimo na malisho. Pamoja na zoezi hili la kuhama kuendelea, niwahakikishie wananchi ambao bado hawajaamua kuhama kuwa Serikali itaendelea kutoa huduma za kijamii na katika utekelezaji wa zoezi hili tutaendelea kuzingatia misingi ya sheria, kanuni, taratibu na haki za binaadamu” aliongeza Hamza.
Mwakilishi wa kamishna wa Uhifadhi NCAA, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya maendeleo ya Jamii, Gloria Bideberi ameainisha kuwa, Serikali kupitia NCAA inaendelea na zoezi la kuelimisha, kuandikisha na kuhamisha wananchi wanaohama kwa hiari na kuongeza kuwa mwananchi anayejiandikisha akishathaminishiwa mali zake, taratibu za malipo hufanyika kwa muda mfupi na ndani ya wiki mbili mwananchi husika anahamishwa kutoka ndani ya hifadhi.

Kamishna Bideberi ameongeza kuwa sambamba na zoezi la kuhamisha wananhi wanaojiandikisha kuhama kwa hiari, shughuli za uhifadhi na utalii zinaendelea vizuri, maeneo wananchi waliyohama tayari uoto wa asili umeanza kurejea na wageni kutoka ndani na nje ya nchi wanaendelea kutembelea kwa wingi vivutio vya utalii vilivyoko katika hifadhi hiyo. 
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wanaohama kwa hiari, Elizabeth Saiboko kutoka Kijiji cha Nainokanoka amebainisha kuwa ameamua kuhama ndani ya hifadhi ili kuwa huru zaidi na kutafuta kesho iliyobora kwa watoto wake kwa kuwa katika tarafa ya Ngorongoro sheria za uhifadhi zinauiya baadhi ya shughuli za kiuchumi kama kilimo, ujenzi wa nyumba za kudumu, kumiliki vyombo vya moto na uhuru wa kutembea  kwa saa 24 tofauti na maeneo mengine nje ya hifadhi.

WAHITIMU WA CHUO CHA PASIANSI NI HAZINA ADHIMU KWA MALIASILI NA UTALII NCHINI.

WAHITIMU WA CHUO CHA PASIANSI NI HAZINA ADHIMU KWA MALIASILI NA UTALII NCHINI.

September 07, 2024


Na Sixmund J. Begashe

Sekta binafsi wanaojishughulisha na uhifadhi wa wanyamapori au biashara zinazoendana na uhifadhi wa wanyampori zimetakiwa kutoa nafasi za ajira kwa vijana waliohitimu katika Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi ili kuongeza tija katika shughuli za Uhifadhi na Utalii kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea wanachi maendeleo kupitia Maliasili na Utalii.

Wito huo umetolewa kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dunstan Kitandula Jijini Mwanza, kwenye mahafali ya 59 ya Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi.

Mhe. Kitandula amesema wahitimu wa mafunzo ya Uaskari wa Wanyamapori na Himasheria, Uongozaji na Usalama wa Watalii na mafunzo ya muda mfupi kwa askari wa vijiji kutoka maeneo mbalimbali ni azina muhimu kwa Uhifadhi na Utalii hivyo ni vyema ikatumika vizuri kwa maslai mapana ya Taifa.

Aidha Mhe. Kitandula anetumia fursa hiyo kuwapongeza na kuwashukuru wafadhili wa Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW) kwa kulipia ada za masomo na mahitaji mengine iliyofanikisha kuhitimu mafunzo kwa baadhi ya wanachuo hao.

Akitoa Taarifa ya mafunzo hayo Mkuu wa Chuo hicho Bw. Jeremiah Msigwa amefafanua kuwa kati ya wanachuo 374 waliodahiliwa,Wanachuo 354 wamepewa vyeti vya kuhitimu mafunzo kulingana na viwango (grade) mbalimbali vya ufaulu wakiwemo wanachuo 222 wa kozi ya BTCWLE, 70 wa kozi ya TCWLE; 34 wa kozi ya BTCTGTS na 04 wa kozi ya TCTGTS.


SERIKALI YAAGIZA SHERIA YA USAJILI JUMUIYA KUZINGATIWA

September 07, 2024

 




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na Mkewe Mama Mbonimpaye Mpango wakikabidhiwa zawadi ya Biblia Takatifu kutoka kwa Muasisi wa Kanisa la New Life Outreach Tanzania Mwinjilisti Dkt. Egon Falk na Mkewe Bi. Hanna Falk mara baada ya kushiriki kilele cha Sherehe za Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 50 ya Kanisa la New Life Outreach Tanzania iliyofanyika katika kanisa hilo eneo la Sakina mkoani Arusha tarehe 07 Septemba 2024.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akishiriki kilele cha Sherehe za Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 50 ya Kanisa la New Life Outreach Tanzania iliyofanyika katika kanisa hilo eneo la Sakina mkoani Arusha tarehe 07 Septemba 2024.

Na Mwandishi wetu, Arusha

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa rai kwa viongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Ofisi ya Msajili wa Jumuiya, kusimamia kikamilifu Sheria ya Usajili wa Jumuiya pamoja na kanuni zake ili kuhakikisha kuwa Taasisi zinazosajiliwa zikiwemo za kidini zinatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia malengo na masharti ya usajili wake.

Makamu wa Rais ametoa rai hiyo wakati alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kilele cha Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 50 ya Kanisa la New Life Outreach iliyofanyika katika kanisa hilo Sakina mkoani Arusha. Amesema hivi sasa yameibuka mafundisho ya baadhi ya viongozi wa dini yanayowaaminisha wafuasi wao kutegemea miujiza zaidi ili kupata maendeleo badala ya kufanya kazi kwa bidii.

Ameongeza kwamba imeshuhudiwa kuongezeka kwa wahubiri wanaojilimbikizia fedha na mali binafsi kutokana na sadaka na mauzo ya vitu mbalimbali na wengi wa wahanga wa mahubiri ya aina hiyo ni wananchi wanaokabiliwa na shida au matatizo mbalimbali ya maisha.

Makamu wa Rais amewasihi viongozi wa dini kuungana na serikali kukemea vikali mafundisho na matendo hayo yasiyofaa katika jamii na yasiyozingatia sheria za nchi. Pia ametoa wito kwa viongozi wote kuwahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii, maarifa na uzalendo, huku wakimuomba Mwenyezi Mungu abariki kazi zao.

Halikadhalika Makamu wa Rais amesema hivi sasa kuna mmomonyoko mkubwa wa maadili katika jamii hali inayopelekewa na matumizi holela ya mitandao ya kijamii, ambapo wananchi hususan vijana wengi wanadhani ili kuwa kijana wa kisasa, inawalazimu kuiga mambo yanayooneshwa kwenye mitandao hiyo yakiwemo yale yasiyo endana na mila na desturi.

Amesema kukosekana kwa hofu ya Mungu katika jamii kunapelekea kuongezeka kwa matukio ya mauaji ya kikatili, ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto na wanawake, familia za mzazi mmoja, watoto waliozaliwa nje ya ndoa, migogoro ya ndoa, talaka, migogoro ya mirathi na ardhi, ubadhirifu wa mali za umma na matukio ya watu kujinyonga.
Aidha Makamu wa Rais amekemea tabia za uzembe na kutozingatia sheria za usalama barabarani ambazo zimepelekea kushamiri kwa ajali mbaya za barabarani zinazogharimu maisha ya wananchi wengi.

Ametoa rai kwa wakaguzi wa magari wa LATRA na Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani kutimiza wajibu wao ili kudhibiti magari mabovu yasiingie barabarani na kuhakikisha vidhibiti mwendo vinafanya kazi, pamoja na kukagua sifa za madereva hasa wa mabasi ya abiria na malori. 

Ameongeza kwamba wamiliki wa Mabasi na Malori wanapaswa kuhakikisha magari yao yanakuwa na madereva walau 2 kwa safari zote ndefu zinazozidi kilomita 300. Vilevile ameagiza Wakala ya Barabara Nchini (TANROADS) kuhakikisha alama za tahadhari zinawekwa katika maeneo yote hatarishi ya barabara kuu.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa wasafiri wote nchini kuzingatia kufunga mikanda wakati wote wa safari na kutoa taarifa kwa Kikosi cha Usalama Barabarani pale dereva wa chombo wanachosafiria anapoendesha kwa mwendo mkali kupita kiasi.

Pia Makamu wa Rais amewasihi viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla kushirikiana na serikali katika kukabiliana na athari za uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Amesema uhai wa wanadamu katika dunia unatishiwa na uharibifu wa mazingira ambao umekithiri ambapo pamoja na jitihada mbalimbali za kitaifa na kimataifa zinazochukuliwa kukabiliana na hali hiyo, lakini bado matokeo yake si ya kuridhisha. 

Ameongeza kwamba uharibifu wa misitu na ukataji wa miti unaonekana katika maeneo mbalimbali ya nchi ikiwemo mkoani Arusha.
Makamu wa Rais amesema Serikali itaendelea kuenzi mchango mkubwa wa madhehebu ya Dini, katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii na itaendelea kusimamia na kulinda haki ya kuabudu kwa wananchi wote kwa mujibu wa ibara ya 19 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kwamba wananchi wanaendelea kuishi katika mazingira ya haki na amani.

Kwa upande wake Muasisi wa Kanisa la New Life Outreach Tanzania Mwinjilisti Dkt. Egon Falk ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa kibali cha kuhubiri neno la Mungu kwa miaka 50.

Amesema Kanisa hilo litaendelea kufuata sheria na taratibu za nchi wakati wa utoaji wa huduma ya kuhubiri neno la Mungu na huduma nyingine za kijamii. Kanisa hilo linamiliki Shule mbili za msingi na moja ya sekondari ambazo zimekuwa zikitoa ufadhili wa masomo kwa watoto wanaopitia mazingira magumu ya Maisha.
CHATANDA AZINDUA MSAADA WA KISHERIA INAYORATIBIWA NA KAMATI YA HAKI NA SHERIA YA UWT

CHATANDA AZINDUA MSAADA WA KISHERIA INAYORATIBIWA NA KAMATI YA HAKI NA SHERIA YA UWT

September 07, 2024





MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda, akizindua kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna_DODOMA


MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda ,amezindua kampeni ya msaada wa Kisheria inayoratibiwa na Kamati ya Haki na Sheria ya UWT yenye lengo la kuwasaidia wanawake na makundi maalum kupata haki ya msaada wa Kisheria nchini.

Bi.Chatanda akizungumza mara baada ya kuzindua kamati hiyo iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.

Amesema kuwa lengo la kampeni hiyo ni kuunga mkono jitihada za awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kupitia kampeni ya Mama Samia Legal Aid Chini ya Wizara ya Katiba na Sheria inayofanya vizuri kwa sasa.

“Kampeni hii ya utoaji wa msaada wa kisheria itakuwa inafanya kazi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi yenye lengo la kutoa huduma za msaada wa kisheria na kuhakikisha upatikanaji wa haki sawa kwa wote kwa kuzingatia zaidi wanawake ,wasichana,watu wanaoishi na ulemavu na makundi mengine hatarishi,”amesema Bi.Chatanda

Amesema kuwa UWT pamoja na wadau wengine wanalenga kuhakikisha kwamba elimu ya kisheria na msaada wa kisheria inafika kwa watu wote hasa wanawake na makundi maalum.

“UWT inalenga kuchangia jitihada za kuhakikisha upatikanaji wa haki kwa wote kuhusiana na matatizo ya ardhi,matukio ya ukatili wa kijinsia kwa watoto na wanawake urithi,Ndoa,kesi za madai na jinai.”amesema

Aidha ametoa maagizo kwa makatibu wa mikoa na wilaya kama watendaji kutoa ushirikiano wa kutosha pindi zoezi hilo la utoaji msaada wa kisheria litakapoaza kila jumamosi ya mwisho wa mwezi na kuhakikisha ripoti ya uendeshaji wa zoezi hilo.

Pia ametoa rai kwa wananchi hasa wanawake nchini kutumia fursa hiyo ya utoaji wa msaada wa kisheria ambayo imekwenda kuanza leo hapa Dodoma na baadae kwenye mikoa yote nchini kwa siku zijazo.ambapo kwenye viwanja vya Chinangali itakwenda kufanyika leo na kesho Septemba 8,2024.


kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo na Naibu Waziri TAMISEMI, Zainab Katimba amesema imeanzishwa kampeni ya msaada wa kisheria itakayoanza kwenye mikoa 10 na kila jumamosi ya mwisho wa mwezi kwenye ofisi za UWT kutakuwa na watoa msaada kisheria.

Mhe.Katimba amesema kuwa Wanawake, watoto na watu wenye mahitaji maalum ndio walengwa kwenye kampeni hiyo na wameandaa program maalum kufikia watoto shuleni ili kupata elimu ya kujilinda na ukatili.


” Tunaandaa kanzi data ya mawakili ambao wako ndani ya UWT Ili kuwa na timu kubwa ya watu watakao toa msaada kisheria kwa wananchi katika Mikoa waliyopo,”amesema Mhe.Katimba


Aidha amefafanua kuwa Rais Dk.Samia aliona wananchi wanahitaji msaada ndio maana alianzisha kampeni ya msaada wa kisheria ya mama Samia ambayo imekuwa na matokeo chanya

Katika hatua nyingine amesema kupitia kampeni hiyo wametengeneza programu ya kuwafikia watoto na kuwajengea uelewa namna ya kuepuka vitendo vya ukatili.

“Kutakuwa na programu maalumu ambayo itaaenda kuwafikia watoto na kutoa uelewa namna wanavyoweza kuepuka na vitendo vya ukatili,”amesema

Naye Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma Pili Mbaga ,amesema kuwa uzinduzi wa Kampeni hiyo imekuja wakati mwafaka kukiwa na matukio mengi yasiyofaa katika jamii.

“Kampeni hii imekuja wakati mwafaka kutokana na mambo ambayo yamekuwa yakijitokeza na tunaamini itakuwa muarobaini wa matukio,”amesem



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda, akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda,akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.





Mwenyekiti wa Kamati ya Haki na Sheria ya UWT, Zainab Katimba ,akielezea malengo ya kampeni hiyo wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



KATIBU wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma Bi.Pili Mbaga,akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septe.ba 7,2024 jijini Dodoma.



MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Mhe.Subira Mgalu,akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septe.ba 7,2024 jijini Dodoma.



SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda (hayupo pichani), wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda, akizindua kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.

WMA, TAKUKURU WATEKELEZA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA

September 07, 2024

 Na Veronica Simba, WMA Dodoma


Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Dodoma imetoa elimu ya vipimo kwa Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), hivyo kutimiza maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan yanayozitaka Mamlaka na Taasisi za Umma kupanga na kutekeleza kwa pamoja majukumu mbalimbali ya Serikali.

Akifungua Semina hiyo ya siku moja iliyofanyika jijini Dodoma, Septemba 6, 2024, Katibu Tawala wa Mkoa, Kaspar Mmuya amepongeza ushirikiano wa Taasisi hizo mbili unaolenga kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais na kuwahudumia wananchi ipasavyo.

“Nimefurahishwa na ushirikiano wa Taasisi hizi mbili wenye lengo la kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuhusu dhana ya kufikiri kwa pamoja na kutenda kwa pamoja kama Serikali.”

Aidha, Katibu Tawala Mmuya amewataka washiriki kutumia semina hiyo kupambanua endapo kuna mapungufu yoyote katika Sheria ya Vipimo inayosimamiwa na WMA na kutafuta suluhisho la pamoja ili kuboresha utekelezaji wake.

Vilevile, amewataka WMA kuendelea kutoa elimu ya vipimo kwa wafanyabiashara na walaji ili pande zote mbili zipate kilicho stahiki. Pia, ameongeza kwamba katika utoaji elimu, wakulima waeleweshwe kuachana na utamaduni wa kutumia madalali bali wauze mazao yao katika maghala.

“Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo kwamba mazao yauzwe kwenye maghala na huko kwenye maghala kuwe na mizani ambazo zimekaguliwa na kuhakikiwa na Wakala wa Vipimo ili kumlinda mlaji na mfanyabiashara,” ameeleza Mmuya.

Mmuya ametoa wito kwa wafanyabiashara, walaji wa bidhaa na huduma mbalimbali kuzingatia matumizi ya vipimo sahihi na kuwakumbusha kwamba sheria ya vipimo imewapa WMA mamlaka ya kutoza faini kwa yeyote atakayekiuka mwongozo wa sheria hiyo.

Amewataka WMA na TAKUKURU kuwa mfano kwa sheria wanazozisimamia na kuchukuliana hatua baina yao endapo kutabainika ukiukwaji wa sheria.

“TAKUKURU, mtumishi yeyote wa WMA akitenda ndivyo sivyo kwa kujihusisha na rushwa basi achukuliwe hatua, vivyo hivyo kwa WMA, mkibaini mtumishi wa TAKUKURU anajihusisha na uvunjifu wa sheria ya vipimo katika shughuli zake kama mtanzania wa kawaida ikiwemo kilimo, biashara na nyinginezo, msisite kumchukulia hatua,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa WMA Mkoa wa Dodoma, Karim Zuberi amesema lengo la kutoa semina hiyo kwa watumishi wa TAKUKURU ambao ni watumiaji wa vipimo, ni kuwapatia uelewa ili wajue haki zao wanaponunua bidhaa au kupata huduma mbalimbali.

“Kupitia semina hii watapata uelewa ni kwa namna gani kipimo kinatakiwa kuwa kabla, wakati na baada ya kununua bidhaa au kupata huduma,” amesema Zuberi.

Vilevile, amesema malengo mengine ni kutekeleza moja ya majukumu ya WMA ambalo ni utoaji elimu ya vipimo kwa jamii kupitia makundi mbalimbali kama wafanyabiashara, viongozi, wanasiasa, watumishi wa umma na mengineyo ambapo TAKUKURU ni kundi mojawapo.

Amesema, lengo jingine ni kupata maoni ya TAKUKURU kuhusu namna bora ya kutekeleza sheria ya vipimo endapo watabaini mapungufu wakati wa uwasilishwaji mada katika semina husika.

Naye Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Dodoma, Victor Swela ameishukuru WMA kuona umuhimu wa kuandaa semina hiyo ili kuwajengea uelewa wa masuala ya kivipimo hivyo kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kiufanisi katika sekta hiyo.

“Tutashirikiana na wenzetu wa WMA kuwaelimisha wananchi na kusimamia kuhakikisha kila upande unazingatia matumizi ya vipimo sahihi kwa manufaa ya pande zote yaani wafanyabiashara na walaji.”
PIC%201C
Mgeni Rasmi, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Kaspar Mmuya, akizungumza wakati akifungua semina kuhusu matumizi ya vipimo sahihi iliyoandaliwa na Wakala wa Vipimo (WMA), Mkoa wa Dodoma kwa watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Septemba 06, 2024 jijini Dodoma.
PIC%202
Meneja, Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Dodoma, Karim Zuberi akizungumza wakati wa semina kuhusu matumizi ya vipimo sahihi iliyoandaliwa WMA, kwa watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Septemba 06, 2024 jijini Dodoma.
PIC%203B
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Dodoma, Victor Swela akizungumza wakati wa semina kuhusu matumizi ya vipimo sahihi iliyoandaliwa na Wakala wa Vipimo (WMA), Mkoa wa Dodoma kwa watumishi wa TAKUKURU, Septemba 06, 2024 jijini Dodoma.
PIC%204i
PIC%204G
Sehemu ya watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Dodoma wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa semina kuhusu matumizi ya vipimo sahihi iliyoandaliwa na Wakala wa Vipimo (WMA), Mkoa wa Dodoma kwa watumishi wa TAKUKURU, Septemba 06, 2024 jijini Dodoma.

PIANO SUNDAYS ARE GOLDEN WITH JOHNNIE WALKER: DJ KAYGEE TAKES THE STAGE AT 1245

September 07, 2024
The buzz from last weekend's Piano Sunday at 1245 in partnership with Serengeti Breweries (SBL), is still reverberating through the city. As promised, the night was nothing short of spectacle, featuring a dazzling array of entertainment and indulgence.

RAIS DK. MWINYI KUSHIRIKI SHEREHE ZA MIAKA 50 YA SIKU YA USHINDI MSUMBIJI

September 07, 2024

 




RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amewasili jijini Maputo, Msumbiji akitokea Indonesia na kupokewa kwa gwaride maalum na ujumbe wake akiwemo Mkewe Mama Mariam Mwinyi.

Katika uwanja wa ndege wa Maputo amepokelewa na viongozi mbalimbali wa juu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Msumbiji akiwemo Waziri wa Afya wa nchi hiyo.

Rais Dk. Mwinyi atashiriki Sherehe za Miaka 50 ya Siku ya Ushindi nchini Msumbiji.

Kuhudhuria kwake katika sherehe hizo kunatokana na mualiko Maalum kutoka kwa mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi.

📅 07 Septemba 2024 📍Maputo, Msumbiji




RAIS SAMIA AWAHIMIZA DIASPORA KUWEKEZA NCHINI

September 07, 2024

 


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Watanzania wakiwemo wafanyakazi, wanafunzi na wafanyabiashara wanaoishi nchini China (Diaspora) kwenye mkutano uliofanyika jijini Beijing tarehe 06 Septemba, 2024.


· Atumia saa 7 kuongea na Wawekezaji na Viongozi wa Makampuni
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa Watanzania wanaoishi nje ya Nchi (Diaspora) kuchangamkia fursa za uwekezaji zinazopatikana katika sekta mbalimbali nchini.

Rais Samia ametoa wito huo alipokuwa akizungumza na Diaspora waishio nchini China katika mkutano uliojumuisha watanzania wanaofanya kazi nchini humo, wafanyabiashara na wanafunzi uliofanyika jijini Beijing tarehe 6 Septemba 2024.

Akizungumza na Diaspora hao waliojitokeza kwa wingi, wakionesha furaha na shauku kubwa ya kuzungumza na Rais Samia, aliwaeleza kuwa licha ya fursa lukuki za kiuchumi zilizopo nchini Serikali imefanya maboresho ya sera na sheria mbalimbali ili kutoa fursa na kutanua wigo kwa Diaspora kuwekeza nchini.

Rais Samia amezitaja fursa hizo zinazopatikana katika sekta mbalimbali ikiwemo ujenzi, viwanda, kilimo na madini. Aliongeza kufafanua kuwa, katika sekta ya ujenzi hivi sasa Serikali imeandaa utaratibu mahususi kwa Diaspora, unaowapa fursa ya kujengewa na kumiliki nyumba nchini.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwaeleza Diaspora kuhusu hatua liyopigwa na Serikali katika kuboresha utoaji huduma za kijamii kwa Wananchi katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, na usafirishaji akitolea mfano wa treni iendayo kwa haraka (SGR) ambayo katika kipindi kifupi imeleta mageuzi makubwa kwenye sekta hiyo na ujenzi wake ukiwa unaendelea. Sekta zingine ni nishati, kilimo, maji, mawasiliano na ukuaji wa demokrasia.

“Nyumbani tuko vizuri, mfano sasa hivi safari ya kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma inachukua saa 3 hadi 4 pekee kwa kutumia treni yetu mpya tuliyoizindua hivi karibuni. Tumefanya maboresho makubwa ya sera na sheria ili kuwapa fursa ya kuendesha shughuli za kiuchumi kwa urahisi. Njoeni muwekeze nymbani”. Alisema Rais Samia.

Mbali na hayo amepongeza juhudi na uzalendo unaoendelea kuonyeshwa na Diaspora katika kuchangia shughuli za maendeleo nchini ikiwemo kuleta watalii, wawekezaji na kusaidia kuratibu shughuli za matibabu. Aliongeza kusema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la fedha zinazotumwa nyumbani (remittance) kutoka ughaibuni,

Vilevile, Rais Samia ametoa wito kwa Diaspora wa nchini humo na kwa nchi zingine, hususan kwa jamii ya wanafunzi kujiandisha katika vyama vyao vya Jumuiya kwenye maeneo waliyopo. Akasisitiza kuwa hatua hiyo hiyo, licha kusadia kutambuana na kukuza umoja wao inarahisisha namna ya kuwafikia wanapohitaji huma mbalimbali hasa wakati zinapotokea changamoto ikiwemo majanga kama vile mlipuko wa magonjwa.



Katika hatua nyingine Rais Samia akiwa jijini Beijing amekutana na kufanya mazungumzo na Wawekezaji na Viongozi wa Makampuni Sita (6) makubwa ya nchini humo ikiwemo China Academy of Space Corporation (CASC), China Electronics Corporation, Transsion Group, Weihua Group, China Railway Construction Corporation (CRCC), Acme Consultant Engineers PTE Limited na CND jijini Beijing, tarehe 06 Septemba, 2024.



Katika zoezi hilo alilolifanya kwa takribani saa 7 mfulilulizo bila mapunziko, aliambatana na Watendandaji na Mawaziri wanaosimamia sekta mbalimbali wakiwemo; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabiti Kombo (Mb.), Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb.), Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda – Zanzibar Mhe. Omar Said Shaaban, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Alexander Mkumbo (Mb.), Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega (Mb.).

Wengine ni Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde (Mb.) Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Bw. Mohamed Khamis Abdullah na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Bw. Gilead Teri.

Rais Samia alikuwa nchini China kushiriki Mkutano wa Kilele wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika tarehe 4-6 Septemba 2024.




Matukio mbalimbali wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungu na Wawekezaji na Viongozi wa Makampuni mbalimbali ya China Academy of Space Corporation (CASC), China Electronics Corporation, Transsion Group, Weihua Group, China Railway Construction Corporation (CRCC) pamoja na Acme Consultant Engineers PTE Limited na CND ya nchini China jijini Beijing, China tarehe 06 Septemba.

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AAPISHWA KUWA KAMISHNA WA TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA, AAHIDI USHIRIKIANO

September 07, 2024

  

Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, Prof. Ibrahim Hamis Juma Kushoto akimuapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Hamza Johari kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Septemba 07, 2024 jijini Dar es salaam.

Jaji Mkuu wa Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Prof. Ibrahim, Hamis Juma akizungumza mara baada ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari kuwa Kamishna wa TumeTume ya Utumishi wa Mahakama Septemba 07, 2024 jijini Dar es salaam.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuapishwa kuwa Kamishna wa TumeTume ya Utumishi wa Mahakama Septemba 07, 2024 jijini Dar es salaam.



Picha ya pamoja.

Na Avila Kakingo, Michuzi Tv
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali ni mtu muhimu sana sio tu kwa mahakama bali Bunge na serikali na pengine ndio maana hula viapo vitatu ikionesha umuhimu wa nafasi yake.

Hayo yamesemwa leo Septemba 07, 2024 na Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Hamis Juma wakati wa kumuapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari kuwa Kamishna n mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Mahakama.

Amesema kuwa ndio maana anakula viapo vitatu, ambapo ni viongozi wachache sana wanakula viapo vingi zaidi kuliko wengine.

"Hii inaonesha umuhimu wa nafasi yake kutokana na kuwa mtetezi mkuu wa Mahakama mara nyingi watu huwa hawauoni umuhimu wake ...." 

Prof. Juma amesema kuwa kama kunatokea mkwaruzano wowote na kiongozi wa muhimili mwingine au akivuka anga na kuingia kwenye anga la Mahakama kwa kutokujua amesema wananjia nyingi za mashauriano kwa kutumia Mwanasheria mkuu wa Serikali kufikisha ujumbe na kuelimishana kwamba hayo simajukumu yake ni majukumu ya watu wengine kwa kufanya hivyo kumesaidia.

"Aliyevuka anga akielimishwa anashukuru sana anasema nilikuwa sijui kwamba hii anga nilikuwa sitakiwi kufika. Hizo ndio kazi kuu kwani anakuwa mtetezi wa mahakama na ametusaidia sana."

Pia Prof. Juma amemuasa ahakikishe anafahamu kila kitu kinachoendelea ndani ya mihimili ya serikali lakini pia twatatoa ushirikiano kwenye kila kitu muhimu, kama kuna nyaraka muhimu zimetoka, sera   ni muhimu aelewe, kwani hajui taarifa zitaenda kutumika wapi.

Kwa upande wa Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na aliyekuwa  Mwanasheria Mkuu wa Serikali,  Dkt. Eliezer Feleshi, amesema kuwa wana matumaini makubwa na Mwanasheria huyo katika usimaizi wa sheria. 

"Nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali ni nafasi ya pekee, anaiwezesha tume kuwa na afisa ambaye kwa dhamana yake anaingia akiwa na uwakilishi kwenye mihimili mingine ya serikali, yeye yupo serikalini anaingia kwenye mabaraza mengi na anaelewa nini kinaendelea Serikalini lakini pia anapoingia bungeni anahakikisha hakuna Matope. 

Pia asema kuwa atampa ushirikiano wa kutosha kwa kufanya kazi kwa ufanisi na  kumwezesha kufanya kazi kwa umahiri zaidi.

 Kwa upande wa  Mwanasheria mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa anatambua kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni daraja katika mihimili mitatu ya serikali.

Pia amesema atajitajidi kufanya kazi kwa pamoja, na kuhakikisha kwamba malengo ambayo watajiwekea watayatimiza.

"Nilazima sasa kama Ofisi ya Mwanasheria mkuu wa Serikali tuhakikishe kwamba tunatekeleza majukumu yetu ipasavyo na ule ushiriki wetu katika maeneo yote yanayohitaji mchango tutafanya hivyo kwa weledi lakini pia kwaharaka kutoa huduma ambazo ni bora na zenye tija kwa Taifa letu." Amesema Johari