WADAU WA SOKA SONGEA KUJADILI UREJESHWAJI WA MAJIMAJI LIGI KUU TANZANIA BARA
Na Mwandishi Wetu,Songea.
Kampuni
ya Tanzania Mwandi ikishirikiana na Majimaji FC, imeandaa mkutano wa wadau wote
wa soka mkoani Ruvuma chini ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mh. Said Mwambungu,
mkutano utakaofanyika katika ukumbi wa Centenary tarehe 10. 08. 2013, kuanzia
saa 2 asubuhi.
Lengo
kubwa la mkutano ni kurejesha makali ya 1985, 1986 na 1998 kwa klabu ya soka ya
Majimaji kwa kuiunda upya kiuchumi chini ya mfumo wa Kampuni, kuijengea uwezo
wa kimkakati na kiuendeshaji ili iweze kushiriki kwa mafanikio Ligi Daraja la
Kwanza na hatimaye kurejea Ligi Kuu msimu ujao.
Itakumbukwa
kuwa Majimaji FC ni klabu ambayo imezalisha magwiji wengi wa soka Tanzania kama
Abdala Kibadeni ‘Mputa’, Madaraka Suleimani ‘Mzee wa Kiminyio’, Peter Tino,
Steven Mapunda ‘Garincha’, Hamis Gaga, Idd Pazi, Omary Hussein ‘Machinga’ na
Mdachi Kombo na ni klabu ambayo ilikuwa na ushindani mkubwa kwa Simba na Yanga.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya Habari na Mkurugenzi Mtendaji wa
Kampuni ya Tanzania Mwandi, Bwana Teonas Aswile amewaalika wafadhili na wadau
wote wenye mapenzi mema na Majimaji FC kujitokeza na kushiriki katika zoezi la
mjadala wa muundo mpya wa Majimaji na hata kununua hisa kwani sasa Majimaji
Kampuni haitakuwa na longolongo zozote.
“Binafsi
nawahimiza wafadhili wa soka kwamba hii ni fursa adimu nyingine ya kuwekeza
fedha zao mahali salama. Majimaji itakuwa ikiendeshwa kikampuni na miradi
mbalimbali itaanzishwa na klabu ikiwemo upande wa ukandarasi na kuuza wachezaji
nje ya nchi. Kwahiyo atakayenunua hisa atafaidika mara mbili.” alisema Teonas
Aswile.
Akizungumzia
wachokoza mada wakuu wa Majimaji Revival Conference, Aswile amesema kuwa Wakala
wa Kimataifa wa FIFA na Mwanasheria Maarufu nchini, Dkt Damas Ndumbaro pamoja
na Bwana Silas Mwakibinga, mhasibu na mdau mkubwa wa michezo ambaye ameshashika
nafasi mbalimbali.
Kwa
sasa maandalizi kwaajili ya Mkutano wa Wadau wa Majimaji FC “Wanalizombe”
yanaendelea vyema na wanaohitaji taarifa wanaweza kuwasiliana na Bwana Nasib
Mahinya kwa 0655 468800.
Pia
viongozi wa Majimaji FC kama Katibu Mkuu Majimaji FC 0752 622887
Imetolwa
na;
Tanzania
Mwandi Co Ltd.
Phone:
+25522 2120677 or +255756 829071
Fax:
+255 22 2122976
Email:
ceo@tanzaniamwandi.co.tz,
Website: www.tanzaniamwandi.co.tz/events.html
RATIBA LIGI DARAJA LA KWANZA AGOSTI 14
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Ratiba
ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2013/2014 inayoshirikisha timu
24 zilizo katika makundi matatu zikicheza kwa mikondo miwili (nyumbani
na ugenini) inatarajiwa kutolewa Agosti 14 mwaka huu.
Kundi
A linaundwa na timu za Burkina Moro ya Morogoro, JKT Mlale (Ruvuma),
Kimondo SC (Mbeya), Kurugenzi Mufindi (Iringa), Majimaji (Ruvuma),
Mkamba Rangers (Morogoro), Polisi (Iringa) na Polisi (Morogoro).
African
Lyon (Dar es Salaam), Friends Rangers (Dar es Salaam), Green Warriors
(Dar es Salaam), Ndanda (Mtwara), Polisi (Dar es Salaam), Tessema (Dar
es Salaam), Transit Camp (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam)
zinaunda kundi B.
Timu
za kundi C ni JKT Kanembwa (Kigoma), Mwadui (Shinyanga), Pamba
(Mwanza), Polisi (Dodoma), Polisi (Mara), Polisi (Tabora), Stand United
(Shinyanga) na Toto Africans (Mwanza).
Tunapenda
kukumbusha kuwa dirisha la usajili kwa madaraja yote ni moja ambapo
usajili wa hatua ya kwanza ni kuanzia Juni 15 hadi Agosti 3 mwaka huu
wakati hatua ya pili ni Agosti 14 hadi 29 mwaka huu. Dirisha dogo
litafunguliwa Novemba 15 hadi Desemba 15 mwaka huu.
WAAMUZI VPL KUFANYA MTIHANI WA UTIMAMU WA MWILI
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Waamuzi
wote wa daraja la kwanza (Class I) wanaotaka kuchezesha Ligi Kuu ya
Vodacom (VPL) msimu wa 2013/2014 wanatakiwa kuhudhuria mtihani wa
utimamu wa mwili (physical fitness test) utakaofanyika katika vituo
viwili.
Mtihani
huo utafanyika Agosti 12,13 na14 mwaka huu katika vituo vya Dar es
Salaam na Morogoro. Kituo cha Mwanza kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya
Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Manyara, Mara, Mwanza, Shinyanga,
Simiyu, Singida na Tabora.
Kituo
cha Dar es Salaam kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya Arusha, Dar es
Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara,
Njombe, Pwani, Ruvuma na Tanga.
Washiriki
wote wanakumbushwa kuwa ni lazima wafuate utaratibu huo wa vituo, na si
vinginevyo. Pia waamuzi waliofungiwa (sio maisha) wanatakiwa kushiriki
katika mtihani huo.
MTIHANI WA UWAKALA WA WACHEZAJI, MECHI SEPT 26
Na Boniface Wambura ,Dar es Salaam.
Mtihani wa uwakala wa wachezaji (players agent) na uwakala wa mechi (match agent) wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika Alhamisi ya Septemba 26 mwaka huu saa 4 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Mtihani wa uwakala wa wachezaji (players agent) na uwakala wa mechi (match agent) wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika Alhamisi ya Septemba 26 mwaka huu saa 4 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Kutakuwa
na jumla ya maswali 20 kwenye mtihani huo, 15 yanatoka FIFA kuhusiana
na kanuni za kimataifa za mpira wa miguu na matano yatatoka TFF
kuhusiana na kanuni mbalimbali zinazotawala mchezo huo nchini.
Kwa
ambao wangependa kufanya mtihani huo utakaokuwa katika lugha ya
Kiingereza ambayo ni moja kati ya lugha nne rasmi za FIFA wanatakiwa
kujisajili TFF kwa ada ya dola 50 za Marekani ambapo watapewa utaratibu
na maeneo ambapo mtihani huo unalenga.
Mtihani huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi, na muda wa kufanya mtihani hautazidi dakika 90.
Mpaka
sasa Tanzania ina mawakala watano wa wachezaji wanaotambuliwa na FIFA.
Mawakala hao ni John Ndumbaro, Mehdi Remtulla, Ally Saleh, Yusuf
Bakhresa na Said Tully.
Subscribe to:
Posts (Atom)