WANACHAMA WA CHAMA HICHO MKOANI TANGA WAKIMSIKILIZA KATIBU WA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA AMBAYE HAYUPO PICHANI LEO |
KATIBU WA CHADEMA KANDA YA KASKAZINI,AMANI GOLUGWA AKISISITIZA JAMBO LEO. |
CHAMA cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema)kimesema kuwa licha ya kuwepo msuguano wa ndani lakini
kimetamba kuwa kitachukua kata zote sita zilizopo kanda ya kaskazini katika
uchaguzi utakaofanyika hivi karibuni hapa nchini.
Uchaguzi huo wa marudio unatokana na kata za Kiomoni,Mtae mkoani Tanga na Sombetini mkoani Arusha,Kiborolioni mkoani Kilimanjaro na Karachimbi Kiteto mkoani Manyara kutokuwa na madiwani wake kutokana na baadhi yao kujiuzulu na wengine kufariki dunia.
Tambo hizo zilitolewa na Katibu
wa Chadema Kanda ya Kaskazini,Amani Golugwa wakati akizungumza na viongozi wa
chama hicho mkoani hapa kwenye mafunzo ya Chadema ni msingi ambayo yalikuwa na
lengo la kuwajengea uwezo pamoja na kukabidhi vifaa vya awali vya kampeni kwa
kata zinazokabiliwa na uchaguzi huo ambazo ni Kiomoni na Mtae