MWENGE WA UHURU WAMALIZA MBIO ZAKE MKOANI RUKWA

July 16, 2015

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya Kushoto akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Ibrahim Msengi Mwenge wa Uhuru baada ya kumaliza ziara yake Mkoani Rukwa na kuanza ziara zake Mkoani Katavi tarehe 15 Julai 2015.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya (wa nne kulia mbele) na wakimbiza mwenge kitaifa na kimkoa wakiukimbiza Mwenge wa Uhuru kwa ajili ya kuukabidhi Mkoani Katavi tarehe 15 Julai 2015 baada ya kumaliza ziara yake Mkoani Rukwa.
 Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Hassan Kimanta (wa kwanza mbele) na wakimbiza Mwenge kitaifa na kimkoa wakiukimbiza Mwenge wa Uhuru Wilayani Nkasi mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Kalundi Wilayani humo tarehe 14 Julai 2015.
Moja ya mtambo wa kisasa wa umwagiliaji katika shamba la umwagiliaji la Ntatumbila Wilayani Nkasi. Mradi huu wa shamba la umwagiliaji na mifugo lina ukubwa wa hekta 1,000 na linamilikiwa na kuendeshwa na wazawa ambapo mpaka kukamilika kwake utagharimu fedha za kitanzania shilingi bilioni 46.
Miongoni mwa wamiliki wa shamba hilo na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa ndugu Juma Khamis Chum wakipiga picha ya pamoja na Mwenge wa Uhuru mara baada ya uzinduzi wa mradi wa umwagiliaji katika shamba hilo la Ntatumbila Wilayani Nkasi.
(Na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)
Mkurugenzi Mkuu mpya TCRA amtembelea Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Mkurugenzi Mkuu mpya TCRA amtembelea Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

July 16, 2015

1
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akimkaribisha Mkurugenzi Mkuu mpya wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Ally Yahaya Simba(Kushoto) alipomtembelea ofisini kwake leo, Dkt.Ally Yahaya Simba ameteuliwa kushika nafasi ya Prof. John Nkoma aliyemaliza Muda wake.
2
Mkurugenzi Mkuu mpya wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Ally Yahaya Simba(Kushoto) akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili ofisini kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga.
3
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akimueleza Dkt. Ally Yahaya Simba (Kushoto) umuhimu wa kuendelea kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya mawasiliano,alipomtembelea leo ofisini kwake.
4
Mkurugenzi Mkuu mpya wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Ally Yahaya Simba akiongea na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga na kumhakikishia kufanya kazi kwa pamoja kwa maslahi ya Taifa hasa katika kuiendeleza Sekta ya Mawasiliano Nchini.
5
 Watendaji wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga (mwenye suti nyekundu) alipotembelewa na Mkurugenzi Mkuu mpya wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Ally Yahaya Simba (kulia kwa Katibu Mkuu) aliyeteuliwa kushika nafasi ya Prof. John Nkoma aliyemaliza Muda wake.
6
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene akiwaeleza jambo Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (Hawapo pichani), walipotembelewa na Mkurugenzi Mkuu mpya wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Ally Yahaya Simba.Kulia kwake ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Raphael Hokororo.
7
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene akiagana na Mkurugenzi Mkuu mpya wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt.Ally Yahaya Simba(kushoto)
Picha na Hassan Silayo-MAELEZO
 President Kikwete meets UN High Commissioner for Refugees Antonio Guterres in Geneva

President Kikwete meets UN High Commissioner for Refugees Antonio Guterres in Geneva

July 16, 2015
 mail.google.com
The United Nations High Commissioner for Refugees UNHCR Mr.Antonio Guterres welcomes to his Geneva office President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete The President paid a courtesy call on him today and held talks on the influx of Refugees in Tanzania
mail.google.comm
 The United Nations High Commissioner for Refugees UNHCR Mr.Antonio Guterres introduces President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete to him some of his senior staff members.
.m
The United Nations High Commissioner for Refugees UNHCR Mr.Antonio Guterres and President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete shake hands when the nlatter paid a courtesy call on him today and held talks on the influx of Refugees in Tanzania.
Photos by Freddy Maro

MGOMBEA UBUNGE VITI MAALUMU ARUSHA,NEEMA AHAIDI KUINUA VIJANA KIUCHUMI

July 16, 2015

SAM_3817
Katibu wa vijana umoja wa vijana  UVCCM wilaya ya Arusha mjini Jamali Khimji akimkabidhi fomu ya ubunge viti maalum Bi.Neema Kiusa(27)katika ofisi za umoja huo jijini Arusha, ahaidi kuinua vijana kiuchumi endapo atapata nafasi ya kuwa Mbunge wa vijana Mkoa wa Arusha.
(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
SAM_3820
Neema Kiusa(27) Mgombea ubunge viti maalumu kupitia  chama cha Mapinduzi ambaye pia ni mjumbe wa baraza la vijana wilaya ya Longido akionyesha fomu aliyochukua leo.
SAM_3821
Neema Kiusa(27)ambaye ni mgombea ubunge viti maalumu kupitia  chama cha Mapinduzi  akiwa na mumewe Andrea Shija, pia ni mama wa mtoto mmoja
SAM_3824
Neema Kiusa(27)Mgombea ubunge viti maalumu kupitia  chama cha Mapinduzi ambaye pia ni mjumbe wa baraza la vijana wilaya ya Longido akitoka katika ofisi za umoja wa vijana wa ccm mkoa wa Arusha baada ya kuchukua fomu .
…………………………………….
Mgombea ubunge kupita kundi la vijana (UVCCM) Neema Kiusa  leo amechukua fomu ya kuwania nafasi ya ubunge viti maalumu Mkoa wa Arusha,ambapo amesema kuwa shauku yake kubwa ni kuwatumikia vijana kwa kutatua changamoto ya ajira 
Neema ambaye pia ni mjumbe wa baraza la vijana Wilaya ya Longido alisema kuwa ndoto yake ya kuwatumikia vijana ni ndoto yake ya muda mrefu sana hivyo endapo atapata nafasi hiyo atashirikiana na vijana bega kwa bega kuleta maendeleo katika Mkoa wa Arushaa
Pia mgombea huyo alitoa shukrani kwa mume wake  anayempa ushirikiano mkubwa wa kufanikisha ndoto yake ya kutumikia vijana ambapo aliwataka wanaume wengine kuonyesha ushirikiano kwa wake zao endapo wataonyesha nia ya kuwania nafasi za uongozi
Kwa upande wake Katibu wa vijana UVCCM wilaya ya Arusha mjini Jamali Khimji amewataka vijana wa chama cha mapinduzi kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za nafasi za ubunge viti maalumu kundi la vijana katika mkoa wa Arusha
Khimji alisema kuwa kijana anayetakiwa kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ni kijana wa kwanzia umri wa miaka 21-30 na awe ametimiza vigezo vya chama hicho

OFISI YA RAIS, TUME YA MIPANGO YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

July 16, 2015


Mapema wiki iliyopita Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ilitembelea miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini ili kukagua utekelezaji wake. Miradi hiyo ni pamoja na Kituo cha kuzalisha samaki Morogoro, Skimu ya Umwagiliaji Iringa vijijini, Maghala ya COWABAMA Iringa Vijijini, Ujenzi wa Barabara ya Iringa – Dodoma, Bwawa la Mtera, Ujenzi wa Barabara ya Manyoni – Itigi, utandikaji wa Reli eneo kati ya Kitaraka na Malongwe, Shamba la Kitengule, One Stop Border Post Mutukula, Mkongo wa Taifa Mutukula na Upanuzi wa mradi wa maji safi, Bomba Kuu la Ziwa Victoria.  
Katika kufanikisha uratibu wa miradi ya maendeleo, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango hufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi hiyo kwa kuzielekeza Wizara zinazotekeleza miradi kuwasilisha taarifa za utekelezaji kila robo mwaka. Aidha, Tume ya Mipango hutembelea miradi ya maendeleo kuona hali halisi ya utekelezaji ikiwa ni pamoja na kubaini mafanikio na changamoto na hatimaye kutoa ushauri katika ngazi husika kuhusu namna ya kukabiliana na changamoto hizo.
Moja ya Majukumu ya Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ni kuratibu utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kitaifa ya Kimkakati, Miradi ya Matokeo Makubwa Sasa (MMS) na miradi mingine muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa Taifa. Miradi imeainishwa katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2011/12 – 2015/16) na ile ya Matokeo Makubwa Sasa iliyoibuliwa katika mfumo wa kimaabara.
Naibu Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bibi. Florence Mwanri (wa nne kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Ufuatiliaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bw. Omari Abdallah (wa kwanza kushoto) na maafisa kutoka kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango pamoja na wataalam wa Mradi wa Kituo cha Kuzalisha Samaki kilichopo Kingolwira Mkoani Morogoro wakiangalia sehemu maalum ya kukuzia vifaranga vya samaki baada ya kutotoleshwa.
Naibu Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi. Florence Mwanri (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Ufuatiliaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bw. Omari Abdallah (wa kwanza kulia) pamoja na maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakipata maelezo kuhusu mradi wa ujenzi wa barabara ya Iringa – Dodoma, hatua ulipofikia na changamoto zilizopo kutoka kwa Mtaalamu Elekezi wa mradi Bw.Robin de Kock (mwenye kofia).
Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi. Florence Mwanri (wa tatu kulia) akiangalia kazi ya ujenzi wa barabara ya Iringa – Dodoma inavyoendelea wakati alipotembelea mradi huo pamoja na maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango. Pamoja nao ni Mtaalamu Elekezi wa mradi Bw.Robin de Kock (mwenye kofia katikati).
Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bibi. Florence Mwanri (katikati), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Ufuatiliaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bw. Omari Abdallah (wa pili kushoto) pamoja na maofisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakipewa maelezo kuhusu bwawa la kuzalisha umeme la Mtera kutoka kwa Meneja wa Kituo Bw. Abdallah Ikwasa (wa nne kushoto). Hii ni sehemu ambapo uzalishaji wa umeme unafanyika. Bwawa la Mtera linapatikana katika mikoa ya Iringa na Dodoma. Lina uwezo wa kuzalisha MW 80 ambao unaoingizwa katika Gridi ya Taifa.
Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bibi. Florence Mwanri (wa kwanza kushoto) na maofisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakipata maelezo kuhusu mradi wa ujenzi wa reli kutoka Kitaraka hadi Malongwe mkoani Tabora kutoka kwa Bw. Raphael Mwandumbya (mwenye kofia) ambaye ni Mkaguzi wa ujenzi wa reli hiyo. Mradi huu ni sehemu ya ujenzi na ukarabati unaoendelea katika Reli ya kati ambao una urefu wa kilometa 89.
Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bibi. Florence Mwanri (wa pili kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Ufuatiliaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bw. Omari Abdallah (wa kwanza kushoto) na maafisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiangalia uharibifu wa barabara ambao unafanywa na wananchi wasio waaminifu kwa kuchota kokoto pembezoni mwa barabara hiyo ambayo bado inaendelea kujengwa. Barabara hii inajengwa na Nicholas O’Dwyer & company Ltd Consulting Engineers ambapo kipande cha Manyoni hadi Itigi kipo katika hatua za mwisho kukamilika. Lengo la mradi ni kuendelea kujenga barabara ya Manyoni – Itigi kwa kiwango cha lami katika sehemu tatu za utekelezaji ambazo ni: Manyoni – Itigi – Chaya (KM 89.35), Chaya - Nyahua (KM 90), na Nyahua – Tabora (KM 85).
Jengo kwa ajili ya kutolea huduma za mpakani (One Stop Border Post) Mtukula, mradi ambao unahusisha ujenzi wa miundombinu inayosaidia utolewaji wa huduma bora na za kisasa mpakani mwa Tanzania na Uganda. Lengo la mradi wa One Stop Border Post ni kukamisha vituo vya utoaji huduma za pamoja mipakani kati ya Tanzania na nchi za jirani.
Timu ya maofisa kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiongozwa na Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bibi. Florence Mwanri (wa tatu kushoto) wakipata maelezo kutoka kwa wataalam wanaohusika na Mkongo wa Taifa. Lengo la mradi kwa mwaka 2014/2015 ni mapitio ya miundombinu ya Mkongo na mifumo kwa ajili ya maboresho, ujenzi Awamu ya III sehemu ya kwanza ya upanuzi wa mkongo kwa maeneo yaliyobaki katika awamu I na II na uhakiki wa ubora wa Mkongo.
Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bibi. Florence Mwanri (wa kwanza kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Idara Mipango na Ufuatiliaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bw. Omary Abdallah (wa kwanza kulia) na wataalam kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakipata maelezo kuhusu mafanikio na changamoto za Mradi wa Ranchi ya Taifa Misenyi kutoka kwa Meneja wa Mradi Bw. Martin Ladislaus (katikati). Shamba hili la mifugo lipo Karagwe, mkoa wa Kagera. Ni moja kati ya mashamba makubwa 9 nchini ya uwekezaji, limepimwa na kupata hati miliki.
Ujumbe kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ukiongozwa na Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango Bibi. Florence Mwanri (mwenye t’shirt nyeusi) wakiangalia sehemu ya kuogeshea ng’ombe. Wengine ni Meneja wa Mradi Ranchi ya Taifa Misenyi, Kagera Bw. Martin Ladislaus (wa tatu kulia) na Meneja wa Mradi Ranchi ya Kitengule, Kagera Bw. Hemedi M. Seif (wa pili kulia).

DKT MAGUFULI NA MH SULUHU WALIVYOPOKELEWA KWA SHANGWE ZANZIBAR LEO

July 16, 2015


 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwa kwenye gari la wazi pamoja na mgombea mwenza Mhe.Samia Suluhu Hassan kwenye mitaa ya Michenzani Zanzibar.

Mhe. Magufuli aliwasili Zanzibar kwa lengo la kutambulishwa kwa wanachama wa CCM Zanzibar akiongozana na mgombea mwenza Mhe.Samia Suluhu Hassan ambapo wote kwa pamoja walipata kuwasalimia wananchi wa Zanzibar kwenye viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
 Maelfu ya watu wakiufuata msafara wa mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Mhe. John Pombe Magufuli aliyeongozana na mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan



 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli akivishwa skafu na chipukizi wa CCM Zanzibar mara baada ya kuwasili Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
 Mgombea Mwenza kwa tiketi ya CCM Mhe. Samia Suluhu Hassan akivishwa skafu na chipukizi wa CCM nje ya jengo la Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.


 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli akisalimiana na wazee maarufu wa Zanzibar
 Mhe. Magufuli akiwasili kwenye kaburi la muasisi wa Mapinduzi na Rais wa Kwanza wa Serikali Mapinduzi ya Zanzibar ,Hayati Sheikh Abeid Amani Karume
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John P.Magufuli pamoja na mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan wakiomba dua mbele ya kaburi la Hayati Abeid Aman Karume muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar.

 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha Wageni kwenye Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.

 Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Magufuli nje ya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar kwenye sherehe fupi ya kutambulishwa wagombea wa CCM kwa wanachama wa CCM.
  Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mgombea Mwenza Mhe. Samia Hassan Suluhu.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Mhe. John Magufuli akiwasalimu wananchi waliojitokeza kwenye sherehe fupi za kumtambulisha kwenye viwanja vya Afisi Kuu CCM Zanzibar.

 Kila mtu alitaka kumgusa.
 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Zanzibar waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja vya Afisi Kuu Zanzibar kwenye sherehe fupi ya kumtambulisha kwa wanachama pamoja na mgombea mwenza Mhe. Samia Suluhu Hassan,kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM(Zanzibar) na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe.Ali Mohamed Shein.
 Wananchi wakishangilia


 Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akihutubia wakazi wa Zanzibar waliojitokeza kwa wingi kushuhudia sherehe fupi za kutambulishwa kwa wagombea wa nafasi ya Urais kwa kupitia CCM kwenye viwanja vya Afisi Kuu.


 Mgombea mwenza wa nafasi ya Urais Mhe. Hassan Suluhu Hassan akizungumza kwenye sherehe fupi za utambulisho nje ya Afisi kuu ya CCM Zanzibar.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Magufuli akiwasalimu wakazi wa Zanzibar waliojitokeza kwa wingi kwenye sherehe za kumtambulisha yeye na mgombea mweza kwenye viwanja vya Afisi Kuu Zanzibar.
 Wakazi wa Zanzibar wakimsikiliza mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Magufuli kwenye viwanja vya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiagana na mgombea wa ueais kwa kupitia CCM Dk.John Magufuli.