MABAHARIA JIENDELEZENI KIELIMU ILI MPANUE WIGO WA AJIRA KIMATAIFA.

June 26, 2023


Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala akisisitiza jambo kwa wadau wa sekta ya Uchukuzi kwa njia ya maji na Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Mwanza na Mikoa ya Jirani(hawapo pichani) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi Stella Katondo akisisitiza jambo kwa Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala na Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani (hawapo pichani) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi Stella Katondo akimuongoza Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala kukagua mabanda ya maonesho ya wadau wa usafiri kwa njia ya maji wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala akigawa vyeti vya pongezi kwa Mabaharia waliofanya Vitendo vya kijasiri vya uokozi kwa nyakati mbalimbali wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala ( katikati kwa waliokaa) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023





Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala ( katikati kwa waliokaa) wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023




Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na mikoa ya jirani wakifuatilia mada kutoka kwa Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Kwaya ya Watumishi wa Jiji la Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi Stella Katondo walipotembelea banda la Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023




Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Medali zao mara baada ya kumaliza kushiriki mbio za KM 7 za Seafarers Marathon zilizoanzia kwenye Mwalo wa Kirumba na kumalizikia kwenye viwanja vya Furahisha ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023



Baadhi ya Mabaharia, Wafanyakazi wa wizara, Taasisi na Wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Jiji la mwanza na Mikoa ya jirani wakiwa kwenye picha ya pamoja na Medali zao mara baada ya kumaliza kushiriki mbio za KM 7 za Seafarers Marathon zilizoanzia kwenye Mwalo wa Kirumba na kumalizikia kwenye viwanja vya Furahisha ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza Tarehe 25 Juni,2023




Na Mwandishi wetu Mwanza


Serikali imewataka Mabaharia kote Nchini kuzidi kujiendeleza kielimu na kuchapa kazi kwa bidii ili waaminike kwenye ajira hususan za kimataifa ili waweze kupata fursa zaidi za kufanya shughuri za ubaharia nje ya Nchi kwa manufaa yao na Nchi kwa ujumla.


Hayo yamesemwa leo na Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala wakati wa akihitimisha maonesho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha vilivyopo katika Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza kuanzia Tarehe 22 Juni, 2023 na kufikia tamati Tarehe 25 Juni,2023.


Mhe.Masala amesema Mabaharia huendesha na kuwezesha uchumi wa nchi zao na Dunia kukua, kwa kulitambua hilo Serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Awamu ya Nane ya Mapinduzi Zanzibar inayoongozwa na Mhe. Dkt Hussein Ally Mwinyi kwa kushirikiana na vyama vya Mabaharia, wamiliki wa vyombo vya usafiri majini na taasisi mbalimbali za kimataifa zimefanya kila liwezekanalo kuhakikisha kazi za Ubaharia na taaluma yake zinatambuliwa nchini na nje ya nchi sasa kuliko wakati mwingine wowote ule.

“Serikali imehakikisha Mabaharia wanapewa heshima inayostahili kama zilivyo taaluma nyingine sasa ni wakati wenu sasa Mabaharia kote Nchini kutumia fursa hii kujiendeleza zaidi kitaaluma ili mzidi kuaminika kwenye ajira za kimataifa” amesisitiza Masala

Mhe. Masala amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inawajali sana Mabaharia kwani katika mkoa wa Mwanza imekarabati Meli za MV Victoria , MV Butiama,Mv Umoja na kujenga meli mpya ya MV Mwanza ambazo zitasaidia kuongeza upatikanaji wa ajira kwa Mabaharia

Akimkaribisha Mgeni rasmi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta ya Uchukuzi Bi.Stella Katondo amesema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilijiunga na Shirika la Bahari Duniani(IMO) lenye majukumu ya kukuza na kusimamia utendaji wa Sekta ya Usafiri majini, kusimamia ulinzi, usalama na uhifadhi wa mazingira ya maji tangu mwaka 1974 ambapo walikubaliana Kusherehekea Siku ya Mabaharia Duniani kila mwaka ifikapo tarehe 25 Juni,2023

Bi. Stella amesema Maadhimisho haya ya siku ya Mabaharia Duniani yanayoambatana na kauli mbiu
“Miaka 50 ya MARPOL uwajibikaji wetu unaendelea” yaliyofanyika Kitaifa Jijini Mwanza kuanzia tarehe 22 Juni,2023 na kufikia tamati tarehe 25 Juni,2023 yalikutanisha Taasisi, Wizara na wadau wote wa Sekta ya Uchukuzi kwa njia ya Maji Nchini kwa lengo la kutambua umuhimu wa kazi ya Mabaharia na kuwaenzi mabaharia ambao ni kiungo muhimu sana kwa uchukuzi kwa njia ya maji na kukuza uchumi wa Taifa na Dunia

Maonesho ya siku ya Mabaharia Duniani yaliyoanza tarehe 22 mpaka 25 Juni, 2023 na kufanyika kitaifa Jijini Mwanza yameandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi-Sekta Uchukuzi kwa Tanzania Bara kupitia Shirika la uwakala wa Meli Tanzania(TASAC) na Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Zanzibar(ZMA), Pamoja na wadau mbalimbali wa Uchukuzi kwa njia ya maji Nchini.

TSB KUTUMIA MCHEZO WA YOGA KUHAMASISHA ZAO LA MKONGE

June 26, 2023


Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona wakati wa Shughuli ya Kimataifa ya Mchezo wa Yoga iliyofanyika kwenye Hotel ya Mkonge Jijini Tanga.

Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh akizungumza 

Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh kulia akiongoza mchezo wa Yoga 
Washiriki wa mchezo wa Yoga wakiendelea nao kwenye Ukumbi wa Hotel ya Mkonge Jijini Tanga 
Mchezo wa Yoga ukiendelea
Mchezo wa Yoga ukiendelea
Wageni mbalimbali wakifuatilia mchezo huo
Picha ya pamoja na kikundi cha Yoga cha Jijini Tanga
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Tanga (TPC) Lulu George ambaye ni miongoni mwa wachezaji wa mchezo huo 


Na Oscar Assenga,Tanga

BODI ya Mkonge Tanzania (TSB) imeweka bayana kwamba itatumia pia mchezo wa Yoga kuhamasisha Kilimo cha zao la Mkonge ili kuweza kupanua wigo mpana ili kuongeza idadi ya wakulima.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona wakati wa Shughuli ya Kimataifa ya Mchezo wa Yoga iliyofanyika kwenye Hotel ya Mkonge Jijini Tanga.

Kambona ambaye alialikwa kwenye shughuli hiyo kama mgeni Alisema mashuhuri kwenye shughuli ya kimataifaa ya Yoga ambapo Tanga wana wanachama wengi ambapo aliweza kujionea shughuli zinazoendelea.

Alisema kwamba baada ya kuona shughuli hizo amejifunza kwamba mchezo wa Yoga ni mchezo muhimu kwa ajili ya afya ya akili na kuweza kuona namna mazoezi yanavyofanyika tumeshuhudia walimu kutoka nchini India wakifundisha kupitia videeo Conference akionyeha mazoezi yanavyokwenda.

Aidha alisema kwamba hivyo wameona ni hatua muhimu kwao kufika na kuna uwekezako wa kutumia mchezo wa Yoga kuhamasisha kilimo cha zao la mkonge kutokana na kwamba wao kila kila fursa wanaiutumia kuona namna ya kuiunganisha na zao la Mkonge.

Alisema kwamba na jambo hilo linafanyika hoteli ya Mkonge ambayo ni Brand kubwa ya zaio la Mkonge Tanga na amefurahi sana na Taasisi ya Yoga ni jambo nzuri sana.

Kwa upande wake Mwalimu wa Yoga kwa upande wa Tanga Darshana Minesh aliitaka jamii kutambua umuhimu wa Yoga kwa afya ya mwili,akili na roho na kwamba yatawasaidia katika kuleta mitazamo chanya kwenye mambo mbalimbali ya maisha yao.

"Yoga ni muhimu sana kwenye afya ya mwili ,akili na roho na mtu akifanya hatajutia maamuzi ya kujiunga kwani ataona mabadiliko makubwa kwenye maisha yake," alisisitiza Mratibu huyo wa Yoga kwa Mkoa wa Tanga.