RAIS DKT. MAGUFULI AHUTUBIA KATIKA KUTANGAZA JINA RASMI LA KITUO CHA AMANI NA USALAMA KILICHOPEWA JINA LA MWALIMU JULIUS NYERERE KATIKA MAKAO MAKUU YA UMOJA WA AFRICA (AU) ADDIS ABABA NCHINI ETHIOPIA

January 29, 2017

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia Viongozi Wakuu wa Mataifa mbalimbali hawapo (pichani) katika Jengo jipya la Kituo cha Amani na Usalama kilichopewa jina Rasmi la Mwalimu Julius Nyerere, Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kutangazwa rasmi kwa Jina la Mwalimu Julius Nyerere katika kituo hicho cha Amani na Usalama.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Rais wa Rwanda Paul Kagame wakati wakielekea katika Kituo cha Amani na Usalama cha Makao Makuu ya Umoja wa Afrika kilichopewa jina la Rais wa kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere, Addis Abba nchini Ethiopia. PICHA NA IKULU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na viongozi wa mataifa mabalimbali wakiwa katika picha ya pamoja katika jengo jipya la kituo cha Amani na Usalama (JULIUS NYERERE) lililopo katika Makao makuu ya Umoja wa Afrika Addis Ababa nchini Ethiopia.

AZAM MARINE YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA MKOANI TANGA YASHUSHA MELI ITAKAYOKWENDA PEMBA NA UNGUJA KUTOKA MKOANI TANGA

January 29, 2017
Meli Kubwa inayoweza kuingia abiria na mizigo kwa pamoja ambayo itafanya safari zake kati ya Tanga-Unguja na Pemba ikiwa inaingia bandari ya Tanga leo wakati wa uzinduzi wake ambapo uwekezaji huo mkubwa umefanywa na kampuni ya Azam Marine ili kuwanusuru wananchi wa mkoa wa Tanga na changamoto za usafiri huo

Meli Kubwa inayoweza kuingia abiria 1600 na magari hamsini yenye mizigo kwa pamoja ambayo itafanya safari zake kati ya Tanga-Unguja na Pemba ikiwa inaingia bandari ya Tanga leo wakati wa uzinduzi wake ambapo uwekezaji huo mkubwa umefanywa na kampuni ya Azam Marine
 Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed wa pili kulia akitazama namna wananchi wanavyoshuka kwenye meli hiyo itakayopunguza adha na usumbufu kwa wananchi wanaosafiri kutoka mkoani Tanga kwenda Unguja na Pemba

Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed katikati akizungumza na watumishi wa mamlaka ya Bandari Mkoani Tanga wakati wa ujio wa meli hiyo kwenye bandari ya Tanga kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Tryphoni Ntipi kushoto ni PRO wa Mamlaka hiyo,Moni Jarufu.
 Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed katikati akisalimiana na Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,
Tryphoni Ntipi wakati wa ujio wa meli hiyo kushoto ni
PRO wa Mamlaka hiyo,Moni Jarufu.
Mazungumzo yakiendelea
Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ujio wa meli hiyo kulia  Mkurugenzi Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa vyombo vya majini (SUMATRA) Kaptain Mussa Mandia
Mkurugenzi Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa vyombo vya majini (SUMATRA) Kaptain Mussa Mandia katikati akizungumza na waandishi wa habari kushoto ni  Meneja Mkuu wa Azam Marine Husein Mohammed
Nahodha wa Meli hiyo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufika Bandari ya Tanga.
 Waandishi wa Habari wakiwa kazini kushoto ni Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania katikati ni Mariam Shedafa wa Azam TV
 Vifaa vya uokozi wakati wa majanga ya ajali hivyo
 Baadhi ya Sehemu ya VIP ndani ya Meli hiyo kama inavyo onekana 

Mara wataka kompyuta za Bayport kuelekezwa shule za kata

January 29, 2017
Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, akimkabidhi kompyuta sita Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Ado Mapunda kwa ajili ya kuongeza ufanisi katika ofisi za umma mkoani Mara. Wengine kwenye tukio hilo ni watumishi wa Bayport, akiwamo Meneja wa Kanda ya Ziwa wa Bayport, Lugano Kasambala wa kwanza kushoto. Picha na Mpiga Picha Wetu Mara.

Na Mwandishi Wetu, Mara
SERIKALI ya Mkoa Mara kwa kupitia Katibu Tawala wake, Mheshimiwa Ado Mapunda, imewaagiza watendaji wa serikali mkoani humo kuhakikisha kompyuta walizopewa na Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, zinaelekezwa kwenye shule za kata ili kuchangia ukuzaji wa kiwango cha elimu.

Mheshimiwa Mapunda aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati anapokea kompyuta sita kutoka Bayport zilizoelekezwa katika Halmashauri ya Tarime, Rorya na Manispaa ya Musoma, huku kila ofisi ikipata kompyuta mbili ikiwa ni mwendelezo wa ugawaji wa vitendea kazi kutoka kwenye taasisi hiyo inayojihusisha na mikopo ya fedha taslimu kwa watumishi wa umma na wafanyakazi wa kampuni zilizoidhinishwa.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Katibu Tawala huyo alisema lengo la Mkoa wao ni kuona kiwango cha elimu kinapiga hatua kubwa, hivyo wameona msaada huo uelekezwe zaidi katika shule za kata kwa ajili ya kuhifadhi kumbukumbu muhimu za wanafunzi wao.

Alisema kufanya hivyo kutaongeza ukuzaji wa elimu ya wanafunzi wa mkoani Mara, ili iwe njia ya kuandaa wataalamu wazuri kwa kutumia vema teknolojia ya kompyuta inayoboresha utendaji wa kazi.

“Tunashukuru wenzetu wa Bayport wa Kanda ya Ziwa pamoja na Makao Makuu kwa kutuletea msaada huu mkubwa kwetu ambao kwa hakika tutautumia vizuri katika Mkoa huu wa Mara ili ulete tija kama mlivyokusudia wakati mnafikiria kusambaza.

“Ofisi yetu imeagiza kompyuta hizi zisambazwe katika baadhi ya shule za kata kwa kuzitumia kwa namna moja ama nyingine ili wanafunzi wetu wasonge mbele zaidi kwa kuanzia kurekodi vizuri takwimu zao kama njia ya kugundua tunafanya juhudi za kutuvusha hatua ya juu zaidi,” Alisema Mapunda.

Naye Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, alisema ndoto zao zinaelekea kukamilika kuhakikisha kwamba msaada wa kompyuta zao unafika kwa haraka kama walivyokusudia na kuuzindua mwaka jana jijini Dar es Salaam.

“Kompyuta tulizotoa Mara na Kanda ya Ziwa ni mwendelezo wetu wa kutoka kwenye kompyuta 125 tulizomkabidhi Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, huku 80 zikielekezwa mikoani na kuufanya mzigo wote ufikie 205 wenye thamani ya Sh Milioni 500,” Alisema Mercy.


Mbali na Mara, Bayport pia walikabidhi kompyuta mbili kwa Halmashauri ya Wilaya Misungwi, mkoani Mwanza na kuifanya Kanda ya Ziwa kuvuna kompyuta nane za taasisi hiyo ambapo pia ilitangaza kuwa utaratibu huo wa kufikisha kompyuta utaendelea katika wilaya na mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara wakiamini utasaidia kuongeza ufanisi katika ofisi za umma.

RAIS DKT. MAGUFULI AHUDHURIA KIKAO CHA UMOJA WA AFRIKA (AU) MJINI ADDIS ABABA ETHIOPIA

January 29, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Manuel Olveira Guterres wakati alipokuwa kwenye mojawapo ya vikao vya Umoja wa Afrika (AU) vinavyofanyika katika Makao makuu yake mjini Addis Ababa nchini Ethipia. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustine Mahiga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakati alipokuwa kwenye mojawapo ya vikao vya Umoja wa Afrika (AU) vinavyofanyika katika Makao makuu yake mjini Addis Ababa nchini Ethipia. PICHA NA IKULU

MLIMBWENDE WA SHINDANO LA MISS KIBOSHO 2017 JIJINI MWANZA APATIKANA.

January 29, 2017
Baada ya mtifuano mkali wa kumtafuta mlimbwende wa shindano la MISS KIBOSHO 2017 kufanyika kwa mara ya kwanza usiku wa ijumaa Januari 27,2017 na jana jumamosi Januari 28,2017 katika Ukumbi wa Kibosho Luxury Bar Kiseke Ilemela Jijini Mwanza, hatimaye mshindi amejulikana.

Mshindi wa shindano hilo lililofana vyema alikuwa ni Kephlin Jacob (katikati), nafasi ya pili ni Aida Gazar (kulia) na nafasi ya tatu ni Caren Nestory (kushoto), ambapo wanyange hao walifanikiwa kupenya na kuibuka na ushini huo miongoni mwa wanyange 10 walioshiriki shinano hilo.

Miss Kibosho 2017 iliandaliwa na Raju Entertainment kwa ushirikiano wa karibu na Kibosho Luxury Bar and Guest House Kiseke, Wema Salon, Mama Ngenda Sakon, Top Model na Hangano Cultural Group lengo lake ikiwa ni kukuza vipaji vya urembo kitaifa na kimataifa.
Na Binagi Media Group
Miss Kibosho 2017 Kephlin Jacob (katikati), Miss Kibosho 2017 nambari mbili, Aida Gazar (kulia) na Miss Kibosho nambari tatu ni Caren Nestory (kushoto).
Awali hatua ya tatu bora ilikwena kwa washiriki, Caren Nestory (kushoto), Kephlin Jacob (katikati) na Aida Gazar (kulia)
Awali washiriki waliotinga nafasi tabo bora ni Caren Nestory, Jackline Moses, Denzry Michael, Kelphine Jacob na Aida Gazar.
Washiriki wote 10 wa Miss Kibosho 2017 ambao ni Caren Nestory, Dorice Ezra, Jullieth Michael, Elizabeth Faustine, Christina Lucas, Nasra Ramadhan, Jacline Moses, Denzry Michael, Kephlin Jacob na Aida Gazar.