COASTAL UNION,MGAMBO SHOOTING ZASHINDWA KUONYESHANA UMWAMBA,ZAWAGAWANA POINTI MOJA MOJA.

October 03, 2015








KOCHA MKUU WA COASTAL UNION,JACKSON MAYANJA AKITOA MAELEKEZO KWA WACHEZAJI WAKE WAKATI WA MECHI HIYO IKIENDELEA.


Mama Samia Suluhu Asimikwa Umalkia Wilayani Maswa, Wamwita ngole

Mama Samia Suluhu Asimikwa Umalkia Wilayani Maswa, Wamwita ngole

October 03, 2015

New Picture (1)
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa nafasi ya urais, Mama Samia Suluhu Hassan (kulia) akisimikwa kuwa Malkia wa Wasukuma Wilaya ya Maswa na akinamama wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania ya CCM (UWT) alipowasili Jimbo la Maswa Mashariki kufanya mkutano wa hadhara wa kampeni kunadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa wanaMaswa.
………………………………………………………………………………….
Na Thehabari.com
MGOMBEA mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa nafasi ya urais, Mama Samia Suluhu Hassan leo amepewa heshima ya kusimikwa kuwa malkia wa Wasukuma Wilaya ya Maswa na kupewa jina jipya la Ng’walu Majura.
Mama Samia Suluhu amepewa heshima hiyo leo na Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania ya CCM (UWT) alipowasili Jimbo la Maswa Magharibi kufanya mkutano wa hadhara wa kampeni kunadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa wanaMaswa.
Mama Suluhu ambaye amepewa jina jipya la heshima hiyo la Ng’walu Majura alivishwa mavazi maalum ya kimila ya heshima ‘Ngole’ yaani malkia na kukabidhiwa mkuki maalum, ungo na usinge pamoja na kupewa zawadi anuai za vyakula vya kimila kwa kabila la Wasukuma eneo hilo.
Wakimpa heshima hiyo akinamama wa UWT walisema Mama Samia Suluhu amepewa heshima hiyo kwa kuwa ni mwanamke aliyekuja kuibua mambo mazuri kwa ushindi wa CCM na Tanzania kwa wanawake. Akinamama hao waliahidi kumuunga mkono ili kuhakikisha anashinda na kuwatoa kimasomaso Wanawakea wa Tanzania.
Kwa upande wake Mama Samia Suluhu amewashukuru akinamama hao kwa heshima na zawadi mbalimbali walizompa na kuwaahidi kupigania maslahi yao zaidi endapo chama chake kitafanikiwa kuunda Serikali katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25, 2015. Alisema licha ya kupigania maendeleo ya taifa zima yeye kama mwanamama ana ajenda maalum za kuwapigania akinamama kuanzia huduma za kijamii hadi uwezeshwaji kwao ili kuleta usawa na maendeleo kwa jamii hiyo.
Alisema amepokea kilio cha maji Maswa na kwa kuwa wanawake ndio waathirika wakubwa wa ukosefu wa maji atahakikisha Maji yanapatikana kupitia miradi anuai inayotekelezwa eneo hilo na kwa kuanzia watachimba visima 10 maeneo mbalimbali ya Maswa ili kuwapatia maji wakazi wa maeneo hayo.
Mapema majira ya asubuhi Mama Samia Suluhu alifanya mkutano wa kampeni katika Jimbo la Meatu akiinadi ilani ya CCM kwa wananchi, ambapo aliwaomba kuichagua CCM kwani imepanga kufanya mengi kwa wanaMeatu ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara, ujenzi wa malambo na majosho kwa ajili ya kuhudumia mifugo yao.
Alisema ili kuondoa migogoro kwa wafugaji na wakulima safari hii Serikali itakayoundwa na CCM imepanga kupima ardhi yote ya vijiji na Wilaya na kisha kuainisha mipaka ya wakulima na wafugaji na kuwamilikisha jamii hizo kumaliza migogoro.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com
MAMA SALMA KIKWETE AKIONGEA NA WANACHAMA WA UWT WA MKOA WA MARA.

MAMA SALMA KIKWETE AKIONGEA NA WANACHAMA WA UWT WA MKOA WA MARA.

October 03, 2015

X1 
Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi,CCM, Mama Salma Kikwete akiwapungia mkono viongozi na wanachama wa UWT wa Mkoa wa Mara wakati akiwasili kwenye ukumbi wa Musoma Community Centre kwa ajili ya mkutano wa ndani na wanachama hao-Octoba 3, 2015.
X3 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na wanachama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Mkoa wa Mara wakati alipokutana nao kwenye ukumbi wa Musoma Community Centre.
X2Umati wa wajumbe wa Umoja wa Wanawake (UWT) wa Mkoa wa Mara wakimsikiliza kwa makini Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) wakati alipokuwa akiongea nao Mjini Musoma.
PICHA NA JOHN LUKUWI.

WATANZANIA WAASWA KUWAPELEKA WATOTO WAO KATIKA SHULE YA SEKONDARI IMPERIAL ILIYOPO CHALIZE MSOLWA MKOANI PWANI

October 03, 2015

Wanafunzi wa kidato cha kwanza wa Shule ya Sekondari ya Imperial wakielekea kupandisha bendera ya Taifa wakati wakisherekea mwaka mmoja wa shule hiyo iliyopo Chalinze Msolwa mkoani Pwani.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Imperial wakiwa  ndani ya darasa la Komputa
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Imperial wakijibu maswali ya kuhusiana na komputa katika darasa hilo.
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Imperial, Ivonne Mnyitafu akitoa ufafanuzi kwa wazazi pamoja na walimu wa shule hiyo.
Mwalimu wa Taluma  wa Shule ya Sekondari ya Imperial, Peter Mwanda akizungumza katika siku ya Imperial iliyofanyika leo katika shule hiyo iliyopo Chalinze Msolwa mkoani Pwani.
Wazazi wakiwasikiliza wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Imperial wakati wa kusherekea siku ya Impirial iliyofanyika Shuleni hapo leo.
Wazazi waliowatembelea wanafunzai wa shule ya Sekondari Imperial wakielekea katika chumba cha masomo ya Sayansi (Laboratory) wakati waliposherekea siku ya Imperial iliyofanyika leo katika shule hiyo iliyopo Chalinze-Msolwa mkoani Pwani.
wanafunzai wa shule ya Sekondari Imperial wakifanya majaribio ya masomo ya Sayansi ambayo ni Fizikia pamoja na Kemia katika chumba hicho cha majaribio ya masomo hayo shuleni hapo leo.
Mkuu wa Shule na Mkurugenzi Mtendaji wa shule ya Sekondari Imperial, Arup Mukhopadhyay akitolea ufafanuzi moja ya kifaa kinachotumika kuchuja maji ambayo yamechanganywa na mchanga mbele ya wazazi na walezi waliofika shuleni hapo kwaajili  ya siku ya Imperial iliyofanyika leo shuleni hapo.
Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Sekondari Imperial,Buhela Lunogelo akiwapongeza kuwapongeza wanafunzi wa shule hiyo mara baada ya kufanya majaribio ya masomo ya Kemia na Fizikia shuleni hapo leo.Kulia ni Mkuu wa Shule na Mkurugenzi Mtendaji wa shule ya Sekondari Imperial, Arup Mukhopadhyay.
Baadhi ya wazazi wakichukua kumbukumbu zao (Taswira mbalimbali) wakati wanafunzi wa shule hiyo wakifanya majaribio ya masomo ya Fizikia na Kemia katika chumba hicho katika shule ya Sekondari Imperial leo.
Baadhi ya wanafunzi  shule ya Sekondari Imperial wakifafanua somo la hesabu la pembe zinazoundwa na pembe tatu mbele ya wageni waalikwa na wazazi au walezi wao (hawapo pichani) waliohudhulia katika siku ya Imperial iliyofanyika Chalinze Msolwa mkoani Pwani leo.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Imperial wakifanya mdahalo katika siku  Imperial iliyofanyika leo katika shule hiyo.
Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Sekondari Imperial, Buhela Lunogelo akizungumza na waandishi wa habari leo katika shule hiyo kuhusiana na maendeleo pamoja na uzuri wa taaluma inayotolewa katika shule hiyo kuwa ni ya kimataifa, aidha amewaomba wazazi wenye watoto wanataka kusoma kidato cha kwanza mpaka cha nne wawapeleke watoto wao katika shule hiyo iliyonzishwa Machi 3 Mwaka huu.
 Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Sekondari Imperial, Buhela Lunogelo akiwapa zawadi wanafunzi wa shule hiyo leo Chalize Msolwa Mkoani Pwani, kushoto ni Mkuu wa Shule na Mkurugenzi Mtendaji wa shule ya Sekondari Imperial, Arup Mukhopadhyay.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Imperial wakiwa katika picha ya pamoja wakiwa na vikombe na vyeti vyao walivyozawadiwa leo
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Imperialwakitoa burudani katika siku ya Imperial iliyofanyika leo mkoani Pwani.

WANANCHI WA KIJIJI CHA KENYAMANYORI WILAYANI TARIME WANASTAHILI PONGEZI.

October 03, 2015

Kwa mbali kabisa, Kamera ya Binagi Media Group-BMG ikapata fursa ya kunasa picha za Shule ya Sekondari Kenyamanyori ambayo ilijengwa kwa nguvu za Wananchi miaka michache iliyopita na kuanza kupokea wanafunzi mwaka 2013 baada ya kukamilika ambapo wanafunzi waliokuwa kidato cha pili katika shule zilizokuwa mbali walihamia shuleni hapo na kuendelea na kidato cha pili huku wengine walichaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huo.
Na:George Binagi-GB Pazzo
Ni ukweli usiopingika kuwa uongozi wa kijiji hicho pamoja na wananchi wake ambao asilimia kubwa ni wakulima, wanastahili pongezi kwani wazo lao la kujenga shule ya sekondari ni wazo bora na limewasaidia watoto wa kijiji hicho na wale wanaotoka vijiji jirani kupata elimu karibu zaidi hivyo ni vyema wakaendelea kushirikiana na serikali pamoja na wahisani wengi katika kuhakikisha kwamba wanaiboresha zaidi shule hiyo ili iweze kuwa mkombozi kwa ajili ya watoto wao kielimu.
Kulia ni jengo la Utawala na Majengo mengine matatu kushoto ni majengo ya maabara tatu za Sayansi
Majengo mawili ya Maabara
Jengo moja la Maabara
Jengo la Utawala
Madarasa
Vyoo 
Kuna majengo mawili ya nyumba za waalimu ambayo yamefikia hatua hii na moja limekamilika.
Shamba la Shule

NHC YAZINDUA UUZAJI WA NYUMBA ZA BIASHARA NA MAKAZI ZA MOROCCO SQUARE,WAZIRI KIRUKI AIPONGEZA NHC KWA UFANISI

October 03, 2015

Na Francis Dande
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki, amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa mpango wake wa kujenga nyumba bora na kuwauzia wananchi kwa ajili ya  makazi na biashara.

Waziri Kairuki aliyasema  hayo juzi  jijini Dar es Salaam alipokuwa akizindua  mauzo ya nyumba  za biashara  na makazi zilizojengwa eneo la Morocco Square,  Kinondoni,  jijini Dar es Salaam.

Aliwapongeza Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu na wenzake kwa  kazi nzuri wanayoifanya kwa kiasi kikubwa katika kuleta  uhai na taswira nzuri ya  shirika hilo.

Alisema kuwa serikali inatambua kuwa  makazi  ni jambo  muhimu kwa maendeleo ya taifa, ndiyo  maana imekuwa ikichukua hatua  mbalimbali ili kuwezersha sekta  ya nyumba kuwa endelevu na yenye  tija kwa wananchi  na uchumi wa nchi.

Alibainisha kuwa moja ya mambo yaliyofanyika katika kukuza sekta hii ni kuwa  na Sheria ya Mikopo ya nyumba (The Mortgage Financing (Special Provision Act) ya  mwaka  2008,  iliyoanzishwa  kuweza kuwafanya wadau wa sekta ya  nyumba wakiwemo waendelezaji, wanunuzi wa nyumba  na taasisi za fedha  kushiriki kikamilifu katika kukukuza sekta hii muhimu.

Aidha , alisema tangu kuwapo kwa  sheria  hiyo, tangu mwaka 2008 kumeshuhudiwa benki 19 kati ya  zaidi ya benki 50 zilizopo nchini zikitoa  mikopo ya nyumba kwa  Watanzania, 16  kati ya  hizo zikiwa zimesaini makubaliano na  na Shirika la Nyumba la Taifa ili kuweza  kutoa mikopo kwa Watanzania wanao nunua nyumba zinazojengwa na NHC.

Naibu waziri huyo alisema kuwa  kutokana na  kuwepo kwa  changamoto  ya riba kubwa  ya  mikopo ya nyumbva inayotozwa  na benki mbalimbali ambayo ni kati ya asilimia 18  na 25, serikali itaendelea  kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Benki Kuu ya Tanzania ili kuona namna bora ya kuewezesha  benki  kupunguza riba  katika  mikopo ya nyumba ili Watanzania wengi waweze kukopa na kununua  nyumba.

Aliwahimiza Watanzania  kutumia  fursa zilizopo za mikopo ya Benki kununua  nyumba zinazojengwa na NHC, ikiwamo kujitokeza  kwa wingi kununua nyumba hizo za  za mradi wa  Morocco Square ambao una nyumba za ofisi hoteli, makzi na maduka makubwa.

 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mauzo ya nyumba za biashara na makazi-Morocco Square uliofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. (Picha na Francis Dande)
 Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo.
  Naibu Wazriri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu. 
 Wageni waalikwa.
 Wageni waalikwa.
  Naibu Wazriri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu. 
 Burudani ya muziki.
Burudani ikiendelea.
  Naibu Wazriri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu.  
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akizungumza katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akizungumza katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akizungumza katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akizungumza katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akizungumza katika hafla hiyo.