April 01, 2014

Salaam. Kocha Mkuu wa Simba,  Zdavko Logarusic ‘Loga’  ametimiza mechi 10 za Ligi Kuu Bara akiwa amekusanya pointi 12  lakini amezidiwa na Abdalah Kibadeni, ambaye aliinoa na timu  hiyo kwenye mzunguko wa kwanza kwani alikusanya pointi 20 katika idadi hiyo ya mechi.
April 01, 2014

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA YAKUMBANA NA CHANGAMOTO ZA BARABARA WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimueleza jambo Mbunge wa jimbo la Nkasi Kaskazini,Mh.Ali Mohammed Kessy,walipokuwa wakitembea kwa miguu kufuatia msafara huo kukumbana na changamoto ya barabara mapema jana jioni katikati ya Msitu wa hifadhi ya wilaya ya Nkasi.Ndugu Kinana na Msafara wake ulikuwa umetoka kijiji cha Namanyere kuelekea kijiji cha Mwampemba kusikiliza matatizo ya Wananchi na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopangwa kutekelezwa kwenye Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010.
 
Barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 100,lakini iliwachukua zaidi ya masaa 12 kwenda na kurudi kutokana na ubovu wa barabara.Ndugu Kinana yuko Mkoani Rukwa,Katavi na Kigoma kwa ziara ya siku 21 ya kuimarisha Chama cha CCM,kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo kiwemo na kuzisikiliza kero mbalimbali za wananchi
 Ndugu Kinana akishiriki kuweka mawe sehemu korofi,angalau kusaidia Lori hilo pichani lililolala ndani ya msitu huo kwa siku mbili,wapite nae msafara wake uweze kuendelea na safari.
 Sehemu korofi ya Barabara ikiwekwa sawa ili lori lipite na kisha msafara nao uweze kupita,lakini hata hivyo zilitumika juhudi kubwa kuvusha msafara wa Kinana na hatimae kuendelea na safari ya kuelekea kijiji kingine.
April 01, 2014

SSRA YATOA TAARIFA KUHUSU UANDIKISHWAJI WANACHAMA KATIKA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII NCHINI

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA),Ansgar Mushi (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu uandikishwaji wa wanachama wapya wa mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Sheria wa SSRA, Ibrahim Ngabo.      

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA),Ansgar Mushi (wa pili kushoto), akisoma taarifa hiyo kwa waandishi wa habari. Kutoka kulia ni Ofisa Habari wa SSRA, Mr Stewart,Mkurugenzi wa Idara ya Fedha na Utawala, Mohamed Nyasamo, Mkurugenzi wa Sheria  , Ibrahim Ngabo na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasaishaji, Sarah Kibonde.
April 01, 2014

*MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA BODI YA HUDUMA ZA MAKTABA TANZANIA, JIJINI DAR

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa na Mkutubi wa Jiji, Lusekelo Mwalugelo, Gazeti la Mambo Leo la Mwaka 1923 ambalo ni moja kati ya magazeti ya zamani, wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonyesho kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania, yaliyofanyika leo kwenye viwanja vya Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa baadhi ya vitabu na Ofisa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Mture Educational Publishers Ltd, Bupe Mwasaga, wakati alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonyesho kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania, yaliyofanyika leo kwenye viwanja vya Maktaba Kuu ya Taifa jijini Dar es Salaam.
April 01, 2014

*MKUU WA MKOA WA GEITA AZINDUA MCHAKATO WA UANZISHWAJI WA MFUKO WA AFYA YA JAMII WA TIBA KWA KADI (TIKA)

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Magalula Said Magalula akifungua mkutano wa wadau mkoani Geita unatakaojadili mchakato wa uanzishaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii ujulikanao kama Tiba kwa Kadi (TIKA).
Katibu Tawala wa Mkoa  Severine Kahitwa akieleza umuhimu wa kuwa na utaratibu wa TIKA ndani ya Halmashauri ya Mji wa Geita.
April 01, 2014

Kesi dhidi ya Rais Kenyatta yaahirishwa


Rais Uhuru Kenyatta
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC imehairisha kesi dhidi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta hadi tarehe saba Oktoba mwaka huu.
 Rais Kenyatta anatuhumiwa kwa makosa ya jinai kufuatia machafuko ya baada ya uchaguzi wa mkwaka 2007 - 2008, madai ambayo ameyakanusha.
April 01, 2014

RAIS DKT. SHEIN AMKARIBISHA IKULU YA ZANZIBAR WAZIRI CHIKAWE

PIX 1 (2) 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akimkaribisha ofisini kwake Ikulu mjini Zanzibar, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe. Waziri Chikawe alifika ofisini hapo kwa lengo la kujitambulisha kwa Rais huyo baada ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Viongozi hao pia walijadiliana masuala mbalimbali ya kuimarisha ulinzi na usalama wa Tanzania Bara na Visiwani. Katikati ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima. (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
PIX 2 (2) 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akimsikiliza kwa makini, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (katikati) alipokuwa akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu ya Zanzibar leo.  Waziri Chikawe alifika ofisini hapo kwa lengo la kujitambulisha kwa Rais huyo baada ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Viongozi hao pia walijadiliana masuala mbalimbali ya kuimarisha ulinzi na usalama wa Tanzania Bara na Visiwani. Kushoto ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima.  (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
PIX 3 (2) 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (watatu kushoto), Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima (wapili kulia), Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (wapili kushoto). Kulia ni Mkurugenzi wa Vitambulisho vya Taifa, Ofisi ya Zanzibar, Vuai Suleiman. Kushoto ni Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdan Omary Makame. Waziri Chikawe alifika Ikulu ya Zanzibar kwa lengo la kujitambulisha kwa Rais Shein baada ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Viongozi hao pia walijadiliana masuala mbalimbali ya kuimarisha ulinzi na usalama wa Tanzania Bara na Visiwani. Kushoto ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima.  (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
April 01, 2014
SERIKALI ITAHAMISHA NA KUWONDOKA WANANCHI WAISHIO KANDO KANDO YA BONDE LA MTO MKOMAZI-JK

NA OSCAR ASSENGA,KOROGWE

SERIKALI imesema itahamisha makaburi na itawaondoa wananchi wote  wanaoishi kando kando ya bonde la mto mkomazi kwa kuwalipa fidia za makazi na mimea yao ili kupisha ujenzi wa  bwawa kwa ajili kuinua na  kuendeleza  kilimo cha umwagiliaji.




Rai hiyo ilitolewa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dokta Jakaya Mrisho Kikwete  wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara  uliofanyika katika viwanja vya mamlaka ya mji wa mombo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za maendeleo ya wananchi wilayani korogwe.
April 01, 2014

BARAZA LA MADIWANI LA MJI KOROGWE LAUPOKEA KWA MIKONO MIWILI MPANGO

Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Lewis Kalinjuna akiongoza kikao cha Baraza la Madiwani katika kupitisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Kikao hicho cha mwisho kimefanyika Machi 29, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Pembeni ni Mwenyekiti wa Hamashauri ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, Mheshimiwa Angello Bendera (kulia), Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtonga, Mheshimiwa Francis Komba (kushoto).
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu akitoa maelezo machache juu ya TIKA. Pembeni ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji ambaye ni Diwani wa Kata ya Mtonga, Mheshimiwa Francis Komba na Mwenyekiti wa Hamashauri ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, Mheshimiwa Angello Bendera.
April 01, 2014

WAZIRI CHIKAWE ATUA ZANZIBAR KUTEMBELEA IKULU, NIDA NA UHAMIAJI LEO

PIX 1 (1) 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (kushoto) akipokelewa na Naibu Waziri wa wizara yake, Pereira Ame Silima, wakati alipotua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo. Kulia ni Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdan Omary Makame. Waziri Chikawe amewasili Zanzibar kwa ajili ya ziara ya kikazi. (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
PIX 2 (1) 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (kushoto) akimsalimia Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu wakati alipotua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa  wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo. Waziri Chikawe amewasili Zanzibar kwa ajili ya ziara ya kikazi. (Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
PIX 3 (1) 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mathias Chikawe (wa pili kushoto) akiwa na NaibuWaziri wa wizara yake, Pereira Ame Silima (kushoto), Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu na Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdan Omary Makame, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa  wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo Waziri Chikawe amewasili Zanzibar kwa ajili ya ziara ya kikazi. (Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
April 01, 2014

TUESDAY, APRIL 01, 2014


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.compress@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA UMMA


Uingereza inajivunia kuwa nchi inayoongoza katika uwekezaji nchini Tanzania na itaendelea kuisaidia Tanzania katika jitihada zake za kiuchumi na kuleta maendeleo .

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron amemuambia Rais Kikwete wakati wa mazungumzo yaliyofanyika 10 Downing Street, Leo tarehe 31 March, 14, ambapo ndipo yalipo Makao Makuu ya Waziri Mkuu wa Uingereza.

"Tunafurahia sana uhusiano wetu na kujivunia kuwa tunaongoza katika  Uwekezaji nchini Tanzania" Bw. Cameron amesema na kumhakikishia Rais Kikwete kuwa Uingereza iko tayari kutoa misaada zaidi.