Showing posts with label afya. Show all posts
Showing posts with label afya. Show all posts
SERIKALI, SEKTA BINAFSI KUIMARISHA HUDUMA ZA DHARURA KUCHOCHEA AJIRA NCHINI

SERIKALI, SEKTA BINAFSI KUIMARISHA HUDUMA ZA DHARURA KUCHOCHEA AJIRA NCHINI

March 05, 2026 Add Comment






Na Abduly Iddy, Dar es Salaam

Serikali imesema ushirikiano kati yake na Sekta binafsi utaendelea kuwa chachu muhimu ya kuimarisha huduma za afya nchini, hususan katika kuboresha huduma za dharura kupitia mpango wa kuanzisha uzalishaji wa magari ya wagonjwa (ambulance) mkoani Tanga.

Akizungumza Machi 5, 2026 jijini Dar es Salaam katika kikao cha maandalizi ya kuanzisha uzalishaji wa magari hayo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe.Batilda Burian, amesema Serikali inakaribisha uwekezaji huo unaofanywa kwa kushirikiana na SO Company Limited kwani utaimarisha upatikanaji wa huduma za dharura za afya nchini hususan magari ya wagonjwa.

Amesema uzalishaji wa ambulance ndani ya nchi utaongeza upatikanaji wa magari ya kisasa ya kuwahudumia wagonjwa na kupunguza muda wa kuwafikia wananchi wanaohitaji msaada wa haraka wa kitabibu, hatua itakayosaidia kuokoa maisha ya watu.

“Mradi huu ni hatua muhimu tunapoimarisha mfumo wetu wa huduma za afya. Kupatikana kwa ambulance zinazozalishwa hapa nchini kutarahisisha usambazaji wake katika maeneo mbalimbali, hususan ya pembezoni,” amesema, RC Batlida.

Aidha, amesema mradi huo pia utaleta manufaa ya kiuchumi kwa kufungua fursa za ajira kwa vijana, kukuza wazalishaji wa ndani wa vipuri na kuchochea maendeleo ya sekta zinazohusiana na uzalishaji wa vifaa vya magari na huduma za afya.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Dharura na Maafa kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Erasto Sylvanus, amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ili kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa ufanisi na kuchangia maendeleo ya sekta ya afya pamoja na uchumi wa taifa.

Mradi huo unatarajiwa kuimarisha huduma za dharura za afya huku ukifungua fursa mpya za ajira na maendeleo ya kiuchumi nchini.

RAS TANGA- MIKAKATI ENDELEVU SULUHISHO KUKABILI DHARURA ZA KIAFYA

RAS TANGA- MIKAKATI ENDELEVU SULUHISHO KUKABILI DHARURA ZA KIAFYA

March 05, 2026 Add Comment








Na Andrea Kadege, WAF-Korogwe

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Rashid Mchatta ameagiza kuwekwa kwa mikakati endelevu itakayoiwezesha jamii kukabiliana na majanga ya dharura yanayopelekea athari kiafya, kwa ufanisi zaidi.

Bw. Mchatta ameyasema hayo leo Machi 05, 2026 wakati akifunga kikao kazi cha tathmini ya matukio na athari za kiafya mkoani Tanga, kilichoandaliwa na Wizara ya Afya Idara ya Dharura na Maafa kwa kushirikiana na Mradi wa Usalama wa Afya Duniani unaotekelezwa na asasi zisizo za kiserikali za PATH na CIHEB Tanzania, kilichofanyika Wilayani Korogwe.

“Maazimio yote yaliyojadiliwa yawekwe katika mpango kazi wenye malengo yanayopimika, muda wa utekelezaji na mgawanyo wa majukumu kwa kila sekta” amesema Bw. Mchatta

Aidha, amesema kwa kuwa idadi kubwa ya washiriki katika kikao kazi hicho ni wajumbe wa kamati ya maafa ya mkoa hivyo, amesisitiza kuwekwa kwa mikakati endelevu na ya muda mrefu kuhakikisha kuwa majanga ya dharura yanakabiliwa ili kulinda afya ya jamii.

Katika hatua nyingine ameishukuru na kuipongeza Wizara ya Afya kwa kuandaa kikao kazi hicho, huku akitambua mchango wa ushirikiano baina ya serikali na wadau wa maendeleo, mashirika yasiyo ya kiserikali (PATH na CIHEB Tanzania) pamoja na sekta binafsi katika kuimarisha utayari wa kukabiliana na dharura.

Naye Mratibu-Udhibiti Maafa na Dharura kutoka Wizara ya Afya Dkt. Saumu Nungu amesema kwa ngazi ya mikoa, Tanga umekuwa mkoa wa nne kufanyiwa tathmini ya matukio na athari za kiafya, huku akieleza kuwa kupitia mpango kazi utakaoandaliwa, Mkoa wa Tanga utakuwa na uwezo wa mapema wa kukabiliana na dharura za kiafya pindi zitakapotokea.

Amebainisha kuwa baada ya mpango huo kuandaliwa, utawasilishwa Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa kwa ajili ya mapitio kisha kusainiwa na kuidhinishwa ili utekelezaji wake uwe wa lazima na unaosimamiwa kikamilifu ili uweze kuwa wenye tija.

Kwa upande wake Mratibu wa Vituo vya Operesheni za Dharura za Afya ya Jamii kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Idara ya Afya Dkt. Ernest Kyungu ameeleza kuwa mafanikio katika kukabiliana na majanga ya kiafya yanetokana na maandalizi ya mapema, uratibu wa sekta mtambuka na uwekezaji katika elimu ya kinga kwa jamii.

Amesitiza kuwa Tanga inapaswa kujenga mfumo madhubuti unaojumuisha hatua za kabla ya janga, wakati wa janga na baada ya janga ili kupunguza madhara kwa wananchi kwa kuzingatia jiografia yake hususani mipaka ya bahari na bandari pamoja na mpaka wa nchi jirani ya Kenya.

Naye kiongozi wa Ufuatiliaji wa Magonjwa ya Mlipuko na yaliyopewa kipaumbele kutoka Mradi wa Usalama wa Afya Duniani unaotekelezwa na asasi zisizo za kiserikali za PATH na CIHEB Tanzania Dkt. Said Sheuya, ameeleza kuwa kupitia ushirikiano uliopo baina ya Wizara ya Afya na wadau mbalimbali , wamefanikiwa kuendesha mafunzo kwa wataalam, kuimarisha mifumo ya taarifa na kuongeza upatikanaji wa rasilimali muhimu za kukabiliana na majanga.

Kwa ujumla, kikao hicho kimeweka msingi wa maboresho ya kimkakati katika sekta ya afya mkoani Tanga, huku utekelezaji wa mpango kazi utakaoidhinishwa ukitarajiwa kuwa dira ya kuhakikisha ulinzi wa afya ya jamii unaimarika na athari za majanga zinapunguzwa kwa kiwango kikubwa.

WAZIRI MCHENGERWA -HAKUNA MGONJWA WA UVIKO-19 ,MAFUA MAKALI NA KIPINDUPINDU TANZANIA

February 27, 2026 Add Comment


Na Mwandishi  wetu– WAF, Dar es Salaam.


Wizara ya Afya imewataka wananchi kuendela kuchukua tahadhari na kufuatilia ushauri wa kitaalam ili kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali kama ilivyoelezwa katika taarifa kwa umma  ya   Mganga Mkuu wa Serikali hivi karibuni


Hayo yamebainishwa leo Februari 27, 2026 Jijini Dar es salaam na Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa alipofanya ziara ya kimakakati katika hospitali ya Rufaa Mkoa Amana kwa lengo la kukagua utolewaji wa huduma za afya pamoja na maendeleo ya uboreshaji wa miundombinu ya hospitali hiyo

Aidha amesema, Serikali bado inaendelea kufuatilia kwa ukaribu juu ya mienendo  ya  magonjwa mbalimbali kama kipindu pindu, Dengue na UVIKO-19 hususani katika kipindi hiki cha mvua  huku akisistiza kwamba hakuna kisa chochote UVIKO, cha mgonjwa aliyelazwa katika hospitali nchini


“Napenda kuwahakikishia wananchi na Watanzania wote Serikali yenu ipo makini na inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa maambukizi ya UVIKO-19 nchini na kimataifa, lakini pia tunasisitiza umuhimu wa kila mmoja kuendelea kuchukua tahadhari na kuzingatia ushauri wa kitaalamu unaotolewa na wataalamu wa afya ili kulinda afya binafsi na ya jamii kwa ujumla,” amesema Mhe. Mchengerwa.

Mhe. Mchengerwa amewataka Watanzania kujiandikisha na kulipia bima ya afya kwa wote sababu gharama za matibabu zinaweza kuwa kikwazo kwa wananchi wa hali ya chini hasa wanapohitaji kufanyiwa huduma za kibingwa na kibingwa bobezi


Waziri Mchengerwa amesema kuwepo kwa bima ya afya kwa wote kuendana sanjari na upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya na hospitali ili kukamilisha dhamira ya serikali katika kurahisisha huduma za afya kwa wananchi 


Katika ziara hiyo, Mhe. Mchengerwa ameambatana na Katibu Mkuu Dkt. Seif Shekalaghe pamoja na menejimenti ya Wizara ya Afya, ambapo alikagua hali ya upatikanaji wa huduma, kusikiliza changamoto zinazowakabili watumishi na wagonjwa, na kueleza mikakati madhubuti ya serikali katika kuimarisha ubora na ufanisi wa huduma za afya kwa wananchi.

RC SENDIGA AZINDUA NA KUHAMASISHA UTEKELEZAJI WA BIMA YA AFYA KWA WOTE MKOANI MANYARA

December 21, 2025 Add Comment

 

 

Babati, Manyara Desemba 19, 2025: Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, leo Desemba 19, 2025 amezindua rasmi na kuhamasisha utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote (NHIF) katika Mkoa wa Manyara, akisisitiza umuhimu wa kila mwananchi kuwa na bima ya afya ili kupata huduma za matibabu kwa urahisi na kwa gharama nafuu.

Uzinduzi huo umefanyika katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) mjini Babati, na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wataalamu wa afya, wawakilishi wa mpango wa kitaifa wa Bima ya Afya kwa Wote pamoja na wananchi mbalimbali.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Sendiga amesema mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kutimiza ahadi ya siku 100 za kuanzisha mfumo utakaohakikisha kila Mtanzania anakuwa na bima ya afya.
“Mfumo huu unalenga kumwondolea mwananchi mzigo wa gharama kubwa za matibabu na kuhakikisha kila mmoja, bila kujali kipato chake, anapata huduma bora za afya kwa wakati,” amesema Mhe. Sendiga.

Aidha, amewaelekeza Wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya mkoani Manyara kuhakikisha mpango wa Bima ya Afya kwa Wote unatekelezwa kwa kuzingatia miongozo, kanuni na taratibu zilizowekwa, ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali.

Sambamba na hilo, Mhe. Sendiga amesisitiza kuwa ni wajibu wa viongozi na watendaji wote kwenda kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kujiunga na mpango huo, ili waweze kunufaika na huduma za afya kwa uhakika.

Kwa upande wake, Bi. Janeth Kibambo, Mwakilishi wa Timu ya Kitaifa ya Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, amesema lengo kuu la mfumo huo ni kuhakikisha wananchi wote wanakuwa na uwezo wa kupata huduma za afya katika vituo vyote vya umma na binafsi vilivyosajiliwa, bila kikwazo cha kifedha.
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Andrew Method, ameeleza kuwa mkoa umejipanga kikamilifu kutekeleza mpango huo, akibainisha kuwa changamoto ya wananchi kushindwa kugharamia matibabu imekuwa kubwa, hivyo kuanzishwa kwa Bima ya Afya kwa Wote ni mwarobaini muhimu katika kuboresha sekta ya afya.

Dkt. Method ameongeza kuwa Mkoa wa Manyara uko tayari kuupokea na kuutekeleza mpango huo kikamilifu, kwa kushirikiana na vituo vyote vya afya na wadau mbalimbali, ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na endelevu.

Uzinduzi wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote mkoani Manyara unatarajiwa kuongeza wigo wa upatikanaji huduma za afya, kupunguza vifo vinavyotokana na ukosefu wa matibabu kwa wakati, na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla.

KARNE YA AI: 'SADC BADO KUNA PENGO LA MAWASILIANO YA SAYANSI'

December 02, 2025 Add Comment




Na Veronica Mrema - Pretoria 

Ulimwengu wa sayansi na teknolojia unasonga kwa kasi ya ajabu. Mataifa makubwa duniani yanawekeza kwenye ubunifu, utafiti wa kisayansi, na teknolojia za kisasa.

Teknolojia kama akili unde, kilimo cha kisasa na tiba za kibunifu zaidi zinabadilisha maisha katika mataifa makubwa duniani.

Karne ya akili unde [AI], roketi zinavuka anga, kuna uvumbuzi na gunduzi nyingi katika teknolojia mpya kwa kasi ambayo dunia haijawahi kushuhudia.

Mataifa makubwa yanawekeza, yanashirikiana, na yanapasha habari za sayansi kwa umma wao kwa kasi.

Lakini upande mwingine wa dunia, ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika [SADC], bado kuna pengo kubwa katika mawasiliano ya sayansi. 

Watafiti wanagundua, Serikali zinafanya miradi, taasisi zinavumbua, lakini taarifa 'hazitembei' kwa kasi inayohitajika.

Bado haziwafikii vema wananchi wake, hazijengi uelewa na hazifanyi sayansi kuwa sehemu ya maisha ya kila siku.

Ndani ya SADC, bado kuna pengo kubwa kati ya maendeleo ya ki-sayansi na jinsi ambavyo taarifa hizo zinavyowafikia wananchi.

"Kwa sababu nchi nyingi za SADC bado hazina mkakati wa mawasiliano katika masuala ya sayansi,".

Yameelezwa hayo na Mkurugenzi Mkuu wa Ushirikiano wa Kimataifa na Afrika, Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (DSTI), Afrika Kusini Mwampei Chaba.

Ni wakati alipokuwa akifungua mdahalo wa siku moja wa waandishi wa masuala ya sayansi kutoka nchi 18 wanachama wa SADC.

Amesema kutokana na pengo lililopo katika upashanaji habari kuhusu maendeleo ya sayansi katika nchi hizo, ndiyo maana DSTI iliona vema kuwaleta pamoja waandishi wa habari na kufanya mdahalo huo.

Ni katika mkutano wa kimataifa wa waandishi wa habari za masuala ya sayansi [WCSJ2025] unaofanyika Pretoria nchini Afrika Kusini.

Akifungua mjadala huo, aliweka wazi changamoto kubwa wanazokutana nazo waandishi wa sayansi katika ukanda huu.

“Nchi nyingi katika SADC bado hazina mkakati wa ushirikiano katika mawasiliano kuhusu sayansi. Hiyo ndiyo sababu upashanaji habari za sayansi unakumbwa na changamoto nyingi.”

Ameongeza "Ukosefu wa mkakati huo unawafanya waandishi wengi kukosa ushirikiano wanaohitaji kutoka kwa Serikali zao.

"Mnashindwa kuwa karibu na watafiti, mnakosa mazingira rafiki ya kupata habari, pamoja na fursa za ufadhili au mwaliko kwenye matukio muhimu yanayohusu sayansi na uvumbuzi.

Amesisitiza "Kwa hivyo, katika nchi yako na unataka kupata ushirikiano kutoka Serikali [kuandika kuhusu habari fulani inayohusu sayansi] au unataka watambue kazi yako.

"Unataka kufadhiliwa kwa baadhi ya kazi zako. Unataka kualikwa kwenye matukio [kwa wengi wenu], itakuwa ngumu kwa kuwa hawana mkakati wa ushirikiano kuhusu hilo," amesema.

"Mkirudi nchini mwenu kafuatilieni hili kwa undani, nendeni mkaulize wizara [zinazohusika na masuala ya] sayansi, wizara za mawasiliano [iwapo] wameandaa mkakati?.

Hii ni mara ya kwanza kwa Bara la Afrika kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa waandishi wa habari za sayansi, afya, mazingira na mambo mengine yanayohusiana na hayo.

Mdahalo huo kwa ajili ya waandishi wa habari kutoka SADC ulilenga kuwaleta pamoja kujadiliana namna gani watasukuma mbele masuala ya sayansi ndani ya nchi zao kwa upashanaji habari.

"Hii ni warsha ya mafunzo yenye umuhimu mkubwa kwetu. wazo hili lilikuja kwetu mwaka 2022 tulipoandaa Mkutano wa Sayansi Duniani (World Science Forum).

"..,, ambao ulikuwa wa kwanza kuandaliwa barani Afrika. Kwa hivyo, tulitengeneza historia mwaka 2022 kwa kuandaa mkutano wa Sayansi Duniani barani Afrika. 

"Kisha tukaamua kuwa kuleta fursa kama hii barani Afrika bila waandishi, waandishi wa sayansi kuwa kwenye chumba, kungekuwa kupoteza. 

Ameongeza "Tunawezaje kuwasilisha kile tunachofanya katika mkutano, kama idara, kama serikali barani Afrika, kama taasisi zinazofanya utafiti, ikiwa hatuna uandishi wa sayansi kwenye chumba?

"Pia tuligundua kuwa waandishi wa sayansi bado hawana uwezo wa kutosha kuhusiana na uandishi na kuandika makala za sayansi. 

"Hivyo basi, tuliona hitaji la kuunda ushirikiano. Na Stellenbosch alishirikiana nasi kwa kiwango kikubwa. 

Amesema walianza kupanga warsha ya mafunzo, yenye vipengele vingi, ambayo itasaidia kujenga uwezo wa waandishi wa habari katika kuwasilisha kazi tunazofanya kwa ufanisi zaidi. 

"UNESCO ilifadhili baadhi ya wajumbe mwaka 2022, na imeendelea kuwa mshirika wetu tangu wakati huo. 

"Sekretari ya SADC pia imekuwa mshirika wetu, na tunashukuru sana michango waliyotoa kwa waandishi wa SADC kuungana nasi. 

"Chama cha Waandishi wa Sayansi wa Afrika Kusini (SASJA) pia kimeungana nasi, na sisi pia tuko kwenye mshirika mkubwa katika mkutano mwingine wa kihistoria," amebainisha,

Amesema mkutano wa WCSJ2025 walioandaa mwaka huu unatengeneza historia mpya nyingine na walitaka kuwa sehemu ya historia hiyo.

Amesema Afrika Kusini waliunda mkakati wa mawasiliano na ushirikiano katika masuala ya sayansi tangu mwaka 2015 na kwamba walichelewa mno kuunda.

"Taasisi yetu ilianzishwa Juni 2004, hivyo karibu miaka 11 baadaye, tu wakati huo tu tulikuwa na mkakati wa ushirikiano wa sayansi unaotekelezwa kwa sasa, na mchakato wa ukaguzi upo.

Amebainisha "Mwaka huu SADC ilishiriki katika G20. Tulikuwa Rais wa G20 na GSTI ilipanga kile kinachoitwa Wiki ya Utafiti na Ubunifu [Research and Innovation Week]. 

"Pia tulipitisha hati maalumu inayoitwa Azimio la Ushirikiano wa Sayansi wa G20 (G20 Science Engagement Resolutions). 

"Hati hiyo inahimiza nchi za G20 kuweka sayansi kati-kati ya jamii inahimiza kuongeza ufahamu katika jamii zetu kuhusu thamani ya sayansi, na kuwasilisha sayansi kwa njia jamii zinaweza kuelewa.

"Kwa nini tunapaswa kufanya hivyo? Ni kwa nini hii ni muhimu? Sayansi haifadhiliwi vya kutosha, na hili ni changamoto katika jamii nzima.

Amesisitiza "Ikiwa thamani ya sayansi haifahamiki, ikiwa athari ya sayansi haijulikani kwa serikali zetu, jamii zetu, wafadhili wetu na wachangiaji.

"Basi mpango wa kufafanua ni ninyi walioko hapa. Ninyi ndio midomo yetu. Ninyi ndio mabalozi wetu wa kuwasilisha sayansi kwa jamii. 

"Mara sayansi itakapofahamika, mara thamani ya sayansi itakapothibitishwa kwenye hatua za vitendo, kwenye jamii, kwenye vijiji.

"Basi mna nafasi nzuri ya kupata ufadhili kutoka Serikalini, ufadhili kutoka kwa wafadhili na kadhalika. 

"Kwa hivyo, jukumu lenu ni muhimu sana, na tunategemea ninyi kusaidia kuunganisha pengo," amesema na kuongeza, 

"Napenda kuwahimiza kwamba katika wiki hii, mchukue fursa ya warsha nyingi zinazofanyika kuhamasisha sayansi. 

"Matumizi ya data, sita-sita kusema kwamba sayansi inapaswa kuwa kati-kati ya jamii, elimu, viwanda, ili kuendesha maendeleo kwa ujumla. 

"Na haiwezi kuwa katikati ikiwa ninyi hufahami jinsi ya kuwasilisha sayansi. Nami naamini hatuhitaji kuwa wanasayansi ili kuelewa sayansi. 

"Sayansi inapaswa kufafanuliwa kwa mtu wa miaka 85 na mtoto wa miaka 5. Bila kutumia maneno magumu. 

Amesisitiza "Ikiwa mtu hawezi kueleza, ikiwa mwanasayansi unayemhoji hawezi kueleza sayansi yao kwa njia unayoielewa, basi hawafanyi kazi nzuri. 

"Na pia unapaswa kuwa na uwezo wa kuhimiza wanasayansi kuzungumza na kuwasilisha sayansi kwa njia kila mtu anaweza kuelewa.

Amehoji "Je, unajua waandishi mashuhuri wa sayansi barani Afrika? Kwa nini haingewezekana iwe wewe?

"Kwa nini haingewezekana iwe wewe?” aliuliza, akiwahimiza washiriki kuwa wao wenyewe wanaweza kuwa waandishi mashuhuri wa sayansi Barani Afrika. 

“Kuna waandishi wa sayansi mashuhuri duniani kote, lakini sio barani Afrika. Afrika inahitaji sayansi kwa maendeleo zaidi kuliko kanda nyingine yoyote duniani. 

"Hivyo basi, tufanye lengo letu kuwa na waandishi mashuhuri wa sayansi katika jamii zetu, nchi zetu, ndani ya SADC na barani kote. 

Amesisitiza "Vinginevyo, mbona mko hapa? Kwa nini mko hapa ikiwa hatutumiwe kile tulicho nacho kuwasilisha sayansi na kuifanya iwe ‘fashionable’?”

Amehimiza waandishi wa habari kutumia vema majukwaa ya kidigitali kama fursa ya kufikisha taarifa muhimu zinazohusu sayansi kwa kundi la vijana ambalo kubwa lipo kwenye majukwaa hayo.

"Kila mtu yupo TikTok, kila mtu yupo YouTube, lakini lazima tuone maudhui ya sayansi pia kwenye TikTok au YouTube. 

"Tumia majukwaa haya maarufu kuwasilisha sayansi. Tuwafikie vijana walipo kwenye YouTube, Instagram na mitandao mingine na kuwapa elimu ya sayansi kwa njia wanayoielewa.”

Picha zote kwa hisani ya DSTI

WAZIRI MCHENGERWA ATOA SIKU 21 ZA KUANDALIWA KWA WITO WA KUVUTIA WAWEKEZAJI WA VIWANDA VYA DAWA NA VIFAA TIBA NCHINI

WAZIRI MCHENGERWA ATOA SIKU 21 ZA KUANDALIWA KWA WITO WA KUVUTIA WAWEKEZAJI WA VIWANDA VYA DAWA NA VIFAA TIBA NCHINI

November 25, 2025 Add Comment




Na WAF – Dar es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa ametaka ndani ya siku 21 Wizara ya Afya kupitia Idara ya Huduma za Dawa na ofisi ya Mfamasia Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba nchini (TMDA) kuandaa wito wa uoneshaji wa nia (Call of Expression of Interest) ili kuvutia wawekezaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba.

Akizungumza mbele ya Wataalam wa Sekta ya Afya Novemba 24, 2025 katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam, Waziri Mchengerwa amesema hatua hiyo inalenga kuvutia wawekezaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba hapa nchini ili kuongeza uzalishaji wa ndani na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje.

“Tuandae ‘Call of Expression of Interest’na tuwaonyeshe yale ambayo tunaweza kushirikiana nao katika utengenezaji wa dawa lakini pia tuwakaribishe katika uwekezaji wa viwanda vingi vya dawa na vifaa tiba hapa nchini” amesisitiza Waziri Mchengerwa huku akitoa siku 21 kwa wito huo kuwa umeandaliwa na kutolewa.

Amesema kuwa uwekezaji wa viwanda vya dawa hapa nchini utairahisishia Serikali katika kusimamia ubora wa bidhaa zinazozalishwa kwa usalama wa afya za Watanzania huku pia kuipunguzia Serikali gharama kubwa ya kununua bidhaa za afya kutoka nje ya nchi.



BALOZI YAKUB APONGEZA MUHIMBILI KUPELEKA WATOA HUDUMA ZA KIBINGWA WENGI NCHINI COMORO

October 01, 2025 Add Comment


Balozi wa Tanzania nchini Comoro Saidi Yakub ameipongeza Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kupeleka idadi kubwa ya madaktari bingwa bobezi katika kambi ya matibabu nchini humo  ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alilolitoa wakati wa ziara yake visiwani humo.

Akizungumza hii leo katika mahojiano maalumu na Afisa Habari kutoka Idara ya Habari ya MNH,  Balozi Yakub amesema hospitali hiyo imepeleka jumla ya madaktari bingwa saba wa mgonjwa mbalimbali ukilinganisha na taasisi nyingine zinazoshiriki kambi hiyo.

" Hospitali ya Muhimbili imetuletea zaidi ya madaktari saba na katika wataalam hao watakuwa katika mgonjwa ya figo, ngozi, macho, meno,  masuala ya uzazi kwa akina mama pamoja na magonjwa ya kinamama"



Aidha, Balozi Yakub ameongeza kuwa licha ya kambi ya matibabu kuanza kuanza Oktoba 04, 2025, tayari  zaidi ya watu 1000 wamekwisha kujisajili ili kupata huduma za kibingwa na ubingwa bobezi.