UNDP WAFANYA KONGAMANO LA VIJANA, LENGO NI KUWASAIDIA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI

March 07, 2016
Hawa Dabo
Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini, Awa Dabo akitoa neno la ufunguzi katika kongamano la vijana na maendeleo, kongamano lililofanyika katika Ukumbi wa Nkrumah uliopo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam limefanya kongamano la vijana na maendeleo kujadili jinsi vijana wanavyoweza kutumika kusaidia kuleta maendeleo nchini na kubadili mfumo wa vijana katika kufanya maamuzi yaliyo sahihi.
Akizungumzia kongamano hilo limelofanyika siku ambayo UNDP imetiza miaka 50 tangu kuanzishwa, Mkurugenzi Msaidizi wa UNDP nchini, Amon Manyama alisema kuwa vijana wana nafasi kubwa katika jamii na kama wakitumika vizuri wanaweza kusaidia kupatikana kwa maendeleo na hivyo kupitia kongamano hilo wanataraji kuwapa mbinu mpya.
Alisema mbali ya kuangala jinsi wanavyoweza kusaidia kupatikana kwa maendeleo pia wanajadili kwa pamoja ili kuona jinsi gani wanaweza kubadili mfumo wa vijana wa kufanya maamuzi ambao wengi wao wamekuwa wakifanya maamuzi ambayo baadae yanaonekana kutokuwa sahihi.
“Tunafanya kongamano hili na vijana kutoka vyuo mbalimbali ili kuona mustakabali wa vijana wa Tanzania, kuona jinsi gani wanaweza kusaidia kupatikana kwa maendeleo Tanzania na hata kubadili mfumo wao wa kufanya maamuzi,” alisema Manyama.
Youth and Development Symposium UNDP, Tanzania
IMG_5271
Mkurugenzi Msaidizi wa UNDP nchini na mshereheshaji wa kongamano hilo, Amon Manyama akizungumza katika kongamano la vijana na maendeleo.
Nae Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini, Awa Dabo alisema vijana wana nafasi kubwa kusaidia uapatikanaji wa maendeleo nchini na wao kama UNDP wamekuwa wakisaidia na serikali ili kuwasaidia vijana kwa kuwapa mbinu ambazo wanaweza kutumia ili kufikia malengo waliyonayo.
Alisema licha ya kuwepo changamoto zilizopo katika sera ya vijana lakini pia vijana wamepoteza udhubutu wa kufanya maamuzi na hivyo kongamano hilo wanaweza kukuza uwezo wao wa kujiamini na kufanya maamuzi ambayo yanakuwa ni sahihi.
“Vijana wanatakiwa kuwa na malengo na kukuza uwezo wa kujiamini … vijana wanaweza kusaidia kupatikana maendeleo Tanzania na wana hamasa ya kusaidia kupatikana maendeleo hivyo wanatakiwa kupewa nafasi katika kufanya maamuzi,” alisema Bi. Dabo.
IMG_5296
Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini, Awa Dabo akitoa neno la ufunguzi katika kongamano la vijana na maendeleo, kongamano lililofanyika katika Ukumbi wa Nkrumah uliopo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
IMG_5323
Sehemu ya vijana kutoka vyuo mbalimbali wakimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini, Awa Dabo wakati akitoa neno la ufunguzi wa kongamano hilo.
Kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia kwa Mkuu wa Idara ya Uchumi, Jehovaness Aikaeli alisema vijana wanaweza kutumiwa kama fursa hasa katika kipindi hiki ambacho kunakuwa na vijana wengi ambao wanatoka vijijini na kukimbilia mijini na hivyo kama wakishirikishwa wanaweza kusaidia kupatikana maendeleo.
IMG_5369
Mkuu wa Idara ya Uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jehovaness Aikaeli akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano hilo.
Nae mmoja wa vijana aliyeshiriki katika kongamano hilo, Ncheye Revina alisema mifumo inayotumika sasa nchini inawabana vijana kusaidia kupatikana kwa maendeleo na kama watakuwa wanataka vijana wahusike kikamilifu basi wawatolee vikwazo vinavyowabana kushiriki akitolea mfano katika ajira kwa ajili wengi kutaka wafanyakazi walio na uzoefu mkubwa wa kazi jambo ambalo ni ngumu kupata vijana.
IMG_5571
Mmoja wa vijana aliyeshiriki katika kongamano hilo, Ncheye Revina.
IMG_5413
Benedict Kikove kutoka Ubalozi wa Japan nchini akiwaelezea vijana fursa zilizopo kwa vijana na changamoto wanazokumbana nazo wakati wa kongamano la vijana na maendeleo lililoandaliwa na UNDP.
IMG_5450
Afisa Mipango wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kujitolea (UNV), Stella Karegyesa akifuatilia kwa makini kongamano la vijana na maendeleo.
Hawa Bayumi
Meneja Huduma za Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kushoto) nae alikuwa ni miongoni mwa watoa mada katika kongamano hilo.
IMG_5666Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (National Information Officer-UNIC), Bi. Usia Nkhoma- Ledama (wa kwanza kulia) akifuatilia kilichokuwa kikiendelea katika kongamano hilo lililoandaliwa na UNDP.
IMG_5394Fatma Mohamed kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kujitolea (UNV) akizungumzia changamoto wanazokutana nazo vijana katika kutafuta mafanikio.
IMG_5507Mwakilishi wa Wizara ya Katiba na Sheria kutoka Zanzibar, Saleh Mubarak akielezea washiriki jinsi serikali inavyowasaidia vijana katika kongamano la vijana na maendeleo.
IMG_5390
Baadhi ya washiriki wa kongamano hilo ambao ni vijana na wadau kutoka mashirika na taasisi mbalimbali nchini lililofanyika katika Ukumbi wa Nkrumah uliopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Youth Symposium -UNDP Tanzania
Youth Symposium -UNDP Tanzania
IMG_5679
Afisa wa Utawala Bora kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Godfrey Mulisa akielezea jinsi washirika wa maendeleo wanavyotoa fursa kwa vijana na jinsi fursa hizo zinavyoweza kuwasaidia vijana wa Tanzania.
IMG_5687
Mkurugenzi Mkazi Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA), Natalia Kanem akizungumza wakati wa kongamano hilo.
IMG_5749
Pichani juu na chini ni vijana kutoka vyuo mbalimbali nchini wakishiriki kutoa maoni kwenye kongamano hilo.
Youth Symposium -UNDP Tanzania
IMG_5796
Makamu Mkurugenzi Mkazi wa UNDP nchini, Titus Osundina akitoa neno la hitimisho la kongamano la vijana na maendeleo.

MSAADA KWA NDUGU YETU AHMED ALBAITY UNAHITAJIKA (VIDEO)

March 07, 2016
albety
Ukiwa ndugu, jamaa na rafiki, bado mchango wako wa hali na mali unahitajika kwa ajili ya ndugu na mpendwa wetu, Ahmed Albaity (pichani) ilikuweza kuendelea na hali yake ya matibabu. Waweza kuhabarika zaidi kupitia taarifa hii ya video hapa chini. Karibuni sana.

SERIKALI YAZISHAURI TAASISI ZA KIBENKI NCHINI KUWA NA VILABU VYA MICHEZO NA MASHINDANO

March 07, 2016
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imezishauri Taasisi za Kibenki zilizopo nchini kuanzisha timu na vilabu vya michezo ili kukuza michezo pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa vijana walio wengi ambao wana vipaji lakini hawana timu za kuwaendeleza.
Hayo yamebainishwa kupitia kwa Waziri mwenye dhamana, Mh. Nape Nnauye mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa kukabidhi zawadi mbalimbali ikiwemo tuzo za wachezaji bora walioshinda katika michezo maalum ya BRAZUKA KIBENKI iliyoandaliwa na benki ya Barclays na wadau wengine.
Waziri Nape amebainisha kuwa, Nia ya Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inakuza michezo na kuwa na fursa za kiuchumi kupitia michezo hivyo taasisi hizo zinazo fursa ya kuongeza ajira na ustawi mzuri wa michezo endapo zitaanzisha timu za michezo na kimashindano kwani zinaweza na zinao wajibu huo.
Kwa mujibu wa Mratibu wa michuano hiyo, Nasikiwa Berya alieleza kuwa, jumla ya timu 16 zilishiriki huku ikianza 28 Novemba 2015 na kufikia tamati 20 Februari 2016 ilikuwa ni ya aina yake na kutoa mwangaza wa kimaendeleo wa kimichezo ambapo pia imesaidia kuimarisha afya, ushikamano na undugu kwa baina ya wachezaji na washangiliaji ambao wengi wao walitoka katika mabenki shiriki 15 ikiwemo matawi yao ya Tanzania Bara na Visiwani.
Katika tukio hilo, washindi mbalimbali walipatiwa vyeti vya shukrani hii ni pamoja na wadhamini wa mashindano hayo ikiwemo kutoka mabenki, kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) na makampuni mengine walipewa vyeti vya shukrani katika kufanikisha michuano hiyo.
Tazama MO tv Online, kuona tukio hilo hapa:
Imeandaliwa na Andrew Chale,Modewjiblog/MO tv)Nao
Mwakilishi kutoka MeTL Group, Bw.Zainul Mzige (kulia) akikabidhi cheti cha ushindi kwa Mchezaji Nuhu Mkuchu kutoka benki ya NMB.
nape bora
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye akikabidhi tuzo ya golikipa bora, Gabriel Bernard.
Nape boraa
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye akikabidhi tuzo ya mfungaji bora mchezaji kutoka benki ya NMB, Ahmed Nassoro.
nape ddfBaadhi ya washiriki na wageni mbalimbali walifika katika tukio hilo...
nape ff
Mratibu wa michuano hiyo Brazuka Kibenki, Bi. Nasikiwa Berya akikabidhi cheti kwa mmoja wa washindi wa michuano hiyo..
nape fg
Mratibu wa michuano hiyo, Nasikiwa Berya akikabidhi cheti kwa mshindi..
nape h
Waratibu wa mashindano ya Brazuka Kibenki, Bi.Nasikiwa Berya akiwa na Raymond Bunyinyiga wakifurahia jambo kutoka kwa Waziri wa Habari, Nape Nnauye. (Hayupo pichani).
Nape mchezji
Waziri Nape akimkabidhi tuzo ya mchezaji Bora, Ahmed Nassoro.
nape na maliz
Rais wa shirikisho la Soka nchini, (TFF), Jamal Malinzi akikabidhi cheti cha ushind kwa moja ya washiriki wa michuano ya Brazuka Kibenki.
nape oo
Mratibu wa michuano hiyo, Nasikiwa Berya akikabidhi cheti kwa mshiriki..
nape rr
Baadhi ya washiriki..
nape vbc
zoezi likiendelea..
nape vbv
Utoaji wa vyeti ukiendelea..
Nape yu
Waziri Nape akimkabidho tuzo, Kocha Bora, Bw. Mohamed Hussen 'Machinga' ambaye aliwahi kuwa mchezaji wa timu za Taifa na klabu kubwa za Tanzania ikiwemo Simba.
NAPE ZANI
Mwakilishi kutoka MeTL Group, Zainul Mzige akikabidhi cheti kwa mmoja wa washindi wa michuano ya Brazuka Kibenki. Zainul alikabidhi cheti hicho akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group), Mohammed Dewji 'MO'.
nape zx
Waziri Nape akimkabidhi cheti Rais wa TFF, Jamali Malinzi, ambapo cheti hicho ni maalum kwa TFF kuongeza mchango wao kaatika kukuza michezo nchini..
Nape4rt
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Nape112
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Nape112
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Napecheti
Rais wa TFF akikabidhi tuzo hizo
naper tyu
Utoaji wa tuzo hizo ukiendelea..
napess
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
NAPESSS
wageni waalikwa na washiriki kutoka mabenki mbalimbali..
Napeww
Waziri Nape akitoa tuzo hizo..
Npaae
Mwakilishi kutoka MeTL Group, Zainul Mzige akitoa vyeti kwa washiriki
Npe2
Baadhi ya washindi walifanikiwa kutwaa tuzo hizo za Brazuka Kibenki kutoka benki ya NMB.
Npe222
Wachezaji bora 11, wakipata picha ya pamoja..
npe44
Waziri Nape Nnauye akitoa nasaha fupi katika tukio hilo..
Nape22
Mwandishi Mwandamizi wa habari wa mtandao wa Modewjiblog, Bw. Andrew Chale akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi kutoka MeTL Group, Zainul Mzige.
Npe33
Baadhi wa washriki na washindi wa Brazuka Kibenki..
Nape2
Hapa ilikuwa ni furaha kwa washiriki katika tukio hilo la Brazuka Kibenki..
Nape
Ilikuwa ni mwendo wa kucheza na kufurahia Kibrazuka..
Nape
Waziri Nape akipeana mkono naMwakilishi wa MeTL Group, Zainul Mzige katika meza kuu ya wageni waalikwa. Zainul Mzige alimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa MeTL Group, Mohammed Dewji 'MO'.
Nape222
Baadhi ya washiriki wakipata picha za ukumbusho katika tukio hilo.