WAVUVI WATAKIWA KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA KUEPUKA VIFO, KUPOTEZA MALI

April 08, 2022

 


Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua kulia akiwaonyesha wavuvi wa Mwalo wa Sahare Jijini Tanga namna ya kuvaa vifaa vya kujiokolea wanapokuwa majini wakati alipokwenda akizungumza na wavuvi, wamiliki wa vyombo, manahodha na wananchi wa Vijiji vya Monga Vyeru wilayani Mkinga na Mwalo wa Sahare Jijini Tanga mkoani Tanga kutoa elimu ya umuhimu wa usalama na utunzaji wa mazingira
Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua kulia akiwaonyesha wavuvi wa namna ya kuvaa vifaa vya kujiokolea wanapokuwa majini wakati alipokwenda akizungumza na wavuvi, wamiliki wa vyombo, manahodha na wananchi wa Vijiji vya Monga Vyeru wilayani Mkinga mkoani Tanga  kutoa elimu ya umuhimu wa usalama na utunzaji wa mazingira
Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua kulia akiwaonyesha wavuvi wa Mwalo wa Sahare Jijini Tanga vifaa vya kujiokolea wanapokuwa baharini ambavyo ni muhimu kuhakikisha wanakuwa navyo kabla ya kuingia majini kufanya shughuli zao wakati wa utoaji wa elimu ya umuhimu wa usalama na utunzaji wa mazingira

Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua kulia akisisitiza jambo kwa wavuvi wa mwalo wa Sahare Jijini Tanga wakati wa utoaji wa elimu ya umuhimu wa usalama na utunzaji wa mazingira
Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua kulia akisisitiza jambo wakati akizungumza na wavuvi, wamiliki wa vyombo, manahodha na wananchi wa Vijiji vya Monga Vyeru wilayani MkingaAfisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua kulia akizungumza  jambo wakati akizungumza na wavuvi, wamiliki wa vyombo, manahodha na wananchi wa Vijiji vya Monga Vyeru wilayani Mkinga


AFISA Uhusiano Mwandamizi wa Shirika la TASAC Kitengo cha Mahusiano na Masoko Amina Miruko akizungumza wakati wa utoaji wa elimu
kwa wavuvi, wamiliki wa vyombo, manahodha na wananchi wa Vijiji vya Monga Vyeru wilayani Mkinga

Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua kulia akifuatilia kwa umakini maswali kutoka kwa wavuvi,wamiliki wa vyombo



Afisa Masoko Mwandamizi wa Shirika la TASAC Martha Kalvin akieleza jambo kwa wavuvi kuhusu umuhimu wa usalama wawapo kwenye shughuli zao

Sehemu ya wavuvi,wamiliki wa vyombo na manahodha wakimsikiliza Ofisa Mfawidhi wa TASAC Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua elimu ya umuhimu wa usalama na utunzaji wa mazingira.

NA OSCAR ASSENGA, TANGA.

SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limesisitiza umuhimu wa wavuvi kuzingatia usalama ikiwemo kuwataka kuacha kufanya kazi kwa mazoea wanapokuwa katika shughuli za Uvuvi wawapo majini ili kuwaepusha na vifo,majeruhi na kupoteza mali.

Huku wakisisitiziwa umuhimu wa kuwa na vifaa vya kujiokolea wanapokuwa majini ili viweze kuwasaidia kuepukana na ajali ambazo wanaweza kukumbana nazo.

Wito huo ulitolewa leo na Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Captain Christopher Shalua wakati na akizungumza na wavuvi, wamiliki wa vyombo, manahodha na wananchi wa Vijiji vya Monga Vyeru wilayani Mkinga na Mwalo wa Sahare Jijini Tanga mkoani Tanga walipokwenda kutoa elimu ya umuhimu wa usalama na utunzaji wa mazingira.

Alisema kwamba ni muhimu kwao kuweza kuhakikisha wanazingatia usalama wakati wanapokwenda kufanya shughuli zao kwani hilo litawaepusha na majanga ambayo wanaweza kukutana nayo na kupelekea kupata majeraha au kupoteza maisha na mali.

“Serikali imeona hilo ni jambo la msingi sana na ndio maana tumeona leo tuje hapa Monga Vyeru kuwapa elimu hii ya usalama  na utunzaji wa mazingira hususani mnapokuwa kwenye shughuli zenu hili ni jambo hilo lakini pia kuhakikisha mnakuwa na vifaa vya uokozi”Alisema

“Kwani tunatambua kwamba pia wavuvi wana familia hivyo elimu hii itaweza kuwasaidia kupunguza ajali,kuondoa vifo na kupunguza majeruhi na kuacha familia kuwa tegemezi”Alisema

Afisa Mfawidhi huyo alisema shughuli za usalama sio jambo la mtu mmoja bali ni watu wote hivyo lazima wahakikisha wanazingitia sheria za usalama ikiwemo kuvaa majaketi ya kujiokolea "life jacket" ili yaweze kuwasaidia pindi wanapokumbana na dhoruba baharini waweze kujiokoa.

“Lakini pia kuhakikisha tunakuwa tunazingatia usalama tuwapo majini moto unawaka kutokana na mafuta hauwezi kuuzima na maji ni lazima uhakikisha unatumia mchanga au poda maalumu “Alisema

Hata hivyo alisema ni muhimu na vizuri kwa wenye vyombo vinavyotumika kwa ajili ya shughuli za uvuvi wanakuwa na watu wenye ujuzi na kufanya kazi za majini ikiwemo wajibu wa mmiliki kutii sheria bila shuruti kuhakikisha usalama wake.

Hata hivyo Afisa Mfawidhi huyo aliwataka kuhakikisha kabla hawajaingia majini kuendelea na shughuli zao lazima wawe na cheti kutoka kwenye Shirika hilo ambavyo vinawaruhusu kufanya kazi majini.

“Lakini suala jingine sheria imemuelekeza Afisa Uvuvi asipope leseni ya uvuvi mpaka awe amepata cheti cha Shirika la TASAC cha kuruhusiwa kufanya kazi majini ”Alisema

ULEGA-TUTAENDELEA KULINDA RASILIMALI ZA UVUVI ILI ZIWALINDE WATANZANIA

April 08, 2022

 

.Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (kushoto) akimueleza Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye (kulia) namna Wizara yake ilivyojipanga kuwainua wavuvi wa Ziwa Tanganyika muda mfupi baada ya kufika ofisini kwa Mkuu wa mkoa huyo leo (08.04.2022).Mkurugenzi Mkazi wa Kampuni ya kimataifa ya kusafirisha mizigo ya DHL, Bw. Paulo Makolosi (kulia) akimuonesha Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalla Ulega jinsi kampuni hiyo inavyofanya kazi zake ikiwa ni muda mfupi kabla ya makabidhiano ya Boti ya doria ya uvuvi yaliyofanyika leo (08.04.2022) kwenye Fukwe za Hoteli ya Hiltop mkoani Kigoma.Mkurugenzi Mkazi wa Kampuni ya kimataifa ya kusafirisha mizigo ya DHL, Bw. Paulo Makolosi (kushoto) akimkabidhi Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalla Ulega boti ya doria ya Uvuvi kwenye hafla iliyofanyika leo (08.04.2022) kwenye Fukwe za Hoteli ya Hiltop mkoani Kigoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah.


 

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa Wizara yake itahakikisha inalinda rasilimali za Uvuvi wakati wote ili ziendelee kuwa mkombozi kwa wananchi wanaozunguka vyanzo mbalimbali vya maji ya asili vilivyopo hapa nchini.

Mhe. Ulega ameyasema hayo leo (08.04.2022) wakati wa hafla ya makabidhiano ya boti ya doria ya uvuvi iliyotolewa na Kampuni ya kimataifa usafirishaji wa mizigo ya DHL tukio lililofanyika kwenye ufukwe wa hotel ya Hiltop mkoani Kigoma.

"Kwa sasa tuna kikosi cha wataalam ambacho ni kitengo cha kulinda rasilimali zilizopo katika Ziwa Tanganyika na mtu anaweza asielewe umuhimu wa kazi inayofanyika lakini ni lazima tutekeleze jukumu hili ili kuhakikisha rasilimali hizi zinakinufaisha kizazi kilichopo na kijacho na ninatambua suala hili sio jepesi kwetu kwa sababu kuna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakinufaika kwa kutumia njia zisizo halali kwenye shughuli zao za Uvuvi" Amesisitiza Ulega.

Mhe. Ulega amesema kuwa Wizara ina mpango wa kukiongezea zaidi uwezo kikosi kazi hicho ili kiweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ambapo alibainisha kuwa wameshawasilisha mawazo ya kukiongezea nguvu kikosi hicho kwa mamlaka za juu ili kiweze kuwa na vitendea kazi vya kisasa na kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo wakati wakitekeleza majukumu yao.

"Hawa wanaobeza kazi ya ulinzi wa Rasilimali hizi siku wakiamka na kukuta hakuna samaki watakosa shughuli ya kufanya na watatuuliza wataalam tulikuwa tunafanya shughuli gani hivyo naomba muendelee na shughuli yenu ya ulinzi wa rasilimali hizi ili tuendelee kuunga mkono kampeni ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya Uchumi wa buluu ambao utamnufaisha kila mwananchi na Taifa kwa ujumla" Amesema Ulega.

Mhe. Ulega ameipongeza kampuni hiyo kwa kutoa boti hiyo ya ulinzi wa rasilimali za Uvuvi ambapo mbali na kutekeleza jukumu hilo la msingi amewataka wataalam watakaoisimamia kuhakikisha inatumika kutoa msaada hata kwa wavuvi watakaokumbana na changamoto mbalimbali wakiwa kwenye shughuli zao majini.

Mhe. Ulega ameishukuru kampuni ya DHL kwa msaada wa boti hiyo ambayo inafanya idadi ya jumla ya boti za doria zinazofanya kazi kwa upande wa Ziwa Tanganyika kuwa 10 huku nyingine ya 11 itakayokuwa ukanda wa Kigoma ikitarajiwa kutolewa na Serikali kabla ya Mwezi Mei mwaka huu.

"Sisi pale Wizarani tumekubaliana Dagaa la Kigoma liwe moja ya mazao yetu ya kimkakati na DHL wameiona hiyo fursa ambapo wao wameamua kujikita kwenye kuongeza thamani ya bidhaa hiyo mpaka inafika kwa mlaji huko nje ya nchi na niwaombe wadau wengine wenye nia ya kutumia fursa zilizopo Ziwa Tanganyika na kwingineko waje kwa sababu Serikali yetu inawakaribisha sana wawekezaji wenye nia ya kukuza uchumi wa mwananchi na kuongeza pato la Taifa " Amesema Ulega.

Akibainisha umuhimu wa boti hiyo kwa upande wa shughuli za Uvuvi, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah amesema kuwa itasaidia kuwezesha uvunaji endelevu wa rasilimali za uvuvi katika Ziwa Tanganyika.

"Kwa mujibu wa taarifa ya takwimu za Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya mwaka 2018 inaonesha kuwa Ziwa Tanganyika linaajiri moja kwa moja wavuvi 26612 ambao hutumia vyombo vya uvuvi 11506 na zaidi ya watu laki 7 hunufaika na shughuli zinazofanyika upande wa Ziwa Tanganyika" Amesema Dkt. Tamatamah.

Mbali na boti hiyo Dkt. Tamatamah amesema kuwa boti nyingine 9 zinazofanya kazi kwa upande wa Ziwa Tanganyika zipo katika vituo vya Kipili, Kasanga, Ikola na moja ikiwa katika kituo cha Buhingu.

Kwa upande wake Mkurugenzi mkazi wa kampuni hiyo hapa nchini Bw. Paulo Makolosi amesema kuwa wakati wanafika mkoani Kigoma walikuta wasafirishaji wa dagaa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upoteaji wa mizigo yao ikiwa njiani, kupotea kwa ubora wa mazao hayo na kutokuwa na vifungashio bora vya kusafirishia mizigo yao.

"Dagaa walikuwa wakiuzwa kwenye mifuko maarufu kama "shangazi kaja" hivyo tukachukua jukumu la kulialika Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ambalo lilitoa mafunzo zaidi ya mara sita hapa Kigoma ambapo tuligharamia kila kitu ili kuhakikisha wafanyabiashara wa Kigoma wanabadilika na kufanya shughuli zao kwa kuzingatia viwango stahiki" Amesema Makolosi.

Ameongeza kuwa baada ya kumaliza mafunzo hayo, waliamua kutoa msaada wa vifungashio ambavyo vitasaidia kuzifanya bidhaa hizo zinazosafirishwa kutopoteza ubora wake hata zikikaa kwa muda mrefu.
 
Katika kuhakikisha sekta ya Uvuvi inaendelea kukua, Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imewekeza kwenye miundombinu ya masoko na mialo ya kisasa ya kupokelea samaki ukiwemo mwalo wa Kibirizi uliopo Kigoma, soko la Kasanga lililopo Sumbawanga, mwalo wa Ikola uliopo Katavi na soko la Kirando lililopo mkoani Rukwa.