RAIS MAGUFULI AKUTANA NA RAIS WA JICA
JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI
YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425 |
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21
Agosti, 2017 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirika la Kimataifa la
Maendeleo la Japan (JICA),Bwana Shinichi Kitaoka Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Katika
Mazungumzo hayo Bw. Kitaoka amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa uongozi mzuri na
wa mfano hususani katika kupambana na rushwa na msukumo mkubwa anaoutoa katika
maendeleo hususani katika kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda. Jitihada zinazosaidia kuimarisha uchumi na kuboresha
huduma za kijamii na kuahidi kuwa JICA itaendelea kuwa mshirika mkubwa wa
maendeleo kwa Tanzania.
Bw.
Kitaoka ambaye ni mara yake ya kwanza kuitembelea Tanzania kama Rais wa JICA
amemuahidi Rais Dkt Magufuli kuwa miradi yote ya maendeleo ya nyuma na ya sasa
inayotekelezwa kwa pamoja kati ya
Tanzania na JICA itamalizika kwa wakati ikiwemomradi wa ujenzi wa
barabara za juu (Flyover) wa TAZARA
unaoendelea kujengwa hivi sasa,mradi wa ujenzi wa barabara ya Mwenge - Moroco
yenye urefu wa kilomita 4 nukta 3 pamoja na mradi wa ujenzi wa daraja la
Gerezani.
“Tumefikia
makubaliano mazuri kuhusiana na miradi tunayoendelea kuitekeleza hapa nchini na
wananchi watarajie kuona kazi zikifanyika kuanzia mwezi june,mwakani hususani
katika ujenzi wa daraja la gerezani na mingineyo”
Kwa
upande wake Mhe. Dkt Rais Magufuli amemshukuru Rais huyo wa Shirika la
Kimataifa la Maendeleo la JapanBw. Shinichi Kitaoka kwa uamuzi wake wa kuja
Tanzania na amemhakikishia kuwa Tanzania inatambua mchango mkubwa ambao Japan
inautoa katika maendeleo ya Tanzania kupitia JICA, na kwamba itaendeleza na
kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wake na Japan katika masuala mbalimbali.
Mhe.
Rais Magufuli ameishukuru JICA kwa kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi
mikubwa ya ujenzi jijini Dar es Salaamikiwemo upanuzi wa barabara ya Mwenge –
Morocco, utakaoiwezesha barabara hiyo kuwa na zaidi ya njia nane, ujenzi wa
barabara ya TAZARA, ujenzi wa Daraja la Gerezani njia nne, na barabara ya
Bendera tatu hadi Kamata.
“Tunathamini
sana mchango unaotolewa na walipa kodi wa Japan kupitia JICA katika kutekeleza
miradi ya maendeleo hapa nchini na ninakuomba kuangalia uwezekano wa kufadhili
na kujenga miundo mbinu na miradi mbalimbali ya maendeleo katika Makao Makuu ya
nchi Dodoma ambako serikali imedhamiria kuhamia huko ili kuweka alama ya
urafiki na mahusiano mema yaliyopo kati ya Tanzania na Japan”
Mazungumzo
hayo yamehudhuriwa na Balozi wa Japan hapa nchini Mhe. Masaharu Yoshida,Katibu
Mkuu wizara ya Fedha na Mipango Doto James,Katibu Mkuu Ujenzi Mhandisi Joseph
Nyamhanga na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini Mhandisi Patrick
Mfugale.
Emmanuel
Buhohela,
Mwandishi
wa Habari,Msaidizi wa Rais,
Dar
es Salaam.
21
Agosti, 2017
UBER YAZINDUA HUDUMA YA MADEREVA NA WASAFIRI KUCHATI KWA KUTUMIA PROGRAMU HIYO
Dar es Salaam
Tarehe 21 Agosti 2017…Kampuni ya Uber nchini Tanzania imetangaza zana mpya
maarufu kama “Kuchati Ndani ya Programu” inayowawezesha madereva na wasafiri
kuandikiana ujumbe kwa kutumia programu hiyo bila malipo.
Kinyume na hapo
awali ambapo madereva na wasafiri wangetumia Ujumbe Mfupi (SMS) au kupiga simu,
zana hii inaleta unafuu kwa madereva na wasafiri hivyo basi kuwapunguzia kadhia
ya gharama za kupiga simu sambamba na kuharakisha mawasiliano bila kuondoka kwenye
programu ya Uber.
Maboresho haya ni
juhudi endelevu za Uber na yanalenga kuimarisha wigo wa wasafiri na madereva
wanapotumia programu ya Uber.
Zana hii mpya ni
rahisi sana kuitumia. Msafiri anapoita gari, kuna kitufe cha ‘Kuwasiliana’
kwenye menyu inayoonekana chini ya skrini. Wasafiri wanaweza kuwaandikia ujumbe
madereva, na madereva vivyo hivyo. Ujumbe utaonesha kwamba umepokelewa baada ya
kuutuma.
Kwa upande
mwingine, madereva watakiri kwamba wamesoma ujumbe kwa kugusa kwenye programu
ya Uber ili watume ujumbe wa ‘bomba’. Ili wasijichanganye barabarani.
Aidha wasafiri na madereva wanaweza kuona kama ujumbe wao waliotuma umesomwa.
Meneja Msimamizi wa
Uber nchini Tanzania Bw. Alfred Msemo amehoji kwamba, “Kila safari nzuri huanza
pale msafiri anapochukuliwa kwa gari, kwa hiyo tunajituma kutafuta mbinu za
kumchukua msafiri bila usumbufu wowote kwa msafiri au dereva. Kipengele hiki
cha Kuchati kitakuwa afueni kwa wasafiri na madereva wanapotaka kuwasiliana ili
kusaidiana kutafuta mwafaka wa changamoto za safari kama vile, kufungwa kwa
barabara au kutoa maelezo ya mahali walipo.”
Kadhalika,
kipengele hiki kinatoa njia mbadala ya wasafiri na madereva kupiga simu
wanapotaka kuwasiliana. Hata hivyo, ili mtu atumie kipengele hiki anatakiwa awe
anatumia toleo la sasa la program ya Uber.
“Huu ni mwanzo tu
wa mchakato wa kuimarisha huduma za kutuma ujumbe moja kwa moja kwenye programu
ili kufanikisha wigo wa mawasiliano yasiyo na changamoto kwa wateja wetu, na
kuwasaidia kuwasiliana katika ulimwengu wa utandawazi na ulimwengu halisi”
amenukuliwa Bw. Msemo.
RANGI ZA KANSAI PLASCON ZATAMBULISHWA RASMI JIJINI ARUSHA
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kansai Plascon Tanzania Amin Habib akihutubia wageni waalikwa katika ya hafla ya kununua oparesheni za Kampuni ya Rangi ya Sadolin nchini. |
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kansai Plascon Tanzania Amin Habib akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya hafla ya kununua oparesheni za Kampuni ya Rangi ya Sadolin nchini. |
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kansai Plascon Tanzania Amin Habib, akiongea Na Distributors wa Arusha kuhusu ununuaji wa operasheni za Kampuni ya Rangi ya Sadolin. |
Wadau wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya hafla ya kununua oparesheni za Kampuni ya Rangi ya Sadolin nchini |
Kansai Plascon yainunua Kampuni ya rangi ya Sadolin ya Tanzania
Arusha: Kampuni ya Kansai Plascon Afrika ltd. Ambayo ni kampuni tanzu ya kampuni ya rangi ya Kansai iliyoko Japan, imehitimisha makubaliano yake ya kununua shughuli za rangi za Sadolin nchini Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki. Hii ilitangazwa na Deodatus Makumpa Meneja wa Kanda ya Kaskazini, Plascon Tanzania wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari katika Hotel ya Arusha Jijini Arusha
Kampuni ya rangi ya Kansai ni kampuni ya kimataifa ambayo inaendesha shughuli zake nchini Japan, China, Mashariki ya Kati, Ulaya na Afrika. Bidhaa zake inazotoa zinajumuisha upambaji, Viwanda, rangi za kulinda na mitambo, ina vituo vya utafiti na maendeleo nchini Japan, India na Afrika Kusuni.
“Tumefurahishwa na mafanikio haya. Kupitia haya, tutaweza kutumia nembo yenye nguvu ya urithi wa Kansai, uwezo wa kimataifa wa kiufundi, na utendaji wa kuaminika, kutupatia uwezo mpya, kuweza kupata teknolojia mpya na utambuzi ambao ni muhimu zaidi katika kuendelea kukuza nembo hii,” alisema Makumpa
Akiongea kuhusu sababu za kuinunua, Gary van der Merwe, Rais wa Kampuni ya Plascon Afrika Mashariki alisema kwamba makubaliano haya yanadhihirisha nia ya Kansai Plascon katika kujiendeleza zaidi duniani. “Afrika Mashariki ni moja kati ya ukanda ambao unakuwa haraka zaidi kiuchumi barani Afrika. Kwa ukuaji wa kasi wa daraja la kati, kuongezeka kwa nguvu ya utumiaji na kukua kwa miji, huu ni muda muafaka wa kuingiza sokoni bidhaa zetu mbali mbali kwaajili ya kuboresha zaidi mtindo wa maisha yao wakati huo huo tukiwa tunaongeza kuenea kwetu duniani”.
Ununuzi huu hautakuwa na mabadiliko katika uongozi wa juu na nafasi zozote zingine katika kampuni ya Sadolin. Kampuni itaendelea kufanya shughuli zake kama ambavyo ilikuwa ikifanya kwa kutumia wafanyakazi waliopo. Amin Habib ambaye anakalia kiti cha Mkurugenzi Mtendaji amesema kwamba ununuzi huu utapelekea katika matokeo bora na ufanisi zaidi ambao utanufaisha kampuni hii ya rangi. Kuanzia katika teknolojia mpya na iliyoboreshwa kutoka katika kampuni ya rangi ya Kansai ambayo ni kampuni ya kumi ya rangi duniani.
Tangu ianzishwe mwaka 1967 nchini Tanzania, kampuni ya rangi ya Sadolin imekua na kuwa kampuni kubwa zaidi ya uzalishaji wa rangi, ikiwa inajivunia zaidi ya 50% ya soko katika rangi za kulinda naza kutengenezea magari.
Amin Habib amewahakikishia wateja kwamba mabadiliko haya hayatakuwa na athari zozote katika utaratibu wa uendeshaji wa shughuli za kampuni uliopo sasa. Lakini mabadiliko yanakuja na mbinu bora za uendeshaji kwaajili ya kuwahudumia vyema wateja, kwa ufanisi zaidi na kwa bidhaa zenye kiwango ambazo hawakutarajia.” Wauzaji wetu wote, Maghala na maduka yatabakia kuwa wazi kuwahudumia kwa bei ile ile nzuri ambayo wamekuwa ukiifurahia kwa miaka mingi. Katika miezi michache ijayo, tukiwa tunakamilisha mabadiliko, tutaanza kuingia katika kutekeleza makubaliano ya mkataba, kumalizia bidhaa zenye nembo ya Sadolin kutoka katika maghala yetu na kuwasisitiza wateja wetu kuuliza bidhaa zenye nembo ya Plascon kutoka kwa wauzaji wao”.
Kwa kutambua kwamba kununua na kujiunga kwa makampuni huja na hali ya kutokuwa na uhakika katika mtazamo wa raslimali watu na mtazamo wa kiuendeshaji, Gary van der Merwe alisema kwamba kwa kuwa Sadolin kama biashara tayari ilikuwa inaendesha shughuli zake kwa ufanisi, mkakati utakuwa ni kuboresha zaidi na kuongeza katika uendeshaji uliopo ili kuboresha ufanisi.
“Tutafanya kazi ya kupanua zaidi teknolojia ya hali ya juu iliyopo ambayo tumeikuta ikiwa inafanyakazi. Lengo letu litabakia katika kuwekeza katika teknolojia ya kiwango cha juu kuwapa wateja wetu rangi za kiwango cha juu zaidi katika soko.” Alisema.
Lengo letu ni kudumisha nafasi yetu kama wazalishaji wa rangi wanaoongoza Tanzania na Afrika Mashaririki kwa kuendelea kuboresha ili kuweza kufikia mahitaji ya wateja wetu yanayobadilika kila siku na kubakia washindani katika soko. “Soko la Tanzania wanaweza kutarajia kuanza kutumia application ya simu ya Plascon Visualizer, ambayo itawaruhusu watu kucheza na kufanya majaribio ya rangi kwaajili ya nyumba zao na miradi yao kabla ya kwenda kwa wauzaji kutoa oda zao.”
Sadolin imefurahia nafasi yake na kushikilia soko la rangi katika kanda hii. Ununuzi huu utaongeza mapato ya Kansai Plascon na nafasi yake kama ambavyo inataka kuimarisha nafasi yake kama kampuni ya rangi inayoongoza Afrika.
Subscribe to:
Posts (Atom)