HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TANZANIA YASHIRIKI JUKWAA LA UTALII, BIASHARA NA UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA MISRI

June 08, 2026 Add Comment
Cairo, Misri,

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbasi leo Juni 8, 2026 ameshiriki Ufunguzi wa Jukwaa la Utalii, Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Misri linalofanyika jijini Cairo, likiwakutanisha viongozi wa Serikali, taasisi za utalii, wafanyabiashara, wawekezaji na wadau mbalimbali kutoka nchi hizo mbili kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kukuza fursa za biashara, uwekezaji na utalii.

ARUSHA KUWA KITOVU CHA WATAFITI WA AFYA, WASHIRIKI 450 KUKUTANA KATIKA KONGAMANO LA NIMR

June 08, 2026 Add Comment

 Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Prof. Said Aboud

📍8 Juni, 2026
Arusha

Takribani washiriki 450 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kushiriki katika Kongamano Kuu la 33 la Mwaka la Kisayansi la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) litakalofanyika jijini Arusha kuanzia Juni 9 hadi 11, 2026. Mgeni rasmi katika ufunguzi wa kongamano hilo anatarajiwa kuwa Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa (Mb.), Waziri wa Afya.

RAIS SAMIA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI KILICHOFANYIKA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

June 08, 2026 Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 08 Juni, 2026.







 

 

MPANGO KAZI WA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI AFDP WAFANYIWA MAPITIO

June 08, 2026 Add Comment


NA; Mwandsihi Wetu – Chato

Wataalamu kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP ) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu wamekutana Mjini Chato Mkoani Geita tarehe 8 Juni 2026 kwa lengo la kufanyia mapitio mpango kazi wa Programu hiyo.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi hicho, Mhandisi Enock Nyanda, Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Sekta za Uchumi na Uzalishaji Idara ya Tawala za Mikoa Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI alisema lengo la wataalam hao kukutana ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya kikao cha Mawaziri kilichofanyika mapema mwezi Mei mwaka huu.
Katika kikao hicho pamoja na mambo mengine kiliwataka wataamu hao kufanya mapitio ya kiutendaji katika mpango kazi wa utekelezaj wa Programu hiyo ikiwa ni pamoja na kuwasilisha na kujadili kazi, mapitio ya bajeti sambamba na kufanya tathmini fupi ya kila utekelezaji wa Programu.

Aidha timu hiyo ya wataalam pia itaandaa shughuli zitakazotekelezwa na program kwa mwaka 2027 ilikuweza kufikia malengo pamoja na kutembelea maeneo ya utekelezaji wa Mradi ya Rubambagwe Wilayani Chato pamoja na Kilimi Wilayani Nzega Mkoani Tabora.

Sekta zinazotekeleza Progreamu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) ni Pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Kilimo, Shirika la Uvuvi nchini TAFICO, Shirika la Uvuvi Zanzibar ZAFICO, Wizara ya uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Wakala wa Mbegu Nchini ASA, Taasisi ya Uthibiti wa Ubora wa Mbengu Nchini TOSCI na Taasisi ya utafiti wa Mbegu za Kilimo Nchini TARI














SERIKALI YAINGIA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO NA DIT KUIMARISHA USIMAMIZI WA MAAFA

June 08, 2026 Add Comment
Na, mwandishi wetu – Dar es Salaam

SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) imeingia Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) na Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) yenye lengo la kuimarisha usimamizi wa maafa nchini kwa kutumia sayansi, teknolojia na ubunifu.

WAZIRI MAVUNDE KUFUNGUA WIKI YA 11 YA UTAFITI NA UBUNIFU UDSM

June 08, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yatakayofanyika kuanzia Juni 9 hadi 11, 2026, yakilenga kuonesha mchango wa utafiti na ubunifu katika maendeleo ya taifa.

RAYTON KWEMBE: TULIWEKEZA KWENYE RASILIMALI WATU NDIO MAANA FORBES IMETUTAMBUA KAMA KAMPUNI YENYE UBORA WA JUU UJENZI WA MELI NCHINI

June 08, 2026 Add Comment

  


Na Mwandishi Wetu 

Jarida la Forbes Africa limetaja Kampuni ya Kitanzania, Dar es Salaam Merchant Group - DMG, kama kampuni bora ya daraja la kwanza “Class One” katika eneo la ujenzi na ukarabati wa meli nchini Tanzania.

Jarida hilo maarufu Afrika na duniani limeitaja DMG mara baada ya ufanisi mkubwa kwenye ukarabati unaoendelea wa Meli ya MV Liemba - meli kongwe zaidi duniani inayobeba abiria, iliyotengenezwa na Wajerumani zaidi ya miaka 110 iliyopita.

GCLA YASISITIZA UDHIBITI WA KEMIKALI HATARISHI

June 08, 2026 Add Comment
Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko, akizungumza wakati akifungamkutano Mkuu wa mwaka wa Wakaguzi wa Kemikali na Maabara za Kemia(hawapo pichani), mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteliya Arusha Corridor Spring Juni 5-6, 2026.

VIJANA NA WASOMI MKOANI MWANZA WAHIMIZWA UZALENDO NA UJASIRIAMALI KATIKA KONGAMANO

June 08, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

​Katika jitihada za kuimarisha chachu ya maendeleo, Kongamano la Wasomi lililoandaliwa na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Seneti Mkoa wa Mwanza, limefanyika leo, Juni 07, 2026, katika Chuo cha Uvuvi Nyegezi, likilenga kuwajengea vijana uwezo katika nyanja za uongozi, uchumi, afya, na itikadi ya chama.

SMZ YATAJA MAFANIKIO YA BIMA YA LAZIMA KWA WAGENI

Kajunason June 07, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Arusha.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imetumia Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Karibu-KiliFair 2026 kutangaza mafanikio ya mpango wa bima ya lazima kwa wasafiri, ikieleza kuwa umeimarisha usalama wa wageni na kuchangia ukuaji wa sekta ya afya pamoja na mapato ya utalii visiwani humo.

Mpango huo ulioanza kutekelezwa rasmi Oktoba 1, 2024, unawataka wageni wote wa kimataifa wanaoingia Zanzibar kuwa na bima ya usafiri kabla ya kuwasili. Tangu kuanzishwa kwake, mpango huo umeendelea kuwa chanzo muhimu cha mapato, ukiingiza wastani wa dola za Marekani milioni moja, sawa na zaidi ya Sh bilioni 2.6 kila mwezi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) kwenye viwanja vya Magereza jijini Arusha, Ofisa Mauzo wa shirika hilo, Abdul-Halim Muhammad, alisema maonesho hayo yamewapa fursa ya kutoa elimu kwa watalii, wawekezaji na wadau wa sekta ya utalii kuhusu umuhimu wa bima hiyo.

“Tunashiriki Karibu-KiliFair kuongeza uelewa kuhusu bima hii ya lazima na kueleza namna inavyowanufaisha wageni huku ikichangia maendeleo ya huduma muhimu Zanzibar,” alisema.

Kwa mujibu wa utaratibu huo, wageni wengi wa kimataifa hulipa dola 44 za Marekani kwa kila safari ya kuingia Zanzibar, huku wageni kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wakilipia dola 22 pekee. Watoto wenye umri wa miaka mitatu hadi 17 hulipa dola 22, huku walio chini ya umri huo wakisamehewa.

Muhammad alisema bima hiyo inawawezesha wageni kupata huduma za matibabu ya dharura na msaada mwingine muhimu wanapokuwa Zanzibar, hatua inayopunguza changamoto za kifedha na kuhakikisha wanapata huduma kwa haraka wanapozihitaji.

Alisema sehemu ya mapato yanayokusanywa kupitia mfuko huo hutumika kugharamia huduma za afya kwa wageni waliokatiwa bima, huku fedha zinazobaki zikielekezwa katika kuimarisha huduma za afya kwa wananchi na wageni kwa ujumla.
“Mpango huu ulianzishwa baada ya mamlaka kubaini kuwepo kwa matukio ya mara kwa mara ya watalii na wawekezaji kuhitaji matibabu ya dharura huku kukiwa na sintofahamu kuhusu nani angegharamia huduma hizo. Sasa mfumo huu umeondoa changamoto hiyo,” alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa KiliFair Promotions, Dominic Shoo, alisema Karibu-KiliFair 2026 imeendelea kuthibitisha nafasi yake kama maonesho makubwa ya utalii na biashara Afrika Mashariki kwa kuwakutanisha wadau kutoka zaidi ya nchi 40 duniani.

Alisema maonesho hayo yamevutia zaidi ya waoneshaji 500 na wanunuzi wa huduma za utalii wapatao 20,000, hatua inayochochea uwekezaji, ushirikiano wa kibiashara na upanuzi wa masoko ya utalii katika ukanda wa Afrika Mashariki.

“Karibu-KiliFair ni jukwaa muhimu la kuitangaza Tanzania na Afrika Mashariki kimataifa. Kadri wadau wanavyoongezeka kushiriki, ndivyo fursa za biashara, uwekezaji na ukuaji wa sekta ya utalii zinavyozidi kuongezeka,” alisema Shoo. 

MIGODI YA BARRICK YA BULYANHULU NA NORTH MARA YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI NA KUFUATILIA MRADI WA UREJESHAJI UOTO ASILI MTO TIGHITE

June 07, 2026 Add Comment

        

Wafanyakazi wa Barrick North Mara wakipanda miti kando kando ya Mto Tighite katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani Wilayani Tarime , Mkoani Mara.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi baada ya kushiriki zoezi la upandaji wa miti kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira duniani.
Afisa Mahusiano ya Jamii Mwandamizi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu , Zuwena Senkondo akimwagilia mti baada ya upandaji katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani

***

Kampuni ya Barrick inayoendesha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga, kupitia migodi yake ya Bulyanhulu na North Mara imeadhimisha Siku ya Mazingira Dunia 2026 kwa kushirikiana na jamii zinazoizunguka kwa kupanda miti, kufanya usafi kwenye shule na kukagua maendeleo ya mradi wa kurejesha uoto wa asili wa Mto Tighite uliopo wilayani Tarime.

BALOZI MATINYI AHIMIZA WAFANYABIASHARA WA TANZANIA KUSHIRIKI MAONESHO ALGIERS

June 07, 2026 Add Comment

 

Matinyi, akisalimiana na Waziri wa Biashara ya Kimataifa wa Algeria, Mhe. Kamel Rezig, wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Biashara ya Afrika jijini Algiers, mwishoni mwa wiki.

UDSM KUNG'ARA KWA UBUNIFU WA MADINI, AI NA NISHATI JADIDIFU

June 07, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinatarajia kuadhimisha Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu kuanzia Juni 9 hadi 11, 2026, katika Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere, huku Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akitarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Maadhimisho hayo yatakayowakutanisha watafiti, wabunifu, wanafunzi, sekta binafsi, taasisi za umma na wadau wa maendeleo, yanalenga kuonesha mchango wa utafiti na ubunifu katika kuharakisha maendeleo ya taifa na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Utafiti, Profesa Nelson Boniface, alisema maadhimisho ya mwaka huu yataongozwa na kaulimbiu isemayo: "Kutumia Utajiri wa Madini wa Tanzania katika Kukuza Nishati Jadidifu, Mageuzi ya Kidijitali na Usalama wa Jamii."

Alisema kaulimbiu hiyo imechaguliwa kutokana na umuhimu wa madini katika maendeleo ya teknolojia za kisasa ikiwemo Akili Mnemba (AI), vituo vya kuhifadhi taarifa (Data Centres), magari ya umeme na nishati jadidifu.

“Tunataka kuonesha namna Tanzania inaweza kutumia rasilimali zake za madini kuchochea mageuzi ya kidijitali, kuimarisha usalama wa nishati na kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” alisema Profesa Boniface.

Aliongeza kuwa maadhimisho hayo yatahusisha maonesho ya tafiti na ubunifu, mawasilisho ya kitaaluma, makongamano pamoja na majadiliano ya ushirikiano wa kimkakati yatakayowawezesha washiriki kubadilishana maarifa na kujenga mitandao ya kitaaluma na kibiashara.

Kwa mujibu wa UDSM, maadhimisho hayo yatatoa nafasi kwa watafiti na wabunifu kuonesha suluhisho mbalimbali za kisayansi na kiteknolojia zinazolenga kukabiliana na changamoto za maendeleo nchini katika sekta za madini, nishati, kilimo, afya na uchumi wa kidijitali.

Profesa Boniface alisema chuo kinaendelea kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kuunganisha taaluma, ubunifu na maendeleo ya taifa kwa kuwafikia wananchi, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo.

"Utafiti na ubunifu ni msingi wa maendeleo endelevu. Tunawaalika Watanzania wote kushiriki katika Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu UDSM 2026 ili kujionea kazi na mafanikio ya watafiti na wabunifu wetu," alisema.

MAADHIMISHO YA 11 YA UTAFITI NA UBUNIFU UDSM KUANGAZIA UCHUMI WA KIDIJITALI

Kajunason June 07, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinatarajia kuadhimisha Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu kuanzia Juni 9 hadi 11, 2026, katika Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere, huku Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akitarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Maadhimisho hayo yatakayowakutanisha watafiti, wabunifu, wanafunzi, sekta binafsi, taasisi za umma na wadau wa maendeleo, yanalenga kuonesha mchango wa utafiti na ubunifu katika kuharakisha maendeleo ya taifa na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Utafiti, Profesa Nelson Boniface, alisema maadhimisho ya mwaka huu yataongozwa na kaulimbiu isemayo: "Kutumia Utajiri wa Madini wa Tanzania katika Kukuza Nishati Jadidifu, Mageuzi ya Kidijitali na Usalama wa Jamii."

Alisema kaulimbiu hiyo imechaguliwa kutokana na umuhimu wa madini katika maendeleo ya teknolojia za kisasa ikiwemo Akili Mnemba (AI), vituo vya kuhifadhi taarifa (Data Centres), magari ya umeme na nishati jadidifu.

“Tunataka kuonesha namna Tanzania inaweza kutumia rasilimali zake za madini kuchochea mageuzi ya kidijitali, kuimarisha usalama wa nishati na kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi,” alisema Profesa Boniface.

Aliongeza kuwa maadhimisho hayo yatahusisha maonesho ya tafiti na ubunifu, mawasilisho ya kitaaluma, makongamano pamoja na majadiliano ya ushirikiano wa kimkakati yatakayowawezesha washiriki kubadilishana maarifa na kujenga mitandao ya kitaaluma na kibiashara.

Kwa mujibu wa UDSM, maadhimisho hayo yatatoa nafasi kwa watafiti na wabunifu kuonesha suluhisho mbalimbali za kisayansi na kiteknolojia zinazolenga kukabiliana na changamoto za maendeleo nchini katika sekta za madini, nishati, kilimo, afya na uchumi wa kidijitali.

Profesa Boniface alisema chuo kinaendelea kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kuunganisha taaluma, ubunifu na maendeleo ya taifa kwa kuwafikia wananchi, wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo.

"Utafiti na ubunifu ni msingi wa maendeleo endelevu. Tunawaalika Watanzania wote kushiriki katika Maadhimisho ya 11 ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu UDSM 2026 ili kujionea kazi na mafanikio ya watafiti na wabunifu wetu," alisema.

MUHEZA YAANZA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2026

June 06, 2026 Add Comment

 

DC awapongeza wananchi kwa mwitikio mkubwa wa Jogging

Na Oscar Assenga, Muheza

MAANDALIZI ya kuupokea Mwenge wa Uhuru 2026 katika Wilaya ya Muheza yamezidi kushika kasi baada ya wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki mazoezi ya Jogging yaliyoandaliwa ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na tukio hilo muhimu la Kitaifa.

Akizungumza baada ya mazoezi hayo, Mkuu wa Wilaya ya Muheza Ayoub Sebabili  aliwapongeza wananchi kwa mwitikio wao mkubwa, akisema ushiriki huo unaonyesha utayari wa wakazi wa wilaya hiyo kuupokea Mwenge wa Uhuru unaotarajiwa kuwasili Juni 23 mwaka huu.

Alisema mazoezi hayo yamelenga kuwaweka wananchi katika hali nzuri ya afya, kuimarisha mshikamano na kuwaandaa kimwili na kiakili kuelekea mapokezi ya mwenge huo.

“Tunawashukuru wananchi wote waliojitoa kushiriki mazoezi haya. Hii ni ishara nzuri ya ushirikiano katika maandalizi ya tukio muhimu la kitaifa ambalo Wilaya ya Muheza itakuwa mwenyeji wake,” alisema.

Mkuu huyo wa wilaya alibainisha kuwa jogging nyingine itafanyika Juni 13 mwaka huu na kutoa wito kwa wananchi ambao hawakupata nafasi ya kushiriki safari hii kujitokeza kwa wingi ili kuwa sehemu ya maandalizi hayo.

Alisisitiza kuwa mazoezi hayo ya kilomita tano yanafanyika kwa mwendo wa kawaida ili kuwezesha kila mwananchi kushiriki bila kujali umri au hali yake ya kiafya.

“Tunawakaribisha vijana, wanawake, wazee pamoja na watu wenye ulemavu kushiriki mazoezi haya. Lengo letu ni kuona wananchi wote wanakuwa sehemu ya maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru 2026,” alisema.

Muheza inatarajia kuupokea rasmi Mwenge wa Uhuru Juni 23, huku maandalizi mbalimbali yakiendelea kufanyika kuhakikisha tukio hilo linafanyika kwa mafanikio na kuacha alama chanya kwa wananchi wa wilaya hiyo.

KAPINGA: DHANA YA TAKA SIFURI INAFUNGUA FURSA ZA BIASHARA NA VIWANDA.

KAPINGA: DHANA YA TAKA SIFURI INAFUNGUA FURSA ZA BIASHARA NA VIWANDA.

June 06, 2026 Add Comment

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amesema dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa ni fursa muhimu ya kukuza sekta ya viwanda, kuongeza thamani ya malighafi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza katika kikao cha mawaziri kilichofanyika jijini Istanbul nchini Uturuki, Juni 5, 2026, kilichobeba mada ya Mageuzi ya Kijani ya Viwanda: Mtazamo wa taka sifuri na urejeshaji bidhaa, Kapinga amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta ya viwanda huku ikisisitiza matumizi bora ya rasilimali na uhifadhi wa mazingira. Ameeleza kuwa dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa inatoa fursa kwa nchi zinazoendelea kupitia matumizi endelevu ya malighafi, kupunguza upotevu baada ya mavuno, kupunguza uzalishaji wa taka na kuongeza thamani ya bidhaa zinazotengenezwa viwandani. Kapinga amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kuunganisha masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika sera na mipango ya maendeleo ya viwanda kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ufanisi wa nishati na teknolojia rafiki kwa mazingira. Aidha, amesisitiza kuwa mafanikio ya mageuzi ya kijani yanategemea uwekezaji wa kutosha, upatikanaji wa teknolojia za kisasa pamoja na ushirikiano madhubuti kati ya serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo. Amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kuendeleza viwanda vinavyoongeza thamani ya rasilimali, kudhibiti taka na kuvutia uwekezaji huku akiwakaribisha wafanyabiashara kuwekeza nchini kwa lengo la kujenga uchumi imara na shindani.

Mkutano huo umeandaliwa na Serikali ya Uturuki kupitia taasisi ya Zero Waste Foundation inayosimamiwa na Mwenza wa Rais wa Uturuki Bibi Emine Erdoğan na umeleta pamoja washiriki zaidi ya 3,000 kutoka nchi zote duniani, pamoja na taasisi za kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Umoja wa Mataifa, Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu na Shirika la Maendeleo na Biashara la Umoja wa Mataifa (UNCTAD).

LONDO – TBS NDIYO NGUZO KUU YA KULINDA AFYA ZA WALAJI.

LONDO – TBS NDIYO NGUZO KUU YA KULINDA AFYA ZA WALAJI.

June 06, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb) amelitaja Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa ni nguzo kuu ya kulinda afya za walaji na kuchochea ustawi wa viwanda nchini.

Amebainisha hayo Katika hafla maalum ya maadhimisho ya Miaka 50 ya Shirika hilo pamoja na Utoaji wa Tuzo kwa watumishi wa sasa na wastaafu kwa kutambua mchango wao uliojenga misingi imara ya udhibiti wa ubora Juni 6,2026, Jijini Dar es Salam.

Mhe. Londo Mhe.Londo amebainisha kuwa Kutokana na kukua kwa kasi kwa uwekezaji katika sekta za viwanda, kilimo, madini, na nishati, kuna uhitaji wa uwepo wa mifumo thabiti ya uhakiki wa ubora ili kulinda soko la ndani hivyo Kupitia huduma zake za upimaji na utoaji wa alama za ubora, TBS imekuwa chachu ya kukuza viwanda vya ndani na kuongeza imani ya walaji, jambo linaloiwezesha Tanzania kunufaika kikamilifu na fursa za masoko makubwa ikiwemo Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA).

Aidha alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kukuza uchumi kupitia maboresho ya miundombinu ya usafirishaji, nishati, na mifumo ya kidijitali na ameeleza kuwa maboresho ya sera na sheria yanalenga kuvutia uwekezaji na kuimarisha sekta binafsi, huku akiiasa TBS kuhakikisha kuwa ongezeko la uzalishaji nchini linaenda sambamba na uzingatiaji wa viwango vinavyotambulika duniani.

Akiangazia mustakabali wa miaka 50 ijayo, Mhe. Londo alieleza kuwa dunia inabadilika kwa kasi kiteknolojia na kiushindani, hivyo kuna mahitaji makubwa ya kuwa na TBS ya kisasa inayoendeshwa kwa maarifa hivyo Shirika hilo limetakiwa kuwekeza kwenye maabara zenye vifaa vya kisasa zaidi, kuongeza wataalamu wenye ujuzi wa hali ya juu, na kuimarisha mifumo ya kidijitali yenye ufanisi ili kuendana na kasi ya maendeleo ya sayansi na ubunifu duniani.

Mkakati huo wa kuimarisha mifumo ya viwango unaelezwa kuwa msingi imara wa kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye uchumi wa kisasa, jumuishi, na unaotegemea uzalishaji wenye thamani kubwa. Mhe. Londo aliongeza kuwa kusimamiwa vyema kwa usalama na ubora wa bidhaa kutasababisha bidhaa na huduma za Kitanzania kukubalika kwa urahisi katika soko la kimataifa na kikanda.

Vile vile Naibu Waziri alitoa rai kwa sekta binafsi, wazalishaji, na wafanyabiashara kuendelea kushirikiana kwa karibu na TBS ili kujenga utamaduni endelevu wa uzingatiaji viwango na uzalishaji wenye tija.