HABARI ZETU
Loading...

HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

LINDI,MTWARA,KAGERA NA RUKWA KUPATA UMEME WA GRIDI NDANI YA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

June 22, 2026 Add Comment




Serikali imesema katika mwaka wa fedha 2026/2027 itatekeleza miradi mbalimbali ya umeme ikiwemo kuunganisha mikoa ya Lindi, Mtwara, Kagera na Rukwa kwenye gridi ya taifa ya umeme ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma hiyo nchini.


Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma  Juni 22, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema umeme si anasa tena bali ni hitaji la msingi kwa maisha ya wananchi jambo linaloiifanya Serikali kuendelea kuwekeza fedha nyingi katika sekta hiyo.



Amesema Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini ili kuhakikisha nishati hiyo inawafikia wananchi katika maeneo mbalimbali.


Waziri  Ndejembi ameeleza kuwa umeme unaozalishwa katika Bwawa la Julius Nyerere unasafirishwa kupitia Chalinze kuelekea Morogoro na Dodoma, huku pia ukiunganishwa kwenye njia ya usafirishaji umeme ya Zuzu ili uweze kufika mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza.


Ameongeza  kuwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali itahakikisha mkandarasi anayetekeleza mradi wa njia ya umeme ya Songea–Tunduru–Masasi–Mahumbika anatekeleza kazi kwa wakati huku Serikali ikiendelea kutoa malipo  yatakayomwezesha mkandarasi huyo kufanya kazi bila kukwama na hivyo kuwezesha mikoa ya Lindi na Mtwara kupata umeme kutoka gridi ya taifa.


Aidha, amesema Serikali inaendelea kukamilisha miradi ya njia za kusafirisha umeme kutoka Iringa kwenda Mbeya, Songwe na Rukwa pamoja na mradi wa Benako–Kyaka ambao unalenga kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo husika.


Kwa upande wa usambazaji wa umeme vijijini, Mhe.Ndejembi amesema Serikali imepanga kupeleka umeme katika vitongoji 9,009  huku idadi ya vitongoji vitakavyofikiwa na huduma hiyo ikiendelea kuongezeka katika miaka inayofuata.


Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini vinafikiwa na huduma ya umeme, hatua itakayochochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi.


“Ni kazi kubwa ambayo inakwenda kufanywa, lakini Serikali imejipanga kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma ya umeme wa uhakika." Amesisitiza Waziri Ndejembi

MAFANIKIO YA USAMBAZAJI UMEME -MHANDISi MRAMBA AIPONGEZA REA NA TANESCO

June 22, 2026 Add Comment




📌*Wakandarasi wa umeme wakaribishwa Zambia kutekeleza miradi*


Dar es Salaam


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa huduma ya umeme, kutoka hatua ya kusambaza umeme kwenye mikoa hadi kufikia ngazi ya  vitongoji, ambapo  amewapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa mchango wao katika mafanikio hayo.


Mhandisi Mramba ametoa pongezi hizo  leo Juni 22, 2026, jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo na vyeti kwa wasimamizi wa miradi kutoka REA na wakandarasi waliotekeleza   miradi ya umeme vijijini na vitongojini na kuikamilisha kwa wakati.


Amesema hadi sasa asilimia 62 ya vitongoji nchini vimefikiwa na huduma ya umeme, huku Serikali ikilenga kuhakikisha vitongoji vyote vinaunganishwa na umeme ifikapo mwaka 2030 kupitia mpango wa kuunganisha wateja wa mwisho (Last Mile Household Electrification).



Katika hafla hiyo, Mhandisi Mramba amewataka wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya umeme nchini kuhakikisha wanazingatia muda, ubora na gharama, akisisitiza kuwa Wizara itaendelea kufuatilia kwa karibu utendaji wao. 


Amesema Serikali haitaacha kujadiliana na wakandarasi pale changamoto zinapotokea lakini kwa watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo hawatapewa fursa ya kushiriki miradi mingine ya Serikali.


Katika kikao hicho, Mhandisi Mramba pia alimkaribisha  Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ya Zambia anayeshughulikia masuala ya umeme, Mhandisi Arnold Simwaba ambaye yupo nchini  pamoja na ujumbe wake  kwa ziara ya kikazi katika miradi ya umeme.

Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Nishati nchini Zambia amesema wakandarasi walioonyesha uwezo mkubwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme nchini Tanzania wanakaribishwa pia kushiriki katika utekelezaji wa miradi ya umeme nchini Zambia.



Kwa upande wake, mwakilishi wa wakandarasi ambaye kampuni yake ya Derm Electric imefanya vizuri katika miradi ya umeme vijijini na vitongojini, Ridhuani  Mringo  amesema wakandarasi wazawa wanapaswa kuendelea kutekeleza miradi kwa uadilifu, weledi na uaminifu ili kuendelea kujenga imani ya Serikali na kuongeza nafasi ya kampuni za ndani kushiriki katika utekelezaji wa miradi mikubwa na ya kimkakati.



BARRICK NORTH MARA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KATIKA MADINI KWA KUTOA MSAADA GEREZA LA TARIME NA KWENYE JAMII

June 22, 2026 Add Comment


Mkuu wa Wilaya, Meja Edward Gowele (aliyevaa shati la bluu), viongozi wa Gereza la Tarime na wafanyakazi wanawake kutoka Barrick North Mara wakiwa katika hafla ya kukabidhi misaada gerezani hapo.

ABBASI AONGOZA KIKAO CHA PILI CHA BODI YA USIMAMIZI WA MRADI WA FORLAND

June 22, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi akiwa na Mwenyekiti mwenza ambaye ni Naibu Balozi wa Finland Bw. Tomi Lounio, wameongoza Kikao cha Pili cha Bodi ya Usimamizi wa Mradi wa Maendeleo ya Matumizi ya Ardhi, Misitu na Mnyororo wa Thamani(FORLAND).

MWENYEKITI MPYA WA BODI YA USHAURI ADEM DKT. DACHI AONGOZA KIKAO CHAKE CHA KWANZA,

June 22, 2026 Add Comment
📍Bagamoyo, Tanzania

Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ushauri ya ADEM, Dkt. Hillary A. Dachi, amewasili rasmi chuoni hapo na kuongoza kikao chake cha kwanza tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, ambapo Bodi ilikutana kujadili masuala mbalimbali ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa taasisi na kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu nchini.
RAIS DKT. SAMIA AMUAGA RAIS WA NAMIBIA DKT. NETUMBO NDAITWAH

RAIS DKT. SAMIA AMUAGA RAIS WA NAMIBIA DKT. NETUMBO NDAITWAH

June 22, 2026 Add Comment

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Dkt, Netumbo Nandi-Ndaitwah katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 22 Juni, 2026. Rais Mhe. Dkt. Ndaitwah amehitimisha Ziara yake ya Kitaifa ya siku 4 nchini Tanzania ambapo pamoja na kufanya mazungumzo na Rais Mhe. Dkt. Samia pia alitembelea Kambi ya Kihistoria ya Wapigania Uhuru wa nchi yake, Kongwa mkoani Dodoma.        

WATALAAM WA REA ZAMBIA KUJIFUNZA MAFANIKIO YA TANZANIA KATIKA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI

June 22, 2026 Add Comment

Viongozi wa Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) kutoka nchini Zambia wamewasili nchini kwa ajili ya ziara ya kujifunza na kubadilishana ujuzi na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).


REA Zambia ambao wameongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Zambia anayeshughulikia Umeme, Mhandisi Arnold Simwaba wamewasili leo Juni 21, 2026 katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupokelewa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Tanzania, Wilson Nyamanga pamoja na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kiutoka REA Tanzania, Mhandisi Jones Olotu, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa REA Tanzania, Renatus Msangira.

Uongozi wa REA Zambia utakuwa nchini kwa ziara ya kikazi ya Siku 7 ambapo pamoja na vikao vya kubadilishana ujuzi, wajumbe hao wanatarajiwa kutembelea miradi mbalimbali ya umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini.







MWENGE UHURU WARIDHISHWA NA MRADI WA MAJI WA SH.MILIONI 233.4 TANGA

June 22, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga,TANGA.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, amepongeza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya kuboresha upatikanaji wa maji safi katika eneo la Mzizima hadi Mikocheni, akisema unadhihirisha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kusogeza huduma muhimu karibu na wananchi.

Mwenge wa Uhuru 2026 umetembelea na kukagua mradi huo unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA) katika Kata ya Mzizima, ambapo viongozi wa mbio hizo walieleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wake.


Akizungumza baada ya ukaguzi huo na kushiriki katika zoezi la kumuunganishia mteja mpya huduma ya maji safi, Mwang’onda alisema Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza mkakati wa kuboresha huduma za maji nchini ili kumtua mama ndoo kichwani.

Alisema dhamira hiyo inaonekana kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa katika sekta ya maji nchini, huku akiipongeza Tanga UWASA kwa usimamizi mzuri wa mradi huo ambao unalenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi, Mhandisi Aaron Chanimbaga, akisoma taarifa ya utekelezaji alisema mradi huo wenye thamani ya Shilingi milioni 233.4 umefikia asilimia 50 ya utekelezaji.

Alieleza kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba mwaka huu na unalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 4,780 kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama kwa uhakika.

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 zinaongozwa na kauli mbiu isemayo: “Tanzania ni yetu sote, tushirikiane kwa pamoja kuleta maendeleo.”








WAZIRI AWESO ATOA MAAGIZO KWA RUWASA PANGANI

June 21, 2026 Add Comment
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang'onda (wa pili kushoto) akizungumza kwenye mradi wa maji wa Mikocheni/Mkwaja. Kushoto kwake ni Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso na kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Mhe Ayubu Sebabili


Na Mwandishi Wetu, PANGANI


WAZIRI wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, ameagizi Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, kuunganisha mtandao wa majisafi na salama kwenye makazi ya watu katika kijiji cha Mkwaja.


Mhe. Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Pangani, ameyasema hayo leo Juni 20, 2026 kijijini hapo, alipokaribishwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa upanuzi mtandao wa maji kutoka ‘mradi mama’ uliopo kijiji cha Mikocheni.
Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Raiyan Mohamed Rashid, akimtishwa ndoo ya maji mmoja wa wakazi wa kijiji cha Mkwaja wilayani Pangani,  Mkoa wa Tanga kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji uliofika kijijini hapo kutokea kijiji jirani cha Mikocheni.



Mwenge wa Uhuru wenye kauli mbiu inayosema, “Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo” ulifika kwenye mradi huo wa kwanza baada ya kuingia katika Halmashauri ya Pangani kutokea Handeni.


Mhe. Aweso amesema, kwa vile Mwenge umechagiza maendeleo wilayani humo kwa vipindi tofauti, ipo haja ya kuendeleza hali hiyo kwa kuingiza maji kwenye makazi ya watu, badala ya kuishia kwenye vituo 12 vya kuchotea maji (DPs) vilivyopo Mkwaja.


Amesema, usambazaji majisafi na salama ni utekelezaji wa ahadi za Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kumtua ndo mama kichwani.


Kwa mujibu wa Mhe. Aweso, kati ya vijiji 12,333 vilivyopo nchini, 10,758 vimefikiwa na huduma ya majisafi na salama wakati 1,575 vitafikiwa ifikapo 2030.


Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Pangani, Mhandisi Rajab Hussein, amesema upanuzi wa mradi wa Mikocheni ni matokeo ya upatikanaji maji kwa wastani wa lita 480,000 kwa siku, wakati mahitaji ya Mikocheni pekee ni lita 40,000.


Kwa mujibu wa Mhandisi Hussein, mahitaji yaliyobainika kwa matumizi katika kijiji cha Mkwaja ni lita 65,000 kwa siku na kufanya jumla yake kuwa lita 105, hivyo kuwa na lita 375,000 za ziada.

Ni picha ya uzinduzi wa mradi wa maji.

Amesema kupitia upanuzi wa mradi huo, RUWASA imejenga tenki lenye uwezo wa kuchukua lita 90,000 na kuwekwa kwenye mnara wa urefu wa mita sita, hivyo kuwa na uwezo wa kusambaza maji kijijini Mkwaji kupitia DPs zilizopo.


Naye Mwang’onda amesema agizo la Mhe. Aweso kwa RUWASA kuunganisha mtandao wa maji kwenye makazi ya watu ni kuuheshimisha Mwenge na kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mwang’onda amesema historia imeandikwa kwa Mhe. Rais Dkt Samia kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji majisafi na salama sehemu kubwa ya nchi.


Kwa hali, Mwang’onda, amehimiza wananchi kuwekeza zaidi katika amani, umoja na mshikamano, ili kufikia maono ya Mhe. Rais Dkt Samia kuwa na maendeleo endelevu.


MWISHO.





WANANCHI WAHOJI UHAKIKI MFUMO WA VIPIMO VYA DATA: “TUNACHOLIPIA HAKITOSHI”

June 21, 2026 Add Comment


Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA


Wakazi wa Jiji la Dodoma wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuingilia kati na kusimamia ipasavyo matumizi sahihi ya vipimo vya vifurushi vya intaneti “bando” pamoja na muda wa maongezi wakidai kupoteza data zao kwa haraka na bila uwazi.

Wananchi hao wametoa wito wa kuwepo kwa uwazi na ukomo sahihi wa muda wa matumizi ya data, wakisema ni haki yao kupata kile wanacholipia.

Baadhi ya wakazi waliozungumza jijini hapa wameeleza kusikitishwa na namna megabytes (MBs) au gigabytes (GBs) wanazonunua zinavyoisha kwa muda mfupi hata pale wanapokuwa hawatumii simu zao kikamilifu, jambo linaloashiria kasoro kwenye usahihi wa vipimo hivyo

Meneja wa Wakala wa vipimo mkoa wa Dodoma Said Ibrahim, anasema wakala umepokea maoni hayo ya wadau na kuongeza kuwa umeshaanza mchakato wa kusimamia uhakiki ikiwemo katika vifurushi vya intaneti (Bando) na muda wa maongezi.




“ZERO MALARIA” YA BARRICK YAFIKIA KAYA ELFU 44 MSALALA

June 21, 2026 Add Comment

 

Afisa Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa vyeti kwa washiriki wa zoezi la upuliziaji dawa majumbani kwenye mazalia ya mbu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa “Zero Malaria” unaolenga kuimarisha juhudi za kutokomeza ugonjwa wa malaria katika jamii zinazozunguka mgodi huo.

Mratibu wa Wadudu Wadhulifu ngazi ya Wilaya, Jullieth Petro, akimwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa vyeti kwa washiriki wa zoezi la upuliziaji dawa majumbani kwenye mazalia ya mbu, yaliyoandaliwa katika kutekeleza mradi wa “Zero Malaria” unaofadhiliwa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu.
Mkurugenzi wa Gekahil, Bw. Gerald Elias, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa vyeti kwa washiriki wa zoezi la upuliziaji dawa majumbani kwenye mazalia ya mbu, yaliyoandaliwa katika utekelezaji wa mradi wa “Zero Malaria” unaofadhiliwa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa lengo la kuimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria katika jamii.

*HAKUNA MASIKA YASIYOKUWA NA KIANGAZI*

June 20, 2026 Add Comment


Usemi usemao hakuna marefu yasiyokuwa na ncha umetimia leo ambapo jumla ya maafisa na Askari 29 kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) wamehitimu mafunzo ya mabadiliko ya kimuundo leo tarehe 20 Juni, 2026 katika Kituo cha Mafunzo ya Jeshi la Uhifadhi kilichopo Mlele mkoani Katavi.

Akifunga mafunzo hayo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TAWA Meja Jenerali (Mstaafu) Hamis Semfuko amewataka wahitimu kuzingatia taratibu na sheria na amri zote za Jeshi la Uhifadhi

“Mmepata mafunzo ya kubadilika kimuundo kutoka raia kuwa Jeshi, matumaini yangu ni kuwa kila mmoja wetu hapa mtabadilika na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa katika kusimamia uhifadhi na rasilimali za nchi”,alisema Meja Jenerali (Mst) Semfuko.

Mkuu wa wilaya ya Mlele Mhe. Majid Mwanga amewapongeza wahitimu hao na kuwataka kuwa mfano mwema wa uzalendo, maadili na ujasiri katika utendaji kazi.

Kwa upande wake Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Abdul-Razaq Badru amewahimiza wahitimu hao kutumia mafunzo waliyoyapata kuimarisha uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.

Kaimu Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) Mlage Kabange amesema ushirikiano uliooneshwa kati ya TAWA na Ngorongoro katika kusimamia mafunzo hayo unaonesha kuimarika kwa Jeshi la Uhifadhi nchini na ari ya kusimamia rasilimali za Wanyamapori na Misitu.

Akitoa taarifa kuhusu mafunzo hayo mkuu wa mafunzo Meja Breyman Rulenguka amesema Jumla wa watumishi 29 wamefaulu na kupata alama za kuridhisha ambapo mwanafunzi mmoja pekee hakuweza kuhitimu kutokana na sababu za kiafya.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa katika kituo hicho kwa lengo la kuimarisha Jeshi la Uhifadhi na utendaji kazi wake.




.