HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
GOLDEN VALUE WAPATIWA ELIMU YA NISHATI KATIKA MAONESHO YA WIKI YA MAZINGIRA DUNIANI 2026
Na Mwandishi Wetu,
Meneja wa Shule ya Golden Value Bi. Nuru Nyundo, ameongoza wanafunzi wa darasa la nne na la sita kutembelea banda la Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake katika Maonesho ya Wiki ya Mazingira Duniani 2026 yanayoendelea katika katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma
Ziara hiyo imelenga kuwapatia wanafunzi elimu kuhusu sekta ya nishati na mchango wake katika uhifadhi wa mazingira.
Wakiwa katika banda hilo, wanafunzi walipata fursa ya kujifunza kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, nishati jadidifu na teknolojia mbalimbali zinazosaidia kupunguza uharibifu wa mazingira.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bi. Nyundo amesema kuwa kuwashirikisha wanafunzi katika maonesho hayo ni njia muhimu ya kuwajengea uelewa wa mapema kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira na kutumia nishati kwa njia endelevu ili kulinda afya na mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Kwa upande wake, mwanafunzi Maria Yusuph wa darasa la sita amepongeza elimu inayotolewa katika banda la Wizara ya Nishati, akisema imewasaidia kuelewa umuhimu wa kutumia nishati safi ya kupikia na namna inavyoweza kulinda afya za wananchi pamoja na mazingira. Alisema elimu hiyo itamsaidia kuwa balozi wa matumizi ya nishati safi shuleni na nyumbani.
Aidha, wanafunzi hao walitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Nishati na kupata maelezo kutoka kwa wataalamu kuhusu huduma na miradi inayotekelezwa ili kuongeza upatikanaji wa nishati safi na ya uhakika nchini.
Maonesho ya Wiki ya Mazingira Duniani 2026 yalianza Juni 1 na yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 5, 2026 jijini Dodoma, yakitoa fursa kwa wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu uhifadhi wa mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

WALIMU 3,153 WASHIRIKI SHINDANO LA STADI ZA UFUNDISHAJI
habari
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetangaza kuwa jumla ya walimu 3,153 wamejisajili kushiriki Shindano la Taifa la Nne la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Awali na Msingi pamoja na Shindano la Pili la Stadi za Ufundishaji kwa Walimu wa Shule za Sekondari Tanzania Bara,ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuendelea kuimarisha ubora wa ufundishaji na ujifunzaji nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 2, 2026, jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, amesema kuwa hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa mashindano hayo itafanyika Juni 6, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Amesema mashindano hayo yanatoa fursa kwa walimu kuonesha umahiri wao wa kitaaluma, ubunifu na matumizi ya mbinu bora za ufundishaji darasani, huku yakitumika pia kama sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA).
"Kati ya walimu 3,153 waliosajiliwa kupitia Mfumo wa National Teaching Skills Competition System (TSCS), walimu 1,263 walitimiza masharti yote ya ushiriki kwa kuwasilisha video za ufundishaji pamoja na maandalio ya masomo kwa ajili ya tathmini."amesema Mhe.Ameir
Amesema mchakato wa tathmini umekamilika na tayari orodha teule ya walimu watano bora imepatikana katika kila eneo la ushindani, huku mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa zawadi akitarajiwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.
Mhe. Ameir ameeleza kuwa mshindi wa kwanza katika kila kundi atazawadiwa Shilingi milioni 2.5, cheti cha pongezi, cheti cha ushindi pamoja na kompyuta mpakato. Aidha, shule anayofundisha mshindi huyo itapatiwa projekta kwa ajili ya kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.
Katika hatua nyingine, amesema shule zitakazotoa washindi wa kwanza katika maeneo ya Kusoma kwa Darasa la Awali, Kiingereza kwa Darasa la Kwanza na Ufaraguzi wa Zana kwa Darasa la Pili zitapatiwa vibao vya kielektroniki 100 vyenye thamani ya Shilingi milioni tano.
Serikali inaendelea kutumia mashindano hayo kama nyenzo ya kuhamasisha ubunifu, kuongeza ari ya utendaji kwa walimu na kuibua mbinu bora za ufundishaji zitakazochangia kuinua viwango vya elimu nchini.
Kaulimbiu ya shindano la mwaka huu ni “UFUNDISHAJI BORA, TAIFA IMARA.

JUKWAA LA BIASHARA LA VIWANGO KUFANYIKA JUNI 5 MLIMANI CITY
habariWAWILI WAHUKUMIWA MAISHA KWA BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA
habariTANZANIA YASHIRIKI KIKAO CHA KAMATI YA UTEKELEZAJI WA VIWANGO VYA KAZI, GENEVA
habariRAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONDOKA NCHINI KUELEKEA SHIRIKISHO LA URUSI KWA ZIARA YA KITAIFA
habari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.
.jpeg)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Shirikisho la Urusi kwa ziara ya Kitaifa itakayoanza tarehe 3 hadi 5 Juni, 2026 kwa mualiko wa Rais wa Shirikisho la Urusi, Mheshimiwa Vladimir Putin.


NAIBU WAZIRI KWAGILWA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO KWENYE MAONESHO KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI
habari
*Aipongeza TANESCO kuendelea kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kwa umeme.
*Ahimiza TANESCO kuendelea kupanda miti kwa wingi kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme
Na. Mariam Juma, Dodoma
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kwagilwa Reuben leo Juni 01, 2026 ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwenye Maonesho kuelekea Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Center (JKCC) Jijini Dodoma.
Akizungumza katika banda hilo Mhe. Kagilwa ameipongeza TANESCO kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika utunzaji wa Mazingira hasa katika kuendelea kuhamasisha wananchi kupika kwa kutumia Nishati Safi ya umeme hali ambayo inasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira.
Aidha ametumia nafasi hiyo kuisisitiza TANESCO kuendelea kupanda miti kwa wingi kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme ili kuendelea kutunza mazingira.
” Niwapongeze TANESCO kwa kuendelea kuhamasisha utunzaji wa mazingira hususani kupitia Nishati Safi ya kupikia kwa umeme, pia niwasisitize kuongeza juhudi za upandaji miti kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme”.
Awali akielezea ushiriki wa TANESCO katika maonesho hayo Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja Mkoa wa Dodoma James Vesso amesema lengo ni kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kwa umeme hali inayosaidia kuokoa muda na kutunza mazingira.
“Sisi kama TANESCO tunaendelea kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kutumia Nishati Safi ya kupikia kwa umeme ili kutunza mazingira pamoja na kueleza mikakati ya Shirika juu ya utunzaji wa mazingira katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme”


DKT.JAFO AWAPAMBANIA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII NCHINI
habari
MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum leo Juni 1,2026 bungeni jijini Dodoma.

MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo,akichangia hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum leo Juni 1,2026 bungeni jijini Dodoma.
......
MBUNGE wa Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ameitaka Serikali kuboresha mazingira ya kazi kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii nchini ikiwemo kuwapatia magari ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.
Akichangia hotuba ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum bungeni, Dkt. Jafo amesema maafisa hao ni nguzo muhimu katika kusukuma maendeleo ya jamii na wanastahili kuwezeshwa kwa vitendea kazi vinavyokidhi mahitaji ya kazi zao.
Amesema Maafisa Maendeleo ya Jamii ni mawakala wa mabadiliko katika jamii kwa kuwa karibu kila programu ya maendeleo inayotekelezwa nchini inahitaji ushiriki wao wa moja kwa moja, hivyo ni muhimu kupewa heshima na mazingira bora ya kufanyia kazi.
Dkt. Jafo ameeleza kuwa pamoja na magari, maafisa hao wanapaswa kuwa na ofisi zenye hadhi na rasilimali za kutosha zitakazowawezesha kuwafikia wananchi kwa urahisi na kutoa huduma stahiki.
Aidha, ameishauri Serikali kuanzisha vitengo vya Maendeleo ya Jamii katika wizara zote na taasisi za umma zaidi ya 325 ili kuhakikisha masuala ya maendeleo ya jamii yanapewa kipaumbele na kuratibiwa kwa ufanisi katika sekta mbalimbali.
Pia amependekeza kuanzishwa kwa Kitengo cha Uratibu wa Sekta ndani ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii kitakachosaidia kuunganisha taarifa za maendeleo kutoka wizara na taasisi mbalimbali, hatua ambayo alisema itaiwezesha nchi kuwa na mfumo imara wa kufuatilia maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.

WANAFUNZI 246,197 WALIOPANGIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO WANAPASWA KURIPOTI SHULENI JULAI 04, 2026 – PROF. SHEMDOE
habari
Na OWM – TAMISEMI, Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 246,197 wakiwemo wasichana 114,102 na wavulana 132,095 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2026 wanatakiwa kuripoti shuleni kuanzia Julai 04, 2026 hadi Julai 31, 2026 kwakuwa muhula wa kwanza wa masomo utaanza Julai 06, 2026.
Prof. Shemdoe amesema hayo leo Juni 01, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo ya Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Magogoni Jijini Dar es Salaam, wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi kwa mwaka 2026.
“Wanafunzi 172,114 sawa na asilimia 69.9 wakiwemo wasichana 85,987 na wavulana 86,127 wenye sifa wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika shule za sekondari za Serikali 856 zikiwemo shule za bweni 825, kutwa 25 na kutwa na bweni sita (06),” amefafanua Prof. Shemdoe.
Aidha, Prof. Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 74,083 sawa na asilimia 30.1 wakiwemo wasichana 28,115 na wavulana 45,968 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.
“Wanafunzi 3,144 wakiwemo wasichana 1,170 na wavulana 1,974 wamechaguliwa kujiunga na fani mbalimbali katika vyuo 04 vya elimu ya ufundi, vyuo hivyo ni Chuo cha Ufundi cha Arusha (ATC), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) na Chuo cha Maendeleo ya Maji (WMDI),” ameeleza Prof. Shemdoe.
Prof. Shemdoe amesisitiza kwamba, uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi umefanyika kwa kuzingatia ufaulu na nafasi zilizopo katika shule; hivyo, hakutakuwa na fursa ya kufanya mabadiliko yoyote ya Shule kutokana na ukosefu wa nafasi.
Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi zilizotumika kujenga miundombinu bora ya shule za kidato cha tano na vyuo vya kati ambayo itatumika kuwahudumia wanafunzi 246,197 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi mwaka 2026.

MWENYEKITI WA CCM TANGA YAKABIDHI MILIONI 500 KUKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI WAKE
siasa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimeongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wake wa ujenzi wa nyumba 36 za watumishi baada ya Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo, Rajab Abdulrahman, kukabidhi shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo unaotekelezwa katika wilaya tisa za mkoa huo.
Fedha hizo zilikabidhiwa kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, katika hatua inayodhihirisha dhamira ya chama ya kuboresha mazingira ya kazi na makazi kwa viongozi wake wa ngazi za wilaya.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Rajab alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu na kwamba utakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji wa watumishi pamoja na shughuli za chama katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

Alieleza kuwa mradi huo una thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5, huku fedha zote zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wake zikiwa tayari zimepatikana kupitia michango ya wanachama, viongozi na wadau mbalimbali wa chama.
"Mradi huu unagharimu jumla ya shilingi bilioni 2, milioni 500 na laki 250. Fedha hizi zimepatikana kupitia michango mbalimbali ikiwemo milioni 56 zilizotolewa awali, milioni 10 kutoka kwa MNEC pamoja na michango iliyokusanywa kutoka wilaya zote za mkoa," alisema Rajab.

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa kukamilika kwa nyumba hizo kutasaidia kutatua changamoto za makazi kwa baadhi ya viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya, jambo litakaloongeza utulivu wa kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Alisema nyumba hizo si tu kwamba zitakuwa makazi ya viongozi, bali pia ni uwekezaji wa muda mrefu wa chama katika kujenga taasisi imara yenye uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendelea kuwahudumia wanachama wake.

"Tunajenga misingi ya chama kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Viongozi wanaweza kubadilika, lakini miundombinu tunayojenga leo itaendelea kulitumikia chama kwa miaka mingi ijayo," alisisitiza.
Rajab aliongeza kuwa ujenzi wa chama ni jukumu endelevu linalohitaji mshikamano wa wanachama wote, akisisitiza kuwa maendeleo ya chama hayawezi kupatikana bila ushiriki wa pamoja wa wanachama wake.

Kutokana na hilo, aliwataka wana-CCM wa Mkoa wa Tanga kuendelea kuchangia kwa hali na mali, kutumia elimu na uzoefu wao pamoja na nguvu kazi katika kukiimarisha chama.
Kwa upande wake, Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, alisema mradi huo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa chama wa kuimarisha utendaji wake katika ngazi za wilaya kwa kuhakikisha viongozi wanapata mazingira bora ya kazi na makazi.
Alifafanua kuwa kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo zitatumika na viongozi muhimu wa chama na jumuiya zake.

"Kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo ni nyumba ya Katibu wa CCM wa Wilaya, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Vijana, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi pamoja na nyumba ya Katibu wa UWT," alisema Kizigo.

Alieleza kuwa uwepo wa nyumba hizo utasaidia kupunguza gharama za upangaji wa makazi, kuimarisha upatikanaji wa viongozi katika maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za chama na jumuiya zake.
Kwa mujibu wa Kizigo, kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuijengea CCM Mkoa wa Tanga miundombinu imara itakayosaidia kuendeleza shughuli zake za kisiasa, kiutawala na kijamii kwa ufanisi zaidi katika miaka ijayo.

TANZANIA KUWA NA MKAKATI MAALUM WA MAWASILIANO WAKATI WA MLIPUKO WA MAGONJWA YA MIFUGO
habari
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Benezeth Lutege, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness K. Meena. Warsha hiyo imefanyika leo Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha.

Mkurugenzi Msaidizi wa Epidemiolojia na Magonjwa ya Mifugo Yanayovuka Mipaka (TADs) akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Habari II wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Chiku Makwai, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Sheria I wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Denis Ukaka, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Na Chiku Makwai – ARUSHA
Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, limeanza mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa nchi katika kuzuia, kudhibiti na kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo.
Warsha ya kuandaa rasimu hiyo imefunguliwa leo, Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Agness K. Meena.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Dkt. Lutege amesema mawasiliano yenye ufanisi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti na kukabili milipuko ya magonjwa ya mifugo kwa kuwa huwezesha utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati kwa wadau wote wanaohusika.
Amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari na mwitikio wa haraka ili kuhakikisha magonjwa ya mifugo yanagunduliwa na kudhibitiwa mapema kabla hayajasababisha athari kubwa kwa uzalishaji, biashara ya mifugo na afya ya jamii.
“Mkakati huu utaweka msingi wa kuwa na mfumo mmoja wa kitaifa wa mawasiliano ya dharura utakaoongoza utoaji wa taarifa, ushirikishwaji wa wadau na usimamizi wa mawasiliano wakati wa matukio ya milipuko ya magonjwa ya mifugo,” amesema Dkt. Lutege.
Aidha, amebainisha kuwa magonjwa mbalimbali ya mifugo, ikiwemo Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever), yanahitaji uratibu madhubuti wa mawasiliano ili kuhakikisha wananchi na wadau wanapata taarifa sahihi zitakazowawezesha kuchukua hatua stahiki kwa wakati.
Warsha hiyo imewakutanisha wataalamu wa mifugo, afya ya wanyama, mawasiliano na wadau wengine kutoka taasisi za Serikali pamoja na mashirika ya kimataifa kwa lengo la kujadili mbinu bora za mawasiliano ya hatari, usimamizi wa taarifa za dharura na mikakati ya kuimarisha mwitikio wakati wa milipuko ya magonjwa.
Washiriki pia wanatarajiwa kujadili matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa taarifa pamoja na namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya afya ya wanyama na afya ya binadamu kwa kuzingatia dhana ya Afya Moja (One Health).
Kupitia warsha hiyo, Tanzania inatarajia kuwa na mkakati madhubuti wa mawasiliano ya dharura utakaosaidia kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema, kuongeza mwitikio wa haraka wakati wa matukio ya dharura na kulinda ustawi wa mifugo sambamba na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.





