HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
DKT. BATILDA BURIAN ATOA WITO WA KUTEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU
habariKWAGILWA AFUNGIA KIWANDA CHA HANGJIN STEEL MKURANGA KWA UKIUKWAJI WA SHERIA ZA MAZINGIRA
habariWAZIRI WA FEDHA MGENI RASMI HALFA YA ULENGE KUGAWA MIGUU BANDIA 100 TANGA,MBUNGE AFUNGUKA "NAREJESHA FADHILA"
habariNa Mwandishi wa diGOtv, Tanga
WAZIRI wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Musa Omar (Mb) anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika hafla kubwa na ya kihistoria ya ugawaji wa miguu bandia 100 kwa watu wenye ulemavu mkoani Tanga, iliyoandaliwa na Ofisi ya Mbunge wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Mhandisi Mwanaisha Ulenge.
Hafla hiyo kubwa inatarajiwa kufanyika *Jumanne, tarehe 14 Julai 2026*, katika ukumbi wa *Regal Naivera* jijini Tanga kuanzia saa 2:00 asubuhi.
Hatua hii inamfanya Mhe. Mhandisi Ulenge kuweka rekodi ya kuwa Mbunge wa kwanza mkoani Tanga kufanya shughuli kubwa za kijamii na kugusa maisha ya watu moja kwa moja tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka jana. Utendaji huu unaendelea kumuweka karibu zaidi na makundi mbalimbali mkoani humo kutokana na utu wake na dhamira ya dhati ya kulipa fadhila kwa kura nyingi alizopigiwa.
Akizungumzia msukumo wake wa kuandaa tukio hilo linalogusa maisha ya wanyonge, Mhe. Ulenge ameweka wazi kuwa yeye ni mtumishi wa wananchi na anachokifanya ni kurudisha fadhila kwao.
"Hii nafasi niliyokuwa nayo ni ya watu. Kurejesha kidogo ninachopata pamoja na wadau wangu ni jambo kubwa kwangu, kwa sababu watu ndiyo walionifikisha hapa," alisema Mhe. Ulenge kwa hisia.
*Mafunzo ya Sheria ya Asilimia 30 (Manunuzi ya Umma)*
Ukiachilia mbali zoezi la ugawaji wa miguu hiyo bandia ili kuwarudishia uwezo wa kutembea, hafla hiyo itakwenda sambamba na utoaji wa mafunzo maalum kwa makundi maalum (Vijana, Wanawake, na Watu wenye Ulemavu).
Kwa kuwa Mgeni Rasmi ni Waziri wa Fedha anayesimamia sera za kiuchumi, mafunzo hayo yatalenga kuwajengea uwezo washiriki namna ya kunufaika na *Sheria ya asilimia 30 (30%) ya Manunuzi ya Umma*. Lengo ni kuwapa uelewa utakaowawezesha kupata zabuni za kiserikali na kujikwamua kiuchumi badala ya kutegemea misaada pekee.
Wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo wanaendelea kupongeza hatua hii ya Mhe. Ulenge, huku maandalizi ya kumpokea Waziri wa Fedha na kukamilisha zoezi hili yakiwa yamepamba moto jijini Tanga.
MBUNGE KILINDI,KITETO WAENDELEZA UJIRANI MWEMA MIRADI YA MAENDELEO
siasaKatika kuonesha ujirani mwema Mbunge wa Kiteto Edward Ole Lekaita na Mbunge wa Kilindi Salehe Mhando wameamua kushirikiana kuhakikisha barabara ya Lengatei- Songe inatengenezwa kwa kiwango cha changarawe na kupitika kwa mwaka mzima.
Mbali ya kushirikiana kusimamia Ujenzi wa barabara hiyo pia Wabunge hao wameshiriki shughuli ya uzinduzi wa shule ya awali na msingi Kijiji cha Lesiot Kata ya Lengatei Kiteto.
MAGOTI AIPONGEZA TET KWA MABORESHO YA MITAALA
habariUBIA WA BARRICK NA TWIGA WAZIDI KUWA KIOO CHA USHIRIKIANO WA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI TASNIA YA MADINI
habari 

MYCOELY BALOZI MPYA WA MAZINGIRA NCHINI
habariUTORO NA VIGODORO VYATAJWA KUCHANGIA UFAULU HAFIFU, POLISI KATA YAISHUKURU TANGAYETU
elimuPolisi Kata wa Kata ya Nguvumali, Jiji la Tanga, Inspekta Sharifu Kiswamba, amesema utoro wa wanafunzi na tabia ya kukesha kwenye vigodoro ni miongoni mwa sababu zinazochangia kushuka kwa kiwango cha ufaulu katika shule za sekondari.
Inspekta Kiswamba alitoa kauli hiyo wakati wa mafunzo maalumu ya kuwajengea wanafunzi mbinu za kujifunza kwa ufanisi na kujiandaa vizuri kwa mitihani, yanayoendeshwa na Tanzania Centre for Education (TCE) kwa kushirikiana na Botnar Foundation na Inovex kupitia Mradi wa TangaYetu.
Alisema mradi huo unahusisha shule 10 zilizobainika kuwa na changamoto ya matokeo hafifu ya kitaaluma, ukiwa na lengo la kuwajengea wanafunzi uwezo wa kujifunza kwa ufanisi na kuongeza kiwango cha ufaulu.
"Kama Polisi Kata tunaushukuru Mradi wa TangaYetu pamoja na wadau wake kwa kuanzisha mafunzo haya. Tunaamini yatasaidia kubadilisha mtazamo wa wanafunzi, kuongeza nidhamu na hatimaye kuinua ufaulu katika shule zetu," alisema.
Alieleza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea kushirikiana na viongozi wa kata, walimu na jamii kuhakikisha wanafunzi wanaotoroka masomo wanafuatiliwa na kurejeshwa shuleni ili wasikose haki yao ya elimu.
"Tunatoa onyo kwa wanafunzi wanaotoroka masomo. Tutakaowakuta wakizurura wakati wa vipindi vya masomo watachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu, ikiwemo kupelekwa ofisini kwa hatua zaidi za kinidhamu," alisema.
Inspekta Kiswamba alisema pia tabia ya wanafunzi kushinda vijiweni na kukesha kwenye vigodoro imeendelea kuwa changamoto inayochangia kuporomoka kwa nidhamu na kuathiri maendeleo yao kitaaluma.
"Hatutavumilia tabia hii. Tutaendelea kufanya doria na kushirikiana na viongozi wa mitaa pamoja na wazazi kuhakikisha wanafunzi wanazingatia masomo na kujiepusha na mazingira yanayoharibu mustakabali wao," alisisitiza.
Aidha, aliwataka wazazi na walezi kutekeleza wajibu wao wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao kwa kuhakikisha wanahudhuria masomo, wanapata muda wa kujisomea na kuepuka vitendo vinavyoweza kuhatarisha elimu yao.
Alisema mafanikio ya sekta ya elimu yanahitaji ushirikiano wa karibu kati ya wazazi, walimu, viongozi wa serikali za mitaa, Jeshi la Polisi na wadau wa maendeleo, akieleza kuwa jitihada zinazofanywa na Mradi wa TangaYetu ni sehemu ya suluhisho la changamoto zinazolikabili eneo hilo.
Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za Mradi wa TangaYetu za kuboresha matokeo ya kitaaluma katika shule zenye changamoto kwa kuwajengea wanafunzi stadi za kujifunza, nidhamu na maandalizi bora ya mitihani.
JAB YAHIFADHI URITHI WA TASNIA YA HABARI KUPITIA ITHIBATI YA MAISHA
habari
MBUNGE ADO SHAIBU AKUTANA NA TANZANIA ONE KUTOKA TUNDURU
Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Mh. Ado Shaibu Ado amekutana na kufanya mazungumzo na Ndugu Biriat Yafet Biriat ambaye kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwa ngazi ya kidato cha sita ndiye kinara wa kufaulu nchi nzima (Tanzania One)
Mh. Ado amesema ameamua kukutana na mwanafunzi huyo aliyehitimu shule ya Ndanda Wilayani Masasi akitokea Wilayani Tunduru kwa sababu ufaulu wake ambao haujawahi kutokea kwa kiwango hicho Wilayani Tunduru umeiletea heshima kubwa wilaya ya Tunduru.
Mbali na kumpongeza Mh. Ado alikubali maombi ya Ndugu Biriat kusaidiwa simu, laptop na fedha za kujikimu na kushughulikia michakato yote hadi pale atapojiunga rasmi na kupata mkopo wa Serikali. Ndugu Ado alimnunulia simu, kumkabidhi fedha taslimu milioni moja na kumpa ahadi ya kumuagizia laptop. Amesema kuwa atatoa ushirikiano kwa mahitaji mengine ya kielimu yatayoibuka.
Kwa upande wake Ndugu Biriat amemshukuru Ndugu Ado kwa msaada wake akiamini hatua hiyo inafungua milango zaidi kwa wadau wengine.
TEA YAHIMIZWA KUENDELEA KUIMARISHA SEKTA YA ELIMU
habariTEA YATAKA RASILIMALI ZAIDI KWA AJILI YA MAENDELEO YA ELIMU
habariDIAMOND APONGEZA USIMAMIZI WA JAB KATIKA SEKTA YA HABARI
habari




























