HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
NPCC YATOA ELIMU YA UDHIBITI WA SUMU KUVU KITETO
habariWATAALAMU WA MAZINGIRA WATAJWA KUWA NGUZO MUHIMU KUFANIKISHA DIRA YA TAIFA 2050 NA KUCHOCHEA USHIRIKIANO WA KIKANDA**
habariWATAALAMU KWENYE MAFUNZO YA KUKABILIANA NA MAAFA WATAKIWA KUYATUMIA KUKABILIANA NA MAAFA.
habariDCEA YATEKETEZA EKARI 68 ZA MASHAMBA YA BANGI TABORA
habariUTT AMIS YASHIRIKI MEI MOSI, YAHAMASISHA WANANCHI KUWEKEZA MIFUKO YA PAMOJA
habariDKT.SAMIA ASISITIZA HAKI NA MASLAHI YA WAFANYAKAZI .
habari
Na Mwandishi Wetu, Njombe.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kulinda haki za wafanyakazi na kuboresha maslahi yao ili kuongeza tija na maendeleo ya taifa.
Akihutubia katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe leo Mei Mosi, Rais Samia amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya kazi pamoja na kuhakikisha mishahara na stahiki za wafanyakazi zinazingatia hali halisi ya uchumi.
“Wafanyakazi ni muhimili muhimu wa uchumi wetu. Serikali yangu itaendelea kusimamia maslahi yenu, ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya kazi na kuhakikisha haki zenu zinalindwa,” amesema Rais Samia.
Aidha, ameeleza kuwa serikali itaendelea kufanya maboresho katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu na miundombinu, hatua ambayo inalenga kurahisisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi kwa wafanyakazi.
Katika hotuba yake, Rais Samia amewataka waajiri kuzingatia sheria za kazi, kutoa mikataba halali na kuhakikisha usalama wa wafanyakazi mahali pa kazi unazingatiwa ipasavyo.
Kwa upande wao, viongozi wa vyama vya wafanyakazi walitumia fursa hiyo kuwasilisha changamoto mbalimbali ikiwemo gharama ya maisha, mishahara midogo na ukosefu wa ajira kwa vijana, wakiiomba serikali kuendelea kuchukua hatua za kuboresha hali hiyo.
Maadhimisho ya Mei Mosi mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo: “Ulinzi wa Haki za Wafanyakazi, Chachu ya Maendeleo ya Taifa,” yakilenga kuhamasisha usawa, haki na ustawi wa wafanyakazi nchini.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, vyama vya wafanyakazi pamoja na wadau wa sekta ya ajira kutoka maeneo mbalimbali nchini.









EWURA YADHIHIRISHA NIDHAMU NA BIDII KATIKA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI
habari
Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
...
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, Mei 1, 2026, imeungana na wafanyakazi wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), maadhimisho yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Rais Samia amewahimiza waajiri na waajiriwa kote nchini kuendeleza ushirikiano, kuaminiana, na kutanguliza maslahi ya taifa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira na ustawi wa wafanyakazi, huku akiwataka kuongeza bidii na ufanisi kazini. Aidha, alibainisha wazi kuwa Serikali inathamini mchango wa wafanyakazi na itaendelea kuwaunga mkono katika juhudi za maendeleo ya nchi.
Katika maadhimisho hayo, EWURA imewakilishwa na wafanyakazi wake bora kutoka idara na vitengo mbalimbali. Wafanyakazi hao walichaguliwa kwa kura za wenzao kwa kuzingatia vigezo muhimu kama vile utendaji uliotukuka, nidhamu ya kazi, ubunifu pamoja na kujituma kazini.
Wawakilishi hao walishiriki katika maandamano rasmi yaliyopita mbele ya mgeni rasmi, wakibeba mabango yenye ujumbe wa kuhamasisha mshikamano na uwajibikaji kazini.
Ushiriki wao umeonesha dhamira ya EWURA kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Wafanyakazi wa EWURA wakishiriki maandamano ya Mei Mosi mbele ya Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wafanyakazi wa EWURA, wakati wa maandamano ya Maadhimisho ya Sherehe za Meimosi leo.
WAHITIMU 12 NIT WAHITIMU MAFUNZO YA AWALI YA LUGHA YA KIJAPANI
habariNA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
Wahitimu 12 wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wamehitimu mafunzo ya awali ya lugha ya Kijapani, hatua inayolenga kuongeza ujuzi na ushindani wao katika soko la ajira la ndani na kimataifa.
WMA YASHIRIKI MAADHINISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI MEI MOSI
habari
Wakala wa Vipimo (WMA) imeungana na wafanyakazi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali nchi nzima kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani.
Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa kila Mwaka tarehe 1 Mei na kaulimbiu ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mwaka 2026 ni *"Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".
Wakala imeshiriki katika maadhimisho hayo Kitaifa Mkoani Njombe ambapo watumishi wa Mkoa huo wameongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA Bw. Alban Kihulla.
Pamoja na ushiriki wa Kitaifa kadharika, WMA imeshiriki kuadhimisha siku ya Wafanyakazi katika ngazi za Mikoa kupitia ofisi za Mikoa za Kivipimo.
Uongozi wa WMA unaendelea kuwahimiza watumishi wake kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatoa huduma sahihi kwa wananchi kwa kusimamia matumizi sahihi ya Vipimo katika sekta mbalimbali.






CRJE–UDSM PARTNERSHIP PUTS STUDENTS TO THE TEST IN REAL-WORLD BRIDGE CHALLENGE
habari

MZUMBE YAUNGANISHA WATAFITI NA JAMII KUKABILI ATHARI ZA TABIANCHI NA CHANGAMOTO ZA MAJI
habariOryx Gas Tanzania Yaimarisha Upatikanaji wa Nishati Safi Kupitia Maduka Maalum
habariTANZANIA NA JAPAN KUFUNGUA MILANGO MIPYA YA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA NISHATI
NishatiUshirikiano kati ya Tanzania na Japan katika sekta ya nishati unaingia hatua mpya, huku juhudi zikielekezwa zaidi katika kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi na teknolojia za kisasa za uzalishaji umeme.
Hatua hiyo imebainishwa jijini Dar es Salaam leo tarehe 30 Aprili,2026 wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia,Dkt. James Mataragio alipokutana na Mwakilishi Mkuu mpya wa Japan International Cooperation Agency, Dkt. Kuge Katsuya.
Katika kikao hicho Dkt. Mataragio ameweka wazi Mkakati wa Serikali kuifanya sekta ya nishati kuwa kivutio kikubwa cha mitaji ya kimataifa hususan kutoka Japan.
Amesema kuwa pamoja na historia ndefu ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, hatua inayofuata inapaswa kulenga uwekezaji mkubwa zaidi unaoweza kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati nchini.
“Huu ni wakati wa kuhamasisha kampuni binafsi na taasisi za kifedha kutoka Japan kuja kuwekeza moja kwa moja katika miradi ya nishati Tanzania,” amesisitiza.
Akizungumzia ushirikiano wa Tanzania na Japan Dkt. Mataragio amesema JICA imekuwa mdau wa muda mrefu katika sekta ya nishati nchini na wameshiriki katika miradi ya Uandaaji wa Mpango kabambe wa Matumizi ya Gesi Asilia Nchini (Natural Gas Utilization Master Plan -NGUMP), wametoa fursa za kuwajengea uwezo wataalamu katika Matumizi ya gesi asili pamoja na utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya umeme.
Aidha Dkt. Mataragio amembushia ahadi ya muda mrefu ya Japan ya kuwezesha Mradi wa umeme wa megawati 300 mkoani Mtwara.
Kwa upande wake, Dkt. Kuge ameashiria mwelekeo mpya wa ushirikiano utakaojikita katika Mafunzo ya teknolojia ya nishati ya nyuklia, Uzalishaji wa umeme kupitia gesi asilia kwa ufanisi mkubwa zaidi na Kuunganisha Tanzania na wawekezaji binafsi kutoka Japan
Ahadi hiyo inaashiria uwezekano wa Tanzania kunufaika na teknolojia za kisasa zaidi za nishati kutoka Japan, moja ya nchi zinazoongoza duniani katika ubunifu wa nishati.
Mkutano huo umeonesha wazi kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Japan hauishii katika misaada, bali sasa unaelekea kwenye uwekezaji mkubwa na ubadilishanaji wa teknolojia hatua inayoweza kubadilisha kabisa sekta ya nishati nchini













