HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

EWURA YATOA MSAADA WA MASHUKA 455 HOSPITALI YA MKOA WA IRINGA

EWURA YATOA MSAADA WA MASHUKA 455 HOSPITALI YA MKOA WA IRINGA

February 10, 2026 Add Comment

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, 10 Februari 2026, imetoa msaada wa mashuka 455 katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa ili kuboresha huduma za kimatibabu hospitalini hapo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa azimio la Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo, lililofanyika mkoani humo tarehe 9 hadi 10 Februari 2026.

Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Iringa, Bi. Nuru Siyovelwa, alipokea msaada huo kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa, na kueleza kuwa, mashuka yamekuwa hayatoshelezi katika hospitali za mkoa huo, hivyo ameishukuru EWURA kwa kuguswa kwani yatasaidia kutoa huduma bora kwa wananchi.

Naye Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dkt. Alfred Mwakalebela, alieleza kuwa mashuka hayo yatapunguza changamoto iliyokuwepo ya upungufu wa mashuka, kwani kwa siku, kila mgonjwa anatakiwa kutumia mashuka 6, ilhali kwa sasa huduma hiyo haitoshelezi kwa kila mgonjwa.

Akiwasilisha msaada huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Meneja wa EWURA Kanda ya Kati, Mha. Hawa Lweno, alisema kuwa EWURA itaendelea na utaratibu wa kutoa mchango kwa jamii katika masuala mbalimbali ikiwemo afya.

KWAGILWA AKAGUA ICU YA KISASA HANDENI MJI, KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA

KWAGILWA AKAGUA ICU YA KISASA HANDENI MJI, KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA

February 10, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Reuben Kwagilwa, amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Wagonjwa Mahututi (ICU) katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni, mradi unaolenga kuondoa changamoto ya muda mrefu ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi.

Mhe. Kwagilwa amefanya ukaguzi huo leo Februari 10, 2026, wakati wa ziara yake ya kikazi hospitalini hapo, ambapo alipata fursa ya kujionea hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi huo pamoja na maendeleo yaliyofikiwa hadi sasa.

Katika ziara hiyo, alipokea maelezo ya kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa Halmashauri kuhusu maendeleo ya ujenzi, hali ya utekelezaji wa mradi pamoja na matarajio ya kukamilika kwake.

Ujenzi wa jengo hilo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuendelea kuboresha miundombinu ya sekta ya afya, kusogeza huduma muhimu karibu na wananchi pamoja na kuongeza uwezo wa hospitali kutoa huduma za dharura na kuokoa maisha ya wagonjwa.

Jengo hilo la kisasa linatarajiwa kuwa na mfumo wa hewa tiba (Oxygen) pamoja na vifaa maalum vya ufuatiliaji wa wagonjwa mahututi vitakavyowezesha uangalizi wa karibu wa hali zao.

SHINDA BODA: PIGABET YAGEUZA MICHEZO YA KUBAHATISHA KUWA FURSA YA KIUCHUMI KWA VIJANA

February 10, 2026 Add Comment

 

Dar es Salaam, Februari 10, 2026: Katika hatua inayoonesha mwelekeo mpya wa michezo ya kubahatisha nchini, PigaBet imezindua kampeni ya “SHINDA BODA” inayolenga si burudani pekee, bali pia kuwawezesha wachezaji—hasa vijana—kujipatia mtaji wa kujiajiri na kujiongezea kipato kupitia ushindi wa pikipiki mpya kila wiki.

Kampeni hiyo inawapa wachezaji wawili kila wiki fursa ya kushinda boda boda, zawadi ambayo kwa wengi imekuwa nyenzo muhimu ya kujiajiri au kuongeza kipato cha kila siku. Kupitia mfumo wa PigaPoints, kila mchezaji anayeshiriki michezo ya PigaBet ikiwemo Sports Betting, Casino na Aviator hujikusanyia pointi kwa kila bet au raundi, hali inayoongeza nafasi yake ya kuingia kwenye droo ya ushindi.

Akizungumza kuhusu dira ya kampeni hiyo, Meneja Masoko wa PigaBet, Arthur Kazora, alisema kampeni ya Shinda Boda inalenga kuwafanya wachezaji waone thamani ya muda na ushiriki wao.

“Tumelenga kumwezesha mchezaji kubadili ushindi kuwa fursa ya maisha. Boda si zawadi tu, ni chombo cha ajira, ni mtaji na ni mwanzo wa safari ya kujitegemea kiuchumi,” alisema Kazola.

Tofauti na kampeni nyingi za awali, Shinda Boda imebuniwa kuunganisha burudani, ushindi na uwezeshaji wa kiuchumi. Wachezaji hawazuiliwi na mchezo mmoja pekee, bali wanaruhusiwa kucheza michezo mbalimbali ndani ya jukwaa la PigaBet, jambo linalowawezesha kukusanya pointi zaidi na kuongeza nafasi ya ushindi.

PigaBet pia imeendelea kuvutia wachezaji kwa promosheni zinazolinda na kuongeza thamani ya mchezaji, ikiwemo 10% Cashback kila Jumatatu kwa bet zilizopotea, Win Boost hadi 1000%, pamoja na huduma ya 2UP na Cashout, vinavyompa mchezaji udhibiti zaidi wa michezo yake.

Kwa kutambua nguvu ya mitandao ya kijamii, kampeni hiyo pia imefungua milango kwa content creators kupitia PigaBet Content Creator Challenge, itakayoratibiwa na mshirika wao WAKA.WIN. Kupitia mpango huo, wabunifu wa maudhui watapata nafasi ya kunufaika kifedha kwa kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha kampeni.

Wadau wa michezo ya kubahatisha na vijana kwa ujumla wamehimizwa kujisajili kupitia www.pigabet.co.tz na kushiriki kampeni hiyo, huku PigaBet ikisisitiza umuhimu wa kucheza kwa uwajibikaji kwa watu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.

Kwa mtazamo mpya unaoangazia ajira na uwezeshaji, Shinda Boda imejipambanua kama kampeni inayotazama mbali zaidi ya ushindi wa muda mfupi, na kuweka msingi wa matumaini mapya kwa vijana wanaotafuta fursa za kujikwamua kiuchumi.

NAIBU WAZIRI MAGHEMBE AKUTANA NA BALOZI WA CUBA NCHINI, MHE. YORDENIS VERA

February 10, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ngwaru J. Maghembe (Mb.), amefanya mazungumzo na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Yordenis Despaigne Vera, katika Ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar Es Salaam tarehe 10 Februari, 2026.
WADAU WA BIASHARA SHINYANGA WAPONGEZA JITIHADA ZA BARAZA LA USHINDANI

WADAU WA BIASHARA SHINYANGA WAPONGEZA JITIHADA ZA BARAZA LA USHINDANI

February 09, 2026 Add Comment

Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bw. David Lyamongi,akizungumza wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa kibiashara wadau na wafanyabiashara wa mkoa wa Shinyanga iliyofanyika  katika Ukumbi wa Makindo, Shinyanga.

Na.Mwandishi Wetu-SHINYANGA

Baraza la Ushindani, kwa niaba ya Mwenyekiti wake, Mhe. Jaji Rose Ally Ebrahimu, limewashukuru wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Shinyanga kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika semina ya kuwajengea uwezo iliyofanyika  katika Ukumbi wa Makindo, Shinyanga.

Semina hiyo imelenga kuwaongezea wadau uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa kibiashara, haki zao kama wafanyabiashara pamoja na taratibu za kuwasilisha rufaa endapo hawataridhishwa na maamuzi ya mamlaka za udhibiti.

Akifungua semina hiyo, Bw. David Lyamongi, aliyemwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga, CP Salumu Hamduni, aliwataka wadau na wafanyabiashara kutumia vyema fursa hiyo ya kujifunza ili kuimarisha shughuli zao za kibiashara.

Aidha, aliishukuru Baraza la Ushindani kwa kuwaletea wakazi wa Shinyanga elimu muhimu inayolenga kulinda haki zao katika biashara na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.

Akizungumza katika semina hiyo, Msajili wa Baraza la Ushindani, Mhe. Mbegu Kaskasi, alisema kuwa Baraza la Ushindani ni chombo cha Serikali kilichoanzishwa kwa lengo la kusikiliza na kutatua migogoro ya ushindani wa kibiashara. Alisisitiza kuwa Baraza linaendelea kutoa elimu kwa umma ili kuhakikisha wadau na wafanyabiashara wanalifahamu, kulifikia kwa urahisi na kulitumia ipasavyo wanapohitaji haki.

Kwa upande wake Mjasiriamali kutoka Mkoa wa Shinyanga , Bw. Dedani Rutazibwa,alipongeza Baraza la Ushindani kwa kuandaa semina hiyo ya kuwajengea uwezo wadau. Alisema kutokana na umuhimu wa chombo hicho, ameiomba Serikali kupitia Baraza la Ushindani kuendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali katika ngazi tofauti, ili wafanyabiashara waweze kufahamu haki zao pamoja na mamlaka sahihi za kuwasilisha rufaa zinazotokana na maamuzi ya mamlaka za udhibiti na Tume ya Ushindani.

Naye  Mkazi wa Shinyanga Mwl. Zezema Nyangaki, alisema kuwa elimu aliyopata kupitia semina hiyo imemfungua macho, akieleza kuwa awali hakuwa na uelewa kuhusu uwepo wa mamlaka za udhibiti zinazopokea malalamiko ya wafanyabiashara. Aliongeza kuwa mafunzo hayo yamemsaidia kufahamu kuwa endapo hataridhishwa na maamuzi ya mamlaka hizo, anaweza kukata rufaa katika Baraza la Ushindani ili kupata haki yake kwa mujibu wa sheria.

BILIONi 109.4 KUPELEKA UMEME VITONGOJI 660 TABORA

February 09, 2026 Add Comment


📍Tabora


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewatambulisha wakandarasi wawili mkoani Tabora watakaotekeleza miradi ya kupeleka umeme vitongojini awamu ya Pili B (HEP 2B) kwenye majimbo saba ya mkoa wa Tabora kwa gharama ya shilingi bilioni 109.4  utakaoanza kutekelezwa katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa. 


Wakandarasi hao wametambulishwa leo Februari 9, 2026 kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Paul Chacha, ili waanze utekelezaji wa miradi hiyo ya kupeleka umeme kwenye vitongoji 660 mkoani humo.

Akizungumza mara baada ya kutambulishwa kwake wakandarasi hao ambao ni kampuni ya M/s Namis Corporate Ltd na M/s Sinotec Company Ltd, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paul Chacha  ameishukuru Serikali kupitia REA kwa kutoa fedha hizo ili kupeleka umeme kwenye vitongoji 660 mkoani humo.

"Serikali kupitia REA imefanya kazi kubwa. Tunasisitiza miradi hii ikamilike kwa muda uliopangwa na tutaendelea kuusimamia ipasavyo ili mkandarasi aweze kutekeleza majukumu yake pasipo changamoto yeyote katika kipindi chote cha utekelezaji wa mradi," Amesema Mhe. Chacha. 


Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Mussa Muze amesema Serikali imefanikiwa kufikisha umene katika vijiji vyote 724 katika mkoa wa Tabora, vitongoji 1,525 kati ya 3,749 sawa na asilimia 40 ya vitongoji vyote.

Ameongeza kuwa, mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji awamu ya pili B (HEP 2B) ulibuniwa na Serikali kwa lengo la kukamilisha mpango wa Serikali wa kufikisha umeme katika vitongoji vyote ifikapo mwaka 2030.

Naye, Msimamizi wa Miradi kutoka kampuni ya Sinotec Co. Ltd  Bw. Zhang Jianguang ameishukuru Serikali kupitia REA kwa kupewa fursa ya kutekeleza mradi huo mkubwa. Amesema watahakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati, watashirikiana na wananchi na kutoa kipaumbele cha ajira kwa wazawa ili miradi hiyo ilete tija kwa wananchi na nchi kwa ujumla.


Mwisho

NAIBU WAZIRI WA AFYA AITAKA JAMII KUACHA UNYANYAPAA DHIDI YA WENYE KIFAFA

February 09, 2026 Add Comment


Wananchi wametakiwa kuwajali na kuachana na vitendo vya unyanyapaa dhidi ya wagonjwa wa kifafa, kwani asilimia kubwa ya wagonjwa hao hushindwa kupata ushirikiano kutoka kwa familia na jamii zinazowazunguka, jambo linalosababisha kuchelewa kupata matibabu na kufika hospitalini wakiwa katika hali mbaya zaidi kiafya.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kifafa Duniani yaliyofanyika leo Februari 06, 2026 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) amesema kuwa wizara inaandaa miongozo na taratibu mbalimbali kuhakikisha kuwa wagonjwa wa kifafa wanaishi katika mazingira salama na yenye staha.

"Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonesha kuwa watu takribani milioni 50 duniani wanaishi na kifafa, huku milioni 6 wakigundulika kila mwaka. Watu wenye kifafa wana hatari ya vifo mara tatu zaidi, huku Afrika ikiripoti viwango vya juu mara 4 hadi 6 zaidi. Zaidi ya asilimia 80 ya mzigo wa kifafa duniani unabebwa na nchi zenye kipato cha chini na cha kati, ikiwemo Tanzania.” amesema Dkt. Samizi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Dkt. Julieth Magandi, ameeleza kuwa Unyanyapaa bado ni changamoto kubwa kwa wagonjwa wa kifafa kwani baadhi ya jamii bado wanaamini kifafa kinarogwa, ni laana au ni ugonjwa wa kurithi, hali ambayo si ya kweli. Ameongeza kuwa kifafa ni ugonjwa unaotibika na kudhibitika kitaalamu, hivyo jamii inapaswa kuachana kabisa na mila potofu na badala yake kuwapa wagonjwa hawa msaada na heshima wanayostahili.

Aidha, akiwasilisha wasilisho lake katika mkutano huo, Rais wa Chama cha Kifafa nchini, Profesa William Matuja, amesema kuwa elimu kwa jamii ni silaha muhimu katika mapambano dhidi ya kifafa, akisisitiza kuwa endapo jamii itaelimishwa ipasavyo, wagonjwa wengi watajitokeza mapema kupata matibabu na kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine.