HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
BODI YA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI MIRADI YA REA
📌*Watembelea Banda la REA kwenye maonesho ya Sabasaba*
📌*Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa miradi ya nishati safi Vijijini*
Leo tarehe 5 Julai, 2026 kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) wametembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika maonesho yanayoendelea ndani ya Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katika banda hilo, wajumbe wa REB wameelezwa kuhusu utekelezaji wa miradi ya usambazaji umeme kwenye maeneo ya vitongoji na uwezeshaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inayoendelea nchini.
*Karibu Sabasaba, karibu Banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)*
PROF. KABUDI AHAMASISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU SABASABA
habariWAZIRI SANGU AKUTANA NA MZEE WA UPAKO NA MTUME MALISA
habariDKT. MUNISI: TAASISI ZA DINI NI WADAU MUHIMU KATIKA MAENDELEO YA TAIFA
habariTRA YAWEKA REKODI MPYA YA MAKUSANYO, YAKUSANYA SH. TRILIONI 37.96 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026
habari
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeweka rekodi mpya katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya jumla ya Shilingi trilioni 37.96 katika mwaka wa fedha 2025/26, sawa na asilimia 105.24 ya lengo la kukusanya Shilingi trilioni 36.07.SERIKALI KUTEKELEZA MRADI WA UMEME JUA KATIKA VISIWA SABA MUSOMA
habari
Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga shilingi milioni 273.6 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme wa jua katika visiwa saba vya Wilaya ya Musoma ikiwemo Nyasaungu, Muroba, Kagongo, Nyamasanje, Rukuba na Iriga, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais, Mhe. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya umeme bila kujali eneo analoishi.
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kutatua kero za wananchi katika Jimbo la Musoma Vijijini.
Amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa umeme ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo tayari vimefikiwa na huduma hiyo, huku hatua zinazofuata zikielekezwa katika kufikisha umeme kwenye vitongoji vilivyosalia.
Amebainisha kuwa kati ya vitongoji 374 vilivyopo, takribani 100 pekee ndivyo bado havijafikiwa na umeme huku zaidi ya vitongoji 50 vikiwa katika hatua za utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme.
Aidha, amesema Serikali imepokea maombi ya Mbunge wa Musoma Vijijini ya kuhakikisha vitongoji vyote ambavyo havina umeme vinafikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2027, akieleza kuwa lengo hilo linaendana na dhamira ya Serikali inayolenga kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinaunganishwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.
Sambamba na hilo, Mhe. Salome amesema Wizara ya Nishati imeendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya uzalishaji mali, ikiwemo maeneo ya wachimbaji wa migodi wilayani Musoma Vijijini.
Kuhusu baadhi ya wananchi ambao miundombinu ya umeme imepita karibu na makazi yao lakini hawajaunganishwa na huduma hiyo, amemuelekeza Meneja wa TANESCO Wilaya ya Musoma kuhakikisha wananchi hao wanaunganishiwa umeme.
Katika hatua nyingine, amewahimiza wananchi wa Musoma Vijijini kutumia nishati safi ya kupikia, akibainisha kuwa Serikali imetoa ruzuku ya zaidi ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ili kuyawezesha kupatikana kwa gharama nafuu.
SALOME MAKAMBA : WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000
habari
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeelekeza kuwa wananchi wote ambao wamepitiwa na miundombinu ya umeme lakini bado hawajaunganishiwa huduma hiyo waunganishiwe kwa gharama ya Shilingi 27,000 tu.
Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Julai 3, 2026, katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Butiama, mkoani Mara, katika ziara ya Waziri Mkuu, Mhe. Mwigulu Nchemba.
Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Salome amemuelekeza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mara pamoja na Meneja wa TANESCO Wilaya ya Butiama kubaini maeneo yote ambayo nyaya za umeme zimepita juu ya kaya za wananchi lakini bado hawajaunganishwa na huduma husika ili hatua stahiki zichukuliwe, ikiwemo kufunga transfoma katika maeneo yenye uhitaji.
Amesisitiza kuwa umeme ni nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi, akieleza kuwa unachochea ukuaji wa uchumi, huboresha huduma za afya na kuinua ustawi wa wananchi, hivyo Serikali itaendelea kuhakikisha wananchi wote wanaostahili wanafikiwa na huduma hiyo.
Aidha, amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga zaidi ya Shilingi bilioni 38 kwa ajili ya utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini katika Mkoa wa Mara. Fedha hizo zitawezesha kuendelea kusambaza umeme katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa na hivyo kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Ameongeza kuwa, kufuatia maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali itahakikisha vitongoji 51 ambavyo havina umeme mkoani Mara vinafikiwa na nishati hiyo.
Kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, Mhe.Salome amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
Amesema katika Mkoa wa Mara tayari Serikali imesambaza majiko ya gesi zaidi ya 19,000 na majiko banifu zaidi ya 8,000 ili kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kulinda afya za wananchi na kuhifadhi mazingira.
Katika mkutano huo wa hadhara, wananchi waliwasilisha jumla ya kero sita, ambapo kero tatu zilipatiwa ufumbuzi papo hapo, huku hatua za kushughulikia kero zilizobaki zikiendelea kuchukuliwa na Serikali.





DKT. MUNISI: MAHUSIANO MEMA NI NGUZO MUHIMU YA UTEKELEZAJI DIRA YA TAIFA 2050
habariTANZANIA YATAMBULIWA KWA MCHANGO WAKE KATIKA UHURU WA UMOJA WA VISIWA VYA COMORO WAKATI WA MHADHARA MAALUM WA KIDIPLOMASIA
WAANDISHI WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KUHUSU DAWA ZA KULEVYA
habariNEMC YAJA NA KIJIJI CHA MAZINGIRA MAONESHO SABASABA
habariTANZANIA IPO TAYARI KUELEKEA AFCON 2027
habariKIPANGULA ASISITIZA WELEDI WA UANDISHI WA HABARI SABASABA
habari

WAZIRI SANGU: TAASISI ZA DINI NI NGUZO YA AMANI, MAADILI NA MALEZI BORA
habariBARRICK-TWIGA , SERIKALI WAZINDUA MRADI WA ‘BARRICK FUTURE FORWARD EDUCATION PROGRAM AWAMU YA PILI KIBAIGWA, DODOMA
habari
Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa Barrick–Twiga Future Forward Education Program uliozinduliwa Kibaigwa, mkoani Dodoma, na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe.








































