HABARI ZETU
Loading...

HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MRADI WA FUNZA WACHANGIA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA UFUGAJI

June 04, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imeendelea kuwaibua na kuwawezesha wabunifu nchini kupitia mafunzo yanayolenga kugeuza ubunifu wao kuwa fursa za ajira na maendeleo ya kiuchumi.

SERIKALI YAZINDUA GRAND CHALLENGES TANZANIA KUCHOCHEA UBUNIFU WA KUTATUA CHANGAMOTO ZA TAIFA

June 04, 2026 Add Comment
SERIKALI imezindua jukwaa jipya la kitaifa la ubunifu litakalowawezesha wanasayansi, watafiti na wabunifu kubuni suluhisho za ndani kwa changamoto zinazoikabili nchi katika sekta za afya, usalama wa chakula, mabadiliko ya tabianchi na teknolojia, hatua inayotarajiwa kuharakisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

SERIKALI YAENDELEA NA UANDAAJI WA KANUNI ZA BIMA ZA KILIMO KULINDA WAKULIMA

June 04, 2026 Add Comment



Na Jordan Mbwambo WF, Dodoma


Serikali imesema inaendelea kukamilisha mchakato wa uandaaji wa Kanuni za Bima za Kilimo ambazo zitasaidia kuongeza upatikanaji wa kinga kwa wakulima dhidi ya majanga yanayoathiri mazao, mifugo, misitu na sekta ya uvuvi nchini.


Hayo yamebainishwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Laurent Luswetula (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ilemela, Mhe. Kafiti William Kafiti, aliyetaka kujua wakati ambao Serikali itakamilisha Kanuni hizo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali.


Mhe. Luswetula alisema kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Fedha inaendelea na utafiti na maboresho katika Sekta ya Bima ya Kilimo ili kuhakikisha mfumo huo unakuwa shirikishi na wenye kuvutia uwekezaji kwa wadau wa ndani na nje ya nchi.


“Serikali inaendelea na utafiti kuhusu bima katika mnyororo wa kilimo (mazao, mifugo, misitu na uvuvi) ili pamoja na mambo mengine kuwa na Kanuni zinazovutia uwekezaji katika bima ya kilimo na kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima ili kupata huduma za bima kwa urahisi na haraka”, alisema Mhe. Luswetula.


Aliongeza kuwa, Serikali inakusudia kuhakikisha kanuni hizo zinakuwa rafiki kwa wakulima na wakati huo huo zikichochea ushiriki wa sekta binafsi katika kutoa huduma za bima ya kilimo nchini.


Aidha, alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya bima kuhakikisha mfumo huo unakuwa endelevu na unaonufaisha wakulima kwa upana zaidi.


DKT.SAMIA SULUHU HASSAN ATUNUKU SHAHADA KWA WATANZANIA ASEMA NI YAO

June 04, 2026 Add Comment




Na Beda Msimbe,TBN, Moscow

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) huku akiitoa shahada hiyo kwa Watanzania.



Shahada hiyo ilitolewa na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni,2026.

Rais Mhe. Dk Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania,

pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii,

Akizungumza baada ya kupewa shahada hiyo Rais Samia alisema kwamba heshima aliyopewa si ya mafanikio yake binafsi bali ni utambuzi wa juhudi na matarajio ya watanzania wote.

Alisema shahada hiyo ni ishara ya utambuzi wa dhamira ya pamoja ya Watanzania wote katika kuleta maendeleo,ushirikiano na ustawi wa binadamu.

“Nilipokea kwa furaha habari za kutunukiwa heshima hii,lakini mara moja nikatambua kwamba si yangu peke yangu. Ni heshima inayoitambua dhamira yetu ya pamoja ya maendeleo, ushirikiano na maendeleo ya binadamu” alisema Dk Samia.


Hii ni shahada yake ya nane kutolewa kwa Rais Samia .


Aidha alisema shahada hiyo  aliyopewa leo ni ishara ya urafiki wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi ikiwa ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya elimu katika kuunganisha mataifa.


Aidha alisema heshima hiyo inaakisi uhusiano wa kudumu kati ya nchi za Tanzania na Urusi ambazo zimeendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali hususani elimu kwa miongo kadhaa sasa.

Katika hotuba yake ambayo viongozi wa watanzania waliopo  Urusi na vyuo vya Urusi walisema ni iluiyiojaa mamlaka makubwa, Rais Samia alisema kwa miaka mingi watanzania walikuwa wanapata elimu inayochangia maendeleo  ya Tanzania katika Nyanja mbalimbali jambo ambalo pia  limeimarisha mahusiano ya watu wa pande zote mbili,

“Mama amezungumza nchi yetuj ina sifa sana. Tena sifa njema kwa kupata mwaliko wa Rais Vladmir Putin kuja hapoa ni kutambulika kwa Tanzania ni ishara njema na hotuba ya mama imeakisi matarajio” alisema Jefrey Mashauri Mwenyekiti wa wanafunzi wa Tanzania shirikishoi la Urusi (TASCARU).


Naye Mwenyekit wa watanznaia wanaoishi Urusi Pascal Gura alisema watanzania 300 wanaosihi hapo wameona fahari kubwa kukutana na kumsikiliza Rais Samia akionesha ni kwa namna gani kama Taifa Tanzania linaendelea kuwika.


Rais Samia katika hotuba yake alionesha jinsi Tanzania inavyoweza kufanikisha mambo wanaposaidiana na kushirikiana kwa maendeleo ya taifa.


Pia alikumbusha vijana kujipatia elimu huku wakizingatia kauli ya baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere ambaye alifundisha kwamba maendeleo lazima daima yaweke mwanadamu katikati ya kila jambo.


Aidha alitaka vijana kuangalia taifa lao na kwamba dokumentari iliyooneshwa kabla ya kutunukiwa shahada kuhusu maendeleo ya Tanzania inawaonesha dhamira ya watanzania na ni muhumu kwao watambue umuhimu wao kwa taifa huku huku wakiyaakisi maneno ya baba wa taifa katika utumishi wao.

Tangu kuanzishwa kwa chuo hicho miaka ya 1960 watanzania 1,100 wamepata utaalamu mbalimbali kupitia hucho hicho.Idadi hiyo ni kati ya wanafunzi 5000 ambao wamepata taaluma zao nchini Urusi katika Nyanja mbalimbali ikiwamo udaktari uhandisi na wataalamu wa sayansi.


Rais katika hotuba yake pia alizungumzia makubaliano kadhaa yaliyotiwa saini  yenye lengo la kuleta ushirikiano wa aina yake katika utafiti na elimu na ufundishaji.

Mwisho

MWANZA KINARA KATIKA USIMAMIZI WA MAAFA

June 04, 2026 Add Comment




Na, mwandishi wetu - Mwanza


Mkoa wa Mwanza umetajwa kuwa Kinara kwa kuratibu na kusimamia ipasavyo shughuli za kukabiliana na maafa, majanga na mawasiliano ya dharura kutokana na hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya utayari na mwitikio wa dharura.

Sifa hizo zimetolewa Juni 4, 2026 na wataalamu wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa yanayofanyika mkoani Mwanza kwa siku mbili yakilenga kuongeza uwezo wa kukabiliana na majanga.

Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Said Mtanda amesema maafa yameendelea kuwa tishio kubwa duniani kutokana na athari zake kwa maisha ya watu, uchumi na maendeleo ya jamii.

Ametaja baadhi ya majanga yanayoikabili Tanzania kuwa ni mafuriko, ukame, maporomoko ya ardhi, matetemeko ya ardhi, mioto ya misitu na magonjwa ya mlipuko.

Kutokana na kuongezeka kwa matukio hayo Mhe. Mtanda amezitaka Wilaya zote Mkoani humo kuwa na mipango kazi na mifumo imara ya usimamizi wa maafa ili kuhakikisha maandalizi, mwitikio wa haraka na urejeshaji wa hali unafanyika kwa ufanisi.

Aliongezea kuwa, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeendelea kuimarisha usimamizi wa maafa kwa kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2024 pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022.


Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa mafunzo hayo yatawajengea uwezo viongozi na wataalamu katika utekelezaji wa sera, sheria na miongozo ya usimamizi wa maafa katika maeneo yao.

Aidha, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Wilayani Kwimba, uliojumuisha tani tisa za mahindi, mablanketi, ndoo na vifaa vya wanafunzi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa eneo la utafiti kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bw. Vanvaco Luvanda amesema mafunzo hayo ya siku mbili yanaendelea kutolewa nchini kote kwa lengo la kuongeza utayari na uwezo wa kitaalamu wa kukabiliana na maafa yanapotokea.

Alifafanua kuwa, uwepo wa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka ambapo uzoefu unaonesha kuwa athari za maafa zinaendelea kuongezeka kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ongezeko la shughuli za kibinadamu na changamoto nyingine zinazoweza kusababisha maafa.


=MWISHO=

WAZIRI SANGU AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA 114 ILO

June 04, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akifuatilia agenda zilizokuwa zikijadiliwa katika Mkutano wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaoendela Jijini Geneva, Uswisi leo Juni 4, 2026.

DCEA, VETA Kuibua Matumaini Mapya kwa Waraibu Waliopona

June 04, 2026 Add Comment

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) zimeingia makubaliano ya ushirikiano yatakayowezesha waraibu waliopona matumizi ya dawa za kulevya kupata mafunzo ya ufundi stadi, hatua inayolenga kuwajengea uwezo wa kujitegemea kiuchumi na kuzuia kurejea kwenye matumizi ya dawa hizo.

TIMU KUTOKA OFISI YA WAZIRI MKUU YAFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU TAWALA MWANZA KUHUSU MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA

June 04, 2026 Add Comment




Na, mwandishi wetu - Mwanza

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mwanza Bw. Henry Mwaijega amekutana na kufanya mazungumzo timu ya Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu walipomtembelea ofisini kw


ake leo 04 Juni, 2026 Jijini Mwanza.


Timu hiyo ipo mkoani Mwanza kwa lengo la kuongoza mafunzo ya usimamizi wa maafa kwa Kamati za Usimamizi wa Maafa mkoa pamoja na wadau mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha utayari, uratibu na uwezo wa kukabiliana na majanga katika ngazi ya mkoa.

Pamoja na mafunzo hayo, wanatarajia kuzindua Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha mkoa wa mwanza tarehe 05 juni, 2026.





=MWISHO=

ISW KUANDAA KONGAMANO LA KWANZA LA KIMATAIFA LA UWEZESHAJI WA WATU NA USTAWI WA JAMII

June 04, 2026 Add Comment
Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW) kimetangaza kufanyika kwa Kongamano lake la Kwanza la Kimataifa la Uwezeshaji wa Watu na Ustawi wa Jamii, litakalofanyika Juni 5, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC) jijini Dar es Salaam.

MRADI WA FOLUR KUSHUSHA MIONGOZO YA KIMATAIFA MAENEO YA UTENDAJI ZANZIBAR

June 04, 2026 Add Comment


Na Anangisye Mwateba, Zanzibar


MRADI wa Mifumo ya Chakula, Matumizi ya Ardhi na Urejesho wa Mandhari ya Misitu nchini Tanzania (FOLUR), unatarajia kutoa mafunzo maalum kwa viongozi wa serikali za vijiji na shehia mbalimbali visiwani Zanzibar. Hatua hiyo inalenga kujenga uwezo wa kiutendaji na kuhakikisha jamii inatekeleza shughuli za mradi huo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Akifungua mafunzo hayo kwa maafisa ugani wa kilimo na misitu upande wa Zanzibar, Mratibu wa mradi huo, Bi. Miza Suleiman Khamis, alisema dhumuni kubwa ni kuwawezesha watendaji hao kubaini, kuepuka au kupunguza athari hasi zinazoweza kujitokeza kabla hazijaletea madhara wanajamii na mazingira yao.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Kitengo cha Jinsia, Usalama wa Mazingira na Jamii wa mradi huo, Bw. Revocatus Kadoshi, alibainisha kuwa viongozi wa shehia na maafisa ugani watafundishwa miongozo minne mikuu.

Miongoni mwa miongozo hiyo ni Mpango wa Usimamizi wa Mazingira na Jamii (ESMP), unaohusu udhibiti wa matumizi ya rasilimali na kuzuia uhamishaji wa watu usio wa hiari.

Bw. Kadoshi alifafanua kuwa mwongozo huo unalenga kudhibiti na kupunguza athari za kimazingira na kijamii wakati wa utekelezaji wa mradi. Aliongeza kuwa hatua hiyo inaenda sambamba na matakwa ya Mwongozo wa Sera na Taratibu Jumuishi za Ulinzi wa Kijamii za Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF).

"Viongozi hawa pia watafundishwa kuhusu Usimamizi Shirikishi wa Visumbufu. Huu unalenga kulinda afya na usalama wa jamii kwa kudhibiti athari zitokanazo na matumizi ya viuatilifu na mbolea," alisema Bw. Kadoshi.

Aidha, mafunzo hayo yatahusisha mbinu za usimamizi wa mazingira zinazohakikisha ustawi wa jamii, usalama mahali pa kazi, pamoja na usafi wa mazingira wakati wote wa utekelezaji wa shughuli za mradi huo.

Vilevile Aliongeza kuwa, ili kuhakikisha usalama wa jamii, mradi umeweka utaratibu maalumu wa kupokea nakufanyia kazi malalamiko kutoka kwa mwanajamii au kikundi cha kijamii kuhusiana na shughuli zinazotekelezwa na mradi. Hii inalwnga kuhakikisha jamii inashiriki vema kwenye shighuli za mradi na wanakuwa na nafasi ya kutoa dukuduku au lalamiko wakati wowote.




WFP KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA NCHINI

June 04, 2026 Add Comment


Na mwandishi wetu – Morogoro



Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula la Duniani (World Food Programme -WFP) limesema litaendeleza mashirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha masuala ya menejimenti ya maafa yanaendelea kutekelezwa kwa tija na malengo yaliyokusudiwa kwa kuimarisha uwezo wa kitaalamu na Kiteknolojia kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Hayo yameelezwa na Naibu Mkurugenzi wa WFP Tanzania Bi. Christine Mendes wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura inayoendelea mkoani Morogoro.

Bi.Christine alisema ushirikiano hususan katika kuwezesha utekelezaji wa Mradi wa Field-Based Preparedness Project (FBPP), ambapo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mradi huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uwezo wa taifa katika sekta ya utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji.

Aidha, alieleza kuwa zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura linawakilisha hatua muhimu katika kuendelea kujitolea kwa Tanzania katika kuimarisha utayari wa kitaifa katika uratibu wa masuala ya maafa.


“Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, Mradi wa Matayarisho ya Uwandani (FBPP) umetoa mafanikio yaliyounganishwa ambayo yameimarisha kwa kiasi kikubwa utayarishaji wa vifaa na mfumo wa kukabiliana na dharura wa Tanzania,” alisema.

Aliongezea kuwa WFP itaendeleza ushirikiano wake na Serikali na kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono masuala ya menejimenti ya maafa ili kuyafikia matarajio kwa pamoja kwa kuwa na mfumo wa kukabiliana na hali ya dharura wa kitaifa wenye kasi zaidi, ulioratibiwa vyema na unaostahimili zaidi wenye uwezo wa kutoa hatua za kibinadamu kwa wakati unaofaa.

“Tutumie fursa hii kikamilifu, sio tu kupima mifumo, lakini kuimarisha mifumo, hivyo tuthibitishe tena dhamira yetu ya pamoja ya kujitayarisha kwa kuwajibika na kulenga kwa dhati kuokona maisha”alisisitiza Bi.Christine.



WAZIRI SANGU: SERIKALI KUENDELEA KUKUZA USTAWI WA SEKTA YA KAZI NA USHIRIKIANO KIMATAIFA

June 03, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akisalimiana na Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Umoja wa Mataifa Nchini Uswisi, Mhe. Dkt. Abdallah Possi alipotembelea ofisi za Ubalozi huo leo Juni 3, 2026.

RAIS VLADMIR PUTIN: URUSI KUFUNGUA FURSA MPYA ZA UCHUMI TANZANIA

June 03, 2026 Add Comment

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladmir Putin pamoja na ujumbe wake katika Ikulu ya Kremlin Jijini Moscow, tarehe 03 Juni, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow nchini Urusi tarehe 03 Juni, 2026.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladmir Putin katika Ikulu ya Kremlin Jijini Moscow, tarehe 03 Juni, 2026. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladmir Putin katika Ikulu ya Kremlin Jijini Moscow, tarehe 03 Juni, 2026.

…………. 

Na Beda Msimbe, TBN, Moscow

Urusi imesema itaendelea kufungua fursa mbalimbali za kiuchumi kwa Tanzania kwa manufaa ya pande zote mbili katika kuimarisha ushirikiano wa maendeleo.
Aidha, taifa hilo lenye jumla ya miradi 70 nchini Tanzania yenye thamani ya dola za Marekani milioni 434.22, ambayo imewezesha ajira zaidi ya 3,018, limesema litazitangaza zaidi fursa hizo katika Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi unaotarajiwa kufanyika kesho kutwa.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao chake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Urusi, Vladimir Putin, amesema taifa lake limekuwa likifuatilia kwa karibu mageuzi mbalimbali yanayofanyika nchini Tanzania na kuridhishwa na kasi ya maendeleo yake.
Putin amesema mazungumzo yake na Rais Samia yamekuwa yenye manufaa makubwa kwa mataifa yote mawili na kuahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Urusi na Tanzania katika sekta mbalimbali za maendeleo.
Kwa upande wake, Rais Samia amesema ziara yake katika Shirikisho la Urusi ina umuhimu mkubwa wa kihistoria kwake binafsi na kwa taifa la Tanzania kwa ujumla.
“Ziara yangu ina umuhimu wa pekee wa kihistoria kwangu binafsi na kwa nchi yangu. Imepita zaidi ya nusu karne tangu kufanyika kwa ziara ya mwisho ya kiserikali ya Tanzania nchini Urusi. Hivyo, kwangu hii ni safari ya kihistoria sana kuja Urusi kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa pande mbili pamoja na maendeleo endelevu kwa wananchi wetu. Kwa niaba yangu na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa mwaliko huu,” alisema Rais Samia.
Aidha, Rais Samia alikumbusha mchango mkubwa wa Urusi katika harakati za Tanzania za kupigania uhuru na kumpongeza Rais Putin kwa maadhimisho ya miaka 81 ya ushindi katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia yaliyofanyika Mei 9 mwaka huu.
Rais Samia aliwasili jijini Moscow kwa ziara yake ya kwanza nchini Urusi, ambayo pia ni ziara ya kwanza ya kiongozi wa Tanzania nchini humo katika kipindi cha zaidi ya miaka 50, kwa ajili ya mazungumzo rasmi na Rais Putin.
Kwa mujibu wa viongozi hao, mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha zaidi uhusiano wa kirafiki na ushirikiano kati ya Tanzania na Urusi. Vilevile, walibadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali ya kikanda na kimataifa yenye maslahi kwa mataifa yao.