HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DKT. MWIGULU AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MADARAJA YA MKWAJUNI NA KIGOGO, DAR ES SALAAM.

April 26, 2026 Add Comment

 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 26, 2026 anafanya ziara katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mkwajuni lenye urefu wa mita 20 na kimo cha mita 5.5 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 11.6

Pia Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amekagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigogo lenye urefu wa mita 50 kimo cha mita 8.9 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa mita 625 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 17.7.









TAIFA GESI YATOA ELIMU YA MATUMIZI SALAMA YA GESI NJOMBE

April 26, 2026 Add Comment







Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya Taifa Gesi imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi na salama ya gesi, sambamba na kuhamasisha usalama mahali pa kazi katika maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani.

Akizungumza katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema, Njombe, Mtaalamu wa Masuala ya Afya, Mazingira, Usalama na Ulinzi Mahali pa Kazi kutoka Taifa Gesi, Aurelius Marcus Mdemu, alisema kampuni hiyo imeshiriki maadhimisho hayo yanayoanza Aprili 24 hadi 29, 2026 kwa lengo la kutoa elimu kwa wateja na jamii kwa ujumla.




Alisema kupitia banda lao, wanaonesha vifaa mbalimbali vinavyotumika kazini ili kuimarisha usalama wa wafanyakazi, pamoja na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya gesi na faida zake. Aidha, alieleza kuwa wanajitahidi kuondoa hofu na dhana potofu zilizopo miongoni mwa watumiaji wa gesi.

“Tunawaonesha wananchi namna Taifa Gesi inavyoweka kipaumbele kwenye usalama wa wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vifaa kinga vinavyotakiwa kutumika muda wote wakiwa kazini,” alisema Mdemu.








Kwa upande wake, Afisa Masoko wa Chapa wa Taifa Gesi, Santina Ngaponda, alisema maonyesho hayo yameandaliwa na OSHA, yalianza Aprili 24 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 29 mwaka huu.

Ngaponda aliwahimiza wakazi wa Njombe na maeneo ya jirani kutembelea banda la Taifa Gesi ili kupata elimu kutoka kwa wataalamu wa usalama, kujifunza matumizi sahihi ya gesi, pamoja na kuona vifaa vya usalama vinavyotumika kazini na umuhimu wake.


Aidha, aliongeza kuwa kampuni hiyo inatoa punguzo maalum la bei ya gesi na vifaa vyake, pamoja na zawadi mbalimbali kwa wateja watakaotembelea banda hilo.


Naye Meneja Mauzo wa Kanda ya Nyasa wa Taifa Gesi, Arnold Salewa, alisema wanaendelea kutumia maonyesho hayo kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi pamoja na kuuza bidhaa zao kwa bei ya promosheni.

Alisema kanda hiyo inajumuisha mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma, na kwamba pia wanatoa fursa kwa wananchi wanaotaka kuwa mawakala wao, kwa kuwapatia elimu ya biashara na usimamizi salama wa mitungi ya gesi.

Salewa alisisitiza kuwa Taifa Gesi ipo mstari wa mbele kuhakikisha kaya, migahawa na taasisi mbalimbali zinaanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu, ili kupunguza athari za matumizi ya mkaa na kuni kwa mazingira na afya za Watanzania.

Aliongeza kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa, huku Taifa Gesi ikiendelea kuwa chaguo sahihi kwa watumiaji wengi nchini.

TRA KARIAKOO YASHIRIKI MKUTANO MKUU WA JWK, YASISITIZA UWASILISHAJI WA RITANI KWA WAKATI

April 25, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeshiriki kikamilifu katika Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo (JWK) uliofanyika katika ukumbi wa soko la Kariakoo, jijini Dar es Salaam.

DCEA YANUFAIKA NA TEKNOLOJIA YA KISASA KATIKA VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA

April 25, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imepokea vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa kimaabara kutoka Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC), ikiwa ni pongezi baada ya kutambua mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika udhibiti wa dawa za kulevya nchini.

WAMILIKI WA HOTELI WATAKIWA KUJIANDAA KUNUFAIKA NA AFCON 2027

April 25, 2026 Add Comment
Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji (Mb), akiwa katikati katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Hoteli ya Manyara’s Secret, iliyopo ndani ya Pori Tengefu la Mto wa Mbu, Wilaya ya Monduli, Mkoani Arusha.

GASCO YATOA ELIMU YA USALAMA KAZINI, YAVUTIA WANANCHI KATIKA MAADHIMISHO YA OSHA

April 25, 2026 Add Comment
Watumishi wa GASCO katika picha ya pamoja kwenye maonesho ya OSHA-mkoani Njombe

TALGWU TAWI LA RUWASA LAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAPYA, MHANDISI RASHID ATETEA UENYEKITI

April 25, 2026 Add Comment

Chama cha Wafanyakazi Serikali za Mitaa (TALGWU), tawi la RUWASA, kimefanya mkutano mkuu wa uchaguzi wa viongozi wapya ambapo Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Mhandisi Rashid Abdallah, amefanikiwa kutetea nafasi yake ya uenyekiti.

Uchaguzi huo ulifanyika Aprili 24, 2026 jijini Dodoma, katika mazingira ya uwazi na ushirikishwaji mpana wa wanachama, waliotekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kuchagua viongozi watakaoongoza tawi hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Katika uchaguzi huo, viongozi waliochaguliwa ni pamoja na Mhandisi Rashid Abdallah (Mwenyekiti wa Tawi), Ibrahim Fungo (Katibu wa Tawi), Tumaini Gwatalile (Mwenyekiti wa Makundi Maalum – Wanawake), Ashura Nkunya (Katibu wa Makundi Maalum – Wanawake), Victoria Charles (Mjumbe wa Makundi Maalum – Vijana), na Adam Suleiman (Mjumbe wa Makundi Maalum – Watu wenye Ulemavu).

Uongozi huo mpya unatarajiwa kuimarisha mshikamano miongoni mwa wanachama, kulinda na kutetea maslahi yao, pamoja na kuendeleza maendeleo ya chama katika tawi la RUWASA.








WAZIRI KAPINGA AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI WAZAWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA VIWANDA

April 25, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewahimiza wawekezaji wazawa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya viwanda, ikisisitiza kuwa imeendelea kuboresha na kurahisisha mazingira ya biashara ili kuongeza uwekezaji wa ndani.

EACCA YAAPISHA MAKAMISHNA WAPYA KUIMARISHA USHINDANI WA BIASHARA AFRIKA MASHARIKI

April 23, 2026 Add Comment
-Moshi, Kilimanjaro

Katika hatua kubwa inayolenga kuleta mapinduzi kwenye soko huria na kumlinda Mlaji. Mamlaka ya Ushindani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCA) zimekutana Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro leo Aprili 23, 2026 na kuwaapisha rasmi wajumbe wapya wanne kutoka Nchi za Tanzania, Somalia, Uganda na DRC ambao watasimamia mazingira mazuri ya ushindani wa biashara na walaji kwa Jumuiya hiyo.

NJOMBE KUPOKEA MAADHIMISHO YA KITAIFA YA USALAMA NA AFYA MAHALA PA KAZI

April 23, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imewataka waajiri na wafanyakazi nchini kuyatazama upya mazingira ya kazi ili kuhakikisha yanakuwa salama na rafiki kwa afya, hususan afya ya akili.

TEA, WIZARA YA ELIMU ZANZIBAR KUSHIRIKIANA KUIMARISHA MIRADI YA ELIMU

April 23, 2026 Add Comment
Naibu Katibu Mkuu (Taaluma) Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dkt. Mwanakhamis Ameir (kulia) na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha (kushoto) wakisaini mkataba maalum kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya elimu visiwani Unguja na Pemba.

WAMILIKI WA VISIMA TANGA WAPEWA SIKU 7, WATAKIWA KULIPIA LESENI AU KUCHUKULIWA HATUA

April 23, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga,TANGA

MKURUGENZI wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani Segule Segule amewataka wamiliki  wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kauli hiyo ameitoa baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.

Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.

Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.

Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.

Wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Onyo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Segule Segule, baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.

Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.

Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.

Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.

SERIKALI YAHAKIKISHA UPATIKANAJI WA MAFUTA LICHA YA CHANGAMOTO ZA KIMATAIFA

April 23, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Serikali imesema itaendelea kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa mafuta nchini licha ya changamoto za kimataifa zinazoathiri mnyororo wa usambazaji wa nishati hiyo , ikiwemo vita inayoendelea katika Ukanda wa Mashariki ya Kati.

Akizungumza bungeni jijini Dodoma wakati wa uwasilishaji wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2026/27 ,Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Deogratius Ndejembi, alisema kuwa Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa za mafuta ya petroli kwa uhakika.

“Sambamba na kuimarika kwa upatikanaji wa umeme, nchi yetu pia imeendelea kuwa na uhakika wa upatikanaji wa bidhaa za mafuta ya petroli licha ya changamoto za kimataifa zilizotokana na vita baina ya Marekani, Israel na Iran,” alisema Mhe. Ndejembi.

Alifafanua kuwa vita hiyo imesababisha athari kubwa katika usambazaji wa mafuta duniani, ikiwemo kufungwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz ambao hupitisha zaidi ya asilimia 20 ya mafuta yote duniani, pamoja na kuathiri miundombinu ya uzalishaji na uhifadhi wa mafuta.

“Hali hii imeathiri kwa kiasi kikubwa nchi za Mashariki ya Kati ambako Tanzania inaagiza takribani asilimia 59 ya mafuta yake, huku asilimia 41 ikitoka India ambayo nayo hutegemea mafuta ghafi kutoka ukanda huo huo,” aliongeza.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Ndejembi alisema Serikali imechukua hatua za haraka na za kimkakati ili kulinda usalama wa nishati nchini. Moja ya hatua hizo ni kuliwezesha Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuagiza mafuta ya kutosha kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo.

Aidha, alisema Serikali inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa soko la mafuta duniani na iko tayari kuchukua hatua zaidi kulingana na mabadiliko yatakayotokea.



Njombe Yaweka Rekodi ya Ubora katika Usimamizi wa Taka na Usafi wa Jamii

April 23, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekabidhi tuzo kwa Mkoa wa Njombe ikiwa ni Mshindi wa Jumla wa Shindano la Afya na Usafi wa Mazingira kwa Mwaka 2024.

CALL FOR STANDALONE ENVIRONMENT MINISTRY AS RUVUMA DIALOGUE SPARKS ACTION ON WATER GOVERNANCE

April 22, 2026 Add Comment

 

A multi-stakeholder dialogue on water governance in Ruvuma Region has reignited calls for the establishment of a dedicated Ministry of Environment, as stakeholders push for stronger, more coordinated action to address climate change and safeguard water resources.

TEA YAHIMIZA HALMASHAURI KUIMARISHA MIFUKO YA ELIMU KUCHOCHEA MAENDELEO YA SEKTA

April 22, 2026 Add Comment

WITO umetolewa kwa viongozi wa Serikali za Mitaa nchini kuimarisha ushirikiano na Mamlaka ya Elimu Tanzania(TEA) katika uanzishwaji na uendeshaji wa Mifuko ya Elimu ya Halmashauri ili kuongeza kasi ya maendeleo ya sekta ya elimu.

TVLA YATOA ELIMU KWA WAUZAJI WA CHANJO ZA MIFUGO KUSINI MWA TANZANIA

April 22, 2026 Add Comment
Afisa Masoko wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Bw. Fihiri Mbawala, akitoa ufafanuzi kwa Bi. Rauhya Omary, muuzaji wa duka la pembejeo za mifugo la Manispaa ya Lindi, tarehe 22 Aprili 2026, kuhusu mbinu bora za kuhakikisha mazingira ya uhifadhi wa chanjo yanazingatia viwango vinavyotakiwa ili kudumisha ubora na ufanisi wake, wakati wa ziara ya utoaji elimu ya matumizi sahihi ya chanjo zilizofanyika mikoa ya Lindi na Mtwara.

TANZANIA YAENDELEA KUWA MFANO KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UJANGILI NA BIASHARA HARAMU YA NYARA

April 22, 2026 Add Comment
Na Mwandishi wetu Itigi, Singida

Timu kutoka Uganda ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii, Wanyamapori na Malikale Bi. Doreen S. Katusiime yafanya ziara ya mafunzo Itigi.

BARRICK KUENDELEA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI KUBORESHA ELIMU WILAYANI KAHAMA

April 22, 2026 Add Comment

  

Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Naibu Meya wa Manispaa ya Kahama na Diwani wa Kata ya Mwendakulima, Shabani Mikongoti, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Naibu Meya wa Manispaa ya Kahama na Diwani wa Kata ya Mwendakulima, Shabani Mikongoti, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwendakulima, Bi. Neema Mfumya, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwendakulima, Bi. Neema Mfumya, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Agnes Julius akisoma risala kwa niaba ya wahitimu katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akigawa vyeti kwa wahitimu katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akiwa katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akigawa vyeti kwa wahitimu katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Wahitimu wakiwa katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.

***

Kampuni ya Barrick nchini yenye ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora katika mazingira salama na rafiki kwa kujifunzia.