HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
MKURUGENZI MKUU REA APOKEA TUZO YA USHINDI WA REA SABASABA 2026
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy, leo Julai 14, 2026, amepokea tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (Government Institutions Exhibitor), ambayo REA ilitwaa katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.
Tuzo hiyo imewasilishwa kwake na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya watumishi walioshiriki katika maonesho hayo.
Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mha. Saidy amewapongeza watumishi wa Wakala kwa juhudi, kujituma na ushirikiano wao ulioiwezesha REA kutwaa tuzo hiyo.
Aidha, amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na ushirikiano katika kutekeleza miradi ya REA vijijini na vitongojini, ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma za nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Mwisho
TAFITI ZINAZOFANYWA NA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA ZINA MCHANGO MKUBWA KATIKA TAIFA
Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 9,2026.
........................
TAFITI zinazofanywa na Tume ya kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), zimekuwa na mchango mkubwa katika Taifa hasa katika kuanzishwa kwa sheria mpya.
Hayo
yamebainishwa na Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya
Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi alipokuwa akizungumza na waandishi
wa habari katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba
Julai 9,2026.
‘’ Tafiti
tunazozifanya zina mchango mkubwa katika taifa kwani baadhi zimeleta sheria
na nyingine zilileta vifungu katika sheria,” alisema Chanzi.
Alisema hapo
awali maendeleo ya kidijitali yalikuwa siyo makubwa lakini yalipokuja Tume hiyo
ilifanya tafiti mwaka 2005 ambayo ilizaa sheria mbili, sheria ya miamala ya
kielektroniki na makosa ya kimtandao.
“Hatukuwa na sheria hizo hivyo baada ya utafiti tulipendekeza Serikalini na ilitunga hizo sheria na ndiyo maana tunaona watu wana udhubutu wa kutuma hela kwa njia ya kimtandao bila ya kuwa na wasiwasi wowote kwa kuwa wanajua zipo sheria,” alisema Chanzi.
Alisema
mwaka 2020 Tume hiyo ilifanya tafiti kuhusiana na ulinzi wa taarifa binafsi
kutokana na kuwa na umuhimu wake kama ambavyo zinavyolindwa katika katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.
Alisema
katika kuendana na kidijitali Tume imetekeleza wajibu wake na inaendelea na
utekelezaaji huo ambapo kwa sasa inafanya utafiti wa Akili Mnemba (AI) na hayo yote ni mapinduzi yay a kidijitali na
wao kama tume wanazifanya tafiti hizo na kuishauri Serikali iweze kuchukua
hatua zinazofaa kulingana na jamii yetu.
Chanzi
aliongeza kuwa wanaendelea kufanya tafiti na wanapozikabidhi sheria zimekuwa
zikitungwa jambo ambalo wanajivunia.
“Tafiti
tunazo zifanya siyo tu za kidijitali kwa mfano tulifanya teknolojia ya DNA
ambayo zamani ilikuwa haipo lakini Tume ilifanya tafiti na kukabidhi ripoti na
sheria ikatungwa na kwa kuwa tulikuwa na teknolojia lakini bila ya kuiwekea
sheria ya kuisimamia ingeweza kusababisha yasipatikane matokeo chanya ambayo
yangehitajika.
Chanzi
amesema misingi ambayo waliiweka kwenye ripoti zao wameweza kuiona ipo ndani ya
sheria na kuonesha jinsi gani mapendekezo wanayotoa yanavyochukuliwa na
kufanyiwa kazi.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.
TRA KUWAZAWADIA VIJANA 1020 WENYE MAWAZO BUNIFU
RAIS DKT.MWINYI AJIONEA MAFANIKIO YA TANESCO MAONESHO YA SABASABA
habari📌 Miradi mipya ya kusafirisha umeme kuimarisha upatikanaji wa umeme Zanzibar
📌 Serikali yawekeza Dola za Marekani milioni 282 kuongeza upatikanaji wa umeme na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo amejionea mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya umeme na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma kwa wananchi na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Katika ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, Mhe. Dkt. Mwinyi alipata fursa ya kujionea miradi ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme, teknolojia za matumizi bora ya umeme ikiwemo majiko sanifu yanayotumia umeme kwa ufanisi, huduma ya Luku Janja pamoja na mfumo wa Smart House unaomwezesha mtumiaji kufuatilia matumizi ya umeme kupitia simu ya mkononi.
Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa kujenga njia mpya tatu za kusafirisha umeme kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar kupitia nyaya zitakazopita chini ya bahari.
Ameeleza kuwa njia hizo zitajumuisha Dar es Salaam–Unguja, Tanga–Pemba na Kisiju–Mafia, na kwamba kukamilika kwake kutaongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na uwezo wa kuhudumia ongezeko la mahitaji ya umeme yanayotokana na ukuaji wa viwanda, sekta ya utalii, uwekezaji na shughuli nyingine za kiuchumi visiwani Zanzibar.
Bw. Twange amesema Serikali pia inaendelea kutekeleza mradi wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 282, ambapo Dola milioni 6 zimetengwa mahsusi kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).
“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea katika sekta ya umeme. Kupitia mradi huu wa Dola za Marekani milioni 282, tunaendelea kuimarisha miundombinu ya umeme, huku sehemu ya fedha hizo ikielekezwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na ZECO,” amesema Bw. Twange.
Aidha, amesema TANESCO imeendelea kuleta ubunifu wa kidijitali kupitia mfumo wa Smart House, unaomwezesha mwananchi kufuatilia matumizi ya umeme wa nyumba yake kupitia simu ya mkononi, hatua inayosaidia matumizi bora na yenye tija ya umeme.
Vilevile, Bw. Twange amesema mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme umefikia mafanikio makubwa, ambapo zaidi ya asilimia 90 ya wananchi waliopata majiko hayo wanaendelea kuyalipia kwa utaratibu wa makato kupitia ununuzi wa umeme wa LUKU, hatua inayorahisisha wananchi kumudu gharama za kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Jitihada hizo ni sehemu ya utekelezaji wa maono ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme ya uhakika na kutumia nishati safi katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, ikiwemo katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115, umeendelea kuweka msingi wa upatikanaji wa umeme wa kutosha unaowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
DG RUWASA AWAELEKEZA MAMENEJA WA MIKOA NA WILAYA KUZISHIRIKISHA CBWSOs KATIKA PROGRAMU ZOTE
habariREA YANG'ARA SABASABA 2026
🏆 *RAIS MWINYI ASHUHUDIA REA IKITWAA TUZO YA MUONESHAJI BORA WA TAASISI ZA SERIKALI*
🤝 *REA YAWASHUKURU WADAU KWA MCHANGO WAO KATIKA MAFANIKIO HAYO*
📍 Dar es Salaam
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameshuhudia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ukitwaa Tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (*Government Institutions Exhibitor*) katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.
Tuzo hiyo imepokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa REA, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya Wakala.
REA inawashukuru wadau wote waliotembelea banda lake, kujionea mafanikio na utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini, pamoja na kuendelea kuunga mkono jitihada za Wakala za kupeleka nishati ya umeme kwenye vitongoji.
Mwisho
NEEC YALETA ELIMU YA MITAJI KARIBU NA WANANCHI RUKWA
MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO SABASABA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), na kampuni zake Tanzu katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Mha.Mramba ametembelea banda hilo ili kuona huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo.
RAIS MWINYI ATEMBELEA BANDA LA NISHATI SABASABA
NishatiRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba mara baada ya kufika katika Banda la Wizara ya Nishati katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Kushoto kwa Katibu Mkuu ni Mkurugezi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO), Lazaro Twange.
MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA NISHATI SABASABA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Akiwa katika banda la Wizara, Mhandisi Mramba amepata maelezo kutoka kwa wataalam wa Wizara ya Nishati kuhusu elimu inayoendelea kutolewa kwa wananchi wanaotembelea maonesho hayo.
Elimu hiyo inahusu huduma zinazotolewa na Wizara na Taasisi zake pamoja na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya nishati, ikiwemo umeme, mafuta, gesi asilia, nishati jadidifu na nishati safi ya kupikia, sambamba na hatua zinazochukuliwa na Serikali kuboresha upatikanaji wa huduma za nishati nchini.
MHANDISI MRAMBA AVUTIWA NA KASI YA REA KUSAMBAZA UMEME KWENYE VITONGOJI
NishatiKatibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu) Mha. Felchesmi Mramba ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini pamoja na mafanikio ya usambazaji umeme kwenye vitongoji.
Mha. Mramba amesema hayo leo Julai 13, 2026 alipotembelea banda la REA kwenye Kilele cha maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)
ELIMU YA UTOAJI WA MIKOPO KWA MAKUNDI MAALUM IONGEZEKE - RABIA
Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.
Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.
“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.
.jpeg)








































.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)


