HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MHE.SALOME AZINDUA MFUMO WA KUAGIZA GESI YA KUPIKIA KIDIJITALI

June 25, 2026 Add Comment



📌*Unalenga kurahisisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi*



Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amezindua mfumo wa kidijitali wa kuagiza gesi ya kupikia uitwao Orion Gas, unaomilikiwa na kampuni ya Hygge, utakaowezesha wateja kuagiza mitungi ya gesi mtandaoni na kufikishiwa bila gharama za usafirishaji. 


Mfumo huo utaanza kutumika katika mkoa wa Dar es Salaam kama sehemu ya kurahisisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Akizungumza Juni 25, 2026 wakati akifunga Maonesho na Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia yaliyofanyika katika Ukumbi wa EACLC, Ubungo jijini Dar es Salaam, Mhe. Salome  amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka mkazo mkubwa katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024–2034 unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.


Amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta hiyo, ikiwemo kuondoa baadhi ya kodi na ushuru kwenye vifaa vya nishati safi ya kupikia ili kupunguza gharama kwa watumiaji. 

Amesema juhudi mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali pamoja na wadau zimeanza kuzaa matunda ambapo matumizi ya nishati safi ya kupikia yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 28.9 kwa sasa.

Mhe. Salome ametoa wito kwa sekta binafsi kuongeza uwekezaji katika uzalishaji na usambazaji wa teknolojia za nishati safi, taasisi za fedha kuweka mifumo rafiki ya mikopo kwa wafanyabiashara na wananchi, pamoja na vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa umma.


Ameeleza kuwa mwitikio mkubwa wa wadau wa ndani na nje ya nchi katika Maonesho na Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia unaonesha kuwa ajenda hiyo sasa imekuwa kipaumbele muhimu cha kitaifa. Amesema kongamano hilo limefanikiwa kuikutanisha Serikali, sekta binafsi na washirika wa maendeleo katika jukwaa moja la kujadili suluhisho za kuharakisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.


Katika hatua nyingine Mhe. Salome ametoa wito kwa wananchi na wadau mbalimbali kushiriki  Mbio za Kitaifa za Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Marathon) zitakazofanyika Juni 27, 2026 jijini Dar es Salaam  ili kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa ajili ya kulinda afya, mazingira na ustawi wa jamii.


SALOME MAKAMBA AFUNGA MAONYESHO YA NISHATI EXPO 2026

June 25, 2026 Add Comment

 



📌*Apongeza juhudi za REA kusambaza Nishati Safi ya kupikia vijijini*


📍Dar es Salaam


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba leo tarehe 25 Juni, 2026 amefunga rasmi Maonesho na Kongamano la Nishati Safi Expo 2026  yaliyofanyika katika ukumbi wa EACLC jijini Dar es Salaam


Akiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ameipongeza REA kwa kuendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji. 

"Naipongeza REA kwa kazi kubwa mnayoifanya katika kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na naendelea kuwahimiza wananchi kuendelea kutumia teknolojia mpya za nishati safi ili kulinda afya, mazingira na kuboresha ustawi wa jamii, " Ameongeza Mhe. Makamba. 


Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza na kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha malengo ya Taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yanafikiwa kwa manufaa ya Watanzania wote.

Aidha, Mhe. Makamba ameelezwa hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha wananchi wanahama kutoka katika matumizi ya nishati zisizo safi na zisizo salama kwenda kwenye teknolojia bora za nishati safi ya kupikia.



Vilevile, Mha wa miradi Francis Manyama amemfafanulia  kuwa kupitia maonesho hayo, REA imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na kuonesha teknolojia mbalimbali ikiwemo matumizi ya kuni mbadala, majiko banifu, majiko ya umeme na teknolojia nyingine rafiki kwa mazingira.


Alieleza kuwa washiriki mbalimbali wakiwemo baba lishe, mama lishe, washiriki kutoka asasi za kirai, na mashirika ya binafisi, walimu na wadau wengine walitembelea banda la REA na kupata elimu pamoja na kujionea teknolojia hizo zinazochochea matumizi ya nishati safi nchini.


Aidha, Mha. Manyama alimueleza Mhe. Makamba kuwa REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo usambazaji wa majiko banifu 200,000 katika mikoa 25 ya Tanzania Bara pamoja na usambazaji wa mitungi ya gesi ya LPG ya kilo sita ipatayo 3,255 kwa kila Wilaya kwa lengo la kurahisisha upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi.

Vilevile, alibainisha kuwa Wakala unatekeleza mradi wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi katika taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa siku, ambapo utekelezaji wake unafanyika kwa ushirikiano na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) pamoja na Jeshi la Magereza.


Katika hatua nyingine, alieleza kuwa REA kupitia TPDC imetekeleza mradi wa kusambaza gesi asilia ya kupikia katika kaya zilizopo mikoa ya Lindi na Pwani, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa nishati safi na salama kwa wananchi wa maeneo hayo. Pia alieleza kua Wakala kupitia STAMICO utawezesha usimikaji wa mashine ya kuzalisha mkaa mbadala katika mkoa wa Geita ili kurahisha upatikanaji endelevu wa nishati ya kupikia kwa wingi na wakati.


Mwisho

MTAKUWWA YAANZA OPERESHENI YA MALEZI BORA NA ULINZI WA WATOTO MWANZA

June 25, 2026 Add Comment


Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto Mkoa wa Mwanza (MTAKUWWA) imezindua kampeni ya “Amsha Ari” yenye lengo la kuhamasisha malezi bora, kuzuia mmomonyoko wa maadili na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani Mwanza.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika katika Soko la Milongo, Mwenyekiti Mwenza wa MTAKUWWA Mkoa wa Mwanza, Yassin Ally, amesema kampeni hiyo itatekelezwa kwa mfumo wa nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa na pango kwa pango ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Amesema baadhi ya maeneo hayo yamekuwa hatarishi kwa malezi ya watoto, hivyo kampeni hiyo imelenga kufikia makundi mbalimbali ya jamii kupitia mbinu tofauti za utoaji elimu na uhamasishaji.

Kwa upande wao, wajumbe wa MTAKUWWA Mkoa wa Mwanza ambao ni viongozi wa dini, wameitaka jamii, hususan waumini wao, kuzingatia malezi bora ya watoto na kujiepusha na vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wafanyabiashara wa Soko la Milongo lililopo Kata ya Milongo, Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, wameipongeza kampeni hiyo kwa kutoa elimu inayopinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kuhamasisha jamii kuendelea kudumisha amani nchini




 

KCMC YAPATA TIBA MIONZI: SERIKALI YAWEKEZA BILIONI 5.5 KUSOGEZA HUDUMA ZA SARATANI KARIBU NA WANANCHI

June 24, 2026 Add Comment

Na John Mapepele, WAF – Kilimanjaro

Tanzania imeandika ukurasa mpya katika mapambano dhidi ya saratani baada ya Serikali kuzindua rasmi Jengo la Tiba Mionzi katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC), hatua inayotarajiwa kuwanufaisha maelfu ya wagonjwa wa Kanda ya Kaskazini na nchi jirani.

WANANCHI WAHIMIZWA KUTUMIA LANDMAX KUEPUKA UTAPELI WA ARDHI

June 24, 2026 Add Comment

Na Hamida Ramadhan,Dodoma

MBUNGE wa Jimbo la Mbozi, Onesmo Mnkondya, amewataka wananchi na madalali wanaohusika na biashara ya ardhi kutumia huduma za Landmax Real Estate Company Limited ili kufanya uwekezaji kwa usalama na kuondokana na migogoro inayotokana na mauzo au ununuzi usio rasmi wa ardhi.

Mnkondya, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Landmax Real Estate Company Limited, amesema hayo Juni 24, 2026 jijini Dodoma wakati wa hafla ya uzinduzi wa ofisi za kampuni hiyo.

Amesema Landmax imeanzishwa kwa lengo la kuwasaidia wananchi kupata ardhi salama na makazi bora huku ikichangia kupunguza migogoro ya ardhi.

Aidha, amebainisha kuwa kampuni hiyo inatoa huduma mbalimbali ikiwemo uuzaji na ununuzi wa ardhi na mali isiyohamishika, ushauri wa uwekezaji wa ardhi, usimamizi wa mali, urasimishaji wa nyaraka za ardhi, uendelezaji wa miradi, tafiti za soko pamoja na ushirikiano katika miradi ya maendeleo.

“Tunawaalika wananchi na madalali wote wanaotaka kununua au kuuza ardhi kufika ofisini kwetu ili wapate huduma bora na salama,” amesema Mnkondya.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amezitaka Halmashauri zote za Mkoa huo kufanya kazi kwa kasi na ufanisi ili kuendana na kasi ya wawekezaji wa sekta binafsi.

Amesema ucheleweshaji wa huduma kwa wawekezaji unaweza kudhoofisha maendeleo ya uchumi wa Taifa na kuathiri mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya nchi.

“Ukiichelewesha sekta binafsi, unakuwa unadhoofisha mchango wao katika ujenzi wa Taifa ni muhimu Halmashauri na taasisi nyingine za umma kufanya kazi kwa kasi inayolingana na wawekezaji,” amesema Senyamule.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Clayton Chipando, amewataka wananchi kutumia huduma za Landmax Real Estate Company Limited ili kujiepusha na matapeli wanaojihusisha na biashara za ardhi na mali isiyohamishika.

Amesema matukio ya utapeli yamekuwa yakiongezeka kutokana na baadhi ya watu kutumia njia zisizo rasmi katika miamala ya ardhi, hivyo ni muhimu wananchi kutumia kampuni zinazotoa huduma za kitaalamu na zinazofuata taratibu za kisheria.

“Ndugu zangu kama mnavyojua matapeli siku hizi wamekuwa wengi na wajanja, hivyo ili kuwa salama tumieni kampuni ya Landmax,” amesema Baba Levo

Ameongeza kuwa" Kupitia huduma za kitaalamu zinazotolewa na kampuni hiyo, wananchi watapata uhakika wa umiliki wa ardhi na kufanya uwekezaji wao kwa kujiamini zaidi, " Amesema.








 

YOGE TO CONVENE A REGION POLICY SUMMIT ON INCLUSIVE FRESHWATER GOVERNANCE IN RUVUMA, TANZANIA

June 24, 2026 Add Comment

 

The Youth Environmental Justice and Gender Equality (YOGE), with support from IUCNs BRIDGE Women Leadership Grants, will on June 25th, 2026 convene a one‑day Region Policy Summit on Inclusive Water Governance in Ruvuma Basin, Tanzania.
WRRB YAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU KUONGEZA UFANISI WA STAKABADHI ZA GHALA

WRRB YAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU KUONGEZA UFANISI WA STAKABADHI ZA GHALA

June 24, 2026 Add Comment

Bodi ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeanza rasmi utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kuimarisha usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wake zinatatuliwa bila kurudi kwenye biashara holela ya mazao.

Akitoa taarifa baada ya kutembelea mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Morogoro na Iringa ikiwa ni utekelezaji wa maagizo hayo aliyoyatoa kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi hiyo Mei 19, 2026 jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Bw. Asangye Bangu, amesema katika ziara hiyo amekutana na viongozi wa mikoa, wilaya na Kamati za Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kujionea namna mfumo huo unavyotekelezwa kwenye zao la ufuta.

“Nimeridhishwa na namna serikali za mikoa zinavyoendelea kushirikiana na WRRB katika kuhakikisha mfumo unasimamiwa vizuri. Viongozi wote tuliokutana nao wameonesha utayari mkubwa wa kusimamia utekelezaji wa mfumo huu na kushughulikia changamoto zinazojitokeza,” amesema.

Amesema moja ya maelekezo makubwa yaliyotolewa na Waziri Mkuu ni kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika mfumo huo hazitumiki kama sababu ya kurejea katika biashara holela ya mazao, bali zitafutiwe ufumbuzi kwa wakati.

Kwa mujibu wa Bw. Bangu, changamoto zilizotajwa na Waziri Mkuu zinahusisha miundombinu ikiwamo ujenzi wa maghala, matengenezo ya barabara na uwepo wa mazingira bora ya kurahisisha usafirishaji wa mazao yanayopitia katika mfumo huo. Amesema WRRB imeweka mikakati mahsusi ya kuhakikisha ubora wa mazao unaimarishwa kwa kushirikiana na wakuu wa mikoa na wilaya ili bidhaa zote zinazopelekwa maghalani zikidhi viwango vinavyotakiwa.

“Tumewaelekeza waendesha maghala kuzingatia kikamilifu miongozo iliyotolewa na taasisi husika. Kwa sasa zao lililo sokoni ni ufuta na tayari miongozo ya utekelezaji imetolewa na COPRA,” amesema.

Kuhusu upungufu wa maghala, Bw. Bangu amesema tayari WRRB imeanza mazungumzo na halmashauri mbalimbali ili kuona namna ya kutumia fursa ya uwekezaji katika miundombinu ya maghala ambayo itaongeza ufanisi wa mfumo huo na kuwafikisha wakulima karibu zaidi na minada.

Kadhalika, amesema WRRB kwa kushirikiana na COPRA pia imeanza kuangalia uwezekano wa kuongeza mazao mengine kwenye mfumo ikiwamo karanga, njugu mawe na choroko ili kuongeza idadi ya wanufaika.

Akizungumzia changamoto ya mdororo wa bei, Bangu amesema wananchi wamekuwa wakilinganisha bei za sasa na zile za miaka mitatu iliyopita bila kuzingatia mabadiliko ya soko la dunia, hivyo WRRB imeendelea kutoa elimu kuhusu mwenendo wa bei katika masoko ya kimataifa.

Pia amesema baadhi ya maeneo yamekumbwa na upungufu wa uzalishaji kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na ukosefu wa mbegu bora, na kwamba WRRB imeanza mazungumzo na Jeshi la Magereza ili kutumia mashamba yake kuongeza uzalishaji wa mbegu.

“Niwahakikishie wananchi kuwa mfumo huu ni imara na tunaendelea kutatua changamoto zote zinazojitokeza. Tukishirikiana na wadau wote, tutamkomboa mkulima wa Tanzania na kuhakikisha anapata thamani halisi ya mazao yake,” alisema.

RC MTANDA AIAGIZA KWIMBA DC KUTUMIA MAPATO YA NDANI KWA MIRADI YA KIMKAKATI

June 24, 2026 Add Comment



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kwa kufikia malengo kwenye ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha miaka minne mfululizo ambapo amewataka kutumia mapato hayo kujenga miradi mikubwa ya kimkakati.


Ametoa agizo hilo leo tarehe 24 juni, 2026 wakati akihutubia Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na Maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) 2024/25 ambapo wamepata hati safi.

Mhe. Mtanda amesema ni wakati sasa kwa halmashauri kuwekeza kwenye miradi mikubwa ambayo italeta makusanyo makubwa zaidi na kuongeza wigo wa ukusanyaji mapato badala ya kujenga miradi mingi midogo pekee ambayo kimsingi haitumiki kurejesha fedha.

"Tumieni asilimia 40 ya makusanyo yenu kwa mujibu wa sheria kufanya hata mradi mmoja mkubwa ambao utakuwa alama kama wa uwanja wa mpira ambao mtajihakikishia ukusanyaji wa mapato kwa siku za mbeleni na sio kubaki na miradi midogo tu." Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka halmashauri hiyo kumaliza tatizo la maji kwenye hospitali ya wilaya ndani ya siku 14 kwa kuhakikisha wanaongeza wigo wa usambazaji kutoka kwenye chanzo cha kisima kirefu cha mita 24 kilichojengwa na wahisani Doris Mollel Foundation ili yafike katika majengo yote ya kutolea huduma.

Naye, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mkoa wa Mwanza Ndugu Richson Ringo amesema katika ukaguzi wa hesabu za mwaka 2024/25 halmashauri ya wilaya ya Kwimba imepata hati safi na kwamba mwenendo huo ni wa miaka mitano mfululizo.

Ameongeza kuwa pamoja na halmashauri hiyo kupata hati safi za ukaguzi kwa miaka 3 mfululizo lakini wanapaswa kuifanyia kazi hoja moja ya muda mrefu, pamoja na kujibu hoja na mapendekezo 36 yaliyo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kama ambavyo wamezijibu hoja 35 kati ya 79 zilizoibuliwa.




 

VICTORY ATTORNEYS & CONSULTANTS AND EXODUS INVESTMENT FIRM LAUNCH TANZANIA'S FIRST INTEGRATED PRIVATE WEALTH DESK FOR HIGH-NET-WORTH INDIVIDUALS

June 24, 2026 Add Comment

   

Benedict Ishabakaki, Executive Partner at Victory Attorneys & Consultants (right), and Ramadhan Kagwandi, CEO of Exodus Advisory, sign a partnership agreement for the operationalization of the first integrated private wealth desk in Dar es Salaam.
***

Dar es Salaam, Tanzania 

Victory Attorneys & Consultants and Exodus Investment Firm have formally announced the establishment of the Private Wealth Management Desk, a joint advisory platform designed to deliver integrated investment, legal, tax and legacy structuring services exclusively to high-net-worth individuals and families in Tanzania and across the region.

KAMPUNI ZA ALGERIA ZATAFUTA WABIA WA BIASHARA NA UWEKEZAJI TANZANIA

June 24, 2026 Add Comment

     


Balozi Mobhare Matinyi akimwonesha Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Géant Electronics, Abdelkrim Mebarkia, vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji nchini Tanzania kwenye banda la Tanzania katika Maonesho ya 57 ya Biashara ya Kimataifa ya Algiers (FIA) yanayoendelea nchini Algeria.
Balozi Mobhare Matinyi akipata maelezo ya kitaalam kuhusu uzalishaji wa nyasi bandia zinazotambuliwa na FIFA kutoka kwa Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa kampuni ya Tapidor ya Algeria, Yahia Ballalou (kulia). Kushoto ni Bounouare Adel, Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa wa Tapidor.
Balozi Mobhare Matinyi akizungumza na washiriki wa taasisi za Serikali ya Tanzania, Robert Mtendawema (kushoto) ambaye ni Meneja wa Tehama na Takwimu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Gilbert Lyimo (wa pili kulia) ambaye ni Kaimu Mhasibu Mkuu wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) na Omary Mafita (kulia), Afisa Hesabu Mkuu wa WRRB.
 Wageni mbalimbali wakitembelea banda kuu la nchi washiriki kwenye Maonesho ya 57 ya Biashara ya Kimataifa ya Algiers (FIA) yanayoendelea nchini Algeria.

***

Algeria, Algiers

Kampuni za Algeria zinazojishughulisha na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zikiwemo za viwandani na kilimo zinatafuta wabia wa kufanya nazo biashara ya mazao na uwekezaji katika sekta ya viwanda nchini Tanzania.

BARRICK YAWEZESHA KONGAMANO LA AIESEC ZANZIBAR

June 24, 2026 Add Comment

          

Mkuu wa wilaya ya Kati Zanzibar Rajab Ali Rajab akiongea katika kongamano hilo
Afisa Rasilimali Watu Mwandamizi wa Barrick Pius Kitunda akiongea na Wanafunzi na washiriki katika kongamano hilo.
Mkuu wa wilaya ya Kati Zanzibar Rajab Ali Rajab akibadilisha mawazo na Afisa Raslimali Watu Mwandamizi wa Barrick Pius Kitunda wakati wa kongamano hilo
Wageni meza kuu
  Wanafunzi kutoka vyuo vya elimu ya juu Zanzibar wameipongeza kampuni ya Barrick nchini na wadau mbalimbali kwa kudhamini kongamano la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu ili ya kuwajengea uwezo wa kujiamini na kutambua fursa mbalimbali za kimaisha.
FCC YAONGEZA UHAMASISHAJI KUELEKEA SIKU YA UDHIBITI WA BIDHAA BANDIA

FCC YAONGEZA UHAMASISHAJI KUELEKEA SIKU YA UDHIBITI WA BIDHAA BANDIA

June 24, 2026 Add Comment

Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) imeendelea kuimarisha kampeni ya utoaji elimu kwa umma kuhusu madhara ya biashara ya bidhaa bandia, ikisisitiza kuwa utengenezaji, usambazaji na uuzaji wa bidhaa hizo ni kosa la jinai linaloadhibiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Akizungumza leo Juni 22, 2026, katika eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa FCC, Bi. Roberta Feruzi, amesema bidhaa bandia zina athari kubwa kwa uchumi, afya na usalama wa wananchi, huku zikidhoofisha ushindani wa haki katika biashara.

Amesema watu watakaobainika kujihusisha na biashara ya bidhaa bandia wanaweza kukabiliwa na adhabu ya kifungo cha kati ya miaka minne hadi 15 jela pamoja na faini inayofikia kati ya Shilingi milioni 10 na milioni 50, kulingana na masharti ya sheria husika.

Bi. Feruzi ameeleza kuwa FCC inaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za ndani na kimataifa katika kudhibiti bidhaa bandia ili kuhakikisha haziingii nchini, hazisambazwi katika soko la ndani, wala kutumiwa kama njia ya kupitishwa kwenda mataifa mengine kupitia mifumo ya usafirishaji.

Amebainisha kuwa nafasi ya Tanzania kama lango muhimu la biashara na usafirishaji katika ukanda wa Afrika Mashariki inaifanya nchi kuwa miongoni mwa maeneo yanayoweza kutumiwa na wahalifu kusafirisha bidhaa bandia, hali inayohitaji ushirikiano wa karibu kati ya serikali, sekta binafsi na wananchi katika kupambana na tatizo hilo.

Kwa mujibu wa Bi. Feruzi, biashara ya bidhaa bandia si changamoto ya Tanzania pekee, bali ni tatizo la kimataifa linalosababishwa na watu wasio waaminifu wanaotafuta faida kwa kutumia kazi, ubunifu na alama za biashara za wengine kinyume cha sheria.

Ametoa wito kwa wananchi na wafanyabiashara kuwa makini wanaponunua au kuuza bidhaa, huku akiwahimiza kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapobaini uwepo wa bidhaa zinazohisiwa kuwa bandia.

Vilevile, amesema Tanzania itaadhimisha Siku ya Kitaifa ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Juni 25, 2026, yakiwa na  kauli mbiu isemayo: "Linda Maisha na Masoko Dhidi ya Pombe, Vilainishi na Sigara Bandia" ambapo maadhimisho hayo yatatumika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu athari za bidhaa bandia na kuimarisha juhudi za kitaifa na kimataifa za kupambana na biashara hiyo haramu.

Amesisitiza kuwa mafanikio ya vita dhidi ya bidhaa bandia yanategemea ushirikiano wa wadau wote, ikiwemo Serikali, wafanyabiashara , wazalishaji na wananchi, ili kulinda uchumi wa taifa, afya za watumiaji na mazingira ya biashara yenye ushindani wa haki.