HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

KAPINGA: DHANA YA TAKA SIFURI INAFUNGUA FURSA ZA BIASHARA NA VIWANDA.

KAPINGA: DHANA YA TAKA SIFURI INAFUNGUA FURSA ZA BIASHARA NA VIWANDA.

June 06, 2026 Add Comment

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amesema dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa ni fursa muhimu ya kukuza sekta ya viwanda, kuongeza thamani ya malighafi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza katika kikao cha mawaziri kilichofanyika jijini Istanbul nchini Uturuki, Juni 5, 2026, kilichobeba mada ya Mageuzi ya Kijani ya Viwanda: Mtazamo wa taka sifuri na urejeshaji bidhaa, Kapinga amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta ya viwanda huku ikisisitiza matumizi bora ya rasilimali na uhifadhi wa mazingira. Ameeleza kuwa dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa inatoa fursa kwa nchi zinazoendelea kupitia matumizi endelevu ya malighafi, kupunguza upotevu baada ya mavuno, kupunguza uzalishaji wa taka na kuongeza thamani ya bidhaa zinazotengenezwa viwandani. Kapinga amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kuunganisha masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika sera na mipango ya maendeleo ya viwanda kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ufanisi wa nishati na teknolojia rafiki kwa mazingira. Aidha, amesisitiza kuwa mafanikio ya mageuzi ya kijani yanategemea uwekezaji wa kutosha, upatikanaji wa teknolojia za kisasa pamoja na ushirikiano madhubuti kati ya serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo. Amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kuendeleza viwanda vinavyoongeza thamani ya rasilimali, kudhibiti taka na kuvutia uwekezaji huku akiwakaribisha wafanyabiashara kuwekeza nchini kwa lengo la kujenga uchumi imara na shindani.

Mkutano huo umeandaliwa na Serikali ya Uturuki kupitia taasisi ya Zero Waste Foundation inayosimamiwa na Mwenza wa Rais wa Uturuki Bibi Emine ErdoÄŸan na umeleta pamoja washiriki zaidi ya 3,000 kutoka nchi zote duniani, pamoja na taasisi za kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Umoja wa Mataifa, Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu na Shirika la Maendeleo na Biashara la Umoja wa Mataifa (UNCTAD).

LONDO – TBS NDIYO NGUZO KUU YA KULINDA AFYA ZA WALAJI.

LONDO – TBS NDIYO NGUZO KUU YA KULINDA AFYA ZA WALAJI.

June 06, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb) amelitaja Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa ni nguzo kuu ya kulinda afya za walaji na kuchochea ustawi wa viwanda nchini.

Amebainisha hayo Katika hafla maalum ya maadhimisho ya Miaka 50 ya Shirika hilo pamoja na Utoaji wa Tuzo kwa watumishi wa sasa na wastaafu kwa kutambua mchango wao uliojenga misingi imara ya udhibiti wa ubora Juni 6,2026, Jijini Dar es Salam.

Mhe. Londo Mhe.Londo amebainisha kuwa Kutokana na kukua kwa kasi kwa uwekezaji katika sekta za viwanda, kilimo, madini, na nishati, kuna uhitaji wa uwepo wa mifumo thabiti ya uhakiki wa ubora ili kulinda soko la ndani hivyo Kupitia huduma zake za upimaji na utoaji wa alama za ubora, TBS imekuwa chachu ya kukuza viwanda vya ndani na kuongeza imani ya walaji, jambo linaloiwezesha Tanzania kunufaika kikamilifu na fursa za masoko makubwa ikiwemo Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA).

Aidha alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kukuza uchumi kupitia maboresho ya miundombinu ya usafirishaji, nishati, na mifumo ya kidijitali na ameeleza kuwa maboresho ya sera na sheria yanalenga kuvutia uwekezaji na kuimarisha sekta binafsi, huku akiiasa TBS kuhakikisha kuwa ongezeko la uzalishaji nchini linaenda sambamba na uzingatiaji wa viwango vinavyotambulika duniani.

Akiangazia mustakabali wa miaka 50 ijayo, Mhe. Londo alieleza kuwa dunia inabadilika kwa kasi kiteknolojia na kiushindani, hivyo kuna mahitaji makubwa ya kuwa na TBS ya kisasa inayoendeshwa kwa maarifa hivyo Shirika hilo limetakiwa kuwekeza kwenye maabara zenye vifaa vya kisasa zaidi, kuongeza wataalamu wenye ujuzi wa hali ya juu, na kuimarisha mifumo ya kidijitali yenye ufanisi ili kuendana na kasi ya maendeleo ya sayansi na ubunifu duniani.

Mkakati huo wa kuimarisha mifumo ya viwango unaelezwa kuwa msingi imara wa kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye uchumi wa kisasa, jumuishi, na unaotegemea uzalishaji wenye thamani kubwa. Mhe. Londo aliongeza kuwa kusimamiwa vyema kwa usalama na ubora wa bidhaa kutasababisha bidhaa na huduma za Kitanzania kukubalika kwa urahisi katika soko la kimataifa na kikanda.

Vile vile Naibu Waziri alitoa rai kwa sekta binafsi, wazalishaji, na wafanyabiashara kuendelea kushirikiana kwa karibu na TBS ili kujenga utamaduni endelevu wa uzingatiaji viwango na uzalishaji wenye tija.

SERIKALI YATAMBUA UBUNIFU WA WALIMU KWA TUZO NA VIWANJA

June 06, 2026 Add Comment

-Walimu 35 walioshinda tuzo za ufundishaji kupatiwa viwanja
UADILIFU NA UWAZI VYATAJWA KUWA NGUZO ZA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

UADILIFU NA UWAZI VYATAJWA KUWA NGUZO ZA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

June 06, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu ametoa onyo kali kwa watu wanaojihusisha na udanganyifu na uchakachuaji wa taarifa katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kusisitiza itaendelea kuchukua hatua ili kuhakikisha misingi ya uadilifu na uwazi inazingatiwa ipasavyo.

Bangu,ametoa onyo hilo baada ya kufanya kikao kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro, kilichohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na viongozi na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Amesema mfumo huo unaendelea kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya uadilifu na uwazi, huku WRRB ikiendelea kushirikiana na mamlaka za mikoa, wilaya na halmashauri kusimamia utekelezaji wake.

“Moja ambalo nataka kuliweka wazi kwa Watanzania ni kwamba mfumo huu unafanya kazi kwa kuzingatia uadilifu. Kuna maeneo mengi mfumo unafanya vizuri, lakini tumeanza kuona baadhi ya watu wakiingiza taarifa zisizo sahihi kwenye mfumo kwa lengo la kujipatia fedha. Nataka nitoe onyo kali kwao kwamba tunasimamia mfumo huu kwa karibu na hatua stahiki zitachukuliwa,” amesema Bangu.

Ameeleza kuwa WRRB imeweka utaratibu wa kufanya uhakiki wa bidhaa zilizopo maghalani kabla ya kutolewa kwa katalogi za mauzo ili kuhakikisha wanunuzi wanapata taarifa sahihi kuhusu kiasi cha mazao yaliyopo.

Bangu pia amewahamasisha wakulima wa ufuta kuendelea kuuza mazao yao kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kupata masoko yenye ushindani na kuongeza kipato chao.

Amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha mazingira ya biashara ya mazao kupitia mfumo huo, jambo linalowezesha wakulima kunufaika zaidi na jasho lao.

“Wilaya ya Malinyi imeonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mfumo huu. Miaka michache iliyopita kulikuwa na changamoto, lakini sasa tumeridhishwa na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha wakulima wananufaika na mapato yao yanaongezeka,” amesema.

Katika hatua nyingine, WRRB imekabidhi msaada wa vifaa vya usafi na vyakula kwa Hospitali ya Wilaya ya Malinyi ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za uwajibikaji kwa jamii.

Akikabidhi msaada huo katika Wodi ya Wazazi ya hospitali hiyo, Bangu amesema WRRB itaendelea kushirikiana na jamii sambamba na kutekeleza majukumu yake ya kusimamia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala nchini.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Dk. Julius Nyasongo, aliyepokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Wakili Sebastian Waryuba, ameishukuru WRRB kwa msaada huo akisema utasaidia kuboresha ustawi wa akina mama wanaopata huduma hospitalini hapo.

“Msaada huu utakuwa na mchango mkubwa kwa akina mama wanaopata huduma katika hospitali yetu. Tunawashukuru WRRB kwa kuendelea kushirikiana na sekta ya afya na jamii kwa ujumla,” amesema Dk. Nyasongo.

     

MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA TANESCO CHAMWINO

June 06, 2026 Add Comment




Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu. Wazo Mwang’onda ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa jengo la utawala la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma leo Juni 06, 2026.


Ujenzi wa jengo hilo utagharimu kiasi cha Sh Milioni 326 ambapo mpaka sasa tayari kiasi cha Sh Milioni 228 kimeshatumika.

Akizungumza mara baada ya kukagua na kuzindua ujenzi wa mradi huo, Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge, Ndugu Mwang'onda ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kupitia Wizara ya Nishati kwa namna inavyoendelea kuboresha na kusogeza huduma za umeme kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Chamwino ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema ujenzi wa mradi wa jengo hilo ni muendelezo wa utekelezaji wa ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya umeme.

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutaboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wa TANESCO na kuongeza ufanisi wa huduma na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi lakini kuhamasisha wananchi kutumia nishati safi.

Mwenge wa Uhuru umekagua na kuzindua miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya Sh Bilioni 3 kwenye Wilaya hiyo.



RAIS DKT. SAMIA ATANGAZA UTALII ALIPANIA SOKO LA URUSI

June 06, 2026 Add Comment


Na Beda Msimbe,TBN, Petersburg, Urusi

Ushirikiano wa miaka 65 ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi sasa unatafsiriwa kuwa daraja imara la maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku sekta ya utalii ikichukua mwelekeo mpya wa kimkakati kuvutia masoko ya kimataifa likiwemo la Urusi. 

Alisema anatambua soko la Urusi ni kubwa naTanzania ipo tayari kulihudumia kwa kuondoa vikwazo kadhaa ikiwamo kuwezesha kupatikana kwa safari za moja kwa moja kutoka Moscow hadi Dar es Salaam na Zanzibar.

Rais alisema hayo wakati akihutubia wawakilishi kutoka nchi 130 duniani zilizoshiriki mkutano wa kiuchumi wa kimkataifa wa Petersburg Juni 5, 2026.

Katika jukwaa hilo la kiuchumi, Rais  Samia  alitangaza kuwa kuanzia Julai 2 mwaka huu, Shirika la Ndege la Tanzania, Air Tanzania, litaanza safari za moja kwa moja kati ya Dar es Salaam, Moscow, na Zanzibar kwa lengo la kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia laki tano ifikapo mwaka 2030 na hatimaye milioni moja. 

Hatua hii inaenda sambamba na ushindi wa tuzo za kimataifa ambapo hifadhi ya Serengeti imetajwa kuwa bora zaidi Afrika na Zanzibar kupewa tuzo kama eneo bora la mikutano na mapumziko. 

Rais Samia alihitimisha kwa kutoa rai kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa na nchi za Afrika ziko tayari kukua kupitia mifumo yao kama soko huru la Afrika, akisisitiza kuwa Tanzania imefungua milango yote kwa wabunifu na wafanyabiashara wanaotaka kushiriki katika safari hii mpya ya mabadiliko.


mwisho

TANZANIA IKO TAYARI KWA BIASHARA, UWEKEZAJI NA UBUNIFU

June 06, 2026 Add Comment

 


Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg, Urusi

Katika hotuba ya kihistoria iliyotolewa kwenye Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg nchini Urusi, Rais wa Tanzania amewahakikishia viongozi wa dunia na wawekezaji wa kimataifa kuwa nchi hiyo iko tayari kwa biashara, uwekezaji mkubwa, na ubunifu wa kisasa ili kuendana na ushindani wa soko la kimataifa. 

Rais Samia akihutubia Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la Saint PeterburgTanzania imefanya mageuzi makubwa ya kisheria na kitaasisi ikiwemo kuanzisha kituo kimoja cha huduma ambapo usajili wa kampuni sasa huchukua hadi saa 24 tu.

Alisema hatua hiyo imechangia kupaa kwa uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje hadi kufikia dola bilioni 12 mwaka 2025 ikilinganishwa na dola bilioni 3 tu za mwaka 2021.

 Ili kuchochea ukuaji huu wa viwanda na biashara, aliwaambia washiriki wa jukwaa hilo kutoka nchi takribani 130 kwamba serikali imeweka msisitizo mkubwa katika usindikaji wa madini ya mkakati ndani ya nchi kama vile dhahabu, neli, graphite, na helium badala ya kusafirisha malighafi ghafi.



Aidha alifunguka kuhusu viwanda vya mbolea na kusema kwamba uwekezaji kwenye viwanda vya mbolea kwa kushirikiana na Urusi na kuendeleza miradi mikubwa kama Eneo Maalum la Kiuchumi la Bagamoyo na Bandari ya Kimataifa ya Mangapwani kule Zanzibar.

Akizungumzia ujenzi wa uchumi wa kisasa unaoendeshwa na teknolojia na miundombinu madhubuti Rais Samia amesema bado inatafuta washirika katika hilo kwani ni nguzo kuu inayoiweka Tanzania katika nafasi ya kipekee ya kiushindani kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 inayolenga kufikia uchumi wa kipato cha kati cha juu wa dola za Marekani trilioni moja.

Akizungumza katika moja ya hotuba zake iliyojaa msisimko katika jukwaa hilo, Rais Samia alibainisha kuwapo kwa mapinduzi makubwa ya miundombinu ikiwemo mtandao wa reli ya kisasa ya SGR inayounganisha Bandari ya Dar es Salaam na nchi jirani, pamoja na mipango ya upanuzi wa reli hadi Musoma na Ukanda wa Kusini kuelekea Malawi na Msumbiji.

Katika upande wa ubunifu na mawasiliano, alisema Tanzania inakaribisha wawekezaji kwani imekuwa nchi iko vizuri katika mwasiliano ikiwa imefikia asilimia 95 ya upatikanaji wa broadband na inapanua mkongo wa taifa wa mawasiliano ili kuwa kitovu cha kidijiti kwa nchi saba zisizo na bahari.                                                                                 Aidha, akizunguzma mustakabali wa nishati, Rais Samia alitangaza mpango wa taifa wa nishati ya nyuklia kwa matumizi ya amani kupitia teknolojia ya vinu vidogo kwa kushirikiana na kampuni ya Rostam ili kukidhi mahitaji ya megawati 80,000 ifikapo mwaka 2030, jambo linalothibitisha utayari wa Tanzania kuongoza mabadiliko ya kiuchumi Afrika.

TBS NDIYO NGUZO KUU YA KULINDA AFYA ZA WALAJI- LONDO

June 06, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb) amelitaja Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa ni nguzo kuu ya kulinda afya za walaji na kuchochea ustawi wa viwanda nchini.

RAIS PUTIN AIKUBALI TANZANIA AELEZA JINSI ILIVYO MUHIMU

June 06, 2026 Add Comment

 


 Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg


Rais Vladimir Putin wa Urusi amesema Tanzania ni lango kuu la kimkakati linalounganisha soko la Afrika Mashariki na masoko ya kimataifa.

Aidha amesema katika uchumi wa dunia unaozidi kubadilika kuelekea mifumo ya nguzo nyingi za kiuchumi, taifa la Tanzania umuhimu mkubwa katika kuyfanikisha ustawi wa jamii mbalimbalio.

Akizungumza Juni 5 katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg la mwaka 2026 Rais Putin amesema kuwa Tanzania katika utendaji ni taifa la kimkakati katika ukanda wa Afrika Mashariki unaofanana na ule wa nchi ya Uzbekistan katika ukanda wa Asia ya Kati ikifanya kazi kama kiungo muhimu sana kati ya uchumi wa kikanda na vituo vikuu vya biashara ya kimataifa duniani.

Kiongozi huyo amebainisha hayo wakati akizungumzia mataifa ambayo kutokana na nafasi zao za kijiografia na mahusiano yao ya kiuchumi yanageuka kuwa madaraja muhimu kati ya kanda tofauti duniani na kuongeza kuwa mataifa yenye uwezo wa kuoanisha maendeleo yao ya ndani na miunganisho madhubuti kwenye vituo vipya vya ukuaji wa uchumi wa kimataifa yanazidi kuwa muhimu wakati mifumo ya biashara ya kimataifa inavyoendelea kubadilika.

Kauli hizi nzito kutoka kwa Rais Putin zinakuja wakati ambao Tanzania inaendelea kupanua kwa kasi miundombinu yake ya usafirishaji ikiwemo bandari na njia za biashara za kikanda ili kuimarisha nafasi yake kama kitovu kikuu cha biashara kwa ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati na hivyo kutafsiri kwa vitendo malengo makubwa ya ukuaji wa kiuchumi.

Rais Samia Suluhu Hassana alishiriki katika jukwaa hilo amnbapo alipata nafasi ya kuelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na uwekezaji na pia biashara.

Aidha alisema kwamba Tanzania ipo tayari kushirikiana na mataifa yoyote ikiwamo Russia ili kupeleka fursa mbalimbali za maendeleo kwa wananchi wake. Akijibu swali kwamba Russia ina vikwazo, Rais Samia alisema Tanzania haina vikwazo inafanyakazi na washirika wote wanaoitakia mema nchi yake.


SERIKALI YATAKA USHAURI WA WANAFUNZI UHAMIE KIDIJITALI

June 06, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga,TANGA


SERIKALI imekipongeza Chama cha Washauri wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TACOGA) kwa kuendelea kuandaa mafunzo yanayolenga kuimarisha uwezo wa kitaaluma na kiutendaji wa washauri wa wanafunzi, wanasihi na viongozi wa serikali za wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali nchini.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Tanga,Mkurugezi wa Maendeleo ya Jinsia kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Badru Abdnur alisema mafunzo hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kuwajengea washiriki uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili wanafunzi katika taasisi za elimu ya juu.

Alisema katika kipindi cha mafunzo hayo, washiriki walipata nafasi ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao, pamoja na kupata mbinu mpya zitakazowawezesha kuboresha huduma wanazozitoa kwa wanafunzi.

"Nawapongeza viongozi wa TACOGA kwa ubunifu na maono yao ya kuhakikisha mafunzo haya yanafanyika kila mwaka. Bila uongozi imara, kuandaa mafunzo ya aina hii si jambo rahisi," alisema.

Aliongeza kuwa hatua hiyo inaonesha utambuzi wa umuhimu wa maendeleo endelevu ya kitaaluma kwa watendaji wanaohusika na huduma za wanafunzi pamoja na viongozi wa serikali za wanafunzi.

Badru alibainisha kuwa mada zilizowasilishwa zimegusa maeneo nyeti yanayoathiri ustawi na maendeleo ya wanafunzi, ikiwemo afya ya akili, maadili, matumizi ya teknolojia na uongozi bora.

Alisema dunia ya sasa inabadilika kwa kasi kutokana na maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia, hali inayowafanya vijana kuwa miongoni mwa makundi yanayoathirika zaidi na mabadiliko hayo.

"Vijana wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo afya ya akili, matumizi mabaya ya teknolojia, matumizi ya dawa za kulevya na mmomonyoko wa maadili. Hivyo, kuna haja ya kuendelea kuwajengea uwezo na kuwapa mwongozo sahihi ili wawe raia wema na wazalendo," alisema.

Aidha, aliwakumbusha washiriki kuwa serikali na jamii kwa ujumla zinategemea sana mchango wa washauri na wanasihi katika kuwajenga wanafunzi. 

Alisema wazazi na walezi wana matumaini makubwa kwa maafisa hao kwa kuwa vijana wengi wanaojiunga na vyuo vikuu bado wana umri mdogo na wanahitaji mwongozo, uangalizi na malezi ya karibu.

Kwa mujibu wake, kutokana na nafasi hiyo muhimu, TACOGA ina wajibu mkubwa wa kuchangia mageuzi ya maendeleo ya taifa kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Alitoa wito kwa chama hicho kuwekeza zaidi katika mifumo ya kiteknolojia ili kuendana na mazingira ya sasa ya kidijitali. Alisema ni muhimu kuanzisha mifumo ya kimtandao na programu za simu zitakazowezesha wanafunzi kupata huduma za ushauri kwa haraka na kwa urahisi bila kuathiri muda wao wa masomo.

Pia aliwataka kuendelea kujenga uwezo wa wanachama wao kupitia mafunzo endelevu ya saikolojia, unasihi na mbinu mpya za utoaji wa huduma ili kuwawezesha washauri na wanasihi kutoa suluhisho stahiki na la kisasa kwa changamoto zinazowakabili wanafunzi.

Vilevile, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha viashiria vya kupima matokeo ya kazi zinazofanywa na TACOGA kwa kuwekeza katika tafiti ndogo ndogo za kutathmini kama huduma zinazotolewa zinaleta matokeo chanya katika ufaulu wa wanafunzi na maendeleo yao ya kijamii na kitaaluma.

Mgeni rasmi huyo pia alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya ofisi za washauri wa wanafunzi na madawati ya jinsia pamoja na vitengo vya kuzuia ukatili wa kijinsia katika vyuo vikuu. Alisema kuna muunganiko mkubwa wa majukumu kati ya taasisi hizo, hivyo ushirikiano ukiimarishwa utasaidia kupunguza mzigo wa kazi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wanafunzi.

Alisema maarifa na stadi zilizopatikana kupitia mafunzo hayo zinatarajiwa kuwafanya washiriki kuwa mabalozi wa mabadiliko katika taasisi zao na kuchangia kufikiwa kwa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TACOGA, Sophia Nchimbi, alisema chama hicho kimeendelea kuandaa mafunzo hayo kwa lengo la kuwawezesha maafisa wa ofisi za washauri wa wanafunzi katika vyuo vikuu kutekeleza majukumu yao kwa weledi zaidi.

Alisema washiriki walipata mafunzo yaliyohusu nidhamu chanya, usimamizi wa tabia, unasihi, matumizi salama ya mitandao ya kijamii, afya ya akili, malezi ya wanafunzi, uongozi bora na usimamizi wa madawati ya jinsia katika vyuo vikuu.

"Mafunzo haya yanatusaidia kupata ufumbuzi wa changamoto mbalimbali tunazokutana nazo katika maeneo yetu ya kazi. Maarifa tunayopata yanatupa uwezo wa kuwahudumia wanafunzi kwa ufanisi zaidi," alisema Nchimbi.

Alisema mada kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii zimewawezesha washiriki kuelewa namna bora ya kuwaelekeza wanafunzi kutumia teknolojia kwa manufaa ya elimu badala ya matumizi yasiyofaa.

Nchimbi alisema pia washiriki walipata elimu kuhusu namna ya kusimamia madawati ya jinsia ili kuhakikisha wanafunzi wanaokumbana na changamoto mbalimbali wanapata msaada kwa wakati na kwa usahihi.

Aliongeza kuwa TACOGA imekuwa ikifanikiwa kuendesha mafunzo hayo kutokana na ushirikiano mkubwa wa wanachama na wadau mbalimbali wanaochangia maendeleo ya huduma za ushauri kwa wanafunzi.

Jumla ya washiriki 94 kutoka vyuo mbalimbali nchini walishiriki mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Tanga.






NEMC YAMTUZA JACKLINE KWA UFAFANUZI BORA WA UCHUMI MZUNGUKO

June 06, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limemtambua mwanafunzi wa Darasa la Sita, Jackline Eliabi wa Shule ya Msingi Manyinga, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, kwa uwasilishaji wake bora wa dhana ya Uchumi Mzunguko katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.
TPDC YAKABIDHI KARAKANA YA KISASA YA CNG KWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

TPDC YAKABIDHI KARAKANA YA KISASA YA CNG KWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

June 06, 2026 Add Comment





Dar es Salaam, Juni 5, 2026

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekabidhi rasmi Karakana ya kuongeza mfumo wa matumizi ya gesi asilia Iliyoshindiliwa kwenye vyombo vya usafiri (CNG Conversion Workshop) kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hatua inayotarajiwa kuimarisha matumizi ya nishati safi nchini pamoja na kukuza ujuzi wa kitaalamu katika teknolojia ya gesi asilia.

Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam, ambapo TPDC iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Uwekezaji, Bw.Derick Moshi, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC. Kwa upande wa UDSM, karakana hiyo ilipokelewa na Naibu Mkuu wa Chuo Prof. Bernadeta Kilian.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Bw. Derick Moshi alisema kuwa ujenzi wa karakana hiyo ni sehemu ya jitihada za TPDC katika kuunga mkono mkakati wa Serikali wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi na nafuu kwa wananchi.

“Kukamilika na kukabidhiwa kwa karakana hii ni hatua muhimu katika kukuza matumizi ya gesi asilia Iliyoshindiliwa (CNG) nchini. Mbali na kutoa huduma za kuongeza mifumo ya CNG kwenye magari, karakana hii itatumika kujenga wataalamu wazalendo kupitia mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa uhandisi wa UDSM,” alisema Bw. Moshi.

Aliongeza kuwa mradi huo umegharimu shilingi bilioni 1.52 za Kitanzania na ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano kati ya TPDC na UDSM yaliyowekwa kupitia Mkataba wa Upangishwaji Ardhi uliosainiwa mwaka 2022.

Kwa mujibu wa Bw. Moshi, karakana hiyo ina vifaa vya kisasa vinavyowezesha ufungaji wa mifumo ya CNG kwenye vyombo vya usafiri, ukaguzi wa usalama wa mifumo hiyo pamoja na matengenezo yake, hatua itakayochangia kupunguza gharama za matumizi ya nishati kwa watumiaji wa magari nchini.

Kwa upande wake, Prof. Bernadeta Kilian aliishukuru TPDC kwa kutekeleza ahadi yake ya kujenga na kukabidhi karakana hiyo, akieleza kuwa miundombinu hiyo itakuwa kichocheo muhimu katika maendeleo ya elimu, utafiti na ubunifu wa teknolojia za nishati nchini.

“Kupokea karakana hii ni hatua kubwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Miundombinu hii itawapa wanafunzi wetu nafasi ya kupata mafunzo ya vitendo yanayokidhi mahitaji ya soko la ajira na wakati huo huo kusaidia maendeleo ya sekta ya nishati nchini,” alisema Prof. Kilian

Alisisitiza kuwa UDSM itaendelea kushirikiana na TPDC katika tafiti, ubunifu na maendeleo ya teknolojia zinazochangia matumizi bora ya rasilimali za gesi asilia kwa manufaa ya Taifa.

Karakana hiyo imejengwa ndani ya eneo la Kituo Mama cha kujaza gesi asilia (CNG Mother Station) kilichopo UDSM na inatarajiwa kuwa kituo muhimu cha utoaji huduma za CNG pamoja na mafunzo ya kitaalamu kwa wanafunzi na wadau wa sekta ya usafiri.

Kupitia uwekezaji huo, TPDC inaendelea kutekeleza dhamira ya Serikali ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi, salama na nafuu, sambamba na kuongeza ushiriki wa taasisi za elimu ya juu katika maendeleo ya sekta ya nishati nchini.