
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho ametembelea banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katika Banda la Wizara amepata maelezo kuhusu Sera ya Nishati ya Mwaka 2015 pamoja na mikakati mingine inayosimamiwa na Wizara ya Nishati ukiwemo Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Mkakati wa Matumizi Bora ya Nishati na Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia.



HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
WAZIRI NDEJEMBI AJADILI AWAMU YA PILI YA MRADI WA UMEME WA JUA KISHAPU NA WASHIRIKA WA MAENDELEO.
habari
Na Mwandishi Wetu - Paris, Ufaransa
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi kutoka Wizara ya Fedha ya Ufaransa, Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) pamoja na kampuni ya SAGECOM, kwa lengo la kujadili utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa Uzalishaji Umeme wa Jua wa Megawati 100 unaotekelezwa katika Wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga.
Mazungumzo hayo yamefanyika leo, Julai 6, 2026, katika Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Paris, Ufaransa.

Katika kikao hicho, Mhe. Ndejembi ameishukuru Serikali ya Ufaransa kupitia Wizara yake ya Fedha na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu wa Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya nishati. Amesema ushirikiano huo umeendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha upatikanaji wa nishati ya uhakika na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa AFD, Bi. Sandra Kassab, ameipongeza Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati kwa hatua kubwa iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi ya nishati, hususan ile inayolenga kuongeza uzalishaji wa umeme na kuimarisha matumizi ya nishati safi. Aidha, ameahidi kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ufanisi na kuleta manufaa kwa wananchi wa Tanzania.



“WOMEN TAKING OVER” YA BARRICK YAWATIA MOYO WANAWAKE KUTOBAKI NYUMA SEKTA YA MADINI
habari

KIGOGO WA CHADEMA TANGA RASHID JUMBE ATANGAZA KUMALIZA SAFARI YA MIAKA 30 UPINZANI,AHAMIA CCM
siasa>Asema kasi ya maendeleo chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amani, uchumi, afya, maji na miundombinu vimemshawishi kubadili msimamo wa kisiasa.
Na Oscar Assenga,TANGA
Baada ya zaidi ya miaka 30 ya kuwa mwanasiasa wa upinzani, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Tanga, Rashid Jumbe, amefanya uamuzi mkubwa wa kisiasa kwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Jumbe, ambaye kwa muda mrefu alikuwa mmoja wa viongozi mashuhuri wa Chadema mkoani Tanga, amesema uamuzi wake umetokana na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na juhudi za Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha amani, umoja na ustawi wa wananchi.
Akizungumza wakati wa hafla ya kumpokea ndani ya CCM iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, Jumbe alisema hakufanya uamuzi huo kwa papara, bali baada ya kutafakari kwa kina na kujiridhisha kuhusu mwelekeo wa maendeleo ya taifa.
"Nilikuwa mpinzani kwa zaidi ya miaka 30, lakini leo nimeamua kuhitimisha safari hiyo. Kilichonishawishi zaidi ni kazi kubwa inayofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea Watanzania maendeleo na kuhakikisha amani ya nchi inalindwa," alisema.
Alieleza kuwa pia amevutiwa na utekelezaji wa falsafa ya 4R inayosisitiza maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya, akisema imeongeza mshikamano na kuimarisha mazingira ya maendeleo nchini.
Akizungumzia Mkoa wa Tanga, Jumbe alisema mabadiliko yanayoonekana katika sekta mbalimbali ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya kuufungua mkoa huo kiuchumi.
Alitaja kuongezeka kwa shughuli katika Bandari ya Tanga, ujenzi wa bandari kavu pamoja na utekelezaji wa miradi mingine ya kimkakati kuwa miongoni mwa hatua zilizochochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za biashara.
"Nimekuwa nikipaza sauti kwa miaka mingi nikitaka Tanga ifunguliwe kiuchumi. Leo naona hilo limefanyika. Mizigo imeongezeka bandarini, bandari kavu zimejengwa na shughuli za biashara zinaendelea kukua," alisema.
Katika sekta ya afya, Jumbe alisema maboresho yaliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na ujenzi wa zahanati katika kata na mitaa mbalimbali vimempa imani kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma kwa wananchi.
Aidha, alisema upanuzi wa huduma za maji na umeme pamoja na utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni miongoni mwa hatua zinazoonyesha dhamira ya Serikali ya kuinua maisha ya Watanzania.
"Nilijiuliza ni hoja gani itanifanya nibaki upinzani wakati maendeleo yanaonekana wazi. Tanga ina amani, huduma zinaimarika na wananchi wanaendelea kunufaika na miradi ya maendeleo," alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, alisema chama hicho kinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano ili kuongeza uwezo wake wa kusimamia maendeleo na kuwatumikia wananchi.
Alisema tangu alipopewa dhamana ya kuongoza CCM mkoani humo, ameweka mkakati wa kuimarisha chama kupitia ushirikiano na wanachama pamoja na kuwakaribisha viongozi kutoka vyama vingine vya siasa.
Rajab alisema mkakati huo umeendelea kuzaa matunda, akieleza kuwa kujiunga kwa Rashid Jumbe ni ishara ya kuongezeka kwa imani ya baadhi ya viongozi wa upinzani kwa juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali.
"Jumbe alikuwa mmoja wa viongozi wakubwa wa upinzani katika Wilaya ya Tanga. Tuliahidi kwamba tutamshawishi aje kushirikiana nasi katika kujenga chama na kuwaletea wananchi maendeleo, na leo tumefanikiwa," alisema.
NHIF TANGA YATOA ELIMU YA BIMA NA KUFANYA UPIMAJI WA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA KANISA LA KKKT USHIRIKA WA MAKORORA TANGA
afyaNa Oscar Assenga,TANGA
Wazazi, walezi na waajiri nchini wamehimizwa kuhakikisha watoto wanawakatia bima ya afya mapema ili kuwaepusha na changamoto za gharama kubwa za matibabu na kuwawezesha kupata huduma za afya kwa wakati wanapougua.
Wito huo umetolewa leo na Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Tanga, Macrina Clemens, wakati wa utoaji wa elimu kuhusu bima ya afya ulioambatana na zoezi la upimaji wa afya na usajili wa wanachama wa vifurushi mbalimbali katika Kanisa la KKKT Ushirika wa Makorora, jijini Tanga.
Akizungumza na waumini wa kanisa hilo, Macrina alisema afya ni mtaji muhimu kwa maendeleo ya familia na Taifa, hivyo kujiunga na bima ya afya ni uwekezaji unaowalinda wananchi dhidi ya gharama zisizotarajiwa za matibabu.
Alisema wazazi wanaowakatia watoto wao bima ya afya hupata uhakika wa matibabu wakati wowote mtoto anapougua, jambo linalowapa utulivu wa akili na kuwawezesha watoto kuendelea na masomo bila kukatishwa na changamoto za kifedha.
“Mzazi anapokuwa na bima ya afya kwa mtoto wake anakuwa na uhakika wa kupata matibabu kwa wakati, hivyo kuepuka usumbufu wa kutafuta fedha za dharura kila ugonjwa unapojitokeza,” alisema.
Macrina alisema wanafunzi wanaosoma katika shule mbalimbali wanaweza kujiunga na bima ya afya kupitia shule zao kwa gharama ya Sh50,400 kwa mwaka mzima wa masomo, huku watoto ambao bado hawajaanza shule wakijiunga kupitia vifurushi mbalimbali vinavyotolewa na NHIF.
Alisema Serikali inaendelea kutekeleza azma ya kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa na bima ya afya, hivyo akazitaka taasisi za elimu, wazazi, walezi, waajiri na wamiliki wa kampuni binafsi kutumia fursa hiyo kuwaandikisha watoto na wafanyakazi wao.
“Bima ya afya si gharama, ni kinga ya maisha. Ukiwa na bima unakuwa na uhakika wa kupata daktari, dawa na huduma za matibabu bila kubeba mzigo mkubwa wa kifedha pale unapougua,” alisema.
NHIF imeendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya wananchi kuhusu umuhimu wa bima ya afya ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuongeza idadi ya Watanzania wanaonufaika na huduma hiyo na kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini.
BODI YA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI MIRADI YA REA
📌*Watembelea Banda la REA kwenye maonesho ya Sabasaba*
📌*Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa miradi ya nishati safi Vijijini*
Leo tarehe 5 Julai, 2026 kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) wametembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika maonesho yanayoendelea ndani ya Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katika banda hilo, wajumbe wa REB wameelezwa kuhusu utekelezaji wa miradi ya usambazaji umeme kwenye maeneo ya vitongoji na uwezeshaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inayoendelea nchini.
*Karibu Sabasaba, karibu Banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)*
PROF. KABUDI AHAMASISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU SABASABA
habariWAZIRI SANGU AKUTANA NA MZEE WA UPAKO NA MTUME MALISA
habariDKT. MUNISI: TAASISI ZA DINI NI WADAU MUHIMU KATIKA MAENDELEO YA TAIFA
habariTRA YAWEKA REKODI MPYA YA MAKUSANYO, YAKUSANYA SH. TRILIONI 37.96 KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026
habari
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeweka rekodi mpya katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya jumla ya Shilingi trilioni 37.96 katika mwaka wa fedha 2025/26, sawa na asilimia 105.24 ya lengo la kukusanya Shilingi trilioni 36.07.SERIKALI KUTEKELEZA MRADI WA UMEME JUA KATIKA VISIWA SABA MUSOMA
habari
Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga shilingi milioni 273.6 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme wa jua katika visiwa saba vya Wilaya ya Musoma ikiwemo Nyasaungu, Muroba, Kagongo, Nyamasanje, Rukuba na Iriga, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Rais, Mhe. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma ya umeme bila kujali eneo analoishi.
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ya kutatua kero za wananchi katika Jimbo la Musoma Vijijini.
Amesema Serikali imepiga hatua kubwa katika upatikanaji wa umeme ambapo vijiji vyote katika jimbo hilo tayari vimefikiwa na huduma hiyo, huku hatua zinazofuata zikielekezwa katika kufikisha umeme kwenye vitongoji vilivyosalia.
Amebainisha kuwa kati ya vitongoji 374 vilivyopo, takribani 100 pekee ndivyo bado havijafikiwa na umeme huku zaidi ya vitongoji 50 vikiwa katika hatua za utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme.
Aidha, amesema Serikali imepokea maombi ya Mbunge wa Musoma Vijijini ya kuhakikisha vitongoji vyote ambavyo havina umeme vinafikiwa na huduma hiyo ifikapo mwaka 2027, akieleza kuwa lengo hilo linaendana na dhamira ya Serikali inayolenga kuhakikisha vitongoji vyote nchini vinaunganishwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.
Sambamba na hilo, Mhe. Salome amesema Wizara ya Nishati imeendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo ya uzalishaji mali, ikiwemo maeneo ya wachimbaji wa migodi wilayani Musoma Vijijini.
Kuhusu baadhi ya wananchi ambao miundombinu ya umeme imepita karibu na makazi yao lakini hawajaunganishwa na huduma hiyo, amemuelekeza Meneja wa TANESCO Wilaya ya Musoma kuhakikisha wananchi hao wanaunganishiwa umeme.
Katika hatua nyingine, amewahimiza wananchi wa Musoma Vijijini kutumia nishati safi ya kupikia, akibainisha kuwa Serikali imetoa ruzuku ya zaidi ya asilimia 50 kwenye majiko ya gesi ili kuyawezesha kupatikana kwa gharama nafuu.











.jpg)
.jpg)






















