HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI AWESO ATOA MAAGIZO KWA RUWASA PANGANI

June 21, 2026 Add Comment
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang'onda (wa pili kushoto) akizungumza kwenye mradi wa maji wa Mikocheni/Mkwaja. Kushoto kwake ni Waziri wa Maji, Mhe Jumaa Aweso na kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Mhe Ayubu Sebabili


Na Mwandishi Wetu, PANGANI


WAZIRI wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, ameagizi Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, kuunganisha mtandao wa majisafi na salama kwenye makazi ya watu katika kijiji cha Mkwaja.


Mhe. Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Pangani, ameyasema hayo leo Juni 20, 2026 kijijini hapo, alipokaribishwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa upanuzi mtandao wa maji kutoka ‘mradi mama’ uliopo kijiji cha Mikocheni.
Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Raiyan Mohamed Rashid, akimtishwa ndoo ya maji mmoja wa wakazi wa kijiji cha Mkwaja wilayani Pangani,  Mkoa wa Tanga kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji uliofika kijijini hapo kutokea kijiji jirani cha Mikocheni.



Mwenge wa Uhuru wenye kauli mbiu inayosema, “Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo” ulifika kwenye mradi huo wa kwanza baada ya kuingia katika Halmashauri ya Pangani kutokea Handeni.


Mhe. Aweso amesema, kwa vile Mwenge umechagiza maendeleo wilayani humo kwa vipindi tofauti, ipo haja ya kuendeleza hali hiyo kwa kuingiza maji kwenye makazi ya watu, badala ya kuishia kwenye vituo 12 vya kuchotea maji (DPs) vilivyopo Mkwaja.


Amesema, usambazaji majisafi na salama ni utekelezaji wa ahadi za Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kumtua ndo mama kichwani.


Kwa mujibu wa Mhe. Aweso, kati ya vijiji 12,333 vilivyopo nchini, 10,758 vimefikiwa na huduma ya majisafi na salama wakati 1,575 vitafikiwa ifikapo 2030.


Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Pangani, Mhandisi Rajab Hussein, amesema upanuzi wa mradi wa Mikocheni ni matokeo ya upatikanaji maji kwa wastani wa lita 480,000 kwa siku, wakati mahitaji ya Mikocheni pekee ni lita 40,000.


Kwa mujibu wa Mhandisi Hussein, mahitaji yaliyobainika kwa matumizi katika kijiji cha Mkwaja ni lita 65,000 kwa siku na kufanya jumla yake kuwa lita 105, hivyo kuwa na lita 375,000 za ziada.

Ni picha ya uzinduzi wa mradi wa maji.

Amesema kupitia upanuzi wa mradi huo, RUWASA imejenga tenki lenye uwezo wa kuchukua lita 90,000 na kuwekwa kwenye mnara wa urefu wa mita sita, hivyo kuwa na uwezo wa kusambaza maji kijijini Mkwaji kupitia DPs zilizopo.


Naye Mwang’onda amesema agizo la Mhe. Aweso kwa RUWASA kuunganisha mtandao wa maji kwenye makazi ya watu ni kuuheshimisha Mwenge na kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mwang’onda amesema historia imeandikwa kwa Mhe. Rais Dkt Samia kuboresha huduma za kijamii ikiwemo upatikanaji majisafi na salama sehemu kubwa ya nchi.


Kwa hali, Mwang’onda, amehimiza wananchi kuwekeza zaidi katika amani, umoja na mshikamano, ili kufikia maono ya Mhe. Rais Dkt Samia kuwa na maendeleo endelevu.


MWISHO.





WANANCHI WAHOJI UHAKIKI MFUMO WA VIPIMO VYA DATA: “TUNACHOLIPIA HAKITOSHI”

June 21, 2026 Add Comment


Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA


Wakazi wa Jiji la Dodoma wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuingilia kati na kusimamia ipasavyo matumizi sahihi ya vipimo vya vifurushi vya intaneti “bando” pamoja na muda wa maongezi wakidai kupoteza data zao kwa haraka na bila uwazi.

Wananchi hao wametoa wito wa kuwepo kwa uwazi na ukomo sahihi wa muda wa matumizi ya data, wakisema ni haki yao kupata kile wanacholipia.

Baadhi ya wakazi waliozungumza jijini hapa wameeleza kusikitishwa na namna megabytes (MBs) au gigabytes (GBs) wanazonunua zinavyoisha kwa muda mfupi hata pale wanapokuwa hawatumii simu zao kikamilifu, jambo linaloashiria kasoro kwenye usahihi wa vipimo hivyo

Meneja wa Wakala wa vipimo mkoa wa Dodoma Said Ibrahim, anasema wakala umepokea maoni hayo ya wadau na kuongeza kuwa umeshaanza mchakato wa kusimamia uhakiki ikiwemo katika vifurushi vya intaneti (Bando) na muda wa maongezi.




“ZERO MALARIA” YA BARRICK YAFIKIA KAYA ELFU 44 MSALALA

June 21, 2026 Add Comment

 

Afisa Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa vyeti kwa washiriki wa zoezi la upuliziaji dawa majumbani kwenye mazalia ya mbu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa “Zero Malaria” unaolenga kuimarisha juhudi za kutokomeza ugonjwa wa malaria katika jamii zinazozunguka mgodi huo.

Mratibu wa Wadudu Wadhulifu ngazi ya Wilaya, Jullieth Petro, akimwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa vyeti kwa washiriki wa zoezi la upuliziaji dawa majumbani kwenye mazalia ya mbu, yaliyoandaliwa katika kutekeleza mradi wa “Zero Malaria” unaofadhiliwa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu.
Mkurugenzi wa Gekahil, Bw. Gerald Elias, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa vyeti kwa washiriki wa zoezi la upuliziaji dawa majumbani kwenye mazalia ya mbu, yaliyoandaliwa katika utekelezaji wa mradi wa “Zero Malaria” unaofadhiliwa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa lengo la kuimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria katika jamii.

*HAKUNA MASIKA YASIYOKUWA NA KIANGAZI*

June 20, 2026 Add Comment


Usemi usemao hakuna marefu yasiyokuwa na ncha umetimia leo ambapo jumla ya maafisa na Askari 29 kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) wamehitimu mafunzo ya mabadiliko ya kimuundo leo tarehe 20 Juni, 2026 katika Kituo cha Mafunzo ya Jeshi la Uhifadhi kilichopo Mlele mkoani Katavi.

Akifunga mafunzo hayo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TAWA Meja Jenerali (Mstaafu) Hamis Semfuko amewataka wahitimu kuzingatia taratibu na sheria na amri zote za Jeshi la Uhifadhi

“Mmepata mafunzo ya kubadilika kimuundo kutoka raia kuwa Jeshi, matumaini yangu ni kuwa kila mmoja wetu hapa mtabadilika na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa katika kusimamia uhifadhi na rasilimali za nchi”,alisema Meja Jenerali (Mst) Semfuko.

Mkuu wa wilaya ya Mlele Mhe. Majid Mwanga amewapongeza wahitimu hao na kuwataka kuwa mfano mwema wa uzalendo, maadili na ujasiri katika utendaji kazi.

Kwa upande wake Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Abdul-Razaq Badru amewahimiza wahitimu hao kutumia mafunzo waliyoyapata kuimarisha uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.

Kaimu Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) Mlage Kabange amesema ushirikiano uliooneshwa kati ya TAWA na Ngorongoro katika kusimamia mafunzo hayo unaonesha kuimarika kwa Jeshi la Uhifadhi nchini na ari ya kusimamia rasilimali za Wanyamapori na Misitu.

Akitoa taarifa kuhusu mafunzo hayo mkuu wa mafunzo Meja Breyman Rulenguka amesema Jumla wa watumishi 29 wamefaulu na kupata alama za kuridhisha ambapo mwanafunzi mmoja pekee hakuweza kuhitimu kutokana na sababu za kiafya.

Mafunzo hayo ni mwendelezo wa mafunzo yanayotolewa katika kituo hicho kwa lengo la kuimarisha Jeshi la Uhifadhi na utendaji kazi wake.




.

WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI-

June 20, 2026 Add Comment

 WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI -MD TWANGE



📌Asema TANESCO inajenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima


📌Aeleza mpango wa kusambaza majiko sanifu ya umeme  takribani Mil 1


📌Awapongeza Wafanyakazi kwa ubunifu na jitihada za kuwahudumia wateja kwa ufanisi.


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amewaondoa hofu wananchi kuhusu matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, akisema kuwa TANESCO imejipanga kujenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima.


Mkurugenzi huyo amesema hayo Juni 19, 2026, alipotembelea banda la TANESCO katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali, mkoani Dodoma.


Amesema shirika linatambua kuwa mahitaji ya umeme yanaendelea kuongezeka kutokana na kukua kwa shughuli za kiuchumi, hivyo jitihada zinaendelea kufanyika kuhakikisha umeme unawafikia wananchi kwa ubora na uhakika kwa matumizi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.

“TANESCO inafanya kazi kubwa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Aidha, sasa tunashuhudia matumizi ya umeme katika vyombo vya usafiri. Sisi kama wazalishaji wa umeme tunaonesha njia kwa kuwa tuna vyombo vingi vya usafiri vinavyotumia umeme. Tumejipanga kujenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima,” alifafanua Bw. Twange.


Bw. Twange pia amefafanua kuhusu mpango wa ukopeshaji wa majiko sanifu ya umeme kwa wananchi, unaowawezesha kulipa kidogo kidogo kupitia manunuzi ya Luku. Amesema kuwa, kwa kushirikiana na wadau , takribani majiko milioni 1 yatasambazwa katika kipindi cha miaka miwili hadi mitatu.



“Tunatumia mbinu mbalimbali kuwaelimisha wananchi na kuwaondoa hofu kuhusu matumizi ya  umeme  kupikia. Tunawakopesha majiko ya umeme  na wanalipa kidogo kidogo kupitia mfumo wa manunuzi ya Luku. Wadau kutoka sekta binafsi wametuunga mkono, na tunatarajia kusambaza majiko karibu milioni 1 katika kipindi cha miaka miwili hadi mitatu,” aliongeza Bw. Twange.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala, Bi. Beatrice Kimoleta, Licha ya kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji kwa kutembelea Banda la TANESCO  kujionea namna wananchi wanavyohudumiwa, amesema Shirika linajivunia watendaji  wenye dhamira ya kuwahudumia wananchi kwa ubunifu na weledi mkubwa.


“Tunaomba wateja wetu muendelee kutuamini, Tunafahamu kuwa umeme ni huduma muhimu kwa kila Mtanzania, hivyo tunaendelea kuongeza jitihada za kutoa huduma bora, ya uhakika na yenye ufanisi zaidi, tunaimani na watumishi wetu katika kuhakikisha wananchi wananufaika na nishati ya umeme katika fursa mbalimbali ,” alisisitiza Bi. Kimoleta.


Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Kitaifa kwa mwaka 2026 yanaendelea kufanyika katika Viwanja vya Chinangali, mkoani Dodoma, na yanatarajiwa kuhitimishwa rasmi  Juni 23, 2026.

WAZIRI KAPINGA AIPONGEZA TBS KWA KUIWEKA TANZANIA KWENYE RAMANI YA UBORA

WAZIRI KAPINGA AIPONGEZA TBS KWA KUIWEKA TANZANIA KWENYE RAMANI YA UBORA

June 20, 2026 Add Comment

Na.Alex Sonna-DODOMA

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limepongezwa kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitakiwa kuendelea kwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia na mabadiliko ya soko la dunia ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kimataifa.

Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga,wakati wa maadhimisho ya kilele cha miaka 50 ya shirika hilo yaliyofanyika katika ofisi zake zilizopo Njedengwa jijini Dodoma, sambamba na uzinduzi wa kitabu kinachoelezea historia, mafanikio na mchango wa taasisi hiyo katika kukuza ubora wa bidhaa na huduma nchini.

Waziri Kapinga amesema TBS imekuwa nguzo muhimu katika kulinda afya na usalama wa wananchi kupitia usimamizi wa viwango vya bidhaa mbalimbali, huku ikichangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa sekta za uzalishaji, biashara na viwanda nchini.

Ameeleza kuwa katika kipindi hiki ambacho dunia inaendelea kubadilika kwa kasi kupitia teknolojia na ubunifu, TBS inapaswa kuwa na dhana ya kujitegemea zaidi kwa kuimarisha mifumo ya kisasa ya utoaji huduma na kuongeza uwezo wake wa kitaalamu ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

"Tunapoadhimisha miaka 50 ya TBS, tunashuhudia mchango mkubwa wa taasisi hii katika kujenga imani ya bidhaa za Tanzania. Hata hivyo, ni muhimu kuendelea kuwekeza katika teknolojia, ubunifu na ushirikiano na sekta binafsi ili kuhakikisha bidhaa zetu zinakidhi viwango vya kimataifa," amesema Kapinga.

Aidha, Waziri huyo amesisitiza umuhimu wa TBS kuendelea kufanya kazi kwa karibu na sekta binafsi ili kuongeza ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini na kusaidia kutafsiri kwa vitendo maono ya Tanzania ya kuwa taifa lenye uchumi wa viwanda unaozalisha bidhaa zenye ushindani mkubwa katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,amesema  maadhimisho hayo  ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyofikiwa na kuweka mikakati mipya ya kuifanya taasisi hiyo kuwa ya kisasa zaidi na yenye uwezo mkubwa wa kukabiliana na changamoto za karne ya 21.

Dkt. Katunzi amesema TBS itaendelea kuimarisha maabara za kisasa, kuongeza matumizi ya teknolojia za kidijitali na kuwekeza katika rasilimali watu ili kuhakikisha huduma za viwango zinakuwa bora zaidi, za haraka na zenye kuaminika.

"TBS inatambua kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa, huku teknolojia na mazingira ya biashara vikibadilika, hivyo shirika hilo linapaswa kuendelea kuwa imara, bunifu na lenye uwezo wa kujibu changamoto mpya zinazoibuka."aamesema Dkt. Katunzi

Amebainisha kuwa kwa kipindi cha nusu karne, TBS imekuwa mhimili muhimu wa maendeleo ya viwanda na biashara nchini kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa na kuuzwa zinazingatia viwango vinavyotakiwa, jambo ambalo limeongeza imani ya walaji na kufungua fursa za biashara katika masoko mbalimbali duniani.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mariam Ditopile Mzuzuri, amesema TBS imekuwa mhimili muhimu katika kulinda maslahi ya walaji, kuimarisha ushindani wa bidhaa za Tanzania na kuchochea ukuaji wa sekta za uzalishaji nchini.

 Ditopile amesema ipo haja ya kufanyika kwa mapitio ya kina ya Sera ya Ubora wa Bidhaa ili iweze kuakisi mabadiliko makubwa yaliyotokea katika nyanja za sayansi, teknolojia, biashara na uzalishaji tangu sera hiyo ilipoanzishwa.

"Tunapoipongeza TBS kwa mafanikio ya miaka 50, ni muhimu pia kuangalia mbele na kufanya maboresho yatakayoiwezesha taasisi hii kuendelea kuwa nguzo ya maendeleo ya viwanda, biashara na kilimo katika mazingira ya sasa ya kiteknolojia," amesema Ditopile.

Ditopile amesema imejijengea rekodi ya kuwa taasisi muhimu katika kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa, kuuzwa na kutumiwa nchini zinakidhi viwango vinavyotakiwa kwa ajili ya kulinda afya, usalama na maslahi ya watumiaji.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Viwango Afrika (ARSO), Dkt. Hermogene Nsengimana, amesema Julai 2026 Tanzania itakuwa nchi ya saba barani Afrika kupata Alama ya Ubora ya Afrika (Africa Quality Mark) kwenye bidhaa zake.

Amesema kwa hatua hiyo, Tanzania itaungana na Rwanda, Togo, Senegal, Ethiopia, Nigeria na Zimbabwe katika nchi zinazotumia alama hiyo ya ubora inayolenga kuimarisha viwango vya bidhaa barani Afrika.

Amesema Shirikisho la Viwango Afrika limekwisharatibu na kuoanisha takribani viwango 2,600 vinavyolenga sekta za kipaumbele ikiwemo usindikaji wa mazao ya kilimo, sekta ya magari, dawa na bidhaa za afya, usafirishaji na ugavi, pamoja na nguo na bidhaa za ngozi.

Ameeleza kuwa kwa sasa takribani bidhaa 500 katika ngazi ya Afrika zinapitiwa ili kupata Alama ya Ubora ya Afrika, hatua itakayosaidia kurahisisha biashara ndani ya Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA).

Amesema bidhaa za Tanzania ambazo kwa sasa zinabeba alama ya TBS, zitapata fursa ya kuwekewa alama ya ubora ya Afrika, jambo litakaloongeza ushindani na upatikanaji wa masoko katika nchi mbalimbali za bara hilo.