HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts

WAFANYABIASHARA KARIAKOO WAPO TAYARI KWA MFUMO WA IDRAS
habari
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi,akizungumza wakati wa mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo.
Na.Mwandishi Wetu- KARIAKOO
Wafanyabiashara wameukubali mfumo wa Usimamizi wa Kodi za ndani (IDRAS) ,huku wakijiandaa kuupokea Jumatatu ya tarehe 9 Februari mwaka huu.
Akizungumza leo 6.2.2026 jijini Dar es salaam katika mafunzo ya mfumo mpya kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo (JWK) Bw. Severin Mushi amesema wapo tayari kuanza kuutumia mfumo huo kwa ushirikiano wa karibu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Mwenyekiti huyo amesema kupitia mafunzo ambayo wamepatiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanaamini mfumo utakuwa msaada kwao na kuondoa changamoto mbalimbali ambazo zilikuwepo.
Amesema mafunzo hayo yamekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara kwa kuwa yameondoa hofu iliyokuwepo awali na kuwapa uelewa wa pamoja kuhusu matumizi ya mfumo huo.
Bw. Mushi amesema wamejiandaa kuupokea mfumo wa IDRAS, akieleza kuwa jambo lolote jipya huwa linaogopesha kwa wanaolipokea.
Amebainisha kuwa mabadiliko ya kiteknolojia hayaepukiki katika dunia ya sasa, hivyo wafanyabiashara wanapaswa kuendana nayo ili kuboresha ufanisi wa ulipajikodi.
Hata hivyo, Mushi ametoa rai kwa TRA kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kutatua changamoto ya mtandao katika baadhi ya maeneo ya biashara, hususani Kariakoo ili kuleta ufanisi wa matumizi mazuri ya mfumo mpya wa IDRAS kwa walipakodi.
Aidha, ametoa wito kwa wafanyabiashara wote kuwa tayari kuupokea mfumo wa IDRAS na kushirikiana na Serikali pamoja na TRA kwa karibu, akisisitiza kuwa lengo kubwa ni kuhakikisha ulipaji wa kodi unakuwa rahisi na wenye tija.
“Tumejiandaa kuupokea mfumo kuanzia Jumatatu ya tarehe 9 mwezi huu Kikubwa ni kushirikiana na Serikali kuhakikisha tunalipa kodi na mifumo ya ulipaji iwe rahisi,” amesema Bw. Mushi.
Aidha,Mwenyekiti huyo amependekeza kuwepo kwa kipindi cha mpito cha mafunzo ili kuwapa wafanyabiashara nafasi ya kuuelewa mfumo huo Zaidi na kuleta ufanisi sahihi wa utekelezaji wake.
“Angalau miezi mitatu ya mwanzo iwe ni ya mafunzo na kuwaelimisha watu namna ya kutumia mfumo, watakapokuwa wameuelewa, tutakwenda pamoja,”- Bw. Mushi.

INDIA YAELEZWA TUNDA LA MTI WA KATI LILILIWA NGORONGORO
habariIndia imefikiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kupata simulizi nzuri ya Eden inayosimuliwa kwenye vitabu vya dini inayoelezwa kwamba Adam na Eva walikula tunda la Mti wa kati.
Katika maonesho ya kimataifa ya utalii yanayofanyika India tarehe 6-7 Januari, 2026 Afisa Masoko Mkuu Michael Makombe anatoa elimu kwa washiriki kuhusu kasoko ya Ngorongoro kuwa ni Eden inayozungumzwa kwenye vitabu vya dini.
“Ngorongoro tuna amini kuwa ndiyo Eden kutokana na kuwa na vitu vyote ambavyo Mungu amevitaja katika sifa za Bustani ya Eden.
Amevitaja vitu hivyo kuwa ni mandhari ya kuvutia,wanyama na ndege, matunda ya aina zote,misitu na mimea,wadudu,maji na miamba yenye mapango yenye muundo unaomfanya binadamu aweze kuwasiliana na Mungu.
Ngorongoro yenye utajiri wa Vivutio imetambuliwa na mtandao wa World Travel Awards kama kivutio bora cha utalii kwa mwaka 2023 na 2025 vivutio ambavyo vipo sehemu moja na hivyo kudhihirisha Eden iliyotajwa kwenye vitabu vya dini

UMEME VITONGOJINI WACHOCHEA UCHAKATAJI MAZAO KATAVI
Nishati
*Wakandarasi watakiwa kuacha maneno, ahadi na michakato wamalize mradi kwa wakati
*Bilioni 57.3 kupeleka umeme vitongoji 358 mkoani Katavi
*Ajira kupewa kipaumbele
Katavi
Imeelezwa kuwa mradi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Awamu ya Pili B (HEP 2B) unakwenda kuongeza na kuchocchea uchakataji wa mazao ambayo kwa kiasi kikubwa wananchi wa mkoa wa Katavi wanazalisha mazao katika mkoa huo.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoto leo tarehe 6 Februari, 2026 mara baada ya kutambulishwa kwake mkandarasi Kampuni ya M/s ETDCO Ltd atakayetekeleza mradi wa HEP 2B wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 358 kwa wakazi zaidi ya 11,536 mkoani Katavi.
“Kwa sasa badala ya kuuza mazao ghafi tutaiza bidhaa, suala hili la kupatikana kwa umeme litakwenda kuipandisha bei za mazao kwa sababu yatachakatwa katika hali nzuri na zitauzwa bidhaa badala ya kuuza malighafi,” Amesema RC. Mrindoto.
Vilevile, ameongeza kuwa upatikanaji wa umeme wa uhakika kupitia mradi wa HEP 2B utakwenda kukuza uchumi, kukuza uwekezaji na kuleta ajira kwa vijana, wanawake, wazee na makundi mbalimbali katika mkoa huo.
“Nimsisitize mkandarasi kujipanga sawasawa uingie kazini kwa miguu yote miwili ukiwa na kasi kubwa kwa sababu wanachohitaji wananchi ni umeme wala sio maneno au ahadi, sio ratiba, sio michakato,” Amesema RC Mrindoto.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Bw. Mussa Muze amesema lengo kuu la utekelezaji wa mradi wa HEP 2B ni kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi katika vitongoji vya mkoa wa Katavi na kusaidia maendeleo jumuishi ya kijamii na kiuchumi.
Naye, Msimamizi wa Miradi ya REA mkoa wa Katavi, Mha. Gilbert Furia amesema, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa rai kwa wananchi wa mkoa wa Katavi kushiriki vema katika utekelezaji wa mradi, na kutumia fursa ya kuletewa umeme kuweza kujiinua kiuchumi.
Pia, Mkandarasi kutoka Kampuni ya M/s ETDCO Ltd, Mha. Abdalah Mitenda amemueleza RC Mrindoto kuwa katika mradi huo wakandarasi watapewa kipaumbele kufanya shughuli mbalimbali zitakazokuwa zinafanyika katika mradi huo na kuwataka kuchangamkia fursa.


SAKURA GIRLS YAINGIA KWENYE ORODHA YA TAASISI ZINAZOTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Nishati
Baada ya Ofisi ya Makamu wa Rais kutoa waraka wa katazo kwenye taasisi zote zinazolisha watu zaidi ya mia moja nchini kuachana na matumizi ya Nishati isiyo safi na kuhamia kwenye nishati safi ya kupikia, Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Sakura yaingia kwenye Orodha ya Taasisi zinazotumia Nishati Safi ya Kupikia.
Hayo yametabanaishwa Februari 05, 2026 wakati timu ya wataalam kutoka Wizara ya Nishati ilipotembelea shuleni hapo kukagua mradi wa LPG na GAS Vaporizer unaofadhiliwa na Shirika la KAGLA Eco Friendly wakishirikia na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan, JICA.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mkuu wa Shule hiyo Bw. Thomas Rubeni amesema Shule ipo milimani na eneo hili kuna baridi kali wakati wa asubuhi, jioni na msimu wa Masika ambapo hali ya hewa hiyo huathiri afya za wanafunzi hivyo uwepo wa mfumo wa gesi utasaidia wanafunzi kupata maji moto na kupunguza hewa ukaa kwani matumizi ya kuni yanachangia kwa kiasi kikubwa uwepo wa hewa ya ukaa kwenye mazingira.
Aliongeza kuwa uwepo wa nishati safi ya kupikia utawasaidia wapishi kupika kwa urahisi na kwa wakati”
Kwa upande wake Mpishi wa shule hiyo Rahel Elisante ameeleza kuwa toka wameanza kutumia ya gesi wameepukana na adha mbalimbali za kimazingira na kiafya.
“ Tunafurahi na tunashukuru kwa kupata gesi kwani mwanzo tulikuwa tunapata shida mfano wakati wa baridi na mvua kuni zinakua mbichi na kutoa moshi na kuchelewesha kuiva chakula kwa wakati ila sasa hivi tunatumia gesi ambayo inarahisisha kazi yetu ya kila siku’ Bi. Elisante.
Naye mwakilishi wa wanafunzi Lidya Lebayo wa Sakura amesema upatikanaji wa gesi utawasidiia kupata maji moto ya uhakika katika vipindi vyote wawapo shule na pia kupata chakula kitamu kisicho na harufu ya moshi.

INDIA YAELEZWA TUNDA LA MTI WA KATI LILILIWA NGORONGORO
habariIndia imefikiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kupata simulizi nzuri ya Eden inayosimuliwa kwenye vitabu vya dini inayoelezwa kwamba Adam na Eva walikula tunda la Mti wa kati.
Katika maonesho ya kimataifa ya utalii yanayofanyika India tarehe 6-7 Februari, 2026 Afisa Masoko Mkuu Michael Makombe anatoa elimu kwa washiriki kuhusu kasoko ya Ngorongoro kuwa ni Eden inayozungumzwa kwenye vitabu vya dini.
“Ngorongoro tuna amini kuwa ndiyo Eden kutokana na kuwa na vitu vyote ambavyo Mungu amevitaja katika sifa za Bustani ya Eden.
Amevitaja vitu hivyo kuwa ni mandhari ya kuvutia,wanyama na ndege, matunda ya aina zote,misitu na mimea,wadudu,maji na miamba yenye mapango yenye muundo unaomfanya binadamu aweze kuwasiliana na Mungu.
Ngorongoro yenye utajiri wa Vivutio imetambuliwa na mtandao wa World Travel Awards kama kivutio bora cha utalii kwa mwaka 2023 na 2025 vivutio ambavyo vipo sehemu moja na hivyo kudhihirisha Eden iliyotajwa kwenye vitabu vya dini



MATUMIZI MITA ZA MALIPO KABLA YASHIKA KASI TANGA
habariNa Oscar Assenga,Tanga
MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (TangaUWASA) imeendelea na zoezi maalum la kufunga mita za malipo kabla (Pre-paid Meters) katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Tanga, hatua inayolenga kuboresha ukusanyaji wa mapato na kudhibiti matumizi ya maji.
Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TangaUWASA, Mhandisi Geofrey Hilly, alipokuwa akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga katika kikao cha wadau kilichofanyika Februari 5, 2026 kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuwasilisha taarifa ya maendeleo ya upatikanaji Huduma.
Kabla ya kikao hicho, Waheshimiwa Madiwani walipata fursa ya kutembelea na kujionea maendeleo ya utekelezaji Mradi wa Hatifungani wenye thamani ya Shillingi Bilioni 53.12 unaotekelezwa katika kituo cha Kuzalisha maji Mowe na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2026.
Mhandisi Hilly alisema mradi huo umelenga kuimarisha upatikanaji wa huduma ya uhakika kwa wananchi kwa saa 24 na aliongeza kuwa hadi sasa zaidi ya mita za malipo kabla 4,500 tayari zimesambazwa na kufungwa kwa wateja na kuwa mita hizo zinamsaidia mteja kutumia kiasi cha maji kulingana na fedha aliyolipia, hivyo kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Aliongeza kuwa utekelezaji wa mradi huo una lenga kuongeza uwezo wa uzalishaji na usambazaji wa maji kutoka mita za ujazo 45,000 kwa siku zilizopo sasa hadi kufikia mita za ujazo 60,000 kutokana na uboreshaji wa miundombinu ya Mtambo, ulazaji wa mabomba makubwa yenye kipenyo cha milimita 600, upanuzi wa kituo cha kusafisha na kutibu maji cha Mowe, ujenzi wa tangi kubwa la kuhifadhi maji lenye mita za ujazo 35,000 pamoja na kuimarisha utunzaji na uhifadhi wa vyanzo vya maji.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TangaUWASA, Dk. Fungo Ali Fungo, alisema kikao hicho ni mwanzo mzuri wa ushirikiano wa karibu kati ya mamlaka na Madiwani, akisisitiza kuwa mikutano hiyo itakuwa ni utaratibu wa kawaida.
“Tutakutana mara kwa mara kwa kuwa Madiwani ni kiungo muhimu kati yetu na wananchi. Maswali mengi ya wananchi huanzia kwao, hivyo ni muhimu kuwa na majadiliano ya karibu,” alisema Dk. Fungo.
Aliongeza kuwa kikao hicho kililenga pia kuwajengea Madiwani uelewa wa kazi zinazotekelezwa na TangaUWASA ili kuwa na uelewa wa pamoja na ufahamu mzuri wa yote yanayoendelea katika kufanikisha adhma ya Serikali ya upatikanaji wa huduma ya uhakika kwa wananchi.
Nae kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Mhe. Selebosi Mustafa, aliipongeza TangaUWASA kwa kuandaa kikao kazi hicho mapema baada ya madiwani kuapishwa, akisema ni mfano mzuri wa taasisi kujenga uelewa na kuimarisha ushirikiano na viongozi wa wananchi.
Alisema lengo ni kujenga uhusiano, kuimarisha uwakilishi wa mamlaka kwa wananchi na kuwapa madiwani nafasi ya kushiriki kikamilifu katika kusimamia huduma za maji. Aidha, alishauri TangaUWASA kupanga muda wa kutosha kwa ajili ya madiwani kutembelea miradi yote ya maji na vyanzo vyake ili kujionea hali halisi ya kazi zinazotekelezwa.
Katika kikao hicho, madiwani walipata fursa ya kuuliza maswali na kutoa maoni mbalimbali yaliyojibiwa na Mhandisi Geofrey Hilly kwa kushirikiana na wataalamu wa Mamlaka hiyo.
Katika hatua nyingine, Madiwani walimpongeza Afisa Uhusiano wa TangaUWASA, Bi. Devotha Mayala, kwa utendaji kazi wake uliotukuka, wakisema amekuwa akipokea simu na kutoa msaada kwa wakati wowote.
“Kwa kweli nichukue nafasi hii kumpongeza Devotha kwa kazi kubwa anayoifanya mchana na usiku kwa kuwasikiliza wateja na kutatua changamoto zinazowasilishwa.




