HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
TADB YAIMARISHA USHIRIKIANO NA REDIO ZA KIJAMII KUKUZA KILIMO
habariSERIKALI YARIDHISHWA NA MWENENDO WA KIWANDA CHA SATURN CORPORATION
habariVyuo vikuu 9 vya Malasyia kushiriki maonesho Dar
habariUPATIKANAJI UMEME KUENDELEA KUIMARIKA MKOANI IRINGA— MHE. SALOME
habari
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Iringa.
Amesema tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aingie madarakani, Mkoa wa Iringa umepokea zaidi ya shilingi bilioni 124 kwa ajili ya kuimarisha huduma ya umeme na kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma hiyo kwa lengo la kuwawezesha kujiletea maendeleo ya kiuchumi.
Mhe. Salome ameyasema hayo leo Mei 23, 2026 wakati akijibu hoja za wananchi mkoani Iringa, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba.

Amesema changamoto za umeme zilizokuwa zikikabili baadhi ya maeneo ikiwemo Kata ya Mafifi tayari zimeshapatiwa ufumbuzi na wananchi wanaendelea kupata huduma ya umeme wa uhakika. Hata hivyo, amesema katika Mtaa wa Mosi huduma hiyo bado haijafika ipasavyo ambapo tayari maelekezo yametolewa kwa TANESCO na REA kuhakikisha wananchi wa eneo hilo wanaunganishiwa umeme kwa wakati.

Pia ameeleza kuwa Serikali imeendelea kuweka mazingira rafiki ya wananchi kuunganishiwa umeme kwa gharama nafuu ya shilingi elfu 27,000 tu, huku akielekeza kuwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya mjini lakini kiuhalisia wanaishi mazingira ya vijijini waunganishiwe umeme kwa gharama hiyo pia.
Katika kuimarisha zaidi huduma ya umeme mkoani Iringa, amesema Serikali kupitia Wizara ya Nishati inaendelea kuongeza uwezo wa Kituo cha Kupokea na Kusambaza Umeme cha Mufindi ambapo Mkoa huo utaanza kupata umeme kutoka megawati 60 hadi megawati 260.

Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kubadilisha transfoma katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji ili kuwezesha viwanda kufanya kazi muda wote na wananchi kuendelea kupata umeme wa uhakika.
Sambamba na hayo, Mhe. Salome amesisitiza umuhimu wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi wa Mkoa wa Iringa ili kulinda mazingira na kuboresha afya na maisha ya wananchi.

Amesema Serikali inaendelea kutoa ruzuku ya majiko ya gesi na majiko banifu kwa wananchi wa vijijini na kuwahamasisha kuachana na matumizi ya kuni na mkaa.
RAIS MSTAAFU DKY JAKAYA MRISHO KIKWETE AKUTANA NA MAKUNDI YA UPINZANI CHINI SUDAN KUSINI JIJINI DAR ES SALAAM
habariMikutano ya ngazi ya juu iliyohusisha makundi mbalimbali ya upinzani nchini Sudan Kusini imefanyika jijini Dar es Salaam tarehe 21 na 22 Mei, 2026 ikiwa ni sehemu ya juhudi mpya za kufufua mchakato wa amani jumuishi baada ya kusuasua kwa utekelezaji wa makubaliano ya amani ya mwaka 2018.
Mazungumzo hayo yaliongozwa na Rais wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye ni Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu.
Majukumu yake makuu yanajumuisha: Upatanishi wa Amani: Kusimamia diplomasia ya kuzuia migogoro na kuongoza mazungumzo jumuishi ili kutatua changamoto za kisiasa na kiusalama katika ukanda huo.
Ushirikiano wa Kikanda: Kufanya kazi kwa karibu na jumuiya na taasisi mbalimbali kama vile IGAD na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ili kujenga misingi thabiti ya amani na usalama.
Kwa ujumla, mikutano hiyo ilionyesha dhamira ya Umoja wa Afrika na wadau wa kikanda katika kuimarisha mazungumzo ya kisiasa na kuhakikisha mazingira ya amani na utulivu yanaimarishwa kuelekea uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu nchini Sudan Kusini.
Mikutano hiyo pia ililenga kuisaidia Umoja wa Afrika kupata picha kamili ya hali ya kisiasa na kiusalama nchini Sudan Kusini kabla ya uchaguzi uliotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huo wa 2026.
NLD YATETEA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI
siasa
>Sheria Isichague Chama
NA OSCAR ASSENGA, TANGA
Katibu Mkuu wa Chama cha NLD, Doyo
Hassan Doyo, amesema mjadala unaoendelea kuhusu hatua zinazochukuliwa na Ofisi
ya Msajili wa Vyama vya Siasa umeonyesha jinsi baadhi ya Watanzania wanavyotoa
hukumu za haraka bila kutafakari misingi ya sheria.
Doyo alisema kumekuwa na mtazamo
kwamba Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inalenga zaidi vyama vya upinzani,
huku ukweli ukiwa ni kwamba taasisi hiyo inasimamia sheria bila kuangalia
itikadi ya chama husika.
Akizungumza wakati wa ziara ya chama
hicho mkoani Tanga, alisema hatua zilizochukuliwa hivi karibuni dhidi ya baadhi
ya viongozi wa kisiasa zinatokana na matamshi yaliyotafsiriwa kuwa na viashiria
vya uvunjifu wa sheria za vyama vya siasa.
“Sheria iko wazi. Chama au kiongozi
anayekiuka taratibu anaweza kupewa adhabu ya faini, kusimamishwa shughuli au
hata kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria. Hii siyo kwa chama fulani pekee,”
alisema.
Alieleza kuwa baada ya viongozi wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoa kauli zilizozua mjadala, Ofisi ya
Msajili iliwaandikia barua ya kutaka maelezo. Hatua hiyo, kwa mujibu wa Doyo,
ilitafsiriwa vibaya na baadhi ya wananchi pamoja na wanaharakati waliodai kuwa
upinzani unaonewa.
Hata hivyo alisema hali hiyo
imebadilika baada ya mmoja wa viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) naye
kuandikiwa barua kufuatia matamshi yake ya kisiasa.
“Watu walidhani sheria inafanya kazi
kwa upande mmoja, lakini sasa imeonekana wazi kuwa anayevunja sheria ndiye
anayechukuliwa hatua, bila kujali anatoka chama gani,” alisema.
Doyo alisema vyama vya siasa
vinapaswa kutambua kuwa vimesajiliwa kwa mujibu wa sheria na hivyo vina wajibu
wa kuendesha shughuli zake ndani ya mipaka ya kisheria.
Alionya kuwa siasa zisizo na nidhamu
zinaweza kupelekea uvunjifu wa amani na kuhatarisha usalama wa Taifa.
“Ukianza kufanya siasa nje ya
sheria, maana yake unaondoka kwenye misingi ya kisiasa na kinachofuata ni
migogoro na vurugu. Taifa haliwezi kujengwa kwa misingi ya shinikizo na
vitisho,” alisema.
Aidha, aliitaka Ofisi ya Msajili wa
Vyama vya Siasa kuendelea kusimamia sheria kwa uthabiti bila kuogopa presha za
kisiasa kutoka kwa wanasiasa au wanaharakati.
Kwa mujibu wa Doyo, uwepo wa taasisi
imara zinazotekeleza sheria kwa haki ndiyo msingi wa kulinda amani na utulivu
wa nchi.
Katika ziara hiyo ya NLD iliyoanzia
Pangani na kuelekea Lushoto, chama hicho kimesema kinaendelea kutoa elimu kwa
wananchi kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria, taratibu na kanuni za kisiasa ili
kuimarisha demokrasia na mshikamano wa Taifa.
KILO 504 ZA HEROIN ZATEKETEZWA, DCEA YAIMARISHA ELIMU NA HUDUMA KWA WARAIBU
habariCHALAMILA: VIWANGO NI MSINGI WA AFYA, BIASHARA NA UCHUMI IMARA
habariTUME YA MADINI YAANZA KUTUMIA MFUMO WA IDRAS KUONGEZA UFANISI, MAPATO
habariZIARA KWA VITENDO ZAWANOA WADAU WA MAZIWA MBEYA
habariSERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUBORESHA MASLAHI YA WATUMISHI WA UMMA
habari.jpeg)
.jpeg)
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, leo ameshiriki ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 13 wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) uliofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Ngurdoto, mkoani Arusha.
Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, na umewakutanisha zaidi ya wanachama 5,050 wa TAPSEA kutoka Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, taasisi mbalimbali za umma pamoja na wajumbe kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.
Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi aliwataka wajumbe wa mkutano huo, ambao pia unatarajiwa kuchagua viongozi wapya wa chama hicho, kuzingatia haki, mshikamano na maslahi ya taasisi yao, huku akisisitiza umuhimu wa kuepuka migogoro na mambo yanayoweza kukipotezea mwelekeo chama hicho muhimu kwa maendeleo ya utumishi wa umma nchini.
Kwa upande wake, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, aliwakumbusha wajumbe hao juu ya juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha ustawi wa watumishi wa umma nchini.
Alieleza kuwa Serikali imeendelea kupandisha madaraja watumishi, kuboresha miundo na vyeo vya kazi, pamoja na kulipa madeni mbalimbali ya mishahara na stahiki za watumishi, huku akiahidi kuwa juhudi hizo zitaendelea kadri hali ya bajeti ya Serikali itakavyoruhusu.
“Tumekuwa tukifanya maboresho haya hatua kwa hatua, na dhamira yetu ni kuhakikisha watumishi wa umma wanaendelea kunufaika na matunda ya Serikali yao,” alisema Mhe. Ridhiwani.
Mkutano huo wa TAPSEA unatarajiwa kujadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya taaluma ya uandishi na uendesha ofisi pamoja na mustakabali wa chama hicho nchini.

.jpeg)

SALOME: NGUZO ZA ZEGE NA CHUMA KUTUMIKA KUKABILI CHANGAMOTO YA KUANGUKA KWA NGUZO ZA UMEME ZA MITI.
habari
NAIBU Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kubadilisha nguzo chakavu kwa kuweka nguzo imara zaidi, zikiwemo nguzo za zege na chuma, pamoja na kuimarisha misingi ya nguzo katika maeneo yenye udongo laini ili kukabili changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme.
Salome ameeleza hayo leo, Mei 22, 2026, Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Sara Msafiri Ally, Mbunge wa Mvomero, aliyetaka kujua ni lini Serikali itatatua changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika Tarafa ya Mgeta.
Akijibu swali hilo, Salome amesema Serikali inatambua uwepo wa changamoto ya kuanguka kwa nguzo za umeme katika baadhi ya maeneo ya Tarafa ya Mgeta kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo mvua nyingi, uwepo wa udongo usiohimilivu pamoja na uchakavu wa baadhi ya nguzo.
Amesema Serikali kupitia TANESCO inaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa miundombinu ya umeme ili kubaini na kushughulikia changamoto hizo mapema pindi zinapojitokeza.Aidha, Salome amefafanua kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati imetenga bajeti maalum ya kubadilisha nguzo za miti katika maeneo yote yenye unyevunyevu pamoja na maeneo yenye shughuli mbalimbali za kibinadamu.
Kadhalika, ametoa wito kwa wananchi kuacha matumizi mabaya ya ardhi, ikiwemo kuchoma moto ovyo mashambani, jambo ambalo limekuwa likiathiri miundombinu ya umeme kwa kuunguza nguzo za umeme.
WAZIRI DKT. GWAJIMA ASISITIZA UWAJIBIKAJI NA MAZINGIRA BORA YA KAZI KWA WATUMISHI
habariNDEJEMBI AZUNGUMZA NA BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA
habari
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tone Tinnes yaliyolenga kuimarisha na kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika sekta ya nishati.
Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 22, 2026 katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam.
Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ikiwemo mashirikiano ya kimkakati katika uendelezaji wa gesi, umeme, nishati jadidifu pamoja na kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na juhudi za kukuza sekta ya nishati kwa nchi hizo mbili.
Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Kamishna wa Mafuta na Gesi kutoka wizara ya nishati, Bw. Goodluck Shirima, Mkurugenzi wa Maendeleo na Uzalishaji kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Bw. Paschal Njiko pamoja na wataalamu wengine.DCEA YATUNUKIWA TUZO KWA KUIMARISHA NYUMBA ZA UPATAJI NAFUU
habariMD TWANGE AELEZA KUTORIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI WA MRADI WA HALE
habari
Na Mwandishi Wetu, Korogwe, Tanga
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange ameeleza kutoridhishwa na kasi ya mkandarasi anayetekeleza mradi wa maboresho ya Kituo cha Kufua Umeme cha Hale kutokana na kuchelewa kukamilika kwa Mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2022.
Bw. Twange ameyasema hayo leo Aprili 22, 2026 wakati wa ziara yake ya ukaguzi katika mradi wa Hale pamoja na mradi wa usafishaji wa bwawa la Mto Pangani iliyopo katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambapo amemtaka mkandarasi wa Mradi wa Hale kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuongeza wafanyakazi pamoja na muda wa kufanya kazi ili ukamilike kwa wakati.
“Siridhishwi sana na mwenendo wake. Mkandarasi amewahi kuomba nyongeza ya muda mara mbili na nimepata taarifa kuwa yuko kwenye hatua za kuomba nyongeza nyingine ya tatu. Ndio maana nimekuja kuona kuna nini,” amesema Bw. Twange.
Amesema mradi huo una maeneo saba ya utekelezaji ambapo maeneo mawili tayari yamekamilika huku mengine yakiendelea na utekelezaji.
“Nimezungumza na msimamizi wa mradi, mhandisi mshauri pamoja na mkandarasi na nimewaelekeza wakae pamoja kuhakikisha ifikapo mwisho wa mwezi Julai mradi huu uwe umekamilika,” amesema Bw. Twange

Aidha, kuhusu mradi wa usafishaji wa bwawa la Pangani, Bw. Twange amesema matarajio ya TANESCO ni kuhakikisha kazi hiyo inakamilika ndani ya muda uliopangwa ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa msimu wa mvua.
“Matarajio yetu ni kutoupitiliza mwaka mmoja ili tumalize kabla ya msimu unaokuja wa mvua,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, Bw. Twange amesema TANESCO kwa sasa inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya umeme nchini yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 13.4.
Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Mradi wa Hale Mha. Kulwa Byemelo amesema maagizo yaliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji yatatekelezwa ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

“Mradi huu utakapokamilika utaimarisha upatikanaji wa umeme katika wilaya mbalimbali zinazochukua umeme kutoka kituo cha Hale pamoja na wilaya za Handeni, Muheza na Korogwe,” amesema Byemelo.
Ziara hii ni moja ya mikakati ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme pamoja na kubaini changamoto zinazojitokeza na kuhakikisha zinatatuliwa kwa wakati na miradi ina kamilika ili watanzania waweze kuendelea kufurahia upatikanaji wa umeme wa uhakika.


TUME YA TAIFA YA MIPANGO YAWAKUTANISHA WADAU MAJADILIANO ATHARI ZA MGONGORO UKANDA WA GHUBA KWA TANZANIA
habari
Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam
Tume ya Taifa ya Mipango kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP leo Mei 22, imefanya mjadala uliyowakutanisha wadau wa maendeleo, sekta binafsi, asasi za kiraia, watafiti na taasisi za elimu ya juu kujadili hatua mbalimbali na afua zinazoweza kutumika ili kukabiliana na athari za mgogoro wa ukanda wa Ghuba.
Akifungua mjadala huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo amesema kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua madhubuti na za kimkakati ili kupunguza athari zinazotokana na mgogoro wa Ghuba kiuchumi na kwa wananchi.
Mhe. Mkumbo amesema hayo leo Mei, 22 jijini Dar es Salaam katika mjadala wa kitaalamu ulioandaliwa na Tume ya Taifa ya Mipango kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa UNDP kwa lengo la kujadili athari, uhimilivu na fursa zinazotokana na mgogoro huo.
Akitaja hatua hizo, Prof. Mkumbo amesema kuwa ni pamoja na kufuatilia kwa karibu bei na upatikanaji wa mafuta, chakula, mbolea na usafiri, kulinda kaya zilizo katika mazingira hatarishi, kuimarisha akiba na usambazaji wa biadhaa muhimu.
“tutahakikisha wananchi wanaendelea kupata chakula cha kutosha na mbolea kwa bei himilivu, vile vile tutaendelea kufanya uthibiti wa gharama za nishati, ikiwa ni pamoja na kutumia fursa za maliasili tulizonazo kama Gesi asilia, madini, utalii na fursa ya miundombinu ya usafiri kuimarisha uchumi wa taifa” amesema Prof. Mkumbo.
Hatua hizo, zinalenga kukabiliana na athari kama vile kupanda kwa bei ya mafuta, usafirishaji na mbolea kunakoweza kuathiri maisha ya wananchi, uzalishaji na bajeti ya Serikali, hivyo Serikali itaendelea kuchukua hatua za haraka ili kuwalinda.
Aidha, Mheshimiwa Waziri ameeleza kuwa pamoja na changamoto hizo, mgogoro huo wa Ghuba unatoa fursa ya kipekee ya kiuchumi kwa Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla, hasa katika kuvutia uwekezaji mpya kwenye sekta ya nishati.
"Mgogoro huu unatoa mwanya mkubwa wa uwekezaji katika miundombinu ya mafuta, ikiwemo ujenzi wa viwanda vya kikanda vya kusafisha na kuchakata mafuta (regional refineries)," amesema Prof. Mkumbo.

Awali akimkaribisha Mhe. Waziri, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida alieleza kuwa mkutano huo unahusisha wadau wa maendeleo, sekta binafsi, asasi za kiraia, watafiti na taasisi za elimu ya juu kujadili hatua mbalimbali na afua zinazoweza kutumika ili kukabilia na athari za mgogoro huo.
Majadiliano hayo yalihudhuriwa na Mratibu Mkaazi wa Umoja wa Mataifa Bi. Susan Namondo na Mwakalishi Mkaazi wa Umoja wa Mtaifa, na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania Bw. Shigeki Komatsubaram.







FCC YABAINI VIPURI NA VILAINISHI BANDIA SOKONI
habariTBS YAFANIKIWA KUPATA ITHIBATI YA UMAHIRI YA KIWANGO CHA KIMATAIFA
habariSERIKALI KUIMARISHA MAABARA ZA VIWANDA
habariTBS YASOGEZA HUDUMA KARIBU, YAJENGA MAABARA MPYA DODOMA, MWANZA NA ARUSHA
habariRAIA WA IRAN APATIKANA NA HATIA YA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA
habariWAHASIBU, WACHUMI WATAKIWA KUFUATA SHERIA KUEPUKA UDUKUZI WA MIFUMO
habariKUELEKEA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA NYUKI DUNIANI MKOANI TABORA
habariTANZANIA YAJIPANGA KUIMARISHA TEKNOLOJIA YA NYUKLIA

TUME ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imeshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Uvumbuzi wa Nishati ya Nyuklia Barani Afrika (NEISA 2026) uliofanyika Mei 19, 2026 mjini Kigali, Rwanda, ukiwakutanisha viongozi wa kitaifa, wataalamu wa nishati, wawekezaji pamoja na mashirika ya kimataifa kujadili mustakabali wa nishati ya nyuklia barani Afrika.
Mkutano huo ulilenga kujadili namna bora ya kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme, kupunguza uchafuzi wa mazingira, kusaidia maendeleo ya viwanda, kukuza ubunifu wa teknolojia za nyuklia pamoja na kuvutia uwekezaji katika miradi ya nishati kwa ajili ya kuimarisha uchumi endelevu.
Katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alisema Tanzania inaendelea kutathmini matumizi ya nishati ya nyuklia kama sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kuongeza vyanzo vya nishati nchini.
Rais Samia alieleza kuwa teknolojia mpya za Small Modular Reactors (SMRs) na Micro Modular Reactors (MMRs) zinaweza kuwa suluhisho sahihi kwa nchi zinazoendelea kutokana na uwezo wake wa kuzalisha nishati kwa ufanisi na usalama zaidi.
Aidha, alitaja maeneo muhimu yanayopaswa kupewa kipaumbele katika maendeleo ya sayansi na teknolojia ya nyuklia kuwa ni pamoja na mifumo imara ya udhibiti, wataalamu wenye ujuzi pamoja na usimamizi madhubuti wa usalama kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.
Alisisitiza kuwa matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika uzalishaji wa nishati yanahitaji maandalizi ya mifumo ya udhibiti, uwezo wa taasisi, upatikanaji wa fedha, uelewa wa wananchi na ushirikiano wa kikanda.
Katika ushiriki wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania, Profesa Najat Kassim Mohammed alihudhuria mkutano huo akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Nyuklia na Huduma za Ufundi, Dkt. Remigius Kawala.
Profesa Najat alipata fursa ya kushiriki kikao cha ndani kilichoongozwa na Rais Samia ambapo alitoa ufafanuzi kuhusu maendeleo ya nyuklia nchini pamoja na miradi inayotekelezwa na TAEC kwa kushirikiana na International Atomic Energy Agency.
Miongoni mwa mipango hiyo ni Rays of Hope unaolenga kuimarisha huduma za uchunguzi na matibabu ya saratani nchini, Atoms4Food unaohamasisha matumizi ya teknolojia ya nyuklia katika sekta ya kilimo pamoja na ushiriki wa TAEC katika mpango wa matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwa uzalishaji wa umeme.
Profesa Najat alisisitiza umuhimu wa Tanzania kuendelea kuwekeza katika utafiti, usalama na mafunzo ya wataalamu ili kuhakikisha matumizi salama na endelevu ya teknolojia ya nyuklia katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, kilimo, viwanda, utafiti wa madini na uzalishaji wa nishati.
Kupitia mkutano huo, TAEC ilipata nafasi ya kubadilishana uzoefu na wataalamu kutoka mataifa mbalimbali kuhusu usalama wa nyuklia, mifumo ya udhibiti wa teknolojia za nyuklia pamoja na uwekezaji katika miundombinu ya kisasa ya nishati.
Aidha, ushiriki wa Tanzania katika NEISA 2026 uliendana na maono ya serikali ya kukuza sekta ya nishati na kuimarisha ushirikiano wa kikanda ndani ya Afrika Mashariki.
Katika mkutano huo, viongozi mbalimbali wa Afrika walisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kuendeleza miradi ya nyuklia, kuongeza uwekezaji na kujenga uwezo wa wataalamu wa ndani.
Kwa ujumla, ushiriki wa TAEC katika NEISA 2026 umeiwezesha Tanzania kuendelea kujijengea nafasi katika mjadala wa kimataifa kuhusu mustakabali wa nishati ya nyuklia barani Afrika pamoja na kufungua fursa mpya za ushirikiano wa kitaalamu, kiteknolojia na kiuchumi kwa maendeleo endelevu ya taifa.
Mkutano wa NEISA 2026 uliandaliwa kwa ushirikiano wa International Atomic Energy Agency, United Nations Economic Commission for Africa, World Nuclear Association pamoja na Rwanda.

MCHENGERWA: MAPAMBANO YA MALARIA YANAHITAJI NGUVU YA PAMOJA
habariMRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME CHALINZE–DODOMA KUKAMILIKA AGOSTI 2026 : MD TWANGE
Nishati
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Zuzu, Dodoma, unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 18, 2026.
Akizungumza Mei 20, 2026 wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo katika mikoa ya Morogoro na Dodoma, Bw. Twange amesema mradi huo ni muhimu kwa kuwa unasafirisha umeme unaozalishwa moja kwa moja kutoka katika Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere ambao unapita Chalinze hadi Dodoma.

Amesema utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na upanuzi wa vituo vya kupokea na kupoza umeme vya Chalinze na Zuzu, Dodoma, ambapo kukamilika kwake kutaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwa ajili ya shughuli za uwekezaji pamoja na kuongeza fursa mbalimbali za kiuchumi nchini.
Amesema Serikali Chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa kiasi cha Shilingi Bil 514 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi huo ambao utachochea shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kuendana na kasi ya ongezeko la mahitaji.

“Leo tumefanya ukaguzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma. Njia hii ni muhimu kwa kuwa inaongeza uwezo wa kusafirisha umeme kutoka Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere kwenda kwa watumiaji mbalimbali. Idadi ya watu imeongezeka na shughuli za kiuchumi zimeongezeka hivyo tumeingia makubaliano sasa mradi huu utakamilika Agosti 18, 2026,” alisisitiza Bw. Twange.
Ameeleza kuridhishwa na hatua iliyofikiwa huku akimtaka mkandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

“Tumekubaliana kuongeza wataalamu na vifaa vya kutosha ili kuhakikisha mradi huu unakamilika ndani ya muda ulioainishwa ,” ameongeza.
Kwa upande wake, Meneja wa Mradi, Mhandisi Newtone Lingstone, amesema mradi huo wenye urefu wa kilometa 345 Kutoka Chalinze hadi Dodoma unafadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Tanzania, huku kazi za upanuzi wa vituo vya kupokea na kupoza umeme vya Chalinze na Dodoma zikiendelea vizuri.

Kukamilika kwa mradi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma wenye msongo wa Kilovoti 400 utaimarisha na hali ya upatikanaji wa umeme si kwa Mkoa wa Dodoma pekee, bali katika maeneo mbalimbali nchini.





.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)




