HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI KATAMBI MBELE YA KAMATI YA MAMBO YA NJE,ULINZI NA USALAMA

March 11, 2026 Add Comment


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Miradi iliyopo katika Vyombo vya Usalama vilivyopo chini ya wizara yake kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje,Ulinzi na Usalama.

Amewasilisha Taarifa hizo leo jijini Dodoma ikiwa ni utaratibu wa kamati hiyo kupokea Taarifa za Utekelezaji wa Miradi iliyotolewa fedha za Serikali.



VIGEZO VINNE VYA KUMPATA MREMBO WA KIHADZABE,KARIBU JIOPAKI YA NGORONGORO

March 11, 2026 Add Comment




Wahadzabe ni kabila linalopatikana pembezoni mwa ziwa Eyasi na habari za maisha yao zimehifadhiwa makumbusho ya Urithi Jiopaki liyopo Karatu.


Baadhi ya vidume vinatamani kuwaoa wasichana wa kihadzabe  lakini kuwapata si kazi rahisi, lazima utumize vigezo vinne kama ifuatavyo; 


Kwanza *Usitahiriwe* , Kabila hili linaamini kwamba mwanaume kutahiriwa hupunguza utaalam wa mambo na kufanya  mwili wako kuwa legelege.


Pili, uwezo wa *kula Mizizi , matunda na nyama pori,* wakiamini kuwa vitu hivyo hukupa nguvu ya kutosha na Jembe la kazi wakati wa tendo la ndoa na huitaji kutafuta Vumbi la Congo kama wala Chipsi mjini.


Tatu uwezo wa *kulenga shabaha,* wakiamini kwamba hutamlaza njaa  kila siku utarudi na nyama pori ambayo ni chakula hapo nyumbani.


Nne *usiwe na mchepuko* , wakiamini mtu anayechepuka anaweza kuuawa wakati wowote akifumaniwa kwa kuzini na pia kuleta maradhi nyumbani.


Karibuni makumbusho ya  Jiopaki na eneo la  ziwa Eyasi kwa wahadzabe ujue kuwa mcheza kwao hutuzwa

DKT.MAGEMBE ATAKA KILA MWAJIRI AHAKIKISHE MTUMISHI WAKE ANAKUWA NA UHAKIKA WA MATIBABU KUELEKEA BIMA YA AFYA KWA WOTE

March 10, 2026 Add Comment




Na Hassan Kimweri, WAF - Dar es Salaam


Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Grace Magembe amewataka waajiri kuhakikisha kila muajiriwa anakuwa na uhakika wa matibabu kuelekea utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050. 


Dkt. Magembe amesema hayo leo Machi 10, 2026 baada ya wasilisho la maandalizi ya Bima ya Afya kwa Wote kwenye mkutano na Wakurugenzi Wakuu wa Makampuni ya Tanzania (CEO Roundtable of Tanzania – CEOrt) uliofanyika jijini Dar es Salaam na kuwakutanisha viongozi kutoka serikalini, sekta binafsi na washirika wa maendeleo. 



"Serikali inaendelea kuimarisha utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kuwa na ubunifu wa vyanzo vya fedha pamoja na kuanzisha kitita muhimu kitakachohakikisha kila mwananchi anapata huduma muhimu za afya katika vituo vyote vya kutolea huduma nchini," amesema Dkt. Magembe

Aidha, Dkt. Magembe amesema Serikali imeanza utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambapo utekelezaji wake unafanyika kwa awamu, awamu ya kwanza ilianza Januari 6, 2025 kwa kuwatambua zaidi ya familia milioni 3.6 kidijitali kwa kushirikiana na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa," amesema Dkt. Magembe

Katika hatua nyingine, Dkt. Magembe amesema Serikali imeanzisha Mfuko wa kugharamia huduma za Afya (Health Equity Fund) utakaosaidia kugharamia huduma za afya kwa wananchi wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu kupitia vyanzo mbalimbali.

Pia, amesema Serikali imeanza kuchukua hatua za kupunguza utegemezi wa misaada ya wahisani katika sekta ya afya kwa kuimarisha zaidi vyanzo vya ndani vya fedha na kutafuta mbinu mpya za ubunifu zitakazochangia kugharamia huduma za afya nchini.

Hata hivyo, ameeleza dhamira ya Serikali kuimarisha viwanda vya ndani vya dawa na bidhaa za afya ili kuhakikisha upatikanaji wa dawa unakuwa wa uhakika, kuongeza ajira na kukuza sekta binafsi kuelekea utekelezaji wa bima ya afya kwa wote. 

Mwisho, Serikali imewahimiza wawekezaji kutumia fursa zilizopo katika sekta hiyo, huku ikiendelea kukuza ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi katika uzalishaji wa dawa na vifaa tiba nchini. 



MCHAWI WA MWANAMKE SI MWANAMKE

March 10, 2026 Add Comment


Wanawake watumishi wa Mamlaka  Hifadhi ya Ngorongoro katika muendelezo wa  kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, wamedhihirisha kwamba mchawi wa mwanamke si mwanamke  kwa kutembelea  shule ya Sekondari ya wasichana Ngorongoro na kuwapa tabasamu la  msaada wa vifaa mbalimbali


Akiongea kwa Niaba ya Kamishna wa Uhifadhi, Afisa Uhifadhi Mkuu Sarah Lushu ameeleza kuwa vitu ambavyo Mamlaka vinajumuisha vyakula, Sabuni, vifaa vya kujifunzia, taulo la kike, Vyombo vya kuogea, kupikia na kufulia na mahitaji mbalimbali mahususi kwa wanafunzi wanawake ilo kuwaongezea tabasabu na kuonyesha nguvu ya mwanamke katika Jamii.

"Msaada huu ni sehemu ya jitihada za Shirika kupitia kamishna wa Uhifadhi kuimarisha uhusiano na jamii iliyopo ndani ya Hifadhi na kuhakikisha kuwa wanafunzi hasa wa kike wanapata mahitaji muhimu ya kuwapa utulivu wa kusoma na kupata ufaulu mzuri" alifafanua PCO Sarah.

Msaada huu unadhihirisha wazi kuwa wanawake ni watu wa kusaidiana na mchawi wa mwanamke sio Mwanamke.

KAMATI YA BUNGE YAAGIZA UDHIBITI WA USAHIHI WA VIPIMO UONGEZEWE NGUVU

KAMATI YA BUNGE YAAGIZA UDHIBITI WA USAHIHI WA VIPIMO UONGEZEWE NGUVU

March 10, 2026 Add Comment

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wakala wa Vipimo (WMA) kuongeza nguvu katika kudhibiti usahihi wa vipimo ili kuhakikisha huduma wanazopata wananchi zinaendana na thamani halisi ya fedha wanayotumia

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), Wakati Kamati hiyo ili pokea Taarifa ya Wizara ya Viwanda na Biashara kuhusu utekelezaji ya Miradi ya Maendeleo kwa mwaka 2025/26 kutoka Wakala wa Vipimo (WMA) na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Taasisi zake yake Machi 10, 2026 , Bungeni jijini Dodoma.

Mwanyika amesisitiza kuwa vita dhidi ya lumbesa haipaswi kuachiwa WMA pekee, bali inahitaji nguvu ya pamoja kati ya Halmashauri, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na Serikali Kuu ili kufanya oparesheni za nchi nzima.

Nao, Wajumbe wa Kamati hiyo walizipongeza WMA na CBE kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali na kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali yaliyolenga kuboresha utekelezaji wa Miradi hiyo kwa ufanisi.

Naye, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb), alifafanua kuwa msingi wa Tanzania ya Viwanda ni kilimo ambapo WMA inatekeleza jukumu la kumlinda mkulima, huku akibainisha kuwa idadi kubwa ya watumishi wa Wakala huyo wanazalishwa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), jambo linaloashiria kuwepo kwa uhusiano mkubwa wa kikazi baina ya taasisi hizo mbili.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Kihulla, amesema kuwa taasisi hiyo, kwa wakishirikiana na mamlaka nyingine za Serikali pamoja na sekta binafsi, wanaenda kupata suluhisho la kudumu la malalamiko ya wananchi ambayo yamekuwa yakiwasilishwa kwa muda mrefu kuhusu ukosefu wa usahihi wa vipimo katika maeneo mbalimbali ikiwemo lumbesa.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Prof. Edda Lwoga amesema miradi ya majengo inayojengwa kwenye Kampasi mbalimbali za Chuo hicho mara itakapokamilika itaboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza udahili wa wanafunzi katika chuo hicho.

WIZARA YA NISHATI YAPOKEA TRIL.1 ZA MIRADI YA MAENDELEO

March 10, 2026 Add Comment




 ðŸ“ŒNi asilimia 61 ya bajeti ya 2025/26


Na Mwandishi Wetu, Dodoma


WIZARA ya Nishati imepokea Sh. trilioni 1.150 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, sawa na asilimia 61 ya bajeti ya maendeleo iliyoidhinishwa kwa mwaka wa fedha 2025/26.


Taarifa hiyo imetolewa Machi 10, 2026 na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya sekta ya nishati kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Subira Mgalu, katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma.

Mhe.Ndejembi amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 wizara imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayolenga kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini.

Amesema katika fedha zilizopokelewa hadi sasa, Sh. bilioni 410.04 ni fedha za ndani na Sh. bilioni 740.30 ni fedha za nje ambazo zimeendelea kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya sekta ya nishati.

Ameongeza kuwa miradi hiyo inajumuisha upelekaji wa umeme vijijini na vitongojini, utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi asilia, ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta ya petroli pamoja na kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Kwa mujibu wa Ndejembi, katika mwaka wa fedha 2025/26 Wizara ya Nishati iliidhinishiwa kutumia jumla ya Sh trilioni 1.965, ambapo Sh trilioni 1.886 sawa na asilimia 95.97 zilitengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo huku Sh bilioni 79.23 sawa na asilimia 4.03 zikiwa kwa matumizi ya kawaida.

Amefafanua kuwa kati ya fedha za maendeleo zilizoidhinishwa, Sh trilioni 1.466 ni fedha za ndani na Sh bilioni 420.49 ni fedha za nje.

Ndejembi ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa miongozo na maelekezo ambayo imekuwa ikitoa na kuchangia mafanikio katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Amesisitiza kuwa wizara itaendelea kupokea ushauri na maoni ya kamati hiyo pamoja na kutoa ushirikiano unaostahili ili kuimarisha maendeleo ya sekta ya nishati nchini.



WALAJI KUNUFAIKA NA UFUATILIAJI WA FCC KWENYE MIKATABA YA UPANDE MMOJA

March 10, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu
Dar es Salaam, Machi 10, 2026. Tume ya Ushindani (FCC) imesema itaendelea kusimamia kwa karibu haki za walaji kwa taasisi na kampuni zinazotumia mikataba iliyoandaliwa kwa upande mmoja, ili kuhakikisha watumiaji wa huduma na bidhaa hawapati hasara kutokana na mikataba hiyo.
Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, alipokuwa akizungumza katika semina ya wadau kutoka taasisi na kampuni zinazotumia mikataba ya upande mmoja, iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Ngasongwa alisema FCC inaendelea kufuatilia kwa karibu mikataba ya aina hiyo ili kuhakikisha haikiuki haki za walaji katika soko. Alifafanua kuwa mikataba ya upande mmoja hutumiwa sana na taasisi mbalimbali kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakati, lakini ni muhimu iwe chini ya uangalizi ili kuepuka matumizi yanayoweza kuwa kinyume na sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.
Alisema semina hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa utoaji wa elimu kwa wadau kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mlaji Duniani, yanayolenga kuongeza uelewa kuhusu haki na wajibu wa walaji pamoja na watoa huduma.
“Ninatambua kuwa mikataba inayoandaliwa kwa upande mmoja ina faida katika kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakati. Hata hivyo, FCC ina jukumu la kuifuatilia kwa karibu, kwani bila uangalizi kunaweza kuwa na mambo yanayofanyika kinyume na maslahi ya walaji katika soko,” alisema Ngasongwa.
Aliongeza kuwa hata pale taasisi zinapotaka kuunganisha huduma au mikataba yao, ni muhimu kufanya tathmini ya kina ili kubaini kama kuna vipengele vinavyoweza kukiuka masharti ya ushindani au kuathiri ubora wa huduma kwa walaji.
Ngasongwa alisisitiza kuwa kila mtu ni mlaji kwa namna moja au nyingine, hivyo ni muhimu kuhakikisha thamani ya fedha inayotolewa na mteja inaendana na ubora wa huduma au bidhaa anayopata. Alisema hali hiyo pia husaidia kujenga uaminifu kati ya watoa huduma na walaji.
Aidha, alisema FCC itaendelea kukutana na makundi mbalimbali ya wadau kwa lengo la kuwapa uelewa mpana kuhusu majukumu ya taasisi hiyo na umuhimu wa kuzingatia sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), Tusekelege Mwaikasu, alisema semina hiyo ni muhimu kwa taasisi za kifedha kwani itawasaidia kuboresha utoaji wa huduma kwa walaji kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika.
Alisema benki, kupitia umoja wao, zimekuwa zikitekeleza kampeni ya “Niko Fiti”, inayolenga kuhakikisha huduma za kifedha zinatolewa kwa ubora na kwa kuzingatia mahitaji ya walaji.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindqni Ushindani Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa akizungumza wakati akifungua Semina kwa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa upande mmoja jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Udhibiti wa Mienendo ya Bidhaa inayokatazwa na Sheria ya Ushindani FCC, Bi.Magdalena Utouh  akizunguza wakati wa kuhitimisha semina ya wadau wa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa na upande mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa FCC,Bi. Roberta Feruzi akitoa maelezo kuhusiana na Semina ya wadau wa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa upande mmoja jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA ) Bi.Tusekelege Mwaikasu akitoa neno kwa niaba ya wadau katika mkutano na FCC ,jijini Dar es Salaam. Mkutano ukiendelea Kaimu Mkurugenzi Mkurugenzi Mkuu wa FCC Khadija Ngasongwa akiwa katika matukio picha za za pamoja makundi mbalimbali.