HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
TIPER YAANDIKA HISTORIA, YAKABIDHI SERIKALI GAWIO LA SH. BILIONI 15
habariUKARABATI WA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA HALE WAFIKIA ASILIMIA 83 YA UTEKELEZÀJI
📌 Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba
📌 Kukamilika kwake kutaongeza ufanisi wa uzalishaji na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani
Na Mwandishi Wetu, Korogwe – Tanga
Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini, huku Mradi wa Ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale wilayani Korogwe, mkoani Tanga, ukifikia asilimia 83 ya utekelezaji.
Akikagua maendeleo ya Mradi huo tarehe 29 Juni, 2026 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb), amemtaka mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi ndani ya muda uliopangwa, akisisitiza kuwa Serikali haitakuwa tayari kuongeza muda wa mkataba wa utekelezaji wa mradi huo.
Waziri Ndejembi amesema kukamilika kwa ukarabati wa Kituo cha Hale kutaimarisha ufanisi wa uzalishaji wa umeme, kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi katika Mkoa wa Tanga na maeneo ya jirani.
“Mkandarasi ahakikishe anakamilisha mradi huu kwa muda uliopangwa ifikapo Julai 31 mwaka huu, ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika pamoja na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi,” amesema Mhe. Ndejembi.
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Usambazaji Umeme TANESCO, Mhandisi Timoth Mgaya, amesema mradi huo unagharimu dola za Kimarekani milioni 24.81, sawa na takribani shilingi bilioni 64, na hadi sasa umefikia asilimia 83 ya utekelezaji.
“Mradi huu unagharimu dola milioni 24.81 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 64. Hadi sasa utekelezaji umefikia asilimia 83, na tunaendelea kushirikiana na mkandarasi kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika ndani ya muda uliopangwa,” amesisitiza Mhandisi Mgaya
Mradi wa ukarabati wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho, kuboresha utegemevu wa uzalishaji wa umeme na kuendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika kwa wananchi.
Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Hale ni kituo cha kwanza cha kuzalisha umeme kwa kutumia maji nchini. Kilijengwa kati ya mwaka 1961 na 1964 na kina uwezo wa kuzalisha takribani megawati 21. Ukarabati unaoendelea unalenga kuongeza ufanisi wa kituo hicho ili kiendelee kutoa mchango mkubwa katika Gridi ya Taifa kwa miaka ijayo.
TWIGA – BARRICK KINARA KUTOA GAWIO KWA SERIKALI 2026, YATOA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 221.9
habariDMG YATUNUKIWA TUZO KWA MAGEUZI YA SEKTA YA MELI
habari 
Morogoro, Tanzania – June 27, 2026_ — Dar es Salaam Merchant Group (DMG) has clinched the coveted _Best Maritime Technology Company of the Year_ award at the 2026 Morogoro Business Awards, cementing its position as a leader in Tanzania’s technological transformation of the blue economy.
NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU KAZI,AJIRA NA MAHUSIANO DKT EVELINE MUNISI AKIPATA MAELEKEZO KWA VIJANA WANAOPATA MAFUNZO YA UANAGENZI
DKT. KIJAJI AELEKEZA MAAFISA UHIFADHI KUHAKIKISHA MAENEO YA HIFADHI YANALINDWA NA KUHIFADHIWA
DKT MUNISI: PROGRAMU YA TAIFA YA UKUZAJI UJUZI YAENDELEA KUWAJENGA VIJANA
MANISPAA YA MOSHI YAKANUSHA KUBADILI MATUMIZI YA ENEO LA UHURU PARK..
habariTHBUB YAWAFIKIA ZAIDI YA WANANCHI 89,000 KUPITIA ELIMU YA HAKI ZA BINADAMU
habariNa Mwandishi Wetu- Dar es Salaam
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeendelea kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa kuwafikia zaidi ya wananchi 89,000 kupitia njia mbalimbali za utoaji elimu katika mwaka wa fedha 2025/2026.
Elimu hiyo ilitolewa kupitia mafunzo kwa makundi mbalimbali ya jamii, vipindi vya redio na televisheni, mitandao ya kijamii, huduma ya ujumbe mfupi wa simu (Bulk SMS) pamoja na usambazaji wa vipeperushi na machapisho ya elimu.
Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa Tume hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma, Mawasiliano,Utafiti na Nyaraka wakati akiongea na vyombo vya habari katika viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara saba saba leo Juni 29,2029
Bi. Mnanka amesema katika kipindi hicho, wananchi zaidi ya 80,000 walifikishiwa ujumbe wa elimu kupitia simu za mkononi, huku vipeperushi 39,129 na vitabu 200 vya elimu vikisambazwa kwa wananchi ili kuongeza uelewa kuhusu haki za binadamu, utawala bora na namna ya kuwasilisha malalamiko THBUB.
Aidha, Tume ilirusha vipindi 79 vya elimu kupitia redio na televisheni, hatua iliyochangia kuwafikia wananchi wengi zaidi nchini.
THBUB imesema itaendelea kutumia teknolojia na majukwaa mbalimbali kuhakikisha elimu ya haki za binadamu inawafikia Watanzania wengi zaidi.
Pia, Bi. Mnanka amesema THBUB imeendelea kuwekeza katika elimu ya haki za binadamu kwa kutoa mafunzo kwa zaidi ya washiriki 9,300 kutoka makundi mbalimbali ya jamii nchini katika mwaka wa fedha 2025/2026.
Akitoa takwimu ya walionufaika na mafunzo hayo, Bi. Mnanka ametaja makundi hayo kuwa ni pamoja na askari wa Jeshi la Polisi 827, waandishi wa habari 324, madiwani 60, wanafunzi zaidi ya 8,000 na walimu 121 kutoka vyuo vikuu tisa pamoja na taasisi nyingine za elimu.
Mafunzo hayo yalilenga kuongeza uelewa kuhusu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kuheshimu haki hizo.
“…..kuwajengea uwezo makundi mbalimbali katika jamii ni hatua muhimu ya kuimarisha utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu na kuzuia vitendo vya uvunjifu wa haki na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora…..” amesema Bi.Mnanka.
IRELAND YAHAKIKISHA KUENDELEA KUFADHILI MIRADI YA USAWA WA KIJINSIA VYUONI
habariWAZIRI NDEJEMBI -MRADI WA EACOP WAELEKEA UKINGONI MELI YA KWANZA KUBEBA MAFUTA JANUARI 2027
habari
Na Oscar Assenga, Tanga
WAZIRI wa Nishati, Dkt. Deogratius Ndejembi, amesema ujenzi wa Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) umefikia asilimia 86, huku mafuta ya kwanza yakitarajiwa kupokelewa katika Kituo cha Chongoleani, Tanga, na kusafirishwa Januari mwaka 2027.
Dkt. Ndejembi alisema hayo leo baada ya kutembelea eneo la mradi Chongoleani, mkoani Tanga, kujionea maendeleo ya utekelezaji wake, ambapo alieleza kuwa matarajio ni kukamilisha ujenzi huo ifikapo mwisho wa Agosti mwaka huu.
Alisema kazi nyingi muhimu zimekamilika na kilichobaki ni hatua za mwisho ikiwemo kukamilisha miundombinu ya umeme ili kuwezesha mitambo ya kusukuma mafuta kufanya kazi.
"Nimefurahishwa na maendeleo ya mradi. Kazi kubwa imefanyika na tunaamini ifikapo mwisho wa Agosti ujenzi utakuwa umekamilika. Ratiba inaonyesha kuwa meli ya kwanza itachukua mafuta ghafi kutoka Chongoleani mwezi Januari, 2027," alisema.
Hata hivyo, alisema changamoto iliyobaki ni kukamilika kwa njia ya umeme kutoka Majani Mapana kuelekea eneo la mradi, huku akiutaka mkandarasi anayetekeleza kazi hiyo chini ya Tanesco kuhakikisha anakamilisha mradi huo kwa wakati.
Alionya kuwa mkandarasi atakayeshindwa kutekeleza kazi hiyo ndani ya muda uliopangwa atachukuliwa hatua, ikiwemo kuondolewa katika orodha ya wakandarasi wanaofanya kazi na Tanesco.
Dkt. Ndejembi alisema EACOP ni mradi wa kimkakati kwa Tanzania, Uganda na ukanda mzima wa Afrika Mashariki, akibainisha kuwa bomba hilo lenye urefu wa zaidi ya kilomita 1,400 ni la kwanza duniani lenye mfumo wa kupashwa joto katika urefu wake wote.
Alisema Serikali ya Tanzania imewekeza zaidi ya Sh bilioni 973 kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), ambalo linamiliki asilimia 15 ya hisa za mradi huo kwa kushirikiana na kampuni za UNOC, TotalEnergies na CNOOC.
Aidha, aliwataka Watanzania kuendelea kutumia fursa zinazotokana na mradi huo, akieleza kuwa zaidi ya Watanzania 3,000 wamepata ajira za moja kwa moja, huku vijana wengine zaidi ya 100 wakipelekwa Madimba kwa mafunzo ya kuongeza ujuzi kabla ya kuajiriwa.
Aliongeza kuwa zaidi ya vijana 400 kutoka Chongoleani wamepatiwa mafunzo na kuajiriwa katika maeneo mbalimbali ya mradi huo, huku fursa nyingine nyingi zikiendelea kujitokeza.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, alisema mradi huo umeendelea kuleta manufaa makubwa kwa mkoa huo kupitia ongezeko la shughuli za Bandari ya Tanga, mapato ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na fursa za ajira kwa wananchi.
Alisema vifaa vingi vya mradi vimepitia Bandari ya Tanga kabla ya kusafirishwa katika maeneo mbalimbali ya utekelezaji wa bomba hilo, jambo lililochochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi.
Balozi Burian alisema pia mradi huo umezingatia viwango vya kimataifa vya utunzaji wa mazingira, akieleza kuwa shughuli za uvuvi zinaendelea kama kawaida na hakuna viumbe hai walioathirika kutokana na ujenzi wa gati na miundombinu mingine.
Aliongeza kuwa kupitia mradi huo, Halmashauri na jamii zinazozunguka eneo la mradi zimenufaika na miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa uwanja wa mpira unaotumiwa na klabu ya Coastal Union.

Naye Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Huduma za Mradi wa EACOP, Jofrey Mponda, ambaye pia alizungumza kwa niaba ya uongozi wa EACOP Tanzania, alisema mradi umefikia hatua za mwisho za utekelezaji, huku zaidi ya asilimia 90 ya kazi ikiwa imekamilika.
Alisema mradi huo unaounganisha mikoa 18 ya Tanzania na wilaya 27 umeingia katika hatua ya ukaguzi na makabidhiano ya mifumo mbalimbali, ikiwemo vituo vya kusukuma mafuta, matenki ya kuhifadhi mafuta na miundombinu mingine muhimu.

Mponda alisema pampu sita za kusukuma mafuta zimejengwa, mbili zikiwa nchini Uganda na nne nchini Tanzania, huku pampu mbili za kupunguza shinikizo la mafuta zikiwa Chongoleani.
Alibainisha kuwa matenki manne ya kupokelea mafuta tayari yamekamilika, huku kazi iliyobaki ikiwa ni kuunganisha mfumo wa umeme ili kuwezesha mitambo yote kuanza kufanya kazi kwa wakati.
Alisema EACOP inaendelea kushirikiana kwa karibu na Tanesco kuhakikisha miundombinu ya umeme inakamilika ifikapo Septemba mwaka huu, hatua itakayowezesha maandalizi ya kupokea mafuta ya kwanza mwezi Januari, 2027.
TAMISEMI YAWAKARIBISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LAKE SABASABA
habariGEL yataka wanafunzi warejee na maarifa ya kulijenga taifa
habariMWENGE WA UHURU WARIDHISHWA NA MIRADI YA BILIONI 2.159 SAME
MALIKALE, HAZINA INAYOPASWA KUENZIWA KWA VIZAZI VIJAVYO
habari
TRA YAKABIDHI VIFAA TIBA VYA SH. MILIONI 162 HOSPITALI YA RUFAA YA MWANANYAMALA
habari
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekabidhi vifaa tiba mbalimbali vyenye thamani ya Sh. Milioni 162 katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya TRA na utoaji wa Tuzo za Rais kwa Mlipakodi Bora zinazotarajiwa kutolewa Julai Mosi mwaka huu Mlimani City Jijini Dar es Salaam. TRA YAPANDA MITI 3850 NCHI NZIMA KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 30
habari
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imepanda miti 3850 nchi nzima ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake huku Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo Bw. Yusuph Juma Mwenda ikiutaka umma kuitunza miti hiyo kwa lengo la kuhifadhi mazingira.
Abdulmalik Mollel awaandaa walimu Dodoma kuiwakilisha Tanzania Korea Kusini
habariMSALABS, BARRICK BULYANHULU WATOA MSAADA KWA MAKUNDI YENYE MAHITAJI MAALUM NYANG'HWALE
habari
Wafanyakazi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na MSALABS wakifurahi katika picha ya pamoja na watu wenye ulemavu
Afisa wa Kampuni ya MSALABS akikabidhi Baiskeli kwa mama mlemavu katika hafla hiyo , huku mnufaika akiwa mwenye furaha na matumaini
'RUVUMA NI GHALA LA CHAKULA, SI LA MIFUGO MINGI' – YOGE
habari 
KAMISHNA MKUU WA TRA AWAPA UBALOZI WASTAAFU WA TAASISI HIYO
habari 






































