HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

KIKOSI CHA DHARURA NA UOKOAJI CHA BARRICK NORTH MARA CHAOKOA WANANCHI WALIOZINGIRWA NA MAJI TARIME

March 10, 2026 Add Comment

Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime
Shughuli za uokoaji wakulima waliozingirwa na mafuriko katika eneo la mashambani kijijini Matongo wilayani Tarime
 Faida za kuwepo mwekezaji mwenye uwezo, teknolojia za kisasa na mahusiano mazuri na jamii umedhihirika kutokana na Kikosi cha Dharura na Uokoaji (ERT) kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara kimesaidia kuokoa watu 22 wakiwemo watoto waliokuwa wamekwama kwa kuzingirwa na mafuriko katika kijiji cha Matongo, wilayani Tarime.

MAAFISA ELIMU MIKOA 26 WAPATIWA MAFUNZO ARUSHA

March 10, 2026 Add Comment
Mafunzo ya siku tano kwa Maafisa Elimu kutoka mikoa 26 ya Tanzania Bara yameanza rasmi jijini Arusha, yakilenga kuwajengea uwezo viongozi hao katika utekelezaji wa majukumu yao ya kiutendaji.

TANZANIA YASHIKA NAFASI YA NNE KWA UWEKEZAJI SEKTA YA MADINI AFRIKA

March 10, 2026 Add Comment

 

▪️Ni ya 4 barani Afrika, nyuma ya Botswana, Morocco na Zambia

▪️Alama ya Tanzania yapanda hadi 68.04 mwaka 2025 kutoka 62.75 (2024) na 46.38 (2023)

▪️Tanzania yaorodheshwa nafasi ya 15 duniani kwenye Best Practices Mineral Potential Index kwa alama 75.00

▪️Utafiti uliwahusisha wataalam na viongozi 2,304 wa kampuni za utafiti na uchimbaji.

▪️Rais Samia apongezwa kwa mazingira mazuri ya Uwekezaji Tanzania

Tanzania imeendelea kuimarisha nafasi yake kama kivutio cha kimataifa cha uwekezaji kwenye sekta ya madini baada ya kuorodheshwa miongoni mwa maeneo yanayoongoza barani Afrika, kwa mujibu wa ripoti ya Fraser Institute, Annual Survey of Mining Companies 2025.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Tanzania imepata nafasi ya 34 kati ya maeneo 68 duniani yaliyotathminiwa katika Investment Attractiveness Index (IAI), kielezo kinachotumiwa na wawekezaji na kampuni za utafiti wa madini kuamua wapi waelekeze mitaji ya utafiti na maendeleo ya miradi.  

Katika muktadha wa Afrika, Tanzania imeendelea kushika nafasi ya juu kwa kuwa ya 4 barani Afrika katika IAI, ikifuata Botswana, Morocco na Zambia, hatua inayothibitisha ushindani wa Tanzania katika kuvutia mitaji ya kimataifa ya utafiti na uwekezaji wa madini.  

Ripoti inaonesha pia mwenendo chanya wa kupanda kwa alama za Tanzania, ambapo alama ya IAI imefikia 68.04 mwaka 2025, ikilinganishwa na 62.75 mwaka 2024 na 46.38 mwaka 2023 mwenendo unaoashiria kuongezeka kwa uaminifu na mvuto wa Tanzania kwa wawekezaji wa sekta ya madini.  

Kwa maelezo ya ripoti, IAI hujengwa kwa kuzingatia vipengele viwili vikuu vinavyoongoza maamuzi ya uwekezaji: uwezo wa kijiolojia wa rasilimali (mineral potential) na mazingira ya jumla ya kufanya biashara kwenye sekta husika. Ripoti hiyo inaeleza kuwa katika hesabu yake, asilimia 60 ya uzito huenda kwenye mineral potential na asilimia 40 huenda kwenye policy framework, ili kutoa taswira ya mvuto wa eneo husika kwa uwekezaji wa utafiti na uchimbaji.  

Katika kipengele cha Best Practices Mineral Potential Index kinachoangalia mvuto wa kijiolojia kama eneo lingekuwa na kanuni bora zaidi duniani Tanzania imeorodheshwa nafasi ya 15 duniani kwa alama 75.00, jambo linaloonesha kwa uwazi ukubwa wa fursa na uwezo wa rasilimali madini zilizopo nchini.  

Utafiti huu wa Fraser Institute ni miongoni mwa rejea muhimu zinazotumiwa kimataifa na sekta binafsi, taasisi za utafiti na wadau mbalimbali kutathmini mwenendo wa masoko ya uwekezaji wa madini. Kwa mujibu wa taarifa ya utafiti, dodoso lilipelekwa kwa viongozi na wataalam 2,304 wa kampuni za utafiti na uchimbaji, na waliotoa majibu waliripoti matumizi ya pamoja ya takribani Dola za Marekani bilioni 4.2 kwenye shughuli za utafiti wa madini mwaka 2025.  

Kwa Tanzania, nafasi hii inaongeza msukumo kwenye jitihada za Serikali za kuendelea kuimarisha sekta ya madini kama nguzo muhimu ya uchumi ikiwemo kuongeza utafiti, kuvutia mitaji mikubwa ya uendelezaji wa miradi, na kukuza ushiriki wa Watanzania katika mnyororo mzima wa thamani wa madini.  

Wataalamu wa uchumi na wadau wa sekta ya madini nchini wamempongeza Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa kuvutia uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya madini nchini Tanzania,huku wengi wakibashiri kuwa sekta ya madini kuwa nguzo kuu ya uchumi wa Tanzania kwa miaka michache ijayo.





RC TANGA KAMATI ZA USHAURI NGAZI ZA KISHERIA ZITASAIDIA KUPUNGUZA MASHAURI DHIDI YA SERIKALI NA VITENDO VYA UONEVU

March 10, 2026 Add Comment


Na Oscar Assenga,TANGA


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amezindua Kamati za Ushauri wa Kisheria ngazi ya mkoa na wilaya na kliniki ya Sheria bila malipo huku akieleza kwamba zitasaidia kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali kutokana na kukutanisha mawakili wa Serikali.

Aliyasema hayo leo kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga ambako kilifanyika uzinduzi wa Kamati hizo ambapo alisema pia wale wa taasisi mbalimbali na kuwasaidia wananchi wenye changamoto mbalimbali kupata ufumbuzi.

Alisema uwepo wa huduma hizo utawawezesha mawakili wa Serikali kusimamia utawala wa Sheria katika kushirikiana na wadau wengine katika kutatua kero za wananchi na kupunguza malalamikko ya kisheria kutoka kwa wananchi.

“Lakini pia kutoa elimu ya Sheria kwa umma katika kushughulikia changamoto mbalimbali katika maeneo yao pamoja na kutoa elimu kwa viongozi na maafisa wa Serikali waweze kutoa maamuzi kwa mujibu wa Sheria”Alisema




Aidha alisema pia itapunguza vitendo vya uonevu na vinavyovunja sheria na taratibu za nchi nah ii itawezesha mimi na wakuu wa wilaya kushughulikia masuala ya miradi ya maendeleo badala ya kuhangaika na migogoro ya wananchi .

“Lakini nanukuu katika kitabu cha Mathayo 5:9 Yesu anasema “Heri wapatanishi ,maana hao wataitwa wana wa Mungu”.Hii inaonyesha kuwa kazi ya kupatanisha ni ya Kiungu na inampendeza Mungu”

“Pia kwenye Qur’an inasititiza sana kutenda haki (Uadilifu)kama wajibu Mkuu wa kidini na kijami,ikiamrisha kusimamia haki hata kama ni dhidi ya nafsi zenu waziazi ,au jamaa (Quran 4:1:35,5.8).Uadilifu ni msingi wa imani,ukihimiza kulinda haki za wengine ,kuondoa chuki na kutoa fidia kwa wahasiriwa”Alisema

Aidha aliwataka wadau waelewe kuwa jukumu la kutatua migogoro katika maisha ya watanzania sio la Serikali pekee bali ni la wote wa maendeleo huku akieleza kazi kubwa Serikali iliyonayo ni pamoja na kutengeneza mazingira mamzuri yanayoweza kusaidia kamati hizo.

Alisema hilo linatokana na uwepo wa migogoro mingi katika jamii hasa migogoro ya ardhi na mirathi hivyo kamati hizo zinatakiwa kukaa kila mara kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake ya kusikiliza malalamiko ya ksiheria na kutoa elimu kwa umma kwa kushirikiana na ofisi za wakuu wa wilaya.

Hata hivyo alitoa rai kwamba kuna haja ya kuhakikisha kuwa kamati za mkoa na wilaya zinafanya mambo mbalimbali ili kukabiliana na migogoro ikiwemo kuendelea kuboresha kiwango cha utoaji wa huduma ya ushauri wa kisheria na kuongeza wigo na upatikanaji katika maeneo ambayo hayajafanikiwa kufikiwa hasa maeneo ya nje ya jiji.

Mkuu huyo wa mkoa alizitaka kujiwekea utaratibu wa kuandaa kliniki za kisheria bila malipo kwa utaratibu wa kuwafuata wananchi katika maeneo yaona hiyo inatokana na wapo wananchi wengine ambao wanaogopa kuingia kwenye ofisi za Serikali pamoja na wengine hawana uwezo wa kusafiri na kwenda kwenye ofisi hizo.

“Lakini hakikisheni mnapopokea malalamiko au migogoro mnaifuatilia mpaka mwisho ili kujiridhisha namna gani imemalizika na kuweka kumbukumbu ya kufungua na kufunga migogoro hii lengo likiwa kuzuia walalamikaji kurudi kuwasilisha malalamiko yaliyopita hasa pale anapoona uongozi umebadilika “Alisema

Hata hivyo nitoa wito kwa wananchi wote wa mkoa wa Tanga wenye migogoro kutumia nafasi hii kuwasilisha migogoro yenu katika kliniki ya Sheria bila malipo iliyoanza leo kwenye viwanja vya Tangamano mpaka Machi 15 mwaka huu .

Awali akzungumza akizungumza Mkurugenzi wa Uratibu na Huduma za Ushauri kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Neema Ringo alisema kwamba wamekuja mkoani Tanga kutoa huduma kwa wananchi za kisheria kwa maana yake kutekeleza wajibu wake katika kuwahudumia wananchi ambao ndio wanaipa mamlaka Serikali.

Alisema wakiwa mkoani Tanga watapata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuweza kuzipatia ufumbuzi huku akiwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo kwa kujitokeza kwa wingi kuweza kupata huduma








ASILIMIA 89 YA VITONGOJI NKASI VIMEFIKIWA NA UMEME- MHE.SALOME

March 10, 2026 Add Comment

 


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema asilimia 89 ya vitongoji 724 wilayani Nkasi Mkoa wa Rukwa  vimesambaziwa umeme, na vitongoji vilivyosalia  vitakuwa vimesambaziwa nishati hiyo ifikapo 2030.

Mhe. Salome amesema hayo katika Mji wa Namanyere, Wilaya ya Nkasi, Mkoa wa Rukwa wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba.

“Sisi Sekta ya Nishati jukumu letu ni kuhakikisha Watanzania wote wanapata umeme wa uhakika wakati wote. Hapa Nkasi kwa sasa wanatumia umeme kutoka nchini Zambia kupitia makubaliano ya kikanda ya kuuza na kununua umeme ili kuweka mfumo imara wa upatikanaji wa umeme. Hata hivyo, tunatarajia kama kila kitu kitakwenda sawa, Nkasi itapata umeme wa gridi ifikapo mwezi Mei mwaka huu,” amesema Mhe. Salome




Ameongeza kuwa, mradi wa kupeleka umeme wa gridi mkoani Rukwa unaendelea vizuri na mara umeme huo utakapofika mkoani humo,  wananchi watanufaika na umeme wa uhakika  huku pia wakiwa na nafasi ya kupata umeme wa ziada kutoka nchini Zambia. Aidha, kituo cha umeme cha Sumbawanga kinatarajiwa kutumika pia katika biashara ya umeme kwa nchi jirani, ikiwemo Zambia.

Akizungumza na wananchi katika Mji wa Namanyere, Mhe.Salome amewahamasisha kuachana na matumizi ya nishati isiyo safi kama kuni na mkaa na badala yake watumie nishati safi ya kupikia.

Amesema Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia, ikiwemo kutoa ruzuku ya hadi asilimia 85 kwa majiko banifu na ruzuku ya asilimia 50 kwa mitungi ya gesi ya kilo sita.


WAZIRI MHE. NDEJEMBI ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MRADI WA KITUO CHA KUPOKEA NA KUPOZA UMEME IGANJO – MBEYA

March 10, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu, Mbeya.


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Kituo cha Kupokea na Kupoza Umeme wa Kilovoti 400 cha Iganjo mkoani Mbeya, ambao kwa sasa umefikia takribani asilimia 60 ya utekelezaji wake.

Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo Machi 8, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika eneo la Iganjo jijini Mbeya ambao ni sehemu ya Mradi wa Njia kusafirisha Umeme kutoka mkoa wa Irunga hadi Mkoa wa Rukwa (TAZA).

“Kwa ujumla wake kazi hapa zinaenda vizuri sana. Niwapongeza Shirika la Umeme TANESCO kwa kazi ya usimamizi mzuri wa mradi huu,” amesema Mhe. Ndejembi

Akieleza faida za mradi huo amesema kuwa utaachangia kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Mbeya pamoja na mikoa jirani.

“Mradi huu utaongeza nguvu ya upatikanaji wa umeme kwa sababu kwa sasa Mkoa wa Mbeya unapata umeme kutoka kwenye njia ya kilovoti 220 lakini mradi huu utakua ni kilovoti 400. Wananchi watanufaika na mradi huu kwa sababu umeme utapoozwa na kusambazwa kwa Wananchi,” ameongeza Mhe. Ndejembi

Aidha, ameeleza kuwa serikali inayoongozwa na Rais wa awamu ya sita Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwekeza katika miradi mikubwa ya kimkakati ya nishati ili kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Tanzania - Zambia (TAZA) Mha. Elias Makunga amesema mradi wa kituo cha Iganjo unaendelea vizuri licha ya changamoto ndogo zilizojitokeza katika hatua za usambazaji wa vifaa.

“Mradi wa kituo cha Iganjo uko asilimia 60 ya utekelezaji, ujenzi wa misingi umekamilika kwa asilimia 89. Upande wa usambazaji wa vifaa kutoka China tuko asilimia 89, lakini tumekuwa na changamoto kidogo katika upande wa upokeaji wa vifaa unaohusiana na kuboresha mfumo wa TRA,” amesema Mha. Makunga

Mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Rukwa ukikamilika unatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi muhimu katika kuimarisha Gridi ya Taifa na kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika katika ukanda wa Nyanda za Juu Kusini.



BALOZI WA IRELAND NA NM-AIST WAJADILI UTEKELEZAJI WA SAMIA SCHOLARSHIP DS/AI+

BALOZI WA IRELAND NA NM-AIST WAJADILI UTEKELEZAJI WA SAMIA SCHOLARSHIP DS/AI+

March 09, 2026 Add Comment

Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Nicola Brennan na uongozi wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) wamejadiliana namna ya kuimarisha utekelezaji wa mpango wa Samia Scholarship Extended DS/AI+ unaolenga kujenga wataalamu wa Akili Bandia (AI) na Sayansi ya Takwimu (Data Science) nchini.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo iliyofanyika tarehe 9 Machi 2026 katika Taasisi hiyo jijini Arusha, Makamu Mkuu wa NM-AIST, Prof. Maulilio Kipanyula, amesema katika awamu ya kwanza ya mpango huo wanafunzi 34 wa Kitanzania wamepata nafasi ya kusoma katika vyuo vikuu vya Ireland.

Ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) pamoja na NM-AIST inapanga kuandaa *bootcamp* maalum kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi watakaofuata kunufaika na mpango huo.

Kwa upande wake, Balozi Brennan ameipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira ya kuwekeza katika elimu ya juu katika fani za AI, Data Science na Sayansi shirikishi, akibainisha kuwa wanafunzi wa Kitanzania watapata elimu yenye viwango vya kimataifa katika vyuo vikuu vya Ireland.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuongeza ushiriki wa wanawake katika masomo ya STEM na kuhimiza taasisi na wabunifu kuhakikisha matokeo ya tafiti yanafika sokoni ili kuchangia maendeleo ya uchumi, usalama wa chakula na ajira.

Katika ziara hiyo, Balozi Brennan pia alitembelea maabara, kituo cha kompyuta chenye uwezo mkubwa (HPC), Data Driven Institute (DDI) pamoja na vituo vya ubunifu vya NM-AIST ili kujionea mchango wa taasisi hiyo katika maendeleo ya sayansi na teknolojia nchini.

PROF. MKUMBO: SEKTA BINAFSI NI MUHIMU KUFANIKISHA MPANGO WA NNE WA MAENDELEO

March 09, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Serikali inatarajia zaidi ya asilimia 70 ya fedha za utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano zitatoka katika sekta binafsi kupitia uwekezaji na mifumo ya ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP).

SENYAMULE AHIMIZA MAKUNDI YA WANAWAKE KUSHIRIKI ZABUNI ZA UMMA.

SENYAMULE AHIMIZA MAKUNDI YA WANAWAKE KUSHIRIKI ZABUNI ZA UMMA.

March 09, 2026 Add Comment

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rosemary Senyamule, ameipongeza Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma kwa kusimamia vizuri upatikanaji wa fursa za Ununuzi wa Umma kwa makundi maalum, hususan wanawake, hatua ambayo imeendelea kuwasaidia kiuchumi na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo.

Akizungumza leo Machi 8, 2026 katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Mbande, Wilayani Kongwa Mkoa wa Dodoma, Bi. Senyamule amesema kuwa usimamizi mzuri wa PPRA umewezesha makundi ya wanawake kunufaika na zabuni mbalimbali za serikali kupitia mfumo wa kielektroniki wa Usimamizi wa Ununuzi -NeST.

Amesema kuwa hadi sasa vikundi vya wanawake vimefanikiwa kupata zabuni za serikali zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 16, hatua inayodhihirisha kuwa sera ya kutoa kipaumbele kwa makundi maalum inaleta matokeo chanya katika kuwawezesha wanawake kiuchumi.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa zaidi ya vikundi 500 vya wanawake vimesajiliwa kwenye mfumo wa NeST, jambo linaloonesha mwitikio wa wanawake katika kutumia fursa za ununuzi wa umma zinazotolewa na Serikali.

Aidha, Bi. Senyamule amewataka wanawake wote nchini kuendelea kuunda vikundi vingi zaidi ili waweze kunufaika na fursa hizo za zabuni za serikali, akisisitiza kuwa serikali imeweka mazingira rafiki yanayowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa nchi.

“Ni muhimu wanawake mkajiunga katika vikundi na kujisajili katika mfumo wa NeST ili mpate nafasi ya kushiriki katika zabuni za serikali.

Fursa hizi zipo kwa ajili yenu na zinaweza kuwasaidia kukuza biashara na kuinua kipato chenu,” amesema.

Ameongeza kuwa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyopatikana katika kuwawezesha wanawake na kuhamasisha juhudi zaidi za kuhakikisha wanawake wanapata nafasi sawa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Msimizi wa Kituo cha Msaada wa Kitaalam kwa Wateja wa NeST - PPRA ( NeST Customer Technical Support Center) Bi. Asifiwe Makweta amesema Mamlaka ina shauku kuona vikundi vya kina Mama vonaongezeka siku hadi siku ili kuhakikisha fursa hizi za serikali zinawafikia walengwa kiyakinifu kwa makundi yote ikiwemo Wanawake ili kuleta uhai wa ushiriki wa makundi maalum bila kubaki nyuma kwa kundi lolote.

"Pamoja na kufikia idadi ya kusajili makundi 500 ya Wanawake kwenye mfumo wa NeST bado haijafikia idadi ya makundi tunayotamani kusajili kwenye Mfumo wa NeST ili kushiriki katika fursa hii ya asilimia 30 ya zabuni kwa makundi hayo ambayo ni Vijana, wanawake, Wazee na watu wenye ulemavu"amesema Bi. Makweta.