HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
MFAMASIA MAGIGE: VYOMBO VYA HABARI NI NGUZO YA ULINZI WA AFYA YA JAMII
habariPPP KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA 2050
habariMTAKUWWA MAGU YAKUMBUSHWA KUELIMISHA JAMII DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA
MTAKUWWA YATAKA ELIMU ZAIDI DHIDI YA UKATILI MAGU .
NIDA yakabidhi Serikali zaidi ya shilingi bilioni 61
habari
Rostam Azizi apokea tuzo ya heshima kwa kukuza uwekezaji nchini
habari
Mwenyekiti wa Taifa Group na mfanyabiashara mashuhuri, Bw. Rostam Azizi, ametunukiwa Tuzo ya Juu ya Heshima ya Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) kwa kutambua mchango wake katika kukuza uwekezaji, kuunda ajira, kuboresha huduma za jamii na kuchochea maendeleo ya uchumi wa Taifa.
Tuzo hiyo ilikabidhiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, aliyekuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji la Mwaka 2026 lililoandaliwa na TNCC katika Hoteli ya Johari Rotana, Dar es Salaam.
Akizungumza katika kongamano hilo, Dkt. Mwigulu alisema Serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji kupitia maboresho ya sera, sheria, kanuni na mifumo ya utoaji huduma ili kuiwezesha sekta binafsi kuwa injini ya ukuaji wa uchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
"Ajenda ya sekta binafsi ni ajenda ya Taifa. Hatuwezi kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 bila sekta binafsi yenye nguvu na inayoshirikiana kwa karibu na Serikali," amesema.
Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushughulikia mapendekezo ya sekta binafsi ili kuondoa vikwazo vya biashara na kuongeza ushindani wa bidhaa na huduma za Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.
Kupitia uwekezaji wake katika sekta mbalimbali, Bw. Rostam Azizi amechangia uundaji wa maelfu ya ajira, kukuza uwekezaji na kuboresha huduma za jamii, hatua zilizochangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya uchumi wa Taifa.
Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Bw. Rostam Azizi aliishukuru Serikali na TNCC kwa kutambua mchango wake, akisema tuzo hiyo ni motisha ya kuendelea kushiriki katika maendeleo ya Taifa."Ninapokea tuzo hii kwa heshima kubwa.
Naihusisha na juhudi za pamoja kati ya sekta binafsi na Serikali katika kujenga uchumi imara. Nawapongeza pia wadau wote waliotunukiwa tuzo mbalimbali leo kwa mchango wao katika kuimarisha sekta binafsi na kukuza uchumi wa Taifa," amesema.
Katika hafla hiyo, Waziri Mkuu pia alikabidhi tuzo mbalimbali kwa wadau wengine, akiwemo Bi. Emma Kawawa, Bw. David Mwaibula, Bw. Imani Kajula, Bw. Elibariki Mmasi na Bi. Mercy Emmanuel Sila, kwa mchango wao katika kuendeleza sekta binafsi, kuboresha mazingira ya biashara na kuimarisha shughuli za TNCC.

Katibu Mkuu CCM akutana na Balozi wa Umoja wa Ulaya Kujadili Ushirikiano wa Maendeleo
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Christine Grau, Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, katika Ofisi ya Katibu Mkuu wa CCM, Lumumba, Dar es Salaam.
Mazungumzo hayo yamefanyika jana Juni 30,2026, ikiwa ni sehemu ya ziara ya kumuaga Balozi Grau anayehitimisha kipindi chake cha uwakilishi nchini Tanzania. Viongozi hao walitathmini ushirikiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya na kujadili namna ya kuuendeleza kwa manufaa ya pande zote mbili.Katika mazungumzo hayo, viongozi hao walibadilishana mawazo kuhusu umuhimu wa kuimarisha misingi ya utawala bora, amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa kama nguzo ya maendeleo endelevu ya Taifa. Katika muktadha huo, CCM ilisisitiza dhamira yake ya kuendelea kujenga Taifa linaloongozwa kwa misingi ya haki, uwajibikaji na utulivu wa kisiasa.
Pia, ilitambua changamoto zilizojitokeza nchini katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu uliopita na umuhimu wa hatua ambazo Serikali inaendelea kuzichukua katika kuimarisha imani ya wananchi, ikiwemo kuundwa kwa Tume ya Uchunguzi, Tume ya Upelelezi wa Jinai na hatua nyingine za kisheria zinazolenga kuhakikisha ukweli, uwajibikaji na haki vinaendelea kutawala katika kulinda amani na mshikamano wa Taifa.
Aidha, ilielezwa kuwa ajenda ya kuendelea kuimarisha demokrasia nchini, ikiwemo mchakato wa Katiba Mpya ambao umeainishwa katika Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2025–2030, inabaki kuwa sehemu muhimu ya maono ya muda mrefu ya kuimarisha utawala bora na mshikamano wa Taifa.
Viongozi hao pia walitambua nafasi ya vijana katika mustakabali wa maendeleo ya Tanzania na umuhimu wa kuhakikisha kizazi hicho kinaendelea kuwa sehemu ya safari ya Taifa kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na ujenzi wa uchumi wenye ushindani na maendeleo jumuishi.
CCM inathamini ushirikiano wake na Umoja wa Ulaya na inaamini kuwa ushirikiano huo utaendelea kuimarika kwa kuzingatia misingi ya kuheshimiana, maslahi ya pamoja na dhamira ya pamoja ya kuendeleza maendeleo endelevu ya Tanzania.
RC BATILDA AZIELEKEZA HALMASHAURI TANGA KUDHIBITI CHANZO CHA HOJA ZA CAG
habari
HALMASHAURI za Wilaya, Miji na Jiji mkoani Tanga, zimeagizwa kuzuia vyanzo vinavyosababisha hoja zinazoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Agizo hilo limetoa leo Juni 30, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt Batilda Burian, alipozungumza kwenye vikao maalum vya kujadili hoja za CAG katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri za Lushoto na Bumbuli.
Amesema, taarifa za CAG kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, inaonesha halmashauri hizo zimefanikiwa kupata hati inayoridhisha, ikiwa ni Ishara ya ufanisi, weledi na kujituma kwa watumishi na watendaji.
Amesema, hali hiyo inapaswa kuendelezwa ili kufikia malengo msingi ya Serikali katika kutoa huduma bora kwa wananchi.
Hata hivyo, Mhe. Balozi Dkt Batilda amesema, pamoja na mafanikio hayo, halmashauri hizo zinatakiwa kudhibiti vitendo vinavyosababisha hoja za ukaguzi.
Awali, taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Nje, Mkoa wa Tanga, Hamu Mwakasola, ilieleza kuwa kutolewa hati inayoridhisha haimaanishi kuwepo mifumo mizuri ya udhibiti wa ndani, bali kutokuwepo dosari kubwa wakati wa ukaguzi.
“Inamaanisha hapakuwa dosari kubwa zilizobainika wakati wa ukaguzi ambazo zingemzua Mkaguzi kutoa maoni, au kumlazimu kutoa hati yenye mashaka au hati mbaya,” amesema
Naye Katibu Tawala Mkoa (RAS) wa Tanga, Rashid Mchatta, pamoja na mambo mengine, amewahimiza watumishi na umma, kuendeleza mahusiano mema ili kuongeza ufanisi na tija mahali pa kazi.
Amesema, viongozi, watendaji na watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wanapaswa kutambua ‘uzito’ wa hadhi ya Ofisi ya CAG katika ukaguzi wa hesabu uliopo katika ngazi za kimataifa.
Mchatta amesema utambuzi wa ubora huo utachangia kuboresha utendaji kazi na kupunguza kwa kiasi kikubwa hoja za ukaguzi, hali itakayoifanya CAG kutekeleza vema wajibu wake wa ushauri wa kitaalamu kwa taasisi husika.
Mwisho
WATANZANIA KUNUFAIKA NA UMEME WA UHAKIKA; MRADI WA CHALINZE–DODOMA WAFIKIA ASILIMIA 89 YA UTEKELEZAJI
habari




OFISI YA WAZIRI MKUU NA TAASISI YA CHAKULA NA LISHE TANZANIA KUSHIRIKIANA KUANDAA MPANGO WA LISHE TAIFA
Na Mwandishi wetu- Dodoma
Na Mwandishi Wetu- Dodoma
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Bi. Debora Charwe amesema, Serikali ipo katika mchakato wa kuandaa Mpango wa Muda Mrefu wa Lishe wa Taifa (NN-LTP) ili kuongeza jitihada za sekta mtambuka katika kuboresha utekelezaji wa lishe kwa kipindi cha miaka 25 ijayo.
Bi. Debora ameyasema hayo leo tarehe 30 Juni, 2026 wakati akifungua Warsha ya mafunzo kuhusu kuandaa mpango wa muda mrefu wa lishe wa Taifa (National Nutrition Long Term Plan 2026-2050) ambayo inafanyika jijini Dodoma kwa siku tatu kuanzia Juni 30 hadi Julai 02, 2026
Amesema, mafunzo hayo yanatolewa kwa Wataalam kutoka ngazi ya Wizara mbalimbali kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu uandaaji wa mipango ya muda mrefu wa lishe inayojumuisha sekta mtambuka pamoja na kubadilishana uzoefu kusaidia katika usanifu, muundo na taratibu za utekelezaji wa Mpango wa muda mrefu wa Lishe wa Taifa.
Vilevile Bi. Debora amefafanua kuwa, mpango huo unaandaliwa chini ya usimamaizi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) na wadau wengine wa maendeleo kwa kuzingatia haja ya kuifanya lishe kuwa moja ya kichocheo na kipimo katika kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania kufikia 2050.
Aidha, warsha hiyo imehusisha Afisa viungo wa lishe kutoka Wizara mbalimbali zikiwemo Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) pamoja na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda, Wizara ya Maji na Wizara ya Mambo na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
==MWISHO==













.jpg.jpeg)















.jpg)










.jpg)



