HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
WAZABUNI WA KILWA, LINDI NA MTWARA WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MODULI YA MALALAMIKO, RUFAA KATIKA MFUMO WA NeST
habari
Akielezea kuhusu mafunzo hayo ya siku tano (kuanzia tarehe 16 - 20 Februari, 2026), Meneja wa Usimamizi wa Rufaa na Sheria (PPAA), Bi. Florida Mapunda amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kutoa elimu kwa wadau wa ununuzi wa Umma kuhusu taratibu za uwasilishaji na ushughulikiaji wa malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST kama ilivyoelekezwa katika Sheria ya Ununuzi wa Umma. WATUMISHI WAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MRADI WA EACOP KWA KUZINGATIA UHIFADHI WA MAZINGIRA
*Na mwandishi wetu, Tanga.*
Watumishi wa Wizara ya Nishati wameipongeza Serikali na Wanahisa wengine wa EACOP kwa kutoa fedha za kutekeleza mradi mkubwa wa kimkakati wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP). Pamoja na pongezi hizo Kampuni ya EACOP imepongezwa kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira katika hatua zote za utekelezaji wa mradi hususani viumbe hai katika maeneo yote yanayopitiwa.
Kauli hiyo imetolewa Februari 22, 2026, Chongoleani, Tanga na mwakilishi wa watumishi hao Bw. Benson Lukuta akiwa Mkuu wa Msafara katika ziara iliyofanywa na watumishi wa Wizara ya Nishati kutembelea mradi huo.
Bw. Lukuta pia kwa niaba ya watumishi aliushukuru Uongozi wa Wizara kwa kufanikisha ziara hii muhimu kwa watumishi kufahamu na kujione Miradi inayosimamiwa na Wizara.
![]() |
Ziara hiyo ililenga kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo mkubwa, hususan jinsi unavyozingatia uhifadhi wa mazingira, ulinzi wa viumbe hai katika maeneo yanayopitiwa na manufaa kwa jamii katika maisha ya kila siku na ujuzi.
“Utekelezaji wa mradi huu wa kimkakati umezingatia sana uhifadhi wa mazingira na kuleta manufaa kwa jamii zinazouzunguka. Mradi huu unaounganisha Tanzania na Uganda na ni mojawapo ya miradi mikubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki, ukiwa na lengo la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Bandari ya Tanga, Tanzania,” alisema Lukuta.
Kwa upande wake, Bw. Thomas De Mauleon Mwakilishi wa Kampuni ya EACOP, alisema mradi huo una manufaa makubwa kwa Watanzania, si tu kiuchumi bali pia kijamii na kitaalamu.
Aidha, amesema mpaka sasa mradi umeweza kutoa ajira za moja kwa moja kwa Watanzania 10,000, huku wananchi 170 wakipatiwa mafunzo maalum ili kufikia viwango vya kimataifa katika ujenzi wa miradi ya mafuta na gesi.
Pia, kupitia miradi ya kijamii, EACOP imeboresha barabara na huduma za maji katika maeneo yanayopakana na Mradi. Takribani kilomita 27 za barabara za changarawe zimeboreshwa, zikiwemo: Barabara ya Kagongwa hadi Sojo (km 18), Handeni kuelekea Kambi Na. 15 (km 2.1), barabara ya kuunganisha eneo kuu la Mradi Chongoleani (km 7.2).
Hatua hizi zinaongeza urahisi wa usafirishaji, kuunganisha jamii na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika maeneo yanayopitiwa na mradi.
Waziri Mavunde Apongeza Ushirikiano Benki Ya CRDB na Tume ya Madini Uwezeshaji Wachimbaji Wadogo wa Madini
RC DENDEGO AMPA TANO DKT SAMIA UTEKELEZAJI KWA VITENDO MRADI WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Nishati📍Singida
Katika nchi inayokumbwa na changamoto za kiafya, mazingira na umasikini, nishati safi ya kupikia si tu hitaji la msingi bali ni kichocheo cha maendeleo ya kweli kwa watu na Taifa kwa ujumla.
Katika kukabiliana na ukataji miti ambapo takribani asilimia 16 ya eneo la nchi tayari limegeuka kuwa janga, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ilizindua mkakati wa kitaifa wa nishati safi ya kupikia unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya watu wanaachana na matumizi ya kuni na mkaa ifikapo mwaka 2034.
Akizungumza ofisini kwake leo tarehe 23 Februari 2026 mara baada ya kupokea ujumbe wa wataalamu kutoka Wakala wa Nishati Vijijini - REA waliopo mkoani Singida kwa ajili ya kuutambulisha mradi wa uuzwaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku, Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara katika utekelezaji wa mkakati wa nishati safi ya kupikia.
Vilevile Mhe Dendego amesema kuwa Rais Samia ni kinara wa utekelezaji wa Nishati safi Afrika hivyo mkoa wa Singida upo tayari na utaanza kugawa majiko hayo banifu katika wilaya zote za mkoa wa Singida ili mpaka kufikia mwaka 2030 mkoa huo uwe umetengeneza alama kubwa kwa wananchi wake kabla hata ya kufikia mwaka 2034.
Pia, amesema kuwa mkoa wa Singida umepokea mitungi ya gesi zaidi ya 18,000 ambayo imesambazwa kwa wananchi ili kutokomeza kabisa nishati chafu ya kupikia.
Kwa upande wake Mhandisi Raya Majallah kutoka REA-Idara ya Nishati Jadidifu na Teknolojia Mbadala akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Singida ameutambulisha mradi wa uuzwaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika mkoa huo ambapo amesema kuwa Wakala wa Nishati Vijijini umeandaa mpango huo wa uuzaji wa majiko banifu 200,000 kwa bei ya ruzuku yenye ufanisi mkubwa katika utumiaji wake.
Mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kuni na mkaa kidogo ili kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati Pamoja na athari za moshi zitokanazo na matumizi katika majiko ya kawaida.
Mhandisi Majallah amesema kuwa mikataba hiyo ilisainiwa Mei 9, 2025 na itatekelezwa ndani ya miezi 15 ambapo gharama ya mradi huo ni Shilingi Milioni 340,288,200 kwa mkoa wa Singida na ruzuku inayotolewa na wakala wa nishati vijijini-REA ni shilingi milioni 289,230,504.47 sawa na asilimia 85 ya gharama ya mradi huku wananchi wakichangia Shilingi 51,057,691.53 sawa na asilimia 15 ya gharama ya mradi.
MWISHO
SERIKALI YATOA BILIONI 8 KUJENGA KITUO CHA UMEME IMALILO-SIMIYU
📌 Kituo cha Imalilo kukamilika Mei 2026, kuimarisha ubora wa umeme Bariadi
📌 Serikali yatoa Shilingi Bilioni 8 kugharamia mradi kwa asilimia 100
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya umeme inayotekelezwa Mkoani Simiyu kwa lengo la kujionea maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo na kuhakikisha inakamilika kwa wakati.
Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na ujenzi wa Kituo cha Kupokea na Kusambaza Umeme cha Imalilo pamoja na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 220 (220kV) kutoka Shinyanga hadi Simiyu.
Akizungumza mara baada ya ziara hiyo iliyofanyika tarehe 21 Februari 2026, Bw. Twange alisema mradi wa Kituo cha Imalilo ulianza kutekelezwa mwezi Oktoba 2025 na wataalamu wa ndani wa Shirika, na unatarajiwa kukamilika ifikapo Mei 2026.
“Baada ya muda mrefu tumeanza kutekeleza mradi huu kupitia wataalamu wetu wa ndani ambapo tulianza mwezi Oktoba 2025, na tunatarajia kuukamilisha mwezi Mei 2026,” alisema Bw. Twange.
Alifafanua kuwa kwa sasa wananchi wa Bariadi wanategemea umeme kutoka mikoa jirani ya Shinyanga, Mwanza na Mara, hali inayosababisha kupungua kwa ubora wa umeme kutokana na umbali mrefu unaosafiri.
Alisema kukamilika kwa Kituo cha Imalilo kutaondoa changamoto hiyo na kuimarisha miundombinu ya umeme, hivyo kuhakikisha wananchi wa Bariadi wanapata umeme wa uhakika kuanzia Juni 2026.
“Kwa sasa wananchi wa Bariadi wanategemea umeme kutoka mikoa ya Mwanza, Mara na Shinyanga, hali inayosababisha ubora wa umeme kupungua. Ujenzi wa kituo hiki utaimarisha miundombinu na kuondoa changamoto hizo kuanzia Juni 2026,” aliongeza.
Kwa sasa utekelezaji wa mradi wa Kituo cha Kupokea na Kusambaza Umeme cha Imalilo umefikia asilimia 20.75. Mradi huo unagharimu takribani Shilingi bilioni 8, fedha zinazofadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya kwanza
TAIFA GAS WAKUTANA NA WADAU KUWEKA MIKAKATI YA KUTOA HUDUMA BORA ZAIDI KWA WATEJA
habariINEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO

Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma waliokua katika kituo cha mafunzo cha Maposeni Sekondari wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi.
Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma waliokua katika kituo cha mafunzo cha Josephat Mokuwa wakisikiliza nasaha za viongozi wa Uchaguzi.
.jpeg)

.jpeg)







































.jpeg)
.jpeg)


