HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

COUNTDOWN TO SEPT 1: MV LIEMBA FINAL TRIALS UNDERWAY

August 16, 2026 Add Comment

  

By Staff Writer - Kigoma

KIGOMA — The horn of MV Liemba echoed across Lake Tanganyika again over the weekend for the first time in more than eight years, as Minister for Transport Prof. Makame Mbarawa led the first phase of technical  trials of the newly rehabilitated vessel. 

WMA YASHIRIKI CRDB BANK MARATHON 2026

August 16, 2026 Add Comment

  

 Na WMA – Dar es Salaam

16 Agosti 2026

Wafanyakazi wa Wakala wa Vipimo (WMA) wameshiriki katika CRDB Bank Marathon 2026, iliyofanyika jijini Dar es Salaam, ambapo watumishi kutoka Makao Makuu Dodoma na WMA Mkoa wa Dar es Salaam waliungana na washiriki wengine katika mbio hizo.

FEDHA ZA CSR ZA BARRICK NORTH MARA ZAENDELEA KUFANIKISHA MIRADI YA KUBORESHA ELIMU TARIME

August 16, 2026 Add Comment

  


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (wa pili kulia), akifurahi kuzindua mradi wa jengo la utawala la Shule ya Sekondari Mjini Kati uliotekelezwa kwa fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kutoka mgodi wa Barrick North Mara. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele na viongozi wengine wa wilaya.

TAKUKURU YAKABIDHI VIFAA MUHIMU VYA WATOTO WACHANGA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA -BOMBO

August 16, 2026 Add Comment




TAASISI ya Kuzuia na Kupambana ana Rushwa nchini (TAKUKURU) imekabidhi vifaa muhimu vya kisasa kwa ajili ya kuimarisha huduma kwa watoto wachanga hususani waliozaliwa kabla ya wakati (njiti) katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo.

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo Leo Agosti 15,2026 imepokea vifaa muhimu vya kisasa kwa ajili ya kuimarisha huduma kwa watoto wachanga, hususan waliozaliwa kabla ya wakati.

Vifaa hivyo, ambavyo ni Phototherapy na Infant Warmer, vimetolewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini-TAKUKURU ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Hospitali ya Bombo katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Akikabidhi vifaa hivyo katika hafla fupi iliyofanyika Hospitalini hapa, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU nchini, Bw. Crispin Chalamila, amesema taasisi hiyo imeamua kutoa msaada huo baada ya kuona juhudi zinazofanywa na Hospitali ya Bombo katika kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Tanga wanapata huduma bora za afya.

Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo, Dkt. Husein Mangaa, ameishukuru TAKUKURU kwa msaada huo wa thamani kubwa na kwamba vitaongeza uwezo wa hospitali katika kutoa huduma kwa watoto wachanga wanaohitaji uangalizi maalum.

Naye Daktari Bingwa wa Watoto, Dkt. Mohamed Saleh, ameipongeza TAKUKURU kwa kuunga mkono juhudi za hospitali, akieleza kuwa vifaa hivyo vitasaidia wataalam kutoa huduma kwa ufanisi zaidi kwa watoto wachanga.

Uongozi wa Hospitali ya Bombo umeeleza kuwa upatikanaji wa vifaa hivyo ni hatua nyingine muhimu katika kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga na maeneo jirani.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Tanga, Dadi Kolimba ambaye alimwakilisha mkuu wa mkoa wa Tanga na viongozi kutoka timu ya Afya ya mkoa wa Tanga ikiongozwa na Kaimu Mganga mkuu wa Mkoa wa Tanga Bwana Imani Clemence.












WAZIRI KABUDI -SERIKALI ITAENDELEA KUTHAMINI MCHANGO WA LUKUVI

August 16, 2026 Add Comment



Na Mwandishi wetu-Iringa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe. Prof, Palamagamba Kabudi amesema Serikali itaendelea kuheshimu na kuthamini mchango wa kiuongozi uliotolewa na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu) Marehemu William Lukuvi.

Hayo ameyasema  wakati wa ibada ya Misa Takatifu ya kumaliza Msiba  iliyofanyika nyumbani kwa Marehemu Idodi Mkoani Iringa na kuhudhuriwa na wananchi na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali.

Alisema, “Enzi za uhai wake Waziri Lukuvi alinisaidia kufahamu shughuli mbalimbali za Bunge na serikali na hivyo kupata weledi mzuri mambo mengi kutokana na uzoefu aliyokuwa nao,”


Aidha uwezo wake wa kusimamia nidhamu ipasavyo Bungeni ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano kati ya Serikali na Bunge ilimfanya aendelee kuaminiwa katika kazi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu.

Kwa Upande Mama Germana Lukuvi Mjane wa Marehemu ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe, Rais Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kushikamana na familia tangu walipopata msiba.

Awali Mbunge wa Isimani Mhe, Emanuela Mtatifikolo alisema Marehemu Lukuvi ataendelea kuishi kwenye mioyo ya wananchi wa Isimani, kwa mageuzi makubwa ya maendeleo aliyoyafanya.


“Uwakilishi wake kwa wananchi wa Jimbo la isimani na kwa kushirikiana na Serikali aliwezesha Jimbo la Isimani kunufaika na ujenzi wa barabara ya lami uimarishaji wa Huduma za afya na kuendelea kuboresha miundo mbinu ya elimu szambamba na umeme,” alibainisha




MWISHO



NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA AGGREY MWANRI AWA MGENI RASMI MKUTANO WA HADHARA UBUNGO

August 15, 2026 Add Comment

Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Aggrey Mwanri (MCC), leo Agosti 15, 2026, amekuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano wa Hadhara wa Jimbo la Ubungo, ulioandaliwa na Mbunge wa Jimbo hilo, Prof. Kitila Mkumbo, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji.


Kabla ya kushiriki mkutano huo, Ndugu Mwanri alipokewa katika Ofisi za CCM Mkoa wa Dar es Salaam na Sekretarieti ya CCM Mkoa, chini ya Katibu wa CCM Mkoa, Ndugu Mkandawire.

Aidha, alipokea taarifa fupi kuhusu utendaji wa Chama katika Mkoa huo na kuwashukuru viongozi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa usimamizi mzuri wa Chama na Serikali.

Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Mwanri amesisitiza umuhimu wa Wabunge, Madiwani pamoja na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kufanya mikutano ya hadhara mara kwa mara ili kuwapa wananchi mrejesho kuhusu utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na CCM wakati wa Uchaguzi.

Aidha, amewasihi wananchi kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akieleza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Dar es Salaam na maeneo mengine nchini.

Kwa upande wake, Prof. Kitila Mkumbo aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM mbele ya wananchi wa Jimbo la Ubungo, akieleza hatua zilizochukuliwa katika kuboresha miundombinu, hususan sekta ya barabara.

Prof. Kitila amesema ataendelea kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi na Serikali katika kuhakikisha wananchi wa Ubungo wanaendelea kupata huduma na maendeleo yanayostahili.




KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE.

KAMATI YA BUNGE YAISHAURI SERIKALI KUIONGEZA WATAALAM OSHA

August 15, 2026 Add Comment
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Chakoma, akifanya majumuisho ya michango ya Wajumbe wa Kamati katika kikao cha Kamati hiyo kilicholenga kupitia taarifa ya utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Namba 297, Toleo ya 2023 katika mwakawa fedha 2025/2026.

RAIS DKT.SAMIA SULUHU HASSAN KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22

August 15, 2026 Add Comment

 

*******

Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) chenye uwezo wa kuzalisha Megawati 2,115, tarehe 22 Agosti 2026, katika eneo la mradi lililopo Rufiji, Mkoa wa Pwani.

Amesema hayo tarehe 15 Agosti, 2026 jijini Dar es Salaam  katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi huo utakaohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wageni kutoka ndani na nje ya nchi, wananchi na wadau wa maendeleo.

" Uzinduzi huu wa mradi wa umeme wa  Julius Nyerere ni tukio la kihistoria na hatua muhimu katika safari ya Tanzania ya kujenga mfumo wa nishati ya uhakika nchini, sambamba na kuchochea shughuli za uzalishaji, uwekezaji na ukuaji wa uchumi, huu ni mradi mkubwa zaidi wa kuzalisha umeme kuwahi kutekelezwa nchini kwa kutumia fedha za ndani za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukiwa na uwekezaji wa takribani Shilingi trilioni 7.452." Amesema Mhe. Ndejembi

Akifafanua kuhusu mradi huo, amesema JNHPP imeendelea kuongeza kiwango cha umeme kinachoingia katika Gridi ya Taifa na hivyo kusaidia kupunguza changamoto za upungufu wa uzalishaji zilizokuwa zikichangia mgao wa umeme nchini, 

ambapo hadi tarehe 31 Mei 2026, kituo hicho kilikuwa kimezalisha takribani asilimia 44.9  ya umeme wote uliozalishwa na kuingia katika Gridi ya Taifa katika kipindi cha mwaka mmoja

Hivyo kituo hicho kimekuwa kikichangia takribani nusu ya umeme wote unaotumika nchini Tanzania.

Kuhusu gharama za mradi huo, Mhe. Ndejembi amesema fedha iliyotumika kujenga mradi huo ni takriban dola za Marekani Bilioni 3.35 sawa na Shilingi za Tanzania Trilioni 7.452 ambapo pamoja na mradi huo kukusudiwa kuzalisha umeme, utasaidia pia kwenye kudhibiti mafuriko katika mto Rufiji, kilimo cha umwagiliaji, utalii na matumizi ya binadamu.

Ameeleza kuwa ujenzi wa mradi wa JNHPP ulianza Juni 2019 na kukamilika Machi 2025 ambapo uwezo wa Bwawa la kutunza maji ni Mita za ujazo Bilioni 33 (Takribani mara 10 ya Bwawa la Mtera). Bwawa hili ni ziwa la kujenga na linashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika maziwa yaliyoko nchini (Baada ya Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa) huku kituo cha kuzalisha umeme cha JNHPP kinashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika bara la Afrika.

Ameongeza kuwa uwekezaji wa JNHPP unaendana moja kwa moja na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ambapo mradi huo  ni sehemu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali za kuongeza uzalishaji wa umeme, kuimarisha Gridi ya Taifa na kuweka mazingira bora kwa uchumi kukua kwa kasi.

Katika mkutano huo Waziri Ndejembi amewaalika  Watanzania wote kufuatilia na kushiriki katika tukio hilo ambalo ni kielelezo cha mafanikio  makubwa katika historia ya sekta ya nishati na maendeleo ya Taifa.






DG CHALAMILA: HATUTAMUANGUSHA RAIS DKT .SAMIA SULUHU VITA DHIDI YA RUSHWA

August 15, 2026 Add Comment

 




Na Oscar Assenga, Kilindi

MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Crispian Chalamila amemuahidi Rais Samia Suluhu Hassan kuwa taasisi hiyo itaendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kuhakikisha vita dhidi ya rushwa nchini vinafanikiwa.

Chalamila alisema hayo  wakati akizindua jengo jipya la ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Kilindi, mkoani Tanga, akisema Serikali imeendelea kuiwezesha taasisi hiyo kwa rasilimali watu, fedha na vitendea kazi ili kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa.

Alisema uwekezaji huo ni ishara ya dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu katika kuhakikisha TAKUKURU inakuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

“Kwa niaba ya menejimenti ya TAKUKURU, nitoe shukrani za dhati kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha taasisi hii kwa rasilimali watu, vitendea kazi na fedha,” alisema.

Chalamila alisema uwezeshaji huo umewezesha taasisi kujenga ofisi katika mikoa na wilaya mbalimbali, jambo linalowapa watumishi mazingira bora ya kufanyia kazi na wananchi kupata huduma kwa mazingira rafiki.


Ofisi 93 kufikia 2027

Chalamila alisema TAKUKURU imeweka mkakati wa kutenga bajeti kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa ofisi zake, huku akieleza kuwa taasisi hiyo ina ofisi 145 katika mikoa yote 26, wilaya 111 na vituo maalumu sita.

Alisema kati ya ofisi hizo, majengo 70 yanamilikiwa na TAKUKURU na yanapatikana katika mikoa 23, wilaya 46 na kituo maalumu kimoja.

“Majengo yanayoendelea kujengwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 na 2026/2027 ni 23, ambayo yanajumuisha ofisi tatu za mikoa na ofisi 20 za wilaya,” alisema.

Alisema kukamilika kwa miradi hiyo kutafanya hadi mwaka 2027 TAKUKURU kuwa na majengo 93 yanayomilikiwa na taasisi hiyo.

Hata hivyo, alisema bado kuna ofisi 52 ambazo hazijafikiwa na mpango huo wa ujenzi, zikiwa katika mikoa miwili, wilaya 45 na vituo maalumu vitano.

Kwa upande wa jengo la TAKUKURU Kilindi, Chalamila alisema limegharimu Sh450.7 milioni hadi kukamilika, ikiwa ni ongezeko la Sh3.1 milioni, sawa na asilimia 0.7 ya bajeti ya awali.

Alisema ongezeko hilo lilitokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa mradi.

Aliwapongeza wataalamu wa TAKUKURU, Mkoa wa Tanga na Wilaya ya Kilindi kwa kuhakikisha ujenzi wa jengo hilo unakamilika kwa wakati.

Pia aliwataka watumishi wa TAKUKURU katika wilaya ya  Kilindi na maeneo mengine yenye majengo mapya kuyatunza pamoja na vitendea kazi walivyopewa ili yaweze kutumika kwa muda mrefu.

“Serikali imewawezesha kwa kiwango kikubwa. Hilo ni deni ambalo tunapaswa kulilipa kwa kufanya kazi kwa bidii na weledi zaidi ili dhamira ya Serikali ya kuitokomeza rushwa nchini itimie,” alisema.

DC aomba jenereta

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Hashim Mgandilwa, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuziwezesha taasisi zake kuwa na miundombinu bora inayorahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mgandilwa alisema ujenzi wa jengo hilo ni hatua muhimu kwa wilaya hiyo, ambayo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya upungufu wa miundombinu ya ofisi.

Hata hivyo, aliomba TAKUKURU kuangalia uwezekano wa kuiwezesha ofisi hiyo kupata jenereta kutokana na changamoto ya kukatika kwa umeme katika eneo hilo.

“Jengo ni zuri, lakini haitakuwa na maana kama mwananchi akija kupata huduma anaambiwa umeme umekatika. Tunaomba muone namna ya kupata jenereta ili huduma ziendelee muda wote,” alisema.

Alisema Serikali tayari imeweka mpango wa kuimarisha umeme katika eneo hilo na imetenga Sh98 milioni kwa ajili ya ujenzi wa kituo kidogo cha kupoza umeme.

TAKUKURU Kilindi yapata ofisi baada ya miaka 20

Kwa upande wake, Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Ramadhan Ndwatah, alisema kabla ya kupata jengo hilo, taasisi hiyo ilifanya kazi katika majengo ya kupanga kwa takribani miaka 20.

Alisema kuanzia mwaka 2005 hadi 2010 walikuwa katika majengo ya kupanga Kata ya Songe, kabla ya kuhamia Kata ya Bokwa, Kijiji cha Legeza Mwendo, ambako walikaa hadi mwaka 2026.

Ndwatah alisema hali hiyo ilisababisha changamoto mbalimbali, ikiwamo majengo kutokidhi mahitaji ya kisasa ya ofisi, changamoto za mawasiliano na ulazima wa kufanya ukarabati mara kwa mara.

Alisema pia kuwepo kwa ofisi katika majengo ya makazi ya watu kulikuwa kunawafanya baadhi ya wananchi kukosa uhuru wa kufika kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa utulivu.

“Tunamshukuru Mkurugenzi Mkuu kwa uamuzi wa kutujengea jengo hili la kisasa. Litasaidia wananchi wa Kilindi kufika kwa uhuru na kupata huduma katika mazingira bora,” alisema.

Jengo hilo jipya linatarajiwa kuongeza ufanisi wa TAKUKURU Wilaya ya Kilindi katika kutekeleza majukumu yake, ikiwamo kupokea taarifa na malalamiko ya wananchi kuhusu vitendo vya rushwa.

TRAMEPRO: VIJANA WALINDE MAZINGIRA, WAJENGE UCHUMI WA KIJANI

Kajunason August 15, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO) limewataka vijana kutumia ubunifu, sayansi na teknolojia kama nyenzo za kujenga uchumi, kuzalisha ajira na kulinda mazingira, likisisitiza kuwa wao ndiyo nguvu ya mabadiliko ya sasa na si viongozi wa kesho pekee.

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa TRAMEPRO, Boniventura Ferdinand Mwalongo, katika maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani yaliyofanyika Agosti 15, 2026. Amesema Tanzania ina takribani vijana milioni 20.6 wenye umri wa miaka 15 hadi 35, sawa na asilimia 34.4 ya wananchi wote kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, hivyo ni muhimu kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Mwalongo amesema dunia inaingia kwa kasi katika matumizi ya akili mnemba (AI), teknolojia za kidijitali, bioteknolojia na nishati jadidifu, hali inayowalazimu vijana kujikita katika maarifa, utafiti na ubunifu ili wawe wabunifu wa teknolojia badala ya kuwa watumiaji pekee wa teknolojia zinazobuniwa na wengine.

Ameeleza kuwa licha ya changamoto zinazowakabili vijana, zikiwemo ukosefu wa ajira, mitaji, ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko, taarifa potofu na athari za mabadiliko ya tabianchi, bado wana nafasi kubwa ya kubadilisha changamoto hizo kuwa fursa kupitia ujasiriamali, matumizi sahihi ya teknolojia na uwekezaji katika sekta mbalimbali za uzalishaji.

Kwa mujibu wa TRAMEPRO, ulinzi wa mazingira unapaswa kuwa sehemu ya maisha ya kila kijana kwani maendeleo endelevu hayawezi kupatikana bila kuhifadhi udongo, maji, misitu, hewa na bioanuwai. Shirika hilo limesisitiza kuwa vijana wanapaswa kuwa walinzi wa rasilimali za asili huku wakizitumia kwa busara ili kunufaisha kizazi cha sasa na kijacho.

Aidha, Mwalongo amesema Tanzania ina utajiri mkubwa wa mimea tiba na maarifa ya jadi ambayo yanaweza kuwa chanzo cha ajira, utafiti na uchumi wa kijani iwapo yataendelezwa kwa kuzingatia misingi ya kisayansi, ubora na sheria. Amewahimiza vijana kujitokeza kuwekeza katika kilimo cha mimea tiba, uchakataji, uzalishaji wa bidhaa zenye thamani, teknolojia na biashara zinazohusiana na sekta hiyo.

TRAMEPRO pia imeiomba Serikali na wadau wa maendeleo kuendelea kuwekeza katika elimu, tafiti, vituo vya ubunifu, mitaji, viwanda na masoko ili kuwajengea vijana uwezo wa kujitegemea na kuzalisha ajira. Shirika hilo limehimiza familia, viongozi wa dini, wazee wa mila, mashirika ya kiraia na sekta binafsi kushiriki katika malezi na uwezeshaji wa vijana wenye maadili, maarifa na uwezo wa kushindana katika uchumi wa dunia.

Akihitimisha ujumbe wake, Mwalongo amewataka vijana kutambuliwa kwa kazi, ubunifu, uadilifu na mchango wao katika maendeleo ya taifa badala ya idadi yao, akisisitiza kuwa uwekezaji kwa vijana wa leo ndiyo msingi wa kujenga Tanzania na Afrika yenye uchumi shindani, mazingira salama na maendeleo endelevu.

DKT.SAMIA SULUHU HASSAN KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22

August 15, 2026 Add Comment



Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP) chenye uwezo wa kuzalisha Megawati 2,115, tarehe 22 Agosti 2026, katika eneo la mradi lililopo Rufiji, Mkoa wa Pwani.


Amesema hayo tarehe 15 Agosti, 2026 jijini Dar es Salaam katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi huo utakaohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wageni kutoka ndani na nje ya nchi, wananchi na wadau wa maendeleo.


" Uzinduzi huu wa mradi wa umeme wa Julius Nyerere ni tukio la kihistoria na hatua muhimu katika safari ya Tanzania ya kujenga mfumo wa nishati ya uhakika nchini, sambamba na kuchochea shughuli za uzalishaji, uwekezaji na ukuaji wa uchumi, huu ni mradi mkubwa zaidi wa kuzalisha umeme kuwahi kutekelezwa nchini kwa kutumia fedha za ndani za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukiwa na uwekezaji wa takribani Shilingi trilioni 7.452." Amesema Mhe. Ndejembi


Akifafanua kuhusu mradi huo, amesema JNHPP imeendelea kuongeza kiwango cha umeme kinachoingia katika Gridi ya Taifa na hivyo kusaidia kupunguza changamoto za upungufu wa uzalishaji zilizokuwa zikichangia mgao wa umeme nchini,
ambapo hadi tarehe 31 Mei 2026, kituo hicho kilikuwa kimezalisha takribani asilimia 44.9 ya umeme wote uliozalishwa na kuingia katika Gridi ya Taifa katika kipindi cha mwaka mmoja
Hivyo kituo hicho kimekuwa kikichangia takribani nusu ya umeme wote unaotumika nchini Tanzania.


Kuhusu gharama za mradi huo, Mhe. Ndejembi amesema fedha iliyotumika kujenga mradi huo ni takriban dola za Marekani Bilioni 3.35 sawa na Shilingi za Tanzania Trilioni 7.452 ambapo pamoja na mradi huo kukusudiwa kuzalisha umeme, utasaidia pia kwenye kudhibiti mafuriko katika mto Rufiji, kilimo cha umwagiliaji, utalii na matumizi ya binadamu.


Ameeleza kuwa ujenzi wa mradi wa JNHPP ulianza Juni 2019 na kukamilika Machi 2025 ambapo uwezo wa Bwawa la kutunza maji ni Mita za ujazo Bilioni 33 (Takribani mara 10 ya Bwawa la Mtera). Bwawa hili ni ziwa la kujenga na linashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika maziwa yaliyoko nchini (Baada ya Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa) huku kituo cha kuzalisha umeme cha JNHPP kinashika nafasi ya nne kwa ukubwa katika bara la Afrika.


Ameongeza kuwa uwekezaji wa JNHPP unaendana moja kwa moja na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ambapo mradi huo ni sehemu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali za kuongeza uzalishaji wa umeme, kuimarisha Gridi ya Taifa na kuweka mazingira bora kwa uchumi kukua kwa kasi.


Katika mkutano huo Waziri Ndejembi amewaalika Watanzania wote kufuatilia na kushiriki katika tukio hilo ambalo ni kielelezo cha mafanikio makubwa katika historia ya sekta ya nishati na maendeleo ya Taifa.

SERIKALI YAWEKA MKAKATI WA KUPUNGUZA MUDA WA MELI ZA MAFUTA BANDARINI

August 15, 2026 Add Comment




DAR ES SALAAM. 


Serikali imeweka mkakati wa kupunguza muda ambao meli za mafuta hutumia bandarini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza ufanisi katika upokeaji, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za mafuta nchini.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, anayeshughulikia Mafuta na Gesi Dkt. James Mataragio, amesema hayo wakati wa ziara ya kukagua miundombinu ya mafuta katika eneo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER), Leo Augosti 14,2026 Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mataragio amesema Serikali inalenga kuhakikisha meli zinazowasili nchini zinapata huduma kwa wakati, zinashusha mafuta kwa ufanisi na kuondoka bandarini bila ucheleweshaji usio wa lazima.

“Ni matarajio ya Serikali kuona meli zikifika, zinashusha mafuta na kuondoka. Kila taasisi inapaswa kufahamu jukumu lake na kujipanga ipasavyo,” amesema.


Ameeleza kuwa moja ya changamoto zinazochangia meli kukaa bandarini kwa muda mrefu ni kasi ndogo ya upokeaji na uondoshwaji wa mafuta katika baadhi ya maghala binafsi. Hali hiyo husababisha meli kusubiri na kuongeza msongamano bandarini.

Kutokana na changamoto hiyo, Dkt. Mataragio ameutaka Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuimarisha usimamizi wa wamiliki wa maghala binafsi na kuhakikisha wanaweka miundombinu inayokidhi mahitaji ya uendeshaji.


Amesema wamiliki wa maghala wanapaswa kuboresha pampu na vifaa vingine vinavyotumika kupokea mafuta, hasa vinapokuwa vimechakaa au havina uwezo unaohitajika.



Kwa mujibu wa Dkt. Mataragio, ucheleweshaji wa meli bandarini huongeza gharama za uendeshaji, zikiwemo gharama za meli kusubiri, ambazo hatimaye zinaweza kuathiri bei ya mafuta kwa mwananchi.


Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon, amesema taasisi hiyo itakutana na wadau muhimu katika sekta ya mafuta, wakiwemo kampuni za uuzaji wa mafuta (OMCs) na TPA, kwa ajili ya kupitia na kuboresha Mwongozo wa Taratibu za Uendeshaji (Standard Operating Procedure Manual).


Amesema mapitio hayo yanalenga kuweka wazi majukumu, muda wa utekelezaji na uwajibikaji wa kila mdau katika mchakato wa upokeaji na uhamishaji wa mafuta.


Hatua hiyo inatarajiwa kuimarisha uratibu kati ya meli na maghala ya kupokea mafuta, kupunguza muda wa meli kukaa bandarini na kudhibiti gharama zinazotokana na ucheleweshaji.


Katika ziara hiyo, Dkt. Mataragio aliambatana na Kamishna wa Mafuta kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Goodluck Shirima; Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon; Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Abed Gallus Abed; pamoja, Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Mashariki, Mhandisi Lorivii Long’idu na wataalam kutoka Wizara ya Nishati.