HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TEA YAFUNGUA MILANGO YA ELIMU BORA PEMBA

September 10, 2026 Add Comment
PEMBA — Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bw. Khamis Abdulla Said, ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa kuendelea kufadhili miradi ya maendeleo ya elimu Unguja na Pemba, akisema hatua hiyo inasaidia kuboresha mazingira ya ujifunzaji na kuinua ubora wa elimu visiwani humo.

MHANDISI MRAMBA AMSHUKURU MAKAMU WA RAIS KWA KUACHA ALAMA SEKTA YA NISHATI

September 09, 2026 Add Comment


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba, amempongeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa mchango mkubwa alioutoa katika kuendeleza Sekta ya Nishati wakati akiwa Waziri wa Nishati.


Akizungumza wakati wa kumuaga Makamu wa Rais leo, Septemba 09, 2026, katika Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma, Mha. Mramba amesema Mhe. Ndejembi ameiongoza sekta hiyo katika kipindi kilichokuwa na changamoto mbalimbali za kimataifa, ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia.

Amesema, pamoja na changamoto hizo, kupitia weledi na uongozi bora, Mhe. Ndejembi alihakikisha upatikanaji wa mafuta nchini unaendelea kuwa wa uhakika na bei zinaendelea kuwa himilivu kwa wananchi.

Mha. Mramba amefafanua kuwa katika kipindi cha uongozi wa Mhe. Ndejembi, kumeshuhudiwa kasi katika utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi, sambamba na kuimarika kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu ya nishati, ikiwemo Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), ambao utekelezaji wake umeongezeka kutoka takribani asilimia 79 hadi kufikia asilimia 92.

Aidha, amesema Mhe. Ndejembi ameacha alama katika kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme nchini kuelekea lengo la Megawati 8,000 ifikapo mwaka 2030. Vilevile, amewezesha utekelezaji wa miradi ya kupeleka umeme katika vitongoji 9,009 pamoja na kukamilika kwa Mradi wa Julius Nyerere Hydro Power Project (JNHPP), wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 2,115.

Katika eneo la nishati safi, Mha. Mramba amesema matumizi ya nishati safi ya kupikia yameongezeka na kufikia asilimia 28.9, huku idadi ya vituo vya kujaza gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) ikiongezeka kutoka 11 hadi 19.


Ameongeza kuwa hatua kubwa pia zimepigwa katika matumizi ya magari yanayotumia umeme, hatua ambayo inaendelea kuimarisha nafasi ya Tanzania katika kukuza matumizi ya nishati safi na kuwa kitovu cha nishati katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Kwa niaba ya Wizara ya Nishati na taasisi zake, Mha. Mramba amemshukuru Mhe. Ndejembi kwa uongozi, malezi na ushirikiano alioutoa kwa watendaji wa Wizara na taasisi zake, akiahidi kuwa Wizara itaendelea kulinda na kuendeleza misingi aliyoiweka ili Sekta ya Nishati izidi kusonga mbele.


Aidha, amemtakia Mhe. Ndejembi kheri katika majukumu yake mapya ya kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuongoza Taifa, huku akimuombea afya njema, maisha marefu na hekima katika kutekeleza majukumu hayo kwa manufaa ya Watanzania.

MAKAMU WA RAIS AAGWA RASMI NA WIZARA YA NISHATI

September 09, 2026 Add Comment



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameagwa rasmi na Menejimenti ya Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zilizo chini yake katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Kambarage Treasury Square, Dodoma. Jumatano Septemba 09, 2026.

 

Hafla hiyo imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughukia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, Menejimenti ya Wizara na Wakurugenzi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo.


Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu wa Rais amewaasa Viongozi na Watendaji hao kuendelea kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Wasaidizi wake ili waendelee kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia Watanzania.

 


Aidha, Makamu wa Rais amewataka Viongozi na Watendaji hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu na uzalendo ili kutimiza matarajio ya wananchi kwa Serikali.


Imetolewa na 

Ofisi ya Makamu wa Rais

09 Septemba 2026

Dodoma.

SALOME-MHE NDEJEMBI TUNAOMBA UENDELEE KUWA MLEZI WA WIZARA YA NISHATI

September 09, 2026 Add Comment




Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amemshukuru Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa uongozi, malezi na ushirikiano alioutoa katika kipindi cha zaidi ya miezi kumi walichofanya kazi pamoja katika Wizara ya Nishati.


Mhe. Salome ameyabainisha hayo leo Septemba 09,2026 wakati akizungumza waati wa kumuaga Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi mbaye awali alikuwa Waziri wa Nishati iliyofanyika katika ukumbi wa Hazina jijini Dodoma.


Amesema katika kipindi cha uongozi wake amejifunza umuhimu wa upendo, kuthaminiana na kushirikiana katika kutekeleza majukumu ya Serikali, akieleza kuwa kupitia Mhe. Ndejembi ameweza kuwa moja ya Manaibu Waziri bora katika Bunge na Baraza la Mawaziri.


"Katika kipindi cha uongozi wako nimejifunza mambo matatu ikiwemo upendo na kuthaminiana  na kuwa na mahusiano mazuri, kufanya kazi kwa ushirikiano pamoja na kuwa na uthubutu wa kufanya maamuzi kwa kuangalia maslahi ya Taifa bila kujali maslahi binafsi hivyo sisi kama familia ya Nishati tunaendelea kukuombea katika majukumu yako mapya uendelee kuwa na utii na hekima katika ufanyaji kazi wako". Amesisitiza Mhe. Salome.


Amesema kupitia Uongozi wa Mhe Ndejembi viongozi na watendaji wa Wizara ya Nishati wataendelea kusimamia misingi iliyowekwa  katika kuendeleza Sekta ya Nishati huku akisisitiza kukamilisha kwa wakati miradi ya maendeleo aliyoicha katika uongozi wake kipindi alichokua Waziri wa Nishati.


Sambamba na hilo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kumuamini Mhe. Deogratius Ndejembi na kumpa nafasi ya kulitumikia Taifa katika ngazi za juu za uongozi, jambo lililoendelea kuimarisha uaminifu na imani kwa Wizara ya Nishati katika utekelezaji wa majukumu yake kwa maslahi ya Taifa.


Mhe. Salome ameongeza kuwa, pamoja na kuwa Mhe. Ndejembi umeondoka katika Wizara ya Nishati, tunaomba uendelee kuwa sehemu ya familia ya Wizara ya Nishati, uwe mlezi wetu na tutakapohitaji ushauri, tunaomba utupokee  na kuwaongoza, napale tunapokosea utukosoe ili tuweze kujirekebisha na kuendelea kuijenga na kuiimarisha Sekta ya Nishati nchini.

SAPP KUFUNGUA FURSA KWA TANZANIA KUWA KITOVU CHA BIASHARA YA UMEME KUSINI MWA AFRIKA

September 09, 2026 Add Comment




📌Nchi 18 Zakutana Zanzibar kujadili usalama wa nishati ya umeme kusini mwa Afrika


📌Kuuza au kununua umeme kutaongeza mapato ya taifa na kuimarisha usalama wa nishati nchini


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar


Mikutano ya 67 ya Jumuiya ya Umeme ya Kusini mwa Afrika (SAPP) inayofanyika Zanzibar imefungua fursa mpya kwa Tanzania kuimarisha nafasi yake kama kitovu cha biashara ya umeme katika ukanda wa Kusini mwa Afrika, huku ikitarajiwa kuongeza mapato ya taifa kupitia mauzo ya umeme na kuimarisha usalama wa nishati katika ukanda huo.


Mikutano hiyo imewakutanisha wajumbe kutoka nchi wanachama 18 wa SAPP kwa lengo la kujadili masuala ya biashara ya umeme, uendeshaji wa mifumo ya umeme, uwekezaji katika miundombinu ya nishati na usalama wa nishati katika nchi zilizoko ukanda wa Kusini mwa Afrika.


Akifungua mikutano hiyo Septemba 8, 2026 katika Hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar, Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Bw. Haji Mohamed Haji, amesema kuimarishwa kwa uunganishaji wa gridi za umeme kati ya nchi wanachama kutarahisisha biashara ya umeme kuvuka mipaka na kuwezesha nchi zenye ziada ya umeme kuziuzia nchi zinazokabiliwa na upungufu wa nishati.

Amesema ushirikiano huo utaongeza ufanisi wa matumizi ya rasilimali za nishati zilizopo katika ukanda, kupunguza gharama za uzalishaji wa umeme na kuimarisha uthabiti wa mifumo ya umeme.


“Kwa kuunganisha mifumo ya gridi za taifa na kuwezesha biashara ya umeme kuvuka mipaka, nchi za SADC zitaweza kupunguza changamoto za upungufu wa umeme, kuimarisha uthabiti wa gridi na kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi,” amesema Haji.

Kwa Tanzania, mikutano hiyo inafanyika wakati nchi ikiwa imeongeza kwa kiwango kikubwa uwezo wake wa kuzalisha umeme kupitia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) uliokamilika pamoja na uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya usafirishaji wa umeme inayounganisha maeneo mbalimbali ya nchi na nchi jirani.

Ongezeko hilo la uzalishaji wa umeme linaipa Tanzania nafasi ya kunufaika zaidi na soko la kikanda la umeme kwa kuuza ziada ya nishati katika nchi wanachama wa SAPP, hatua inayotarajiwa kuongeza mapato ya taifa, kuvutia uwekezaji zaidi katika sekta ya nishati na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Akizungumza katika ufunguzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa SAPP, Mhandisi Stephen Dihwa, amesema mikutano hiyo ni jukwaa muhimu la nchi wanachama kubadilishana uzoefu, kuimarisha ushirikiano wa kiufundi na kuweka mikakati ya pamoja ya kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika, nafuu na endelevu katika ukanda.


“Mikutano hii inatoa fursa kwa kamati mbalimbali za kitaalamu za SAPP kuwasilisha kazi zao, kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la changamoto zinazoikabili sekta ya umeme. Lengo letu ni kuhakikisha wananchi katika ukanda wa Kusini mwa Afrika wanapata umeme wa uhakika, unaopatikana kwa gharama nafuu na unaozingatia uendelevu,” amesema Dihwa.


Mikutano hiyo inayofanyika kuanzia Septemba 7 hadi 11, 2026 inatarajiwa kutoa maazimio yatakayosaidia kuimarisha biashara ya umeme kati ya nchi wanachama, kuongeza uwekezaji katika miundombinu ya usafirishaji wa umeme na kuimarisha usalama wa nishati katika ukanda.


Kwa Tanzania, maendeleo hayo yanatajwa kuwa hatua muhimu katika safari ya kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza biashara ya umeme barani Afrika, huku yakifungua fursa za kuongeza mapato ya fedha za kigeni, kuimarisha usalama wa nishati na kuchangia maendeleo ya kiuchumi ya taifa.

UNESCO PUTS GIRLS AT THE HEART OF TANZANIA’S DIGITAL FUTURE

September 09, 2026 Add Comment

The room comes alive as the girls settle into their groups.

Around the tables, conversations begin.

One idea leads to another as the students share their views, listen to their colleagues and work together to understand the challenges they have been given.

As part of the UNESCO-BNU project, this is learning by participation.


The girls are not sitting back and waiting for answers.

They are thinking for themselves, exchanging ideas and challenging one another as they work towards a common solution.

You can see the teamwork taking shape.


Some students speak. Others listen carefully. Ideas are added, discussed and refined.

What looks like a simple classroom discussion is becoming something much bigger—a practical exercise in critical thinking, collaboration and confidence.


And gradually, each group begins to shape its ideas into something they can share.

The discussions continue, the ideas become clearer, and the girls prepare for the next moment.

It is time to stand up and let the whole class hear what they have created together.





BOOTCAMP AT MSALATO GIRLS SCHOOL IN DODOMA BEGAN WITH THE GIRLS TAKING AN ACTIVE

September 09, 2026 Add Comment

 BOOTCAMP — DAY ONE


DODOMA, TANZANIA — September 8, 2026.

Day One of the Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma began with the girls taking an active role in the learning process.


Working in groups, the students engaged in discussions, sharing ideas and exploring different challenges that could be addressed through technology.


The discussions gave the girls an opportunity to work together, listen to different perspectives and develop ideas as a team.

After the group discussions, the students came together for presentations.


Standing before the whole class, the groups presented the ideas they had developed during their discussions, giving each student an opportunity to participate and share what her group had explored.


Through this process, the girls were beginning to build important skills in teamwork, communication, confidence and problem-solving.


It was the first practical step of the Bootcamp—moving from discussion to presentation, and creating a foundation for the hands-on technology sessions that followed.


Day One had begun with an important lesson: ideas become more powerful when they are shared, challenged and developed together.



TEA YATENGA SH1.3 BILIONI KUJENGA HOSTELI IPA PEMBA

September 09, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imetenga takribani Sh1.3 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa hosteli katika Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar (IPA) Kampasi ya Pujini Pemba, hatua inayolenga kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia chuoni hapo.

PAWO YATAKA WANAWAKE KUSHIRIKISHWA KATIKA UJENZI WA AMANI

September 08, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KATIBU Mkuu wa Shirika la Wanawake la Kiafrika (PAWO), Dkt. Grace Kabayo, ameitaka jamii kuhakikisha wanawake wanashirikishwa kikamilifu katika maamuzi yanayohusu amani, usalama na maendeleo, akisisitiza kuwa wanawake si waathirika wa migogoro pekee bali ni viongozi na wajenzi muhimu wa amani.

NECTA: WATAHINIWA MILIONI 1.16 KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA

September 08, 2026 Add Comment


Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza kuwa Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) kwa mwaka 2026 utafanyika Septemba 9 na 10, ukihusisha watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 nchini.

Katibu Mtendaji wa NECTA, Prof. Said A. Mohamed, amesema kati ya watahiniwa hao, wavulana ni 531,467 sawa na asilimia 45, huku wasichana wakiwa 637,182 sawa na asilimia 55.


Amesema watahiniwa 1,081,204 sawa na asilimia 93 watafanya mtihani kwa Kiswahili, huku 87,445 sawa na asilimia saba wakifanya kwa lugha ya Kiingereza.


Kwa mujibu wa Prof. Mohamed, watahiniwa wenye mahitaji maalumu 4,867 pia wamesajiliwa kufanya mtihani huo. Kati yao, 82 ni wasioona, 1,591 wenye uoni hafifu, 999 wenye uziwi, 576 wenye ulemavu wa akili na 1,619 wenye ulemavu wa viungo.


Amesema masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, English Language, Sayansi na Teknolojia, Hisabati, Maarifa ya Jamii na Stadi za Kazi, pamoja na Uraia na Maadili.


Prof. Mohamed amesema mtihani huo ni wa mwisho kufanyika kwa kutumia mtaala wa sasa, huku ukilenga kupima maarifa na ujuzi walioupata wanafunzi katika miaka saba ya elimu ya msingi na kutumika katika mchakato wa uchaguzi wa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari.


Amesema maandalizi yote ya mtihani huo yamekamilika, yakiwemo usambazaji wa karatasi za mitihani na nyaraka muhimu katika halmashauri zote nchini, mafunzo kwa wasimamizi pamoja na kuweka mikakati ya kuhakikisha usalama wa vituo vya mitihani.


Amewataka wasimamizi wa mitihani kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kuzingatia kanuni za mitihani, huku wakihakikisha watahiniwa wote wanapata fursa ya kufanya mtihani kwa muda uliopangwa.


Kwa watahiniwa wenye mahitaji maalumu, amesema NECTA imeweka utaratibu wa kuwapatia maandishi ya nukta nundu kwa wasioona, maandishi yaliyokuzwa kwa wenye uoni hafifu na muda wa ziada wa dakika 20 kwa kila saa katika somo la Hisabati na dakika 10 kwa kila saa kwa masomo mengine.


Aidha, amewataka watahiniwa kuepuka vitendo vya udanganyifu, akisisitiza kuwa matokeo ya mwanafunzi atakayebainika kufanya udanganyifu yatafutwa kwa mujibu wa kanuni.


Amewataka wamiliki na wakuu wa shule kutokuingilia majukumu ya wasimamizi wakati wa mtihani, akionya kuwa NECTA inaweza kufuta kituo cha mtihani endapo itabaini uwepo wake unahatarisha usalama wa mtihani.


Pia ameitaka jamii kutoa ushirikiano kwa kuhakikisha mitihani inafanyika kwa amani na utulivu, ikiwemo kuheshimu maeneo ya mitihani na kuepuka kuingia shuleni wakati wa uendeshaji wa mtihani.


NECTA imetoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za vitendo vya udanganyifu kupitia namba 0759 360 000 au barua pepe esnecta@necta.go.tz.


Mtihani huo utafanyika Jumatano, Septemba 9, na Alhamisi, Septemba 10, 2026.

ALGERIA YATOA MKONO WA USHIRIKIANO KWA TANZANIA KATIKA SEKTA YA DAWA

Kajunason September 08, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu.

ALGIERS: Tanzania na Algeria zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza uzalishaji wa bidhaa hizo na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na la Afrika.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda vya Dawa wa Algeria, Dkt. Wassim Kouidri, katika ofisi za wizara hiyo jijini Algiers.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Matinyi alimweleza Waziri Kouidri kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania kuendeleza sekta ya viwanda vya dawa, ikiwemo kuweka vivutio maalum kwa wawekezaji.

Alisema tayari viwanda vitano vya dawa vinaendelea kujengwa nchini, huku vingine vikitazamiwa kuanzishwa katika kipindi kijacho.

“Serikali imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha viwanda vya dawa na vifaa vya tiba katika ukanda wa nchi za mashariki, kati na kusini mwa Afrika wenye watu takriban milioni 350,” alisema Balozi Matinyi.

Kwa upande wake, Waziri Kouidri aliahidi ushirikiano wa Serikali ya Algeria katika kuisaidia Tanzania kupata utaalamu wa kisasa wa utengenezaji wa dawa na vifaa tiba.

“Ni kweli, Tanzania ipo kwenye eneo zuri la kimkakati la ukanda mkubwa wa Afrika na Algeria iko tayari kushirikiana nayo kitaalamu ili kuhakikisha inafikia malengo yake,” alisema.

Aidha, Balozi Matinyi alikaribisha ziara ya Mamlaka ya Taifa ya Bidhaa za Dawa ya Algeria (ANPP), inayotarajiwa nchini Tanzania mwezi Oktoba mwaka huu kwa mwaliko wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA).

Ziara hiyo inalenga kujadili namna bora ya kuimarisha ushirikiano wa kitaalamu kati ya mamlaka hizo katika sekta ya dawa.

Tanzania pia imeendelea kujijengea heshima barani Afrika katika udhibiti wa dawa baada ya kuwa nchi ya kwanza barani humo kufikia kiwango cha daraja la tatu la ukaguzi wa dawa (ML3) mwaka 2018, chini ya tathmini ya viwango vya Shirika la Afya Duniani (WHO).

Kiwango hicho hupima ubora na ufanisi wa mifumo ya udhibiti na ukaguzi wa dawa katika nchi.

Tangu mwaka 2020, nchi nyingine tisa za Afrika zimefikia kiwango cha ML3. Nchi hizo ni Afrika Kusini, Ethiopia, Ghana, Misri, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Senegal na Zimbabwe.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna nchi ya Afrika iliyofikia kiwango cha juu zaidi cha ML4.

Kwa upande wa Algeria, nchi hiyo ni miongoni mwa vinara wa sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba barani Afrika ikiwa na viwanda 230, sawa na takriban theluthi moja ya viwanda 690 vilivyopo barani humo.

Ushirikiano huo unatarajiwa kusaidia Tanzania kuongeza uwezo wa uzalishaji wa dawa na vifaa tiba, kupunguza utegemezi wa bidhaa zinazoagizwa kutoka nje na kuongeza nafasi ya nchi katika soko la dawa la Afrika.

DODOMA GIRLS OPEN GENDER AND ICT DEBATE

September 08, 2026 Add Comment



DODOMA, September 8, 2026: Girls taking part in an Information and Communication Technology (ICT) Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma have begun exploring how gender perceptions can influence their participation in technology, while learning how digital skills can be used to address real challenges facing their communities.

The Bootcamp is part of a project implemented by UNESCO in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, aimed at promoting gender-transformative digital skills education and increasing girls’ participation in technology and Science, Technology, Engineering and Mathematics (STEM).


The first day of the Bootcamp opened with a simple but thought-provoking question: “What is sex? What is gender?”

The question sparked a discussion among the students, who shared their understanding and experiences before examining how gender roles and expectations affect their daily lives, education and access to technology.



Through the discussions, the students were encouraged to reflect on who does what, who makes decisions and who has access to opportunities at home and at school.

They also examined how social and cultural beliefs can influence the way girls view technology and their own ability to pursue careers in ICT and other STEM-related fields.

Challenging stereotypes

A major part of the training focused on challenging stereotypes that can discourage girls from participating in science and technology.


Among the perceptions discussed were the beliefs that science and technology are mainly for boys and that women are less suited to leadership positions.

Such attitudes can affect girls’ confidence, educational choices and future career opportunities, particularly in fields related to STEM.

The training therefore encourages girls to recognise these barriers and understand that their gender should not determine their ability to learn, create or lead in technology.

The discussions also highlighted the importance of addressing the digital gender gap, particularly in relation to access to ICT, the cost of technology and the knowledge and skills required to use digital tools effectively.

Technology for real-life solutions

The Bootcamp has gone beyond teaching students how to use digital devices. It is also helping them understand how technology can be applied to solve problems in education, the economy and access to essential services.

One of the areas explored by the students was the relationship between gender, ICT and water services.

The students discussed how digital technology can support the monitoring of water use, reporting of broken water infrastructure and leakages, identifying areas experiencing water shortages and using information to better understand and plan for water needs.

The exercise is intended to help the girls see technology not simply as a tool for communication or learning, but as a practical means of developing solutions to challenges affecting people in their communities.

From technology users to innovators

Another key message from the Bootcamp is the need for girls to move beyond being consumers of technology and become active creators and innovators.



The students are encouraged to contribute ideas, design and test solutions, work together and explore ways in which technology can respond to challenges affecting their schools and communities.

This approach is intended to build not only digital skills, but also confidence, creativity, problem-solving abilities and leadership among girls.

The UNESCO-BNU project places emphasis on creating opportunities for girls to develop practical digital skills and participate in activities that can strengthen their interest and confidence in technology and STEM.

For the girls at Msalato, the first day of the Bootcamp has therefore marked the beginning of a wider journey—one that seeks to change the way they see themselves in the digital world.

From discussing gender roles to exploring how ICT can help address challenges such as water access, the students are beginning to see technology as a tool for innovation, empowerment and social change.

The broader goal is to ensure that girls are not left behind in the digital transformation, but are equipped to participate, innovate and help shape the future of technology in Tanzania.

For the girls of Msalato, the digital journey has begun.

DC MPOGOLO: WALIMU NI WAZALISHAJI WA WATAALAMU NA VIONGOZI

Kajunason September 08, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu.

DAR ES SALAAM: Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amewapongeza walimu wa Kata ya Ukonga kwa mchango wao katika jamii, akisema wamekuwa msingi muhimu wa uzalishaji wa wataalamu na viongozi mbalimbali nchini.

Mhe. Mpogolo ameyasema hayo wakati wa sherehe ya walimu wa Kata ya Ukonga, inayojulikana kama UKONGA DAY, iliyofanyika Ukonga jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mpogolo amesema walimu wana nafasi kubwa katika maendeleo ya Taifa kwa kuwa ndio wanaowaandaa wanafunzi kuwa wataalamu na viongozi wanaokuja kuliongoza na kulitumikia Taifa.
Amesema mchango wa walimu hauishii darasani pekee, bali unaendelea kuonekana kupitia mafanikio ya wanafunzi wao katika nyanja mbalimbali za maisha.

Mhe. Mpogolo ametoa pongezi hizo kufuatia hotuba ya utangulizi iliyotolewa na mgeni maalum wa hafla hiyo, Mhe. Jerry Silaa, ambaye pia ni mlezi wa walimu wa Kata ya Ukonga.

Mhe. Silaa ana historia ya kipekee na eneo hilo, kwani amezaliwa katika Kata ya Ukonga na kusoma katika Shule ya Msingi Ukonga.
Katika safari yake ya maisha, amekuwa akirejea katika eneo hilo na kutoa shukrani kwa walimu wa Kata ya Ukonga, akiwatambua kuwa miongoni mwa watu waliochangia kwa kiasi kikubwa mafanikio yake.

Aidha, Mhe. Mpogolo amesema walimu ni miongoni mwa watu wanaofurahia mafanikio ya wale waliowafundisha, akieleza kuwa mafanikio ya mwanafunzi ni sehemu ya mafanikio ya mwalimu.

Amesema tofauti na baadhi ya watu ambao wanaweza kuwa na wivu wanapowaona wenzao wakifanikiwa, walimu hufurahia kuona wanafunzi wao wakipiga hatua na kufikia mafanikio makubwa.

Kwa mujibu wa Mhe. Mpogolo, hali hiyo inaonesha umuhimu wa kutambua na kuthamini mchango wa walimu katika kujenga jamii na Taifa kwa ujumla.