HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

BOOTCAMP AT MSALATO GIRLS SCHOOL IN DODOMA BEGAN WITH THE GIRLS TAKING AN ACTIVE

September 09, 2026 Add Comment

 BOOTCAMP — DAY ONE


DODOMA, TANZANIA — September 8, 2026.

Day One of the Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma began with the girls taking an active role in the learning process.


Working in groups, the students engaged in discussions, sharing ideas and exploring different challenges that could be addressed through technology.


The discussions gave the girls an opportunity to work together, listen to different perspectives and develop ideas as a team.

After the group discussions, the students came together for presentations.


Standing before the whole class, the groups presented the ideas they had developed during their discussions, giving each student an opportunity to participate and share what her group had explored.


Through this process, the girls were beginning to build important skills in teamwork, communication, confidence and problem-solving.


It was the first practical step of the Bootcamp—moving from discussion to presentation, and creating a foundation for the hands-on technology sessions that followed.


Day One had begun with an important lesson: ideas become more powerful when they are shared, challenged and developed together.



TEA YATENGA SH1.3 BILIONI KUJENGA HOSTELI IPA PEMBA

September 09, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imetenga takribani Sh1.3 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa hosteli katika Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar (IPA) Kampasi ya Pujini Pemba, hatua inayolenga kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia chuoni hapo.

PAWO YATAKA WANAWAKE KUSHIRIKISHWA KATIKA UJENZI WA AMANI

September 08, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KATIBU Mkuu wa Shirika la Wanawake la Kiafrika (PAWO), Dkt. Grace Kabayo, ameitaka jamii kuhakikisha wanawake wanashirikishwa kikamilifu katika maamuzi yanayohusu amani, usalama na maendeleo, akisisitiza kuwa wanawake si waathirika wa migogoro pekee bali ni viongozi na wajenzi muhimu wa amani.

NECTA: WATAHINIWA MILIONI 1.16 KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA

September 08, 2026 Add Comment


Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza kuwa Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) kwa mwaka 2026 utafanyika Septemba 9 na 10, ukihusisha watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 nchini.

Katibu Mtendaji wa NECTA, Prof. Said A. Mohamed, amesema kati ya watahiniwa hao, wavulana ni 531,467 sawa na asilimia 45, huku wasichana wakiwa 637,182 sawa na asilimia 55.


Amesema watahiniwa 1,081,204 sawa na asilimia 93 watafanya mtihani kwa Kiswahili, huku 87,445 sawa na asilimia saba wakifanya kwa lugha ya Kiingereza.


Kwa mujibu wa Prof. Mohamed, watahiniwa wenye mahitaji maalumu 4,867 pia wamesajiliwa kufanya mtihani huo. Kati yao, 82 ni wasioona, 1,591 wenye uoni hafifu, 999 wenye uziwi, 576 wenye ulemavu wa akili na 1,619 wenye ulemavu wa viungo.


Amesema masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, English Language, Sayansi na Teknolojia, Hisabati, Maarifa ya Jamii na Stadi za Kazi, pamoja na Uraia na Maadili.


Prof. Mohamed amesema mtihani huo ni wa mwisho kufanyika kwa kutumia mtaala wa sasa, huku ukilenga kupima maarifa na ujuzi walioupata wanafunzi katika miaka saba ya elimu ya msingi na kutumika katika mchakato wa uchaguzi wa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari.


Amesema maandalizi yote ya mtihani huo yamekamilika, yakiwemo usambazaji wa karatasi za mitihani na nyaraka muhimu katika halmashauri zote nchini, mafunzo kwa wasimamizi pamoja na kuweka mikakati ya kuhakikisha usalama wa vituo vya mitihani.


Amewataka wasimamizi wa mitihani kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kuzingatia kanuni za mitihani, huku wakihakikisha watahiniwa wote wanapata fursa ya kufanya mtihani kwa muda uliopangwa.


Kwa watahiniwa wenye mahitaji maalumu, amesema NECTA imeweka utaratibu wa kuwapatia maandishi ya nukta nundu kwa wasioona, maandishi yaliyokuzwa kwa wenye uoni hafifu na muda wa ziada wa dakika 20 kwa kila saa katika somo la Hisabati na dakika 10 kwa kila saa kwa masomo mengine.


Aidha, amewataka watahiniwa kuepuka vitendo vya udanganyifu, akisisitiza kuwa matokeo ya mwanafunzi atakayebainika kufanya udanganyifu yatafutwa kwa mujibu wa kanuni.


Amewataka wamiliki na wakuu wa shule kutokuingilia majukumu ya wasimamizi wakati wa mtihani, akionya kuwa NECTA inaweza kufuta kituo cha mtihani endapo itabaini uwepo wake unahatarisha usalama wa mtihani.


Pia ameitaka jamii kutoa ushirikiano kwa kuhakikisha mitihani inafanyika kwa amani na utulivu, ikiwemo kuheshimu maeneo ya mitihani na kuepuka kuingia shuleni wakati wa uendeshaji wa mtihani.


NECTA imetoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za vitendo vya udanganyifu kupitia namba 0759 360 000 au barua pepe esnecta@necta.go.tz.


Mtihani huo utafanyika Jumatano, Septemba 9, na Alhamisi, Septemba 10, 2026.

ALGERIA YATOA MKONO WA USHIRIKIANO KWA TANZANIA KATIKA SEKTA YA DAWA

Kajunason September 08, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu.

ALGIERS: Tanzania na Algeria zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza uzalishaji wa bidhaa hizo na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na la Afrika.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda vya Dawa wa Algeria, Dkt. Wassim Kouidri, katika ofisi za wizara hiyo jijini Algiers.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Matinyi alimweleza Waziri Kouidri kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania kuendeleza sekta ya viwanda vya dawa, ikiwemo kuweka vivutio maalum kwa wawekezaji.

Alisema tayari viwanda vitano vya dawa vinaendelea kujengwa nchini, huku vingine vikitazamiwa kuanzishwa katika kipindi kijacho.

“Serikali imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha viwanda vya dawa na vifaa vya tiba katika ukanda wa nchi za mashariki, kati na kusini mwa Afrika wenye watu takriban milioni 350,” alisema Balozi Matinyi.

Kwa upande wake, Waziri Kouidri aliahidi ushirikiano wa Serikali ya Algeria katika kuisaidia Tanzania kupata utaalamu wa kisasa wa utengenezaji wa dawa na vifaa tiba.

“Ni kweli, Tanzania ipo kwenye eneo zuri la kimkakati la ukanda mkubwa wa Afrika na Algeria iko tayari kushirikiana nayo kitaalamu ili kuhakikisha inafikia malengo yake,” alisema.

Aidha, Balozi Matinyi alikaribisha ziara ya Mamlaka ya Taifa ya Bidhaa za Dawa ya Algeria (ANPP), inayotarajiwa nchini Tanzania mwezi Oktoba mwaka huu kwa mwaliko wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA).

Ziara hiyo inalenga kujadili namna bora ya kuimarisha ushirikiano wa kitaalamu kati ya mamlaka hizo katika sekta ya dawa.

Tanzania pia imeendelea kujijengea heshima barani Afrika katika udhibiti wa dawa baada ya kuwa nchi ya kwanza barani humo kufikia kiwango cha daraja la tatu la ukaguzi wa dawa (ML3) mwaka 2018, chini ya tathmini ya viwango vya Shirika la Afya Duniani (WHO).

Kiwango hicho hupima ubora na ufanisi wa mifumo ya udhibiti na ukaguzi wa dawa katika nchi.

Tangu mwaka 2020, nchi nyingine tisa za Afrika zimefikia kiwango cha ML3. Nchi hizo ni Afrika Kusini, Ethiopia, Ghana, Misri, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Senegal na Zimbabwe.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna nchi ya Afrika iliyofikia kiwango cha juu zaidi cha ML4.

Kwa upande wa Algeria, nchi hiyo ni miongoni mwa vinara wa sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba barani Afrika ikiwa na viwanda 230, sawa na takriban theluthi moja ya viwanda 690 vilivyopo barani humo.

Ushirikiano huo unatarajiwa kusaidia Tanzania kuongeza uwezo wa uzalishaji wa dawa na vifaa tiba, kupunguza utegemezi wa bidhaa zinazoagizwa kutoka nje na kuongeza nafasi ya nchi katika soko la dawa la Afrika.

DODOMA GIRLS OPEN GENDER AND ICT DEBATE

September 08, 2026 Add Comment



DODOMA, September 8, 2026: Girls taking part in an Information and Communication Technology (ICT) Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma have begun exploring how gender perceptions can influence their participation in technology, while learning how digital skills can be used to address real challenges facing their communities.

The Bootcamp is part of a project implemented by UNESCO in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, aimed at promoting gender-transformative digital skills education and increasing girls’ participation in technology and Science, Technology, Engineering and Mathematics (STEM).


The first day of the Bootcamp opened with a simple but thought-provoking question: “What is sex? What is gender?”

The question sparked a discussion among the students, who shared their understanding and experiences before examining how gender roles and expectations affect their daily lives, education and access to technology.



Through the discussions, the students were encouraged to reflect on who does what, who makes decisions and who has access to opportunities at home and at school.

They also examined how social and cultural beliefs can influence the way girls view technology and their own ability to pursue careers in ICT and other STEM-related fields.

Challenging stereotypes

A major part of the training focused on challenging stereotypes that can discourage girls from participating in science and technology.


Among the perceptions discussed were the beliefs that science and technology are mainly for boys and that women are less suited to leadership positions.

Such attitudes can affect girls’ confidence, educational choices and future career opportunities, particularly in fields related to STEM.

The training therefore encourages girls to recognise these barriers and understand that their gender should not determine their ability to learn, create or lead in technology.

The discussions also highlighted the importance of addressing the digital gender gap, particularly in relation to access to ICT, the cost of technology and the knowledge and skills required to use digital tools effectively.

Technology for real-life solutions

The Bootcamp has gone beyond teaching students how to use digital devices. It is also helping them understand how technology can be applied to solve problems in education, the economy and access to essential services.

One of the areas explored by the students was the relationship between gender, ICT and water services.

The students discussed how digital technology can support the monitoring of water use, reporting of broken water infrastructure and leakages, identifying areas experiencing water shortages and using information to better understand and plan for water needs.

The exercise is intended to help the girls see technology not simply as a tool for communication or learning, but as a practical means of developing solutions to challenges affecting people in their communities.

From technology users to innovators

Another key message from the Bootcamp is the need for girls to move beyond being consumers of technology and become active creators and innovators.



The students are encouraged to contribute ideas, design and test solutions, work together and explore ways in which technology can respond to challenges affecting their schools and communities.

This approach is intended to build not only digital skills, but also confidence, creativity, problem-solving abilities and leadership among girls.

The UNESCO-BNU project places emphasis on creating opportunities for girls to develop practical digital skills and participate in activities that can strengthen their interest and confidence in technology and STEM.

For the girls at Msalato, the first day of the Bootcamp has therefore marked the beginning of a wider journey—one that seeks to change the way they see themselves in the digital world.

From discussing gender roles to exploring how ICT can help address challenges such as water access, the students are beginning to see technology as a tool for innovation, empowerment and social change.

The broader goal is to ensure that girls are not left behind in the digital transformation, but are equipped to participate, innovate and help shape the future of technology in Tanzania.

For the girls of Msalato, the digital journey has begun.

DC MPOGOLO: WALIMU NI WAZALISHAJI WA WATAALAMU NA VIONGOZI

Kajunason September 08, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu.

DAR ES SALAAM: Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amewapongeza walimu wa Kata ya Ukonga kwa mchango wao katika jamii, akisema wamekuwa msingi muhimu wa uzalishaji wa wataalamu na viongozi mbalimbali nchini.

Mhe. Mpogolo ameyasema hayo wakati wa sherehe ya walimu wa Kata ya Ukonga, inayojulikana kama UKONGA DAY, iliyofanyika Ukonga jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mpogolo amesema walimu wana nafasi kubwa katika maendeleo ya Taifa kwa kuwa ndio wanaowaandaa wanafunzi kuwa wataalamu na viongozi wanaokuja kuliongoza na kulitumikia Taifa.
Amesema mchango wa walimu hauishii darasani pekee, bali unaendelea kuonekana kupitia mafanikio ya wanafunzi wao katika nyanja mbalimbali za maisha.

Mhe. Mpogolo ametoa pongezi hizo kufuatia hotuba ya utangulizi iliyotolewa na mgeni maalum wa hafla hiyo, Mhe. Jerry Silaa, ambaye pia ni mlezi wa walimu wa Kata ya Ukonga.

Mhe. Silaa ana historia ya kipekee na eneo hilo, kwani amezaliwa katika Kata ya Ukonga na kusoma katika Shule ya Msingi Ukonga.
Katika safari yake ya maisha, amekuwa akirejea katika eneo hilo na kutoa shukrani kwa walimu wa Kata ya Ukonga, akiwatambua kuwa miongoni mwa watu waliochangia kwa kiasi kikubwa mafanikio yake.

Aidha, Mhe. Mpogolo amesema walimu ni miongoni mwa watu wanaofurahia mafanikio ya wale waliowafundisha, akieleza kuwa mafanikio ya mwanafunzi ni sehemu ya mafanikio ya mwalimu.

Amesema tofauti na baadhi ya watu ambao wanaweza kuwa na wivu wanapowaona wenzao wakifanikiwa, walimu hufurahia kuona wanafunzi wao wakipiga hatua na kufikia mafanikio makubwa.

Kwa mujibu wa Mhe. Mpogolo, hali hiyo inaonesha umuhimu wa kutambua na kuthamini mchango wa walimu katika kujenga jamii na Taifa kwa ujumla.
SERIKALI YATOA ONYO KWA WANAOHUSIKA NA UDANGANYIFU MITIHANI

SERIKALI YATOA ONYO KWA WANAOHUSIKA NA UDANGANYIFU MITIHANI

September 08, 2026 Add Comment

Serikali imesema udanganyifu katika mitihani ya kitaifa umepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kuimarishwa kwa usimamizi wa mitihani nchini.

Kauli hiyo imetolewa Septemba 7, 2026 mkoani Ruvuma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Prof. Carolyne Nombo, alipofika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na kuazungumzia utekelezaji wa masuala mbalimbali ya elimu ikiwemo maandalizi ya mtihani wa Taifa wa darasa la saba unaotrajia kufanyika nchini kote Septemba 9 na 10, 2026.

Ameeleza kuwa mitihani ya kitaifa ni suala nyeti linalohitaji usimamizi madhubuti, hivyo viongozi wa elimu katika ngazi zote wanapaswa kuhakikisha taratibu zote za mitihani zinafuatwa.

“Udanganyifu umepungua kwa kiasi kikubwa, nawasihi wanafunzi wa darasa la saba manaotarajia kufanya mitihani yenu kutojiingiza katika udanganyifu wowote wa mitihani, tuzingatie taratibu zote za mitihani,” amesisitiza Prof. Nombo

Aidha, amezitaka kamati za mitihani za mikoa na viongozi wa elimu kuendelea kushirikiana katika kusimamia mitihani, huku akiwapongeza kwa hatua ambazo tayari zimechukuliwa katika kupunguza udanganyifu.

Amebainisha kuwa, Serikali itaendelea kuchukua hatua pale inapobaini vitendo vya udanganyifu, hasa vile vinavyohusisha kupanga kwa pamoja kati ya wanafunzi, walimu au wasimamizi wa mitihani.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Songea Mhe. Wilman Kapenjama amesema mkoa umejiandaa vema katika kusimamia mtihani huo kwa hali ya usalama bila changamoto yoyote.

BESTA AWAAGIZA MAMENEJA 26 KUKAGUA BARABARA KABLA YA MVUA ZA EL NIÑO

September 08, 2026 Add Comment


Na Boniphace John, OKULY BLOG - DODOMA


Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) umewaagiza Mameneja wa Mikoa yote 26 nchini kufanya ukaguzi wa miundombinu ya barabara, madaraja, makalavati na maeneo mengine hatarishi, ili kuchukua hatua za haraka kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.

Wito huo umetolewa jijini Dodoma Septemba 7,2026 na Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Mohamed Besta, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa barabara ya Ntyuka–Mvumi–Kikombo pamoja na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Mhandisi Besta amesema TANROADS inapaswa kuwa makini kwa kutambua mapema maeneo yanayoweza kuathiriwa na mvua na kuhakikisha hatua stahiki zinachukuliwa kabla ya mvua kuanza.

Amesema ukaguzi huo ni muhimu kutokana na changamoto zilizowahi kujitokeza katika baadhi ya maeneo wakati wa mvua, akitoa mfano wa Daraja la Mutikila ambalo Desemba mwaka jana liliathiriwa na mvua na kusababisha usafiri wa magari na wananchi kukwama.

 “Natoa rai kwa mameneja wote wa mikoa 26 waende wakafanye ukaguzi na kuangalia ni namna gani wanaweza kupunguza athari zinazoweza kutokana na mvua za El Niño,” amesema Mhandisi Besta.

Amesema pamoja na Daraja la Mutikila, TANROADS inahakikisha kazi katika madaraja ya Mangungo na Kikombo, pamoja na madaraja mengine yanayotekelezwa katika mradi huo, zinakamilishwa kwa wakati ili yaweze kupitika wakati wa mvua.

Mhandisi Besta pia amemtaka mkandarasi wa mradi huo kuongeza kasi ya utekelezaji wa kazi ili kukamilisha sehemu iliyobaki na kuwawezesha wananchi kunufaika na barabara hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Zuhura Amani, mradi huo una urefu wa jumla ya kilomita 76 na unatekelezwa kwa awamu mbili.

Amesema awamu ya kwanza inayotekelezwa sasa inahusisha kilomita 25 na imefikia asilimia 67.9 ya utekelezaji.

Kati ya kilomita hizo, kilomita 8.6 ziko upande wa Ntyuka kuelekea Mvumi, huku upande wa Kikombo ukiwa na kilomita 14.4, ikiwemo kilomita tano zinazounganisha barabara hiyo na barabara inayoelekea Makao Makuu ya Jeshi.

Mhandisi Amani amesema mkandarasi wa mradi huo ni CHICO, ambaye tayari amekamilisha ujenzi wa sehemu kubwa ya barabara, ambapo kilomita 23.2 kati ya 25 zimefikia kiwango kinachohitajika.

Amesema kazi kubwa zilizobaki ni pamoja na kujaza tuta la barabara, kuunganisha maeneo ya madaraja na kukamilisha miundombinu ya kupitisha maji katika maeneo ya Mutikila, Mangungo na Kikombo, pamoja na daraja la reli ya MGR.

Amesema TANROADS tayari imeanza kuimarisha maeneo ya madaraja yaliyokuwa yakileta changamoto wakati wa mvua kwa kutumia kifusi, kuimarisha kingo za matuta na kufungua njia za mito, hatua inayolenga kuhakikisha watumiaji wa barabara wanaendelea kupita kwa usalama.

Kwa mujibu wa Mhandisi Amani, TANROADS inatarajia madaraja ya Mutikila, Mangungo na Kikombo kukamilika na kufikia hatua ya kupitika kabla ya kuanza kwa mvua, hatua ambayo itasaidia kupunguza usumbufu kwa wananchi na watumiaji wengine wa barabara.