HABARI ZETU
Loading...

HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

PROF. SHEMDOE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MADARASA LINDI

PROF. SHEMDOE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MADARASA LINDI

September 15, 2026 Add Comment

Na: OWM – TAMISEMI, Mchinga – Lindi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa madarasa manne na ofisi moja ya Mkuu wa Shule ya Msingi Mkwajuni, Kata ya Kitomanga, Manispaa ya Lindi, ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo yake ya kuhakikisha shule hiyo inarejeshewa miundombinu iliyoharibiwa na maafa.

Shule hiyo ilikumbwa na maafa Januari 29, 2026, ambapo madarasa mawili, ofisi ya Mwalimu Mkuu, nyumba mbili za walimu na vyoo vya wanafunzi viliezuliwa, huku darasa moja likiangukiwa na mkorosho.

Prof. Shemdoe ameweka jiwe la msingi katika mradi huo Septemba 14, 2026, alipofika shuleni hapo kukagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa hayo na ofisi ya Mkuu wa Shule, unaogharimu Shilingi Milioni 96. Ujenzi huo ulianza baada ya hoja iliyowasilishwa Bungeni na Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Mhe. Salma Rashid Kikwete, akiomba Serikali kutoa usaidizi wa haraka kufuatia maafa yaliyolikumba shule hiyo. 

Kufuatia hoja hiyo, Prof. Shemdoe alimuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi kuhakikisha fedha zinapatikana kwa haraka kwa ajili ya ujenzi wa madarasa hayo manne, agizo ambalo lilitekelezwa.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Prof. Shemdoe amesema Serikali imeonesha utayari wa kuchukua hatua za haraka pale wananchi wanapokabiliwa na changamoto zinazohitaji suluhisho la dharura.

“Mhe. Mkuu wa Mkoa, tuliomba ridhaa kwa Mhe. Rais ya kuomba fedha za kujenga madarasa haya manne ziletwe mara moja, na leo hii wote tumeshuhudia madarasa manne mazuri pamoja na ofisi ya Mkuu wa Shule hii ya Mkwajuni yaliyotokana na juhudi za Mbunge Mhe. Salma Rashid Kikwete za kuomba usaidizi wa haraka,” amesema Prof. Shemdoe.

Aidha, Prof. Shemdoe amewahakikishia wananchi wa Kata ya Kitomanga kuwa OWM–TAMISEMI italeta fedha nyingine kwa ajili ya kujenga madarasa zaidi katika shule hiyo, ili hatimaye shule hiyo iwe na madarasa mapya na kuondokana na matumizi ya madarasa ya zamani yaliyopo katika hifadhi ya barabara.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Mhe. Salma Rashid Kikwete, amemshukuru Prof. Shemdoe kwa kuweka jiwe la msingi katika katika Shule ya Msingi Mkwajuni, huku akimuomba kuendelea kusaidia upatikanaji wa majengo mengine ya madarasa na ofisi ili walimu wapate mazingira bora zaidi ya kufanyia kazi na wanafunzi kujifunza katika mazingira salama na rafiki.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kumuamini na kumpa jukumu la kusimamia upatikanaji wa maendeleo kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi.

Mhe. Malima pia amemshukuru Mhe. Rais kwa utayari wake wa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akiahidi kuendelea kuwatumikia wananchi wa Lindi kwa bidii na moyo wa uzalendo.

Katika ziara yake mkoani Lindi Septemba 14, 2026, Prof. Shemdoe pia ametembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo Mradi wa Bandari ya Uvuvi ya Kilwa Masoko; Mradi wa ujenzi wa Jengo la Wazazi (Maternity Ward) na Jengo la Wodi ya Matibabu ya Watoto Wachanga (NCU) katika Hospitali ya Wilaya ya Kinyonga; Mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi katika eneo la Sekondari Mkunyule, Kata ya Mandawa; pamoja na Mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Kitomanga ‘B’.        

SERIKALI HAITAVUMILIA WAFANYABIASHARA WA MKONGE WANAOFANYA UDANGANYIFU KATIKA MASOKO YA NJE

September 15, 2026 Add Comment

 




Na Oscar Assenga, TANGA

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara ,Dennis Londo amesema Serikali haitawavumilia wafanyabiashara wa mkonge wanaofanya udanganyifu katika masoko ya nje huku akiitaka Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) kuchukua hatua za haraka dhidi ya wafanyabiashara wanaodaiwa kuchukua fedha kutoka kwa wanunuzi wa nje bila kupeleka bidhaa walizoahidi, ikisema vitendo hivyo vinahatarisha uaminifu wa Tanzania katika masoko ya kimataifa.

Amesema tabia hiyo ya baadhi ya wafanyabiashara inachafua taswira ya nchi na kuwaweka katika mazingira magumu wafanyabiashara wengine wanaofuata taratibu na kufanya biashara kwa uaminifu.

Londo alitoa kauli hiyo jijini Tanga wakati wa kikao kazi kati ya TSB, Chama cha Wakulima wa Mkonge (SAT) na wafanyabiashara wa zao hilo.

Amesema Tanzania inaendesha uchumi wa soko huria, lakini uhuru huo haupaswi kutumiwa kama mwanya wa kufanya biashara kinyume cha sheria au kukiuka misingi ya uaminifu katika masoko ya kimataifa.




“Nimesikia hapa wafanyabiashara wakilalamika kwamba wakati mwingine wanataka kukamatwa kwa sababu kuna baadhi ya wafanyabiashara wamefanya udanganyifu kwenye soko. Mtu akifanya hivyo anashindwa kujua kwamba huku nje yeye anatambulika kama Tanzania na wala si kampuni yake,” amesema.

Amesema Serikali haiwezi kuvumilia vitendo vinavyoweza kuilazimisha nchi kutumia muda na rasilimali nyingi kurejesha uaminifu na taswira yake katika masoko ya kimataifa.

Kutokana na hali hiyo, Naibu Waziri ameiagiza TSB, kwa kushirikiana na wadau wengine wa zao hilo, kuchukua hatua mapema dhidi ya wafanyabiashara watakaobainika kufanya vitendo hivyo ili kulinda soko la mkonge na maslahi ya wafanyabiashara wanaofuata sheria.




“Pamoja na kwamba Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri ya kibiashara, hatuwezi kuvumilia hilo,” amesema.
TSB: WACHUKUA FEDHA, HAWAPELEKI MIZIGO

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TSB, Saddy Kambona, amesema changamoto hiyo ni miongoni mwa mambo aliyokutana nayo katika ziara zake kwenye masoko ya mkonge duniani.

Amesema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakichukua fedha kutoka kwa wanunuzi wa nje, lakini baadaye kushindwa kupeleka mizigo, hali ambayo imeanza kuchafua jina la Tanzania katika masoko hayo.




“Kwenye ziara yangu nimekutana na malalamiko kwamba kuna wafanyabiashara wamechukua fedha halafu wameshindwa kupeleka mizigo. Watu wanafanya udanganyifu kwenye masoko ya nje,” amesema Kambona.

Amesema wafanyabiashara watakaobainika kufanya vitendo hivyo wanaweza kuchukuliwa hatua, ikiwamo kufutiwa usajili au leseni zao.

Kwa mujibu wa Kambona, hatua hizo zinalenga kulinda uaminifu wa biashara ya mkonge kutoka Tanzania na kuhakikisha wafanyabiashara wanaofanya biashara kwa kufuata taratibu hawaathiriwi na vitendo vya watu wachache.


UZALISHAJI MKONGE WAPANDA

Pamoja na changamoto hiyo, Kambona amesema uzalishaji wa mkonge nchini umeendelea kuongezeka, kutoka tani 36,000 mwaka 2020 hadi kufikia tani 75,000 mwaka 2025.

Amesema mwaka 2020 wakulima wakubwa walichangia asilimia 68 ya uzalishaji wa mkonge, huku wakulima wadogo wakichangia asilimia 32.

Hata hivyo, amesema hali hiyo imebadilika kutokana na juhudi za kuwawezesha wakulima wadogo, ambapo mwaka 2025 walichangia asilimia 55 ya uzalishaji, huku wakulima wakubwa wakichangia asilimia 45.


WAFANYABIASHARA: TUNABEBESHWA DHAMBI ZA WACHACHE

Wafanyabiashara wa mkonge walioshiriki kikao hicho wamesema vitendo vya wachache vimekuwa na madhara kwa wafanyabiashara waaminifu kutoka Tanzania, ambao wakati mwingine hujikuta wakihusishwa na tuhuma au kesi zinazotokana na biashara zisizofanyika kwa uaminifu.

Gasper Daudi wa Harvest Agritech Limited amesema baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakisababisha matatizo katika masoko ya nje, hali inayowaathiri hata wale wanaofanya biashara kwa kufuata sheria.



Amesema ni muhimu Serikali na TSB kuweka mifumo madhubuti ya kuhakikisha wafanyabiashara wanaokiuka taratibu wanachukuliwa hatua mapema.



Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Aja Tanzania Limited, Happiness Nyiti, ameomba Wizara ya Viwanda na Biashara kuweka mpango maalumu wa kurejesha uaminifu katika masoko ambayo tayari yameathiriwa na vitendo vya baadhi ya wafanyabiashara.


“Vitendo hivi vinachafua taswira ya nchi yetu. Tunaomba Naibu Waziri atusaidie kuweka mpango mzuri wa kutengeneza taswira ya nchi yetu kwenye maeneo ambayo yanaonekana waziwazi kwamba imani ya wafanyabiashara wa zao hilo kutoka Tanzania imeshuka,” amesema Nyiti.



Amesema hatua hiyo ni muhimu kwa kuwa Tanzania ina wafanyabiashara wengi wanaozingatia ubora na uaminifu, lakini juhudi zao zinaweza kuathiriwa na vitendo vya wachache.

Amesema kurejesha uaminifu katika masoko ya kimataifa kutasaidia kuongeza fursa za biashara na kuchochea zaidi uzalishaji wa mkonge nchini.

TBS YATAHADHARISHA MATUMIZI YA VIPODOZI VYENYE VIAMBATA SUMU

September 14, 2026 Add Comment
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeonya wananchi kuhusu matumizi ya vipodozi visivyo salama, likisema bidhaa hizo zinaweza kusababisha madhara makubwa kiafya, ikiwemo magonjwa sugu kama saratani.

ENG.JOYCE BARAVUGA- SHULE ZIHAKIKISHE MAFUNZO YA TEHAMA YANAENDELEA

September 14, 2026 Add Comment

Mratibu wa Mafunzo ya Kidijitali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Eng. Joyce Baravuga, amesema mafanikio ya Mradi wa Kuziba Pengo la Kidijitali: Kuhakikisha Elimu ya Ujuzi wa Kidijitali Inayozingatia Usawa wa Kijinsia kwa Wanawake na Wasichana (Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls) yatategemea kwa kiasi kikubwa utayari wa shule kuendeleza mafunzo na shughuli za Klabu za TEHAMA (ICT Clubs) baada ya kumalizika kwa Kambi ya Mafunzo (Boot Camp).

Eng. Baravuga amewapongeza wakuu wa shule zilizochaguliwa kushiriki katika programu hiyo, akisema utayari na uthubutu wa shule ni miongoni mwa vigezo vilivyozingatiwa katika uteuzi.

Amesema shule hizo zinapaswa kuwa wadau muhimu wa programu hiyo kwa kuhakikisha maarifa na ujuzi unaopatikana kupitia mafunzo unaendelea kutumika shuleni na kuwafikia wanafunzi wengine.

Amewataka walimu na wakuu wa shule kuhakikisha Klabu za TEHAMA zinaendelea baada ya wanafunzi kurejea shuleni, ili kuwapa wasichana nafasi ya kuendelea kujifunza, kufanya mazoezi na kuendeleza ubunifu wao katika teknolojia.

Aidha, amewataka walimu, hususan wanaohusika na TEHAMA, kushiriki kikamilifu katika mafunzo hayo na kuhakikisha maarifa yanayopatikana hayabaki kwa wanafunzi walioshiriki pekee, bali yanawafikia wanafunzi wengine shuleni.

Eng. Baravuga pia amesisitiza umuhimu wa kukusanya taarifa za utekelezaji wa shughuli za mafunzo kila siku, akisema taarifa hizo zitasaidia kupima mafanikio ya programu, kubaini changamoto na mapungufu, pamoja na kuweka msingi wa kuboresha utekelezaji katika hatua zijazo.

Amesema ukusanyaji wa taarifa kwa wakati utasaidia pia kutambua maeneo yanayohitaji kupewa msukumo zaidi na kuhakikisha malengo ya programu yanafikiwa.

Vilevile, amesisitiza umuhimu wa wanafunzi kuchaguliwa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa bila upendeleo, ili kuhakikisha fursa zinazotolewa kupitia programu hiyo zinawafikia walengwa kwa usawa.

Eng. Baravuga amesema ushiriki wa shule, walimu na viongozi wa shule ni muhimu katika kuhakikisha Kambi ya Mafunzo haibaki kuwa tukio la muda mfupi, bali inakuwa mwanzo wa kujenga mazingira endelevu ya kujifunza, kutumia na kubuni kupitia TEHAMA miongoni mwa wanafunzi.

DR.FAITH SHAYO : LER US BUILD GIRLS INTEREST IN ICT

September 14, 2026 Add Comment

MOROGORO. Dr. Faith Shayo has called for greater efforts to build girls’ interest, confidence and enthusiasm in Information and Communication Technology (ICT), saying that creating interest is an important first step towards encouraging more girls to participate in technology.

Speaking during preparations for the ICT Boot Camp in Morogoro, Dr. Shayo said the programme is not primarily about providing girls with digital devices, but about helping them develop an interest in technology and understand its potential to improve their lives and communities.

She said access to devices remains important, but the immediate priority is to give girls the opportunity to learn, explore technology and develop the confidence to use it creatively.

“We want to build girls’ interest and enthusiasm in ICT. We want them to see that they can use technology to develop solutions to challenges in their communities,” she said.

Dr. Shayo said a key outcome of the programme is the establishment and strengthening of ICT Clubs in participating schools, providing girls with a space where they can continue learning, practising their skills and developing innovative ideas beyond the Boot Camp.


The programme is expected to reach 500 girls, with activities continuing after the Boot Camp. The girls will return to their schools and continue participating in ICT Club activities under the guidance of teachers and school leaders.

She said experts will continue visiting the schools to follow up on the progress of the clubs, while Project Coordinator Mr. Ginarious Ernest will also visit selected schools as part of the follow-up process.

Dr. Shayo said the practical nature of the Boot Camp is intended to help girls move beyond simply learning about technology and begin exploring how ICT can be used to address real challenges in their communities.

The Boot Camp is scheduled to officially begin tomorrow at Kilakala Secondary School in Morogoro, bringing together girls from 10 schools as part of the UNESCO-BNU project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls.”

WASICHANA MOROGORO KUGEUKIA TEHAMA KUTATUA CHANGAMOTO ZA JAMII

September 14, 2026 Add Comment








MOROGORO: Wasichana kutoka shule 10 za Mkoa wa Morogoro kesho wanaingia katika Kambi ya Mafunzo (Boot Camp) ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), wakiwa na lengo la kujifunza, kubuni na kutumia teknolojia kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika maisha ya kila siku.

Kambi hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kuziba Pengo la Kidijitali: Kuhakikisha Elimu ya Ujuzi wa Kidijitali Inayozingatia Usawa wa Kijinsia kwa Wanawake na Wasichana (Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls), unaotekelezwa na UNESCO kwa ufadhili wa Chuo Kikuu cha Beijing Normal (BNU), kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo, leo wadau wa mpango huo wamekutana katika Ukumbi wa Odema Hotel, Morogoro, kwa kikao cha maandalizi kilicholenga kuweka mikakati ya kuhakikisha mafunzo hayo yanaacha matokeo yanayoendelea hata baada ya wanafunzi kurejea shuleni.

Mradi huo unalenga kuongeza fursa kwa wasichana kupata ujuzi wa kidijitali, kuwajengea hamasa na uelewa kuhusu masomo na taaluma za TEHAMA, pamoja na kukabiliana na mitazamo ya kijinsia inayoweza kuwafanya wasichana kuona teknolojia kama eneo linalohusishwa zaidi na wavulana.

Miongoni mwa maeneo muhimu ya utekelezaji wa mradi huo ni kuimarisha uwezo wa walimu, kuongeza fursa kwa wasichana kujifunza ujuzi wa kidijitali, pamoja na kuanzisha na kuimarisha Klabu za TEHAMA (ICT Clubs), malezi na ushauri wa kitaalamu (mentorship) na shughuli za ubunifu.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Faith Shayo amesema msisitizo wa mafunzo hayo si kuwapatia wasichana maarifa ya TEHAMA kwa muda mfupi, bali kuwajengea hamasa na shauku ya kuendelea kujifunza na kutumia teknolojia.

Amesema hatua hiyo ni muhimu katika kuwafanya wasichana waone kwamba TEHAMA inaweza kuwa sehemu ya maisha yao, masomo yao na njia ya kutengeneza suluhisho kwa changamoto zinazowazunguka. “Lengo ni kuwajengea hamasa watoto wa kike ili waweze kupenda masomo ya sayansi na kuona uwezo wa TEHAMA katika teknolojia,” amesema Dkt. Shayo.

Amesema jumla ya wasichana 500 wanalengwa kunufaika na mpango huo, huku akisisitiza kuwa Kambi ya Mafunzo ya wiki hii si mwisho wa programu.

Baada ya mafunzo, wanafunzi watarudi katika shule zao na kuendelea na shughuli za Klabu za TEHAMA, huku wataalamu wakiendelea kuzifuatilia shule hizo na walimu pamoja na wakuu wa shule wakitarajiwa kusimamia mwendelezo wa klabu hizo.

Kwa kuzingatia nafasi kubwa ya kilimo katika Mkoa wa Morogoro, wanafunzi watatumia ujuzi watakaoupata kubuni suluhisho linalolenga sekta hiyo.

Miongoni mwa ubunifu unaotarajiwa kuwasilishwa ni Mkulima Mahiri (Smart Farmer), mfumo unaolenga kutumia Akili Bandia (Artificial Intelligence – AI) kumsaidia mkulima kutambua tatizo linaloweza kuikabili mimea.

Kupitia mfumo huo, mkulima ataweza kupiga picha ya mmea kwa kutumia simu, kisha mfumo kuchambua picha hiyo na kumsaidia kubaini tatizo linaloweza kuwa limeathiri mmea.

Ubunifu mwingine utahusu mfumo wa kuripoti matukio na changamoto zinazowakabili wananchi, ikiwemo matatizo ya maji, barabara na huduma nyingine muhimu katika jamii.

Kwa kufanya hivyo, Kambi hiyo inalenga kuwatoa wanafunzi katika nafasi ya kuwa watumiaji wa teknolojia pekee na kuwajengea uwezo wa kuwa wabunifu na watatuzi wa changamoto kupitia TEHAMA.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia amesema Wizara ina jukumu la kuandaa sera na miongozo, lakini utekelezaji wa sera hizo unahitaji ushirikiano wa wadau mbalimbali.

Ameishukuru UNESCO, BNU, wawezeshaji kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) pamoja na viongozi wa shule kwa kushiriki katika mpango huo, akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha wasichana wanapata fursa sawa za kujifunza na kutumia TEHAMA.

Amesema jamii inapaswa kuacha mitazamo inayoweza kuwafanya watoto wa kike waachwe nyuma katika matumizi ya teknolojia na badala yake kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika masomo ya sayansi na TEHAMA.

Kwa upande wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Eng. Joyce Baravuga, Mratibu wa Mafunzo ya Kidijitali (E-Learning Coordinator), amesema programu hiyo ni hatua muhimu katika kuimarisha elimu ya kidijitali nchini.

Amepongeza wakuu wa shule zilizochaguliwa kushiriki, akisema utayari na uthubutu wa shule ni miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa katika uteuzi huo.

Eng. Baravuga amewataka walimu na wakuu wa shule kuwa wadau wakuu wa mpango huo kwa kuhakikisha Klabu za TEHAMA zinaendelea baada ya wanafunzi kurejea shuleni na kwamba maarifa yanayopatikana yanawafikia wanafunzi wengine.

Aidha, amewataka walimu na wawezeshaji kukusanya taarifa za utekelezaji wa shughuli za mradi kila siku ili kuwezesha kupima mafanikio, kubaini mapungufu na kutoa msingi wa kuboresha programu katika hatua zijazo.

Amesisitiza pia umuhimu wa wanafunzi kuchaguliwa kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa bila upendeleo, ili kuhakikisha fursa zinazotolewa zinawafikia walengwa kwa usawa.

Mradi wa Kuziba Pengo la Kidijitali unalenga pia kuongeza uelewa wa walimu, wazazi, viongozi wa shule na jamii kuhusu umuhimu wa ushiriki wa wasichana katika elimu na taaluma zinazohusiana na TEHAMA.

Morogoro ni miongoni mwa maeneo yanayolengwa katika utekelezaji wa shughuli za mradi huo, pamoja na Dodoma.

Kesho, macho yanaelekezwa Shule ya Sekondari Kilakala, ambako wasichana kutoka shule 10 wataanza rasmi Kambi ya Mafunzo, wakibeba si tu matarajio ya kujifunza TEHAMA, bali pia nafasi ya kuonesha kwamba teknolojia inaweza kuwa nyenzo ya kubadili maisha na kutatua changamoto za jamii.

Kwa mradi huu, kuziba pengo la kidijitali hakumaanishi kuwapa wasichana teknolojia pekee, bali kuwapa maarifa, ujasiri na nafasi ya kuitumia teknolojia kuunda mustakabali wao.

FROM DODOMA TO MOROGORO:UNESCO ICT CLUBS PROGRAMME OPENS NEW DIGITAL OPPORTUNITIES FOR GIRLS

September 14, 2026 Add Comment

MOROGORO, September 14, 2026: The journey to equip girls with the digital skills, confidence and opportunities they need to participate in the technology-driven future has moved to Morogoro.

Following the official launch of the UNESCO-BNU ICT Clubs programme in Dodoma on September 7, 2026, UNESCO, in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, today launched the Morogoro phase of the initiative, which will run from September 14 to 18, 2026.


The programme is being implemented under the UNESCO-BNU project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls,” aimed at addressing the gender gap in digital education and expanding opportunities for women and girls to participate meaningfully in the digital economy and technology sector.

The Morogoro phase builds on the experience gained in Dodoma, where participating students were introduced to practical digital learning and innovation through ICT Clubs.

Rather than limiting technology education to theory, the programme gives girls opportunities to learn by doing—developing skills in coding, computational thinking, problem-solving, digital creativity, visual and audio content production, and the safe and responsible use of technology.

The experience in Dodoma demonstrated the value of creating spaces where girls can explore technology, ask questions, experiment with ideas and develop solutions to real-life challenges.

More importantly, the initiative seeks to nurture confidence and aspiration, enabling girls to see technology not simply as something they consume or use, but as a field in which they can create, innovate and build careers.

Speaking during the Morogoro launch, UNESCO Tanzania Head of Education Sector, Dr Faith Shayo, encouraged girls to take advantage of the opportunities provided through the ICT Clubs and to challenge perceptions that technology-related learning and careers are primarily for boys.

She emphasized the importance of creating learning environments where girls feel confident to experiment, make mistakes, ask questions and develop their abilities in technology.

The message is clear: girls should not only be users of technology; they should also be creators, innovators and future leaders in the digital world.

FROM LEARNING TO CREATING

Through the ICT Clubs, students are expected to gain practical experience while developing creativity, collaboration, problem-solving and leadership skills.

The programme will also connect girls with women ICT professionals through mentorship, giving them opportunities to learn from their experiences and gain a broader understanding of education, employment and career pathways in the technology sector.

For a girl writing her first line of code, developing a digital idea or using technology to solve a community problem, such experiences can represent more than a new skill.

They can be the beginning of a new ambition.

The ambition to become a programmer, engineer, developer, digital creator, entrepreneur, innovator—or a future leader in technology.

ICT INNOVATION BOOTCAMP STARTS TOMORROW

The Morogoro programme continues tomorrow, September 15, 2026, with an ICT Innovation Bootcamp at Kilakala Secondary School, a girls’ school.

The Bootcamp will provide participants with hands-on opportunities to strengthen their digital skills, develop innovative ideas and work collaboratively on technology-based solutions to real-life challenges in their communities.

The activities will reinforce the programme’s emphasis on practical learning, creativity and innovation, while encouraging girls to explore their potential in ICT.

The Morogoro activities will continue through September 18, 2026.

A SHARED COMMITMENT

The initiative is being implemented in collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), the Prime Minister’s Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), and the Tanzania Institute of Education (TIE).

Across Dodoma and Morogoro, the programme is expected to strengthen ICT Clubs in 20 public schools, directly benefiting 500 girls and 40 teachers.

The ICT Clubs are intended to provide safe, inclusive and supportive learning environments where students can develop digital skills, creativity, leadership and collaboration, while gaining greater awareness of opportunities in ICT-related education and careers.

As the programme moves from Dodoma to Morogoro, the goal remains the same: to ensure that girls are not left behind in the digital transformation.

They must have the opportunity to learn technology.

They must have the confidence to use it.

They must have the freedom to create with it.

And they must have the opportunity to build their future through it.

From Dodoma to Morogoro, the journey continues—one girl, one skill and one digital opportunity at a time.

The future of technology needs girls. Let us give them the skills, confidence and opportunity to build it.

#UNESCO #BNU #GirlsInICT #ICTClubs #DigitalSkills #DigitalEducation #GirlsInTechnology #ClosingTheDigitalDivide #Morogoro #Tanzania

CBE YAZINDUA PROGRAMU ZA DOUBLE DEGREE, UANAGENZI

September 14, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kimeanzisha programu mbili mpya za shahada zinazolenga kuwaandaa vijana kuwa wataalamu wenye ujuzi wa kimataifa, teknolojia na uwezo wa kutatua changamoto za kiuchumi na kijamii.

WAZIRI PROF.SHEMDOE AZITAKA WILAYA,HALMASHAURI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA MVUA ZA EL NINO

September 14, 2026 Add Comment

Na: OWM – TAMISEMI, Kilwa – Lindi


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amezielekeza Wilaya na Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinafanya kazi ya kuzibua mitaro na mifereji ya maji ili kujiandaa na kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kunyesha kuanzia mwezi Oktoba 2026 hadi Februari 2027, kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Septemba 13, 2026 akiwa Somanga, wilaya ya Kilwa, katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani Lindi, yenye lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhimiza uwajibikaji kwa viongozi na watumishi wa umma katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuwahamasisha kushiriki katika shughuli za maendeleo.

Prof. Shemdoe amewataka Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Mameneja wa TARURA Wilaya nchini kote, kuhakikisha wanashirikiana na taasisi nyingine katika kujiandaa na kuwa na utayari wa kukabiliana na athari za mvua za El Niño kwa kuhakikisha miundombinu ya kupitisha maji inakuwa katika hali nzuri na inakidhi mahitaji.

“Nimuelekeze Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kushirikiana na wananchi kuzibua mifereji ya maji iliyoziba ili kipindi cha mvua za El Niño maji yasipate nafasi ya kuchepuka na kuvamia makazi ya wananchi na kuleta madhara,  Mkuu wa Wilaya ya Kilwa simamia jambo hili,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Katika hatua nyingine, akijibu ombi la wananchi wa kata ya Kinjumbi la kujengewa kwa kiwango cha lami 

barabara ya Kinjumbi yenye urefu wa kilomita 30, Prof. Shemdoe amesema ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami utachukua muda mrefu, hivyo amemuelekeza Meneja wa TARURA kufanya tathmini ya gharama za kuikarabati kwa kiwango cha changarawe na kuwasilisha gharama hizo ofisini kwake ili bajeti ya fedha za matengenezo itumike kuikarabati na kuiwezesha kutumika muda wote.

Maelekezo ya Prof. Shemdoe kwa wilaya na halmashauri kujiandaa kukabiliana na athari za mvua za El Niño ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa katika kikao kazi  Septemba 11, 2026 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, aliyezitaka Wizara, Mamlaka na Taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka za kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua hizo zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba 2026.

Aidha, maelekezo hayo ya Prof. Shemdoe kwa wilaya na halmashauri kujiandaa kukabiliana na athari za mvua za El Niño ni muendelezo wa hatua za utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuboresha usafi wa mazingira katika miji na majiji, aliyoyatoa Septemba 2, 2026 wakati akiwaapisha Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala aliowateua Agosti 27, 2026.



Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Somanga, mkazi wa kata ya Somanga, wilaya ya Kilwa, Bw. Hashimu Omary Changadua, ameishukuru na kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea shule mbili za sekondari, soko la kimkakati na kituo cha afya, pamoja na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya wananchi.


Mara baada ya kuzungumza na wananchi wa Somanga, Prof. Shemdoe aliendelea na ziara yake kwa kutembelea na kukagua ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao linalojengwa na halmashauri ya Kilwa, pamoja na ujenzi wa soko la wajasiriamali wadogo katika kijiji cha Njianne, kata ya Tingi, katika halmashauri hiyo.

RUWASA YAKABIDHI PIKIPIKI KUBORESHA HUDUMA ZA MAJI RUNGWE

September 14, 2026 Add Comment

Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imekabidhi pikipiki kwa Kamati ya Watumia Maji Ngazi ya Jamii (CBWSO) ya MIMAKI, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utoaji na usimamizi wa huduma za maji kwa wananchi.

MWANA FA AZINDUA RASMI AWESO CUP ,TIMU 80 KUCHUKUANA KUMPATA BINGWA

September 13, 2026 Add Comment






Na Oscar Assenga, PANGANI

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma ‘Mwana FA’, amezindua rasmi Mashindano ya Aweso Cup katika Kijiji cha Sakura wilayani Pangani huku akizitaka klabu kubwa nchini pamoja na wadau wa soka, kufuatilia mashindano hayo kwa lengo la kuibua vipaji vipya.

Mwinjuma amesema  hayo katika Kijiji cha Sakura, Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, wakati akizindua rasmi Mashindano ya Kombe la Aweso, yanayoshirikisha jumla ya timu 80 kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.

Ambapo alisema Pangani ina vijana wengi wenye vipaji ambao wanahitaji kupewa nafasi ya kuonekana na watu wanaoweza kuwasaidia kufikia viwango vya juu.

Amesema uwekezaji unaofanyika leo katika michezo unaweza kuleta matokeo makubwa kwa vijana na Taifa kwa ujumla hapo baadaye.

“Ukiwekeza leo, kuna faida kubwa kesho. Tunawekeza kwenye michezo, maendeleo na utalii. Tunataka kuitoa Pangani pangoni na kuipandisha hadi kupaa angani,” amesema Mwinjuma.

Amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya michezo, huku ikiweka mkazo pia katika ugunduzi, malezi na utunzaji wa vipaji vya vijana.

TIMU YA U17 MFANO

Mwinjuma ametumia mafanikio ya timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 (U17) kama mfano wa matokeo ya uwekezaji katika vipaji.

Amesema timu hiyo imeonyesha uwezo mkubwa kwa kufika fainali ya michuano ya Afrika, kabla ya kupoteza mchezo huo, na baadaye kufuzu kwa mara ya kwanza kushiriki Kombe la Dunia.

Kwa mujibu wa Mwinjuma, Serikali imeendelea kusambaza mawakala na wataalamu katika maeneo mbalimbali ambako kuna mashindano ili kuhakikisha vipaji vinagunduliwa na kuendelezwa.

“Wadau wa michezo, Aweso Cup ina vipaji vingi. Kuna zaidi ya timu 80 zinazoshiriki. Tunawaomba wadau wa timu za Taifa, Simba, Yanga na klabu nyingine waje kuwaona vijana hawa kwa sababu wanaweza kufanya mambo makubwa,” amesema.

Amesema ni wakati sasa kwa wadau wa michezo kuanza “kuwathamini vyao” kwa kuwapa vijana wa Pangani na maeneo mengine nafasi ya kuonyesha uwezo wao.

Mashindano ya Aweso Cup yanatarajiwa kuwa jukwaa muhimu kwa vijana wa Pangani kuonyesha vipaji vyao, huku wadau wa michezo wakitarajiwa kutumia mashindano hayo kama sehemu ya kutafuta wachezaji wenye uwezo wa kuendelezwa zaidi.

Awali akizungumza  Waziri wa Maji na Mbunge wa Pangani kwa tiketi ya CCM, Jumaa Aweso, amewataka wadau wa michezo nchini kujitokeza katika mashindano mbalimbali ili kubaini na kuendeleza vipaji vya vijana.

Amesema mashindano hayo yameandaliwa kwa lengo la kuwapa vijana nafasi ya kuonyesha uwezo wao katika michezo, huku akisisitiza kuwa uwepo wa viongozi, makocha na wadau wengine ni muhimu katika kuwasaidia vijana wenye vipaji kufikia hatua kubwa zaidi.

“Wadau wa michezo tunapaswa kujitokeza katika mashindano kama haya kwa sababu hapa ndipo vipaji vinapopatikana. Vijana wanahitaji kuonekana, kutambuliwa na kupewa nafasi ya kuendeleza vipaji vyao,” alisema Aweso.

Amesema uwekezaji katika michezo unaweza kuwa sehemu muhimu ya kuwainua vijana kiuchumi, ikiwamo kuwapatia ajira na fursa nyingine kupitia michezo pamoja na sekta ya utalii.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ambaye pia ni Katibu Tawala wa Wilaya hiyo (DAS), Esther Gama, alisema mashindano hayo yatachezwa kwa mfumo wa mtoano (Knock-out) na kutaja zawadi nono zinazowasubiri washindi ambapo Mshindi wa Kwanza (Bingwa):Tsh Milioni 10, Mshindi wa Pili: Tsh Milioni 5,Mshindi wa Tatu: Tsh Milioni 3 huku Kikundi Bora cha Ushangiliaji: Pikipiki aina ya Boxer.

BARRICK YAFANIKISHA UJENZI WA MADARASA KUNUFAISHA WANAFUNZI WA JAMII YA KIMASAI LONGIDO

September 13, 2026 Add Comment


   

Meneja Mkazi wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido akisalimiana na wananchi na wazee wa kimila wa Kijiji cha Kiseriani kata ya Engikaret , Wilaya ya Longido mara baada ya uzinduzi wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi ya Shikinzi wilayani Longido.

BARRICK NORTH MARA, JUMUIYA YA WATUMIA MAJI WAFANIKISHA UPANDAJI MITI 47,200 KUHIFADHI MTO TIGHITE

September 13, 2026 Add Comment

 


Sehemu ya viongozi na wafanyakazi wa Barrick North Mara (kulia), viongozi wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini na Kijiji cha Matongo wakikagua maendeleo ya mradi huo Siku ya Mazingira Duniani 2026. (Picha za Maktaba)
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini, Mwita Seri, akiwa kwenye kitalu cha miche ya asili inayooteshwa kwa ajili ya kupandwa kandokando ya Mto Tighite.
Ushirikiano wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite (JWMT) na Kampuni ya Barrick kupitia Mgodi wake wa dhahabu wa North Mara umefanikisha upandaji wa miti ya asili 47,2000 kati ya 50,000 ambao utasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kulinda chanzo hicho cha maji kinachotegemewa katika shughuli mbalimbali za ustawi wa jamii na utunzaji wa mazingira.