HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
DKT. NCHIMBI: MASLAHI YA TAIFA YATANGULIZWE KATIKA USIMAMIZI WA MAZINGIRA
habari*************
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. EmmaculateSware pamoja na Watumishi waliofanya kazi pamoja na Makamu wa Raiswakati akifanya kazi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira(NEMC). Picha hiyo imepigwa mara baada ya Makamu wa Rais kukamilishaziara aliyoifanya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mikocheni Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Julai 2026. 
MTATIFIKOLO ASEMA SABASABA NI JUKWAA LA BIASHARA NA MAENDELEO
habariIRINGA – Mbunge wa Jimbo la Ismani, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo, amezindua rasmi maonesho na sherehe za Sabasaba zinazofanyika katika Kata ya Ilolo Mpya, Tarafa ya Pawaga, wilayani Ismani, huku akiwataka wananchi kutumia maonesho hayo kujifunza, kufanya biashara na kuimarisha mshikamano wa kijamii.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Mtatifikolo alisema maonesho ya Sabasaba ni fursa muhimu kwa wananchi kukutana, kubadilishana uzoefu, kuuza na kununua bidhaa mbalimbali pamoja na kujifunza fursa za maendeleo kutoka kwa washiriki na wageni wanaotoka maeneo mbalimbali nchini.



"Mnatakiwa kutumia maonesho haya kama jukwaa la kujifunza, kufanya biashara na kujenga mahusiano yatakayochochea maendeleo ya Ismani na wananchi wake," alisema Mtatifikolo.
Mbunge huyo pia aliwataka vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani.



Aidha, aliwahimiza wazazi na walezi kuendelea kuwalea watoto katika misingi ya maadili, uzalendo na uwajibikaji ili kujenga kizazi kitakachochangia maendeleo ya taifa.
"Malezi bora ndiyo msingi wa kujenga taifa lenye vijana wenye nidhamu, uzalendo na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi," alisisitiza.
Maonesho hayo ya Sabasaba yanajumuisha shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi, zikiwemo maonesho ya bidhaa, michezo ya mpira wa miguu, ngoma za asili pamoja na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.



Waandaaji wa maonesho hayo wamesema lengo ni kutoa fursa kwa wananchi kuonesha bidhaa na huduma zao, kuhamasisha biashara ndogondogo na kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo na sanaa.
Sherehe hizo hufanyika kila mwaka baada ya wananchi kumaliza shughuli za uvunaji, zikiwa sehemu ya kuimarisha mshikamano wa jamii, kuchochea biashara na kutoa burudani kwa wakazi wa Ismani na maeneo jirani.
Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo walieleza kufurahishwa na maandalizi ya maonesho hayo, wakisema yameendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Jimbo la Ismani.
UKAGUZI WA VIBALI VYA ARDHI WAWANASA WAWEKEZAJI WANAOKWEPA KODI ZANZIBAR
habari📌_*Kamisheni ya Ardhi, ZRA na ZAECA yaweka kambi Nungwi kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi katika mahoteli.*_
📌_*Ukaguzi waongeza ukusanyaji wa mapato na kuwezesha utoaji wa mikataba ya ardhi kwa wawekezaji.*_
Kamisheni ya Ardhi Zanzibar kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA), imefanya ziara maalumu ya ukaguzi wa vibali vya ardhi kwa wawekezaji wa mahoteli katika Shehia ya Banda Kuu, Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi na kuhakikisha ukusanyaji wa kodi ya ardhi unaimarishwa.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaskazini A, Dkt. Farid Mohammed Haji @faridhaji_ , aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya Laila Burhan Ngozi, amesema ukaguzi huo umelenga kubaini wawekezaji wanaokiuka masharti ya umiliki wa ardhi, ikiwemo kutolipa kodi ya ardhi kwa Serikali.
Amesema ukaguzi huo umezaa matokeo chanya baada ya kuwabaini baadhi ya wawekezaji ambao hawakuwa wametekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi, hatua iliyowezesha mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi Zanzibar, Mussa Kombo, amesema ukaguzi huo ni sehemu ya mkakati wa Kamisheni wa kuhakikisha wawekezaji wote wanatekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi kwa wakati na kuzingatia masharti ya umiliki wa ardhi. Ameeleza kuwa zoezi hilo pia limechangia kuongeza mapato ya Serikali kupitia malipo ya kodi ya ardhi, sambamba na utoaji wa mikataba ya ardhi kwa baadhi ya wawekezaji ambao hapo awali hawakuwa na mikataba hiyo.
Amesisitiza kuwa utoaji wa mikataba hiyo utaimarisha uwazi na uhalali wa umiliki wa ardhi, huku ukichangia usimamizi bora wa rasilimali za ardhi Zanzibar na kuhakikisha sheria za ardhi zinaendelea kuheshimiwa na kutekelezwa ipasavyo.
TAASISI 300 KUFUNGIWA MIFUMO YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA 2026/2027
habari
Katika juhudi za kuhakikisha kuwa Tanzania inafikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo 2034, Serikali katika mwaka wa fedha 2026/2027 itasambaza mifumo ya nishati safi ya kupikia katika taasisi 300 zinazolisha watu zaidi ya 100.
Hayo yamesemwa na Mtaalam kutoka Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, Wizara ya Nishati, Bw. Omari Khalifa wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (SabaSaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwl.Nyerere jijini Dar es Salaam.
Khalifa amesema mpango huo utatekelezwa katika bajeti ya mwaka huu wa fedha kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambapo jumla ya shilingi bilioni 15 ambazo ni fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo.
Ameeleza kuwa mifumo itakayofungwa inajumuisha gesi ya LPG, majiko banifu, mkaa mbadala pamoja na majiko ya umeme kwa lengo la kuboresha huduma za upishi, kulinda mazingira na kuimarisha afya ya watumiaji.
Katika utekelezaji wa mpango huo kampuni mbalimbali zinazotoa huduma ya mifumo ya nishati safi ya kupikia zitafaidika kupitia fursa zitakazotangazwa na REA huku taasisi hiyo ikisimamia usimikaji wa mifumo hiyo katika taasisi zitakazokidhi vigezo vilivyowekwa.




TTCL YAENDELEA KUWEKEZA KATIKA VITENDEA KAZI, YAKABIDHI MAGARI SITA
habariMFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA KWA PAMOJA WAIMARISHA UPATIKANAJI, UDHIBITI WA BEI NA MAPATO YA TAIFA
habariVISUKUKU MIMEA VYATOA MWANGA KATIKA UTAFITI WA MAFUTA NA GESI ASILIA NCHINI
habariDar es Salaam
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu mchango wa sayansi ya visukuku mimea (Palynology) katika utafiti wa mafuta na gesi asilia kupitia Banda la TPDC kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).
Mtafiti Mwandamizi wa Visukuku Mimea wa TPDC, Bw. Johanes Kakoki, alisema uchambuzi wa visukuku mimea kama dinoflagellates ( viumbe vidogo sana vya majini aina ya planktoni) , chavua (pollen) na mbeguchembe (spores) husaidia kubaini umri wa miamba na uwezo wake wa kuzalisha na kuhifadhi mafuta au gesi asilia.
Aliongeza kuwa taarifa hizo huunganishwa na tafiti za kijiolojia, kijiofizikia na kijiokemia ili kuongeza usahihi wa kubaini maeneo yenye rasilimali za mafuta na gesi, huku teknolojia za kisasa zikiboresha ufanisi wa tafiti na kupunguza gharama.
Kupitia maonesho hayo, TPDC inaendelea kuelimisha wananchi kuhusu hatua za utafiti wa mafuta na gesi asilia na mchango wa tafiti za kisayansi katika maendeleo ya sekta na uchumi wa Taifa.
*#Tunaboreshamaishanakuwezeshamaendeleo*

KABUDI: USAFI WA MAZINGIRA SASA NI AJENDA YA KIMKAKATI YA MAENDELEO YA TAIFA
habari
KATIKA hatua inayoashiria mabadiliko ya kimkakati katika usimamizi wa mazingira nchini, Serikali imeweka bayana mwelekeo mpya wa kuimarisha usafi wa mazingira kama nyenzo muhimu ya kupunguza magonjwa, kuongeza tija ya kiuchumi na kuharakisha maendeleo ya miji na vijiji.
Mkakati huo umeibuliwa jijini Dodoma leo July 2,2026 katika Kongamano la Kitaifa la Usafi wa Mazingira lililoambatana na uzinduzi wa mwongozo wa mpango jumuishi wa usimamizi wa huduma za usafi wa mazingira, ambalo limeweka msisitizo mpya wa kuunganisha huduma za usafi katika mfumo mmoja jumuishi unaolenga kuwafikia wananchi wote bila kuacha makundi yaliyo pembezoni.
Akizungumza katika kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Profesa Palamagamba Kabudi,amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira kuwa agenda ya kimkakati inayohitaji utekelezaji wa kisera, kitaasisi na kijamii kwa pamoja.
Amesema usafi wa mazingira sasa hautazamwi tena kama shughuli za kawaida za kijamii, bali ni sekta yenye mchango wa moja kwa moja katika afya ya umma, ustahimilivu wa miji na ukuaji wa uchumi.
Prof.Kabudi amesisitiza kuwa mkakati wa sasa unalenga kuhakikisha huduma jumuishi za usafi wa mazingira zinaimarishwa ili kupunguza tofauti za upatikanaji kati ya mijini na vijijini, pamoja na kuongeza ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji na utupaji taka.
“Tunajenga mfumo ambao unafanya usafi wa mazingira kuwa huduma ya msingi inayofika kwa kila Mtanzania,” amesema Kabudi.
Ameongeza kuwa mafanikio ya mkakati huo yanategemea mabadiliko ya tabia kwa wananchi sambamba na uwekezaji katika miundombinu ya kisasa ya usafi wa mazingira.
Aidha, ametumia kongamano hilo kumpongeza Rais Samia kwa kuendelea kuongoza ajenda ya nishati safi ya kupikia, akisema ni sehemu muhimu ya mkakati mpana wa kulinda mazingira na kupunguza uchafuzi unaotokana na nishati chafu.
Katika hoja ya kiufundi, Kabudi ameonya juu ya kuendelea kwa tabia ya utupaji taka kwenye mitaro ya maji ya mvua, akisema vitendo hivyo vinadhoofisha mifumo ya miji na kuongeza hatari ya mafuriko na magonjwa ya mlipuko.
Amesisitiza kuwa uwekezaji katika usafi wa mazingira ni sehemu ya mkakati wa taifa wa kulinda afya ya umma na kupunguza gharama za matibabu zinazotokana na magonjwa yanayohusiana na mazingira.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fedha wa EWURA, Stanley Mahembe,aliyemwakilishi Mkurugenzi Mkuu amesema bado kuna pengo kubwa la kitaasisi katika usimamizi wa majitaka, akibainisha kuwa ni mamlaka 24 pekee kati ya 84 ndizo zilizo na mipango ya matibabu ya majitaka na tope la kinyesi.
Amesema hali hiyo inaonyesha umuhimu wa kuharakisha utekelezaji wa mwongozo mpya wa usimamizi wa mazingira uliozinduliwa katika kongamano hilo.
Naye Naibu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA, Ngosi Mwihava, amesema kupitia bajeti ya shilingi trilioni 1.12 iliyopitishwa kwa ajili ya Wizara ya Maji, kuna matumaini makubwa ya kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya maji taka na usafi wa mazingira, ili kuendana na lengo la Maendeleo Endelevu (SDG) namba 6 linalohusu upatikanaji wa maji safi na usafi wa mazingira kwa wote.
Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, Kunti Majala, amesema changamoto za mazingira zinaendelea kuchangia vifo vinavyoweza kuzuilika, hivyo kuhitaji mkakati wa elimu na usimamizi kuimarishwa zaidi.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, amesema ongezeko la kasi la watu katika mji wa Dodoma linahitaji mkakati madhubuti wa usafi wa mazingira unaoendana na ukuaji wa mji huo.
Kongamano hilo ni sehemu ya utekelezaji wa dira mpya ya taifa ya kuimarisha mifumo ya usafi wa mazingira, kwa lengo la kujenga miji salama, yenye afya na endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.












