HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WAZIRI SANGU AIELEZA ILO MAMBO SITA YANAYOIPAISHA TANZANIA KATIKA SEKTA YA KAZI

June 05, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akizingumza katika Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani ( ILO), leo Juni 5, 2026, Jijini Geneva, Uswisi.

JAB KUPUNGUZA VIKWAZO VYA ITHIBATI KWA WAHITIMU WA HABARI

Kajunason June 05, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amewashauri Waandishi wa Habari nchini kuipa thamani na heshima taaluma ya habari kwa kuzingatia nadhifu ya mavazi na mienendo yao wanapotekeleza majukumu ya kitaaluma.

Wakili Kipangula ametoa ushauri huo leo Juni 5, 2026 wakati akiwasilisha mada kuhusu “Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Enzi ya Kidijiti: Wajibu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari” kwenye Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari.

Amesema uandishi wa habari ni taaluma muhimu inayotambulika kama muhimili wa nne usio rasmi katika jamii, hivyo ni wajibu wa waandishi wenyewe kuhakikisha wanaijengea heshima kupitia mwenendo, maadili na namna wanavyojiwasilisha mbele ya jamii.

Wakili Kipangula amesema mwonekano wa mwandishi wa habari unaweza kuwa sehemu ya kujenga imani kwa jamii na vyanzo vya habari vinavyotoa taarifa mbalimbali kwa vyombo vya habari.

“Kwa hiyo hata mtu unavyoenda kumhoji mtu akikuona jinsi ulivyo anajua huyu mtu ataeleza kitu cha msingi na huyu mtu anaeleweka na ni wa maana,” amesema Wakili Kipangula.

Amesisitiza kuwa pamoja na kuzingatia maadili, sheria na weledi katika ukusanyaji na uchakataji wa habari, Waandishi wa Habari wanapaswa kutambua kuwa taswira wanayoijenga mbele ya jamii ni sehemu muhimu ya kuimarisha hadhi ya taaluma hiyo na kuongeza imani ya wananchi kwa vyombo vya habari.

ORYX GAS YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUFANYA USAFI SOKO LA FERI

June 05, 2026 Add Comment

Kampuni ya Oryx Gas imeadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kwa kufanya usafi katika Soko la Kimataifa la Samaki Feri jijini Dar es Salaam na kukabidhi vifaa vya usafi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha utunzaji wa mazingira na matumizi ya nishati safi.

TADB YAPOKEA TUZO KWA KUENDELEZA KILIMO ENDELEVU NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

June 05, 2026 Add Comment
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetunukiwa Tuzo  leo tarehe 5 Juni 2026,  Siku ya Mazingira Duniani  kutokana na mchango wake mkubwa katika kuendeleza kilimo himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, matumizi endelevu ya rasilimali za asili na uwekezaji katika teknolojia rafiki kwa mazingira.

Katibu Mkuu wa CCM akutana na Balozi wa Uingereza Kujadili Ushirikiano wa Maendeleo na Dira 2050”

June 05, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Asha-Rose Migiro, leo Ijumaa Juni 5,2026 amefanya mazungumzo na Mheshimiwa Marianne Young, Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, katika Makao Makuu ya CCM, Dodoma.

TPDC YAKABIDHI KARAKANA YA KISASA YA CNG KWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.

June 05, 2026 Add Comment
Dar es Salaam, Juni 5, 2026

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekabidhi rasmi Karakana ya kuongeza mfumo wa matumizi ya gesi asilia Iliyoshindiliwa kwenye vyombo vya usafiri (CNG Conversion Workshop) kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hatua inayotarajiwa kuimarisha matumizi ya nishati safi nchini pamoja na kukuza ujuzi wa kitaalamu katika teknolojia ya gesi asilia.

DKT. KIJAJI: NYUMBA ZA IBADA ZIWE CHANZO CHA MSHIKAMANO NA AMANI KWA TAIFA

June 05, 2026 Add Comment



KONDOA, DODOMA

Mbunge wa Jimbo la Kondoa ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amesisitiza kuwa nyumba za ibada zinapaswa kuwa sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja na amani miongoni mwa wananchi na si  kuwa chanzo cha migawanyiko katika jamii.

Dkt. Kijaji ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akifungua rasmi Msikiti wa Filimo uliopo Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.


Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Kijaji amesema kuwa nyumba za ibada zina nafasi kubwa katika kujenga maadili mema, kuimarisha upendo na kukuza mshikamano wa kijamii, hivyo zinapaswa kutumika kwa malengo hayo kwa manufaa ya Taifa.

“Msikiti huu uwe chachu ya mshikamano ndani ya jamii yetu. Nawapongeza viongozi wa dini kwa kusimama katika haki na kuendelea kuhubiri amani na umoja miongoni mwa wananchi,” alisema Dkt. Kijaji.


Aidha, aliongeza  kuwa kila mtu ana wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu katika jamii na mbele za Mungu, akibainisha kuwa maendeleo yanayopatikana katika Jimbo la Kondoa yanalenga kuwanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.

"Ninachokifanya ndani ya jimbo letu ni kwa ajili ya maendeleo ya Wakondoa wote. Tunapaswa kuendelea kushirikiana na kuishi kwa upendo ili kuleta maendeleo endelevu,” alisisitiza.

Vilevile , Dkt. Kijaji alitumia fursa hiyo  kuwahamasisha waumini na wananchi wa eneo hilo  kuendelea kujenga na kuendeleza nyumba za ibada ili zitumike katika kukuza maadili mema na kuimarisha imani katika jamii. 

Katika hatua nyingine, amewataka  vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vingine vinavyohatarisha mustakabali wao, huku akiwataka viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pia amesisitiza  umuhimu wa malezi bora kwa watoto na vijana, akiwataka wazazi na walezi kuwajenga katika misingi ya maadili mema ili kuwa raia wema na wenye mchango chanya kwa maendeleo ya Taifa.

MRADI WA FUNZA WACHANGIA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA UFUGAJI

June 04, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imeendelea kuwaibua na kuwawezesha wabunifu nchini kupitia mafunzo yanayolenga kugeuza ubunifu wao kuwa fursa za ajira na maendeleo ya kiuchumi.

SERIKALI YAZINDUA GRAND CHALLENGES TANZANIA KUCHOCHEA UBUNIFU WA KUTATUA CHANGAMOTO ZA TAIFA

June 04, 2026 Add Comment
SERIKALI imezindua jukwaa jipya la kitaifa la ubunifu litakalowawezesha wanasayansi, watafiti na wabunifu kubuni suluhisho za ndani kwa changamoto zinazoikabili nchi katika sekta za afya, usalama wa chakula, mabadiliko ya tabianchi na teknolojia, hatua inayotarajiwa kuharakisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

SERIKALI YAENDELEA NA UANDAAJI WA KANUNI ZA BIMA ZA KILIMO KULINDA WAKULIMA

June 04, 2026 Add Comment



Na Jordan Mbwambo WF, Dodoma


Serikali imesema inaendelea kukamilisha mchakato wa uandaaji wa Kanuni za Bima za Kilimo ambazo zitasaidia kuongeza upatikanaji wa kinga kwa wakulima dhidi ya majanga yanayoathiri mazao, mifugo, misitu na sekta ya uvuvi nchini.


Hayo yamebainishwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe.Laurent Luswetula (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ilemela, Mhe. Kafiti William Kafiti, aliyetaka kujua wakati ambao Serikali itakamilisha Kanuni hizo ili kuongeza na kupatikana kwa kinga kwa wakulima na mazao mbalimbali.


Mhe. Luswetula alisema kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Fedha inaendelea na utafiti na maboresho katika Sekta ya Bima ya Kilimo ili kuhakikisha mfumo huo unakuwa shirikishi na wenye kuvutia uwekezaji kwa wadau wa ndani na nje ya nchi.


“Serikali inaendelea na utafiti kuhusu bima katika mnyororo wa kilimo (mazao, mifugo, misitu na uvuvi) ili pamoja na mambo mengine kuwa na Kanuni zinazovutia uwekezaji katika bima ya kilimo na kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima ili kupata huduma za bima kwa urahisi na haraka”, alisema Mhe. Luswetula.


Aliongeza kuwa, Serikali inakusudia kuhakikisha kanuni hizo zinakuwa rafiki kwa wakulima na wakati huo huo zikichochea ushiriki wa sekta binafsi katika kutoa huduma za bima ya kilimo nchini.


Aidha, alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya bima kuhakikisha mfumo huo unakuwa endelevu na unaonufaisha wakulima kwa upana zaidi.


DKT.SAMIA SULUHU HASSAN ATUNUKU SHAHADA KWA WATANZANIA ASEMA NI YAO

June 04, 2026 Add Comment




Na Beda Msimbe,TBN, Moscow

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) huku akiitoa shahada hiyo kwa Watanzania.



Shahada hiyo ilitolewa na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni,2026.

Rais Mhe. Dk Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania,

pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii,

Akizungumza baada ya kupewa shahada hiyo Rais Samia alisema kwamba heshima aliyopewa si ya mafanikio yake binafsi bali ni utambuzi wa juhudi na matarajio ya watanzania wote.

Alisema shahada hiyo ni ishara ya utambuzi wa dhamira ya pamoja ya Watanzania wote katika kuleta maendeleo,ushirikiano na ustawi wa binadamu.

“Nilipokea kwa furaha habari za kutunukiwa heshima hii,lakini mara moja nikatambua kwamba si yangu peke yangu. Ni heshima inayoitambua dhamira yetu ya pamoja ya maendeleo, ushirikiano na maendeleo ya binadamu” alisema Dk Samia.


Hii ni shahada yake ya nane kutolewa kwa Rais Samia .


Aidha alisema shahada hiyo  aliyopewa leo ni ishara ya urafiki wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi ikiwa ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya elimu katika kuunganisha mataifa.


Aidha alisema heshima hiyo inaakisi uhusiano wa kudumu kati ya nchi za Tanzania na Urusi ambazo zimeendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali hususani elimu kwa miongo kadhaa sasa.

Katika hotuba yake ambayo viongozi wa watanzania waliopo  Urusi na vyuo vya Urusi walisema ni iluiyiojaa mamlaka makubwa, Rais Samia alisema kwa miaka mingi watanzania walikuwa wanapata elimu inayochangia maendeleo  ya Tanzania katika Nyanja mbalimbali jambo ambalo pia  limeimarisha mahusiano ya watu wa pande zote mbili,

“Mama amezungumza nchi yetuj ina sifa sana. Tena sifa njema kwa kupata mwaliko wa Rais Vladmir Putin kuja hapoa ni kutambulika kwa Tanzania ni ishara njema na hotuba ya mama imeakisi matarajio” alisema Jefrey Mashauri Mwenyekiti wa wanafunzi wa Tanzania shirikishoi la Urusi (TASCARU).


Naye Mwenyekit wa watanznaia wanaoishi Urusi Pascal Gura alisema watanzania 300 wanaosihi hapo wameona fahari kubwa kukutana na kumsikiliza Rais Samia akionesha ni kwa namna gani kama Taifa Tanzania linaendelea kuwika.


Rais Samia katika hotuba yake alionesha jinsi Tanzania inavyoweza kufanikisha mambo wanaposaidiana na kushirikiana kwa maendeleo ya taifa.


Pia alikumbusha vijana kujipatia elimu huku wakizingatia kauli ya baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere ambaye alifundisha kwamba maendeleo lazima daima yaweke mwanadamu katikati ya kila jambo.


Aidha alitaka vijana kuangalia taifa lao na kwamba dokumentari iliyooneshwa kabla ya kutunukiwa shahada kuhusu maendeleo ya Tanzania inawaonesha dhamira ya watanzania na ni muhumu kwao watambue umuhimu wao kwa taifa huku huku wakiyaakisi maneno ya baba wa taifa katika utumishi wao.

Tangu kuanzishwa kwa chuo hicho miaka ya 1960 watanzania 1,100 wamepata utaalamu mbalimbali kupitia hucho hicho.Idadi hiyo ni kati ya wanafunzi 5000 ambao wamepata taaluma zao nchini Urusi katika Nyanja mbalimbali ikiwamo udaktari uhandisi na wataalamu wa sayansi.


Rais katika hotuba yake pia alizungumzia makubaliano kadhaa yaliyotiwa saini  yenye lengo la kuleta ushirikiano wa aina yake katika utafiti na elimu na ufundishaji.

Mwisho

MWANZA KINARA KATIKA USIMAMIZI WA MAAFA

June 04, 2026 Add Comment




Na, mwandishi wetu - Mwanza


Mkoa wa Mwanza umetajwa kuwa Kinara kwa kuratibu na kusimamia ipasavyo shughuli za kukabiliana na maafa, majanga na mawasiliano ya dharura kutokana na hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya utayari na mwitikio wa dharura.

Sifa hizo zimetolewa Juni 4, 2026 na wataalamu wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa mafunzo ya Kamati za Usimamizi wa Maafa yanayofanyika mkoani Mwanza kwa siku mbili yakilenga kuongeza uwezo wa kukabiliana na majanga.

Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa Said Mtanda amesema maafa yameendelea kuwa tishio kubwa duniani kutokana na athari zake kwa maisha ya watu, uchumi na maendeleo ya jamii.

Ametaja baadhi ya majanga yanayoikabili Tanzania kuwa ni mafuriko, ukame, maporomoko ya ardhi, matetemeko ya ardhi, mioto ya misitu na magonjwa ya mlipuko.

Kutokana na kuongezeka kwa matukio hayo Mhe. Mtanda amezitaka Wilaya zote Mkoani humo kuwa na mipango kazi na mifumo imara ya usimamizi wa maafa ili kuhakikisha maandalizi, mwitikio wa haraka na urejeshaji wa hali unafanyika kwa ufanisi.

Aliongezea kuwa, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeendelea kuimarisha usimamizi wa maafa kwa kutumia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2024 pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022.


Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa mafunzo hayo yatawajengea uwezo viongozi na wataalamu katika utekelezaji wa sera, sheria na miongozo ya usimamizi wa maafa katika maeneo yao.

Aidha, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa msaada kwa waathirika wa mafuriko Wilayani Kwimba, uliojumuisha tani tisa za mahindi, mablanketi, ndoo na vifaa vya wanafunzi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa eneo la utafiti kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bw. Vanvaco Luvanda amesema mafunzo hayo ya siku mbili yanaendelea kutolewa nchini kote kwa lengo la kuongeza utayari na uwezo wa kitaalamu wa kukabiliana na maafa yanapotokea.

Alifafanua kuwa, uwepo wa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka ambapo uzoefu unaonesha kuwa athari za maafa zinaendelea kuongezeka kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ongezeko la shughuli za kibinadamu na changamoto nyingine zinazoweza kusababisha maafa.


=MWISHO=

WAZIRI SANGU AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA 114 ILO

June 04, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akifuatilia agenda zilizokuwa zikijadiliwa katika Mkutano wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) unaoendela Jijini Geneva, Uswisi leo Juni 4, 2026.

DCEA, VETA Kuibua Matumaini Mapya kwa Waraibu Waliopona

June 04, 2026 Add Comment

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) zimeingia makubaliano ya ushirikiano yatakayowezesha waraibu waliopona matumizi ya dawa za kulevya kupata mafunzo ya ufundi stadi, hatua inayolenga kuwajengea uwezo wa kujitegemea kiuchumi na kuzuia kurejea kwenye matumizi ya dawa hizo.

TIMU KUTOKA OFISI YA WAZIRI MKUU YAFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU TAWALA MWANZA KUHUSU MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA

June 04, 2026 Add Comment




Na, mwandishi wetu - Mwanza

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mwanza Bw. Henry Mwaijega amekutana na kufanya mazungumzo timu ya Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu walipomtembelea ofisini kw


ake leo 04 Juni, 2026 Jijini Mwanza.


Timu hiyo ipo mkoani Mwanza kwa lengo la kuongoza mafunzo ya usimamizi wa maafa kwa Kamati za Usimamizi wa Maafa mkoa pamoja na wadau mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha utayari, uratibu na uwezo wa kukabiliana na majanga katika ngazi ya mkoa.

Pamoja na mafunzo hayo, wanatarajia kuzindua Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha mkoa wa mwanza tarehe 05 juni, 2026.





=MWISHO=

ISW KUANDAA KONGAMANO LA KWANZA LA KIMATAIFA LA UWEZESHAJI WA WATU NA USTAWI WA JAMII

June 04, 2026 Add Comment
Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW) kimetangaza kufanyika kwa Kongamano lake la Kwanza la Kimataifa la Uwezeshaji wa Watu na Ustawi wa Jamii, litakalofanyika Juni 5, 2026 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC) jijini Dar es Salaam.

MRADI WA FOLUR KUSHUSHA MIONGOZO YA KIMATAIFA MAENEO YA UTENDAJI ZANZIBAR

June 04, 2026 Add Comment


Na Anangisye Mwateba, Zanzibar


MRADI wa Mifumo ya Chakula, Matumizi ya Ardhi na Urejesho wa Mandhari ya Misitu nchini Tanzania (FOLUR), unatarajia kutoa mafunzo maalum kwa viongozi wa serikali za vijiji na shehia mbalimbali visiwani Zanzibar. Hatua hiyo inalenga kujenga uwezo wa kiutendaji na kuhakikisha jamii inatekeleza shughuli za mradi huo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.

Akifungua mafunzo hayo kwa maafisa ugani wa kilimo na misitu upande wa Zanzibar, Mratibu wa mradi huo, Bi. Miza Suleiman Khamis, alisema dhumuni kubwa ni kuwawezesha watendaji hao kubaini, kuepuka au kupunguza athari hasi zinazoweza kujitokeza kabla hazijaletea madhara wanajamii na mazingira yao.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Kitengo cha Jinsia, Usalama wa Mazingira na Jamii wa mradi huo, Bw. Revocatus Kadoshi, alibainisha kuwa viongozi wa shehia na maafisa ugani watafundishwa miongozo minne mikuu.

Miongoni mwa miongozo hiyo ni Mpango wa Usimamizi wa Mazingira na Jamii (ESMP), unaohusu udhibiti wa matumizi ya rasilimali na kuzuia uhamishaji wa watu usio wa hiari.

Bw. Kadoshi alifafanua kuwa mwongozo huo unalenga kudhibiti na kupunguza athari za kimazingira na kijamii wakati wa utekelezaji wa mradi. Aliongeza kuwa hatua hiyo inaenda sambamba na matakwa ya Mwongozo wa Sera na Taratibu Jumuishi za Ulinzi wa Kijamii za Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF).

"Viongozi hawa pia watafundishwa kuhusu Usimamizi Shirikishi wa Visumbufu. Huu unalenga kulinda afya na usalama wa jamii kwa kudhibiti athari zitokanazo na matumizi ya viuatilifu na mbolea," alisema Bw. Kadoshi.

Aidha, mafunzo hayo yatahusisha mbinu za usimamizi wa mazingira zinazohakikisha ustawi wa jamii, usalama mahali pa kazi, pamoja na usafi wa mazingira wakati wote wa utekelezaji wa shughuli za mradi huo.

Vilevile Aliongeza kuwa, ili kuhakikisha usalama wa jamii, mradi umeweka utaratibu maalumu wa kupokea nakufanyia kazi malalamiko kutoka kwa mwanajamii au kikundi cha kijamii kuhusiana na shughuli zinazotekelezwa na mradi. Hii inalwnga kuhakikisha jamii inashiriki vema kwenye shighuli za mradi na wanakuwa na nafasi ya kutoa dukuduku au lalamiko wakati wowote.




WFP KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA NCHINI

June 04, 2026 Add Comment


Na mwandishi wetu – Morogoro



Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula la Duniani (World Food Programme -WFP) limesema litaendeleza mashirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha masuala ya menejimenti ya maafa yanaendelea kutekelezwa kwa tija na malengo yaliyokusudiwa kwa kuimarisha uwezo wa kitaalamu na Kiteknolojia kwa kutumia teknolojia za kisasa.

Hayo yameelezwa na Naibu Mkurugenzi wa WFP Tanzania Bi. Christine Mendes wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura inayoendelea mkoani Morogoro.

Bi.Christine alisema ushirikiano hususan katika kuwezesha utekelezaji wa Mradi wa Field-Based Preparedness Project (FBPP), ambapo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mradi huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uwezo wa taifa katika sekta ya utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji.

Aidha, alieleza kuwa zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura linawakilisha hatua muhimu katika kuendelea kujitolea kwa Tanzania katika kuimarisha utayari wa kitaifa katika uratibu wa masuala ya maafa.


“Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, Mradi wa Matayarisho ya Uwandani (FBPP) umetoa mafanikio yaliyounganishwa ambayo yameimarisha kwa kiasi kikubwa utayarishaji wa vifaa na mfumo wa kukabiliana na dharura wa Tanzania,” alisema.

Aliongezea kuwa WFP itaendeleza ushirikiano wake na Serikali na kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono masuala ya menejimenti ya maafa ili kuyafikia matarajio kwa pamoja kwa kuwa na mfumo wa kukabiliana na hali ya dharura wa kitaifa wenye kasi zaidi, ulioratibiwa vyema na unaostahimili zaidi wenye uwezo wa kutoa hatua za kibinadamu kwa wakati unaofaa.

“Tutumie fursa hii kikamilifu, sio tu kupima mifumo, lakini kuimarisha mifumo, hivyo tuthibitishe tena dhamira yetu ya pamoja ya kujitayarisha kwa kuwajibika na kulenga kwa dhati kuokona maisha”alisisitiza Bi.Christine.