HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TEA, WIZARA YA ELIMU ZANZIBAR KUSHIRIKIANA KUIMARISHA MIRADI YA ELIMU

April 23, 2026 Add Comment
Naibu Katibu Mkuu (Taaluma) Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dkt. Mwanakhamis Ameir (kulia) na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha (kushoto) wakisaini mkataba maalum kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya elimu visiwani Unguja na Pemba.

WAMILIKI WA VISIMA TANGA WAPEWA SIKU 7, WATAKIWA KULIPIA LESENI AU KUCHUKULIWA HATUA

April 23, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga,TANGA

MKURUGENZI wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani Segule Segule amewataka wamiliki  wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kauli hiyo ameitoa baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.

Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.

Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.

Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.

Wamiliki wa visima vya maji katika Wilaya ya Tanga wamepewa siku saba kuhakikisha wanalipia leseni za matumizi ya maji ya chini ya ardhi, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Onyo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Segule Segule, baada ya ukaguzi maalum kubaini kuwepo kwa wamiliki wengi wa visima wanaotumia maji bila kuwa na leseni halali, hali inayosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Ukaguzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Green Cities unaofadhiliwa na GIZ, unaolenga kutambua visima vilivyopo, ubora wa maji pamoja na kiasi cha maji kinachopatikana. Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani, Halmashauri ya Jiji la Tanga na Tanga UWASA.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Segule amesema baadhi ya wamiliki wa visima wamekuwa wakichanganya kati ya leseni ya uchimbaji na ile ya matumizi, akisisitiza kuwa sheria inahitaji kila mmiliki kulipia leseni ya matumizi kila mwaka.

“Kuna watu wanadhani wakishapata leseni ya kuchimba visima wanakuwa wamemaliza kila kitu. Siyo kweli. Sheria inawataka kulipia leseni ya matumizi kila mwaka kwa shilingi 300,000. Tumewapa elimu na sasa tumewapa siku saba—wasipotekeleza, hatua zitachukuliwa,” amesema Segule kwa msisitizo.

Katika zoezi hilo, timu ya wataalamu iliyojumuisha wahandisi, wataalamu wa maabara na maafisa wa serikali za mitaa ilifanya ukaguzi wa kina wa visima katika maeneo mbalimbali, ikiwemo shule, zahanati, vituo vya afya, nyumba za ibada, makazi binafsi na maeneo ya shughuli za kiuchumi kama viwanda na ufyatua matofali.

Kwa upande wao, baadhi ya wamiliki wa visima wameonyesha utayari wa kufuata maelekezo hayo, wakikiri umuhimu wa maji hayo katika shughuli zao za kila siku.

“Tutakwenda ofisini kesho kufuata utaratibu wa kulipia leseni. Maji haya yanatusaidia sana katika kazi zetu za kufyatua matofali,” amesema Joseph Samwel wa Katemi Enterprises.

Naye Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Saruji, Fahad Salumu, amesema tathmini hiyo imewasaidia kupata picha halisi ya idadi ya visima vilivyopo pamoja na ubora wa maji katika eneo lake.

Wakati huohuo, Mkaguzi wa ubora wa maji kutoka maabara ya Bodi hiyo, Mpajieli Joseph, amesema tayari sampuli 30 za maji zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kina zaidi.

Akitoa mfano wa matokeo ya awali, mtaalamu wa maji ya chini ya ardhi, Nice Ninja, amesema vipimo vya mwanzo katika Shule ya Sekondari Maweni vinaonyesha maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwemo kunywa, huku uchunguzi zaidi ukiendelea maabara kuu.

Hata hivyo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani imesema taarifa kamili ya tathmini hiyo itatolewa mara baada ya kukamilika kwa mradi wa Green Cities.

SERIKALI YAHAKIKISHA UPATIKANAJI WA MAFUTA LICHA YA CHANGAMOTO ZA KIMATAIFA

April 23, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Serikali imesema itaendelea kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa mafuta nchini licha ya changamoto za kimataifa zinazoathiri mnyororo wa usambazaji wa nishati hiyo , ikiwemo vita inayoendelea katika Ukanda wa Mashariki ya Kati.

Akizungumza bungeni jijini Dodoma wakati wa uwasilishaji wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2026/27 ,Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Deogratius Ndejembi, alisema kuwa Serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa za mafuta ya petroli kwa uhakika.

“Sambamba na kuimarika kwa upatikanaji wa umeme, nchi yetu pia imeendelea kuwa na uhakika wa upatikanaji wa bidhaa za mafuta ya petroli licha ya changamoto za kimataifa zilizotokana na vita baina ya Marekani, Israel na Iran,” alisema Mhe. Ndejembi.

Alifafanua kuwa vita hiyo imesababisha athari kubwa katika usambazaji wa mafuta duniani, ikiwemo kufungwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz ambao hupitisha zaidi ya asilimia 20 ya mafuta yote duniani, pamoja na kuathiri miundombinu ya uzalishaji na uhifadhi wa mafuta.

“Hali hii imeathiri kwa kiasi kikubwa nchi za Mashariki ya Kati ambako Tanzania inaagiza takribani asilimia 59 ya mafuta yake, huku asilimia 41 ikitoka India ambayo nayo hutegemea mafuta ghafi kutoka ukanda huo huo,” aliongeza.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Ndejembi alisema Serikali imechukua hatua za haraka na za kimkakati ili kulinda usalama wa nishati nchini. Moja ya hatua hizo ni kuliwezesha Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuagiza mafuta ya kutosha kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo.

Aidha, alisema Serikali inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa soko la mafuta duniani na iko tayari kuchukua hatua zaidi kulingana na mabadiliko yatakayotokea.



Njombe Yaweka Rekodi ya Ubora katika Usimamizi wa Taka na Usafi wa Jamii

April 23, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekabidhi tuzo kwa Mkoa wa Njombe ikiwa ni Mshindi wa Jumla wa Shindano la Afya na Usafi wa Mazingira kwa Mwaka 2024.

CALL FOR STANDALONE ENVIRONMENT MINISTRY AS RUVUMA DIALOGUE SPARKS ACTION ON WATER GOVERNANCE

April 22, 2026 Add Comment

 

A multi-stakeholder dialogue on water governance in Ruvuma Region has reignited calls for the establishment of a dedicated Ministry of Environment, as stakeholders push for stronger, more coordinated action to address climate change and safeguard water resources.

TEA YAHIMIZA HALMASHAURI KUIMARISHA MIFUKO YA ELIMU KUCHOCHEA MAENDELEO YA SEKTA

April 22, 2026 Add Comment

WITO umetolewa kwa viongozi wa Serikali za Mitaa nchini kuimarisha ushirikiano na Mamlaka ya Elimu Tanzania(TEA) katika uanzishwaji na uendeshaji wa Mifuko ya Elimu ya Halmashauri ili kuongeza kasi ya maendeleo ya sekta ya elimu.

TVLA YATOA ELIMU KWA WAUZAJI WA CHANJO ZA MIFUGO KUSINI MWA TANZANIA

April 22, 2026 Add Comment
Afisa Masoko wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Bw. Fihiri Mbawala, akitoa ufafanuzi kwa Bi. Rauhya Omary, muuzaji wa duka la pembejeo za mifugo la Manispaa ya Lindi, tarehe 22 Aprili 2026, kuhusu mbinu bora za kuhakikisha mazingira ya uhifadhi wa chanjo yanazingatia viwango vinavyotakiwa ili kudumisha ubora na ufanisi wake, wakati wa ziara ya utoaji elimu ya matumizi sahihi ya chanjo zilizofanyika mikoa ya Lindi na Mtwara.

TANZANIA YAENDELEA KUWA MFANO KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UJANGILI NA BIASHARA HARAMU YA NYARA

April 22, 2026 Add Comment
Na Mwandishi wetu Itigi, Singida

Timu kutoka Uganda ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii, Wanyamapori na Malikale Bi. Doreen S. Katusiime yafanya ziara ya mafunzo Itigi.

BARRICK KUENDELEA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI KUBORESHA ELIMU WILAYANI KAHAMA

April 22, 2026 Add Comment

  

Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Naibu Meya wa Manispaa ya Kahama na Diwani wa Kata ya Mwendakulima, Shabani Mikongoti, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Naibu Meya wa Manispaa ya Kahama na Diwani wa Kata ya Mwendakulima, Shabani Mikongoti, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwendakulima, Bi. Neema Mfumya, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwendakulima, Bi. Neema Mfumya, akizungumza katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Agnes Julius akisoma risala kwa niaba ya wahitimu katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akigawa vyeti kwa wahitimu katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akiwa katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi, akigawa vyeti kwa wahitimu katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, yaliyofanyika Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.
Wahitimu wakiwa katika Mahafali ya 14 ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari Mwendakulima, Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.

***

Kampuni ya Barrick nchini yenye ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora katika mazingira salama na rafiki kwa kujifunzia.

𝐖𝐀𝐁𝐔𝐍𝐆𝐄 𝐖𝐀𝐂𝐇𝐀𝐑𝐔𝐊𝐀 𝐁𝐔𝐍𝐆𝐄𝐍𝐈, 𝐖𝐀𝐓𝐀𝐊𝐀 𝐍𝐄𝐌𝐂 𝐊𝐔𝐏𝐄𝐖𝐀 𝐌𝐄𝐍𝐎

April 22, 2026 Add Comment
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameibuka na hoja nzito wakichangia bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), wakitaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kupewa mamlaka kamili pamoja na rasilimali za kutosha ili liweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

ORYX GAS YAWAFIKIA WASHIRIKI 5,000 KWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA GESI SAFI

April 21, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imetoa seti 200 za mitungi ya Oryx kwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono Mpango wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

DKT.MATARAGIO ATEMBELEA MAONESHO YA WIKI YA NISHATI DODOMA

April 21, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu,


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt.James Mataragio, ametembelea maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea jijini Dodoma.


Hayo yamefanyika katika siku ya pili tangu kuanza kwa maonesho hayo Aprili 20, 2026, ambapo wadau mbalimbali wa sekta ya nishati wanashiriki kuonesha huduma, teknolojia na ubunifu wao.



Katika maonesho hayo, Dkt. Mataragio amepata fursa ya kutembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zinazojihusisha na masuala ya nishati, akijionea shughuli na maendeleo yanayofanywa katika sekta hiyo nchini.

Akizungumza wakati wa maonesho hayo, Dkt. Mataragio amesisitiza umuhimu wa kuendeleza sekta ya mafuta na gesi asilia ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa, akibainisha kuwa rasilimali hizo zina mchango mkubwa katika uzalishaji wa nishati na mapato ya Serikali.

Ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji katika sekta ya mafuta na gesi, ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa gesi asilia, ili kuwavutia wawekezaji zaidi na kuongeza tija katika sekta hiyo.

Aidha, amehimiza taasisi na wadau wa sekta hiyo kutumia maonesho hayo kama jukwaa la kubadilishana uzoefu, kuonesha teknolojia mpya, na kujenga ushirikiano utakaosaidia kuendeleza uchimbaji, uchenjuaji na matumizi bora ya mafuta na gesi nchini.

Katika maonesho hayo, Dkt. Mataragio aliambatana na Bi. Ziana Mlawa, ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Nishati, ambapo ameshiriki katika kutembelea mabanda na kujionea shughuli mbalimbali zinazooneshwa na wadau wa sekta hiyo.



MALIASILI YAIBURUZA HAZINA,YAZOA MEDALI 4

April 21, 2026 Add Comment



Na. Sixmund Begashe, Njombe 


Timu za Maliasili Sports Club chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, zimeendelea kuwanyanyasa wapinzani wao kwa kushinda Michezo mbalimbali ya Mei Mosi inayoendekea Mkoani Njombe. 

Timu ya Kamba Maliasili Wanaume katika kumtafuta mshindi wa kwanza kundi  "A"  imeiburaza vibaya timu ya Hazina kwa 2-1, mchezo ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa hamu kubwa na washabiki wa timu hizo. 

Kwa upande wa Mchezo wa riadha, wakimbiaji wa Maliasili Bw. Elibariki Buko ameshika nafasi ya 3 katika mbio za Mita 3000 na nafasi ya 3 tena kata 800, Bi. Pily Samwel naye akishika nafasi ya 3 katika mbio 3000, huku Bi. Jehovaness Sarakikya akinyakuwa nafasi ya 3 Mita 800.

Katika mashindano hayo ya mwaka huu, Wizara ya Maliasili imeshiriki pia katika michezo ya Draft pamoja na urushaji wa Tufe.


WIZARA yakutana na Wabunge wa Tanzania EALA: Yasisitiza Kuimarisha Nafasi ya Tanzania Kikanda

April 21, 2026 Add Comment
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imekutana na kuzungumza na Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam Aprili 21, 2026.

KATIBU MKUU CCM, UJUMBE MTANDAO WA VIONGOZI WANAWAKE AFRIKA WAFANYA MAZUNGUMZO

April 21, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 21 Aprili 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mtandao wa Viongozi Wanawake wa Afrika (African Women Leaders Network - AWLN), ulioongozwa na Marais wastaafu wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Ellen Johnson Sirleaf, na Jamhuri ya Shirikisho la Kidemokrasia ya Ethiopia, Mhe. Sahle-Work Zewde, jijini Dar es Salaam.
EWURA YAHAMASISHA UJENZI WA VITUO VIJIJINI CNG WIKI YA NISHATI DODOMA

EWURA YAHAMASISHA UJENZI WA VITUO VIJIJINI CNG WIKI YA NISHATI DODOMA

April 21, 2026 Add Comment

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-Mzalendo blog-DODOMA

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), leo 21 Aprili 2026, imetumia fursa ya Wiki ya Nishati kuwahamasisha waheshimiwa wabunge kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini pamoja na vituo vya CNG ili kuendelea kusogeza huduma kwa wananchi.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa EWURA, Bw. Wilfred Mwakalosi, alisema kuwa EWURA inatumia maonesho hayo kutoa elimu kuhusu namna inavyohakikisha upatikanaji wa huduma za nishati na maji kwa wakati na kwa gharama nafuu.

Amebainisha kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi, hivyo kuwajengea uelewa kuhusu udhibiti, fursa za uwekezaji na utaratibu wa kupokea na kushughulikia migogoro na malalamiko kutawawezesha kuwasilisha taarifa sahihi kwa wananchi kuhusu juhudi za Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za umeme, mafuta na gesi asilia.

Akizungumza katika maonesho hayo, Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi, amesema elimu inayotolewa pia inalenga kuwafahamisha wananchi jinsi EWURA inavyosimamia upatikanaji wa huduma za mafuta nchini kwa kuzingatia ubora uliopitishwa na gharama sahihi.

Aidha, amewahamasisha wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji katika sekta hiyo, hususan ujenzi wa vituo vya mafuta vya gharama nafuu vijijini na mijini pamoja vituo vya kujazia gesi asilia kwenye magari (CNG).

Kwa upande wake, Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,amesema  elimu inayotolewa imejikita katika kueleza namna EWURA inavyosimamia upangaji wa viwango vya bei za huduma za umeme, mafuta na gesi asilia. Aliongeza kuwa mamlaka hiyo huweka mizania kati ya maslahi ya watoa huduma na watumiaji, na kwamba wabunge waliopata elimu hiyo wataweza kuiwasilisha ipasavyo kwa wananchi katika maeneo yao.

Akizungumzia sekta ya gesi asilia, Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza, amesema  EWURA itaendelea kusimamia ubora wa miundombinu ya gesi asilia nchini na kuhamasisha matumizi yake, hususan katika magari.

Amebainisha kuwa hadi sasa vituo 18 vimepata leseni ya EWURA kutoa huduma ya gesi asilia, huku vituo sita vingine vikiwa katika hatua za mwisho za kupata leseni katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Aidha, mipango inaendelea kwa baadhi ya makampuni kusambaza gesi asilia iliyokandamizwa katika mikoa ya Morogoro na Dodoma.

Kwa upande wa sekta ya umeme, Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba, amewahamasisha wabunge na wadau wanaotembelea maonesho hayo kutumia mafundi umeme wenye leseni kutoka EWURA ili kuhakikisha usalama wa nyumba na mali zao. Alisema EWURA inaendelea kutoa leseni kwa mafundi umeme wenye sifa stahiki, ambapo zaidi ya leseni 1,000 zilitolewa katika mwaka wa fedha uliopita.

Naye Ofisa Rasilimali Watu Mkuu, Bi. Limi Kahabi, amesema EWURA ni mwajiri anayezingatia misingi ya usawa na haki katika mchakato wa ajira, akisisitiza kuwa taasisi hiyo huajiri kwa kuzingatia sifa, weledi na usawa kwa wote.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Kaimu Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mchumi wa EWURA Bi. Achilana Mtingele,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

 Ofisa Mkuu, Usimamizi wa Rasilimali Watu,Bi. Limi Kahabi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Umeme, Lulu Chilumba,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Mafuta, Mhandisi. Ibrahim Kajugusi,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mhandisi Mwandamizi wa Gesi Asilia, Mhandisi Evaline Rweikiza,akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye banda la EWURA wakati wa maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho  ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) wakiwa katika picha ya pamoja siku ya pili ya Maonesho  ya Wiki ya Nishati 2026 yanayofanyikia katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma

KATIBU MKUU MAFUTA NA GESI ASILIA AHAMASISHA WANANCHI KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

April 21, 2026 Add Comment




📌Asema ni utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2050


📌Aeleza  miradi ya kimkakati ya umeme inaongeza uzalishaji  wa umeme nchini


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi asilia, Dkt. James Mataragio, ametoa wito kwa wananchi kutumia nishati safi ya kupikia kama sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2050 inayolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi ambayo ni  salama na endelevu.


Dkt. Mataragio ametoa kauli hiyo Aprili 21, 2026, alipotembelea banda la TANESCO eneo la nishati safi ya kupikia kwa umeme , katika maonesho ya Wiki ya Nishati yanayoendelea katika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma.


Amesema kuwa Serikali inaendelea kuweka mkazo katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ikiwa ni pamoja na umeme, ili kulinda afya za wananchi na mazingira kwa ujumla, Aidha, ameipongeza TANESCO kwa juhudi zake za kuelimisha na kuhamasisha wananchi kutumia umeme kupikia.



‘’ Bajeti ya Nishati inatarajiwa kusomwa Bungeni, miongoni mwa mambo tunayotekeleza katika Bajeti yetu ni Dira ya Taifa ya mwaka 2050 ,hapo kuna kipengele cha nishati safi ya kupikia na kwa ujumla Taasisi zetu ikiwemo TANESCO  zinahamasisha matumizi ya nishati  safi ya  kupika kwa umeme,’’alifafanua Dkt Mataragio.


Kwa upande wake, Mbunge kutoka  Manyara, Mhe. Justina Rahhi, amesifu teknolojia ya majiko ya umeme yanayotumia nishati kidogo, akieleza kuwa yana uwezo wa kupunguza matumizi ya mkaa na kuni.

“Nimejifunza kuwa majiko haya yanatumia umeme kidogo sana ukilinganisha na mkaa. Ni muhimu teknolojia hii iwafikie wananchi wa vijijini ili waweze kunufaika na matumizi ya nishati safi,” amesema Mhe. Rahhi

Naye Mbunge wa Viti Maalum kutoka mkoa wa Ruvuma, Mhe. Mariam Nyoka, amepongeza kuimarika kwa huduma ya umeme katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, akieleza kuwa hali hiyo itasaidia kuongeza matumizi ya nishati safi.



Katika maonesho hayo ya Wiki ya Nishati, TANESCO pia imewasilisha teknolojia mpya ya magari yanayotumia umeme, ambayo yanaelezwa kuwa na gharama nafuu zaidi kwa matumizi ikilinganishwa na magari yanayotumia nishati nyingine.