HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TRAMEPRO YAENZI URITHI WA NELSON MANDELA, YATAKA JAMII KUJENGA AMANI

Kajunason July 19, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania(TRAMEPRO Tanzania ) limetoa mwitokwa Watanzania, Waafrika na jumuiya ya kimataifa kuendelea kujenga jamii inayoheshimu utu wa kila mtu, kuwekeza katika elimu, afya, sayansi, mazingira na amani.

TRAMEPRO imetoa mwito huo leo Julai 18,2026 katika kukimbizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela aliyekuwa Rais wa nchi ya Afrika Kusini.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu TRAMEPRO Tanzania Boniventura Mwalongo amesema wanaungana na mataifa ya Afrika na dunia kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Hayati Nelson Mandela mmoja wa viongozi mashuhuri waliobadilisha historia ya dunia kwa kupigania uhuru, usawa, haki za binadamu na maridhiano.

Pia amesema mambo ya kujifunza kupitia kutoka kwa Nelson Mandela ni kwamba elimu ni silaha yenye nguvu zaidi ya kubadilisha dunia, msamaha ni nguvu, si udhaifu; hujenga taifa lenye umoja.

Mengine ni uvumilivu na subira vinaweza kushinda hata changamoto kubwa, Uongozi ni huduma, si nafasi ya kutawala wengine, haki na usawa ni msingi wa maendeleo endelevu.

"Mandela anatufundisha pia umoja wa Waafrika na kuheshimiana ni nguzo ya maendeleo ya bara letu. Afya, mazingira na maendeleo vinapaswa kwenda pamoja kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, " amesema Mwalongo.

Akieleza zaidi amesema kwa waratibu asili Asili,TRAMEPRO Tanzania inaona mafunzo makubwa kutoka kwa Mandela katika kujenga umoja wa sekta, kuzingatia maadili ya taaluma, kuendeleza utafiti, kuhifadhi mimea tiba, kulinda mazingira na kushirikiana na taasisi za kisayansi ili tiba asili ichangie kikamilifu afya na maendeleo ya jamii.

Kuhusu historia ya Nelson Mandela alizaliwa Julai 18, 1918 katika kijiji cha Mvezo, Mkoa wa Eastern Cape, Afrika Kusini. Jina lake la asili, Rolihlahla, katika lugha ya Kixhosa humaanisha mtu anayetikisa tawi la mti, na kwa maana ya kawaida huashiria mtu mwenye kuhoji au kupinga hali iliyopo.

Alipoanza shule ya msingi, mwalimu wake alimpa jina la Nelson, kama ilivyokuwa desturi ya wakati huo katika shule nyingi za kikoloni.

Mandela alizaliwa katika familia ya kifalme ya kabila la Thembu. Baba yake aliitwa Gadla Henry Mphakanyiswa Mandela, aliyekuwa mshauri wa mfalme wa Thembu, na mama yake aliitwa Nosekeni Fanny Mandela.

Kutoka kwa wazazi wake alijifunza heshima, uwajibikaji, uongozi na umuhimu wa kuitumikia jamii.

Katika elimu, Mandela alianza masomo katika shule za wamisionari, akaendelea katika Chuo cha Healdtown, kisha akasoma katika Chuo Kikuu cha Fort Hare.

Baadaye alisomea sheria katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand, ambako alijiandaa kuwa mwanasheria na mtetezi wa haki za wanyonge. Elimu yake ilimpa msingi wa kuelewa sheria na kuitumia kutetea usawa na utu wa binadamu.

Mandela aliongoza mapambano dhidi ya mfumo wa ubaguzi wa rangi (Apartheid). Kutokana na msimamo wake, alifungwa gerezani kwa miaka 27, lakini hakukata tamaa wala kuacha kuamini kuwa amani na maridhiano vinaweza kushinda chuki. Baada ya kuachiwa huru mwaka 1990, aliongoza mazungumzo yaliyoweka msingi wa Afrika Kusini mpya yenye demokrasia.

Mwaka 1994, Nelson Mandela aliingia katika historia kwa kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini aliyechaguliwa kidemokrasia. Uongozi wake ulijengwa juu ya maridhiano, msamaha na umoja wa kitaifa. Mwaka 1993, alitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kwa mchango wake katika kumaliza Apartheid kwa njia ya amani.

UANAGENZI UTAWATOA VIJANA KIMAISHA: WAZIRI SANGU

July 19, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akifuatilia maelezo ya Kijana Mnufaika wa Mafunzo ya Uanagenzi Fani ya Ufundi Bomba, Ismail Mbogo alipotembea Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), kampasi ya Rukwa.

St Anne Marie Academy yasomesha waliofiwa na wazazi tangu mwaka 2029

July 19, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

Waziri wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka ameangalia maonesho ya sayansi wataka wakaguzi wa shule kutenda haki kwa shule binafsi na kuziona kama mshirika wa maendeleo badala ya mshindani.

MASAUNI: UHIFADHI WA UDONGO NI MSINGI WA MAENDELEO ENDELEVU

July 19, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, akizungumza na wadau mbalimbali wa mazingira kabla ya kushiriki matembezi yaliyolenga kuhamashisha jamii katika Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira yaliyofanyika Julai 19, 2026 jijini Dar es Salaam.

BODI YA NISHATI VIJIJINI YARIDHISHWA NA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA GEREZA LA MANYONI

July 19, 2026 Add Comment
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeridhishwa na hatua, ubunifu na kasi ya mageuzi yanayotekelezwa na Gereza la Manyoni, mkoani Singida, katika kuachana na nishati isiyo safi na kuanza kutumia bidhaa na teknolojia za Nishati Safi ya Kupikia.

SHIRIKA LA FROM HEARTS 2 HANDS LAJENGA MAKTABA YA KISASA KUNUFAISHA WANAFUNZI 737 WA JAMII YA KIMASAI , MONDULI

July 19, 2026 Add Comment

   

Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Gloriana Kimath akipata maelezo mbalimbali kuhusu Maktaba hiyo kutoka kwa mwanzilishi wa From Hearts 2 Hands , Dkt. Briana Greene (kushoto) wakati wa uzinduzi rasmi wa maktaba wilayani Monduli.
Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Gloriana Kimath (kulia0 akipata maelezo mbalimbali kuhusu Maktaba hiyo kutoka kwa mwanzilishi wa From Hearts 2 Hands , Dkt. Briana Greene wakati wa uzinduzi rasmi wa maktaba wilayani Monduli.
Mkuu wa Wilaya ya Monduli , Gloriana Kimath akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maktaba mpya iliyojegwa na Shirika la From Hearts 2 Hands kupitia mwanzilishi wake , Dkt. Briana Greene (kulia kwa Mkuu wa Wilaya) ambayo inafungua fursa ya kujifunza , utamaduni wa kujisomea , kupanua maarifa na kuongeza ufaulu wanafunzi wa Shule ya Msingi Lendikinya ya jamii ya wafugaji wa kimasai wilayani Monduli.
Mkuu wa Wilaya ya Monduli , Gloriana Kimath akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maktaba mpya iliyojegwa na Shirika la From Hearts 2 Hands kupitia mwanzilishi wake , Dkt. Briana Greene (kulia kwa Mkuu wa Wilaya) ambayo inafungua fursa ya kujifunza , utamaduni wa kujisomea , kupanua maarifa na kuongeza ufaulu wanafunzi wa Shule ya Msingi Lendikinya ya jamii ya wafugaji wa kimasai wilayani Monduli.
Sehemu ya muonekano wa ndani wa maktaba hiyo ya kisasa
Sehemu ya muonekano wa ndani wa maktaba hiyo ya kisasa.
Sehemu ya muonekano wa nje wa maktaba hiyo ya kisasa.
***

SHIRIKA la From Hearts 2 Hands kupitia mwanzilishi wake , Dkt Briana Greene limezindua maktaba ya kisasa ambayo inaweza kuhudumia wanafunzi 737 wa Shule ya Msingi Lendikinya kutoka jamii ya wafugaji wa kimasai wilayani Monduli.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo , Mkuu wa Wilaya ya Monduli (DC), Gloriana Kimath ameipongeza taasisi hiyo kwa kujenga maktaba ambayo ni miongoni mwa maktaba bora zaidi katika Mkoa wa Arusha.

Amesema ushirikiano kati ya Serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali umeendelea kuleta matokeo chanya katika kuboresha huduma za jamii, hususan sekta ya elimu hapa nchini.

"Ninatamani wakuu wa wilaya nyingine waje waione maktaba hii na wajifunze. Ni mradi wa mfano ambao umeongeza thamani kubwa katika elimu ya Wilaya ya Monduli," ameongeza.

Kimath amefafanua kwamba pamoja na uzuri wa jengo hilo, jambo muhimu zaidi ni kuhakikisha maktaba inatumika ipasavyo kwa kujenga utamaduni wa watoto kujisomea vitabu na kujifunza maarifa mapya.

Amesema ndani ya maktaba hiyo kuna vitabu vya historia, sayansi, lugha, sanaa na vifaa vya kujifunzia vitakavyowawezesha watoto kukuza vipaji na ubunifu wao.

Amewataka wazazi kuhakikisha watoto wanaendelea kujisomea hata wanaporejea nyumbani badala ya kuacha jukumu hilo kwa walimu pekee.

"Wazazi wana nafasi kubwa ya kuwajengea watoto utamaduni wa kusoma. Mtoto akitoka shuleni aendelee kupata muda wa kujisomea nyumbani," amefafanua.

Kimath amewahimiza wazazi wa jamii ya Kimasai kutowabagua watoto wa kike katika kupata elimu, akisema wao pia wana uwezo wa kufikia nafasi mbalimbali za uongozi.

"Mimi ni mtoto wa kike na leo nimekuwa Mkuu wa Wilaya wa kwanza mwanamke Monduli. Kama wazazi wangu wasingenisomesha, nisingefika hapa. Mtoto wa kike anaweza, tusimkatize ndoto zake kwa ukeketaji, ndoa za utotoni au vitendo vingine vinavyomnyima haki ya elimu," amesema.

Pia amewataka wananchi na viongozi wa kijiji kuilinda maktaba hiyo ili idumu kwa vizazi vijavyo, akisisitiza ni mali ya jamii nzima na si ya mtu mmoja ili kufanya vizuri kitaaluma.

Amewahimiza wakazi wa Monduli kuendelea kuwekeza katika elimu, akibainisha kuwa wilaya hiyo imeendelea kufanya vizuri kitaaluma.

"Elimu ndiyo ufunguo wa maisha. Katika matokeo ya Kidato cha Nne Mkoa wa Arusha, Monduli iliongoza, na katika matokeo ya Kidato cha Sita hatukuwa na Daraja la nne wala sifuri. Tukishirikiana Serikali, wazazi na walezi, tunaweza kufanya vizuri zaidi hadi ngazi ya taifa," amesema.

Akizungumza baada ya uzinduzi huo, Dk. Briana Greene amesema uwekezaji katika elimu ni njia bora ya kubadilisha maisha ya watoto wa jamii ya wafugaji na kuwapa nafasi ya kufikia ndoto zao.

Ameongeza kwamba alianza kusaidia shule hiyo kwa kujenga tenki hilo la na miundombinu ya maji baada ya kubaini changamoto zilizokuwepo, kabla ya kuendelea na ujenzi wa maktaba kupitia taasisi yake ya From Hearts 2 Hands.

"Elimu ndiyo msingi wa maendeleo ya jamii yoyote,tunataka watoto wa Lendikinya wapate fursa sawa na watoto wengine duniani. Hii ndiyo sababu tuliamua kujenga maktaba yenye vitabu na vifaa vitakavyowasaidia kujifunza kwa njia mbalimbali," amesema.

Amesema maktaba hiyo imejengwa baada ya kuona umuhimu wa wanafunzi kupata vitabu karibu ili vifungue fursa ya kujifunza zaidi.

"Nakumbuka nilikuja Lendikinya na niliona watoto wakihitaji maji,tukatengeneza tenki la maji nikaona wanahitaji maktaba waweze kujisomea vitabu,nikaamua kuijenga hapa nashukuru kwa Serikali kwa ushirikiano wa kufanikisha hili".

"Natumaini utamaduni mzuri wa kimasai ikifanikiwa huku watoto wakipata fursa ya kupanua mawazo yao na kupata maarifa mapya yanayoweza kuleta maendeleo katika jamii yao ninafuraha kubwa kukutana nanyi na kuweza kutoa mchango wangu kwa jamii,"ameongeza.

Amewataka wazazi wa jamii ya Kimasai kuhakikisha wanawapeleka watoto wote shule, hususan wasichana, akisema elimu ndiyo njia ya kuvunja mzunguko wa umaskini na kuwawezesha watoto kujitegemea baadaye.

"Pia nawaomba wanafunzi kuitunza maktaba hii na vifaa vyote vilivyomo. Hii ni rasilimali yenu na itawasaidia kukua kielimu na kutimiza ndoto zenu," amesema.

Akizungumza kwa niaba ya wazazi, diwani wa Kata ya Sepeko Joseph Kimaay, ameshukuru kwa ujenzi wa maktaba hiyo na kuwa itasaidia kukuza na kuboresha elimu.

"Katika kata na wilaya yetu kwa ujumla hakuna maktaba kama hui,tunashukuru kwa msaada huu na tunaamini bila ushirikiano mzuri wa Serikali na wadau binafsi leo tusingekuwa na jengo kama hili,tunaamini itaboresha elimu ya watoto wetu,"ameongeza.

Akisoma risala kabla ya uzinduzi huo, Mwalimu Mkuu Solomon. Godfrey amesema mradi huo ni wa kipekee katika Wilaya ya Monduli na unatarajiwa kubadilisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi wa shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 1977.

Amesema shule hiyo ina wanafunzi 737, wakiwemo wavulana 331 na wasichana 406, pamoja na walimu wanane.

Godfrey ameongeza kuwa maktaba hiyo imewekewa samani, vitabu vya aina mbalimbali, vifaa vya michezo, muziki, sanaa, kompyuta na maeneo maalumu ya watoto kujifunzia kwa vitendo na kuwa uwepo wa maktaba hiyo utasaidia kuongeza utamaduni wa kujisomea kwa wanafunzi, walimu na jamii, kuchochea ubunifu, kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza kiwango cha ufaulu kutoka asilimia 86.02 kilichofikiwa mwaka 2025.

Mbali na maktaba hiyo, amesema shirika hilo limekuwa likitekeleza miradi mingine ya maendeleo katika kijiji hicho ikiwemo ujenzi wa tanki la maji lenye uwezo wa kuhifadhi lita 100,000, ugawaji wa matenki ya maji kwa wananchi, ujenzi wa nyumba za kuvunia maji ya mvua na ugawaji wa chupa 700 za kubebea maji kwa wanafunzi.

Naye mwanafunzi wa Darasa la Sita, Riziki Papaking, amewashukuru wadau wa elimu kwa kufanikisha ujenzi wa maktaba hiyo, akisema itawawezesha kupata mazingira bora ya kujisomea na kuongeza ufaulu wao.

"Tunawashukuru wadau wa elimu kwa kutujengea maktaba hii. Itatupa nafasi ya kujisomea zaidi, kuongeza maarifa, kufanya vizuri katika masomo na kutimiza ndoto zetu," amesema Riziki.

Wanafunzi 737 wa Shule ya Msingi Lendikinya wilayani Monduli wanatarajiwa kunufaika na maktaba ya kisasa iliyojengwa na shirika la From Hearts 2 Hands, huku wadau wakisema mradi huo utakuza utamaduni wa kujisomea, kuongeza ufaulu na kuwapa watoto wa jamii ya wafugaji fursa sawa za elimu.

REA YAONDOA GIZA KITONGOJI CHA SIMANJIRO, FURAHA YATAWALA

July 18, 2026 Add Comment
-Wananchi wapongeza, waeleza matumaini ya ajira na maendeleo

MAKONDA: Uwekezaji wa afya waifanya Dira ya Taifa 2050 kuwa halisi

July 18, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Arusha

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Arusha, Paul Christian Makonda, ameridhishwa na maboresho yanayoendelea katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center inayotoa huduma kwa ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, ALMC–JKCI Arusha.

WAZAZI WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO MALEZI NA ULINZI WA MTOTO

July 17, 2026 Add Comment


Wazazi wametakiwa kutimiza wajibu wao katika malezi na ulinzi wa mtoto ili kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama yasiyo na vitendo vya ukatili.

Wito huo umetolewa na Mkaguzi Msaidizi Emmanuel Kisiri, ambaye ni Polisi wa Kata ya Ikoma, Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara,alipokuwa akitoa elimu ya Polisi Jamii katika nyumba ya Abwire Thomas hivi karibuni.

Mkaguzi Msaidizi Kisiri amesema wazazi wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuwalea, kuwafuatilia na kuwalinda watoto wao dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia pamoja na changamoto nyingine zinazoweza kuhatarisha ustawi wao.

Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya wazazi, jamii na vyombo vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kujenga mazingira bora ya malezi na kuhakikisha haki za watoto zinazingatiwa.


OPERESHENI YA POLISI TANGA YANASA WATUHUMIWA 200 WENGINE 51 WAHUKUMIWA

July 17, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, Tanga

Operesheni zilizoendeshwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga kwa kipindi cha Juni 1 hadi Julai 16, 2026 zimewezesha kukamatwa kwa watuhumiwa 200 wanaodaiwa kuhusika na makosa mbalimbali ya jinai, huku watuhumiwa 51 wakitiwa hatiani na mahakama na kuhukumiwa vifungo tofauti, wakiwamo wawili waliofungwa miaka 30 gerezani.

Makosa yanayowakabili watuhumiwa hao ni pamoja na unyang'anyi wa kutumia nguvu, wizi, biashara ya dawa za kulevya, kupatikana na mali zinazodhaniwa kuwa za wizi, umiliki wa nyara za Serikali, uharibifu wa miundombinu ya umma, matumizi ya noti bandia na makosa mengine ya jinai.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Muchunguzi, alisema mafanikio hayo yametokana na operesheni maalumu na doria zilizofanyika katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Alisema kati ya watuhumiwa waliokamatwa, kesi za watu 51 zilikamilika na kufikishwa mahakamani, ambako walipatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu mbalimbali kwa makosa ya kulawiti, kubaka, kuzini na maharimu, kusafirisha dawa za kulevya, wizi wa mifugo, kuvunja na kuiba, kujeruhi, kutishia kuua, kuingia nchini bila kibali pamoja na makosa mengine.
Watatu wafungwa miaka 30

Muchunguzi alisema waliohukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani ni Julius Mustafa, aliyepatikana na hatia ya kulawiti, Kilimo Issaya aliyetiwa hatiani kwa kosa la kuzini na maharimu na Sadiki Waziri aliyepatikana na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya.

Aliongeza kuwa watuhumiwa wengine walihukumiwa vifungo vya miaka mitano gerezani kwa makosa ya wizi wa mifugo pamoja na makosa mengine ya jinai.

Dawa za kulevya zanasa 29

Akizungumzia operesheni za kupambana na dawa za kulevya, Muchunguzi alisema watuhumiwa 29 walikamatwa wakiwa na dawa hizo za aina mbalimbali.

Alisema watuhumiwa 14 walikutwa na mabunda 750 ya mirungi yenye uzito wa kilogramu 45, huku watuhumiwa wengine 15 wakinaswa na bangi ikiwa katika mfumo wa misokoto 114, pakiti 126, vifurushi vitano na kete 120.

Katika operesheni hizo, polisi pia walikamata pikipiki 20 zisizo na namba za usajili ambazo zinaendelea kuchunguzwa kubaini uhalali wa umiliki wake na kama zilitumika kutekeleza vitendo vya uhalifu.
Nyara za Serikali, mali za wizi zakamatwa

Operesheni hizo pia zilisababisha kukamatwa kwa watuhumiwa watano waliokuwa na nyara za Serikali na mali zinazohusiana na wanyamapori.

Mbali na hilo, polisi walinasa vifaa mbalimbali vinavyodhaniwa kuwa vya wizi, vikiwamo vifaa vya miundombinu ya TANESCO, vifaa vya miundombinu ya barabara, noti bandia za fedha za Kenya, televisheni 10, simu za mkononi 25 pamoja na mali nyingine zinazochunguzwa kubaini uhalali wa umiliki wake.

Muchunguzi alisema operesheni dhidi ya uhalifu zitaendelea kuimarishwa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tanga, huku akiwataka wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zitakazowezesha kuwabaini wahalifu na kuzuia vitendo vya uhalifu.

Alisema ushirikiano wa wananchi umeendelea kuwa nguzo muhimu katika mafanikio ya operesheni hizo na kwamba jeshi hilo litaendelea kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote watakaobainika kujihusisha na uhalifu.








UFADHILI WA REA WAONGEZA TIJA KWA WAZALISHAJI WA CHUMVI IRAMBA

July 17, 2026 Add Comment
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kufadhili mradi wa uzalishaji wa chumvi ya asili maarufu kama chumvi ya Kilyoma katika Kata ya Ntwike, Wilaya ya Iramba.

SERIKALI YASISITIZA UKUZAJI TIJA KATIKA SEKTA YA UMMA

July 17, 2026 Add Comment
Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania Mhe. Eunje Ahn (kulia) akikabidhi zawadi kwa Kaimu Mkurugenzi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi wa Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusinao  Bi. Alana Nchimbi, mara baada ya hafla ya mafunzo ya ukuzaji tija kwa vijana na wanawake walionufaika na programu za KOICA yaliyolenga kuimarisha utendaji wa kazi katika utumishi wa umma. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dodoma tarehe 16 Julai 2026.

KAMPUNI ZA WAZAWA ZATAKIWA KUTEKELEZA MIRADI KWA UFANISI ILI KUSHINDANA KIMATAIFA

July 17, 2026 Add Comment
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu, amezitaka kampuni za wazawa zinazotekeleza miradi ya kusambaza umeme vitongojini kufanya kazi kwa ufanisi na weledi ili kujijengea uwezo wa kushindana kimataifa na kupata miradi nje ya nchi.

KATIBU MKUU CCM AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA

July 16, 2026 Add Comment
Katibu Mkuu Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Dkt. Asha-Rose Migiro, amefanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tone Tinnes, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Mfumo wa kidijitali wa JKCI kuboresha usajili na matibabu ya wagonjwa

July 16, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Arusha

Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), imezindua mfumo wa kidijitali wa usajili wa wagonjwa na teknolojia mpya ya kisasa ya Dozee ya kufuatilia hali ya mgonjwa hata kiwa nyumbani.

Kafulila Kutoa Mhadhara wa Umma SUA Kuhusu Ubia na Mageuzi ya Kilimo

July 16, 2026 Add Comment
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), kwa kushirikiana na Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP-Centre), imeandaa Mhadhara wa Umma utakaotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa PPP-CENTRE, David Kafulila, siku ya Ijumaa, Julai 17, 2026.

NEEC YAHITIMISHA MAFUNZO YA FURSA ZA MITAJI NA PROGRAMU ZA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI MKOANI RUKWA

July 16, 2026 Add Comment

Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC), kwa kushirikiana na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Rukwa, Mhe. Jacquline Mzindakaya, limehitimisha mafunzo ya utoaji elimu kuhusu fursa za mitaji kupitia mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi yaliyofanyika katika halmashauri zote nne za Mkoa wa Rukwa.

MCT YAFANYA MKUTANO WA MASHAURIANO NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI, YAIMARISHA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI

July 16, 2026 Add Comment


Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura, akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Siku Mbili wa Mashauriano kati ya MCT na viongozi wa vyombo vya habari unaofanyika mkoani Morogoro Julai 16–17, 2026. Mkutano huo unajadili mafanikio, changamoto na mustakabali wa tasnia ya habari nchini katika kipindi cha miaka 30 ya mfumo wa kujisimamia.

UMEME KUBADILISHA MAISHA YA WANANCHI VITONGOJINI

July 15, 2026 Add Comment
Serikali imedhamiria kubadilisha maisha ya wananchi vitongojini kupitia usambazaji wa umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wananchi wamehimizwa kuchangamkia kuunganishiwa umeme kwenye vitongoji vilivyofikiwa.

MHE.KILAKALA AIPONGEZA WIZARA YA NISHATI KWA KUENDELEA KUTOA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 15, 2026 Add Comment




Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kuandaa Warsha ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wanahabari na Maafisa habari, akisema mafunzo hayo ni hatua muhimu ya kuhakikisha elimu sahihi inawafikia wananchi na kuimarisha utekelezaji wa ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.


Akizungumza Julai 14, 2026 wakati wa ufunguzi wa Warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari, Maafisa Mawasiliano Serikalini wa Mikoa, Taasisi, Wizara pamoja na Taasisi zilizo  chini ya Wizara ya Nishati kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya nishati safi ya kupikia inayofanyika katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro amesema Mkoa wa Morogoro una vyanzo vingi vya maji vinavyopaswa kulindwa, hivyo ajenda ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia itasaidia kuhifadhi mazingira kwa kupunguza ukataji wa miti, kulinda afya za wananchi pamoja na kutunza vyanzo hivyo vya maji kwa manufaa ya kizazinkijacho.



Amesema elimu inayotolewa kupitia warsha hii ikiwafikia wananchi kwa usahihi, itasaidia kuongeza uelewa kuhusu maana na faida za nishati safi ya kupikia, hususan kwa jamii za vijijini, jambo litakalowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika juhudi za kulinda mazingira na kutumia nishati salama na nafuu.


Mhe. Kilakala amewataka washiriki kutoka Mikoa mbalimbali nchini kutumia maarifa waliyoyapata katika warsha hiyo kwa weledi mkubwa wanaporejea kwenye maeneo yao ya kazi kwani mafunzo haya yataongeza hamasa na kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na elimu ya nishati safi ya kupikia na hivyo kuchangia kufikiwa kwa malengo ya taifa ya kuhakikisha asilimia 80 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.

*ELIMU YA UMEME NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA WANANCHI ARUMERU MASHARIKI*

July 15, 2026 Add Comment



📌*Umeme sasa ni Kitongoji kwa Kitongoji*

📌*Nishati safi ya Kupikia kwa kila mwananchi*

📍*Arusha*

Wananchi wa Wilaya ya Arumeru Mashariki mkoani Arusha wameendelea kupata elimu kuhusu huduma za umeme na matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia ziara ya uhamasishaji iliyofanywa na maafisa wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Elimu hiyo ilitolewa leo wakati maafisa wa REA walipotembelea baadhi ya vijiji na vitongoji vinavyotekelezwa miradi mbalimbali ya nishati, ikiwemo miradi ya usambazaji wa umeme katika vitongoji pamoja na uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kama vile gesi na majiko banifu.

Katika ziara hiyo, wananchi walipatiwa elimu kuhusu taratibu za kufanya maombi ya kuunganishiwa umeme, gharama za uunganishaji wa huduma hiyo pamoja na tahadhari ya kujiepusha na matapeli maarufu kama vishoka, ambao huwalaghai wananchi kwa kuwatoza fedha kinyume na utaratibu rasmi.

Aidha, wananchi walihimizwa kujiunga na huduma ya umeme wakati mkandarasi bado yupo katika eneo la mradi, kwani hatua hiyo hurahisisha upatikanaji wa huduma kwa gharama nafuu. Walielezwa kuwa Serikali tayari imegharamia ujenzi wa miundombinu ya kufikisha umeme katika maeneo yao, hivyo mwananchi anabaki na jukumu la kuweka mfumo wa waya (wiring) ndani ya nyumba na kulipia gharama ya kuunganishiwa umeme ya shilingi 27,000 tu.

Maafisa wa REA pia waliwahimiza wananchi kutumia umeme kwa shughuli za uzalishaji mali ili kuongeza kipato na kuboresha maisha yao. Walisisitiza kuwa dhana ya “Kijijini kama Mjini” inapaswa kutekelezwa kwa vitendo kupitia matumizi ya umeme katika biashara, viwanda vidogo, huduma za kijamii na shughuli nyingine za maendeleo, badala ya kubaki kuwa nadharia.

Vilevile, wananchi walikumbushwa umuhimu wa kutunza miundombinu ya umeme kwa kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi hiyo. Walihimizwa kushiriki kulinda miundombinu hiyo na kutoa taarifa kwa mamlaka husika pindi wanapoona vitendo vinavyoweza kuhatarisha au kuharibu huduma ya umeme.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za REA za kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu huduma za umeme na matumizi ya nishati safi ya kupikia, ili kuongeza matumizi ya nishati hizo na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika maeneo ya vijijini.

*Mwisho.*




 

KAMATI YA KITAIFA YA UFUNGAJI MIGODI YAKAGUA MPANGO WA UFUNGAJI MGODI WA BARRICK BULYANHULU

July 15, 2026 Add Comment
Meneja wa Mahusiano ya Jamii wa Barrick Bulyanhulu, Agapit Paul, akitoa maelezo kuhusu shughuli za uendeshaji wa mgodi kwa wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi (NMCC) wakati wa ziara yao ya kikazi mgodini.

SHERIA BORA NI MSINGI WA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050 – MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

July 15, 2026 Add Comment
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amefungua mafunzo ya tatu ya Bespoke kwa Mawakili wa Serikali, yalioandaliwa na kuratibiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambayo yameanza tarehe 15 Julai, 2026 na yatahimishwa tarehe 17 Julai, 2026 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano Arusha (AICC) Jijini Arusha.

OSHA YATAJWA MIONGONI MWA TAASISI ZA KIMKAKATI NCHINI

July 15, 2026 Add Comment
Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Usimamizi Rasilimali Watu katika Taasisi za Umma-Ofisi ya Msajili wa Hazina, Bw. Hussein Kakurwa, akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Bodi ya Ushauri katika mafunzo elekezi ya Bodi ya OSHA yaliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha Mkoani Pwani.

WANAHABARI NI WASHIRIKA MUHIMU WA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 15, 2026 Add Comment




Naibu Waziri wa Nishati amesema vyombo vya habari na maafisa mawasiliano Serikalini ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kutokana na nafasi yao ya kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni pamoja na majukwaa ya kidijitali.


Hayo ameyabainisha leo Julai 14, 2026 wakati akifungua Warsha ya Kuwajengea Uwezo Waandishi wa Habari na Maafisa Mawasiliano Serikalini kutoka katika Wizara na Taasisi  kuhusu Uandishi na Uhamasishaji wa Masuala ya Nishati Safi ya Kupikia, inayofanyika katika ukumbi wa Morena hoteli mkoani Morogoro.

Amesema vyombo vya habari si wasambazaji wa taarifa pekee bali ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kwa kutoa taarifa sahihi huku akibainisha kuwa kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni, makala pamoja na maudhui ya kidijitali, wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga uelewa wa wananchi, kuondoa dhana potofu na kuhamasisha mabadiliko chanya ya tabia kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia  kwani katika zama za mawasiliano ya kidijitali, taarifa moja sahihi inaweza kuwafikia mamilioni ya wananchi ndani ya muda mfupi na kuleta mabadiliko makubwa katika jamii.

Amefafanua kuwa, taarifa zisizo sahihi zinaweza kusababisha upotoshaji na kuchelewesha utekelezaji wa ajenda muhimu za maendeleo akimnukuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) uliofanyika jijini Arusha, amesema watu wanaweza kushiriki kubomoa Tanzania, lakini hawawezi kusaidia kuijenga hivyo amesisitiza kuwa wanahabari wana wajibu wa kutumia kalamu na keybord zao kuandika habari zenye ukweli, zenye kujenga matumaini na kuunga mkono juhudi za maendeleo ya Taifa badala ya taarifa zinazoweza kupotosha wananchi.

Aidha Mhe. Salome ameeleza kuwa, matarajio ya Serikali ni kuwa mafunzo hayo yatawaongezea washiriki maarifa na ujuzi wa kuandaa habari zenye usahihi, ushahidi na weledi wa hali ya juu, pamoja na kuandaa maudhui yanayoonesha mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia, ubunifu wa sekta binafsi na fursa zilizopo katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo.

Ameongeza kuwa warsha hiyo itawajengea uwezo washiriki kuhusu sera, mikakati na mwelekeo wa Serikali katika sekta ya nishati safi ya kupikia, matumizi sahihi ya takwimu pamoja na namna bora ya kuripoti kuhusu teknolojia mbalimbali zinazopatikana nchini ili kuandaa taarifa zenye ubora na zinazojenga uelewa wa wananchi.


Aidha, amewataka washiriki kutumia kikamilifu fursa ya mafunzo hayo kujenga ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati, Idara ya Habari MAELEZO, washirika wa maendeleo, sekta binafsi na vyombo vya habari, akisisitiza kuwa mawasiliano sahihi ni nguzo muhimu ya kufanikisha ajenda ya nishati safi ya kupikia na kufikia lengo la asilimia 80 ya matumizi ifikapo mwaka 2034.



USHIRIKIANO WA ORYX GAS NA SKAUTI KUCHOCHEA MATUMIZI SALAMA YA NISHATI SAFI

July 15, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Tanzania imezindua kitabu cha Mwongozo wa Matumizi Salama ya Gesi ya LPG na kusaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu na Chama cha Skauti Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha elimu ya matumizi salama ya gesi ya kupikia kwa wananchi kupitia mtandao wa vijana wa Skauti nchini.

NAIBU WAZIRI SALOME AWASILI MOROGORO KUFUNGUA WARSHA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 15, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, akiwasili katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro kwa ajili ya kufungua warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari pamoja na Maafisa Mawasiliano wa Serikali kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya Nishati Safi ya Kupikia.

Warsha hiyo imeandaliwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF), kupitia Mradi wa CookFund unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Salome ameambatana na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Nishati, Bi. Nteghenjwa Hosseah na Meneja wa Mradi wa CookFund – UNCDF, Bw. Imanuel Muro.




LINDI KUENEZA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA WOTE

July 15, 2026 Add Comment







📌 Majiko banifu 5,776 kusambazwa mkoani Lindi




Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, amesema Mkoa wa Lindi umeanza kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya juhudi za kufikia lengo la kitaifa la kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Bi. Omary amesema hayo leo, Julai 15, 2026, alipokutana na Afisa Mshauri Mwandamizi wa Masuala ya Kiufundi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Deusdedit Malulu, aliyeambatana na uongozi wa Kampuni ya Tango Energy Limited, inayotekeleza usambazaji wa majiko banifu mkoani Lindi.

“Nawapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Tunamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na tutaendelea kutoa elimu ili iwafikie wananchi wote,” amesema Bi. Omary.

Kwa upande wake, Mha. Malulu amesema jumla ya majiko banifu 5,776 yameanza kusambazwa na Kampuni ya Tango Energy Limited katika maeneo ya Lindi, Ruangwa, Nachingwea, Liwale na Kilwa.

Mha. Malulu amewataka wananchi katika maeneo hayo kuchangamkia fursa ya kupata majiko banifu kwa bei nafuu ya ruzuku ya shilingi 7,600 tu kwa jiko.

Naye, Meneja wa Mauzo wa Tango Energy Limited, Bw. Emmanuel Ibrahim, amesema mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kiasi kidogo cha kuni na mkaa, hatua inayolenga kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati pamoja na athari za moshi unaotokana na matumizi ya majiko ya kawaida.

Kupitia mradi huo, Tango Energy Limited itasambaza jumla ya majiko banifu 5,776 kwa wananchi kwa bei ya ruzuku. Bei halisi ya jiko moja ni TZS 50,847.46, lakini Serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85, hivyo mwananchi atanunua jiko kwa TZS 7,600 tu.