
HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
RAIS MSTAAFU JAKAYA MRISHO KIKWETE ASHIRIKI UFUNGUZI WA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA UMOJA WA AFRIKA ADDIS ABABA
Mheshimiwa Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, katika nafasi zake za Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Elimu Duniani – Global Partnership for Education (GPE) – pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Maji Kusini mwa Afrika – Global Water Partnership Southern Africa (GWPSA), ameshiriki katika Ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika, uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia.
Katika mkutano huo wa ngazi ya juu, Rais Mstaafu alipata fursa ya kuonana na kufanya mazungumzo mafupi na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, pia alikutana na kufanya mazungumzo na Wakuu wa Nchi na Serikali waliopo madarakani, Wakuu wa Nchi Wastaafu wenzie pamoja na viongozi mbalimbali kutoka Barani Afrika, wakijadiliana masuala ya maendeleo, elimu na rasilimali maji kwa mustakabali wa Bara la Afrika.
Ushiriki wake katika mkutano huo umeendeleza mchango wa Tanzania katika mijadala ya kimkakati inayolenga kuimarisha ushirikiano na maendeleo endelevu.
![]() |
MBUNGE WA TANGA MJINI AAGANA NA WAGENI KUTOKA QATAR NA OMAN
MBUNGE WA TANGA MJINI AAGANA NA WAGENI KUTOKA QATAR NA OMAN WALIOKUJA KUJITOLEA TANGA MJINI.
Mapema leo asubuhi, Mheshimiwa Kassimu Amari Mbaraka (Makbel), Mbunge wa Tanga Mjini, alikutana na kuagana rasmi na wageni wake kutoka Mataifa ya Qatar na Oman waliokuja Mkoani Tanga kwa dhamira ya kujitolea na kuchangia maendeleo ya kijamii.
Wageni hao walifika Jijini Tanga kwa ajili ya kushiriki katika ukarabati wa Shule ya Msingi Tongoni, pamoja na kutoa msaada wa vifaa vya malazi katika Shule ya Wanafunzi wenye mahitaji maalum, hatua iliyopokelewa kwa furaha na shukrani kubwa kutoka kwa wananchi na uongozi wa Jiji la Tanga.
Katika mazungumzo yao ya kuagana yaliyofanyika ofisini kwa Mheshimiwa Mbunge, wageni hao walieleza kufurahishwa kwao na ukarimu mkubwa walioupata kutoka kwa wananchi wa Tanga pamoja na ushirikiano wa karibu kutoka kwa viongozi wa Jiji.
Walisema wameguswa sana na mapokezi mazuri na mshikamano waliouona, wakaahidi kuendeleza ushirikiano huo kwa maslahi mapana ya maendeleo ya Tanga.
Ikumbukwe kuwa wakati wa kampeni zake, Mheshimiwa Mbunge alisisitiza umuhimu wa kutumia fursa ya Diaspora kama chachu ya maendeleo ya Tanga.
Ujio wa wageni hao ni ishara ya utekelezaji wa maono hayo, yakionesha namna ushirikiano wa Kimataifa unavyoweza kuleta matokeo chanya kwa jamii.
Kwa upande wake, Mheshimiwa Mbunge aliwashukuru sana wageni hao kwa moyo wao wa kujitolea na mchango wao mkubwa wa kijamii na kimaendeleo.
Kama ishara ya kuthamini juhudi zao, aliwakabidhi vyeti vya shukrani kwa niaba ya wananchi wa Tanga Mjini.
*Imetolewa na Idara ya* *habari mawasiliano ofisi ya Mbunge*
*Tanga Mjini*
GOOD NEWS FOR TANZANIA DIGITAL CONTENT CREATORS AS NEW LICENCE FEES ANNOUNCED
The Government has announced a historic measure that could significantly transform the landscape of Tanzania’s digital content industry.
Speaking at the Annual Broadcasting Service Providers Conference (ABC 2026) in Dodoma, the Deputy Minister for Information, Culture, Arts and Sports, Hamisi Mwinjuma, revealed that the licence fee for online content creators has been reduced from TSh 500,000 to just TSh 50,000, with an application fee of only TSh 10,000.
This represents a reduction of more than 90 per cent — a move widely interpreted as opening a new door for young innovators, bloggers, and digital creators who had previously struggled with the high cost of compliance.
The decision follows nearly a year of strategic consultations between the Tanzania Bloggers Network (TBN) and the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), aimed at addressing financial barriers that had constrained the growth of digital journalism and online content production in the country.
In addition, licence fees for Online Content Aggregators have been reduced from TSh 1,000,000 to TSh 100,000.
A new “Amateur” category has also been introduced specifically for emerging young creators, enabling them to formalise their activities and nurture their talents without heavy financial burdens.
Within the broader context of a rapidly expanding digital economy, this decision is expected to stimulate employment, creativity, and tax revenue generation — in line with the development vision championed by President Samia Suluhu Hassan.
If effectively implemented, these reforms may well mark the beginning of a new chapter for Tanzania’s digital creative sector.
URAMBO NA KALIUA ZIPO TAYARI KWA UWEKEZAJI-WAZIRI NDEJEMBI
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema wilaya za Urambo na Kaliua mkoani Tabora zipo tayari kwa uwekezaji, hususan wa viwanda kwani umeme unaopatikana katika Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme Urambo unatosheleza na hata kuzidi mahitaji ya sasa.
Amesema hayo leo, tarehe 14 Februari 2026, wakati akikagua mradi wa njia ya kusafirisha umeme msongo wa Kilovoti 132 kutoka Tabora hadi Urambo na Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Uhuru - Urambo cha Megawati 24.
“Urambo ipo tayari kwa uwekezaji. Uwezo wa kituo cha Urambo ni megawati 24, lakini matumizi ya wilaya mbili za Kaliua na Urambo ni megawati 2.5 wakati wa mchana na wakati wa usiku ambacho ni kipindi watu wengi wanakuwa majumbani, kiwango cha juu cha matumizi ni megawati 7,” amesisitiza Ndejembi.
Ndejembi amesema lengo na dhamira ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kunakuwa na nishati ya umeme ya uhakika ili kuendelea kuchochea uwekezaji katika maeneo yote nchini, kwani nishati ya umeme ni kichocheo cha sekta zote.
Amesema wilaya za Urambo na Kaliua zimejikita zaidi katika kilimo hususan zao la Tumbaku, zao ambalo linahitaji kuongezewa thamani kupitia viwanda vilivyokuwa vinahitaji umeme wa uhakika.
Aidha, Ndejembi amesisitiza kuwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tayari ametoa zaidi ya trilioni 1.9 kwa Wizara ya Nishati kupitia TANESCO kwa ajili ya Mradi wa Gridi Imara kujenga vituo vya kupoza na njia za kusafirisha umeme wa kutosha na wa uhakika katika maeneo mbalimbali nchini.
![]() |
Kadhalika, Mhe. Ndejembi amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Urambo, Magreth Sitta ambaye alitoa eneo la hekari 20 lililotumika kujenga Kituo hicho cha Kupooza Umeme.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange, amesema mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme Urambo ulianza kutekelezwa Septemba 2021 kwa gharama ya shilingi bilioni 44. Kati ya hizo, bilioni 24 zilitumika kujenga njia ya kusafirisha umeme, bilioni 16 zimejenga kituo cha kupoza na bilioni 4 ilitumika kufidia wananchi waliopitwa na mradi.
Twange amesema kituo hicho kilianza kufanya kazi mwezi Machi 2025, ambapo ujenzi wa njia ya umeme pamoja na kituo cha kupokea na kupooza umeme vyote vimekamalika kwa asilimia 100.
KAYA FOUNDATION YAKABIDHI VITI MWENDO, BIMA ZA AFYA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU
habariWAZIRI MCHENGERWA AFANYA MAZUNGUMZO YA KUOKOA VIFO VYA MAMA NA MTOTO NA BOSI WA STBF
Na John Mapepele, Addis Abbaba
Waziri wa Afya, Mheshimiwa Mohamed Omari Mchengerwa, leo Februari 14, 2026 amekutana na Makamu wa Rais wa Susan Thompson Buffet Foundation (STBF), Prof Senait Fisseha, jijini Addis Ababa kwenye Mkutano wa pembezoni mwa kilele cha Kongamano la 39 la Umoja wa Afrika na kufanya mazungumzo ya kimkakati katika kukabiliana na changamoto ya vifo vya mama na mtoto.
STBF ni miongoni mwa wafadhili wakubwa wa Serikali katika uimarishaji wa mifumo ya afya hususani katika kupunguza vifo vitokanavyo uzazi.
Aidha, Mheshimiwa Waziri Mchengerwa akiwa na Katibu Mkuu, Dkt. Seif Shekalaghe amelishukuru STBF kwa msaada wa fedha wa kiasi cha Dola za Marekani milioni 36.8 zilizotolewa kati ya 2021 - 2025 ambazo zimesaidia katika kuimarisha mifumo ya afya na hivyo kuchangia katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, watoto na vijana.
Mheshimiwa Mchengerwa alichukuwa fursa hii kumuomba Prof. Sinait kuangalia mpango wa Tanzania wenye nia kuendeza ajenda ya kukinga na kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi kupitia uimarishaji wa mifumo ya afya.
Kwa upande wake, Prof. Fisseha ameshukuru kwa ushirikiano uliopo baina ya Taasisi yake na Serikali ya Tanzania katika kipindi chote cha utekelezaji wa mradi huo.
"Ninashukuru kuona kuwa ajenda ya kukinga na kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi Afrika ipo mikononi mwa Rais mwanamke Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye amefanya kazi nzuri ". Amefafanua Prof. Fisseha
Vilevile ameahidi kuwa STBF litaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuweka raslimali fedha ili kuimarisha mifumo ya afya kwenye huduma za mama na mtoto.
Tanzania ni nchi inayopigiwa mfano na nchi za Umoja wa Afrika kwa kufanya vizuri katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
WAZIRI NDEJEMBI AWASILI TABORA KWA ZIARA YA KIKAZI
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amewasili wilayani Urambo Mkoani Tabora kwa ziara ya Kikazi na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Dkt. Khamis Mkanachi, leo tarehe 14 Februari 2026.
Katika Ziara hiyo Waziri Ndejembi atatembelea na kukagua Kituo cha kupooza na Kusambaza umeme wilayani Urambo pamoja na kutembelea na kukagua kiwanda kiwada cha kuzalisha Nguzo za Zege katika Manispaa ya Tabora.
TANROADS Dodoma yapokea bilioni 15.6 Kutoka Mfuko wa Barabara
habari
WANANCHI WATAKIWA KUTAMBUA HAKI ZAO ILI KUJENGA SOKO HURU, SHINDANI NA LA HAKI
habari
KIGOMA
Baraza la Ushindani(FCT), moja ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, imeendesha kikao cha kuwajengea uwezo watumiaji wa huduma, wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kigoma kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za ushindani na taratibu za rufaa.
Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Lake Tanganyika Hotel na kuhudhuriwa na wadau kutoka sekta mbalimbali za biashara na huduma.
Akifungua kikao hicho, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Ndg. Deogratias Sangu, aliwataka wananchi kutumia elimu waliyoipata kuelewa haki zao katika ushindani na udhibiti wa soko. Alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani utasaidia kupunguza migogoro isiyo ya lazima, kuimarisha uwajibikaji wa taasisi na kujenga mazingira ya Soko yenye usawa na haki.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa FCT, Mhe. Jaji Rose Ally Ebrahim, alisema Baraza lina jukumu la kusikiliza na kuamua rufaa zinazotokana na maamuzi ya Fair Competition Commission (FCC) pamoja na mamlaka za udhibiti wa sekta mbalimbali ikiwemo LATRA, EWURA, TCRA, TCAA na PURA.
Aliwahimiza wananchi wa Kigoma kulitumia Baraza hilo wanapokuwa hawajaridhishwa na maamuzi ya vyombo husika, akisisitiza kuwa mfumo wa rufaa umewekwa kisheria ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati na kwa uwazi.
“Watu wakijua wapi pa kupata haki, wanapunguza gharama za kuhangaika kutoka sehemu moja ya huduma hadi nyingine,” alisema Mhe. Jaji Ebrahim, akisisitiza kuwa elimu ya sheria ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha wananchi na wafanyabiashara kukua kiuchumi.
Wadau waliohudhuria kikao hicho waliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kuimarisha taasisi zinazolinda na kusimamia haki za wafanyabiashara na watumiaji wa huduma.
Walisema juhudi hizo zinaonyesha dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika uchumi kupitia mfumo wa ushindani ulio wazi, shindani na wa haki, unaochochea ukuaji wa biashara na ustawi wa taifa.
































