HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
MHE.KILAKALA AIPONGEZA WIZARA YA NISHATI KWA KUENDELEA KUTOA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kuandaa Warsha ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wanahabari na Maafisa habari, akisema mafunzo hayo ni hatua muhimu ya kuhakikisha elimu sahihi inawafikia wananchi na kuimarisha utekelezaji wa ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.
Akizungumza Julai 14, 2026 wakati wa ufunguzi wa Warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari, Maafisa Mawasiliano Serikalini wa Mikoa, Taasisi, Wizara pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya nishati safi ya kupikia inayofanyika katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro amesema Mkoa wa Morogoro una vyanzo vingi vya maji vinavyopaswa kulindwa, hivyo ajenda ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia itasaidia kuhifadhi mazingira kwa kupunguza ukataji wa miti, kulinda afya za wananchi pamoja na kutunza vyanzo hivyo vya maji kwa manufaa ya kizazinkijacho.
Amesema elimu inayotolewa kupitia warsha hii ikiwafikia wananchi kwa usahihi, itasaidia kuongeza uelewa kuhusu maana na faida za nishati safi ya kupikia, hususan kwa jamii za vijijini, jambo litakalowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika juhudi za kulinda mazingira na kutumia nishati salama na nafuu.
Mhe. Kilakala amewataka washiriki kutoka Mikoa mbalimbali nchini kutumia maarifa waliyoyapata katika warsha hiyo kwa weledi mkubwa wanaporejea kwenye maeneo yao ya kazi kwani mafunzo haya yataongeza hamasa na kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na elimu ya nishati safi ya kupikia na hivyo kuchangia kufikiwa kwa malengo ya taifa ya kuhakikisha asilimia 80 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.
*ELIMU YA UMEME NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA WANANCHI ARUMERU MASHARIKI*
SHERIA BORA NI MSINGI WA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050 – MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
habariOSHA YATAJWA MIONGONI MWA TAASISI ZA KIMKAKATI NCHINI
habariWANAHABARI NI WASHIRIKA MUHIMU WA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
NishatiNaibu Waziri wa Nishati amesema vyombo vya habari na maafisa mawasiliano Serikalini ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kutokana na nafasi yao ya kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni pamoja na majukwaa ya kidijitali.
Hayo ameyabainisha leo Julai 14, 2026 wakati akifungua Warsha ya Kuwajengea Uwezo Waandishi wa Habari na Maafisa Mawasiliano Serikalini kutoka katika Wizara na Taasisi kuhusu Uandishi na Uhamasishaji wa Masuala ya Nishati Safi ya Kupikia, inayofanyika katika ukumbi wa Morena hoteli mkoani Morogoro.
Amesema vyombo vya habari si wasambazaji wa taarifa pekee bali ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kwa kutoa taarifa sahihi huku akibainisha kuwa kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni, makala pamoja na maudhui ya kidijitali, wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga uelewa wa wananchi, kuondoa dhana potofu na kuhamasisha mabadiliko chanya ya tabia kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia kwani katika zama za mawasiliano ya kidijitali, taarifa moja sahihi inaweza kuwafikia mamilioni ya wananchi ndani ya muda mfupi na kuleta mabadiliko makubwa katika jamii.
Amefafanua kuwa, taarifa zisizo sahihi zinaweza kusababisha upotoshaji na kuchelewesha utekelezaji wa ajenda muhimu za maendeleo akimnukuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) uliofanyika jijini Arusha, amesema watu wanaweza kushiriki kubomoa Tanzania, lakini hawawezi kusaidia kuijenga hivyo amesisitiza kuwa wanahabari wana wajibu wa kutumia kalamu na keybord zao kuandika habari zenye ukweli, zenye kujenga matumaini na kuunga mkono juhudi za maendeleo ya Taifa badala ya taarifa zinazoweza kupotosha wananchi.
Aidha Mhe. Salome ameeleza kuwa, matarajio ya Serikali ni kuwa mafunzo hayo yatawaongezea washiriki maarifa na ujuzi wa kuandaa habari zenye usahihi, ushahidi na weledi wa hali ya juu, pamoja na kuandaa maudhui yanayoonesha mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia, ubunifu wa sekta binafsi na fursa zilizopo katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo.
Ameongeza kuwa warsha hiyo itawajengea uwezo washiriki kuhusu sera, mikakati na mwelekeo wa Serikali katika sekta ya nishati safi ya kupikia, matumizi sahihi ya takwimu pamoja na namna bora ya kuripoti kuhusu teknolojia mbalimbali zinazopatikana nchini ili kuandaa taarifa zenye ubora na zinazojenga uelewa wa wananchi.
Aidha, amewataka washiriki kutumia kikamilifu fursa ya mafunzo hayo kujenga ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati, Idara ya Habari MAELEZO, washirika wa maendeleo, sekta binafsi na vyombo vya habari, akisisitiza kuwa mawasiliano sahihi ni nguzo muhimu ya kufanikisha ajenda ya nishati safi ya kupikia na kufikia lengo la asilimia 80 ya matumizi ifikapo mwaka 2034.
USHIRIKIANO WA ORYX GAS NA SKAUTI KUCHOCHEA MATUMIZI SALAMA YA NISHATI SAFI
habariNAIBU WAZIRI SALOME AWASILI MOROGORO KUFUNGUA WARSHA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
NishatiNaibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, akiwasili katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro kwa ajili ya kufungua warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari pamoja na Maafisa Mawasiliano wa Serikali kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya Nishati Safi ya Kupikia.
Warsha hiyo imeandaliwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF), kupitia Mradi wa CookFund unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya.
Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Salome ameambatana na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Nishati, Bi. Nteghenjwa Hosseah na Meneja wa Mradi wa CookFund – UNCDF, Bw. Imanuel Muro.
LINDI KUENEZA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA WOTE
habari Nishati
📌 Majiko banifu 5,776 kusambazwa mkoani Lindi
Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, amesema Mkoa wa Lindi umeanza kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya juhudi za kufikia lengo la kitaifa la kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
Bi. Omary amesema hayo leo, Julai 15, 2026, alipokutana na Afisa Mshauri Mwandamizi wa Masuala ya Kiufundi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Deusdedit Malulu, aliyeambatana na uongozi wa Kampuni ya Tango Energy Limited, inayotekeleza usambazaji wa majiko banifu mkoani Lindi.
“Nawapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Tunamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na tutaendelea kutoa elimu ili iwafikie wananchi wote,” amesema Bi. Omary.
Kwa upande wake, Mha. Malulu amesema jumla ya majiko banifu 5,776 yameanza kusambazwa na Kampuni ya Tango Energy Limited katika maeneo ya Lindi, Ruangwa, Nachingwea, Liwale na Kilwa.
Mha. Malulu amewataka wananchi katika maeneo hayo kuchangamkia fursa ya kupata majiko banifu kwa bei nafuu ya ruzuku ya shilingi 7,600 tu kwa jiko.
Naye, Meneja wa Mauzo wa Tango Energy Limited, Bw. Emmanuel Ibrahim, amesema mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kiasi kidogo cha kuni na mkaa, hatua inayolenga kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati pamoja na athari za moshi unaotokana na matumizi ya majiko ya kawaida.
Kupitia mradi huo, Tango Energy Limited itasambaza jumla ya majiko banifu 5,776 kwa wananchi kwa bei ya ruzuku. Bei halisi ya jiko moja ni TZS 50,847.46, lakini Serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85, hivyo mwananchi atanunua jiko kwa TZS 7,600 tu.







WAZIRI KOMBO APOKEA RASMI KOMBE LA USHINDI WA WANADIPLOMASIA DHIDI YA WABUNGE KATIKA BONANZA LA CRDB
habariZAIDI YA WAKAZI 5,000 BABATI WAFURAHIA MAJISAFI MRADI WA BILIONI 1.9
habariWanufaika waipongeza kambi ya matibabu Arusha
habariEAC YAIMARISHA MFUMO WA KURAHISISHA BIASHARA ZA MIPAKANI
habariNa Oscar Assenga,MKINGA
JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC) imeeleza itaendelea kuimarisha utekelezaji wa Mfumo Rahisi wa Biashara (Simplified Trade Regime-STR) ili kurahisisha biashara za mipakani, kuwawezesha wafanyabiashara wadogo kuongeza uzalishaji, kupanua masoko ya bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda na kupunguza gharama za biashara.
Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayeshughulikia Forodha, Biashara na Fedha, Annette Semuwamba, wakati alipotembelea Kituo cha Huduma cha Pamoja Mpakani (One Stop Border Post-OSBP) cha Horohoro wilayani Mkinga, mkoani Tanga.
Ziara hiyo ni sehemu ya tathmini ya utekelezaji wa Mfumo Rahisi wa Biashara katika vituo saba vya Huduma vya Pamoja Mpakani vilivyopo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Semuwamba alisema EAC itaendelea kushirikiana na nchi wanachama na wadau mbalimbali kuhakikisha wafanyabiashara wadogo wanaovuka mipaka wanapata mazingira rafiki kupitia taratibu rahisi za forodha.
“Tumefurahishwa kuona biashara kati ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inaendelea kukua. Kinachotutia moyo zaidi ni kwamba bidhaa nyingi zinazovuka mipaka ni bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda wetu,” alisema.
Alisema uwekezaji uliofanywa katika miundombinu ya vituo vya Huduma vya Pamoja Mipakani umechangia kupunguza muda wa kuhudumia mizigo na wasafiri, kupunguza gharama za biashara na kusaidia kushusha bei za bidhaa kwa walaji.
Aidha, aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa kufunga mashine ya kisasa ya ukaguzi wa mizigo (scanner) katika mpaka wa Horohoro/Lunga Lunga, akisema hatua hiyo itaharakisha ukaguzi na uondoshaji wa mizigo.
Semuwamba alipendekeza pia kuanzishwa kwa mfumo wa kubadilishana picha za mizigo iliyokaguliwa kwa kutumia mashine hizo kati ya vituo vya Huduma vya Pamoja Mipakani ili kupunguza gharama za uwekezaji wa vifaa hivyo katika maeneo mengine ya mipakani.
Awali, Mkuu wa Kituo cha Huduma cha Pamoja Mpakani Horohoro, Shadrack Mbonea, alisema kituo hicho kimechangia kwa kiasi kikubwa kurahisisha biashara na usafirishaji wa mizigo kati ya Tanzania na Kenya.
Alisema Horohoro ni miongoni mwa vituo saba vya Huduma vya Pamoja Mipakani nchini vinavyowezesha wasafiri, magari na mizigo kupata huduma zote za mipakani katika eneo moja badala ya kuhudumiwa kila upande wa mpaka.
“Kituo hiki kilianza majaribio ya utoaji wa huduma kwa mfumo wa One Stop Border Post mwezi Septemba 2021 na tangu wakati huo kimeendelea kufanya kazi kwa mafanikio makubwa,” alisema.
Mbonea alisema kituo hicho kina taasisi 19 za Serikali zinazoongozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), zikiwemo Idara ya Uhamiaji, Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), TASAC, Tume ya Madini, Idara ya Uvuvi, Idara ya Mifugo, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Alisema taasisi hizo zina jukumu la kukusanya mapato ya Serikali, kurahisisha biashara, kulinda jamii dhidi ya bidhaa hatarishi, kutekeleza sera za biashara, kukusanya takwimu za biashara za mipakani na kudhibiti magendo.
Kwa mujibu wa Mbonea, hapo awali mfumo wa OSBP ulikuwa ukifanya kazi kwa saa 12 kwa siku, hali iliyowalazimu wasafiri na wasafirishaji wa mizigo kukamilisha taratibu za forodha katika kila upande wa mpaka.

Alisema kupitia makubaliano kati ya Tanzania na Kenya, huduma sasa zinatolewa kwa saa 24, hatua iliyopunguza muda wa kusubiri na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma.
Aidha, alisema kituo hicho kinatekeleza Mfumo Rahisi wa Biashara unaowawezesha wafanyabiashara wadogo wanaosafirisha bidhaa zenye thamani isiyozidi dola za Marekani 2,000 kutumia taratibu rahisi za forodha.
“Tumeanzisha dawati maalumu la kuwahudumia wafanyabiashara wadogo, tumerahisisha utaratibu wa ukadiriaji wa kodi kwa kutumia fomu ya F88 na tunatambua Vyeti Rahisi vya Asili ya Bidhaa vinavyotolewa na mamlaka za Kenya,” alisema.
Aliongeza kuwa kituo hicho pia kinatekeleza Mfumo wa Himaya Moja ya Forodha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Single Customs Territory-SCT), ambao umechangia kupunguza muda wa uondoshaji wa mizigo, kushusha gharama za biashara na kuondoa vikwazo vya biashara ndani ya ukanda.
Alisema ushirikiano kati ya Horohoro na Lunga Lunga umeimarisha mapambano dhidi ya magendo kupitia doria za pamoja, mikutano ya kila robo mwaka na utoaji wa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu taratibu za biashara za mipakani.
Takwimu zinaonyesha kuwa thamani ya bidhaa zinazouzwa nje kupitia mpaka wa Horohoro/Lunga Lunga imeongezeka kutoka Sh milioni 306.4 mwaka wa fedha 2022/23 hadi Sh milioni 548 mwaka 2024/25. Aidha, thamani ya bidhaa zinazoingizwa nchini kupitia mpaka huo imeongezeka kutoka Sh milioni 134.7 hadi Sh milioni 175.9 katika kipindi hicho.
Ongezeko hilo linaakisi mafanikio ya juhudi za EAC na nchi wanachama katika kuimarisha biashara za mipakani, kuongeza ushindani wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya.
MASWI: NGOS NI NGUZO MUHIMU YA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050
habariMKURUGENZI MKUU REA APOKEA TUZO YA USHINDI WA REA SABASABA 2026
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy, leo Julai 14, 2026, amepokea tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (Government Institutions Exhibitor), ambayo REA ilitwaa katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.
Tuzo hiyo imewasilishwa kwake na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya watumishi walioshiriki katika maonesho hayo.
Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mha. Saidy amewapongeza watumishi wa Wakala kwa juhudi, kujituma na ushirikiano wao ulioiwezesha REA kutwaa tuzo hiyo.
Aidha, amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na ushirikiano katika kutekeleza miradi ya REA vijijini na vitongojini, ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma za nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Mwisho
TAFITI ZINAZOFANYWA NA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA ZINA MCHANGO MKUBWA KATIKA TAIFA
Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 9,2026.
........................
TAFITI zinazofanywa na Tume ya kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), zimekuwa na mchango mkubwa katika Taifa hasa katika kuanzishwa kwa sheria mpya.
Hayo
yamebainishwa na Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya
Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi alipokuwa akizungumza na waandishi
wa habari katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba
Julai 9,2026.
‘’ Tafiti
tunazozifanya zina mchango mkubwa katika taifa kwani baadhi zimeleta sheria
na nyingine zilileta vifungu katika sheria,” alisema Chanzi.
Alisema hapo
awali maendeleo ya kidijitali yalikuwa siyo makubwa lakini yalipokuja Tume hiyo
ilifanya tafiti mwaka 2005 ambayo ilizaa sheria mbili, sheria ya miamala ya
kielektroniki na makosa ya kimtandao.
“Hatukuwa na sheria hizo hivyo baada ya utafiti tulipendekeza Serikalini na ilitunga hizo sheria na ndiyo maana tunaona watu wana udhubutu wa kutuma hela kwa njia ya kimtandao bila ya kuwa na wasiwasi wowote kwa kuwa wanajua zipo sheria,” alisema Chanzi.
Alisema
mwaka 2020 Tume hiyo ilifanya tafiti kuhusiana na ulinzi wa taarifa binafsi
kutokana na kuwa na umuhimu wake kama ambavyo zinavyolindwa katika katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.
Alisema
katika kuendana na kidijitali Tume imetekeleza wajibu wake na inaendelea na
utekelezaaji huo ambapo kwa sasa inafanya utafiti wa Akili Mnemba (AI) na hayo yote ni mapinduzi yay a kidijitali na
wao kama tume wanazifanya tafiti hizo na kuishauri Serikali iweze kuchukua
hatua zinazofaa kulingana na jamii yetu.
Chanzi
aliongeza kuwa wanaendelea kufanya tafiti na wanapozikabidhi sheria zimekuwa
zikitungwa jambo ambalo wanajivunia.
“Tafiti
tunazo zifanya siyo tu za kidijitali kwa mfano tulifanya teknolojia ya DNA
ambayo zamani ilikuwa haipo lakini Tume ilifanya tafiti na kukabidhi ripoti na
sheria ikatungwa na kwa kuwa tulikuwa na teknolojia lakini bila ya kuiwekea
sheria ya kuisimamia ingeweza kusababisha yasipatikane matokeo chanya ambayo
yangehitajika.
Chanzi
amesema misingi ambayo waliiweka kwenye ripoti zao wameweza kuiona ipo ndani ya
sheria na kuonesha jinsi gani mapendekezo wanayotoa yanavyochukuliwa na
kufanyiwa kazi.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.
TRA KUWAZAWADIA VIJANA 1020 WENYE MAWAZO BUNIFU
RAIS DKT.MWINYI AJIONEA MAFANIKIO YA TANESCO MAONESHO YA SABASABA
habari📌 Miradi mipya ya kusafirisha umeme kuimarisha upatikanaji wa umeme Zanzibar
📌 Serikali yawekeza Dola za Marekani milioni 282 kuongeza upatikanaji wa umeme na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo amejionea mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya umeme na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma kwa wananchi na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Katika ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, Mhe. Dkt. Mwinyi alipata fursa ya kujionea miradi ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme, teknolojia za matumizi bora ya umeme ikiwemo majiko sanifu yanayotumia umeme kwa ufanisi, huduma ya Luku Janja pamoja na mfumo wa Smart House unaomwezesha mtumiaji kufuatilia matumizi ya umeme kupitia simu ya mkononi.
Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa kujenga njia mpya tatu za kusafirisha umeme kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar kupitia nyaya zitakazopita chini ya bahari.
Ameeleza kuwa njia hizo zitajumuisha Dar es Salaam–Unguja, Tanga–Pemba na Kisiju–Mafia, na kwamba kukamilika kwake kutaongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na uwezo wa kuhudumia ongezeko la mahitaji ya umeme yanayotokana na ukuaji wa viwanda, sekta ya utalii, uwekezaji na shughuli nyingine za kiuchumi visiwani Zanzibar.
Bw. Twange amesema Serikali pia inaendelea kutekeleza mradi wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 282, ambapo Dola milioni 6 zimetengwa mahsusi kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).
“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea katika sekta ya umeme. Kupitia mradi huu wa Dola za Marekani milioni 282, tunaendelea kuimarisha miundombinu ya umeme, huku sehemu ya fedha hizo ikielekezwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na ZECO,” amesema Bw. Twange.
Aidha, amesema TANESCO imeendelea kuleta ubunifu wa kidijitali kupitia mfumo wa Smart House, unaomwezesha mwananchi kufuatilia matumizi ya umeme wa nyumba yake kupitia simu ya mkononi, hatua inayosaidia matumizi bora na yenye tija ya umeme.
Vilevile, Bw. Twange amesema mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme umefikia mafanikio makubwa, ambapo zaidi ya asilimia 90 ya wananchi waliopata majiko hayo wanaendelea kuyalipia kwa utaratibu wa makato kupitia ununuzi wa umeme wa LUKU, hatua inayorahisisha wananchi kumudu gharama za kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Jitihada hizo ni sehemu ya utekelezaji wa maono ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme ya uhakika na kutumia nishati safi katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, ikiwemo katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115, umeendelea kuweka msingi wa upatikanaji wa umeme wa kutosha unaowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
DG RUWASA AWAELEKEZA MAMENEJA WA MIKOA NA WILAYA KUZISHIRIKISHA CBWSOs KATIKA PROGRAMU ZOTE
habariREA YANG'ARA SABASABA 2026
🏆 *RAIS MWINYI ASHUHUDIA REA IKITWAA TUZO YA MUONESHAJI BORA WA TAASISI ZA SERIKALI*
🤝 *REA YAWASHUKURU WADAU KWA MCHANGO WAO KATIKA MAFANIKIO HAYO*
📍 Dar es Salaam
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameshuhudia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ukitwaa Tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (*Government Institutions Exhibitor*) katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.
Tuzo hiyo imepokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa REA, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya Wakala.
REA inawashukuru wadau wote waliotembelea banda lake, kujionea mafanikio na utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini, pamoja na kuendelea kuunga mkono jitihada za Wakala za kupeleka nishati ya umeme kwenye vitongoji.
Mwisho
NEEC YALETA ELIMU YA MITAJI KARIBU NA WANANCHI RUKWA
MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO SABASABA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), na kampuni zake Tanzu katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Mha.Mramba ametembelea banda hilo ili kuona huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo.







































