HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

NAIBU KATIBU MKUU FEDHA AAGIZA UJENZI WA MCHAKATO WA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU (BUSINESS PROCESSES) ZA KIDIGITALI

May 15, 2026 Add Comment

Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, akizungumza kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, wakati akifungua mafunzo kwa Menejimenti ya Wizara kuhusu Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza Kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kushoto), na Mhasibu Mkuu Wizara ya Fedha Fungu 21 CPA. Sostheness Mafuru (kulia) wakifuatilia mawasilisho mbalimbali yaliyotolewa na Wawezeshaji kutoka Kampuni ya Ushauri (KPMG) wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Wizara ya Fedha CPA, Evalisto Mwalongo, akitoa utambulisho wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Baadhi ya viongozi wa Idara, Vitengo na Watumishi wa Wizara ya Fedha, wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani), wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani), wakati wa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21 Wizara ya Fedha, CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara ya Fedha baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21, Wizara ya Fedha CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Fedha baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Meza kuu ikiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo (katikati), Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha Bw. Kenneth Nindie (kulia), na Mhasibu Mkuu Fungu 21 Wizara ya Fedha CPA. Sostheness Mafuru (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya maandalizi, baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, yaliyohusisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Morogoro)


Na. Chedaiwe Msuya, WF, Morogoro


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, amekiagiza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini cha Wizara ya Fedha kuratibu ujenzi wa mchakato wa utekelezaji wa majukumu (business processes) za kidigitali ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa majukumu ya Wizara.

Maagizo hayo yametolewa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Chotto Sendo, wakati akifungua mafunzo mafunzo ya Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani wa Wizara ya Fedha, kwa
Menejimenti ya Wizara hiyo, yaliyofanyika katika Hotel ya Morena mkoani Morogoro.

Alisema business processes mpya zinazotakiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa Mfumo wa Ununuzi (NeST), ufuatiliaji na udhibiti wa mapato kupitia big data analysis, ufuatiliaji wa miradi ya PPP, miradi ya alternative financing, ulipaji wa michango ya Serikali kwenye taasisi za kimataifa, na ufuatiliaji wa mapato yasiyo ya kodi.

Aidha, Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (M&E) kimetakiwa kuhakikisha kuwa business processes hizo zinajengwa kwa mfumo wa kielektroniki ili kurahisisha ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara ili kuimarisha uwajibikaji, uwazi na ufanisi wa mifumo ya kiutendaji.

Bw. Sendo, alifafanua kuwa mafunzo hayo yataiwezesha Menejimenti na Watumishi wa Wizara kuelewa dhana na mbinu za udhibiti wa ndani, kujifunza namna ya kuchambua viashiria hatarishi, na kuimarisha business processes zilizopo.

“Mwongozo huu utakuwa na manufaa makubwa ikiwemo kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na tathmini kwa njia za kidigitali, kuwezesha Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani kufanya tathmini kwa mujibu wa Mwongozo wa Kimataifa wa Ukaguzi wa Ndani wa mwaka 2024, na kuweka vigezo vya kupima ufanisi wa mifumo ya kiutendaji”, alisisitiza Bw. Sendo.

Aliwasisitiza washiriki wa mafunzo hayo kufuatilia kwa umakini ili kuutumia Mwongozo huo kuboresha mfumo wa udhibiti wa ndani katika maeneo yao ya kazi ili kuimarisha uchumi wa taifa kupitia usimamizi bora wa rasilimali za umma.

Naye Kaimu Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Kenneth Nindie, alitoa rai kwa Idara zote za Serikali kuhakikisha wanatumia vizuri Mwongozo huo ili uweze kuwasaidia kuweka taratibu vizuri na malengo ya Wizara yanafikiwa kwa ufasaha.

Kwa upande wake, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali Msaidizi Bw. Abraham Msechu, amesema kuwa mafunzo yatasaidia Menejimenti ya Wizara kupata uelewa wa Mwongozo wa Udhibiti wa Ndani na kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ndani.

Akizungumzia mafunzo hayo mmoja wa washiriki, Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Madeni, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama, aliahidi kuyafanyia kazi mafunzo yote waliyopata katika Idara na Vitengo ili kufikia malengo ya Serikali katika udhibiti wa ndani.


Mafunzo hayo yamewajumuisha Menejimenti ya Wizara ya Fedha pamoja na Watumishi wa Wizara na Wawezeshaji kutoka Kampuni ya Ushauri (KPMG).

JUMUIYA YA UMOJA WA ULAYA (EU) YASHIRIKIANA NA SERIKALI KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA NCHI KIGOMA

May 15, 2026 Add Comment

       

Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Bunge na Uratibu na wenye Ulemavu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU) imeanza utekelezaji wa mradi wa Mwitikio wa Kikanda dhidi ya Uhamaji Unaotokana na Mabadiliko ya Tabia nchi  (Regional Responses to Climate Displacement in Subsaharan Africa- RE2CLID) unaolenga kujenga uhimilivu wa jamii zinazoishi maeneo yanayozunguka Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi.
MHE. MMUYA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA MAWAZIRI WA MAAFA SADC ZIMBABWE

MHE. MMUYA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA MAWAZIRI WA MAAFA SADC ZIMBABWE

May 15, 2026 Add Comment






MASVINGO – ZIMBABWE

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Sita (6) wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi unaofanyika Masvingo, Zimbabwe.

Aidha, Mkutano huo pamoja na masuala mengine umejadili maendeleo yaliyopatikana katika utekelezaji wa programu za kikanda na masuala ya kimkakati katika utekelezaji wa afua mbalimbali katika Usimamizi wa maafa,pia mkutano huo utatumika kama jukwaa kwa Mawaziri kuimarisha ushirikiano na Washirika wa Maendeleo wa Kimataifa na Jumuiya ya Wafadhili kuhusu uwekezaji katika Usimamizi wa Maafa ili kujenga ustahimilivu wa kikanda.

Naibu Waziri Ameongozana na mwenyeji wake ambaye ni Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. CP-Suzan Kaganda, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. Jim Yonazi, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig.Jenerali Hosea Ndagala, Mkurugenzi Msaidizi Urasimishaji Makazi kutoka ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Nicholaus Mwakasege, Mratibu wa Maafa Dkt. Baltazar Leba, Bw. Abubakar Juma kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Msaidizi wa naibu waziri Bw. Blastus Kahemela, Msaidizi wa katibu mkuu Bw. Januari Kitunsi, pamoja na afisa habari Ofisi ya Waziri Mkuu, Bi. Nyamagory Kitwara.


MBEYA YANUFAIKA MAFUNZO KUJIANDAA KUKABILIANA NA MAAFA

May 15, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu- MBEYA

Mkurugenzi msaidizi wa Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano  ya Dharura kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bi. Jane Kikunya amewataka Wajumbe wa Timu  ya kukabiliana na Dharura na Uendeshaji  wa Kitio  cha Operesheni  na Mawasiliano  ya Dharura ya  Mkoa wa  Mbeya kufanya kazi kwa ushirikiano, mshikamano na mawasiliano ya karibu ili kutekeleza wajibu wao kwa weledi na ufanisi unaotakiwa.

Mkurugenzi huyo, ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku tano yanayolenga kuziandaa timu za kukabiliana na Maafa za Mkoa huo.

Aidha, mafunzo hayo  ambayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu yanatolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Wataalamu ya Usimamizi  wa Maafa, Wajumbe wateule wa Timu ya kukabiliana na Dharura ya Mkoa na wataalamu wa Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Waratibu wa Maafa Mkoa na Halmashauri.

Vilevile, Bi. Jane amesema mafunzo hayo yatakuwa mhimili muhimu katika kuhakikisha Mkoa unajiandaa vyema ili kukabiliana na matukio ya dharura kwa haraka hivyo ni lazima timu lengwa ifanye kazi kwa mshikamano ili kuleta ufanisi unaohitajika.

Kwa upande wao  wanufaika wa mafunzo hayo wameishukuru Serikali kwa namna inavyofanya jitihada kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira salama.

Hivyo, wameahidi kutumia elimu hiyo ya kukabiliana na maafa pindi yanapotokea kuokoa maisha ya watu, mali zao  na kurejesha hali.




*MWISHO*



PURA YAWAKARIBISHA WAWEKEZAJI KATIKA VITALU VYA MAFUTA NA GESI

May 14, 2026 Add Comment
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), Mhandisi Charles Sangweni, amesema kuwa sekta ya mafuta na gesi asilia nchini Tanzania ina fursa kubwa na zenye mvuto kwa uwekezaji, hivyo kuwahimiza wadau mbalimbali wa sekta hiyo kuchangamkia fursa zilizopo.

KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA METROLOJIA

May 14, 2026 Add Comment
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limezindua huduma za Maabara ya Metrolojia katika Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, hatua inayotarajiwa kuongeza upatikanaji wa huduma za ugezi kwa haraka, kwa ufanisi na kwa gharama nafuu zaidi kwa wadau wa ukanda huo.

USHINDANI WA HAKI WAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI TANZANIA

May 14, 2026 Add Comment
SERIKALI imeendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji kupitia kuimarisha sera za ushindani wa haki zinazosaidia biashara kushindana kwa uwazi, kuongeza ubunifu na kuwalinda walaji.
TANZANIA YATOA SOMO KWA NCHI ZA SADC KUHUSU USIMAMIZI WA MAAFA

TANZANIA YATOA SOMO KWA NCHI ZA SADC KUHUSU USIMAMIZI WA MAAFA

May 14, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu, Zimbabwe

Tanzania imeendelea kung’ara katika ukanda wa Kusini mwa Afrika baada ya kutajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mifumo madhubuti ya usimamizi wa maafa, hatua inayozifanya nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujifunza kupitia uzoefu wake.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya wakati akimwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Mhe. Balamagamba Kabudi wakati wa Mkutano wa Sita wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa nchi wanachama wa SADC unaofanyika mjini Masvingo, Zimbabwe.

Amesema Tanzania imefanikiwa kuimarisha mifumo ya kuzuia, kupunguza madhara, kujiandaa na kurejesha hali baada ya maafa kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya uratibu wa maafa nchini.

Kwa mujibu wa Mhe. Mmuya amesema moja ya mafanikio makubwa ni kuanzishwa kwa Kituo cha Ufuatiliaji wa Mwenendo wa Majanga na Tahadhari ya Mapema (National Emergency Operation and Communication Center Situation Room), ambacho kinafanya kazi saa 24 kila siku kufuatilia na kuchambua taarifa za majanga.

“Kwa kupitia kituo hiki, Serikali imeweza kupata taarifa za mapema kuhusu majanga yanayoweza kutokea, kufanya uchambuzi wa madhara na kuweka mikakati ya haraka ya kukabiliana nayo,” alisema Mhe Mmuya

Aliongeza kuwa matumizi ya teknolojia ya kisasa katika ukusanyaji na uchambuzi wa takwimu za wakati halisi yamechangia kuongeza ufanisi wa maamuzi na kurahisisha utoaji wa taarifa rasmi kwa wananchi kuhusu namna ya kujiandaa dhidi ya maafa.

“Tunatumia takwimu za sasa na za zamani kutabiri hatari zinazoweza kujitokeza, jambo ambalo linaisaidia Serikali kupanga kwa usahihi hatua za kurejesha hali na kuendelea kulinda maisha ya wananchi,” alisisitiza.

Aidha, aliwaalika wajumbe kutoka nchi wanachama wa SADC kutembelea Tanzania ili kujionea namna mifumo hiyo inavyofanya kazi pamoja na ubunifu unaotumika katika usimamizi wa maafa.

Mkutano huo wa siku nne umezikutanisha nchi 16 wanachama wa SADC pamoja na wataalamu wa kitaifa na mashirika ya kimataifa kujadili utekelezaji wa programu za kikanda za usimamizi wa maafa na namna ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda.

Pamoja na mambo mengine, mkutano huo unatarajiwa kuwa jukwaa muhimu kwa mawaziri na washirika wa maendeleo kujadili uwekezaji katika sekta ya usimamizi wa maafa kwa lengo la kujenga ustahimilivu wa kikanda dhidi ya majanga mbalimbali yanayoendelea kujitokeza duniani.



TANZANIA YAKAMILISHA MFUMO WA KUREJESHA HALI BAADA YA MAAFA

May 14, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu - Masvingo, Zimbabwe.

TANZANIA imekamilisha maandalizi ya Mfumo wa Taifa wa Kurejesha Hali Baada ya Maafa, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa Taifa kukabiliana na athari za majanga yanapotokea.


Mfumo huo unatajwa kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Tanzania wa kukabiliana na ongezeko la maafa yanayochangiwa na mabadiliko ya tabianchi, huku ukitoa mwongozo wa hatua za haraka za kurejesha huduma za kijamii, miundombinu muhimu pamoja na shughuli za kiuchumi katika maeneo yaliyoathirika.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya akimwakilisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi katika Mkutano wa Sita wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri wenye dhamana ya Usimamizi wa Maafa katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika Mei 11 hadi 14 mjini Masvingo, Zimbabwe.

Alisema mfumo huo umezingatia matumizi ya mifumo ya kisayansi na teknolojia ili kupata taarifa sahihi na za haraka kuhusu madhara ya maafa.


“Mfumo huu utawezesha tathmini ya uharibifu na madhara kwa kutumia mifumo ya kisayansi na teknolojia ili kubainisha kwa haraka hasara katika sekta za uzalishaji wa kiuchumi, miundombinu, huduma za kijamii na sekta mtambuka,” alisema Mhe. Mmuya.


Kwa mujibu wa Mhe.Mmuya, mfumo huo pia umeweka utaratibu wa kuwa na mpango jumuishi wa kurejesha hali katika sekta zilizoathirika huku ukitaka madhara ya maafa kuzingatiwa katika mipango na bajeti za maendeleo za taifa na mamlaka za chini.

Katika hatua nyingine, alisema Tanzania imezindua Mwongozo wa Taifa wa Ugharamiaji wa Maafa wa mwaka 2025 unaolenga kupanua wigo wa upatikanaji wa fedha kwa ajili ya usimamizi wa maafa na shughuli za kurejesha hali kupitia vyanzo vya ndani na nje ya nchi.


“Miongozo hii inaonesha dhamira ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuweka mazingira rafiki ya kisera na kimkakati pamoja na kuimarisha ushirikiano wa kikanda, kimataifa na sekta binafsi katika usimamizi wa maafa,” alisema

Kwa mujibu wa Mmuya, Tanzania imewekeza katika mifumo himilivu ya chakula na kilimo kutokana na mchango mkubwa wa sekta hiyo katika uchumi wa nchi na ajira kwa wananchi wengi wa ukanda wa kusini mwa Afrika.


Alieleza kuwa kupitia dhana ya Jenga Kesho iliyo Bora (BBT), serikali inaendelea kuwekeza katika matumizi ya teknolojia, taarifa za hali ya hewa, ujenzi wa miundombinu inayozingatia vihatarishi vya majanga pamoja na kuimarisha huduma za kijamii katika maeneo yaliyoathirika.


“Tunaamini ushirikiano wa kikanda na kimataifa ukitekelezwa kwa kuzingatia vipaumbele vya kitaifa utaongeza kasi ya kugeuza hatari za maafa kuwa fursa ya kuimarisha ustahimilivu wa kikanda,” alieleza


Tanzania pia imezialika nchi wanachama wa SADC kutembelea nchini humo kwa ajili ya kubadilishana uzoefu katika maeneo mbalimbali, ikiwemo matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa maafa, mifumo ya tahadhari ya mapema, usimamizi wa takwimu pamoja na ujenzi wa Kituo cha Taifa cha Usimamizi wa Maafa kinachotarajiwa kuwa kituo cha umahiri katika ukanda wa SADC mara kitakapokamilika.


=MWISHO=

JUKWAA LA WANAWAKE NA KODI NI HATUA MUHIMU YA KUENDELEZA USAWA WA KIJINSIA NA KUKUZA UCHUMI SHIRIKISHI -CPA CASTRO

May 14, 2026 Add Comment



 Na Paskal Mbunga, Tanga

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga imesema kwamba Jukwaa la Wanawake na Kodi ni hatua muhimu inayodhihirisha dhamira ya kuendeleza usawa wa kijinsia na kukuza uchumi shirikishi nchini.

Hayo yalisemwa na  Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Tanga, CPA Castro John wakati akifungua Jukwaa la Wanawake na Kodi ambapo  alisema ni dhamira ya dhati ya kujenga mfumo wa kodi unaoshirikisha makundi yote ya jamii, hususan wanawake ambao ni nguzo muhimu ya uchumi wa Taifa.


Alisema takwimu zinaonesha wanawake wanachangia kwa kiwango kikubwa katika shughuli mbalimbali za kiuchumi zikiwemo biashara ndogondogo, kilimo, huduma, viwanda vidogo pamoja na biashara za kati na kubwa.

Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2024/2025, wanawake nchini, wakiwemo wa Mkoa wa Tanga, wanakadiriwa kushiriki katika nguvu kazi kwa asilimia 80, huku wakimiliki asilimia 54 ya biashara ndogo, za kati na kubwa.

“Bila ushiriki wa wanawake, juhudi za kuongeza wigo wa walipa kodi na kuongeza mapato ya ndani haziwezi kufikia malengo yaliyokusudiwa,” alisema CPA Casto John.

Alifafanua kuwa TRA imeanzisha Jukwaa hilo maalumu kwa lengo la kutoa elimu sahihi ya kodi, kusikiliza changamoto za wanawake wafanyabiashara, kujenga ushirikiano wa karibu pamoja na kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari na kwa wakati.

Aidha, alisema TRA imejikita katika kuboresha huduma kwa kuzingatia ushirikishwaji, uwazi, weledi na urahisi wa upatikanaji wa huduma. Aliongeza kuwa elimu ya kodi na mahusiano bora ni msingi muhimu wa kuongeza utii wa kodi.

Kupitia jukwaa hilo, wanawake watapata nafasi ya kupata ushauri kuhusu masuala ya kodi, kujifunza fursa mbalimbali pamoja na kuelewa wajibu wao wa kikodi.

“Tunataka mwanamke ajisikie salama, aheshimiwe na ashiriki kikamilifu katika mfumo wa kodi bila hofu wala kikwazo chochote,” alisema.

CPA Casto John alisisitiza kuwa kodi ndiyo injini ya maendeleo ya Taifa kwani mapato yake yanagharamia huduma muhimu kama elimu, afya, barabara, maji safi na miradi mingine ya kimkakati.

“Kila mwanamke anayelipa kodi anakuwa mshirika wa moja kwa moja wa Serikali katika kujenga Tanzania yenye uchumi imara na huduma bora kwa wananchi wake,” aliongeza.

Pia aliwataka wanawake kutumia jukwaa hilo kujifunza, kuuliza maswali na kuwa mabalozi wa utamaduni wa kulipa kodi katika jamii zao.

Aidha, aliwataka wadau wa sekta mbalimbali pamoja na taasisi za kifedha kuendelea kushirikiana na TRA katika kuwawezesha wanawake kukuza biashara zao kwa kuzingatia misingi ya kikodi.

Kwa upande mwingine, aliwahimiza wanawake wafanyabiashara kujisajili katika mfumo wa kodi na kutekeleza wajibu wao kwa hiari na kwa wakati.

“Kulipa kodi si wajibu wa kisheria tu, bali ni mchango wa moja kwa moja katika kujenga Taifa. Wanawake wakisimama kiuchumi, familia na jamii vinaimarika,” alisema.

Katika hatua nyingine, alisisitiza umuhimu wa kutumia mipaka rasmi ya biashara kwa wafanyabiashara wanaovuka mipaka kupitia maeneo ya Horohoro na Pangani, huku akiwataka kuachana na biashara za magendo na matumizi ya njia zisizo rasmi.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara nchini, JW Ismail Masound, alisema jukwaa hilo lina umuhimu mkubwa kutokana na malengo ya Dira ya Taifa ya mwaka 2050 ambapo sekta binafsi inatarajiwa kuwa mhimili mkubwa wa ukuaji wa uchumi.

Alisema majukwaa hayo yanasaidia kuwawezesha wanawake na wafanyabiashara kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa kwa kuongeza ushiriki wao katika shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Mkoa wa Tanga (TWCC), Aziza Ramadhani, alisema jukwaa hilo litawasaidia wanawake kuelewa umuhimu wa kulipa kodi katika kukuza uchumi wa Mkoa wa Tanga na Taifa kwa ujumla.

“Hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha Mkoa wa Tanga unalipa kodi kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya jamii,” alisema.

Aliongeza kuwa jukumu la jukwaa hilo ni kuwaunganisha wanawake wa Mkoa wa Tanga ili kuwapa nafasi ya kujifunza, kushirikiana na kupata fursa mbalimbali za kiuchumi ndani na nje ya mkoa huo.

Aidha, alisema wamekuwa wakitoa mafunzo mbalimbali ikiwemo kuanzisha mashamba darasa kwa vijana wa kiume na wa kike, huku akiwakaribisha wanawake wajasiriamali kushiriki katika shughuli za maendeleo zinazochangia ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Tanga na Taifa kwa ujumla.




MIKOA YA KANDA ZIWA YAFIKIWA NA ELIMU UFUATILIAJI NA TATHIMINI KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

May 14, 2026 Add Comment

      

Na Mwadishi wetu- Mwanza

Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuchukua hatua thabiti za kuimarisha mifumo ya usimamizi wa utendaji na uwajibikaji kwa kutoa Elimu Tathimini na Ufuatiliaji kwa Wataalam wa serikali ili kuleta maendeleo wananchi. 

Katika  juhudi hizo, viongozi na wataalam kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa wamekutana  leo tarehe 14 Mei, 2026 Mkoani Mwanza katika kikao kazi maalum kilichojumuisha Mikoa ya Mwanza, Kigoma, Geita, Simiyu, Kagera, Shinyanga na Marakwa lengo kuu ni kujadili na kuimarisha utekelezaji wa Mwongozo Jumuishi wa Ufuatiliaji na Tathmini.
RC MTWARA AELEZA MANUFAA YA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA KWA UCHUMI WA WAKULIMA

RC MTWARA AELEZA MANUFAA YA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA KWA UCHUMI WA WAKULIMA

May 14, 2026 Add Comment

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanal Donald Msengi, amewashauri Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwahimiza wakulima kutumia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ili kuleta mabadiliko chanya kiuchumi na kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao.

Akizungumza  wakati wa Mafunzo ya Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kwa Viongozi wa Chama na Serikali kutoka mkoa wa Dodoma yaliyofanyika mkoani Mtwara, Kanal Msengi amesema mfumo huo umeleta mafanikio makubwa kwa vyama vya ushirika mkoani humo kwa kuviwezesha kuwa imara kiuchumi. Ameeleza kuwa kupitia mfumo huo, vyama vimefanikiwa kufanya uwekezaji mbalimbali ikiwemo ujenzi wa maghala, ununuzi wa magari, uanzishaji wa viwanda pamoja na kuchangia huduma za kijamii kama elimu, afya na maji.

“Ni muhimu viongozi mkatumia nafasi zenu kuwahamasisha wakulima na wanaushirika kutumia mfumo huu, kwani umeleta manufaa makubwa na una uwezo wa kuleta mageuzi chanya kwa sekta ya kilimo,” amesema Kanal Msengi.

Naye Kaimu Mrajis Msaidizi wa Mkoa wa Mtwara, Robert Nzunza, amebainisha hatua muhimu za mchakato wa stakabadhi za ghala kuwa ni pamoja na maandalizi ya msimu wa mauzo, ukusanyaji wa mazao ghalani, usafirishaji wa mazao kwenda ghala kuu, mapokezi ya mazao, mauzo kupitia minada ya mtandao, malipo ya fedha kupitia vyama vikuu (Unions), malipo kwa wakulima na wadau, pamoja na utoaji wa mizigo ghalani.

Kwa upande wake Mkuu wa msafara huo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka mkoa wa Dodoma, Donald Mejetii, amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuwajengea uwezo viongozi hao ili waweze kuwahamasisha wakulima wa Dodoma kutumia mfumo huo kwa tija zaidi.

Viongozi wa Chama na Serikali kutoka mkoa wa Dodoma wapo mkoani Mtwara kwa ziara ya kujifunza Mfumo wa Stakabadhi za Ghala katika vyama vya ushirika na namna unavyoweza kuinua kipato cha mkulima. Katika ziara hiyo pia wametembelea Chama Kikuu cha Ushirika cha MAMCU LTD pamoja na Chama cha Msingi Mayanga AMCOS.