HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

ELIMU YA UFUNDI KUPITIA VETA YAWEKWA MBELE KUINUA VIJANA

ELIMU YA UFUNDI KUPITIA VETA YAWEKWA MBELE KUINUA VIJANA

April 29, 2026 Add Comment

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza wakati akifungua  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akizungumza wakati akifungua  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza wakati wa   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda (hayupo pichani) wakati wa  Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua   Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo uliofanyika leo Aprili 29,2029 jijini Dodoma.

....

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema utekelezaji wa mageuzi ya elimu unaoendelea nchini ni sehemu ya dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha vijana wanapatiwa ujuzi, maarifa na uwezo unaowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa taifa.

Ameyasema hayo leo  Aprili 29, 2026 katika Mkutano wa 37 wa Baraza la Wafanyakazi wa wizara hiyo, Prof. Mkenda amesisitiza kuwa sekta ya elimu inabeba wajibu mkubwa katika maendeleo ya nchi na kwamba, wajibu wa Wizara ni kuhakikisha mipango yote inatekelezwa kwa ufanisi na kwa kasi.

Waziri Mkenda ameongeza kuwa kuanzishwa kwa Wizara maalum ya maendeleo ya vijana ni uthibitisho wa umuhimu wa kundi hilo katika maendeleo ya taifa na kuwa elimu ya ufundi kupitia VETA, ni msingi wa kuwaandaa vijana kuzalisha na kushiriki katika uchumi wa kisasa.  "Utekelezaji wa elimu ya miaka 10 ya lazima na uimarishaji wa shule za Sekondari na shule za amali unatekelezwa kwa ushirikiano wa karibu na Ofisi ya Rais – TAMISEMI, na hata sekta binafsi hasa katika kuhakikisha upatikanaji wa shule karibu na makazi ya wananchi na ununuzi wa vifaa vya kisasa kwa ajili ya mafunzo ya ufundi."amesema Prof. Mkenda Katika kuhimiza ubunifu na uwajibikaji, Prof. Mkenda amewataka watumishi wa Wizara kuendeleza kasi ya utendaji na kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata taarifa kuhusu utekelezaji na mafanikio ya serikali katika maeneo ya sekta ya elimu, sayansi, teknolojia na ubunifu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,amesema Serikali inaendelea kuimarisha usimamizi wa ajira na rasilimaliwatu kwa kuzingatia malengo na maono ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan hususan katika utekelezaji wa Kifungu cha 73 cha Sheria ya Ajira kinachohusu uhusiano kazini.

Prof. Nombo amesema kuwa kupitia mkutano huo, wajumbe watapitia mpango na bajeti ya wizara pamoja na masuala ya utawala na usimamizi wa rasilimali watu pamoja na kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuboresha afya na usalama mahali pa kazi. Prof. Nombo amesisitiza kuwa mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi ni nguzo muhimu ya kufanikisha ubora na uaminifu katika utendaji kazi,  "Dhamira ya Wizara ni kuona watumishi wanafanya kazi kwa bidii, kwa uadilifu na kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kuendeleza mageuzi yanayoendelea katika elimu."amesema Prof. Nombo Aidha, amewashukuru wajumbe wa Baraza hilo kwa ushirikiano wao na amewataka kuendekeza juhudi za kuimarisha mifumo ya usimamizi ndani ya Wizara.

USALAMA NA USTAWI WA MFANYAKAZI SI CHAGUO, NI KIPAUMBELE CHETU

April 29, 2026 Add Comment

Kampuni ya GASCO imeeleza kuwa usalama na ustawi wa mfanyakazi ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa shughuli zake za kila siku, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya kuhakikisha mazingira salama, rafiki na yenye kuchochea tija kazini.

MIAKA 40 YA NEMC : SAFARI YA UTHABITI NA WITO WA HATUA

April 29, 2026 Add Comment
Na Mwandishi wetu

Katika dunia inayokabiliwa na changamoto kubwa za mabadiliko ya tabianchi, ongezeko la uchafuzi wa mazingira na kupungua kwa rasilimali asilia, hadithi ya Tanzania inajitokeza kama mfano wa matumaini, uthabiti na maamuzi ya kimkakati. Maadhimisho ya miaka 40 ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) si tukio la kawaida—ni kielelezo cha dhamira ya Taifa kulinda uhai wake huku likiendeleza uchumi wake.

PPP YAJIPANGA KUWA CHOMBO MUHIMU CHA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA

April 29, 2026 Add Comment
Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP Centre) kimesema mafanikio ya utekelezaji wa ajenda ya ubia nchini yameongeza kwa kiasi kikubwa thamani ya miradi ya maendeleo, huku kikitoa wito wa kufanyiwa maboresho kwa Sheria ya Utumishi wa Umma ili kuongeza uwajibikaji na kulinda maslahi ya walipa kodi.

DKT. MAULID AONGOZA KIKAO CHA BODI YA CHUO CHA MAJI

April 29, 2026 Add Comment
Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Maji (Water Institute) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dr. Maulid J. Maulid wamekutana Aprili 28, 2026 jijini Dar Es Salaam kwa kikao cha 46 cha Bodi hiyo kujadili masuala ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utoaji wa huduma za kitaaluma na miradi ya maendeleo itakayoboresha ufundishaji na ujifunzaji.

OFISI YA WAZIRI MKUU YAINOA TIMU YA KUKABILIANA NA MAAFA MKOA WA DODOMA

April 27, 2026 Add Comment





Na Mwandishi wetu- DODOMA

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu, amesema Ofisi yake ikishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Menejimenti ya Maafa ipo katika hatua ya kuanzisha Kituo cha Operasheni ya Dharura katika Mkoa ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2004.

Dkt. Kazungu ameyasema hayo leo tarehe 27 Aprili,2026 jijini Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku nne ya kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa Timu ya kukabiliana na dharura ya Mkoa ambayo yameandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa pamoja na uanzishaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura cha Mkoa.

NEMC, ZEMA WABADILISHANA UZOEFU KATIKA TATHMINI ZA ATHARI ZA MAZINGIRA

April 27, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) wamekutana Aprili 27,2026 katika ziara ya mafunzo, kwa lengo la kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa majukumu ya kimazingira, hasa mchakato wa ufanyaji wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na jamii katika miradi mikubwa na mchakato wa kupata vyeti vya kimazingira ili kuhakikisha maendeleo yanaendana na uhifadhi wa mazingira.

MIGODI YA BARRICK TANZANIA YAFIKISHA ELIMU YA USALAMA KWENYE JAMII MAONESHO YA OSHA NJOMBE

April 27, 2026 Add Comment

 


Mkuu wa Mkoa wa Njombe , Mhe. Anthony Mtaka akipokea moja ya mitungi ya gesi uliotolewa na Barrick
Mkuu wa Mkoa wa Njombe , Mhe. Anthony Mtaka akipokea Zawadi ya begi kutoka Afisa Mifumo ya Usalama wa Barrick, Beatrice Amos.
Afisa wa Usalama kutoka Mgodi wa Barrick Mgodi North Mara, Maisori Mniko akizima moto kwa vitendo katika mafunzo ya siku moja ya kupambana na majanga ya moto.
Afisa Msimamizi wa Usalama kutoka Barrick North Mara, Athanas Mtenga akitoa elimu ya usalama mahala pa kazi kwa wajasiriamali wa Mkoani wa Njombe.
Baadhi ya timu ya wafanyakazi wa Barrick kwenye maonesho
Majaji wa OSHA wakipita katika banda la maonesho la Barrick.

CCM NA CPC MAANDALIZI YA KUPOKEA UGENI

April 27, 2026 Add Comment

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdalla Hamid akiwa kwenye kikao kazi na Kansela wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, Ndugu Xu Sujiang, leo Jumatatu tarehe 27 Aprili 2026, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea ugeni wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CPC na Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Mhe. Liu Haixing, anayetarajiwa kufanya ziara rasmi nchini Tanzania, mwezi Mei 2026.

#KazinaUtuTunasongaMbele



BARRICK YAWEZESHA WANAFUNZI VYUO VIKUU MOROGORO KUPATIWA UTAMBUZI WA FURSA KUPITIA AIESEC 2026

April 27, 2026 Add Comment

  

Picha ya pamoja ya wadhamini na viongozi wa AIESEC Tanzania
Wanafunzi na wageni waalikwa wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa kongamano la AIESEC lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro
Wafanyakazi wa Barrick katika kongamano hilo

***
Wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Morogoro wamepata fursa ya kupata elimu ya kuchangamkia fursa za kupata mafanikio kupitia elimu yao katika kongamano lililoandaliwa na taasisi ya AIESEC lililodhaminiwa na Barrick kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

KAMISHNA LUOGA AONGOZA WATAALAMU KUTOKA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA AU KUHUSU NISHATI NA UCHUKUZI

April 27, 2026 Add Comment




Wizara ya Nishati na Wizara ya Uchukuzi za Tanzania zimeshiriki katika Mkutano wa 5 wa mwaka wa Kamati Maalum ya Wataalamu ya Umoja wa Afrika kuhusu Uchukuzi na Nishati (Specialised Technical Committee (STC) on Transport and Energy), unaofanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini 


Ushiriki wa Tanzania kwa ngazi ya wataalamu unaongozwa na Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga, aliyeongoza ujumbe wa sekta kushiriki katika majadiliano ya kimkakati yanayolenga kuimarisha maendeleo ya miundombinu ya nishati na uchukuzi barani Afrika.

Wataalamu wengine walioshiriki mkutano huo ni Mkurugenzi wa Usalama wa Usafiri na Mazingira wa Wizara ya Uchukuzi, Bi. Stella Katondo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bw. Mohamed Salum, pamoja na wataalamu wengine kutoka katika sekta husika.

Mkutano huo wa wataalamu umeanza Aprili 27 hadi 29, 2026, ambapo unajadili masuala mbalimbali ya sekta ya nishati na uchukuzi ikiwemo kuongeza uwekezaji katika nishati jadidifu, matumizi ya gesi asilia, pamoja na kuimarisha miundombinu ya umeme wa kuvuka mipaka.

Mkutano huo utafuatiwa na kikao cha Mawaziri kitakachofanyika Aprili 30, 2026, ambapo Tanzania pia itashiriki.

Katika majadiliano hayo, nchi wanachama zinaangazia mikakati ya kuboresha upatikanaji wa nishati ya uhakika na nafuu, pamoja na kuendeleza mifumo jumuishi ya uchukuzi ikiwemo reli, barabara, anga na usafiri wa majini ili kurahisisha biashara na usafirishaji barani Afrika



CBE YAENDELEZA MAZINGIRA JUMUISHI KUPITIA MIKAKATI YA KIJINSIA

April 27, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Imeelezwa kuwa usawa wa kijinsia unaendelea kuwa nguzo muhimu katika kufanikisha maendeleo endelevu, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuimarisha utawala bora katika jamii na taifa kwa ujumla.

MKOA WA NJOMBE KUSHIRIKIANA NA OMR, WIZARA YA MALIASILI KUDHIBITI MAJANGA YA MOTO

April 27, 2026 Add Comment
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Antony Mtaka akizungumza na Wanamichezo wanaoshiriki Mashindano ya Mei Mosi, 2026 Mkoani humo wakati waliofika katika Ofisiza Mkoa huo Aprili 27, 2026 kwa ajili ya zoezi la upandaji Miti kupitia kampeni ya 27 ya kijani, Mti wa Mama inayofanyika tarehe ya Kila mwezi.

OMR YATWAA USHINDI NAFASI YA TATU KARATA WANAWAKE

April 27, 2026 Add Comment


OFISI ya Makamu wa Rais imebuka mshindi wa nafasi ya tatu kupitia mchezo wa karata upande wa wanawake katika Mashindano ya Michezo ya Mei Mosi, 2026 yanayoendelea Mkoani Njombe.

KIKUNDI CHA WE ARE FAMILY CHAWAFIKIA WAGONJWA OCEAN ROAD CANCER INSTITUTE

April 27, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Kikundi cha We Are Family kinachowahusisha wenza wa majaji nchini, kimetembelea wagonjwa wa saratani katika Ocean Road Cancer Institute jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira yao ya kufanya matendo ya huruma kwa jamii.

‘JOURNEY TO ZERO’ YA BARRICK YAVUTIA WENGI MAONESHO YA OSHA 2026

April 26, 2026 Add Comment

Kamishina wa Kazi Ofisi ya Waziri Mkuu , Kazi , Ajira na Watu Wenye Ulemavu , Suzan Mkangwa akipata maelezo kutoka kwa Afisa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi  kutoka Mgodi wa Barrick North Mara, Michael Bernard (wa kwanza kulia) , alipotembelea banda la Barrick North Mara kwenye maonesho yanayoendelea kwenye viwanja vya Mji Mwema Mkoa wa Njombe
Baadhi ya wanafunzi wakipata mafunzo ya kudhibiti majanga ya moto katika maonesho haya yanayoendelea kwenye viwanja vya Mji Mwema Mkoa wa Njombe

***

KAFULILA ATOA WITO WA KUULINDA MUUNGANO

April 26, 2026 Add Comment

Katika kuadhimisha miaka 62 ya Muungano wa Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPPC), David Kafulila, amesema mafanikio ya Muungano huo yanatokana zaidi na mshikamano wa watu kuliko mifumo ya kiserikali.

DKT. MWIGULU AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MADARAJA YA MKWAJUNI NA KIGOGO, DAR ES SALAAM.

April 26, 2026 Add Comment

 Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Aprili 26, 2026 anafanya ziara katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Mkwajuni lenye urefu wa mita 20 na kimo cha mita 5.5 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 11.6

Pia Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amekagua mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigogo lenye urefu wa mita 50 kimo cha mita 8.9 na barabara unganishi zenye jumla ya urefu wa mita 625 ambalo hadi kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 17.7.