HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

RAIS MUSEVENI ABARIKI KUREJEA KWA SHUGHULI ZA NATION MEDIA GROUP NCHINI UGANDA

July 28, 2026 Add Comment

 

Kampuni ya Taifa Group leo Julai 28,2026 imetangaza kurejea kwa shughuli za kampuni yake tanzu ya Nation Media Group nchini Uganda kufuatia idhini iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni.

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA MSONGO WA KILOVOLTI 400 CHALINZE–DODOMA MBIONI KUKAMILIKA

July 28, 2026 Add Comment



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma uko kwenye hatua za mwisho za utekelezaji wake, huku ujenzi ukiwa umekamilika kwa asilimia 94 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 21, 2026.


Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 28, 2026, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Bi. Irene Gowelle, amesema ili kuwezesha ukamilishaji wa kazi za mradi huo kutakuwepo na katizo la muda la umeme katika baadhi ya maeneo nchini kwa ratiba maalumu kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itakua Julai 30 hadi Agosti 4 na ya pili itaanza Agosti 11 hadi 17, 2026.


Gowelle amesema hatua hiyo ni sehemu ya maandalizi ya ombi la Mkandarasi anayetekeleza mradi huo kampuni ya TBEA ambayo inalenga kuhakikisha kazi zinafanyika kwa hali ya usalama .


“Mradi huu umefikia hatua muhimu sana ya utekelezaji ambapo kipindi hiki, baadhi ya njia za kusafirisha umeme za kilovolti 220 na 132 zitalazimika kuzimwa kwa muda ili kuruhusu kazi za kuvuta na kuunganisha nyaya mpya kufanyika kwa usalama. Hii ni hatua ya kawaida katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu ya kusafirisha umeme na inalenga kukamilisha mradi huu wenye manufaa makubwa kwa Taifa,” amesema Bi. Gowelle.


Amefafanua kuwa baadhi ya maeneo katika mikoa iliyoko Kanda ya Kati, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Magharibi na Kanda ya Kusini Magharibi inaweza kuathiriwa kwa nyakati tofauti kulingana na ratiba za utekelezaji wa kazi hizo.


Bi. Gowelle amesema TANESCO itaendelea kutoa taarifa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na majukwaa mbalimbali ya mawasiliano ili kuwawezesha wateja kupanga matumizi yao ya umeme kwa kuzingatia ratiba zitakazotolewa.


Aidha, amesisitiza kuwa Tanzania ina umeme wa kutosha na kwamba katizo hilo ni la muda, likiwa ni sehemu ya kukamilisha mradi huo wa kimkakati unaolenga kuimarisha uwezo wa usafirishaji wa umeme nchini. Ameongeza kuwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara haitahusika katika ratiba hiyo ya katizo.


Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Kilovolti 400 Chalinze–Dodoma, Mhandisi Newton Mwakifwamba, amesema mradi huo wenye urefu wa kilomita 345 na thamani ya takribani shilingi bilioni 514 umefadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Amesema mradi unahusisha ujenzi wa njia mpya ya kusafirisha umeme pamoja na upanuzi wa vituo vya kupokea na kusambaza umeme vya Chalinze na Dodoma.


“Katika hatua hizi za mwisho, tutafanya kazi za kuvusha na kuunganisha njia mpya ya umeme katika maeneo ya Mkambarani, Kikombo na Mkonze. Hatua hizi ni muhimu ili kuhakikisha mradi unaanza kufanya kazi kwa ufanisi na usalama,” amesema Mhandisi Mwakifwamba.


Ameongeza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutaimarisha uwezo wa mfumo wa taifa wa usafirishaji umeme na kuwezesha usafirishaji wa umeme unaozalishwa katika Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere kwenda maeneo mbalimbali ya nchi, hatua itakayoimarisha uhakika wa upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.







RAIS MUSEVENI ABARIKI KUREJEA KWA SHUGHULI ZA NATION MEDIA GROUP NCHINI UGANDA

July 28, 2026 Add Comment



Kampuni ya Taifa Group leo imetangaza kurejea kwa shughuli za kampuni yake tanzu ya Nation Media Group nchini Uganda kufuatia idhini iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni.


Uamuzi huu ni hatua muhimu katika uwekezaji wa kikanda, maendeleo ya sekta ya habari na ustawi wa ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kupitia kampuni tanzu yake, Taarifa Limited, Taifa Group ndiyo mbia mkuu wa Nation Media Group na inaendelea kujitolea katika uwekezaji wenye uwajibikaji, utawala bora wa kampuni na maendeleo endelevu kote katika kanda hii.


Akizungumzia hatua hiyo, Mwenyekiti wa Taifa Group, Bw. Rostam Azizi, alitoa shukrani zake za dhati kwa Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni kwa kuruhusu kurejea kwa shughuli za Nation Media Group nchini Uganda. Pia alitoa shukrani kwa Jenerali Muhoozi Kainerugaba, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda (UPDF), kwa uungaji mkono wake katika mchakato mzima uliopelekea matokeo haya chanya akisema,


“Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais Yoweri Kaguta Museveni kwa uamuzi huu muhimu, na kwa Jenerali Muhoozi Kainerugaba kwa uungaji mkono wake katika mchakato mzima uliopelekea matokeo haya chanya.


Tunajivunia uamuzi huu na tunadumisha azma yetu thabiti ya kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Uganda kupitia uwekezaji wenye uwajibikaji, ushirikiano wa muda mrefu na ujenzi wa thamani endelevu.


Kama mbia mkuu wa Nation Media Group, tunaunga mkono kikamilifu dhamira ya Kampuni hiyo ya kufuata misingi ya uandishi wa habari wa haki, uwiano, uhuru na uwajibikaji, unaotoa taarifa, kuelimisha na kuchangia vyema katika mijadala ya umma. Tunashiriki dhima kuu ya Kampuni hiyo ya kuleta athari chanya katika jamii, na tunaamini kuwa vyombo vya habari imara, vya kitaalamu na vinavyozingatia uwajibikaji vina jukumu muhimu katika kusaidia maendeleo ya taifa, utawala bora na ushirikiano wa kikanda.”


"Uamuzi huu unaonyesha thamani ya mazungumzo, kuheshimiana na ushirikiano wa kikanda. Taifa Group itaendelea kuwekeza katika fursa zinazozalisha ajira, kuimarisha taasisi na kuendeleza ustawi wa pamoja katika Afrika Mashariki."


Mwenyekiti wa Nation Media Group, Bw Joe Muganda, alisema Kundi hilo sasa litazingatia kujenga upya uwepo wake, kuungana tena na watazamaji na kuimarisha mchango wake katika sekta ya vyombo vya habari nchini Uganda.


"Tunakaribisha fursa ya kurejesha shughuli nchini Uganda na kuunganishwa tena na watazamaji wetu, wafanyakazi, washirika wa kibiashara na jumuiya.


"Kipaumbele chetu cha haraka kitakuwa kurejesha majukwaa yetu kwa uwajibikaji, kuimarisha maudhui ya ndani na kuwapa Waganda uandishi wa habari wa kuaminika, muhimu na wa ubunifu katika magazeti, matangazo na njia za digital.


"Nation Media Group itatumia uwezo wake wa kikanda na uzoefu ili kusaidia tasnia ya habari yenye uthabiti, yenye mtazamo wa mbele nchini Uganda, huku ikitengeneza fursa za talanta, biashara na ushiriki wa umma."


Kurejeshwa kwa shughuli hizo kunaonyesha uhusiano wa kudumu kati ya Uganda na Tanzania na dhamira pana ya serikali za Afrika Mashariki na sekta binafsi ya kukuza utangamano wa kikanda, uwekezaji wa mipakani na ushirikiano wa kiuchumi.


Nation Media Group inapojenga upya shughuli zake nchini Uganda, itaendelea kutumia uwepo wake kote nchini Kenya, Uganda, Tanzania na Rwanda ili kuunganisha watazamaji, kuimarisha mazungumzo ya kikanda na kusaidia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya Afrika Mashariki. Taifa Group itaendelea kushirikiana na serikali, taasisi, wafanyabiashara na jumuiya kote kanda ili kupanua fursa za kiuchumi endelevu na kusaidia ustawi wa muda mrefu wa Afrika Mashariki.

RAIS SAMIA AAPISHA VIONGOZI WAPYA, ATOA MAELEKEZO MAZITO YA UADILIFU, USHIRIKIANO NA UWAJIBIKAJI

July 28, 2026 Add Comment


Na Mwandishi wetu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaapisha Naibu Makatibu Wakuu wawili na kushuhudia viongozi wanne wakila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma, huku akiwataka kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, ushirikiano, uwajibikaji na kuzingatia maslahi ya wananchi.

Akizungumza katika hafla iliyofanyika Ikulu, Tunguu, Zanzibar, Rais Samia amesema uteuzi wa viongozi hao unaonesha imani ambayo Serikali imewawekea, hivyo wanapaswa kuhakikisha wanatoa huduma bora, kufanya kazi kwa weledi na kuleta matokeo yanayogusa maisha ya Watanzania.

Rais Samia ameielekeza Ofisi ya Makamu wa Rais kuendelea kuimarisha usimamizi wa masuala ya Muungano kwa kushughulikia changamoto zinazojitokeza kupitia ushirikiano, ili kuendelea kuulinda na kuuimarisha Muungano wa Tanzania. Pia amesisitiza umuhimu wa kusimamia kwa karibu programu za uhifadhi wa mazingira na hatua za kukabiliana na changamoto zinazotishia ustawi wa Taifa.

Aidha, ameagiza Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kuendelea kuboresha usimamizi wa watumishi wa umma kwa kuweka mazingira yatakayowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuongeza ubora wa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika sekta ya uchukuzi, Rais Samia amesisitiza kuongezwa kasi ya utekelezaji wa miradi ya reli, barabara, bandari na meli, pamoja na kutathmini fursa za kupanua biashara ya anga ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ili kuongeza mchango wake katika maendeleo ya uchumi.

Kwa upande wa sekta ya sheria, ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kuendelea kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi kupitia kampeni za msaada wa kisheria, ili huduma hizo ziweze kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa wakati.

Vilevile, Rais Samia ameitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuongeza juhudi katika kukuza biashara na kuboresha usimamizi wa maonesho ya biashara nchini. Pia ameliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuimarisha ulinzi na usimamizi wa hifadhi za taifa na rasilimali za utalii, akieleza kuwa sekta hiyo ni nguzo muhimu ya uchumi wa Taifa.

Kwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha nafasi yake kama chombo cha Serikali na sauti ya Taifa kwa kuongeza ubora wa maudhui, weledi wa watumishi na ufanisi katika utoaji wa huduma za habari.

Walioapishwa ni Dkt. Latifa Mohammed Khamis, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano, pamoja na Bi. Prisca Burton Lwangili, aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Viongozi wengine walioapa Kiapo cha Uadilifu ni Bw. Ephraim Balozi Mafuru, Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE; Bw. Salum Nassor Mnuna, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA; Bw. Massana Gibril Mwishawa, Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA; na Bi. Asha Dachi Mbaruk, Mkurugenzi Mkuu wa TBC.


RC DKT BATILDA -MIKOKO NI UHAI WA PWANI ISIHARIBIWE

July 28, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,TANGA

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, amewataka wananchi kuacha ukataji holela wa mikoko na kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wake, akisema misitu hiyo ni muhimu kwa kulinda fukwe, kuhifadhi viumbe wa majini na kuimarisha uchumi wa jamii za pwani.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, ameitaka jamii kuachana na tabia ya ukataji holela wa miti ya mikoko katika maeneo ya mwambao wa Bahari ya Hindi, akionya kuwa endapo vitendo hivyo vitaendelea vinaweza kuhatarisha makazi ya viumbe wa majini, maisha ya wananchi wanaotegemea rasilimali za bahari pamoja na usalama wa fukwe.



Dkt. Burian alitoa kauli hiyo Juni 28 wakati wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Uhifadhi wa Ikolojia ya Mikoko yaliyofanyika katika eneo la Donge Mnyanjani, Jijini Tanga. 

Alisema Mkoa wa Tanga umebarikiwa kuwa na ukanda mpana wa pwani pamoja na misitu ya mikoko yenye umuhimu mkubwa wa kiikolojia na kiuchumi katika wilaya za Mkinga, Pangani, Muheza na Jiji la Tanga.

Alieleza kuwa mikoko ni ngao muhimu inayolinda mwambao wa bahari dhidi ya mmomonyoko wa ardhi, huku pia ikiwa mazalia ya samaki na makazi ya viumbe wengine wa majini wanaochangia kuimarisha sekta ya uvuvi na kipato cha wananchi wa maeneo ya pwani.


"Mikoko ya Tanga si tu inalinda mwambao wa bahari dhidi ya mmomonyoko wa ardhi, bali ni chanzo muhimu cha maisha ya wavuvi na jamii nyingi za pwani. Kwa miaka ya hivi karibuni Mkoa wa Tanga umeendelea kuwa mfano wa uhifadhi wa mazingira unaokwenda sambamba na maendeleo ya utalii wa ikolojia," alisema Dkt. Batilda Burian.

Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza umuhimu wa kurejesha maeneo yaliyoharibiwa kwa kupanda mikoko mipya ili kurejesha mazingira katika hali yake ya awali kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Aidha, aliwataka viongozi wa serikali za mitaa, vikundi vya wavuvi, wanawake, vijana, wanafunzi pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo Scouts kuendelea kushiriki kikamilifu katika juhudi za uhifadhi wa mikoko huku wakizingatia sheria na taratibu za usimamizi wa misitu.


"Tunapanda mikoko leo, lakini bado tunakabiliwa na changamoto kubwa ya uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na mifuko ya plastiki, chupa na taka nyingine zinazotupwa ovyo kwenye fukwe zetu. Ni wajibu wetu kuendelea kutoa elimu kwa watoto na vijana kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mikoko, kwa sababu tunapohifadhi mikoko tunalinda maisha yetu, chakula chetu, uchumi wetu na mazingira ya watoto wetu," alisisitiza Dkt. Burian.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Kamishna wa Uhifadhi kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Husein Msuya, alisema Siku ya Kimataifa ya Uhifadhi wa Ikolojia ya Mikoko huadhimishwa kila mwaka ifikapo Juni 28, baada ya kuanzishwa na UNESCO mwaka 2015 kwa lengo la kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa mifumo ya ikolojia ya mikoko na wajibu wa kuihifadhi.

Alisema Tanzania ina takribani hekta 158,100 za misitu ya mikoko iliyopo katika wilaya mbalimbali za ukanda wa pwani, zikiwemo Tanga, Pangani na Mkinga, ambapo misitu hiyo ina mchango mkubwa katika kuhifadhi bioanuwai, kuzuia mmomonyoko wa fukwe, kuhifadhi kaboni na kukuza uchumi kupitia uvuvi pamoja na utalii wa ikolojia.
Wananchi wahamasisha uhifadhi wa mikoko

Mkazi wa Jiji la Tanga, Abdalah Mwalimu, alisema wananchi wana wajibu wa kutunza mikoko kwa kuwa ndiyo kinga ya kwanza dhidi ya athari za mawimbi makubwa na mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri maeneo ya pwani.


"Mikoko ni uhai wetu. Tukiiharibu, tutakuwa tumeharibu mazalia ya samaki, tumepunguza kipato cha wavuvi na kuhatarisha usalama wa fukwe. Kila mmoja wetu anapaswa kushiriki kupanda na kuitunza," alisema Abdalah Mwalimu.

Kwa upande wake, mkazi mwingine wa Jiji la Tanga, Fatuma Omari, alisema elimu ya uhifadhi wa mazingira inapaswa kuendelea kutolewa kwa wananchi wote ili kuongeza uelewa wa umuhimu wa kupanda mikoko na kulinda fukwe.


"Kupanda mikoko ni uwekezaji wa maisha ya baadaye. Tunapaswa kuwafundisha watoto wetu kupenda mazingira ili waendeleze jukumu hili na kuhakikisha fukwe zetu zinabaki salama kwa vizazi vijavyo," alisema Fatuma Omari.

Fatuma aliongeza kuwa ushirikiano kati ya wananchi, serikali na taasisi zinazoshughulika na uhifadhi wa mazingira ni muhimu katika kuhakikisha mikoko inaendelea kulindwa na kurejeshwa katika maeneo yaliyoharibiwa.

Abdalah naye alihimiza vijana kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kampeni za upandaji wa mikoko na usafi wa fukwe, akisema hatua hiyo itasaidia kuhifadhi mazingira, kuongeza uzalishaji wa samaki na kukuza uchumi wa jamii za pwani kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.









RC GEITA KUZINDUA MAONE SHO YA NANE NANE NYAMHONGOLO

July 28, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Geita anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima (Nane Nane) ya Kanda ya Ziwa Magharibi yatakayofanyika Agosti 2, 2026, katika Viwanja vya Nyamhongolo vilivyopo Manispaa ya Ilemela, mkoani Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, amesema maonesho hayo, yanayoandaliwa kwa ushirikiano kati ya mikoa ya Mwanza na Geita, yataanza Agosti 1 na kuhitimishwa Agosti 8, 2026.

Mtanda amesema maonesho ya mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo, "Tambua Soko, Ongeza Tija, Tekeleza Dira ya Taifa 2050," ambayo inalenga kuwahamasisha wakulima, wafugaji na wavuvi kuzalisha kwa kuzingatia mahitaji ya soko.

Amesema uzalishaji wenye tija unapaswa kuambatana na uelewa wa mahitaji ya soko, ikiwemo ubora wa bidhaa, bei na muda wa mahitaji, ili kuwawezesha wazalishaji kupanga shughuli zao kwa ufanisi na kuongeza kipato.

"Kilimo, ufugaji na uvuvi vinapaswa kuendelea kubadilika kutoka shughuli za kujikimu na kuwa biashara zenye tija zitakazochochea maendeleo ya wananchi na uchumi wa Taifa," amesema Mtanda.

Ameeleza kuwa maonesho hayo yatashirikisha mamlaka 14 za serikali za mitaa kutoka mikoa ya Mwanza na Geita, taasisi nane za fedha, taasisi 30 za serikali, kampuni 15 za zana za kilimo pamoja na kampuni za utalii na bustani za wanyama, zikiwemo Kasa Zoo na Chato Group.

Aidha, amesema zaidi ya wakulima, wafugaji na wavuvi 614 wanatarajiwa kushiriki kwa kuonesha bidhaa, huduma na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuongeza tija katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Mtanda amewakaribisha wadau wote, wakiwemo waoneshaji, taasisi za utafiti na mafunzo, taasisi za fedha, wakulima, wafugaji, wavuvi na wananchi kwa ujumla, kushiriki katika maonesho hayo ili kujifunza teknolojia mpya, kubadilishana uzoefu na kutumia fursa mbalimbali za biashara zitakazopatikana.



 

TBS YAKUTANA NA WADAU WA VIPODOZI, YASISITIZA VIWANGO NA USALAMA

July 28, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limekutana na wadau wa sekta ya vipodozi nchini kwa lengo la kutoa elimu kuhusu matakwa ya viwango, ubora na usalama wa bidhaa hizo zinazotumika kwa kiasi kikubwa na Watanzania.

WATAALAM WA NDANI WAFANIKISHA UPASUAJI WA MASHINE ZA USIKIVU (Cochlear Implant) KWA MARA YA KWANZA

July 28, 2026 Add Comment
Na Abduly Madenge, WAF – Dar es Salaam

Tanzania imeandika historia mpya katika sekta ya afya baada ya wataalamu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kufanikisha kwa mara ya kwanza upasuaji wa kupandikiza mashine za usikivu (Cochlear Implant) kwa kutumia wataalamu wa ndani pekee, bila kutegemea wataalamu kutoka nje ya nchi.

Global Education Fair 2026 yawafikia washiriki 1,113

July 27, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

GLOBAL Education Link (GEL) imesema jumla ya wanafunzi, wazazi na walezi 1,113 wamefikiwa na kupatiwa huduma kupitia maonesho ya Global Education Fair 2026 yaliyofanyika Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam.

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

July 27, 2026 Add Comment




Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imeingia hatua mpya ya kuongeza vyanzo vya uzalishaji umeme baada ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa umeme kwa nguvu ya Jua Kishapu utakaozalisha jumla ya megawati 100.



Hatua hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha jumla ya megawati 50 na kuingizwa katika Gridi ya Taifa, jambo lililoongeza uwezo na uthabiti wa gridi hiyo na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini.





Akizungumza katika hafla hiyo Julai 27, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema sekta ya nishati ni mhimili wa maendeleo ya Taifa ambapo Serikali inaendelea kufanya jitihada za kuongeza vyanzo mseto vya uzalishaji wa umeme (Energy Mix) ili kuhakikisha Tanzania haitegemei chanzo kimoja pekee cha uzalishaji wa umeme.

"Wananchi wa maeneo haya walikuwa wanategemea umeme uliokuwa unasafirishwa kutoka umbali mrefu. Kukamilika kwa mradi huu kutaifanya Tanzania kuwa na mfumo salama zaidi wa umeme na kuwa nchi ya mfano katika uzalishaji wa umeme unaostahimili mabadiliko ya tabianchi," amefafanua Mhe. Ndejembi.

Aidha, amelishukuru Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia ufadhili wa mkopo wenye masharti nafuu. Amesema ushirikiano huo unaonesha imani kubwa ya washirika wa maendeleo katika usimamizi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati nchini.

Pia ameipongeza TANESCO kwa kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ya umeme inayobadili taswira ya sekta ya nishati nchini, huku akiitaka kuhakikisha mradi huo unasimamiwa kwa karibu katika kila hatua ili ukamilike ndani ya muda uliopangwa na kuanza kuwanufaisha wananchi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, amesema utekelezaji wa mradi huo unaonesha dhahiri dhamira ya Wizara ya Nishati ya kuelekeza asilimia 97 ya bajeti yake katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

"Hatua hii ya utiaji saini ni matokeo ya diplomasia nzuri ya Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, iliyowafanya washirika wetu wa maendeleo kuendelea kuiamini Tanzania katika utekelezaji wa miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme. Tunaamini Tanzania itaendelea kuwa na umeme wa kutosha," amesisitiza Mhe. Mgalu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO, Mhe. Balozi Zuhura Bundala, amesema Bodi ilisimamia kwa karibu utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi huo na kuridhishwa na namna ulivyotekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha iliyowekezwa. Amesema utiaji saini wa awamu ya pili ni hatua nyingine muhimu inayodhihirisha mafanikio ya mradi huo.



Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema gharama za mradi mzima wa Umeme wa Jua wa Kishapu wenye uwezo wa kuzalisha megawati 150 ni takribani Shilingi bilioni 323. Kati ya fedha hizo, awamu ya kwanza yenye uwezo wa kuzalisha megawati 50 imegharimu Shilingi bilioni 118.6, huku awamu ya pili yenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 ikitarajiwa kugharimu takribani Shilingi bilioni 204.4.

"Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miezi 17 kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia TANESCO na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), ambalo limetoa mkopo wenye masharti nafuu," amefafanua Bw. Twange.

Mkataba huo umesainiwa kati ya TANESCO na muungano wa makampuni mbili kutoka Ufaransa na Tunisia, ambayo ni Sagemcom Energy, Telecom SAS na STEG International Services.









WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAWASILISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO KWA WADAU

July 27, 2026 Add Comment

  


📌 Naibu Katibu Mkuu afungua rasmi kikao kazi kwa wadau 

📌 Asema Sekta ya Utalii, Wanyanyamapori na Malikale ni kichocheo kikubwa cha uchumi wa Taifa

📌 Kutoa vipaumbele vinavyopimika kufikia lengo la watalii milioni 8 ifikapo 2030

Na Neema Chalila Mbuja

NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Nkoba Mabula leo Julai 27, 2026 amefungua rasmi Kikao Kazi cha Wadau wa Sekta ya Utalii kujadili Rasimu ya Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2030, wenye lengo la kutoa mwelekeo  wa utekelezaji wa pamoja wa malengo yaliyowekwa na vipaumbele vyake.

FLYING HORSE YAZINDUA OFISI ARUSHA, SHIJA AHAMASISHA UBORA

July 27, 2026 Add Comment

  

Kampuni ya ALC Lubricants, wazalishaji na wasambazaji wa vilainishi vya magari kupitia chapa ya Flying Horse, imefungua rasmi ofisi yake ya kwanza ya Kanda ya Kaskazini katika Jiji la Arusha, hatua inayotarajiwa kurahisisha upatikanaji wa bidhaa zake kwa wateja wa Arusha, Kilimanjaro na mikoa mingine ya ukanda huo.

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

July 27, 2026 Add Comment



Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius J. Ndejembi (Mb.), leo Julai 27, 2026, ameshuhudia utiaji saini wa mkataba wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa Umeme wa Jua wa Kishapu wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 100, utakaotekelezwa katika eneo la Ngunga, Wilaya ya Kishapu, Mkoa wa Shinyanga.


Mkataba huo wenye thamani ya shilingi bilioni 204.7 umesainiwa kati ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na mwakilishi wa mkandarasi anayetekeleza mradi huo, kampuni za Sagemcom Energy & Telecom SAS na STEG International Services.


Waziri Ndejembi amesema mradi wa Umeme wa Jua wa Kishapu ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuimarisha mseto wa vyanzo vya uzalishaji wa umeme (Energy Mix), ikiwa ni utekelezaji wa azma ya kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika, wa gharama nafuu na unaotokana na vyanzo vya nishati jadidifu.


Amefafanua kuwa, mradi huo unatekelezwa kwa awamu mbili zenye uwezo wa jumla wa kuzalisha Megawati 150. Awamu ya kwanza yenye uwezo wa Megawati 50 iligharimu shilingi bilioni 118.3 na kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za utekelezaji.


Aidha, Waziri Ndejembi amesema awamu ya pili yenye uwezo wa Megawati 100, ambayo utekelezaji wake umeanza rasmi kupitia utiaji saini wa mkataba utagharimu shilingi bilioni 204.7. Jumla ya gharama za utekelezaji wa awamu zote mbili ni shilingi bilioni 323.


Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka vyanzo vya nishati jadidifu, kuimarisha uthabiti wa mfumo wa umeme nchini na kuchangia kufikiwa kwa lengo la Serikali la kuwa na mseto wa vyanzo vya uzalishaji wa umeme pamoja na kufikia uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha kukidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye.


Hafla hii imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba; Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita; Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba; Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, pamoja na viongozi wengine wa Serikali, Chama cha Mapinduzi na wadau wa sekta ya nishati.






CHADEMA MUHEZA YAJITENGA NA ALIYEKUWA KATIBU WAO

July 27, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Tanga

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Muheza mkoani Tanga kimesema hakihusiki na vitendo vinavyodaiwa kufanywa na aliyekuwa Katibu wa chama hicho wilayani humo, Joseph Mwakidasi, huku kikiwataka wanachama kuendelea kudumisha mshikamano na kuepuka makundi yanayoweza kukigawa chama.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Katibu wa CHADEMA Jimbo la Muheza, Michael Mhina, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matukio yaliyojitokeza ndani ya chama katika siku za hivi karibuni.

Mhina alisema Julai 8 mwaka huu viongozi wa chama waliona kupitia vyombo vya habari taarifa za Mwakidasi akimtuhumu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, kutumia vibaya fedha zinazochangwa na wanachama kupitia kampeni ya "Tone Tone".

Alisema kutokana na uzito wa tuhuma hizo, Kamati Tendaji ya Wilaya ilikutana kwa dharura Julai 9 na kumuita Mwakidasi ili afafanue chanzo cha madai yake, lakini hakufika wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa m hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki kwenye kikao hicho wala kutoa maelezo.

Mhina alidai kuwa Julai 20, Mwakidasi aliwasili katika ofisi za CHADEMA Wilaya ya Muheza akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi kutoka wilaya nyingine pamoja na watu ambao, kwa mujibu wa chama hicho, si viongozi wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa mweka hazina wa chama.

Kwa mujibu wa Mhina, watu hao walifanya kikao ndani ya ofisi hizo na baadaye kurekodi na kusambaza taarifa mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii, jambo alilodai lilisababisha taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.

"Baada ya matukio hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki na yaliyofanywa na watu hao," alisema Mhina.

Alisema viongozi wa chama wilayani humo wanaendelea kumuunga mkono Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, pamoja na Mwenyekiti wa chama, Tundu Lissu.

Pia aliomba vyombo vya dola kuchunguza madai ya kuwahamasisha wananchi kuhudhuria mkutano kwa ahadi ya kulipwa fedha, akisisitiza kuwa CHADEMA haina utaratibu wa kuwalipa wanachama kushirikiio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa shughuli za chama.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Ally Mahanyu, alisema chama kinapinga vitendo vinavyodaiwa kufanywa na Mwakidasi kwa madai kuwa vilikiuka taratibu za chama.

Mahanyu alisema viongozi walimuita Mwakidasi mara kadhaa kwenye vikao vya Kamati Tendaji ili kutoa maelezo, lakini hakuitikia wito huo.

Aidha, alivitaka vyombo vya dola kuchunguza matukio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.

Aliwataka wanachama wa CHADEMA kuendelea kuwa watulivu, kuwaamini viongozi wao na kushiriki shughuli za ujenzi wa chama kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA Wilaya ya Muheza, Isa Mwaikani, alisema baraza hilo pia lilimuita Mwakidasi kutoa maelezo kuhusu tuhuma alizozielekeza kwa Heche, lakini hakuitikia wito huo.

Mwaikani alisema viongozi wa chama walishangazwa na tuhuma hizo kwa kuwa, kwa mujibu wa muundo wa uongozi wa chama, Makamu Mwenyekiti hahusiki na usimamizi wa fedha.

"Hatuelewi amepata wapi ujasiri wa kumtuhumu kiongozi wa juu wa chama bila kuwasilisha ushahidi kwenye vikao halali vya chama," alisema.

Aliongeza kuwa wanachama wengi wa CHADEMA Muheza wameendelea kubaki ndani ya chama na hali ya kisiasa wilayani humo ni tulivu.



Akijibu tuhuma hizo, aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Joseph Mwakidasi, alisema madai yanayotolewa dhidi yake hayana ukweli na kwamba anaendelea kutetea nafasi yake ndani ya chama.



Alisema hana mpango wa kuhamia chama kingine cha siasa na anasubiri maamuzi ya vikao vya chama kuhusu nafasi yake.



Kuhusu tuhuma alizomwelekeza John Heche, Mwakidasi alisema suala hilo linatokana na mijadala iliyofanyika katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika Dodoma, akidai baadhi ya taarifa zilizokuwa siri zilivuja kutoka ndani ya chama.



Mwisho.