HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

ALAMA YA UBORA YA AFRIKA YAZINDULIWA RASMI

July 31, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Denis Londo, amesema ubora wa bidhaa ni nguzo muhimu katika kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kwenye soko la kimataifa na kufanikisha azma ya nchi ya kujenga uchumi wenye thamani ya dola za Marekani trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO WAAHIDI KUSHIRIKIANA NA TRA KULIPA KODI KWA HIARI

July 31, 2026 Add Comment
Kariakoo, 31 Julai, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Kariakoo imeendelea kuimarisha ushirikiano na walipakodi kupitia mikutano ya ana kwa ana (Outreach) inayolenga kusikiliza, kutatua changamoto na kutoa elimu ya kodi ili kuwawezesha walipakodi kutekeleza wajibu wao kwa hiari.

WAZIRI MKUU AZINDUA BOTI MBILI ZA DORIA NA UOKOZI

July 31, 2026 Add Comment


-Atoa siku 14 Kituo cha Kitaifa cha Oparesheni kianze kufanya kazi

RAIS DKT SAMIA SULUHU AWASILI JIJINI LUANDA NCHINI ANGOLA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MBILI

July 31, 2026 Add Comment
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola Mhe. Tete Antonio baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026 kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana Waziri wa Mambo ya Nje wa Angola Mhe. Tete Antonio baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026 kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.





USHIRIKIANO WA WAZAZI WAWASHA MOTO WA UFAULU NGUVUMALI

July 31, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Tanga


WAZAZI, walezi, walimu na viongozi wa Kata ya Nguvumali jijini Tanga wameanzisha mkakati wa pamoja wenye lengo la kutokomeza matokeo ya Daraja Sifuri katika mitihani ya taifa, wakiamini ushirikiano wa wadau wote wa elimu ndiyo ufunguo wa kuongeza ufaulu wa wanafunzi.


Azimio hilo lilifikiwa katika kikao cha wazazi na walezi kilichofanyika katika Shule ya Sekondari Nguvumali, ambapo wadau hao walikubaliana kuimarisha ushirikiano kati ya shule, familia na serikali za mitaa ili kuboresha matokeo ya wanafunzi wa Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.

Akizungumza katika mkutano huo ambao uliitishwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo Ibrahim Okash, Diwani wa Kata ya Nguvumali, Mustapha Selebosi, alisema hatua hiyo inalenga kubadili taswira ya elimu katika kata hiyo kwa kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunza na kufanya vizuri katika mitihani ya taifa.


Alisema mafanikio ya wanafunzi hayawezi kupatikana bila ushiriki wa karibu wa wazazi, walezi, walimu na viongozi wa jamii.


"Siwezi kuitwa Meya wakati kata yangu inafanya vibaya katika mitihani ya taifa. Ni wajibu wetu sote kuhakikisha tunafuatilia maendeleo ya watoto wetu na kuweka mazingira yatakayowawezesha kufanya vizuri," alisema Selebosi.

Aliongeza kuwa kuboresha mfumo wa ufundishaji, kuongeza usimamizi wa wanafunzi na kuwajibisha kila mdau wa elimu ni miongoni mwa mikakati itakayosaidia kuinua kiwango cha ufaulu katika shule za kata hiyo.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Centre for Education (TCE), Yusuf Ogutu, alisema Kata ya Nguvumali ni miongoni mwa shule 10 zilizobainika kuwa na changamoto ya ufaulu, hali iliyosababisha kujumuishwa katika mpango maalumu wa mafunzo unaolenga kuongeza uwezo wa wanafunzi kujifunza kwa ufanisi na kujiandaa vizuri kwa mitihani.


Alisema mpango huo unatekelezwa na TCE kwa kushirikiana na Botnar Foundation na Inovex kupitia mradi wa Tanga Yetu, ukiwa na lengo la kuboresha ubora wa elimu katika shule za serikali.


Kwa mujibu wa Ogutu, changamoto kubwa kwa wanafunzi wengi si ukosefu wa ufundishaji, bali ni kutofahamu namna ya kujibu maswali ya umahiri, kuelewa uzito wa mada mbalimbali na kutumia mbinu sahihi za kufanya mitihani.


"Tumekuja na mafunzo haya ili kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa kuelewa badala ya kukariri. Tunawafundisha namna ya kuchambua muhtasari wa masomo, kutambua mada zenye uzito katika mitihani na kuelewa matumizi ya vitenzi vinavyotumika katika maswali," alisema.


Alieleza kuwa mafunzo hayo pia yanawajengea wanafunzi uwezo wa kupanga muda wa kujisomea, kujiandaa kabla ya mtihani, kufanya mitihani kwa ufanisi na kutathmini utendaji wao baada ya kumaliza mitihani.


Ogutu alisema taasisi hiyo pia imeanza kufanya utafiti katika shule zote 27 za sekondari za serikali zilizopo Jiji la Tanga ili kubaini sababu zinazosababisha kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.


Alisema matokeo ya utafiti huo yatawezesha wadau wa elimu kuweka mikakati ya muda mrefu ya kuboresha ubora wa elimu na kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule hizo.


Naye Inspekta wa Polisi wa Kata ya Nguvumali, Sharifu Kiswamba, alisema pamoja na juhudi zinazoendelea kufanywa, utoro na tabia ya baadhi ya wanafunzi kuzurura mitaani wakati wa masomo bado ni changamoto kubwa inayochangia matokeo duni.


Aliwataka wazazi kuongeza usimamizi wa watoto wao na kushirikiana kwa karibu na walimu pamoja na viongozi wa kata ili kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria masomo kikamilifu na kutumia muda wao kujifunza.


Hata hivyo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Nguvumali Ibrahim Okash alipongeza juhudi hizo akieleza kwamba vitasaidia kuwezesha kuongezeka kwa ufaulu kutokana na ushirikiano katika jambo lolote lile ni muhimu kwa ajili ya ustawi wake.


Alisema kwamba mkutano huo ni muhimu kwa sababu unawawezesha kukutana na wazazi na walezi ili kuweza kuweka nguvu za pamoja kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake ipasavyo ili kuweza kuchangia ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne na pili 


Mwisho

TRA KARIAKOO YAWAELIMISHA WAFANYABIASHARA KUHUSU MABADILIKO YA SHERIA ZA KODI 2026/2027

July 31, 2026 Add Comment
Kariakoo, Julai 30, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa kikodi Kariakoo imeendesha semina maalum kwa wafanyabiashara ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuendelea kutoa elimu ya kodi na kuwajengea uelewa kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi yaliyoanza kutumika kwa mwaka 2026/2027.

MD TWANGE AWATAKA WANASHERIA WA TANESCO KUENDELEA KUSIMAMIA MAADILI NA TAALUMA

July 31, 2026 Add Comment


📌 Afungua Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO jijini Mwanza


📌 Awasisitiza kutoa ushauri wa kisheria kwa wakati na kulinda maslahi ya Shirika


Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amewataka wanasheria wa shirika kuendelea kusimamia maadili ya taaluma, kutoa ushauri wa kisheria kwa wakati na kulinda maslahi ya shirika ili kuimarisha utendaji na kuhakikisha TANESCO inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Bw. Twange ameyasema hayo wakati akifungua Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO lililoanza Julai 28, 2026 jijini Mwanza, likiwakutanisha wanasheria kutoka Makao Makuu, Ofisi za Kanda na Kampuni Tanzu za TANESCO kwa lengo la kujengeana uwezo na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya kisheria yanayohusu utendaji wa shirika.

Akizungumza katika ufunguzi wa jukwaa hilo, Bw. Twange amewapongeza wanasheria hao kwa mchango wao katika kulinda maslahi ya shirika na kuhakikisha shughuli zake zinafanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu.

“Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya. Ushauri wa kisheria unaotolewa kwa wakati umekuwa ukisaidia TANESCO kufanya maamuzi sahihi na kuepusha migogoro ambayo ingeweza kuzuilika mapema,” amesema Bw. Twange.

Amewasisitiza kuendelea kuzingatia maadili ya taaluma, kutunza siri za kazi na kutoa ushauri wa kitaalamu unaolinda maslahi ya shirika.

“Kila mmoja wetu ana wajibu wa kulinda taasisi. Kwa upande wa wanasheria, hilo linaanza na kuzingatia maadili ya taaluma, kutunza siri za kazi na kuhakikisha kila ushauri unaotolewa unalinda maslahi ya TANESCO na kuimarisha utendaji wake,” amesema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa TANESCO, Wakili Sundi Mahalu, amesema idara hiyo itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ili kuhakikisha shughuli za shirika zinaendelea kufanyika kwa kuzingatia misingi ya utawala bora na sheria.

“Jukwaa hili linatupa nafasi ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuimarisha uwezo wetu wa kitaaluma ili tuendelee kutoa huduma bora za kisheria zinazochangia mafanikio ya TANESCO,” amesema Wakili Mahalu.

Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO linafanyika kwa siku tatu likiwa sehemu ya mkakati wa shirika wa kuendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wake wa sheria, hatua inayochangia ufanisi wa utendaji, usimamizi bora wa masuala ya kisheria na ulinzi wa maslahi ya shirika.


MOROCCO YAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI NA TANZANIA

July 31, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mahusiano ya kidiplomasia kati ya Ufalme wa Morocco na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yameendelea kuimarika kwa kasi tangu ziara ya kihistoria ya Kiserikali ya Mfalme Mtukufu Mohammed VI nchini Tanzania mwaka 2016, huku ushirikiano katika sekta mbalimbali ukizidi kupanuka na kuleta manufaa kwa mataifa yote mawili.

LRCT YAFANYA WARSHA YA NAFASI YA SHERIA YA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

July 31, 2026 Add Comment

 



Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania  Bw. Burhan Kishenyi, akizungumza Julai 30, 2026 wakati akifungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
...........................................
Na Mwandishi Wetu Dodoma


Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania  Bw. Burhan Kishenyi, leo tarehe 30.07.2026 amefungua warsha ya uelimishaji kuhusu Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, Sura ya 183, inayolenga kuimarisha uelewa wa wadau katika kuhakikisha sheria hiyo inatekelezwa kwa ufanisi sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Warsha hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, jijini Dodoma, na imewakutanisha washiriki kutoka taasisi mbalimbali za umma na wadau wanaoshughulika na masuala ya haki na ustawi wa watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Bw. Kishenyi amesema kuwa utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ni msingi muhimu katika kujenga jamii jumuishi inayotoa fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi. 

Amesisitiza kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inaweka msisitizo katika ushirikishwaji wa makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili kuchangia kikamilifu maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, amewataka washiriki kutumia warsha hiyo kujadili kwa kina wajibu wa kila taasisi katika kutekeleza matakwa ya sheria, kubadilishana uzoefu na kuibua mapendekezo yatakayosaidia kuondoa vikwazo vinavyokwamisha upatikanaji wa haki na huduma kwa watu wenye ulemavu.

Washiriki wa warsha hiyo wanatarajiwa kujengewa uwezo kuhusu tafsiri na utekelezaji wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, pamoja na namna ya kuoanisha utekelezaji wake na malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kujenga Tanzania jumuishi, yenye usawa, haki na maendeleo endelevu kwa wananchi wote.

Kwa upande wake , Bw. Harold Sungusia, Rais Mstaafu wa TLS ambaye pia ni wakili wa kujitegemea  alisisitiza umuhimu wa kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika mchakato wa maboresho ya sheria ili kuhakikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inatekelezwa kwa misingi ya usawa, haki na ushirikishwaji.

Akizungumza katika mkutano uliojadili mwelekeo wa maboresho ya sheria na maendeleo ya taifa, Bw. Sungusia alisema kuwa sheria bora zinapaswa kuzingatia mahitaji ya makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, ili wasibaki nyuma katika safari ya maendeleo.

Alieleza kuwa ushiriki wa watu wenye ulemavu katika utoaji wa maoni na maamuzi kuhusu sheria ni muhimu kwa sababu unasaidia kutunga na kuboresha sheria zinazolinda haki zao na kuondoa vikwazo vinavyowazuia kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii, kiuchumi na kisiasa.

Aidha, alibainisha kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji mfumo wa sheria unaohakikisha fursa sawa kwa wananchi wote bila ubaguzi wa aina yoyote.

Bw. Sungusia alisema kuwa kujenga taifa lenye maendeleo endelevu kunategemea uwepo wa sheria jumuishi zinazolinda haki za kila mwananchi na kuweka mazingira yanayowawezesha watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Washiriki wa mkutano huo walikubaliana kuwa ushirikishwaji wa makundi maalumu katika mchakato wa maboresho ya sheria ni nguzo muhimu ya kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kujenga jamii yenye usawa na haki kwa wote.
Wadau mbalimbali wakishiriki warsha hiyo.

Wadau wakichangia mada katika warsha hiyo.
Michango mbalimbali ikitolewa katika warsha hiyo.
Warsha hiyo ikiendelea
Michango ikiendelea kutolewa.
Taswira ya warsha hiyo.
 

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONDOKA NCHINI KUELEKEA LUANDA NCHINI ANGOLA KUSHIRIKI KATIKA UZINDUZI WA HOSPITALI ILIYOPEWA JINA LA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

July 31, 2026 Add Comment

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Luanda, Angola ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hospitali iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tarehe 31 Julai, 2026. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mama Maria Nyerere muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kuelekea Luanda, Angola ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hospitali iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tarehe 31 Julai, 2026. 



WABUNIFU WA KITANZANIA KUONYESHA TEKNOLOJIA ZAO TANGA

July 30, 2026 Add Comment
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ametangaza maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kwa mwaka 2026, yatakayofanyika kuanzia Agosti 15 hadi 24 katika viwanja vya michezo vya Shule ya Sekondari Usagara, jijini Tanga.

MAMBAMIAMBA YAINGIA RASMI KATIKA SAFARI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 30, 2026 Add Comment

 





Wananchi wa Kata ya Mambamiamba, Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, leo Julai 30, 2026, wamejengewa uelewa kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la Tanzania Women Empowerment Network (TAWEN).


Hafla hiyo imezikutanisha taasisi mbalimbali za Serikali, wadau wa maendeleo na wananchi, ambapo kila taasisi imepata fursa ya kuwasilisha huduma zake pamoja na kuelezea fursa zinazopatikana katika sekta zake. Wizara ya Nishati ilitumia fursa hiyo kutoa elimu kuhusu faida za matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwemo kulinda afya, kuhifadhi mazingira na kupunguza gharama za matumizi ya nishati.


Akiwasilisha mada, Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati, Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, Mha. Benezeth Kabunduguru, amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034), unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034, kutoka asilimia 28.6 mwaka 2025.


Amesema lengo hilo litafikiwa kupitia ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, wadau wa maendeleo na wananchi katika kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na kuendelea kutoa elimu kuhusu faida za matumizi yake. Ameongeza kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia yanachangia kulinda afya za wananchi kwa kupunguza athari za moshi unaotokana na matumizi ya kuni na mkaa, kuhifadhi mazingira kwa kupunguza ukataji wa miti, pamoja na kuokoa muda na gharama zinazotumika katika shughuli za kupikia, hususan kwa wanawake na watoto.


Aidha, amewahimiza wananchi wa Kata ya Mambamiamba kuchangamkia matumizi ya teknolojia mbalimbali za nishati safi ya kupikia zinazopatikana nchini ili kuongeza matumizi ya nishati hiyo na kuunga mkono juhudi za Serikali za kufikia malengo ya Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TAWEN, Balozi Amina Salum Ali, ameipongeza Wizara ya Nishati na taasisi zake kwa kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia. Amesema juhudi hizo zinaongeza uelewa wa wananchi na kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu matumizi ya nishati.


Ameongeza kuwa TAWEN itaendelea kushirikiana na Wizara ya Nishati pamoja na wadau wengine kuhakikisha elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia inawafikia wanawake na jamii kwa ujumla ili kuongeza matumizi ya nishati hiyo kwa manufaa ya afya, mazingira na maendeleo ya kiuchumi ya wananchi.


LILIAN LIUNDI: MAZINGIRA WEZESHI NI UFUNGUO WA KUONGEZA USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA SEKTA YA USAFIRI WA UMEME

July 30, 2026 Add Comment

     

Mwanzilishi wa Mradi wa Pink Ride na Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP aliyemaliza muda wake, Lilian Liundi, akizungumza wakati wa mafunzo kwa wanawake madereva wa bajaji kuhusu usafiri wa umeme na usawa wa kijinsia, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwanzilishi Mradi wa Pink Ride wa Wanawake Madereva wa Magari ya Magurudumu Matatu( Bajaj) na Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP aliyemaliza muda wake, Lilian Liundi amesema mabadiliko kuelekea matumizi ya vyombo vya usafiri vinavyotumia nishati ya umeme yanapaswa kuambatana na sera na mazingira wezeshi yatakayoongeza ushiriki wa wanawake katika sekta ya usafiri na kuwawezesha kunufaika na fursa za kiuchumi zinazojitokeza.

TIBAMAZOEZI YATAJWA KUWA SULUHISHO LA MAUMIVU YA MUDA MREFU

July 30, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

Hospitali ya Medinova Specialized Polyclinic imezindua rasmi huduma ya Tibamazoezi (Physiotherapy) ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupanua huduma za kibingwa na kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini.

TADB YAIMARISHA NGUVU YA WAKULIMA KUELEKEA DIRA YA MAENDELEO 2050

July 30, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imesema imeendelea kuimarisha nafasi yake katika kufadhili sekta ya kilimo nchini baada ya mtaji wake kuongezeka kutoka Sh bilioni 60 hadi Sh bilioni 452.16, hatua iliyowezesha kupanua utoaji wa mikopo na huduma za kifedha kwa wakulima, wafugaji na wavuvi.

WAANDISHI WA HABARI WAPATIWA MAFUNZO YA WELEDI NA MAADILI

Kajunason July 30, 2026 Add Comment

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam, Julai 29, 2026

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza rasmi kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini, yakilenga kuimarisha weledi, maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa waandishi wa habari wa Bongo FM jijini Dar es Salaam, redio dada ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya JAB, Tido Mhando, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wa kuelewa na kutekeleza matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229, kwa kuzingatia weledi, maadili na uwajibikaji.

“Mafunzo haya ni utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari. Leo tumeanza rasmi na waandishi wa habari wa Bongo FM, tutaendelea kwa vyombo vingine pia kwa sababu, kutakuwa na mafunzo ya muda mfupi na ya muda mrefu. Hivyo, mafunzo haya yawe fursa ya kujenga uwezo na kuweka msingi imara wa kukuza na kulinda taaluma ya uandishi wa habari kwa kuongeza maarifa na weledi,” amesema Wakili Kipangula.

Akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, historia na uanzishwaji wake, katika mafunzo hayo yaliyoanza leo tarehe 29 Julai, 2026 katika ukumbi wa Bodi, Wakili Kipangula amesema sheria hiyo imeweka msingi wa kuimarisha taaluma ya habari kwa kubainisha viwango vya weledi, maadili na uwajibikaji

Amesisitiza kuwa JAB itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo kwa kuzingatia haki, uwazi na kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari, huku ikihakikisha taaluma ya habari inalinda maslahi ya umma..

Aidha, amewataka waandishi wa habari kuzingatia sheria na maadili katika kila hatua ya ukusanyaji, uchakataji na usambazaji wa habari ili kujiepusha na madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na ukiukaji wa taaluma.

Amesema kuzingatia misingi hiyo kunajenga weledi, kunalinda heshima ya taaluma na kuimarisha imani ya jamii kwa vyombo vya habari.
Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.

Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

"Mafunzo haya yametupatia maarifa muhimu yatakayotusaidia kutekeleza majukumu yetu kwa kuzingatia maadili, sheria na viwango vya taaluma ya uandishi wa habari. Tunaamini yatachangia kuboresha utendaji wetu na kuongeza uwajibikaji katika kuhabarisha umma," wamesema washiriki hao.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.

MAHAKAMA YAMFUNGA MIAKA 30 JELA KWA KUSAFIRISHA KILO 75.15 ZA MIRUNGI

July 29, 2026 Add Comment
Mahakama ya Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga imemhukumu Isa Musini Rashidi  maarufu kama Hamidu kifungo cha miaka 30 jela baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kusafirisha kilo 75.15 za dawa za kulevya aina ya mirungi (Khat).

PSSSF YAFIKIA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM TANGA

July 29, 2026 Add Comment





Tanga, Julai 28, 2026

Katika kuendeleza dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSI) chini ya kampeni yake ya #PSSSFKaribuNaJamii, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umekabidhi rasmi mradi wa miundombinu wenye thamani ya Shilingi milioni 25 katika Shule ya Msingi Majani Mapana iliyopo mkoani Tanga.

Mradi huo unahusisha ujenzi wa chumba cha darasa, chumba cha mapumziko pamoja na vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bw. Kwame Temu alieleza kuwa msaada huo unalenga kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalum wanapata haki yao ya msingi ya elimu. 

Alisisitiza kuwa hatua hiyo itawasaidia wanafunzi hao kujifunza katika mazingira yanayowawezesha kujifunza kwa ufanisi, kushiriki katika michezo na kukuza vipaji vyao mbalimbali.