HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TANZANIA, MAREKANI KUIUNGANISHA AFRIKA KWENYE SEKTA YA AFYA

September 04, 2026 Add Comment

Na John Mapepele – WAF

Washington, D.C.

Serikali ya Tanzania imekubaliana na Chama cha Wafanyabiashara cha Marekani (U.S. Chamber of Commerce) mjini Washington, D.C na Serikali ya Marekani kufanya utekelezaji wa kimkakati wa mkataba wa sekta ya afya ulioingiwa hivi karibuni ili kuzinufaisha pande zote mbili,huku wakiifanya Tanzania kuwa muhimili wa uzalishaji na usambazaji dawa na vifaa tiba katika bara la Afrika.

SHANGWE CHEM CHEM SAFARI LODGE WAKISHINDA TENA TUZO HOTEL BORA YA KIFAHARI AFRIKA

September 04, 2026 Add Comment

  

Mussa Juma,Babati
mussasiwa@gmail.com 

Kwa mwaka wa pili mfululizo, hoteli ya kitalii ya Chem Chem Safari Lodge imeshinda tuzo ya hotel Bora ya kifahari barani Afrika katika tuzo ambazo ziliandaliwa na shirika la kimataifa la Utalii, World Travel Awards (WTA).

TCAA NA UMOJA WA ULAYA WATHIBITISHA DHAMIRA YA KUIMARISHA USIMAMIZI WA USALAMA WA USAFIRI WA ANGA

September 04, 2026 Add Comment

 


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA).
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA).
Kiongozi wa Ujumbe wa EASA Bw. Jose Miguel Manso Angulo akizungumza wakati wa kikao hicho.

***
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari, amethibitisha dhamira ya Mamlaka hiyo ya kujenga Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya kiwango cha kimataifa barani Afrika, yenye matarajio ya kufikia viwango vinavyolingana na mamlaka za usafiri wa anga za Ulaya katika ubora wa udhibiti, umahiri wa kitaalamu, ufanisi wa kiutendaji na usimamizi wa usalama wa anga.

WALIMU KUTUMIA TEHAMA KUBORESHA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI

September 04, 2026 Add Comment


ARUSHA, Septemba 4, 2026 — Mafunzo ya siku nne ya Umahiri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa Walimu Tanzania (ICT Competency Standards for Teachers in Tanzania - ICT CSTT) yameahirishwa leo jijini Arusha, huku walimu wakihimizwa kutumia maarifa na stadi walizojifunza kuboresha ufundishaji, ujifunzaji, tathmini pamoja na kuwawezesha waalimu wenzao.
Mafunzo hayo yaliyofanyika Gold Crest Hotel kuanzia Septemba 1 hadi 4, 2026, yamewajengea washiriki uwezo wa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Akili Bandia (AI), rasilimali za kidijitali na mifumo ya kujifunzia kwa njia ya mtandao katika kazi za kila siku za mwalimu.
Akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Bw. Mathias Innocent Mvula, amebainisha kuwa kukamilika kwa mafunzo hayo kunapaswa kuwa mwanzo wa utekelezaji wa maarifa na stadi hizo katika shule za na za jirani.


Kwa mtazamo wake, thamani ya uwekezaji huo itaonekana kupitia mabadiliko katika ufundishaji na ujifunzaji, badala ya kuishia kwenye vyeti. Amewataka washiriki kutekeleza mipango kazi waliyoandaa wakati wa mafunzo na kuonesha hatua watakazochukua katika utekelezaji wanaporejea shuleni.
Akieleza mazingira mapya ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 Toleo la mwaka 2023, Bw. Mvula amebainisha kuwa maendeleo ya teknolojia, hususan Akili Unde, yamebadilisha namna watu wanavyopata taarifa na maarifa, hali inayohitaji walimu kuongeza uwezo wa kutumia zana hizo kwa malengo ya kuinua ubora wa elimu.


Amebainisha pia kuwa simu za mkononi na vifaa vingine vya kidijiti vinaweza kuwa nyenzo muhimu za kujifunzia na kufundishia vinapotumiwa kwa usahihi. Hata hivyo, matumizi ya teknolojia yanapaswa kwenda sambamba na mabadiliko ya sera na mitaala yanayolenga kujenga umahiri wa mwanafunzi.
Kwa mujibu wa Bw. Mvula, elimu ya sasa inalenga kumwandaa mwanafunzi kutumia maarifa na stadi katika maisha halisi, kukabiliana na changamoto na kutumia fursa za kiuchumi, badala ya kutegemea ajira pekee. Ameeleza kuwa kuimarishwa kwa mikondo ya amali ni miongoni mwa hatua zinazolenga kuongeza uwezo huo.
Katika kuendana na mabadiliko hayo, Bw. Mvula ametoa wito kwa walimu kuendelea kutumia fursa za Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA), akibainisha kuwa ujifunzaji kwa njia ya mtandao unawapa nafasi ya kuongeza uwezo kitaaluma na kitaalamu bila kulazimika kurejea chuoni mara kwa mara.


Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuweka mifumo endelevu ya kuimarisha umahiri wa walimu, ikiwemo utaratibu wa kutambua mafunzo kabilishi mbalimbali ya kuwajengea uwezo walimu ili kuboresha elimu nchini. 
MKOA WATAKA UJUZI UONEKANE SHULENI
Akizungumza katika hafla hiyo, Afisa Elimu Mkoa wa Arusha, Bw. Vicent Boniface Kayombo, amewataka walimu walioshiriki katika mafunzo hayo kuwa kiungo cha kusambaza maarifa kwa walimu wenzao na kuhakikisha ujuzi walioupata unatafsirika katika vitendo vya ufundishaji na ujifunzaji shuleni.
Kayombo ameeleza kuwa Mkoa wa Arusha una mpango wa utekelezaji wa MEWAKA katika shule za msingi na sekondari, hivyo walimu walioshiriki katika mafunzo hayo wana nafasi muhimu ya kusaidia kufanikisha mpango huo kwa kushirikisha wenzao na kuchochea matumizi yenye tija ya TEHAMA katika shule zao.
VETA YAPANIA KUIMARISHA UJUZI KUPITIA USHIRIKIANO NA WAAJIRI

VETA YAPANIA KUIMARISHA UJUZI KUPITIA USHIRIKIANO NA WAAJIRI

September 04, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imewaalika waajiri na wamiliki wa viwanda nchini kuendelea kushirikiana na mamlaka hiyo katika kuandaa na kuendeleza wataalamu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na kuchochea maendeleo ya Taifa.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore, alitoa kauli hiyo jana jijini Dodoma wakati wa hafla ya kusaini Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya VETA na Kampuni ya Van Mo, inayolenga kuimarisha ushirikiano katika kuwaendeleza vijana wenye ujuzi na kuwawezesha kupata ajira mara baada ya kuhitimu mafunzo yao.

Makubaliano hayo yaliyosainiwa katika Ukumbi wa Mikutano wa VETA Makao Makuu yalihusisha CPA Kasore kwa upande wa VETA na Meneja Mkuu wa Van Mo, Fathi Ahmed Ally. Kampuni hiyo inajihusisha na shughuli mbalimbali zikiwemo usafirishaji, uchukuzi, uuzaji wa mafuta, umiliki wa majengo na ardhi, kilimo, utalii pamoja na shughuli za uzalishaji viwandani.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, pande hizo zinalenga kuongeza upatikanaji wa wahitimu wenye umahiri, tija, ubunifu, maadili na wanaozingatia usalama kazini, huku Van Mo ikitoa fursa za ajira kwa wahitimu wa VETA wenye sifa zinazohitajika.

Aidha, ushirikiano huo utasaidia kuoanisha programu za mafunzo ya ufundi stadi na mahitaji halisi ya sekta ya viwanda na biashara pamoja na kuwawezesha wanafunzi kupata mafunzo kwa vitendo katika maeneo ya kazi.

Maeneo ya ushirikiano yaliyoainishwa katika MoU hiyo ni pamoja na mafunzo ya udereva wa magari makubwa, usimamizi wa vyombo vya usafiri, uchukuzi na uhifadhi wa mizigo, usimamizi wa mnyororo wa ugavi, ukaguzi na ukarabati wa magari pamoja na mifumo ya umeme na elektroniki ya magari. Maeneo mengine ni uendeshaji wa maghala na usimamizi wa stoo, uendeshaji wa vituo vya mafuta, ujenzi, usimamizi wa majengo na miundombinu, utalii na ukarimu pamoja na kilimo na uhifadhi wa mazao.

Akizungumza baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo, Kasore alisema ushirikiano huo pia utasaidia kuwajengea uwezo wakufunzi na kuhakikisha mafunzo yanayotolewa na VETA yanaendana na mahitaji ya soko la ajira.

Alisema VETA itaendelea kushirikiana na waajiri na wamiliki wa viwanda ili kutambua fursa zilizopo na kuhakikisha wahitimu wanapata nafasi za ajira katika viwanda na maeneo mengine yenye uhitaji wa wataalamu wenye ujuzi.

“Tutahakikisha pia wenzetu wa Van Mo wanapohitaji wataalamu wenye ujuzi mbalimbali, sisi VETA tuweze kusaidia kuwapata. Sambamba na hilo, ushirikiano huu una maslahi mapana kwa wananchi katika kupata fursa za ajira,” alisema Kasore.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Van Mo, Fathi Ahmed Ally, alisema kampuni hiyo imelenga kutoa ajira kwa takribani vijana 500 wenye ujuzi mbalimbali waliohitimu katika vyuo vya VETA.

Alisema kampuni hiyo imeamua kushirikiana na VETA kutokana na ubora wa ujuzi unaopatikana kwa wahitimu wake, hususan katika fani zinazohusiana na shughuli za usafirishaji ambazo ni muhimu katika utekelezaji wa shughuli za kampuni hiyo.

“Kilichotuvutia kuja VETA ni kutokana na wahitimu kutoka katika vyuo hivi kuwa na ujuzi ambao sisi tunauhitaji katika kampuni yetu, hususan shughuli za usafirishaji. Hivyo tumeona hapa ndipo mahali sahihi pa kuwapata vijana wenye ujuzi huo,” alisema Fathi.

KLINIKI YA VIWANGO KUSOGEZA HUDUMA KARIBU KWA WADAU WA VIPODOZI NA CHAKULA

September 04, 2026 Add Comment
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeandaa kliniki ya viwango katika maeneo ya Soko Kuu la Biashara Kariakoo na Mwenge jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kusogeza huduma za kitaalamu karibu na wafanyabiashara wa bidhaa za chakula na vipodozi ili kuwawezesha kuendesha biashara zinazokidhi viwango.

TCAA NA UMOJA WA ULAYA WATHIBITISHA DHAMIRA YA KUIMARISHA USIMAMIZI WA USALAMA WA USAFIRI WA ANGA

September 04, 2026 Add Comment

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza   wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka  Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA)
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza   wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka  Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA)
 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari, amethibitisha dhamira ya Mamlaka hiyo ya kujenga Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya kiwango cha kimataifa barani Afrika, yenye matarajio ya kufikia viwango vinavyolingana na mamlaka za usafiri wa anga za Ulaya katika ubora wa udhibiti, umahiri wa kitaalamu, ufanisi wa kiutendaji na usimamizi wa usalama wa anga.


Alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa wataalamu wa msaada wa kujengeana uwezo kutoka Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA), kilichofanyika tarehe 3 Septemba 2026 katika Makao Makuu ya TCAA jijini Dar es Salaam. Dkt. Bakari aliushukuru Umoja wa Ulaya kwa kuendelea kutoa msaada na kuonyesha imani katika maendeleo ya Tanzania. Pia alieleza juhudi zinazofanywa na TCAA kuimarisha mifumo yake ya usimamizi, ikiwemo uundaji na utekelezaji wa Mfumo wake wa ndani wa TCAA wa Huduma za Usafiri wa Anga (Civil Aviation Services Portal – CASP), ambao ulipewa pongezi na timu ya EASA.

Timu ya EASA ilieleza kuridhishwa kwake na maendeleo na juhudi zilizooneshwa na TCAA wakati wa ziara hiyo ya siku tatu. Aidha, timu hiyo ilitambua maendeleo yaliyofikiwa na kuhimiza TCAA kuendeleza kasi katika kushughulikia masuala yote muhimu ya usimamizi wa usalama wa anga.

Kwa upande wake Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Ulaya alithibitisha dhamira ya EU ya kuendelea kuisaidia Tanzania kupitia msaada wa kitaalamu, mbinu za utekelezaji wa vitendo na kubadilishana ujuzi. Aidha, alieleza kuwa Umoja wa Ulaya umetenga Euro milioni 2 kwa ajili ya msaada unaohusiana na kuboresha zaidi Masuala ya usafiri wa anga nchini.

Ujumbe wa EASA uliongozwa na Bw. Jose Miguel Manso Angulo akiambatana na Bw. Gustavo Juan Roman Barba na Bw. Antonio Portales Pelaez.

Ujumbe huo, uliofika nchini kwa siku tatu kuanzia tarehe 1 hadi 3 Septemba 2026, ulifuatilia maendeleo ya Nchi (State) katika utekelezaji wa hatua za marekebisho pamoja na kuimarisha usimamizi wa usalama wa Usafiri wa anga. Majadiliano yalihusu maeneo ya ki sheria, muundo wa taasisi, uchunguzi wa ajali ndege, utoaji wa leseni kwa eneo la rasilimali watu la Usafiri wa anga, ubora wa ndege kwa matumizi (airworthiness) na uendeshaji wa ndege, pamoja na kufanya vikao na waendeshaji wa mashirika ya ndege kuhusu hoja zilizobainishwa, Mipango ya Hatua za Marekebisho (Corrective Action Plans) na ufuatiliaji wa utekelezaji wake.

Ujumbe huo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za Tanzania za kuimarisha usimamizi wa usalama wa Usafiri wa anga na kuonesha maendeleo endelevu kuelekea kutimiza matakwa ya kuondolewa kwenye Orodha ya Usalama wa Anga ya Umoja wa Ulaya (European Union Air Safety List).

MRADI WA UMEME MPOMVU – GGM KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI GEITA – MHE. SALOME

September 04, 2026 Add Comment

 


Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inaendelea kuimarisha miundombinu ya umeme nchini kupitia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Mpomvu hadi kituo cha kupokea na kupoza umeme cha GGM, wenye urefu wa takribani kilomita 6.7.


Akizungumza Septemba 3, 2026, jijini Dodoma, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi huo, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema kukamilika kwa mradi huo kutaimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika na kuchochea shughuli za kiuchumi, ikiwemo uzalishaji, ajira, ongezeko la mapato na uwekezaji.




Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na TANESCO na wadau wa sekta ya nishati kuhakikisha miundombinu ya umeme inaendana na kasi ya ukuaji wa mahitaji.


“Serikali itaendelea kushirikiana na TANESCO na wadau wote wa sekta ya nishati kuhakikisha miundombinu ya umeme inaendana na kasi ya ukuaji wa mahitaji. Tunataka kuona umeme unaozalishwa nchini ukitumika kikamilifu kuchochea uzalishaji, kuongeza ajira, kuongeza mapato na kuvutia uwekezaji zaidi. Mradi huu ni kielelezo cha falsafa hiyo,” amesema Mhe. Salome.




Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema mradi huo unatekelezwa kwa miezi 18 kutoka tarehe ya utiaji saini mkataba ukilenga kukidhi ongezeko la mahitaji ya umeme kwa GGM.

“Mradi huu unagharimu takribani Shilingi bilioni 63.19 za Kitanzania na kutokana na kuwa GGM ni miongoni mwa wateja wetu wakubwa wenye kuchangia kiasi kikubwa cha mapato kwa Shirika, tutahakikisha mradi huu unafanikiwa kama inavyotarajiwa kukidhi ongezeko la mahitaji yao kwa manufaa ya pande zote mbili na pato la Taifa kwa ujumla,” amesema Bw. Twange.



Aidha, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO, Mhe. Balozi Zuhura Bundala, amesema utiaji saini wa mkataba huo ni sehemu ya hatua za kimkakati za kujenga uwezo wa TANESCO kukidhi mahitaji ya wateja na kufungua fursa za uwekezaji na ajira.

“Utiaji saini huu ni sehemu ya kimkakati kujenga uwezo wa TANESCO kukidhi mahitaji ya wateja na kufungua fursa za uwekezaji na ajira. Bodi tutaendelea kuisimamia TANESCO kukidhi ongezeko la hitaji la umeme kwa kuimarisha na kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu ya umeme,” amesema Mhe. Bundala.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO kwa namna inavyosimamia Shirika katika ujenzi wa uchumi wa kisasa kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


“Niipongeze Bodi ya Wakurugenzi TANESCO kwa namna mnavyosimamia Shirika hili kujenga uchumi wa kisasa kuelekea Dira 2050. Utekelezaji wa mradi huu unatupa nguvu zaidi kwa sababu sekta zote, nishati na madini, zipo chini yetu,” amesema Mhe. Mgalu.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashimu Komba, akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa huo amesema Uongozi wa Mkoa umejipanga kushirikiana na mkandarasi wa mradi huo kuhakikisha utekelezaji wake haupati kikwazo, akisisitiza umuhimu wa nishati ya umeme katika kuchochea maendeleo ya sekta mbalimbali.


“Ni dhahiri, nishati ya umeme inachagiza maendeleo ya sekta zote. Tunampongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyosukuma kwa dhati agenda ya nishati ya umeme kuwafikia wananchi. Mamlaka ya Mkoa imejipanga kushirikiana na Mkandarasi wa mradi wa umeme wa Mpomvu–GGM kuhakikisha mradi haupati kikwazo,” amesisitiza Mhe. Komba.


Kukamilika kwa mradi huo, kutatoa fursa ya njia ya awali ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoto 33 iliyokuwa ikipelekea umeme GGM, kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika Mkoa wa Geita na maeneo ya pembezoni , vilevile kuwezesha wananchi kuendesha shughuli zao za uzalishaji kwa ufanisi, pamoja na kuweka mazingira wezeshi kwa uwekezaji mpya ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuimarisha na kuongeza uwezo wa mfumo wa usafirishaji na usambazaji wa umeme kukidhi mahitaji ya sasa na yajayo.




TBS YAIBUKA MSHINDI WA PILI KATIKA MAONESHO YA 21 YA BIASHARA AFRIKA MASHARIKI (MEATF)

September 04, 2026 Add Comment

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeibuka mshindi wa pili katika kundi la Taasisi za Udhibiti wakati wa Maonesho ya 21 ya Biashara Afrika Mashariki (MEATF), yanayofanyika katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.

TUME YA TAIFA YA UNESCO YASHIRIKI UZINDUZI WA MWONGOZO WA MAWASILIANO KATI YA MZAZI NA MTOTO ZANZIBAR

September 03, 2026 Add Comment



ZANZIBAR, Septemba 3, 2026 — Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania imeshiriki katika uzinduzi wa Mwongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto kuhusu Haki ya Afya ya Uzazi (Parent-Child Communication – PCC Toolkit), unaolenga kuimarisha mawasiliano ndani ya familia na kusaidia kulinda afya na ustawi wa watoto na vijana Zanzibar.

Mwongozo huo unazinduliwa leo katika Hoteli ya Verde Zanzibar na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar, Mheshimiwa Zawadi Amour Nassor, katika hafla iliyowakutanisha viongozi na wadau mbalimbali wanaohusika na afya, ulinzi na ustawi wa watoto.


Mwongozo huo umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar na UNESCO, ukiwa na lengo la kuwasaidia wazazi na walezi ku

anzisha mazungumzo sahihi na yenye kujenga na watoto kuhusu afya ya uzazi, mabadiliko ya ukuaji, usalama na namna ya kujilinda dhidi ya mazingira yanayoweza kuhatarisha afya na ustawi wao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mheshimiwa Zawadi anasema Serikali ya Zanzibar imejizatiti kuhakikisha watoto wanakulia katika mazingira salama, wanasikilizwa na hawabaki nyuma, akisisitiza kuwa malezi na ulinzi wa mtoto ni jukumu la pamoja.

Anasema afya ya uzazi ni sehemu ya afya na ustawi wa mtoto, hivyo wazazi, walezi, taasisi na jamii wanapaswa kushirikiana katika kuwapatia watoto taarifa sahihi na mazingira yanayowawezesha kukua kwa usalama.


“Mtoto ni kama mbegu; ukimlea vizuri atakuwa na afya bora,” anasema.

Naibu Waziri pia anawataka wadau kuimarisha ushirikiano katika kukabiliana na changamoto zinazochangia ukatili na udhalilishaji wa watoto, akisisitiza umuhimu wa kuzuia matukio hayo kabla hayajatokea.

Anasema changamoto hizo zinahitaji ushirikiano wa karibu baina ya taasisi, jamii na wadau mbalimbali, huku akigusia pia umuhimu wa wanaume kushiriki kikamilifu katika juhudi za kuzuia na kukabiliana na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.

“Tuzuie matukio yanayosababisha udhalilishaji ili tuweze kupata taifa bora,” anasisitiza.

Kwa upande wa UNESCO, Mr Mathias Luhanya, National Project Officer, anasema mwongozo huo umefanyiwa kazi tangu mwaka 2020, na kufikia hatua ya kuzinduliwa rasmi ni matokeo ya uvumilivu, juhudi na ushirikiano wa wadau mbalimbali.

Anasema mwongozo huo unalenga kumsaidia mzazi kuelewa namna bora ya kuzungumza na mtoto kuhusu afya ya uzazi, kumsaidia kuelewa mabadiliko anayopitia na kutambua mazingira yanayoweza kuhatarisha afya na usalama wake.

Ushiriki wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania katika uzinduzi huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya UNESCO, Serikali ya Zanzibar na wadau wa kitaifa katika kuendeleza programu zinazolenga elimu, afya, ulinzi na ustawi wa watoto na vijana.

Hatua hiyo pia inaendana na juhudi za UNESCO za kuwawezesha watoto na vijana kupata maarifa na mazingira salama yanayowasaidia kulinda afya zao na kufikia uwezo wao.

Akizungumza kuhusu ushirikiano huo, Mheshimiwa Zawadi anaishukuru UNESCO kwa kushirikiana na Serikali ya Zanzibar katika kufanikisha uzinduzi wa mwongozo huo, akisisitiza kuwa mafanikio katika kumlinda mtoto yanahitaji dhamira na ushirikiano wa pamoja.

“Penye nia pana njia.”

Uzinduzi wa mwongozo huo unaweka msisitizo kwamba kumlinda mtoto ni jukumu la pamoja la mzazi, familia, jamii, Serikali, taasisi na wadau wa maendeleo, ili kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama, wanasikilizwa na wanapata fursa ya kuwa na afya bora na maisha yenye ustawi.

MAKAMU WA RAIS NDEJEMBI ATOA MAELEKEZO KUHUSU BEI YA SARUJI

September 03, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

MAKAMU wa Rais wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, ametoa maeekezo kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kukaa meza moja na wazalishaji wa saruji nchini ili kuweka mikakati ya haraka itakayohakikisha saruji inapatikana kwa wingi na bei nafuu.

MAAFISA ELIMU KATA WAPEWA JUKUMU KUKUZA UFAULU TANGA

September 03, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu, TANGA

MAAFISA Elimu Kata katika Jiji la Tanga wameanza kushirikishwa katika mafunzo ya walimu yanayotolewa kupitia mradi wa Tanga Yetu, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa mafunzo hayo na hatimaye kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Mafunzo hayo yanaendeshwa na Taasisi ya Tanzania Centre for Education  kupitia mradi wa Tanga Yetu, unaodhaminiwa na Botnar Foundation kwa kushirikiana na Inovet, ukiwa na lengo la kuchangia kuboresha elimu na kuongeza ufaulu wa wanafunzi pia yakilenga 

Pia yakilenga kuwajengea walimu uwezo wa kutumia teknolojia na rasilimali za kidijitali katika ufundishaji, huku Maafisa Elimu Kata wakipewa nafasi ya kufuatilia mafunzo hayo ili waweze kuyasimamia wanaporejea shuleni.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Centre for Education Yusuf Ogutu alisema ushiriki wa Maafisa Elimu Kata ni muhimu kwa kuwa wao ndio wanaohusika na usimamizi wa shughuli za elimu katika kata zao.

Alisema kupitia ushiriki huo, Maafisa Elimu Kata wataweza kufahamu maudhui yanayofundishwa, changamoto zinazowakabili walimu na hatua zinazoweza kuchukuliwa kuhakikisha mafunzo yanakuwa na matokeo yaliyokusudiwa.

“Ni jambo la muhimu kwa Maafisa Elimu Kata kujua kinachofanyika katika mafunzo haya ili wanaporudi shuleni waweze kusimamia na kufuatilia utekelezaji wake,” alisema.

Kwa mujibu wa mtoa maelezo huyo, mafunzo hayo pia yanawalenga kuwajengea walimu uwezo wa kutumia Digital Learning ili kurahisisha upatikanaji wa mitihani, notisi, vitabu na rasilimali mbalimbali za kujifunzia zinazopatikana kwenye mitandao.

Alisema matumizi ya teknolojia yatawasaidia walimu kupata nyenzo mbalimbali za kufundishia na kujifunzia kwa urahisi, pamoja na kuwawezesha kutumia mifumo ya E-Learning katika kuboresha ufundishaji.

Aidha, alisema Maafisa Elimu Kata watakuwa na jukumu la kufuatilia ushiriki wa walimu katika mafunzo hayo, kutambua walimu ambao hawajashiriki na kuhakikisha maudhui yaliyofundishwa yanafanyiwa kazi shuleni.

“Maafisa Elimu Kata ndio wanaosimamia shule katika kata zao. Kupitia wakuu wa shule wataweza kufuatilia ni walimu gani wamehudhuria mafunzo na ni kwa kiwango gani wanatumia maarifa waliyopata,” alisema.

Alisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha mafunzo yanayotolewa hayabaki darasani pekee, bali yanafikia wanafunzi kupitia maboresho ya ufundishaji na matumizi sahihi ya rasilimali za kidijitali.

Kwa upande mwingine, Maafisa Elimu Kata walipata fursa ya kufuatilia changamoto zinazowakabili walimu wakati wa kutumia teknolojia na nyenzo mbalimbali za kidijitali, ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi ambapo mafunzo  hayo yanaendelea kwa awamu kulingana na masomo yanayolengwa.

Jana ilikuwa siku ya mwisho ya mafunzo kwa walimu wa masomo ya Historia, Jiografia na Business Studies, huku wiki hii yakitarajiwa kuendelea kwa walimu wa masomo ya Sayansi, Fizikia, Baiolojia, Kemia na Hisabati.


NEMC YATOA TAHADHARI KUELEKEA MVUA ZA EL NIÑO

September 03, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limewataka Watanzania kuchukua tahadhari na kuimarisha utunzaji wa mazingira kuelekea mvua za El Niño, likisema utupaji holela wa taka na uharibifu wa miundombinu ya maji unaweza kuongeza hatari ya mafuriko.

JUBILEE LIFE INSURANCE YAZINDUA BIDHAA TATU MPYA ZA BIMA YA MAISHA

September 03, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KAMPUNI ya Jubilee Life Insurance Tanzania imezindua bidhaa tatu mpya za bima ya maisha zinazolenga kuwasaidia Watanzania katika uwekaji akiba, maandalizi ya elimu, ulinzi wa maisha na mahitaji mengine ya kifedha ya baadaye.

FROM LESSON NOTES TO DIGITAL LEARNING :DR.LUCIAN EQUIPS TEACHERS WITH PRACTICAL PRESENTATION SKILLS

September 03, 2026 Add Comment

 


ARUSHA — A classroom lesson does not have to remain on paper. With the right digital skills, a teacher can transform ordinary lesson notes into a clear, visual and engaging learning experience for students.

This was the focus of a practical session facilitated by Dr. Lucian Ngezei, from the University of Dodoma (UDOM) during the ongoing digital education training, where teachers were introduced to the step-by-step development of digital teaching presentations using Microsoft PowerPoint, as well as WPS Office for teachers using tablets.

Using Photosynthesis as a practical example, Dr. Lucian guided teachers in developing a complete lesson presentation, beginning with the lesson objectives, followed by the meaning of photosynthesis, illustrations, conditions necessary for photosynthesis, its applications and a summary.

Rather than filling slides with lengthy notes, teachers were encouraged to present one key idea at a time, supported by appropriate illustrations. Dr. Lucian introduced the Six-by-Six rule to help teachers make their slides simple, readable and focused.

The training was deliberately practical. Each teacher was given 10 minutes to create slides, applying the principles demonstrated. Teachers also used Mwalimu Julius Kambarage Nyerere as another example through which they practised selecting key information, organising ideas and adding relevant visual elements.

For teachers who have not yet acquired these skills, the lesson from the training is clear: digital teaching does not require a teacher to be a technology expert. It begins with the willingness to learn and the ability to use simple tools purposefully.

A teacher who masters these skills can develop digital resources for different subjects, explain difficult concepts more effectively, stimulate classroom discussion and make learning more visual and learner-centred.

More importantly, these skills support the direction of Tanzania’s new curriculum, which places greater emphasis on competence, creativity, critical thinking, practical skills and active participation in learning.

The message from the training is therefore simple: the digital transformation of education begins with a digitally empowered teacher. Every teacher can learn these skills, and every lesson can become an opportunity to use technology meaningfully to improve learning.

PBPA YAWAWEZESHA MAMA LISHE KURASINI KUHAMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

September 03, 2026 Add Comment
Dar es Salaam, Septemba 3, 2026

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mhandisi Bruno Tarimo, amewahimiza mama na baba lishe kuachana na matumizi ya kuni na mkaa wa kawaida na kuhamia katika nishati safi ya kupikia ili kulinda afya zao, kuhifadhi mazingira na kuongeza ufanisi wa biashara zao.

KAZI 294 ZIFUZU KUINGIA HATUA YA KURA SAMIA KALAMU AWARDS 2026

September 03, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Septemba 3, 2026: Kazi 294 zimefuzu kuingia hatua ya kupigiwa kura na wananchi katika msimu wa pili wa Tuzo za Samia Kalamu Awards (SKA 2026).

Kazi hizo zimechujwa kutoka katika kazi 3,003 zilizowasilishwa na waombaji 985 na kufanyiwa tathmini na jopo la majaji kwa kuzingatia ubora, ubunifu, utafiti, maadili ya taaluma, athari kwa jamii na mchango katika maendeleo ya nchi.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo, Septemba 3, 2026, Mwenyekiti wa Maandalizi ya tuzo ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mha. Peter Mwasalyanda, amewakaribisha wananchi kupiga kura kuchagua washindi kupitia tovuti https://www.samiaawards.tz/ au kutuma ujumbe mfupi wenye neno “SKA”, likifuatiwa na namba ya mshiriki kwenda namba 15200.

Zoezi la upigaji kura limeanza leo, Septemba 3, 2026, na litafungwa Septemba 30, 2026.

Naye Mwenyekiti Mwenza wa Mashindano hayo na Mkurugenzi wa TAMWA, Dkt. Rose Reuben, amesema mashindano hayo yamewaleta pamoja waandishi wa habari kutoka maeneo ya vijijini na mijini, akisisitiza kuwa washiriki watashindana kwa kuzingatia ubora wa kazi zao na si umaarufu wao.
Kwa mujibu wa mmoja wa majaji wa mashindano hayo, Bi. Beatrice Bandawe, amesema kuwa miongoni mwa maeneo yaliyopatiwa kipaumbele katika kazi zilizowasilishwa ni pamoja na afya, jinsia na makundi maalum, mazingira pamoja na elimu.

Samia Kalamu Awards ni tuzo za kitaifa zinazoratibiwa kwa ushirikiano wa TCRA, Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB).

Aidha TCRA, TAMWA, na JAB zinaendelea kuwaomba wadau kujitokeza kudhamini tuzo za SKA 2026 kwa dhumuni la kutambua, kuenzi na kuhamasisha uandishi wa habari wenye ubora, weledi na ubunifu katika kuchochea maendeleo ya nchi.