HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MRADI WA UMEME SIMIYU KUFUNGUA FURSA ZA UWEKEZAJI NA KUCHOCHEA SHUGHULI ZA KIUCHUMI WANANCHI

September 16, 2026 Add Comment






📌 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb.) aipongeza TANESCO kwa kutekeleza Mradi kwa kutumia wataalamu wa ndani

📌 MD Twange asema mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme umefikia asilimia 82 ya utekelezaji wake




Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amekagua ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Imalilo mkoani Simiyu ambapo ameeleza kukamilika kwa mradi huo kutafungua fursa za uwekezaji na kuboresha huduma ya upatikanaji wa umeme kwa wananchi.

Mhe. Mwigulu ameyasema hayo leo Septemba 14, 2026 katika eneo la mradi wa Imalilo wakati akikagua utekelezaji wake.

"Nawapongeza sana Wizara ya Nishati kwa kutekeleza mradi huu kupitia TANESCO kwa kutumia wataalamu wa ndani hongereni sana" amesema Mhe. Dkt. Mwigulu

Dkt. Mwigulu akizungumzia kuhusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Ibadakuli, Shinyanga hadi Imalilo, Simiyu, Dkt. Mwigulu amesema Serikali itatoa fedha kuhakikisha mradi huo unakamalika na kuwa na tija kwa Taifa.

Awali, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Bw. Lazaro Twange amesema mradi umetekelezwa kwa kutumia wataalamu wa ndani na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja.

"Mhe. Waziri Mkuu mradi huu umefikia asilimia 82 ya utekelezaji wake na utakamilkika katika muda ambao tumeupanga" amesema Bw. Twange. Aidha amesema gharama ya utekelezaji wa mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme umegarimu shilingi bilioni 27, ambapo mpaka sasa Serikali imetumia shilingi bilioni 15 na kazi zote za msingi zimekamilika na ujenzi unaendelea.

Mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Imalilo unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa huduma ya umeme katika mikoa ya Simiyu, Mara na maeneo jirani.


















WATAALAMU NA WATAFITI WAHIMIZWA KUAINISHA VIPAUMBELE VYA KIMKAKATI KUELEKEA MKUTANO WA COP 12

September 15, 2026 Add Comment
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

JUKWAA LA MIFUMO YA CHAKULA LAZINDULIWA DAR

September 15, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

JIJI la Dar es Salaam limezindua Jukwaa la Mifumo ya Chakula litakalokuwa chombo cha kuunganisha wadau mbalimbali katika kuboresha upatikanaji wa chakula salama, bora na chenye lishe kwa wakazi wa jiji hilo.
FCC YATAJWA CHACHU YA SOKO HURU NA USHINDANI WA HAKI

FCC YATAJWA CHACHU YA SOKO HURU NA USHINDANI WA HAKI

September 15, 2026 Add Comment

Na.Mwandishi Wetu

Tume ya Ushindani ya Somali  imefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania kwa lengo la kujifunza uzoefu na mbinu zinazotumiwa na Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika kusimamia ushindani wa kibiashara, kudhibiti bidhaa bandia na kulinda maslahi ya walaji.

Ziara hiyo imefanywa na Mkurugenzi wa Masuala ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia na Kamishna wa Mamlaka ya Ushindani ya Afrika Mashariki (EACA), Bw. Ahmed Warsame pamoja na Mkurugenzi wa Biashara na Upatikanaji wa Masoko wa Wizara ya Biashara na Viwanda ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Bw. Abdihalim Osman.

Katika ziara hiyo, ujumbe huo umekutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, pamoja na uongozi wa Tume, ambapo walipata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kukuza na kulinda ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, uongozi wa ujumbe wa Somalia umepongeza utendaji wa FCC, ukieleza kuwa uzoefu wa Tanzania katika kusimamia ushindani na kulinda mlaji ni muhimu kwa Somalia katika kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa soko na kukuza mazingira bora ya biashara.

Ujumbe huo umeeleza kuwa kujifunza kutoka FCC kutasaidia kuongeza uelewa na uwezo wa taasisi za Somalia katika kukabiliana na changamoto zinazohusu ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwadhuru walaji.

Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema  kuwa Tanzania ipo tayari kuendelea kushirikiana na taasisi za Somalia na nchi nyingine katika kubadilishana uzoefu, maarifa na mbinu bora za usimamizi wa ushindani na ulinzi wa walaji.

Ziara hiyo ya siku moja imekuwa fursa muhimu kwa Somalia kujifunza uzoefu wa Tanzania katika eneo la ushindani wa kibiashara, udhibiti wa bidhaa bandia na ulinzi wa mlaji, hatua inayotarajiwa kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi na kuchangia katika ujenzi wa masoko yenye ushindani wa haki na biashara endelevu.

WATAALAMU NA WATAFITI WAHIMIZWA KUANISHA VIPAUMBELE VYA KIMKAKATI KUELEKEA MKUTANO WA COP 12.

September 15, 2026 Add Comment
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Paul Deogratius akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Wakili Mkuu wa Serikali Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Vaileth Machary akizungumza jambo wakati wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Uchumi wa Buluu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Magdalena Ngotolainyo akizungumza na Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Afisa Takwimu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Bi. Caroline Gweso akizungumza jambo wakati wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.
Mratibu wa Mipango ya Bahari kutoka Shirika la Uhifadhi wa Maizngira Duniani (WWF) Dkt. Modesta Medard akizungumza jambo wakati wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Watendaji Waandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Sophia Kivina na Zahara Suleiman wakifuatilia kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Wataalamu na watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi wamehimizwa kubainisha vipaumbele vya kimkakati ili kuhakikisha Tanzania inanufaika vyema na Mkutano wa 12 wa Mkataba wa Nairobi unaotarajia kufanyika nchini kuanzia tarehe 6-9 Oktoba, mwaka huu.


Maafisa Waandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Bi. Salome Musangile na Bi. Vaileth Machary wakijadialiana jambo wakati wa wa kikao cha Wataalamu na Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Hayo yamesemwa Septemba 15, 2026 Mjini Zanzibar na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma wakati akifungua kikao cha wataalamu kuhusu Maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama zinazotekeleza Mkataba wa Nairobi (COP 12).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) Sheha Mjaja Juma (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar muda mfupi baada ya kufungua kikao cha Watalaamu na  Watafiti kutoka Wizara, Taasisi za Umma na sekta binafsi kuhusu maandalizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama Zinazotekeleza Mkatab awa Nairobi kuhusu Usimamizi wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi. Kikao hicho kimefanyika Septemba 15, 2026 Unguja, Zanzibar.

Mjaja amesema Mkutano wa COP 12 unafanyika katika kipindi muhimu ambapo Tanzania Bara na Zanzibar zinatekeleza ajenda za maendeleo za muda mrefdu kupitia Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.


“Dira hizi zinatambua umuhimu wa matumizi endelevu ya rasilimali za asili, ulinzi wa mazingira na kujenga uchumi unaostahimili mabadiliko ya tabianchi, hivyo ni fursa muhimu kuainisha mijadala ya kikanda na mikakati ya uchumi wa buluu” amesema Mjaja.

Kwa mujibu wa Mjaja amewataka wataalamu hao kuhakikisha changamoto kuhusiana na uchafuzi wa bahari, taka za plastiki, uharibifu wa matumbawe, uvuvi usio endelevu zinapata majibu ya pamoja na kuweza kufanyiwa kazi.

Mjaja amebainisha masuala muhimu ya wataalamu hao yanayopaswa kuzingatiwa ni mbinu za kuimarisha uchumi wa buluu endelevu, uhifadhi wa mifumo ikolojia ikiwemo mikoko, matumbawe na maeneo oevu.

Amesema afya ya bahari na ukanda wa pwani ni msingi wa afya ya jamii, usalama wa chakula, ajira, kipato na ustawi wa wananchi ambao unabeba mustakabali endelevu wa maisha na ustawi wa jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Paul Deogratius amesema malengo ya mkutano huo ni pamoja na kupokea taarifa ya utekelezaji wa Mkataba wa Nairobi na pamoja na kupokea taarifa ya mapato na matumizi ya fedha.

Dkt. Paul piua amebainisha manufaa ya Mkutano wa COP 12 ni pamoja na kuiwezesha Tanzania kuimarisha diplomasia ya mazingira katika majukwaa ya kikanda na kimataifa, kuvutia uwekezaji katika sekta za uvuvi, utalii, nishati na usafiri.

“Tanzania imeendelea kuweka mkazo katika masuala ya uhifadhi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi sambamba na matumizi endelevu ya rasilimali na kukuza uchumi wa Buluu” amesema Dkt. Deogratius.

Naye Mkuu wa Sekretarieti ya Mkataba wa Nairobi, Dkt. Jaredi Bosire ameipongeza maandalizi ya Serikali ya Tanzania kuelekea Mkutano wa COP 12 na kuzitaka Nchi wanachama kuiga mfano huo kuelekea mikutano ijayo.

Amesema mkutano wa COP 12 umeweza kuvutia idadi kubwa ya washiriki ambapo hadi kufikia sasa jumla ya washiriki 800 wameweza kujisajili katika tovuti ya Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP).

Dkt. Bosire amesema katika Mkutano huo pia umepanga kuwa na jumla ya mikutano ya pembezoni takribani 50 ikilinganisha na mikutano 40 ya aina hiyo iliyofanyika katika mkutano uliofanyika Madagascar mwaka 2024.

Mkataba wa Nairobi kuhusu Usimamizi na Uendelezaji wa Mazingira ya Bahari na Ukanda wa Pwani ya Magharibi ya Bahari ya Hindi unatekelezwa na Nchi Wanachama 10 ambazo ni Tanzania, Komoro, Kenya, Somalia, Madagascar, Mauritius, Msumbiji, Shelisheli na Ufaransa.

WAZIRI MASAUNI AITAMBUA NEMC KAMA MLEZI WA GREEN SUMMIT

September 15, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Hamad Yusuf Masauni, amelitambua na kulipongeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa nafasi yake muhimu kama Mlezi na mdau wa kitaasisi wa Tanzania Green Summit.

MAKATIBU WAKUU WAKUTANA KUPITIA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MUDA WA KATI WA PROGRAMU YA AFDP

September 15, 2026 Add Comment



Na; Mwandishi Wetu- Dar es Salaam

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi ameongoza Kikao cha Makatibu Wakuu kutoka katika  Wizara  zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), Wakuu wa Taasisi pamoja na Wakurugenzi wa Sekta, pamoja na wataalam kutoka katika sekta hizo  na Ujumbe Kutoka Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Mtaa wa Magogoni Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Septemba 2026.

Kikao hicho kimefanyika baada ya ziara maalumu ya wataalamu kutoka IFAD na AFDP kukamilisha ziara ya kutembelea maeneo yanayotekeleza Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi ya kupima matokeo utekelezaji wa program ya muda wa kati (MTR)

Pamoja na mambo mengine IFAD wamepongeza Serikali kwa Kusimamia vyema Shughuli za Programu kwa kuleta matokeo chanya kwa wananchi..Aidha  kikao hicho kimepokea wasilisho la dondoo lnayoainisha hoja za makubaliano yaliyopendekezwa kuhusiana na mwenendo wa utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP).



GASTECH 2026: GESI YA TANZANIA KUIWEKA NCHI KATIKA RAMANI YA DUNIA

GASTECH 2026: GESI YA TANZANIA KUIWEKA NCHI KATIKA RAMANI YA DUNIA

September 15, 2026 Add Comment


BANGKOK, Thailand:


Tanzania imeeleza dhamira yake ya kuchukua nafasi muhimu katika kuunda kizazi kijacho cha uzalishaji na usambazaji wa gesi asilia duniani, kwa kuendeleza rasilimali zake kwa viwango vya juu na kujenga mnyororo jumuishi wa thamani wa gesi.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, wakati akishiriki mjadala wa kimataifa wenye mada “The New Energy Powers: Who Will Shape the Next Era of Gas Supply?” katika Mkutano wa Gastech 2026 unaofanyika Bangkok, Thailand.

Mjadala huo umeangazia mabadiliko yanayoendelea katika soko la gesi duniani, changamoto za kijiografia na kisiasa, mabadiliko ya mahitaji ya nishati, kuibuka kwa vyanzo vipya vya usambazaji wa gesi pamoja na namna nchi zenye rasilimali ya gesi zinavyoweza kujipanga kuwa miongoni mwa wazalishaji na wasambazaji muhimu kuelekea kizazi kipya.

Akizungumza katika mjadala huo, Mhe. Salome amesema uzoefu wa Tanzania umeonyesha kuwa na rasilimali kubwa ya gesi pekee hakutoshi, bali thamani ya rasilimali hiyo huonekana pale inapoweza kubadilishwa kuwa nishati ya uhakika, yenye ushindani na inayochochea maendeleo ya kiuchumi.

Amesema historia ya gesi nchini Tanzania, ikiwemo ugunduzi wa gesi katika Songo Songo katika miaka ya 1970 na kuanza kwa uzalishaji wa kibiashara mwaka 2004, inatoa fundisho kwamba ugunduzi wa rasilimali pekee hauleti thamani bila uwekezaji, miundombinu, sera rafiki kwa uwekezaji, soko linalokua na dhamira ya pamoja kati ya Serikali na sekta binafsi.

Tanzania kwa sasa ina zaidi ya trilioni 57 za futi za ujazo za gesi asilia zilizogunduliwa, huku sehemu kubwa ya rasilimali hizo ikiwa katika maeneo ya bahari kuu.

Pamoja na rasilimali hizo kubwa, Tanzania imeendelea kutumia gesi ya nchi kavu na maji ya kina kifupi kama kichocheo cha maendeleo ya Taifa.

Kwa mujibu wa Mhe. Salome, Songo Songo na Mnazi Bay zimekuwa nguzo muhimu katika mfumo wa nishati wa Tanzania, zikichangia uzalishaji wa umeme na kuwezesha matumizi ya gesi katika viwanda, taasisi, kaya na sekta ya usafirishaji kupitia matumizi yanayokua ya gesi asilia iliyobanwa (CNG).

Kuunganisha Gesi na Soko la Dunia Mhe. Makamba amesema moja ya mafanikio muhimu ya Tanzania ni kuanza kuunganisha rasilimali za gesi na masoko ya Dunia, huku matumizi ya gesi yakipanuka kutoka katika uzalishaji wa umeme hadi viwanda, taasisi, kaya na sekta ya usafirishaji.

Amesema kwa sasa, matumizi ya gesi nchini katika uzalishaji wa umeme ni asilimia 69 huku asilimia 27 ikitumika viwandani, asilimia 3 katika usafirishaji na asilimia 1 katika taasisi na kaya.

Amesema mgawanyo huo unaonyesha kuwa Tanzania haitumii gesi kama rasilimali ya nishati pekee, bali pia kama kichocheo cha maendeleo ya viwanda, kuimarisha usalama wa nishati na kukuza uchumi wa Taifa.

Aidha Mhe. Salome amesisitiza kuwa matumizi ya gesi katika soko la ndani na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kuuza gesi nje ya nchi havipaswi kuonekana kama mikakati inayokinzana, bali kama sehemu ya mkakati mpana wa kukuza soko la gesi na kuongeza thamani ya rasilimali hiyo kwa Taifa.

Amesema masoko ya ndani na kikanda yanaweza kutoa manufaa ya kiuchumi kwa haraka, kujenga miundombinu na kuongeza uwezo wa ndani, wakati miradi mikubwa ya kuuza gesi katika masoko ya kimataifa inafungua fursa za uwekezaji mkubwa, teknolojia na upatikanaji wa masoko ya kimataifa.

Tanzania katika kizazi kipya cha gesi duniani

Akijibu swali la msingi la mjadala kuhusu nchi zitakazokuwa mstari wa mbele katika kizazi kipya cha usambazaji wa gesi duniani, Mhe. Makamba amesema si lazima ziwe nchi zenye rasilimali nyingi zaidi, bali zile zitakazokuwa na mikakati bora ya uwekezaji, miundombinu ya usambazaji, upatikanaji wa masoko ya kimataifa na ushirikishwaji mpana wa wananchi katika mnyororo wa thamani wa gesi.

Amesema Tanzania ina fursa ya kuwa miongoni mwa nchi hizo kutokana na ukubwa wa rasilimali zake, nafasi yake ya kimkakati katika ukanda wa Afrika Mashariki, ongezeko la mahitaji ya nishati pamoja na juhudi zinazoendelea za kuendeleza miundombinu na masoko ya gesi.

Mhe. Makamba amesema Tanzania inalenga kuhakikisha kuwa rasilimali ya gesi inatumika kuongeza usalama wa nishati nchini, kuchochea uwekezaji na viwanda, kuongeza ajira na mapato ya Taifa, huku ikiiwezesha nchi kushiriki kikamilifu katika mnyororo wa thamani wa gesi wa kikanda na kimataifa.

Amesema hatua hizo zinaifanya Tanzania kuwa na nafasi ya kutumia rasilimali zake za gesi si kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya sasa pekee, bali pia kujenga msingi wa ushindani wa Taifa katika kizazi kijacho cha soko la gesi duniani.




DKT JAKAYA KIKWETE AHANI MSIBA WA NDUGU WA MBUNGE WA ZAMANI WA NKASI

DKT JAKAYA KIKWETE AHANI MSIBA WA NDUGU WA MBUNGE WA ZAMANI WA NKASI

September 15, 2026 Add Comment




Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, amemtembelea na kumpa pole Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Nkasi, Mhe. Ally Mohamed Keissy, kufuatia msiba wa shimeji yake – dada wa mkewe uliotokea hivi karibuni.

Dkt Kikwete akioneshwa nyumba aliyowahi kushi akiwa afisa wa CCM miaka ya 1980 alipomtembelea na kumpa pole Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Nkasi, Mhe. Ally Mohamed Keissy, kufuatia msiba wa shimeji yake – dada wa mkewe uliotokea hivi karibuni.

NCAA YAWAPIGA MSASA MALAIGWANAN

September 15, 2026 Add Comment

 

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa Malaigwanani ,wazee na kina mama maarufu wapatao 33 kutoka kata 11 za ndani ya eneo la hifadhi Ngorongoro ili kuwajengea uwezo wa kutambua fursa mpya za kiuchumi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Kamishina Msaidizi Mwandamizi anayeshughulikia huduma za jamii bi Gloria Bideberi amesema lengo la semina hiyo ni kuhakikisha Malaigwanani na wazee hao wanapata elimu ya kutosha kuhusu ujasiriamali na namna ya kutumia fursa zinazopatikana katika maeneo yao.

Bi. Gloria alieleza kwamba elimu hiyo itakwenda sambamba na ziara za kujifunza kwa vitendo, ambapo washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ikiwemo kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za maziwa Tanga Fresh kilichopo Mkoani Tanga ili kujifunza namna bidhaa zinavyozalishwa, kuendelezwa na kufikishwa katika masoko.

“Lengo la mafunzo haya ni kuhakikisha kuwa wananchi hawa wanapata elimu ya kutosha na kuwawezesha kutembelea maeneo mbalimbali ya uzalishaji wa bidhaa ili kujifunza kwa vitendo zaidi,” alisema Gloria

Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kuimarisha ushiriki wa jamii katika maendeleo endelevu ya eneo la Hifadhi Ngorongoro.