HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
KAPINGA ABAINISHA KUUZA MAZAO GHAFI NI HASARA
habariWAZIRI KAPINGA AAGIZA MIRADI YOTE YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI
habariKAPINGA: ZAMA ZAKUFUNGIA BIASHARA ZIMEPITWA NA WAKATI.
habariZOEZI LA UVUTAJI NYAYA AWAMU YA PILI ENEO LA KIKOMBO NA MKONZE KATIKA MRADI WA CHALINZE-DODOMA KUANZA KESHO
habari📌TANESCO yasema baadhi ya Mikoa ya Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kusini Magharibi na Kanda ya ziwa kupata umeme kwa ratiba maalumu
📌Lengo ni kumpisha Mkandarasi kuendelea na utekelezaji wa Mradi huo wa kusafirisha umeme Msongo wa Kilovolti 400 ambao uko mbioni kukamilika.
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewakumbusha wananchi kuwa, kuanzia Agosti 11 hadi 17, 2026, mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 Chalinze–Dodoma ataendelea na zoezi la uvutaji wa nyaya kwa awamu ya pili katika eneo la Kikombo na Mkonze, Dodoma, katika mradi huo ambao uko mbioni kukamilika.
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Bi. Irene Gowelle, amesema hatua hiyo imekuja baada ya awamu ya kwanza ya uvutaji wa nyaya kutoka Chalinze hadi Mkambarani, Morogoro, kufanyika kwa mafanikio makubwa.
Amesema kutokana na kazi hiyo, baadhi ya mikoa itapata umeme kwa ratiba maalumu. Mikoa hiyo ni ile inayopatikana katika Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kusini Magharibi na Kanda ya Ziwa. Aidha, amesisitiza kuwa mikoa ambayo haitaathirika katika kanda hizo ni pamoja na Morogoro na Tanga.
Ameongeza kuwa mikoa inayotoka katika Kanda hizo zitakosa umeme kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni. Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kukamilisha mradi huo, ambao unatarajiwa kuwa na mchango chanya katika kuimarisha mfumo wa usafirishaji na upatikanaji wa umeme nchini.
‘’Hii ni awamu ya pili ya zoezi la uvutaji wa nyaya katika eneo la Kikombo na Mkonze Mkoani Dodoma, niwaondoe hofu wananchi kwamba tutaendelea kutoa ratiba za upatikanaji wa umeme kupitia mitandao yake ya kijamii, ili kuwawezesha wananchi kupanga shughuli zao kulingana na ratiba hiyo’’alisisitiza Bi. Gowelle.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma unatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026. Kukamilika kwake kutaongeza uwezo wa mfumo wa usafirishaji wa umeme nchini na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme yenye ubora na uhakika kwa wananchi.
NDEJEMBI AWASHA UMEME MWANUBI, ASEMA UMEME NI HITAJI LA MSINGI KWA WATANZANIA
Nishati
📌 Ahimiza wananchi kuunganishiwa huduma ya umeme na kuitumia kuongeza tija
📌 Shule, zahanati na maeneo mengine ya huduma za kijamii kupewa kipaumbele
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewasha umeme katika Kitongoji cha Mwanubi mkoani Shinyanga na kusema kuwa huduma ya umeme ni hitaji la msingi kwa Watanzania na nyenzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Akizungumza wakati wa hafla ya kuwasha umeme katika kitongoji hicho, Mhe. Ndejembi amesema kufikishwa kwa umeme vijijini kunapaswa kwenda sambamba na matumizi yenye tija, ikiwemo kuongeza thamani ya mazao, kuendeleza biashara na shughuli za uzalishaji pamoja na kuboresha utoaji wa huduma za kijamii.
Amesema Serikali inaendelea kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma ya umeme, hususan katika maeneo ya vijijini, ili nishati hiyo iwe kichocheo cha uzalishaji, ongezeko la kipato na uboreshaji wa maisha ya wananchi.
Mhe. Ndejembi amewahimiza wananchi ambao miundombinu ya umeme imewafikia kuchangamkia fursa hiyo kwa kuunganishiwa huduma kwa gharama nafuu ya shilingi 27,000, na kutumia umeme katika shughuli mbalimbali za uzalishaji na kujiletea maendeleo.
Aidha, ameiagiza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kufanya tathmini ya maeneo ambayo bado hayajafikiwa na miundombinu ya umeme ili yaingizwe katika mipango ya utekelezaji na kufikishiwa huduma hiyo.
Pia, amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme kuongeza kasi ya kusimika nguzo na kujenga miundombinu katika maeneo yaliyosalia ili wananchi wengi zaidi waweze kufikiwa na kuunganishiwa huduma ya umeme.
Amesisitiza kuwa shule, zahanati na maeneo mengine muhimu ya kutolea huduma za kijamii yanapaswa kupewa kipaumbele katika kufikishiwa umeme ili kuongeza ufanisi na kuboresha huduma zinazotolewa kwa wananchi.
Aidha Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wanapata nishati ya uhakika.
Ameeleza kuwa uwekezaji huo unalenga kuwezesha wananchi kutumia umeme katika shughuli za uzalishaji, kuongeza thamani ya mazao, kukuza biashara, kuongeza fursa za ajira na kuboresha huduma za kijamii.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita ameishukuru Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha huduma ya umeme katika vijiji vyote vya Mkoa wa Shinyanga, akieleza kuwa hatua hiyo imefungua fursa mbalimbali za maendeleo kwa wananchi.
Amesema upatikanaji wa umeme katika maeneo ya vijijini umeendelea kubadilisha maisha ya wananchi kwa kuchochea shughuli za kiuchumi, kuongeza fursa za uzalishaji na ajira pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.
Naye, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Herini Mhina, amesema Wakala unaendelea kutekeleza miradi ya kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji mbalimbali nchini ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi, hususan katika maeneo ya vijijini, wanapata huduma hiyo.
Mha. Mhina amesema REA itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi hiyo ili kupanua wigo wa upatikanaji wa umeme na kuwawezesha wananchi kutumia nishati hiyo katika shughuli za kiuchumi, uzalishaji na utoaji wa huduma za kijamii.
Nao wananchi wa Kitongoji cha Mwanubi wameishukuru Serikali kwa kuwafikishia huduma ya umeme katika kitongoji chao, wakieleza kuwa hatua hiyo itachochea shughuli za kiuchumi na kijamii na kuboresha maisha yao.
Wamesema ujio wa umeme utafungua fursa mpya za biashara na uzalishaji, kuongeza thamani ya mazao pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu katika eneo hilo.
Hafla ya kuwasha umeme katika Kitongoji cha Mwanubi ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia REA za kupanua wigo wa upatikanaji wa umeme vitongojini na kuhakikisha nishati hiyo inakuwa kichocheo cha maendeleo endelevu ya wananchi.
WANDONDI, WANDWEWE WATOA WITO WA KULINDA MAISHA NA AMANI
habari
SERIKALI YAMTAKA MKANDARASI KUONGEZA KASI UJENZI WA BARABARA YA KAHAMA-KAKOLA UNAOWEZESHWA NA MIGODI YA BARRICK NCHINI
habariMAHAKAMA YA RUFAA YAIPA USHINDI IPTL, PAP KATIKA USD 168M MGOGORO DHIDI YA STANDARD CHARTERED
habari
SERIKALI KUJA NA MRADI MAALUMU WA KUSAMBAZA UMEME KWENYE MAENEO YA UZALISHAJI
KAHAMA, SHINYANGA
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, Serikali inaandaa mradi maalumu wa kusambaza umeme katika maeneo ya uzalishaji, hususan maeneo yenye shughuli za uchimbaji wa madini, kwa lengo la kuwawezesha wazalishaji kutumia nishati ya uhakika na kupunguza utegemezi wa dizeli.
Mhe. Ndejembi ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Msalala, Mhe. Mabula Magangila, aliyeomba Serikali kupeleka umeme katika maeneo ya uzalishaji, akieleza kuwa baadhi ya wachimbaji madini katika jimbo hilo bado wanatumia dizeli kuendesha shughuli zao za uzalishaji.
Mbunge huyo pia ameieleza Serikali kuwa vitongoji 98 katika Jimbo la Msalala bado havijaunganishwa na huduma ya umeme.
Akijibu hoja hiyo, Mhe. Ndejembi amesema Serikali tayari imeanza maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo maalumu kwa kushirikiana na Wizara ya Madini, ambao utalenga kusogeza huduma ya umeme moja kwa moja kwenye maeneo yenye shughuli za uzalishaji, hususan maeneo ya migodi.
Amesema hatua hiyo inalenga kuongeza tija katika uzalishaji, kupunguza gharama zinazotokana na matumizi ya dizeli pamoja na kuwawezesha wachimbaji na wazalishaji kutumia nishati ya umeme iliyo nafuu, ya uhakika na endelevu.
Kuhusu upatikanaji wa umeme vijijini katika Jimbo la Msalala, Mhe. Ndejembi amesema vijiji vyote tayari vimefikiwa na huduma ya umeme, huku Serikali ikiendelea na jitihada za kuwafikishia huduma hiyo wananchi waliopo katika vitongoji ambavyo bado havijaunganishwa, ikiwemo vitongoji 98 vilivyotajwa.
Aidha, akizungumzia upatikanaji wa umeme katika Jimbo la Kahama Mjini, Mhe. Ndejembi amesema tayari amefanya mazungumzo na Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. Benjamini Ngaiwa, kwa lengo la kubainisha maeneo yaliyopo ndani ya Manispaa ya Kahama ambayo, licha ya kuwa ndani ya eneo la mjini, yana sifa na taswira za maeneo ya vijijini.
Amesema maeneo hayo yataangaliwa ili yaweze kunufaika na utaratibu wa Serikali wa kuunganishiwa umeme kwa gharama ya Shilingi 27,000 kwa mteja, kama ilivyoelekezwa.
Mhe. Ndejembi amesema Serikali itaendelea kuweka kipaumbele katika upanuzi wa miundombinu ya umeme na kuhakikisha nishati inafika katika maeneo yenye shughuli za kiuchumi na uzalishaji, ili kuongeza tija, kuchochea uwekezaji na kuboresha maisha ya wananchi.

NDEJEMBI: BILIONI 6.7 KWA AFYA YA WANANCHI, JENGO LA MAMA NA MTOTO LIKAMILISHWE KWA WAKATI
habariMhe. Ndejembi ametoa agizo hilo leo Agosti 9, 2026, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo na kubaini kuwa, licha ya taarifa kuonesha mradi umefikia asilimia 80, hali halisi ya utekelezaji hairidhishi na haioneshi kiwango hicho cha maendeleo.
Amesema Serikali imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya, hivyo fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo zinapaswa kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa na kuleta matokeo chanya kwa wananchi.
Ameitaka Manispaa ya Kahama kukaa pamoja na mkandarasi na kupitia changamoto zote zinazokwamisha utekelezaji wa mradi huo, ili zipatiwe ufumbuzi wa haraka na ujenzi uendelee kwa kasi inayostahili.
“Fedha hizi Shilingi bilioni 6.7 si fedha kwa ajili ya Halmashauri kuzichukua na kukaa nazo, ni fedha kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa Kahama kwa huduma bora za afya. Tunatamani kuona fedha hizi zinaongeza thamani kwa wananchi wa Kahama, hivyo mhakikishe mnasimamia jengo hili likamilike kwa wakati,” amesema Mhe. Ndejembi.
Aidha, Mhe. Ndejembi amewapongeza viongozi wa Manispaa ya Kahama kwa hatua wanazochukua katika kutenga na kuelekeza rasilimali katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayolenga kuboresha huduma za afya kwa wananchi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutenga Shilingi bilioni 5.6 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD) pamoja na Jengo la Vipimo katika Hospitali hiyo.
Mhe. Mhita amesema uwekezaji huo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kuboresha miundombinu na huduma za afya nchini, akieleza kuwa Rais anatambuliwa kwa msisitizo mkubwa anaouweka katika kuboresha afya ya mama na mtoto.
Amesema fedha hizo zimekuwa chachu kwa Mkoa na Halmashauri kuongeza juhudi na kutenga fedha kutoka katika mapato ya ndani kwa ajili ya kuendelea kuboresha huduma za afya, huku akimhakikishia Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga kuwa Mkoa utaendelea kuusimamia kwa karibu mradi huo hadi utakapokamilika.
Aidha, Mhe. Mhita amemshukuru Mhe. Ndejembi kwa kuendelea kuuwezesha Mkoa wa Shinyanga katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati, hususan katika sekta ya nishati, ikiwemo mradi wa umeme unaoendelea katika Wilaya ya Kishapu.




Global Education Link yawafunda wanaokwenda kusoma India
habari
NM-AIST KINARA WA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA KASKAZINI 2026
habari
Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imeibuka kinara miongoni mwa Taasisi za Elimu katika Maonesho ya 33 ya Kilimo, Mifugo na Sherehe za Nanenane Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika katika Viwanja vya Themi Njiro, Arusha.
Akizungumzia ushindi huo, Prof. Maulilio Kipanyula, Makamu Mkuu wa NM-AIST, amesema bidhaa bora zinahitaji utafiti na NM-AIST kama Taasisi inayotanguliza ubunifu, imeendelea kubadilisha matokeo ya tafiti kuwa teknolojia zinazotoa suluhisho kwa changamoto za wakulima na wafugaji.
Amesema teknolojia mbalimbali zinazooneshwa na Taasisi, ikiwemo Mfumo wa Ng’ombe Smart, zinalenga kuongeza tija katika ufugaji wa ng’ombe wa maziwa kwa kuwezesha ufuatiliaji wa uzalishaji wa maziwa na taarifa muhimu za mifugo.
Aidha, Prof Kipanyula amesema mwaka huu NM-AIST imekuja na teknolojia zinazolenga kuongeza thamani ya mazao, yakiwemo tumbaku, mazao ya chakula pamoja na vyakula vya mifugo kama kuku na ng’ombe.
Prof. Kipanyula amesisitiza kuwa NM-AIST inaendelea kujipanga kuwa kinara katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hususan katika maeneo ya utafiti na maendeleo, sayansi, teknolojia na ubunifu, pamoja na mabadiliko ya kidijitali.
“Ushindi huu ni chachu ya kuendelea kufanya vizuri zaidi. Mwaka ujao tutakuja na teknolojia mpya kabisa. Mwaka huu tumefanikiwa kuzalisha takribani patent 40, jambo tunalojivunia na linalotupa nguvu ya kuendelea kuzalisha teknolojia na bunifu zenye tija kwa sekta ya kilimo na mifugo.”


RC MAKALLA AIPONGEZA NM-AIST KWA UBUNIFU NA TAFITI ZINAZOCHOCHEA MAPINDUZI KATIKA KILIMO NA MIFUGO
habari
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makalla, ameipongeza Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) kwa tafiti na bunifu mbalimbali zinazolenga kuongeza tija katika sekta za kilimo na mifugo.
Mhe. Makalla amesema kuwa ametembelea banda la NM-AIST na kujionea teknolojia mbalimbali za kilimo na mifugo, pamoja na bunifu zinazolenga kuongeza thamani ya mazao na bidhaa za mifugo.
Amesisitiza kuwa mapinduzi ya kweli hayawezi kufanyika bila utafiti, teknolojia na ubunifu, akieleza kuwa NM-AIST imekuwa ikifanya vizuri katika kuibua na kuendeleza teknolojia zinazolenga kutatua changamoto za jamii.
“Kilimo bila utafiti, teknolojia na dhana za kisasa hakiwezi kuleta mabadiliko makubwa. Taasisi za utafiti zinatuelekeza na kutupeleka kwenye kilimo na ufugaji wenye tija,” amesema Mhe. Makalla.
Aidha, Mhe. Makalla amesema maendeleo ya sekta za kilimo, mifugo na uvuvi hayapaswi kupimwa kwa kuongezeka kwa uzalishaji pekee, bali pia kwa uwezo wa kuzalisha kwa tija, ubora na kuzingatia mahitaji ya soko, kama inavyosisitizwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Ameeleza kuwa Dira hiyo inalenga kujenga uchumi shindani unaoongozwa na maarifa, teknolojia, ubunifu na uongezaji wa thamani, hivyo taasisi za utafiti kama NM-AIST zina nafasi muhimu katika kufanikisha azma hiyo.
Mhe. Makalla ameyasema hayo wakati akihitimisha Maonesho ya 32 ya Kilimo, Mifugo na Sherehe za Nanenane Kanda ya Kaskazini, yaliyofanyika katika Viwanja vya Themi Njiro, Arusha.


BARAZA LA USHINDANI LAJA NA MFUMO WA KIDIJITALI KURAHISISHA RUFAA ZA WANANCHI
habari

TBS YAWAFUNGULIA WAJASIRIAMALI NJIA YA MASOKO KUPITIA UBORA WA BIDHAA
habari
WAZIRI NDEJEMBI AMTAKA MKANDARASI KUONGEZA KASI UJENZI WA BARABARA YA KAHAMA- BULYANHULU JCT-KAKOLA
Nishati
KAHAMA, SHINYANGA
Waziri wa Nishati na Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, Mhe. Deogratius Ndejembi, amemtaka Mkandarasi wa Barabara ya Kahama–Bulyanhulu Jct–Kakola, M/s China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC), kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo ili ukamilike kwa wakati na kuwawezesha wananchi kuanza kunufaika na miundombinu hiyo.
Mhe. Ndejembi ametoa agizo hilo leo, Agosti 9, 2026, mkoani Shinyanga, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 73 inayojengwa kwa kiwango cha lami.

Amesema hadi sasa kilomita 32 kati ya 73 zimekamilishwa kwa kuwekwa lami, huku kazi nyingine za ujenzi zikiendelea katika maeneo mbalimbali ya mradi.
SERIKALI YATENGA BILIONI 38 KUPIMA VIJIJI VYOTE TANZANIA, YAAGIZA KLINIKI ZA ARDHI KILA KATA
habariSerikali imetangaza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameridhia utoaji wa kiasi cha shilingi bilioni 38 kwa ajili ya kufanikisha mpango wa kupima vijiji vyote nchini ili kumaliza migogoro ya ardhi.
Hayo yameelezwa leo Julai 1, 2026 katika viwanja vya Sokoni Mugumu Wilaya ya Serengeti mkoani Mara na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya alipokuwa akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, ambaye yuko katika ziara ya kikazi ya siku tano mkoani humo.
Katika hatua ya haraka ya kusogeza huduma kwa wananchi, Mhe. Mmuya amemuagiza Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Mara pamoja na timu yake, kuhakikisha wanaratibu na kuanzisha kliniki za ardhi katika kila kata.
"Hakikisheni mnaratibu uwepo wa kliniki za ardhi katika kila kata ili muwasikilize wananchi hawa na msione kila changamoto mpewazo ni ya mazoea. Hapana, amekuja kwako kwa sababu ana jambo la kusikilizwa na litatuliwe," alisema Naibu Waziri Mmuya.
Mhe. Mmuya alieleza kuwa wizara ya Ardhi iliwasilisha mpango na maombi ya fedha bungeni kufuatia maelekezo ya awali ya Waziri Mkuu, na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akaidhinisha shilingi bilioni 38 kwa ajili ya kupima jumla ya vijiji 12,333 vya Tanzania.
"Mpaka hivi ninavyoongea, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kipindi chake kifupi tu ameweza kupima vijiji 4,873. Na ametupatia maelekezo kuwa ndani ya kipindi chake, vijiji vyote vilivyobakia tuvipime." Aliongeza Naibu Waziri Kaspar Mmuya
Katika hatua nyingine Mhe. Mmuya amesema Wizara ya Ardhi itashirikiana bega kwa bega na Ofisi ya Rais - TAMISEMI ili kuhakikisha maagizo hayo yanatekelezwa kikamilifu katika vijiji vyote vilivyosalia nchini.
Aidha, Mhe. Mmuya alieleza kuwa Wilaya ya Serengeti ina kata 30 na vijiji 78. Ameuhakikishia uongozi wa wilaya hiyo kuwa vijiji vyote 78 vimeshaingizwa kwenye mpango wa upimaji ndani ya kipindi cha miaka mitano ya Rais Samia Suluhu Hassan.
"Kupima vijiji hivi ndiyo dawa kubwa ya kutatua changamoto ya mipaka kati ya kijiji na kijiji. Lakini ni dawa kubwa ya kutatua changamoto ya kugombania matumizi ya ardhi ya mtu mmoja mmoja, taasisi na taasisi, au serikali na wananchi," alisema Naibu Waziri Kaspar Mmuya.
WAZIRI NDEJEMBI AANZA ZIARA MAALUM MKOANI SHINYANGA
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi (Mb.), amewasili mkoani Shinyanga kwa ziara maalum ya kikazi ya kukagua utekelezaji na kuzindua miradi ya maendeleo, pamoja na kuzungumza na wananchi katika wilaya za Mkoa wa Shinyanga.
Waziri Ndejembi, ambaye ni Mlezi wa Mkoa wa Shinyanga Kiserikali, mara baada ya kuwasili amefika katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Mboni Mhita, tarehe 09 Agosti 2026.
Waziri Ndejembi akiwa mkoani hapo, atakagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Kahama – Kakola, mradi wa ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama, kukagua ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Shinyanga, pamoja na kuwasha umeme wa REA katika Kitongoji cha Mwanubi, Kolandoto.
AJIRA ZAIDI YA 420 ZAZALISHWA KUPITIA UJENZI WA KITUO CHA EACOP PS4 MBOGWE
NishatiMBOGWE,
Zaidi ya wananchi 420 wamepata ajira zisizo za ujuzi kupitia utekelezaji wa ujenzi wa Kituo cha Kuongeza Msukumo wa Mafuta (PS4) cha Mbogwe, kinachotekelezwa chini ya Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).
Hayo yameelezwa Agosti 8, 2026 na Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Bw. Derick Moshi, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho kilichopo Wilaya ya Mbogwe, mkoani Geita.
Bw. Moshi amesema utekelezaji wa mradi huo umeendelea kutoa manufaa kwa Watanzania, ambapo takribani asilimia 80 ya fursa zinazotokana na mradi zimenufaisha Watanzania, ikiwemo ajira, mafunzo na ushiriki wa wazawa katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali.
Amesema zaidi ya ajira hizo, mradi umetoa mafunzo kwa wananchi kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), hatua iliyowawezesha kupata ujuzi na uzoefu unaohitajika katika kushiriki kwenye miradi mikubwa ya kimkakati.
“Mradi huu umeendelea kuwa fursa kwa Watanzania, siyo tu kupitia ajira, bali pia kupitia mafunzo yanayowawezesha vijana kupata ujuzi na uzoefu wa kushiriki katika miradi mikubwa ya kimkakati,” amesema Bw. Moshi.
Aidha, Bw. Moshi ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa ujenzi wa PS4, ambao umefikia asilimia 88 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 2026.
Amesema utekelezaji wa mradi huo umezingatia pia ushirikishwaji wa jamii inayozunguka mradi kupitia ajira, utekelezaji wa miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) pamoja na maboresho ya miundombinu, ikiwemo barabara na huduma za maji.
Ameeleza kuwa vituo vya kuongeza msukumo wa mafuta vya Muleba (PS3) na Mbogwe (PS4) ni sehemu muhimu ya miundombinu ya EACOP, kwa kuwa vina jukumu la kupokea na kuongeza msukumo wa mafuta ili yaweze kusafirishwa kwa ufanisi kupitia bomba hilo kuelekea kituo cha mwisho cha Kiteto.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Huduma wa EACOP ambaye pia ni Kaimu Meneja wa EACOP Tanzania, Bw. Geofrey Mponda, amesema vituo vya kuongeza msukumo wa mafuta ni miundombinu muhimu katika kuhakikisha usafirishaji wa mafuta kupitia EACOP unafanyika kwa ufanisi na kwa kuzingatia viwango vinavyotakiwa.
Amesema utekelezaji wa Mradi wa EACOP umeendelea kuwa chachu ya fursa kwa Watanzania, hususan vijana, kwa kuwa umetoa ajira kwa wenye ujuzi na wasio na ujuzi, huku ukiwawezesha pia kupata uzoefu wa vitendo katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.
“EACOP imeendelea kuwa chachu ya fursa kwa Watanzania. Vijana wamepata ajira na wengine wamepata fursa ya kujifunza na kujenga uzoefu ambao utawasaidia kushiriki katika miradi mingine mikubwa ya kimkakati,” amesema Mponda.
Naye Mwakilishi wa Kampuni ya EACOP katika eneo la mradi (EACOP Company Site Representative), Bw. Kamal Maalouli, amesema PS4 ni miongoni mwa vituo vikubwa na muhimu katika utekelezaji wa Mradi wa EACOP.
Amesema kampuni imeendelea kuweka juhudi zote kuhakikisha ujenzi wa kituo hicho unakamilika kwa wakati uliopangwa na kukidhi viwango vinavyohitajika ili kiweze kutekeleza jukumu lake katika mfumo wa usafirishaji wa mafuta kupitia EACOP.
Mradi wa EACOP unahusisha ujenzi wa bomba lenye urefu wa takribani kilomita 1,443 kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani, Tanga nchini Tanzania, ambapo sehemu kubwa ya bomba hilo inapita nchini Tanzania.































