HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

FCC KUSHIRIKIANA NA WADAU KUPIGA VITA BIDHAA BANDIA

FCC KUSHIRIKIANA NA WADAU KUPIGA VITA BIDHAA BANDIA

September 02, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu

KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amewataka wadau wa sekta ya umma na binafsi kuongeza ushirikiano katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia, akisema biashara hiyo inahatarisha uwekezaji, ushindani wa haki na usalama wa watumiaji.

Ngasongwa ameyasema hayo leo Septemba 2, 2026 Jijini Dar es Salaam wakati akimwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, katika Kongamano la Ulinzi dhidi ya Bidhaa Bandia na Uwekezaji lililoandaliwa na Kampuni ya NANOSILIKAN kwa kushirikiana na FCC, TISEZA, TCCIA na TPSF, katika Hoteli ya Johari Rotana.

Amesema bidhaa bandia haziathiri ushindani wa kibiashara pekee, bali pia zinawaumiza wazalishaji wanaofuata sheria ambao hulipa gharama za ubunifu, upimaji, viwango, usajili, ajira na kodi, wakati wazalishaji wa bidhaa bandia huepuka gharama hizo na hivyo kushindana kwa njia isiyo ya haki.

“Katika ushindani wa kawaida, mzalishaji bora au mwenye ufanisi zaidi ndiye anayeshinda. Lakini kwenye bidhaa bandia, anayeshinda ni yule anayekwepa gharama zinazofanya bidhaa iwe halali,” amesema

Ngasongwa amesema athari kubwa zaidi ya bidhaa bandia humwangukia mlaji, akitolea mfano mbegu bandia ambazo mkulima anaweza kugundua tatizo baada ya msimu kupita, dawa ambazo hazitibu ugonjwa uliokusudiwa na vipuri bandia vya magari ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama wa watumiaji. Alisema kwa kuwa madhara hayo yanaweza kujitokeza kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa, ni muhimu kuweka mifumo ya kuzuia bidhaa bandia kufika kwa mlaji.

Kwa mujibu wa Ngasongwa, utekelezaji wa sheria pekee hauwezi kumaliza tatizo hilo kwa kuwa maafisa wa ukaguzi hawawezi kuwepo katika kila duka na kila muamala nchini, hivyo ni muhimu kuwawezesha walaji kushiriki katika kuthibitisha uhalali wa bidhaa kabla ya kufanya manunuzi. Alisema njia hiyo inaweza kusaidia kuzuia madhara kabla hayajatokea, huku akisisitiza kuwa jukumu la Serikali la kusimamia sheria na kulinda walaji linaendelea.

Aidha, aliwataka wafanyabiashara na wazalishaji kutoa taarifa kwa FCC wanapobaini bidhaa zao zikighushiwa, kusajili na kutunza kumbukumbu za alama za biashara zao pamoja na kushirikiana katika kutoa taarifa kuhusu wahusika wa biashara ya bidhaa bandia.

Kongamano hilo limewakutanisha wawakilishi wa Serikali, taasisi za udhibiti, sekta binafsi, wafanyabiashara, taasisi zinazohusika na haki miliki pamoja na wadau wa maendeleo, kwa lengo la kujadili namna bora ya kulinda uwekezaji, wafanyabiashara na walaji dhidi ya athari za bidhaa bandia nchini.

MAVUNDE AZINDUA PROGRAMU YA MBT NYAMONGO, VIJANA NA WANAWAKE KUNUFAIKA

September 02, 2026 Add Comment

 

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akizindua Programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT) katika eneo la Nyamongo, mkoani Mara, inayolenga kupanua fursa za maeneo ya uchimbaji, taarifa za kijiolojia na leseni kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Helikopta ikifanya utafiti wa madini kwa njia ya anga katika eneo la Nyamongo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya MBT, hatua itakayosaidia kupata taarifa za kijiolojia kwa ajili ya utafiti wa kina na uchorongaji katika maeneo yaliyotengwa kwa wachimbaji wadogo.

JAB YAKAZA SHERIA NA MAADILI KATIKA UTANGAZAJI WA MAUDHUI

Kajunason September 02, 2026 Add Comment

  

Na Mwandishi Wetu.

 Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imekutana na kufanya mazungumzo na watangazaji na waandaaji wa kipindi cha Good Morning kinachorushwa na Wasafi FM, ambapo imewakumbusha umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya uandishi wa habari katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Kikao hicho kimefanyika leo, Septemba 2, 2026, katika Makao Makuu ya JAB, Mtaa wa Jamhuri, jijini Dar es Salaam, kikilenga kuimarisha uelewa wa watangazaji hao kuhusu misingi ya weledi, uwajibikaji na matumizi sahihi ya majukwaa ya habari.

Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amefafanua matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229; Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Sura ya 306; pamoja na kanuni zake zinazopaswa kuzingatiwa katika utayarishaji na utangazaji wa maudhui.

Wakili Kipangula ameeleza kuwa kuzingatia sheria na maadili ni msingi wa kulinda heshima ya taaluma, haki za watu wanaohusika katika maudhui na imani ya jamii kwa Waandishi wa Habari.
Baada ya mazungumzo hayo, watangazaji wakongwe Gelard Hando na Hilary Mtuta, maarufu kama Zembwela, walikabidhiwa vitambulisho vyao vya ithibati ya uandishi wa habari baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.

Makabidhiano hayo yamekamilisha hatua ya kuwatambulisha rasmi kama Waandishi wa Habari wenye ithibati, wenye wajibu wa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, maadili na uwajibikaji.

WMA YAIMARISHA UWAJIBIKAJI NA WELEDI WA WATUMISHI GEITA

September 02, 2026 Add Comment


Na. WMA – Geita

2 Septemba, 2026

📍 “Vipimo Sahihi, Huduma Bora, Haki kwa Wote”

Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Christopher Mwakibinga, amefanya kikao kazi na watumishi wa WMA Mkoa wa Geita, akisisitiza umuhimu wa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu, pamoja na kuongeza uwajibikaji na weledi katika utekelezaji wa majukumu.

RAIS DKT. SAMIA AWAAPISHA WAKUU WA MIKOA NA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA IKULU

September 02, 2026 Add Comment


Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha Ndugu Richard Marcellino Kayombo kuwa Katibu Tawala, Mkoa wa Pwani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha CP Salum Rashid Hamduni kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha Mhe.
Stanslaus Haroon Nyongo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha Mhe.Alexander Pastory Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Viongozi wakila kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02
Septemba, 2026.

Viongozi pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya Uapisho wa Wakuu wa mikoa ya Mbeya, Geita, Pwani, Mwanza pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani katika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akizungumza na Viongozi baada ya kuwaapisha Wakuu wa mikoa ya Mbeya, Geita, Pwani, Mwanza pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani katika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kwenye picha na Wakuu wa Mikoa baada ya hafla ya Uapisho wa Viongozi mbalimbali iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.