HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
BARRICK BULYANHULU YAKABIDHI JENERETA KUBWA LA KISASA KITUO CHA AFYA BUGARAMA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI
HABARICCM YATOA ONYO KWA WATAKAOTAFUNA FEDHA ZA SOKO PANGANI.
HABARIMWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM) Mkoa wa Tanga,Rajabu Abdallah, ametoa Sh milioni 100 kwa ajili
ya ujenzi wa Soko Kuu la Mikinguni, Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga huku akiwaonya
watakaokula pesa hizo.
Kauli hiyo imetolewa na Mweyekiti
huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM wakati wa kukabidhi mfano wa hundi
ya thamani hiyo na kusema kuwa hatomvumilia mtendaji yoyote atakaebainika
kutumia vibaya fedha hizo tofauti na
zilivyotarajiwa.
Aidha alisema kumekuwa na mazoea ya baadhi ya watumishi kutumia vibaya pesa za miradi ya kimaendeleo jambo ambalo linakwamisha maendeleo na kudumaza huduma za kijamii kwa wananchi na kuongeza migogoro baina ya chama na Serikali kwa ujumla.
Fedha hizo ni sehemu ya Sh milioni 300
zinazokadiriwa kugharimu ujenzi wa soko hilo, ambalo linatarajiwa kuanza
kujengwa katika mwaka wa fedha 2026/2027.
Soko hilo linatarajiwa kuwa miongoni
mwa miradi itakayochochea shughuli za kiuchumi kwa wananchi na wafanyabiashara
wa Kata ya Mikinguni, huku likitarajiwa kutumia fursa zitakazotokana na ujenzi
wa Barabara ya Tanga–Bagamoyo.
Akizungumza na wananchi wa Kata ya Mikinguni, Kijiji cha Stahabu, mara baada ya kukabidhi hundi hiyo, Abdallah aliagiza Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kusimamia kwa karibu ujenzi wa soko hilo ili kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.
Alisema kukamilika kwa mradi huo
kutasaidia kuboresha mazingira ya biashara na kuongeza fursa kwa wananchi wa
eneo hilo.
“Kazi ya Chama ni kusimamia
Serikali kuhakikisha inatekeleza iliyoyaahidi kwenye Ilani yake. Watendaji
hampaswi kukaa maofisini, tunataka mkatatue kero za wananchi. Mtaalamu yeyote
anayeona Chama kinamfuatilia ajue kabisa Tanga haimfai,” alisema.
AWESO
APIGA STOP MICHANGO MITIHANI
Katika hatua nyingine, Mbunge wa
Pangani na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amekabidhi mashine ya kuchapisha
mitihani kwa Shule ya Sekondari ya Mikinguni, ambayo imepewa jina lake.
Aweso alisema amefanya hivyo baada
ya kupata taarifa kwamba wanafunzi wa shule hiyo wamekuwa wakichangishwa fedha
kila unapofika muda wa kufanya mitihani.
Alisema suala hilo sasa limetatuliwa
na kupiga marufuku michango hiyo kwa wanafunzi.
Aidha, Aweso alisema atakutana na
wananchi wa Wilaya ya Pangani, hususan wanawake, kujadili namna ya kuwawezesha
kiuchumi ili waweze kukabiliana na changamoto ya mikopo yenye riba kubwa.
“Mmetuchagua tumekuwa viongozi,
tumeona mnavyoumia na mikopo chechefu na kausha damu. Hivi karibuni tutakaa
kikao cha pamoja na kuona namna gani ya kuwezeshana kiuchumi ili mpate faida ya
kutuchagua sisi vijana wenu tuwatumikie,” alisema.
PANGANI
YAFUNGUKA KIUCHUMI
Wilaya ya Pangani inaendelea kupata
miradi mbalimbali inayolenga kuongeza shughuli za kiuchumi, ikiwamo ujenzi wa
Barabara ya Tanga–Bagamoyo.
Mbali na barabara hiyo, zipo pia
mipango ya utekelezaji wa miradi mingine ya uwekezaji, ikiwamo ujenzi wa
kiwanda cha sukari na kiwanda cha madini, hatua inayotarajiwa kuongeza fursa za
biashara na ajira kwa wakazi wa wilaya hiyo.
mwisho
WAKUU WA TAASISI ZA MUUNGANO WATAKIWA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI
WASTAAFU WAONYWA DHIDI YA MATAPELI KUPOTEZA MAFAO YAO
Na Marco Maduhu, SHINYANGA
WASTAAFU nchini wametakiwa kuwa makini na watu wanaojitambulisha kama mawakala wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), wakihimizwa kutumia njia rasmi za mfuko huo katika kuhakiki taarifa zao na kufuatilia mafao yao ili kuepuka kutapeliwa na kupoteza fedha zao.
Tahadhari hiyo imetolewa leo, Septemba 18, 2026, na Afisa Msimamizi wa PSSSF Mkoa wa Simiyu, Salum Mwegelo, wakati wa semina ya PSSSF kwa waandishi wa habari kutoka Klabu za Waandishi wa Habari za Shinyanga na Simiyu pamoja na Mtandao wa Wanablogu Tanzania (Tanzania Bloggers Network – TBN), iliyofanyika mjini Shinyanga.
Mwegelo amesema baadhi ya wastaafu wamekuwa katika hatari ya kutapeliwa kutokana na kutumia watu wasio rasmi wanaodai kuwa wanaweza kuwasaidia katika taratibu za kuhakiki taarifa, kufuatilia au kupata mafao yao.
![]() |
Amesema watu hao wanaweza kuomba taarifa nyeti za wastaafu, ikiwemo namba za siri za akaunti za fedha na taarifa nyingine binafsi, ambazo zinaweza kutumiwa kufanya miamala bila ridhaa ya wahusika.
“Mawakala hao huwarubuni wastaafu na kuomba namba za siri na taarifa muhimu, ikiwemo taarifa za akaunti zao, na kisha kuzitumia kufanya miamala bila ridhaa ya wahusika na kusababisha kupoteza mafao,” amesema Mwegelo.
Mwegelo amesisitiza kuwa PSSSF haina mawakala wanaotoa huduma kwa niaba ya mfuko huo, hivyo wastaafu wanapaswa kuwa na tahadhari dhidi ya mtu yeyote anayejitambulisha kama wakala wa PSSSF na kuwaomba taarifa zao za siri.
Amesema wastaafu wanapaswa kutumia njia rasmi zinazotolewa na PSSSF, ikiwemo kufika katika ofisi za mfuko huo au kutumia mifumo ya kidijitali inayowawezesha wanachama na wastaafu kufuatilia na kuhakiki taarifa zao kwa usalama.
Amesema matumizi ya mifumo ya kidijitali ni miongoni mwa njia zinazoweza kuwasaidia wanachama kupata taarifa zao kwa urahisi bila kulazimika kuwapa watu wengine taarifa zao binafsi au za kifedha.
Kwa upande wake, Afisa Uhusiano wa PSSSF, Abdul Njalo, amewataka waandishi wa habari na wanablogu kutumia taaluma yao kuwafikishia wananchi taarifa sahihi kuhusu huduma za mfuko huo, hususan elimu inayohusu haki, wajibu na taratibu za kupata mafao.
Njalo amesema vyombo vya habari, blogu na majukwaa ya kidijitali vina nafasi kubwa katika kuhakikisha elimu hiyo inawafikia wanachama na wastaafu kwa lugha rahisi na inayoeleweka, huku akiwataka waandishi na wanablogu kuthibitisha taarifa kabla ya kuzifikisha kwa umma.
Amesema elimu sahihi inaweza kusaidia kuwawezesha wanachama na wastaafu kutambua njia halali za kupata huduma za PSSSF na kuchukua tahadhari dhidi ya watu wanaoweza kutumia mwanya wa ukosefu wa taarifa kuwahadaa.
Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga, Greyson Kakuru, amesema semina hiyo imekuwa na umuhimu mkubwa kwa waandishi wa habari na wanablogu kwa kuwa imewapa uelewa zaidi kuhusu huduma za PSSSF na masuala yanayowahusu wanachama na wastaafu.
Kakuru amesema maarifa yaliyopatikana yatawasaidia waandishi na wanablogu kuandaa na kusambaza habari zenye usahihi, huku wakitoa elimu kwa jamii kuhusu namna ya kutumia huduma za PSSSF na kujilinda dhidi ya utapeli.
Amesema ushirikiano kati ya PSSSF na vyombo vya habari pamoja na wanablogu ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kwa wakati na kutumia huduma za hifadhi ya jamii kwa uelewa zaidi.
Naye Mratibu wa Tanzania Bloggers Network (TBN) Kanda ya Ziwa, Kadama Malunde, amepongeza PSSSF kwa kuandaa semina hiyo, akisema mafunzo kama hayo ni muhimu kwa waandishi wa habari na wanablogu kwa kuwa yanawaongezea uelewa wa masuala wanayopaswa kuyafikisha kwa jamii.
Malunde amesema waandishi na wanablogu wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha kila taarifa wanayoitoa kwa umma inathibitishwa, ina usahihi na inatoka katika vyanzo vinavyoaminika, hususan katika kipindi hiki ambacho taarifa za kidijitali zinaweza kusambaa kwa kasi kubwa.
“Semina kama hii ni muhimu kwa sababu inatupa nafasi ya kujifunza na kuongeza uelewa. Tukiwa waandishi na wanablogu, jukumu letu si kuchapisha taarifa tu, bali kuhakikisha taarifa tunazowafikishia wananchi ni sahihi, zimehakikiwa na zina manufaa kwa jamii,” amesema Malunde.
SERIKALI YAAGIZA UKAGUZI MAENEO YA UWEKEZAJI NCHINI
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amewaagiza Makamishna wa Ardhi Wasaidizi katika mikoa yote nchini kufanya ukaguzi wa maeneo ya uwekezaji yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali kwa lengo la kubaini maeneo yasiyoendelezwa na kutoa taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe
Dkt. Akwilapo ametoa agizo hilo Septemba 18, 2026, mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika maeneo ya uwekezaji ya Kongani ya Viwanda ya KAMAKA pamoja na kiwanda cha Nondo cha Gain Company Limited kilichopo Mlandizi, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani.
Amesema Wizara ya Ardhi, imebaini kuwepo kwa maeneo ambayo yalipewa wawekezaji kwa ahadi ya kuanzisha viwanda au shughuli nyingine za uzalishaji, lakini hayajaendelezwa kwa muda uliokubaliwa.
“Tuna taarifa kuna waliochukua maeneo wakasema watatengeneza viwanda lakini bado hawajafanya hivyo. Natoa maelekezo makamishna kufanya ukaguzi na kuwasilisha taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe kwa maeneo yasiyoendelezwa kadri ya mikataba waliyoingia,” amesema Dkt. Akwilapo.
Aidha, Waziri huyo amewataka wamiliki wote wa ardhi ambao hawazingatii masharti ya uendelezaji maeneo waliyopewa kuhakikisha wanayaendeleza kwa wakati, vinginevyo wizara itachukua hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.
Amesisitiza kuwa, hatua hizo zitawahusu wawekezaji wazawa na wa kigeni, akieleza kuwa kwa wawekezaji wazawa hatua inaweza kujumuisha kubadilisha milki za ardhi walizopewa, huku kwa wawekezaji wa kigeni wizara ikishirikiana na taasisi husika, ikiwemo TISEZA, katika kushughulikia masuala ya umiliki na uwekezaji.
Dkt. Akwilapo amesema, hatua hiyo inalenga pia kujibu malalamiko kutoka kwa wananchi ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa ajili ya uwekezaji, lakini baadaye hayakuendelezwa.
Ameeleza kuwa, hali hiyo imekuwa ikisababisha wananchi kuhoji sababu za maeneo kutolewa kwa wawekezaji ambao hawajaanza shughuli za maendeleo kwa muda mrefu.
Awali Mhe Dkt Akwilapo alielezwa kuwa eneo la Kongani ya Viwanda Mlandizi wilayani Kibaha mkoa wa Pwani linakabiliwa na changamoto kadhaa kama vile upatikanaji wa maji na ubovu wa barabara hali waliyoieleza kuwa inayosababisha kero katika usafirishaji bidhaa na malighafi.
Hata hivyo, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wameeleza kuanza kuchukua hatua za dharura kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi wa muda mfupi na mrefu
Ziara ya Dkt. Akwilapo katika Mkoa wa Pwani imelenga kujionea kwa karibu shughuli za uwekezaji na matumizi ya ardhi katika maeneo hayo, pamoja na kutathmini namna bora ya kuendeleza maeneo ya uwekezaji kwa kuzingatia mipango ya matumizi ya ardhi na maendeleo endelevu.
Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi za kutambua fursa na changamoto zinazohusiana na ardhi na uwekezaji, kwa lengo la kuimarisha matumizi bora ya ardhi, kuvutia uwekezaji na kuchochea maendeleo ya wananchi.
----------mwisho---------
Green Acres yajivunia umahiri wa taaluma
HABARIROSTAM AZIZI: UONGOZI IMARA, SERA BORA NA MIFUMO THABITI VITAAMUA MUSTAKABALI WA UWEKEZAJI AFRIKA MASHARIKI
HABARIMAKAMU WA RAIS AAGIZA MAWAZIRI WATATU KUTATUA MGOGORO WA MIPAKA PUGU NDANI YA SIKU SABA
Na: OWM–TAMISEMI, Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewaagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Waziri wa Maliasili na Utalii kufika ndani ya siku saba katika Dampo la Pugu kwa ajili ya kutatua mgogoro wa muda mrefu wa wananchi kuhusu mipaka ya kiutawala na mpaka wa Msitu wa Kazimzumbwi.
Makamu wa Rais ametoa agizo hilo Septemba 18, 2026, jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wananchi wa Pugu mara baada ya kufanya ziara katika Dampo la Pugu, linalohudumia Mkoa wa Dar es Salaam kwa kupokea taka, na kusikiliza kero zinazowakabili wananchi wa eneo hilo.
“Nikiwa Dampo kuna wazee wangu waliwasilisha malalamiko juu ya kubuguziwa katika Msitu wa Kazimzumbwi, wakidai hawajui kama wako eneo gani la utawala, Pwani au Dar es Salaam. Hivyo, ninawaelekeza Mawaziri wa TAMISEMI, Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wa Maliasili na Utalii kuhakikisha ndani ya siku saba wawe wamefika hapa kutatua changamoto hiyo ya wananchi kubuguziwa,” amesema Mhe. Ndejembi.
Aidha, Mhe. Ndejembi amewataka mawaziri hao watakapofika katika eneo hilo kuzungumza na wananchi na kuhakikisha katika kutatua changamoto hiyo wanatumia taarifa rasmi ya Serikali kuhusu mipaka ya kiutawala, yaani Government Notice (GN) iliyochapishwa katika Gazeti la Serikali, kama msingi wa kubaini mipaka husika.
Akizungumza kwa niaba ya mawaziri wenzake, Waziri wa Nchi, OWM–TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameahidi kutekeleza maelekezo hayo ya Makamu wa Rais kwa kufika katika eneo hilo ndani ya siku saba na kuzungumza na wananchi kwa ajili ya kutafuta suluhisho la mgogoro huo.
“Mhe. Makamu wa Rais, tumepokea maelekezo yako ya kutatua mgogoro huu wa wananchi wa mipaka ya kiutawala na Msitu wa Kazimzumbwi ndani ya siku saba. Hivyo, mimi Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa TAMISEMI, Dkt. Akwilapo, Waziri wa Ardhi, na Dkt. Ashatu Kijaji, Waziri wa Maliasili, tutakuja kuzungumza na wananchi ili kutatua mgogoro huo,” amesema Prof. Shemdoe.
Aidha, Prof. Shemdoe ameahidi kutekeleza maelekezo ya Makamu wa Rais ya kuzisimamia Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam kuleta vitendea kazi, ikiwemo tingatinga (bulldozer), kwa ajili ya kuboresha mazingira na kuongeza ufanisi wa huduma ya upokeaji wa taka katika Dampo la Pugu.
Prof. Shemdoe amesema tayari amemwelekeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuanza kufuatilia utekelezaji wa agizo hilo ili kuhakikisha vitendea kazi vinapatikana na hatua zinazohitajika zinachukuliwa.
Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumshukuru na kumpongeza Makamu wa Rais, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kufanya ziara katika Dampo la Pugu, kusikiliza kero za wananchi na kutoa maelekezo ya hatua za haraka kuchukuliwa kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa utendaji kazi wa dampo hilo linalohudumia Mkoa wa Dar es Salaam.
TANZANIA KUWA MWENYEJI WA KONGAMANO LA MITAALA AFRIKA
HABARITPi YASHIRIKIANA NA JAMII KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA
HABARIJAB YAWANOA WAANDISHI WA WASAFI MEDIA MEDIA KUHUSU SHERIA NA MAADILI






.jpg)




































