HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
MAMBAMIAMBA YAINGIA RASMI KATIKA SAFARI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Nishati

Wananchi wa Kata ya Mambamiamba, Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, leo Julai 30, 2026, wamejengewa uelewa kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la Tanzania Women Empowerment Network (TAWEN).
Hafla hiyo imezikutanisha taasisi mbalimbali za Serikali, wadau wa maendeleo na wananchi, ambapo kila taasisi imepata fursa ya kuwasilisha huduma zake pamoja na kuelezea fursa zinazopatikana katika sekta zake. Wizara ya Nishati ilitumia fursa hiyo kutoa elimu kuhusu faida za matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwemo kulinda afya, kuhifadhi mazingira na kupunguza gharama za matumizi ya nishati.
Akiwasilisha mada, Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati, Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, Mha. Benezeth Kabunduguru, amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034), unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034, kutoka asilimia 28.6 mwaka 2025.
Amesema lengo hilo litafikiwa kupitia ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, wadau wa maendeleo na wananchi katika kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na kuendelea kutoa elimu kuhusu faida za matumizi yake. Ameongeza kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia yanachangia kulinda afya za wananchi kwa kupunguza athari za moshi unaotokana na matumizi ya kuni na mkaa, kuhifadhi mazingira kwa kupunguza ukataji wa miti, pamoja na kuokoa muda na gharama zinazotumika katika shughuli za kupikia, hususan kwa wanawake na watoto.
Aidha, amewahimiza wananchi wa Kata ya Mambamiamba kuchangamkia matumizi ya teknolojia mbalimbali za nishati safi ya kupikia zinazopatikana nchini ili kuongeza matumizi ya nishati hiyo na kuunga mkono juhudi za Serikali za kufikia malengo ya Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TAWEN, Balozi Amina Salum Ali, ameipongeza Wizara ya Nishati na taasisi zake kwa kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia. Amesema juhudi hizo zinaongeza uelewa wa wananchi na kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu matumizi ya nishati.
Ameongeza kuwa TAWEN itaendelea kushirikiana na Wizara ya Nishati pamoja na wadau wengine kuhakikisha elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia inawafikia wanawake na jamii kwa ujumla ili kuongeza matumizi ya nishati hiyo kwa manufaa ya afya, mazingira na maendeleo ya kiuchumi ya wananchi. 

LILIAN LIUNDI: MAZINGIRA WEZESHI NI UFUNGUO WA KUONGEZA USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA SEKTA YA USAFIRI WA UMEME
habari
TIBAMAZOEZI YATAJWA KUWA SULUHISHO LA MAUMIVU YA MUDA MREFU
habariTADB YAIMARISHA NGUVU YA WAKULIMA KUELEKEA DIRA YA MAENDELEO 2050
habariWAANDISHI WA HABARI WAPATIWA MAFUNZO YA WELEDI NA MAADILI
habari
Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.
PSSSF YAFIKIA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM TANGA
elimu habari
Tanga, Julai 28, 2026
Katika kuendeleza dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSI) chini ya kampeni yake ya #PSSSFKaribuNaJamii, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umekabidhi rasmi mradi wa miundombinu wenye thamani ya Shilingi milioni 25 katika Shule ya Msingi Majani Mapana iliyopo mkoani Tanga.
Mradi huo unahusisha ujenzi wa chumba cha darasa, chumba cha mapumziko pamoja na vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bw. Kwame Temu alieleza kuwa msaada huo unalenga kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalum wanapata haki yao ya msingi ya elimu.
MANYARA YAWEKA REKODI MPYA YA HISANI, SHILINGI BILIONI 1.3 ZATIKISA DAR
habari










































