HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
WAFANYABIASHARA WA KARIAKOO WAAHIDI KUSHIRIKIANA NA TRA KULIPA KODI KWA HIARI
habariRAIS DKT SAMIA SULUHU AWASILI JIJINI LUANDA NCHINI ANGOLA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU MBILI
habariRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro Luanda, tarehe 31 Julai, 2026, kwa ajili ya Ziara ya Kikazi ya siku mbili nchini Angola, kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mhe. João Manuel Gonçalves Lourenço.
USHIRIKIANO WA WAZAZI WAWASHA MOTO WA UFAULU NGUVUMALI
habari
Na Mwandishi Wetu, Tanga
WAZAZI, walezi, walimu na viongozi wa Kata ya Nguvumali jijini Tanga wameanzisha mkakati wa pamoja wenye lengo la kutokomeza matokeo ya Daraja Sifuri katika mitihani ya taifa, wakiamini ushirikiano wa wadau wote wa elimu ndiyo ufunguo wa kuongeza ufaulu wa wanafunzi.
Azimio hilo lilifikiwa katika kikao cha wazazi na walezi kilichofanyika katika Shule ya Sekondari Nguvumali, ambapo wadau hao walikubaliana kuimarisha ushirikiano kati ya shule, familia na serikali za mitaa ili kuboresha matokeo ya wanafunzi wa Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.
Akizungumza katika mkutano huo ambao uliitishwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo Ibrahim Okash, Diwani wa Kata ya Nguvumali, Mustapha Selebosi, alisema hatua hiyo inalenga kubadili taswira ya elimu katika kata hiyo kwa kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunza na kufanya vizuri katika mitihani ya taifa.
Alisema mafanikio ya wanafunzi hayawezi kupatikana bila ushiriki wa karibu wa wazazi, walezi, walimu na viongozi wa jamii.
"Siwezi kuitwa Meya wakati kata yangu inafanya vibaya katika mitihani ya taifa. Ni wajibu wetu sote kuhakikisha tunafuatilia maendeleo ya watoto wetu na kuweka mazingira yatakayowawezesha kufanya vizuri," alisema Selebosi.
Aliongeza kuwa kuboresha mfumo wa ufundishaji, kuongeza usimamizi wa wanafunzi na kuwajibisha kila mdau wa elimu ni miongoni mwa mikakati itakayosaidia kuinua kiwango cha ufaulu katika shule za kata hiyo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Centre for Education (TCE), Yusuf Ogutu, alisema Kata ya Nguvumali ni miongoni mwa shule 10 zilizobainika kuwa na changamoto ya ufaulu, hali iliyosababisha kujumuishwa katika mpango maalumu wa mafunzo unaolenga kuongeza uwezo wa wanafunzi kujifunza kwa ufanisi na kujiandaa vizuri kwa mitihani.
Alisema mpango huo unatekelezwa na TCE kwa kushirikiana na Botnar Foundation na Inovex kupitia mradi wa Tanga Yetu, ukiwa na lengo la kuboresha ubora wa elimu katika shule za serikali.
Kwa mujibu wa Ogutu, changamoto kubwa kwa wanafunzi wengi si ukosefu wa ufundishaji, bali ni kutofahamu namna ya kujibu maswali ya umahiri, kuelewa uzito wa mada mbalimbali na kutumia mbinu sahihi za kufanya mitihani.
"Tumekuja na mafunzo haya ili kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa kuelewa badala ya kukariri. Tunawafundisha namna ya kuchambua muhtasari wa masomo, kutambua mada zenye uzito katika mitihani na kuelewa matumizi ya vitenzi vinavyotumika katika maswali," alisema.
Alieleza kuwa mafunzo hayo pia yanawajengea wanafunzi uwezo wa kupanga muda wa kujisomea, kujiandaa kabla ya mtihani, kufanya mitihani kwa ufanisi na kutathmini utendaji wao baada ya kumaliza mitihani.
Ogutu alisema taasisi hiyo pia imeanza kufanya utafiti katika shule zote 27 za sekondari za serikali zilizopo Jiji la Tanga ili kubaini sababu zinazosababisha kushuka kwa ufaulu wa wanafunzi katika mitihani ya Kidato cha Pili na Kidato cha Nne.
Alisema matokeo ya utafiti huo yatawezesha wadau wa elimu kuweka mikakati ya muda mrefu ya kuboresha ubora wa elimu na kuongeza kiwango cha ufaulu katika shule hizo.
Naye Inspekta wa Polisi wa Kata ya Nguvumali, Sharifu Kiswamba, alisema pamoja na juhudi zinazoendelea kufanywa, utoro na tabia ya baadhi ya wanafunzi kuzurura mitaani wakati wa masomo bado ni changamoto kubwa inayochangia matokeo duni.
Aliwataka wazazi kuongeza usimamizi wa watoto wao na kushirikiana kwa karibu na walimu pamoja na viongozi wa kata ili kuhakikisha wanafunzi wanahudhuria masomo kikamilifu na kutumia muda wao kujifunza.
Hata hivyo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Nguvumali Ibrahim Okash alipongeza juhudi hizo akieleza kwamba vitasaidia kuwezesha kuongezeka kwa ufaulu kutokana na ushirikiano katika jambo lolote lile ni muhimu kwa ajili ya ustawi wake.
Alisema kwamba mkutano huo ni muhimu kwa sababu unawawezesha kukutana na wazazi na walezi ili kuweza kuweka nguvu za pamoja kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake ipasavyo ili kuweza kuchangia ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne na pili
Mwisho
TRA KARIAKOO YAWAELIMISHA WAFANYABIASHARA KUHUSU MABADILIKO YA SHERIA ZA KODI 2026/2027
habariMD TWANGE AWATAKA WANASHERIA WA TANESCO KUENDELEA KUSIMAMIA MAADILI NA TAALUMA
habari.jpg)
📌 Afungua Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO jijini Mwanza
📌 Awasisitiza kutoa ushauri wa kisheria kwa wakati na kulinda maslahi ya Shirika
Na Mwandishi Wetu, Mwanza
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. Lazaro Twange, amewataka wanasheria wa shirika kuendelea kusimamia maadili ya taaluma, kutoa ushauri wa kisheria kwa wakati na kulinda maslahi ya shirika ili kuimarisha utendaji na kuhakikisha TANESCO inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Bw. Twange ameyasema hayo wakati akifungua Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO lililoanza Julai 28, 2026 jijini Mwanza, likiwakutanisha wanasheria kutoka Makao Makuu, Ofisi za Kanda na Kampuni Tanzu za TANESCO kwa lengo la kujengeana uwezo na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya kisheria yanayohusu utendaji wa shirika.
Akizungumza katika ufunguzi wa jukwaa hilo, Bw. Twange amewapongeza wanasheria hao kwa mchango wao katika kulinda maslahi ya shirika na kuhakikisha shughuli zake zinafanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu.
“Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya. Ushauri wa kisheria unaotolewa kwa wakati umekuwa ukisaidia TANESCO kufanya maamuzi sahihi na kuepusha migogoro ambayo ingeweza kuzuilika mapema,” amesema Bw. Twange.
Amewasisitiza kuendelea kuzingatia maadili ya taaluma, kutunza siri za kazi na kutoa ushauri wa kitaalamu unaolinda maslahi ya shirika.
“Kila mmoja wetu ana wajibu wa kulinda taasisi. Kwa upande wa wanasheria, hilo linaanza na kuzingatia maadili ya taaluma, kutunza siri za kazi na kuhakikisha kila ushauri unaotolewa unalinda maslahi ya TANESCO na kuimarisha utendaji wake,” amesema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa TANESCO, Wakili Sundi Mahalu, amesema idara hiyo itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ili kuhakikisha shughuli za shirika zinaendelea kufanyika kwa kuzingatia misingi ya utawala bora na sheria.
“Jukwaa hili linatupa nafasi ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuimarisha uwezo wetu wa kitaaluma ili tuendelee kutoa huduma bora za kisheria zinazochangia mafanikio ya TANESCO,” amesema Wakili Mahalu.
Jukwaa la Wanasheria wa TANESCO linafanyika kwa siku tatu likiwa sehemu ya mkakati wa shirika wa kuendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wake wa sheria, hatua inayochangia ufanisi wa utendaji, usimamizi bora wa masuala ya kisheria na ulinzi wa maslahi ya shirika.
MOROCCO YAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI NA TANZANIA
habariLRCT YAFANYA WARSHA YA NAFASI YA SHERIA YA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050
habari
RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONDOKA NCHINI KUELEKEA LUANDA NCHINI ANGOLA KUSHIRIKI KATIKA UZINDUZI WA HOSPITALI ILIYOPEWA JINA LA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
habari 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na viongozi mbalimbali kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam kabla ya kuondoka nchini, kuelekea Luanda, Angola ambapo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hospitali iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, tarehe 31 Julai, 2026.
WABUNIFU WA KITANZANIA KUONYESHA TEKNOLOJIA ZAO TANGA
habariMAMBAMIAMBA YAINGIA RASMI KATIKA SAFARI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Nishati

Wananchi wa Kata ya Mambamiamba, Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, leo Julai 30, 2026, wamejengewa uelewa kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la Tanzania Women Empowerment Network (TAWEN).
Hafla hiyo imezikutanisha taasisi mbalimbali za Serikali, wadau wa maendeleo na wananchi, ambapo kila taasisi imepata fursa ya kuwasilisha huduma zake pamoja na kuelezea fursa zinazopatikana katika sekta zake. Wizara ya Nishati ilitumia fursa hiyo kutoa elimu kuhusu faida za matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwemo kulinda afya, kuhifadhi mazingira na kupunguza gharama za matumizi ya nishati.
Akiwasilisha mada, Mtaalamu kutoka Wizara ya Nishati, Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, Mha. Benezeth Kabunduguru, amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034), unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034, kutoka asilimia 28.6 mwaka 2025.
Amesema lengo hilo litafikiwa kupitia ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, wadau wa maendeleo na wananchi katika kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na kuendelea kutoa elimu kuhusu faida za matumizi yake. Ameongeza kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia yanachangia kulinda afya za wananchi kwa kupunguza athari za moshi unaotokana na matumizi ya kuni na mkaa, kuhifadhi mazingira kwa kupunguza ukataji wa miti, pamoja na kuokoa muda na gharama zinazotumika katika shughuli za kupikia, hususan kwa wanawake na watoto.
Aidha, amewahimiza wananchi wa Kata ya Mambamiamba kuchangamkia matumizi ya teknolojia mbalimbali za nishati safi ya kupikia zinazopatikana nchini ili kuongeza matumizi ya nishati hiyo na kuunga mkono juhudi za Serikali za kufikia malengo ya Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TAWEN, Balozi Amina Salum Ali, ameipongeza Wizara ya Nishati na taasisi zake kwa kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia. Amesema juhudi hizo zinaongeza uelewa wa wananchi na kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu matumizi ya nishati.
Ameongeza kuwa TAWEN itaendelea kushirikiana na Wizara ya Nishati pamoja na wadau wengine kuhakikisha elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia inawafikia wanawake na jamii kwa ujumla ili kuongeza matumizi ya nishati hiyo kwa manufaa ya afya, mazingira na maendeleo ya kiuchumi ya wananchi. 

LILIAN LIUNDI: MAZINGIRA WEZESHI NI UFUNGUO WA KUONGEZA USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA SEKTA YA USAFIRI WA UMEME
habari
TIBAMAZOEZI YATAJWA KUWA SULUHISHO LA MAUMIVU YA MUDA MREFU
habariTADB YAIMARISHA NGUVU YA WAKULIMA KUELEKEA DIRA YA MAENDELEO 2050
habariWAANDISHI WA HABARI WAPATIWA MAFUNZO YA WELEDI NA MAADILI
habari
Kwa upande wake, Dkt. Egbert Mkoko, akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Uandishi wa Habari, amesema maadili ni nguzo muhimu ya taaluma inayojengwa katika misingi ya ukweli, usahihi, haki, mizania, uwajibikaji na kutanguliza maslahi ya umma.Amesisitiza kuwa mwandishi wa habari hapaswi kuongozwa na kasi ya kuwahi kuripoti habari, shinikizo la mitandao ya kijamii, umaarufu au maslahi binafsi, bali na ukweli na uwajibikaji.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, akiwemo Bi. Irene Kilango na Bw. Anord Philemon, wameishukuru JAB kwa kuandaa mafunzo hayo, wakisema yamewaongezea uelewa kuhusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya taaluma na wajibu wa mwandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mpango endelevu wa JAB wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini ili kuhakikisha wanazingatia Sheria ya Huduma za Habari, maadili, weledi na viwango vya taaluma katika utekelezaji wa majukumu yao, kwa lengo la kuimarisha ubora wa huduma za habari na kulinda maslahi ya umma.
PSSSF YAFIKIA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM TANGA
elimu habari
Tanga, Julai 28, 2026
Katika kuendeleza dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSI) chini ya kampeni yake ya #PSSSFKaribuNaJamii, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umekabidhi rasmi mradi wa miundombinu wenye thamani ya Shilingi milioni 25 katika Shule ya Msingi Majani Mapana iliyopo mkoani Tanga.
Mradi huo unahusisha ujenzi wa chumba cha darasa, chumba cha mapumziko pamoja na vifaa mbalimbali vya michezo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bw. Kwame Temu alieleza kuwa msaada huo unalenga kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalum wanapata haki yao ya msingi ya elimu.




.jpeg)





.jpg)

.jpg)






















