HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TUME YA TAIFA YA UNESCO YASHIRIKI UZINDUZI WA MWONGOZO WA MAWASILIANO KATI YA MZAZI NA MTOTO ZANZIBAR

September 03, 2026 Add Comment



ZANZIBAR, Septemba 3, 2026 — Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania imeshiriki katika uzinduzi wa Mwongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto kuhusu Haki ya Afya ya Uzazi (Parent-Child Communication – PCC Toolkit), unaolenga kuimarisha mawasiliano ndani ya familia na kusaidia kulinda afya na ustawi wa watoto na vijana Zanzibar.

Mwongozo huo unazinduliwa leo katika Hoteli ya Verde Zanzibar na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar, Mheshimiwa Zawadi Amour Nassor, katika hafla iliyowakutanisha viongozi na wadau mbalimbali wanaohusika na afya, ulinzi na ustawi wa watoto.


Mwongozo huo umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar na UNESCO, ukiwa na lengo la kuwasaidia wazazi na walezi ku

anzisha mazungumzo sahihi na yenye kujenga na watoto kuhusu afya ya uzazi, mabadiliko ya ukuaji, usalama na namna ya kujilinda dhidi ya mazingira yanayoweza kuhatarisha afya na ustawi wao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mheshimiwa Zawadi anasema Serikali ya Zanzibar imejizatiti kuhakikisha watoto wanakulia katika mazingira salama, wanasikilizwa na hawabaki nyuma, akisisitiza kuwa malezi na ulinzi wa mtoto ni jukumu la pamoja.

Anasema afya ya uzazi ni sehemu ya afya na ustawi wa mtoto, hivyo wazazi, walezi, taasisi na jamii wanapaswa kushirikiana katika kuwapatia watoto taarifa sahihi na mazingira yanayowawezesha kukua kwa usalama.


“Mtoto ni kama mbegu; ukimlea vizuri atakuwa na afya bora,” anasema.

Naibu Waziri pia anawataka wadau kuimarisha ushirikiano katika kukabiliana na changamoto zinazochangia ukatili na udhalilishaji wa watoto, akisisitiza umuhimu wa kuzuia matukio hayo kabla hayajatokea.

Anasema changamoto hizo zinahitaji ushirikiano wa karibu baina ya taasisi, jamii na wadau mbalimbali, huku akigusia pia umuhimu wa wanaume kushiriki kikamilifu katika juhudi za kuzuia na kukabiliana na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.

“Tuzuie matukio yanayosababisha udhalilishaji ili tuweze kupata taifa bora,” anasisitiza.

Kwa upande wa UNESCO, Mr Mathias Luhanya, National Project Officer, anasema mwongozo huo umefanyiwa kazi tangu mwaka 2020, na kufikia hatua ya kuzinduliwa rasmi ni matokeo ya uvumilivu, juhudi na ushirikiano wa wadau mbalimbali.

Anasema mwongozo huo unalenga kumsaidia mzazi kuelewa namna bora ya kuzungumza na mtoto kuhusu afya ya uzazi, kumsaidia kuelewa mabadiliko anayopitia na kutambua mazingira yanayoweza kuhatarisha afya na usalama wake.

Ushiriki wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania katika uzinduzi huo unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya UNESCO, Serikali ya Zanzibar na wadau wa kitaifa katika kuendeleza programu zinazolenga elimu, afya, ulinzi na ustawi wa watoto na vijana.

Hatua hiyo pia inaendana na juhudi za UNESCO za kuwawezesha watoto na vijana kupata maarifa na mazingira salama yanayowasaidia kulinda afya zao na kufikia uwezo wao.

Akizungumza kuhusu ushirikiano huo, Mheshimiwa Zawadi anaishukuru UNESCO kwa kushirikiana na Serikali ya Zanzibar katika kufanikisha uzinduzi wa mwongozo huo, akisisitiza kuwa mafanikio katika kumlinda mtoto yanahitaji dhamira na ushirikiano wa pamoja.

“Penye nia pana njia.”

Uzinduzi wa mwongozo huo unaweka msisitizo kwamba kumlinda mtoto ni jukumu la pamoja la mzazi, familia, jamii, Serikali, taasisi na wadau wa maendeleo, ili kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama, wanasikilizwa na wanapata fursa ya kuwa na afya bora na maisha yenye ustawi.

MAKAMU WA RAIS NDEJEMBI ATOA MAELEKEZO KUHUSU BEI YA SARUJI

September 03, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

MAKAMU wa Rais wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, ametoa maeekezo kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kukaa meza moja na wazalishaji wa saruji nchini ili kuweka mikakati ya haraka itakayohakikisha saruji inapatikana kwa wingi na bei nafuu.

MAAFISA ELIMU KATA WAPEWA JUKUMU KUKUZA UFAULU TANGA

September 03, 2026 Add Comment



Na Mwandishi Wetu, TANGA

MAAFISA Elimu Kata katika Jiji la Tanga wameanza kushirikishwa katika mafunzo ya walimu yanayotolewa kupitia mradi wa Tanga Yetu, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa mafunzo hayo na hatimaye kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Mafunzo hayo yanaendeshwa na Taasisi ya Tanzania Centre for Education  kupitia mradi wa Tanga Yetu, unaodhaminiwa na Botnar Foundation kwa kushirikiana na Inovet, ukiwa na lengo la kuchangia kuboresha elimu na kuongeza ufaulu wa wanafunzi pia yakilenga 

Pia yakilenga kuwajengea walimu uwezo wa kutumia teknolojia na rasilimali za kidijitali katika ufundishaji, huku Maafisa Elimu Kata wakipewa nafasi ya kufuatilia mafunzo hayo ili waweze kuyasimamia wanaporejea shuleni.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Centre for Education Yusuf Ogutu alisema ushiriki wa Maafisa Elimu Kata ni muhimu kwa kuwa wao ndio wanaohusika na usimamizi wa shughuli za elimu katika kata zao.

Alisema kupitia ushiriki huo, Maafisa Elimu Kata wataweza kufahamu maudhui yanayofundishwa, changamoto zinazowakabili walimu na hatua zinazoweza kuchukuliwa kuhakikisha mafunzo yanakuwa na matokeo yaliyokusudiwa.

“Ni jambo la muhimu kwa Maafisa Elimu Kata kujua kinachofanyika katika mafunzo haya ili wanaporudi shuleni waweze kusimamia na kufuatilia utekelezaji wake,” alisema.

Kwa mujibu wa mtoa maelezo huyo, mafunzo hayo pia yanawalenga kuwajengea walimu uwezo wa kutumia Digital Learning ili kurahisisha upatikanaji wa mitihani, notisi, vitabu na rasilimali mbalimbali za kujifunzia zinazopatikana kwenye mitandao.

Alisema matumizi ya teknolojia yatawasaidia walimu kupata nyenzo mbalimbali za kufundishia na kujifunzia kwa urahisi, pamoja na kuwawezesha kutumia mifumo ya E-Learning katika kuboresha ufundishaji.

Aidha, alisema Maafisa Elimu Kata watakuwa na jukumu la kufuatilia ushiriki wa walimu katika mafunzo hayo, kutambua walimu ambao hawajashiriki na kuhakikisha maudhui yaliyofundishwa yanafanyiwa kazi shuleni.

“Maafisa Elimu Kata ndio wanaosimamia shule katika kata zao. Kupitia wakuu wa shule wataweza kufuatilia ni walimu gani wamehudhuria mafunzo na ni kwa kiwango gani wanatumia maarifa waliyopata,” alisema.

Alisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha mafunzo yanayotolewa hayabaki darasani pekee, bali yanafikia wanafunzi kupitia maboresho ya ufundishaji na matumizi sahihi ya rasilimali za kidijitali.

Kwa upande mwingine, Maafisa Elimu Kata walipata fursa ya kufuatilia changamoto zinazowakabili walimu wakati wa kutumia teknolojia na nyenzo mbalimbali za kidijitali, ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi ambapo mafunzo  hayo yanaendelea kwa awamu kulingana na masomo yanayolengwa.

Jana ilikuwa siku ya mwisho ya mafunzo kwa walimu wa masomo ya Historia, Jiografia na Business Studies, huku wiki hii yakitarajiwa kuendelea kwa walimu wa masomo ya Sayansi, Fizikia, Baiolojia, Kemia na Hisabati.


NEMC YATOA TAHADHARI KUELEKEA MVUA ZA EL NIÑO

September 03, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limewataka Watanzania kuchukua tahadhari na kuimarisha utunzaji wa mazingira kuelekea mvua za El Niño, likisema utupaji holela wa taka na uharibifu wa miundombinu ya maji unaweza kuongeza hatari ya mafuriko.

JUBILEE LIFE INSURANCE YAZINDUA BIDHAA TATU MPYA ZA BIMA YA MAISHA

September 03, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KAMPUNI ya Jubilee Life Insurance Tanzania imezindua bidhaa tatu mpya za bima ya maisha zinazolenga kuwasaidia Watanzania katika uwekaji akiba, maandalizi ya elimu, ulinzi wa maisha na mahitaji mengine ya kifedha ya baadaye.

FROM LESSON NOTES TO DIGITAL LEARNING :DR.LUCIAN EQUIPS TEACHERS WITH PRACTICAL PRESENTATION SKILLS

September 03, 2026 Add Comment

 


ARUSHA — A classroom lesson does not have to remain on paper. With the right digital skills, a teacher can transform ordinary lesson notes into a clear, visual and engaging learning experience for students.

This was the focus of a practical session facilitated by Dr. Lucian Ngezei, from the University of Dodoma (UDOM) during the ongoing digital education training, where teachers were introduced to the step-by-step development of digital teaching presentations using Microsoft PowerPoint, as well as WPS Office for teachers using tablets.

Using Photosynthesis as a practical example, Dr. Lucian guided teachers in developing a complete lesson presentation, beginning with the lesson objectives, followed by the meaning of photosynthesis, illustrations, conditions necessary for photosynthesis, its applications and a summary.

Rather than filling slides with lengthy notes, teachers were encouraged to present one key idea at a time, supported by appropriate illustrations. Dr. Lucian introduced the Six-by-Six rule to help teachers make their slides simple, readable and focused.

The training was deliberately practical. Each teacher was given 10 minutes to create slides, applying the principles demonstrated. Teachers also used Mwalimu Julius Kambarage Nyerere as another example through which they practised selecting key information, organising ideas and adding relevant visual elements.

For teachers who have not yet acquired these skills, the lesson from the training is clear: digital teaching does not require a teacher to be a technology expert. It begins with the willingness to learn and the ability to use simple tools purposefully.

A teacher who masters these skills can develop digital resources for different subjects, explain difficult concepts more effectively, stimulate classroom discussion and make learning more visual and learner-centred.

More importantly, these skills support the direction of Tanzania’s new curriculum, which places greater emphasis on competence, creativity, critical thinking, practical skills and active participation in learning.

The message from the training is therefore simple: the digital transformation of education begins with a digitally empowered teacher. Every teacher can learn these skills, and every lesson can become an opportunity to use technology meaningfully to improve learning.

PBPA YAWAWEZESHA MAMA LISHE KURASINI KUHAMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

September 03, 2026 Add Comment
Dar es Salaam, Septemba 3, 2026

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mhandisi Bruno Tarimo, amewahimiza mama na baba lishe kuachana na matumizi ya kuni na mkaa wa kawaida na kuhamia katika nishati safi ya kupikia ili kulinda afya zao, kuhifadhi mazingira na kuongeza ufanisi wa biashara zao.

KAZI 294 ZIFUZU KUINGIA HATUA YA KURA SAMIA KALAMU AWARDS 2026

September 03, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Septemba 3, 2026: Kazi 294 zimefuzu kuingia hatua ya kupigiwa kura na wananchi katika msimu wa pili wa Tuzo za Samia Kalamu Awards (SKA 2026).

Kazi hizo zimechujwa kutoka katika kazi 3,003 zilizowasilishwa na waombaji 985 na kufanyiwa tathmini na jopo la majaji kwa kuzingatia ubora, ubunifu, utafiti, maadili ya taaluma, athari kwa jamii na mchango katika maendeleo ya nchi.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo, Septemba 3, 2026, Mwenyekiti wa Maandalizi ya tuzo ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mha. Peter Mwasalyanda, amewakaribisha wananchi kupiga kura kuchagua washindi kupitia tovuti https://www.samiaawards.tz/ au kutuma ujumbe mfupi wenye neno “SKA”, likifuatiwa na namba ya mshiriki kwenda namba 15200.

Zoezi la upigaji kura limeanza leo, Septemba 3, 2026, na litafungwa Septemba 30, 2026.

Naye Mwenyekiti Mwenza wa Mashindano hayo na Mkurugenzi wa TAMWA, Dkt. Rose Reuben, amesema mashindano hayo yamewaleta pamoja waandishi wa habari kutoka maeneo ya vijijini na mijini, akisisitiza kuwa washiriki watashindana kwa kuzingatia ubora wa kazi zao na si umaarufu wao.
Kwa mujibu wa mmoja wa majaji wa mashindano hayo, Bi. Beatrice Bandawe, amesema kuwa miongoni mwa maeneo yaliyopatiwa kipaumbele katika kazi zilizowasilishwa ni pamoja na afya, jinsia na makundi maalum, mazingira pamoja na elimu.

Samia Kalamu Awards ni tuzo za kitaifa zinazoratibiwa kwa ushirikiano wa TCRA, Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB).

Aidha TCRA, TAMWA, na JAB zinaendelea kuwaomba wadau kujitokeza kudhamini tuzo za SKA 2026 kwa dhumuni la kutambua, kuenzi na kuhamasisha uandishi wa habari wenye ubora, weledi na ubunifu katika kuchochea maendeleo ya nchi.

WANANCHI WAPEWA NAFASI KUCHAGUA KAZI BORA SKA 2026

September 03, 2026 Add Comment





Na Mwandishi Wetu.
Dar es Salaam, Septemba 3, 2026: Wananchi wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kupigia kura kazi 294 za uandishi wa habari na makala za maendeleo zilizofuzu katika Samia Kalamu Awards 2026.


Wito huo umetolewa leo, Septemba 3, 2026, na Mwakilishi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa habari (JAB) Prudence Constantine, wakati wa mkutano wa kutangaza kuanza kwa zoezi la upigaji kura litakalodumu hadi Septemba 30, 2026.


Prudence amesema kura za wananchi ni sehemu muhimu ya mchakato wa kumpata mshindi, kwa kuwa zinatoa nafasi kwa jamii kutambua na kuunga mkono kazi zilizoleta mchango au athari chanya katika maisha ya watu na maendeleo ya Taifa.


Amesema wananchi, wakiwa watumiaji wa maudhui ya habari, wana nafasi ya kuchagua kazi wanazoona zimefanya vizuri, zimeakisi mahitaji na maslahi ya jamii na kusaidia kuibua au kuelimisha kuhusu masuala muhimu ya maendeleo.


Wananchi wanaweza kupiga kura kupitia tovuti ya www.samiaawards.tz na kufuata maelekezo yaliyowekwa ili kuchagua kazi wanayoipendelea.


Pia, kura zinaweza kupigwa kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kwa kutuma neno “SKA”, likifuatiwa na namba ya mshiriki kwenda 15200.


Akizungumza kuhusu Kazi 294 zilizofuzu kupigiwa kura Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandishi Peter Mwasalyanda amesema kazi hizo zimefuzu baada ya tathmini ya kazi 3,003 zilizowasilishwa na waombaji 985. Jopo la majaji lilifanya tathmini kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa na kuteua kazi zilizopata alama za juu.


Naye Mwenyekiti Mwenza wa Mashindano hayo na Mkurugenzi wa TAMWA, Dkt. Rose Reuben, amesema mashindano hayo yamewaleta pamoja waandishi wa habari kutoka maeneo ya vijijini na mijini, akisisitiza kuwa washiriki watashindana kwa kuzingatia ubora wa kazi zao na si umaarufu wao.


Kwa mujibu wa mmoja wa majaji wa mashindano hayo, Bi. Beatrice Bandawe, amesema kuwa miongoni mwa maeneo yaliyopatiwa kipaumbele katika kazi zilizowasilishwa ni pamoja na afya, jinsia na makundi maalum, mazingira pamoja na elimu.


Samia Kalamu Awards zinaandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA kwa Kuhsirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) pamoja na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) zikilenga kutambua, kuenzi na kuhamasisha ubora, weledi na ubunifu katika uandishi wa habari na utayarishaji wa makala za maendeleo nchini.















NOMBO: MAFUNZO ENDELEVU KWA WALIMU KUIMARISHWA

NOMBO: MAFUNZO ENDELEVU KWA WALIMU KUIMARISHWA

September 03, 2026 Add Comment

Serikali imeweka mkazo katika kutafuta suluhisho la changamoto ya wanafunzi kuacha shule, hususan wavulana, baada ya kubainika kuwa ongezeko la utoro linaweza kuwa kikwazo katika utekelezaji wa mageuzi ya elimu nchini.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema hayo Septemba 03, 2026, Jiji Dodoma alipokutana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Elke Wisch.

Prof. Mkenda amebainisha kuwa pamoja na juhudi zinazofanyika kuboresha elimu, changamoto ya watoto kuacha shule inahitaji juhudi za pamoja, kwani makadirio ya serikali ya wanafunzi watakaoendelea na elimu yanaweza kuathiriwa iwapo tatizo hilo halitadhibitiwa.

Amesema serikali inaendelea kuweka mikakati ya kuzuia utoro, ikiwemo kuimarisha utekelezaji wa mwongozo wa wanafunzi waliokatisha masomo kurejea shule na kushughulikia changamoto zinazowakabili watoto hao katika maeneo mbalimbali.

Prof. Mkenda amesisitiza kuwa utekelezaji wa mageuzi ya elimu hauishii katika kuandaa sera na mipango pekee, bali unahitaji ushirikiano wa karibu na wadau katika kutatua changamoto halisi zinazowazuia watoto kuendelea na masomo.

Aidha, ameiomba UNICEF kuendelea kushirikiana na serikali katika kupunguza utoro, kusaidia wanafunzi waliokatisha masomo kurejea shuleni na kuimarisha fursa za watoto kupata elimu.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, amesema kuwa serikali inaendelea kuimarisha Mafunzo Endelevu ya Kitaaluma kwa Walimu ili kuwa na mbinu mpya za ufundishaji na zinazoshirikisha wanafunzi kikamilifu katika mchakato wa ujifunzaji.

Mwakilishi wa UNICEF, Elke Wisch, ameipongeza seikali ya Tanzania kwa hatua kubwa inayopiga katika utekelezaji wamageuzi ya sekta ya elimu, akisisitiza kuwa mageuzi hayo ni msingi wa kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na kuandaa kizazi kitakachoweza kuendesha uchumi wa kisasa.