HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

NAIBU WAZIRI MAKAMBA AITAA PBPA KUENDELEA KUTOA ELIMU KWA UMMA

August 13, 2026 Add Comment

 



Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb.), ameitaka Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuendelea kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma ili wananchi wawe na uelewa mpana kuhusu majukumu ya Wakala na mchango wake katika kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.

Mhe. Makamba ametoa wito huo alipotembelea banda la PBPA katika maonesho yanayofanyika Viwanja vya Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya Tamasha la Kizimkazi 2026.

Amesema ni muhimu wananchi wakaendelea kuelimishwa kuhusu Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja na namna PBPA inavyotekeleza majukumu yake katika kusimamia uagizaji wa bidhaa za mafuta kwa lengo la kuhakikisha nchi inakuwa na uhakika wa upatikanaji wa bidhaa hiyo muhimu.


Aidha, Mhe. Makamba ameipongeza PBPA kwa utendaji wake katika kutekeleza majukumu yake na kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkaguzi wa Mafuta wa PBPA, Bw. Issa Mwitazy, amemweleza Naibu Waziri kuwa Wakala unaendelea kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha nchi inakuwa na kiwango cha kutosha cha mafuta ili kukidhi mahitaji ya soko.

Bw. Mwitazy amesema ushiriki wa PBPA katika Tamasha la Kizimkazi umetoa fursa kwa wananchi na wadau mbalimbali kupata elimu na ufafanuzi kuhusu majukumu ya Wakala pamoja na namna Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja unavyofanya kazi.


Ameongeza kuwa PBPA inaendelea kudumisha ushirikiano mzuri na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) katika masuala yanayohusu sekta ya mafuta.


Tamasha la Kizimkazi 2026, ambalo ni msimu wa tatu, linafanyika kuanzia Agosti 12 hadi 14, 2026, likiwa na lengo la kuibua na kufungua fursa mbalimbali za maendeleo, huku likibeba kaulimbiu “Kizimkazi 2026, Fursa na Shangwe.”

KIZIMKAZI 2026: WIZARA YA NISHATI YAENDELEA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

August 13, 2026 Add Comment


Wataalam wa Wizara ya Nishati wanaendelea kutoa elimu na ufafanuzi kwa wananchi wanaotembelea Banda la Wizara na taasisi zake katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026, yanayofanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Wananchi wanapata fursa ya kufahamu shughuli, miradi na huduma mbalimbali zinazotekelezwa katika sekta ya nishati, ikiwemo masuala ya umeme, mafuta, gesi asilia na nishati safi ya kupikia.


Karibu tukuhudumie.



DKT.DOTO BiTEKO ANOGESHA MASHINDANO YA NGALAWA TAMASHA KIZIMKAZI

August 13, 2026 Add Comment




Naibu Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko amesema kuwa mashindano ya ngalawa race ni miongoni mwa matukio makubwa ya kiburudani yanayoipamba Kizimkazi Festival 2026.


Mashindano hayo yamefanyika Kizimkazi, Kusini Unguja Agosti 12, 2026 yaliyokuwa na ushindani mkubwa ambapo Nassor Pandu wa Mkunguni ameibuka mshindi wa mashindano ya ngalawa ikiwa ni sehemu ya shughuli mbalimbali zinazoendelea katika Tamasha la Kizimkazi.

“ Ni dhahiri kwamba mashindano haya yamekuwa muhimu kwa vijana na jamii kwa ujumla. Tukio hili limewaleta pamoja wadau mbalimbali na kuchangia kwa kiasi kikubwa juhudi za kuboresha mazingira ya michezo na burudani,” amesema Dkt. Biteko.

Dkt. Biteko ameongeza kuwa mashindano ya Ngalawa race Kizimkazi Festival yameendelea kutoa fursa za kiuchumi kwa vijana mbalimbali katika kushindana hadi kupata timu mbili bora za Mchangamle na Mkunguni ambapo kila timu imehusisha manahodha 10.



Mwisho.

KAPINGA: SERIKALI YALENGA HUDUMA ZA AFYA KUMFIKIA KILA MWANANCHI

August 13, 2026 Add Comment
Wananchi mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya huduma za afya, hatua iliyowarahisishia upatikanaji wa huduma hizo bila kulazimika kusafiri umbali mrefu.
WAZIRI KAPINGA AHAIDI KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA MTWARA

WAZIRI KAPINGA AHAIDI KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA MTWARA

August 13, 2026 Add Comment

Wananchi mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya huduma za afya, hatua iliyowarahisishia upatikanaji wa huduma hizo bila kulazimika kusafiri umbali mrefu.

Hayo yamejiri, katika siku ya tatu ya ziara ya kikazi ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), mkoani humo, yenye lengo la kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita.

Wananchi hao wamesema wanapata huduma za afya kwa wakati na kwa urahisi, jambo walilolieleza kuwa limepunguza changamoto ya kufuata matibabu katika maeneo ya mbali.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Waziri Kapinga amesema Serikali inalenga kuboresha huduma za afya ili wananchi wapate matibabu kwa urahisi na kuendelea na shughuli zao za uzalishaji, hivyo kuimarisha uchumi wa familia na Taifa.

Amesema kusogeza huduma za afya karibu na wananchi ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma muhimu kwa wakati.

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akisisitiza kuwa ushirikiano ni msingi wa maendeleo.

Katika siku ya tatu ya ziara hiyo, Waziri Kapinga ametembelea miradi mbalimbali katika Majimbo ya Nanyamba, Mtwara Mjini na Mtwara Vijijini, ikiwemo kuzindua Kituo cha Afya Msangamkuu, kuzindua mabweni mawili na kutoa taulo za kike kwa wanafunzi wa Shule ya Wasichana Mtwara, kukagua ujenzi wa Shule ya Amali Chikota, pamoja na kutembelea Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Tandahimba.

ALC GROUP YATOA MSAADA KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM PU­GU

August 13, 2026 Add Comment

    

Jamii, kampuni binafsi na wadau mbalimbali wametakiwa kuongeza juhudi za kusaidia wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia huduma za afya, vifaa saidizi na mahitaji ya kielimu ili kuwawezesha kupata elimu bora na kutimiza ndoto zao.

Wito huo umetolewa na Elvis Lyimo, Mkuu wa Idara ya Elimu Maalum katika Shule ya Sekondari Pugu, wakati ALC Group, wauzaji wa vilainishi vya Flying Horse Lubricant, ilipofika shuleni hapo na kutoa msaada kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Kupitia msaada huo, wanafunzi 50 wamepatiwa bima ya afya, huku baadhi yao wakipatiwa viti mwendo pamoja na kompyuta kwa ajili ya kuwawezesha kushiriki vizuri zaidi katika masomo na shughuli zao za kila siku.

Lyimo amesema msaada huo una umuhimu mkubwa kwa wanafunzi wenye ulemavu, hususan wale wanaotoka katika familia zenye uwezo mdogo kiuchumi na ambao mara nyingi hukabiliwa na changamoto ya kupata huduma za afya na vifaa muhimu vya kuwasaidia katika ujifunzaji.
“Msaada huu utawasaidia wanafunzi wenye ulemavu wa viungo na changamoto ya kuandika, ambao wengi wao wanatoka katika familia zenye hali duni kiuchumi,” amesema Lyimo.

Amesema baadhi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum hukabiliwa na changamoto za kupata viti mwendo, magongo ya kutembelea, magodoro, vifaa vya kujifunzia na mahitaji mengine muhimu, huku gharama za matibabu zikiwa changamoto kwa familia nyingi.

Kwa mujibu wa Lyimo, Shule ya Sekondari Pugu ina jumla ya wanafunzi 85 wenye mahitaji maalum, hali inayofanya mahitaji ya huduma na vifaa kuwa makubwa zaidi licha ya Serikali kuendelea kutoa huduma mbalimbali.
Amesema ushiriki wa wadau zaidi ni muhimu katika kuziba pengo lililopo na kuhakikisha wanafunzi hao wanapata fursa sawa ya elimu na maendeleo.

WAZAZI WATAKIWA KUTOWAFICHA WATOTO WENYE ULEMAVU

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Pugu, Patrick Sinyinza, amewataka wazazi na walezi kutowaficha watoto wenye ulemavu majumbani, bali kuwapeleka shuleni ili wapate elimu na fursa ya kuendeleza vipaji na uwezo wao.

Sinyinza amesema watoto wenye mahitaji maalum wana uwezo mkubwa wa kufanya vizuri kitaaluma iwapo watapewa mazingira rafiki, msaada na fursa zinazostahili.

Amesema msaada uliotolewa na ALC Group umefika wakati muafaka kwa kuwa wanafunzi wenye ulemavu wanahitaji huduma za afya mara kwa mara pamoja na vifaa vinavyowawezesha kushiriki kikamilifu katika masomo.

“Wazazi wasiwanyime watoto wenye ulemavu haki yao ya kupata elimu kwa kuwaficha nyumbani. Watoto hawa wana uwezo mkubwa wa kufanya vizuri kitaaluma,” amesema Sinyinza.
Ameeleza kuwa Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha miundombinu na mazingira ya shule ili kuwawezesha wanafunzi wenye na wasio na ulemavu kusoma pamoja katika mazingira yanayozingatia mahitaji yao.

Shule ya Sekondari Pugu ina jumla ya wanafunzi 989 na walimu 74, ambapo walimu 26 wamepatiwa mafunzo maalum ya elimu ili kuwawezesha kuwahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum.

MWANAFUNZI MWENYE MAHITAJI MAALUM APATA ALAMA SABA

Sinyinza amesema mafanikio ya wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule hiyo ni ushahidi kuwa ulemavu si kikwazo cha kufikia mafanikio ikiwa mwanafunzi atapatiwa msaada unaostahili.

Ametoa mfano wa mwanafunzi wa Kidato cha Sita aliyefanya mtihani mwaka huu na kupata alama saba na Daraja la Kwanza, akisema mafanikio hayo yanaonyesha uwezo mkubwa walionao wanafunzi wenye mahitaji maalum.

“Hii inaonyesha uwezo mkubwa walionao watoto hawa. Wapo wanafunzi wasio na ulemavu ambao hawakupata alama saba, lakini mwanafunzi mwenye mahitaji maalum ameweza kufanya hivyo. Wanachohitaji ni msaada na fursa,” amesema.

ALC GROUP YAAHIDI KUENDELEA KUSAIDIA

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya msaada huo, Emmanuel Shija, Balozi wa ALC Group, wauzaji wa vilainishi vya Flying Horse Lubricant, ambaye pia ni Bingwa wa WBC Muay-Thai Tanzania, amesema mchango huo ni sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa kampuni kwa jamii.

Shija amesema kampuni imeamua kuanza na wanafunzi 50 kwa kuwapatia bima za afya, viti mwendo na kompyuta, huku ikiweka mkakati wa kuendelea kusaidia wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Amesema watu wenye ulemavu na wanaoishi katika mazingira magumu mara nyingi husahaulika katika jamii, hivyo ALC Group imeona umuhimu wa kutumia sehemu ya mafanikio yake kusaidia kuboresha maisha ya kundi hilo.

“Watu ambao wana changamoto au wanaoishi katika mazingira magumu mara nyingi husahaulika na jamii. Tumeamua kuanza na wanafunzi 50 kwa kuwapatia bima za afya, viti mwendo na kompyuta kwa sababu tunaamini ni muhimu kuwakumbuka na kuwasaidia wanaohitaji msaada,” amesema Shija.

Amesema ALC Group itaendelea kugharamia bima za afya kwa baadhi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum ili kuwawezesha kupata matibabu kwa wakati na kupunguza mzigo wa gharama kwa familia zao.

Aidha, amesema kampuni hiyo itaendelea kutoa vifaa vya usafiri kwa baadhi ya wanafunzi, ikiwemo baiskeli za magurudumu matatu, ili kuwawezesha wanafunzi wenye changamoto za ulemavu wa viungo kusafiri kwa urahisi na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kila siku.

Shija amesema lengo la kampuni si kutoa msaada wa mara moja pekee, bali kujenga utamaduni endelevu wa kuirudishia jamii sehemu ya mafanikio yanayopatikana kupitia shughuli za kampuni.

“Lengo letu si kutoa msaada wa mara moja, bali kujenga utamaduni wa kutoa na kuirudishia jamii sehemu ya mafanikio tunayoyapata. Tunaamini kila taasisi ina nafasi ya kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya watu wenye mahitaji maalum,” amesema.

WANAFUNZI WASHUKURU MSAADA

Kwa upande wa wanafunzi, Thobias Masumbulko, aliyewakilisha wanafunzi wenzake, ameishukuru ALC Group kwa msaada huo na kusema vifaa vilivyotolewa vina umuhimu mkubwa katika maisha yao.

Amesema wakati mwingine watu wanaweza kuona msaada kama huo kuwa ni mdogo, lakini kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum una thamani kubwa kwa sababu unawapatia vitu ambavyo hapo awali walikosa.

“Tunawashukuru kwa kile mlichotupatia. Mnaweza kufikiri ni kidogo, lakini kwetu ni kitu kikubwa kwa sababu ni vitu ambavyo hatukuwa navyo kabla,” amesema.

Masumbulko amewataka wazazi na jamii kwa ujumla kutowatenga watoto wenye ulemavu, akisisitiza kuwa wana uwezo wa kufanya mambo makubwa iwapo watapewa fursa na msaada unaostahili.

Ameeleza pia kuwa walimu wa shule hiyo wamekuwa na mchango mkubwa katika kuwajengea wanafunzi wenye mahitaji maalum kujiamini na kuwahamasisha kuangalia uwezo wao badala ya kujikita katika changamoto zao.

PROFESA KABUDI AHIMIZA MATUMIZI SAHIHI YA ALAMA ZA TAIFA

August 12, 2026 Add Comment

    

Na Mwandishi wetu- DODOMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, amehimiza wananchi kuendelea kuzingatia matumizi sahihi ya alama za Taifa, hususan rangi na mwonekano wa Bendera ya Taifa, kwa mujibu wa sheria.

KAFULILA KUONGOZA MHADHARA WA UMMA KUHUSU NAFASI YA UBIA (PPP) KATIKA MAENDELEO YA WATU

August 12, 2026 Add Comment
Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre) kinatarajiwa kufanya mhadhara wa umma utakaolenga kujadili mchango wa ubia kati ya sekta umma na sekta binafsi katika kuchochea maendeleo ya watu na uchumi wa taifa.

RAIS SAMIA ATAMBUA MCHANGO WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE KATIKA KUFANIKISHA MDAHALO WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

August 12, 2026 Add Comment


KIZIMKAZI, ZANZIBAR


Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake imetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kufanikisha Mdahalo wa Nishati Safi ya Kupikia, uliofanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 11 Agosti 2026.


Tuzo hiyo imetolewa usiku wa kuamkia tarehe 12 Agosti 2026 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kupokelewa kwa niaba ya Wizara ya Nishati na taasisi zake na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba.


Mdahalo huo, uliokuwa na lengo la kujadili namna ya kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia iliyo endelevu, salama na nafuu kwa wananchi na taasisi, uliwakutanisha wadau mbalimbali kutoka Serikalini, sekta binafsi, washirika wa maendeleo, taasisi za fedha, wanateknolojia, watafiti na asasi za kiraia.

Mdahalo huo uliandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiatives Foundation (MIF), kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha na kuchagiza hatua za pamoja katika kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.


Katika Mdahalo huo, Serikali iliendelea kusisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, washirika wa maendeleo, taasisi za fedha na wadau wengine.


Tuzo hiyo ni ishara ya kutambua mchango na ushirikiano wa Wizara ya Nishati na taasisi zake katika kufanikisha Mdahalo huo, unaolenga kuchagiza mjadala na hatua madhubuti kuelekea kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

TAMASHA LA KIZIMKAZI KUFUNGUA FURSA KIUCHUMI

August 12, 2026 Add Comment




NA MWANDISHI WETU- ZANZIBAR


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga ameshiriki katika uzinduzi wa Viwanja vya Kufurahisha Watoto vya Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar tarehe 12 Agosti, 2026 vilivyozinduliwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. 


Uzinduzi huo ni miongoni mwa matukio yatakayofanyika wakati wa  Tamasha la Kizimkazi 20226 linalofanyika wa siku tatu Kuanzia Agosti 12 hadi 14 mwaka huu.

Katika tamasha hilo ambalo limejizoelea umaarufu mkubwa pia kutakuwa maonyesho, burudani na programu mbalimbali za kuvutia zinazolenga kutangaza utalii, uwekezaji na utamaduni wa Kizimkazi.

Kizimkazi Festival ni tamasha la wananchi wa Kizimkazi. Dhamira yake ni kuitangaza Kizimkazi kama eneo lenye historia, utamaduni, vivutio vya utalii na fursa nyingi za uwekezaji kwa manufaa ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla.

Aidha malengo ya Tamasha la Kizimkazi ni kutangaza fursa za uwekezaji, kutangaza vivutio vya utalii pamoja na kuhifadhi na kuenzi utamaduni wa Kizimkazi.

Wakati kwa upande wa fursa za uwekezaji ni Utalii na hoteli, Uchumi wa Buluu, Uvuvi, Biashara na huduma mbalimbali, pamoja na miradi mingine ya mandeleo.


Miradi itakayozinduliwa wakati wa tamasha la Kizimkazi ni uzinduzi wa mradi wa maji Kizimkazi, uzinduzi wa kiwanja cha watoto KibuTeni,ufunguzi wa nyumba za kuishi Bopar Enterprises, Jiwe la msingi Salaam Cane Restaurant-K/Dimbani.


Miradi mingine itakayozinduliwa ni mradi wa mabweni mapya -Hasnu Makame Sekondari-Kibuteni ,jiwe la msingi jengo la maendeleo Kibuteni na uzinduzi wa hoteli la kitalii ya Johari-K Mkunguni.


Kauli mbiu”KIZIMKAZI Kumenoga”

TIBA ASILI NI URITHI WA AFRIKA, SASA IPEWE NGUVU YA SAYANSI NA UWEKEZAJI

Kajunason August 12, 2026 Add Comment
Tunapoelekea kuadhimisha Siku ya Tiba Asili ya Mwafrika tarehe 31 Agosti 2026, Afrika inakabiliwa na swali moja kubwa: Je, tutaendelea kutumia urithi wa tiba asilia kama ulivyo, au tutautafiti, kuuthibitisha, kuuboresha na kuugeuza kuwa sehemu ya suluhisho la afya na uchumi wa kizazi kijacho?

Na Mwandishi Wetu

Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO) limetoa wito kwa Serikali, watafiti, vyuo vikuu, sekta binafsi na wadau wa afya kushirikiana kuifanya tiba asili kuwa nguzo muhimu ya huduma za afya, maendeleo ya sayansi na ukuaji wa uchumi wa Afrika.

Wito huo umetolewa wakati Afrika ikijiandaa kuadhimisha Siku ya Tiba Asili ya Mwafrika itakayoadhimishwa Agosti 31, 2026, yenye kaulimbiu inayosisitiza umuhimu wa utafiti na maendeleo katika tiba asili ili kufikia huduma bora za afya kwa wote.

TRAMEPRO imesema kwa karne nyingi jamii za Afrika zimekuwa zikitumia mimea tiba na maarifa ya jadi katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za afya, lakini maarifa hayo yako hatarini kupotea kutokana na wazee na wataalamu wanaoyamiliki kuzeeka huku mengi yakiwa hayajaandikwa.

Shirika hilo limeeleza kuwa pamoja na kupotea kwa maarifa, uharibifu wa mazingira, ukataji wa misitu, mabadiliko ya tabianchi na uvunaji holela wa mimea tiba vinaendelea kutishia mustakabali wa tiba asili barani Afrika.

Kwa mujibu wa TRAMEPRO, kulinda tiba asili kunamaanisha pia kulinda bioanuwai, mazingira na urithi wa maarifa ya jadi ambayo yamekuwa msingi wa huduma za afya kwa vizazi vingi.

Aidha, shirika hilo limesema sekta ya tiba asili inahitaji takwimu sahihi kuhusu wataalamu, vituo vya huduma, mimea tiba, bidhaa zinazozalishwa na idadi ya wananchi wanaotumia huduma hizo ili kusaidia kupanga sera, uwekezaji na maendeleo ya sekta hiyo.

TRAMEPRO imeeleza kuwa dunia imeanza kutambua nafasi ya tiba asili kufuatia kupitishwa kwa Mkakati wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wa Tiba Asili wa mwaka 2025–2034, unaolenga kuimarisha ushahidi wa kisayansi, usalama, ubora na ujumuishaji wa tiba asili katika mifumo ya afya.

Shirika hilo limesisitiza kuwa Afrika inapaswa kuwa kinara wa utafiti, ubunifu na uzalishaji wa bidhaa za tiba asili badala ya kubaki msambazaji wa malighafi zinazoongezewa thamani nje ya bara.

Aidha, limebainisha kuwa Tanzania ina rasilimali muhimu ikiwemo mimea tiba, wataalamu, vyuo vikuu na taasisi za utafiti, lakini kunahitajika ushirikiano mkubwa zaidi ili kuunganisha utafiti, maabara, uzalishaji wa bidhaa salama na masoko.

TRAMEPRO pia imesisitiza umuhimu wa kuimarisha mifumo ya kuthibitisha usalama, ubora na ufanisi wa dawa za asili, pamoja na kuweka utaratibu wa kufuatilia madhara yanayoweza kujitokeza kwa watumiaji.

Kwa upande wa mazingira, shirika hilo limependekeza kuanzishwa kwa mashamba ya mimea tiba, kuhamasisha kilimo endelevu na kuongeza juhudi za kuhifadhi misitu na bioanuwai ili kuhakikisha rasilimali hizo zinaendelea kuwepo kwa vizazi vijavyo.

Aidha, limeeleza kuwa sekta ya tiba asili ina uwezo mkubwa wa kuchochea uchumi kupitia mnyororo wa thamani unaohusisha kilimo cha mimea tiba, utafiti, uzalishaji wa bidhaa, biashara na ajira kwa vijana.

TRAMEPRO imewataka wataalamu wa tiba asili kukumbatia sayansi, teknolojia na utafiti ili kuongeza ubora wa huduma na kuimarisha imani ya jamii, huku ikisisitiza kuwa matumizi ya teknolojia za kisasa, ikiwemo akili mnemba (AI), yanaweza kusaidia kuhifadhi maarifa na kuharakisha tafiti.

Shirika hilo limependekeza pia kuanzishwa kwa ajenda mpya ya kitaifa ya tiba asili itakayojumuisha utafiti, uhifadhi wa maarifa ya jadi, uwekezaji, matumizi ya teknolojia, usajili wa bidhaa na ulinzi wa haki za jamii zinazomiliki maarifa hayo.

TRAMEPRO imehitimisha kwa kutoa wito kwa Serikali, watafiti, vyuo vikuu, sekta binafsi, mashirika ya kiraia na wananchi kushirikiana kujenga tiba asili yenye ushahidi wa kisayansi, salama, yenye viwango, inayolinda mazingira na kuchangia huduma bora za afya pamoja na maendeleo ya uchumi wa Taifa.
NGASONGWA AANZA ZIARA MWANZA, ATOA WITO WA KWA WAFANYABIASHARA

NGASONGWA AANZA ZIARA MWANZA, ATOA WITO WA KWA WAFANYABIASHARA

August 12, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, ameanza ziara ya kikazi mkoani Mwanza kwa lengo la kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia na kukuza ushindani wa haki katika soko.

Katika ziara hiyo, iliyofanyika leo Agosti 12, 2026, Bi. Ngasongwa amekutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Ndugu Balandya Elikana, ambapo wamejadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika kudhibiti uingizaji, uzalishaji na usambazaji wa bidhaa bandia.

Akizungumza katika kikao hicho, Balandya amesema udhibiti wa bidhaa bandia ni muhimu katika kuhakikisha bidhaa halali zinapata fursa sawa ya kushindana katika soko, hatua ambayo itasaidia kuchochea shughuli za kiuchumi na kuongeza kasi ya maendeleo ya Taifa.

"Kuimarisha udhibiti wa bidhaa bandia kutasaidia kuwalinda wafanyabiashara wanaofuata sheria, kuongeza imani ya wananchi kwa bidhaa zinazouzwa sokoni na kuchochea ukuaji wa uchumi."amesema Balandya

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema Tume itaendelea kuchukua hatua dhidi ya uingizaji, uzalishaji na usambazaji wa bidhaa bandia ili kuhakikisha bidhaa halali zinapata mazingira bora ya ushindani katika soko.

Bi.Ngasongwa amesema kuwa  hatua hizo ni sehemu ya jitihada za FCC za kulinda ushindani wa haki, kuwalinda wafanyabiashara wanaozingatia sheria na kuhakikisha shughuli za kibiashara zinafanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.