HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MWANA FA AZINDUA RASMI AWESO CUP ,TIMU 80 KUCHUKUANA KUMPATA BINGWA

September 13, 2026 Add Comment






Na Oscar Assenga, PANGANI

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma ‘Mwana FA’, amezindua rasmi Mashindano ya Aweso Cup katika Kijiji cha Sakura wilayani Pangani huku akizitaka klabu kubwa nchini pamoja na wadau wa soka, kufuatilia mashindano hayo kwa lengo la kuibua vipaji vipya.

Mwinjuma amesema  hayo katika Kijiji cha Sakura, Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, wakati akizindua rasmi Mashindano ya Kombe la Aweso, yanayoshirikisha jumla ya timu 80 kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.

Ambapo alisema Pangani ina vijana wengi wenye vipaji ambao wanahitaji kupewa nafasi ya kuonekana na watu wanaoweza kuwasaidia kufikia viwango vya juu.

Amesema uwekezaji unaofanyika leo katika michezo unaweza kuleta matokeo makubwa kwa vijana na Taifa kwa ujumla hapo baadaye.

“Ukiwekeza leo, kuna faida kubwa kesho. Tunawekeza kwenye michezo, maendeleo na utalii. Tunataka kuitoa Pangani pangoni na kuipandisha hadi kupaa angani,” amesema Mwinjuma.

Amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya michezo, huku ikiweka mkazo pia katika ugunduzi, malezi na utunzaji wa vipaji vya vijana.

TIMU YA U17 MFANO

Mwinjuma ametumia mafanikio ya timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 (U17) kama mfano wa matokeo ya uwekezaji katika vipaji.

Amesema timu hiyo imeonyesha uwezo mkubwa kwa kufika fainali ya michuano ya Afrika, kabla ya kupoteza mchezo huo, na baadaye kufuzu kwa mara ya kwanza kushiriki Kombe la Dunia.

Kwa mujibu wa Mwinjuma, Serikali imeendelea kusambaza mawakala na wataalamu katika maeneo mbalimbali ambako kuna mashindano ili kuhakikisha vipaji vinagunduliwa na kuendelezwa.

“Wadau wa michezo, Aweso Cup ina vipaji vingi. Kuna zaidi ya timu 80 zinazoshiriki. Tunawaomba wadau wa timu za Taifa, Simba, Yanga na klabu nyingine waje kuwaona vijana hawa kwa sababu wanaweza kufanya mambo makubwa,” amesema.

Amesema ni wakati sasa kwa wadau wa michezo kuanza “kuwathamini vyao” kwa kuwapa vijana wa Pangani na maeneo mengine nafasi ya kuonyesha uwezo wao.

Mashindano ya Aweso Cup yanatarajiwa kuwa jukwaa muhimu kwa vijana wa Pangani kuonyesha vipaji vyao, huku wadau wa michezo wakitarajiwa kutumia mashindano hayo kama sehemu ya kutafuta wachezaji wenye uwezo wa kuendelezwa zaidi.

Awali akizungumza  Waziri wa Maji na Mbunge wa Pangani kwa tiketi ya CCM, Jumaa Aweso, amewataka wadau wa michezo nchini kujitokeza katika mashindano mbalimbali ili kubaini na kuendeleza vipaji vya vijana.

Amesema mashindano hayo yameandaliwa kwa lengo la kuwapa vijana nafasi ya kuonyesha uwezo wao katika michezo, huku akisisitiza kuwa uwepo wa viongozi, makocha na wadau wengine ni muhimu katika kuwasaidia vijana wenye vipaji kufikia hatua kubwa zaidi.

“Wadau wa michezo tunapaswa kujitokeza katika mashindano kama haya kwa sababu hapa ndipo vipaji vinapopatikana. Vijana wanahitaji kuonekana, kutambuliwa na kupewa nafasi ya kuendeleza vipaji vyao,” alisema Aweso.

Amesema uwekezaji katika michezo unaweza kuwa sehemu muhimu ya kuwainua vijana kiuchumi, ikiwamo kuwapatia ajira na fursa nyingine kupitia michezo pamoja na sekta ya utalii.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ambaye pia ni Katibu Tawala wa Wilaya hiyo (DAS), Esther Gama, alisema mashindano hayo yatachezwa kwa mfumo wa mtoano (Knock-out) na kutaja zawadi nono zinazowasubiri washindi ambapo Mshindi wa Kwanza (Bingwa):Tsh Milioni 10, Mshindi wa Pili: Tsh Milioni 5,Mshindi wa Tatu: Tsh Milioni 3 huku Kikundi Bora cha Ushangiliaji: Pikipiki aina ya Boxer.

BARRICK YAFANIKISHA UJENZI WA MADARASA KUNUFAISHA WANAFUNZI WA JAMII YA KIMASAI LONGIDO

September 13, 2026 Add Comment


   

Meneja Mkazi wa Barrick nchini , Dkt. Melkiory Ngido akisalimiana na wananchi na wazee wa kimila wa Kijiji cha Kiseriani kata ya Engikaret , Wilaya ya Longido mara baada ya uzinduzi wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi ya Shikinzi wilayani Longido.

BARRICK NORTH MARA, JUMUIYA YA WATUMIA MAJI WAFANIKISHA UPANDAJI MITI 47,200 KUHIFADHI MTO TIGHITE

September 13, 2026 Add Comment

 


Sehemu ya viongozi na wafanyakazi wa Barrick North Mara (kulia), viongozi wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini na Kijiji cha Matongo wakikagua maendeleo ya mradi huo Siku ya Mazingira Duniani 2026. (Picha za Maktaba)
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini, Mwita Seri, akiwa kwenye kitalu cha miche ya asili inayooteshwa kwa ajili ya kupandwa kandokando ya Mto Tighite.
Ushirikiano wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite (JWMT) na Kampuni ya Barrick kupitia Mgodi wake wa dhahabu wa North Mara umefanikisha upandaji wa miti ya asili 47,2000 kati ya 50,000 ambao utasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kulinda chanzo hicho cha maji kinachotegemewa katika shughuli mbalimbali za ustawi wa jamii na utunzaji wa mazingira.

RAIS MSTAAFU DKT KIKWETE AANZA ZIARA YA MIRADI YA JAMII SALAMA WILAYA YA SIKONGE TABORA

September 13, 2026 Add Comment




Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, akiongea na uongozi wa Tabora baada ya kuwasili mkoani humo  Septemba 12, 2026 kwa ziara ya siku tatu.

………….

Septemba 13, 2026, Dkt Kikwete anaanza ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Jamii Salama katika Wilaya ya Sikonge, mkoani Tabora.

Kabla ya kukagua zahanati mpya na nyumba mbili za watumishi, Dkt Kikwete atatembelea kliniki tembezi katika Kitongoji cha Ipembe, Kata ya Kiloli, Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, ili kujionea huduma zinazotolewa kwa wananchi wa maeneo ya pembezoni.

Mradi huo unatekelezwa na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF), kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais–TAMISEMI, Wizara ya Afya na mamlaka za Mkoa wa Tabora. Ushirikiano huo umefanikisha ujenzi wa zahanati mbili za kisasa na nyumba nne za watumishi katika wilaya za Sikonge na Uyui.

Dkt Kikwete, Muasisi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya JMKF, atakagua namna uwekezaji huo utakavyorahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa zaidi ya wakazi 36,000 wa vijiji hivyo na maeneo jirani.

Kesho, Septemba 14, atatembelea kliniki tembezi, zahanati mpya na nyumba mbili za watumishi katika Kijiji cha Gengesita, Kata ya Kizengi, Wilaya ya Uyui.

Mradi umefadhiliwa na S. C. Johnson & Son, Inc. ya Marekani, inayounga mkono afya, ustawi wa familia na mapambano dhidi ya malaria duniani, hasa katika jamii zenye changamoto za kufikiwa kirahisi.


MANARA: AWESO CUP INA DOUMBIA WENGI

September 13, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, PANGANI

MSEMAJI wa Timu za Taifa za Tanzania, Haji Manara, amesema mashindano ya Aweso Cup 2026 yameibua vipaji vingi vya soka ambavyo kwa uwezo wake vinaweza kuizidi hata thamani ya mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Doumbia.

Manara alitoa kauli hiyo wakati akizungumza katika uzinduzi rasmi wa michuano hiyo uliofanyika katika Uwanja wa Sakura, Pangani, Mkoa wa Tanga, akisisitiza kuwa Tanzania ina hazina kubwa ya vipaji vinavyohitaji kuibuliwa na kuendelezwa.

Kwa utani ulioibua shangwe na vicheko kutoka kwa mashabiki waliohudhuria uzinduzi huo, Manara alisema kiwango cha baadhi ya wachezaji alichokiona katika michuano hiyo kinaonyesha kuwa Pangani inaweza kuwa chanzo cha wachezaji wengi wenye uwezo wa kucheza soka la juu.

“Huyu Doumbia wa Simba anaweza kupatikana mara tano ndani ya michuano hii. Tumeshuhudia vipaji vikubwa sana hapa Pangani,” alisema Manara.

Kauli hiyo aliitoa huku akitumia fursa hiyo kuwataka wadau wa soka nchini kuendelea kuwekeza katika vipaji vya ndani badala ya kutegemea zaidi usajili wa wachezaji kutoka nje ya nchi.

Alisema Tanzania ina vijana wengi wenye uwezo mkubwa ambao wakipewa nafasi, mafunzo na mazingira mazuri wanaweza kufikia viwango vya juu na kuwa sehemu ya mafanikio ya soka la Taifa.

“Wakati mwingine badala ya kuwekeza kutafuta vipaji nje, tuna vipaji bora zaidi ndani ya Tanzania. Tusiishie tu kutafuta wachezaji nje, hata nyumbani hapa Pangani tumeona mechi zimechangamka,” alisema.

Manara, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kariakoo, alisema idadi kubwa ya timu zinazoshiriki Aweso Cup ni ishara kwamba eneo hilo lina msingi mzuri wa kukuza vipaji vya soka.

Alisema kuwepo kwa takribani timu 80 katika jimbo moja la uchaguzi kunapaswa kuwa chachu kwa viongozi na wadau wa michezo kuangalia namna ya kuviendeleza vipaji hivyo kwa ajili ya soka la baadaye.

Katika hotuba yake, Manara pia alikumbusha historia ya Pangani katika kuzalisha wachezaji wenye majina makubwa, akimtaja nyota wa zamani wa Yanga, Fadili Bwanga, ambaye aliwahi kucheza soka la kulipwa nje ya nchi.

Michuano ya Aweso Cup 2026 imeandaliwa chini ya usimamizi wa Mbunge wa Pangani ambaye pia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, ikiwa na lengo la kuibua na kukuza vipaji vya soka katika jimbo hilo.

Mashindano hayo yalizinduliwa rasmi na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma ‘MwanaFA’, katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na mashabiki wa soka.

Manara alimpongeza Aweso kwa kuandaa mashindano hayo na kusema hatua hiyo ni muhimu katika kuwapa vijana nafasi ya kuonyesha vipaji vyao.

Aidha, aliahidi kuendelea kufuatilia michuano hiyo hadi hatua ya fainali.

PROF. SHEMDOE AONGOZA VIONGOZI OWM–TAMISEMI KUMFARIJI RAIS SAMIA KUFUATIA KIFO CHA MUMEWE, MAALIM HAFIDH AMEIR HASSAN

September 13, 2026 Add Comment


 Picha mbalimbali za viongozi wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, walipofika nyumbani kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, kumfariji kufuatia msiba wa kuondokewa na Mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.

Viongozi wengine walioambatana na Mhe. Waziri Prof. Shemdoe kumfariji Mheshimiwa Rais ni Naibu Katibu Mkuu OWM–TAMISEMI, Bw. Sospeter Mtwale, na Naibu Katibu Mkuu OWM–TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila.

Katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI inamtakia Mheshimiwa Rais afya njema, subira, faraja na utulivu, na inawatakia wafiwa wote moyo wa kustahimili majonzi ya kumpoteza mpendwa wao.

TUME YA TAIFA YA UNESCO YAUNGANA NA RAIS DKT.SAMIA KATIKA KIPINDI CHA MAOMBOLEZO

September 12, 2026 Add Comment


Kizimkazi, Kusini Unguja — Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Hamisi Masanja Malebo, ameungana na viongozi wengine wa Wizara katika kumtembelea na kumpa pole Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 11 Septemba 2026 nyumbani kwa Rais Samia, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo ujumbe huo ulifika kutoa pole na faraja kwa Rais pamoja na familia yake katika kipindi hiki cha maombolezo.

Prof. Malebo, akiwa sehemu ya ujumbe huo wa viongozi, aliungana na viongozi wengine wa Wizara kuwasilisha salamu za pole kwa Rais Samia na familia yake kufuatia msiba wa Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia tarehe 7 Septemba 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar.

Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaungana na Rais Samia, familia, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huo katika kipindi hiki cha huzuni na maombolezo.

Tume inatoa pole kwa Rais Samia na familia yake, huku ikiwaombea nguvu, faraja na moyo wa subira katika kipindi hiki cha majonzi.

Tume ya Taifa ya UNESCO inaendelea kuungana na familia katika kuomboleza msiba huo na kuenzi kumbukumbu ya Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.



TANZANIA YAZIDI KUIMARISHA NAFASI YAKE KATIKA BIASHARA YA UMEME KIKANDA

September 12, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Zanzibar


Tanzania imeendelea kuimarisha nafasi yake katika biashara ya umeme kikanda, huku Mradi wa Kuunganisha Gridi za Umeme Tanzania na Zambia ukifikia asilimia 90 ya utekelezaji na kutarajiwa kukamilika Februari 2027, hatua itakayoiunganisha Tanzania na soko la umeme la Kusini mwa Afrika na kuongeza fursa za biashara ya umeme kuvuka mipaka.


Akizungumza, Septemba 11, 2026, katika ufunguzi wa Mkutano wa 67 wa Kamati ya Usimamizi ya Jumuiya ya Umeme ya Kusini mwa Afrika (SAPP), Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini wa Zanzibar, Mhe. Seif Kombo, amesema kuimarisha biashara ya umeme kuvuka mipaka ni muhimu katika kuongeza upatikanaji wa nishati, kuimarisha usalama wa gridi na kupunguza gharama za umeme katika ukanda huo.

Ameeleza kuwa Tanzania, kupitia Serikali na TANESCO, inaendelea kuwekeza katika kuimarisha miunganisho ya gridi, ikiwemo Mradi wa Tanzania-Zambia wa msongo wa kilovoti 400 ambao, utakapokamilika, utaongeza uwezo wa Tanzania kushiriki katika biashara ya umeme ndani ya SAPP.

“Kuimarisha biashara ya umeme kuvuka mipaka kutaziwezesha nchi kutumia kikamilifu rasilimali za nishati zilizopo, kuongeza upatikanaji wa umeme na kuimarisha usalama wa gridi,” amesema Mhe. Kombo.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi ya SAPP, Andrew Etzinger, amesema ushirikiano wa kikanda ni muhimu katika kuimarisha usalama wa nishati, hususan wakati mabadiliko ya tabianchi, ukame na matukio ya hali ya hewa yanapoendelea kuathiri mifumo ya uzalishaji wa umeme.

Amesema kukamilika kwa muunganisho wa Tanzania na Zambia kutakuwa hatua muhimu katika kuunganisha SAPP na Jumuiya ya Biashara ya Umeme Mashariki mwa Afrika (EAPP), hivyo kupanua wigo wa ushirikiano na biashara ya umeme kati ya nchi za Afrika Mashariki na Kusini.



Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Usafirishaji Umeme wa TANESCO, Mha. Zakaria Mgalama, amesema mkutano huo umetoa fursa kwa nchi wanachama na wadau wa sekta ya umeme kujadili namna ya kuimarisha biashara ya umeme, miundombinu na usalama wa nishati katika ukanda huo.



“Kwa Tanzania, kukamilika kwa Mradi wa Tanzania-Zambia kutakuwa hatua muhimu katika kuongeza uwezo wa nchi kushiriki kikamilifu katika biashara ya umeme ya kikanda, ikiwemo kuuza umeme katika masoko ya nchi wanachama wa SAPP,” amesema Mha. Mgalama.


Muunganisho huo pia utaimarisha nafasi ya Tanzania katika mtandao mpana wa biashara ya umeme unaounganisha Afrika Mashariki na Kusini, na kuongeza fursa za matumizi bora ya uwezo wa uzalishaji na miundombinu ya umeme iliyopo.


Mikutano ya 67 ya SAPP, iliyofanyika Zanzibar kuanzia Septemba 7 hadi 11, 2026, imejadili masuala ya mipango ya mifumo ya umeme, miundombinu ya usafirishaji, biashara ya umeme na hatua za kuimarisha usalama wa nishati katika ukanda wa Kusini mwa Afrika.

DC RUKIA AWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHARI ZA MVUA ZA EL NIÑO

September 12, 2026 Add Comment


Wananchi wa Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro, wametakiwa kuchukua tahadhari dhidi ya uwezekano wa kunyesha kwa mvua kubwa katika kipindi kijacho kufuatia taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuhusu mwenendo wa hali ya hewa na uwezekano wa mvua za El Niño.


Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Mhe. Rukia Zuberi ambapo amesema wananchi wanaoishi katika maeneo hatarishi, yakiwemo mabondeni, maeneo ya jirani milima au mito, pamoja na maeneo yenye uwezekano wa kukumbwa na mafuriko au maporomoko ya ardhi, wanashauriwa kuchukua hatua tahadhari mapema, ikiwemo kuhama maeneo hayo, kuweka akiba ya chakula na mahitaji muhimu kwa matumizi wakati wa mvua hizo.

Pia amewahimiza wananchi kuhakikisha kuwa mitaro, mifereji na njia za maji zinakuwa safi na hazijazibwa na taka, ili kuwezesha maji kupita kwa urahisi hatua inayolenga kupunguza uwezekano wa maji kujaa katika maeneo ya makazi, kusababisha mafuriko na uharibifu wa mali na kuhatarisha maisha ya watu.

Kuhusu watoto, wazazi na walezi wametakiwa kuwa waangalifu na kutowaruhusu kwenda shuleni wakati mvua zinapokuwa kubwa na mazingira yakiwa hatarishi huk, viongozi katika maeneo mbalimbali wakielekezwa kusimamia utekelezaji wa tahadhari hizo, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha usafi wa njia za maji unafanyika kwa wakati.

TMA imesema mvua hizo zinatarajiwa kuanza kunyesha kuanzia mwishoni mwa Septemba 2026 na kuendelea hadi Januari 2027, Wananchi wa Mwanga wametakiwa kuendelea kufuatilia taarifa rasmi kutoka TMA na Serikali, pamoja na kuzingatia maelekezo yatakayotolewa ili kupunguza madhara yanayoweza kusababishwa na mvua hizo.


 

BRIDGE TANZANIA YAUNGANISHA ELIMU,UJUZI NA FURSA ZA KIUCHUMI KWA VIJANA GEITA

September 12, 2026 Add Comment



GEITA: Kwa vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu, kukosa ajira si lazima kuwe na maana ya kukosa kabisa fursa za kufanya kazi; wakati mwingine changamoto kubwa ni kukosa maarifa na ujuzi unaowawezesha kuzitambua na kuzitumia fursa zilizopo.

Hilo ndilo linalolenga kushughulikiwa na Mradi wa BRIDGE Tanzania, unaotekelezwa na Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini, kwa kuwapatia vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu elimu ya msingi na ujuzi wa vitendo unaoweza kuwawezesha kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kiuchumi.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, vijana 210 tayari wamepatiwa mafunzo kupitia mradi huo, huku baadhi yao wakianza kutumia ujuzi walioupata katika uzalishaji wa bidhaa mbalimbali, zikiwemo sabuni za miche, sabuni za maji na vyakula vya mifugo.


Mafunzo hayo pia yanahusisha kusoma, kuandika, kuhesabu na ujasiriamali, yakilenga kuwajengea vijana uwezo unaoweza kutumika katika maisha yao na katika mazingira ya soko.

Akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya (District Steering Committee) ya Mradi wa BRIDGE Tanzania kilichofanyika Nzera, Geita, Mratibu Msaidizi wa Kitaifa wa mradi huo, Adriano Adrian Hyera, alisema hadi sasa vijana 210 katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita wamepatiwa mafunzo.

Alisema mradi huo unaweka mkazo katika kuwapa vijana fursa ya kupata maarifa na ujuzi ambao unaweza kuwasaidia kujenga uwezo wa kujitegemea.


“Lengo si kuwapa vijana mafunzo pekee, bali kuwajengea uwezo ambao wataweza kuutumia baada ya mafunzo ili kujipatia kipato na kujitegemea,” alisema Hyera.

Kwa mujibu wa muundo wa mradi, vijana ambao hawakupata fursa ya kukamilisha elimu ya msingi hupewa nafasi ya kujenga uwezo katika kusoma, kuandika na kuhesabu, kabla ya kuendelea na mafunzo ya ujuzi wa vitendo unaoendana na mazingira yao na fursa zinazopatikana katika soko.

Mtazamo huo unaweka msisitizo katika kuunganisha elimu na ujuzi wa vitendo, ili kijana anapomaliza mafunzo asiishie kuwa na maarifa ya darasani pekee, bali awe na uwezo wa kutumia ujuzi huo katika shughuli za uzalishaji na kujiajiri.

Katika utekelezaji wake Geita, mradi unawawezesha vijana kujifunza kwa vitendo na pia unatoa vifaa na mahitaji muhimu kwa ajili ya mafunzo, ili kuwapa nafasi ya kufanya mazoezi ya uzalishaji wakati wa kujifunza.

Baadhi ya vijana walionufaika na programu hiyo wamesema mafunzo yamewajengea uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji na kuwapa mtazamo mpya kuhusu namna wanavyoweza kutumia ujuzi wao kama njia ya kujipatia kipato.

Ujuzi huo unawapa pia nafasi ya kutengeneza bidhaa ambazo zinaweza kutumika katika jamii na, kwa kuzingatia ubora na mahitaji ya soko, kuwa sehemu ya shughuli zao za kiuchumi.

Kutoka elimu ya msingi hadi ujuzi wa soko

Kwa mtazamo wa mradi, elimu na ujuzi haviwekwi katika maeneo mawili tofauti, bali vinaunganishwa ili kumjengea kijana uwezo wa kutumia maarifa yake katika mazingira halisi.

Baada ya kujenga msingi wa kusoma, kuandika na kuhesabu, kijana hupewa ujuzi wa vitendo unaozingatia eneo analotoka na fursa zinazopatikana katika soko.

Hii inalenga kuwapa vijana ambao hawakumaliza elimu rasmi nafasi ya kupata ujuzi unaoweza kuwasaidia kushindana katika shughuli za kiuchumi pamoja na vijana wengine waliopitia njia rasmi za elimu na mafunzo ya ufundi.

Kwa maana hiyo, BRIDGE Tanzania inalenga kujenga daraja kati ya elimu, ujuzi na soko, badala ya kuishia katika utoaji wa mafunzo pekee.

Vijana wahimizwa kutumia fursa za mikopo

Akizungumzia hatua zinazofuata baada ya mafunzo, Hyera aliwashauri vijana kujiunga katika vikundi vya watu watano ili waweze kuchangamkia fursa za mikopo zinazotolewa na Halmashauri.

Alisema ushiriki katika vikundi unaweza kuwasaidia vijana kutumia ujuzi walioupata katika shughuli za kiuchumi na kutafuta fursa za kukuza shughuli zao.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa mafunzo wanayopata vijana yanaunganishwa na fursa za mitaji na uzalishaji, ili kuongeza uwezekano wa ujuzi huo kuleta matokeo katika maisha yao.

Majaribio yenye matarajio ya kupanuka

BRIDGE Tanzania ni mpango wa majaribio unaotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Kaskazini A Unguja.

Mradi una lengo la kuwafikia vijana 3,000 katika kipindi cha miaka mitano, sawa na takribani vijana 600 kila mwaka.

Majaribio hayo yanatoa nafasi ya kutathmini namna ya kuwaunganisha vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu na elimu ya msingi, ujuzi wa vitendo na fursa za kiuchumi.

Matokeo na uzoefu unaopatikana katika maeneo ya utekelezaji utasaidia katika kutathmini namna mfumo huo unavyoweza kuimarishwa na, baada ya tathmini, kupanuliwa katika maeneo mengine nchini.

Tume ya UNESCO katika utekelezaji

Utekelezaji wa BRIDGE Tanzania unaenda sambamba na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kuwawezesha vijana kupata maarifa, ujuzi na fursa za kushiriki katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya Taifa.

Kupitia Tume ya Taifa ya UNESCO, ushirikiano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Korea Kusini umegeuzwa kuwa fursa ya kuwafikia vijana ambao kwa sababu mbalimbali hawapo katika mfumo rasmi wa elimu.

Tume ya Taifa ya UNESCO, kwa jukumu lake la kuratibu, kutathmini na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za UNESCO nchini, inaendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kuhakikisha programu zinazotekelezwa zinachangia mahitaji na vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania.

Kwa BRIDGE Tanzania, msisitizo ni kuhakikisha kijana aliye nje ya mfumo rasmi hapotezi fursa ya kujenga uwezo. Badala yake, anapewa nafasi ya kujifunza, kupata ujuzi na kuutumia katika kujenga maisha yake.

Kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wilaya kilichofanyika Nzera, Geita, kilitoa nafasi kwa wadau kupitia utekelezaji wa mradi, mafanikio, changamoto na hatua zinazoweza kuchukuliwa ili kuongeza manufaa yake kwa vijana.

Kwa vijana hao 210 wa Geita, safari inaanzia katika kujenga msingi wa elimu na ujuzi; lakini lengo kubwa ni kuwawezesha kutumia uwezo huo katika ulimwengu halisi wa kazi, uzalishaji na kujitegemea. https://www.instagram.com/reel/DczGOqpqA74/?igsi=ZHVqMjQwemwyYTU=

JUMUIYA YA MARIDHIANO NA AMANI YAMFARIJI RAIS SAMIA

September 12, 2026 Add Comment

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa Salumu, akiongoza ujumbe wa jumuiya hiyo kumfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 11 Septemba 2026, kufuatia kufiwa na mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar, tarehe 7 Septemba 2026.

WIZARA, RUWASA ZASAINI MIKATABA YA UTENDAJI KUFIKIA VIJIJI 1,575

September 12, 2026 Add Comment
WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, ameshiriki utiaji saini mikataba ya kiutendaji kati ya Wizara ya Maji na Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), hatua inayolenga kubadili utendaji kutoka mazoea hadi mfumo unaopimika na wenye uwajibikaji.

RUWASA WAKABIDHIWA CHETI CHA ITHIBATI ISO 9001:2015

September 12, 2026 Add Comment
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) imekabidhi cheti cha ubora wa huduma kwa wakala wa maji na usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ikiwa ni Ishara ya utoaji huduma bora ya maji nchini.

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ATEMBELEA KIWANJA CHA UJENZI WA VIWANGO HOUSE ARUSHA

September 12, 2026 Add Comment
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb), ametembelea kiwanja kinachotarajiwa kujengwa Viwango House eneo la Mateves, Mkoani Arusha.

WANAFUNZI 150 WA KITANZANIA KUNUFAIKA NA FURSA YA ELIMU YA JUU ALGERIA

September 11, 2026 Add Comment

    



Balozi wa Tanzania Nchini Algeria, Mobhare Matinyi
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda
***
Tanzania imepata nafasi 150 za ufadhili wa masomo ya elimu ya juu nchini Algeria kwa mwaka 2026, zikilenga wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya sayansi.

KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA MRADI WA UMEME IGANJO-SAZA

September 11, 2026 Add Comment


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa hatua ya kuanza kutekeleza Mradi wa Ujenzi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovoti 220 kutoka Iganjo mkoani Mbeya hadi Saza mkoani Songwe, akisema mradi huo utakuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi.


Mhe. Mgalu amesema hayo tarehe 11 Septemba 2026 katika eneo la Saza, Mkwajuni, Wilaya ya Songwe, Mkoa wa Songwe, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi huo.

Amesema Kamati inaamini kukamilika kwa mradi huo kutachochea shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii, ikiwemo uchimbaji wa madini, kilimo na biashara, sambamba na kuongeza fursa za ajira na kipato kwa wananchi katika maeneo yatakayonufaika na mradi huo.

Mhe. Mgalu amesema Kamati imeendelea kuhimiza utekelezaji wa miradi ya umeme inayolenga kuchochea shughuli za uzalishaji katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo maeneo yenye shughuli za uchimbaji wa madini.

Ameeleza kuwa Kamati iliielekeza Wizara kuhakikisha umeme wa uhakika unafikishwa katika maeneo ya wachimbaji wa madini ili kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ufanisi katika shughuli zao, jambo ambalo Wizara ya Nishati imeendelea kulifanyia kazi.

Aidha, Mhe. Mgalu ameishauri Wizara kuangalia uwezekano wa kufikisha umeme wa uhakika mapema  katika mkoa huo kupitia miradi mbalimbali wakati wananchi wakiendelea kusubiri Mradi wa Iganjo–Saza unaotarajiwa kutekelezwa kwa kipindi cha miezi 18.


Kuhusu ushauri huo,  Serikali  tayari ilianza  kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kutekeleza mradi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Mwakibete-Mbeya kuelekea Wilaya ya Songwe, ambao unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu.