HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
TEA NA UNICEF WATEKELEZA MRADI WA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1 WA UJENZI WA VITUO 10 VYA ELIMU YA AWALI YA UFUNDI
habariWAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI
Nishati
Na Mwandishi Wetu - Tunduru, Ruvuma
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameonesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Songea hadi Masasi kupitia Tunduru na kuagiza mkandarasi kuongeza juhudi ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati uliopangwa.
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya mradi huo leo Julai 22, 2026, Mhe. Ndejembi amesema Serikali haitakuwa tayari kuona miradi ya kimkakati inayogusa maisha ya wananchi ikicheleweshwa bila sababu za msingi.

Amesema mradi huo ni miongoni mwa miradi muhimu ya Sekta ya Nishati inayopewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutokana na mchango wake katika kuimarisha upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Kusini.

“Maendeleo ya mradi huu hayaridhishi ukilinganisha na muda uliopita tangu utekelezaji wake uanze. Serikali inatarajia kuona kasi kubwa zaidi ya utekelezaji katika kipindi kilichobaki. Nimemuagiza Katibu Mkuu kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maelekezo haya na kuhakikisha hatua stahiki zinachukuliwa iwapo hakutakuwa na maboresho yanayoonekana,” amesema Mhe. Ndejembi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mhe. Boniface Magiri, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, amesema Mkoa utaendelea kushirikiana na Serikali Kuu katika kufuatilia utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha unakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi kwa wakati.

Naye Mhe. Sikudhani Chikambo kwa niaba ya wabunge wa Mkoa wa Ruvuma, viongozi hao wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya umeme ambayo itachochea ukuaji wa uchumi, uwekezaji na kuboresha huduma za kijamii katika maeneo ya Kusini mwa Tanzania.

Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa msongo wa kilovoti 220 kutoka Songea kupitia Tunduru hadi Masasi unatekelezwa na Mkandarasi Kalpataru Power kutoka India. Mradi huo unatarajiwa kuiunganisha Mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye Gridi ya Taifa pamoja na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Wilaya ya Tunduru na maeneo jirani.


HUKUMU YA TIKTOKER GHANA -SOMO KWA UHURU WA KUJIELEZA NA WAJIBU WA WATUMIAJI WA MITANDAO
Hivi karibuni, Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Accra ilimuhukumu Camilla Alhassan, mshawishi maarufu wa TikTok (Tiktoker), kifungo cha mwaka mmoja jerezani. Adhabu hii ilitolewa baada ya mshtakiwa kukiri makosa ya kusambaza taarifa za uongo na kufanya tabia ya kuudhi (offensive conduct) dhidi ya Rais John Dramani Mahama.
Kesi hii inaashiria hatua kubwa katika udhibiti wa maudhui ya kidijitali barani Afrika na inaibua maswali muhimu kuhusu mipaka ya uhuru wa kujieleza na wajibu wa kisheria wa watumiaji wa mitandao ya kijamii.
Hukumu dhidi ya Alhassan inasimama juu ya *misingi miwili mikuu* ya kisheria inayolenga kulinda usalama wa jamii na sifa za watu
Mosi, Kusambaza Taarifa za Uongo (False News) - Sheria za Ghana zinakataza utengenezaji au usambazaji wa taarifa ambazo mtengenezaji anajua au ana sababu ya kuamini kuwa ni za uongo, hususan kama zinaweza kusababisha hofu au taharuki miongoni mwa jamii.
Pili, Tabia ya Kuudhi (Offensive Conduct) - Matumizi ya lugha au madai yanayolenga kudhalilisha, kuchochea chuki, au kuhatarisha amani ya umma—katika muktadha huu, kumhusisha kiongozi wa nchi na matendo ya ushirikina na kafara ya wanyama kwa malengo ya kisiasa.
Sakata hili linaangazia athari kubwa za mitandao ya kijamii katika nyanja za siasa na utulivu wa kijamii:-
*Mmomonyoko wa Imani ya Kisiasa:* Kudai kuwa Rais alifanya matambiko kwa kuzika ng'ombe 32 nchi nzima kulilenga kuchafua sifa yake na kupunguza uaminifu wake mbele ya wapiga kura, jambo linaloweza kuathiri mchakato wa kidemokrasia.
*Silaha ya Algorithm na Ushawishi:* Kama "Tiktoker," Alhassan alitumia nguvu ya ushawishi wake (clout) kupata watazamaji wengi. Katika zama za kidijitali, taarifa za kusisimua na za uzushi husambaa haraka kuliko ukweli, jambo linalofanya madhara yake kuwa makubwa na ya haraka.
*MAANA YA HUKUMU HII KWA MUSTAKABALI WA KIDIJITALI (IMPLICATIONS)*
Uamuzi wa Jaji kukataa ombi la mawakili wa Alhassan la kupunguza adhabu una ujumbe mzito
Mahakama imeweka wazi kuwa umaarufu wa mtandaoni (social media fame) sio ngao dhidi ya sheria. Kifungo hiki kinatumika kama onyo kwa waundaji wengine wa maudhui (content creators) kuwa uhuru wa kujieleza unaambatana na wajibu.
Aidha, Kesi hii inaongeza msukumo kwa serikali za Kiafrika kuimarisha mifumo ya kufuatilia na kuchukua hatua dhidi ya uhalifu wa kimtandao (cybercrime).
*USHAURI WANGU*
Hukumu ya Camilla Alhassan ni kielelezo cha namna mifumo ya sheria inavyolazimika kubadilika ili kukabiliana na changamoto mpya zinazoletwa na teknolojia.
Wakati mitandao ya kijamii ikiendelea kuwa jukwaa kuu la mijadala ya umma, kesi hii inakumbusha jamii kuwa maneno yana madhara ya kisheria, na kwamba ulimwengu wa kidijitali unapaswa kuongozwa na ukweli, maadili, na heshima kwa utu wa wengine.
Kama Tanzania Tuna paswa kuchukua hatua za wazi kwa wahalifu wa mitandao na kama nilivyo shauri mara zote tunaweza kupitia hatua tatu ili tuweze kukuza uelewa kwa wananchi na hatimae watakao kaidi zaidi tuwawajibishe kwa mujibu wa sheria za nchi
*Hatua ya Kwanza :* Wahalifu wakwamatwe na kwa uwazi watangazwe na kuonywa kisha waachiwe - Hii itakua somo kwa wengine ambao wana kawaida ya kufata mkumbo kwenye kutenda uhalifu wa kimtandao na wakidhani serikali imelala
*Hatua Ya Pili:* Mhalifu anapo rudia akamatwe tena kwa uwazi na kulipishwa faini kwa mujibu wa sheria zetu - Pesa zitakazo patikana kwneye hili ziwekwe kwenye mfuko maalum utakao saidia kuimarisha udhibiti wa uhalifu mtandao kupitia elimu ya uelewa na nyezo nyingine za udhibiti
*Hatua ya tatu:* Mhalifu anapo rudia mara ya tatu kunakua hakuna tena namna ila ni kufungwa kwa mujibu wa sheria za nchi yetu na hili liwe somo kwa wengine wote.
Naomba kuwasilisha.
*Yusuph Kileo ,*
Mtaalam wa usalama mtandao na Uchunguzio wa makosa ya Kidigitali
Dar Es Salaam, Tnazania
19 - July - 2026.
CCM YATHIBITISHA MSINGI WA KUHUDUMIA WANANCHI KWA VYAMA TAWALA AFRIKA
CCM
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdalla Hamid , ameshiriki Mkutano Mkuu wa Chama cha Botswana National Front (BNF) unaofanyika mjini Jwaneng, Botswana, akiwakilisha Chama Cha Mapinduzi.
Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Rabia amesisitiza kuwa kila chama tawala kina wajibu wa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu, kuimarisha misingi ya utawala bora, na kuendelea kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wananchi bila kuchoka.
Aidha, amekisii Chama cha BNF kuendelea kuzingatia maslahi ya wananchi katika utekelezaji wa sera na maamuzi yake, pamoja na kuhakikisha kuwa hakuna mwananchi anayebaki nyuma katika mchakato wa maendeleo ya taifa.
Aidha,Ndg. Rabia amempongeza Rais wa Chama cha Botswana National Front (BNF) na Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Duma Gideon Boko kwa ushindi wa Chama chake na kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Jamhuri ya Botswana.
Ameeleza kuwa kuchaguliwa kwa Rais Boko na Chama cha BNF ni kielelezo cha imani waliyopewa na wananchi wa Botswana na amewatakia mafanikio katika kuwaletea maendeleo na ustawi wao.
DC NYAMWESE AWATAKA WAKURUGENZI KUSIMAMIA FEDHA ZA SERIKALI KWA UADILIFU
habari
Na Oscar Assenga, Tanga
TANZANIA MGENI RASMI MAONESHO YA UFUGAJI NYUKI AFRIKA NCHINI ALGERIA
habari
Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe Mobhare Matinyi, akizungumza na vyombo vya habari vya Algeria wakati akitangaza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekubali mwaliko wa kuwa mgeni rasmi katika Maonesho ya Ufugaji wa Nyuki barani Afrika (Africa Bee Expo) yatakayofunguliwa jijini Algiers mnamo Septemba 3, 2026.WAZIRI SANGU: BONDE LA ZIWA RUKWA NI HAZINA YA AJIRA KWA VIJANA
habariNEWALA KUNUFAIKA NA UMEME WA UHAKIKA
habari📌*Ni baada ya kukamilika kwa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 33 Masasi - Mtwara*
📌*Mradi umeimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa Wilaya ya Newala na maeneo jirani.*
📌*MD Twange asema thamani ya mradi ni takribani shilingi bilioni 4.65*
📍Newala, Mtwara | Julai 22, 2026
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amezindua rasmi mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 33 kutoka Masasi hadi Newala, akieleza kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi na kuweka mazingira wezeshi kwa ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika Wilaya ya Newala.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa njia hiyo, Mhe. Ndejembi amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kuwekeza katika miradi ya kimkakati ya umeme ili kuhakikisha huduma ya nishati inawafikia wananchi wengi zaidi na kuwa chachu ya maendeleo.
"Njia hii ya umeme ni msingi wa kukuza uchumi, kuongeza uzalishaji, kuvutia uwekezaji na kuboresha upatikanaji wa umeme kwa Wilaya ya Newala," amesema Mhe. Ndejembi.
Aidha, Waziri Ndejembi amesema Serikali itaendelea kuhakikisha Mikoa ya Lindi na Mtwara inapata umeme wa uhakika ikiwa ni pamoja na kuiunganisha Mikoa hiyo na umeme wa gridi ya Taifa.
Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Newala, Mhe. Mwangi Kundya amesema miradi mbalimbali imeendelea kutekelezwa Mkoa wa Mtwara.
"Mheshimiwa Waziri niipongeze Serikali kwani Vijiji vyote vya Mkoa wa Mtwara 785 vinapata huduma ya umeme". Amesema Mhe. Mwangi.
Ameongeza kuwa katika kuboresha huduma kwa wateja mkoa wa Mtwara umepokea vitendea kazi yakiwemo magari kumi na moja, bajaji nne na pikipiki tisa.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema Serikali imekuwa ikiboresha uwekezaji na upatikanaji wa umeme Mikoa ya Mtwara na Lindi.
"Mahitaji ya Lindi na Mtwara yameendelea kuongezeka na Serikali imewekeza kwenye uzalishaji na hivi sasa Mkoa wa Mtwara tunazalisha zaidi ya megawati 50". Amesema Mha. Mramba.
Awali akitoa taarifa za utekelezaji wa mradi Mkurugenzi Mtendaji TANESCO, Bw. Lazaro Twange amesema ujenzi wa njia hiyo umetekelezwa kwa shilingi bilioni 4.56 kwa umbali wa Kilometa 76 kutoka Masasi hadi Newala.
"Mheshimiwa mgeni rasmi kabla ya mradi huu kutekelezwa Wilaya ya Newala ilikuwa ikipata umeme kutokea Mtwara kupitia Nanyumbu umbali wa kilometa 170, hali iliyochangia tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara". Amesema Bw. Twange.
Ameongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa njia hiyo ya umeme kumeimarisha upatikanaji wa umeme na kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme kwa Wilaya hiyo.
Aidha, Serikali kupitia TANESCO imetenga takribani shilingi bilioni 5.27 kwa ajili ya kujenga kituo cha kubadilishia umeme (Switching Station) kitakacho saidia kuboresha upatikanaji wa umeme na kukidhi mahitaji ya sasa na ya badaye ya wananchi na wawekezaji wa Wilaya ya Newala.
Mbunge wa Newala Vijijini Dkt. Yahaya Nawanda kwa niaba ya Wabunge wa Mkoa wa Mtwara ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme Mkoa wa Mtwara.


































