HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

BRELA YASUKUMA MAGEUZI YA KIDIGITALI KATIKA BIASHARA

BRELA YASUKUMA MAGEUZI YA KIDIGITALI KATIKA BIASHARA

April 15, 2026 Add Comment

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

...

VIJANA nchini Tanzania wanaendelea kurasimisha shughuli zao za biashara kwa kasi, hali inayoashiria kuongezeka kwa ushiriki wao katika uchumi rasmi na mchango wao katika juhudi za maendeleo ya taifa.

Hayo yameelezwa leo Aprili 15,2026 na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw.Godfrey Nyaisa, wakati wa Semina kwa madiwani wa halmashauri ya Dodoma .

Bw.Nyaisa amesema takwimu za BRELA zinaonesha kuwa maelfu ya kampuni, majina ya biashara na alama za biashara na huduma (trade and service marks) zilizosajiliwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita zinamilikiwa na vijana. Hali hii inaonesha wazi kuongezeka kwa mchango wa vijana katika sekta za viwanda na biashara nchini.

"Kampuni 5,045 zimesajiliwa, ambapo 3,120 zinamilikiwa na vijana. Aidha, majina ya biashara 8,792 yamesajiliwa, kati ya hayo 4,938 ni ya vijana. Kwa upande wa alama za biashara, jumla ya 1,018 zimesajiliwa, nyingi zikiwa zinamilikiwa na vijana. Vilevile, leseni za biashara daraja la “A” 5,430 zimetolewa, ambapo takribani nusu yake zimekwenda kwa vijana."amesema Bw.Nyaisa

Amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo madiwani kuhusu taratibu za usajili wa biashara, utoaji wa leseni pamoja na ulinzi wa haki miliki, ili waweze kuwasaidia wafanyabiashara katika kata zao kwa ufanisi zaidi.

Hata hivyo amempongeza Meya wa Jiji la Dodoma kwa kushiriki mafunzo hayo, hatua hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya kuboresha mazingira ya biashara katika mji mkuu wa nchi. Pia ametambua mchango wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma chini ya uongozi wa Rosemary Senyamule kwa ushirikiano wake katika kutoa elimu ya biashara na msaada wa kitaalamu.

Ameeleza kuwa mafunzo hayo yanahusisha maeneo muhimu kama usajili wa kampuni, majina ya biashara, alama za biashara, hati miliki (patents), pamoja na utoaji wa leseni za viwanda na leseni za biashara daraja la “A”.

Aidha, amebainisha kuwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, BRELA imefanya maboresho mbalimbali ya kurahisisha mazingira ya kufanya biashara, ikiwemo kuanzisha mifumo ya kidijitali inayowezesha huduma kupatikana mtandaoni kupitia simu za mkononi.

Hata hivyo, Nyaisa ametaja changamoto ya utofauti katika utoaji wa leseni za biashara katika ngazi za serikali za mitaa. Alieleza kuwa baadhi ya wafanyabiashara hupewa leseni daraja la “B” badala ya “A” kimakosa, hali inayosababisha mkanganyiko.

Amewataka madiwani kutumia mafunzo hayo kutatua changamoto hizo na kuwa mabalozi wa kuhamasisha urasimishaji wa biashara, hususan kwa vijana, wanawake na wajasiriamali wadogo.

“Baada ya mafunzo hayo, tunatarajia muwe mabalozi wazuri katika maeneo yenu na kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika ngazi za chini,” amesema.

Kwa upande wake, Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwona Chaula,amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuwajengea uwezo madiwani wanaofanya kazi kwa karibu na wananchi katika ngazi ya msingi. Aliongeza kuwa yatawasaidia kuelewa vyema taratibu za usajili na utoaji wa leseni za biashara ili waweze kuwasaidia wananchi katika shughuli zao za kila siku za kiuchumi.

Mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati mpana wa BRELA wa kujenga uchumi shindani na jumuishi kwa kuongeza ushiriki wa wananchi katika shughuli rasmi za biashara nchini.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe Alimwona Chaula,akizungumza wakati wa  ufunguzi wa mafunzo ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) Bw Godfrey Nyaisa,akitoa ufafanuzi kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakati wa mafunzo kwa madiwani hao juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo 15,2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakisikiliza elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini. Mafunzo haya yamelenga kuwajengea ufahamu juu ya masuala ya urasimishaji biashara ili kuleta chachu za mabadiliko katika Kata wanazoziongoza. Mafunzo hayo yametolewa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Kampuni na Majina ya Biashara Bw Isdor Nkindi, akitoa elimu kwa Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA). Mafunzo hayo yametolewa na BRELA yaliyofanyika leo Aprili 15, 2026 jijini Dodoma

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Paschal Inyasi Chinyele,akichangia mada wakati wa semina ya madiwani wa Halmashauri ya Dodoma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usajili wa Leseni (BRELA) yakilenga kuwajengea elimu juu ya Huduma zitolewazo na BRELA katika kuwezesha biashara nchini yaliyofanyika leo Aprili 15,2026  jijini Dodoma.

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

Madiwani wa Halmashauri ya Dodoma wakichangia mada juu ya Huduma zitolewazo na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuwezesha biashara nchini katika semina iliyoandaliwa na BRELA leo tarehe 15 Aprili, 2026 jijini Dodoma

KATIBU MKUU CCM AKUTANA NA UJUMBE MAALUMU WA JUMUIYA YA MADOLA

April 15, 2026 Add Comment


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Asha-Rose Migiro, leo tarehe 15 Aprili 2026 amefanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Lazarus Chakwera, katika Ofisi za CCM Lumumba, jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yalijikita katika hali ya kisiasa nchini pamoja na matukio ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

Mhe. Chakwera yupo nchini Tanzania kwa ziara maalum katika nafasi yake kama Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Mhe. Shirley Ayorkor Botchwey.

Kikao hicho ni sehemu ya mashauriano yake na wadau mbalimbali wa kitaifa kwa lengo la kubadilishana mawazo kuhusu maendeleo ya kisiasa baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025, pamoja na juhudi zinazoendelea za kuimarisha amani, demokrasia na mshikamano wa kitaifa nchini Tanzania.








MINISTER KOMBO MEETS TANZANIAN STUDENTS IN MAURITIUS; CALLS FOR DISCIPLINE AND PATRIOTISM

April 14, 2026 Add Comment

      

On 13th April, 2026, the Minister for Foreign Affairs and East African Cooperation, Ambassador Kombo, met and held discussions with Tanzanian students studying in Mauritius, where he used the opportunity to offer important guidance regarding their academic lives and their role as representatives of Tanzania abroad.

TCDC YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA WACHEZAJI

TCDC YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA WACHEZAJI

April 14, 2026 Add Comment

Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) Dkt. Benson Ndiege kushirikiana na Uongozi wa TCDC Sports Club wanunua vifaa vya michezo kwa wachezaji 42 kuelekea mashindano ya Michezo ya Meimosi mjini Njombe.

Vifaa hivyo vimekabidhiwa leo Aprili 14, 2026 jijini Dodoma wakati wa kuwaaga wanamichezo wakielekea mjini Njombe.

Vifaa vilivyonunuliwa ni jezi za mprira wa miguu, viatu, mipira na vifaa vingine vya michezo.

CCM YAPONGEZA KASI YA UJENZI BARABARA YA LAMI KAHAMA - KAKOLA UNAOFADHILIWA NA MIGODI YA BARRICK NCHINI

April 14, 2026 Add Comment

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi ya (CCM) wilayani Kahama mkoani Shinyanga, imepongeza kasi ya Ujenzi wa Barabara ya Kahama-Kakola yenye urefu wa Kilomita 73 Inayojengwa kwa kiwango cha lami kwa Ufadhili Migodi ya Barrick nchini ya Bulyanhulu na North Mara itakayogharimu kiasi cha shilingi bilioni 101.2.Ujenzi wa barabara hii unatekelezwa kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation.

CCM TANGA KUOKOA MILIONI 90 KWA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI

April 14, 2026 Add Comment









Na Oscar Assenga, Tanga

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman amesema mkakati wao wa  ujenzi wa nyumba za watumishi kila wilaya ni hatua itakayosaidia kuokoa kiasi kikubwa cha fedha zilizokuwa zikitumika kulipia pango.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya chama mkoani humo, mwenyekiti huyo alisema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa nyumba hizo, akiwapongeza wadau wote walioshiriki kuchangia mradi huo.

“Kwa ujumla mmefanya kazi kubwa sana. Nawashukuru wadau wote walioshiriki, kwa sababu walichotoa si msaada tu, bali ni uwekezaji ambao utaendelea kuzaa matunda,” alisema.

Alifafanua kuwa kabla ya ujenzi huo, baadhi ya watumishi wa chama walikuwa wakilipa hadi shilingi 200,000 kwa mwezi kwa pango, huku wengine wakilipa zaidi, hali iliyokuwa ikiigharimu CCM kiasi kikubwa cha fedha kwa mwaka.

Alisema kwa makadirio ya haraka, chama kilikuwa kinatumia fedha nyingi kwa mwaka katika wilaya moja kwa ajili ya pango, na endapo wilaya zote za mkoa zitakamilisha ujenzi wa nyumba za watumishi, CCM itaokoa hadi shilingi milioni 90 kwa mwaka.

“Fedha hizi zitasaidia kufanya shughuli nyingine za maendeleo ndani ya chama. Huu ni ubunifu ambao umehimizwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa pamoja na Kamati Kuu,” aliongeza.

Aidha, alisema ujenzi wa nyumba hizo pia unalenga kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wa chama, kwa kuhakikisha wanapata makazi bora na salama baada ya kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Alisisitiza umuhimu wa kuendelea na juhudi hizo ili kuhakikisha miradi yote inakamilika katika mkoa mzima wa Tanga, huku akieleza imani kuwa kwa ushirikiano uliopo, malengo hayo yatafikiwa.

Katika hatua nyingine, mwenyekiti huyo alielekeza kuhakikisha maeneo yote ya chama yanakuwa na hati miliki halali, pamoja na kulindwa kwa kupanda miti ya kivuli na matunda ili kuhifadhi mazingira na kuepusha migogoro ya ardhi.

Aliwataka viongozi wa chama ngazi ya wilaya kuhakikisha wanazingatia sheria za ardhi, ikiwa ni pamoja na kulipa kodi ya pango la ardhi na kufuata taratibu zote za umiliki.

Kwa upande wake, alisisitiza kuwa uwekezaji katika miundombinu ya chama ni muhimu kwa ustawi wa chama hicho,

DCEA YAKAMATA BOTI YA MWENDOKASI IKISAFIRISHA SHEHENA YA MIRUNGI KUTOKA KENYA

April 14, 2026 Add Comment

 

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanikiwa kukamata boti ya mwendokasi iliyokuwa ikisafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi kutoka Mombasa, Kenya kupitia Bagamoyo, mkoani Pwani. 
DC MKUDE AKABIDHI VYOMBO VYA USAFIRI TANESCO MKOA WA ARUSHA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA

DC MKUDE AKABIDHI VYOMBO VYA USAFIRI TANESCO MKOA WA ARUSHA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA

April 14, 2026 Add Comment






*Ni katika muendelezo wa mkakati wa TANESCO wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi.

*Awataka kutumia vyombo hivyo kwa kazi husika za TANESCO.

Na Mwandishi Wetu, Arusha

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mkoani Arusha Mhe. Joseph Mkude amekabidhi vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO Mkoa wa Arusha ili kuimarisha utoaji wa huduma mbalimbali za Shirika kwa wananchi.

Akizungumza tarehe 13, Aprili 2026 wakati wa hafla ya kukakabidhi vitendea kazi hivyo iliyofanyika katika Ofisi za TANESCO Mkoa wa Arusha amesema hatua hiyo ya kukabidhi vitendea kazi hivyo ni hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma za umeme wa uhakika bila vikwazo vyoyote.

Amesema vitendea kazi hivyo vinakwenda kuongeza ufanisi katika utendaji kazi kwa watumishi wa TANESCO katika wilaya za Mkoa wa Arusha na kuwawezesha kutatua changamoto za wateja kwa wakati kwani Magari pamoja na Bajaji zitawawezesha kuyafikia maeno mengi zaidi ili kufikisha huduma ya umeme.

Amewataka Watumishi wa TANESCO Mkoa wa Arusha kuhakikisha wanatumia vyema vitendea kazi hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa na Shirika na wala sio kwa matumizi yao binafisi ambayo hayana faida wala mchango wowote kwa Shirika hasa katika kutoa huduma kwa wananchi.

“Haya Magari tuliyopatiwa katika Mkoa wetu yanakwenda kugawiwa katika kila wilaya naomba yakatumike ipasavyo kwa malengo yaliyokusudiwa, tusitumie Magari haya kwa mambo yetu binafsi yasiyo na tija katika kutoa huduma kwa wananchi”.

Kwa upande wake Meneja wa Huduma za Usalama TANESCO Bw. Lenin Kiobya amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan iliwezesha kununuliwa kwa Magari Makubwa na Madogo zaidi ya 500 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Bw. Kiobya amesema kati ya Magari hayo zaidi ya 500, Malori ya ukubwa mbalimbali ikiwemo tani 10 na tani 7 yapo 215 ambayo yanakwenda kuwa msaada Mkubwa zaidi katika huduma za matengenezo ya umeme kwa wakati hali itakayochangia kuongeza ufanisi wa kazi ndani ya Shirika.

Aidha, amesema kwa Mwaka wa Fedha ujao 2026/2027 Serikali imetenga zaidi ya bilioni 200 ili kununua vitendea kazi hivyo lengo likiwa ni kumaliza kabisa upungufu wa vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO katika maeneo yote nchini.

“Serikali iliwezesha TANESCO kuweza kunua Magari 556 kwa mwaka huu wa fedha 2025/2026 ili kurahisisha utoaji wa huduma ya umeme kwa wananchi, na kwa mwaka ujao wa fedha 2026/ 2027 Serikali imetenga zaidi ya bilioni 200 ili kununua vitendea kazi hivyo lengo likiwa ni kumaliza kabisa upungufu wa vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO”

Meneja wa TANESCO Mkoa wa Arusha Mhandisi Kisika Kisika amesema TANESCO katika Mkoa huo wamepokea vitendea kazi mbalimbali ikiwemo Magari makubwa 2, Gari aina ya Landcruser (4), Bajaji moja (1) vitakavyokwenda kuboresha zaidi huduma kwa wateja katika Mkoa huo.

“Tunaishukuru Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kutupatia vitendea kazi hivi ambavyo kwa sasa tunakwenda kuvitumia kufikisha huduma kwa wananchi kwa haraka zaidi.