HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TANESCO IMEJIPANGA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NINO -MD TWANGE

September 18, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema limejipanga kukabiliana na athari za mvua za El NiƱo kwa kuimarisha miundombinu, kuandaa timu za dharura na kuchukua tahadhari katika mabwawa ya kuzalisha umeme.


Akizungumza katika kipindi cha Aridhio cha TBC, Septemba 17, 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema shirika limefanya tathmini ya miundombinu yake na kubaini maeneo hatarishi.


“Tumefanya kikao na Mamlaka ya Hali ya Hewa na tathmini ya miundombinu yetu, hivyo maeneo hatarishi tunayafahamu na tumeanza kuchukua hatua,” amesema Bw. Twange


Amesema maandalizi hayo yameanza pia katika maeneo mbalimbali, ikiwemo Dar es Salaam, kwa kuimarisha nguzo za umeme zilizoonekana kuwa katika hali ya kuchoka.


“Kama Dar es Salaam tumeanza, kwa ajili ya kurekebisha nguzo za miti ambazo zina dalili ya kuchoka ili tuweze kuweka nguzo nyingine,” ameongeza Bw. Twange.


Aidha, amesema TANESCO imeandaa timu za dharura zitakazoshughulikia changamoto za wateja endapo zitatokea wakati wa mvua hizo.


“Tumeziandaa timu zetu za dharura kwa maana ya _“emergency”_ team zetu kwa maana ya kushughulika wateja wetu watakapokuwa wanatupigia simu,” amethibitisha.


Kwa upande wa mabwawa ya kuzalisha umeme wa maji, amesema TANESCO inafuatilia hali ya maji katika mabwawa yake, huku ikitambua uwezekano wa El NiƱo kusababisha ongezeko kubwa la maji.


“Sisi tuna eneo jingine la vituo vyetu vya kuzalisha umeme wa maji. Mabwawa kama Mwalimu Nyerere, Mtera, Kidatu, Kihansi. Maji kwetu ni huduma muhimu na tunayafurahia kwa ajili ya kuwa na kiwango cha kutosha cha maji kinachotuwezesha kuzalisha umeme,” amesema.


Hata hivyo, amesema maji mengi kupita kawaida yanaweza pia kuwa na madhara kwa wananchi wanaoishi karibu na mabwawa hayo, hivyo TANESCO imeanza kutoa elimu na kuchukua tahadhari.


“Lakini kutokana na El NiƱo huenda tukapata maji mengi kuliko ilivyo kawaida. Na maji yale yanaweza kuleta madhara kwa majirani ambao wanazunguka maeneo ya mabwawa yetu,” ameongeza


“Tumeshaanza kazi kwa kushirikiana na viongozi wa maeneo hayo kutoa elimu kwa wananchi lakini ni sisi wenyewe kuchukua tahadhari ili maji yatakapokuwa mengi basi yasije yakaleta madhara kwa majirani na wananchi walio karibu na mabwawa yetu ya kuzalisha umeme,” ameongeza Twange.


TANESCO imesema itaendelea kuchukua tahadhari na kuimarisha utayari wake kukabiliana na athari za El NiƱo, huku wananchi wakihimizwa kushirikiana na shirika hilo kwa kutoa taarifa mapema na kuzingatia usalama wa umeme.

RC TANGA: WASTAAFU LINDENI MAFAO YENU, TUMIENI MIFUMO YA KIDIJITALI

September 17, 2026 Add Comment

Mkuu wa mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian akizungumza katika semina ya PSSSF kwa maafisa Rasilimaliwatu wa mkoa wa Tanga kilichofanyika mapema leo Septemba 17, 2026 ikiwa na lengo la kuwaelimisha huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko na hasa kuwahamasisha kuwasilisha madai ya wanachama kwa wakati na matumizi ya kidigitali.



NA MWANDISHI WETU, TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian amewataka wastaafu kulinda mafao yao dhidi ya matapeli, huku akiupongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa kuhamasisha matumizi ya mifumo ya kidijitali inayorudisha heshima na tabasamu kwa wastaafu.


Akifungua semina ya PSSSF kwa waajiri iliyofanyika jijini Tanga iliyowakutanisha Maafisa Rasilimaliwatu na Utawala 120 kutoka taasisi mbalimbali za Serikali, Balozi Dkt. Batilda alieleza kuwa maboresho hayo yanaendana na maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutoa huduma bora, za haraka na bila vikwazo. "Niwapongeze sana PSSSF kwa hatua hii inaowezesha Mafao kulipwa kwa haraka," alisema.

Meneja wa PSSSF Kanda ya Kaskazini Mashariki, Kwame Temu, aliwahimiza waajiri kutoa taarifa za watumishi wapya ndani ya siku 30 ili wasajiliwe mapema na kuwahamasisha watumishi kutumia kikamilifu mifumo ya kielektroniki. Kwa upande wake, Afisa Mfawidhi wa Mkoa wa Tanga, Bi. Hanim Babika, alisisitiza waajiri kufanyia kazi changamoto ya kugongana kwa taarifa na kuhakikisha wafanyakazi wa mikataba kusajiliwa.

Akitoa ushuhuda, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Bw. Rashid Mchatta alisema elimu inayotolewa na PSSSF imebadili kabisa maisha ya wastaafu wa sasa, kwani wanatoka utumishi wakiwa wanajiamini na wenye uelewa mpana wa uwekezaji. "Sekretari wangu alipostaafu, alikuja ofisini kwangu mwenye furaha, ananieleza habari za fursa za uwekezaji tu baada ya kupata mafunzo ya PSSSF," alisema Katibu Tawala.

PSSSF inaendelea kuwasihi wanachama na wastaafu nchini kutumia mifumo rasmi ya kielektroniki ili kupata huduma kwa haraka, uwazi na usalama zaidi ambayo ni PSSSF Member Portal na PSSSF Kiganjani, aidha wawawe na changamoto kutumia simu ya bure kuwasiliana na Mfuko ambazo ni 0800110055.

Meneja wa PSSSF Kanda ya Kaskazini Mashariki, Bw. Kwame Temu akizungumza katika semina kwa maafisa Rasilimaliwatu na Utawala wa Mkoa wa Tanga.


UWEKEZAJI WA BARRICK NORTH MARA WAENDELEA KUUNGWA MKONO NA JAMII ZINAZOISHI JIRANI

September 17, 2026 Add Comment

 


Mkuu wa Wilaya ya Tarime, (DC) Meja Edward Gowele, akizungumza na wakazi wa vijiji vya Matongo na Nyangoto kuhusu mradi huo wa TSF.

LATRA, OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI WAIMARISHA USHIRIKIANO WA KISHERIA KATIKA SEKTA YA USAFIRI

September 17, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamekutana na kufanya Mafunzo ya siku mbili yanayolenga kubadilishana uzoefu na kuimarisha uelewa kuhusu majukumu na utekelezaji wa Sheria katika sekta ya usafiri.

WALIMU ZANZIBAR WAHIMIZWA KUFANYA UJIFUNZAJI WA KIDIJITALI KUWA SEHEMU YA KILA SIKU DARASANI

September 17, 2026 Add Comment



Mkurugenzi wa Idara ya Elimu ya Sekondari Zanzibar, Asya Iddi Issa, akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Jukwaa la Elimu ya Teknolojia (EdTech) la mwaka 2026, lililoandaliwa chini ya Mpango wa Mafunzo na Elimu Kazini (INSET), unaolenga kuimarisha uwezo wa walimu katika kutumia teknolojia na mbinu za kidijitali kuboresha ufundishaji na ujifunzaji. Hafla hiyo imefanyika katika Kituo cha Kitaifa cha Rasilimali Walimu (NTRC), Kiembe Samaki, Zanzibar, Alhamisi, Septemba 17, 2026. Jukwaa hilo, lenye kaulimbiu “Kuonesha Ujifunzaji wa Kidijitali, Ubunifu na Mustakabali wa Elimu Zanzibar”, limeandaliwa na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar (MoEVT), Lyra Africa pamoja na shule 10 za sekondari zinazoshiriki katika mradi huo. Kushoto ni Bi Vivian Koka wa JMKF na kulia ni Bi Trust Mwalyango wa JMKF pia.


Mkurugenzi wa Idara ya Elimu ya Sekondari Zanzibar, Asya Iddi Issa, akiwa katika picha na washiriki na waandaji wa Jukwaa la Elimu ya Teknolojia (EdTech) la mwaka 2026, lililoandaliwa chini ya Mpango wa Mafunzo na Elimu Kazini (INSET), unaolenga kuimarisha uwezo wa walimu katika kutumia teknolojia na mbinu za kidijitali kuboresha ufundishaji na ujifunzaji. Hafla hiyo imefanyika katika Kituo cha Kitaifa cha Rasilimali za Walimu (NTRC), Kiembe Samaki, Zanzibar, Alhamisi, Septemba 17, 2026. Jukwaa hilo, lenye kaulimbiu “Kuonesha Ujifunzaji wa Kidijitali, Ubunifu na Mustakabali wa Elimu Zanzibar”, limeandaliwa na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar (MoEVT), Lyra Africa pamoja na shule 10 za sekondari zinazoshiriki katika mradi huo. Kulia kwake ni Bi Vivian Koka wa JMKF na Mkuu wa Kituo cha Kitaifa cha Rasilimali Walimu Bw. Mohamed Khamis Suleiman na kushoto kwake ni Bi Trust Mwalyango wa JMKF.




ZANZIBAR — Septemba 17, 2026: WalimuvisiwaniZanzibar wamehimizwakutumiateknolojia kwa vitendokatikaufundishajiwakila siku,badalayakujadilituumuhimuwaujifunzajiwakidijitali.

Wito huo umetolewa na Mkurugenziwa Idara ya Elimu ya Sekondari Zanzibar, Asya Iddi Issa, wakati akifungua rasmi mafunzo ya Jukwaa la EdTech la kwanza kufanyika visiwani, lililoandaliwa chini ya Mpango wa Mafunzo na Elimu Kazini (INSET)unaolenga kuimarisha uwezo wa walimu katika kuboresha ufundishaji.

Jukwaa hilo liliandaliwa na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete (JMKF),kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar (MoEVT), Lyra Africa na shule 10 za sekondari zinazoshiriki katika mradi huo.

Jukwaa hilo lilifanyika katika Kituo cha Kitaifa cha Rasilimali za Walimu (NTRC), Kiembe Samaki, Zanzibar, likiwa nakauli mbiu: “Kuonesha Ujifunzaji wa Kidijitali, Ubunifu na Mustakabali wa Elimu Zanzibar.”

Bi. Issa alisema walimu wengi tayari wanamiliki vifaa vya kisasa vya kidijitali, lakini vifaa hivyo havitumiki kikamilifu katika ufundishaji, utafiti na maendeleo yao ya kitaaluma.


“Walimu wanapaswa kufanya kila linalowezekana kutekeleza kwa vitendo yale wanayojifunza. Pia wanapaswa kufanya juhudi za makusudi kuelewa na kukubali matumizi ya teknolojia,badala ya kuwategemea walimu wa TEHAMA pekee,” alisema.

Alisisitiza kuwa ujumuishaji wa teknolojia ni jukumu la walimu wote, akiwataka kutumia simu na kompyuta kuandaa masomo, kutafuta maarifa, kuboresha ufundishaji na kuwasaidia wanafunzi kufikiri kwa upana zaidi.

“Vifaa vya kidijitali vilivyo mikononi mwetu havipaswi kubaki kwaajili ya kupiga simu, kutuma ujumbe na burudani pekee. Vinapaswa kuwa zana za kuandaa masomo, kutafuta maarifa, kuboresha ufundishaji na kuwasaidia wanafunzi kufikiri kwa upanazaidi,” alisema.

Pia aliwahimiza walimu na wanafunzi kutumia akili bandia (AI) kama nyenzo yakufanya utafiti, kupata vifaa vya kujifunzia, kuzalisha mawazo na kupanua maarifa. Hata hivyo, alionya kuwa teknolojia hiyo haipaswi kutumiwa kuendeleza udanganyifu wa kitaaluma, ikiwemo kufanya udanganyifu katika mitihani, kunakilikazi za watu wengine au kuandaa tasnifu na kazi za shule bila ushiriki wakweli wa mhusika.

“Akili bandia inapaswa kusaidia ujifunzaji, si kuchukua nafasi ya juhudi, uadilifu au fikra tunduizi,” alisema.

Jukwaa hilo liliwakutanisha maafisa wa wizara, maafisa waelimu, wakuu washule, walimu wa TEHAMA, viongozi wa Jumuiya za Kujifunza kwa Pamoja, wanafunzi na washirika wa utekelezaji kutoka shule 10 zinazoshiriki katika mradi huo.

Wakati wa jukwaa hilo, wanafunzi kutoka shule mbalimbali za sekondari walionesha ubunifu wao wa kidijitali, vipaji na mafanikio ya ujifunzaji, wakitoa mfano wa vitendo wa matumizi yanayoongezeka ya teknolojia katika elimu Zanzibar.

STRENGTHENING UNESCO–TANZANIA COOPERATION

September 17, 2026 Add Comment


Dar es Salaam, Tanzania: The Tanzania National Commission for UNESCO and UNESCO continue to strengthen their cooperation in advancing shared priorities in education, science, culture, communication and information, and sustainable development.

The photograph was taken during an official engagement at the UNESCO Office, UN House, PSSSF Tower Complex, Dar es Salaam, reflecting the continued collaboration between the two institutions in support of UNESCO’s mandate and Tanzania’s development priorities.

Pictured from left: Prof. Hamisi Masanja Malebo, Executive Secretary, Tanzania National Commission for UNESCO; and Mr Michel Toto, UNESCO Country Representative in Tanzania.



šŸ“ø Photo: Tanzania National Commission for UNESCO


#UNESCOTanzania #TanzaniaNationalCommissionforUNESCO #UNESCO #Tanzania #SustainableDevelopment

MOROGORO GIRLS INSPIRED TO EXPLORE SCIENCE AND TECHNOLOGY

September 17, 2026 Add Comment


UNESCO and Beijing Normal University (BNU) provide students from 10 schools with opportunities to explore ICT, innovation and pathways into STEM careers

MOROGORO, TANZANIA – 17 September 2026:

For a group of Form One girls from 10 secondary schools across Morogoro Region, technology is beginning to mean much more than simply using a smartphone or accessing the internet. It is becoming a space where they can learn, create, solve problems and imagine new possibilities for their future.

This shift in perspective is at the heart of a three-day girls’ Bootcamp being held at Kilakala Girls Secondary School from 16 to 18 September 2026, under the UNESCO–Beijing Normal University (BNU) project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls.


The journey began on 15 September 2026 with a meeting held at Odema Hotel in Morogoro, before the students moved into the Bootcamp phase, which officially began on 16 September 2026 at Kilakala Girls Secondary School, where the training is continuing until tomorrow, 18 September 2026.

The project is implemented by UNESCO with funding support from Beijing Normal University (BNU), technical support from the UNESCO International Research and Training Centre for Rural Education (UNESCO-INRULED), and in collaboration with the Government of the United Republic of Tanzania.



The initiative seeks to strengthen girls’ digital skills, increase their interest and understanding of ICT education and careers, and challenge gender stereotypes and expectations that can discourage girls from pursuing technology-related fields.

Helping Girls See Their Place in Science and Technology

For many of the girls participating in the Bootcamp, the experience provides an opportunity to look at technology from a different perspective.

Rather than seeing ICT as something mainly associated with boys or as a tool for basic communication, the girls are being encouraged to see themselves as potential innovators, researchers, engineers, entrepreneurs and creators of digital solutions.

This approach responds directly to one of the challenges identified by the project: gender stereotypes and social expectations that may portray technology as a male-dominated field, affecting girls’ confidence, interest and sense of belonging in ICT-related education and careers.

By creating opportunities for girls to engage with digital skills and female role models, the project aims to help them recognise that their future can include technology—not only as users, but also as creators and problem-solvers.

When Technology Meets Real-Life Challenges

One of the sessions during the Bootcamp, “Gender, Technology and ICT in the Agriculture Sector,” delivered by Dr Lily Makalanga Bogohe, demonstrates how technology can be connected to everyday challenges facing communities.

The session highlighted the important contribution of women to food production while drawing attention to barriers that can limit women’s access to digital technologies, including the cost of smartphones and data, limited digital skills, and social and gender-related constraints.

At the same time, the session explored how digital technologies can create opportunities for women and girls, including access to market information, weather information, mobile financial services and other digital resources that can support livelihoods and decision-making.

The lesson for the girls is clear: technology is not separate from real life. It can be used to understand problems, develop solutions and improve the way people live and work.

Challenging the Idea That Technology Is “For Boys”

The Bootcamp also creates space to question one of the persistent barriers to girls’ participation in technology: the belief that science and technology are primarily for boys.

The project recognises that limited female role models and restricted exposure to ICT education and career pathways can influence how girls perceive their own possibilities.

Through practical learning, mentorship and exposure to technology-related opportunities, the girls are being encouraged to build confidence and develop a stronger understanding of where digital skills can take them.

The message is not simply about teaching girls how to use technology. It is about helping them understand that they can participate in shaping the technologies and solutions that respond to the needs of their communities.

Starting the STEM Journey Early

The Bootcamp comes at an important stage in the girls’ education. As Form One students, they are at an early point in their secondary school journey, when exposure to new fields of knowledge can help shape their interests and aspirations.

The project’s focus on digital skills, ICT education and career pathways provides an opportunity for girls to begin exploring fields related to science, technology, engineering and mathematics (STEM), while developing the confidence to consider ICT-related studies and careers.

The broader objective is to ensure that girls are not left behind as technology continues to transform education, employment and society.

By investing in girls’ digital skills today, the initiative contributes to a future in which more women can participate meaningfully in technology, innovation and digital transformation.

From Learning to Possibility

The Bootcamp is more than a three-day learning activity. It is an opportunity for girls to see possibilities that may not previously have been visible to them.

As the sessions continue at Kilakala Girls Secondary School, the experience is helping participants connect digital skills with real-world challenges, explore their interests and begin thinking about the role technology could play in their education and future careers.

Ultimately, the project seeks to create an environment in which girls can develop the skills, confidence and understanding needed to participate in the digital world on equal terms. Its communication approach also places emphasis on documenting girls’ experiences, achievements, role models and pathways into ICT education and careers.

For the girls of Morogoro, the journey is only beginning.

Science and technology are not only for boys. Girls, too, can learn, innovate, create solutions and help shape the digital future.

SERIKALI INAWEKEZA KWENYE MADINI KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA, KUONGEZA FURSA ZA AJIRA - PROF. SHEMDOE

September 17, 2026 Add Comment



Na: OWM – TAMISEMI, Ruangwa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira bora ya uwekezaji na usimamizi wa rasilimali madini, kwa lengo la kuhakikisha utajiri wa madini unatumika kikamilifu katika kujenga uchumi wa taifa na kuongeza fursa za ajira kwa wananchi.

Prof. Shemdoe amesema hayo Septemba 16, 2026, akiwa Ruangwa mkoani Lindi, wakati akifungua Maonesho ya Madini na Fursa za Uwekezaji mkoani humo.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa sekta ya madini haibaki kuwa ya uchimbaji pekee, bali inakuwa kichocheo cha viwanda, teknolojia, ajira, biashara, ubunifu na maendeleo ya jamii,” amesisitiza Prof. Shemdoe.


Katika kuhakikisha lengo hilo linatimia, Prof. Shemdoe ameyataka makampuni makubwa yaliyowekeza katika sekta ya madini kuangalia namna bora ya kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya uchenjuaji wa madini mkoani Lindi, hususan katika maeneo yenye rasilimali hizo, ili wananchi wanaozunguka maeneo hayo wanufaike zaidi kupitia fursa za ajira.


Prof. Shemdoe amesema maonesho hayo ni jukwaa muhimu linalowaunganisha Serikali, wananchi, wawekezaji katika sekta mbalimbali za uchumi, wataalam pamoja na taasisi za kifedha, kwa ajili ya kujenga uelewa mpana kuhusu rasilimali zilizopo na fursa za uwekezaji, pamoja na namna sekta mbalimbali za uchumi, ikiwemo madini, zinavyoweza kuongeza ajira, mapato na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.


“Nilipofika hapa nilitembelea mabanda mbalimbali yaliyowakutanisha wachimbaji wakubwa, wadogo, wanaoleta teknolojia, akina mama, vijana na taasisi za kifedha, ili wakitoka hapa watoke na fursa mbalimbali zinazotokana na uwekezaji katika sekta ya madini,” ameeleza Prof. Shemdoe.




Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema mkoa huo si maskini, bali changamoto ni wananchi wake kuwa maskini, kwani mkoa hauwezi kuitwa maskini wakati una utajiri wa madini mbalimbali, jambo aliloliona kupitia maonesho hayo.

Mhe. Malima ameahidi kuwa ofisi yake itaendelea kusimamia maonesho kama hayo ya madini ili yaendelee kuibua fursa na kuvutia uwekezaji utakaowanufaisha wananchi.


Aidha, Mhe. Malima amesema anatarajia kuwa ndani ya kipindi cha uongozi wa miaka mitano wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, mkoa wa Lindi utakuwa umetambua fursa zake, kuzipa kipaumbele na hatimaye kuwa miongoni mwa mikoa yenye mapato makubwa nchini.



Naye Mbunge wa Ruangwa ambaye pia ni Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, amesema Ruangwa ina kiwanda kikubwa cha graphite, huku akieleza kuwa madini yaliyopo wilayani humo si graphite, dhahabu na kopa pekee, bali yapo madini mengine mengi.


Mhe. Mmuya amesema kutokana na uwepo wa rasilimali hizo, Ruangwa imeendelea kunufaika na mapato yatokanayo na sekta ya madini, ambapo mwaka jana wilaya hiyo ilichangia kiasi cha shilingi bilioni 2.9.







TUME YA TAIFA YA UNESCO YAJADILI UANZISHWAJI WA SHULE ZA BLUU ZANZIBAR

September 17, 2026 Add Comment

Kikao kinaweka msingi wa kuimarisha elimu kuhusu bahari, uhifadhi wa mazingira na uchumi wa buluu

ZANZIBAR: Tume ya Taifa ya UNESCO inafanya mashauriano na Menejimenti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar kuhusu uanzishwaji wa Programu ya Shule za Bluu (Blue Schools Programme), inayolenga kuwajengea wanafunzi uelewa na maarifa kuhusu umuhimu wa bahari katika maisha ya binadamu, uhifadhi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi na fursa za uchumi wa buluu.

Kikao hiki kinaendelea Zanzibar, huku Tume ya Taifa ya UNESCO ikiwakilishwa na Naibu Katibu Mtendaji wa Tume, Dkt. Khamis Khalid Said. Majadiliano yanajikita katika kujenga uelewa wa pamoja kuhusu programu hiyo na kuweka msingi wa hatua zinazofuata kuelekea uanzishwaji wake Zanzibar.

Programu ya Shule za Bluu inalenga kukuza Elimu kuhusu Bahari (Ocean Literacy) kwa kuwawezesha wanafunzi kuelewa bahari, uhusiano wake na maisha ya binadamu na namna shughuli za binadamu zinavyoathiri mazingira ya baharini.

Kupitia mpango huo, shule zinapata fursa ya kuunganisha elimu ya bahari na mazingira, uendelevu na maisha ya jamii, huku wanafunzi wakijengewa uwezo wa kutambua thamani ya bahari na wajibu wao katika kuitunza.

Kwa Zanzibar, ambako bahari ni sehemu muhimu ya mazingira, maisha ya jamii na shughuli mbalimbali za kiuchumi, kuimarisha elimu kuhusu bahari katika shule kunatoa fursa ya kuwaandaa wanafunzi kuwa kizazi kinachotambua thamani ya rasilimali hizo na umuhimu wa kuzitumia kwa njia endelevu.

Elimu hiyo inagusa maeneo mbalimbali, yakiwemo uhifadhi wa mazingira ya baharini, mabadiliko ya tabianchi, uchafuzi wa bahari, matumizi endelevu ya rasilimali za bahari na fursa za uchumi wa buluu.

ELIMU YA BAHARI KUELEKEA TANZANIA YA 2050

Majadiliano kuhusu Shule za Bluu yanaendana na mwelekeo mpana wa Tanzania wa kuwekeza katika elimu, ujuzi, sayansi, teknolojia na ubunifu, pamoja na matumizi endelevu ya rasilimali kwa ajili ya maendeleo ya muda mrefu.

Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inaweka mkazo katika kujenga rasilimali watu yenye maarifa na ujuzi, kukuza ubunifu na kuimarisha matumizi endelevu ya rasilimali za Taifa.

Katika muktadha huo, elimu kuhusu bahari inatoa fursa ya kuwaandaa wanafunzi mapema kuelewa fursa na changamoto zinazohusiana na bahari, ikiwemo nafasi ya uchumi wa buluu katika maendeleo ya Tanzania.

Kujenga uelewa huo shuleni kunaweza pia kusaidia kuandaa kizazi chenye uwezo wa kutumia maarifa, sayansi na ubunifu kutafuta suluhisho la changamoto za mazingira na mabadiliko ya tabianchi.

KUJENGA KIZAZI CHENYE UFAHAMU WA BAHARI

Dhana ya Shule za Bluu inaweka mwanafunzi katika nafasi ya kuwa sehemu ya kujifunza, kutafakari na kuchukua hatua kuhusu mazingira yanayomzunguka.

Kupitia elimu hiyo, wanafunzi wanaweza kuelewa uhusiano kati ya bahari, mazingira, uchumi na maisha ya jamii, na namna maamuzi ya sasa yanavyoweza kuathiri rasilimali za bahari kwa vizazi vijavyo.

Kwa mtazamo huo, shule inaweza kuwa sehemu muhimu ya kujenga utamaduni wa kuhifadhi mazingira, huku walimu na wanafunzi wakishirikiana na jamii katika kukuza uelewa kuhusu bahari na matumizi yake endelevu.

TUME YA TAIFA YA UNESCO YAWEKA MSINGI WA HATUA ZINAZOFUATA

Akizungumzia kikao hicho, Dkt. Khamis Khalid Said anaeleza kuwa majadiliano yanawezesha kujenga uelewa wa pamoja kati ya Tume ya Taifa ya UNESCO na Menejimenti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar kuhusu Programu ya Shule za Bluu.

“Kikao hiki kinatuwezesha kujenga uelewa wa pamoja kuhusu Programu ya Shule za Bluu na kuweka msingi wa namna nzuri ya kuendelea na hatua zinazofuata kuelekea uanzishwaji wa programu hii Zanzibar,” anasema Dkt. Khamis.

Kikao kinaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tume ya Taifa ya UNESCO na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar katika kuangalia namna elimu kuhusu bahari inaweza kuimarishwa katika mazingira ya shule na kuhusishwa na mahitaji ya maendeleo ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Hatua hii pia inaendana na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha elimu na ujuzi, kukuza sayansi, teknolojia na ubunifu, pamoja na kuhimiza matumizi endelevu ya rasilimali katika kuchochea maendeleo ya Taifa.

Katika safari kuelekea Tanzania ya 2050, kuwekeza katika elimu kuhusu bahari kunaweza kusaidia kujenga kizazi chenye maarifa, ujuzi na ubunifu wa kutambua fursa za uchumi wa buluu na wakati huo huo kuwa na uelewa wa wajibu wa kulinda mazingira ya baharini.

Kwa kuanzia shuleni, elimu kuhusu bahari inaweza kuwa msingi wa kujenga kizazi kinachoifahamu bahari, kinathamini rasilimali zake na kinakuwa tayari kushiriki katika kuzitunza kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Tume ya Taifa ya UNESCO inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuendeleza programu zinazotumia elimu, sayansi, utamaduni na mawasiliano kama nyenzo za kuchangia maendeleo endelevu ya Tanzania.

MOI YAANZA KUTUMIA MBINU MPYA KUTIBU KIHARUSI

September 17, 2026 Add Comment
Na Abdallah Nassoro - MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) imeanza kutumia technolojia ya kisasa kutoa matibabu ya kibingwa ya upasuaji wa ubongo kwa wagonjwa wa kiharusi inayongeza ufanisi wa matibabu Kwa wagonjwa.

NEMC YATAKA UBUNIFU WA MAZINGIRA KUGEUZWA KUWA FURSA

September 16, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa wito wa kujenga mifumo itakayowezesha ubunifu na fursa za mazingira kugeuzwa kuwa miradi inayotekelezeka, inayoweza kufadhiliwa na kukua.

WADAU WA USAFIRISHAJI WAKUTANA KUIMARISHA BIASHARA YA KIKANDA

September 16, 2026 Add Comment

 

Kigoma, Septemba 16, 2026

Wadau mbalimbali wa sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji wamekutana mjini Kigoma katika kikao cha siku moja kilichoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kwa lengo la kujadili fursa na changamoto zinazohusiana na usafirishaji wa mizigo na namna ya kuimarisha biashara katika ukanda wa Magharibi na Maziwa Makuu.

Kikao hicho kimehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka katika sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji, ambapo Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano miongoni mwa wadau katika kuimarisha ufanisi wa usafirishaji na kukuza biashara ya kikanda.

Kwa upande wa TPA, Naibu Mkurugenzi Mkuu, Mha. Dkt. Baraka Mdima, ameshiriki kikao hicho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, akiwakilisha uongozi wa Mamlaka katika majadiliano yaliyolenga kubaini maeneo ya kimkakati ya kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji kupitia Bandari ya Kigoma.

Majadiliano katika kikao hicho yamejikita katika kubaini changamoto zinazokwamisha mtiririko wa mizigo, zikiwemo vikwazo visivyo vya kiforodha, ucheleweshaji na gharama za usafirishaji, pamoja na kutafuta suluhu za pamoja zitakazoboresha mazingira ya biashara na kuongeza ushindani wa njia za usafirishaji.

Aidha, wadau wamejadili umuhimu wa kuimarisha matumizi ya Bandari ya Kigoma kama lango muhimu la biashara katika ukanda wa Maziwa Makuu, hususan kupitia Ushoroba wa Kati (Central Corridor) unaoiunganisha Tanzania na nchi jirani.

Kikao hicho pia kimekuwa fursa ya kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wengine wa mnyororo wa usafirishaji katika kuboresha huduma, kupunguza muda na gharama za usafirishaji, na kuweka mazingira rafiki zaidi kwa biashara ya ndani na ya kikanda.

Kwa ujumla, kikao hicho kimeendelea kuonesha umuhimu wa majadiliano ya pamoja katika kutatua changamoto za usafirishaji na kutumia fursa zilizopo katika ukanda wa Magharibi, huku Bandari ya Kigoma ikiendelea kuwa sehemu muhimu ya kuunganisha biashara ya Tanzania na masoko ya nchi za Maziwa Makuu.











TANZANIA YAWEKA SAUTI YAKE RIYADH, YASISITIZA AI YENYE LUGHA, UTAMADUNI NA MASLAHI YA TAIFA

September 16, 2026 Add Comment


RIYADH, SAUDI ARABIA: 

Tanzania imesisitiza umuhimu wa kujenga na kutumia akili unde (Artificial Intelligence – AI) inayozingatia lugha, utamaduni, mazingira na mahitaji ya jamii, huku ikieleza dhamira ya kuimarisha uwezo wa ndani wa nchi katika teknolojia hiyo na kuongeza nafasi ya Kiswahili katika ulimwengu wa akili unde.

Msisitizo huo umetolewa katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde linalofanyika mjini Riyadh, Saudi Arabia, ambapo Tanzania imeshiriki katika mjadala wa kimataifa kuhusu hatua za vitendo zinazoweza kuchukuliwa na nchi ili kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanaenda sambamba na maadili, uwajibikaji, usalama na maendeleo jumuishi.

Katika mchango wake kwenye mjadala huo, mwakilishi wa Tanzania aliishukuru UNESCO na Serikali ya Saudi Arabia kwa kuandaa jukwaa hilo, akieleza kuwa majadiliano hayo yana umuhimu mkubwa katika kuzipa nchi nafasi ya kubadilishana uzoefu na kutafuta suluhisho la pamoja kuhusu fursa na changamoto zinazoletwa na maendeleo ya akili unde.

Aidha, Tanzania iliishukuru UNESCO kwa kuiunga mkono Serikali katika kutekeleza Mbinu ya Tathmini ya Utayari wa Akili Unde (Readiness Assessment Methodology – RAM) mwaka 2024, ambayo matokeo yake yalizinduliwa mwaka 2025.

Tathmini hiyo iliisaidia Tanzania kubaini maeneo mbalimbali yanayohitaji kuimarishwa ili kujenga mazingira wezeshi kwa maendeleo na matumizi salama, jumuishi na yenye maadili ya akili unde.

TANZANIA YASISITIZA KUJENGA UWEZO WA NDANI

Akieleza baadhi ya mapengo yaliyobainika, mwakilishi wa Tanzania alitaja umuhimu wa kuhakikisha lugha mbalimbali zinapata nafasi katika mifumo ya akili unde, akisisitiza kuwa nchi zinahitaji kujenga uwezo wa ndani ili teknolojia hiyo iweze kuakisi mazingira na mahitaji ya jamii zao.

Alieleza kuwa utegemezi mkubwa wa mifumo ya akili unde iliyotengenezwa nje unaweza kuibua changamoto zinazohusiana na uwakilishi wa tamaduni, usalama na umiliki wa data, pamoja na ulinganifu wa mifumo hiyo na sheria na maadili ya nchi husika.

Kwa msingi huo, Tanzania imeona umuhimu wa kuwekeza katika uwezo wa ndani wa kutengeneza na kutumia mifumo ya akili unde inayozingatia lugha na mazingira ya Tanzania, sambamba na kuimarisha miundombinu ya data na mifumo ya kitaifa ya usimamizi wa teknolojia hiyo.

Mwelekeo huo unaendana na hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuimarisha mageuzi ya kidijitali nchini. Serikali imetangaza mageuzi ya kidijitali kuwa miongoni mwa vipaumbele katika Bajeti ya mwaka 2026/2027, huku ikiendelea na maandalizi ya Mkakati wa Taifa wa Akili Unde.

KISWAHILI KUPATA NAFASI KATIKA MAPINDUZI YA AI

Moja ya hoja muhimu iliyowasilishwa na Tanzania Riyadh ni umuhimu wa kuendeleza mfumo mkubwa wa lugha (Large Language Model – LLM) wa Kiswahili, ili kuwezesha lugha hiyo kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya teknolojia za akili unde.

Tanzania imeeleza nia ya kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo UNESCO, katika kuendeleza mfumo huo, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa teknolojia kuelewa na kutumia Kiswahili kwa ufasaha na kwa kuzingatia mazingira ya watumiaji wake.

Kiswahili kinachukua nafasi muhimu katika maisha ya Watanzania na ni miongoni mwa lugha zinazotumika na idadi kubwa ya watu barani Afrika. Kwa hiyo, uwekezaji katika teknolojia inayoweza kuelewa na kutumia Kiswahili una umuhimu katika kupanua ushiriki wa wananchi katika mapinduzi ya kidijitali.

Hatua hii pia inaendana na mwelekeo wa Serikali wa kuendeleza rasilimali na zana za lugha ya Kiswahili kwa ajili ya mifumo ya akili unde na uchakataji wa lugha asilia.

MAGEUZI YA KIDIJITALI KUELEKEA TANZANIA YA MAENDELEO

Mjadala wa Tanzania katika jukwaa hilo unaakisi mwelekeo mpana wa Serikali katika kutumia teknolojia za kisasa kama kichocheo cha maendeleo ya Taifa.

Katika hatua mbalimbali, Serikali imeendelea kuweka mazingira ya matumizi ya akili unde, ikiwemo kuimarisha sera na mifumo ya kidijitali, kulinda taarifa binafsi na kujenga uwezo wa rasilimali watu katika teknolojia zinazochipukia.

Mkakati wa Taifa wa Uchumi wa Kidijitali wa 2024–2034 pamoja na hatua zinazoendelea katika eneo la akili unde vinaweka msingi wa kutumia teknolojia za kisasa katika kuongeza ufanisi wa huduma, kukuza ubunifu na kuchochea shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wa elimu, Serikali pia imeendelea kuweka msisitizo katika matumizi sahihi ya teknolojia mpya, ikiwemo akili unde, katika ufundishaji, ujifunzaji, utafiti na ujenzi wa uwezo wa walimu na wanafunzi.

TANZANIA NA AJENDA YA AI BARANI AFRIKA

Katika mjadala huo wa kimataifa, Tanzania imeendelea kuangazia pia nafasi ya Afrika katika mapinduzi ya akili unde, ikisisitiza umuhimu wa bara hilo kuongeza uwezo wake katika sayansi, teknolojia, utafiti, ubunifu na ujuzi wa kidijitali.

Kwa Tanzania, Afrika inapaswa kuwa zaidi ya mtumiaji wa teknolojia hiyo; inahitaji pia kujenga uwezo wa kuzalisha maarifa, data, mifumo na ubunifu unaozingatia mazingira ya Kiafrika.

Hii inamaanisha kuongeza uwekezaji katika wataalamu, taasisi za utafiti, miundombinu ya kidijitali na rasilimali za lugha za Kiafrika ili kuhakikisha maendeleo ya akili unde yanawanufaisha wananchi na kuchangia maendeleo ya bara.

UNESCO NA TANZANIA ZASHIRIKI KUJENGA AI YENYE MAADILI

Ushiriki wa Tanzania katika jukwaa la Riyadh unaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na UNESCO katika eneo la teknolojia zinazochipukia na matumizi yake yenye uwajibikaji.

Kupitia Tathmini ya Utayari wa Akili Unde, Tanzania imepata fursa ya kutathmini mazingira yake ya kitaifa na kubaini maeneo yanayohitaji kuimarishwa katika sera, mifumo ya kitaasisi, uwezo wa watu, miundombinu na matumizi ya teknolojia hiyo.

Kwa upande mwingine, ushiriki katika mijadala ya kimataifa kama ya Riyadh unaipa Tanzania nafasi ya kushirikisha uzoefu wake, kujifunza kutoka kwa nchi nyingine na kuendelea kujenga ushirikiano wa kimataifa katika eneo la akili unde.

Hatua hizi zinaendana na dhamira ya Serikali ya kutumia mageuzi ya kidijitali, sayansi, teknolojia na ubunifu kama nyenzo za kuongeza fursa za maendeleo na kujenga Tanzania inayokwenda sambamba na mabadiliko ya kiteknolojia duniani.

TANZANIA YAANGALIA MUSTAKABALI WA TEKNOLOJIA

Kwa ujumla, ujumbe wa Tanzania katika Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde umeweka mkazo katika kujenga teknolojia inayozingatia watu, lugha na mazingira yao.

Kupitia mjadala huo, Tanzania imeendelea kuonyesha umuhimu wa kuunganisha maendeleo ya teknolojia na mahitaji ya jamii, huku ikisisitiza kuwa akili unde inapaswa kutumika kwa kuzingatia maadili, usalama, haki, utofauti wa lugha na tamaduni, pamoja na vipaumbele vya maendeleo ya Taifa.

Ushiriki huo unaendelea kuifanya Tanzania kuwa sehemu ya mjadala wa kimataifa kuhusu mustakabali wa akili unde, wakati Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kujenga mazingira wezeshi ya mageuzi ya kidijitali na matumizi ya teknolojia kwa maendeleo ya Taifa.

Jukwaa la Nne la Kimataifa la UNESCO la Maadili ya Akili Unde linaendelea mjini Riyadh, Saudi Arabia, likiwakutanisha viongozi, wataalamu, watafiti, watunga sera na wadau kutoka sehemu mbalimbali duniani kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na utawala wa akili unde unaozingatia maadili na uwajibikaji.

SIJARIDHISHWA NA KASI YA WAKANDARASI KIKIM NA AMACO YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA BARABARA, STENDI NA SOKO LINDI - PROF. SHEMDOE

September 16, 2026 Add Comment


Na: OWM – TAMISEMI, Lindi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Mkandarasi KIKIM Contractors Limited kwa kushirikiana na mbia wake AMACO Enterprises katika Manispaa ya Lindi.

Miradi hiyo inahusisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 5.3, Stendi ya Mabasi Mitwero, Soko Kuu la Matopeni na Ofisi ya Mradi, inayotekelezwa na Serikali kupitia Mradi wa Ustawishaji Miji Tanzania (TACTIC).


Prof. Shemdoe ameeleza kutoridhishwa kwake na kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo Septemba 15, 2026, mara baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Mitwero na Soko Kuu la Matopeni, ambapo alibaini kuwa utekelezaji wake umefikia asilimia 23, huku ikiwa imesalia miezi mitano kabla ya muda wa kukamilisha na kukabidhi miradi hiyo.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo, Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, kuhakikisha suala la utekelezaji wa mikataba hiyo linashughulikiwa kwa mujibu wa masharti ya mikataba, ili kuharakisha utekelezaji na kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.


“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, hawa wanaotukwamisha ni wakandarasi wazawa ambao usipowapa kazi wanalalamika. Hivyo, Mheshimiwa RC, hawa wana mikataba, shughulikia suala hili kwa mujibu wa mkataba, kwani wakandarasi hawa wanaonekana ni wababaishaji,” amesema Prof. Shemdoe.


Aidha, Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Lindi kukutana na wakandarasi hao ili wampe mpango mkakati wa kukamilisha miradi hiyo haraka iwezekanavyo, na kuwasilisha kwake mpango kazi huo ifikapo Septemba 23, 2026.Vilevile, ameelekeza kuwa kila baada ya wiki mbili apatiwe mrejesho wa utekelezaji wa mpango huo, ili kufahamu hatua zinazochukuliwa na maendeleo ya miradi hiyo.


Akieleza chanzo cha kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mwakilishi wa Mhandisi Mshauri kutoka kampuni ya Interconsult Ltd, ambaye pia ni Mhandisi Mkazi, Mhandisi Rashidi Abdallah, amesema changamoto hiyo imetokana na mkandarasi kutokuwa amejipanga vyema kiutendaji, kutokuwa na rasilimaliwatu ya kutosha na kutumia vibaya fedha za awali alizolipwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi.

Naye mmoja wa Wakurugenzi wa kampuni zilizopewa kandarasi hizo, John Daniel, amekiri kuwa wamechelewa kutekeleza miradi hiyo kutokana na uzembe, huku akieleza kuwa wamejipanga kufanya kazi usiku na mchana baada ya kuzifanyia kazi changamoto zilizokuwa zikikwamisha utekelezaji.


Bw. Daniel ameomba kukutana na Mkuu wa Mkoa wa Lindi ili kuwasilisha mpango kazi wao, huku akimuomba Mkuu wa Mkoa kuwawekea malengo ya muda mfupi yatakayowawezesha kukamilisha kandarasi yao kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Kighoma Malima, amesema atakutana na wakandarasi hao ili wamueleze mkakati wanaokuja nao wa kukamilisha miradi yote ndani ya miezi mitano iliyobaki.


Mhe. Malima amewataka wakandarasi hao, wakati wa kikao hicho, kuwa tayari kuridhia kutoa mkataba mdogo (sub-contract) kwa mkandarasi mwingine kutekeleza sehemu ya mradi endapo wataona hawana uwezo wa kuikamilisha kwa wakati.


Katika ziara yake ya Septemba 15, 2026, Prof. Shemdoe alitembelea na kukagua pia utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Daraja la Ng’uni katika Kata ya Nanganga, ujenzi wa shule mpya ya msingi eneo la Shule ya Sekondari Kitandi, ujenzi wa Kituo cha Afya Chiola Nachingwea, pamoja na kufanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mtuha, Nachingwea DC.







DKT. MWIGULU: NDANI YA WIKI MOJA TUTACHUKUA HATUA KUSHUSHA BEI YA SARUJI

September 16, 2026 Add Comment


WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema ndani ya wiki moja, Serikali itachukua hatua ya kuhakikisha bei ya saruji inakuwa himilivu kwa wananchi, baada ya kubaini malalamiko ya kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo Simiyu.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumanne, Septemba 15, 2026) wakati akizungumza na wananchi wa Bariadi Mjini, mkoani Simiyu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya CCM Saba Saba.

“Serikali tumeliona hilo. Serikali sikivu tumesikia hilo. Nimewatuma wataalamu ndani ya wiki moja wawe wameshapata ufumbuzi. Tutatoa tamko la njia ya kushusha bei ya saruji ili kila Mtanzania aweze kumudu. Katika baadhi ya maeneo bei ya saruji imefikia zaidi ya sh. 26,000 na katika baadhi ya mikoa ya mipakani imefikia sh. 32,000,” amesema na kusisitiza kuwa Serikali inataka wananchi waweze kumudu gharama za ujenzi wa nyumba na miradi mingine ya maendeleo.

Kuhusu zao la pamba, Waziri Mkuu amesema ameielekeza Wizara ya Kilimo ikutane na wadau wa pamba ndani ya mwezi mmoja na ifikapo Oktoba 15, 2026 apelekewe mapendekezo rasmi kuhusu bei na mfumo bora wa ununuzi wa zao hilo ili kuhakikisha wakulima wananufaika zaidi.

“Nimeipokea hoja hii. Nimeelekeza Wizara ya Kilimo ikae na wadau wa pamba ndani ya mwezi mmoja. Ifikapo tarehe 15 mwezi wa 10, niwe nimeshapata mapendekezo rasmi yaliyorejea mifumo ambayo tumeshaitumia na kubaini upi ni mfumo bora ili tuweze kuhakikisha kwamba wakulima wananufaika,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema pia Serikali imebadilisha utaratibu wa kodi kwa wenye biashara mpya, ambapo mfanyabiashara anayeanzisha biashara atapewa muda wa kuimarisha biashara yake kabla ya kuanza kubeba mzigo wa kodi. “Zamani ilikuwa mtu akianzisha tu biashara, siku hiyo hiyo anaanza kudaiwa kodi. Sasa tumefuta, atasubiriwa mwaka mzima ili biashara yake iimarike,” amesema.

Amesema hatua hizo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kujenga uchumi shirikishi, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kutekeleza sehemu kubwa ya shughuli za maendeleo.

Mapema, akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa Bariadi Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Andrea Mathew, amemshukuru Waziri Mkuu kwa ziara hiyo na kueleza kuwa Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo hilo ikiwemo inayogusa sekta za maji, elimu, afya na barabara.

Mhandisi Kundo amesema mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria wenye thamani ya sh. bilioni 440 unaendelea kutekelezwa mkoani humo, huku Serikali ikiwa imetoa sh. milioni 460 kupitia TARURA kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Majaida–Munambala katika Mto Ndoba.

Kuhusu ujenzi wa soko la kisasa la Bariadi mjini, Mhandisi Kumndo amesema ujenzi wake unaendelea, huku akiomba kasi ya mkandarasi iongezwe ili mradi huo ukamilike kwa wakati.

Akigusia barabara za Bariadi Mjini, Mhandisi Kundo amesema Serikali imeweka mpango wa kuhakikisha kilomita zote 8.6 zilizotengewa ujenzi zinajengwa kwa awamu mbili, ambapo kilomita tano zitajengwa katika awamu ya kwanza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Said Mtanda, amesema Serikali ya Mkoa itasimamia na kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri Mkuu wakati wa ziara hiyo na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji katika Ofisi ya Waziri Mkuu.

“Maagizo na maelekezo yako uliyoyatoa katika ziara yako hii tunayasimamia, tuyatekeleze, na kuleta ripoti ya utekelezaji katika ofisi yako ya Waziri Mkuu,” amesema.