HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

Global Education Fair 2026 yawafikia washiriki 1,113

July 27, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

GLOBAL Education Link (GEL) imesema jumla ya wanafunzi, wazazi na walezi 1,113 wamefikiwa na kupatiwa huduma kupitia maonesho ya Global Education Fair 2026 yaliyofanyika Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam.

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

July 27, 2026 Add Comment




Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imeingia hatua mpya ya kuongeza vyanzo vya uzalishaji umeme baada ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa umeme kwa nguvu ya Jua Kishapu utakaozalisha jumla ya megawati 100.



Hatua hiyo imekuja baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha jumla ya megawati 50 na kuingizwa katika Gridi ya Taifa, jambo lililoongeza uwezo na uthabiti wa gridi hiyo na kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo mbalimbali nchini.





Akizungumza katika hafla hiyo Julai 27, 2026, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema sekta ya nishati ni mhimili wa maendeleo ya Taifa ambapo Serikali inaendelea kufanya jitihada za kuongeza vyanzo mseto vya uzalishaji wa umeme (Energy Mix) ili kuhakikisha Tanzania haitegemei chanzo kimoja pekee cha uzalishaji wa umeme.

"Wananchi wa maeneo haya walikuwa wanategemea umeme uliokuwa unasafirishwa kutoka umbali mrefu. Kukamilika kwa mradi huu kutaifanya Tanzania kuwa na mfumo salama zaidi wa umeme na kuwa nchi ya mfano katika uzalishaji wa umeme unaostahimili mabadiliko ya tabianchi," amefafanua Mhe. Ndejembi.

Aidha, amelishukuru Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia ufadhili wa mkopo wenye masharti nafuu. Amesema ushirikiano huo unaonesha imani kubwa ya washirika wa maendeleo katika usimamizi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati nchini.

Pia ameipongeza TANESCO kwa kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ya umeme inayobadili taswira ya sekta ya nishati nchini, huku akiitaka kuhakikisha mradi huo unasimamiwa kwa karibu katika kila hatua ili ukamilike ndani ya muda uliopangwa na kuanza kuwanufaisha wananchi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, amesema utekelezaji wa mradi huo unaonesha dhahiri dhamira ya Wizara ya Nishati ya kuelekeza asilimia 97 ya bajeti yake katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

"Hatua hii ya utiaji saini ni matokeo ya diplomasia nzuri ya Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, iliyowafanya washirika wetu wa maendeleo kuendelea kuiamini Tanzania katika utekelezaji wa miradi ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme. Tunaamini Tanzania itaendelea kuwa na umeme wa kutosha," amesisitiza Mhe. Mgalu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO, Mhe. Balozi Zuhura Bundala, amesema Bodi ilisimamia kwa karibu utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi huo na kuridhishwa na namna ulivyotekelezwa kwa kuzingatia thamani ya fedha iliyowekezwa. Amesema utiaji saini wa awamu ya pili ni hatua nyingine muhimu inayodhihirisha mafanikio ya mradi huo.



Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema gharama za mradi mzima wa Umeme wa Jua wa Kishapu wenye uwezo wa kuzalisha megawati 150 ni takribani Shilingi bilioni 323. Kati ya fedha hizo, awamu ya kwanza yenye uwezo wa kuzalisha megawati 50 imegharimu Shilingi bilioni 118.6, huku awamu ya pili yenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 ikitarajiwa kugharimu takribani Shilingi bilioni 204.4.

"Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miezi 17 kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia TANESCO na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), ambalo limetoa mkopo wenye masharti nafuu," amefafanua Bw. Twange.

Mkataba huo umesainiwa kati ya TANESCO na muungano wa makampuni mbili kutoka Ufaransa na Tunisia, ambayo ni Sagemcom Energy, Telecom SAS na STEG International Services.









WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAWASILISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO KWA WADAU

July 27, 2026 Add Comment

  


📌 Naibu Katibu Mkuu afungua rasmi kikao kazi kwa wadau 

📌 Asema Sekta ya Utalii, Wanyanyamapori na Malikale ni kichocheo kikubwa cha uchumi wa Taifa

📌 Kutoa vipaumbele vinavyopimika kufikia lengo la watalii milioni 8 ifikapo 2030

Na Neema Chalila Mbuja

NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Nkoba Mabula leo Julai 27, 2026 amefungua rasmi Kikao Kazi cha Wadau wa Sekta ya Utalii kujadili Rasimu ya Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2030, wenye lengo la kutoa mwelekeo  wa utekelezaji wa pamoja wa malengo yaliyowekwa na vipaumbele vyake.

FLYING HORSE YAZINDUA OFISI ARUSHA, SHIJA AHAMASISHA UBORA

July 27, 2026 Add Comment

  

Kampuni ya ALC Lubricants, wazalishaji na wasambazaji wa vilainishi vya magari kupitia chapa ya Flying Horse, imefungua rasmi ofisi yake ya kwanza ya Kanda ya Kaskazini katika Jiji la Arusha, hatua inayotarajiwa kurahisisha upatikanaji wa bidhaa zake kwa wateja wa Arusha, Kilimanjaro na mikoa mingine ya ukanda huo.

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

July 27, 2026 Add Comment



Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius J. Ndejembi (Mb.), leo Julai 27, 2026, ameshuhudia utiaji saini wa mkataba wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa Umeme wa Jua wa Kishapu wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 100, utakaotekelezwa katika eneo la Ngunga, Wilaya ya Kishapu, Mkoa wa Shinyanga.


Mkataba huo wenye thamani ya shilingi bilioni 204.7 umesainiwa kati ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na mwakilishi wa mkandarasi anayetekeleza mradi huo, kampuni za Sagemcom Energy & Telecom SAS na STEG International Services.


Waziri Ndejembi amesema mradi wa Umeme wa Jua wa Kishapu ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuimarisha mseto wa vyanzo vya uzalishaji wa umeme (Energy Mix), ikiwa ni utekelezaji wa azma ya kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika, wa gharama nafuu na unaotokana na vyanzo vya nishati jadidifu.


Amefafanua kuwa, mradi huo unatekelezwa kwa awamu mbili zenye uwezo wa jumla wa kuzalisha Megawati 150. Awamu ya kwanza yenye uwezo wa Megawati 50 iligharimu shilingi bilioni 118.3 na kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za utekelezaji.


Aidha, Waziri Ndejembi amesema awamu ya pili yenye uwezo wa Megawati 100, ambayo utekelezaji wake umeanza rasmi kupitia utiaji saini wa mkataba utagharimu shilingi bilioni 204.7. Jumla ya gharama za utekelezaji wa awamu zote mbili ni shilingi bilioni 323.


Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka vyanzo vya nishati jadidifu, kuimarisha uthabiti wa mfumo wa umeme nchini na kuchangia kufikiwa kwa lengo la Serikali la kuwa na mseto wa vyanzo vya uzalishaji wa umeme pamoja na kufikia uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha kukidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye.


Hafla hii imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba; Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita; Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba; Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, pamoja na viongozi wengine wa Serikali, Chama cha Mapinduzi na wadau wa sekta ya nishati.






CHADEMA MUHEZA YAJITENGA NA ALIYEKUWA KATIBU WAO

July 27, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Tanga

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Muheza mkoani Tanga kimesema hakihusiki na vitendo vinavyodaiwa kufanywa na aliyekuwa Katibu wa chama hicho wilayani humo, Joseph Mwakidasi, huku kikiwataka wanachama kuendelea kudumisha mshikamano na kuepuka makundi yanayoweza kukigawa chama.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Katibu wa CHADEMA Jimbo la Muheza, Michael Mhina, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matukio yaliyojitokeza ndani ya chama katika siku za hivi karibuni.

Mhina alisema Julai 8 mwaka huu viongozi wa chama waliona kupitia vyombo vya habari taarifa za Mwakidasi akimtuhumu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, kutumia vibaya fedha zinazochangwa na wanachama kupitia kampeni ya "Tone Tone".

Alisema kutokana na uzito wa tuhuma hizo, Kamati Tendaji ya Wilaya ilikutana kwa dharura Julai 9 na kumuita Mwakidasi ili afafanue chanzo cha madai yake, lakini hakufika wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa m hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki kwenye kikao hicho wala kutoa maelezo.

Mhina alidai kuwa Julai 20, Mwakidasi aliwasili katika ofisi za CHADEMA Wilaya ya Muheza akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi kutoka wilaya nyingine pamoja na watu ambao, kwa mujibu wa chama hicho, si viongozi wala wanachama wa CHADEMA. Alisema waliingia ofisini baada ya kuchukua funguo kutoka kwa mweka hazina wa chama.

Kwa mujibu wa Mhina, watu hao walifanya kikao ndani ya ofisi hizo na baadaye kurekodi na kusambaza taarifa mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii, jambo alilodai lilisababisha taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.

"Baada ya matukio hayo, Julai 21 tuliamua kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili vifanye uchunguzi kuhusu kilichotokea. Sisi kama CHADEMA Muheza hatuhusiki na yaliyofanywa na watu hao," alisema Mhina.

Alisema viongozi wa chama wilayani humo wanaendelea kumuunga mkono Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, John Heche, pamoja na Mwenyekiti wa chama, Tundu Lissu.

Pia aliomba vyombo vya dola kuchunguza madai ya kuwahamasisha wananchi kuhudhuria mkutano kwa ahadi ya kulipwa fedha, akisisitiza kuwa CHADEMA haina utaratibu wa kuwalipa wanachama kushirikiio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa shughuli za chama.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Ally Mahanyu, alisema chama kinapinga vitendo vinavyodaiwa kufanywa na Mwakidasi kwa madai kuwa vilikiuka taratibu za chama.

Mahanyu alisema viongozi walimuita Mwakidasi mara kadhaa kwenye vikao vya Kamati Tendaji ili kutoa maelezo, lakini hakuitikia wito huo.

Aidha, alivitaka vyombo vya dola kuchunguza matukio yote yaliyotokea katika ofisi za chama, akidai hatua zilizochukuliwa na Mwakidasi na wenzake zilichangia taharuki miongoni mwa wanachama na wananchi wa Muheza.

Aliwataka wanachama wa CHADEMA kuendelea kuwa watulivu, kuwaamini viongozi wao na kushiriki shughuli za ujenzi wa chama kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA Wilaya ya Muheza, Isa Mwaikani, alisema baraza hilo pia lilimuita Mwakidasi kutoa maelezo kuhusu tuhuma alizozielekeza kwa Heche, lakini hakuitikia wito huo.

Mwaikani alisema viongozi wa chama walishangazwa na tuhuma hizo kwa kuwa, kwa mujibu wa muundo wa uongozi wa chama, Makamu Mwenyekiti hahusiki na usimamizi wa fedha.

"Hatuelewi amepata wapi ujasiri wa kumtuhumu kiongozi wa juu wa chama bila kuwasilisha ushahidi kwenye vikao halali vya chama," alisema.

Aliongeza kuwa wanachama wengi wa CHADEMA Muheza wameendelea kubaki ndani ya chama na hali ya kisiasa wilayani humo ni tulivu.



Akijibu tuhuma hizo, aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Muheza, Joseph Mwakidasi, alisema madai yanayotolewa dhidi yake hayana ukweli na kwamba anaendelea kutetea nafasi yake ndani ya chama.



Alisema hana mpango wa kuhamia chama kingine cha siasa na anasubiri maamuzi ya vikao vya chama kuhusu nafasi yake.



Kuhusu tuhuma alizomwelekeza John Heche, Mwakidasi alisema suala hilo linatokana na mijadala iliyofanyika katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika Dodoma, akidai baadhi ya taarifa zilizokuwa siri zilivuja kutoka ndani ya chama.



Mwisho.









DC BAHI AKABIDHI GARI RUWASA, AMKARIBISHA MENEJA MPYA MKOA

July 27, 2026 Add Comment



Mkuu wa wilaya ya Bahi Mhe. Joachim Thobias Nyingo amekabidhi gari jipya aina ya ‘Toyota Pickup’ kwa Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wa wilaya hiyo Mha. Hopeness Liundi huku akitoa wito wa kutumia vizuri kitendea kazi hicho kwa kuongeza kasi ya utendaji kazi kwa tija ili kufikia lengo la kumtua mama ndoo kichwani kwa kuwafikishia huduma ya Majisafi ya bomba wananchi wa wilaya hiyo.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika katika ofisi ya Meneja RUWASA Mkoa wa Dodoma Julai 27, 2026 na kuhudhuriwa na Meneja wa Mkoa huo Mha. Beatrice Kasimbazi pamoja na watumishi wengine wa mkoa huo.

Akizungumza kabla ya kuzindua na kukabidhi gari hilo, Mhe. Nyingo aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuiwezesha RUWASA na kuboresha utendaji wao wa kazi ikionesha dhamira ya dhati ya serikali kuwafikishia wananchi huduma muhimu ya majisafi ya bomba.

Hivi karibuni, Serikali kupitia RUWASA ilinunua na kugawa magari 22 katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kuboresha na kuimarisha utendaji wa taasisi katika kusimamia na kufuatilia miradi na huduma ya maji katika maeneo ya vijijini.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mkuu wa wilaya Nyingo amemkaribisha Meneja mpya wa RUWASA wa mkoa wa Dodoma Mha. Beatrice Kasimbazi ambaye amehamishiwa mkoani humo akitokea mkoa wa Pwani, huku akitoa wito kwa watumishi wa wilaya hiyo kumpokea na kumpa ushirikiano katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya serikali na kuwahudumia wananchi.








NAIBU WAZIRI LONDO AWATAKA WAZALISHAJI KUTUMIA HUDUMA ZA TBS

July 27, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

UWEKEZAJI unaofanywa katika Taasisi ya Viwango Tanzania (TBS) umeongeza uwezo wa taasisi hiyo kulinda afya za Watanzania, thamani ya fedha za wananchi na kusaidia bidhaa zinazozalishwa nchini kushindana katika masoko ya ndani na kimataifa.

MADEREVA WASISITIZWA USAFIRISHAJI SALAMA WA KEMIKALI

July 25, 2026 Add Comment
Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kusini, Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Hadija Mwema (aliyesimama) akizungumza na wawezeshaji pamoja na madereva wanaosafirisha makaa ya mawe, wakati akifungua mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali kwa madereva zaidi ya 90 mkoani Ruvuma. Mafunzo hayo yamefanyika kwa siku mbili kuanzia Julai 23 hadi 24, 2026, wilayani Songea. Ruvuma.

GCLA YAKUTANA NA WADAU KUIMARISHA USAFIRISHAJI WA SALFA

July 25, 2026 Add Comment
Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti wa GCLA, Daniel Ndiyo akizungumza wakati akiwakaribisha wadau wakemikali aina ya Sulphur katika kikao cha wadau hao kilichofanyika katika ukumbiwa Hazina Dar es Salaam Julai 24, 2026.

WMA YAUNGANA NA RAIS DKT. SAMIA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA DODOMA

July 25, 2026 Add Comment

 

Wakala wa Vipimo (WMA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa iliyofanyika katika Viwanja vya Mnara wa Mashujaa, Mtumba, jijini Dodoma, ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

TOHASA YAANZISHA KAMPENI YA ‘KUWA MAKINI OKOA MAISHA’ KWA BODABODA

July 25, 2026 Add Comment
CHAMA cha Wataalamu wa Masuala ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi (TOHASA) kwa kushirikiana na OSHA, WCF, SAFETY AND SECURITY, JAFFERJEE na TMHS GROUP wamezindua kampeni ya “Kuwa Makini Okoa Maisha” inayolenga kuwajengea madereva wa bodaboda uelewa wa sheria na matumizi salama ya barabara ili kupunguza ajali na kuokoa maisha.

MAHAFALI YA 69 KOLANDOTO: BODI YATAKA HADHI YA CHUO KIKUU

July 25, 2026 Add Comment

Baadhi ya wahitimu 191 wa Chuo cha Sayansi za Afya Kolandoto wakiwa katika Mahafali ya 69 tangu kuanzishwa kwa chuo hicho na ya 14 tangu kipate usajili mpya kwa jina la Chuo cha Sayansi za Afya Kolandoto, yaliyofanyika Julai 24, 2026.

ORYX GAS YAGAWA MITUNGI 600, YAONGEZA KASI YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI BAGAMOYO

July 24, 2026 Add Comment
KAMPUNI ya Oryx Gas imekabidhi mitungi ya gesi ya kupikia 600 kwa makundi mbalimbali ya wajasiriamali wakimo mama lishe huku Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Subira Mgalu akieleza kuwa uamuzi wa Oryx kugawa mitungi hiyo kunakwenda kuondoa kabisa athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya nishati chafu kama kuni na mkaa.

EKARI 291 ZA BANGI ZATEKETEZWA MKOANI MARA

July 24, 2026 Add Comment
Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo, amesema kilimo cha bangi katika Mkoa wa Mara kimepungua kwa takribani asilimia 80 kutokana na operesheni endelevu zinazotekelezwa na Serikali katika kukabiliana na uzalishaji wa dawa za kulevya.

WANAFUNZI WAHIMIZWA KUJIKITA KATIKA MASOMO YA SAYANSI KUNUFAIKA NA FURSA ZA SCHOLARSHIP ZA SERIKALI

July 24, 2026 Add Comment

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Hussein Mohamed Omar,  akiongea na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Bustani (hawapo pichani) alipotembelea shule hiyo na kukagua maabara mbili za Sayansi zilizojengwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).

TRAMEPRO YATAKA AKAUNTI BANDIA ZA MITANDAONI ZICHUKULIWE HATUA

Kajunason July 24, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO) limetoa tahadhari kwa wananchi kuhusu kuongezeka kwa vitendo vya utapeli wa mitandaoni vinavyotumia majina, picha na nembo za viongozi wa Serikali, taasisi na watu maarufu kwa lengo la kuwalaghai wananchi na kujipatia fedha kwa njia zisizo halali.

Katibu Mkuu wa TRAMEPRO ambaye pia ni mtaalamu wa tiba asili, Boniventura Mwalongo, alisema matapeli wamekuwa wakisambaza matangazo yanayodai viongozi, wafanyabiashara au taasisi mbalimbali zinatoa mikopo, ruzuku, misaada au fursa za uwekezaji wa haraka, huku wakitumia ushuhuda wa uongo kuwashawishi wananchi.

Mwalongo aliwataka wananchi kutothamini taarifa hizo bila kuzithibitisha kupitia mamlaka au taasisi husika, akisisitiza kuwa ni muhimu kutumia taarifa zinazotolewa kupitia njia rasmi pekee na kuepuka kutuma fedha, nyaraka au taarifa binafsi kwa watu wasiojulikana.

Alisema matumizi mabaya ya nembo za vyombo vya habari na majina ya viongozi wa kitaifa katika kusambaza taarifa za uongo yanachochea upotoshaji wa umma, hupunguza imani kwa taasisi na yanaweza kuhatarisha usalama, amani na mshikamano wa Taifa.

Mbali na hilo, TRAMEPRO imeeleza kuwa bado kuna haja ya kuimarisha mapambano dhidi ya mila potofu zinazodhuru afya, utu na haki za binadamu, ikibainisha kuwa baadhi ya vitendo hivyo vinaendelea kufanyika kwa siri katika maeneo mbalimbali nchini.

Shirika hilo limeitaka Serikali kuimarisha mapambano dhidi ya utapeli wa mitandaoni kwa kushirikisha vyombo vya dola na mamlaka zinazohusika, huku ikiendelea kutoa elimu kuhusu matumizi salama ya mitandao ya kijamii na huduma za kidijitali.

Aidha, TRAMEPRO imezitaka mamlaka za mawasiliano na usalama kuchukua hatua za haraka dhidi ya akaunti bandia na mitandao inayotumiwa kufanya utapeli, pamoja na kushirikiana na kampuni za mitandao ya kijamii kuziondoa akaunti zinazojifanya viongozi au taasisi.

Mwalongo amewataka wananchi kutokuwa wepesi wa kuamini matangazo yanayoahidi fedha, mikopo au ruzuku bila uthibitisho, akisisitiza umuhimu wa kuhakiki taarifa kupitia ofisi au tovuti rasmi.

Alisema jamii salama na yenye maendeleo endelevu hujengwa kwa msingi wa ukweli, elimu, uwajibikaji na ushirikiano, huku akitoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya utapeli wa mitandaoni, taarifa za uongo na mila potofu.

WAJASIRIAMALI BAGAMAYO WAPATIWA MAFUNZO MATUMIZI SALAMA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 23, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

KATIKA kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, Oryx Gas Tanzania imetoa mafunzo ya matumizi salama na sahihi ya gesi ya kupikia kwa makundi ya wajasiriamali mbalimbali yakiwemo mama na baba lishe.

BARRICK KUENDELEA KUNUFAISHA WATANZANIA KUPITIA UTEKELEZAJI WA SERA YA MAUDHUI YA NDANI

July 23, 2026 Add Comment

 


Waziri wa Madini , Anthony Mavunde akiongea kwenye ufunguzi wa Jukwaa la tano la utekelezaji wa ushirikishwaji wa watanzania kwenye sekta ya madini nchini, unaondelea jijini Mwanza.
Waziri wa Madini , Anthony Mavunde , akipata maelezo ya utekelezaji wa sheria na kanuni za Maudhui ya ndani kutoka kwa Meneja Ugavi wa Barrick, Victor Ndamgoba alipotembelea banda hilo

WAZIRI MAVUNDE AELEKEZA USIMAMIZI THABITI WA SHERIA ILI ASILIMIA 90 YA BIDHAA NA HUDUMA MIGODINI KUFANYWA NA WATANZANIA

July 22, 2026 Add Comment
-Ampongeza Rais Samia kwa kuwa kinara wa ushirikishwaji wa Watanzania migodini

TEA NA UNICEF WATEKELEZA MRADI WA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1 WA UJENZI WA VITUO 10 VYA ELIMU YA AWALI YA UFUNDI

July 22, 2026 Add Comment
Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), kwa kushirikiana na UNICEF, inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa vituo 10 vya Elimu ya Awali ya Ufundi (IPOSA) wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja, kwa lengo la kuwapatia fursa ya mafunzo ya ufundi vijana waliokosa kunufaika na elimu ya msingi kutokana na sababu mbalimbali.

Mradi huo unatekelezwa katika mikoa ya Dodoma, Tabora, Dar es Salaam, Kigoma na Songwe. Kwa sasa, ujenzi unaendelea vizuri na umefikia hatua ya maboma katika maeneo yote ya utekelezaji.

Katika kufuatilia maendeleo ya mradi huo, kuanzia Julai 20 hadi 21, 2026, timu ya wataalamu kutoka UNICEF ikiongozwa na Mhandisi Mohamed Hindi pamoja na Afisa Elimu Bi. Jennifer Mberesero, ilifanya ziara ya ukaguzi katika miradi inayotekelezwa mkoani Dodoma. Baada ya ukaguzi huo, timu hiyo ilifanya kikao kazi na wataalamu wa TEA wanaosimamia utekelezaji wa mradi.

Lengo la kikao hicho lilikuwa kujadili hatua zilizofikiwa, kutathmini maendeleo ya utekelezaji na kuimarisha ushirikiano kati ya pande hizo mbili ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotarajiwa.

Aidha, ujumbe huo ulikutana na Mkurugenzi Mkuu wa TEA Dkt. Erasmus Kipesha na kumpa taarifa kuhusu maendeleo ya mradi.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Mkurugenzi Mkuu Dkt. Kipesha aliwashukuru wataalamu wa TEA na UNICEF kwa usimamizi mzuri wa mradi na kuwataka kuendelea kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa ndani ya muda uliopangwa.