HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

RAIS MUSEVENI WA UGANDA AWASILI NCHINI KWA ZIARA RASMI

August 05, 2026 Add Comment

 




Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni, amewasili jijini Dar kwa ziara rasmi ya siku mbili kuanzia tarehe 5-6 Agosti 2026, kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Rais Museveni pamoja na ujumbe wake amepokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar Es Salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Mahmoud Thabit Kombo, pamoja na Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Kanali Mstaafu Fred Mwesigye na viongozi waandamizi wa Serikali.

Akiwa nchini, Rais Museveni anatarajiwa kufanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake, Rais Samia Suluhu Hassan Ikulu jijini Dar Es Salaam, yatakayojikita katika kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, biashara, uwekezaji, miundombinu na sekta nyingine za kimkakati kwa manufaa ya nchi zote mbili.

Ziara hii ni ya pili kwa Mheshimiwa Rais Museveni nchini Tanzania katika mwaka 2026. Ziara  yake yakwanza ilifanyika  Februari 2026, ambapo viongozi hao walijadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa pande mbili, pamoja na utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) uliofanyika mwezi Machi 2026.

Ziara hii inatarajiwa kutoa msukumo mpya katika utekelezaji wa maamuzi yaliyokwishafikiwa na kuimarisha zaidi ushirikiano wa kimkakati kati ya Tanzania na Uganda kwa manufaa ya wananchi wa nchi zote mbili.

TANZANIA KUNUFAIKA NA SH. BILIONI 10 ZA BIASHARA YA KABONI

August 05, 2026 Add Comment
Na; Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Tanzania inatarajiwa kuingiza zaidi ya Sh bilioni 10 kutokana na mauzo ya biashara ya kaboni baada ya Serikali kuidhinisha miradi minne itakayouza tani milioni 4.2 za kaboni katika soko rasmi la kimataifa la biashara ya Kaboni.
KAULIMBIU YA PSSSF YA ‘TUNALIPA JANA’ INAFANYIKA KWA VITENDO- WAZIRI SANGU

KAULIMBIU YA PSSSF YA ‘TUNALIPA JANA’ INAFANYIKA KWA VITENDO- WAZIRI SANGU

August 05, 2026 Add Comment



Lindi, Agosti 5, 2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema kaulimbiu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) ya "Tunalipa Jana" si kauli tu, bali inatekelezwa kwa vitendo na imeonyesha ukwasi wa Mfuko huo kupitia ulipaji wa mafao kwa wakati kwa wanachama wanaostaafu.

Mhe. Sangu ameyasema hayo Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo, Manispaa ya Lindi, ambapo alizungumza na wanachama, wastaafu na wananchi waliotembelea banda hilo.

"Wastaafu wengine wanashangaa kuona fedha zimeingia kwenye akaunti zao mara tu wanapotoka kazini na kujiuliza, 'Hizi fedha ni zangu kweli?' Hilo linaonesha wazi ukwasi wa Mfuko wa PSSSF na utekelezaji wa kaulimbiu ya Tunalipa Jana," amesema Mhe. Sangu.

Ameongeza kuwa hata wastaafu wanaopokea pensheni za kila mwezi hulipwa ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi, na wakati mwingine hupokea malipo yao kabla ya watumishi walio bado kazini kupokea mishahara yao.

"Wastaafu wetu tumewapa kipaumbele. Mafanikio haya yametokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo yameuwezesha Mfuko kuendelea kukua na kutoa huduma bora kwa wanachama na wastaafu," amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw. Jafari Merai Mgala, amesema mafanikio ya utoaji wa huduma kwa haraka na kwa ufanisi yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na maboresho ya mifumo ya TEHAMA.

Amesema kwa sasa mwanachama au mstaafu anaweza kuwasilisha madai ya mafao akiwa mahali popote kupitia simu janja, kompyuta au kifaa kingine chenye uwezo wa kuunganishwa na intaneti, hatua iliyorahisisha upatikanaji wa huduma za Mfuko.

"Natoa wito kwa wanachama na wananchi wote wa Kanda ya Kusini kutembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Nanenane ili kupata elimu kuhusu huduma zetu pamoja na kufahamu fursa mbalimbali zinazotolewa na Mfuko," amesema Bw. Mgala.

Mwisho

KAULIMBIU YA PSSSF YA ‘TUNALIPA JANA’ INAFANYIKA KWA VITENDO- WAZIRI SANGU

August 05, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (MB) (Mwenye Suti) akisikiliza maelezo ya Huduma zinazopatikana katika banda la Mfuko wa PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Mahusiano,  Mh.Deus Sangu (MB) (wanne kushoto),  akipokea zawadi toka kwa Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw.  Jafari Merai Mgala, alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini, Viwanja vya Nganga Mkoani Lindi Agosti 5, 2026.

Wananchi wakiwa kwenye banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu, alipokuwa akizungumza kwenye Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini kwenye Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi Agosti 5, 2026

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu (MB) (Mwenye Suti) akiwasili kwenye Banda la PSSSF ndani ya maonesho ya Kilimo (Nanenane)  yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo Manispaa ya Lindi, Agosti 5, 2026.

Lindi, Agosti 5, 2026


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema kaulimbiu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) ya "Tunalipa Jana" si kauli tu, bali inatekelezwa kwa vitendo na imeonyesha ukwasi wa Mfuko huo kupitia ulipaji wa mafao kwa wakati kwa wanachama wanaostaafu.

Mhe. Sangu ameyasema hayo Agosti 5, 2026, alipotembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Kusini yanayoendelea katika Viwanja vya Ngongo, Manispaa ya Lindi, ambapo alizungumza na wanachama, wastaafu na wananchi waliotembelea banda hilo.

"Wastaafu wengine wanashangaa kuona fedha zimeingia kwenye akaunti zao mara tu wanapotoka kazini na kujiuliza, 'Hizi fedha ni zangu kweli?' Hilo linaonesha wazi ukwasi wa Mfuko wa PSSSF na utekelezaji wa kaulimbiu ya Tunalipa Jana," amesema Mhe. Sangu.

Ameongeza kuwa hata wastaafu wanaopokea pensheni za kila mwezi hulipwa ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi, na wakati mwingine hupokea malipo yao kabla ya watumishi walio bado kazini kupokea mishahara yao.

"Wastaafu wetu tumewapa kipaumbele. Mafanikio haya yametokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo yameuwezesha Mfuko kuendelea kukua na kutoa huduma bora kwa wanachama na wastaafu," amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa PSSSF Kanda ya Kusini, Bw. Jafari Merai Mgala, amesema mafanikio ya utoaji wa huduma kwa haraka na kwa ufanisi yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na maboresho ya mifumo ya TEHAMA.

Amesema kwa sasa mwanachama au mstaafu anaweza kuwasilisha madai ya mafao akiwa mahali popote kupitia simu janja, kompyuta au kifaa kingine chenye uwezo wa kuunganishwa na intaneti, hatua iliyorahisisha upatikanaji wa huduma za Mfuko.

"Natoa wito kwa wanachama na wananchi wote wa Kanda ya Kusini kutembelea banda la PSSSF katika Maonesho ya Nanenane ili kupata elimu kuhusu huduma zetu pamoja na kufahamu fursa mbalimbali zinazotolewa na Mfuko," amesema Bw. Mgala.

Mwisho

TIRDO YATUMIA TEKNOLOJIA KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YA KILIMO

August 05, 2026 Add Comment
SHIRIKA la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limesema linaendelea kuwasaidia wakulima na wajasiriamali kuongeza thamani ya mazao, kupunguza gharama za uzalishaji na kupata masoko kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa, maabara za ubora na suluhisho za nishati.
WAKAGUZI WA MAFUTA WAIMARISHA UDHIBITI WA UBORA WAKATI WA UPAKUAJI

WAKAGUZI WA MAFUTA WAIMARISHA UDHIBITI WA UBORA WAKATI WA UPAKUAJI

August 05, 2026 Add Comment

Serikali, kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), inasimamia upakuaji wa shehena za mafuta kutoka melini hadi kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta, ili kuhakikisha usalama na uzingatiaji wa viwango vya ubora vinavyotakiwa.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, Afisa Ubora wa Mafuta wa PBPA, Mhandisi Cyrill Makembe, amesema mchakato wa upakuaji wa mafuta unahusisha hatua mbalimbali zinazohitaji uangalizi wa karibu wa wataalamu.

Amesema Wakaguzi wa Mafuta (Petroleum Inspectors) hufuatilia mchakato mzima wa upakuaji ili kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa na ubora wa mafuta unalindwa katika kila hatua.

“Mafuta yanapowasili nchini, Wakaguzi wa Mafuta hufuatilia hatua mbalimbali za upakuaji ili kuhakikisha yanakidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa,” amesema Mhandisi Makembe.

Ameeleza kuwa ufuatiliaji huo huanza mafuta yakiwa ndani ya meli na kuendelea wakati wa upakuaji na usafirishaji kupitia miundombinu maalumu, hadi yanapofikishwa kwenye maghala yaliyokusudiwa kwa ajili ya kuhifadhiwa.

Kwa mujibu wa Mhandisi Makembe, Baada ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuidhinisha ubora wa bidhaa za mafuta kabla Meli haijaanza zoezi la Upakuaji ,Wakaguzi wa Mafuta wanajukumu la kuhakikisha kuwa taratibu za usalama na masharti ya upakuaji yanazingatiwa katika mchakato mzima wa upakuaji wa mafuta hayo. Hatua hiyo inalenga kulinda ubora wa mafuta na kuhakikisha shughuli za upakuaji zinafanyika kwa usalama.

Aidha, ukaguzi huo unalenga kubaini mapema changamoto zozote zinazoweza kuathiri ubora wa mafuta wakati wa upakuaji, usafirishaji au uhifadhi. Hatua hiyo husaidia kuhakikisha mafuta yanayopokelewa yanaendelea kuwa katika hali inayokubalika na TBS hadi yanapofikishwa kwenye maghala husika.

TRAMEPRO YAHIMIZA UNYONYESHAJI KWA AFYA YA MAMA NA MTOTO

Kajunason August 05, 2026 Add Comment
Dar es Salaam, Agosti 5, 2026 – Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira Tanzania (TRAMEPRO) limetoa wito kwa Serikali, wataalamu wa afya, wataalamu wa tiba asili, wakunga, wadau wa mazingira na jamii kwa ujumla kushirikiana katika kulinda afya na uhai wa mama na mtoto, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Duniani yanayoendelea kuanzia Agosti 1 hadi 7, 2026.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, TRAMEPRO limesema linaungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Shirika la Afya Duniani (WHO), UNICEF, Wizara ya Afya na wadau wengine wa afya duniani katika kuhamasisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama kama njia muhimu ya kuboresha afya ya watoto na akina mama.

Shirika hilo limeeleza kuwa Wiki ya Unyonyeshaji Duniani ilianzishwa mwaka 1992 na World Alliance for Breastfeeding Action (WABA) kwa ushirikiano na WHO na UNICEF, kufuatia Azimio la Innocenti la mwaka 1990, lenye lengo la kulinda, kuhamasisha na kuunga mkono unyonyeshaji wa maziwa ya mama duniani.

Kwa mujibu wa TRAMEPRO, unyonyeshaji wa maziwa ya mama ni moja ya njia bora za kupunguza vifo vya watoto wachanga na kuboresha afya ya mama. Shirika hilo limeunga mkono mapendekezo ya WHO yanayosisitiza mtoto kuanza kunyonya ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa, kupewa maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya kwanza, na kuendelea kunyonyeshwa pamoja na vyakula vya nyongeza hadi miaka miwili au zaidi.

TRAMEPRO pia limebainisha kuwa Tanzania hupata wastani wa watoto kati ya milioni 2.2 na 2.4 wanaozaliwa hai kila mwaka, huku Afrika ikichangia takribani asilimia 70 ya vifo vya akina mama duniani. Aidha, zaidi ya watoto wachanga milioni moja hufariki kila mwaka barani humo kutokana na sababu zinazoweza kuzuilika, ikiwemo kuzaliwa kabla ya wakati, maambukizi, kukosa hewa wakati wa kuzaliwa na utapiamlo.

Shirika hilo limeeleza kuwa afya ya mama na mtoto haiwezi kutenganishwa na mazingira bora, likisisitiza umuhimu wa upatikanaji wa maji safi, lishe bora, usafi wa mazingira, hewa safi na uhifadhi wa bioanuwai. Pia limefafanua kuwa mimea tiba, ambayo ni sehemu ya tiba asili, hutegemea mazingira salama na uhifadhi wa misitu pamoja na vyanzo vya maji.

Katika taarifa hiyo, TRAMEPRO limetoa wito maalumu kwa wataalamu wa tiba asili, wakunga wa jadi na wakunga wataalamu kuzingatia sheria, maadili ya taaluma na ushahidi wa kisayansi katika utoaji wa huduma. Pia limewahimiza kuwashauri wajawazito kuhudhuria kliniki mapema, kujifungulia katika vituo vya afya, kutambua dalili za hatari mapema na kushirikiana kwa karibu na wataalamu wa afya ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Aidha, shirika hilo limetoa wito kwa Serikali kuendelea kuwekeza katika huduma za afya ya uzazi, kuongeza idadi ya wakunga na wahudumu wa afya, kuimarisha lishe, chanjo, maji safi na usafi wa mazingira, pamoja na kuwekeza katika tafiti za tiba asili salama.

TRAMEPRO pia limealika Wizara, taasisi za Serikali, mashirika ya kimataifa, asasi za kiraia, vyuo vikuu, taasisi za utafiti, sekta binafsi na washirika wa maendeleo kushirikiana katika kuendeleza tafiti, elimu ya afya, uhifadhi wa mimea tiba na ulinzi wa mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Shirika hilo limemalizia kwa kusisitiza kuwa kulinda afya ya mama na mtoto ni jukumu la kila mwananchi na kwamba ushirikiano kati ya sekta ya afya, tiba asili na uhifadhi wa mazingira ni msingi wa kujenga Taifa lenye watoto wenye afya, akina mama salama na maendeleo endelevu.

TAASISI 54 ZA UMMA KUWASILISHA TAARIFA ZA UTENDAJI WA UWEKEZAJI BUNGENI

August 05, 2026 Add Comment


      

Dodoma. Jumla ya taasisi za umma 54 zinatarajiwa kuwasilisha taarifa za utendaji wa uwekezaji mbele ya Kamati za Kudumu za Bunge kwa muda wa wiki tatu, katika mchakato unaolenga kuwezesha uchambuzi wa thamani na utendaji wa mitaji ya umma pamoja na utekelezaji wa mipango ya kimkakati ya taasisi husika.

MKANDARASI AKAMILISHA AWAMU YA KWANZA UVUTAJI NYAYA MRADI WA CHALINZE–DODOMA

August 05, 2026 Add Comment





➡️ TANESCO yawashukuru wateja kwa uvumilivu na kutangaza awamu ya pili kuanza Agosti 11–14 katika maeneo ya Kikombo na Mkonze - Dodoma

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema Mkandarasi amekamilisha kwa mafanikio awamu ya kwanza ya kazi za uvutaji wa nyaya katika eneo la Mkambarani, Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya hatua za mwisho za utekelezaji wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa habari Agosti 5, 2026 katika eneo la Mkambarani, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Bi. Irene Gowelle, amesema zoezi hilo, ambalo lilipangwa kufanyika ndani ya siku sita, limekamilika kwa mafanikio na kwa wakati uliopangwa, hatua ambayo imewezesha kurejea kwa huduma ya umeme katika mikoa yote iliyokuwa imeathiriwa na kazi hiyo na kufanya shughuli kuendelea kama kawaida.

Bi. Gowelle amesema kukamilika kwa mradi huo kutaimarisha na kuongeza uwezo wa Gridi ya Taifa, hatua itakayowezesha usafirishaji wa umeme kwa uhakika zaidi katika maeneo mbalimbali nchini na hivyo kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla

Aidha amewashukuruwananchi na wateja wa TANESCO kwa uvumilivu, ushirikiano waliouonesha katika kipindi chote cha utekelezaji wa kazi hizo.


Ameongeza kuwa TANESCO itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya umeme kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma hiyo nchini.

“Kazi hii imefanyika kwa mafanikio makubwa na kwa wakati uliopangwa. Tunawashukuru sana wateja wetu kwa uvumilivu wao. Kwa sasa huduma ya umeme imerejea kama kawaida. Hata hivyo, napenda kuwakumbusha kuwa zoezi hili litaendelea kwa awamu ya pili katika maeneo ya Mkonze na Kikombo kuanzia Agosti 11 hadi 14. Tutawatangazia ratiba mapema ili muweze kupanga shughuli zenu kulingana na ratiba ya upatikanaji wa umeme,” alisema Bi. Gowelle.






Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Chalinze–Dodoma, Mhandisi Newton Mwakifwamba, amesema awamu ya kwanza ya uvutaji wa nyaya ilitekelezwa katika eneo la Mkambarani, ikihusisha uvutaji wa nyaya juu ya reli ya SGR, juu ya njia za umeme za Msongo wa Kilovolti 220 za Morogoro I na Morogoro II, pamoja na njia ya Msongo wa Kilovolti 132, na kwamba kazi zote zimefanyika kwa ufanisi mkubwa.

Ameeleza kuwa awamu ya pili ya uvutaji wa nyaya itafanyika katika maeneo ya Kikombo na Mkonze Dodoma kuanzia Agosti 11 hadi 14, ambapo shughuli hizo zitafanyika kwa wakati mmoja. Kutokana na hali hiyo, kutakuwa na katizo la umeme kwa muda katika baadhi ya maeneo ili kutoa nafasi ya utekelezaji salama wa kazi hizo.




“Umuhimu wa mradi huu ni mkubwa kwa kuwa utaongeza uwezo wa njia zilizopo za kusafirisha umeme. Mradi huu wa Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma utaimarisha uwezo wa Gridi ya Taifa na kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme nchini"alisisitiza Mha. Mwakifwamba

Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma umefikia asilimia 94 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika Agosti 21, 2026. Kukamilika kwake kutaongeza uwezo wa mfumo wa usafirishaji wa umeme nchini na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme yenye ubora na uhakika kwa wananchi.

WAMILIKI VITUO VYA KULEA WATOTO WAHIMIZWA KUWEKEZA KWA WALEZI WENYE TAALUMA

August 05, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

WAMIKI wa vituo vya kulelea watoto nchini wamehimizwa kuwekeza katika mafunzo ya kitaalamu kwa walezi ili kuboresha ubora wa huduma za malezi na makuzi ya awali ya watoto, kufuatia kuongezeka kwa mahitaji ya wataalamu katika sekta hiyo.

BARRICK NORTH MARA YAZIDI KUBORESHA MAISHA YA WANANCHI TARIME KUPITIA UTEKELEZAJI WA MKAKATI ENDELEVU

August 05, 2026 Add Comment

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Michael Mwang'onda (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Gowele (kushoto mwenye skafu) wakifurahia uwekaji jiwe la msingi wa jengo la mama na mtoto katika kituo cha afya Magoto kata ya Nyaikonga mradi unaogharamiwa na Barrick North Mara.

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KUDHIBITI TAKA ZA PLASTIKI.

August 05, 2026 Add Comment
Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha kunakuwa na uwiano kati ya udhibiti wa taka za plastiki, ulinzi wa mazingira na ukuaji wa sekta ya viwanda ili uchumi wa nchi uendelee kuimarika.

GOVERNMENT URGED TO RECOGNIZE COMMUNITY NETWORKS TO BRIDGE TANZANIA’S DIGITAL DIVIDE

August 05, 2026 Add Comment

  


By Rose Ngunangwa

The government has been urged to legally recognize Community Networks within Tanzania’s ICT policy and regulatory framework to expand internet connectivity in underserved areas and promote sustainable development.
TBA YAFUNGUA FURSA MPYA ZA UWEKEZAJI KATIKA MAKAZI NA MAJENGO YA BIASHARA

TBA YAFUNGUA FURSA MPYA ZA UWEKEZAJI KATIKA MAKAZI NA MAJENGO YA BIASHARA

August 04, 2026 Add Comment
 

Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

Na.Mwandishi Wetu

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umefungua fursa mpya za uwekezaji katika sekta ya makazi, majengo ya biashara na maendeleo ya miji, hatua inayolenga kuboresha huduma kwa wananchi, kuvutia mitaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Meneja wa TBA Mkoa wa Dodoma, Qs. Emmanuel Wambura, amesema hayo katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma.

Amesema TBA imeendelea kutekeleza kwa ufanisi miradi mbalimbali ya Serikali katika sekta tofauti, ikiwemo ujenzi wa majengo ya Wizara ya Kilimo na taasisi zake, ofisi za Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), vituo vya afya pamoja na taasisi nyingine za umma.

Kwa mujibu wa Qs. Wambura, utekelezaji wa miradi hiyo unalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha mazingira ya kazi katika taasisi za Serikali.

“TBA inaendelea kutekeleza dhamana yake ya kuhakikisha Serikali inapata majengo bora, salama na ya kisasa. Miradi mingi ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, huku mingine ikiwa katika hatua za mwisho kukamilika ili wananchi waanze kunufaika na huduma zinazotolewa kupitia miundombinu hiyo,” amesema Qs. Wambura.

Amesema mbali na miradi ya Serikali, TBA imeweka mkazo katika kuendeleza miradi ya makazi na miji ya kisasa, ikiwemo mradi wa ujenzi wa nyumba 3,500 katika eneo la Nzuguni jijini Dodoma, ambao unaendelea kutekelezwa.

Amebainisha kuwa wakala huo umefungua fursa za uwekezaji kupitia mfumo wa ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP), ambapo tayari baadhi ya wawekezaji, ikiwemo kampuni ya Fit Group kutoka Nigeria, wameonyesha nia ya kuwekeza katika mradi huo wa makazi.

Aidha, amesema TBA imeandaa maeneo yenye fursa kubwa za uwekezaji katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Arusha, ambapo wawekezaji wanakaribishwa kuwekeza katika nyumba za makazi, majengo ya biashara, hoteli, ofisi na maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao.

Qs. Wambura amefafanua kuwa Mkoa wa Dodoma pekee una eneo la takribani hekta 630 lililoandaliwa kwa ajili ya uwekezaji, likiwa na miundombinu muhimu na mazingira rafiki kwa shughuli za biashara.

“Taratibu za uwekezaji ni wazi na rahisi. Tunawakaribisha Watanzania na wawekezaji kutoka nje ya nchi kushirikiana nasi katika kuendeleza miradi yenye tija kwa uchumi wa Taifa. Tunahitaji wawekezaji wenye uwezo na wanaozingatia sheria za nchi ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa,” amesema.

Katika hatua nyingine, amesema TBA imepanua wigo wa shughuli zake hadi kusimamia miradi ya ujenzi na ukarabati wa majengo ya ubalozi wa Tanzania nje ya nchi kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Amesema hatua hiyo inaonesha kuendelea kuaminiwa kwa uwezo wa kitaalamu wa wakala huo katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ndani na nje ya Tanzania.

Akizungumzia mchango wa TBA katika sekta ya kilimo, Qs. Wambura amesema wakala huo umeendelea kubuni na kusimamia ujenzi wa maghala ya kisasa ya kuhifadhi mazao, maabara za utafiti wa kilimo na miundombinu mingine muhimu inayosaidia kuongeza thamani ya mazao, kuimarisha usalama wa chakula na kukuza ushindani wa sekta hiyo.

Amewakaribisha wananchi, taasisi na wawekezaji kutembelea banda la TBA katika Maonesho ya Nanenane ili kupata taarifa kuhusu huduma zinazotolewa na wakala huo, ikiwemo usanifu wa majengo, ukadiriaji wa gharama za ujenzi, usimamizi wa miradi na fursa mbalimbali za uwekezaji.

“TBA ipo katika mikoa yote 26 ya Tanzania na itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kujenga miundombinu ya kisasa, kuvutia uwekezaji na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,” amesema Qs. Wambura.

Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Dodoma, QS Emmanuel Wambura,akizungumza kwenye banda la TBA  katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni jijini Dodoma.

DKT. TAUSI AONGOZA KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU CHA KUJADILI UTENDAJI WA MRADI WA BRT

August 04, 2026 Add Comment
Na. Mwandishi Wetu – Dar es Salaam

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida ameongoza kikao cha Makatibu Wakuu kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Dkt. Jim Yonazi kilicholenga kujadili utendaji wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka -BRT leo 04 Agosti, 2026 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es Salaam.
TFC YAWAKIKISHIA UPATIKANAJI WA MBOLEA, TANI 33,000 ZA DAP ZAANZA KUSAMBAZWA

TFC YAWAKIKISHIA UPATIKANAJI WA MBOLEA, TANI 33,000 ZA DAP ZAANZA KUSAMBAZWA

August 04, 2026 Add Comment

Serikali kupitia Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) imewahakikishia wakulima nchini upatikanaji wa mbolea ya kutosha kwa msimu wa kilimo wa mwaka huu, ikitangaza kuanza kwa usambazaji wa tani 33,000 za mbolea ya kupandia aina ya DAP zilizowasili nchini kupitia Bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza leo Agosti 4,2026 katika Maonesho ya 49 ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea kitaifa katika viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Uendeshaji Biashara wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), Lameck Borega, amesema kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha wakulima wanapata mbolea kwa wakati, kwa bei nafuu na katika maeneo yote ya nchi.

Amesema TFC, ambayo ni kampuni inayomilikiwa kwa asilimia 100 na Serikali chini ya Wizara ya Kilimo, ina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa mbolea kwa wakulima wote ili kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Bw.Borega amesema kwa msimu wa mwaka huu kampuni imepanga kusambaza takribani tani 200,000 za mbolea za aina mbalimbali, huku meli ya MV Aurora ikiwa tayari imewasili na tani 33,000 za mbolea ya DAP ambazo zimeanza kusafirishwa kwenda vituo vya TFC na kwa mawakala wake nchini kote.

"Mbolea hii imewasili kwa wakati muafaka wakati wakulima wengi wanaendelea kuandaa mashamba yao kwa ajili ya msimu mpya wa kilimo. Lengo letu ni kuhakikisha hakuna mkulima anayekosa mbolea kutokana na ucheleweshaji wa usambazaji," amesema Borega.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kubeba sehemu kubwa ya gharama za mbolea kupitia mpango wa ruzuku ili kupunguza mzigo kwa wakulima. Alifafanua kuwa mfuko mmoja wa kilo 50 wa mbolea ya DAP ungegharimu karibu shilingi 200,000 bila ruzuku, lakini kutokana na msaada wa Serikali mkulima analipa karibu nusu ya gharama hiyo huku Serikali ikigharamia sehemu iliyobaki.

Amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya kuongeza tija katika sekta ya kilimo kwa kuhakikisha pembejeo muhimu zinapatikana kwa gharama zinazomuduwa na wakulima.

Bw.Borega ameongeza kuwa baada ya kukamilika kwa usambazaji wa mbolea ya kupandia, Serikali inatarajia kuingiza nchini tani 40,000 za mbolea ya kukuzia aina ya Urea mwezi Septemba, hatua itakayowezesha wakulima kupata pembejeo zote muhimu katika kipindi sahihi cha uzalishaji.

"Niwaondoe wasiwasi wakulima wote nchini Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha mbolea inapatikana kwa wakati na kwa mfumo wa ruzuku ili kila mkulima aweze kunufaika na kuongeza uzalishaji wa mazao," amesema 

Sambamba na hilo,Bw. Borega amewataka wakulima wanaotembelea Maonesho ya Nanenane kutembelea  banda la TFC ili kupata elimu ya matumizi sahihi ya mbolea, namna ya kunufaika na mfumo wa ruzuku na mahali pa kupata mbolea hizo.

Amesema TFC pia inaendelea kushiriki maonesho ya Nanenane katika kanda mbalimbali nchini ikiwemo Mbeya, Arusha, Mwanza, Simiyu, Iringa na Morogoro, ambako wakulima wanaendelea kupewa elimu ya kitaalamu kuhusu matumizi bora ya mbolea na njia rahisi za kuzipata kupitia mtandao wa vituo na mawakala wa kampuni hiyo.

Hata hivyo amesisitiza kuwa matumizi sahihi ya mbolea ni nguzo muhimu ya kuongeza tija ya kilimo, hivyo akawataka wakulima kutumia fursa ya maonesho hayo kupata elimu itakayowawezesha kuongeza uzalishaji na kuinua kipato chao.

PASTEL, VICHEKO NA SERENGETI PREMIUM APPLE: NDANI YA SHEREHE KUBWA YA MARAFIKI DAR ES SALAAM

August 04, 2026 Add Comment

Urafiki wa kweli ulipata nafasi ya kuadhimishwa kwa namna ya kipekee wakati wanawake kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam walipokutana katika hafla ya Girlfriends Circle, iliyoandaliwa na kampuni ya Eventfully kwa kushirikiana na Serengeti Premium Apple.

SERIKALI YASISITIZA KATAZO LA MIFUKO YA PLASTIKI

August 04, 2026 Add Comment
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Yussuf Masauni pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga(katikati) wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi wakati wa Mkutano wa Wadau Kuhusu Udhibiti wa Taka za Plastiki Nchini, kilichofanyika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam, Agosti 4, 2026.
MFUMO WA SCADA WAIMARISHA UDHIBITI WA MAFUTA NCHINI

MFUMO WA SCADA WAIMARISHA UDHIBITI WA MAFUTA NCHINI

August 04, 2026 Add Comment
 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Mfumo wa Supervisory Control and Data Acquisition (SCADA) yameimarisha udhibiti wa upotevu wa mafuta wakati wa shughuli za ushushaji kutoka melini kwenda kwenye maghala ya kuhifadhia.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, Mhandisi wa PBPA, Bi. Elvira Muganga, alisema mfumo huo unaiwezesha Serikali kufuatilia kwa wakati halisi kiwango cha mafuta kinachopokelewa nchini.

Alisema SCADA hukusanya taarifa kutoka kwenye mita za Serikali zilizowekwa katika maeneo ya kupokelea mafuta na kuziwezesha kulinganishwa na taarifa za mita zilizopo kwenye maghala ya kuhifadhia mafuta.

“Ulinganishaji huu unasaidia kubaini tofauti zinazoweza kujitokeza wakati wa ushushaji na kuhakikisha kiasi cha mafuta kilichopokelewa kinarekodiwa kwa usahihi,” alisema Bi. Muganga.

Alieleza kuwa kabla ya matumizi ya teknolojia hiyo, ufuatiliaji wa shughuli za ushushaji wa mafuta ulikuwa unategemea zaidi taarifa zilizokusanywa kwa njia zisizo za moja kwa moja. Mfumo wa SCADA sasa umeongeza uwezo wa Serikali kupata taarifa sahihi kwa wakati na kusimamia operesheni hizo kwa karibu.

Kwa mujibu wa Muganga, udhibiti huo umeongeza uwazi na usalama katika mapokezi ya mafuta pamoja na kuimarisha usahihi wa taarifa zinazotumika katika ukokotoaji wa mapato ya Serikali.

Aidha, alisema matumizi ya mfumo huo yameifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazotumia teknolojia ya kidijitali kusimamia mapokezi ya bidhaa za mafuta na kudhibiti upotevu unaoweza kutokea wakati wa ushushaji.

Muganga alisema PBPA inatumia Maonesho ya Nanenane kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utendaji wa mfumo huo na mchango wake katika kuhakikisha mafuta yanayoingia nchini yanasimamiwa kwa uwazi na ufanisi.

Aliwahimiza wananchi na wadau wa sekta ya nishati kutembelea banda la PBPA ili kufahamu zaidi kuhusu mfumo wa SCADA, Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja na majukumu mengine ya Wakala.

 

WIZARA YA NISHATI YAENDELEA KUHUDUMIA WANANCHI.

August 04, 2026 Add Comment

 

Wataalam wa Wizara ya Nishati wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya NaneNane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma.

Wizara inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala ya umeme, mafuta, gesi asilia, nishati safi ya kupikia pamoja na fursa mbalimbali zinazopatikana katika sekta ya nishati.


Unapotembelea Maonesho ya NaneNane, karibu utembelee Banda la Wizara ya Nishati na taasisi zake lililopo Government Pavilion Na. 2.