HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP) YAWAFIKIA WAKULIMA,WAVUVI NA JAMII YA WAFUGAJI MKOANI TANGA

September 07, 2026 Add Comment




Na; Mwandishi wetu-Tanga.


Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa la Kuendeleza Kilimo (IFAD) na wataalamu kutoka katika sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) wamekutana Mkoani Tanga Tarehe 7 Septemba 2026  kwa lengo la kufanya mapitio ya Utekelezaji wa Programu hiyo.


Sambamba na hilo timu hiyo itatembelea maeneo yanayotekeleza Programu kwa Mkoa wa Tanga, ambapo kwa upande wa sekta ya kilimo  timu hiyo itatembelea kata ya Msomela iliyopo katika Halmashauri ya Handeni Vijijini ambako programu imehamasisha na kutoa elimu ya kilimo bora kwa jamii ya kimasai ambao kiasili ni wafugaji ambapo wameweza kujishughulisha na kilimo cha mahindi chenye tija. 

Programu imewezesha kuwepo kwa eneo la mashamba darasa (FFS) kwa mazao ya Alizeti, Mahindi na Maharage, na shamba Darasa hilo limeonesha mafanikio kwa kiasi kikubwa, ambapo hekta moja inaweza kuzalisha takribani magunia 20 ya kilo mia moja kila moja, na jamii ya wafugaji sasa inajishulisha na shughuli za Kilimo na kunufaika na upatikanaji wa mazao yanayolimwa.

Kwa upande wa Sekta ya Uvuvi, Programu inaendelea na ujenzi wa soko la kimataifa la Samaki Kipumbwi lililloko katika halmashauri ya Pangani ambapo mpaka sasa ujenzi umefikia asilimia 68% na linategemewa kukamilika ifikapo Oktoba 2026.


Aidha, programu pia inaendelea na ujenzi wa vichanja 40 vya kukaushia dagaa ambavyo vinaweza kukausha takribani tani tano kwa za dagaa kwa wakati mmoja.

Kwa upande mwingine pia Programu ya AFDP inaendelea na ujenzi wa Ghala la baridi na mtambo wa barafu katika soko hilo kwa ajili ya kuhifadhi na kusafirisha samaki.

Awali Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la kimataifa la maendeleo ya Kilimo nchini (IFAD) Bw. Seth Meng alikutana na Kaimu Katibu tawala wa Mkoa wa Tanga Bw.Emmanuel Kisongo na kufanya mazungumzo kuhusiana na utekelezaji wa Programu katika Mkoa sambamba na mafanikio tarajiwa kwa wanachi wa maeneo husika ambapo Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa alieleza kuwa Programu hiyo ni muhimu sana katika kuhamasisha maendeleo ya kilimo na uvuvi katika mkoa huo. 


Aliishukuru IFAD kwa kuweza kuwafikia wananchi wa mkoa huo na kuwataka ikiwezekana kuongeza uwekezaji mkoani hapo.

TANESCO YATUNUKIWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WA UBUNIFU NA MAENDELEO YA NISHATI

September 07, 2026 Add Comment

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya kwa kutambua mchango wa kipekee katika ubunifu na maendeleo ya sekta ya Nishati nchini  ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa Shirika katika kuendeleza sekta hiyo.


Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO katika hafla ya tuzo za ujenzi wa miundombinu na uchimbaji madini kwa mwaka 2026, iliyofanyika Septemba 4, 2026 jijini Dar es Salaam.


Akikabidhi tuzo hiyo Mkurugenzi wa Usajili wa Wakandarasi Wizara ya Ujenzi Mhandisi Rhoben Nkori kwa Niaba ya Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amelipongeza Shirika kwa kuendelea kuimalisha upatikanaji wa Umeme katika Maeneo mbalimbali hapa nchini Hali ambayo imekuwa Chachu ya kuchochea Maendeleo katika sekta mbalimbali hapa nchini.


Tuzo hiyo imetolewa na Chama cha Ujenzi na Miundombinu cha Tanzania (CCIT), ikiwa ni utambuzi wa mchango wa TANESCO katika ubunifu na maendeleo ya nishati nchini.

CRDB NA TRA SACCOS WAZINDUA PESACARD, WANACHAMA KUPATA HUDUMA KWA URAHISI

Kajunason September 06, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, 5 Septemba 2026 – Benki ya CRDB kwa kushirikiana na TRA SACCOS imezindua rasmi TRA SACCOS PESACARD, kadi mpya inayotumia mfumo wa Visa inayolenga kuwapa wanachama wa TRA SACCOS urahisi, uhuru na wigo mpana zaidi wa kupata na kutumia fedha zao, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya TRA SACCOS.

Uzinduzi huo ni hatua muhimu katika ushirikiano wa muda mrefu kati ya Benki ya CRDB na TRA SACCOS, na unaashiria awamu mpya ya mageuzi ya kidijitali katika utoaji wa huduma za kifedha kwa wanachama wa SACCOS hiyo.

Kupitia TRA SACCOS PESACARD, wanachama wataunganishwa na mfumo mpana wa malipo wa Visa na hivyo kuwa na uwezo wa kutoa fedha kupitia ATM pamoja na kufanya malipo katika vituo vya POS vinavyokubali Visa ndani na nje ya Tanzania. 

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel  Chongolo aliipongeza TRA SACCOS kwa kufikisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake, huku akiipongeza Benki ya CRDB kwa kuendelea kutumia uwezo wake wa kiteknolojia na kifedha kusaidia taasisi mbalimbali kupanua huduma za kisasa za kifedha.

“Miaka 20 ni hatua kubwa inayodhihirisha uimara, uaminifu na mchango wa TRA SACCOS katika kuboresha ustawi wa kifedha wa wanachama wake. Nawapongeza viongozi na wanachama kwa kuendelea kubadilika kulingana na mahitaji ya wakati, na Benki ya CRDB kwa kutumia uwezo wake wa kifedha na kiteknolojia kujenga ushirikiano unaorahisisha upatikanaji wa huduma. Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD unaonesha mafanikio tunayoweza kuyapata pale taasisi za fedha na vyama vya ushirika vinapounganisha nguvu katika kukuza ubunifu na ujumuishi wa kifedha.”

Pamoja na uzinduzi wa kadi hiyo, ushirikiano huo umewezesha kuunganishwa moja kwa moja kwa mifumo ya TRA SACCOS na mifumo ya Benki ya CRDB. Maboresho hayo yanamaanisha kuwa mwanachama anaweza kutumia akaunti yake iliyopo ndani ya mfumo wa TRA SACCOS kupata huduma zinazohusiana na PESACARD bila kulazimika kuwa na akaunti katika benki nyingine ya biashara. 

Muunganiko huo pia unatarajiwa kuongeza ufanisi katika utoaji wa mikopo kwa wanachama. Fedha za mikopo zitaweza kutolewa moja kwa moja kupitia mfumo wa TRA SACCOS, hatua inayopunguza michakato ya kuhamisha fedha kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine na hivyo kupunguza muda wa mwanachama kusubiri fedha baada ya mkopo wake kuidhinishwa. 

Katibu wa Benki ya CRDB, Pascal Mihayo, alisema hatua hiyo inaakisi dhamira ya Benki ya kutumia teknolojia na ushirikiano wa kimkakati kutengeneza suluhisho zinazojibu mahitaji halisi ya wateja.

“Kwetu Benki ya CRDB, huu ni zaidi ya uzinduzi wa kadi. Ni uthibitisho wa namna ushirikiano wa muda mrefu unavyoweza kukua na kuzaa suluhisho zinazogusa maisha ya watu moja kwa moja. Kupitia TRA SACCOS PESACARD na muunganiko wa mifumo yetu, tunawapa wanachama uhuru zaidi wa kupata na kutumia fedha zao, huku tukiiwezesha TRA SACCOS kuongeza kasi na ufanisi wa utoaji wa huduma. Haya ndiyo mageuzi ya kidigitali tunayoyasimamia, teknolojia inayorahisisha huduma, inayozisogeza karibu na wananchi na inayoongeza thamani halisi kwa mtumiaji.”

Miongoni mwa maboresho mengine muhimu ni kuunganishwa kwa huduma za TRA SACCOS na mtandao wa Mawakala wa CRDB. Hatua hiyo itawawezesha wanachama kuweka na kutoa fedha kupitia zaidi ya Mawakala 40,000 wa CRDB waliopo maeneo mbalimbali nchini, hivyo kupanua kwa kiasi kikubwa maeneo ambayo mwanachama anaweza kupata huduma. 

Maboresho hayo yana umuhimu mkubwa hususan kwa wanachama waliopo nje ya maeneo yenye matawi ya benki, kwa kuwa yanapunguza utegemezi wa maeneo ya kawaida ya huduma za kifedha na kutumia mtandao mpana wa Benki ya CRDB kupeleka huduma karibu zaidi na mwanachama.

Kwa upande wake, Kamishnawa TRA, Yusuph Mwenda aliishukuru Benki ya CRDB kwa ushirikiano wake, akieleza kuwa PESACARD na muunganiko wa mifumo ni sehemu muhimu ya safari ya TRA SACCOS ya kuboresha na kufanya huduma zake kuwa za kisasa zaidi.

“Tunapoadhimisha miaka 20 ya TRA SACCOS, hatuangalii tu tulikotoka na mafanikio tuliyoyapata; tunaangalia pia tunakotaka kwenda na aina ya taasisi tunayotaka kuijenga kwa ajili ya wanachama wetu. TRA SACCOS PESACARD ni sehemu ya safari hiyo ya baadaye. Inawapa wanachama wetu urahisi, wigo mpana zaidi wa huduma na uwezo mkubwa wa kusimamia miamala yao. Tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kuamini maono yetu na kushirikiana nasi kuleta teknolojia inayoongeza uwezo wetu wa kuwahudumia wanachama vizuri zaidi.”

Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD pia unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya benki za biashara na taasisi za kifedha zinazomilikiwa na wanachama katika kuongeza ujumuishi wa kifedha. Kwa kuunganisha ukaribu wa TRA SACCOS na wanachama wake pamoja na teknolojia, miundombinu na uwezo wa malipo wa Benki ya CRDB, ushirikiano huo unalenga kuunda mazingira rahisi zaidi ya kupata huduma za kisasa za kifedha.

Kwa Benki ya CRDB, hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuendelea kuwekeza katika teknolojia na kubuni suluhisho zinazoboresha uzoefu wa wateja na kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha. Benki hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na TRA SACCOS pamoja na taasisi nyingine katika sekta binafsi na umma kuleta mageuzi ya kidigitali na katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

WADAU WA SEKTA YA AFYA ZAIDI YA 3000 KUSHIRIKi MKUTANO WA KIMATAIFA WA HUDUMA ZA AFYA YA MSINGI

September 06, 2026 Add Comment




Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe,  amesema zaidi ya wadau wa sekta ya afya 3000 kutoka nchi mbalimbali Duniani  watashiriki katika Mkutano wa pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi (IPHCC), jijini Arusha. 



Prof. Shemdoe  amesema hayo mapema leo Septemba 06, 2026 akiwa jijini Dodoma, kabla ya kuelekea Arusha na kuwakaribisha washiriki hao kwenye mkutano huo utakaofanyika kuanzia tarehe 9 hadi 11 Septemba, 2026  katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).


Prof. Shemdoe amesema, yeye binafsi atashiriki katika mkutano huo wenye tija katika kuboresha utoaji wa huduma za afya msingi nchini na afrika kwa ujumla.


Prof. Shemdoe amesema mkutano huo umelenga kutoa uzoefu wa Tanzania katika uboreshaji wa huduma za afya ya msingi, ikiwamo afua zilizopelekea kupunguza vifo vya akina mama na watoto ambapo Tanzania kupitia jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ni kinara katika eneo hilo barani Afika.


Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, mkutano huo umelenga pia kubadilishana uzoefu wa maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika katika huduma za afya ya msingi duniani pamoja na kuandaa mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za afya ya msingi ili kufikia malengo ya kitaifa na Kimataifa, ikiwamo upatikanaji wa Huduma za Afya kwa wote na malengo endelevu ya maendeleo.


Mkutano huo wa kihistoria utawakutanisha washiriki zaidi ya 3000 kutoka Tanzania na mataifa mengine duniani wakiwamo; wataalam wa afya wanaofanya kazi ya kutoa huduma za afya ya msingi, watunga sera, wadau wa maendeleo, watafiti, wahadhiri, wanafunzi, asasi za kiraia na sekta binafsi, ambapo washiriki hao wamejisajiri kupitia tovuti ya   https://iphcconference.tamisemi.go.tz .

KILWA YATAKA UWEKEZAJI ZAIDI KATIKA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

September 06, 2026 Add Comment




Kilwa, Lindi.


Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilwa, Yusuph Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa Serikali kuendelea kuwekeza katika nishati safi ya kupikia ili kuongeza upatikanaji wa nishati hiyo kwa wananchi na kuharakisha utekelezaji wa ajenda ya Taifa ya nishati safi ya kupikia.


Mwinyi alitoa kauli hiyo wakati wa ziara ya ujumbe wa Wizara ya Nishati uliotembelea mradi wa nishati safi ya kupikia unaotumia teknolojia ya haidrojeni ya kijani katika Wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi.


Amesema uwekezaji katika nishati safi ya kupikia ni muhimu kutokana na nafasi ya nishati hiyo katika maisha ya kila siku ya wananchi, akieleza kuwa Serikali inapaswa kuendelea kuweka mazingira yatakayowezesha teknolojia mbalimbali za nishati safi kupatikana na kutumika kwa upana zaidi.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Nolasco Mlay, amesema Serikali inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuendeleza teknolojia za nishati safi ya kupikia, ikiwemo teknolojia bunifu kama haidrojeni ya kijani, ili kuongeza wigo wa chaguo la nishati kwa wananchi.


Mlay amesema kuendelezwa kwa teknolojia hizo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuhakikisha wananchi wanapata nishati safi ya kupikia inayokidhi mahitaji yao, huku akisisitiza umuhimu wa ubunifu, uwekezaji na ushiriki wa sekta binafsi katika kufanikisha azma hiyo.


Amesema teknolojia ya haidrojeni ya kijani inaonesha fursa katika safari ya Taifa ya kuelekea kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia, hivyo ni muhimu kuendelea kufanya tathmini na kutoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi yake salama na yenye ufanisi.


Mlay amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, wataalamu na wananchi ni muhimu katika kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, sambamba na kufikia lengo la asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

UMEME WA UHAKIKA MIGODINI WACHANGIA ZAIDI YA SHILINGI BILIONilI 340 KWA MWAKA

September 06, 2026 Add Comment



Dodoma, Septemba 3, 2026.


Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashimu Komba, amesema upatikanaji wa umeme wa uhakika katika migodi una mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa, ambapo sekta hiyo huchangia zaidi ya Shilingi bilioni 340 kwa mwaka kupitia mrabaha, kodi na tozo mbalimbali.


Mhe. Komba ameyasema hayo Septemba 3, 2026, jijini Dodoma, katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya Mpomvu–GGM yenye msongo wa kilovoti 220 (220kV), pamoja na Kituo cha Kupoza Umeme katika eneo la GGM, mkoani Geita. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi.


Ameipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa juhudi za kuhakikisha umeme unafikishwa katika maeneo ya shughuli za madini, ikiwemo migodi mikubwa kama Geita Gold Mining (GGM), hatua inayosaidia kuongeza uzalishaji na kuchochea ukuaji wa sekta ya madini nchini.

“Tunawapongeza TANESCO kwa kuhakikisha umeme unafika katika maeneo ya migodi mikubwa kama GGM. Umeme wa uhakika ni muhimu katika kuhakikisha shughuli za uzalishaji zinaendelea bila vikwazo na hivyo kuongeza mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa Taifa,” amesema.


Aidha, Mhe. Komba amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi za kuendelea kusogeza huduma ya umeme kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.


Amesema Mkoa wa Geita umefikia hatua ya vijiji vyote 474 kuwa na umeme, huku mkandarasi Central Electrical Installation akiendelea na kazi ya kupeleka umeme katika vitongoji 528 vya mkoa huo.


Katika hatua nyingine, Mhe. Komba amewaalika Watanzania, wachimbaji wadogo, wa kati na wakubwa pamoja na wawekezaji kushiriki katika maonesho ya madini yanayotarajiwa kufanyika Septemba 23, 2026, mkoani Geita.


Amesema maonesho hayo yatatoa fursa kwa wananchi na wadau mbalimbali kujionea fursa zinazotokana na rasilimali za madini zilizopo mkoani Geita na nchini kwa ujumla.


Mhe. Komba pia ameahidi kuwa uongozi wa Mkoa na Wilaya ya Geita utatoa ushirikiano wa karibu kwa mkandarasi pamoja na watumishi wa TANESCO ili kuhakikisha utekelezaji wa mradi wa Mpomvu–GGM unafanyika kwa wakati na bila vikwazo visivyo vya lazima.


Amesema ushirikiano huo ni muhimu katika kuhakikisha mradi unakamilika kwa ufanisi na kuchangia upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa shughuli za uchimbaji na uzalishaji katika sekta ya madini.

BARRICK KIOO CHA UFUNGAJI MIGODI UNAOZINGATIA VIWANGO VYA KIMATAIFA NCHINI

September 06, 2026 Add Comment

    


Sehemu ya wajumbe wa Tawala za Mitaa Tanzania wakiwa kwenye maeneo ya Mgodi wa Barrick Buzwagi.
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) kutoka Njombe wakiwa kwenye ziara ya siku moja Mkoani Shinyanga kwenye mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo kwenye hatua za ufungaji.

TUME YA TAIFA YA UNESCO YASHIRIKI UKUSANYAJI WA MAONI KUHUSU MPANGO WA JUMLA WA USIMAMIZI WA HIFADHI HAI NA MWANADAMU YA RUMAKI

September 06, 2026 Add Comment

Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeshiriki katika zoezi la ukusanyaji wa maoni ya awali ya wadau kuhusu maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi (General Management Plan – GMP) wa Hifadhi Hai na Mwanadamu ya Rufiji–Mafia–Kibiti–Kilwa (RUMAKI), ikiwa ni hatua muhimu katika kuweka msingi wa usimamizi endelevu na shirikishi wa eneo hilo.

Zoezi hilo limejikita katika kupata maoni, uzoefu na mapendekezo ya wadau kuhusu namna bora ya kuimarisha uhifadhi wa mazingira na bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali za asili pamoja na maendeleo ya jamii zinazozunguka na kutegemea rasilimali za RUMAKI.

RUMAKI, inayojumuisha Rufiji, Mafia, Kibiti na Kilwa, ni miongoni mwa Hifadhi Hai zilizotambuliwa na UNESCO na kuingizwa katika Mtandao wa Dunia wa Hifadhi Hai (World Network of Biosphere Reserves – WNBR) mwaka 2023, chini ya Mpango wa UNESCO wa Mwanadamu na Hifadhi Hai (Man and the Biosphere Programme – MAB).

Hifadhi hiyo ina mifumo mbalimbali muhimu ya ikolojia ya pwani na bahari, ikiwemo misitu ya mikoko, miamba ya matumbawe na nyasi bahari. Mifumo hiyo ina mchango mkubwa katika kuhifadhi bioanuai, kulinda mazingira ya pwani, kusaidia shughuli za kiuchumi za jamii na kuongeza uwezo wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Maoni ya wadau yaweka msingi wa mpango

Ukusanyaji wa maoni ya awali ni sehemu muhimu ya mchakato wa kuandaa Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa RUMAKI. Kupitia mchakato huo, wadau wanapata nafasi ya kueleza hali halisi ya eneo, changamoto zinazokabili uhifadhi na matumizi ya rasilimali, pamoja na fursa zinazoweza kuendelezwa kwa manufaa ya jamii na mazingira.

Miongoni mwa wadau wanaohusishwa katika mchakato huo ni viongozi wa Serikali za Mitaa na vijiji, taasisi za Serikali, jamii zinazozunguka Hifadhi Hai, wavuvi, Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe (Beach Management Units – BMUs), taasisi za utafiti, wataalamu na wadau wengine wa maendeleo.

Ushirikishwaji wa wadau katika hatua hii unalenga kuhakikisha kuwa mpango utakaotengenezwa unazingatia mahitaji ya uhifadhi pamoja na hali halisi ya maisha ya jamii zinazotegemea rasilimali za eneo hilo.

Kuunganisha uhifadhi na maendeleo ya jamii

Dhana ya Hifadhi Hai na Mwanadamu inalenga kuweka uwiano kati ya uhifadhi wa bioanuai na maendeleo ya jamii. Kwa mtazamo huo, uhifadhi wa RUMAKI unahitaji kwenda sambamba na matumizi endelevu ya rasilimali zinazosaidia maisha ya wananchi, huku ukihakikisha kuwa rasilimali hizo zinalindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Katika maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi, suala la mgawanyo wa maeneo ya Hifadhi Hai linatarajiwa kuwa miongoni mwa maeneo muhimu ya kuzingatiwa. Hii inahusisha maeneo ya msingi ya uhifadhi (Core Areas), maeneo yanayozunguka maeneo hayo (Buffer Zones) na maeneo ya mpito (Transition Areas), kwa kuzingatia malengo ya uhifadhi na maendeleo endelevu.

Mpangilio huo unalenga kuweka uelekeo unaoeleweka kuhusu shughuli zinazoweza kufanyika katika maeneo mbalimbali, namna ya kulinda maeneo yenye umuhimu mkubwa wa kiikolojia na jinsi ya kuwezesha shughuli za maendeleo zinazozingatia mazingira.

Nafasi ya Tume ya Taifa ya UNESCO

Ushiriki wa Tume ya Taifa ya UNESCO katika zoezi hili unaendana na nafasi yake katika kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa programu na shughuli za UNESCO nchini Tanzania, kwa kushirikiana na taasisi za Serikali na wadau husika.

Kupitia Mpango wa UNESCO wa Mwanadamu na Hifadhi Hai (MAB), Hifadhi Hai hutumika kama maeneo ya kujifunza na kuonesha namna uhifadhi wa bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali, maendeleo ya jamii, utafiti, elimu na ufuatiliaji vinavyoweza kuunganishwa katika eneo moja.

Kwa upande wa Tanzania, utekelezaji wa dhana hiyo katika RUMAKI unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya taasisi za Serikali, mamlaka za Serikali za Mitaa, jamii, wataalamu, taasisi za utafiti na wadau wengine wanaohusika na uhifadhi na maendeleo.

Hatua kuelekea usimamizi endelevu wa RUMAKI

Maoni yatakayokusanywa katika hatua hii yatatoa msingi wa kuendelea na mchakato wa kuandaa Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa RUMAKI. Mpango huo unatarajiwa kusaidia kuweka mwelekeo wa pamoja katika uhifadhi wa bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali, maendeleo ya jamii, utafiti, elimu na ufuatiliaji wa mazingira.

Kwa kuwa RUMAKI inahusisha maeneo ya nchi kavu, pwani na bahari pamoja na jamii zinazotegemea rasilimali hizo, usimamizi wake unahitaji mtazamo unaounganisha mahitaji ya uhifadhi na maendeleo.

Ushiriki wa wadau katika hatua za awali, hivyo, ni muhimu katika kujenga uelewa wa pamoja na kuweka msingi wa mpango unaozingatia mazingira halisi ya RUMAKI.

Maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa Hifadhi Hai na Mwanadamu ya RUMAKI yanaashiria hatua muhimu katika kuimarisha utekelezaji wa dhana ya UNESCO ya Mwanadamu na Hifadhi Hai, kwa lengo la kuhakikisha kuwa uhifadhi wa mazingira na bioanuai unaenda sambamba na maendeleo endelevu na ustawi wa jamii.

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA NHIF KUELEKEA AFCON

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA NHIF KUELEKEA AFCON

September 05, 2026 Add Comment

Serikali imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kujipanga kikamilifu katika maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, hususan katika kuhakikisha wageni watakaofika nchini wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo.

Agizo hilo limetolewa l na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Florence Samizi (Mb.) ambaye amesema NHIF ina jukumu muhimu la kuratibu suala la bima ya afya wakati wa mashindano hayo ili kuhakikisha wageni wanapata huduma za matibabu kwa urahisi pindi wanapohitaji huduma hizo.

“Tuwape uhakika wa huduma bora ili waone fahari kuwapo hapa nchini katika kipindi chote cha mashindano hayo,” amesema Dkt. Samizi.

Amesema maandalizi ya huduma za matibabu yanapaswa kuzingatia pia huduma za dharura pamoja na huduma maalum, ikiwemo za moyo na mifupa, ili kukidhi mahitaji mbalimbali ya afya yatakayoweza kujitokeza wakati wa mashindano.

Aidha alidokeza kuwa tayari Wataalamu kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) wamekagua Vituo vya kutolea huduma kwa alengo la kujiridhisha na wamefurahishwa na utayari unaoonyeshwa katika maandalizi ya huduma za matibabu jambo linaloonesha kuwa Tanzania inajiandaa kuhakikisha AFCON 2027 inafanyika katika mazingira salama na yenye huduma bora.

Ameitaka NHIF kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya, vituo vya kutolea huduma na wadau wengine kuhakikisha mfumo wa huduma za matibabu wakati wa mashindano hayo unakuwa imara, unaopatikana kwa wakati na unaokidhi viwango vinavyohitajika.

Akizungumzia hilo Mkurugenzi Mkuu waa NHIF, Dkt. Irene Isaka alisema kuwa tayari Mfuko umeshajipanga na umeandaa kifurushi maalumu kwa ajili ya wageni wote watakaokuja nchini kwa ajili ya mashindano hayo.

“Tayari tumejipanga na tuna kifurushi ambacho tutakileta Wizarani ili tupate baraka ya Wizara hivyo tunashukuru sana kwa maelekezo haya ambayo yanaboresha na kuhakikisha tunajipanga vyema,” alisema Dkt. Isaka. ‎

NAIBU WAZIRI AVUTIWA NA USAJILI WANACHAMA KIDIGITALI, AITAKA NHIF KUONGEZA KASI YA BIMA YA AFYA KWA WOTE

NAIBU WAZIRI AVUTIWA NA USAJILI WANACHAMA KIDIGITALI, AITAKA NHIF KUONGEZA KASI YA BIMA YA AFYA KWA WOTE

September 05, 2026 Add Comment

‎NAIBU Waziri wa Afya, Mhe Dkt. Florence George Samizi (Mb), amelipongeza Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kuwa moja ya mabaraza bora nchini. Amelitaka baraza kuhakikisha ajenda ya Bima ya Afya kwa wote inawafikia wananchi wengi zaidi.

Nimefurahi kusikia kwamba katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026 Mfuko umeweza kufikia 10.7% ya Wananchi toka 8% ya wananchi iliyodumu kwa takriban miaka 10. Pamoja na pongezi hizo Mh. NAIBU WAZIRI ameutaka Mfuko kutumia TEHAMA na kusajili wanachama wengi zaidi ili kutimiza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikishia wananchi wote huduma za bima ya afya. Hii itasaidia wananchi kuondokana na umaskini pale wanapopata maradhi. ‎Dkt. Samizi ametoa maelekezo Hayo wakati wa mkutano wa nne wa wa Baraza la 4 wafanyakazi NHIF, Jijini Arusha, na kusisistiza menejimenti ya wafanyakazi wa NHIF kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia uadilifu, weledi na uwajibikaji, huku wakisikiliza na kutatua kwa wakati kero za wananchi. ‎Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya. Kutoa huduma bora na kuwa na mfumo wa kupokea mrejesho toka kwa wananchi. ‎Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa NHIF, Dkt. Samizi amesema ni muhimu mfuko huo kuonesha mafanikio yaliyopatikana. Kuwepo kwa NHIF kumesaidia kuboresha huduma za Afya kwa kulipa madai na kutoa mikopo kwa vituo vya afya. Ni vema wanachi wakajulishwa hatua kubwa iliyofikiwa katika huduma za Afya na mchango wa NHIFkatika Sekta hii muhimu. Mlianza na vituo vichache sana mwaka 2001 hivi sasa yaani mwaka wa Fedha 2025/26 mmesajili zaidi ya vituo 10,600 nchi nzima. Ni vema kuonesha namna mlivyokabiliana na changamoto za wakati ule na namna zilivyowasaidia kuboresha Mfuko katika utoaji wa huduma. ‎Amesema mafanikio hayo yanadhihirishwa na kujituma, ushirikiano, umoja na mshikamano miongoni mwa watumishi wa NHIF ili kufikia malengo ya mfuko kwa lengo la kutekeleza jitihada za Serikali za kuhakikisha wananchi wanapata bima ya Afya. ‎Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, ameeleza mafanikio yaliyopatikana ikiwa ni pamoja na kupunguza muda wa kilipa madai toka zaidi ya siku 90 hadi wastan wa siku 50 kwa mwaka wa Fedha 2025/2026. Vile vile alieleza kwamba Mfuko umeendelea kuimarika ambapo ziada imeongezeka kwa 57% Mfuko umepunguza matumizi kwa asilimia13% na uwekezaji umeongezeka kwa 106%.

Hii imewezesha Mfuko kuendeleza kifurushi cha wanafunzi, Toto Afya. Mfuko kusajili kifurushi cha tarangire, Mikumi, Ngorongoro, Serengeti Tanzanite na kifurushi cha vikundi yaani Umoja Afya ambacho ni sh. 60, 000 kwa matibabu ya mwaka mzima.

Vile vile alielezea mikakati inayotekelezwa na mfuko huo katika kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na matumizi ya TEHAMA kwenye usajili, uchakataji madai na kupambana na udanganyifu. Mfuko pia unashirikisha Sekta Binafsi katika usajili wa wanachama na katika huduma za matibabu. ‎Mwakilishi wa chama Cha wafanyakazi TUGHE, Bw.Paul wamepongeza baraza Hilo kuzingati misingi ya Kazi stahiki za wafanyakazi kwenye taasisi hiyo. ‎Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki semina elekezi ya siku mbili wamesema wamepata maarifa na mwelekeo mpya ambao utawasaidia kuboresha utendaji wao wa kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Bima ya Afya kwa wote! Jiunge sasa!

MKENDA: UWEKEZAJI ELIMU YA JUU UENDE SAMBAMBA NA UBORA

MKENDA: UWEKEZAJI ELIMU YA JUU UENDE SAMBAMBA NA UBORA

September 05, 2026 Add Comment
 

Na Alex Sonna, Mzalendo Blog – Dodoma

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ameitaka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kuhakikisha inaweka mfumo bora na wenye ufanisi wa udahili na usajili wa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya juu, ili kuepusha vyuo kupokea wanafunzi wanaozidi uwezo wa miundombinu na wakufunzi waliopo na hivyo kulinda ubora wa elimu.

Profesa Mkenda ametoa kauli hiyo leo, Septemba 5, 2026, jijini Dodoma, baada ya kukutana na Makamu Wakuu wa Vyuo Vikuu pamoja na Wenyeviti wa Mabaraza ya vyuo vikuu nchini, katika kikao kilichojadili masuala mbalimbali yanayohusu elimu ya juu, hususan mchakato wa udahili na usajili wa wanafunzi. Amesema lengo ni kuweka utaratibu utakaowawezesha wanafunzi kupata nafasi za masomo kwa haki na kwa ufanisi, huku ukizingatia uwezo halisi wa kila chuo.

“Tumefanya hivyo kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunatengeneza mfumo mzuri ambao hautaleta utata, hautakuwa na kuweka idadi ya wanafunzi kuliko uwezo wa kufundisha,” amesema Prof. Mkenda,

Waziri Mkenda amewahimiza wanafunzi wanaoomba kujiunga na vyuo vikuu kuendelea kufanya maombi yao huku wakisubiri maelekezo zaidi kutoka TCU kuhusu utaratibu wa udahili. Amesema mfumo unaoandaliwa unalenga kulinda maslahi ya wanafunzi na vyuo, sambamba na kuhakikisha mchakato wa udahili unakuwa wa wazi, rahisi na wenye ufanisi.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kuongeza uwezo wa vyuo vikuu nchini kupitia ujenzi na upanuzi wa kampasi katika mikoa mbalimbali, hatua inayolenga kuongeza nafasi za wanafunzi kupata elimu ya juu. Amesema uwekezaji huo utawezesha kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata fursa za elimu ya juu bila kushusha viwango vya elimu vinavyotolewa.

Profesa Mkenda amesema Tanzania bado haijafikia kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi katika elimu ya juu kinacholengwa, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana na vyuo vikuu kuongeza nafasi za masomo huku ikihakikisha ubora unaendelea kuwa kipaumbele. Amesema Serikali inalenga kuwa na mfumo wa elimu ya juu unaoweza kutoa fursa zaidi kwa vijana sambamba na kuwaandaa kwa mahitaji ya soko la ajira.

Ameongeza kuwa Wizara imepanga kufanya kikao kama hicho na viongozi wa vyuo vya kati vilivyo chini ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), kwa ajili ya kujadili masuala ya ubora wa elimu, udahili na mifumo ya uongozi katika sekta hiyo. Amesema ushirikiano kati ya Serikali, vyuo na wadau wengine ni muhimu katika kuhakikisha uwekezaji unaofanywa katika elimu unazaa matokeo yanayotarajiwa.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, amesema kikao hicho kimejadili masuala mbalimbali yanayohusu udahili wa wanafunzi katika vyuo vya elimu ya juu, ubora wa elimu pamoja na hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuendeleza sekta hiyo.

Amesema wadau hao wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kuboresha mifumo ya udahili, huku wakizingatia mahitaji na mabadiliko yanayoendelea katika sekta ya elimu.

Prof. Kihampa amesema ongezeko linalotarajiwa la wanafunzi kutokana na mabadiliko mbalimbali ya sera linahitaji Serikali, TCU na vyuo vikuu kujiandaa mapema ili kuongeza uwezo wa kutoa elimu bora kwa idadi kubwa ya wanafunzi.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Teolojia cha Lweru, Aggrey Mlimuka, amesisitiza umuhimu wa vyuo vikuu nchini kusimamia ubora wa elimu ili kuhakikisha wahitimu wanakuwa na uwezo na weledi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira.

Amesema vyuo vina wajibu wa kuhakikisha kila taaluma inazalisha wataalamu wenye uwezo, huku akibainisha kuwa endapo vyuo vitashindwa kusimamia ubora, soko la ajira lenyewe litachuja wahitimu kulingana na uwezo wao.

Awali Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Prof. Alfred Sife, amesema vyuo vikuu nchini vimekubaliana kuendelea kuboresha mchakato wa udahili wa wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2026/2027 ili kuhakikisha wanafunzi wanaopokelewa wanakidhi vigezo na kujiunga na programu zinazolingana na taratibu, kanuni na sheria zilizowekwa.

Amesema mjadala mkubwa katika kikao hicho ulihusu mwenendo wa udahili unaoendelea kwa sasa, ambapo dirisha la kwanza la maombi limekamilika na kinatarajiwa kufunguliwa dirisha la pili wiki ijayo.

Kwa mujibu wa Profesa Sife, lengo ni kuhakikisha mfumo wa udahili unaendelea kuimarishwa ili kupata wanafunzi wenye sifa na kuwawezesha kujiunga na programu na vyuo vinavyokidhi mahitaji yao, huku taratibu, kanuni na sheria za udahili zikizingatiwa.

Aidha, Profesa Sife amesema ushirikiano huo ni muhimu katika kuhakikisha vyuo vikuu vinaendelea kuboresha ubora wa elimu katika programu mbalimbali na kutoa wahitimu wenye uwezo unaokidhi mahitaji ya taifa na soko la ajira.

NAIBU WAZIRI DKT. PIUS CHAYA ATEMBELEA KIWANDA CHA DAWA NCHINI CHINA

September 05, 2026 Add Comment


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya  ameanza ziara ya kikazi nchini China yenye lengo la kuvutia wawekezaji wa China kuwekeza nchini Tanzania. Dkt Chaya ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe.Balozi.Dkt. Batilda Buriani.


Katika kuanza kwa ziara hiyo leo, tarehe 5 Septemba 2026, Dkt. Chaya ametembelea kiwanda cha kutengeneza dawa cha Yiling Pharmaceutical Co., Ltd., ambapo amepata fursa ya kujifunza kuhusu shughuli za uzalishaji wa dawa na teknolojia zinazotumika katika kiwanda hicho.


Akizungumza na uongozi wa kampuni hiyo, Dkt. Chaya amewaalika wawekezaji hao kuangalia fursa za kuwekeza nchini Tanzania, akieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira na sera rafiki kwa wawekezaji, hususan katika sekta ya uzalishaji wa dawa na vifaa tiba.


Dkt. Chaya ameeleza kuwa Serikali, kupitia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, inalenga kuimarisha uzalishaji wa dawa na vifaa tiba nchini.

TANESCO YABORESHA MAISHA YA WAFANYAKAZI NYUMBA YA MUNGU

September 05, 2026 Add Comment



*📌 Nyumba za wafanyakazi zakarabatiwa, kuboresha utendaji wa kazi*


*📌 Mtambo wa kisasa wa kuchakata maji wazinduliwa*


📍 MWANGA, KILIMANJARO | Septemba 2, 2026

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limezindua na kukabidhi nyumba zilizokarabatiwa kwa wafanyakazi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme kwa Maji cha Nyumba ya Mungu, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro.


Nyumba hizo, zilizojengwa tangu mwaka 1969, wakati Kituo cha Nyumba ya Mungu kilipoanza kufanya kazi, zimefanyiwa ukarabati mkubwa hatua inayolenga kuboresha mazingira ya makazi na ustawi wa wafanyakazi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi na makabidhiano hayo, Afisa Rasilimali Watu wa Kituo cha Nyumba ya Mungu, Bi. Neema Mwaisaka, amewataka wafanyakazi waliokabidhiwa nyumba hizo kuzitunza ili ziendelee kuwa na thamani na kutumika kwa muda mrefu.


“Natoa rai kwa wafanyakazi ambao tumewakabidhi nyumba hizi wazitunze, kwani Shirika limetumia fedha nyingi katika kuzikarabati,” amesema Bi. Neema.

Kwa upande wao, wafanyakazi waliokabidhiwa nyumba hizo, kupitia mwakilishi wao Masasi Maduka, wameipongeza Menejimenti ya TANESCO kwa kuboresha mazingira yao ya kuishi, wakieleza kuwa mazingira bora ya makazi yataongeza morali, ufanisi na kujituma katika kutekeleza majukumu yao.


“Kuboresha mazingira yetu ya kuishi kutatuongezea morali ya kufanya kazi na kutuwezesha kujituma zaidi katika kutekeleza majukumu yetu,” amesema Masasi.

Katika hatua nyingine, Kituo cha Nyumba ya Mungu kimezindua mtambo wa kisasa wa kuchakata maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu pamoja na matumizi katika mitambo ya kituo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mtambo huo, Mkuu wa Kitengo wa Kituo cha Nyumba ya Mungu, Mha. Andrea Shio, amesema TANESCO imefanya ukarabati na uboreshaji wa mtambo huo ili kuufanya kuwa wa kisasa na kuongeza ufanisi wake.


“Naipongeza Menejimenti ya Shirika kwa ukarabati wa mtambo huu. Maji haya yanatumika kwa matumizi ya binadamu pamoja na kwenye mitambo,” amesema Mha. Shio.


Ukarabati wa nyumba za wafanyakazi pamoja na kuboresha miundombinu muhimu kama mtambo wa kuchakata maji ni sehemu ya jitihada za TANESCO za kuimarisha mazingira ya kazi na makazi, kuongeza ufanisi na kuhakikisha huduma za uzalishaji umeme zinaendelea kutolewa kwa uhakika.

Masauni atoa wito kusimamia agizo la usafi wa mazingira

September 05, 2026 Add Comment
Na; Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Serikali inatoa wito kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji kuhakikisha kuwa wanaweka utaratibu wa kusimamia utekelezaji wa maelekezo ya kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kuwa siku ya usafi wa Mazingira Kitaifa kwa kuzingatia maslahi ya makundi mbalimbali.

WIZARA YA NISHATI YAPONGEZWA KUTEKELEZA MAAGIZO YA KAMATI

September 05, 2026 Add Comment

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara ya Nishati na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kutekeleza maagizo ya Kamati hiyo ya kuwataka Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini kushirikiana katika kutatua changamoto za upatikanaji wa nishati katika sekta ya madini.


Mhe. Mgalu ameyasema hayo Septemba 3, 2026, jijini Dodoma, wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya Mponvu–GGM ya msongo wa kilovolti 220 (kV) pamoja na Kituo cha Kupoza Umeme kitakachojengwa katika eneo la GGM, Geita.

Amesema anafurahishwa na hatua zilizochukuliwa na Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini katika kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Kamati hiyo, hususan kuwezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa migodi ya wachimbaji wadogo, wa kati na wakubwa.


“Tunafarijika kuona maelekezo tuliyoyatoa katika kikao cha Kamati yakitekelezwa. Ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini umewezesha kufikiwa kwa hatua hii kubwa ya kupeleka umeme wa uhakika katika maeneo ya migodi kupitia mradi wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 63,” amesema Mhe. Mgalu.


Aidha, amekumbusha ziara ya Kamati hiyo iliyofanyika Machi 15, 2026, katika Kituo cha Mponvu, Geita, ambapo pamoja na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, walijionea uwekezaji wa zaidi ya shilingi bilioni 50 uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika miundombinu ya umeme.


Amesema ujenzi wa njia mpya ya kusafirisha umeme ya msongo wa kV 220 utakaoiwezesha migodi ya GGM kupata umeme wa uhakika ni hatua muhimu katika kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinafanyika kwa ufanisi na tija zaidi.


“Upatikanaji wa umeme wa uhakika utasaidia migodi kufanya kazi kwa ufanisi, kuongeza uzalishaji na hatimaye kuchangia katika kukuza pato la Taifa kupitia sekta ya madini,” amesema.


Mhe. Mgalu pia ameipongeza TANESCO pamoja na Bodi ya Wakurugenzi kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuboresha huduma ya umeme nchini, akihusisha jitihada hizo na kauli mbiu ya Shirika isemayo “Tunaangaza Maisha Yako.”


Amesema jitihada za kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika ni sehemu muhimu ya kujenga uchumi wa kisasa na kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa kuelekea Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

WAKULIMA BABATI WANUFAIKA NA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP)

September 05, 2026 Add Comment
Na; Mwandishi wetu – Babati

Wakulima wa vijiji vya Endakiso na Orng'adida vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara wameeleza kunufaika na Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kushirikina na Serikali na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, na wenye Ulemavu.

WAKULIMA BABATI WANUFAIKA NA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP)

September 05, 2026 Add Comment




Na; Mwandishi wetu – Babati


Wakulima wa vijiji vya Endakiso na Orng'adida vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara wameeleza kunufaika na Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) kwa kushirikina na Serikali na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, na wenye Ulemavu.



Kwa nyakati Tofauti wakulima kutoka vijiji hivyo wameyasema hayo tarehe 4 Septemba wakati wa ziara ya timu kutoka IFAD inayotathimini maendeleo ya utekelezaji  Programu ya  muda wa kati  (MTR).

Wakulima hao waliweka bayana kuwa, Programu hiyo imeweza kuwaletea teknolojia ya kisasa ya Kilimo Mseto kwa kutumia Mbegu himilivu zinazoweza kuhimili athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.



Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Bw. Ramadhani Iddi Mfumbilo mkulima kutoka katika kijiji cha Mkombozi Kata ya Endasiko alisema, kupitia Programu hii wakulima wameweza kupata mbegu za mahindi aina ya situka na mbegu za lishe ambazo zimepandwa mashambani pamoja na mazao mengine kama vile labulabu ambayo yanaweza kurutubisha ardhi na kuzuia Mmomonyoko wa udongo.

“Majani hayo pia siyo rafiki kwa mifugo kama vile ng’ombe hivyo mifugo itakapovamia shamba la Mkulima si rahisi kuweza kula au kuharibu mazao, na yanakimbiza wadudu waharibifu wa mazao.” Aliendekea kufafanua.

Alibainisha kuwa, Mbegu hizi za Lishe zina uwezo mkubwa wa Kurutubisha Afya ya Familia hasa kwa watoto, kinamama wajazito, wazazi na wazee na pia zimesaidia kupunguza magonjwa ya Utapiamlo kwa watoto.

Aidha, Akiongelea mbegu za Jamii ya Mikunde yaani Maharage aina ya Jesca, alisema, Mbegu hizo zina virutubisho muhimu na vya kipekee hasa kwa watoto.



Kwa upande wake Bi Naseriani Joseph kutoka katika Kijiji cha Orng'adida Kata ya Qash mkulima wa mazao ya Lishe yanayolimwa katika bustani nyumbani maarufu kama '_Kitchen gardens_', alisema kuwa, kupitia Programu ya AFDP wakulima hao waliweza kupata Elimu na Mbegu bora za mazao ya lishe ambayo wanalima Nyumbani na wamepata manufaa mengi kama vile kuwepo kwa mboga nyumbani pamoja na kuwasaidia watoto shule na familia kwa ujumla pamoja na kuimarisha Afya ya familia na kuongeza kipato

“Wanawake tunapata mahitaji yetu muhimu kupitia kilimo hiki kwa upande wa mboga mboga na mazao ya mikunde, tumepata elimu ya maharage lishe tumepata mbegu na tumeyatumia, Maharage yale yameboreshwa yana viini lishe na madini chuma, hivyo afya za familia zinaimarika, natoa tuu wito kwa serikali kuongeza mbegu hizi maana ni adimu na zinazalishwa kwa uchache katika kata yetu. Alisema”


Wataalam hao wanaendelea na ziara hiyo kwa kutembela maeneo tofauti yanayotekeleza programu nchini katika sekta za Kilimo na Uvuvi.