HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
WAZIRI KAKURWA ATOA MWELEKEO WA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYABIASHARA WA MIFUGO
habariTRAMEPRO YAENZI URITHI WA NELSON MANDELA, YATAKA JAMII KUJENGA AMANI
habari
St Anne Marie Academy yasomesha waliofiwa na wazazi tangu mwaka 2029
habariBODI YA NISHATI VIJIJINI YARIDHISHWA NA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA GEREZA LA MANYONI
habariSHIRIKA LA FROM HEARTS 2 HANDS LAJENGA MAKTABA YA KISASA KUNUFAISHA WANAFUNZI 737 WA JAMII YA KIMASAI , MONDULI
habariREA YAONDOA GIZA KITONGOJI CHA SIMANJIRO, FURAHA YATAWALA
habariMAKONDA: Uwekezaji wa afya waifanya Dira ya Taifa 2050 kuwa halisi
habariWAZAZI WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO MALEZI NA ULINZI WA MTOTO
habariWito huo umetolewa na Mkaguzi Msaidizi Emmanuel Kisiri, ambaye ni Polisi wa Kata ya Ikoma, Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara,alipokuwa akitoa elimu ya Polisi Jamii katika nyumba ya Abwire Thomas hivi karibuni.
Mkaguzi Msaidizi Kisiri amesema wazazi wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuwalea, kuwafuatilia na kuwalinda watoto wao dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia pamoja na changamoto nyingine zinazoweza kuhatarisha ustawi wao.
Ameongeza kuwa ushirikiano kati ya wazazi, jamii na vyombo vya ulinzi na usalama ni muhimu katika kujenga mazingira bora ya malezi na kuhakikisha haki za watoto zinazingatiwa.
OPERESHENI YA POLISI TANGA YANASA WATUHUMIWA 200 WENGINE 51 WAHUKUMIWA
habari
Na Oscar Assenga, Tanga
Operesheni zilizoendeshwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga kwa kipindi cha Juni 1 hadi Julai 16, 2026 zimewezesha kukamatwa kwa watuhumiwa 200 wanaodaiwa kuhusika na makosa mbalimbali ya jinai, huku watuhumiwa 51 wakitiwa hatiani na mahakama na kuhukumiwa vifungo tofauti, wakiwamo wawili waliofungwa miaka 30 gerezani.
Makosa yanayowakabili watuhumiwa hao ni pamoja na unyang'anyi wa kutumia nguvu, wizi, biashara ya dawa za kulevya, kupatikana na mali zinazodhaniwa kuwa za wizi, umiliki wa nyara za Serikali, uharibifu wa miundombinu ya umma, matumizi ya noti bandia na makosa mengine ya jinai.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Muchunguzi, alisema mafanikio hayo yametokana na operesheni maalumu na doria zilizofanyika katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Alisema kati ya watuhumiwa waliokamatwa, kesi za watu 51 zilikamilika na kufikishwa mahakamani, ambako walipatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu mbalimbali kwa makosa ya kulawiti, kubaka, kuzini na maharimu, kusafirisha dawa za kulevya, wizi wa mifugo, kuvunja na kuiba, kujeruhi, kutishia kuua, kuingia nchini bila kibali pamoja na makosa mengine.
Watatu wafungwa miaka 30
Muchunguzi alisema waliohukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani ni Julius Mustafa, aliyepatikana na hatia ya kulawiti, Kilimo Issaya aliyetiwa hatiani kwa kosa la kuzini na maharimu na Sadiki Waziri aliyepatikana na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya.
Aliongeza kuwa watuhumiwa wengine walihukumiwa vifungo vya miaka mitano gerezani kwa makosa ya wizi wa mifugo pamoja na makosa mengine ya jinai.
Dawa za kulevya zanasa 29
Akizungumzia operesheni za kupambana na dawa za kulevya, Muchunguzi alisema watuhumiwa 29 walikamatwa wakiwa na dawa hizo za aina mbalimbali.
Alisema watuhumiwa 14 walikutwa na mabunda 750 ya mirungi yenye uzito wa kilogramu 45, huku watuhumiwa wengine 15 wakinaswa na bangi ikiwa katika mfumo wa misokoto 114, pakiti 126, vifurushi vitano na kete 120.
Katika operesheni hizo, polisi pia walikamata pikipiki 20 zisizo na namba za usajili ambazo zinaendelea kuchunguzwa kubaini uhalali wa umiliki wake na kama zilitumika kutekeleza vitendo vya uhalifu.
Nyara za Serikali, mali za wizi zakamatwa

Operesheni hizo pia zilisababisha kukamatwa kwa watuhumiwa watano waliokuwa na nyara za Serikali na mali zinazohusiana na wanyamapori.
Mbali na hilo, polisi walinasa vifaa mbalimbali vinavyodhaniwa kuwa vya wizi, vikiwamo vifaa vya miundombinu ya TANESCO, vifaa vya miundombinu ya barabara, noti bandia za fedha za Kenya, televisheni 10, simu za mkononi 25 pamoja na mali nyingine zinazochunguzwa kubaini uhalali wa umiliki wake.

Muchunguzi alisema operesheni dhidi ya uhalifu zitaendelea kuimarishwa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tanga, huku akiwataka wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zitakazowezesha kuwabaini wahalifu na kuzuia vitendo vya uhalifu.
Alisema ushirikiano wa wananchi umeendelea kuwa nguzo muhimu katika mafanikio ya operesheni hizo na kwamba jeshi hilo litaendelea kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote watakaobainika kujihusisha na uhalifu.
UFADHILI WA REA WAONGEZA TIJA KWA WAZALISHAJI WA CHUMVI IRAMBA
habariSERIKALI YASISITIZA UKUZAJI TIJA KATIKA SEKTA YA UMMA
habariKAMPUNI ZA WAZAWA ZATAKIWA KUTEKELEZA MIRADI KWA UFANISI ILI KUSHINDANA KIMATAIFA
habariKATIBU MKUU CCM AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA
habariMfumo wa kidijitali wa JKCI kuboresha usajili na matibabu ya wagonjwa
habariKafulila Kutoa Mhadhara wa Umma SUA Kuhusu Ubia na Mageuzi ya Kilimo
habariNEEC YAHITIMISHA MAFUNZO YA FURSA ZA MITAJI NA PROGRAMU ZA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI MKOANI RUKWA
habariMCT YAFANYA MKUTANO WA MASHAURIANO NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI, YAIMARISHA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI
habariUMEME KUBADILISHA MAISHA YA WANANCHI VITONGOJINI
habariMHE.KILAKALA AIPONGEZA WIZARA YA NISHATI KWA KUENDELEA KUTOA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kuandaa Warsha ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wanahabari na Maafisa habari, akisema mafunzo hayo ni hatua muhimu ya kuhakikisha elimu sahihi inawafikia wananchi na kuimarisha utekelezaji wa ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.
Akizungumza Julai 14, 2026 wakati wa ufunguzi wa Warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari, Maafisa Mawasiliano Serikalini wa Mikoa, Taasisi, Wizara pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya nishati safi ya kupikia inayofanyika katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro amesema Mkoa wa Morogoro una vyanzo vingi vya maji vinavyopaswa kulindwa, hivyo ajenda ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia itasaidia kuhifadhi mazingira kwa kupunguza ukataji wa miti, kulinda afya za wananchi pamoja na kutunza vyanzo hivyo vya maji kwa manufaa ya kizazinkijacho.
Amesema elimu inayotolewa kupitia warsha hii ikiwafikia wananchi kwa usahihi, itasaidia kuongeza uelewa kuhusu maana na faida za nishati safi ya kupikia, hususan kwa jamii za vijijini, jambo litakalowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika juhudi za kulinda mazingira na kutumia nishati salama na nafuu.
Mhe. Kilakala amewataka washiriki kutoka Mikoa mbalimbali nchini kutumia maarifa waliyoyapata katika warsha hiyo kwa weledi mkubwa wanaporejea kwenye maeneo yao ya kazi kwani mafunzo haya yataongeza hamasa na kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na elimu ya nishati safi ya kupikia na hivyo kuchangia kufikiwa kwa malengo ya taifa ya kuhakikisha asilimia 80 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.
*ELIMU YA UMEME NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA WANANCHI ARUMERU MASHARIKI*
SHERIA BORA NI MSINGI WA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050 – MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
habariOSHA YATAJWA MIONGONI MWA TAASISI ZA KIMKAKATI NCHINI
habariWANAHABARI NI WASHIRIKA MUHIMU WA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
NishatiNaibu Waziri wa Nishati amesema vyombo vya habari na maafisa mawasiliano Serikalini ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kutokana na nafasi yao ya kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni pamoja na majukwaa ya kidijitali.
Hayo ameyabainisha leo Julai 14, 2026 wakati akifungua Warsha ya Kuwajengea Uwezo Waandishi wa Habari na Maafisa Mawasiliano Serikalini kutoka katika Wizara na Taasisi kuhusu Uandishi na Uhamasishaji wa Masuala ya Nishati Safi ya Kupikia, inayofanyika katika ukumbi wa Morena hoteli mkoani Morogoro.
Amesema vyombo vya habari si wasambazaji wa taarifa pekee bali ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kwa kutoa taarifa sahihi huku akibainisha kuwa kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni, makala pamoja na maudhui ya kidijitali, wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga uelewa wa wananchi, kuondoa dhana potofu na kuhamasisha mabadiliko chanya ya tabia kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia kwani katika zama za mawasiliano ya kidijitali, taarifa moja sahihi inaweza kuwafikia mamilioni ya wananchi ndani ya muda mfupi na kuleta mabadiliko makubwa katika jamii.
Amefafanua kuwa, taarifa zisizo sahihi zinaweza kusababisha upotoshaji na kuchelewesha utekelezaji wa ajenda muhimu za maendeleo akimnukuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) uliofanyika jijini Arusha, amesema watu wanaweza kushiriki kubomoa Tanzania, lakini hawawezi kusaidia kuijenga hivyo amesisitiza kuwa wanahabari wana wajibu wa kutumia kalamu na keybord zao kuandika habari zenye ukweli, zenye kujenga matumaini na kuunga mkono juhudi za maendeleo ya Taifa badala ya taarifa zinazoweza kupotosha wananchi.
Aidha Mhe. Salome ameeleza kuwa, matarajio ya Serikali ni kuwa mafunzo hayo yatawaongezea washiriki maarifa na ujuzi wa kuandaa habari zenye usahihi, ushahidi na weledi wa hali ya juu, pamoja na kuandaa maudhui yanayoonesha mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia, ubunifu wa sekta binafsi na fursa zilizopo katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo.
Ameongeza kuwa warsha hiyo itawajengea uwezo washiriki kuhusu sera, mikakati na mwelekeo wa Serikali katika sekta ya nishati safi ya kupikia, matumizi sahihi ya takwimu pamoja na namna bora ya kuripoti kuhusu teknolojia mbalimbali zinazopatikana nchini ili kuandaa taarifa zenye ubora na zinazojenga uelewa wa wananchi.
Aidha, amewataka washiriki kutumia kikamilifu fursa ya mafunzo hayo kujenga ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati, Idara ya Habari MAELEZO, washirika wa maendeleo, sekta binafsi na vyombo vya habari, akisisitiza kuwa mawasiliano sahihi ni nguzo muhimu ya kufanikisha ajenda ya nishati safi ya kupikia na kufikia lengo la asilimia 80 ya matumizi ifikapo mwaka 2034.
USHIRIKIANO WA ORYX GAS NA SKAUTI KUCHOCHEA MATUMIZI SALAMA YA NISHATI SAFI
habariNAIBU WAZIRI SALOME AWASILI MOROGORO KUFUNGUA WARSHA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
NishatiNaibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, akiwasili katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro kwa ajili ya kufungua warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari pamoja na Maafisa Mawasiliano wa Serikali kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya Nishati Safi ya Kupikia.
Warsha hiyo imeandaliwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF), kupitia Mradi wa CookFund unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya.
Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Salome ameambatana na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Nishati, Bi. Nteghenjwa Hosseah na Meneja wa Mradi wa CookFund – UNCDF, Bw. Imanuel Muro.
LINDI KUENEZA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA WOTE
habari Nishati
📌 Majiko banifu 5,776 kusambazwa mkoani Lindi
Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, amesema Mkoa wa Lindi umeanza kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya juhudi za kufikia lengo la kitaifa la kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.
Bi. Omary amesema hayo leo, Julai 15, 2026, alipokutana na Afisa Mshauri Mwandamizi wa Masuala ya Kiufundi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Deusdedit Malulu, aliyeambatana na uongozi wa Kampuni ya Tango Energy Limited, inayotekeleza usambazaji wa majiko banifu mkoani Lindi.
“Nawapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Tunamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na tutaendelea kutoa elimu ili iwafikie wananchi wote,” amesema Bi. Omary.
Kwa upande wake, Mha. Malulu amesema jumla ya majiko banifu 5,776 yameanza kusambazwa na Kampuni ya Tango Energy Limited katika maeneo ya Lindi, Ruangwa, Nachingwea, Liwale na Kilwa.
Mha. Malulu amewataka wananchi katika maeneo hayo kuchangamkia fursa ya kupata majiko banifu kwa bei nafuu ya ruzuku ya shilingi 7,600 tu kwa jiko.
Naye, Meneja wa Mauzo wa Tango Energy Limited, Bw. Emmanuel Ibrahim, amesema mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kiasi kidogo cha kuni na mkaa, hatua inayolenga kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati pamoja na athari za moshi unaotokana na matumizi ya majiko ya kawaida.
Kupitia mradi huo, Tango Energy Limited itasambaza jumla ya majiko banifu 5,776 kwa wananchi kwa bei ya ruzuku. Bei halisi ya jiko moja ni TZS 50,847.46, lakini Serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85, hivyo mwananchi atanunua jiko kwa TZS 7,600 tu.

















































