HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TAIFA GAS YAENDESHA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA UJAZAJI NA USAMBAZAJI WA GESI HARAMU MKOA WA DAR ES SALAAM

September 20, 2026 Add Comment

 

Washiriki wa mafunzo wakionesha vyeti vyao baada ya kukamilisha mafunzo ya matumizi sahihi ya gesi na udhibiti wa ujazaji haramu wa gesi. 

Meneja Mauzo wa Taifa Gas Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Joseph Richard (kulia) akikabidhi cheti kwa mmoja wa washiriki wa mafunzo.

BARRICK BULYANHULU YAKABIDHI JENERETA KUBWA LA KISASA KITUO CHA AFYA BUGARAMA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI

September 20, 2026 Add Comment

Afisa Mahusiano ya Jamii kutoka Barrick Bulyanhulu, Stella Kuyonga (katikati) akingalia zoezi la ufungaji jenereta katika kituo cha afya cha Bugarama ambalo limekabidhiwa na mgodi kusaidia kukabiliana na changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na kuathiri utoaji huduma kwa wananchi.

CCM YATOA ONYO KWA WATAKAOTAFUNA FEDHA ZA SOKO PANGANI.

September 20, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga, PANGANI

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga,Rajabu Abdallah, ametoa Sh milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa Soko Kuu la Mikinguni, Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga huku akiwaonya watakaokula pesa hizo.

Kauli hiyo imetolewa na Mweyekiti huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM  wakati wa kukabidhi  mfano wa hundi ya thamani hiyo na kusema kuwa hatomvumilia mtendaji yoyote atakaebainika kutumia vibaya fedha hizo tofauti  na zilivyotarajiwa.

Aidha alisema kumekuwa na mazoea ya baadhi ya watumishi kutumia vibaya pesa za miradi ya kimaendeleo jambo ambalo linakwamisha maendeleo na kudumaza huduma za kijamii kwa wananchi na kuongeza migogoro baina ya chama  na Serikali kwa ujumla.

 Fedha hizo ni sehemu ya Sh milioni 300 zinazokadiriwa kugharimu ujenzi wa soko hilo, ambalo linatarajiwa kuanza kujengwa katika mwaka wa fedha 2026/2027.

Soko hilo linatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi itakayochochea shughuli za kiuchumi kwa wananchi na wafanyabiashara wa Kata ya Mikinguni, huku likitarajiwa kutumia fursa zitakazotokana na ujenzi wa Barabara ya Tanga–Bagamoyo.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Mikinguni, Kijiji cha Stahabu, mara baada ya kukabidhi hundi hiyo, Abdallah aliagiza Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kusimamia kwa karibu ujenzi wa soko hilo ili kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Alisema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kuboresha mazingira ya biashara na kuongeza fursa kwa wananchi wa eneo hilo.

Kazi ya Chama ni kusimamia Serikali kuhakikisha inatekeleza iliyoyaahidi kwenye Ilani yake. Watendaji hampaswi kukaa maofisini, tunataka mkatatue kero za wananchi. Mtaalamu yeyote anayeona Chama kinamfuatilia ajue kabisa Tanga haimfai,” alisema.

AWESO APIGA STOP MICHANGO MITIHANI

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Pangani na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amekabidhi mashine ya kuchapisha mitihani kwa Shule ya Sekondari ya Mikinguni, ambayo imepewa jina lake.

Aweso alisema amefanya hivyo baada ya kupata taarifa kwamba wanafunzi wa shule hiyo wamekuwa wakichangishwa fedha kila unapofika muda wa kufanya mitihani.

Alisema suala hilo sasa limetatuliwa na kupiga marufuku michango hiyo kwa wanafunzi.

Aidha, Aweso alisema atakutana na wananchi wa Wilaya ya Pangani, hususan wanawake, kujadili namna ya kuwawezesha kiuchumi ili waweze kukabiliana na changamoto ya mikopo yenye riba kubwa.

Mmetuchagua tumekuwa viongozi, tumeona mnavyoumia na mikopo chechefu na kausha damu. Hivi karibuni tutakaa kikao cha pamoja na kuona namna gani ya kuwezeshana kiuchumi ili mpate faida ya kutuchagua sisi vijana wenu tuwatumikie,” alisema.

PANGANI YAFUNGUKA KIUCHUMI

Wilaya ya Pangani inaendelea kupata miradi mbalimbali inayolenga kuongeza shughuli za kiuchumi, ikiwamo ujenzi wa Barabara ya Tanga–Bagamoyo.

Mbali na barabara hiyo, zipo pia mipango ya utekelezaji wa miradi mingine ya uwekezaji, ikiwamo ujenzi wa kiwanda cha sukari na kiwanda cha madini, hatua inayotarajiwa kuongeza fursa za biashara na ajira kwa wakazi wa wilaya hiyo.

mwisho

WAKUU WA TAASISI ZA MUUNGANO WATAKIWA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI

September 19, 2026 Add Comment
ZANZIBAR, Septemba 19, 2026 — Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, amewataka Wakuu wa Taasisi za Muungano kuimarisha ushirikiano na utekelezaji wa majukumu yao ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora bila kujali wanaishi upande gani wa Muungano.

WASTAAFU WAONYWA DHIDI YA MATAPELI KUPOTEZA MAFAO YAO

September 19, 2026 Add Comment




Na Marco Maduhu, SHINYANGA


WASTAAFU nchini wametakiwa kuwa makini na watu wanaojitambulisha kama mawakala wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), wakihimizwa kutumia njia rasmi za mfuko huo katika kuhakiki taarifa zao na kufuatilia mafao yao ili kuepuka kutapeliwa na kupoteza fedha zao.


Tahadhari hiyo imetolewa leo, Septemba 18, 2026, na Afisa Msimamizi wa PSSSF Mkoa wa Simiyu, Salum Mwegelo, wakati wa semina ya PSSSF kwa waandishi wa habari kutoka Klabu za Waandishi wa Habari za Shinyanga na Simiyu pamoja na Mtandao wa Wanablogu Tanzania (Tanzania Bloggers Network – TBN), iliyofanyika mjini Shinyanga.


Mwegelo amesema baadhi ya wastaafu wamekuwa katika hatari ya kutapeliwa kutokana na kutumia watu wasio rasmi wanaodai kuwa wanaweza kuwasaidia katika taratibu za kuhakiki taarifa, kufuatilia au kupata mafao yao.

Amesema watu hao wanaweza kuomba taarifa nyeti za wastaafu, ikiwemo namba za siri za akaunti za fedha na taarifa nyingine binafsi, ambazo zinaweza kutumiwa kufanya miamala bila ridhaa ya wahusika.


“Mawakala hao huwarubuni wastaafu na kuomba namba za siri na taarifa muhimu, ikiwemo taarifa za akaunti zao, na kisha kuzitumia kufanya miamala bila ridhaa ya wahusika na kusababisha kupoteza mafao,” amesema Mwegelo.


Mwegelo amesisitiza kuwa PSSSF haina mawakala wanaotoa huduma kwa niaba ya mfuko huo, hivyo wastaafu wanapaswa kuwa na tahadhari dhidi ya mtu yeyote anayejitambulisha kama wakala wa PSSSF na kuwaomba taarifa zao za siri.


Amesema wastaafu wanapaswa kutumia njia rasmi zinazotolewa na PSSSF, ikiwemo kufika katika ofisi za mfuko huo au kutumia mifumo ya kidijitali inayowawezesha wanachama na wastaafu kufuatilia na kuhakiki taarifa zao kwa usalama.


Amesema matumizi ya mifumo ya kidijitali ni miongoni mwa njia zinazoweza kuwasaidia wanachama kupata taarifa zao kwa urahisi bila kulazimika kuwapa watu wengine taarifa zao binafsi au za kifedha.


Kwa upande wake, Afisa Uhusiano wa PSSSF, Abdul Njalo, amewataka waandishi wa habari na wanablogu kutumia taaluma yao kuwafikishia wananchi taarifa sahihi kuhusu huduma za mfuko huo, hususan elimu inayohusu haki, wajibu na taratibu za kupata mafao.


Njalo amesema vyombo vya habari, blogu na majukwaa ya kidijitali vina nafasi kubwa katika kuhakikisha elimu hiyo inawafikia wanachama na wastaafu kwa lugha rahisi na inayoeleweka, huku akiwataka waandishi na wanablogu kuthibitisha taarifa kabla ya kuzifikisha kwa umma.


Amesema elimu sahihi inaweza kusaidia kuwawezesha wanachama na wastaafu kutambua njia halali za kupata huduma za PSSSF na kuchukua tahadhari dhidi ya watu wanaoweza kutumia mwanya wa ukosefu wa taarifa kuwahadaa.


Naye Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga, Greyson Kakuru, amesema semina hiyo imekuwa na umuhimu mkubwa kwa waandishi wa habari na wanablogu kwa kuwa imewapa uelewa zaidi kuhusu huduma za PSSSF na masuala yanayowahusu wanachama na wastaafu.


Kakuru amesema maarifa yaliyopatikana yatawasaidia waandishi na wanablogu kuandaa na kusambaza habari zenye usahihi, huku wakitoa elimu kwa jamii kuhusu namna ya kutumia huduma za PSSSF na kujilinda dhidi ya utapeli.


Amesema ushirikiano kati ya PSSSF na vyombo vya habari pamoja na wanablogu ni muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kwa wakati na kutumia huduma za hifadhi ya jamii kwa uelewa zaidi.


Naye Mratibu wa Tanzania Bloggers Network (TBN) Kanda ya Ziwa, Kadama Malunde, amepongeza PSSSF kwa kuandaa semina hiyo, akisema mafunzo kama hayo ni muhimu kwa waandishi wa habari na wanablogu kwa kuwa yanawaongezea uelewa wa masuala wanayopaswa kuyafikisha kwa jamii.


Malunde amesema waandishi na wanablogu wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha kila taarifa wanayoitoa kwa umma inathibitishwa, ina usahihi na inatoka katika vyanzo vinavyoaminika, hususan katika kipindi hiki ambacho taarifa za kidijitali zinaweza kusambaa kwa kasi kubwa.


“Semina kama hii ni muhimu kwa sababu inatupa nafasi ya kujifunza na kuongeza uelewa. Tukiwa waandishi na wanablogu, jukumu letu si kuchapisha taarifa tu, bali kuhakikisha taarifa tunazowafikishia wananchi ni sahihi, zimehakikiwa na zina manufaa kwa jamii,” amesema Malunde.

SERIKALI YAAGIZA UKAGUZI MAENEO YA UWEKEZAJI NCHINI

September 19, 2026 Add Comment

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo, amewaagiza Makamishna wa Ardhi Wasaidizi katika mikoa yote nchini kufanya ukaguzi wa maeneo ya uwekezaji yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali kwa lengo la kubaini maeneo yasiyoendelezwa na kutoa taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe


Dkt. Akwilapo ametoa agizo hilo Septemba 18, 2026, mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika maeneo ya uwekezaji ya Kongani ya Viwanda ya KAMAKA pamoja na kiwanda cha Nondo cha Gain Company Limited kilichopo Mlandizi, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani.

Amesema Wizara ya Ardhi, imebaini kuwepo kwa maeneo ambayo yalipewa wawekezaji kwa ahadi ya kuanzisha viwanda au shughuli nyingine za uzalishaji, lakini hayajaendelezwa kwa muda uliokubaliwa.


“Tuna taarifa kuna waliochukua maeneo wakasema watatengeneza viwanda lakini bado hawajafanya hivyo. Natoa maelekezo makamishna kufanya ukaguzi na kuwasilisha taarifa ili hatua stahiki zichukuliwe kwa maeneo yasiyoendelezwa kadri ya mikataba waliyoingia,” amesema Dkt. Akwilapo.

Aidha, Waziri huyo amewataka wamiliki wote wa ardhi ambao hawazingatii masharti ya uendelezaji maeneo waliyopewa kuhakikisha wanayaendeleza kwa wakati, vinginevyo wizara itachukua hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.


Amesisitiza kuwa, hatua hizo zitawahusu wawekezaji wazawa na wa kigeni, akieleza kuwa kwa wawekezaji wazawa hatua inaweza kujumuisha kubadilisha milki za ardhi walizopewa, huku kwa wawekezaji wa kigeni wizara ikishirikiana na taasisi husika, ikiwemo TISEZA, katika kushughulikia masuala ya umiliki na uwekezaji.

Dkt. Akwilapo amesema, hatua hiyo inalenga pia kujibu malalamiko kutoka kwa wananchi ambao maeneo yao yalichukuliwa kwa ajili ya uwekezaji, lakini baadaye hayakuendelezwa.


Ameeleza kuwa, hali hiyo imekuwa ikisababisha wananchi kuhoji sababu za maeneo kutolewa kwa wawekezaji ambao hawajaanza shughuli za maendeleo kwa muda mrefu.


Awali Mhe Dkt Akwilapo alielezwa kuwa eneo la Kongani ya Viwanda Mlandizi wilayani Kibaha mkoa wa Pwani linakabiliwa na changamoto kadhaa kama vile upatikanaji wa maji na ubovu wa barabara hali waliyoieleza kuwa inayosababisha kero katika usafirishaji bidhaa na malighafi.



Hata hivyo, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wameeleza kuanza  kuchukua hatua za dharura kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi wa muda mfupi na mrefu


Ziara ya Dkt. Akwilapo katika Mkoa wa Pwani imelenga kujionea kwa karibu shughuli za uwekezaji na matumizi ya ardhi katika maeneo hayo, pamoja na kutathmini namna bora ya kuendeleza maeneo ya uwekezaji kwa kuzingatia mipango ya matumizi ya ardhi na maendeleo endelevu.


Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi za kutambua fursa na changamoto zinazohusiana na ardhi na uwekezaji, kwa lengo la kuimarisha matumizi bora ya ardhi, kuvutia uwekezaji na kuchochea maendeleo ya wananchi.


----------mwisho---------

Green Acres yajivunia umahiri wa taaluma

September 19, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

Mkururugenzi wa shule ya Green Acres ya Mbezi Beach Salasala jijini Dar es Salaam, Jacklline Rushaigo ameelezea namna shule hiyo ilivyoanza kufundisha Teknojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA ili kwenda sanjari na ulimwengu kidijitali.

ROSTAM AZIZI: UONGOZI IMARA, SERA BORA NA MIFUMO THABITI VITAAMUA MUSTAKABALI WA UWEKEZAJI AFRIKA MASHARIKI

September 19, 2026 Add Comment
Mfanyabiashara maarufu nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi, akizungumza katika Jukwaa la Nne la Biashara la Watendaji Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum).
Mfanyabiashara maarufu nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi, akizungumza katika Jukwaa la Nne la Biashara la Watendaji Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum)
Mfanyabiashara maarufu nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa Group, Rostam Azizi, akiwa katika Jukwaa la Nne la Biashara la Watendaji Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum)

***
Mfanyabiashara maarufu nchini na kanda ya Afrika na Mwenyekiti wa Taifa Group , Rostam Azizi, amehimiza uwepo wa uongozi imara, taasisi madhubuti, sera nzuri na uwazi wa mifumo ili kufungua zaidi fursa za uwekezaji na mitaji ya kimataifa katika nchi za kanda ya Afrika Mashariki.

Akiongea kwenye Jukwaa la nne la Biashara la Watendaji wakuu 200 (200 CEOs Business Forum) linalowakutanisha pamoja wafanyabiashara na wawekezaji nchini, alisema ushirikiano wa kweli kati ya wawekezaji, wafanyabiashara na Serikali utajengwa kwenye misingi ya mifumo mathubuti ya kikodi, kisera kikanuni na sheria nchini na kwenye nchi nyinginezo za Afrika Mashariki.

Rostam alisema wadau wote wanapaswa kujikita kuangalia ni kwa namna ipi tunaweza kuifanya Afrika Mashariki kuwa chaguo kuu la uwekezaji wa mitaji ya mitajiya kimataifa.

“Nianze kwa kuwapongeza waandaaji wa Kongamano la Biashara la Wakurugenzi Wakuu 200 (200 CEOs Business Forum) kwa kuwaleta pamoja viongozi wa Serikali, Sekta binafsi na wawekezaji na suala la msingi la kujadili ni jinsi gani tuanaweza kuifanya Afrika Mashariki kuwa chaguo kuu la mitaji wa kimataifa”, alisema Rostam Azizi.

Alisema rasilimali nyingi za asili, idadi ya watu na eneo la kijiografia havitoshi kuhakikisha uwekezaji wa muda mrefu kutoka kwa wawekezaji wa kimataifa kuja kuwekeza bali pia kunatakiwa uwepo mazingira ya kuwakikishia uhakika,utulivu ,ukuaji na kuwajengea imani.

Alisisitiza jukwaa hili kutoka na maamuzi yenye kuleta athari kubwa kwa utekelezaji wa mitaji na pamoja na mambo mengine kujua sekta zinazokua na ajira jinsi ya utengenezaji wa ajira mpya ndani ya Afrika Mashariki sambamba na kujua taasisi za kifedha zinazowezesha biashara na ufadhili, viwanda vinavyoongeza thamani ya fedha, makampuni ya madini yanayofungua fursa za rasilimali na makampuni ya mawasiliano yanayofanya vizuri ili kuwaunganisha mamilioni ya watu ndani ya Ukanda wa Afrika Mashariki.
“Niruhusuni kuzungumza kutokana na uzoefu wangu, katika kipindi cha zaidi ya miaka thelathini, kupitia Taifa Group pamoja na washirika wetu mbalimbali, nimepata fursa ya kuwekeza katika sekta za mawasiliano, madini, nishati, usafiri wa anga, vyombo vya habari na miundombinu,” amesema Rostam Azizi.

Aliongeza kwamba watu wengi hudhani kuwa uwekezaji unaanza na uchambuzi wa kifedha ambapo si kweli bali wawekezaji wengi wanataka imani na mwelekeo wa nchini husika pamoja na makubaliano kuheshimiwa na sera ambazo zinaweza kutabirika.

Pamoja na mambo mengine alilisitiza umuhimu wa kuwa na taasisi imara na zenye kuaminika na kanuni zilizo wazi na mazingira mazuri ya uwekezaji na madhubuti yanayoweza kutabirika kisheria na kitaasisi ambayo yataleta matokeo chanya.

Alisema Afrika Mashariki si eneo la matarajio pekee ni fursa halisi ambayo inahitaji mageuzi ya haraka ya kidigitali, na mikakati kabambe ya kufikia njia kuu za biashara za dunia ili kufugua milango ya fursa ya mitaji ya kimataifa.

“Ari ya ujasiriamali ndani ya Afrika mashariki na ukauaji wa soko la walaji ni fursa ya kipekee wa wanajumuiya wa kuunganisha nguvu pamoja ili kuleta mapinduzi ya kweli kwenye uwekezaji. Tanzania iko katikati ya fursa hiyo na bandari zetu zinaunganisha uchumi wetu pamoja na nchi jirani zisizo na bandari na dunia tambayo hutoa fursa ya kufikia masoko ya kikanda na kimataifa,”alisisitiza.
Aliongeza kwamba uwekezaji katika bandari, reli ya Standard Gauge Railway (SGR) , nishati , mifumo ya usafirishaji na mawasiliano ya kidigitali unaimarisha nafasi hiyo kwa kupunguza gharama za biashara na kuongeza tija.

Alisema kwa pamoja , nchi za Afrika Mashariki zinawakilisha soko la zaidi ya watu milioni 300, ikiwa na rasilimali nyingi za asili , idadi kubwa ya vijana na miundombinu inayozidi kuimarika.

“Hakuna nchi moja katika ukanda wetu yenye kila faida ya ushindani , hakuna uchumi mmoja wenye kila rasilimali, hakuna soko moja linaloweza kufikia uwezo wake kamili likiwa peke yake,” alisisitiza.

Rostam Azizi alisema ni muhimu kwa serikali za Afrika Mashariki kuanza mchakato wa kuimarisha miumdombinu inayovuka mipaka , kupunguza vikwazo vya kibiashara , kuimarisha ushirikiano wa kifedha na kurahisisha usafirishaji wa mitaji, bidhaa na wataalamu wenye ujuzi ndani ya ukanda huo.

Aliongeza kuwa jukumu la serikali, ni kuendelea kujenga mazingira bora na yanayotabirika kwa uwekezaji na biashara na inajumuisha kudumisha uthabiti wa uchumi wa jumla, kuimarisha miundombinu, kuboresha mazingira ya udhibiti, kuwezesha uwekezaji, kuongeza upatikanaji wa mitaji na kuimarisha taasisi za umma.

Alitoa rai kwa sekta binafsi kuhakikisha zinaongeza tija huku zikiimarisha utawala bora katika biashara zao na kutumia teknolojia za kisasa pia ziendeleze rasilimali watu na zijenge biashara zinazoweza kushindana ndani ya Tanzania, Afrika Mashariki na kwingineko.

MAKAMU WA RAIS AAGIZA MAWAZIRI WATATU KUTATUA MGOGORO WA MIPAKA PUGU NDANI YA SIKU SABA

September 19, 2026 Add Comment


Na: OWM–TAMISEMI, Dar es Salaam.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewaagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Waziri wa Maliasili na Utalii kufika ndani ya siku saba katika Dampo la Pugu kwa ajili ya kutatua mgogoro wa muda mrefu wa wananchi kuhusu mipaka ya kiutawala na mpaka wa Msitu wa Kazimzumbwi.

Makamu wa Rais ametoa agizo hilo Septemba 18, 2026, jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wananchi wa Pugu mara baada ya kufanya ziara katika Dampo la Pugu, linalohudumia Mkoa wa Dar es Salaam kwa kupokea taka, na kusikiliza kero zinazowakabili wananchi wa eneo hilo.

“Nikiwa Dampo kuna wazee wangu waliwasilisha malalamiko juu ya kubuguziwa katika Msitu wa Kazimzumbwi, wakidai hawajui kama wako eneo gani la utawala, Pwani au Dar es Salaam. Hivyo, ninawaelekeza Mawaziri wa TAMISEMI, Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wa Maliasili na Utalii kuhakikisha ndani ya siku saba wawe wamefika hapa kutatua changamoto hiyo ya wananchi kubuguziwa,” amesema Mhe. Ndejembi.

Aidha, Mhe. Ndejembi amewataka mawaziri hao watakapofika katika eneo hilo kuzungumza na wananchi na kuhakikisha katika kutatua changamoto hiyo wanatumia taarifa rasmi ya Serikali kuhusu mipaka ya kiutawala, yaani Government Notice (GN) iliyochapishwa katika Gazeti la Serikali, kama msingi wa kubaini mipaka husika.

Akizungumza kwa niaba ya mawaziri wenzake, Waziri wa Nchi, OWM–TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameahidi kutekeleza maelekezo hayo ya Makamu wa Rais kwa kufika katika eneo hilo ndani ya siku saba na kuzungumza na wananchi kwa ajili ya kutafuta suluhisho la mgogoro huo.

“Mhe. Makamu wa Rais, tumepokea maelekezo yako ya kutatua mgogoro huu wa wananchi wa mipaka ya kiutawala na Msitu wa Kazimzumbwi ndani ya siku saba. Hivyo, mimi Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa TAMISEMI, Dkt. Akwilapo, Waziri wa Ardhi, na Dkt. Ashatu Kijaji, Waziri wa Maliasili, tutakuja kuzungumza na wananchi ili kutatua mgogoro huo,” amesema Prof. Shemdoe.

Aidha, Prof. Shemdoe ameahidi kutekeleza maelekezo ya Makamu wa Rais ya kuzisimamia Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam kuleta vitendea kazi, ikiwemo tingatinga (bulldozer), kwa ajili ya kuboresha mazingira na kuongeza ufanisi wa huduma ya upokeaji wa taka katika Dampo la Pugu.

Prof. Shemdoe amesema tayari amemwelekeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuanza kufuatilia utekelezaji wa agizo hilo ili kuhakikisha vitendea kazi vinapatikana na hatua zinazohitajika zinachukuliwa.

Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumshukuru na kumpongeza Makamu wa Rais, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kufanya ziara katika Dampo la Pugu, kusikiliza kero za wananchi na kutoa maelekezo ya hatua za haraka kuchukuliwa kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa utendaji kazi wa dampo hilo linalohudumia Mkoa wa Dar es Salaam.



TANZANIA KUWA MWENYEJI WA KONGAMANO LA MITAALA AFRIKA

September 19, 2026 Add Comment
TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano la Sita la Jumuiya ya Taasisi za Mitaala Afrika (ACA), litakalofanyika Septemba 22 hadi 25, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.

TPi YASHIRIKIANA NA JAMII KUIMARISHA USAFI WA MAZINGIRA

September 19, 2026 Add Comment
TAASISI ya Tanzania Pathways Initiative (TPi) imeungana na jamii ya Kawe Ukwamani jijini Dar es Salaam katika zoezi la usafi wa mazingira, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha jiji linakuwa safi na salama.

JAB YAWANOA WAANDISHI WA WASAFI MEDIA MEDIA KUHUSU SHERIA NA MAADILI

September 19, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu.

Washiriki wa mafunzo kwa Waandishi wa Habari kutoka Wasafi Media wameeleza kuwa mada zilizotolewa katika mafunzo hayo zimewasaidia kutambua makosa yaliyokuwa yakijirudia katika utekelezaji wa majukumu yao na kuwapatia mwongozo wa kuboresha utendaji.

Wakizungumza wakati wa tathmini ya mafunzo hayo yaliyofanyika Septemba 17 na 18, 2026, katika Ofisi za Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) jijini Dar es Salaam, Gerald Hando, Aggai Kifumu na David Rwenyagira wameeleza kuwa mafunzo yamewaongezea uelewa kuhusu sheria, maadili na uzalendo katika uandishi wa habari.
Wamebainisha kuwa miongoni mwa changamoto zinazowakabili Waandishi wa Habari na wazalishaji wa maudhui ni shinikizo la kuongeza idadi ya wafuasi katika majukwaa ya kidijitali, kukidhi matakwa ya hadhira pana na kasi ya mabadiliko katika mazingira ya kidijitali kuwa kubwa kuliko maboresho ya baadhi ya sheria zinazoongoza shughuli zao.

Kwa mujibu wa washiriki hao, mazingira hayo yanaweza kusababisha baadhi ya Waandishi wa Habari kufanya kazi kwa mazoea au kujikuta wakifanya makosa ya kisheria na kimaadili bila kuwa na uelewa wa kutosha.
Wamesema mafunzo hayo yamewajenga kitaaluma, yamewafungua kutoka katika utendaji wa mazoea na kuwapatia mwongozo wa kufanya maamuzi sahihi katika majukumu yao ya kila siku.

Aidha, wameiomba JAB kuendelea kutoa mafunzo hayo kwa Waandishi wa Habari kutoka vyombo vingine, huku kipaumbele kikitolewa kwa wanaofanya kazi na kuzalisha maudhui kupitia majukwaa ya kidijitali, ambako changamoto za uzingatiaji wa sheria na maadili zimeendelea kujitokeza.
Wamesema kasi ya uzalishaji na usambazaji wa maudhui katika majukwaa hayo imeongeza uwezekano wa kutokea kwa makosa ya kisheria na kimaadili, hivyo elimu endelevu inahitajika ili kuimarisha weledi na uwajibikaji.

Mafunzo hayo yalihusu Sheria ya Huduma za Habari, maadili ya uandishi wa habari na uzalendo, yakilenga kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari na watangazaji wa Wasafi Media kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, viwango vya taaluma na maslahi ya jamii.