HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TCU YATANGAZA AWAMU YA PILI YA UDAHILI WA VYUO KWA MWAKA WA MASOMO 2026/2027

TCU YATANGAZA AWAMU YA PILI YA UDAHILI WA VYUO KWA MWAKA WA MASOMO 2026/2027

September 08, 2026 Add Comment

Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa,akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 8,2026 jijini Dodoma  kuhusu kukamilika kwa awamu ya kwanza na kufunguliwa kwa awamu ya pili ya udahili wa shahada ya kwanza kwa mwaka wa masomo 2026/2027/.

Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Prof. Charles Kihampa,akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 8,2026 jijini Dodoma  kuhusu kukamilika kwa awamu ya kwanza na kufunguliwa kwa awamu ya pili ya udahili wa shahada ya kwanza kwa mwaka wa masomo 2026/2027/.

Na.Alex Sonna-DODOMA 
TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imetangaza kukamilika kwa Awamu ya Kwanza ya udahili wa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na programu za Shahada ya Kwanza kwa mwaka wa masomo 2026/2027 na kuanza kwa Awamu ya Pili ya udahili kuanzia leo, Septemba 8 hadi 21, mwaka huu.
Hayo yamesemwa leo Septemba 8,2026 jijini Dodoma na Katibu Mtendaji wa TCU, Prof. Charles Kihampa, amesema jumla ya waombaji 149,645 waliwasilisha maombi ya kujiunga na vyuo 93 vilivyoidhinishwa kudahili wanafunzi wa Shahada ya Kwanza katika mwaka wa masomo 2026/2027.
Prof. Kihampa amesema katika mwaka huo wa masomo, vyuo vimeongeza programu za Shahada ya Kwanza kutoka 894 mwaka 2025/2026 hadi kufikia 1,019, sawa na ongezeko la programu 125, huku nafasi za udahili zikiongezeka kutoka 205,652 hadi 227,555.
Amesema ongezeko hilo la nafasi 21,903 ni sawa na asilimia 10.7, hatua inayolenga kuongeza fursa kwa vijana wanaohitaji kuendelea na elimu ya juu nchini.
Aidha, ameeleza kuwa katika Awamu ya Kwanza, waombaji 117,334, sawa na asilimia 78.4 ya waombaji wote, wamepata nafasi za udahili katika vyuo walivyoviomba, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka baada ya kukamilika kwa Awamu ya Pili.
 "Waombaji waliopata udahili katika vyuo zaidi ya kimoja wametakiwa kuthibitisha chuo kimojawapo kuanzia Septemba 8 hadi 21, 2026, kwa kutumia namba maalum ya siri iliyotumwa kupitia ujumbe mfupi wa simu au barua pepe waliotumia wakati wa kuomba udahili."amesema Prof. Kihampa
Aidha, TCU imewataka waombaji ambao hawakupata nafasi katika Awamu ya Kwanza, pamoja na wale ambao hawakuweza kuwasilisha maombi, kutumia fursa ya Awamu ya Pili kwa kutuma maombi katika vyuo na programu wanazozipenda. Vyuo pia vimeelekezwa kutangaza programu ambazo bado zina nafasi.
"Tume imewakumbusha waombaji kuwa masuala yote yanayohusu udahili na uthibitisho wa nafasi yanapaswa kuwasilishwa moja kwa moja katika vyuo husika, huku vyuo vikielekezwa kushughulikia changamoto za waombaji kwa haraka kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya udahili," amesisitiza.

UNESCO PUTS GIRLS AT THE HEART OF TANZANIA’S DIGITAL FUTURE

September 08, 2026 Add Comment

DODOMA, September 8, 2026: 

Efforts to prepare Tanzanian girls for the rapidly expanding digital economy are taking a new direction, with UNESCO calling for gender to be placed at the centre of digital skills education to ensure that girls are not left behind in the country’s digital transformation.

The call comes as Tanzania, through collaboration with UNESCO and Beijing Normal University (BNU), implements the “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls” project, an initiative aimed at strengthening digital skills while addressing barriers that continue to limit girls’ participation in technology and innovation.

Gender specialist Dr Rosemarie N. Mwaipopo said digitalisation was no longer simply a matter of access to computers or the internet, but an increasingly important pathway to education, employment, innovation and wider socio-economic development.

She said the country’s digital transformation would have greater impact if girls were given deliberate opportunities to acquire digital skills, participate in innovation and develop the confidence needed to pursue technology-related education and careers.

“Digitalisation is a major influence in societal development, enhancing access to opportunities,” Dr Mwaipopo said, while emphasising the need to confront the persistent gender gap in digital participation.

She questioned why the gap continued to exist globally and in Tanzania despite various innovations, programmes and interventions designed to expand access to technology and digital skills.

According to her, the challenge was not only about whether technology was available, but also about who had the skills, confidence, opportunity and enabling environment to use that technology and turn it into meaningful solutions.

She said this was where the UNESCO-BNU project could make an important contribution by introducing a gender perspective into digital skills education.

CREATING A CRITICAL MASS OF GIRLS IN ICT

Dr Mwaipopo said the project would deliberately select female students to participate in ICT innovation training as part of an affirmative action approach aimed at creating a critical mass of girls with digital knowledge and skills.

She said increasing the number of girls exposed to technology and innovation would help challenge the long-standing perception that ICT and STEM-related fields were predominantly for boys.

The approach, she explained, was intended to create more girls who could confidently engage with technology, develop innovations and eventually pursue careers in the digital sector.

“This is not simply about teaching girls how to use technology. It is about creating opportunities for them to become knowledgeable, confident and active participants in the digital future,” she said.

She said a growing pool of digitally skilled girls could also provide role models for younger generations and contribute to changing community perceptions about the role of women in technology.

CHANGING THE WAY GIRLS LEARN

Dr Mwaipopo said teachers would be equally important in achieving this transformation.

She called for teachers to be equipped with gender-transformative pedagogy, enabling them to recognise and challenge attitudes, practices and social norms that may discourage girls from participating fully in ICT and STEM education.

She said teachers needed to create classrooms where girls felt confident to experiment, ask questions, solve problems and develop technological innovations.

The objective, she said, was to move beyond simply providing equal access to boys and girls towards creating learning environments capable of transforming the conditions that have historically limited girls’ participation.



She said teachers and students would also need greater awareness of gender equality, gender barriers, enabling factors and intersectionality to understand why girls may experience digital education differently depending on their social and economic circumstances.

INNOVATION THAT WORKS FOR EVERYONE

Dr Mwaipopo further challenged students to think about gender when developing ICT solutions.
She said female students should be equipped to apply a gender lens in ICT processes and innovation, ensuring that digital products and solutions were accessible, sensitive to different needs and inclusive.

She explained that successful digital innovation should not only answer the question of whether a technology works, but also consider who can access it, who can use it and who ultimately benefits from it.

Such an approach, she said, would enable girls to see technology as more than computers and coding, but as a powerful tool for addressing real challenges facing families, communities and the country.

BUILDING TANZANIA’S DIGITAL GENERATION

The gender-transformative approach is being implemented alongside efforts to establish and strengthen ICT Clubs in public schools, providing girls with practical opportunities to develop digital skills, participate in innovation and explore technology-related career pathways.

The broader UNESCO-BNU initiative is being implemented in collaboration with the Government of the United Republic of Tanzania, reflecting the importance of partnerships in strengthening digital education and expanding opportunities for women and girls.

Through the project, teachers and female students are expected to gain skills and approaches that can contribute to more inclusive digital learning environments.

For Tanzania, the initiative comes at a time when digital skills are increasingly becoming essential for education, employment, entrepreneurship and innovation.
Its significance therefore extends beyond the classroom.

By deliberately investing in girls’ digital skills today, the country is building a generation capable of participating in and contributing to tomorrow’s technology-driven economy.

The ultimate ambition is to ensure that Tanzanian girls are not merely users of technology, but creators, innovators, entrepreneurs and future leaders in the digital economy.

And by ensuring that no girl is excluded from the digital transformation, Tanzania can strengthen its human capital and build a more inclusive digital future in which every girl has an opportunity to learn, innovate and shape the country’s development.

NEMC YAELEZA NAFASI YAKE KATIKA KONGAMANO LA 5 LA KIMATAIFA LA UCHUMI WA BULUU

September 08, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), katika Kongamano la 5 la Kimataifa la Uchumi wa Buluu, limejipambanua katika sekta ya mazingira kwa kusisitiza umuhimu wa matumizi endelevu ya rasilimali za bahari, mito, maziwa na maeneo ya pwani, sambamba na uhifadhi na usimamizi endelevu wa mazingira.

PSSSF NA TBN WAJENGA USHIRIKIANO MKAKATI WA KUONGEZA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII

September 07, 2026 Add Comment




Dar es Salaam


Katika kile kinachoelezwa kuwa ni hatua madhubuti ya kupanua wigo wa utoaji wa elimu kwa umma, timu ya maofisa wa juu kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imefanya ziara rasmi katika makao makuu ya muda ya Tanzania Bloggers Network (TBN) yaliyoipo Dar es salaam, Kijitonyama na kufanya mazungumzo ya kimkakati na viongozi wakuu wa mtandao huo.


Mazungumzo hayo yaliyolenga kujenga ushirikiano wa manufaa ya pande zote mbili  yamejikita katika kuimarisha uhusiano wa kisekta kwenye masuala ya habari, uelimishaji wa umma, na usambazaji wa maarifa sahihi kuhusu mifumo ya pensheni na uwekezaji nchini.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alieleza utayari wa mtandao huo kusimama kidete kama chombo cha kutoa elimu na kusambaza maarifa sahihi kwa umma na katika nyanja za kidijitali (space). Hata hivyo, alisisitiza kuwa ili kufikia malengo hayo kwa ufanisi zaidi, ni muhimu wanachama wa TBN wenyewe wakapatiwa kwanza mafunzo ya kina na ya kutosha kuhusu shughuli na uendeshaji wa mfuko huo.

Ushirikiano huo unatazamiwa kufungua ukurasa mpya katika matumizi ya vyombo vya habari vya mtandaoni kufikisha elimu ya hifadhi ya jamii kwa wananchi wengi zaidi nchini.


Kwa upande wake, Mkuu wa msafara huo kutoka PSSSF, Abdul Njaidi, alieleza kuwa ziara hiyo inalenga kujenga uhusiano wa karibu na wadau wa sekta ya habari pamoja na kutoa elimu kwa jamii. Aliwahakikishia viongozi wa TBN kuwa maombi na hoja zote zilizowasilishwa zitafanyiwa kazi, akisisitiza kuwa ushirikiano huo mpya unalenga kuhakikisha wananchi wanapata uelewa mpana na sahihi kuhusu masuala ya pensheni na uwekezaji unaofanywa na PSSSF.

Naye Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi, ambaye alishiriki katika mkutano huo, alieleza kuwa mtandao huo wenye historia kubwa unajivunia weledi na ufanisi mkubwa. 

Alisema TBN ipo kwa ajili ya kuhakikisha Tanzania inasomeka vyema katika medani za kidijitali ili kuchochea na kutanua zaidi gurudumu la maendeleo ya taifa.

Katibu wa TBN, Rahel Pallangyo, aliongeza kuwa mtandao huo upo tayari kutoa waandishi wake mahiri na kutumia majukwaa yake mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na za kuaminika zitakazowezesha kufanikiwa kwa utekelezaji wa majukumu ya wananchi na wadau wa maendeleo.


Katika mkutano huo, ujumbe wa PSSSF ulioongozwa na Abdul Njaidi, ulijumuisha maofisa wengine akiwemo Regina Kumba, Grayson Mgunda, na Doreen Lyimo. 

Kwa upande wa TBN, viongozi waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti Beda Msimbe, Katibu Rahel Pallangyo, mtaalamu wa mawasiliano, Cathbert Kajuna na Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi.

Mwisho

VIJANA WATAKIWA KUANDALIWA UONGOZI TANGU WAKIWA WADOGO

September 07, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

VIJANA nchini wametakiwa kupewa mafunzo ya uongozi tangu wakiwa katika umri mdogo ili kuwaandaa kuwa viongozi wenye maadili, uwajibikaji na uwezo wa kuongoza katika nyanja mbalimbali, hatua inayolenga kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

UNESCO LAUNCHES ICT CLUBS TO BUILD GIRLS’ DIGITAL FUTURES

September 07, 2026 Add Comment


DODOMA, September 7, 2026:

 UNESCO, in collaboration with Beijing Normal University (BNU) and the Government of the United Republic of Tanzania, has launched a programme to establish and stren

gthen Information and Communication Technology (ICT) Clubs in public schools in Dodoma and Morogoro, aimed at equipping girls with digital skills, confidence and knowledge to pursue education and careers in technology.




The initiative is being implemented under the UNESCO-BNU project, “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls,” which seeks to reduce the gender gap in digital education and expand opportunities for women and girls to participate fully in the technology sector.







Speaking during the official launch held today at Edema Conference Hall in Kisasa, Dodoma, UNESCO Tanzania Head of Education Sector, Dr Faith Shayo, said the initiative was designed to encourage girls to develop an interest in technology, build confidence and explore opportunities in ICT-related education and careers.



She said the ICT Clubs would provide students with opportunities for practical learning, innovation and the development of skills to use technology to address challenges in their communities.

Dr Shayo said the programme would also involve ICT teachers and student teachers, with the clubs serving as platforms for extracurricular activities that give students practical experience beyond regular classroom lessons.


She said challenges contributing to the digital divide included disparities in access to technology, digital skills and competencies, as well as limited opportunities for girls to gain first-hand knowledge of education and career pathways in technology-related fields.


The programme is being implemented in collaboration with the Ministry of Education, Science and Technology (MoEST), the Prime Minister’s Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), and the Tanzania Institute of Education (TIE).

A total of 20 public schools are expected to participate, with 10 from Morogoro Municipality and 10 from Dodoma City. The programme will directly benefit 500 girls and 40 teachers.


The official launch marks the beginning of a series of activities under the programme, with a four-day ICT Innovation Bootcamp scheduled to begin tomorrow, September 8, at Msalato, and run through Friday, September 11, 2026.

The Bootcamp will provide students with opportunities for practical learning, digital skills development and innovation, including developing and showcasing digital ideas and projects aimed at addressing real-life challenges in their communities.


In Dodoma, participating schools include Dodoma, Kisasa, Nara, Ihumwa, Makole, Mnadani, Hazina, Mtumba and Msalato, all secondary schools.

Through the ICT Clubs, students will receive practical training in computer programming (coding), computational thinking and problem-solving, digital creativity, visual and audio content production, and the safe and responsible use of technology.


The girls will also be connected with women ICT professionals through mentorship programmes, enabling them to learn from their experiences and gain a broader understanding of education, employment and career opportunities in the technology sector.

PMO-RALG STRESSES COLLABORATION

Speaking on behalf of the Prime minister Office – Regional Administration and Local Government (PMO-RALG), Mr. Francis Gervas, from the Education Management Department, thanked UNESCO for partnering with the Government in implementing the initiative.

He stressed the importance of continued collaboration among stakeholders to ensure that the programme achieves its intended objectives and that the results and lessons generated are sustained beyond the implementation period.

Mr. Gervas also called for the initiative to be expanded to other parts of the country so that more girls could benefit, while urging participants and stakeholders to remain committed to its effective implementation.

TEACHER CALLS FOR ATTITUDE CHANGE
Meanwhile, Mr Godfrey Robin Mseti, a teacher at Mtumba, commended the Government and UNESCO for introducing the initiative, saying opportunities and training related to technology had for a long time been perceived as being more accessible to boys and men.

He said society needed to change the perception that ICT-related learning was mainly for boys, stressing that girls also had the ability and should be given equal opportunities to learn, participate in and benefit from technology.

Under the programme, the ICT Clubs are intended to provide safe and inclusive learning environments where students can develop their skills through learning, innovation, leadership and collaboration.
Girls are expected to account for at least 50 per cent of participation in the clubs, with stakeholders encouraged to promote even greater representation.

Overall, the initiative is expected to strengthen ICT Clubs in 20 schools and enable 500 girls to improve their digital skills, confidence, participation and leadership abilities, while increasing their awareness of education and career opportunities in ICT.

The programme seeks to ensure that girls acquire not only the skills to use technology, but also the confidence to view technology as a tool for innovation, education and building their future careers.





PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI (AFDP) YAWAFIKIA WAKULIMA,WAVUVI NA JAMII YA WAFUGAJI MKOANI TANGA

September 07, 2026 Add Comment




Na; Mwandishi wetu-Tanga.


Ujumbe kutoka Mfuko wa Kimataifa la Kuendeleza Kilimo (IFAD) na wataalamu kutoka katika sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) wamekutana Mkoani Tanga Tarehe 7 Septemba 2026  kwa lengo la kufanya mapitio ya Utekelezaji wa Programu hiyo.


Sambamba na hilo timu hiyo itatembelea maeneo yanayotekeleza Programu kwa Mkoa wa Tanga, ambapo kwa upande wa sekta ya kilimo  timu hiyo itatembelea kata ya Msomela iliyopo katika Halmashauri ya Handeni Vijijini ambako programu imehamasisha na kutoa elimu ya kilimo bora kwa jamii ya kimasai ambao kiasili ni wafugaji ambapo wameweza kujishughulisha na kilimo cha mahindi chenye tija. 

Programu imewezesha kuwepo kwa eneo la mashamba darasa (FFS) kwa mazao ya Alizeti, Mahindi na Maharage, na shamba Darasa hilo limeonesha mafanikio kwa kiasi kikubwa, ambapo hekta moja inaweza kuzalisha takribani magunia 20 ya kilo mia moja kila moja, na jamii ya wafugaji sasa inajishulisha na shughuli za Kilimo na kunufaika na upatikanaji wa mazao yanayolimwa.

Kwa upande wa Sekta ya Uvuvi, Programu inaendelea na ujenzi wa soko la kimataifa la Samaki Kipumbwi lililloko katika halmashauri ya Pangani ambapo mpaka sasa ujenzi umefikia asilimia 68% na linategemewa kukamilika ifikapo Oktoba 2026.


Aidha, programu pia inaendelea na ujenzi wa vichanja 40 vya kukaushia dagaa ambavyo vinaweza kukausha takribani tani tano kwa za dagaa kwa wakati mmoja.

Kwa upande mwingine pia Programu ya AFDP inaendelea na ujenzi wa Ghala la baridi na mtambo wa barafu katika soko hilo kwa ajili ya kuhifadhi na kusafirisha samaki.

Awali Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la kimataifa la maendeleo ya Kilimo nchini (IFAD) Bw. Seth Meng alikutana na Kaimu Katibu tawala wa Mkoa wa Tanga Bw.Emmanuel Kisongo na kufanya mazungumzo kuhusiana na utekelezaji wa Programu katika Mkoa sambamba na mafanikio tarajiwa kwa wanachi wa maeneo husika ambapo Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa alieleza kuwa Programu hiyo ni muhimu sana katika kuhamasisha maendeleo ya kilimo na uvuvi katika mkoa huo. 


Aliishukuru IFAD kwa kuweza kuwafikia wananchi wa mkoa huo na kuwataka ikiwezekana kuongeza uwekezaji mkoani hapo.

TANESCO YATUNUKIWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WA UBUNIFU NA MAENDELEO YA NISHATI

September 07, 2026 Add Comment

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya kwa kutambua mchango wa kipekee katika ubunifu na maendeleo ya sekta ya Nishati nchini  ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa Shirika katika kuendeleza sekta hiyo.


Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO katika hafla ya tuzo za ujenzi wa miundombinu na uchimbaji madini kwa mwaka 2026, iliyofanyika Septemba 4, 2026 jijini Dar es Salaam.


Akikabidhi tuzo hiyo Mkurugenzi wa Usajili wa Wakandarasi Wizara ya Ujenzi Mhandisi Rhoben Nkori kwa Niaba ya Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amelipongeza Shirika kwa kuendelea kuimalisha upatikanaji wa Umeme katika Maeneo mbalimbali hapa nchini Hali ambayo imekuwa Chachu ya kuchochea Maendeleo katika sekta mbalimbali hapa nchini.


Tuzo hiyo imetolewa na Chama cha Ujenzi na Miundombinu cha Tanzania (CCIT), ikiwa ni utambuzi wa mchango wa TANESCO katika ubunifu na maendeleo ya nishati nchini.

CRDB NA TRA SACCOS WAZINDUA PESACARD, WANACHAMA KUPATA HUDUMA KWA URAHISI

Kajunason September 06, 2026 Add Comment

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, 5 Septemba 2026 – Benki ya CRDB kwa kushirikiana na TRA SACCOS imezindua rasmi TRA SACCOS PESACARD, kadi mpya inayotumia mfumo wa Visa inayolenga kuwapa wanachama wa TRA SACCOS urahisi, uhuru na wigo mpana zaidi wa kupata na kutumia fedha zao, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya TRA SACCOS.

Uzinduzi huo ni hatua muhimu katika ushirikiano wa muda mrefu kati ya Benki ya CRDB na TRA SACCOS, na unaashiria awamu mpya ya mageuzi ya kidijitali katika utoaji wa huduma za kifedha kwa wanachama wa SACCOS hiyo.

Kupitia TRA SACCOS PESACARD, wanachama wataunganishwa na mfumo mpana wa malipo wa Visa na hivyo kuwa na uwezo wa kutoa fedha kupitia ATM pamoja na kufanya malipo katika vituo vya POS vinavyokubali Visa ndani na nje ya Tanzania. 

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel  Chongolo aliipongeza TRA SACCOS kwa kufikisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwake, huku akiipongeza Benki ya CRDB kwa kuendelea kutumia uwezo wake wa kiteknolojia na kifedha kusaidia taasisi mbalimbali kupanua huduma za kisasa za kifedha.

“Miaka 20 ni hatua kubwa inayodhihirisha uimara, uaminifu na mchango wa TRA SACCOS katika kuboresha ustawi wa kifedha wa wanachama wake. Nawapongeza viongozi na wanachama kwa kuendelea kubadilika kulingana na mahitaji ya wakati, na Benki ya CRDB kwa kutumia uwezo wake wa kifedha na kiteknolojia kujenga ushirikiano unaorahisisha upatikanaji wa huduma. Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD unaonesha mafanikio tunayoweza kuyapata pale taasisi za fedha na vyama vya ushirika vinapounganisha nguvu katika kukuza ubunifu na ujumuishi wa kifedha.”

Pamoja na uzinduzi wa kadi hiyo, ushirikiano huo umewezesha kuunganishwa moja kwa moja kwa mifumo ya TRA SACCOS na mifumo ya Benki ya CRDB. Maboresho hayo yanamaanisha kuwa mwanachama anaweza kutumia akaunti yake iliyopo ndani ya mfumo wa TRA SACCOS kupata huduma zinazohusiana na PESACARD bila kulazimika kuwa na akaunti katika benki nyingine ya biashara. 

Muunganiko huo pia unatarajiwa kuongeza ufanisi katika utoaji wa mikopo kwa wanachama. Fedha za mikopo zitaweza kutolewa moja kwa moja kupitia mfumo wa TRA SACCOS, hatua inayopunguza michakato ya kuhamisha fedha kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine na hivyo kupunguza muda wa mwanachama kusubiri fedha baada ya mkopo wake kuidhinishwa. 

Katibu wa Benki ya CRDB, Pascal Mihayo, alisema hatua hiyo inaakisi dhamira ya Benki ya kutumia teknolojia na ushirikiano wa kimkakati kutengeneza suluhisho zinazojibu mahitaji halisi ya wateja.

“Kwetu Benki ya CRDB, huu ni zaidi ya uzinduzi wa kadi. Ni uthibitisho wa namna ushirikiano wa muda mrefu unavyoweza kukua na kuzaa suluhisho zinazogusa maisha ya watu moja kwa moja. Kupitia TRA SACCOS PESACARD na muunganiko wa mifumo yetu, tunawapa wanachama uhuru zaidi wa kupata na kutumia fedha zao, huku tukiiwezesha TRA SACCOS kuongeza kasi na ufanisi wa utoaji wa huduma. Haya ndiyo mageuzi ya kidigitali tunayoyasimamia, teknolojia inayorahisisha huduma, inayozisogeza karibu na wananchi na inayoongeza thamani halisi kwa mtumiaji.”

Miongoni mwa maboresho mengine muhimu ni kuunganishwa kwa huduma za TRA SACCOS na mtandao wa Mawakala wa CRDB. Hatua hiyo itawawezesha wanachama kuweka na kutoa fedha kupitia zaidi ya Mawakala 40,000 wa CRDB waliopo maeneo mbalimbali nchini, hivyo kupanua kwa kiasi kikubwa maeneo ambayo mwanachama anaweza kupata huduma. 

Maboresho hayo yana umuhimu mkubwa hususan kwa wanachama waliopo nje ya maeneo yenye matawi ya benki, kwa kuwa yanapunguza utegemezi wa maeneo ya kawaida ya huduma za kifedha na kutumia mtandao mpana wa Benki ya CRDB kupeleka huduma karibu zaidi na mwanachama.

Kwa upande wake, Kamishnawa TRA, Yusuph Mwenda aliishukuru Benki ya CRDB kwa ushirikiano wake, akieleza kuwa PESACARD na muunganiko wa mifumo ni sehemu muhimu ya safari ya TRA SACCOS ya kuboresha na kufanya huduma zake kuwa za kisasa zaidi.

“Tunapoadhimisha miaka 20 ya TRA SACCOS, hatuangalii tu tulikotoka na mafanikio tuliyoyapata; tunaangalia pia tunakotaka kwenda na aina ya taasisi tunayotaka kuijenga kwa ajili ya wanachama wetu. TRA SACCOS PESACARD ni sehemu ya safari hiyo ya baadaye. Inawapa wanachama wetu urahisi, wigo mpana zaidi wa huduma na uwezo mkubwa wa kusimamia miamala yao. Tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kuamini maono yetu na kushirikiana nasi kuleta teknolojia inayoongeza uwezo wetu wa kuwahudumia wanachama vizuri zaidi.”

Uzinduzi wa TRA SACCOS PESACARD pia unaonesha umuhimu wa ushirikiano kati ya benki za biashara na taasisi za kifedha zinazomilikiwa na wanachama katika kuongeza ujumuishi wa kifedha. Kwa kuunganisha ukaribu wa TRA SACCOS na wanachama wake pamoja na teknolojia, miundombinu na uwezo wa malipo wa Benki ya CRDB, ushirikiano huo unalenga kuunda mazingira rahisi zaidi ya kupata huduma za kisasa za kifedha.

Kwa Benki ya CRDB, hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuendelea kuwekeza katika teknolojia na kubuni suluhisho zinazoboresha uzoefu wa wateja na kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha. Benki hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na TRA SACCOS pamoja na taasisi nyingine katika sekta binafsi na umma kuleta mageuzi ya kidigitali na katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

WADAU WA SEKTA YA AFYA ZAIDI YA 3000 KUSHIRIKi MKUTANO WA KIMATAIFA WA HUDUMA ZA AFYA YA MSINGI

September 06, 2026 Add Comment




Na: OWM – TAMISEMI, Dodoma


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe,  amesema zaidi ya wadau wa sekta ya afya 3000 kutoka nchi mbalimbali Duniani  watashiriki katika Mkutano wa pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi (IPHCC), jijini Arusha. 



Prof. Shemdoe  amesema hayo mapema leo Septemba 06, 2026 akiwa jijini Dodoma, kabla ya kuelekea Arusha na kuwakaribisha washiriki hao kwenye mkutano huo utakaofanyika kuanzia tarehe 9 hadi 11 Septemba, 2026  katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).


Prof. Shemdoe amesema, yeye binafsi atashiriki katika mkutano huo wenye tija katika kuboresha utoaji wa huduma za afya msingi nchini na afrika kwa ujumla.


Prof. Shemdoe amesema mkutano huo umelenga kutoa uzoefu wa Tanzania katika uboreshaji wa huduma za afya ya msingi, ikiwamo afua zilizopelekea kupunguza vifo vya akina mama na watoto ambapo Tanzania kupitia jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ni kinara katika eneo hilo barani Afika.


Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, mkutano huo umelenga pia kubadilishana uzoefu wa maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika katika huduma za afya ya msingi duniani pamoja na kuandaa mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma za afya ya msingi ili kufikia malengo ya kitaifa na Kimataifa, ikiwamo upatikanaji wa Huduma za Afya kwa wote na malengo endelevu ya maendeleo.


Mkutano huo wa kihistoria utawakutanisha washiriki zaidi ya 3000 kutoka Tanzania na mataifa mengine duniani wakiwamo; wataalam wa afya wanaofanya kazi ya kutoa huduma za afya ya msingi, watunga sera, wadau wa maendeleo, watafiti, wahadhiri, wanafunzi, asasi za kiraia na sekta binafsi, ambapo washiriki hao wamejisajiri kupitia tovuti ya   https://iphcconference.tamisemi.go.tz .

KILWA YATAKA UWEKEZAJI ZAIDI KATIKA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

September 06, 2026 Add Comment




Kilwa, Lindi.


Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilwa, Yusuph Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa Serikali kuendelea kuwekeza katika nishati safi ya kupikia ili kuongeza upatikanaji wa nishati hiyo kwa wananchi na kuharakisha utekelezaji wa ajenda ya Taifa ya nishati safi ya kupikia.


Mwinyi alitoa kauli hiyo wakati wa ziara ya ujumbe wa Wizara ya Nishati uliotembelea mradi wa nishati safi ya kupikia unaotumia teknolojia ya haidrojeni ya kijani katika Wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi.


Amesema uwekezaji katika nishati safi ya kupikia ni muhimu kutokana na nafasi ya nishati hiyo katika maisha ya kila siku ya wananchi, akieleza kuwa Serikali inapaswa kuendelea kuweka mazingira yatakayowezesha teknolojia mbalimbali za nishati safi kupatikana na kutumika kwa upana zaidi.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Nolasco Mlay, amesema Serikali inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuendeleza teknolojia za nishati safi ya kupikia, ikiwemo teknolojia bunifu kama haidrojeni ya kijani, ili kuongeza wigo wa chaguo la nishati kwa wananchi.


Mlay amesema kuendelezwa kwa teknolojia hizo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuhakikisha wananchi wanapata nishati safi ya kupikia inayokidhi mahitaji yao, huku akisisitiza umuhimu wa ubunifu, uwekezaji na ushiriki wa sekta binafsi katika kufanikisha azma hiyo.


Amesema teknolojia ya haidrojeni ya kijani inaonesha fursa katika safari ya Taifa ya kuelekea kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia, hivyo ni muhimu kuendelea kufanya tathmini na kutoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi yake salama na yenye ufanisi.


Mlay amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, wataalamu na wananchi ni muhimu katika kuongeza kasi ya upatikanaji na matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, sambamba na kufikia lengo la asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

UMEME WA UHAKIKA MIGODINI WACHANGIA ZAIDI YA SHILINGI BILIONilI 340 KWA MWAKA

September 06, 2026 Add Comment



Dodoma, Septemba 3, 2026.


Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashimu Komba, amesema upatikanaji wa umeme wa uhakika katika migodi una mchango mkubwa kwa uchumi wa Taifa, ambapo sekta hiyo huchangia zaidi ya Shilingi bilioni 340 kwa mwaka kupitia mrabaha, kodi na tozo mbalimbali.


Mhe. Komba ameyasema hayo Septemba 3, 2026, jijini Dodoma, katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya Mpomvu–GGM yenye msongo wa kilovoti 220 (220kV), pamoja na Kituo cha Kupoza Umeme katika eneo la GGM, mkoani Geita. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi.


Ameipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa juhudi za kuhakikisha umeme unafikishwa katika maeneo ya shughuli za madini, ikiwemo migodi mikubwa kama Geita Gold Mining (GGM), hatua inayosaidia kuongeza uzalishaji na kuchochea ukuaji wa sekta ya madini nchini.

“Tunawapongeza TANESCO kwa kuhakikisha umeme unafika katika maeneo ya migodi mikubwa kama GGM. Umeme wa uhakika ni muhimu katika kuhakikisha shughuli za uzalishaji zinaendelea bila vikwazo na hivyo kuongeza mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa Taifa,” amesema.


Aidha, Mhe. Komba amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi za kuendelea kusogeza huduma ya umeme kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.


Amesema Mkoa wa Geita umefikia hatua ya vijiji vyote 474 kuwa na umeme, huku mkandarasi Central Electrical Installation akiendelea na kazi ya kupeleka umeme katika vitongoji 528 vya mkoa huo.


Katika hatua nyingine, Mhe. Komba amewaalika Watanzania, wachimbaji wadogo, wa kati na wakubwa pamoja na wawekezaji kushiriki katika maonesho ya madini yanayotarajiwa kufanyika Septemba 23, 2026, mkoani Geita.


Amesema maonesho hayo yatatoa fursa kwa wananchi na wadau mbalimbali kujionea fursa zinazotokana na rasilimali za madini zilizopo mkoani Geita na nchini kwa ujumla.


Mhe. Komba pia ameahidi kuwa uongozi wa Mkoa na Wilaya ya Geita utatoa ushirikiano wa karibu kwa mkandarasi pamoja na watumishi wa TANESCO ili kuhakikisha utekelezaji wa mradi wa Mpomvu–GGM unafanyika kwa wakati na bila vikwazo visivyo vya lazima.


Amesema ushirikiano huo ni muhimu katika kuhakikisha mradi unakamilika kwa ufanisi na kuchangia upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa shughuli za uchimbaji na uzalishaji katika sekta ya madini.

BARRICK KIOO CHA UFUNGAJI MIGODI UNAOZINGATIA VIWANGO VYA KIMATAIFA NCHINI

September 06, 2026 Add Comment

    


Sehemu ya wajumbe wa Tawala za Mitaa Tanzania wakiwa kwenye maeneo ya Mgodi wa Barrick Buzwagi.
Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) kutoka Njombe wakiwa kwenye ziara ya siku moja Mkoani Shinyanga kwenye mgodi wa Barrick Buzwagi ambao upo kwenye hatua za ufungaji.

TUME YA TAIFA YA UNESCO YASHIRIKI UKUSANYAJI WA MAONI KUHUSU MPANGO WA JUMLA WA USIMAMIZI WA HIFADHI HAI NA MWANADAMU YA RUMAKI

September 06, 2026 Add Comment

Tume ya Taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeshiriki katika zoezi la ukusanyaji wa maoni ya awali ya wadau kuhusu maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi (General Management Plan – GMP) wa Hifadhi Hai na Mwanadamu ya Rufiji–Mafia–Kibiti–Kilwa (RUMAKI), ikiwa ni hatua muhimu katika kuweka msingi wa usimamizi endelevu na shirikishi wa eneo hilo.

Zoezi hilo limejikita katika kupata maoni, uzoefu na mapendekezo ya wadau kuhusu namna bora ya kuimarisha uhifadhi wa mazingira na bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali za asili pamoja na maendeleo ya jamii zinazozunguka na kutegemea rasilimali za RUMAKI.

RUMAKI, inayojumuisha Rufiji, Mafia, Kibiti na Kilwa, ni miongoni mwa Hifadhi Hai zilizotambuliwa na UNESCO na kuingizwa katika Mtandao wa Dunia wa Hifadhi Hai (World Network of Biosphere Reserves – WNBR) mwaka 2023, chini ya Mpango wa UNESCO wa Mwanadamu na Hifadhi Hai (Man and the Biosphere Programme – MAB).

Hifadhi hiyo ina mifumo mbalimbali muhimu ya ikolojia ya pwani na bahari, ikiwemo misitu ya mikoko, miamba ya matumbawe na nyasi bahari. Mifumo hiyo ina mchango mkubwa katika kuhifadhi bioanuai, kulinda mazingira ya pwani, kusaidia shughuli za kiuchumi za jamii na kuongeza uwezo wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Maoni ya wadau yaweka msingi wa mpango

Ukusanyaji wa maoni ya awali ni sehemu muhimu ya mchakato wa kuandaa Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa RUMAKI. Kupitia mchakato huo, wadau wanapata nafasi ya kueleza hali halisi ya eneo, changamoto zinazokabili uhifadhi na matumizi ya rasilimali, pamoja na fursa zinazoweza kuendelezwa kwa manufaa ya jamii na mazingira.

Miongoni mwa wadau wanaohusishwa katika mchakato huo ni viongozi wa Serikali za Mitaa na vijiji, taasisi za Serikali, jamii zinazozunguka Hifadhi Hai, wavuvi, Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe (Beach Management Units – BMUs), taasisi za utafiti, wataalamu na wadau wengine wa maendeleo.

Ushirikishwaji wa wadau katika hatua hii unalenga kuhakikisha kuwa mpango utakaotengenezwa unazingatia mahitaji ya uhifadhi pamoja na hali halisi ya maisha ya jamii zinazotegemea rasilimali za eneo hilo.

Kuunganisha uhifadhi na maendeleo ya jamii

Dhana ya Hifadhi Hai na Mwanadamu inalenga kuweka uwiano kati ya uhifadhi wa bioanuai na maendeleo ya jamii. Kwa mtazamo huo, uhifadhi wa RUMAKI unahitaji kwenda sambamba na matumizi endelevu ya rasilimali zinazosaidia maisha ya wananchi, huku ukihakikisha kuwa rasilimali hizo zinalindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Katika maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi, suala la mgawanyo wa maeneo ya Hifadhi Hai linatarajiwa kuwa miongoni mwa maeneo muhimu ya kuzingatiwa. Hii inahusisha maeneo ya msingi ya uhifadhi (Core Areas), maeneo yanayozunguka maeneo hayo (Buffer Zones) na maeneo ya mpito (Transition Areas), kwa kuzingatia malengo ya uhifadhi na maendeleo endelevu.

Mpangilio huo unalenga kuweka uelekeo unaoeleweka kuhusu shughuli zinazoweza kufanyika katika maeneo mbalimbali, namna ya kulinda maeneo yenye umuhimu mkubwa wa kiikolojia na jinsi ya kuwezesha shughuli za maendeleo zinazozingatia mazingira.

Nafasi ya Tume ya Taifa ya UNESCO

Ushiriki wa Tume ya Taifa ya UNESCO katika zoezi hili unaendana na nafasi yake katika kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa programu na shughuli za UNESCO nchini Tanzania, kwa kushirikiana na taasisi za Serikali na wadau husika.

Kupitia Mpango wa UNESCO wa Mwanadamu na Hifadhi Hai (MAB), Hifadhi Hai hutumika kama maeneo ya kujifunza na kuonesha namna uhifadhi wa bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali, maendeleo ya jamii, utafiti, elimu na ufuatiliaji vinavyoweza kuunganishwa katika eneo moja.

Kwa upande wa Tanzania, utekelezaji wa dhana hiyo katika RUMAKI unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya taasisi za Serikali, mamlaka za Serikali za Mitaa, jamii, wataalamu, taasisi za utafiti na wadau wengine wanaohusika na uhifadhi na maendeleo.

Hatua kuelekea usimamizi endelevu wa RUMAKI

Maoni yatakayokusanywa katika hatua hii yatatoa msingi wa kuendelea na mchakato wa kuandaa Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa RUMAKI. Mpango huo unatarajiwa kusaidia kuweka mwelekeo wa pamoja katika uhifadhi wa bioanuai, matumizi endelevu ya rasilimali, maendeleo ya jamii, utafiti, elimu na ufuatiliaji wa mazingira.

Kwa kuwa RUMAKI inahusisha maeneo ya nchi kavu, pwani na bahari pamoja na jamii zinazotegemea rasilimali hizo, usimamizi wake unahitaji mtazamo unaounganisha mahitaji ya uhifadhi na maendeleo.

Ushiriki wa wadau katika hatua za awali, hivyo, ni muhimu katika kujenga uelewa wa pamoja na kuweka msingi wa mpango unaozingatia mazingira halisi ya RUMAKI.

Maandalizi ya Mpango wa Jumla wa Usimamizi wa Hifadhi Hai na Mwanadamu ya RUMAKI yanaashiria hatua muhimu katika kuimarisha utekelezaji wa dhana ya UNESCO ya Mwanadamu na Hifadhi Hai, kwa lengo la kuhakikisha kuwa uhifadhi wa mazingira na bioanuai unaenda sambamba na maendeleo endelevu na ustawi wa jamii.

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA NHIF KUELEKEA AFCON

SERIKALI YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA NHIF KUELEKEA AFCON

September 05, 2026 Add Comment

Serikali imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kujipanga kikamilifu katika maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, hususan katika kuhakikisha wageni watakaofika nchini wanapata huduma bora za matibabu bila vikwazo.

Agizo hilo limetolewa l na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Florence Samizi (Mb.) ambaye amesema NHIF ina jukumu muhimu la kuratibu suala la bima ya afya wakati wa mashindano hayo ili kuhakikisha wageni wanapata huduma za matibabu kwa urahisi pindi wanapohitaji huduma hizo.

“Tuwape uhakika wa huduma bora ili waone fahari kuwapo hapa nchini katika kipindi chote cha mashindano hayo,” amesema Dkt. Samizi.

Amesema maandalizi ya huduma za matibabu yanapaswa kuzingatia pia huduma za dharura pamoja na huduma maalum, ikiwemo za moyo na mifupa, ili kukidhi mahitaji mbalimbali ya afya yatakayoweza kujitokeza wakati wa mashindano.

Aidha alidokeza kuwa tayari Wataalamu kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) wamekagua Vituo vya kutolea huduma kwa alengo la kujiridhisha na wamefurahishwa na utayari unaoonyeshwa katika maandalizi ya huduma za matibabu jambo linaloonesha kuwa Tanzania inajiandaa kuhakikisha AFCON 2027 inafanyika katika mazingira salama na yenye huduma bora.

Ameitaka NHIF kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya, vituo vya kutolea huduma na wadau wengine kuhakikisha mfumo wa huduma za matibabu wakati wa mashindano hayo unakuwa imara, unaopatikana kwa wakati na unaokidhi viwango vinavyohitajika.

Akizungumzia hilo Mkurugenzi Mkuu waa NHIF, Dkt. Irene Isaka alisema kuwa tayari Mfuko umeshajipanga na umeandaa kifurushi maalumu kwa ajili ya wageni wote watakaokuja nchini kwa ajili ya mashindano hayo.

“Tayari tumejipanga na tuna kifurushi ambacho tutakileta Wizarani ili tupate baraka ya Wizara hivyo tunashukuru sana kwa maelekezo haya ambayo yanaboresha na kuhakikisha tunajipanga vyema,” alisema Dkt. Isaka. ‎

NAIBU WAZIRI AVUTIWA NA USAJILI WANACHAMA KIDIGITALI, AITAKA NHIF KUONGEZA KASI YA BIMA YA AFYA KWA WOTE

NAIBU WAZIRI AVUTIWA NA USAJILI WANACHAMA KIDIGITALI, AITAKA NHIF KUONGEZA KASI YA BIMA YA AFYA KWA WOTE

September 05, 2026 Add Comment

‎NAIBU Waziri wa Afya, Mhe Dkt. Florence George Samizi (Mb), amelipongeza Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kuwa moja ya mabaraza bora nchini. Amelitaka baraza kuhakikisha ajenda ya Bima ya Afya kwa wote inawafikia wananchi wengi zaidi.

Nimefurahi kusikia kwamba katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026 Mfuko umeweza kufikia 10.7% ya Wananchi toka 8% ya wananchi iliyodumu kwa takriban miaka 10. Pamoja na pongezi hizo Mh. NAIBU WAZIRI ameutaka Mfuko kutumia TEHAMA na kusajili wanachama wengi zaidi ili kutimiza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwafikishia wananchi wote huduma za bima ya afya. Hii itasaidia wananchi kuondokana na umaskini pale wanapopata maradhi. ‎Dkt. Samizi ametoa maelekezo Hayo wakati wa mkutano wa nne wa wa Baraza la 4 wafanyakazi NHIF, Jijini Arusha, na kusisistiza menejimenti ya wafanyakazi wa NHIF kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia uadilifu, weledi na uwajibikaji, huku wakisikiliza na kutatua kwa wakati kero za wananchi. ‎Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya. Kutoa huduma bora na kuwa na mfumo wa kupokea mrejesho toka kwa wananchi. ‎Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa NHIF, Dkt. Samizi amesema ni muhimu mfuko huo kuonesha mafanikio yaliyopatikana. Kuwepo kwa NHIF kumesaidia kuboresha huduma za Afya kwa kulipa madai na kutoa mikopo kwa vituo vya afya. Ni vema wanachi wakajulishwa hatua kubwa iliyofikiwa katika huduma za Afya na mchango wa NHIFkatika Sekta hii muhimu. Mlianza na vituo vichache sana mwaka 2001 hivi sasa yaani mwaka wa Fedha 2025/26 mmesajili zaidi ya vituo 10,600 nchi nzima. Ni vema kuonesha namna mlivyokabiliana na changamoto za wakati ule na namna zilivyowasaidia kuboresha Mfuko katika utoaji wa huduma. ‎Amesema mafanikio hayo yanadhihirishwa na kujituma, ushirikiano, umoja na mshikamano miongoni mwa watumishi wa NHIF ili kufikia malengo ya mfuko kwa lengo la kutekeleza jitihada za Serikali za kuhakikisha wananchi wanapata bima ya Afya. ‎Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Dkt. Irene Isaka, ameeleza mafanikio yaliyopatikana ikiwa ni pamoja na kupunguza muda wa kilipa madai toka zaidi ya siku 90 hadi wastan wa siku 50 kwa mwaka wa Fedha 2025/2026. Vile vile alieleza kwamba Mfuko umeendelea kuimarika ambapo ziada imeongezeka kwa 57% Mfuko umepunguza matumizi kwa asilimia13% na uwekezaji umeongezeka kwa 106%.

Hii imewezesha Mfuko kuendeleza kifurushi cha wanafunzi, Toto Afya. Mfuko kusajili kifurushi cha tarangire, Mikumi, Ngorongoro, Serengeti Tanzanite na kifurushi cha vikundi yaani Umoja Afya ambacho ni sh. 60, 000 kwa matibabu ya mwaka mzima.

Vile vile alielezea mikakati inayotekelezwa na mfuko huo katika kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na matumizi ya TEHAMA kwenye usajili, uchakataji madai na kupambana na udanganyifu. Mfuko pia unashirikisha Sekta Binafsi katika usajili wa wanachama na katika huduma za matibabu. ‎Mwakilishi wa chama Cha wafanyakazi TUGHE, Bw.Paul wamepongeza baraza Hilo kuzingati misingi ya Kazi stahiki za wafanyakazi kwenye taasisi hiyo. ‎Baadhi ya wafanyakazi walioshiriki semina elekezi ya siku mbili wamesema wamepata maarifa na mwelekeo mpya ambao utawasaidia kuboresha utendaji wao wa kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Bima ya Afya kwa wote! Jiunge sasa!