HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

KAMATI YA BUNGE YAAGIZA UDHIBITI WA USAHIHI WA VIPIMO UONGEZEWE NGUVU

KAMATI YA BUNGE YAAGIZA UDHIBITI WA USAHIHI WA VIPIMO UONGEZEWE NGUVU

March 10, 2026 Add Comment

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeiagiza Wakala wa Vipimo (WMA) kuongeza nguvu katika kudhibiti usahihi wa vipimo ili kuhakikisha huduma wanazopata wananchi zinaendana na thamani halisi ya fedha wanayotumia

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), Wakati Kamati hiyo ili pokea Taarifa ya Wizara ya Viwanda na Biashara kuhusu utekelezaji ya Miradi ya Maendeleo kwa mwaka 2025/26 kutoka Wakala wa Vipimo (WMA) na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Taasisi zake yake Machi 10, 2026 , Bungeni jijini Dodoma.

Mwanyika amesisitiza kuwa vita dhidi ya lumbesa haipaswi kuachiwa WMA pekee, bali inahitaji nguvu ya pamoja kati ya Halmashauri, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na Serikali Kuu ili kufanya oparesheni za nchi nzima.

Nao, Wajumbe wa Kamati hiyo walizipongeza WMA na CBE kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali na kutoa maoni na mapendekezo mbalimbali yaliyolenga kuboresha utekelezaji wa Miradi hiyo kwa ufanisi.

Naye, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo (Mb), alifafanua kuwa msingi wa Tanzania ya Viwanda ni kilimo ambapo WMA inatekeleza jukumu la kumlinda mkulima, huku akibainisha kuwa idadi kubwa ya watumishi wa Wakala huyo wanazalishwa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), jambo linaloashiria kuwepo kwa uhusiano mkubwa wa kikazi baina ya taasisi hizo mbili.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bw. Alban Kihulla, amesema kuwa taasisi hiyo, kwa wakishirikiana na mamlaka nyingine za Serikali pamoja na sekta binafsi, wanaenda kupata suluhisho la kudumu la malalamiko ya wananchi ambayo yamekuwa yakiwasilishwa kwa muda mrefu kuhusu ukosefu wa usahihi wa vipimo katika maeneo mbalimbali ikiwemo lumbesa.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Prof. Edda Lwoga amesema miradi ya majengo inayojengwa kwenye Kampasi mbalimbali za Chuo hicho mara itakapokamilika itaboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza udahili wa wanafunzi katika chuo hicho.

WIZARA YA NISHATI YAPOKEA TRIL.1 ZA MIRADI YA MAENDELEO

March 10, 2026 Add Comment




 ðŸ“ŒNi asilimia 61 ya bajeti ya 2025/26


Na Mwandishi Wetu, Dodoma


WIZARA ya Nishati imepokea Sh. trilioni 1.150 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, sawa na asilimia 61 ya bajeti ya maendeleo iliyoidhinishwa kwa mwaka wa fedha 2025/26.


Taarifa hiyo imetolewa Machi 10, 2026 na Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya sekta ya nishati kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Subira Mgalu, katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma.

Mhe.Ndejembi amesema katika mwaka wa fedha 2025/26 wizara imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayolenga kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini.

Amesema katika fedha zilizopokelewa hadi sasa, Sh. bilioni 410.04 ni fedha za ndani na Sh. bilioni 740.30 ni fedha za nje ambazo zimeendelea kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya sekta ya nishati.

Ameongeza kuwa miradi hiyo inajumuisha upelekaji wa umeme vijijini na vitongojini, utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi asilia, ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji na uhifadhi wa bidhaa za mafuta ya petroli pamoja na kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Kwa mujibu wa Ndejembi, katika mwaka wa fedha 2025/26 Wizara ya Nishati iliidhinishiwa kutumia jumla ya Sh trilioni 1.965, ambapo Sh trilioni 1.886 sawa na asilimia 95.97 zilitengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo huku Sh bilioni 79.23 sawa na asilimia 4.03 zikiwa kwa matumizi ya kawaida.

Amefafanua kuwa kati ya fedha za maendeleo zilizoidhinishwa, Sh trilioni 1.466 ni fedha za ndani na Sh bilioni 420.49 ni fedha za nje.

Ndejembi ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa miongozo na maelekezo ambayo imekuwa ikitoa na kuchangia mafanikio katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Amesisitiza kuwa wizara itaendelea kupokea ushauri na maoni ya kamati hiyo pamoja na kutoa ushirikiano unaostahili ili kuimarisha maendeleo ya sekta ya nishati nchini.



WALAJI KUNUFAIKA NA UFUATILIAJI WA FCC KWENYE MIKATABA YA UPANDE MMOJA

March 10, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu
Dar es Salaam, Machi 10, 2026. Tume ya Ushindani (FCC) imesema itaendelea kusimamia kwa karibu haki za walaji kwa taasisi na kampuni zinazotumia mikataba iliyoandaliwa kwa upande mmoja, ili kuhakikisha watumiaji wa huduma na bidhaa hawapati hasara kutokana na mikataba hiyo.
Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, alipokuwa akizungumza katika semina ya wadau kutoka taasisi na kampuni zinazotumia mikataba ya upande mmoja, iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Ngasongwa alisema FCC inaendelea kufuatilia kwa karibu mikataba ya aina hiyo ili kuhakikisha haikiuki haki za walaji katika soko. Alifafanua kuwa mikataba ya upande mmoja hutumiwa sana na taasisi mbalimbali kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakati, lakini ni muhimu iwe chini ya uangalizi ili kuepuka matumizi yanayoweza kuwa kinyume na sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.
Alisema semina hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa utoaji wa elimu kwa wadau kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mlaji Duniani, yanayolenga kuongeza uelewa kuhusu haki na wajibu wa walaji pamoja na watoa huduma.
“Ninatambua kuwa mikataba inayoandaliwa kwa upande mmoja ina faida katika kurahisisha utoaji wa huduma kwa wakati. Hata hivyo, FCC ina jukumu la kuifuatilia kwa karibu, kwani bila uangalizi kunaweza kuwa na mambo yanayofanyika kinyume na maslahi ya walaji katika soko,” alisema Ngasongwa.
Aliongeza kuwa hata pale taasisi zinapotaka kuunganisha huduma au mikataba yao, ni muhimu kufanya tathmini ya kina ili kubaini kama kuna vipengele vinavyoweza kukiuka masharti ya ushindani au kuathiri ubora wa huduma kwa walaji.
Ngasongwa alisisitiza kuwa kila mtu ni mlaji kwa namna moja au nyingine, hivyo ni muhimu kuhakikisha thamani ya fedha inayotolewa na mteja inaendana na ubora wa huduma au bidhaa anayopata. Alisema hali hiyo pia husaidia kujenga uaminifu kati ya watoa huduma na walaji.
Aidha, alisema FCC itaendelea kukutana na makundi mbalimbali ya wadau kwa lengo la kuwapa uelewa mpana kuhusu majukumu ya taasisi hiyo na umuhimu wa kuzingatia sheria za ushindani na ulinzi wa mlaji.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA), Tusekelege Mwaikasu, alisema semina hiyo ni muhimu kwa taasisi za kifedha kwani itawasaidia kuboresha utoaji wa huduma kwa walaji kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika.
Alisema benki, kupitia umoja wao, zimekuwa zikitekeleza kampeni ya “Niko Fiti”, inayolenga kuhakikisha huduma za kifedha zinatolewa kwa ubora na kwa kuzingatia mahitaji ya walaji.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindqni Ushindani Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa akizungumza wakati akifungua Semina kwa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa upande mmoja jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Udhibiti wa Mienendo ya Bidhaa inayokatazwa na Sheria ya Ushindani FCC, Bi.Magdalena Utouh  akizunguza wakati wa kuhitimisha semina ya wadau wa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa na upande mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa FCC,Bi. Roberta Feruzi akitoa maelezo kuhusiana na Semina ya wadau wa Taasisi na Kampuni zenye mikataba iliyoandaliwa upande mmoja jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA ) Bi.Tusekelege Mwaikasu akitoa neno kwa niaba ya wadau katika mkutano na FCC ,jijini Dar es Salaam. Mkutano ukiendelea Kaimu Mkurugenzi Mkurugenzi Mkuu wa FCC Khadija Ngasongwa akiwa katika matukio picha za za pamoja makundi mbalimbali.

SHULE 13 TEMEKE KUANZA KUPIKA KWA UMEME

March 10, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu


GHARAMA za kupika chakula cha wanafunzi katika shule 13 za msingi Wilaya ya Temeke, mkoani Dar es Salaam, zinatarajiwa kupungua kwa kiasi kikubwa kufuatia shule hizo kuanza kutumia nishati ya umeme kupikia badala ya kuni.


Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa majiko ya umeme katika taasisi za elimu ya msingi unaosimamiwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Nishati, Idara ya Elimu ya Awali na Msingi ya Wilaya ya Temeke pamoja na Shirika la Chakula Duniani (WFP).

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo katika Shule ya Msingi Kibasila, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Halima Rukumbwe, amesema awali walikuwa wanatumia kati ya Sh.20,000 hadi Sh.25,000 kwa siku kupika chakula cha wanafunzi 450, ikiwemo uji na chai ya asubuhi pamoja na chakula cha mchana cha wali na maharagwe.

Amesema baada ya kuanza kutumia majiko ya umeme, gharama hizo zimepungua na kufikia kati ya Sh.8,000 hadi Sh.10,000 kwa siku, huku kiasi hicho kikijumuisha pia matumizi ya mota ya kupandisha maji kwa shughuli mbalimbali za shule.

“Mbali na kupunguza gharama, wapishi sasa wanapika chakula kwa muda mfupi zaidi na katika mazingira safi,” amesema Rukumbwe.


Ameongeza kuwa matumizi ya nishati hiyo yamechangia pia kupungua kwa utoro wa wanafunzi, kwani chakula kinapatikana kwa wakati na hivyo kuwahamasisha wanafunzi kuhudhuria masomo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Omar Khalifa amesema mradi huo katika awamu ya kwanza unatekelezwa katika mikoa minne ambayo ni Dar es Salaam (Wilaya ya Temeke), Dodoma (Wilaya ya Dodoma Mjini), Tabora (Wilaya ya Tabora Mjini) na Kigoma.

Naye, Mshauri wa Chakula kutoka Shirika la Chakula Duniani (WFP), Dkt. Geoffrey Ngegwa amesema katika Mkoa wa Dar es Salaam mradi huo unatekelezwa katika shule 13 za Wilaya ya Temeke.

Amesema mbali na Shule ya Msingi Kibasila ambayo tayari imeanza kutumia mfumo huo, shule nyingine zinazoendelea kukamilishiwa miundombinu ni Likwati, Madenge, Umoja, Alhasan Mwinyi, Unubini, Lioness Miburani, Nzasa, Ponde, Wailes, Chemchem na Charambe.

Ameongeza kuwa miundombinu katika shule hizo tayari imekamilika na kinachosubiriwa kwa sasa ni ufungaji wa masufuria ya kisasa ya kupikia (pressure cooker) unaotarajiwa kukamilika mwishoni mwa Machi 2026.


&&&