HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

  WANAFUNZI 246,197 WALIOPANGIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO WANAPASWA KURIPOTI SHULENI JULAI 04, 2026 – PROF. SHEMDOE

WANAFUNZI 246,197 WALIOPANGIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO WANAPASWA KURIPOTI SHULENI JULAI 04, 2026 – PROF. SHEMDOE

June 01, 2026 Add Comment





Na OWM – TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 246,197 wakiwemo wasichana 114,102 na wavulana 132,095 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2026 wanatakiwa kuripoti shuleni kuanzia Julai 04, 2026 hadi Julai 31, 2026 kwakuwa muhula wa kwanza wa masomo utaanza Julai 06, 2026.

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Juni 01, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi Ndogo ya Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Magogoni Jijini Dar es Salaam, wakati akitoa taarifa kwa umma kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi kwa mwaka 2026.

“Wanafunzi 172,114 sawa na asilimia 69.9 wakiwemo wasichana 85,987 na wavulana 86,127 wenye sifa wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika shule za sekondari za Serikali 856 zikiwemo shule za bweni 825, kutwa 25 na kutwa na bweni sita (06),” amefafanua Prof. Shemdoe.

Aidha, Prof. Shemdoe amesema jumla ya wanafunzi 74,083 sawa na asilimia 30.1 wakiwemo wasichana 28,115 na wavulana 45,968 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.

“Wanafunzi 3,144 wakiwemo wasichana 1,170 na wavulana 1,974 wamechaguliwa kujiunga na fani mbalimbali katika vyuo 04 vya elimu ya ufundi, vyuo hivyo ni Chuo cha Ufundi cha Arusha (ATC), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) na Chuo cha Maendeleo ya Maji (WMDI),” ameeleza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amesisitiza kwamba, uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi umefanyika kwa kuzingatia ufaulu na nafasi zilizopo katika shule; hivyo, hakutakuwa na fursa ya kufanya mabadiliko yoyote ya Shule kutokana na ukosefu wa nafasi.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi zilizotumika kujenga miundombinu bora ya shule za kidato cha tano na vyuo vya kati ambayo itatumika kuwahudumia wanafunzi 246,197 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya elimu ya ufundi mwaka 2026.   


CCM TANGA YAKABIDHI MILIONI 500 KUKAMILISHA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI WAKE

June 01, 2026 Add Comment

 


>Yalenga Kuimarisha Ufanisi wa Chama

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimeongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wake wa ujenzi wa nyumba 36 za watumishi baada ya Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo, Rajab Abdulrahman, kukabidhi shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo unaotekelezwa katika wilaya tisa za mkoa huo.

Fedha hizo zilikabidhiwa  kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, katika hatua inayodhihirisha dhamira ya chama ya kuboresha mazingira ya kazi na makazi kwa viongozi wake wa ngazi za wilaya.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Rajab alisema mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu na kwamba utakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha utendaji wa watumishi pamoja na shughuli za chama katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

Alieleza kuwa mradi huo una thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.5, huku fedha zote zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wake zikiwa tayari zimepatikana kupitia michango ya wanachama, viongozi na wadau mbalimbali wa chama.

"Mradi huu unagharimu jumla ya shilingi bilioni 2, milioni 500 na laki 250. Fedha hizi zimepatikana kupitia michango mbalimbali ikiwemo milioni 56 zilizotolewa awali, milioni 10 kutoka kwa MNEC pamoja na michango iliyokusanywa kutoka wilaya zote za mkoa," alisema Rajab.

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa kukamilika kwa nyumba hizo kutasaidia kutatua changamoto za makazi kwa baadhi ya viongozi wa chama katika ngazi ya wilaya, jambo litakaloongeza utulivu wa kazi, uwajibikaji na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Alisema nyumba hizo si tu kwamba zitakuwa makazi ya viongozi, bali pia ni uwekezaji wa muda mrefu wa chama katika kujenga taasisi imara yenye uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kuendelea kuwahudumia wanachama wake.

"Tunajenga misingi ya chama kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Viongozi wanaweza kubadilika, lakini miundombinu tunayojenga leo itaendelea kulitumikia chama kwa miaka mingi ijayo," alisisitiza.

Rajab aliongeza kuwa ujenzi wa chama ni jukumu endelevu linalohitaji mshikamano wa wanachama wote, akisisitiza kuwa maendeleo ya chama hayawezi kupatikana bila ushiriki wa pamoja wa wanachama wake.

Kutokana na hilo, aliwataka wana-CCM wa Mkoa wa Tanga kuendelea kuchangia kwa hali na mali, kutumia elimu na uzoefu wao pamoja na nguvu kazi katika kukiimarisha chama.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, alisema mradi huo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa chama wa kuimarisha utendaji wake katika ngazi za wilaya kwa kuhakikisha viongozi wanapata mazingira bora ya kazi na makazi.

Alifafanua kuwa kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo zitatumika na viongozi muhimu wa chama na jumuiya zake.

"Kila wilaya imepangiwa kujenga nyumba nne ambazo ni nyumba ya Katibu wa CCM wa Wilaya, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Vijana, nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi pamoja na nyumba ya Katibu wa UWT," alisema Kizigo.

Alieleza kuwa uwepo wa nyumba hizo utasaidia kupunguza gharama za upangaji wa makazi, kuimarisha upatikanaji wa viongozi katika maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za chama na jumuiya zake.

Kwa mujibu wa Kizigo, kukamilika kwa mradi huo kutakuwa hatua muhimu katika kuijengea CCM Mkoa wa Tanga miundombinu imara itakayosaidia kuendeleza shughuli zake za kisiasa, kiutawala na kijamii kwa ufanisi zaidi katika miaka ijayo.

TANZANIA KUWA NA MKAKATI MAALUM WA MAWASILIANO WAKATI WA MLIPUKO WA MAGONJWA YA MIFUGO

TANZANIA KUWA NA MKAKATI MAALUM WA MAWASILIANO WAKATI WA MLIPUKO WA MAGONJWA YA MIFUGO

June 01, 2026 Add Comment

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Benezeth Lutege, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness K. Meena. Warsha hiyo imefanyika leo Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha.

Mkurugenzi Msaidizi wa Epidemiolojia na Magonjwa ya Mifugo Yanayovuka Mipaka (TADs) akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Habari II wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Chiku Makwai, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Afisa Sheria I wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Denis Ukaka, akitoa mchango wake katika majadiliano ya Warsha ya Uandaaji wa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, iliyofanyika leo Juni 1, 2026, jijini Arusha.

Na Chiku Makwai – ARUSHA

Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, limeanza mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa nchi katika kuzuia, kudhibiti na kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo.

Warsha ya kuandaa rasimu hiyo imefunguliwa leo, Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Agness K. Meena.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Dkt. Lutege amesema mawasiliano yenye ufanisi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti na kukabili milipuko ya magonjwa ya mifugo kwa kuwa huwezesha utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati kwa wadau wote wanaohusika.

Amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari na mwitikio wa haraka ili kuhakikisha magonjwa ya mifugo yanagunduliwa na kudhibitiwa mapema kabla hayajasababisha athari kubwa kwa uzalishaji, biashara ya mifugo na afya ya jamii.

“Mkakati huu utaweka msingi wa kuwa na mfumo mmoja wa kitaifa wa mawasiliano ya dharura utakaoongoza utoaji wa taarifa, ushirikishwaji wa wadau na usimamizi wa mawasiliano wakati wa matukio ya milipuko ya magonjwa ya mifugo,” amesema Dkt. Lutege.

Aidha, amebainisha kuwa magonjwa mbalimbali ya mifugo, ikiwemo Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever), yanahitaji uratibu madhubuti wa mawasiliano ili kuhakikisha wananchi na wadau wanapata taarifa sahihi zitakazowawezesha kuchukua hatua stahiki kwa wakati.

Warsha hiyo imewakutanisha wataalamu wa mifugo, afya ya wanyama, mawasiliano na wadau wengine kutoka taasisi za Serikali pamoja na mashirika ya kimataifa kwa lengo la kujadili mbinu bora za mawasiliano ya hatari, usimamizi wa taarifa za dharura na mikakati ya kuimarisha mwitikio wakati wa milipuko ya magonjwa.

Washiriki pia wanatarajiwa kujadili matumizi ya teknolojia za kisasa katika utoaji wa taarifa pamoja na namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya afya ya wanyama na afya ya binadamu kwa kuzingatia dhana ya Afya Moja (One Health).

Kupitia warsha hiyo, Tanzania inatarajia kuwa na mkakati madhubuti wa mawasiliano ya dharura utakaosaidia kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema, kuongeza mwitikio wa haraka wakati wa matukio ya dharura na kulinda ustawi wa mifugo sambamba na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa.

DKT. AMOS NUNGU: UBUNIFU NA TEKNOLOJIA NI NGUZO YA UCHUMI WA KILIMO

June 01, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Dunia la Haki Miliki (WIPO) kwa kushirikiana na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) pamoja na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, wamezindua mradi wa miezi 12 utakaotumia teknolojia zilizopo kwenye kanzidata za kimataifa za hakimiliki kuongeza thamani ya mazao, kupunguza gharama za uzalishaji na kuimarisha sekta za kilimo na ufugaji nchini.

BARRICK YAWEZESHA WANAFUNZI VYUO VIKUU KILIMANJARO KUPATIWA UTAMBUZI WA FURSA KUPITIA KONGAMANO LA AIESEC 2026

June 01, 2026 Add Comment
Meneja uzalishaji (Plant Manager wa Barrick Bulyanhulu), Raymond Zakayo akiongea na Wanafunzi katika kongamano hilo
Meneja uzalishaji (Plant Manager wa Barrick Bulyanhulu), Raymond Zakayo akiongea na Wanafunzi katika kongamano hilo
Baadhi ya wafanyakazi wa Barrick walioshiriki kongamano hilo katika picha ya pamoja
Watoa mada kutoka taasisi mbalimbali katika picha ya pamoja na viongozi wa AISEC

****

Wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Kilimanjaro wamepata fursa ya kupata elimu ya kuchangamkia fursa za kupata mafanikio kupitia elimu yao katika kongamano lililoandaliwa na taasisi ya AIESEC.

Katika kongamano hilo la aina yake, lililofanyika katika Chuo cha Ushirika Moshi kwa udhamini wa kampuni ya Barrick nchini, wanafunzi waliweza kujua kwa undani shughuli za Barrick nchini na makampuni mbalimbali makubwa ya kibiashara na jinsi ya kutafuta fursa ya kujiunga nayo pindi wamalizapo masomo yao ya elimu ya juu.

ITHIBATI YAWA KIGEZO KIKUU SAMIA KALAMU 2026

June 01, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

Waandishi wa Habari watakaoshiriki Tuzo za Uandishi wa Habari na Makala za Maendeleo (Samia Kalamu Awards - SKA) 2026 wamelazimika kukidhi sharti la kuwa na ithibati kutoka Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), hatua inayolenga kuimarisha weledi, uwajibikaji na ushindani wa haki katika taaluma hiyo.

Akizindua rasmi mchakato wa kupokea kazi za kushindanishwa, Jumapili Tarehe 31 Mei, 2026, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa SKA, Mha. Peter Mwasalyanda, amesema maandalizi ya mwaka huu yanazingatia maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kutambua mchango wa Waandishi wa Habari za maendeleo nchini.
Mwasalyanda amesema ili kuhakikisha uadilifu, uwazi na ushindani wa haki, maandalizi ya tuzo hizo yanahusisha pia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kama mdau muhimu katika kusimamia weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.

“Tuzo hizi zinalenga kutambua, kuthamini na kuhamasisha uzalishaji wa maudhui ya ndani yenye ubora, yanayochangia kuelimisha, kuhabarisha na kuburudisha, na kuimarisha taswira chanya ya Taifa kupitia habari za maendeleo,” amesema.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amesema tofauti na msimu wa kwanza wa tuzo hizo, mwaka huu washiriki wanapaswa kuhakikisha wamekidhi sharti la ithibati.

“Mtakumbuka Msimu wa kwanza wa Samia Kalamu mambo ya JAB hayakuwepo, kwa hiyo waandishi walishiriki wote bila kujali vigezo vya Ithibati lakini mwaka huu kuna hiki kigezo cha kuwa na ithibati kwa hiyo niwashauri basi wote wanaoshiriki kwenye hizi tuzo wahakikishe wanakuwa na ithibati, wamethibitishwa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.” Amesema Wakili Kipangula na kuongeza;
“Ni muhimu sana kwa sababu ni takwa la kisheria na kitu ambacho hatuwezi kukikwepa. Nawahamasisha tushiriki wote kwa sababu isionekane ni tuzo za watu fulani tu, kila mmoja awasilishe kazi zake,” amesema Kipangula.

Kwa mujibu wa vigezo vya ushiriki vilivyotangazwa, Waandishi wa Habari wa Tanzania Bara wanatakiwa kuwa wamethibitishwa na JAB, huku kwa Zanzibar washiriki wakitakiwa kuwa na kitambulisho cha Mwandishi wa Habari (Press Card).

Tuzo hizo zimeanza kupokea kazi kuanzia Mei 31 hadi Juni 30, 2026 na zinatarajiwa kutolewa kati ya Oktoba na Desemba mwaka huu.

CRJE YAWAKUTANISHA WATOTO WA KICHINA NA TANZANIA KATIKA KUBADILISHANA UTAMADUNI SIKU YA MTOTO DAR ES SALAAM

May 31, 2026 Add Comment

      

By Prosper Makene

CRJE (East Africa) Ltd has celebrated International Children’s Day by putting children at the center of China-Tanzania friendship with aims of planting seeds of trust early, so the next generation sees the partnership as something personal, not only official.

MRADI WA C-SDTP KUWA CHACHU YA MAGEUZI YA TASNIA YA MAZIWA TANZANIA

May 31, 2026 Add Comment
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ( wa nne kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mratibu wa Taifa wa Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP), Dkt. Lazaro Kapella ( wa pili kulia), alipotembelea banda la mradi huo katika Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa mkoani Iringa. Picha na Kadama Malunde
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akizungumza alipotembelea Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) katika Maadhimisho ya 29 ya Wiki ya Maziwa Kitaifa mkoani Iringa.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameutaja mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) kuwa miongoni mwa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali kwa lengo la kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya maziwa nchini, kuongeza uzalishaji, kuimarisha mnyororo wa thamani wa maziwa na kuinua kipato cha wafugaji.

TBS YAIMARISHA ELIMU YA UBORA WA BIDHAA ZA MAZIWA IRINGA

May 31, 2026 Add Comment
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limesema linaendelea kushiriki kikamilifu katika maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kitaifa yanayofanyika mkoani Iringa kwa lengo la kutoa elimu kwa wadau wa sekta ya maziwa na wananchi kuhusu umuhimu wa kuzingatia viwango na ubora wa bidhaa za maziwa.

TI3P YATAJWA KUCHOCHEA MAPINDUZI YA SEKTA NDOGO YA MAZIWA

May 31, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu, Iringa

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Kakurwa, ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa utekelezaji wa Mradi Shirikishi wa Wasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa (TI3P), akisema umekuwa chachu ya mageuzi katika sekta ndogo ya maziwa kwa kuongeza uzalishaji, kuimarisha mnyororo wa thamani na kuboresha maisha yawafugaji nchini.

KUPITIA KLINIKI YA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI, BARRICK NORTH MARA YAWATOA HOFU KUWA HAKUNA MAJI YANAYOTIRIRIKA KUTOKA MGODINI KWENDA KWENYE MAENEO YAO

May 31, 2026 Add Comment
Meneja wa Mahusiano ya Jamii wa mgodi wa Barrick North Mara Francis Uhadi akizungumza
Muonekano wa bwawa la takasumu la mgodi wa North Mara
Sehemu ya wananchi wakiwa katika moja ya mikutano ya kliniki ya kusikiliza kero
Sehemu ya wananchi wakiwa katika moja ya mikutano ya kliniki ya kusikiliza kero

-Mabwawa yake ya takasumu yana viwango vya usalama vya kimataifa

Mgodi wa Barrick North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara unaendelea na kliniki ya siku saba ya kusikiliza malalamiko,kero na migogoro ya wananchi ili kupata utatauzi wa kudumu kwenye vijiji 11 vinavyozunguka mgodi huo ambapo pia kuwaelimisha shughuli mbalimbali za mgodi vilevile kutoa ufafanuzi wa maswali yanayoulizwa na wananchi yakiwemo yanayohusiana na usalama wa maji katika maeneo yao.

LONDO AFUNGA MBEYA CITY EXPO, AAHIDI MAZINGIRA SALAMA KWA SEKTA BINAFSI KUELEKEA DIRA 2050

May 30, 2026 Add Comment
Serikali imeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ili kuipa nafasi pana sekta binafsi kushiriki katika ukuaji wa uchumi na uzalishaji wa ajira kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

KAPINGA AITAKA TBPL KUONGEZA UZALISHAJI NA KUIMARISHA MIKAKATI YA MASOKO

May 30, 2026 Add Comment
Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameagiza Menejimenti ya Kiwanda cha Kuzalisha Bidhaa za Kibaolojia Tanzania (TBPL) kinachomilikiwa na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kuongeza uzalishaji na kuimarisha mikakati ya masoko ili kunufaika na mahitaji makubwa yaliyopo sokoni, kuhakikisha kiwanda kinaendelea kujiendesha kwa ufanisi wa kibiashara

MRADI WA C- SDTP WALETA HAMASA YA UZALISHAJI MAZIWA UNAOZINGATIA MABADILIKO YA TABIANCHI

May 30, 2026 Add Comment
Sehemu ya Wafanyakazi wa Mradi wa C-SDTP wakiwa kwenye banda la maonesho wakati wa Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Iringa.

Na Kadama Malunde - Iringa

Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia mradi wa Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP), kwa kushirikiana na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), imeungana na wadau wengine wa kitaifa maadhimisho ya Wiki ya Maziwa kitaifa katika viwanja vya Mwembe Togwa, mkoani Iringa kuanzia 25 Mei hadi 1 Juni 2026 kwa lengo la kuhamasisha ufugaji wa ng'ombe na uzalishaji wa maziwa unaozingatia mabadiliko ya tabianchi.

TADB YAWAWEZESHA WAFUGAJI WADOGO ZAIDI YA 92, 000 KUPITIA MRADI WA MAZIWA WA TI3P

May 30, 2026 Add Comment
Jumla ya wafugaji wadogo 92,831 na wadau wa mnyororo wa thamani wa maziwawa Tanzania Bara na Visiwani-Zanzibar wamenufaika na Mradi Shirikishi waWasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa (TI3P) tangu ulipoanzishwa mwezi Machi mwaka 2022, ambapo asilimia 30 ya wanufaika hao ni wanawake.

Mradi huo wa miaka minne unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya KilimoTanzania - TADB pamoja na Bill & Melinda Gates Foundation huku ukitekelezwakwa kushirikiana na Heifer International, Land O’Lakes Venture37 pamoja naTanager.

Akiongea wakati wa Maonesho ya Wiki ya Maziwa Mkoani Iringa, Mratibu waMradi wa TI3P, Joseph Mabula amesema mradi huo unalenga kutatua changamoto mbalimbali zilizopo kwenye mnyororo wa thamani wa sekta ndogo ya maziwa ilikuongeza uzalishaji, na kuboresha kipato cha wafugaji wadogo wa maziwa nchinihuku akiishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. SamiaSuluhu Hassan kwa kuipa uzito mkubwa sekta ndogo ya maziwa.

Mabula amesema tangu kuanza kwake, mradi umewezesha utolewaji wa mikopowa Zaidi ya shilingi bilioni 42 kwenye sekta ndogo ya maziwa ikiwalenga wasindikaji wa maziwa, wafugaji, wasambazaji wa pembejeo, pamoja na wadauwengine kwenye mnyororo wa thamani wa sekta ya maziwa.

Fedha hizo zimewezesha uanzishwaji wa viwanda vipya vya kuchakata maziwapamoja na upanuzi na maboresho kwa jumla ya viwanda 17 vya usindikajivimefikiwa kwa uwekezaji wenye thamani ya shilingi bilioni 22.8.

Aidha, mradi umewezesha ununuzi wa mitamba 3,330 yenye thamani ya zaidi yashilingi bilioni 11.09, hatua iliyochangia kuongeza uzalishaji na tija katika sekta yamaziwa nchini.

Kupitia mradi huo, wafugaji wameendelea kupata huduma za ugani, pembejeobora, masoko, pamoja na huduma za kifedha kwa ajili ya uwekezaji katika sektandogo ya maziwa, jumla ya wasindikaji 19 wa maziwa wamenufaika na programuza kuongeza uwezo, huduma za ugani, na ufanisi katika uzalishaji.

Katika kuhamasisha ushirikishwaji wa kijinsia na ukuaji jumuishi, TADB ilitoaruzuku linganifu yenye thamani ya shilingi bilioni 1.4 kwa wafugaji wadogo 1,216, wakiwemo wanawake 397, ili kupunguza changamoto za upatikanaji wa mitambabora, uzalishaji, uchakataji na uwekezaji katika mnyororo wa thamani wa maziwa.

Vilevile, biashara tano (5) zinazomilikiwa na wanawake zilipatiwa mitambo yakuchemshia maziwa yenye thamani ya shilingi milioni 75 ili kuongeza fursa za masoko kwa wafugaji. Wasindikaji wanawake watano (5) walinufaika na ruzuku za TI3P, huku wasindikaji 12 wakipata ruzuku maalum za kuchochea usawa wakijinsia katika biashara zao.

Katika kuboresha ukusanyaji na kuhakikisha ubora wa maziwa, mradiumefanikiwa kuanzisha na kuimarisha vyama vya ushirikia/msingi 45 pamoja navikundi mbalimbali vya wafugaji na wafanyabiashara kwenye seta ndogo yamaziwa. Vikundi hivyo kwa sasa vinakusanya zaidi ya lita 25,664 za maziwa kwasiku,hivyo kuchochea upatikanaji wa maziwa hususani kwa viwanda nawachakataji wadogo wa maziwa.

Mratibu wa Mradi huo, amesema kuwa mradi umefanikiwa kuanzisha vituo 23 vyaukusanyaji wa maziwa nchini kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 1.157 kwakushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwemo vyama vya ushirika, wafugaji, wasindikaji wa maziwa, na washirika katika utekelezaji wa mradi.

Mabula amehihimisha kwa kusema kuwa mradi huo unaendelea kushughulikiachangamoto za kisera na kisheria zinazoathiri ukuaji wa sekta ndogo ya maziwasambamba na kuzingatia masuala mtambuka kama usawa wa kijinsia na lishe bora kwa maendeleo endelevu ya sekta hiyo.

Ametoa wito kwa wadau wote kuendelea kushirikiana katika kutatua changamotozinazoikabili sekta ndogo ya maziwa na kutumia kikamilifu fursa zinazotolewakupitia mradi wa TI3P pamoja na huduma za TADB.

SANGU: TUTAENZI MCHANGO WA WAKILI SWAI

May 29, 2026 Add Comment

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu leo ameongoza watumishi, mawakili na wananchi kumuaga aliyekuwa mtumishi wa Ofisi hiyo, marehemu Wakili Msomi Charles Boaz Swai aliyefariki jana jijini Dodoma.

MIAKA 18 BAADAYE:JK AKUTANA TENA NA CATHERINE,BINTI ALIYEFANYIWA UPASUAJI WA MOYO AKIWA NA MIAKA MINNE

May 29, 2026 Add Comment




Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo Mei 29, 2026 amekutana tena na Bi. Catherine P. Conrad Minja, aliyefanyiwa upasuaji wa moyo kwa mafanikio akiwa na umri wa miaka minne katika taasisi ya  Muhimbili Orthopaedic Institute  (MOI) miaka 18 iliyopita.


Wakati huo madaktari bingwa wa Moyo wa Taasisi ya Moyo ya JKCI walikuwa wakitumia majengo ya MOI kabla jengo lao halijakamilika.


Mara ya kwanza wawili hao walikutana Novemba 14, 2008 wakati Dkt. Kikwete akiwa Rais alipokwenda kumjulia hali Catherine  hapo MOI baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo. Wakati huo Catherine alikuwa mmoja wa wagonjwa wa mwanzo kufanyiwa upasuaji huo katika taasisi hiyo.


Miaka 18 baadaye, Catherine amekua na sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Shahada ya Udaktari katika Chuo Kikuu cha Kairuki  jijini Dar es salaam.


Alifika ofisini kwa Rais Mstaafu kumsabahi na kumshukuru kwa mchango wake katika kuanzisha na kuimarisha huduma za matibabu ya magonjwa ya moyo nchini.


Dkt. Kikwete alimpongeza Catherine kwa kutimiza ndoto yake ya kusomea udaktari, jambo ambalo aliahidi kulifanya alipokuwa mtoto. Alisema amefurahishwa kumuona akiwa mwenye afya njema na akijiandaa kulitumikia taifa kupitia taaluma ya tiba.


Kwa upande wake, Catherine alisema anatamani kuwa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo ili kuwasaidia wagonjwa wenye changamoto kama aliyowahi kupitia yeye mwenyewe, akieleza kuwa hiyo itakuwa ni moja ya njia ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha na afya njema.