HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

FURAHA YA PASAKA KUTIKISA DAR TAMASHA LA MTOKO NA SHUSHO KUFANYIKA MLIMANI CITY

FURAHA YA PASAKA KUTIKISA DAR TAMASHA LA MTOKO NA SHUSHO KUFANYIKA MLIMANI CITY

April 01, 2026 Add Comment

Tamasha la Pasaka ‘Mtoko na Christina Shusho

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi Aprili 5, 2026, siku ya Jumapili ya Pasaka, katika tamasha la ‘Mtoko na Christina Shusho Pasaka’ litakalofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam ambapo wananchi wataruhusiwa kuingia bure.

Kauli mbiu ya tamasha hilo ni “Ushindi wa Milele.”

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Machi 30, 2026, Meneja wa msanii wa muziki wa injili Christina Shusho, Humphrey Gatimu, amesema maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika kwa asilimia 100 na kusisitiza kuwa wananchi wote wanakaribishwa kushiriki bila malipo yoyote.

Amesema tamasha hilo litawakutanisha waimbaji mbalimbali wa muziki wa injili akiwemo Rose Muhando, Joel Lwaga, The Voice, Bella Kombo, Ambwene Mwasongwe, Neema Gospel Choir, Paul Clement na wengine wengi.
“Milango ya ukumbi itafunguliwa rasmi saa nane mchana, hivyo tunawaomba wananchi kujitokeza kwa wingi na kuwahi mapema ili kuepuka changamoto ya kukosa nafasi ndani,” amesema Gatimu.
Aidha, Gatimu amebainisha kuwa matarajio ya waandaaji ni kupanua wigo wa tamasha hilo mwakani kwa kulipeleka katika mikoa mitatu tofauti, huku wakiahidi kuweka wazi maeneo hayo wakati utakapofika.
Kwa upande wake, mwimbaji wa nyimbo za injili, Shusho amesema tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka kipindi cha Pasaka, limekuwa jukwaa muhimu la kuwakutanisha wasanii wa muziki wa injili, waumini pamoja na familia kwa lengo la kusherehekea sikukuu hiyo na kuinua vipaji vipya.
Amesema mafanikio ya tamasha hilo yanatokana na amani iliyopo nchini Tanzania, akimshukuru Mungu kwa kumpatia kibali cha kufanya tamasha pamoja na viongozi wa serikali kwa kuendelea kudumisha utulivu na maendeleo ya taifa.
“Tunawahimiza watu kufika mapema ili waweze kushiriki kikamilifu ibada ya sifa na kuabudu pamoja nasi, kwani kuna mambo mengi mazuri yameandaliwa kwa ajili ya kumtukuza Mungu,” amesema Shusho.
Naye mwimbaji kutoka kundi la The Voice, Obedi Mark amesema tamasha hilo limekuwa chachu kwa wasanii wengi kukuza vipaji vyao sambamba na kueneza ujumbe wa injili kupitia muziki.
Kwa upande wake mwanakwaya wa kwaya ya Mt Cecilia Makuburi, Joseph Atanasi amesema wao kama kwaya watashiriki kikamilifu katika tamasha hilo wakiwa wamejiandaa vyema kuendelea kumsifu Mungu kupitia uimbaji.
WIKI YA HAKI ZA MLAJI YAADHIMISHWA KWA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA

WIKI YA HAKI ZA MLAJI YAADHIMISHWA KWA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA

April 01, 2026 Add Comment
 

Na.Mwandishi Wetu

TUME ya Ushindani (FCC) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imeadhimisha Wiki ya Haki za Mlaji Duniani kwa kutoa msaada wa vifaa tiba katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Shughuli hiyo imefanyika tarehe 31 Machi, 2026 ambapo FCC imekabidhi vifaa tiba vinne vya Oxygen Flow Meter vitakavyosaidia wagonjwa wanaohitaji huduma ya hewa tiba, hususan wale wanaopata changamoto ya kupumua.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mkuu wa FCC Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw.Dickson Mbanga, amesema kuwa tukio hilo ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Haki za Mlaji Duniani pamoja na kutimiza miaka mitatu tangu kuanzishwa kwa ofisi hiyo katika ukanda huo.

Mbanga ameeleza kuwa FCC imeona ni vyema kutumia maadhimisho hayo kwa kutoa mchango wa kijamii utakaoleta tija moja kwa moja kwa wananchi, hasa katika sekta ya afya ambayo ni nyeti na muhimu kwa ustawi wa jamii.

 "Vifaa hivyo vitasaidia kuongeza uwezo wa hospitali katika kuhudumia wagonjwa wanaohitaji msaada wa hewa tiba, hivyo kupunguza changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa utoaji wa huduma hizo."amesema Bw.Mbanga

Kwa upande wake, akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Muuguzi Kiongozi Ndg. Petro Seme ametoa shukrani za dhati kwa FCC kwa msaada huo muhimu.

Seme amesema kuwa vifaa hivyo ni vya kisasa na vina uwezo wa kuhudumia wagonjwa wawili kwa wakati mmoja, jambo ambalo litarahisisha upatikanaji wa huduma ya hewa tiba na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa.

‎WAFANYAKAZI WA TUME YA TAIFA YA MIPANGO WATAKIWA KUWA WABUNIFU NA WELEDI

April 01, 2026 Add Comment

Katibu Mkuu-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt Tausi M. Kida ametoa wito kwa watendaji wa Tume hiyo kufanya kazi kwa weledi, ubunifu na ushirikiano ili kuishi dhana ya kufanya kazi isivyokawaida ili kuyafikia matarajio ya Taifa jumuishi, lenye ustawi, haki na linalojitegemea.

‎Dkt Kida ametoa wito huo leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Taifa ya Mipango.

Aidha, amesisitiza ‎kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan inayo matarajio makubwa kwa Tume ya kuhakikisha inatekeleza ipasavyo majukumu yake kwa weledi, ari na kuzingatia utu.

‎Mkutano huo, umeongozwa na kauli mbiu isemayo: Utumishi Imara ni Msingi wa Utekelezaji wa Dira 2050.





RAIS DKT. SAMIA SULUHU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGOMBEA WA NAFASI YA URAIS WALIOSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA, 2025

April 01, 2026 Add Comment


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Wagombea wa Nafasi ya Urais na Wagombea Wenza kutoka vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Wagombea wa Nafasi ya Urais na Wagombea Wenza kutoka vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Wagombea wa Nafasi ya Urais na Wagombea Wenza kutoka vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Wagombea wa nafasi ya Urais pamoja na Wagombea Wenza wa Vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025 mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.







RAIS MSTAAFU DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE AHANI MSIBA WA RAIS WA ZAMANI WA ALGERIA JENERALI MSTAAFU LIAMINE ZEROUL

April 01, 2026 Add Comment


Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo April 1, 2026 akitia saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa Algeria, Jenerali Mstaafu Liamine Zeroual,  aliyefariki dunia mnamo Machi 28, 2026 akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu. Pamoja naye ni Balozi wa Algeria nchini Mheshimiwa Ghalib Zermane.  Kitabu hicho kimefunguliwa nyumbani kwa Balozi Oysterbay jijini Dar es salaam.

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo April 1, 2026 ametia saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa Algeria, Jenerali Mstaafu Liamine Zeroual,  aliyefariki dunia mnamo Machi 28, 2026 akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu.


Jenerali Zeroual, aliyependwa na kuheshimikka sana, alichaguliwa kuwa rais mwaka 1995 katika kipindi kigumu cha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Algeria. Alianzisha mageuzi ya kisiasa, ikiwa ni pamoja na kuratibu uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi.

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo April 1, 2026 akitia saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa Algeria, Jenerali Mstaafu Liamine Zeroual,  aliyefariki dunia mnamo Machi 28, 2026 akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu. Pamoja naye ni Balozi wa Algeria nchini Mheshimiwa Ghalib Zermane.  Kitabu hicho kimefunguliwa nyumbani kwa Balozi Oysterbay jijini Dar es salaam.

Hata hivyo alijiuzulu mapema mwaka 1998 kabla ya kumaliza muhula wake wa miaka mitano ili kutoa nafasi kwa mpito wa kisiasa, na tangu hapo aliishi maisha ya faragha bila kujihusisha sana na siasa.

Hadi leo anakumbukwa kama kiongozi aliyetoa mchango muhimu katika kuiongoza Algeria katika kipindi cha mpito na changamoto kubwa za kisiasa na kiusalama.

Akiongea na Balozi wa Algeria nchini Mheshimiwa Ghalib Zermane, Dkt Kikwete alisema Algeria na Tanzania imekuwa rafiki wa karibu kwa muda mrefu, na kwamba viongozi wake wote waliopita wamefanya kazi kwa karibu na viongozi wa Tanzania kuanzia Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hususan hususan katika  ukombozi wa bara la Afrika, akiwataja wataja viongozi hao kama Ahmed Ben Bella, Houari Boumédiène, Chadli Bendjedid,  Liamine Zéroual na Abdelaziz Bouteflika

MAFUTA KUPANDA BEI, SERIKALI YAAHIDI SULUHISHO KWA WANANCHI

April 01, 2026 Add Comment


Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kusimamia upatikanaji wa bidhaa za mafuta ya petroli na mafuta mengine ili kuhakikisha bei zake zinaendelea kuwa himilivu, licha ya kuwepo kwa changamoto za kiusalama za kikanda na kimataifa ikiwemo za Mashariki ya Kati zilizosababisha kupanda kwa bei ya mafuta nchini.


“Tumeona bei zimeanza kupanda, tutakaa ndani ya Serikali kuweza kuhakikisha tunakabiliana nalo vipi, ili wananchi wananchi wanaendelea kupata mafuta kwa bei wanazoweza kumudu na kudhibiti kupanda kwa gharama za maisha,” amesema Dkt. Mwigulu 

Amesema hayo leo, tarehe 1 Aprili 2026, wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2026/2027 Bungeni, jijini Dodoma. 


Katika hatua nyingine, amesema Serikali imeendelea kusimamia mifumo ya kuagiza, kuhifadhi na kusambaza mafuta, pamoja na kuongeza uwezo wa kupokea na kuhifadhi mafuta katika bandari za Dar es Salaam na Mtwara.


Aidha, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa ghala la kupokea na kuhifadhi mafuta lenye uwezo wa tani 308,110 katika Bandari ya Dar es Salaam, ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 30.



Ameongeza kuwa miundombinu ya kuhifadhi mafuta katika Bandari ya Mtwara imeongezeka kutoka tani 29,280 hadi tani 110,221, hatua itakayowezesha kupokea meli yenye shehena ya tani 30,000.


Kwa upande mwingine, amesema Serikali imeendelea kuhakikisha ongezeko la matumizi ya gesi asilia, Katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, mtandao wa miundombinu ya usambazaji wa gesi asilia katika viwanda, taasisi na makazi umeongezeka hadi kilomita 243.6, ikilinganishwa na kilomita 184.8 hapo awali.


Kadhalika, amezielekeza Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Nishati kushirikiana kuandaa viwango msawazo (specifications) vitakavyotumika katika mahitaji ya vyombo vya moto vya Serikali, pamoja na kujenga miundombinu ya kutosha ili kuwezesha vyombo hivyo kuanza kutumia gesi asilia iliyoshindiliwa.

RC MALIMA AITAKA COPRA, WAKULIMA KUONGEZA UZALISHAJI MAZAO YA VIUNGO KWA KUZINGATIA UBORA

April 01, 2026 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu,Morogoro



MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Adam Kighoma Malima, ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) pamoja na wakulima kuongeza uzalishaji wa mazao ya viungo kwa kuzingatia ubora, tija na ushindani wa soko la kimataifa, akisisitiza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kufikia dira ya Taifa ya kukuza uchumi kupitia sekta ya kilimo.

Akizungumza katika mkutano wa wadau wa mazao ya viungo uliofanyika mkoani Morogoro, Malima amesema ni lazima wakulima washirikishwe kikamilifu katika kupanga na kutekeleza mikakati ya kilimo, huku akisisitiza umuhimu wa kuwepo kwa mifumo rafiki ya kifedha itakayowawezesha kumudu gharama za uzalishaji hasa kwa mazao yanayochukua muda mrefu kukomaa kama pilipili manga.

Amesema ili kuongeza ushindani wa mazao ya viungo katika soko la dunia, kuna haja ya kuimarisha vyama vya ushirika, kuboresha mbinu za kilimo na kuhakikisha wakulima wanapata elimu sahihi ya kilimo cha kibiashara pamoja na upatikanaji wa masoko ya uhakika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa COPRA, Irene Mlola, amesema mamlaka hiyo imejipanga kuongeza uzalishaji wa mazao ya viungo kutoka tani 22,000 za sasa hadi kufikia tani 50,000 ifikapo mwaka 2030, sambamba na kuongeza ubora na thamani ya mazao hayo kupitia uchakataji.

Mlola amesema kwa sasa thamani ya mauzo ya nje ya mazao ya viungo imefikia takribani shilingi bilioni 497, huku akibainisha kuwa bado kuna fursa kubwa ya kupanua uzalishaji ili kunufaika zaidi na soko la dunia linalokadiriwa kufikia tani milioni 11 ambapo Tanzania inauza tani 1.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Batilda Burian, amesema ni wakati wa Tanzania kuacha kuuza mazao ghafi na badala yake kuongeza thamani kupitia uchakataji, akieleza kuwa mazao ya viungo yana fursa kubwa katika sekta za afya, lishe na vipodozi.

Amesema ukuaji wa soko la bidhaa za asili duniani, ikiwemo superfoods, unatoa nafasi kwa nchi kuongeza uzalishaji na kuimarisha ushindani, huku akihimiza uwekezaji zaidi katika teknolojia ya uchakataji ili kuongeza mapato na ajira.

Kwa upande wao, baadhi ya wakulima walioshiriki mkutano huo wamesema licha ya uwepo wa fursa nyingi katika kilimo cha mazao ya viungo, bado wanakabiliwa na changamoto za miundombinu duni ya barabara, ukosefu wa maghala ya kuhifadhi mazao pamoja na bei zisizo na ushindani kutokana na uwepo wa madalali wachache sokoni.

Wamesema kuna haja ya kuimarishwa kwa mafunzo ya kilimo cha kisasa, upatikanaji wa pembejeo bora na mifumo madhubuti ya masoko ili kuwawezesha kuongeza uzalishaji na kunufaika zaidi na sekta hiyo yenye mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa.

COPRA imewakutanisha wadau ili kuweka juhudi za pamoja kuimarisha kilimo cha mazao ya viungo na kuongeza uzalishaji wenye tija unaolenga kufaidika na soko la ndani na lile la Kimataifa.





TANZANIA INA MAFUTA YA KUTOSHA,LICHA YA BEI KUPANDA KUTOKANA NA VITA YA MASHARIKI YA KATI

TANZANIA INA MAFUTA YA KUTOSHA,LICHA YA BEI KUPANDA KUTOKANA NA VITA YA MASHARIKI YA KATI

April 01, 2026 Add Comment
 

Mabadiliko ya bei za mafuta nchini kwa mwezi Aprili 2026 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na vita inayoendelea kati ya Marekani kwa kushirikiana na Israeli dhidi ya Irani iliyoanza tarehe 28 Februari 2026, mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesema jana.

“Kushambuliwa kwa visima vya mafuta, maghala ya kuhifadhi mafuta na viwanda vya kusafisha mafuta (refineries) pamoja na Irani kufunga Lango la Hormuz linalopitisha takriban asilimia 20 ya mafuta yanayosafirishwa kwenda kwenye masoko mbalimbali duniani, imeathiri hali ya uzalishaji mafuta kwenye nchi za Mashariki ya Kati ambako Tanzania inaagiza kwa kiasi kikubwa; imeongeza gharama za usafirishaji kutokana na kukosekana kwa meli za kusafirisha mizigo na imeongeza gharama za bima za meli za mizigo kutokana na vita,” imeeleza taarifa iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari jana.

Kwa mwezi Aprili 2026, gharama za kuagiza mafuta (premiums) katika Bandari ya Dar es Salaam zimeongezeka kwa wastani wa asilimia 15.3 kwa mafuta ya petroli na asilimia 10.8​ kwa mafuta ya dizeli na hakuna mabadiliko ya gharama kwa mafuta ya taa.

EWURA imesema ongezeko hilo ni janga la kidunia na Tanzania kama sehemu hiyo inachukua hatua mbalimbali kuhakikisha usalama wa upatikanaji wa mafuta nchini na bei himilivu ili kupunguza madhara ya kiuchumi na kijamii. Kutokana na hali hiyo, EWURA imewashauri wananchi kutumia mafuta kwa uangalifu na ufanisi mkubwa.

DID TANZANIA KUTOA ELIMU YA UTUNZAJI MAZINGIRA ROMBO KWA KUTUMIA SANAA YA MAJUKWAANI

March 31, 2026 Add Comment

 




Na. Mwandishi Wetu,


DIVERSITY Initiatives for Development Tanzania (DID TANZANIA) ambao ni waratibu wa mradi wa Sauti za Mabonde "Voices of Valley" uliojikita kutoa elimu ya utunzaji wa Mazingira Wilayani Rombo wanatarajia kufikia Jamii kwa kutumia Sanaa ya majukwaani.


Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa DID Tanzania, Bw. Optatus Nestory Mbararia ambaye ni mratibu mkuu wa mradi amesema kuwa, utafiti wa awali wamebaini uharibifu mkubwa wa Mazingira ikiwemo eneo la chanzo cha maji cha Kamdawi na bonde la Tarakea, unaotokana na shughuli za Kijamii kama uchimbaji mchanga, kubonda kokokoto, ukataji wa miti na Kilimo kisicho rasmi pembezoni mwa vyanzo vya maji.

"Kwa sasa tupo hatua ya mwisho kwa Vijana Wasanii wakifanya mazoezi ya onesho lao kwa njia ya sanaa za jukwaani.


Watafanya maonesho kadhaa ambayo ni ya wazi jukwaani, kufikisha ujumbe." Amesema Optatus Mbararia.

Mradi ni wa mwaka mmoja, ambapo unaenda kutoa elimu kwa Jamii juu ya utunzaji wa Mazingira hususani vyanzo hivyo vya maji na mito mbalimbali Wilayani Rombo, Mkoani Kilimanjaro.


Aidha, amebainisha kuwa, mbali ya utoaji elimu kwa njia ya  Sanaa za majukwaani, Pia watakuwa na shughuli za upandaji miti kama utunzaji wa Mazingira, ambapo miti zaidi ya 1,000 itapandwa katika chanzo cha maji kamdawi na bonde la Mto Tarakea.

"Mradi wetu huu pia tunatarajia kushirikiana na wadau muhimu ikiwemo Halmashauri ya Rombo kupanda miti.


Lakini pia mijadala ya kijamii na Wananchi watatoa maoni yao." Amesema Bw. Optatus Nestory Mbararia.

Kwa Upande wao baadhi ya Wasanii Vijana wamebainisha kuwa wapo tayari na wamejiandaa vyema kufikisha elimu ya utunzaji mazingira kwa njia ya Sanaa za majukwaani 

Dumey Aloys Kijwiti msanii wa sanaa maagizo asema kupitia sanaa ujumbe utafika kwa haraka kwa Jamii.


"Naamini  Sanaa ni njia rahisi kufikisha ujumbe kwa Jamii, ni kitu rahisi zaidi kuliko chochote.


Sanaa ni njia rahisi ya kutatua na kuchanganua na kuleta majibu katika Jamii.


Kwa kupitia mradi wa voices of valley, nikiwa kama mratibu wa maigizo ya jukwaani, naamini na wenzangu tunaendelea vyema kufikisha ujumbe kwa Wananchi.


Sanaa kwa maendeleo Ina aina zake, kwa maana Sanaa Ina hatua zaidi ya Saba, na sie mwisho wa siku tunaenda kufanya Sanaa kwa  maendeleo.


Naamini Jamii itatupokea vizuri kwani tunaenda kuwapa mawazo mapya na kuonesha mambo ambao hayatakiwi kwa Jamii, na kulinda mazingira." Amesema Dumey.


Mradi huo ni program ya Vijana Artwork (Vijanam @rtwork) unasimamiwa na CDEA na Goethe Institut kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).



Mwisho.

KITUO CHA UMEME IFAKARA CHACHOCHEA MAENDELEO KILOMBERO

March 31, 2026 Add Comment



📌Kimetekelezwa na REA kwa gharama ya Tsh. Bilioni 25


📌DC Kilombero aipongeza REA, atoa wito kwa wawekezaji


📌Kimeimarisha upatikanaji wa umeme Ukanda wa Morogoro Kusini


Ifakara, Kilombero

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetumia shilingi bilioni 25 kujenga Kituo cha Kupoza Umeme 1x20MVA, 220/33kv pamoja na njia za kusambaza Umeme katika Wilaya ya Kilombero, hatua ambayo imeboresha upatikanaji wa umeme na kuondoa changamoto ya kukatika kwa nishati hiyo katika wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Machi 31, 2026 wakati wa ziara ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) waliotembelea mradi huo kujionea utekelezaji wake na tija yake kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika ukanda wa Morogoro Kusini.

"Fursa za uwekezaji wilayani hapa zimeongezeka baada ya kukamilika kwa kituo hiki, ninatoa wito kwa wawekezaji kujitokeza kwa wingi kwani tunao umeme wa uhakika na toshelevu," amebainisha Wakili Kyoba. 

Amesema kuimarika kwa huduma ya umeme kumechochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi, hususan katika sekta za viwanda, uchimbaji madini, kilimo na huduma za kijamii.

Kwa upande wake, Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme kutoka REA, Mhandisi Deogratius Nagu, amesema gharama za mradi huo zinahusisha pia usimikaji wa mashine umba (transfoma) pamoja na mifumo yake ya uendeshaji, udhibiti na ulinzi, ujenzi wa njia za kusafirisha umeme za msongo wa kilovolti 33 zenye urefu wa kilometa 70 pamoja na gharama za mshauri elekezi.

Mhandisi Nagu amebainisha kuwa, kituo hicho ni cha kisasa, kikiwa na teknolojia kutoka nchi mbalimbali ikiwemo transfoma kutoka Bulgaria, mifumo ya udhibiti na ulinzi kutoka Hispania pamoja na mifumo ya switching (switchgears) kutoka Ujerumani.

“Kituo hiki kimeondoa changamoto ya upatikanaji wa umeme katika wilaya za Kilombero na Ulanga na kuwezesha wananchi kuendeleza shughuli za uzalishaji na kuongeza thamani ya mazao,” alisema Nagu.

Naye Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, amesema uwekezaji huo unaonesha matumizi sahihi ya rasilimali za umma na mchango wa REA katika kusambaza huduma ya umeme vijijini.

"Tumeshuhudia uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kupitia REA, ni fursa ya maendeleo kwa wananchi ni muhimu tukachangamkia Uwepo wa umeme wa uhakika kujiletea maeendeleo," amesema Balile.

Balile amesema REA imeonyesha mfano wa kipekee kwenye utekelezaji wa majukumu yake na kwamba kazi iliyokwishakamilika ni kubwa na manufaa yake yanaonekana na ametoa wito kwa Taasisi zingine za Serikali kuiga mfano huo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanufaika wa mradi huo wameeleza namna ambavyo Mradi huo umekuwa mkombozi kwao.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kilimo Ifakara, Setina Ngailo, amesema huduma ya umeme imeimarika na kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme iliyokuwa ikiathiri shughuli za shule.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Hospitali ya Kansa ya Good Samaritan, Father Charles Masawe, amesema upatikanaji wa umeme wa uhakika umeongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya kwa kupunguza utegemezi wa jenereta.

Naye Meneja wa Kiwanda cha Kukoboa Mpunga cha Bezelengule, Enos Machumu, amesema uzalishaji umeongezeka kwa kiasi kikubwa kufuatia kuboreshwa kwa huduma ya umeme, hali iliyorejesha wateja na kulinda mitambo dhidi ya uharibifu.

Kwa ujumla, mradi huo unatajwa kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika ukanda wa Morogoro Kusini, huku serikali ikiendelea na juhudi za kusambaza umeme katika vitongoji vilivyobaki ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi wote.