HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
COSTECH YATAKIWA KUBUNI MFUMO RAHISI KUFIKISHA MATOKEO YA TAFITI
habariMAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR ASEMA KUNA UMUHIMU VIJANA WAFUNDISHWE HISTORIA YA CCM
habari
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amesema wakati chama cha Mapinduzi (CCM) kinaadhimisha miaka 49 ya kuzaliwa kwake kuna umuhimu mkubwa vijana wafundishwe historia yake na waijue ikiwemo misingi ya uwepo wake.
Abdulla ambaye pia ni Mlezi wa CCM Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM aliyasema hayo leo wakati wa kilele cha maadhimisho ya kuzaliwa kwa chama hicho yaliyofanyika kimkoa Stendi ya Bombani mjini Muheza. 
Alisema kwamba wakijua msingi wa kuwepo chama hicho na wakitembea watatembea na maono mazuri mno lakini wasipojua bado kuna kitu watakuwa wanawanyima hivyo lazima wajue kwanini TANU na ASP ziliungana.
Aidha alisema pia wajue pia viliingana kwa malengo gani na wafahamu kwanini kuna chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndio chama cha wanyonge hata ukiangalia vijiji vyote Tanzania kila mahali, kata utakuta kuna mradi kama hakuna shule utakuta mradi wa zahanati,barabarani,mradi wa maji na miradi mengine mbalimbali kwa sababu ya kujali maslahi ya wananchi wa Tanzania.
Alisema pia Rais Dkt Samia Suluhu ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho amefanya mambo mengi makubwa na mazuri hivyo wana kila sababu ya kumuenzi na kumtunza ili aweze kuwafanyia mambo mengi na makubwa zaidi.
Alieleza kwamba Rais Dkt Samia katika kipindi cha miaka mitano amefanya mambo makubwa na ahaidi yake miaka mitano hii amehaidi mambo mengi mazuri hivyo wampe ushirikiano ili aweze kutekeleza yale yote aliyohaidi.
Abdulla alisema kwamba CCM ndio chama pekee ambacho kinadumisha muungano wetu kwa Tanganyika na Zanzibar vyama vyengine vinavisikia vikisema tu kwenye kampeni zao wao jambo la kwanza wakipata wanavunja muungano jambo ambalo halina afya kwa ustawi wa maendeleo hapa nchini.
Hata hivyo alisema kwamba hivi sasa watanzania wanahitaji mambo mawili makubwa ambayo ni amani na maendeleo ambayo ndio tunu kubwa ya mafanikio katika jambo lolote lile.
“Leo hii mmeona zile changamoto zilizojitokeza baadhi ya mikoa Octoba 29 ya kutetereka kwa amani kila mmoja hana furaha unatafuta taarifa haupati,hakuna nyumba ya mtanzania inayokosa simu hivyo akikosa kupata habari hivyo kupitia maadhimisho haya wachukue wale wenye mawazo tofauti kuwashawishi watanzania kufanya mambo yasiyokuwa na tija kwa nchi”
Hata hivyo alisema kwamba watanzania wana mahitaji mawili ya amani na maendeleo ukikamilisha hayo umekamilisha kazi na hayo huwezi kuyapata popote zaidi ya CCM.
Pongezi.
Mlezi huyo wa CCM aliwapongeza wananchi wa Tanga kutokana na kudumisha amani Octoba 29 na hivyo kufanya uchaguzi kwa amani na hatimaye uchaguzi ulifanyika kwa hali ya utulivu.

Alisema kwamba kwamba hali ya amani inayozungumzwa haiwasaidii wana CCM pekee bali inasaidia wananchi wote wa Tanzania na hata wasiokuwa watanzania waliopo nchini kwa shughuli zao za maendeleo na njia moja ya kuwekeza sehemu yoyote duniani jambo la kwanza wanaangalia amani wakiona ipo ndio wanaendelea na hatua nyengine.
“Leo tunapoadimisha miaka 49 ya kuzaliwa CCM chama ambacho kinaendelea kuaminiwa na watanzania zaidi ya milioni 60 na ni matumaini yangu watanzania tutaendelea kukikiamini CCM kwa kazi nzuri inayofanyika”Alisema

“Kwa mkoa wa Tanga maendeleo makubwa yanaonekana tumeona Bandari ya Tanga zaidi ya Bilioni 429 Dkt Samia Suluhu ameziweka pale na mkapeleka maombi ya uwanja wa Ndege ambayo Serikali itaanza kuyafanyia kazi”Alisema
Hata hivyo alisema kuna ujenzi wa miradi mbalimbali inaendelea ikiwemo Barabara ya Handeni -Kibirashi- kilindi na inaunganisha na Singida zipo taarifa nje za barabara hizo ameitaja kwa sababu ya kuunganisha na mikoa mingine na Bandari.
Alisema kwamba maana yake barabara ikikamilika wale wote wanaoleta mizigo kutoka nchi jirani watatumia Bandari ya Tanga na ipo miradi mingi inaendelea na ahadi ya CCM ni kumaliza changamoto za wananchi.
Mwisho,
NCHI ZA SAPP ZAKUTANA KUHAMASISHA MATUMIZI BORA YA NISHATI
📍TANESCO kuendesha kampeni ya matumizi bora ya umeme
📍Ni katika kutekeleza kwa kasi Mkakati wa Wizara ya Nishati wa mwaka 2024–2034
Na Mwandiahi Wetu – Zanzibar
Wajumbe wa Nchi Wanachama wa Ujumuiya ya Ushirikiano wa Umeme wa Kusini mwa Afrika (SAPP), zinazotoka katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), wakishirikisha makampuni ya umeme zaidi ya 16 yanayojihusisha na uzalishaji na usambazaji wa umeme, wamekutana Zanzibar kujadili na kuhimiza matumizi bora ya nishati ya umeme.
Mkutano huo wa siku mbili ulioanza tarehe 04 Februari 2026 unalenga kuhakikisha nishati ya umeme inayopatikana katika nchi wanachama inatumika kwa ufanisi na ubora zaidi, ikihusisha matumizi ya umeme kwa kiasi kidogo huku uzalishaji ukiendelea kuongezeka, ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa nchi husika.
Akizungumza katika mahojiano na waandishi wa habari, Meneja Tafiti wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Samweli Kessy, alisema kuwa licha ya gharama kubwa za uzalishaji wa umeme, mashirika ya umeme huuza umeme kwa bei nafuu kwa wananchi, hivyo elimu ya matumizi bora ya umeme ni muhimu katika kuokoa nishati na kuongeza mapato ya taifa kupitia uuzaji wa umeme nje ya nchi.
Aidha, Mhandisi Kessy aliongeza kuwa matumizi bora ya umeme husaidia kupunguza gharama za uzalishaji na wakati huo huo kuchangia katika uhifadhi wa mazingira.
Alisema kuwa kwa upande wa Tanzania, Wizara ya Nishati imeandaa Mkakati wa Matumizi Bora ya Nishati wa mwaka 2024 hadi 2034, unaolenga kuhakikisha wananchi wote wanapatiwa elimu ya matumizi bora ya umeme, hatua itakayopunguza gharama za maisha na kuongeza ufanisi wa matumizi ya huduma ya umeme.
Aliongeza kuwa, kupitia Mkakati wa Mawasiliano wa TANESCO, shirika litaendelea kutumia njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari, redio, televisheni, magazeti pamoja na mikutano ya ana kwa ana ili kuwafikia wananchi na wadau katika ngazi zote.
Mhandisi Kessy alibainisha kuwa mpango huo utahusisha wateja wote, kuanzia wateja wakubwa, wa kati hadi wadogo katika ngazi za mikoa, wilaya, kata na vijiji kote nchini.
Mkutano huo wa siku mbili unatarajiwa kukamilika tarehe 05 Februari 2026.
SERIKALI YABAINISHA MAENEO YA MIRADI YA UMEME WA UPEPO NA JUA,KISHAPU KUZALISHA MW 150
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Serikali imekwishabainisha na kufanya utafiti wa maeneo mbalimbali yanayofaa kuendelezwa kwa ajili ya miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia upepo na jua, ikiwa ni pamoja na Zuzu-Dodoma, Same-Kilimanjaro na Manyoni-Singida.
Mhe. Salome ametoa kauli hiyo leo Februari 05, 2026 bungenini jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mwera, Mhe. Suleiman Mohamed Rashid aliyehoji juu ya mpango wa Serikali wa kutumia vyanzo vya umeme na upepo juu vilivyopo nchini.
" Kwa sasa Serikali inatekeleza mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 150 katika Wilaya ya Kishapu, Shinyanga ambapo awamu ya kwanza ya mradi huo wenye megawati 50 imekamilika na hatua za kuingiza umeme huo katika Gridi ya Taifa zimeanza," Amesema Mhe. Salome.
Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe Esther Malleko aliyehoji mkakati wa Serikali katika kumaliza usambazaji wa umeme kwenye vitongoji vilivyosalia mkoani humo, Mhe. Salome amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na kazi za utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika Mkoa wa Kilimanjaro ambapo hadi kufikia Januari 2026 jumla ya vitongoji 2,032 kati ya 2,258 sawa na asilimia 90 vilipatiwa umeme na kusalia vitongoji 226 ambavyo vitapelekewa umeme kupitia miradi mbalimbali.
VIP SOBER HOUSE YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM ,MSANII MAARUFU WA BONGOFLEVA NDANI YA MJENGO
habari
DCC HANDENI YAPITISHA VIPAUMBELE VYA HANDENI MJI 2026/27
habari
📌Bima ya afya kwa wote yaguswa
Na Augusta Njoji
KAMATI ya Ushauri ya Wilaya ya Handeni (DCC) imepitisha mapendekezo ya rasimu ya Mpango wa Maendeleo na Bajeti ya Sh. bilioni 35 kwa mwaka wa fedha 2026/27 ya Halmashauri ya Mji Handeni, huku miongoni wa vipaumbele vilivyotajwa ni pamoja na kugharamia Bima ya Afya kwa Wote kwa wananchi wasio na uwezo kwa kutumia mapato ya ndani.
Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo kilichofanyika leo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewaagiza Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wahudumu wa Afya kutoa elimu kwa wananchi kwa lugha rahisi ili wahamasike kujiunga na mpango huo wa bima ya afya.
Amesema serikali tayari imetangaza kuanza utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, hivyo ni wajibu wa viongozi na watendaji kuhakikisha wananchi wanaelewa umuhimu wake ili wawe na uhakika wa matibabu wanapohitaji huduma za afya.
“Ni lazima wananchi waelimishwe kwa lugha wanayoielewa ili wajue faida za bima hii, kwani itawasaidia kupata huduma za matibabu kwa uhakika,” amesema Mhe. Nyamwese.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kubaini kama inatekelezwa kwa kuzingatia thamani halisi ya fedha, sambamba na kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amesema rasimu ya mpango na bajeti imeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya wananchi na mikakati ya maendeleo ya Halmashauri.
Ametaja vipaumbele vingine vitakavyotekelezwa kwa kutumia mapato ya ndani kuwa ni pamoja na kutenga Sh milioni 176 kwa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ujenzi wa fremu za maduka ili kuongeza vyanzo vya mapato, utekelezaji wa afua za lishe, ujenzi wa maabara katika shule moja ya sekondari pamoja na kuboresha miundombinu ya mifugo.
Awali, Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dkt. Hudi Muradi, amesema kwa mwaka wa fedha 2026/27 Sh milioni 30 zimetengwa katika mapato ya ndani kwa ajili ya kugharamia bima ya afya kwa wananchi wasio na uwezo na kwamba kwasasa serikali inaendelea na zoezi la uhakiki wa wananchi hao.
Ameongeza kuwa serikali imeimarisha miundombinu ya afya na kuajiri watumishi wapya 58 ili kuboresha utoaji wa huduma katika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.
VIP SOBER HOUSE YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM ,MSANII MAARUFU WA BONGOFLEVA NDANI YA MJENGO
Mati Super Brands Ltd Yazindua Royal Love Challenge 2026 ya Mapenzi ya Kifalme
Benki ya CRDB yaja na ‘Benki Kimpango Wako’ ikiahidi huduma bora zaidi kwa wateja na wadau mwaka 2026

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 19.5 KUTEKELEZA MRADI WA USAMBAZAJI UMEME KWENYE VITONGOJI 127
habari
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta neema ya maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Arusha kwa kuanza utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 127 kwa gharama ya shilingi bilioni 19.5.
Mradi huo unatekelezwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika awamu ya Pili B na unatarajiwa kuwanufaisha wateja 4,086 katika wilaya za Arusha DC, Meru, Karatu, Ngorongoro, Longido na Monduli.
Akizungumza Februari 4, 2026 mkoani Arusha wakati wa hafla ya kumtambulisha mkandarasi aliyeshinda zabuni, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Herini Mhina, amesema utekelezaji wa mradi huo ulianza rasmi Februari 2, 2026 na mkandarasi mzawa Kampuni ya NAKUROI Investment Co. Ltd.
“Tunamshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia utekelezaji wa mradi huu muhimu. Tumewaelekeza wakandarasi kuepuka rushwa, kutumia vibarua wa maeneo husika kwa kazi zisizo za kitaalamu na kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ubora na kwa wakati,” amesema Mhandisi Mhina.
Mhandisi Mhina ameongeza kuwa hadi sasa vitongoji 368 kati ya 1,505 mkoani Arusha vimefikishiwa umeme, huku jitihada zikiendelea kufikisha nishati hiyo katika vitongoji vilivyobaki.
“Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa umeme. REA imejipanga kikamilifu kutekeleza dhamira hiyo kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati,” amefafanua Mhandisi Mhina.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. CPA Amos Makala, ameipongeza REA kwa kutekeleza kwa vitendo maelekezo na dira ya Rais Samia ya kuwaletea wananchi maendeleo.
“Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itatoa ushirikiano wa kutosha kwa mkandarasi na REA kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa mafanikio,” amesema Mhe. Makala.
Naye Meneja wa Mradi kutoka Kampuni ya NAKUROI Investment Co. Ltd, Mhandisi Selestine Egongo, ameishukuru Serikali kwa kuwaamini na kuahidi kutekeleza mradi kwa ufanisi kwa kushirikiana na viongozi na wananchi wa maeneo husika.

MCC NA MLEZI WA MKOA WA TANGA HEMED SULEIMAN ABDULLA AWASILI TANGA
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Mlezi wa Mkoa wa Tanga Kichama ndugu Hemed Suleiman Abdulla amewasili Mkoani Tanga kuhudhuria katika Maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi yanayotarajiwa kufanyika kesho Febuari 5, 2026 katika Uwanja wa Stendi ya Bombani, Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga.
SEKTA YA FEDHA YAITWA KUSUKUMA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Nishati*
Serikali imetoa wito kwa wadau kutoka sekta ya fedha nchini kuanzisha huduma na bidhaa za kifedha zitakazowezesha ajenda ya nishati safi ya kupikia kusambaa zaidi, hususan kwa kuwawezesha wajasiriamali wadogo katika maeneo ya pembezoni na vijijini pamoja na wabunifu wa teknolojia za matumizi ya nishati hiyo.
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba tarehe 4 Februari 2026 wakati akimwakilisha Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi katika uzinduzi wa mradi wa nishati safi ya kupikia katika shule ya sekondari Bunge Wasichana iliyopo mkoani Dodoma.
"Tanzania imepiga hatua kubwa katika ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, matumizi ya nishati hii yameongezeka kutoka asilimia 6.9 mwaka 2021 na kufikia asilimia 23.2 mwaka 2025. Hata hivyo, bado takribani asilimia 77 ya kaya nchini zinatumia nishati isiyo safi ya kupikia, hivyo natoa wito kwa sekta binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kusukuma ajenda hii kwa kuwezesha upatikanaji wa nishati mbalimbali safi za kupikia katika maeneo ya pembezoni na yale ya vijijini." Amesema Mhe. Salome
Aidha, Mhe. Salome amewasisitiza Wasambazaji wa gesi za mitungi kuongeza vituo vya usambazaji na ujazaji wa gesi za mitungi ili kurahisisha upatikanaji wake kwa watumiaji wengi zaidi, pia Wabunifu na vijana walioko vyuoni kufanya tafiti na kubuni nyenzo na teknolojia zitakazowezesha ajenda hii kusambaa na kuwafikia watu wengi.
Kuhusu mradi wa nishati safi ya kupikia aliouzindua Mhe. Salome amesema kuwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali kwa taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za binadamu na kutunza mazingira.
Ameongeza kuwa mfumo huo uliozinduliwa utawezesha chakula kupikwa kwa usafi, kwa haraka, kwa ufanisi, kwa gharama nafuu na bila madhara ya moshi kwa wapishi na wanafunzi huku mazingira yakiendelea kustawi.
Mhe. Salome ameeleza kuwa kuzinduliwa kwa mradi huo ni sehemu ya juhudi za kitaifa zinazoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034 ambapo mpaka sasa tayari asilimia 23.2 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia huku taasisi 1,136 zinazolisha zaidi ya watu 100 kwa siku zikihamia katika matumizi ya nishati hiyo.
Akiwa katika shule hiyo ya Wasichana Bunge, Naibu Waziri amezindua pia Klabu ya Nishati Safi ya Kupikia yaani Clean Cooking School Club ambayo ni ya kwanza kuzinduliwa kwa Tanzania ambayo itakuwa mfano wa kuigwa na shule nyingine nchini katika kueneza elimu ya Nishati Safi ya Kupikia.
Wanafunzi watakaojiunga na klabu hiyo watakuwa Vinara wa Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Champions) na watashirikiana na Wizara ya Nishati na wadau wengine katika kutoa elimu mashuleni na katika jamii pamoja na kubuni teknolojia za nishati safi ya kupikia zitakazolinda afya na mazingira.
Awali Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bunge Wasichana, Richard Msana alisema shule hiyo yenye wanafunzi 555 imefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za nishati ya kupikia baada ya kuachana na matumizi ya kuni na kuhamia katika gesi.
Amesema kuanzia Julai 2020 hadi Mei 2022, shule ilikuwa ikitumia takribani shilingi milioni 10.5 kwa kila miezi mitatu kununua kuni. Baadaye walipoanza kutumia mkaa mbadala, gharama zilishuka hadi kufikia shilingi milioni 2.7 na hivi sasa, kupitia mradi wa matumizi ya gesi, shule imenunua tani moja ya gesi iliyotumika kwa miezi miwili, ambapo matumizi ni wastani wa shilingi milioni 1.3 kwa mwezi, kiwango ambacho ni nafuu zaidi kiuchumi.






































