HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

Oryx Gas Yazindua “Pishi la Kibabe” Ramadhan na Kwaresma

February 20, 2026 Add Comment
Katika kipindi hiki cha Ramadhan na Kwaresma kinachosisitiza ibada, mshikamano na kujitafakari, Oryx Gas Tanzania imezindua kampeni ya “Pishi la Kibabe” yenye lengo la kurahisisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia.

TVLA YATOA ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA CHANJO ZA MIFUGO KWA WAUZAJI WA PEMBEJEO SINGIDA

February 20, 2026 Add Comment

Meneja wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Kanda ya Kati, Dodoma, Dkt. Japhet Nkangaga (kushoto), akipokea changamoto mbalimbali zinazowakabili wafugaji kutoka kwa muuzaji wa pembejeo za mifugo Manispaa ya Singida, Bi. Ester Munuo, tarehe 19 Februari 2026 mkoani Singida, wakati wa ziara ya uhamasishaji kwa wauzaji wa pembejeo za mifugo iliyolenga kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya chanjo ya Matone (TEMEVAC) na taratibu za upatikanaji wa leseni za uuzaji wa viuatilifu vya rejareja na jumla.

RUWASA YAKUTANA NA WADAU KUJADILI MPANGO MKAKATI MIAKA MITANO IJAYO

February 20, 2026 Add Comment


Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imekutana na wadau wake wa ndani na nje ya nchi ikiwemo Wizara ya Maji na Benki ya Dunia katika kikao cha kujadili Mpangomkakati wa miaka mitano wa taasisi hiyo unaotoa mwelekeo wa vipaumbele vya kuimarisha huduma endelevu ya Maji safi ya bomba kwa wakazi wa maeneo ya vijijini katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Akifungua kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Februari 20, 2026, mwakilishi kutoka Wizara ya Maji Mha. Mashaka Sitta ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi wa Uendeshaji na Matengenezo alisema mwelekeo wa RUWASA kuelekeza nguvu zaidi katika kuimarisha huduma endelevu ya maji ni jambo muhimu kwa sasa kwani tayari imeshajenga miradi mingi vijijini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu wa RUWASA Titus Mkapa ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu Mha. Wolta Kirita aliwapongeza na kuwashukuru wadau wote wa maendeleo wanaoshirikiana na taasisi hiyo ambapo alisema baadhi ya vipaumbele katika kipindi cha miaka mitano ijayo ni pamoja na kuhakikisha huduma ya maji vijijini inakuwa imara na endelevu pamoja na kuimarisha eneo la data na takwimu.

Akitoa maelezo ya awali, Mkurugenzi wa Mipango wa RUWASA Enock Wagala alisema kuwa, nyaraka hiyo ya Mpangomkakati wa miaka mitano imeshapitia hatua tofauti za maandalizi na sasa inawasilishwa kwa wadau wa maendeleo hususan wa maji vijijini ili watoe maoni na michango yao katika kuboresha na kuwa sehemu muhimu ya mpangomkakati huo wakati wa utekelezaji wake.

Mkurugenzi Wagala alitaja maeneo makuu Matano ambayo yamepewa kipaumbele zaidi katika Mpangomkakati huo kuwa ni pamoja na uendelevu wa huduma ya maji vijijini, kujenga miradi katika vijiji 1575 vilivyobaki, kuimarisha mbinu za upatikanaji wa fedha, kukamilisha ujenzi wa miradi 878, na kujenga na kuimarisha huduma za usafi wa mazingira vijijini.

Takribani taasisi za wadau 40 walihudhuria kikao hicho ambapo baadhi ya wadau hao ni Wizara ya Maji, Benki ya Dunia, AfDB, Oikos ETS, Water Mission Tanzania, Global Water Center, TAWASANET, Water for Pepople, Netherland Development Organization, UNICEF, CRDB, World Vision Tanzania, Benki ya Equity, NMB, Global Water Partnership Tanzania na DPG WASH Secretariet.








WAKULIMA WA PAMBA WASHAURIWA KUACHA KILIMO CHA MAZOEA NA KULIMA KWA TIJA ZAIDI

WAKULIMA WA PAMBA WASHAURIWA KUACHA KILIMO CHA MAZOEA NA KULIMA KWA TIJA ZAIDI

February 20, 2026 Add Comment
 

Wakulima wa zao la pamba mkoa wa Simiyu ambao ni wanachama wa Vyama vya Ushirika wameshauriwa kulima kwa tija kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kuepukana kilimo cha mazoea ambacho kinawapa hasara.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anamringi Macha katika Mkutano wa 8 Chama Kikuu Simiyu, SIMCU (2018) LTD, uliofanyika leo Februari 20, 2026 Wilayani Maswa Mkoa wa Simiyu, pia amewaahakikishia wakulima kuwa Serikali itaendelea kuwawezesha kwa kutoa rudhuku za mbolea, viuatilifu na kutafuta masoko ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

"Mkulima anapata kilo mia tatu za pamba kwa heka ni hasara na ni upotevu wa muda inabidi tutoke kwenye kilimo cha namna hii..." alisema Mhe. Macha

Akizungumza kwa niaba ya Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Consolata Kiluma, ambaye ni Naibu Mrajis - Uhamasishaji, amewasistiza wajumbe wa bodi za vyama vya Ushirika kuwa waadilifu na waaminifu katika kutekeleza majukumu, na kuwa wabunifu kuleta ushindani kwenye biashara kama kauli mbiu isemavyo "Ushirika ni Biashara" ili kuongeza mapato kwa maslahi ya wanaushirika na Wananchi kwa ujumla.

Aidha, Mrajis Msaidizi Mkoa wa Simiyu Godfrey Mpepo amesema Ushirika umeendelea kuimarika tangu kilipoanzishwa chama kikuu SIMCU Ltd mwaka 2018, ambapo awali vyama vya mkoa huo vilikuwa vikisimamiwa na SHIRECU chama kikuu kutoka mkoa wa Shinyanga.

Naye, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Shemsha Mohamed amewataka wajumbe wa Mkutano huo kuepuka na ubadhilifu wa fedha za wanachama jambo ambalo linarudisha Ushirika nyuma kimaendeleo.

Awali, akitoa taarifa ya Utendaji wa SIMCU(2018) LTD, Meneja Mkuu wa chama hicho, Mercy Atanazi alibainisha kuwa mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe 625 kati ya wajumbe 675 kutoka vyama wanachama 335.

 

WMA WATOA ELIMU KWA WAFANYABIASHARA KUHUSU MATUMIZI SAHIHI YA VIPIMO

February 20, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAKALA wa Vipimo (WMA) wameendelea kuendelea kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu matumizi sahihi ya mizani na vipimo badala ya kutumia nguvu katika utekelezaji wa sheria kwa wale ambao wanakaidi agizo.

BALOZI WA CANADA APONGEZA UENDESHAJI WA BARRICK BULYANHULU

February 20, 2026 Add Comment

       


Balozi wa Canada nchini , Mheshimiwa Emily Burns akiangalia moja ya vifaa vilivyo chini ya mgodi alipotembelea sehemu ya chini ya mgodi (underground) kwenye mgodi wa Barrick Bulyanhulu , wa kwanza kushoto ni Meneja Mkazi wa Barrick nchini, Dkt. Melkiory Ngido.

DKT.MATARAGIO AZUNGUMZA NBC DODOMA

February 19, 2026 Add Comment


📌Waweka mikakati ya kuwawezesha wawekezaji wazawa katika sekta ya Mafuta na Gesi.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia, Dkt. James Mataragio, amefanya kikao na uongozi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) leo tarehe 19 Februari 2026 jijini Dodoma. 


Kikao hicho kililenga kujadili namna ambavyo Wizara ya Nishati na NBC wanavyoweza kushirikiana katika kuwawezesha wawekezaji wazawa, hususan katika sekta ya mafuta na gesi.

Dkt. Mataragio ameipongeza NBC kwa utayari wake wa kuwainua wawekezaji wazawa, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kukuza uchumi wa nchi, hasa kupitia sekta ya nishati. Ameeleza kuwa wapo wadau wengi wazawa wenye nia ya kuwekeza katika mafuta na gesi, lakini wanakumbwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo ukosefu wa mitaji wezeshi ya kutekeleza miradi hiyo.



“Ujio na ushirikiano wenu utasaidia kuwainua wawekezaji wazawa ili waweze kumudu na kuwekeza kikamilifu hapa nchini,” amesisitiza Dkt. Mataragio.


Aidha, ameongeza kuwa Serikali inatamani kuona wawekezaji wazawa wanajenga viwanda, kuanzisha biashara, na kuajiri vijana ili kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira nchini. Pia alibainisha kuwa sekta ya nishati inapaswa kuwa na mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa taifa, huku wawekezaji wazawa wakichukua nafasi muhimu katika maendeleo ya sekta hiyo.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa NBC anayeshughulikia wateja wakubwa na Serikali, Bw. Elvis Ndunguru, amesema benki hiyo imekuwa ikitoa mikopo kwa wawekezaji wadogo na wakubwa ili kusaidia kukuza biashara zao.


Benki ya Taifa ya Biashara  imekuwa ikishirikiana na Serikali na taasisi mbalimbali kutoa huduma za kifedha kwa wawekezaji, hasa katika sekta za kilimo, uvuvi na ufugaji. Sisi kama NBC tupo tayari kushirikiana na Wizara ili kufikia malengo ya Serikali ya kuwawezesha wawekezaji, hususan wazawa,” amesema Ndunguru.


Wizara ya Nishati na NBC zimekubaliana kufanya kazi kwa pamoja ili kuwainua wawekezaji wazawa katika sekta ya nishati kwa lengo la kukuza uwekezaji wa ndani, kutengeneza ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi nchini. 


Ushirikiano huo unatarajiwa kuleta matokeo chanya katika maendeleo ya sekta ya nishati nchini na kusaidia utekelezaji wa malengo ya Serikali ya kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wananchi kwa ujumla.

MAKAMU MWENYEKITI INEC NA WAJUMBE WA TUME WAMTEMBELEA RC SONGWE

February 19, 2026 Add Comment
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk leo Februari 19, 2026 akiwa na Mjumbe wa Tume, Mhe. Dkt. Zakia Mohamed Abubakar wamemtembelea  ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Omari Makame. 

Viongozi hao wa Tume wapo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ambapo wametembelea na kukagua maandalizi ya Uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Shiwinga, Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoani Songwe unaotarajiwa kufanyika Februari 26, 2026.




KAMATI YA BUNGE YAITA WAWEKEZAJI UJENZI WA VITUO VYA GESI ASILIA ILIYOSHINDILIWA (CNG)

February 19, 2026 Add Comment


📌 *Yapongeza kasi ya Serikali ujenzi wa vituo vya CNG*


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, kupitia Mwenyekiti wake Mhe. Subira Mgalu, imetoa wito kwa wawekezaji kuunga mkono Serikali katika ujenzi wa  vituo vya gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi katika Jiji la Dar es Salaam na mikoa mingine ikiwemo Morogoro na Dodoma.


Wito huo umetolewa  tarehe 19 Februari 2026 wakati Kamati hiyo ilipotembelea Kituo Mama cha Gesi Asilia Iliyoshindiliwa (CNG) kilichopo eneo la Mlimani jijini Dar es Salaam.

“Tumeona Serikali tayari ina mpango wa kuongeza ujenzi wa vituo hivi kutokana na uhitaji wa wananchi kuendelea kuongezeka pamoja na unafuu unaopatikana ukitumia CNG kwenye vyomvbo vya usafiri kama vile magari na bajaji, kwani gharama zinapungua kwa asilimia 40 ukilinganisha na mafuta. Hii hii ni fursa kwa sekta binafsi kushirikiana na Serikali kujenga vituo vingi zaidi,” amesema Mhe. Mgalu

Aidha, kamati hiyo imetoa wito kwa Serikali kufunga mfumo wa CNG katika magari yake,  jambo litakalosaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa vyombo hivyo vya usafiri.


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini pia imeipongeza Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)  kwa uwekezaji inaoufanya katika ujenzi wa vituo vya CNG na kupelekea vyombo vya usafiri vipatavyo 15,000 kutumia CNG.

Vilevile, imepongeza  shughuli za utafiti na uendelezaji wa gesi asilia zinazoendelea; ikisema kuwa upatikanaji wa gesi asilia ya kutosha  utawezesha kuendelea kuboresha huduma nyinginezo ikiwemo kupikia majumbani na viwandani.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema tangu kuanza kwa vituo vya CNG nchini, Serikali imekuwa ikiona tija yake na ndiyo maana  inaongeza kasi ya usogezaji wa huduma  hiyo kwa wananchi kwa kuhusisha pia sekta binafsi mfano ukiwa ni uzinduzi wa hivi karibuni wa kituo cha CNG cha Puma kilichopo Salasala ambacho kwa Afrika ndicho kituo kikubwa.

Amesema Serikali pia katika mwaka huu wa fedha imeagiza magari makubwa matano yatakayobeba gesi asilia iliyoshindiliwa na kuisambaza katika vituo vilivyopo katika maeneo ya mbali  ikiwemo Dodoma, Morogoro, Arusha na Tanga, lengo likiwa ni kuhakikisha huduma hiyo inapatikana kutoka eneo moja kwenda jingine.


Kuhusu kubadilisha mfumo wa magari ya Serikali kwenda kwenye CNG, ameeleza kuwa, tayari Serikali imeanza kufanyia kazi suala hilo na moja ya vielelezo ni mabasi mapya ya mwendo kasi ambayo yote yanatumia mfumo wa CNG, jambo ambalo limefanya utoaji wa huduma kwa abiria kuboreka.

Kituo cha CNG Mlimani kina uwezo wa kujaza gesi asilia kwenye magari 1,200 kwa siku huku kikiwa na pampu maalum tatu kwa ajili ya kujaza magari maalum ya kusafirisha CNG kwenda kwenye vituo vidogo vya kujaza gesi kwenye magari (Offline CNG Filling Stations), viwandani, katika taasisi na majumbani.

AKWILAPO AONGOZA MAWAZIRI KIKAO CHA KUTATUA CHANGAMOTO ZA MASHAMBA YA UWEKEZAJI MUHEZA

AKWILAPO AONGOZA MAWAZIRI KIKAO CHA KUTATUA CHANGAMOTO ZA MASHAMBA YA UWEKEZAJI MUHEZA

February 19, 2026 Add Comment





Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Leonard Akwilapo (wa pili kulia) akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga. Wa pili kushoto ni Waziri wa TAMISEMI Prof Riziki Shemdoe na kulia ni Naibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji Dkt. Pius Chaya na Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Ayubu Sebabili.

Na Munir Shemweta, WANMM MUHEZA

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Leonard Akwilapo amewaongoza Mawaziri wenzake wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na Ofisi ya Raisi Mipango na Uwekezaji katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

Kikao hicho kimefanyika tarehe 18 Februari 2026 katika ofisi ya Mkuu wa wilaya Muheza mkoa wa Tanga ikiwa ni utekelezaji wa masuala yaliyojitokeza wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba.

Mawaziri hao ni Prof. Riziki Shemdoe, Waziri wa TAMISEMI na Dkt. Pius Chaya, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji ambao kupitia kikao hicho, kilichohusisha pia wataalamu, viongozi hao walipata fursa ya kuwahoji wananchi walioguswa na migogoro hiyo ya mashamba ya uwekezaji ambayo yaliyofutiwa umiliki mwaka 2016.

Mashamba hayo ni Azimio/ Kilapula Geiglitz, Bwembwera, Kibaranga, Kihuhwi, Lewa pamoja na Saguras yaliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Prof. Riziki Shemdoe (Wa pili kushoto) akizungumza katika kikao cha kujadili utatuzi wa migogoro ya mashamba ya uwekezaji katika wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga.

TFS YAJIPANGA KUIMARISHA HUDUMA KWA WANANCHI NA MAZINGIRA BORA YA KAZI KWA VIJANA

February 19, 2026 Add Comment

 

Morogoro, Februari 19, 2026 — Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo, amewataka viongozi na makamanda wa vituo vya wakala huo kubadili mtazamo wa uongozi kwa kusikiliza wananchi, kuwaelewa vijana wa ajira mpya na kusimamia migogoro ya rasilimali kwa busara, akisisitiza kuwa ofisi za umma hazina kisingizio cha kuchelewesha majibu kwa wananchi.

Akizungumza leo katika siku ya pili ya Mkutano wa Nne wa Viongozi na Makamanda wa Vituo vya TFS unaoendelea katika Ukumbi wa Hoteli ya Kate, Morogoro, Prof. Silayo alisema mabadiliko ya kijamii na kimazingira yanailazimu TFS kuwa na fikra pana zaidi na mbinu mpya za uongozi na utatuzi wa changamoto.

“Serikali imeweka mwelekeo wa kuwasikiliza wananchi. Hivyo, kila kiongozi wa TFS kwa nafasi yake anapaswa kuwa tayari kusikiliza, kujibu na kutatua changamoto zinazoletwa mezani. Ofisi ni ya Serikali; haijalishi ulikuwepo au hukuwepo wakati tatizo linaanza,” alisisitiza.

Prof. Silayo alisema TFS inapaswa kuendana na kasi ya mabadiliko ya kijamii yanayoathiri mitazamo ya vijana wanaoajiriwa sasa, akibainisha kuwa kizazi kipya kina matarajio tofauti kuhusu mazingira ya kazi.

“Leo kijana anaajiriwa akiwa tayari na matarajio maalum. Hatuwezi kuwachukulia kama wasikilizaji tu; tunapaswa kuwaheshimu, kuwaongoza na kuwajengea motisha,” alisema, akihimiza viongozi wa vituo kuwa tayari kupokea mawazo mapya na kuimarisha mazingira ya kazi yanayozingatia utu na heshima.

Akizungumzia athari za mabadiliko ya tabianchi na shinikizo la kijamii, Prof. Silayo alisema ongezeko la mahitaji ya rasilimali linaweza kuchochea migogoro kati ya wananchi na hifadhi, hivyo akawataka viongozi kusimamia hali hiyo kwa weledi.

Alitoa mfano wa baadhi ya wananchi wanaochoma misitu kwa lengo la kujikinga dhidi ya wanyamapori waharibifu, akisema hatua hizo ni matokeo ya “mikakati ya kuishi” inayotokana na msongo wa kimazingira.

“Hatuwezi kupuuza dalili hizi. Ni lazima tuwafikie wananchi, tuwasikilize na tushirikiane nao kabla madhara hayajawa makubwa,” alisema.

Alibainisha kuwa migogoro haiwezi kuepukika kabisa, bali kinachopaswa kusimamiwa ni kiwango chake na namna ya kuimudu kwa ustahimilivu na majadiliano ya wazi.

Kamishna alisisitiza umuhimu wa kushirikiana na mamlaka za wilaya, mikoa pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama katika operesheni na doria maalum, akisema ushirikiano huo husaidia taasisi kuwa na sauti na ulinzi mpana hata pale maofisa wake wanapokosekana.

Alionya dhidi ya tabia ya kuahirisha utekelezaji wa maazimio ya mikutano, akitaka kila azimio liwe na majibu na hatua za utekelezaji kwa wakati.

“Haiwezekani tuwe na azimio la mwaka mzima halafu leo hatuna jibu. Tatizo linaweza kuwa la mfumo, lakini lisiwe la uzembe wa utendaji,” alionya.

Mkutano huo wa siku tano unajadili utekelezaji wa maazimio ya mwaka uliopita, changamoto za kiutendaji katika vituo vya TFS na mikakati ya kuimarisha uhifadhi endelevu wa misitu na nyuki sambamba na kushirikisha michezo (TFS Bonanza) ambayo vyote vimepewa kaulimbiu ya “One Team, One Dream”.

Akihitimisha hotuba yake, Prof. Silayo alitangaza rasmi kuanza kwa shughuli za siku ya pili ya mkutano huo, akiwataka viongozi hao kutumia fursa hiyo kubadilishana uzoefu na kuimarisha mshikamano katika kusimamia rasilimali za misitu kwa manufaa ya taifa.