HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

MKENDA AITAKA COSTECH KUPIMA ATHARI YA MIAKA 40 KATIKA MAENDELEO

July 02, 2026 Add Comment
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ameutaka uongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kufanya tathmini ya kina ya mchango wake katika kipindi cha miaka 40 iliyopita badala ya kujikita katika kusherehekea mafanikio.

DKT. NCHIMBI: MASLAHI YA TAIFA YATANGULIZWE KATIKA USIMAMIZI WA MAZINGIRA

July 02, 2026 Add Comment
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza la Taifala Hifadhi na Usimamizi Mazingira (NEMC) wakati alipofanya ziara MakaoMakuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo tarehe 02 Julai 2026.

*************


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasihi watumishi wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), kufanya kazi kwa bidii, weledi, ushirikiano nakujiepusha na vitendo vya rushwa ili kuifanya Taasisi hiyo kuwa chachu yauhifadhi wa mazingira na maendeleo ya Taifa.

Makamu wa Rais ametoa wito huo, alipofanya ziara Baraza la Taifa la Hifadhina Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Makao Makuu, Mikocheni Jijini Dar es Salaam. Amewataka watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na kutokuwakikwazo katika utekelezaji wa miradi mikubwa kwa kutanguliza maslahi yaTaifa mbele.

Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa kutimiza miaka 40 tangukuanzishwa kwake na kuendelea kuwa chombo kinachohitajika nakutumainiwa nchini.

Aidha, Makamu wa Rais ameipongeza NEMC kwa Mpango Mkakati wa miakaMitano ambao umeanisha vitu mbalimbali vitakavyowezesha usimamizi nautunzanji wa mazingira kwa ufanisi.

Amesema uanzishwaji wa mashindano yauhifadhi wa mazingira ni muhimu kwa kuwa itakua hamasa ya upandaji mitina usafi kitaifa.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ili kudhibiti masuala ya uchafu ni vema pia kuwatambua wanaokuwa wamefanya vibaya katika mashindano ya usafi nakuwataja hadharani ikiwemo kupatiwa vyeti.

Ameiagiza Ofisi ya Makamu waRais, Muungano na Mazingira, kushirikiana na NEMC katika kufanikishamashindano ya usafi na utunzaji mazingira nchini.

Halikadhalika Makamu wa Rais, ameitaka NEMC kutilia mkazo suala la nishatisafi, matumizi ya teknolojia za kisasa katika kulinda mazingira pamoja nakusimamia vema suala la urejerezaji taka.

Makamu wa Rais, amewapongeza Viongozi wa NEMC kwa kuendelea namchakato wa kuifanya NEMC kuwa Mamlaka kamili. Amesema suala hilolinashughulikiwa na katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita limepewaumuhimu wa kipekee.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Emmaculate Sware amesema NEMC imeaandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano yaani mwaka 2026/2027 – 2030/2031 ambao umelenga kuongeza ufanisi wa usimamizi wa mazingira, kuimarisha matumizi ya teknolojia za kidijitali, kuimarisha ukaguzi nautekelezaji wa sheria pamoja na kuchochea uchumi wa kijani na ustahimilivuwa mabadiliko ya tabianchi.

Ziara hiyo imehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais(Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Masauni pamoja na Katibu Mkuu Ofisiya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Emmaculate Swaremara baada ya kuzungumza na Viongozi na Watumishi wa Baraza hilo,alipofanya ziara Makao Makuu ya NEMC, Mikocheni Jijini Dar es Salaam leotarehe 02 Julai 2026.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu waBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Dkt. EmmaculateSware pamoja na Watumishi waliofanya kazi pamoja na Makamu wa Raiswakati akifanya kazi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira(NEMC). Picha hiyo imepigwa mara baada ya Makamu wa Rais kukamilishaziara aliyoifanya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mikocheni Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 02 Julai 2026. 


MTATIFIKOLO ASEMA SABASABA NI JUKWAA LA BIASHARA NA MAENDELEO

Kajunason July 02, 2026 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu

IRINGA – Mbunge wa Jimbo la Ismani, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo, amezindua rasmi maonesho na sherehe za Sabasaba zinazofanyika katika Kata ya Ilolo Mpya, Tarafa ya Pawaga, wilayani Ismani, huku akiwataka wananchi kutumia maonesho hayo kujifunza, kufanya biashara na kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Mtatifikolo alisema maonesho ya Sabasaba ni fursa muhimu kwa wananchi kukutana, kubadilishana uzoefu, kuuza na kununua bidhaa mbalimbali pamoja na kujifunza fursa za maendeleo kutoka kwa washiriki na wageni wanaotoka maeneo mbalimbali nchini.


Aliwahamasisha wananchi wa Kata ya Ilolo Mpya na Jimbo la Ismani kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika shughuli hizo, akieleza kuwa mbali na burudani, maonesho hayo yana mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wananchi na kuimarisha mahusiano ya kijamii.

"Mnatakiwa kutumia maonesho haya kama jukwaa la kujifunza, kufanya biashara na kujenga mahusiano yatakayochochea maendeleo ya Ismani na wananchi wake," alisema Mtatifikolo.

Mbunge huyo pia aliwataka vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani.



Aidha, aliwahimiza wazazi na walezi kuendelea kuwalea watoto katika misingi ya maadili, uzalendo na uwajibikaji ili kujenga kizazi kitakachochangia maendeleo ya taifa.

"Malezi bora ndiyo msingi wa kujenga taifa lenye vijana wenye nidhamu, uzalendo na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi," alisisitiza.

Maonesho hayo ya Sabasaba yanajumuisha shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi, zikiwemo maonesho ya bidhaa, michezo ya mpira wa miguu, ngoma za asili pamoja na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.



Waandaaji wa maonesho hayo wamesema lengo ni kutoa fursa kwa wananchi kuonesha bidhaa na huduma zao, kuhamasisha biashara ndogondogo na kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo na sanaa.

Sherehe hizo hufanyika kila mwaka baada ya wananchi kumaliza shughuli za uvunaji, zikiwa sehemu ya kuimarisha mshikamano wa jamii, kuchochea biashara na kutoa burudani kwa wakazi wa Ismani na maeneo jirani.

Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo walieleza kufurahishwa na maandalizi ya maonesho hayo, wakisema yameendelea kuwa kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Jimbo la Ismani.

UKAGUZI WA VIBALI VYA ARDHI WAWANASA WAWEKEZAJI WANAOKWEPA KODI ZANZIBAR

July 02, 2026 Add Comment


📌_*Kamisheni ya Ardhi, ZRA na ZAECA yaweka kambi Nungwi kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi katika mahoteli.*_


📌_*Ukaguzi waongeza ukusanyaji wa mapato na kuwezesha utoaji wa mikataba ya ardhi kwa wawekezaji.*_


Kamisheni ya Ardhi Zanzibar kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA), imefanya ziara maalumu ya ukaguzi wa vibali vya ardhi kwa wawekezaji wa mahoteli katika Shehia ya Banda Kuu, Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kubaini ukiukwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi na kuhakikisha ukusanyaji wa kodi ya ardhi unaimarishwa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kaskazini A, Dkt. Farid Mohammed Haji @faridhaji_ , aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya Laila Burhan Ngozi, amesema ukaguzi huo umelenga kubaini wawekezaji wanaokiuka masharti ya umiliki wa ardhi, ikiwemo kutolipa kodi ya ardhi kwa Serikali.

Amesema ukaguzi huo umezaa matokeo chanya baada ya kuwabaini baadhi ya wawekezaji ambao hawakuwa wametekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi, hatua iliyowezesha mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi Zanzibar, Mussa Kombo, amesema ukaguzi huo ni sehemu ya mkakati wa Kamisheni wa kuhakikisha wawekezaji wote wanatekeleza wajibu wao wa kulipa kodi ya ardhi kwa wakati na kuzingatia masharti ya umiliki wa ardhi. Ameeleza kuwa zoezi hilo pia limechangia kuongeza mapato ya Serikali kupitia malipo ya kodi ya ardhi, sambamba na utoaji wa mikataba ya ardhi kwa baadhi ya wawekezaji ambao hapo awali hawakuwa na mikataba hiyo.


Amesisitiza kuwa utoaji wa mikataba hiyo utaimarisha uwazi na uhalali wa umiliki wa ardhi, huku ukichangia usimamizi bora wa rasilimali za ardhi Zanzibar na kuhakikisha sheria za ardhi zinaendelea kuheshimiwa na kutekelezwa ipasavyo.

TAASISI 300 KUFUNGIWA MIFUMO YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA 2026/2027

July 02, 2026 Add Comment



Katika juhudi za kuhakikisha kuwa Tanzania inafikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo 2034, Serikali katika mwaka wa fedha 2026/2027 itasambaza mifumo ya nishati safi ya kupikia katika taasisi 300 zinazolisha watu zaidi ya 100.


Hayo yamesemwa na Mtaalam kutoka Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, Wizara ya Nishati, Bw. Omari Khalifa wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (SabaSaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwl.Nyerere jijini Dar es Salaam.


Khalifa amesema mpango huo utatekelezwa katika bajeti ya mwaka huu wa fedha kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambapo jumla ya shilingi bilioni 15 ambazo ni fedha za ndani zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo.


Ameeleza kuwa mifumo itakayofungwa inajumuisha gesi ya LPG, majiko banifu, mkaa mbadala pamoja na majiko ya umeme kwa lengo la kuboresha huduma za upishi, kulinda mazingira na kuimarisha afya ya watumiaji.


Katika utekelezaji wa mpango huo kampuni mbalimbali zinazotoa huduma ya mifumo ya nishati safi ya kupikia zitafaidika kupitia fursa zitakazotangazwa na REA huku taasisi hiyo ikisimamia usimikaji wa mifumo hiyo katika taasisi zitakazokidhi vigezo vilivyowekwa.



TTCL YAENDELEA KUWEKEZA KATIKA VITENDEA KAZI, YAKABIDHI MAGARI SITA

July 02, 2026 Add Comment


Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha mazingira ya kazi kwa kukabidhi magari sita (6) mapya yenye thamani ya Shilingi milioni 903 kwa Meneja wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Meneja wa Network Operations and Maintenance pamoja na Meneja wa Network Planning, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa shughuli za kiutendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.

MFUMO WA UAGIZAJI MAFUTA KWA PAMOJA WAIMARISHA UPATIKANAJI, UDHIBITI WA BEI NA MAPATO YA TAIFA

July 02, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (Petroleum Bulk Procurement Agency - PBPA) umesema mfumo wa uagizaji wa mafuta kwa pamoja umeendelea kuimarisha upatikanaji wa mafuta nchini, kudhibiti mfumuko wa bei, kuhakikisha ubora wa mafuta na kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

VISUKUKU MIMEA VYATOA MWANGA KATIKA UTAFITI WA MAFUTA NA GESI ASILIA NCHINI

July 02, 2026 Add Comment


Dar es Salaam

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu mchango wa sayansi ya visukuku mimea (Palynology) katika utafiti wa mafuta na gesi asilia kupitia Banda la TPDC kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).


Mtafiti Mwandamizi wa Visukuku Mimea wa TPDC, Bw. Johanes Kakoki, alisema uchambuzi wa visukuku mimea kama dinoflagellates ( viumbe vidogo sana vya majini aina ya planktoni) , chavua (pollen) na mbeguchembe (spores) husaidia kubaini umri wa miamba na uwezo wake wa kuzalisha na kuhifadhi mafuta au gesi asilia.


Aliongeza kuwa taarifa hizo huunganishwa na tafiti za kijiolojia, kijiofizikia na kijiokemia ili kuongeza usahihi wa kubaini maeneo yenye rasilimali za mafuta na gesi, huku teknolojia za kisasa zikiboresha ufanisi wa tafiti na kupunguza gharama.


Kupitia maonesho hayo, TPDC inaendelea kuelimisha wananchi kuhusu hatua za utafiti wa mafuta na gesi asilia na mchango wa tafiti za kisayansi katika maendeleo ya sekta na uchumi wa Taifa.


*#Tunaboreshamaishanakuwezeshamaendeleo*

KABUDI: USAFI WA MAZINGIRA SASA NI AJENDA YA KIMKAKATI YA MAENDELEO YA TAIFA

KABUDI: USAFI WA MAZINGIRA SASA NI AJENDA YA KIMKAKATI YA MAENDELEO YA TAIFA

July 02, 2026 Add Comment

KATIKA  hatua inayoashiria mabadiliko ya kimkakati katika usimamizi wa mazingira nchini, Serikali imeweka bayana mwelekeo mpya wa kuimarisha usafi wa mazingira kama nyenzo muhimu ya kupunguza magonjwa, kuongeza tija ya kiuchumi na kuharakisha maendeleo ya miji na vijiji.

Mkakati huo umeibuliwa jijini Dodoma leo July 2,2026 katika Kongamano la Kitaifa la Usafi wa Mazingira lililoambatana na uzinduzi wa mwongozo wa mpango jumuishi wa usimamizi wa huduma za usafi wa mazingira, ambalo limeweka msisitizo mpya wa kuunganisha huduma za usafi katika mfumo mmoja jumuishi unaolenga kuwafikia wananchi wote bila kuacha makundi yaliyo pembezoni.

Akizungumza katika kongamano hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Profesa Palamagamba Kabudi,amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira kuwa agenda ya kimkakati inayohitaji utekelezaji wa kisera, kitaasisi na kijamii kwa pamoja.

Amesema usafi wa mazingira sasa hautazamwi tena kama shughuli za kawaida za kijamii, bali ni sekta yenye mchango wa moja kwa moja katika afya ya umma, ustahimilivu wa miji na ukuaji wa uchumi.

Prof.Kabudi amesisitiza kuwa mkakati wa sasa unalenga kuhakikisha huduma jumuishi za usafi wa mazingira zinaimarishwa ili kupunguza tofauti za upatikanaji kati ya mijini na vijijini, pamoja na kuongeza ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji na utupaji taka.

“Tunajenga mfumo ambao unafanya usafi wa mazingira kuwa huduma ya msingi inayofika kwa kila Mtanzania,” amesema Kabudi.

Ameongeza kuwa mafanikio ya mkakati huo yanategemea mabadiliko ya tabia kwa wananchi sambamba na uwekezaji katika miundombinu ya kisasa ya usafi wa mazingira.

Aidha, ametumia kongamano hilo kumpongeza Rais Samia kwa kuendelea kuongoza ajenda ya nishati safi ya kupikia, akisema ni sehemu muhimu ya mkakati mpana wa kulinda mazingira na kupunguza uchafuzi unaotokana na nishati chafu.

Katika hoja ya kiufundi, Kabudi ameonya juu ya kuendelea kwa tabia ya utupaji taka kwenye mitaro ya maji ya mvua, akisema vitendo hivyo vinadhoofisha mifumo ya miji na kuongeza hatari ya mafuriko na magonjwa ya mlipuko.

Amesisitiza kuwa uwekezaji katika usafi wa mazingira ni sehemu ya mkakati wa taifa wa kulinda afya ya umma na kupunguza gharama za matibabu zinazotokana na magonjwa yanayohusiana na mazingira.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Fedha wa EWURA, Stanley Mahembe,aliyemwakilishi Mkurugenzi Mkuu amesema bado kuna pengo kubwa la kitaasisi katika usimamizi wa majitaka, akibainisha kuwa ni mamlaka 24 pekee kati ya 84 ndizo zilizo na mipango ya matibabu ya majitaka na tope la kinyesi.

Amesema hali hiyo inaonyesha umuhimu wa kuharakisha utekelezaji wa mwongozo mpya wa usimamizi wa mazingira uliozinduliwa katika kongamano hilo.

Naye  Naibu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya EWURA, Ngosi Mwihava, amesema kupitia bajeti ya shilingi trilioni 1.12 iliyopitishwa kwa ajili ya Wizara ya Maji, kuna matumaini makubwa ya kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya maji taka na usafi wa mazingira, ili kuendana na lengo la Maendeleo Endelevu (SDG) namba 6 linalohusu upatikanaji wa maji safi na usafi wa mazingira kwa wote.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, Kunti Majala, amesema  changamoto za mazingira zinaendelea kuchangia vifo vinavyoweza kuzuilika, hivyo kuhitaji mkakati wa elimu na usimamizi kuimarishwa zaidi.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, amesema ongezeko la kasi la watu katika mji wa Dodoma linahitaji mkakati madhubuti wa usafi wa mazingira unaoendana na ukuaji wa mji huo.

Kongamano hilo ni sehemu ya utekelezaji wa dira mpya ya taifa ya kuimarisha mifumo ya usafi wa mazingira, kwa lengo la kujenga miji salama, yenye afya na endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.