HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

FCC YASISITIZA UMUHIMU WA KUJUA HAKI NA WAJIBU WA MLAJI

FCC YASISITIZA UMUHIMU WA KUJUA HAKI NA WAJIBU WA MLAJI

March 20, 2026 Add Comment

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

....

TUME ya Ushindani (FCC) kanda ya Nyanda za Juu Kusini  imetoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa mpana ili waweze kufanya maamuzi sahihi wanaponunua na kutumia bidhaa mbalimbali  ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Akitoa elimu hiyo Mkoani Njombe, Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) Nyanda za Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga, amesisitiza umuhimu wa kila mlaji kufahamu haki zake za msingi.alieza kuwa haki hizo ni pamoja na kupata bidhaa bora, kupata taarifa sahihi kuhusu bidhaa, pamoja na haki ya kulalamika pale mlaji anapodhulumiwa.

Aidha, Bw. Mbanga ameeleza madhara makubwa yatokanayo na matumizi ya bidhaa bandia, akibainisha kuwa bidhaa hizo zinaweza kusababisha athari za kiafya, kupoteza fedha, na kudhoofisha uchumi wa nchi. Amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii zao ili kupunguza matumizi ya bidhaa hizo hatarishi.

“FCC imesisitiza kuwa elimu hii ni endelevu na inalenga kuwafikia makundi mbalimbali ya jamii ili kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi.”amesema Bw. Mbanga

Kwa ujumla, mafunzo hayo yameacha alama chanya kwa wanafunzi wa FDC Njombe, ambapo wengi wao wameeleza kuwa elimu hiyo imewafungua macho na kuwapa nguvu ya kusimamia haki zao kama walaji, huku wakiahidi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia nchini.

Kupitia mafunzo hayo, walikumbushwa kuwa mlaji ana nafasi kubwa katika kulinda afya yake na uchumi wa taifa kwa kuchagua bidhaa zilizo salama na zenye ubora unaokubalika.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Mkuu wa Kanda ya Tume ya Ushindani (FCC) - Nyanda ya Juu Kusini, Bw. Dickson Mbanga,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

  Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC Bw.Anderson Lwiza,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani 2026.

Sehemu ya wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Njombe (FDC) Mkoani Njombe wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia yaliyotolewa  na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YAIPONGEZA SERIKALI KUWAWEZESHA KIUCHUMI WAISHIO NA VVU

March 20, 2026 Add Comment





Na Mwandishi wetu- DAR ES SALAAM


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ambaye pia ni Mbunge wa

Arumeru Magharibi Mhe. Johannes Lukumay ameipongeza  Serikali kuendelea kusaidia kundi la Watu waishio na Maamubikizi Virusi vya 

UKIMWI kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujikwamua kiuchumi.


Mhe. Lukumay ameyasema  hayo tarehe 19 Machi 2026 mara baada ya ziara ya kutembelea Baraza la Watu waishio na maambukizi ya Virusi vya  UKIMWI akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika ( Konga ya Jiji) iliyofanyika   katika Viwanja vya Pugu Mnadani Jijini Dar es Salaam.

 Amesema kuwa watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ni sawa na watu wengine hivyo yapaswa kuwapa kipaumbele katika fursa mbalimbali za kimaendeleo.



Pia Mwenyekiti huyo amelipongeza kundi hilo kwa namna

wanavyojituma katika kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini hivyo  kuziagiza  sekta husika kusaidia katika kuwatafutia masoko kwa ajili ya bidhaa zao.




Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wataendelea kuunga mkono jitihada zao kwa kuongeza nguvu zaidi kwa Wanakonga ili waweze kujikwamua kiuchumi.



Mhe. Nderiananga amempongeza Mkurugenzi wa Jiji, Mkuu wa Wilaya pamoja na Katibu Tawala wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na timu nzima kwa kuwawezesha Wanakonga katika fursa mbalimbali na kuwataka kuendelea na desturi hiyo ya kuwawezesha kwani mwaka huu wa fedha bado haujamalizika.



Aidha  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Elihuruma Mabelya amesema kuwa moja ya eneo waliloliwekea nguvu ni Konga hiyo kwa kuunga mkono shughuli zao za  kiuchumi ili kuhakikisha

wanainuka na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali za maendeleo.





N


UDOM, UNICEF WALETA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KONDOA

UDOM, UNICEF WALETA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KONDOA

March 20, 2026 Add Comment
 

Msimamizi Mkuu wa Mradi, Dkt. Jabhera Matogoro, akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Mdami, wakikagua matumizi ya huduma mtandao darasani kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Amani Abeid Karume iliyopo WIlayani Kondoa.

....

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kwa kushirikiana na UNICEF Tanzania, kimeanza kufungua ukurasa mpya wa maendeleo ya kidijitali katika Wilaya ya Kondoa, mkoani Dodoma, kupitia mradi wa kusambaza huduma ya intaneti kwa shule na jamii.

Katika ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo iliyofanyika leo Alhamisi, tarehe 19 Machi 2026, ikiongozwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Mdami, imeelezwa kuwa hatua kubwa tayari imefikiwa.

Msimamizi wa mradi huo, Dkt. Jabhera Matogoro, amesema vituo 10 tayari vimeunganishwa na huduma ya intaneti ya kasi ya 20Mbps, ikijumuisha shule tano za sekondari na Msingi, na vituo vitano vya jamii, hatua inayotarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika upatikanaji wa taarifa, ujinzaji na ufundishaji.

Ameeleza kuwa mradi huo unalenga kuwezesha walimu, wanafunzi na wananchi kwa ujumla kupata maarifa kwa urahisi kupitia mtandao, sambamba na kuchochea fursa za ajira, ubunifu wa kibiashara na maendeleo ya kijamii katika wilaya hiyo.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akibadilishana mawazo na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kondoa, Bi. Sekela Mwasubila, kuhusu utekelezaji wa mradi wa Huduma ya Mtandao inayotolewa kwa shule 5 na ofisi 5 za Kata.

Miundombinu ya teknolojia ya mawasiliano ya mawimbi ya microwave inayotolewa na kampuni ya Airtel, ikisambaza huduma ya intaneti yenye kasi ya Mbps 20, kupitia Mradi unaofadhiliwa na UNICEF.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Bukulu, Mwl. Joseph Paul, akieleza namna huduma ya mrandao inavyorahisisha ujifunzaji katika maabara ya kompyuta shuleni hapo.

Mkuu wa Shule ya Msingi Isabe, Mwl. Jackline Richard, akizungumza wakati wa ukaguzi wa maendeleo ya mradi wa kusambaza huduma ya mtandao kwa shule na jamii.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Joseph, akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Amani Abeid Karume kuhusu fursa za kujifunza kidijitali, wakati wakikagua huduma ya mtandao imavyofanya kazi shuleni hapo na kusaidia wanafunzi kujifunza.

Msimamizi Mkuu wa Mradi, Dkt. Jabhera Matogoro, akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Bi. Rose Mdami, wakikagua matumizi ya huduma mtandao darasani kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Amani Abeid Karume iliyopo WIlayani Kondoa.

Msimamizi Mkuu wa Mradi, Dkt. Jabhera Matogoro, akitoa maelezo kuhusu utendaji wa teknolojia ya intaneti katika moja ya vituo vilivyonufaika na mradi huo, Chama cha Ushirika cha Mawasiliano.

MHE.MAKAMBA ASHIRIKi UFUNGUZI WA AWALI POWERINH AFRICAN SUMMIT LEO JIJINI WASHINGTON DC

March 19, 2026 Add Comment

 



Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Salome Makamba akiwa ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Else Sia Kanza wameshiriki katika ufunguzi wa awali wa Powering African Summit leo, Machi 19, 2026 jijini Washington Dc.

Mkutano huu wa siku mbili unawakutanisha viongozi wa Serikali, wawekezaji na wadau wa sekta ya nishati kujadili mustakabali wa nishati barani Afrika, fursa za uwekezaji, pamoja na suluhisho endelevu kwa maendeleo ya sekta hiyo.

Katika mkutano huo, Naibu Waziri ameambatana na wataalam kutoka TANESCO, PURA pamoja na REA ambao watashiriki kwenye majadiliano kuhusu upatikanaji wa umeme kwa wote, uwekezaji katika ‘Energy Mix’ pamoja na usimamizi na maendeleo endelevu ya rasilimali za gesi na mafuta.




TRA DODOMA YATOA MKONO WA EID KWA WATOTO YATIMA, YAIMARISHA UPENDO NA MSHIKAMANO

March 19, 2026 Add Comment

 

Kaimu Meneja wa Mkoa wa TRA Dodoma, Bw. Obrey Sillayo, akiambatana na Kaimu Meneja wa Huduma kwa Mlipakodi pamoja na maafisa wengine wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wametoa mkono wa Eid Fitri kwa watoto yatima na wenye mahitaji maalumu katika Kituo cha Kulelea Watoto Yatima Rahmani, ikiwa ni sehemu ya kuonesha upendo na kuimarisha mshikamano na jamii.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Bw. Sillayo amepongeza juhudi za kituo hicho kwa kulea watoto katika misingi bora ya maadili na malezi, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwajali watoto hao kwa ustawi wa taifa.

Aidha, ameeleza kuwa TRA itaendelea kushiriki katika shughuli za kijamii kama sehemu ya kuwajibika kwa jamii na kujenga uhusiano mzuri na wananchi.

Kwa upande wake, Bi. Rukia Hamisi Abdallah ameishukuru TRA kwa mkono huo wa Eid, akieleza kuwa umeleta faraja na matumaini kwa watoto wanaolelewa katika kituo hicho.

Tukio hilo limeacha ujumbe wa upendo, mshikamano na uwajibikaji kwa jamii.







RIPOTI YA EWURA : MOSHI, NZEGA, BIHARAMULO MAMLAKA BORA ZAIDI ZA MAJI NCHINI

RIPOTI YA EWURA : MOSHI, NZEGA, BIHARAMULO MAMLAKA BORA ZAIDI ZA MAJI NCHINI

March 19, 2026 Add Comment

Mamlaka za maji na usafi wa mazingira za Moshi, Nzega na Biharamulo zimetwaa tuzo za mamlaka bora nchini, katika tathmini ya ripoti ya EWURA ya utendaji wa mamlaka za maji iliyozinduliwa na Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Hamidu Aweso (Mb) leo tarehe 19 Machi 2026, mjini Morogoro.

Aidha, mamlaka 27 zilitambuliwa kwa kuwasilisha kwa asilimia 100 tozo ya udhibiti.

Taarifa ya hiyo ya Tathmini imepima Utendaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira 83 zinazotoa huduma katika mikoa, wilaya na miji midogo , katika hafla iliyofanyika mjini Morogoro.

Waziri Aweso ameipongeza EWURA kwa kuandaa taarifa hiyo muhimu iliyobainisha uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika utoaji huduma za maji na usafi wa mazingira nchini.

Kwa mujibu wa EWURA, tathmini hiyo imeonesha mafanikio katika ongezeko la uzalishaji wa maji kwa 19.3%, wateja kufikia milioni 1.8 na mapato kuongezeka kwa 14%. Hata hivyo, changamoto kama upotevu wa maji (42.3%) na uhaba wa miundombinu ya majitaka bado zinaendelea.

Mhe. Aweso amezitaka mamlaka za maji kuendelea kuboresha huduma kwa kuzingatia ubora, uwazi na uendelevu.

TUNAIMARISHA UZALISHAJI NA USAMBAZAJI UMEME KUKIDHI MAHITABI YA UCHUMI UNAOKUA-MHANDISI MRAMBA

March 19, 2026 Add Comment


New Delhi, India


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, ameieleza Jumuiya ya kimataifa kuwa Tanzania inaendelea kuchukua hatua za kimkakati kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usimamizi wa umeme ili kukidhi mahitaji ya uchumi unaokua kwa kasi.


Amesema hayo katika mkutano wa Bharat Electricity Summit 2026 unaofanyika nchini India.


" Tanzania  inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kuzalisha, usafirishaji na usambazaji umeme, lengo letu ni kuhakikisha nchi inakuwa na umeme wa kutosha kwa ajili ya matumizi ya kijamii na kukidhi mahitaji ya kiuchumi ambayo yanazidi kukua kwa kasi, kielelezo cha hatua tunazochukua ni pamoja na utekelezaji wa mradi wa umeme jua wa Kishapu wenye uwezo wa megawati 150, ambao awamu yake ya  kwanza imekamilika na kuzalisha  megawati 50." Amesema Mhandisi  Mramba

Aidha, ametaja mradi wa umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) wenye uwezo wa megawati 2,115 kuwa ni nguzo muhimu katika kuongeza uzalishaji wa umeme wa uhakika nchini.


 Katika kufanikisha utekelezaji wa miradi ya nishati, Mhandisi Mramba amesema Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi  kama sehemu ya mkakati wa kuharakisha maendeleo ya sekta hiyo.


Vilevile amesema kuwa, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya njia za kusafirisha umeme pamoja na kuunganisha gridi ya taifa na nchi jirani,  hatua inayotarajiwa kuongeza usalama wa nishati kupitia biashara ya umeme ya kikanda.


Katika mkutano huo Mhandisi Mramba  amesisitiza umuhimu wa maboresho ya gridi (grid modernisation) pamoja na matumizi ya teknolojia za smart grid, akieleza kuwa Tanzania tayari imeanza safari ya kuelekea katika mifumo hiyo ili kuongeza ufanisi, uthabiti na usalama wa huduma ya umeme.


Vilevile amegusia suala la nishati jadidifu linavyozidi kuwa sehemu muhimu ya mfumo wa umeme akitanabaisha kuwa kuna haja kwa taasisi za mipango na mashirika ya umeme kuimarisha uwezo wa kiufundi na kiutendaji ili kuendana na mabadiliko ya mfumo huo wa kisasa.


Mkutano huo umewakutanisha viongozi na wataalam wa sekta ya nishati kutoka mataifa mbalimbali duniani kujadili mikakati ya kuimarisha mifumo ya umeme, kukuza ushirikiano wa kikanda na kuendeleza matumizi ya teknolojia za kisasa katika sekta hiyo.

ELIMU YA KUMLINDA MLAJI YATOLEWA  KATIKA SHULE YA MSINGI BUNGE

ELIMU YA KUMLINDA MLAJI YATOLEWA KATIKA SHULE YA MSINGI BUNGE

March 19, 2026 Add Comment

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

....

TUME ya Ushindani (FCC) leo Machi 19,2026 imetoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa awali kuhusu umuhimu wa kuchagua na kutumia bidhaa zilizo salama, huku ikisisitiza kuwa walaji wana nafasi kubwa katika kulinda afya zao na za wengine.

Mafunzo hayo pia yameenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani, tukio linaloadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji duniani kote.

Kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho hayo ni “Bidhaa Salama, Imani kwa Mlaji,” ikisisitiza umuhimu wa kuhakikisha bidhaa zote zinazotumiwa na wananchi zinakidhi viwango vya usalama na ubora.

Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC, Thecla Kitosi, amewahamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wazuri wa elimu hiyo kwa jamii zinazowazunguka.

Aidha Bi.Kitosi amewaasa wanafunzi hao kuelewa haki zao kama walaji, pamoja na wajibu wao wa kutoa taarifa kwa FCC wanapobaini au kuwa na mashaka kuhusu usalama wa bidhaa au huduma wanazotumia.

Hata hivyo amewahimiza wanafunzi kuwa mabalozi wazuri kwa jamii zao kwa kuwafahamisha wazazi na ndugu zao juu ya hatari za bidhaa bandia na namna ya kuzitambua.

"FCC itaendelea kutoa   elimu kwa makundi mbalimbali ya jamii, hususan wanafunzi, ni njia muhimu ya kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa, wanaoweza kujilinda dhidi ya bidhaa bandia na huduma zisizo na ubora."amesisitiza Bi.Kitosi

Kwa upande wake Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine, amieleza kuwa bidhaa bandia zinaweza kuwa na athari kubwa kiafya, kiuchumi na hata kijamii. Alifafanua kuwa baadhi ya bidhaa hizo, hususan vipodozi, dawa na vifaa vya umeme, vinaweza kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji kutokana na kutokidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa.

“Ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuwa makini na bidhaa tunazonunua. Hakikisheni mnachunguza nembo za ubora na kununua bidhaa kutoka kwa wauzaji wanaoaminika,” amesisitiza Bi. Diana.

Kwa upande wao, wanafunzi walionesha shauku kubwa kwa kuuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia. Walishukuru kwa elimu hiyo na kuahidi kuitumia ipasavyo katika maisha yao ya kila siku.

Elimu hii ni sehemu ya juhudi za FCC za kuendelea kulinda haki za mlaji pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama na zenye ubora unaokubalika, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

 Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

   

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Maafisa kutoka Tume ya Ushindani(FCC) wakiwa katika picha ya pamoja na  Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Bunge  mara baada ya kukamilisha utoaji wa elimu kwa wanafunzi kuhusiana masuala ya kumlinda mlaji.