HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

UMEME KUBADILISHA MAISHA YA WANANCHI VITONGOJINI

July 15, 2026 Add Comment
Serikali imedhamiria kubadilisha maisha ya wananchi vitongojini kupitia usambazaji wa umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na wananchi wamehimizwa kuchangamkia kuunganishiwa umeme kwenye vitongoji vilivyofikiwa.

MHE.KILAKALA AIPONGEZA WIZARA YA NISHATI KWA KUENDELEA KUTOA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 15, 2026 Add Comment




Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, ameipongeza Wizara ya Nishati kwa kuandaa Warsha ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wanahabari na Maafisa habari, akisema mafunzo hayo ni hatua muhimu ya kuhakikisha elimu sahihi inawafikia wananchi na kuimarisha utekelezaji wa ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.


Akizungumza Julai 14, 2026 wakati wa ufunguzi wa Warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari, Maafisa Mawasiliano Serikalini wa Mikoa, Taasisi, Wizara pamoja na Taasisi zilizo  chini ya Wizara ya Nishati kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya nishati safi ya kupikia inayofanyika katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro amesema Mkoa wa Morogoro una vyanzo vingi vya maji vinavyopaswa kulindwa, hivyo ajenda ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia itasaidia kuhifadhi mazingira kwa kupunguza ukataji wa miti, kulinda afya za wananchi pamoja na kutunza vyanzo hivyo vya maji kwa manufaa ya kizazinkijacho.



Amesema elimu inayotolewa kupitia warsha hii ikiwafikia wananchi kwa usahihi, itasaidia kuongeza uelewa kuhusu maana na faida za nishati safi ya kupikia, hususan kwa jamii za vijijini, jambo litakalowezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika juhudi za kulinda mazingira na kutumia nishati salama na nafuu.


Mhe. Kilakala amewataka washiriki kutoka Mikoa mbalimbali nchini kutumia maarifa waliyoyapata katika warsha hiyo kwa weledi mkubwa wanaporejea kwenye maeneo yao ya kazi kwani mafunzo haya yataongeza hamasa na kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na elimu ya nishati safi ya kupikia na hivyo kuchangia kufikiwa kwa malengo ya taifa ya kuhakikisha asilimia 80 ya wananchi wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo 2034.

*ELIMU YA UMEME NA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA WANANCHI ARUMERU MASHARIKI*

July 15, 2026 Add Comment



📌*Umeme sasa ni Kitongoji kwa Kitongoji*

📌*Nishati safi ya Kupikia kwa kila mwananchi*

📍*Arusha*

Wananchi wa Wilaya ya Arumeru Mashariki mkoani Arusha wameendelea kupata elimu kuhusu huduma za umeme na matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia ziara ya uhamasishaji iliyofanywa na maafisa wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Elimu hiyo ilitolewa leo wakati maafisa wa REA walipotembelea baadhi ya vijiji na vitongoji vinavyotekelezwa miradi mbalimbali ya nishati, ikiwemo miradi ya usambazaji wa umeme katika vitongoji pamoja na uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kama vile gesi na majiko banifu.

Katika ziara hiyo, wananchi walipatiwa elimu kuhusu taratibu za kufanya maombi ya kuunganishiwa umeme, gharama za uunganishaji wa huduma hiyo pamoja na tahadhari ya kujiepusha na matapeli maarufu kama vishoka, ambao huwalaghai wananchi kwa kuwatoza fedha kinyume na utaratibu rasmi.

Aidha, wananchi walihimizwa kujiunga na huduma ya umeme wakati mkandarasi bado yupo katika eneo la mradi, kwani hatua hiyo hurahisisha upatikanaji wa huduma kwa gharama nafuu. Walielezwa kuwa Serikali tayari imegharamia ujenzi wa miundombinu ya kufikisha umeme katika maeneo yao, hivyo mwananchi anabaki na jukumu la kuweka mfumo wa waya (wiring) ndani ya nyumba na kulipia gharama ya kuunganishiwa umeme ya shilingi 27,000 tu.

Maafisa wa REA pia waliwahimiza wananchi kutumia umeme kwa shughuli za uzalishaji mali ili kuongeza kipato na kuboresha maisha yao. Walisisitiza kuwa dhana ya “Kijijini kama Mjini” inapaswa kutekelezwa kwa vitendo kupitia matumizi ya umeme katika biashara, viwanda vidogo, huduma za kijamii na shughuli nyingine za maendeleo, badala ya kubaki kuwa nadharia.

Vilevile, wananchi walikumbushwa umuhimu wa kutunza miundombinu ya umeme kwa kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi hiyo. Walihimizwa kushiriki kulinda miundombinu hiyo na kutoa taarifa kwa mamlaka husika pindi wanapoona vitendo vinavyoweza kuhatarisha au kuharibu huduma ya umeme.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za REA za kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu huduma za umeme na matumizi ya nishati safi ya kupikia, ili kuongeza matumizi ya nishati hizo na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika maeneo ya vijijini.

*Mwisho.*




 

KAMATI YA KITAIFA YA UFUNGAJI MIGODI YAKAGUA MPANGO WA UFUNGAJI MGODI WA BARRICK BULYANHULU

July 15, 2026 Add Comment
Meneja wa Mahusiano ya Jamii wa Barrick Bulyanhulu, Agapit Paul, akitoa maelezo kuhusu shughuli za uendeshaji wa mgodi kwa wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Ufungaji Migodi (NMCC) wakati wa ziara yao ya kikazi mgodini.

SHERIA BORA NI MSINGI WA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050 – MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

July 15, 2026 Add Comment
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amefungua mafunzo ya tatu ya Bespoke kwa Mawakili wa Serikali, yalioandaliwa na kuratibiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambayo yameanza tarehe 15 Julai, 2026 na yatahimishwa tarehe 17 Julai, 2026 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano Arusha (AICC) Jijini Arusha.

OSHA YATAJWA MIONGONI MWA TAASISI ZA KIMKAKATI NCHINI

July 15, 2026 Add Comment
Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Usimamizi Rasilimali Watu katika Taasisi za Umma-Ofisi ya Msajili wa Hazina, Bw. Hussein Kakurwa, akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Bodi ya Ushauri katika mafunzo elekezi ya Bodi ya OSHA yaliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, Kibaha Mkoani Pwani.

WANAHABARI NI WASHIRIKA MUHIMU WA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 15, 2026 Add Comment




Naibu Waziri wa Nishati amesema vyombo vya habari na maafisa mawasiliano Serikalini ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kutokana na nafasi yao ya kufikisha taarifa sahihi kwa wananchi na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni pamoja na majukwaa ya kidijitali.


Hayo ameyabainisha leo Julai 14, 2026 wakati akifungua Warsha ya Kuwajengea Uwezo Waandishi wa Habari na Maafisa Mawasiliano Serikalini kutoka katika Wizara na Taasisi  kuhusu Uandishi na Uhamasishaji wa Masuala ya Nishati Safi ya Kupikia, inayofanyika katika ukumbi wa Morena hoteli mkoani Morogoro.

Amesema vyombo vya habari si wasambazaji wa taarifa pekee bali ni washirika muhimu wa maendeleo ya Taifa kwa kutoa taarifa sahihi huku akibainisha kuwa kupitia habari, vipindi vya redio na televisheni, makala pamoja na maudhui ya kidijitali, wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga uelewa wa wananchi, kuondoa dhana potofu na kuhamasisha mabadiliko chanya ya tabia kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia  kwani katika zama za mawasiliano ya kidijitali, taarifa moja sahihi inaweza kuwafikia mamilioni ya wananchi ndani ya muda mfupi na kuleta mabadiliko makubwa katika jamii.

Amefafanua kuwa, taarifa zisizo sahihi zinaweza kusababisha upotoshaji na kuchelewesha utekelezaji wa ajenda muhimu za maendeleo akimnukuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) uliofanyika jijini Arusha, amesema watu wanaweza kushiriki kubomoa Tanzania, lakini hawawezi kusaidia kuijenga hivyo amesisitiza kuwa wanahabari wana wajibu wa kutumia kalamu na keybord zao kuandika habari zenye ukweli, zenye kujenga matumaini na kuunga mkono juhudi za maendeleo ya Taifa badala ya taarifa zinazoweza kupotosha wananchi.

Aidha Mhe. Salome ameeleza kuwa, matarajio ya Serikali ni kuwa mafunzo hayo yatawaongezea washiriki maarifa na ujuzi wa kuandaa habari zenye usahihi, ushahidi na weledi wa hali ya juu, pamoja na kuandaa maudhui yanayoonesha mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia, ubunifu wa sekta binafsi na fursa zilizopo katika mnyororo wa thamani wa sekta hiyo.

Ameongeza kuwa warsha hiyo itawajengea uwezo washiriki kuhusu sera, mikakati na mwelekeo wa Serikali katika sekta ya nishati safi ya kupikia, matumizi sahihi ya takwimu pamoja na namna bora ya kuripoti kuhusu teknolojia mbalimbali zinazopatikana nchini ili kuandaa taarifa zenye ubora na zinazojenga uelewa wa wananchi.


Aidha, amewataka washiriki kutumia kikamilifu fursa ya mafunzo hayo kujenga ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati, Idara ya Habari MAELEZO, washirika wa maendeleo, sekta binafsi na vyombo vya habari, akisisitiza kuwa mawasiliano sahihi ni nguzo muhimu ya kufanikisha ajenda ya nishati safi ya kupikia na kufikia lengo la asilimia 80 ya matumizi ifikapo mwaka 2034.



USHIRIKIANO WA ORYX GAS NA SKAUTI KUCHOCHEA MATUMIZI SALAMA YA NISHATI SAFI

July 15, 2026 Add Comment


Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Tanzania imezindua kitabu cha Mwongozo wa Matumizi Salama ya Gesi ya LPG na kusaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu na Chama cha Skauti Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha elimu ya matumizi salama ya gesi ya kupikia kwa wananchi kupitia mtandao wa vijana wa Skauti nchini.

NAIBU WAZIRI SALOME AWASILI MOROGORO KUFUNGUA WARSHA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

July 15, 2026 Add Comment

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala, akiwasili katika Ukumbi wa Morena Hotel mkoani Morogoro kwa ajili ya kufungua warsha ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari pamoja na Maafisa Mawasiliano wa Serikali kuhusu uandishi na uhamasishaji wa masuala ya Nishati Safi ya Kupikia.

Warsha hiyo imeandaliwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji (UNCDF), kupitia Mradi wa CookFund unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Salome ameambatana na Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia wa Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Nishati, Bi. Nteghenjwa Hosseah na Meneja wa Mradi wa CookFund – UNCDF, Bw. Imanuel Muro.




LINDI KUENEZA ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA WOTE

July 15, 2026 Add Comment







📌 Majiko banifu 5,776 kusambazwa mkoani Lindi




Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, amesema Mkoa wa Lindi umeanza kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ikiwa ni sehemu ya juhudi za kufikia lengo la kitaifa la kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Bi. Omary amesema hayo leo, Julai 15, 2026, alipokutana na Afisa Mshauri Mwandamizi wa Masuala ya Kiufundi kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Deusdedit Malulu, aliyeambatana na uongozi wa Kampuni ya Tango Energy Limited, inayotekeleza usambazaji wa majiko banifu mkoani Lindi.

“Nawapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Tunamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na tutaendelea kutoa elimu ili iwafikie wananchi wote,” amesema Bi. Omary.

Kwa upande wake, Mha. Malulu amesema jumla ya majiko banifu 5,776 yameanza kusambazwa na Kampuni ya Tango Energy Limited katika maeneo ya Lindi, Ruangwa, Nachingwea, Liwale na Kilwa.

Mha. Malulu amewataka wananchi katika maeneo hayo kuchangamkia fursa ya kupata majiko banifu kwa bei nafuu ya ruzuku ya shilingi 7,600 tu kwa jiko.

Naye, Meneja wa Mauzo wa Tango Energy Limited, Bw. Emmanuel Ibrahim, amesema mradi huo unahusisha usambazaji wa majiko banifu yanayotumia kiasi kidogo cha kuni na mkaa, hatua inayolenga kupunguza matumizi ya vyanzo hivyo vya nishati pamoja na athari za moshi unaotokana na matumizi ya majiko ya kawaida.

Kupitia mradi huo, Tango Energy Limited itasambaza jumla ya majiko banifu 5,776 kwa wananchi kwa bei ya ruzuku. Bei halisi ya jiko moja ni TZS 50,847.46, lakini Serikali imetoa ruzuku ya asilimia 85, hivyo mwananchi atanunua jiko kwa TZS 7,600 tu.


















WAZIRI KOMBO APOKEA RASMI KOMBE LA USHINDI WA WANADIPLOMASIA DHIDI YA WABUNGE KATIKA BONANZA LA CRDB

July 15, 2026 Add Comment
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Mahmoud Thabit Kombo leo Julai 14, 2026 amekabidhiwa rasmi kombe kutoka kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Ngwaru Maghembe linalotokana na ushindi wa timu ya Wanadiplomasia katika Bonanza Kuu la Bunge la Benki ya CRDB lililofanyika tarehe 20 Juni 2026 katika Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.

ZAIDI YA WAKAZI 5,000 BABATI WAFURAHIA MAJISAFI MRADI WA BILIONI 1.9

July 15, 2026 Add Comment
Zaidi ya wananchi 5,000 kutoka vijiji vitatu vya kata ya Endamaghaay, Wilaya ya Babati mkoani Manyara, wameanza kunufaika na mradi wa maji safi na salama ulitekelezwa na wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) uliolenga kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji wenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilion 1.9.

Wanufaika waipongeza kambi ya matibabu Arusha

July 15, 2026 Add Comment
Na mwandishi wetu Arusha.

Zaidi ya wananchi 8,000 kutoka Mkoa wa Arusha na maeneo mengine nchini wamepata huduma za uchunguzi na matibabu bila malipo katika siku mbili za kwanza za kambi maalumu ya afya inayofanyika jijini Arusha.

EAC YAIMARISHA MFUMO WA KURAHISISHA BIASHARA ZA MIPAKANI

July 15, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,MKINGA

JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC) imeeleza itaendelea kuimarisha utekelezaji wa Mfumo Rahisi wa Biashara (Simplified Trade Regime-STR) ili kurahisisha biashara za mipakani, kuwawezesha wafanyabiashara wadogo kuongeza uzalishaji, kupanua masoko ya bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda na kupunguza gharama za biashara.


Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayeshughulikia Forodha, Biashara na Fedha, Annette Semuwamba, wakati alipotembelea Kituo cha Huduma cha Pamoja Mpakani (One Stop Border Post-OSBP) cha Horohoro wilayani Mkinga, mkoani Tanga.


Ziara hiyo ni sehemu ya tathmini ya utekelezaji wa Mfumo Rahisi wa Biashara katika vituo saba vya Huduma vya Pamoja Mpakani vilivyopo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Semuwamba alisema EAC itaendelea kushirikiana na nchi wanachama na wadau mbalimbali kuhakikisha wafanyabiashara wadogo wanaovuka mipaka wanapata mazingira rafiki kupitia taratibu rahisi za forodha.

“Tumefurahishwa kuona biashara kati ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inaendelea kukua. Kinachotutia moyo zaidi ni kwamba bidhaa nyingi zinazovuka mipaka ni bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda wetu,” alisema.

Alisema uwekezaji uliofanywa katika miundombinu ya vituo vya Huduma vya Pamoja Mipakani umechangia kupunguza muda wa kuhudumia mizigo na wasafiri, kupunguza gharama za biashara na kusaidia kushusha bei za bidhaa kwa walaji.

Aidha, aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa kufunga mashine ya kisasa ya ukaguzi wa mizigo (scanner) katika mpaka wa Horohoro/Lunga Lunga, akisema hatua hiyo itaharakisha ukaguzi na uondoshaji wa mizigo.

Semuwamba alipendekeza pia kuanzishwa kwa mfumo wa kubadilishana picha za mizigo iliyokaguliwa kwa kutumia mashine hizo kati ya vituo vya Huduma vya Pamoja Mipakani ili kupunguza gharama za uwekezaji wa vifaa hivyo katika maeneo mengine ya mipakani.

Awali, Mkuu wa Kituo cha Huduma cha Pamoja Mpakani Horohoro, Shadrack Mbonea, alisema kituo hicho kimechangia kwa kiasi kikubwa kurahisisha biashara na usafirishaji wa mizigo kati ya Tanzania na Kenya.

Alisema Horohoro ni miongoni mwa vituo saba vya Huduma vya Pamoja Mipakani nchini vinavyowezesha wasafiri, magari na mizigo kupata huduma zote za mipakani katika eneo moja badala ya kuhudumiwa kila upande wa mpaka.

“Kituo hiki kilianza majaribio ya utoaji wa huduma kwa mfumo wa One Stop Border Post mwezi Septemba 2021 na tangu wakati huo kimeendelea kufanya kazi kwa mafanikio makubwa,” alisema.

Mbonea alisema kituo hicho kina taasisi 19 za Serikali zinazoongozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), zikiwemo Idara ya Uhamiaji, Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), TASAC, Tume ya Madini, Idara ya Uvuvi, Idara ya Mifugo, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Alisema taasisi hizo zina jukumu la kukusanya mapato ya Serikali, kurahisisha biashara, kulinda jamii dhidi ya bidhaa hatarishi, kutekeleza sera za biashara, kukusanya takwimu za biashara za mipakani na kudhibiti magendo.

Kwa mujibu wa Mbonea, hapo awali mfumo wa OSBP ulikuwa ukifanya kazi kwa saa 12 kwa siku, hali iliyowalazimu wasafiri na wasafirishaji wa mizigo kukamilisha taratibu za forodha katika kila upande wa mpaka.

Alisema kupitia makubaliano kati ya Tanzania na Kenya, huduma sasa zinatolewa kwa saa 24, hatua iliyopunguza muda wa kusubiri na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma.

Aidha, alisema kituo hicho kinatekeleza Mfumo Rahisi wa Biashara unaowawezesha wafanyabiashara wadogo wanaosafirisha bidhaa zenye thamani isiyozidi dola za Marekani 2,000 kutumia taratibu rahisi za forodha.

“Tumeanzisha dawati maalumu la kuwahudumia wafanyabiashara wadogo, tumerahisisha utaratibu wa ukadiriaji wa kodi kwa kutumia fomu ya F88 na tunatambua Vyeti Rahisi vya Asili ya Bidhaa vinavyotolewa na mamlaka za Kenya,” alisema.

Aliongeza kuwa kituo hicho pia kinatekeleza Mfumo wa Himaya Moja ya Forodha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Single Customs Territory-SCT), ambao umechangia kupunguza muda wa uondoshaji wa mizigo, kushusha gharama za biashara na kuondoa vikwazo vya biashara ndani ya ukanda.

Alisema ushirikiano kati ya Horohoro na Lunga Lunga umeimarisha mapambano dhidi ya magendo kupitia doria za pamoja, mikutano ya kila robo mwaka na utoaji wa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu taratibu za biashara za mipakani.

Takwimu zinaonyesha kuwa thamani ya bidhaa zinazouzwa nje kupitia mpaka wa Horohoro/Lunga Lunga imeongezeka kutoka Sh milioni 306.4 mwaka wa fedha 2022/23 hadi Sh milioni 548 mwaka 2024/25. Aidha, thamani ya bidhaa zinazoingizwa nchini kupitia mpaka huo imeongezeka kutoka Sh milioni 134.7 hadi Sh milioni 175.9 katika kipindi hicho.

Ongezeko hilo linaakisi mafanikio ya juhudi za EAC na nchi wanachama katika kuimarisha biashara za mipakani, kuongeza ushindani wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya ukanda na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya.

MASWI: NGOS NI NGUZO MUHIMU YA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050

July 14, 2026 Add Comment
Julai 14, 2026 - Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Eliakim Maswi leo amekutana na wajumbe wa Baraza la Taifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NaCoNGO )pamoja na wawakilishi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ngazi za mikoa na wilaya.

MKURUGENZI MKUU REA APOKEA TUZO YA USHINDI WA REA SABASABA 2026

July 14, 2026 Add Comment




Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy, leo Julai 14, 2026, amepokea tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (Government Institutions Exhibitor), ambayo REA ilitwaa katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.


Tuzo hiyo imewasilishwa kwake na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya watumishi walioshiriki katika maonesho hayo.


Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mha. Saidy amewapongeza watumishi wa Wakala kwa juhudi, kujituma na ushirikiano wao ulioiwezesha REA kutwaa tuzo hiyo.


Aidha, amewataka watumishi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na ushirikiano katika kutekeleza miradi ya REA vijijini na vitongojini, ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na huduma za nishati na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.


Mwisho

TAFITI ZINAZOFANYWA NA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA ZINA MCHANGO MKUBWA KATIKA TAIFA

Kajunason July 14, 2026 Add Comment


 Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 9,2026.

........................ 

TAFITI zinazofanywa na Tume ya kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), zimekuwa na mchango mkubwa katika Taifa hasa katika kuanzishwa kwa sheria mpya.

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Kitengo cha Elimu ya Sheria kwa Umma Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Zainabu Chanzi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam Sabasaba Julai 9,2026.

‘’ Tafiti tunazozifanya zina mchango mkubwa katika taifa kwani baadhi zimeleta sheria na nyingine zilileta vifungu katika sheria,” alisema Chanzi.

Alisema hapo awali maendeleo ya kidijitali yalikuwa siyo makubwa lakini yalipokuja Tume hiyo ilifanya tafiti mwaka 2005 ambayo ilizaa sheria mbili, sheria ya miamala ya kielektroniki na makosa ya kimtandao.

“Hatukuwa na sheria hizo hivyo baada ya utafiti tulipendekeza Serikalini na ilitunga hizo sheria na ndiyo maana tunaona watu wana udhubutu wa kutuma hela kwa njia ya kimtandao bila ya kuwa na wasiwasi wowote kwa kuwa wanajua zipo sheria,” alisema Chanzi. 

Alisema mwaka 2020 Tume hiyo ilifanya tafiti kuhusiana na ulinzi wa taarifa binafsi kutokana na kuwa na umuhimu wake kama ambavyo zinavyolindwa katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisema katika kuendana na kidijitali Tume imetekeleza wajibu wake na inaendelea na utekelezaaji huo ambapo kwa sasa inafanya utafiti wa Akili Mnemba (AI)  na hayo yote ni mapinduzi yay a kidijitali na wao kama tume wanazifanya tafiti hizo na kuishauri Serikali iweze kuchukua hatua zinazofaa kulingana na jamii yetu.

Chanzi aliongeza kuwa wanaendelea kufanya tafiti na wanapozikabidhi sheria zimekuwa zikitungwa jambo ambalo wanajivunia.

“Tafiti tunazo zifanya siyo tu za kidijitali kwa mfano tulifanya teknolojia ya DNA ambayo zamani ilikuwa haipo lakini Tume ilifanya tafiti na kukabidhi ripoti na sheria ikatungwa na kwa kuwa tulikuwa na teknolojia lakini bila ya kuiwekea sheria ya kuisimamia ingeweza kusababisha yasipatikane matokeo chanya ambayo yangehitajika.

Chanzi amesema misingi ambayo waliiweka kwenye ripoti zao wameweza kuiona ipo ndani ya sheria na kuonesha jinsi gani mapendekezo wanayotoa yanavyochukuliwa na kufanyiwa kazi.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990. 

TRA KUWAZAWADIA VIJANA 1020 WENYE MAWAZO BUNIFU

July 14, 2026 Add Comment

 


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekuletea mashindano ya Wazo Bunifu yanayolenga kupata suluhisho za kibunifu zitakazochangia kuboresha mfumo wa kodi nchini. Hii ni fursa yako ya kuwasilisha wazo lenye tija na kushindania zawadi ya hadi Shilingi Milioni 50.

Mawazo yatakayowasilishwa yanapaswa kulenga eneo moja au zaidi kati ya yafuatayo ; kupanua wigo wa kodi, kurahisisha ukadiriaji na ulipaji wa kodi kwa biashara ndogo ndogo, kuimarisha huduma za kodi za kidijitali, kupunguza gharama za ukusanyaji wa mapato, kutumia teknolojia za kisasa kama AI, Big Data na Blockchain katika usimamizi wa kodi, pamoja na kuboresha utatuzi wa migogoro ya kodi ili kuwa wa haraka, wazi na wenye kuaminika zaidi.

Kutuma Wazo lako ingia tovuti ya TRA, Bonyeza kitufe cha innovation portal fuata hatua zinazofuata, Mwisho wa kutuma wazo lako bunifu ni julai 31, 2026.

MWISHO WA SHINDANO HILI NI MWEZI HUU WA 7 NI HATARII


RAIS DKT.MWINYI AJIONEA MAFANIKIO YA TANESCO MAONESHO YA SABASABA

July 14, 2026 Add Comment




📌 Miradi mipya ya kusafirisha umeme kuimarisha upatikanaji wa umeme Zanzibar


📌 Serikali yawekeza Dola za Marekani milioni 282 kuongeza upatikanaji wa umeme na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambapo amejionea mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya umeme na teknolojia mbalimbali zinazolenga kuboresha huduma kwa wananchi na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.


Katika ziara hiyo iliyofanyika Julai 13, 2026, Mhe. Dkt. Mwinyi alipata fursa ya kujionea miradi ya uzalishaji na usafirishaji wa umeme, teknolojia za matumizi bora ya umeme ikiwemo majiko sanifu yanayotumia umeme kwa ufanisi, huduma ya Luku Janja pamoja na mfumo wa Smart House unaomwezesha mtumiaji kufuatilia matumizi ya umeme kupitia simu ya mkononi.


Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa kujenga njia mpya tatu za kusafirisha umeme kutoka Tanzania Bara kwenda Zanzibar kupitia nyaya zitakazopita chini ya bahari.

Ameeleza kuwa njia hizo zitajumuisha Dar es Salaam–Unguja, Tanga–Pemba na Kisiju–Mafia, na kwamba kukamilika kwake kutaongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika na uwezo wa kuhudumia ongezeko la mahitaji ya umeme yanayotokana na ukuaji wa viwanda, sekta ya utalii, uwekezaji na shughuli nyingine za kiuchumi visiwani Zanzibar.

Bw. Twange amesema Serikali pia inaendelea kutekeleza mradi wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 282, ambapo Dola milioni 6 zimetengwa mahsusi kwa ajili ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea katika sekta ya umeme. Kupitia mradi huu wa Dola za Marekani milioni 282, tunaendelea kuimarisha miundombinu ya umeme, huku sehemu ya fedha hizo ikielekezwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme kwa kushirikiana na ZECO,” amesema Bw. Twange.


Aidha, amesema TANESCO imeendelea kuleta ubunifu wa kidijitali kupitia mfumo wa Smart House, unaomwezesha mwananchi kufuatilia matumizi ya umeme wa nyumba yake kupitia simu ya mkononi, hatua inayosaidia matumizi bora na yenye tija ya umeme.


Vilevile, Bw. Twange amesema mpango wa ukopeshaji wa majiko ya umeme umefikia mafanikio makubwa, ambapo zaidi ya asilimia 90 ya wananchi waliopata majiko hayo wanaendelea kuyalipia kwa utaratibu wa makato kupitia ununuzi wa umeme wa LUKU, hatua inayorahisisha wananchi kumudu gharama za kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.


Jitihada hizo ni sehemu ya utekelezaji wa maono ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme ya uhakika na kutumia nishati safi katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali, ikiwemo katika Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115, umeendelea kuweka msingi wa upatikanaji wa umeme wa kutosha unaowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

DG RUWASA AWAELEKEZA MAMENEJA WA MIKOA NA WILAYA KUZISHIRIKISHA CBWSOs KATIKA PROGRAMU ZOTE

July 13, 2026 Add Comment


Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Mha. Wolta Kirita, amesisitiza umuhimu wa kushirikisha Vyombo vya Utoaji wa Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (CBWSOs) katika mipango na programu zote zinazolenga kuboresha huduma za maji vijijini ili kuhakikisha huduma hizo zinakuwa endelevu na wananchi wanaendelea kunufaika na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali.

REA YANG'ARA SABASABA 2026

July 13, 2026 Add Comment




🏆 *RAIS MWINYI ASHUHUDIA REA IKITWAA TUZO YA MUONESHAJI BORA WA TAASISI ZA SERIKALI*


🤝 *REA YAWASHUKURU WADAU KWA MCHANGO WAO KATIKA MAFANIKIO HAYO*


📍 Dar es Salaam


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameshuhudia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ukitwaa Tuzo ya Muoneshaji Bora wa Taasisi za Serikali (*Government Institutions Exhibitor*) katika kilele cha Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) 2026.


Tuzo hiyo imepokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa REA, Bi. Martha Chassama, kwa niaba ya Wakala.


REA inawashukuru wadau wote waliotembelea banda lake, kujionea mafanikio na utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini, pamoja na kuendelea kuunga mkono jitihada za Wakala za kupeleka nishati ya umeme kwenye vitongoji. 


Mwisho

NEEC YALETA ELIMU YA MITAJI KARIBU NA WANANCHI RUKWA

July 13, 2026 Add Comment
Mafunzo ya utoaji wa elimu kuhusu fursa za mitaji kupitia mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi yanaendelea kufanyika katika Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, yakilenga kuwaongezea wananchi uelewa kuhusu fursa za kupata mitaji na huduma za maendeleo ya biashara ili kukuza shughuli za kiuchumi.

MHANDISI MRAMBA ATEMBELEA BANDA LA TANESCO SABASABA

July 13, 2026 Add Comment




Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati (Umeme na Nishati Jadidifu), Mhandisi Felchesmi Mramba, ametembelea Banda la Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), na kampuni zake Tanzu katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ambayo leo yanafikia kilele katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Mha.Mramba ametembelea banda hilo ili kuona huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi  wanaotembelea banda hilo.