HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

RAIS SAMIA KUWA MGENI RASMI MKUTANO MKUU WA MAMALISHE NA BABA LISHE JIJINI DAR

April 04, 2026 Add Comment

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano mkubwa wa kitaifa utakaowakutanisha wauzaji chakula (Mamalishe na Babalishe) kutoka mikoa yote nchini.

Mkutano huo umepangwa kufanyika Aprili 11, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Jumamosi Aprili 4,2026 jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Wauzaji Chakula nchini kupitia Umoja wa Mamalishe na Babalishe Tanzania (UMALITA), Avijawa Omari, amesema kuwa wanaiomba Serikali kuwatambua rasmi kama kundi muhimu katika uchumi wa nchi.

Amesema kuwa utambuzi huo utawawezesha wanachama kupata mikopo, fursa za kiuchumi na kukuza ajira kwa vijana na wanawake nchini.

“Tunaomba Serikali ituone rasmi. Utambuzi utarahisisha upatikanaji wa mikopo na kutupa nafasi ya kupanua biashara zetu ili tuzalishe ajira zaidi,” amesema.

Bi Omari ameongeza kuwa mkutano huo utakuwa jukwaa muhimu kwa mamalishe na babalishe kuwasilisha moja kwa moja changamoto zao kwa viongozi wa Serikali kwa lengo la kuongeza kipato, kupanua biashara na kuchangia ukuaji wa ajira nchini.

Aidha, amewataka wanachama na wauzaji chakula wote nchini kujitokeza kwa wingi Aprili 11 katika ukumbi wa JNICC ili kujenga kwa pamoja mustakabali wa biashara zao.

Mkutano huo utafanyika chini ya kaulimbiu “Pika Kishua, Vaa Kishua” (Cook Smart, Dress Smart), inayolenga kuboresha viwango vya utoaji huduma na kuimarisha taswira ya kitaalamu ya wauzaji chakula nchini.

“Sisi ni wajasiriamali tunaojitegemea, na tunalisha taifa asubuhi, mchana, jioni hadi usiku. Tunaomba jamii itambue mchango wetu na kuheshimu kazi tunayoifanya,” aliongeza.

Ameeleza pia kuwa sekta hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo hatari za kiafya na mazingira magumu ya kazi, lakini sasa wameanza kuelekea katika matumizi ya nishati safi na mbinu bora za upishi ili kulinda afya na kukuza biashara.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Babalishe, Ndugu Ngosha, amesisitiza umuhimu wa umoja na ushirikiano miongoni mwa wanachama ili kufikia malengo yao ya kiuchumi na kijamii.

Mkutano huo unatarajiwa kuwa wa kihistoria kwa kuwaunganisha wadau wakuu wa sekta isiyo rasmi na viongozi wa juu wa Serikali kujadili mustakabali wa ajira na ujasiriamali nchini.



DC MWANGA AZITAKA TAASISI ZOTE KUWEKA KIPAUMBELE KATIKA UPANDAJI MITI KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI

April 04, 2026 Add Comment


Wilaya ya Mwanga imeanza kuchukua hatua madhubuti katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, kufuatia wito wa Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Rukia Zuberi, aliyehimiza taasisi za serikali na sekta binafsi kupanda miti ya matunda na vivuli katika maeneo yao.


Wito huo umetolewa wakati wa zoezi la upandaji miti lililofanyika ofisini kwake, likiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha uhifadhi wa mazingira.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Rukia Zuberi alisisitiza kuwa upandaji miti si tukio la muda mfupi, bali ni jukumu endelevu linalohitaji ushirikiano wa kila mwananchi na kila taasisi.



Alieleza kuwa miti ina mchango mkubwa katika kulinda mazingira, kuhifadhi udongo, na kupunguza athari za ukame pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa ndani ya wilaya hiyo na taifa kwa ujumla.


Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya aliwahamasisha wananchi kutumia vizuri msimu wa mvua kwa kupanda miti na kuhakikisha wanaitunza hadi ikue. “Ni muhimu tuendelee kupanda miti na kuitunza kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho,” alisema, akiongeza kuwa kila mtu ana wajibu wa kulinda mazingira kwa vitendo badala ya maneno.


Katika hatua nyingine, Bi. Rukia Zuberi aliwataka wataalamu wa mazingira pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuendelea kusimamia na kuimarisha programu za upandaji miti ndani ya Wilaya hiyo na kuhakikisha miti hiyo inayopandwa inatunzwa.


Pia alizitaka taasisi zote za umma na binafsi kuiga mfano huo kwa kupanda miti katika maeneo yao ya kazi na makazi yao kuhakikisha miti inatunzwa ipasavyo.


Hata hivyo, Bi. Rukia Zuberi alisisitiza umuhimu wa kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika juhudi hizi ili kuifanya Mwanga kuwa wilaya ya kijani na mfano wa uhifadhi bora wa mazingira nchini. 


Alitoa wito kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga kuhakikisha inasimamia kwa karibu utekelezaji wa agizo hilo ili kuhakikisha matokeo chanya yanapatikana kwa maendeleo endelevu ya eneo hilo.

WMA YAIMARISHA UKAGUZI WA VIPIMO KUDHIBITI UFUNGASHAJI USIO SAHIHI

April 04, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) wamekamata magari mawili yaliyokuwa yamepakia mazao kwa kutumia magunia yenye uzito unaozidi kipimo kinachoruhusiwa, katika operesheni ya kushtukiza iliyofanyika katika masoko ya Ilala na Temeke, jijini Dar es Salaam.

TAIFA GESI YAHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI HANDENI

April 03, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga

Kampuni ya Taifa Gesi imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuunga mkono sera ya Serikali ya kuhamasisha matumizi ya nishati rafiki kwa mazingira.

Akizungumza katika tamasha lililofanyika wilayani Handeni, Mkurugenzi wa Masoko wa Taifa Gesi, Oscar Shelukindo, alisema kampuni hiyo imekuwa ikishiriki katika matamasha ya kijamii tangu mwaka jana kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya gesi safi.

Alisema kuwa katika tamasha hilo, wameelekeza nguvu zaidi kwa wakazi wa Handeni, hususan Kata ya Mdoe, ili kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwapa uelewa sahihi kuhusu faida za kutumia nishati hiyo.

“Tunafurahi kuwa hapa leo kutoa elimu ya matumizi ya gesi safi, kuondoa hofu kwa wananchi na kuwahamasisha kuachana na matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira. Pia tunatoa gesi kwa bei nafuu ili kuwavutia zaidi kuitumia,” alisema Shelukindo.

Alifafanua kuwa bado kuna wananchi wengi ambao wana hofu au uelewa mdogo kuhusu matumizi ya gesi ya kupikia, hali inayowafanya kuendelea kutumia nishati kama kuni na mkaa, ambazo si rafiki kwa mazingira na pia zina madhara kiafya.

Kwa mujibu wa Shelukindo, utoaji wa elimu hiyo unalenga kubadili mtazamo wa jamii na kuwasaidia wananchi kuelewa kuwa gesi ni salama, nafuu kwa muda mrefu na rahisi kutumia.

Aidha, alisisitiza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mchango wa sekta binafsi katika kusaidia juhudi za Serikali za kulinda mazingira, kupunguza ukataji wa miti na kuboresha afya za wananchi kupitia matumizi ya nishati safi.

Wananchi waliohudhuria tamasha hilo walipata fursa ya kuuliza maswali, kujifunza matumizi sahihi ya gesi pamoja na kununua bidhaa za gesi kwa bei iliyopunguzwa.

Kwa ujumla, jitihada za Taifa Gesi zinaonesha namna sekta binafsi inavyoweza kushirikiana na Serikali katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi, hatua inayotarajiwa kuleta mabadiliko chanya katika jamii, hususan maeneo ya vijijini.

TAIFA GAS HAITAONGEZA BEI YA GESI

April 03, 2026 Add Comment

Meneja Mkuu wa Taifa Gas nchini Devis Deogratius
Taifa Gas haitapandisha bei ya gesi ya majumbani (LPG) licha ya ongezeko la takribani asilimia 43 ya bei ya gesi hiyo duniani. Hatua hii ni sehemu ya juhudi za kampuni hiyo kuendeleza upatikanaji nafuu wa nishati hiyo pamoja na kupunguza za athari za mabadiliko ya soko la kimataifa kwa wateja wake.

MAFUNZO YA USALAMA WA NYUKLIA YAFUNGWA RASMI TANGA

April 03, 2026 Add Comment

Wataalamu kutoka Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) wamehitimisha mafunzo maalum ya ulinzi na usalama dhidi ya mionzi kwa wafanyakazi wa Maweni Limestone Company. Mafunzo haya, yaliyofunguliwa na Meneja wa Idara ya Ubora wa kampuni hiyo, yalilenga kuwajengea uwezo wafanyakazi wanaoshughulika moja kwa moja na vifaa vya X-Ray Fluorescence (XRF) na nuclear gauges.

Kwa muda wa siku kadhaa, washiriki walipata nafasi ya kujifunza kwa kina kuhusu utambulisho wa mionzi ayonishi, kiasi cha mionzi na vipimo, matumizi ya mionzi, athari zake kiafya, kanuni za ulinzi, mfumo wa kisheria wa Tanzania, majukumu ya Afisa Usalama wa Mionzi (RSO), pamoja na usalama wa nyuklia na udhibiti wa usafirishaji haramu.

Katika hotuba ya kufunga mafunzo, wataalamu wa TAEC walisisitiza umuhimu wa kuimarisha utamaduni wa usalama kazini. “Tunataka kuona kila mfanyakazi akibeba jukumu la kulinda afya yake, wenzake na jamii kwa ujumla. Usalama wa mionzi si jambo la hiari, ni wajibu wa kitaifa,” alieleza Ndugu Mungubariki Nyaki, mkufunzi na msimamizi wa Ofisi ya TAEC Jijini Tanga.

Washiriki walionekana wenye shauku na ari ya kupeleka maarifa mapya kazini. Baadhi walikiri kuwa mafunzo haya yamewapa ujasiri wa kushughulika na vifaa vya mionzi kwa umakini zaidi, huku wengine wakisisitiza umuhimu wa kushirikiana na TAEC ili kuhakikisha viwango vya kitaifa na kimataifa vinazingatiwa.

Mafunzo haya pia yaligusia hatua za dharura endapo ajali za mionzi zitatokea, jambo lililowapa washiriki uelewa wa namna ya kukabiliana na changamoto kwa utulivu na ufanisi.

Kwa ujumla, kufungwa kwa mafunzo haya kumeacha taswira ya matumaini na uwajibikaji. Kampuni ya Maweni Limestone imeonyesha dhamira ya dhati ya kulinda wafanyakazi wake na jamii kwa kuhakikisha teknolojia za kisasa zinatumika kwa usalama na kwa manufaa ya Taifa.





REA YANADI MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA KUSAMBAZA NISHATI VIJIJINI

April 02, 2026 Add Comment


Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeshiriki katika mahojiano maalum kujadili mafanikio na hatua za ujenzi wa Miradi ya Kusambaza Nishati maeneo ya Vijijini yaliyorushwa Mubashara kupitia Luninga ya ITV.


Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mha. Jones Olotu na Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala, Mha. Advera Mwijage wameshiriki katika mahojiano hayo Machi 2, 2026 Jijini Dar es Salaam ambapo walieleza bayana mafanikio na hatua mbalimbali zilizofikiwa za ujenzi wa Miradi ya Kusambaza Nishati Vijijini.

Awali akizungumza katika mahojiano hayo, Mha. Olotu amesema baada ya kuridhishwa na mafanikio ya REA, Serikali iliiongeza fedha na hivyo kuiwezesha kutanua wigo wa Miradi.


"Hadi sasa tumekamilisha Usambazaji umeme kwenye vijiji na tunaendelea na vitongoji. Tulianza na vijiji 506 na tukianza na maeneo ya kipaumbele ya Serikali ambayo yanatoa huduma ya moja kwa moja kwa wananchi ikiwemo makao makuu ya Wilaya, shule, vituo vya afya, visima vya maji," amesema Mha. Olotu.

Kwa upande wake Mha. Advera alisema REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya Nishati Safi ya Kupikia ili kutimiza dhamira ya Serikali ya asilimia 80 ya wananchi wawe wanaotumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo Mwaka 2034. 

Mha. Advera alizungumzia namna ambavyo REA inawezesha miradi mbalimbali ikiwemo ya kuzalisha umeme kwa Nishati ya maji na jua.

"Kwa sasa hivi tunayo miradi mingi inayoendelea kwenye upande wa ujenzi wa gridi ndogo, tumekwishajenga zaidi ya gridi ndogo 70. Zinatumia Nishati ya maji na Nishati ya jua," amesema. 

Amesema kuwa REA vilevile inawezesha wananchi maeneo ya visiwani kupata Nishati ya Umeme kwa lengo la kujiletea maendeleo.

"Tunao Mradi mkubwa ambao unatekelezwa katika visiwa na tunafunga mifumo 20,000 ya Umeme jua kwa hatua za awali kwa bei ya ruzuku: tumemjali Kila mwananchi kupata Nishati hiyo kulingana na kipato chake," amesema Mha. Advera.

Mahojiano hayo yalitoa fursa kwa Jukwaa la Wahariri (TEF) na wananchi kuuliza maswali, kutoa maono na kupongeza hatua zilizofikiwa.



NISHATI SAFI YA FUNGUA MILANGO YA FURSA KWA WATENGENEZA MAUDHUI

April 02, 2026 Add Comment

 



Na Mwandishi Wetu, Mwanza


Watengeneza maudhui nchini wamehamasishwa kutumia ubunifu wao kujipatia kipato kupitia fursa zitokanazo na nishati safi ya kupikia, kwa kuelimisha jamii kupitia kazi zao zikiwemo video za elimu, vichekesho, hadithi na kampeni mbalimbali zitakazowafikia wananchi kwa urahisi.


Wito huo umetolewa Aprili 1, 2026 jijini Mwanza na Mhandisi Nishati kutoka Wizara ya Nishati, Benezeth Kabunduguru, wakati akizungumza katika mafunzo kwa watengeneza maudhui (content creators).


 Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, huku Wizara ya Nishati ikiwa miongoni mwa wawezeshaji wakuu.

Amesema mafunzo hayo yamelenga kuwasaidia watengeneza maudhui kuboresha kazi zao kwa kuzingatia mbinu za kubiasharisha maudhui mtandaoni, kujenga chapa binafsi pamoja na kuzingatia masuala ya hakimiliki.

Kabunduguru ameeleza kuwa watengeneza maudhui wana nafasi kubwa ya kubadilisha mtazamo wa jamii kupitia ubunifu wao, akisisitiza kuwa maudhui yenye ubora na mvuto yanaweza kununuliwa na kuwapatia kipato waandaaji wake, sambamba na kusambaza ujumbe muhimu kwa jamii.

Aidha, amesema Serikali imeweka mkakati wa kuhakikisha ifikapo mwaka 2034 angalau asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia.

 Amebainisha kuwa suluhisho za nishati hiyo tayari zipo na zinaendelea kuwafikia wananchi, huku changamoto kubwa ikiwa ni upatikanaji wa taarifa sahihi kwa watu wengi zaidi.

Kutokana na hali hiyo, amewataka watengeneza maudhui kuchangamkia fursa hiyo kwa kuandaa kazi zitakazolenga kuelimisha kuhusu faida za nishati safi ya kupikia na madhara ya matumizi ya nishati zisizo safi.

Amesisitiza kuwa utoaji wa taarifa sahihi kwa jamii utachochea mabadiliko chanya yatakayoboresha maisha ya wananchi na kulinda afya za Watanzania.


&&&

BoT YASALIA NA RIBA YA MSINGI YA ASILIMIA 5.75 KWA TAHADHARI YA HATARI ZA KIMATAIFA

April 02, 2026 Add Comment

 Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeamua kuendelea kubakiza kiwango chake cha riba ya msingi ya ukopeshaji (benchmark lending rate) katika asilimia 5.75 kwa robo ya pili ya mwaka huu, ikionesha tahadhari kufuatia kuongezeka kwa sintofahamu katika uchumi wa dunia.


Uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha hivi karibuni cha Kamati ya Sera ya Fedha (MPC), ambapo watunga sera walitathmini hatari zinazotokana na mazingira ya kimataifa dhidi ya uimara wa uchumi wa ndani.

Akizungumza kuhusu uamuzi huo, Naibu Gavana wa BoT, Dkt. Yamungu Kayandabila, alisema hatua hiyo inalenga kusawazisha kati ya kukuza uchumi na kudhibiti mfumuko wa bei.

“Haikuwa uamuzi rahisi,” alisema, akieleza kuwa mvutano wa kisiasa unaoendelea katika Mashariki ya Kati umeanza kuathiri mwenendo wa masoko ya dunia.

Alifafanua kuwa mvutano huo umevuruga minyororo ya usambazaji wa bidhaa na kuchangia kupanda kwa bei, hususan mafuta ambayo sasa yamevuka dola za Marekani 100 kwa pipa, juu ya makadirio ya awali.

Katika hatua nyingine, MPC ilitangaza kupunguza wigo wa riba (interest rate corridor) unaozunguka kiwango cha CBR kutoka pointi 200 hadi 150 za msingi (basis points), hatua inayoweka kiwango cha riba ya siku saba kati ya benki katika viwango vya asilimia 4.25 hadi 7.25.

Kwa mujibu wa Dkt. Kayandabila, hatua hiyo inalenga kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa sera ya fedha, huku ikidumisha uthabiti wa bei na kusaidia ukuaji wa uchumi.

Licha ya changamoto za kimataifa, BoT imeeleza kuwa uchumi wa ndani unaendelea kuonesha uimara.

Katika robo ya kwanza ya mwaka, uchumi ulikua kwa asilimia 6.2 Tanzania Bara na asilimia 6.7 Zanzibar, ukichochewa na sekta za ujenzi, kilimo, utalii na huduma za kifedha.

Kwa robo ya pili, ukuaji unatarajiwa kufikia asilimia 6.1 kwa Tanzania Bara na asilimia 6.6 Zanzibar, ingawa hatari za nje zinaweza kuathiri mwenendo huo endapo zitaongezeka.

Kwa upande wa mfumuko wa bei, umeendelea kubaki ndani ya lengo la BoT la asilimia tatu hadi tano. Kwa wastani, ulikuwa asilimia 3.3 Tanzania Bara na asilimia 4.5 Zanzibar, hali iliyochangiwa na utulivu wa bei za chakula pamoja na kiwango cha ubadilishaji fedha.

Hata hivyo, Benki Kuu imeonya kuwa ongezeko la gharama za nishati na usafirishaji linaweza kuongeza shinikizo la mfumuko wa bei katika miezi ijayo.

Katika sekta ya benki, hali imeendelea kuwa imara ambapo kiwango cha mikopo chechefu kimeshuka hadi asilimia 2.9, chini ya kiwango kinachokubalika kisheria, huku benki zikiendelea kuwa na mtaji wa kutosha na ukwasi wa kuridhisha.

Kwa upande wa sekta ya nje, nakisi ya akaunti ya sasa imepungua hadi asilimia 2.2 ya Pato la Taifa (GDP), ikichangiwa na kuongezeka kwa mauzo ya nje ya dhahabu, mazao ya kilimo na huduma za utalii.

Zanzibar nayo imeendelea kufanya vizuri, ikirekodi ziada ya akaunti ya sasa kutokana na mapato ya utalii.

Aidha, akiba ya fedha za kigeni imefikia zaidi ya dola za Marekani bilioni 6.2, kiwango kinachoweza kugharamia uagizaji wa bidhaa kwa karibu miezi mitano, juu ya viwango vya kikanda.

Kwa upande wa mapato ya serikali, makusanyo ya kodi yamevuka malengo kutokana na kuimarika kwa usimamizi na utii wa walipakodi, huku matumizi ya serikali yakiendelea kubaki ndani ya mipaka ya rasilimali zilizopo.

Hata hivyo, MPC imeonya kuwa bado kuna hatari zinazoikabili uchumi.

“Tishio kubwa kwa matarajio ya uchumi ni mzozo unaoendelea Mashariki ya Kati. Endapo utaongezeka, unaweza kuongeza mfumuko wa bei na kupunguza kasi ya ukuaji wa uchumi duniani na nchini,” alisisitiza Dkt. Kayandabila. 








BODI MPYA TFS YAANZA KAZI RASMI, YAPOKEA MPANGO WA BIASHARA 2026/2027

April 02, 2026 Add Comment


Morogoro

Bodi ya Tano ya Ushauri ya Wizara kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imeanza rasmi majukumu yake kwa kufanya kikao cha 47 cha Bodi, ambacho pia ni kikao cha kwanza cha bodi hiyo mpya.

Kikao hicho kimefunguliwa leo Aprili 2, 2026 mkoani Morogoro na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Luteni Mstaafu Chiku Abdallah Sumbu Gallawa, katika Ukumbi wa Kituo cha Mbegu Bora za Miche ya Miti cha TFS.

Kabla ya kikao hicho, wajumbe walifanya vikao vya kamati kuanzia Machi 31 hadi Aprili 1, 2026, kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji ya wakala.

Pamoja na mambo mengine, Bodi ilipokea na kujadili Mpango wa Biashara wa TFS kwa mwaka wa fedha 2026/2027, sambamba na taarifa mbalimbali za utekelezaji wa majukumu ya taasisi.

Kuanza kwa kikao hicho kunafuatia uzinduzi wa Bodi hiyo uliofanywa Februari 13, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji.