HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
SERIKALI YA AWAMU YA SITA YASISITIZA UWEZESHWAJI WA WATU WENYE ULEMAVU
habariKIKUNDI CHA AMANI NCHINI WAFANYA MKUTANO MAALUMU ULIOLENGA KUHAMASISHA UZALENDO NA KUELEZEA MAFANIKIO YA SERIKALI
habariNa Oscar Assenga,Tanga
KIKUNDI cha Amani nchini kimefanya mkutano maalumu leo katika Jiji la Tanga uliolenga kuhamasisha uzalendo, kuelezea mafanikio ya Serikali na kupongeza utekelezaji wa ahadi za siku 100 za Rais tangu alipochaguliwa 2025.
Akizungumza wakati wa mkutano huo Maalumu Mwenyekiti wa Kikundi hicho nchini Hassan Kubebelwa alitoa wito kwa watanzania hususani vijana wametakiwa kuwa wazalendo kwa nchi na kuacha kukubali kushawishiwa na watu wanaoshinda kwenye majukwaa ya mitandao ya kijamii kueleza mabaya pekee na kuficha mazuri mengi yanayofanywa na Serikali
Katika kulitilia mkazo jambo hilo aliiomba Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Jeshi la Polisi, kuongeza kasi ya kuwafuatilia na kuwachukulia hatua kali watu wanaojiita wanaharakati wa mitandaoni wanaotumia majukwaa hayo kupotosha ukweli na kuichafua Serikali
"Lengo la kuja Tanga ni kuwahamasisha wanakikundi wenzetu wasimame kidete kuelezea maendeleo ya miundombinu mkoani hapa na nchi nzima. Tuache kusikiliza upotoshaji wa mitandaoni; Serikali imaleta fedha za mikopo ya asilimia 10 kwenye halmashauri, watu wakope na kujiendeleza badala ya kulalamika," alisisitiza Kubebelwa.
Awali akisoma riskala ya kikundi hicho, Mjumbe wa Kikundi hicho, Rehema
Manyama alieleza katika kipindi cha siku 100, Rais ameonyesha dira kwa
kufanikisha utoaji wa Bima ya Afya kwa wote, kuzalisha ajira kwa vijana ikiwemo
kutoa mikopo.
Aidha alitoa ushauri wake kwa ngazi za mikoa ziendelee kutoa elimu ya
uzalendo na kuimarisha elimu ya amali ili vijana wajiajiri na kuingiza kipato
Naye Mjumbe Zuberi Gogo, alibainisha kuwa ingawa hitilafu ndogo ndogo
haziwezi kukosekana, changamoto kubwa inatokana na baadhi ya watendaji wanaopindisha
taratibu na kuigombanisha Serikali na wananchi. Alitoa wito kwa wananchi
kuelewa taratibu za kiserikali ili wasipotezwe na upotoshaji.
Akizungumzia suala la mikopo, Mjumbe Zainabu Salim Ugata, alifafanua
kuwa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri haina upendeleo, bali
inatolewa kwa vikundi vilivyofuata taratibu zote zilizowekwa. Alisema kikundi
hicho kitaendelea kuzunguka mikoa yote nchini kutoa elimu kwa umma ili kuongeza
uelewa wa mambo ya Serikali.
Washiriki wa mkutano huo waliazimia kuwa ni wajibu wa kila mzalendo kuilinda taswira ya nchi na kuhakikisha kuwa fursa za kiuchumi zinazotolewa na Rais zinawafikia walengwa bila vikwazo.
LUHAGA MPINA ALIVYOSHIRIKI MAZISHI YA MWADHAMA KARDINALI PENGO
habari
Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo,(baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi) Luhaga Joelson Mpina pamoja na Maaskofu Katoliki katika mazishi Mwadhama Askofu Mstaafu Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026Aliyekuwa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo mwaka 2025 (baadae alienguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi), Luhaga Joelson Mpina pamoja na Mwenyekiti wa Zamani wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia katika mazishi ya Askofu Mkuu Mstaafu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kituo cha Hija Pugu jijini Dar Es Salaam tarehe 28 Februari 2026
RAIS SAMIA AWASILI KILIMANJARO AKIELEKEA MKOANI ARUSHA KWA ZIARA YA KIKAZI
habari ziara



JK AKABIDHI TUZO KWA VIONGOZI BORA BARANI AFRIKA
habari
Mwanasheria Mkuu na Waziri wa Katiba wa Ghana Dominic Akuritinga Ayine akipokea Tuzo kwa niaba ya Rais John Mahama wa Ghana

Kanali Chris Magezi, Msemaji wa Jeshi la Wananchi la Uganda akipokea Tuzo kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akikabidhi Tuzo kwa Waziri Mkuu wa Lesotho, Samuel Matekane

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wakati wa Hafla hiyo ya kukabidhi Tuzo kwa Viongozi Bora wa Mwaka wa Afrika kwa Mwaka 2026

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na mwigizaji maarufu Moses Nyarko aliyeshiriki katika Hafla hiyo ya utoaji wa Tuzo kwa Viongozi Bora barani Afrika kwa Mwaka 2026
……………
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekabidhi Tuzo za Viongozi Bora barani Afrika kwa Mwaka 2026 katika Hafla iliyofanyika Accra, Ghana tarehe 28 Februari 2026.
Tuzo hizo zinatolewa na Jarida la Africa Leadership Magazine linaloandaliwa na Taasisi ya Uongozi Afrika (Africa Leadership Organisation) ambayo Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ni Mwenyekiti wa Bodi yake ya Ushauri.
Mshindi wa Jumla wa Tuzo hizo ni Rais John Dramani Mahama wa Ghana, ambaye ametunukiwa Tuzo ya Mwafrika wa Mwaka kwa Mwaka 2026 kwa kutambua mchango wake katika kukuza demokrasia na uchumi nchini Ghana pamoja na kuwa kinara katika kuimarisha utengamano wa kikanda kupitia Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA).
Akihutubia kabla ya kukabidhi Tuzo hiyo ya mshindi wa jumla, Rais Mstaafu Dkt. Kikwete ameeleza kuwa “kila kizazi za uongozi hukutana na changamoto za kipekee za wakati wake na hivyo hulazimika kubuni njia za kipekee za kuzitatua”. Akaongeza kuwa “kipimo mojawapo cha mafanikio katika uongozi ni kuweza kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na kuboresha hali ya jumla ya kimaisha kwa watu unaowaongoza kutoka hali ya chini kwenda hali ya juu zaidi”.
Mbali na Rais Mahama, miongoni mwa watu mashuhuri waliiopata Tuzo hizo ni pamoja na Waziri Mkuu wa Ufalme wa Lesotho, Samuel Matekane aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi nchini Lesotho pamoja na Mkuu wa Majeshi wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba aliyepata tuzo kwa kutambua mchango wake katika kuliimarisha jeshi la Uganda na kukuza diplomasia ya kijeshi katika ukanda wa maziwa makuu.
Rais wa Namibia Netumbo Nandi-Ndaitwah alipata Tuzo ya Kiongozi Bora wa Kisiasa Afrika huku Makamu wa Rais wa Angola Esperança da Costa, Makamu wa Rais wa Angola akioata Tuzo ya Kiongozi Bora Mwanamke barani Afrika.
Tuzo ya Rais Mahama ilipokelewa kwa niaba yake na Mwanasheria Mkuu wa Ghana, ambaye pia ni Waziri wa Sheria wa Ghana, Dominic Akuritinga Ayine wakati tuzo ya Jenerali Kainerugaba ilipokelewa na Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda, Kanali Chris Magezi.
Kila mwaka Jarida la Africa Leadership Magazine huratibu mchakato wa wazi unaojumuisha kupokea mapendekezo ya viongozi mbalimbali wenye sifa ambao hupigiwa kura kwa njia ya mtandao ili kupata washindi. Viongozi wa tasnia mbalimbali zikiwemo uongozi wa kisiasa, diplomasia, biashara na uwekezaji, ujasiriamali, habari, ulinzi na usalama, nk., wanaoshinda hupokea Tuzo hizo kwa kutambua mchango wao katika kusimamia vizuri tasnia zao pamoja na kulea na kuwaandaa vijana wanaowaongoza ili kuja kuwa viongozi bora wa baadaye.
Katika hafla hiyo, jumla ya Tuzo 36 zilitolewa.
















