HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

WMA YASHIRIKI MAADHINISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI MEI MOSI

May 01, 2026 Add Comment


Wakala wa Vipimo (WMA) imeungana na wafanyakazi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali nchi nzima kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani.

Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa kila Mwaka tarehe 1 Mei na kaulimbiu ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mwaka 2026 ni *"Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".

Wakala imeshiriki katika maadhimisho hayo Kitaifa Mkoani Njombe ambapo watumishi wa Mkoa huo wameongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA Bw. Alban Kihulla.

Pamoja na ushiriki wa Kitaifa kadharika, WMA imeshiriki kuadhimisha siku ya Wafanyakazi katika ngazi za Mikoa kupitia ofisi za Mikoa za Kivipimo.

Uongozi wa WMA unaendelea kuwahimiza watumishi wake kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatoa huduma sahihi kwa wananchi kwa kusimamia matumizi sahihi ya Vipimo katika sekta mbalimbali.





CRJE–UDSM PARTNERSHIP PUTS STUDENTS TO THE TEST IN REAL-WORLD BRIDGE CHALLENGE

May 01, 2026 Add Comment

  

Mr. Zhang Cuishan, Deputy General Manager of CRJE

By Prosper Makene 

CRJE (East Africa) Ltd opened the gates of its Mbezi Beach project site on Thursday to host faculty and students from the University of Dar es Salaam’s College of Engineering and Technology (CoET) for a full-day Site Open Day and Youth Bridge Skills Challenge. 

MZUMBE YAUNGANISHA WATAFITI NA JAMII KUKABILI ATHARI ZA TABIANCHI NA CHANGAMOTO ZA MAJI

April 30, 2026 Add Comment
Farida Mangube Morogoro

Juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na changamoto za upatikanaji wa maji zimepata msukumo mpya kufuatia kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya watafiti na jamii kupitia mradi wa kimataifa wa ICP Connect na Lab to Life.

Oryx Gas Tanzania Yaimarisha Upatikanaji wa Nishati Safi Kupitia Maduka Maalum

April 30, 2026 Add Comment
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imesema mkakati wake ni kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia huku pia ikisisitiza umuhimu wa elimu ya mara kwa mara kwa watumiaji ili wawe na uelewa namna bora ya kutumia nishati safi ya kupikia.

TANZANIA NA JAPAN KUFUNGUA MILANGO MIPYA YA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA NISHATI

April 30, 2026 Add Comment


Ushirikiano kati ya Tanzania na Japan katika sekta ya nishati unaingia hatua mpya, huku juhudi zikielekezwa zaidi katika kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi na teknolojia za kisasa za uzalishaji umeme.

Hatua hiyo imebainishwa jijini Dar es Salaam leo tarehe 30 Aprili,2026 wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi Asilia,Dkt.  James Mataragio alipokutana na Mwakilishi Mkuu mpya wa Japan International Cooperation Agency, Dkt. Kuge Katsuya.

Katika kikao hicho Dkt. Mataragio ameweka wazi Mkakati wa Serikali kuifanya sekta ya nishati kuwa kivutio kikubwa cha mitaji ya kimataifa hususan kutoka Japan.

Amesema  kuwa pamoja na historia ndefu ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, hatua inayofuata inapaswa kulenga uwekezaji mkubwa zaidi unaoweza kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati nchini.

“Huu ni wakati wa kuhamasisha kampuni binafsi na taasisi za kifedha kutoka Japan kuja kuwekeza moja kwa moja katika miradi ya nishati Tanzania,” amesisitiza.

Akizungumzia ushirikiano wa Tanzania na Japan Dkt. Mataragio amesema JICA imekuwa mdau wa muda mrefu katika sekta ya nishati nchini na wameshiriki katika miradi ya  Uandaaji wa Mpango kabambe wa Matumizi ya Gesi Asilia Nchini (Natural Gas Utilization Master Plan -NGUMP),  wametoa fursa za kuwajengea uwezo wataalamu katika Matumizi ya gesi asili pamoja na utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya umeme.

Aidha Dkt. Mataragio amembushia ahadi ya muda mrefu ya Japan ya kuwezesha Mradi wa umeme wa megawati 300 mkoani Mtwara.

Kwa upande wake, Dkt. Kuge ameashiria mwelekeo mpya wa ushirikiano utakaojikita katika Mafunzo ya teknolojia ya nishati ya nyuklia, Uzalishaji wa umeme kupitia gesi asilia kwa ufanisi mkubwa zaidi na Kuunganisha Tanzania na wawekezaji binafsi kutoka Japan

Ahadi hiyo inaashiria uwezekano wa Tanzania kunufaika na teknolojia za kisasa zaidi za nishati kutoka Japan, moja ya nchi zinazoongoza duniani katika ubunifu wa nishati.

Mkutano huo umeonesha wazi kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Japan hauishii katika misaada, bali sasa unaelekea kwenye uwekezaji mkubwa na ubadilishanaji wa teknolojia  hatua inayoweza kubadilisha kabisa sekta ya nishati nchini

RAIS SAMIA ATAMBULIWA KUWA KINARA WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA AFRIKA

April 30, 2026 Add Comment




📌 Mawaziri wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika wapendekeza Rais Samia kutangazwa rasmi

Umoja wa Afrika umetambua juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuendeleza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ndani na nje ya nchi, na kumpendekeza kutangazwa rasmi kuwa kinara wa Umoja wa Afrika wa ajenda hiyo.

Hatua hiyo imefikiwa katika Mkutano wa 5 wa Mawaziri wa Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika wanaoshughulikia Nishati na Uchukuzi uliofanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini, tarehe 30 Aprili 2026. Katika mkutano huo Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika ngazi ya Mawaziri.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ametambuliwa na kupendekezwa kuwa kinara wa Afrika kutokana na mchango wake mkubwa katika kusukuma sera, mikakati na ushirikiano wa kimataifa unaolenga kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia, kupunguza athari za kiafya na kimazingira, pamoja na kuboresha maisha ya waafrika, hususan wanawake na watoto.

Akizungumza katika mjadala kuhusu Programu ya Nishati Safi ya Kupikia Afrika, Waziri Ndejembi amesema kuwa mafanikio ya Tanzania katika sekta hiyo yametokana na uongozi madhubuti wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kusukuma ajenda ya nishati safi ya kupikia ndani na nje ya nchi.

Amesema kuwa chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, nishati safi ya kupikia imepewa kipaumbele cha kitaifa na kuingizwa katika Dira ya Taifa ya 2050, ikiwa ni sehemu muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Katika juhudi za kimataifa, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuhamasisha agenda ya nishati safi ya kupikia kupewa kipaumbele katika mipango ya mataifa mbalimbali kupitia majukwaa ya kimataifa ikiwemo mkutano wa COP28 mwaka 2023, pamoja na Mkutano wa Nishati Safi ya Kupikia Barani Afrika uliofanyika Paris mwaka 2024, ambapo zaidi ya dola za Marekani bilioni 2.2 ziliahidiwa kusaidia sekta hiyo.

Kutokana na hatua hiyo ya mapendekezo ya Mawaziri yaliyoanzia katika ngazi ya wataalamu wa Umoja wa Afrika, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuthibitishwa na kutangazwa rasmi kuwa Kinara wa Umoja wa Afrika wa Nishati Safi ya Kupikia katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika utakaofanyika.




WATUMISHI PBPA WAHAMASISHWA KUPIMA AFYA NA KUPATA CHANJO YA HOMA YA INI

April 30, 2026 Add Comment

 

Daktari Johnson Katanga kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road (OCR) amewahimiza watumishi wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kujitokeza kupima afya zao na kupata chanjo ya kujikinga na maambukizi ya *ugonjwa wa Homa ya Ini* (Hepatitis B).


Wito huo umetolewa leo wakati wa zoezi la utoaji elimu ya afya, upimaji wa hiari pamoja na utoaji wa chanjo dhidi ya *ugonjwa wa Hepatitis B* lililofanyika katika ukumbi wa PBPA jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika zoezi hilo, Dkt. Katanga alieleza kuwa chanjo ya Hepatitis B hutolewa kwa awamu tatu, ambapo dozi ya kwanza hutolewa *mara* baada ya mhusika kupimwa *na kuthibitika kuwa kuwa hana maambukizi* , dozi ya pili hutolewa baada ya mwezi mmoja, na dozi ya tatu hutolewa miezi sita tangu kupokea dozi ya kwanza.

Alifafanua kuwa chanjo hiyo ilianza kutolewa kwa watoto nchini tangu mwaka 2002 ikiwa sehemu ya chanjo za kawaida zinazotolewa mara baada ya kuzaliwa. Kutokana na hali hiyo, watu waliozaliwa mwaka 2001 na kurudi nyuma wanashauriwa kupata chanjo hiyo endapo hawajawahi kuipata.

Kuhusu dalili, Dkt. Katanga alisema *u* mgonjwa wa homa ya ini mara nyingi haoneshi dalili katika hatua za awali, hali inayosababisha watu wengi kugundua maambukizi wakiwa tayari wameathirika kwa kiwango kikubwa. Alitaja baadhi ya dalili zinazoweza kujitokeza baadaye kuwa ni pamoja na uchovu uliokithiri, maumivu ya tumbo upande wa juu kulia, *macho na ngozi kuwa na rangi ya njano* , kupoteza hamu ya kula, mkojo kuwa mweusi, kinyesi cheupe, pamoja na kuvimba kwa miguu au tumbo.

Aidha, alieleza kuwa maambukizi ya virusi hivyo yanaweza kutokea kupitia njia mbalimbali ikiwemo kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, ~wakati wa kujifungua~ , kujamiiana bila kinga, kugusana na damu au majimaji ya mwili wa mtu mwenye ~yenye~ maambukizi, kushirikiana vitu vyenye ncha kali kama sindano, pamoja na kuongezewa damu iliyoathiriwa.

“Takwimu zinaonesha kuwa takribani watu milioni 254 duniani wanaishi na virusi vya homa ya ini, huku nchini Tanzania kiwango cha maambukizi kikikadiriwa kuwa asilimia 4. Hali hii ~Hii~ inaonesha umuhimu wa kuchukua hatua mapema,” alisisitiza.

Aliongeza kuwa endapo maambukizi hayatagunduliwa mapema, kati ya asilimia 5 hadi 6 ya waathirika huingia katika hatua ya ugonjwa sugu (chronic), hali inayoweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo saratani ya ini.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa Rasilimaliwatu~Utumishi~ wa PBPA, Bw. Matiko Sanawa, alisema kuwa utoaji wa elimu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Serikali kupitia Waraka wa Utumishi Na. 2 wa mwaka ~2024~2014 unaosisitiza umuhimu wa kulinda afya za watumishi kazini.

Alisema mwajiri ana jukumu la kuhakikisha watumishi wanakuwa na afya njema ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuchangia maendeleo ya taifa.

“Tumewaalika wataalamu kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road ili kutoa elimu, kufanya upimaji wa hiari na kutoa chanjo. Hii ni hatua muhimu katika kuhakikisha watumishi wanakuwa na afya bora,” alisema Bw. Sanawa.
Huu ni Mkakati wa Serikali wa kuimarisha huduma za kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza na ya kuambukiza, kwa kuhamasisha uchunguzi wa mapema na utoaji wa chanjo.

ACHENI KUTANGAZA WATU,TANGAZENI NCHI-WAZIRI MAKONDA

April 30, 2026 Add Comment


Na Immaculate Makilika - MAELEZO

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda amewataka wadau wa sekta ya habari kubadili ajenda ya kutangaza watu badala yake watangaze fursa za uchumi zilizopo nchini.

Ametoa rai hiyo leo Aprili 30, 2026 katika Siku ya Tatu ya Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani iliyofanyika jijini Arusha.

“ Tuache ajenda ya kutangaza watu, tuitangaze nchi yetu. Tubadilishe mkakati kutoka ajenda ya kusifia watu, tuambieni fursa za uchumi zilizopo,” amesema Waziri Makonda

Ameongeza kuwa waandishi wa habari waache kasumba ya kuwaandika vizuri wala rushwa na watu wasio na sifa njema katika jamii, badala yake wafanye kazi zao kwa maslahi ya Taifa.

Ametolea mfano kuwa hakuna idadi ya kutosha ya waandishi wanaoandika kuhusu sekta ya utalii au kilimo kama wanaoandika kuhusu masula ya siasa.

Amezungumzia kuhusu Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 na kuwaasa waandishi wa habari kushiriki kikamilifu ili kufikia malengo yaliyowekwa huku akisisitiza kuhusu umuhimu wa mchango wa Vvyombo vya Habari kwa maendeleo ya nchi.

Aidha, Waziri Makonda amewataka waandishi wa habari kujiridhisha na vyanzo vya taarifa za kabla ya kuzisambaza kwa umma ili kuepuka upotoshaji na migogoro.

Kuhusu mapendekezo yaliyotelewa na wadau wa sekta ya habari ya kuboresha utendaji wa sekta hiyo nchini, Mhe. Makonda amesema Serikali imeyapokea mapendekezo yote 15 na itayafanyia kazi kwa kushirikiana na wadau.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Gerson Msigwa amesema kuwa lengo la Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ni kutathimi na kulinda hali ya uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani.

Ameongeza kuwa kupitia Maadhimisho hayo Serikali itapata fursa ya kukutana na washirika wake wa maendeleo na asasi za kiraia kujadili masuala ya mabadiliko ya utendaji kazi katika sekta ya habari pamoja na kuwaendeleza watayarishaji wa maudhui.

Naye, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tech and Media Convergency (TMC) na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho hayo kwa mwaka 2026, Bi. Asha Abinallah amesema kuwa kupitia Maadhimisho hayo wadau wameandaa mapendekezo kadhaa ikiwemo kuitaka Serikali kuharakisha uanzishwaji wa Mfuko wa Habari na kuandaa sera rafiki za kuvutia uwekezaji katika sekta ya habari.

Vilevile, wameitaka Serikali kupitia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kuendelea kutimiza majukumu yake ikiwemo kuwajengea uwezo wanahabari katika matumizi ya akili unde.

















TANGA YAJIPANGA KUWA KITOVU KIPYA CHA UTALII NA UWEKEZAJI WA FUKWE TANZANIA

April 30, 2026 Add Comment




Na Oscar Assenga, Tanga

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Balozi Batilda Burian, amesema mkoa huo umeanza mkakati maalum wa kukuza na kutangaza utalii wa fukwe pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo, ili kuongeza mchango wake katika uchumi wa Taifa.

Akizungumza leo, amesema ameita wadau mbalimbali kwa ajili ya kujadili na kuweka mikakati ya pamoja ya kuitangaza Tanga, akibainisha kuwa mkoa huo umejaliwa kuwa katika ukanda wa Bahari ya Hindi wenye maeneo mengi yenye fursa za kiuchumi na utalii.

Ametaja baadhi ya maeneo hayo kuwa ni pamoja na Kipumbwi (Pangani), Ushongo, Kwale (Mkinga) na maeneo ya Raskazone jijini Tanga, ambapo kuna mradi wa kuboresha fukwe unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Amesema mradi huo utakapokamilika utafungua fursa za michezo ya maji, matembezi ya boti, kuogelea pamoja na shughuli za kijamii kama harusi.


Aidha, amesema mkoa umeanza kushirikiana na Kampuni ya Makazi Solution pamoja na wadau wa Zanzibar ili kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kuendeleza utalii wa fukwe.

Timu ya wataalamu inatarajiwa kwenda Zanzibar kukutana na Wizara ya Utalii na wadau wengine ili kuimarisha ushirikiano huo.

“Tunajifunza kutoka Zanzibar, ambako maeneo kama Nungwi na Paje yalianza kidogo lakini sasa yamekua vituo vikubwa vya utalii. Sasa ni wakati wa Tanga kuchukua nafasi hiyo,” amesema.

Kwa upande wa uwekezaji, Dkt. Burian ameeleza kuwa mradi wa Kipumbwi Satellite City, unaotekelezwa kwa ushirikiano na Halmashauri ya Pangani na Makazi Solution, unalenga kutoa fursa kwa wananchi na wawekezaji kupata viwanja na kuendeleza eneo hilo.


Amesema eneo la Kipumbwi lina umuhimu mkubwa kimkakati, likiwa kilomita 3 kutoka bandari ya Kipumbwi, kilomita 80 kutoka Tanga, kilomita 60 kutoka Zanzibar kwa njia ya bahari, na kilomita 180 kutoka Dar es Salaam. Pia ujenzi wa barabara ya Tanga–Pangani–Saadani–Bagamoyo unatarajiwa kufungua zaidi ukanda huo wa pwani.

Mbali na fukwe, mkoa wa Tanga una vivutio vingi vya utalii ikiwemo Mapango ya Amboni, Hifadhi ya Taifa ya Saadani, Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, Milima ya Usambara (Lushoto), pamoja na urithi wa kihistoria kama makaburi ya vita ya kwanza ya dunia na Kisiwa cha Toten.

Ameongeza kuwa Tanga pia ni kitovu cha utamaduni wa Kiswahili, likiwa na historia ya muziki wa taarab, vyakula vya asili, pamoja na kuwa chimbuko la lugha ya Kiswahili, ambapo mwanazuoni mashuhuri Sheikh Shaban Robert alizaliwa katika eneo hilo.

Kwa sasa, amesema mkoa unapokea wageni kutoka ndani na nje ya nchi, hususan kutoka Kenya, Ujerumani, Uholanzi na Uswisi, wanaovutiwa na historia, mazingira asilia na utamaduni wa Tanga.

Dkt. Burian amesema jitihada hizo zinaunga mkono azma ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuitangaza Tanzania kupitia kampeni ya Royal Tour na kuongeza idadi ya watalii.

Kwa upande wa uchumi, amesema mkoa wa Tanga kwa sasa unachangia takribani shilingi trilioni 9.8 katika pato la taifa, na una mpango wa kuongeza mchango huo na kufikia nafasi ya pili kitaifa baada ya Dar es Salaam ifikapo mwaka 2028.

Amehitimisha kwa kusema kuwa Tanga ni eneo sahihi kwa uwekezaji na utalii, akiwakaribisha wawekezaji na watalii kutoka ndani na nje ya nchi kuja kutumia fursa zilizopo.Kwa upande wake Afisa Mahusiano kutoka Kampuni ya Makazi Solution(T) Limited Maximilian Lukosi amesma dhamira yako kubwa ni kuufanya mkoa wa Tanga kuwa daraja la watalii ili wakitokea Zanzibar wapiti hapa na ndio waelekee mikoa mingine ikiwemo Kilimanjaro na Arusha