Na Mwandishi Wetu,
Wananchi wa Mvomero wamesema kuwa utekelezaji wa agizo la Serikali la kuhamasisha matumizi ya nishati safi umeanza kuleta matokeo chanya, ikiwemo kupungua kwa ukataji wa miti na uchomaji wa mkaa katika baadhi ya maeneo.
Hayo yameelezwa na baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Mvomero wakati wa ziara ya timu kutoka Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Mfuko wa Maendeleo ya Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), iliyofika wilayani humo kutoa elimu kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Kampeni hiyo imefanyika katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kuhamasisha matumizi ya nishati salama.
Wameeleza kuwa wananchi wengi sasa wameanza kuhamia katika matumizi ya gesi na umeme kwa ajili ya kupikia, jambo linalowasaidia kuokoa muda katika shughuli zao za kila siku pamoja na kujikinga na madhara ya kiafya yanayotokana na moshi wa kuni na mkaa.
Katika kampeni hiyo, wananchi wamepata fursa ya kushuhudia maonesho ya matumizi ya majiko ya gesi na umeme, ambapo walioneshwa jinsi yanavyoweza kupika chakula kwa haraka, kwa gharama nafuu na kuhifadhi ubora pamoja na ladha ya chakula. Hali hiyo imeongeza mwitikio wa wananchi wengi kuanza kutumia nishati safi ya kupikia.



























Dar es salaam –




