HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

TRA DODOMA YATOA MKONO WA EID KWA WATOTO YATIMA, YAIMARISHA UPENDO NA MSHIKAMANO

March 19, 2026 Add Comment

 

Kaimu Meneja wa Mkoa wa TRA Dodoma, Bw. Obrey Sillayo, akiambatana na Kaimu Meneja wa Huduma kwa Mlipakodi pamoja na maafisa wengine wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wametoa mkono wa Eid Fitri kwa watoto yatima na wenye mahitaji maalumu katika Kituo cha Kulelea Watoto Yatima Rahmani, ikiwa ni sehemu ya kuonesha upendo na kuimarisha mshikamano na jamii.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Bw. Sillayo amepongeza juhudi za kituo hicho kwa kulea watoto katika misingi bora ya maadili na malezi, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwajali watoto hao kwa ustawi wa taifa.

Aidha, ameeleza kuwa TRA itaendelea kushiriki katika shughuli za kijamii kama sehemu ya kuwajibika kwa jamii na kujenga uhusiano mzuri na wananchi.

Kwa upande wake, Bi. Rukia Hamisi Abdallah ameishukuru TRA kwa mkono huo wa Eid, akieleza kuwa umeleta faraja na matumaini kwa watoto wanaolelewa katika kituo hicho.

Tukio hilo limeacha ujumbe wa upendo, mshikamano na uwajibikaji kwa jamii.







RIPOTI YA EWURA : MOSHI, NZEGA, BIHARAMULO MAMLAKA BORA ZAIDI ZA MAJI NCHINI

RIPOTI YA EWURA : MOSHI, NZEGA, BIHARAMULO MAMLAKA BORA ZAIDI ZA MAJI NCHINI

March 19, 2026 Add Comment

Mamlaka za maji na usafi wa mazingira za Moshi, Nzega na Biharamulo zimetwaa tuzo za mamlaka bora nchini, katika tathmini ya ripoti ya EWURA ya utendaji wa mamlaka za maji iliyozinduliwa na Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Hamidu Aweso (Mb) leo tarehe 19 Machi 2026, mjini Morogoro.

Aidha, mamlaka 27 zilitambuliwa kwa kuwasilisha kwa asilimia 100 tozo ya udhibiti.

Taarifa ya hiyo ya Tathmini imepima Utendaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira 83 zinazotoa huduma katika mikoa, wilaya na miji midogo , katika hafla iliyofanyika mjini Morogoro.

Waziri Aweso ameipongeza EWURA kwa kuandaa taarifa hiyo muhimu iliyobainisha uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika utoaji huduma za maji na usafi wa mazingira nchini.

Kwa mujibu wa EWURA, tathmini hiyo imeonesha mafanikio katika ongezeko la uzalishaji wa maji kwa 19.3%, wateja kufikia milioni 1.8 na mapato kuongezeka kwa 14%. Hata hivyo, changamoto kama upotevu wa maji (42.3%) na uhaba wa miundombinu ya majitaka bado zinaendelea.

Mhe. Aweso amezitaka mamlaka za maji kuendelea kuboresha huduma kwa kuzingatia ubora, uwazi na uendelevu.

TUNAIMARISHA UZALISHAJI NA USAMBAZAJI UMEME KUKIDHI MAHITABI YA UCHUMI UNAOKUA-MHANDISI MRAMBA

March 19, 2026 Add Comment


New Delhi, India


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, ameieleza Jumuiya ya kimataifa kuwa Tanzania inaendelea kuchukua hatua za kimkakati kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usimamizi wa umeme ili kukidhi mahitaji ya uchumi unaokua kwa kasi.


Amesema hayo katika mkutano wa Bharat Electricity Summit 2026 unaofanyika nchini India.


" Tanzania  inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kuzalisha, usafirishaji na usambazaji umeme, lengo letu ni kuhakikisha nchi inakuwa na umeme wa kutosha kwa ajili ya matumizi ya kijamii na kukidhi mahitaji ya kiuchumi ambayo yanazidi kukua kwa kasi, kielelezo cha hatua tunazochukua ni pamoja na utekelezaji wa mradi wa umeme jua wa Kishapu wenye uwezo wa megawati 150, ambao awamu yake ya  kwanza imekamilika na kuzalisha  megawati 50." Amesema Mhandisi  Mramba

Aidha, ametaja mradi wa umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) wenye uwezo wa megawati 2,115 kuwa ni nguzo muhimu katika kuongeza uzalishaji wa umeme wa uhakika nchini.


 Katika kufanikisha utekelezaji wa miradi ya nishati, Mhandisi Mramba amesema Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi  kama sehemu ya mkakati wa kuharakisha maendeleo ya sekta hiyo.


Vilevile amesema kuwa, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya njia za kusafirisha umeme pamoja na kuunganisha gridi ya taifa na nchi jirani,  hatua inayotarajiwa kuongeza usalama wa nishati kupitia biashara ya umeme ya kikanda.


Katika mkutano huo Mhandisi Mramba  amesisitiza umuhimu wa maboresho ya gridi (grid modernisation) pamoja na matumizi ya teknolojia za smart grid, akieleza kuwa Tanzania tayari imeanza safari ya kuelekea katika mifumo hiyo ili kuongeza ufanisi, uthabiti na usalama wa huduma ya umeme.


Vilevile amegusia suala la nishati jadidifu linavyozidi kuwa sehemu muhimu ya mfumo wa umeme akitanabaisha kuwa kuna haja kwa taasisi za mipango na mashirika ya umeme kuimarisha uwezo wa kiufundi na kiutendaji ili kuendana na mabadiliko ya mfumo huo wa kisasa.


Mkutano huo umewakutanisha viongozi na wataalam wa sekta ya nishati kutoka mataifa mbalimbali duniani kujadili mikakati ya kuimarisha mifumo ya umeme, kukuza ushirikiano wa kikanda na kuendeleza matumizi ya teknolojia za kisasa katika sekta hiyo.

ELIMU YA KUMLINDA MLAJI YATOLEWA  KATIKA SHULE YA MSINGI BUNGE

ELIMU YA KUMLINDA MLAJI YATOLEWA KATIKA SHULE YA MSINGI BUNGE

March 19, 2026 Add Comment

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

....

TUME ya Ushindani (FCC) leo Machi 19,2026 imetoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge kuhusu masuala ya kumlinda mlaji, ikiwemo haki na wajibu wa mlaji pamoja na madhara ya matumizi ya bidhaa bandia katika jamii.

Elimu hiyo imelenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa awali kuhusu umuhimu wa kuchagua na kutumia bidhaa zilizo salama, huku ikisisitiza kuwa walaji wana nafasi kubwa katika kulinda afya zao na za wengine.

Mafunzo hayo pia yameenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani, tukio linaloadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu haki za walaji duniani kote.

Kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho hayo ni “Bidhaa Salama, Imani kwa Mlaji,” ikisisitiza umuhimu wa kuhakikisha bidhaa zote zinazotumiwa na wananchi zinakidhi viwango vya usalama na ubora.

Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC, Thecla Kitosi, amewahamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wazuri wa elimu hiyo kwa jamii zinazowazunguka.

Aidha Bi.Kitosi amewaasa wanafunzi hao kuelewa haki zao kama walaji, pamoja na wajibu wao wa kutoa taarifa kwa FCC wanapobaini au kuwa na mashaka kuhusu usalama wa bidhaa au huduma wanazotumia.

Hata hivyo amewahimiza wanafunzi kuwa mabalozi wazuri kwa jamii zao kwa kuwafahamisha wazazi na ndugu zao juu ya hatari za bidhaa bandia na namna ya kuzitambua.

"FCC itaendelea kutoa   elimu kwa makundi mbalimbali ya jamii, hususan wanafunzi, ni njia muhimu ya kujenga taifa lenye walaji wenye uelewa, wanaoweza kujilinda dhidi ya bidhaa bandia na huduma zisizo na ubora."amesisitiza Bi.Kitosi

Kwa upande wake Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine, amieleza kuwa bidhaa bandia zinaweza kuwa na athari kubwa kiafya, kiuchumi na hata kijamii. Alifafanua kuwa baadhi ya bidhaa hizo, hususan vipodozi, dawa na vifaa vya umeme, vinaweza kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji kutokana na kutokidhi viwango vya ubora vinavyotakiwa.

“Ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuwa makini na bidhaa tunazonunua. Hakikisheni mnachunguza nembo za ubora na kununua bidhaa kutoka kwa wauzaji wanaoaminika,” amesisitiza Bi. Diana.

Kwa upande wao, wanafunzi walionesha shauku kubwa kwa kuuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia. Walishukuru kwa elimu hiyo na kuahidi kuitumia ipasavyo katika maisha yao ya kila siku.

Elimu hii ni sehemu ya juhudi za FCC za kuendelea kulinda haki za mlaji pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama na zenye ubora unaokubalika, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

 Afisa Mlinda Mlaji kutoka FCC ,Thecla Kitosi,akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Mkaguzi wa Bidhaa bandia kutoka FCC Bi.Diana Augustine akitoa elimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani.

Sehemu ya wanafunzi wakisikiliza mada mbalimbali wakati wakipata aelimu kuhusiana madhara ya bidhaa bandia katika shule ya Msingi Bunge iliyotolewa na FCC ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

   

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Wanafunzi wakiuliza maswali mbalimbali kuhusu namna ya kutofautisha bidhaa halisi na bandia mara baada ya kupatiwa elimu na FCC  ikiwa ni sehemu ya kuelekea Maadhimisho ya Wiki ya Siku ya Haki za Mlaji Duniani. 

Maafisa kutoka Tume ya Ushindani(FCC) wakiwa katika picha ya pamoja na  Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Bunge  mara baada ya kukamilisha utoaji wa elimu kwa wanafunzi kuhusiana masuala ya kumlinda mlaji.

TGNP YAWAKUTANISHA VIJANA KUJADILI FURSA NA CHANGAMOTO

March 19, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP), kwa kushirikiana na taasisi ya Sightsavers na YOWDO, umeandaa jukwaa maalumu la vijana na watu wenye ulemavu kwa lengo la kujadili fursa, changamoto na mikakati ya kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa nchi.

MAAFISA UGANI KUONGOZA MAPINDUZI YA KILIMO KILIMANJARO

March 19, 2026 Add Comment




Serikali mkoani Kilimanjaro imeanza utekelezaji wa mkakati maalum wa kuwawezesha maafisa ugani kupitia mafunzo ya kitaalamu, ikiwa ni jitihada za kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo na kuongeza tija kwa wakulima.


Hatua hiyo inalenga pia kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuinua kipato cha wakulima katika mkoa huo.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wakati wa ufunguzi wa mafunzo yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), yaliyofanyika Machi 17, 2026 katika ukumbi wa Manispaa ya Moshi, Katibu Tawala Msaidizi wa Kilimo na Ufugaji, Dkt. Emmanuel Lema alisema maafisa ugani wanapaswa kutumia mbinu za kisasa na ubunifu ili kuwahudumia wakulima kwa ufanisi zaidi.

Alisema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo maafisa hao ili waweze kushauri matumizi sahihi ya mbegu bora, teknolojia za kisasa za kilimo pamoja na mbinu za kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.


Aidha, Dkt. Lema alibainisha kuwa Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha sekta ya kilimo, ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji, kusambaza pembejeo na kuwapatia maafisa ugani vitendea kazi vinavyohitajika. Pia aliwataka maafisa hao kushiriki kikamilifu katika kudhibiti migogoro kati ya wakulima na wafugaji.


Kwa mujibu wa takwimu za mkoa, Kilimanjaro imezalisha tani 1,259,115 za mazao ya chakula katika mwaka wa kilimo 2024/2025, kiwango kinachozidi mahitaji ya tani 773,115.



Naye Afisa Kilimo kutoka COPRA, Bi. Paskalia Sitembela alisema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali katika kutoa mafunzo yatakayochochea uzalishaji wa mazao yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko.


Maafisa ugani walioshiriki mafunzo hayo wameahidi kuyatumia ipasavyo ili kuwafikia wakulima katika maeneo yao na kuwapatia elimu sahihi ya kilimo, hatua itakayosaidia kuongeza uzalishaji wenye tija katika mkoa na taifa kwa ujumla.

STAMICO Yatoa Msaada na Faraja kwa Watoto Yatima wa Umra Orphanage

March 19, 2026 Add Comment
Katika kuendeleza dhamira ya uwajibikaji kwa jamii, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limetembelea Kituo cha Watoto Yatima cha Umra Orphanage jijini Dar es Salaam, na kutoa msaada wa mahitaji muhimu sambamba na kuwapa faraja watoto wanaolelewa kituoni hapo, kuelekea sikukuu ya Idd.

MAAFISA ELIMU KATA WATAKIWA KUJITUMA NA KUWA WAZALENDO KUFANIKISHA MALENGO YA SEKTA YA ELIMU NCHINI

March 18, 2026 Add Comment

NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) itaendelea kutoa fursa za mafunzo endelevu ya viongozi wa elimu wa ngazi mbalimbali na wadau wengine wa elimu ili waweze kuimarisha uongozi, usimamizi na uendeshaji wa shule kwa ajili ya utoaji wa elimu bora nchini. 

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA MAJI WA HATIFUNGANI

March 18, 2026 Add Comment

 



Na Oscar Assenga,TANGA

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira wametembelea maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Maji wa Hatifungani ya Kijani (Green Bond) wenye thamani ya Sh.Bilioni 53.3 unaolenga kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma kwa wakazi wa Jiji la Tanga na wilaya za karibu


Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga UWASA) Machi 17,2026 Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Jackson Kiswaga alisema kwamba wameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo



Mradi huo kwa sasa umefikia asilimia 65 ya utekelezaji wake na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Octoba mwaka huu ambao utakuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi.

“Kwa kweli tumetembelea mradi huu na tumeona namna unavyotekelezwa na kumeridhishwa nao kazi nzuri inaendelea “Alisema



Katika hatua nyengine Mwenyekiti wa Kamati hiyo alimpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuruhusu ushiriki wa sekta binafsi katika uzalishaji wa maji.



Aidha pia aliitaka Wizara ya Maji kuhakikisha wakandarasi wanalipwa kwa wakati ili wasikwamishe kasi ya ujenzi wake

Aliongeza kwamba wanamshukuru Rais kwa kutoa kiasi cha Bilionio 35 kwa ajili ya mradi wa Mkinga-Horohoro kupitia fedha za ndani.



Alisema Kamati hiyo inataka kuona mradi huu unakamilika kwa wakati ili ifikapo mwaka 2030 malengo ya Serikali ya kufikisha maji kwa asilimia 100 yawe yametimia.



Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tanga UWASA, Mhandisi Godfrey Hilly alisema kuwa mradi huo unajumuisha upanuzi wa kituo cha kusukuma maji cha Mabayani kutoka lita milioni 42 hadi milioni 72 kwa siku, na ukarabati wa mtambo wa Mowe utakaofikisha uzalishaji wa lita milioni 60 kwa siku.

Hata hivyo Meneja wa RUWASA Mkoa wa Tanga, Mhandisi Upendo Lugongo alisema mkoa unafikia asilimia 79 ya upatikanaji wa maji,.



Alisema kwa wilaya ya ya Mkinga wakitarajiwa kupanda kutoka asilimia 72.1 hadi 89.03 mara baada ya mradi wa Mkinga-Horohoro kukamilika wenye thamani ya shilingi bilioni 35 utakapokamilika.

Kamati ya Bunge imekagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao katika awamu yake ya kwanza unatarajiwa kuhudumia jumla ya vijiji 17 ndani ya wilaya hiyo.

Mhandisi Upendo alisema mradi huo kwa ujumla umefikia asilimia 65 ya utekelezaji wake. Katika ziara hiyo, Kamati imezindua rasmi upatikanaji wa maji katika Kata ya Mtimbwani, ambapo wananchi wa eneo hilo sasa wameanza kupata huduma ya maji safi ya bomba, ikiwa ni sehemu ya mafanikio ya awali ya mradi huo mkubwa utakaohudumia vijiji 37 utakapokamilika kikamilifu.

Awali akizungumza Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, alimpongeza mkandarasi wa STC huku akieleza kwamba Serikali itaendelea kusimamia ubora wa huduma na kuwashirikisha watu binafsi katika usambazaji ili kuwafikia wananchi wa vijijini haraka zaidi.

Hata hivyo Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Pius Lyanda, aliishauri Serikali kutenga bajeti maalumu kwa ajili ya kuhifadhi vyanzo vya maji na bwawa la Mabayani ili kuzuia uharibifu wa mazingira unaotokana na shughuli za kibinadamu.






BAADA YA SADC KUITAJA TANZANIA KINARA WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA ,KAMISHNA LUOGA ATAKA WATUMISHI KUKUZA MATUMIZI YA NISHATI HIYO.

March 18, 2026 Add Comment




Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Innocent Luoga amewataka Watumishi wa Wizara ya Nishati kuendelea kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini ili kufanikisha ajenda hiyo  ambayo kinara wake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Ameeleza kuwa ajenda ya nishati safi ya kupikia tayari imeanza kuonesha mafanikio nchini na hivyo kupelekea Tanzania kutambuliwa katika maeneo mbalimbali duniani ikiwemo katika nchi zilizo katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Kamishna Luoga amesema hayo tarehe 18 Machi 2026 jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha Tatu cha Mkutano wa Pili wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Nishati kwa niaba ya Ma-Katibu Wakuu wa Wizara ya Nishati.


“Katika Mkutano wa SADC ambao Tanzania ilishiriki hivi karibuni, kupitia hotuba mbalimbali zilizotolewa katika mkutano huo ikiwemo ya mgeni rasmi ambaye ni Rais wa Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa aliitambua na kuipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia, lakini pia katika maazimio ya mwisho yaliyoandaliwa na sekretarieti ya SADC, nchi zote za SADC zilitakiwa kuunga mkono juhudi hizo za Tanzania.” Amesema Kamishna Luoga

Kutokana na hilo, amempongeza Rais, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi anazochukua kufanikisha ajenda ya nishati safi ya kupikia, pia amewapongeza Watumishi Wizara ya Nishati kwa kufanikisha juhudi hizo ambazo zinalenga kuimarisha afya za watanzania na kupunguza uharibifu wa mazingira.

Aidha, katika kikao hicho cha Baraza la Wafanyakazi kilicholenga kujadili, kutoa maoni, ushauri na kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2026/2027, Mhandisi Luoga amewataka wajumbe wa Baraza kujiridhisha kuhusu maeneo yote muhimu ya vipaumbele vya Wizara kama yametengewa fedha ili kuwezesha Wizara kuhudumia watanzania kwa ufanisi.



Vilevile, amewataka Watumishi kuzingatia maadili ya utumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu yao na kujiepusha na utoro, rushwa na kutanguliza uzalendo katika kuwahudumia watanzania.

Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Nishati umehudhuriwa pia na Viongozi wa TUGHE Mkoa na Tawi la Nishati, pamoja wawakilishi kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara