HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
MKE WA RAIS WA SINGAPORE ATEMBELEA KITUO KINACHOZALISHA NGUO ZA PAMBA DAR
habariZAIDI YA KAYA 7,800 TANGA ZANUFAIKA NA MPANGO WA BIMA YA AFYA KWA WOTE
afya
Na Oscar Assenga,TANGA
Zaidi ya wananchi 20,000 kutoka kaya masikini mkoani Tanga wameanza kunufaika na mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, unaolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za matibabu kwa kaya zenye kipato cha chini.
Mpango huo, unaotekelezwa kwa awamu ya kwanza na ya pili, unalenga kuwafikia wananchi walio katika mazingira magumu kiuchumi ili kuwawezesha kupata huduma za afya bila kikwazo cha gharama za matibabu. Ufadhili wa mpango huo unatolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), ukiwa na lengo la kupunguza mzigo wa gharama za matibabu kwa kaya masikini.
Hadi sasa, zaidi ya wanufaika 20,000 kutoka kaya 7,816 wamepatiwa kadi za bima ya afya na wameanza kutumia huduma hizo tangu Machi mwaka huu. Hatua hiyo imeelezwa kuwa imeleta matumaini mapya kwa wananchi wengi ambao hapo awali walikabiliwa na changamoto ya kumudu gharama za matibabu.
Akizungumza katika Maonesho ya Kibiashara ya Mwahako, Daktari Lawi Kupaza kutoka Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Tanga amesema mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa, huku wengi wa walengwa waliostahili tayari wakikabidhiwa kadi zao.
Amesema zoezi hilo linaendelea vizuri katika halmashauri zote za mkoa huo, huku awamu ya pili ikitarajiwa kufikia kaya nyingine 1,300.
“Kwa sasa tunaendelea na ugawaji wa kadi pamoja na uhakiki wa taarifa za wanufaika. Tunawahamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki taarifa zao ili waweze kupata huduma kwa wakati,” amesema Dkt. Kupaza.
Hata hivyo, amekiri kuwepo kwa changamoto ya kuwafikia wanufaika wote kwa wakati kutokana na ukubwa wa maeneo ya utekelezaji na ratiba za shughuli mbalimbali.
“Kuna changamoto ya kuwafikia wanufaika wote kwa wakati kutokana na ratiba na ukubwa wa eneo la utekelezaji. Hata hivyo, watendaji wa kata na vijiji wanaendelea kusaidia katika uhamasishaji,” ameongeza.
Kwa upande wake, Afisa Madai wa NHIF, Neema Kisinga, ameitaka jamii kuendelea kujiunga na bima ya afya ili kujikinga na gharama kubwa za matibabu.
Amesema mfuko huo una vifurushi mbalimbali vinavyowezesha wananchi kupata huduma za afya kwa gharama nafuu, ikiwemo kifurushi cha Tarangire ambacho kinatoa huduma za matibabu, vipimo na ushauri wa daktari kwa gharama nafuu kwa mwaka mzima.
“Kuwa na bima ya afya kunapunguza mzigo wa kulipia huduma kila unapougua au kuhitaji matibabu. Hii ni njia bora ya kujilinda na gharama zisizotarajiwa za afya,” amesema Kisinga.
Mpango huo unaendelea kuonekana kama hatua muhimu katika juhudi za Serikali za kuhakikisha wananchi wote, hususan wa kipato cha chini, wanapata huduma bora za afya bila kuathiriwa na changamoto za kifedha.
BARRICK YATOA SHILINGI 25 BILIONI KWA UDSM ILI KUWEZESHA TAFITI , UFADHILI , KUONGEZA RASILIAMALI WATU KWENYE SEKTA YA MADINI NCHINI
habariWAZIRI MAVUNDE: UTAFITI NA UBUNIFU NI NGUVU YA UKUAJI WA SEKTA YA MADINI
habariMFUMO WA EMS KULETA UWAZI NA UFANISI KATIKA SOKO LA JUMLA LA FEDHA ZA KIGENI
habariNAIBU WAZIRI LONDO ASHIRIKI JUKWAA LA UTALII, BIASHARA NA UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA MISRI
habariTANZANIA YASHIRIKI JUKWAA LA UTALII, BIASHARA NA UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA MISRI
habariARUSHA KUWA KITOVU CHA WATAFITI WA AFYA, WASHIRIKI 450 KUKUTANA KATIKA KONGAMANO LA NIMR
habari
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Prof. Said Aboud
MPANGO KAZI WA PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI AFDP WAFANYIWA MAPITIO
habari
NA; Mwandsihi Wetu – Chato
Wataalamu kutoka katika Sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP ) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu wamekutana Mjini Chato Mkoani Geita tarehe 8 Juni 2026 kwa lengo la kufanyia mapitio mpango kazi wa Programu hiyo.
Akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi hicho, Mhandisi Enock Nyanda, Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Sekta za Uchumi na Uzalishaji Idara ya Tawala za Mikoa Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI alisema lengo la wataalam hao kukutana ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya kikao cha Mawaziri kilichofanyika mapema mwezi Mei mwaka huu.

Aidha timu hiyo ya wataalam pia itaandaa shughuli zitakazotekelezwa na program kwa mwaka 2027 ilikuweza kufikia malengo pamoja na kutembelea maeneo ya utekelezaji wa Mradi ya Rubambagwe Wilayani Chato pamoja na Kilimi Wilayani Nzega Mkoani Tabora.

Sekta zinazotekeleza Progreamu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) ni Pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Kilimo, Shirika la Uvuvi nchini TAFICO, Shirika la Uvuvi Zanzibar ZAFICO, Wizara ya uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Wakala wa Mbegu Nchini ASA, Taasisi ya Uthibiti wa Ubora wa Mbengu Nchini TOSCI na Taasisi ya utafiti wa Mbegu za Kilimo Nchini TARI
SERIKALI YAINGIA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO NA DIT KUIMARISHA USIMAMIZI WA MAAFA
habariWAZIRI MAVUNDE KUFUNGUA WIKI YA 11 YA UTAFITI NA UBUNIFU UDSM
habariRAYTON KWEMBE: TULIWEKEZA KWENYE RASILIMALI WATU NDIO MAANA FORBES IMETUTAMBUA KAMA KAMPUNI YENYE UBORA WA JUU UJENZI WA MELI NCHINI
habari 
VIJANA NA WASOMI MKOANI MWANZA WAHIMIZWA UZALENDO NA UJASIRIAMALI KATIKA KONGAMANO
habari
SMZ YATAJA MAFANIKIO YA BIMA YA LAZIMA KWA WAGENI
afya biashara
Na Mwandishi Wetu, Arusha.Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imetumia Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Karibu-KiliFair 2026 kutangaza mafanikio ya mpango wa bima ya lazima kwa wasafiri, ikieleza kuwa umeimarisha usalama wa wageni na kuchangia ukuaji wa sekta ya afya pamoja na mapato ya utalii visiwani humo.
Mpango huo ulioanza kutekelezwa rasmi Oktoba 1, 2024, unawataka wageni wote wa kimataifa wanaoingia Zanzibar kuwa na bima ya usafiri kabla ya kuwasili. Tangu kuanzishwa kwake, mpango huo umeendelea kuwa chanzo muhimu cha mapato, ukiingiza wastani wa dola za Marekani milioni moja, sawa na zaidi ya Sh bilioni 2.6 kila mwezi.
Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) kwenye viwanja vya Magereza jijini Arusha, Ofisa Mauzo wa shirika hilo, Abdul-Halim Muhammad, alisema maonesho hayo yamewapa fursa ya kutoa elimu kwa watalii, wawekezaji na wadau wa sekta ya utalii kuhusu umuhimu wa bima hiyo.
MIGODI YA BARRICK YA BULYANHULU NA NORTH MARA YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI NA KUFUATILIA MRADI WA UREJESHAJI UOTO ASILI MTO TIGHITE
habari
UDSM KUNG'ARA KWA UBUNIFU WA MADINI, AI NA NISHATI JADIDIFU

MAADHIMISHO YA 11 YA UTAFITI NA UBUNIFU UDSM KUANGAZIA UCHUMI WA KIDIJITALI
biashara habari
MUHEZA YAANZA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2026
michezo
DC awapongeza wananchi kwa mwitikio mkubwa wa Jogging
Na Oscar Assenga, Muheza
MAANDALIZI ya kuupokea Mwenge wa Uhuru 2026 katika Wilaya ya Muheza yamezidi kushika kasi baada ya wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki mazoezi ya Jogging yaliyoandaliwa ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na tukio hilo muhimu la Kitaifa.
Akizungumza baada ya mazoezi hayo, Mkuu wa Wilaya ya Muheza Ayoub Sebabili aliwapongeza wananchi kwa mwitikio wao mkubwa, akisema ushiriki huo unaonyesha utayari wa wakazi wa wilaya hiyo kuupokea Mwenge wa Uhuru unaotarajiwa kuwasili Juni 23 mwaka huu.
Alisema mazoezi hayo yamelenga kuwaweka wananchi katika hali nzuri ya afya, kuimarisha mshikamano na kuwaandaa kimwili na kiakili kuelekea mapokezi ya mwenge huo.
“Tunawashukuru wananchi wote waliojitoa kushiriki mazoezi haya. Hii ni ishara nzuri ya ushirikiano katika maandalizi ya tukio muhimu la kitaifa ambalo Wilaya ya Muheza itakuwa mwenyeji wake,” alisema.
Mkuu huyo wa wilaya alibainisha kuwa jogging nyingine itafanyika Juni 13 mwaka huu na kutoa wito kwa wananchi ambao hawakupata nafasi ya kushiriki safari hii kujitokeza kwa wingi ili kuwa sehemu ya maandalizi hayo.
Alisisitiza kuwa mazoezi hayo ya kilomita tano yanafanyika kwa mwendo wa kawaida ili kuwezesha kila mwananchi kushiriki bila kujali umri au hali yake ya kiafya.
“Tunawakaribisha vijana, wanawake, wazee pamoja na watu wenye ulemavu kushiriki mazoezi haya. Lengo letu ni kuona wananchi wote wanakuwa sehemu ya maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru 2026,” alisema.
Muheza inatarajia kuupokea rasmi Mwenge wa Uhuru Juni 23, huku maandalizi mbalimbali yakiendelea kufanyika kuhakikisha tukio hilo linafanyika kwa mafanikio na kuacha alama chanya kwa wananchi wa wilaya hiyo.

KAPINGA: DHANA YA TAKA SIFURI INAFUNGUA FURSA ZA BIASHARA NA VIWANDA.
habari
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, amesema dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa ni fursa muhimu ya kukuza sekta ya viwanda, kuongeza thamani ya malighafi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.
Akizungumza katika kikao cha mawaziri kilichofanyika jijini Istanbul nchini Uturuki, Juni 5, 2026, kilichobeba mada ya Mageuzi ya Kijani ya Viwanda: Mtazamo wa taka sifuri na urejeshaji bidhaa, Kapinga amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta ya viwanda huku ikisisitiza matumizi bora ya rasilimali na uhifadhi wa mazingira. Ameeleza kuwa dhana ya taka sifuri na urejeshaji bidhaa inatoa fursa kwa nchi zinazoendelea kupitia matumizi endelevu ya malighafi, kupunguza upotevu baada ya mavuno, kupunguza uzalishaji wa taka na kuongeza thamani ya bidhaa zinazotengenezwa viwandani. Kapinga amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kuunganisha masuala ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika sera na mipango ya maendeleo ya viwanda kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi, ufanisi wa nishati na teknolojia rafiki kwa mazingira. Aidha, amesisitiza kuwa mafanikio ya mageuzi ya kijani yanategemea uwekezaji wa kutosha, upatikanaji wa teknolojia za kisasa pamoja na ushirikiano madhubuti kati ya serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo. Amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kuendeleza viwanda vinavyoongeza thamani ya rasilimali, kudhibiti taka na kuvutia uwekezaji huku akiwakaribisha wafanyabiashara kuwekeza nchini kwa lengo la kujenga uchumi imara na shindani.Mkutano huo umeandaliwa na Serikali ya Uturuki kupitia taasisi ya Zero Waste Foundation inayosimamiwa na Mwenza wa Rais wa Uturuki Bibi Emine Erdoğan na umeleta pamoja washiriki zaidi ya 3,000 kutoka nchi zote duniani, pamoja na taasisi za kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Umoja wa Mataifa, Benki ya Maendeleo ya Nchi za Kiarabu na Shirika la Maendeleo na Biashara la Umoja wa Mataifa (UNCTAD).

.jpg)














.jpeg)
.jpeg)










.jpg)


