HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

SAT, I AM ORGANIC WATUMIA SABASABA KUHAMASISHA KILIMO HAI NA AFYA BORA

July 08, 2026 Add Comment

Meneja miradi wa Shirika la kilimo Endelevu Tanzania (SAT), Bw. Peter Mwangalo, akiwaonyesha wananchi na waandishi wa habari (hawapo pichani) bidhaa mbalimbali zinazotokana na kilimo hai, ambacho huzalisha mazao bila matumizi ya kemikali na mbolea zenye madhara, katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam, chini ya uratibu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE).

TANZANIA NA QATAR KUENDELEA KUSHIRIKIANA KUFUNGUA FURSA ZA AJIRA KWA VIJANA

July 07, 2026 Add Comment
Na: OWM (KAM) – Doha, Qatar

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, amesema Tanzania na Qatar zimeendelea kushiurikiana kwa karibu katika sekta mbalimbali, ikiwemo masuala ya ajira ambapo tangu nchi hizo ziliposaini makubaliano ya ushirikiano wa ajira mwaka 2018 mafanikio makubwa yameonekana katika kuongezeka kwa fursa za ajira kwa Watanzania.

UTPC YAWAWEZESHA WAANDISHI WA HABARI WANAWAKE KUKABILIANA NA VITISHO VYA KIDIJITALI

July 07, 2026 Add Comment


Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Usalama wa Kidijitali na Ukatili wa Kijinsia Mtandaoni kwa Waandishi wa Habari Wanawake yaliyofanyika mjini Morogoro.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Usalama wa Kidijitali na Ukatili wa Kijinsia Mtandaoni kwa Waandishi wa Habari Wanawake yaliyofanyika mjini Morogoro.
Washiriki wa mafunzo ya usalama wa kidijitali kwa waandishi wa habari wa kike wakipiga picha ya pamoja

Na Elizabeth Cosmas, Morogoro

Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) umeendesha mafunzo maalumu ya Usalama wa Kidijitali na Ukatili wa Kijinsia Mtandaoni kwa Waandishi wa Habari Wanawake, yakilenga kuimarisha uwezo wao wa kutumia mazingira ya kidijitali kwa usalama, kujiamini na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao ya kitaaluma.

MMS ATEMBELEA WADAU MAONESHO YA SABASABA 2026

July 07, 2026 Add Comment
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, akisaini kitabu cha wageni alipowasilikwemye viwanja vya maonyesho vya Mwalimu Nyerere vilivyopo Barabara ya Kilwa Dar es Salaam Julai 6, 2026.

VIONGOZI NA WATUMISHI WA TRA WASIMAMA NA KUPIGA MAKOFI KWA DAKIKA 1 KUWASHUKURU WALIPAKODI

July 07, 2026 Add Comment

 

Viongozi na watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wamesimama na kupiga makofi kwa muda wa dakika moja wakati wa kikao cha tathmini ya utendaji kazi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ikiwa ni ishara ya kuwapongeza na kuwashukuru Walipakodi kote nchini kwa kuendelea kulipa kodi kwa hiari.

TBS YATOA ELIMU YA UTHIBITISHAJI WA BIDHAA KWA WAJASIRIAMALI SABASABA

July 07, 2026 Add Comment
SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutoa elimu na kuwahamasisha wajasiriamali kuthibitisha ubora wa bidhaa zao ili kukidhi matakwa ya sheria za viwango na kuongeza ushindani wa bidhaa hizo katika soko la ndani na nje ya nchi.

TIRDO YAWAWEZESHA WAJASIRIAMALI KWA TEKNOLOJIA YA KUCHAKATA NGOZI

July 07, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Matumizi ya kemikali katika uchakataji wa ngozi yanatarajiwa kupungua kufuatia ubunifu wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) wa kubuni dawa ya asili inayotokana na mimea, teknolojia inayolenga kulinda mazingira, afya za watumiaji na kuongeza ushindani wa bidhaa za ngozi za Tanzania katika masoko ya ndani na kimataifa.

BODI YA UTALII TANZANIA IMETAKIWA KUZINGATIA UBUNIFU, UWAJIBIKAJI NA UZALENDO KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE PIA KUISHIRIKISHA SEKTA BINAFSI*

July 07, 2026 Add Comment

 



Bodi ya Wakurugenzi ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imetakiwa kuisimamia ipasavyo Taasisi hiyo na kuishirikisha sekta binafsi ili kufikia malengo ya Taifa yaliyokusudiwa katika sekta ya Utalii.


Maelekezo hayo yametolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokutana na kufanya mazungumzo na Wajumbe Bodi hiyo Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufanya tathmini, kushauri na kuboresha ili kuiwezesha TTB kufikia malengo yaliyokusudiwa. 

Ameongeza kuwa ili kufikia malengo ya kuwa na watalii milioni nane ifikapo 2030 ni lazima Sekta binafsi ishirikishwe ipasavyo ili kukuza utalii na kuongeza ushindani wa Tanzania katika soko la kimataifa.

"Tushirikishe sekta binafsi ili tuweze kufikia malengo. Hata jumbe tunazozipeleka kwenye masoko tuwashirikishe sekta binafsi ili tuweze kufanikiwa kufikisha watalii milioni 8 na zaidi ifikapo mwaka 2030. Sekta binafsi iwe sehemu ya maisha yetu ya kila siku," amesema Dkt. Kijaji.

Aidha, ameitaka Bodi hiyo kuweka malengo yanayopimika yatakayowezesha kutathmini utendaji wake na kuongeza ufanisi katika kufikia azma ya Serikali ya kuongeza idadi ya watalii nchini.

Pia, amesisitiza umuhimu wa TTB kuendelea kufanya tafiti na kufuatilia mwenendo wa masoko mbalimbali ya utalii duniani ili kubaini mahitaji ya watalii na kuishauri Serikali pamoja na taasisi zake kuhusu maboresho yanayohitajika.

"Sisi ndio tuliopewa jukumu la kuiuza nchi huko nje, hivyo tunapaswa kuzishauri taasisi nyingine kuhusu mahitaji ya soko la kimataifa. Kwa mfano, TFS na taasisi nyingine zinapaswa kufahamu kwa wakati mahitaji ya watalii ili ziweze kuboresha huduma na bidhaa za utalii," amesema.

Akizungumzia matukio makubwa yanayotarajiwa kufanyika nchini, ikiwemo AFCON na Mkutano wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Kijaji ameitaka Bodi ya Utalii kuhakikisha inajiandaa kikamilifu kutumia matukio hayo kama fursa ya kuitangaza Tanzania na vivutio vyake vya utalii katika masoko ya kimataifa.

"Tunayo matukio kadhaa makubwa yanayokuja mbele yetu. Tujipange vya kutosha kabla ya matukio hayo ili tuyatumie kama fursa ya kuitangaza Tanzania na kuongeza idadi ya watalii," amesema.

Ameongeza kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 unahitaji taasisi zote kupanga na kutekeleza mikakati kwa pamoja ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTB, Mhe. Balozi Dkt. Ramadhani Kitwana Dau, amesema Bodi hiyo imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha inafikia malengo ya Serikali katika sekta ya utalii. Amesisitiza kuwa moja ya malengo makuu ni kufikisha idadi ya watalii zaidi ya milioni 8 ifikapo mwaka 2030, sambamba na kuvuka lengo lililowekwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

Kikao hicho cha Dkt. Kijaji na Bodi ya Wakurugenzi ya TTB kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara, akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara, Dkt. Hassan Abbas, Mkurugenzi wa Utawala, Benard Marcelline; Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Dkt. Theresa Mugobi, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Emmanuel Buhohela, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),  Ephraim Mafuru; pamoja na wajumbe wa Bodi hiyo.






DKT. MWIGULU AALIKA WAFANYABIASHARA WA UFARANSA KUWEKEZA TANZANIA

July 06, 2026 Add Comment
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amewaalika wafanyabiashara wa Ufaransa kuwekeza Tanzania, akisisitiza kuwa mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyopo nchini yanatoa fursa kubwa za kukuza biashara, kuzalisha ajira, kuhamisha teknolojia na ujuzi, pamoja na kuharakisha ujenzi wa uchumi wa viwanda wenye manufaa kwa Tanzania na Ufaransa.

TEA YAONGEZA JUHUDI ZA KUTAFUTA RASILIMALI KUSAIDIA MAGEUZI YA ELIMU

July 06, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA) imeeleza kuwa imejikita katika kutafuta rasilimali zitakazowezesha utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2023, kwa kuwekeza nguvu katika maeneo matatu ya kipaumbele ambayo ni ujenzi wa miundombinu kwa elimu ya lazima ya miaka 10, maendeleo ya mkondo wa amali pamoja na matumizi ya nishati safi na uhifadhi wa mazingira shuleni.

FCC YAIMARISHA ELIMU YA USHINDANI KWA WAFANYABIASHARA SABASABA

July 06, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAFANYABIASHARA na wananchi kwa ujumla wametakiwa kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) kutembelea banda la Tume ya Ushindani (FCC) ili kupata huduma mbalimbali za papo kwa papo pamoja na elimu kuhusu ulinzi wa mlaji, ushindani wa biashara na udhibiti wa bidhaa bandia.

WAZIRI WA ULINZI ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA NISHATI SABASABA

July 06, 2026 Add Comment




Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho ametembelea banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Nyerere jijini Dar es Salaam.


Katika Banda la Wizara amepata maelezo kuhusu Sera ya Nishati ya Mwaka 2015 pamoja na mikakati mingine inayosimamiwa na Wizara ya Nishati ukiwemo Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Mkakati wa Matumizi Bora ya Nishati na Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia.




WAZIRI NDEJEMBI AJADILI AWAMU YA PILI YA MRADI WA UMEME WA JUA KISHAPU NA WASHIRIKA WA MAENDELEO.

July 06, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu - Paris, Ufaransa

Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi kutoka Wizara ya Fedha ya Ufaransa, Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) pamoja na kampuni ya SAGECOM, kwa lengo la kujadili utekelezaji wa awamu ya pili ya Mradi wa Uzalishaji Umeme wa Jua wa Megawati 100 unaotekelezwa katika Wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga.


Mazungumzo hayo yamefanyika leo, Julai 6, 2026, katika Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Paris, Ufaransa.


Katika kikao hicho, Mhe. Ndejembi ameishukuru Serikali ya Ufaransa kupitia Wizara yake ya Fedha na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu wa Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya nishati. Amesema ushirikiano huo umeendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha upatikanaji wa nishati ya uhakika na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa AFD, Bi. Sandra Kassab, ameipongeza Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati kwa hatua kubwa iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi ya nishati, hususan ile inayolenga kuongeza uzalishaji wa umeme na kuimarisha matumizi ya nishati safi. Aidha, ameahidi kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa ufanisi na kuleta manufaa kwa wananchi wa Tanzania.




“WOMEN TAKING OVER” YA BARRICK YAWATIA MOYO WANAWAKE KUTOBAKI NYUMA SEKTA YA MADINI

July 06, 2026 Add Comment

  

Zoezi la kukata keki likiendelea wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini, yaliyoandaliwa na Barrick North Mara chini ya kaulimbiu ya "Women Taking Over."
Baadhi ya wafanyakazi wanawake wa Barrick North Mara, Bulyanhulu pamoja na kampuni za wakandarasi wazawa wakiwa katika picha ya pamoja katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyofanyika katika Mgodi wa Dhahabu wa North Mara chini ya kaulimbiu ya "Women Taking Over"
Maonyesho ya mavazi na sare mbalimbali zinazotumika migodini yalikuwa miongoni mwa vivutio vilivyopamba maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko, akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyofanyika katika Mgodi wa Dhahabu wa North Mara.
Meneja Mahusiano Msaidizi wa Barrick North Mara, Nasieku Kisambu, akisoma risala kwa mgeni rasmi, akieleza mafanikio na shughuli mbalimbali zilizotekelezwa katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyofanyika Mgodi wa Dhahabu wa North Mara.

Baadhi ya washiriki walitunukiwa vyeti
Baadhi ya washiriki walitunukiwa vyeti
Baadhi ya washiriki walitunukiwa vyeti
Baadhi ya wanawake walioshiriki katika picha ya pamoja
Baadhi ya wanawake walioshiriki katika picha ya pamoja
Meneja Mkuu Apolinary Lyambiko akiwa na Maofisa waandamizi wa mgodi wa Barrick North Mara.

***

Katika kuendelea kuhamasisha usawa wa kijinsia na kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta ya madini, Kampuni ya Barrick imefanya maadhimisho makubwa ya Siku ya Wanawake katika Sekta ya Madini yaliyowakutanisha wafanyakazi wanawake kutoka migodi ya North Mara na Bulyanhulu pamoja na wanawake kutoka kampuni mbalimbali za wakandarasi wazawa wanaoshirikiana na migodi hiyo.

KIGOGO WA CHADEMA TANGA RASHID JUMBE ATANGAZA KUMALIZA SAFARI YA MIAKA 30 UPINZANI,AHAMIA CCM

July 06, 2026 Add Comment

 


>Asema kasi ya maendeleo chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, amani, uchumi, afya, maji na miundombinu vimemshawishi kubadili msimamo wa kisiasa.

Na Oscar Assenga,TANGA

Baada ya zaidi ya miaka 30 ya kuwa mwanasiasa wa upinzani, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Tanga, Rashid Jumbe, amefanya uamuzi mkubwa wa kisiasa kwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Jumbe, ambaye kwa muda mrefu alikuwa mmoja wa viongozi mashuhuri wa Chadema mkoani Tanga, amesema uamuzi wake umetokana na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na juhudi za Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha amani, umoja na ustawi wa wananchi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kumpokea ndani ya CCM iliyoongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, Jumbe alisema hakufanya uamuzi huo kwa papara, bali baada ya kutafakari kwa kina na kujiridhisha kuhusu mwelekeo wa maendeleo ya taifa.

"Nilikuwa mpinzani kwa zaidi ya miaka 30, lakini leo nimeamua kuhitimisha safari hiyo. Kilichonishawishi zaidi ni kazi kubwa inayofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea Watanzania maendeleo na kuhakikisha amani ya nchi inalindwa," alisema.

Alieleza kuwa pia amevutiwa na utekelezaji wa falsafa ya 4R inayosisitiza maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya, akisema imeongeza mshikamano na kuimarisha mazingira ya maendeleo nchini.

Akizungumzia Mkoa wa Tanga, Jumbe alisema mabadiliko yanayoonekana katika sekta mbalimbali ni ushahidi wa dhamira ya Serikali ya kuufungua mkoa huo kiuchumi.

Alitaja kuongezeka kwa shughuli katika Bandari ya Tanga, ujenzi wa bandari kavu pamoja na utekelezaji wa miradi mingine ya kimkakati kuwa miongoni mwa hatua zilizochochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za biashara.

"Nimekuwa nikipaza sauti kwa miaka mingi nikitaka Tanga ifunguliwe kiuchumi. Leo naona hilo limefanyika. Mizigo imeongezeka bandarini, bandari kavu zimejengwa na shughuli za biashara zinaendelea kukua," alisema.

Katika sekta ya afya, Jumbe alisema maboresho yaliyofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba pamoja na ujenzi wa zahanati katika kata na mitaa mbalimbali vimempa imani kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma kwa wananchi.

Aidha, alisema upanuzi wa huduma za maji na umeme pamoja na utekelezaji wa mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni miongoni mwa hatua zinazoonyesha dhamira ya Serikali ya kuinua maisha ya Watanzania.


"Nilijiuliza ni hoja gani itanifanya nibaki upinzani wakati maendeleo yanaonekana wazi. Tanga ina amani, huduma zinaimarika na wananchi wanaendelea kunufaika na miradi ya maendeleo," alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga, Rajab Abdurhaman, alisema chama hicho kinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano ili kuongeza uwezo wake wa kusimamia maendeleo na kuwatumikia wananchi.

Alisema tangu alipopewa dhamana ya kuongoza CCM mkoani humo, ameweka mkakati wa kuimarisha chama kupitia ushirikiano na wanachama pamoja na kuwakaribisha viongozi kutoka vyama vingine vya siasa.

Rajab alisema mkakati huo umeendelea kuzaa matunda, akieleza kuwa kujiunga kwa Rashid Jumbe ni ishara ya kuongezeka kwa imani ya baadhi ya viongozi wa upinzani kwa juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali.

"Jumbe alikuwa mmoja wa viongozi wakubwa wa upinzani katika Wilaya ya Tanga. Tuliahidi kwamba tutamshawishi aje kushirikiana nasi katika kujenga chama na kuwaletea wananchi maendeleo, na leo tumefanikiwa," alisema.

NHIF TANGA YATOA ELIMU YA BIMA NA KUFANYA UPIMAJI WA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA KANISA LA KKKT USHIRIKA WA MAKORORA TANGA

July 06, 2026 Add Comment



Na Oscar Assenga,TANGA

Wazazi, walezi na waajiri nchini wamehimizwa kuhakikisha watoto wanawakatia bima ya afya mapema ili kuwaepusha na changamoto za gharama kubwa za matibabu na kuwawezesha kupata huduma za afya kwa wakati wanapougua.

Wito huo umetolewa leo na Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Tanga, Macrina Clemens, wakati wa utoaji wa elimu kuhusu bima ya afya ulioambatana na zoezi la upimaji wa afya na usajili wa wanachama wa vifurushi mbalimbali katika Kanisa la KKKT Ushirika wa Makorora, jijini Tanga.

Akizungumza na waumini wa kanisa hilo, Macrina alisema afya ni mtaji muhimu kwa maendeleo ya familia na Taifa, hivyo kujiunga na bima ya afya ni uwekezaji unaowalinda wananchi dhidi ya gharama zisizotarajiwa za matibabu.

Alisema wazazi wanaowakatia watoto wao bima ya afya hupata uhakika wa matibabu wakati wowote mtoto anapougua, jambo linalowapa utulivu wa akili na kuwawezesha watoto kuendelea na masomo bila kukatishwa na changamoto za kifedha.

“Mzazi anapokuwa na bima ya afya kwa mtoto wake anakuwa na uhakika wa kupata matibabu kwa wakati, hivyo kuepuka usumbufu wa kutafuta fedha za dharura kila ugonjwa unapojitokeza,” alisema.

Macrina alisema wanafunzi wanaosoma katika shule mbalimbali wanaweza kujiunga na bima ya afya kupitia shule zao kwa gharama ya Sh50,400 kwa mwaka mzima wa masomo, huku watoto ambao bado hawajaanza shule wakijiunga kupitia vifurushi mbalimbali vinavyotolewa na NHIF.

Alisema Serikali inaendelea kutekeleza azma ya kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa na bima ya afya, hivyo akazitaka taasisi za elimu, wazazi, walezi, waajiri na wamiliki wa kampuni binafsi kutumia fursa hiyo kuwaandikisha watoto na wafanyakazi wao.

“Bima ya afya si gharama, ni kinga ya maisha. Ukiwa na bima unakuwa na uhakika wa kupata daktari, dawa na huduma za matibabu bila kubeba mzigo mkubwa wa kifedha pale unapougua,” alisema.

NHIF imeendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya wananchi kuhusu umuhimu wa bima ya afya ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuongeza idadi ya Watanzania wanaonufaika na huduma hiyo na kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya nchini.




KABUDI AIPONGEZA DCEA KWA ELIMU YA MADHARA YA DAWA ZA KULEVYA SABASABA,

July 05, 2026 Add Comment

-Awahimiza wananchi kutembelea banda la Ofisi ya Waziri Mkuu

BODI YA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI MIRADI YA REA

July 05, 2026 Add Comment




📌*Watembelea Banda la REA kwenye maonesho ya Sabasaba*


📌*Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa miradi ya nishati safi Vijijini*


Leo tarehe 5 Julai, 2026 kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) wametembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika maonesho yanayoendelea ndani ya Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. 

Katika banda hilo, wajumbe wa REB wameelezwa kuhusu utekelezaji wa miradi ya usambazaji umeme kwenye maeneo ya vitongoji na uwezeshaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inayoendelea nchini. 



*Karibu Sabasaba, karibu Banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)*