HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

DID TANZANIA KUTOA ELIMU YA UTUNZAJI MAZINGIRA ROMBO KWA KUTUMIA SANAA YA MAJUKWAANI

March 31, 2026 Add Comment

 




Na. Mwandishi Wetu,


DIVERSITY Initiatives for Development Tanzania (DID TANZANIA) ambao ni waratibu wa mradi wa Sauti za Mabonde "Voices of Valley" uliojikita kutoa elimu ya utunzaji wa Mazingira Wilayani Rombo wanatarajia kufikia Jamii kwa kutumia Sanaa ya majukwaani.


Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa DID Tanzania, Bw. Optatus Nestory Mbararia ambaye ni mratibu mkuu wa mradi amesema kuwa, utafiti wa awali wamebaini uharibifu mkubwa wa Mazingira ikiwemo eneo la chanzo cha maji cha Kamdawi na bonde la Tarakea, unaotokana na shughuli za Kijamii kama uchimbaji mchanga, kubonda kokokoto, ukataji wa miti na Kilimo kisicho rasmi pembezoni mwa vyanzo vya maji.

"Kwa sasa tupo hatua ya mwisho kwa Vijana Wasanii wakifanya mazoezi ya onesho lao kwa njia ya sanaa za jukwaani.


Watafanya maonesho kadhaa ambayo ni ya wazi jukwaani, kufikisha ujumbe." Amesema Optatus Mbararia.

Mradi ni wa mwaka mmoja, ambapo unaenda kutoa elimu kwa Jamii juu ya utunzaji wa Mazingira hususani vyanzo hivyo vya maji na mito mbalimbali Wilayani Rombo, Mkoani Kilimanjaro.


Aidha, amebainisha kuwa, mbali ya utoaji elimu kwa njia ya  Sanaa za majukwaani, Pia watakuwa na shughuli za upandaji miti kama utunzaji wa Mazingira, ambapo miti zaidi ya 1,000 itapandwa katika chanzo cha maji kamdawi na bonde la Mto Tarakea.

"Mradi wetu huu pia tunatarajia kushirikiana na wadau muhimu ikiwemo Halmashauri ya Rombo kupanda miti.


Lakini pia mijadala ya kijamii na Wananchi watatoa maoni yao." Amesema Bw. Optatus Nestory Mbararia.

Kwa Upande wao baadhi ya Wasanii Vijana wamebainisha kuwa wapo tayari na wamejiandaa vyema kufikisha elimu ya utunzaji mazingira kwa njia ya Sanaa za majukwaani 

Dumey Aloys Kijwiti msanii wa sanaa maagizo asema kupitia sanaa ujumbe utafika kwa haraka kwa Jamii.


"Naamini  Sanaa ni njia rahisi kufikisha ujumbe kwa Jamii, ni kitu rahisi zaidi kuliko chochote.


Sanaa ni njia rahisi ya kutatua na kuchanganua na kuleta majibu katika Jamii.


Kwa kupitia mradi wa voices of valley, nikiwa kama mratibu wa maigizo ya jukwaani, naamini na wenzangu tunaendelea vyema kufikisha ujumbe kwa Wananchi.


Sanaa kwa maendeleo Ina aina zake, kwa maana Sanaa Ina hatua zaidi ya Saba, na sie mwisho wa siku tunaenda kufanya Sanaa kwa  maendeleo.


Naamini Jamii itatupokea vizuri kwani tunaenda kuwapa mawazo mapya na kuonesha mambo ambao hayatakiwi kwa Jamii, na kulinda mazingira." Amesema Dumey.


Mradi huo ni program ya Vijana Artwork (Vijanam @rtwork) unasimamiwa na CDEA na Goethe Institut kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).



Mwisho.

KITUO CHA UMEME IFAKARA CHACHOCHEA MAENDELEO KILOMBERO

March 31, 2026 Add Comment



📌Kimetekelezwa na REA kwa gharama ya Tsh. Bilioni 25


📌DC Kilombero aipongeza REA, atoa wito kwa wawekezaji


📌Kimeimarisha upatikanaji wa umeme Ukanda wa Morogoro Kusini


Ifakara, Kilombero


Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetumia shilingi bilioni 25 kujenga Kituo cha Kupoza Umeme 1x20MVA, 220/33kv pamoja na njia za kusambaza Umeme katika Wilaya ya Kilombero, hatua ambayo imeboresha upatikanaji wa umeme na kuondoa changamoto ya kukatika kwa nishati hiyo katika wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi.


Hayo yameelezwa leo Jumanne Machi 31, 2026 wakati wa ziara ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) waliotembelea mradi huo kujionea utekelezaji wake na tija yake kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika ukanda wa Morogoro Kusini.

"Fursa za uwekezaji wilayani hapa zimeongezeka baada ya kukamilika kwa kituo hiki, ninatoa wito kwa wawekezaji kujitokeza kwa wingi kwani tunao umeme wa uhakika na toshelevu," amebainisha Wakili Kyoba. 


Amesema kuimarika kwa huduma ya umeme kumechochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi, hususan katika sekta za viwanda, uchimbaji madini, kilimo na huduma za kijamii.

Kwa upande wake, Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme kutoka REA, Mhandisi Deogratius Nagu, amesema gharama za mradi huo zinahusisha pia usimikaji wa mashine umba (transfoma) pamoja na mifumo yake ya uendeshaji, udhibiti na ulinzi, ujenzi wa njia za kusafirisha umeme za msongo wa kilovolti 33 zenye urefu wa kilometa 70 pamoja na gharama za mshauri elekezi.


Mhandisi Nagu amebainisha kuwa, kituo hicho ni cha kisasa, kikiwa na teknolojia kutoka nchi mbalimbali ikiwemo transfoma kutoka Bulgaria, mifumo ya udhibiti na ulinzi kutoka Hispania pamoja na mifumo ya switching (switchgears) kutoka Ujerumani.

“Kituo hiki kimeondoa changamoto ya upatikanaji wa umeme katika wilaya za Kilombero na Ulanga na kuwezesha wananchi kuendeleza shughuli za uzalishaji na kuongeza thamani ya mazao,” alisema Nagu.

Naye Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, amesema uwekezaji huo unaonesha matumizi sahihi ya rasilimali za umma na mchango wa REA katika kusambaza huduma ya umeme vijijini.


"Tumeshuhudia uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kupitia REA, ni fursa ya maendeleo kwa wananchi ni muhimu tukachangamkia Uwepo wa umeme wa uhakika kujiletea maeendeleo," amesema Balile.

Balile amesema REA imeonyesha mfano wa kipekee kwenye utekelezaji wa majukumu yake na kwamba kazi iliyokwishakamilika ni kubwa na manufaa yake yanaonekana na ametoa wito kwa Taasisi zingine za Serikali kuiga mfano huo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanufaika wa mradi huo wameeleza namna ambavyo Mradi huo umekuwa mkombozi kwao.


Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kilimo Ifakara, Setina Ngailo, amesema huduma ya umeme imeimarika na kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme iliyokuwa ikiathiri shughuli za shule.


Kwa upande wake, Msimamizi wa Hospitali ya Kansa ya Good Samaritan, Father Charles Masawe, amesema upatikanaji wa umeme wa uhakika umeongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya kwa kupunguza utegemezi wa jenereta.


Naye Meneja wa Kiwanda cha Kukoboa Mpunga cha Bezelengule, Enos Machumu, amesema uzalishaji umeongezeka kwa kiasi kikubwa kufuatia kuboreshwa kwa huduma ya umeme, hali iliyorejesha wateja na kulinda mitambo dhidi ya uharibifu.

Kwa ujumla, mradi huo unatajwa kuwa kichocheo muhimu cha maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika ukanda wa Morogoro Kusini, huku serikali ikiendelea na juhudi za kusambaza umeme katika vitongoji vilivyobaki ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi wote.


-Mwisho-

MKURUGENZI MKUU REA AAGIZA UFANISI KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 9,009

March 31, 2026 Add Comment


Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi, Hassan Saidy amewataka Watumishi wa Wakala kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha ndani ya muda uliopangwa wanafikisha umeme kwenye vitongoji vyote vya Tanzania Bara.
Ametoa maelekezo hayo Machi 30, 2026 Makao Makuu ya REA, Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi na Watumishi wote, ambapo amesema baada ya kusaini Mradi mkubwa wa HEP II (B); Mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 tarehe 17 Januari, 2026 na kuongeza kuwa kazi iliyombele ya kila Mtumishi ni kuhakikisha vitongoji hivyo vinafikishiwa umeme katika kipindi cha miaka mitatu yaani hadi 2029.

Awali ilielezwa kuwa Mradi huo wa HEP II (B) ni muendelezo wa jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) za kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme kwa Wananchi wote wa Tanzania Bara.

Mhandisi Saidy amesema kukamilika kwa Mradi huo wa HEP II (B) pamoja na miradi mingine inayoendelea kutafanya jumla ya vitongoji ambavyo tayari vitakuwa vimefikishiwa umeme kuwa takriban 51,000 kufanya vitongoji vitakavyobakia bila umeme na bila kuwa katika mradi wowote kuwa taklibani 13,000 ambavyo vimepangwa kuanza kusambaziwa umeme ifikapo mwaka 2030 kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2025 – 2030.

Mradi huo unatarajiwa kutoa manufaa ya moja kwa moja kwa Wananchi kwa kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme vitongojini; kuboresha huduma za kijamii hususan katika sekta za afya, elimu na maji; kuwezesha matumizi ya umeme katika shughuli za uzalishaji na kuongeza kipato cha Wananchi pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wa maeneo ya vitogojini pamoja na kuimarisha ustawi wa jamii.

Aidha; Mhandisi, Saidy aliongoza Watumishi wa REA katika zoezi la kuchagua Viongozi wa TUGHE tawini hapo ambapo kwa kauli moja Watumishi waliwachagua Viongozi wao katika ngazi tofauti kama ifuatavyo: – Mwenyekiti wa Tawi ni Bwana Swalehe Kiloza, Katibu wa Tawi ni Mhandisi, Annet Malingumu; Mjumbe wa Halmashauri ya Tawi ni Bwana Issa Sabuni na Mwakilishi wa Kundi la Vijana, Mhandisi, Issac Sanga.

Viongozi wengine ni pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Wanawake ya Tawi la TUGHE REA ni kama ifuatavyo: – Mwenyekiti ni Bi. Wilhelmina Cheyo; Katibu ni Bi. Ruth Emmanuel; Mweka Hazina ni Bi. Aveline Wilfred; Wajumbe Kamati ya Wanawake ni Bi. Happiness Ndunguru na Mhandisi, Bertha Mwaituka.

Vilevile Watumishi wa REA pia walichagua Viongozi kwa upande wa Klabu ya Michezo ya REA ambapo itaongozwa na Bwana Selemani Mtunzy kama Mwenyekiti na Mwenyekiti Msaidizi ni Bwana Samwel Sumwa; Katibu ni Bwana Praygod Ng’hunda; Mweka Hazina ni Bwana Daniel Kisaka wakati Wajumbe wa Kamati Tendaji kwa upande wa Wanaume atakuwa Mhandisi, Thomas Mmbaga na kwa upande wa Wanawake atakuwa Bi. Beatrice Shelukindo.

Wakati huo huo Watumishi wa REA walishiriki kwenye zoezi la kuchagua Viongozi wa Chama cha Kijamii cha Wafanyakazi (REA Social Club) chenye lengo la kusaidiana wakati wa raha na changamoto mbalimbali. Viongozi wa Chama hicho waliochaguliwa ni kama ifuatavyo: Mwenyekiti ni Bwana Elias Gunzer; Katibu ni Bi. Theresia Mang’ung’ula; Mweka Hazina ni Bwana Shukuru Malebeto; Wajumbe wa Kamati Tendaji ni Bwana Pastory Mwijage na Bi. Emmy Chali.





DC NYAMWESE: UWEPO WA BENKI YA NMB NI NYENZO MUHIMU KUCHOCHEA UCHUMI WA WANANCHI

March 31, 2026 Add Comment

Na Oscar Assenga, Handeni

MKUU wa Wilaya ya Handeni, Salum Nyamwese, amesema uwepo wa taasisi za kifedha, ikiwemo Benki ya NMB, ni nyenzo muhimu katika kuchochea na kuimarisha uchumi wa wananchi kupitia sekta mbalimbali kama kilimo, mifugo na biashara ndogondogo.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutilia mkazo juhudi za kuimarisha uchumi wa wananchi wa vijijini ili waweze kujikwamua kiuchumi na kimaendeleo.

Nyamwese alitoa kauli hiyo leo wakati wa tamasha la “NMB Kijiji Day” lililoandaliwa na Benki ya NMB wilayani Handeni, likihusisha matembezi, mbio fupi na mazoezi, kwa lengo la kuwakutanisha wananchi na kuwahamasisha kushiriki shughuli za maendeleo.

Alisema uwepo wa benki hiyo katika tamasha hilo haujalenga kutangaza huduma zake pekee, bali pia kutoa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo upimaji wa afya na uchangiaji wa damu, jambo ambalo lina manufaa makubwa kwa jamii.

“Ninawahimiza wananchi wa Handeni kutumia fursa hii kujitokeza kwa wingi kupata elimu ya fedha, kufungua akaunti na kujifunza namna bora ya kusimamia mapato yao. Ni muhimu pia kuhakikisha mikopo inayopatikana inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuleta tija kwa familia na jamii kwa ujumla,” alisema Nyamwese.

Aidha, alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia wananchi wengi zaidi, hususan waliopo maeneo ya pembezoni kupitia mtandao mpana wa matawi na mawakala.

Awali, akizungumza katika tamasha hilo, Mkuu wa Idara ya Mauzo na Mtandao wa Matawi wa Benki ya NMB Makao Makuu, Donatus Richard, alisema “NMB Kijiji Day” ni jukwaa muhimu la kushirikiana na jamii kupitia utoaji wa elimu ya kifedha na huduma za kibenki.


Alisema kupitia tamasha hilo, benki hiyo hutoa elimu ya masuala ya fedha, kufungua akaunti kwa wananchi na kuimarisha mshikamano wa kijamii, sambamba na kuhamasisha afya na ustawi kupitia michezo na burudani.

Donatus alibainisha kuwa hapo awali huduma nyingi za kibenki zilikuwa zinapatikana zaidi mijini, lakini kuanzia mwaka 2024 benki hiyo ilianza mkakati wa kupeleka huduma hizo vijijini.

“Kwa sasa tuna matawi zaidi ya 248 nchini kote, na hata maeneo yasiyo na matawi tunahakikisha huduma zinapatikana kupitia mawakala. Tumeweza kufikia zaidi ya vijiji 3,000 tangu mwaka 2024 ambavyo hapo awali havikuwa na huduma za kibenki,” alisema.

Aliongeza kuwa juhudi hizo zimeongeza idadi ya wateja, ambapo zaidi ya akaunti milioni mbili zimefunguliwa kuanzia mwaka 2024 hadi Januari mwaka huu.

Kwa mwaka 2026, alisema benki hiyo imejipanga kufikisha huduma za kibenki katika vijiji vingine 2,000 ambavyo bado havijafikiwa, sambamba na kuendelea kushiriki katika shughuli za kijamii kama michezo na upandaji miti ili kulinda mazingira.

Aidha, alisema benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira, ikiwemo kuhimiza matumizi ya nishati safi badala ya mkaa.

“Benki yetu inatambua umuhimu wa kuhifadhi mazingira na tunatambulika kimataifa kwa uwajibikaji wa kijamii. Fedha za wateja wetu ziko salama na wanapata huduma bora kwa wakati,” alisema.

Alibainisha kuwa mwaka 2026 benki hiyo imetambuliwa kwa ubora katika masuala ya uendelevu nchini, ikiwa na zaidi ya matawi 248, mashine za ATM zaidi ya 700, mawakala 73,000 na wateja zaidi ya milioni 10.

Mwisho, alitoa wito kwa wananchi ambao bado hawajafungua akaunti kufanya hivyo ili waweze kunufaika na huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.

Mwisho.

WANANCHI IDODI WAMLILIA LUKUVI

March 31, 2026 Add Comment



NA. MWANDISHI WETU – IDODI IRINGA

Wananchi wamlilia aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge Uratibu na Wenye Ulemavu na Mbunge wa Jimbo la Isimani Marehemu William Lukuvi kwa kazi nzuri alizozifanya wakati akitekeleza majukumu yake katika sekta mbalimbali serikalini na kuwaletea maendeleo katika nyanja mbalimbali.


Hayo yamelezwa kwa wakati tofauti hii leo 30 Machi, 2026 wakati mwili wa marehemu Lukuvi ulipowasili Kijijini Kwake Kata ya Idodi, Wilaya ya Iringa Vijijini ambapo ndipo kunatarajiwa kuwa makazi yake ya milele mara baada ya ibada ya mazishi kijijini hapo.

Wananchi hao wameonesha simanzi kubwa na kumkumbuka kama kiongozi shupavu, na mtetezi wa wanyonge hususan kwa wakazi wa Jimbo Lake la Isimani mkoani Iringa.

Akizungumza na waandishi wa habari Mmoja wa waombolezaji Bw. Kombo  Jumbe amesema Marehemu William Lukuvi aliasisi utaratibu wa kliniki za ardhi wakati akiwa anahudumu kama Waziri wa Ardhi na hivyo kuwezesha wananchi kuhudumiwa kwa  urahisi na kwa haraka.


“Marehemu Lukuvi alituwezesha sisi hupata huduma kwa haraka hasa zilizohusu masuala ya migogoro ya ardhi na kufanya kufikiwa kwa urahisi na watoa huduma katika wizara ya ardhi  na yeye ndiye aliyezindua upatikanaji wa hati za ardhi na kufanya zoezi lile kuwa endelevu” alieleza

Kwa upande wake Bw. Frank Mbindile Mkazi wa Kijiji cha Magozi Wilaya ya Iringa amesema Marehemu William Lukuvi alikuwa ni mtu anayependa kusikiliza shida za watu kwa makundi na hata shida za mwananchi mmoja mmoja na kukiri kuwa wamepoteza mtu muhimu na Lulu kwa Taifa. 


“Ni aina ya kiongozi anayeamini katika kusimamia mambo ya msingi kwa ajili ya maslahi mapana ya wananchi na akizungumza jambo alikuwa anauwezo wa kulisimamia, hivyo wanaisimani tumepoteza kiongozi mkubwa,” alieleza.

=MWISHO=

KILIMANJARO MARATHON 2026: ZAIDI YA MBIO, NI FAHARI YA TAIFA

March 31, 2026 Add Comment

   

 Moshi ilichangamka kwa mara nyingine tena wakati maelfu ya wakimbiaji, mashabiki na wageni walipokusanyika kushiriki Kilimanjaro Marathon 2026. Tukio hili limeendelea kukua na kuwa zaidi ya mbio, likiunganisha michezo, utalii na jamii katika jukwaa moja.

ADEM NA TET KUIMARISHA MISINGI YA UJENZI WA UWEZO KWA WALIMU

March 31, 2026 Add Comment
WAKALA wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu nchini (ADEM) kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) wamefanya warsha maalumu ya kuhakiki Matini ya uendeshaji wa Jumuiya za Kujifunza za walimu na viongozi wa elimu (JzK), ikiwa ni hatua muhimu ya kukusanya maoni ya wadau kwa ajili ya kuboresha nyenzo hiyo.

WMA YATOA MSAADA WA VIFAA VYA UJENZI KWA WAHITAJI DODOMA

March 30, 2026 Add Comment

Katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, Wakala wa Vipimo (WMA) imetoa misaada ya vifaa vya ujenzi wa jiko la kisasa katika Kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu Cha RAHMAN ORPHANAGE CENTER kilichopo Chang'ombe jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kutoa misaada hiyo Meneja wa WMA Mkoa wa Dodoma Said Ibrahimu amesema suala la mazingira safi ya kupikia ni haki ya kila mmoja ndio maana wameamua kama Wakala kutoa misaada hiyo itakayowezesha upishi wa kisasa katika mazingira safi na salama ikiwemo usalama wa chakula kwani kituo hicho wamekuwa wakipika kwa kutumia kuni na mazingira ya Nje ambayo sio salama kwa afya ya watoto hao.

"tunamuunga mkono Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha nishati safi ya kupikia inakuwa katika mazingira safi na salama ndio maana leo kwa niaba ya wafanyakazi wa WMA tumekabidhi Sementi, Marumaru na vifaa vingine vitakavyosaidia ujenzi wa jiko hilo, "amesema Meneja Said

Kadhalika, Mkurugenzi wa kituo hicho Bi. Rukia Abdallah ameishukuru WMA kwa misaada hiyo itakayokwenda kuboresha mazingira ya mapishi katika Kituo hicho chenye idadi ya watoto 120 huku akiomba wadau wengine kujitokeza kuchangia kituo hicho ikiwemo suala la usafiri ili watoto hao waweze kutembelea maeneo mbalimbali kwa ajili ya kujifunza zaidi.

Mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo hicho Hazra Ramadhan ameipongeza Wakala wa Vipimo kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia na kuwaomba kuendelea kuwakumbuka kila mara ili waweze kutimiza malengo yao.







PPP YAONYESHA NJIA KUFIKIA MALENGO YA UMEME MEGAWATI 70,000 IFIKAPO 2050

March 30, 2026 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SEKTA binafsi imeelezwa kuwa nguzo muhimu katika kufanikisha malengo ya Mpango wa Nne wa Maendeleo (FYDP IV), huku Serikali ikisisitiza umuhimu wa kuongeza ushiriki wake katika uwekezaji wa nishati ili kufikia uzalishaji wa megawati 70,000 ifikapo mwaka 2050.

MISA YA KUOMBEA NA KUAGA MWILI WA MAREHEMU MHE.LUKUVI -IRINGA

March 30, 2026 Add Comment

Misa Takatifu ya kuuaga Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), na Mbunge wa Jimbo la Isimani, Marehemu Mhe. William Lukuvi, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu lililopo Kihesa Iringa leo tarehe 30 Machi, 2026 nakuongozwa na Askofu wa Jimbo la iringa Romanus Mihali.


Misa hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Viongozi wa dini pamoja na Waombolezaji kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Iringa na nje ya mkoa huo.

















Mhe. Lukuvi amefariki dunia tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Mkoani Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.