HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

KIPINDI CHA MWAKA 2021-2026 HUDUMA ZA AFYA ZIMEONGEZEKA, ZIMEIMARIKA

May 11, 2026 Add Comment


Na Hassan Kimweri, WAF - Dodoma

Sekta ya afya nchini imepata mafanikio makubwa katika kipindi cha awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yaliyoongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi kupitia ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa vifaa tiba, uoatikanaji wa dawa pamoja na huduma za kibingwa na za dharura nchini.

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema hayo leo Mei 11, 2026 wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Spika wa Bunge Mhe. Mussa Azan Zungu.

"Eneo la vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka kutoka elfu 10,153 mwaka 2021/22 hadi elfu 13,683 kufikia Machi 2026, sawa na ongezeko la vituo 3,530, Zahanati zimeongezeka kutoka elfu 7,189 hadi elfu 8,706 huku hospitali zikiongezeka kutoka mia 404 hadi mia 475 mwaka 2026," amesema Waziri Mchengerwa

Aidha, Waziri Mchengerwa amesema Serikali imeongeza majengo mapya katika hospitali mbalimbali zikiwemo Hospitali ya Muhimbili, KCMC, BMH, Bugando, Mirembe, pamoja na Kibong'oto huku ikiwa imejenga hospitali mpya 10 za rufaa za mikoa, kukarabati hospitali kongwe 50, kukamilisha maboma 980 ya zahanati na kujenga vituo vya afya 390.

Amesema, katika huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto, Serikali imeongeza wodi za watoto wachanga kutoka 80 hadi 438 pamoja na vituo vya upasuaji wa dharura kutoka 445 hadi 630 ambayo ni mafanikio yaliyochangia kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 556 mwaka 2016 hadi vifo 104 mwaka 2022 kwa kila vizazi hai 100,000.

"Katika huduma za uchunguzi na matibabu ya kibingwa, Serikali imenunua na kusimika vifaa tiba vyenye thamani ya Shilingi bilioni 241.6 ambapo mashine za MRI zimeongezeka kutoka 7 hadi 13, CT Scan kutoka 12 hadi 45 pamoja na Digital X-ray kutoka 147 hadi 559," amesema Waziri Mchengerea

Kwa upande wa chanjo, amesema watoto waliopata chanjo ya Pentavalent dozi ya tatu wameongezeka kutoka watoto milioni 2,093,412 hadi milioni 3,186,979 huku kiwango cha chanjo kikiongezeka kutoka asilimia 93 hadi 96, juu ya lengo la kimataifa la asilimia 90.

"Upatikanaji wa dawa na bidhaa za afya umeimarika, Serikali imetoa Shilingi trilioni 1.4 kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba, viwanda vipya 11 vya dawa na vifaa tiba vimeanzishwa huku 'Tanzania Pharmaceutical Industries kikifufuliwa kwa ajili ya uzalishaji wa dawa za VVU nchini," amesema Waziri Mchengerwa

SERIKALI YATOA BILIONI 48.8 BIMA YA AFYA KWA WOTE

May 11, 2026 Add Comment




Na Mwandishi Wetu , Dodoma


Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kaya zisizo na uwezo kwa kutoa Shilingi bilioni 48.8 kwa ajili ya kuwawezesha wananchi wa makundi maalum kupata huduma za afya kwa uhakika. Kupitia utekelezaji huo, jumla ya kaya 172,297 tayari zimefikiwa na kuingizwa kwenye mpango huo, huku wanufaika 463,228 wakianza kupata huduma mbalimbali za matibabu katika vituo vilivyosajiliwa nchini.

Akiwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya Fungu 52 kwa mwaka 2026/27 Waziri wa Afya Mhe. Omary Mchengerwa amesema kuwa, utekelezaji huu unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kujali hali yake ya kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya safari ya kuelekea huduma jumuishi za afya kwa wananchi wote.

Katika kuimarisha sekta ya afya sambamba na utekelezaji wa mpango huo, mabaraza na bodi za kitaaluma yameendelea kusimamia ubora wa huduma kwa kusajili wataalam wa afya 14,310, hatua inayoongeza nguvu kazi muhimu kwa utoaji wa huduma nchini.

Amesema kuwa kuhusu upatikanaji wa huduma za matibabu, jumla ya maduka ya dawa 330 yamesajiliwa pamoja na watarajali 3,004, huku vituo vya kutolea huduma za afya 3,643 vikisajiliwa ili kuongeza upatikanaji wa huduma karibu na wananchi.

Katika kuhakikisha taaluma na maadili yanaendelea kuzingatiwa hususan wakati huu wa kuhudumia wananchi wengi zaidi kupitia mfumo wa Bima ya Afya, vituo binafsi vya afya 654 vimekaguliwa ili kuhakikisha vinakidhi viwango na kutoa huduma salama kwa wananchi.

Mafanikio hayo yanaakisi hatua kubwa ya Serikali katika kujenga mfumo imara wa afya unaojali usawa, ubora na upatikanaji wa huduma kwa wote, huku Bima ya Afya kwa Wote ikiendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

BARRICK YAWEZESHA WANAFUNZI VYUO VIKUU MBEYA KUTAMBUA FURSA KUPITIA KONGAMANO LA AIESEC 2026

May 11, 2026 Add Comment

 

Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mbeya University of Science and Technology ( MUST) Prof. Said Wai akifungua kongamano la AIESEC 2026 lililofanyika katika chuo hicho.
Afisa Mwandamizi wa AIESEC Tanzania, Joshua Samwel akiongea na wanafunzi katika kongamano hilo.

BODI YA REA YAFANYA ZIARA KWENYE KAMPUNI ZA NISHATI SAFI YA KUPIKIA ARUSHA

May 11, 2026 Add Comment


-Mradi wa Nishati Safi ya Kupikia waongeza ajira kwa vijana

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) leo Mei 10, 2026 imefanya ziara katika Kampuni zinazozalisha, kusambaza bidhaa za nishati safi ya kupikia katika Mkoa wa Arusha.

Bodi hiyo ikiwa imeongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu pamoja na Wajumbe wa Bodi hiyo, Mhe. Radhia Msuya na Mhandisi Sophia Mgonja waliweza kutembelea kampuni ya Ignate Energy Access yenye bidhaa za My Sol pamoja na kampuni ya HannyG Investment.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti Kingu, amezipongeza kampuni hizo kwa kuunga mkono kampeni ya Serikali ya Nishati Safi ya Kupikia kwa kuanza kutengeneza pamoja na kusambaza bidhaa za nishati safi ya kupikia huku akitoa wito kwa makampuni mengine kuendelea kuunga mkono kampeni hiyo ili malengo yaliyowekwa ya ifikapo 2034, Asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Awali akitoa taarifa ya utendaji wa kampuni ya My Sol, Meneja Uendeshaji wa Mitambo, Joe Chambua, amesema kuwa pamoja na huduma zingine zinatolewa na kampuni hiyo ikiwamo huduma ya ufungaji wa umeme jua, kampuni hiyo imeanza kutekeleza mradi wa nishati safi ya kupikia kwa kuja na teknolojia rahisi na ya gharama nafuu ya mtambo wa biogasi.

Amesema kuwa wamefanikiwa kufunga mitambo ya biogasi katika taasisi mbalimbali nchini ikiwemo Magereza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa kampuni ya Hanny G Investment, Hanny Mbaria, ambao wanajishughulisha na utengenezaji wa majiko banifu pamoja na mkaa mbadala ameishukuru Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuipa kampuni hiyo kazi ya kusambaza majiko banifu na mkaa mbadala katika shule 53 Tanzania Bara.

Mbaria amesema licha ya mradi wa nishati safi ya kupikia kulinda mazingira lakini pia mradi huo umetoa ajira kwa vijana wengi.

“Kwa sasa kampuni yetu imekua zaidi na tumeajiri vijana wengi zaidi tofauti na hapo awali. Kwa sasa tuna wafanyakazi zaidi ya 120 wenye ajira za kudumu na wasio na ajira za moja kwa moja ni 1000,” amesema Mbaria.








DKT. MWIGULU KUMUWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA MKUTANO WA USHIRIKIANO AFRIKA NA UFARANSA, NCHINI KENYA

May 11, 2026 Add Comment

 WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Mei 10, 2026 ameondoka nchini kuelekea Nairobi, Kenya ambako anatarajia kumuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa Ushirikiano wa Afrika na Ufaransa (Africa Forward: Africa–France Partnership for Innovation and Growth Summit) utakaofanyika Mei 11–12, 2026.

Lengo la mkutano huo ni kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Afrika na Ufaransa katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, teknolojia, nishati, afya, Akili Unde (AI), kilimo, uchumi wa buluu pamoja na viwanda.

Aidha, mkutano huo unalenga kukuza uwekezaji mpya kati ya Afrika na kampuni za Ufaransa, kujenga ushirikiano unaotajwa kuwa wa usawa, pamoja na kujadili mageuzi ya mfumo wa fedha na maendeleo endelevu ya Afrika.

Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi na Serikali unawakutanisha wadau wa maendeleo, wawekezaji pamoja na sekta binafsi, na umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa William Samoei Ruto, na Rais wa Jamhuri ya Ufaransa, Mheshimiwa Emmanuel Macron.



BARABARA YA TOGO IKAMILIKE JUNI, MKATABA UJENZI WA BARABARA YA KIMARIO (BRAZIL) USAINIWE MEI 25 - PROF. SHEMDOE

May 11, 2026 Add Comment



Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameilekeza TARURA na Manispaa ya Kinondoni kuhakikisha ujenzi wa barabara ya Togo unakamilika mwezi Juni, 2026 na mkataba wa ujenzi wa barabara ya Kimario (Brazil) unasainiwa Mei 25, 2026, ili kuwaondolea adha wananchi wa Kinondoni na watumiaji wengine wa barabara hizo zinazojengwa kwa kiwango cha lami kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II).

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo leo Mei 10, 2026 Kinondoni Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na ofisi yake kupitia Wakala ya Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), aliyoifanya kutokana na ombi la wananchi wa Kinondoni kupitia kwa Mbunge wao Mhe. Abbas Tarimba.

“Tunaondoka hapa tukikubaliana kwamba barabara ya Togo itakamilika Juni 2026 na mkataba wa ujenzi wa barabara ya Kimario (Brazil) utasainiwa Mei 25, 2026 hivyo waheshimiwa Madiwani mfuatilie utekelezaji wa maelekezo haya,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Aidha, Prof. Shemdoe amemtaka Meneja wa TARURA Mkoa wa Dar es Salaam Mhandisi Geofrey Mkinga na Meneja wa TARURA Wilaya ya Kinondoni Mhandisi Edwin Kabwote kuhakikisha wanasimamia barabara hizo zikamilike kwa wakati ili kuwaondolea adha wananchi wa Kinondoni na watumiaji wote wa barabara hizo hususani kipindi hiki cha mvua.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha ujenzi wa barabara 17 za DMDP II katika wilaya ya Kinondoni zilizogharimu Shilingi Bilioni 97.7 ambazo zina jumla ya urefu wa wa kilometa 36.483.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Mhe. Abbas Tarimba amemshukuru Waziri wa TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe kwa kufanya ziara ya kukagua miradi hiyo ya maendeleo na kutoa maelekezo mahususi ya kuikamilisha, na kuongeza kuwa wananchi wamejionea wenyewe usikivu wa Waziri huyo wa Serikali ya Awamu ya Sita ambaye ametembelea miradi ya maendeleo jimboni kwake ikiwa ni siku ya jumapili ambayo anapaswa kupumzika.




TUME YATEUA WAGOMBEA 17 UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA ISMANI

May 11, 2026 Add Comment



Na. Mwandishi Wetu, Ismani

Wagombea 17 wameteuliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kugombea ubunge Jimbo la Ismani lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Mkoani Iringa.

Uteuzi huo umefanywa kwa niaba ya Tume na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Ismani, Ndugu. Caroline Angwen Otieno leo tarehe 10 Mei, 2026.

Wagombea walioteuliwa na vyama vyao kwenye mabano ni Ndugu. Emmanuela Kaganda Mtatifikolo (CCM), Ndugu. Farida Issa Mwapungu (MAKINI), Ndugu. Asha Athumani Chuma (UPDP), Ndugu. Protas Shaibu Mgimbila (CCK), Ndugu. Fidelis Daud Mtikile (SAU), Ndugu. Hadija Husen Makawa (ADA-TADEA) Ndugu. Zavely Raurent Seleleka (UDP) na Ndugu. Subira Majuto Kalolo (NLD).

Wengine ni Ndugu. Bernard George Mwingira (DP), Ndugu. Burton Emilyo Chetenge (NCCR-Mageuzi), Ndugu. Mbalinga Christian Thomas (N.R.A), Ndugu. Mark Isdory Mhemela (AAFP), Ndugu. Nassim Yahaya Upete (CUF), Ndugu. Mwaka Lameck Mgimwa (TLP), Ndugu. Asma Abdallah Othman (UMD), Ndugu. Maimuna Martin Lumato (ADC) na Ndugu. Daudi Issa Masasi (CHAUMMA).

Akizungumza baada ya uteuzi huo, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo, Ndugu. Caroline Angwen Otieno amesema kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Tume,

Kampeni kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Ismani pamoja na kata 12 za Tanzania Bara zitaanza kesho tarehe 11 hadi 31 Mei, 2026 na uchaguzi utafanyika siku ya Jumatatu tarehe 01 Juni, 2026.

Baada ya hatua hii ya uteuzi, kinachofuata ni kubandika fomu za uteuzi eneo la wazi kwa ajili ya kuwapa fursa ya kuweka pingamizi wale wanaoruhusiwa kuweka pingamizi kwa mujibu wa sheria.

Baada ya saa 24 kupita na endapo hakutakuwa na pingamizi wagombea hao 17 wataendelea na kampeni kuanzia kesho tarehe 11 hadi 31 Mei, 2026 na uchaguzi utafanyika tarehe 01 Juni, 2026, amesema.

Kata 12 za Tanzania Bara zitakazofanya uchaguzi mdogo wa Udiwani ni Mzimuni iliyopo Manispaa ya Kinondoni; Zongomera, Manispaa ya Kahama; Itilo, Halmashauri ya Mji wa Nzega; Ketare, Halmashauri ya Mji wa Tarime na Nyumbigwa, Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Nyingine ni kata ya Kala iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi; Ziba, Halmashauri ya Wilaya Igunga; Kamsisi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele; Nyamugali, Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe; Namasakata Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru; Bwongera, Halmashauri ya Wilaya ya Chato na Kibiti Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.


















NEMC YAKIJANISHA TANZANIA, YAPANDA MICHE YA MITI ELFU AROBAINI NCHI NZIMA

May 10, 2026 Add Comment
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Halmashauri za Miji, Halmashauri za Wilaya, Shule za msingi, wadau wa mazingira pamoja na Mabalozi wa Mazingira, limepanda miche ya miti elfu arobaini katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho ya miaka 40 tangu kuanzishwa kwa Baraza hilo.

WAZIRI NDEJEMBI ATOA MAELEKEZO MAZITO UTEKELEZAJI MRADI MALAGARASI MW 49.5 KIGOMA

May 10, 2026 Add Comment




📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi


📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya dola milioni 20 za malipo ya awali yaliyotolewa kwa mkandarasi kulinganisha na kazi zilizofanyika




📌Aelekeza kuondolewa mara moja kwa meneja wa mradi upande wa mkandarasi


Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema hajaridhishwa na mwenendo wa utekelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Megawati 49.5 katika maporomoko ya Mto Malagarasi mkoani Kigoma unaotekelezwa na Kampuni ya Dongfang Electric kutokana na kuchelewa kwa kazi pamoja na kutotekeleza masharti ya mkataba waliouingia na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo Mei 10, 2026 wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo ambapo alibaini mkandarasi huyo amekuwa akitoa visingizio badala ya kutekeleza majukumu yake kwa wakati kama mkataba unavyoelekeza.

Akizungumza katika ziara hiyo, amesema Serikali tayari imemlipa mkandarasi zaidi ya dola milioni 20 kama malipo ya awali lakini kiwango cha kazi zilizotekelezwa hakionekani kuendana na fedha zilizotolewa.

Baadhi ya kazi zilizochelewa ni pamoja na ujenzi wa makazi ya wafanyakazi na barabara za mradi, hali ambayo imeonesha kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati.

Aidha, ameielekeza TANESCO pamoja na mshauri mwelekezi kuendelea kumsimamia kwa karibu mkandarasi huyo huku akisisitiza kuwa Serikali haitatoa nyongeza ya fedha wala kuruhusu mabadiliko ya gharama za mradi huo kwani mkandarasi aliwasilisha gharama zake mwenyewe wakati wa zabuni.

Amesema baadhi ya wakandarasi wamekuwa na tabia ya kuomba kazi kwa gharama ndogo ili kupata zabuni na baadaye kuanza kuomba nyongeza ya fedha, jambo ambalo Serikali haitalivumilia.

Katika hatua nyingine, Mhe. Ndejembi ameagiza meneja wa mradi upande wa mkandarasi kuondolewa mara moja kutokana na kile alichokieleza kuwa ni visingizio vinavyochangia kuchelewesha utekelezaji wa kazi. 

Vilevile ameagiza kufanyika kwa ukaguzi maalum wa matumizi ya fedha za malipo ya awali ili kubaini namna fedha hizo zimetumika ukilinganisha na kazi zilizofanyika.


“Mradi huu una umuhimu mkubwa kwa wananchi wa Kigoma, Katavi, Kagera na maeneo ya jirani kwani utaongeza nguvu katika Gridi ya Taifa na kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini. Serikali haitakuwa tayari kuvumilia ucheleweshaji unaosababishwa na uzembe wa wakandarasi,” amesema Mhe. Ndejembi.

Ameielekeza TANESCO ndani ya muda wa wiki mbili kukamilisha ukaguzi huo na kuwasilisha taarifa ofisini kwake.

Aidha, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO kwa juhudi za kufanya vikao vya mara kwa mara na mkandarasi huyo pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za kutatua changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa mradi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TANESCO Bw, Lazaro Twange amesema TANESCO imepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri na itahakikisha yanatekelezwa kwa wakati ili mradi huo ukamilike kama ilivyopangwa.


Mradi wa Malagarasi MW 49.5 unatekelezwa na Kampuni ya Dangfang Electric International Corporation (DEC) kutoka China, ambapo ulianza Aprili 30, 2024 na unatarajiwa kukamilika Oktoba 30, 2027 kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 300.


Kukamilika kwake kutaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme 

Katika mikoa ya Kigoma, Katavi, Kagera na maeneo ya jirani kwani utaongeza nguvu katika Gridi ya Taifa.

KAFULILA: UJUMBE MAALUM SIKU YA MAMA DUNIANI.

May 10, 2026 Add Comment

Kupitia Ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa X (Zamani Twitter) Mwanasiasa na msomi wa masuala ya maendeleo, Mkurugenzi wa kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na binafsi (PPPC), David Kafuila ametoa ujumbe maalum wa maadhimisho ya Siku ya Mama Duniani akisisitiza umuhimu wa malezi bora kwa watoto katika siku 1000 kuamzia kutungwa kwa mimba mpk umri wa 2 zina nafasi kubwa kubwa kuamua ubora wa watoto kiafya na zaidi kiakili.