HABARI MPYA
HABARI
SIASA
ELIMU
Recent Posts
MAAFISA ELIMU MIKOA 26 WAPATIWA MAFUNZO ARUSHA
habariTANZANIA YASHIKA NAFASI YA NNE KWA UWEKEZAJI SEKTA YA MADINI AFRIKA
habari
.jpeg)
RC TANGA KAMATI ZA USHAURI NGAZI ZA KISHERIA ZITASAIDIA KUPUNGUZA MASHAURI DHIDI YA SERIKALI NA VITENDO VYA UONEVU
habariNa Oscar Assenga,TANGA
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amezindua Kamati za Ushauri wa Kisheria ngazi ya mkoa na wilaya na kliniki ya Sheria bila malipo huku akieleza kwamba zitasaidia kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali kutokana na kukutanisha mawakili wa Serikali.
Aliyasema hayo leo kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga ambako kilifanyika uzinduzi wa Kamati hizo ambapo alisema pia wale wa taasisi mbalimbali na kuwasaidia wananchi wenye changamoto mbalimbali kupata ufumbuzi.
Alisema uwepo wa huduma hizo utawawezesha mawakili wa Serikali kusimamia utawala wa Sheria katika kushirikiana na wadau wengine katika kutatua kero za wananchi na kupunguza malalamikko ya kisheria kutoka kwa wananchi.
“Lakini pia kutoa elimu ya Sheria kwa umma katika kushughulikia changamoto mbalimbali katika maeneo yao pamoja na kutoa elimu kwa viongozi na maafisa wa Serikali waweze kutoa maamuzi kwa mujibu wa Sheria”Alisema
Aidha alisema pia itapunguza vitendo vya uonevu na vinavyovunja sheria na taratibu za nchi nah ii itawezesha mimi na wakuu wa wilaya kushughulikia masuala ya miradi ya maendeleo badala ya kuhangaika na migogoro ya wananchi .
“Lakini nanukuu katika kitabu cha Mathayo 5:9 Yesu anasema “Heri wapatanishi ,maana hao wataitwa wana wa Mungu”.Hii inaonyesha kuwa kazi ya kupatanisha ni ya Kiungu na inampendeza Mungu”
“Pia kwenye Qur’an inasititiza sana kutenda haki (Uadilifu)kama wajibu Mkuu wa kidini na kijami,ikiamrisha kusimamia haki hata kama ni dhidi ya nafsi zenu waziazi ,au jamaa (Quran 4:1:35,5.8).Uadilifu ni msingi wa imani,ukihimiza kulinda haki za wengine ,kuondoa chuki na kutoa fidia kwa wahasiriwa”Alisema
Aidha aliwataka wadau waelewe kuwa jukumu la kutatua migogoro katika maisha ya watanzania sio la Serikali pekee bali ni la wote wa maendeleo huku akieleza kazi kubwa Serikali iliyonayo ni pamoja na kutengeneza mazingira mamzuri yanayoweza kusaidia kamati hizo.
Alisema hilo linatokana na uwepo wa migogoro mingi katika jamii hasa migogoro ya ardhi na mirathi hivyo kamati hizo zinatakiwa kukaa kila mara kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake ya kusikiliza malalamiko ya ksiheria na kutoa elimu kwa umma kwa kushirikiana na ofisi za wakuu wa wilaya.
Hata hivyo alitoa rai kwamba kuna haja ya kuhakikisha kuwa kamati za mkoa na wilaya zinafanya mambo mbalimbali ili kukabiliana na migogoro ikiwemo kuendelea kuboresha kiwango cha utoaji wa huduma ya ushauri wa kisheria na kuongeza wigo na upatikanaji katika maeneo ambayo hayajafanikiwa kufikiwa hasa maeneo ya nje ya jiji.
Mkuu huyo wa mkoa alizitaka kujiwekea utaratibu wa kuandaa kliniki za kisheria bila malipo kwa utaratibu wa kuwafuata wananchi katika maeneo yaona hiyo inatokana na wapo wananchi wengine ambao wanaogopa kuingia kwenye ofisi za Serikali pamoja na wengine hawana uwezo wa kusafiri na kwenda kwenye ofisi hizo.
“Lakini hakikisheni mnapopokea malalamiko au migogoro mnaifuatilia mpaka mwisho ili kujiridhisha namna gani imemalizika na kuweka kumbukumbu ya kufungua na kufunga migogoro hii lengo likiwa kuzuia walalamikaji kurudi kuwasilisha malalamiko yaliyopita hasa pale anapoona uongozi umebadilika “Alisema
Hata hivyo nitoa wito kwa wananchi wote wa mkoa wa Tanga wenye migogoro kutumia nafasi hii kuwasilisha migogoro yenu katika kliniki ya Sheria bila malipo iliyoanza leo kwenye viwanja vya Tangamano mpaka Machi 15 mwaka huu .
Awali akzungumza akizungumza Mkurugenzi wa Uratibu na Huduma za Ushauri kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Neema Ringo alisema kwamba wamekuja mkoani Tanga kutoa huduma kwa wananchi za kisheria kwa maana yake kutekeleza wajibu wake katika kuwahudumia wananchi ambao ndio wanaipa mamlaka Serikali.
Alisema wakiwa mkoani Tanga watapata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuweza kuzipatia ufumbuzi huku akiwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo kwa kujitokeza kwa wingi kuweza kupata huduma
ASILIMIA 89 YA VITONGOJI NKASI VIMEFIKIWA NA UMEME- MHE.SALOME
WAZIRI MHE. NDEJEMBI ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA MRADI WA KITUO CHA KUPOKEA NA KUPOZA UMEME IGANJO – MBEYA

Na Mwandishi Wetu, Mbeya.
Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Kituo cha Kupokea na Kupoza Umeme wa Kilovoti 400 cha Iganjo mkoani Mbeya, ambao kwa sasa umefikia takribani asilimia 60 ya utekelezaji wake.
Mhe. Ndejembi ametoa kauli hiyo Machi 8, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika eneo la Iganjo jijini Mbeya ambao ni sehemu ya Mradi wa Njia kusafirisha Umeme kutoka mkoa wa Irunga hadi Mkoa wa Rukwa (TAZA).
“Kwa ujumla wake kazi hapa zinaenda vizuri sana. Niwapongeza Shirika la Umeme TANESCO kwa kazi ya usimamizi mzuri wa mradi huu,” amesema Mhe. Ndejembi
Akieleza faida za mradi huo amesema kuwa utaachangia kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Mbeya pamoja na mikoa jirani.
“Mradi huu utaongeza nguvu ya upatikanaji wa umeme kwa sababu kwa sasa Mkoa wa Mbeya unapata umeme kutoka kwenye njia ya kilovoti 220 lakini mradi huu utakua ni kilovoti 400. Wananchi watanufaika na mradi huu kwa sababu umeme utapoozwa na kusambazwa kwa Wananchi,” ameongeza Mhe. Ndejembi
Aidha, ameeleza kuwa serikali inayoongozwa na Rais wa awamu ya sita Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwekeza katika miradi mikubwa ya kimkakati ya nishati ili kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa Tanzania - Zambia (TAZA) Mha. Elias Makunga amesema mradi wa kituo cha Iganjo unaendelea vizuri licha ya changamoto ndogo zilizojitokeza katika hatua za usambazaji wa vifaa.
“Mradi wa kituo cha Iganjo uko asilimia 60 ya utekelezaji, ujenzi wa misingi umekamilika kwa asilimia 89. Upande wa usambazaji wa vifaa kutoka China tuko asilimia 89, lakini tumekuwa na changamoto kidogo katika upande wa upokeaji wa vifaa unaohusiana na kuboresha mfumo wa TRA,” amesema Mha. Makunga
Mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Rukwa ukikamilika unatarajiwa kuwa miongoni mwa miradi muhimu katika kuimarisha Gridi ya Taifa na kuongeza upatikanaji wa umeme wa uhakika katika ukanda wa Nyanda za Juu Kusini.





BALOZI WA IRELAND NA NM-AIST WAJADILI UTEKELEZAJI WA SAMIA SCHOLARSHIP DS/AI+
habari
Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Nicola Brennan na uongozi wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) wamejadiliana namna ya kuimarisha utekelezaji wa mpango wa Samia Scholarship Extended DS/AI+ unaolenga kujenga wataalamu wa Akili Bandia (AI) na Sayansi ya Takwimu (Data Science) nchini.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo iliyofanyika tarehe 9 Machi 2026 katika Taasisi hiyo jijini Arusha, Makamu Mkuu wa NM-AIST, Prof. Maulilio Kipanyula, amesema katika awamu ya kwanza ya mpango huo wanafunzi 34 wa Kitanzania wamepata nafasi ya kusoma katika vyuo vikuu vya Ireland.
Ameongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) pamoja na NM-AIST inapanga kuandaa *bootcamp* maalum kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi watakaofuata kunufaika na mpango huo.
Kwa upande wake, Balozi Brennan ameipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira ya kuwekeza katika elimu ya juu katika fani za AI, Data Science na Sayansi shirikishi, akibainisha kuwa wanafunzi wa Kitanzania watapata elimu yenye viwango vya kimataifa katika vyuo vikuu vya Ireland.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuongeza ushiriki wa wanawake katika masomo ya STEM na kuhimiza taasisi na wabunifu kuhakikisha matokeo ya tafiti yanafika sokoni ili kuchangia maendeleo ya uchumi, usalama wa chakula na ajira.
Katika ziara hiyo, Balozi Brennan pia alitembelea maabara, kituo cha kompyuta chenye uwezo mkubwa (HPC), Data Driven Institute (DDI) pamoja na vituo vya ubunifu vya NM-AIST ili kujionea mchango wa taasisi hiyo katika maendeleo ya sayansi na teknolojia nchini.

PROF. MKUMBO: SEKTA BINAFSI NI MUHIMU KUFANIKISHA MPANGO WA NNE WA MAENDELEO
habariNA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM
Serikali inatarajia zaidi ya asilimia 70 ya fedha za utekelezaji wa Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano zitatoka katika sekta binafsi kupitia uwekezaji na mifumo ya ubia kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP).

SENYAMULE AHIMIZA MAKUNDI YA WANAWAKE KUSHIRIKI ZABUNI ZA UMMA.
habari
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bi. Rosemary Senyamule, ameipongeza Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma kwa kusimamia vizuri upatikanaji wa fursa za Ununuzi wa Umma kwa makundi maalum, hususan wanawake, hatua ambayo imeendelea kuwasaidia kiuchumi na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo.
Akizungumza leo Machi 8, 2026 katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Mbande, Wilayani Kongwa Mkoa wa Dodoma, Bi. Senyamule amesema kuwa usimamizi mzuri wa PPRA umewezesha makundi ya wanawake kunufaika na zabuni mbalimbali za serikali kupitia mfumo wa kielektroniki wa Usimamizi wa Ununuzi -NeST.
Amesema kuwa hadi sasa vikundi vya wanawake vimefanikiwa kupata zabuni za serikali zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 16, hatua inayodhihirisha kuwa sera ya kutoa kipaumbele kwa makundi maalum inaleta matokeo chanya katika kuwawezesha wanawake kiuchumi.
Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa zaidi ya vikundi 500 vya wanawake vimesajiliwa kwenye mfumo wa NeST, jambo linaloonesha mwitikio wa wanawake katika kutumia fursa za ununuzi wa umma zinazotolewa na Serikali.
Aidha, Bi. Senyamule amewataka wanawake wote nchini kuendelea kuunda vikundi vingi zaidi ili waweze kunufaika na fursa hizo za zabuni za serikali, akisisitiza kuwa serikali imeweka mazingira rafiki yanayowawezesha kushiriki kikamilifu katika uchumi wa nchi.
“Ni muhimu wanawake mkajiunga katika vikundi na kujisajili katika mfumo wa NeST ili mpate nafasi ya kushiriki katika zabuni za serikali.
Fursa hizi zipo kwa ajili yenu na zinaweza kuwasaidia kukuza biashara na kuinua kipato chenu,” amesema.
Ameongeza kuwa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyopatikana katika kuwawezesha wanawake na kuhamasisha juhudi zaidi za kuhakikisha wanawake wanapata nafasi sawa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Msimizi wa Kituo cha Msaada wa Kitaalam kwa Wateja wa NeST - PPRA ( NeST Customer Technical Support Center) Bi. Asifiwe Makweta amesema Mamlaka ina shauku kuona vikundi vya kina Mama vonaongezeka siku hadi siku ili kuhakikisha fursa hizi za serikali zinawafikia walengwa kiyakinifu kwa makundi yote ikiwemo Wanawake ili kuleta uhai wa ushiriki wa makundi maalum bila kubaki nyuma kwa kundi lolote.
"Pamoja na kufikia idadi ya kusajili makundi 500 ya Wanawake kwenye mfumo wa NeST bado haijafikia idadi ya makundi tunayotamani kusajili kwenye Mfumo wa NeST ili kushiriki katika fursa hii ya asilimia 30 ya zabuni kwa makundi hayo ambayo ni Vijana, wanawake, Wazee na watu wenye ulemavu"amesema Bi. Makweta.





.jpeg)




