HABARI

SIASA

ELIMU

Recent Posts

RC MTAMBI ATOA ONYO KWA WANANCHI WATAKAO HUJUMU MIUNDO YA UMEME VITONGOJINI

RC MTAMBI ATOA ONYO KWA WANANCHI WATAKAO HUJUMU MIUNDO YA UMEME VITONGOJINI

February 12, 2026 Add Comment

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi amezitaka Kamati za Ulinzi na Usalama pamoja na Wananchi kuhakikisha wanalinda miundombinu ya umeme pamoja na vifaa vitakavyatumikakutekeleza mradi wa Kupelekea Umeme katika Vitongoji 371 mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa maelekezo hayo leo Februari 12, 2026 Ofisini kwake wakati wa kikao na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kilicholenga kumtambulisha rasmi Mkandarasi wa Mradi huo, NAMIS Corporate L.t.d atakaye hudumia Vitongoji 371 vya Mkoani humo.

“Miradi hii inatekelezwa kwa fedha nyingi kwa lengo la kuboresha maisha ya wananchi na asitokee mtu yoyote akafanya ubadilifu wa kuharibu miundombinu ya umeme pamoja na wizi wa vifaa vya utekelezaji wa mradi huu na kukwamisha kutekelezwa kwa mradi huu.

Nitoe onyo kwa mtu yoyote aliyepanga kufanya uharibifu asijaribu katika Mkoa wa Mara hakika tutawakamata, na tukiwakamata tutawachukulia hatua kali za kisheria,” amesisitiza Kanali Mtambi.

Sambamba na hilo amemtaka Mkandarasi anayetekeleza mradi kuhakikisha anautekeleza mradi huo ndani ya muda wa miaka mitatu kama ulivyopangwa kwenye mkataba, na pia alimsisitiza kuzingatia ubora

Kwa upande wake, Mhandis Ernest Makale Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) amesema kwa Mkoa wa Mara Jumla ya Shilingi Bilioni 38.2 itatumika kusambaza umeme katika Vitongoji 371 huku akiwasisitiza kutumia umeme kujikwamua kiuchumi.

“Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ikiwa na lengo la kuendelea kuboresha maisha ya wananchi vijijini. Lengo kuu likiwa Vitongoje vyote ifikapo 2030 viwe na huduma ya umeme

Tuendelee kutoa rai kwa wananchi kuanza kufanya maandalizi ya kupokea mradi huu kwa kuanza kufanya wiring kwenye nyumba zao pamoja na kutumia uwepo wa umeme kujikwamua kiuchumi kwa kufungua miradi mbalimbali vijijini,” amesema Mhandisi Makale.

RAIS DKT SAMIA SULUHU AWASILI ADDIS ABABA ETHIOPIA KWA AJILI YA KUSHIRIKI MKUTANO WA 39 WA KAWAIDA WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA (AU)

February 12, 2026 Add Comment

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Bole, Jijini Addis Ababa Ethiopia, tarehe 12 Februari, 2026 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 39 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Bole, Jijini Addis Ababa Ethiopia, tarehe 12 Februari, 2026 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 39 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokelewa na Waziri wa Kazi na Ukuzaji wa Ujuzi wa Ethiopia Mheshimiwa Muferihat Kamil Ahmed mara baada ya kuwasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Bole, Jijini Addis Ababa Ethiopia, tarehe 12 Februari, 2026 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 39 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU).

AKWILAPO ATEMBELEA ENEO UNAPOJENGWA UWANJA WA AFCON ARUSHA

February 12, 2026 Add Comment


§ Atoa siku kumi na tano wasiokamilisha malipo ya viwanja vinavyozunguka uwanja kukamilisha

 Asisitiza waliomilikishwa viwanja kufanya maendelezo

Na Munir Shemweta, WANMM ARUSHA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Akwilapo tarehe 11 Februari 2026 ametembeleo eneo unapojengwa uwanja wa kisasa wa mpira kwa ajili Mashindano ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2027) mkoani Arusha.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetekeleza Mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi katika eneo lililopo pembezoni unapojengwa Uwanja wa mpira wa Afcon katika kata ya Olmoti Jiji la Arusha, mkoani Arusha.

Hata hivyo, pamoja na viwanja kuuzwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali lakini kuna baadhi ya waliochukua viwanja kushindwa kukamilisha malipo ndani ya muda huku baadhi waliomilikishwa wakishindwa kuendeleza maeneo yao.

Akiwa katika eneo la uwanja huo, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo alijionea maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo ambapo alipongeza jitihada zinazofanyika za kuhakikisha uwanja huo unakamilika kwa wakati na hatimaye kutumika katika mashindano hayo makubwa ya Afrika.

Akigeukia wananchi waliochukua viwanja na kushindwa kukamilisha malipo kwa wakati, Mhe Akwilapo amewataka kuhakikisha wanafanya malipo ndani ya siku kumi na tano kuanzia tarehe 12 Februari 2026.

"Kuna wananchi walioomba viwanja katika maeneo yanayozunguka uwanja wa AFCON 2027 na kushindwa kukamilisha malipo ya viwanja hivyo, wanatakiwa kulipa ndani ya siku kumi na tano na baada ya hapo tutawanyang'anya na kuwapatia wengine". Amesema Akwilapo

Aidha, amesisitiza wananchi wenye hati milki za ardhi katika eneo linalozunguka uwanja huo kuhakikisha wanafanya maendelezo kwenye maeneo yao huku akiweka bayana kuwa, kama kuna mtu anayedhani hawawezi kufanya maendelezo katika muda wa kuelekea Mashindano ya AFCON 2027 basi airejeshe hati ili kupatiwa wale wanaoweza kufanya maendelezo.

Ujenzi wa mradi wa uwanja wa AFCON Arusha kwa sasa umefikia asilimia 74 na unatarajiwa kukamilika Julai, 2026.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa mpira unaotarajiwa kutumika katika mashindano ya mataifa ya afrika (AFCON 2027) jijini Arusha jana

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo (Kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera wakipata maelezo ya mradi wa viwanja vinavyozunguka uwanja wa AFCON Arusha jana alipofanya ziara katika eneo hilo.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo (wa tatu kulia) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Lucy Kabyemera (kushoto) wakielekea katika uwanja wa AFCON wakati wa ziara ya siku moja katika maeneo ya uwanja huo jana. (PICHA NA WIZARA YA ARDHI)
FCC YAKUTANA NA WAZALISHAJI WA SARUJI KUJADILI HALI YA SOKO NA BEI

FCC YAKUTANA NA WAZALISHAJI WA SARUJI KUJADILI HALI YA SOKO NA BEI

February 12, 2026 Add Comment
Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC Bi. Khadija Ngasongwa, akitoa maelezo kuhusu wajibu wa FCC kwenye kusimamia ushindani na kumlinda mlaji wakati wa kikao kazi na wazalishaji wa saruji nchini kilichofanyika katika ofisi za FCC Februari 11, 2026 Jijini Dar es Salaam.

.............

TUME  ya Ushindani (FCC) imekutana na wadau wa uzalishaji wa ndani wa saruji kwa lengo la kujadili hali ya uzalishaji wa bidhaa hiyo pamoja na namna ya kulinda soko na maslahi ya mlaji.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema kuwa tume hiyo ina utaratibu wa kukutana na wadau wake mara kwa mara ili kujadili masuala yanayohusu ushindani wa soko.
Amesema kikao cha leo kimewaleta pamoja wazalishaji wa saruji kwa ajili ya mahojiano na majadiliano yatakayosaidia kujenga soko lenye ushindani wa haki sambamba na kumlinda mlaji.
Bi. Ngasongwa amesema baada ya majadiliano hayo, FCC itapata mwanga wa kuchambua na kutoa mwelekeo au suluhisho kuhusu hali ya ushindani wa saruji sokoni na athari zake kwa walaji.
Aidha, amesema wazalishaji wa saruji waliwasilisha taarifa (notice) ya kupandisha bei ya bidhaa hiyo, jambo linalohitaji kufanyiwa tathmini ya kina kwa kuzingatia hali halisi ya soko, gharama za uendeshaji pamoja na gharama za malighafi.
“Katika majadiliano haya, tunatarajia kupata matokeo yatakayojenga afya ya soko la saruji na kuhakikisha mlaji analindwa katika upatikanaji wa bidhaa hii muhimu,” amesema Bi. Ngasongwa.
Kikao hicho kimefanyika Februari 11 katika ofisi za FCC, Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC Bi. Khadija Ngasongwa, akitoa maelezo kuhusu wajibu wa FCC kwenye kusimamia ushindani na kumlinda mlaji wakati wa kikao kazi na wazalishaji wa saruji nchini kilichofanyika katika ofisi za FCC Februari 11, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu FCC Bi. Khadija Ngasongwa, akitoa maelezo kuhusu wajibu wa FCC kwenye kusimamia ushindani na kumlinda mlaji wakati wa kikao kazi na wazalishaji wa saruji nchini kilichofanyika katika ofisi za FCC Februari 11, 2026 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wazalishaji wa saruji wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bi. Khadija Ngasongwa akizungumza wakati wa kikao kazi cha wazalishaji wa saruji Februari 11, 2026 jijini Dar es Salaam.

MASHINE ZA UKAGUZI WA MIZIGO ZAKIDHI VIGEZO VYA TAEC KANDA YA ZIWA

February 12, 2026 Add Comment

Serikali kupitia Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imeendelea kuimarisha usimamizi wa matumizi salama ya mionzi nchini kwa kufanya ziara maalum katika Kanda ya Ziwa. Ziara hiyo, iliyohusisha Bodi na Menejimenti ya TAEC, ililenga kukagua na kujionea utendaji kazi wa ofisi zake zilizopo Uwanja wa Ndege wa Mwanza, Bandari ya Mwanza, Ofisi ya TAEC Nyegezi pamoja na Ofisi ya TAEC Sirari.

Katika hatua ya kwanza, wajumbe wa Bodi na Menejimenti walitembelea Uwanja wa Ndege wa Mwanza na kufanya mazungumzo na Meneja wa Uwanja wa Ndege Kanda ya Ziwa, Bi. Rose Comino. Alieleza namna TAEC inavyoshirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege katika ukaguzi wa mashine za kukagulia mizigo (Baggage Scanners) na kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya mashine hizo. Bi. Comino alibainisha kuwa mashine zote zinazotumika kwa ukaguzi wa mizigo zimekidhi matakwa ya kisheria kwa kupata vibali kutoka TAEC. Aidha, alieleza kuwa ujenzi mkubwa unaoendelea kiwanjani utakapokamilika, mashine za ziada za ukaguzi wa mizigo zitafungwa ili kuboresha zaidi huduma kwa abiria.

Mwenyekiti wa Bodi ya TAEC, Profesa Joseph Msambishaka, alisisitiza kuwa lengo la ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano na kuboresha utekelezaji wa majukumu ya pamoja. Mkurugenzi Mkuu wa TAEC, Profesa Najat Kassim Mohammed, alitoa shukrani kwa mapokezi mazuri na kusisitiza kuwa ushirikiano mzuri uliopo ni chachu ya mafanikio ya utekelezaji wa majukumu ya kisheria ya TAEC.

Afisa Ukaguzi wa Mionzi wa TAEC, Bw. Stephani Kapama, alieleza kuwa ofisi hiyo hukusanya wastani wa sampuli 30 kila mwezi kutoka shehena za mizigo na kuzifanyia vipimo ili kubaini uwepo wa mionzi. Pia hufanya ukaguzi wa mionzi kila siku katika maeneo yenye shughuli nyingi za binadamu: eneo la kuhifadhia mizigo, eneo la abiria wanaowasili na eneo la abiria wanaoondoka. Aliongeza kuwa muda wa kuchakata vibali vya mionzi umepungua kutoka siku saba hadi siku moja pekee, hatua iliyoongeza ufanisi wa usafirishaji wa bidhaa na huduma.

Bodi na Menejimenti waliendelea na ziara kwa kuonana na Meneja wa Bandari Kanda ya Ziwa, Bi. Rosemary Ndesamburo. Alieleza namna bandari inavyoshirikiana na TAEC hususani katika ukaguzi wa mashine za midaki zinazotumika kukagua mizigo. TAEC hukagua mashine hizo na kutoa vibali vya matumizi yake kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za matumizi salama ya mionzi. Mamlaka ya Bandari Kanda ya Ziwa inasimamia jumla ya bandari saba ambazo ni Mwanza South, Mwanza North, Nansio (Ukerewe), Kemondo Bay, Bukoba, Musoma na Kisorya.

Bandari hizi ni kiungo muhimu cha usafirishaji wa abiria na mizigo ndani ya Ziwa Victoria na zinashirikiana kwa karibu na TAEC kuhakikisha usalama wa matumizi ya teknolojia ya mionzi.

Bodi na Menejimenti walitembelea pia ofisi ya TAEC iliyopo Nyegezi na kujionea utekelezaji wa kazi mbalimbali zinazotolewa na ofisi ya kanda katika kuhudumia wananchi wa Kanda ya Ziwa. Msimamizi wa Ofisi ya Kanda, Dkt. Suleiman Ameir Suleiman, alieleza kuwa ofisi hiyo hufanya kazi za kila siku ikiwemo utoaji wa elimu kwa shule na jamii juu ya matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia, ukaguzi wa vituo vinavyomiliki vyanzo vya mionzi, upimaji wa mionzi kwenye bidhaa za vyakula vinavyoingia na kutoka ndani ya kanda, upimaji wa viasili vya mionzi kwenye mazingira pamoja na utafutaji wa vyanzo vya mionzi vilivyopotea.

Ziara ya Bodi na Menejimenti ya TAEC katika Kanda ya Ziwa ilihitimishwa kwa kutembelea mpaka wa Sirari, ambapo wajumbe walikutana na viongozi kutoka taasisi mbalimbali za serikali zinazoshirikiana katika kutoa huduma kwa ufanisi mpakani hapo. Afisa Mkuu wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Godfrey Leonard, aliyemuwakilisha Meneja Msaidizi wa TRA Sirari, alieleza namna taasisi zote zilizopo mpakani zinavyoshirikiana kwa karibu kuhakikisha huduma zinatolewa kwa haraka na kwa ufanisi.

Taasisi zinazoshirikiana Sirari ni pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Jeshi la Polisi Tanzania, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (TPDF), Ofisi ya Rais, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Wakala wa Vipimo, Wizara ya Madini, Jeshi la Wanyamapori, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi Kavu (SUMATRA), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), Idara ya Uhamiaji Tanzania na Tanzania Bureau of Standards (TBS).

Mwenyekiti wa Bodi ya TAEC, Profesa Joseph Msambishaka, alieleza kuwa ziara hiyo ililenga kufika mpaka wa Sirari ili wajumbe wapya wa Bodi waweze kufahamu kwa undani namna TAEC inavyotekeleza majukumu yake katika eneo hilo. Alisisitiza kuwa ni busara Bodi kujionea kwa macho yake jinsi kazi za ukaguzi wa mionzi zinavyofanyika mpakani, hususan katika shehena za mizigo, ili kubaini uwepo wa uchafuzi wa mionzi au kuzuia usafirishaji holela wa vyanzo vya mionzi.

Bodi ilipata maelezo kutoka kwa Mkaguzi wa Mionzi wa TAEC, Bw. Kasoga, ambaye alieleza namna ofisi ya TAEC mpakani hapo inavyotekeleza majukumu yake ya kila siku katika kuhakikisha taratibu zote zinafuatwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za matumizi salama ya mionzi. Aidha, wajumbe walitembelea maabara ya TAEC Sirari na kupata maelezo juu ya namna inavyotumika katika ukaguzi wa sampuli za bidhaa mbalimbali, na kujionea vifaa na teknolojia zinazotumika kupima viwango vya mionzi.

Ziara hii imekuwa chachu ya mafanikio kwa wajumbe wa Bodi ya TAEC kujionea kwa karibu utekelezaji wa majukumu ya Tume katika maeneo nyeti ya mipaka, viwanja vya ndege na bandari. Hatua hii imeimarisha ushirikiano wa taasisi za serikali katika kuhakikisha usalama wa wananchi dhidi ya mionzi na kuendeleza matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia nchini. Mafanikio haya ni kielelezo cha dira ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kusimamia kwa maono makubwa na uongozi thabiti juhudi za kulinda afya na usalama wa Watanzania. Kupitia msisitizo wake wa kuimarisha taasisi za kitaifa na kuhimiza matumizi ya sayansi na teknolojia kwa maendeleo endelevu, taifa linaendelea kujengeka katika misingi imara ya usalama, uchumi na ustawi wa wananchi.



VITENGO VYA UFUATILIAJI NA TATHIMINI WIZARA YA MAJI NA NISHATI KUUNGANISHA NGUVU KUSIMAMIA MIRADI

February 11, 2026 Add Comment


Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini vya Wizara ya Maji na Wizara ya Nishati vimekubaliana kushirikiana  katika mifumo ya ufuatiliaji na kusimamia kwa pamoja tathmini ya utekelezaji wa miradi ya nishati na maji ili kuhakikisha kuwa inafanyika kwa ufanisi na hivyo kuwezesha wananchi kupata huduma bora.


Makubaliano hayo yamefikiwa leo katika kikao  kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Maji, Mtumba, jijini Dodoma, kikihusisha wataalam wa ufuatiliaji na tathmini kutoka wizara zote mbili.

Katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Nishati, Bi. Anitha Ishengoma, pamoja na Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Maji, Bi. Diana Kimario, wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano huo ili kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia malengo yaliyokusudiwa.

Bi. Anita Ishengoma amesema vitengo vya ufuatiliaji na tathmini vina jukumu la msingi katika kuhakikisha sera na mipango ya wizara pamoja na taasisi zake inatekelezwa ipasavyo.

“Ni muhimu kwa vitengo vya ufuatiliaji na tathmini kuhakikisha sera na mipango ya wizara na taasisi zake inatekelezwa ipasavyo ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za maji na nishati kwa wananchi,” Amesema

Kwa upande wake, Bi. Kimario kutoka Wizara ya Maji, amesema Wizara ya Maji na Wizara ya Nishati zimekuwa zikifanya kazi kwa ukaribu kwa muda mrefu, hasa katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayogusa sekta zote mbili ukiwemo mradi wa umeme wa Julius Nyerere wa megawati 2,115 hivyo kuunganisha nguvu kwa Wizara hizo mbili kutatoa matokeo chanya zaidi katika utekelezaji wa miradi.


TANGA KUNUFAIKA NA MRADI WA "SCHOOL WaSH" CHINI YA UFADHILI WA ROTARY KUTOKA UHOLANZI.

February 11, 2026 Add Comment

 



Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga(TangaUWASA) imeingia makubaliano maalum na taasisi ya ROTARY inayofanya kazi kwa kushirikiana na Mamlaka za Maji Nchini Uholanzi (VEi) ya kutekeleza mradi wa kuwezesha huduma za kijamii mashuleni kupitia ujenzi wa vyoo (SCHOOL WaSH) kwa shule za msingi katika Jiji la Tanga.

Akizungumza kwa niaba ya uwakilishi wa ROTARY Bi.Emma Lesterhuis ameainisha kuwa mradi huo utatekelezwa na TangaUWASA kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Tanga na utajikita zaidi katika ujenzi wa vyoo kwa baadhi ya shule zenye idadi kubwa ya wanafunzi na uhaba wa matundu ya vyoo.

Nae kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TangaUWASA, Mha. Geofrey Hilly amewashukuru ROTARY kwa kutambulisha mradi huo ambao unaenda kuwezesha jamii hususani wanafunzi kupata huduma muhimu na kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha wakati wote wa utekelezaji wa mradi na usimamizi wake.



Tanga unakuwa Mkoa wa tatu nchini kunufaika na mradi wa "SCHOOL WaSH" ukiungana na Mikoa ya Arusha na Mwanza ambayo utekelezaji wake unaendelea.