KORTI YAAGIZA
TFF IKAMATE MIL 106/- KULIPA WACHEZAJI YANGA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
tumepokea amri ya Mahakama Kuu (Kitengo cha Kazi) kukamata sh. milioni 106 za
klabu ya Yanga kutokana na mapato ya mlangoni kwenye mechi zake ili kuwalipa
waliokuwa wachezaji wake Stephen Malashi na Wisdom Ndlovu.
Tayari tumeanza utekelezaji wa amri hiyo ambapo
katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) dhidi ya Rhino Rangers iliyochezwa
Machi 22 mwaka huu mjini Tabora tumezuia sh. 9,221,250 ambazo ndizo zilizokuwa
mgawo wa Yanga katika mchezo huo ulioingiza jumla ya sh. 38,655,000.