March 25, 2014
KORTI YAAGIZA TFF IKAMATE MIL 106/- KULIPA WACHEZAJI YANGA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tumepokea amri ya Mahakama Kuu (Kitengo cha Kazi) kukamata sh. milioni 106 za klabu ya Yanga kutokana na mapato ya mlangoni kwenye mechi zake ili kuwalipa waliokuwa wachezaji wake Stephen Malashi na Wisdom Ndlovu.

Tayari tumeanza utekelezaji wa amri hiyo ambapo katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) dhidi ya Rhino Rangers iliyochezwa Machi 22 mwaka huu mjini Tabora tumezuia sh. 9,221,250 ambazo ndizo zilizokuwa mgawo wa Yanga katika mchezo huo ulioingiza jumla ya sh. 38,655,000.
March 25, 2014

NAPE AMNADI RIDHIWANI

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Mkoko wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni za kumnadi kumgombea Ubunge jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete ambapo wananchi hao walielezwa kitendo cha kuzuiwa kupiga kura ni sawa na ubakaji wa Demokrasia na CCM itakula sambamba na wabakaji wa Demokrasia.