WAANDISHI WA HABARI MKOANI TANGA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HIFADHI YA MAMLAKA YA NGORONGORO

November 14, 2017
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali mkoani Tanga wakiingia kwenye hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro tayari kuanza ziara ya siku kumi ya mafunzo
 Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakiwa kwenye hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro mkoani Arusha wakati wa ziara ya siku tano kwa ajili ya ziara ya mafunzo kutembelea vivutio vya utalii kulia ni Mwandishi wa Shirika la Utangazaji la TBC ,Bertha Mwambela ambaye ni mratibu wa ziara hiyo kushoto ni Mbonea Herman wa Kituo cha Star TV kulia ni 
 Mratibu wa ziara ya waandishi wa habari mkoani Tanga waliotembelea hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro,Bertha Mwambele kutoka Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) wakiingia ndani ya mamlaka hiyo kulia ni Sussan Uhinga mwandishi wa gazeti la Mtanzania mkoan Tanga  kushoto ni Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka
 Mratibu wa ziara ya Waandishi wa Habari mkoani Tanga ambaye ni Mwandishi wa Shirika la Utangazaji la TBC Bertha Mwambele akiwa kwenye picha eneo la Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro mara baada ya kuwasili kwa ajili ya mafunzo ya siku kumi ikiwemo kutembelea hifadhi hiyo.
Waandishi wa habari wakipiga picha kwenye bango la mamlaka hiyo kabla ya kuanza ziara ya siku kumi kutoka kulia ni Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka,Lilian Lucas wa Mwananchi,Nestory Ngwega wa gazeti la Daily News,Bertha Mwambela wa TBC,Alex wa TATV,Pamela Chaula wa Tanga One Blog
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Ngorongoro,Walter Mairo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kabla ya kuanza ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ya hifadhi wakati wa ziara yao ya siku kumi
 Waandishi wa habari wakipata kifungua kinywa kabla ya kuanza ziara ya mafunzo ya siku kumi
 Mwandishi wa Kituo cha Tanga TV cha Jijini Tanga,Abraham Alex akiwa kwenye eneo la mchanga ambalo umekuwa ukihama mara kwa mara
 Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea eneo la mchanga ambalo limekuwa likihama mara kwa mara
 Waandishi wa habari,Mbaruku Yusuph wa gazeti la Tanzania Daima na Mbonea Hermani wa Star TV wakiangalia eneo la ambalo limegunduliwa fuvu la binadamu wa kwanza wakati wa ziara hiyo
 Jumba la Makumbusho ya Mambo ya Kale ambalo lipo eneo la Mamlaka ya Ngorongoro Mkoani Arusha
Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka kulia akitoa maelekezo kwa waandishi wa habari mara baada ya kutembelea Jumba hilo la Makumbusho
SWEDEN YAIPATIA TANZANIA MSAADA WA KIBAJETI SHILINGI BILIONI 436

SWEDEN YAIPATIA TANZANIA MSAADA WA KIBAJETI SHILINGI BILIONI 436

November 14, 2017

IMG_1575
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (wa pili kushoto) wakisaini Makubaliano ya Msaada wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
IMG_1582
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia)na Mkuu wa Kitengo cha  Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (kushoto) wakisaini Makubaliano ya Msaada wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
IMG_1593
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha  Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (kushoto) wakiwa wameinua juu Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
IMG_1612
Maafisa waandamizi kutoka Ubalozi wa Sweden Nchini Tanzania wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
IMG_1624
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi Amina Khamis Shaaban (Kushoto), Kamishna Msaidizi wa Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bi. Mamelta Mutagwaba na wengine wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
IMG_1641
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msaada wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kutoka Sweden kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa elimu, ambapo amesema msaada huo unatoa fursa kwa  Serikali kupeleka fedha zilizotakiwa kutekeleza majukumu hayo maeneo mengine ya Maendeleo ya Wananchi, hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
IMG_1670
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (kushoto) wakibadilishana Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
IMG_1684
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting (wapili kulia) pamoja na Maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango na Ubalozi wa Sweden wakiwa katika Picha ya pamoja baada ya kusainiwa  Mkataba wa  Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango
……………..
Dares Salaam, Novemba 14, 2017: Sweden imeipatia Tanzania Msaada wa jumla ya Fedha ya Sweden SEK. Bilioni 1.64 ambayo ni sawa na takribani Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na  kusaidia mpango wa elimu. 
Makubaliano ya msaada huo yamesainiwa Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James na Mkuu wa Kitengo cha  Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting.
Bw. James alisema kuwa imesainiwa Mikataba mitatu ya msaada huo ambayo ni; mkataba kwa ajili kusaidia Bajeti ya Serikali wa kiasi cha SEK milioni 600 ambazo ni sawa na Sh. bilioni 159.59 kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2017/18 hadi 2019/2020, ambapo kwa mwaka wa fedha 2017/2018 watatoa takribani Sh. bilioni 53.20.
Alisema fedha hizo zitaelekezwa katika kuboresha uhalisia wa Bajeti ili kuweza kutimiza majukumu ya kisera, kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya kikodi na yasiyo ya kodi na pia kusaidia Serikali kutoa huduma nzuri kwa wananchi kupitia taratibu za manunuzi. 
Mkataba mwingine ni kwa ajili ya kusaidia Mpango wa Elimu kwa Matokeo (EPforR) wa kiasi cha Fedha ya Sweden SEK milioni 885 ambayo ni sawa na Sh. bilioni 235.40 kuanzia mwaka 2017/18 hadi 2020/2021.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Dk. Akwilapo afungua mkutano wa wadau wa elimu

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Dk. Akwilapo afungua mkutano wa wadau wa elimu

November 14, 2017
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo akifungua mkutano wa 9 kwa wadau wa sekta ya elimu nchini ulioandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT). Mkutano huo umeanza leo New Dodoma Hoteli, Mkoani Dodoma. Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Cathleen Sekwao akizungumza leo kwenye mkutano wa 9 wa wadau wa sekta ya elimu nchini ulioandaliwa na TenMeT. Mkutano huo wa siku tatu umeanza leo New Dodoma Hoteli, Mkoani Dodoma. Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Cathleen Sekwao (kulia) akimpongeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo mara baada ya kufungua mkutano wa 9 kwa wadau wa sekta ya elimu nchini ulioandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT). Dk. Mkonongwa Mhadhiri UDSM akiwasilisha mada kwenye mkutano huo.   
Na Joachim Mushi, Dodoma KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo amefungua mkutano wa 9 kwa wadau wa sekta ya elimu nchini ulioandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT) ukiwa na lengo la kuangalia ubora na usawa wa elimu maeneo yote. Warsha hiyo ya siku tatu ambayo imeanza leo mjini Dodoma na kukutanisha mashirika mbalimbali wadau wa elimu kujadili namna ya kuboresha ufudishaji na ujifunzaji kwenye sekta ya elimu pamoja na kuimarisha hali ya utoaji elimu kwa ujumla. Akizungumza katika uzinduzi huo, Dk. Leonard Akwilapo alisema baada ya mafanikio ya awali katika kuongeza udahili wa wanafunzi katika ngazi zote za elimu, yaani kuanzia ngazi ya awali, elimu ya msingi, elimu ya sekondari na elimu ya juu nafasi iliyobaki ni kuboresha elimu yenyewe kwa ujumla. Alisema eneo hilo Serikali itahakikisha wanafunzi wanaohitimu wanapata stadi mbalimbali ambazo zimepangwa kulingana na mtaala katika ngazi hiyo. Aliwataka washiriki wa warsha hiyo kuangalia matatizo na fursa anuai zilizopo kwenye sekta ya elimu, pamoja na njia mbalimbali za kuweza kuboresha kisha mapendekezo hayo yawasiliswe Serikalimi ili kuangalia namna ya kufanyiwa kazi. Alisema katika mfumo wa sasa Serikali inatambua kuwa zipo baadhi ya shule zinazotoa elimu katika mazingira ambayo sio mazuri, lakini lengo lililopo ni kuhakikisha wanafanya maboresho ili kuondoa changamoto hizo. "..Tunatambua kwamba katika mfumo wetu wa elimu bado tuna shule ambazo zina hali ambayo sio nzuri, lengo la Serikali ni kuhakikisha zile shule zote ambazo zina hali mbaya sana zinaboreshwa...mfano zile ambazo zina mapaa ya nyasi tunataka zote tuzitoe ili kuongeza hamasa ya walimu na wanafunzi katika kupata elimu, Serikali kwa sasa tumesha sambaza vifaa kama vya maabara, vitabu na yote ni kuhakikisha tunaboresha," alisema Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Kwa upande wake Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Cathleen Sekwao ambao ni waandaaji wa mkutano huo, alisema sera ya elimu bila ada imekuwa ni nzuri licha ya uwepo wa changamoto mbalimbali ikiwemo ongezeko kubwa la wanafunzi kuanzia mwaka jana. Alizitaja changamoto hizo ni pamoja na upungufu wa vyumba vya madarasa, upungufu wa walimu na miundombinu ya elimu vikiwemo vitendea kazi. Bi. Sekwao alisema Serikali imejitahidi kuhamasisha wananchi kujiunga kusaidiana kukabiliana na changamoto mbalimbali na wao kama asasi za kiraia zinazo tetea elimu bora yenye usawa wamesaidia pia katika ujenzi wa madarasa, uchangiaji wa vifaa na kuhamasisa wananchi kusaidia utatuaji changamoto hiyo. Aidha aliongeza kuwa na wao asasi zisizo za serikali wameungana kuisaidia Serikali ambapo zipo asasi zilizojenga madarasa, zimejenga nyumba za walimu na zingine kuhamasisha wananchi kuchangia maboresho ya elimu hali ambayo imeanza keleta chachu maeneo mbalimbali nchini. Alisema lengo la mkutano huo ni kuangalia usawa wa elimu katika maeneo yote yaani vijijini na mijini ikiwemo kujadiliana na kushauri maboresho yenye tija katika sekta ya elimu kulingana na mahitaji ya sasa.   
Sehemu ya washiriki wa huo uliokutanisha mashirika mbalimbali wadau wa elimu kujadili namna ya kuboresha ufudishaji na ujifunzaji kwenye sekta ya elimu pamoja na kuimarisha hali ya utoaji elimu kwa ujumla wakifuatilia mada mbalimbali. 
Sehemu ya washiriki wa huo uliokutanisha mashirika mbalimbali wadau wa elimu kujadili namna ya kuboresha ufudishaji na ujifunzaji kwenye sekta ya elimu pamoja na kuimarisha hali ya utoaji elimu kwa ujumla wakifuatilia mada mbalimbali. 

TAMWA YAZINDUA WIKI YA KUADHIMISHA MIAKA 30 TANGU KUANZISHWA KWAKE, MHAVILE ATOA NENO

November 14, 2017
Mkurugenzi Mtendaji wa Vituo vya ITV, Radio One, Capital TV na Radio, Joyce Mhavile akizungumza jijini Dar es Salaam leo, wakati akizindua wiki ya miaka 30 ya Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA).
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mstaafu, Fatuma Mwassa, akizungumza na wanahabari katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Tamwa, Eda Sanga, akizungumza katika uzinduzi huo.
Wadau mbalimbali na wanahabari wakiwa kwenye uzinduzi huo. 

Uzinduzi wa wiki hiyo ukiendelea.

Taswira ya ukumbi wa mikutano ulipofanyika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Tamwa, Eda Sanga, akimvalisha vitengMkurugenzi Mtendaji wa Vituo vya ITV, Radio One, Capital TV na Radio, Joyce Mhavile vilivyo na Tamwa kama zawadi kwake. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mstaafu, Fatuma Mwassa
Mhavile, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo akiwa katika picha ya pamoja na wadau kutoka taasisi mbalimbali.
Ofisa Biashara wa Tamwa, Leonida Kanyuma (kulia), akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Joyce Mhavile kuhusu utendaji wa Tamwa.
Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi (C.R.C), Gladness Munuo akitoa maelekezo kwa mgeni rasmi Joyce Mhavile wakati alipokuwa akitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali kwenye uzinduzi huo.
Mtunza kumbukumbu na Taarifa wa TGNP-Mtandao, Speratus Kyaruzi akitoa maelezo mbele ya mgeni rasmi.
Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Shabani Rulimbiye, akimuonesha mgeni rasmi moja ya vipeperushi vya shirika hilo cha  kupinga ukatili wa kijinsia.
Mhavile akizungumza na wajasiriamali wakati alipotembelea mabanda yao.

Suleiman Msuya

WANAWAKE nchini wametakiwa kuonesha uwezo katika nafasi wanazozipata na kauchana na dhana ya kupata upendeleo au kubebwa kama inavyotafsiriwa na jamii.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Vituo vya ITV, Radio One, Capital TV na Radio, Joyce Mhavile wakati akizindua wiki ya miaka 30 ya Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) leo asubuhi jijini Dar es Salaam.

Mhavile alisema wanawake wengi wanaonesha kushindwa kufikia malengo yao katika nafasi mbalimbali ambazo wanapata kuzitumikia kutokana na kuishi na dhana kuwa watapewa upendeleo fulani.

Alisema tatizo hilo lipo kwa wanawake wa makundi yote wakiwemo waaandishi wa habari wafanyabiashara na makundi mengine ambayo yanabakia kulalamika.

“Mi nasema hivi ukipata nafasi katika dunia hii itumie kwa kuonesha uwezo wako ili watu watambue kipaji chako na si kutegemea kubebwa au upendeleo fulani kisa wewe mwanamke hiyo si sawa,” alisema.

Mhavile ambaye alizindua wiki hiyo ikishirikisha maonesha mbalimbali aliwataka wanawake ambao wanashiriki maonesho hayo kutumia vyombo vya habari kujitanga ili bidhaa zao ziweze kufahamika.

Mkurugenzi huyo alisema iwapo kila mwanamke ataondokana na dhana ya kuwezeshwa ni dhahiri kuwa watafanikiwa kwa haraka hivyo ubunifu kwa kila wanalofanya ni muhimu kwa sasa.

MIAKA KUMI NA TANO YA THE FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY,MKURUGENZI AELEZA MIPANGO MIPYA

November 14, 2017

Shirika lisolo la kiserikali ya The Foundation For Civil society linalojihusisha na kujenga uwezo wa asasi za kiraia nchini Tanzania pamoja na Kutoa ruzuku kwa asasi hizo linatimiza miaka kumi na Tano tangu kuannzishwa kwake  na kuanza kufanya kazi.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hii Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo lenye ofisi zake Jijini Dar es salaam Ndugu Francis Kiwanga alisema kuwa kwa miaka kumi na tano ya uwepo wake nchini wamefanikiwa kufanya kazi na Asasi zisizopungua elfu tano nchini ikiwa ni mafanikio makubwa kwa shirika hilo lililojumuisha asasi tofauti.

Nakupa nafasi ya kumsikiliza mkurugenzi wa shirika hilo akieleza kwa undani,kazi walizozifanya kwamiaka 15,changamoto walizopitia nma mipango ya kuendelea kuihudumia jamii kwa sasa.Katibu--- 

MKIKITA WASAINI MKATABA NA FARMSTER YA ISRAEL KUTAFUTA MASOKO YA MAZAO YA MKULIMA KWA MTANDAO WA SIMU

November 14, 2017
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Adam Ngamange (kushoto) na Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Farmster ya Israel, Adam Abramson wakitia sahihi mkataba wa makubaliano ambapo Farmster itatoa huduma za upatikanaji wa masoko ya mazao na bidhaa za wakulima wanachama wa Mkikita kwa njia ya mtandao wa simu. Hafla hiyo ilifanyika viwanja vya Camp of Good Hope, Goba  jijini Dar es Salaam.

Abramson ambaye ni mwasisi wa Farmster aliwaelezea waalikwa waliofika kwenye hafla hiyo jinsi  jinsi ya kujiunga na mtandao huo kwa kutumia simu za smart na za kawaida yaani 'vitochi' ambapo mkulima huingiza namba ya simu 0623 753016 kwa kutuma neno Jambo.

Mkulima atapaswa kutaja jina lake, eneo analoishi yaani shamba lilipo, analima zao gani, heka ngapi na anatarajia kuvuna lini na kwa kiasi gani ambapo huunganishwa moja kwa moja kwa mteja atakayejadiliana bei ya kuuzia.

Wakala Mkuu kati ya Mkulima na Mnunuzi utakuwa ni Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (MKIKITA), kitendo ambacho kitasaidia sana kuuvunja mtandao wa madadali wanaosumbua na kuwaibia wakulima.

Wakulima waliohudhuria hafla hiyo walionekana kufurahishwa na ujio wa teknolojia hiyo mpya na ya kisasa itakayowarahisishia wakulima kupata masoko mazao yakiwa shambani.IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Adam Ngamange (kushoto) akibadilishana hati za makubalino baada ya kutiliana sahihi mkataba  na Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Farmster ya Israel, Adam Abramson ambapo Farmster itatoa huduma za upatikanaji wa masoko ya mazao na bidhaa za wakulima wanachama wa Mkikita kwa njia ya mtandao wa simu
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Dk. Kissui S. Kissui (kushoto), akimpongeza Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Farmster ya Israel, Adam Abramson kutiliana sahihi mkataba wa makubaliano na Mkurugenzi Mtendaji wa  Mkikita, Adam Ngamange (katikati) ambapo Farmster itatoa huduma za upatikanaji wa masoko ya mazao na bidhaa za wakulima wanachama wa Mkikita kwa njia ya mtandao wa simu. 
 Abramson akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo
 Akionesha namba ya kujiunga na mtandao huo
 Wanachama wa Mkikita wakisikiliza wakati mtalaamu huyo akiwaelezea faida mbalimbali atakazopata mkulima kwa kutumia mtandao huo
 Abramson akionesha eneo alipo mmoja wa wakulima aliyejiunga na mtandao huo
 Mkulima akipata maelezo kutoka kwa Abramson