Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James (wa pili kulia) na Mkuu wa Kitengo cha
Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf
Kallsting (wa pili kushoto) wakisaini Makubaliano ya Msaada wa jumla ya
Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango
wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es
Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James (kulia)na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na
Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting
(kushoto) wakisaini Makubaliano ya Msaada wa jumla ya Sh. bilioni 435.79
kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa elimu, katika
ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na
Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting
(kushoto) wakiwa wameinua juu Mkataba wa Msaada wa wa jumla ya Sh.
bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa
elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Maafisa waandamizi kutoka Ubalozi
wa Sweden Nchini Tanzania wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa
Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti
na kusaidia mpango wa elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na
Mipango Jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Fedha na Mipango, Bi Amina Khamis Shaaban (Kushoto), Kamishna Msaidizi
wa Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bi. Mamelta Mutagwaba na wengine
wakishuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Msaada wa wa jumla ya Sh.
bilioni 435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa
elimu, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msaada
wa jumla ya Sh. bilioni 435.79 kutoka Sweden kwa ajili ya Msaada wa
kibajeti na kusaidia mpango wa elimu, ambapo amesema msaada huo unatoa
fursa kwa Serikali kupeleka fedha zilizotakiwa kutekeleza majukumu hayo
maeneo mengine ya Maendeleo ya Wananchi, hafla iliyofanyika Jijini Dar
es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na
Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting
(kushoto) wakibadilishana Mkataba wa Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni
435.79 kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa elimu,
katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James (wa pili kushoto), Mkuu wa Kitengo cha
Ushirikiano na Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf
Kallsting (wapili kulia) pamoja na Maafisa waandamizi kutoka Wizara ya
Fedha na Mipango na Ubalozi wa Sweden wakiwa katika Picha ya pamoja
baada ya kusainiwa Mkataba wa Msaada wa wa jumla ya Sh. bilioni 435.79
kwa ajili ya Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa elimu, katika
ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango
……………..
Dares Salaam, Novemba 14, 2017:
Sweden imeipatia Tanzania Msaada wa jumla ya Fedha ya Sweden SEK.
Bilioni 1.64 ambayo ni sawa na takribani Sh. bilioni 435.79 kwa ajili ya
Msaada wa kibajeti na kusaidia mpango wa elimu.
Makubaliano ya msaada huo
yamesainiwa Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na
Mipango, Bw. Doto James na Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano na Maendeleo
wa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallsting.
Bw. James alisema kuwa imesainiwa
Mikataba mitatu ya msaada huo ambayo ni; mkataba kwa ajili kusaidia
Bajeti ya Serikali wa kiasi cha SEK milioni 600 ambazo ni sawa na Sh.
bilioni 159.59 kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2017/18 hadi 2019/2020,
ambapo kwa mwaka wa fedha 2017/2018 watatoa takribani Sh. bilioni 53.20.
Alisema fedha hizo zitaelekezwa
katika kuboresha uhalisia wa Bajeti ili kuweza kutimiza majukumu ya
kisera, kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya kikodi na yasiyo ya
kodi na pia kusaidia Serikali kutoa huduma nzuri kwa wananchi kupitia
taratibu za manunuzi.
Mkataba mwingine ni kwa ajili ya
kusaidia Mpango wa Elimu kwa Matokeo (EPforR) wa kiasi cha Fedha ya
Sweden SEK milioni 885 ambayo ni sawa na Sh. bilioni 235.40 kuanzia
mwaka 2017/18 hadi 2020/2021.