MAMIA WAJITOKEZA KUMUAGA MWANAHABARI PATRICK MWILLONGO

February 16, 2018
 Mwanahabari Patrick Mwillongo enzi za uhai wake
 Ndugu zake marehemu Patrick Mwillongo wakiwa kwenye ibada ya kumuaga mpendwa wao iliyofanyika nyumbani kwao Kiburugwa Mbagala jijini Dar es Salaam jana.
 Ibada ikiendelea.
 Waombolezaji wakifuatilia ibada hiyo.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Mchungaji Yusuph Peter wa Kanisa na Tanzania Assemblies of God Kingugi jijini Dar es Salaam, akiongoza ibada hiyo.
 Mjane wa marehemu Theresia Conrad akiwa mwenye majonzi kwa kuondokewa na sukari yake mmewe.
 Huzuni katika ibada hiyo.
 Dada wa marehemu akilia mbele ya jeneza lenye mwili wa mdogo wake.
 Mwanahabri Careen akitoa heshima za mwisho. Kushoto ni mwanahabari Kulwa Mwaibale.
 Heshima za mwisho zikiendelea kutolewa. Wa pili kutoka kushoto ni Mwanahabari Dotto Mwaibale na wa tatu ni Kulwa Mwaibale.
 Msafara kuelekea makaburini Chang'ombe ukianza kutokea nyumbani kwao marehemu.
 Jeneza likishushwa kaburini.
 Watoto wa marehemu wakiweka shada la maua kwenye kaburi la mpendwa baba yao.
 Mwanahabari Kulwa Mwaibale akiweka shada la maua katika kaburi la Mwillongo.
Baadhi ya waaandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja na mjane wa marehemu.

Na Dotto Mwaibale

MAJONZI, vilio na simanzi vilitawala wakati wa ibada ya kumuaga Mwanahabari Patrick Mwillongo aliyefariki dunia Machi 12, mwaka huu katika Hospitali Ndogo ya Muhimbili ya Mloganzila iliyopo Kibamba nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu na mazishi yake kufanyika katika makaburi ya Chang'ombe Maduka Mawili.

Akizungumza wakati akitoa mahubiri katika ibada hiyo iliyofanyika jana, Mchungaji Yusuph Peter wa Kanisa na Tanzania Assemblies of God Kingugi aliwakumbusha watu wote waliokuwepo kwenye ibada kujiandaa kwa maana hawajui ni lini watafikwa na mauti.

"Mwenzetu Patrick Mwillongo atunaye tena amekufa sasa sisi tulio hai kwa dini zetu tunapaswa kujitafakari kwa kuacha dhambi na kutubu" alisema Peter.

Katika ibada hiyo na mazishi ya Mwillongo yalihudhiriwa na baadhi ya waandishi wa habari wasiozidi 10, Mkuu wa Wilaya Mstaafu wa Wilaya ya Bagamoyo, Hemed Kipozi na ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Mwillongo.

Marehemu Patrick Mwillongo aliyezaliwa mwaka 1975 enzi za uhai wake alikuwa akiandikia magazeti ya Mtanzania na Jambo Leo na ameacha wajane na  watoto kadhaa. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amina.

Katika tukio la kusikitisha usiku wa kuamkia leo vibaka walivamia katika msiba huo nyumbani kwao marehemu Kiburugwa na kufanikiwa kuiba mikoba ya wafiwa iliyokuwa na simu na vitu vingine.



SERIKALI YAJIPANGA KUWAJENGEA UWEZO WATOA HUDUMA KATIKA SEKTA YA UTALII NA UKARIMU NCHINI

February 16, 2018


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki akizungumza na  wadau wa sekta ya  utalii waliokutana jana katika mkutano uliofanyika jana mjini Dodoma   kwa ajili ya kupitia Rasimu ya kanuni za kusimamia ubora wa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii


 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Deograsias Mdamu ( wa kwanza kulia) akimkaribisha  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki (katikati) kwa ajili ya  kuzungumza na  wadau wa sekta ya  utalii waliokutana jana katika mkutano uliofanyika mjini Dodoma   kwa ajili ya kupitia Rasimu ya kanuni za kusimamia ubora wa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii


Baadhi ya wadau wa sekta ya utalii  wakifuatilia  uwasilishaji wa Rasimu ya kanuni za kusimamia ubora wa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii katika mkutano uliofanyika jana mjini Dodoma   uliowakutanisha wadau wa sekta hiyo kwa ajili ya kupitia rasimu hiyo.



Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utalii, Paskas Mwiru  akizungumza na  wadau wa sekta ya  utalii waliokutana jana katika mkutano uliofanyika mjini Dodoma   kwa ajili ya kupitia Rasimu ya kanuni za kusimamia ubora wa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii



Baadhi ya  wakurugenzi wasaidizi  wakifuatilia  uwasilishaji wa Rasimu ya kanuni za kusimamia ubora wa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii katika mkutano uliofanyika jana mjini Dodoma   uliowakutanisha wadau wa sekta ya Utalii kwa ajili ya kupitia rasimu hiyo.



Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Deograsias Mdamu akisisitiza jambo  katika mkutano uliofanyika jana mjini Dodoma kati ya Wadau wa sekta ya utalii na Wizara  kwa ajili ya kupitia Rasimu ya kanuni za kusimamia ubora wa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii



Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Viwoso  Mkwizu akiwasilisha Rasimu ya kanuni za kusimamia ubora wa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii katika mkutano uliofanyika jana mjini Dodoma   uliowakutanisha wadau wa sekta ya Utalii kwa ajili ya kupitia rasimu hiyo. ( PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-MNRT)

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imewasilisha  rasimu ya   kanuni ya kusimamia watoa huduma katika sekta ya utalii na ukarimu kwa wadau wa sekta hiyo  ili waweze kutoa maoni yao  yatakayosaidia katika kuboresha kanuni hizo ili ziweze kuwasimamia wafanyakazi  kwa kuhakikisha kuwa  huduma zinazotolewa   zinazokidhi viwango vya kimataifa kwa watalii.

Akizungumza  jana mjini Dodoma kwenye  mkutano uliowakutanisha wadau wa sekta hiyo  kwa ajili ya kupitia Rasimu ya kanuni hiyo,  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki alisema Wizara imeandaa rasimu hiyo  ili kutoa nafasi kwa wadau  kuipitia na kutoa maoni yatakayoisaidia katika kuiboresha.

Akizungumzia moja ya  lengo la kanuni hizo ni  kutaka  kuwajengea uwezo wafanyakazi wa tasnia hiyo ili waweza kushindana katika soko la ajira la kitaifa na kimataifa.

Aliongeza kuwa kanuni hizo  pia  zitasaidia  kuwawekea ulinzi na usalama katika taaluma hiyo pamoja na kuleta uwajibikaji na uaminifu katika kutoa huduma kwa vile kutakuwa na  mfumo wa kuwatambua.

Alisema hatua hiyo ya ukusanyaji maoni  imekuja baada ya sekta hiyo ya  kukabiliwa na changamoto ya huduma hafifu zinazotolewa kwa watalii hususani wale wa kimataifa.

Alisema hali hiyo imechangiwa na ukosefu wa chombo cha kusimamia viwango vya huduma zinazotolewa katika sekta hiyo.

Alisema kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu kutoka watalii kuwa huduma wanazopata ni hafifu.

Awali, Mkurugenzi wa idara ya Utalii, Deograsias Mdamu, alisema majadiliano hayo  ya kuboresha  kanuni hizo yatasaidia kuwa na wafanyakazi mahiri na wenye weledi katika tasnia hiyo.

Aliongeza kuwa,  maoni hayo yatapelekea kuunda kanuni bora na shirikishi zitakazosaidia  katika kuwasimamia wafanyakazi na waajiri  katika kutoa huduma  bora kwa watalii kwa kila mmoja kwa nafasi yake.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha waongoza watalii Tanzania, Emannuel Mollell aliipongeza Wizara kwa hatua h iliyofikia ya kuandaa rasimu hiyo kwa vile rasimu hiyo  inatoa muelekeo mzuri  katika sekta ya utalii na ukarimu nchini.

Akichangia maoni Katibu huyo , Emanuel Molleli alisema ni vyema  kanuni  igusie maslahi ya wafanyakazi    kwani hicho kimekuwa  ni kilio chao cha  muda mrefu lakini katika  rasimu hiyo hakuna kipengele chochote kilichozungmzia suala hilo.

Aliongeza kuwa  wafanyakazi wa tasnia hiyo kwa ujumla wake  wamekuwa wakilipwa mshahara midogo sana hali inayoplekea kushusha morali katika kuwahudumia watalii kwa viwango bora.

 Kutokana na uwasilishwaji wa maoni hayo , hali hiyo ilimfanya   Mkurugenzi wa Idara ya hiyo, Mdamu kumjibu    kuwa suala hilo litaangaliwa.

Naye, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Bety Begashe wakati akichangia maoni aliiomba  Wizara iiangalie namna bora itakayosaidia kutoa mafunzo kwa wafanyakazi hao mbali na mitihani itakayokuwa inafanywa na wanatasnia hao.