Na Oscar Assenga, Mkinga.
Kauli ya Mkuu huyo wa wilaya ilisomwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Mkinga Zuwani Makame hivi karibuni aliyemuwakilisha katika uzinduzi wa kampeni ya kilimo cha muhogo iliyoanzishwa na shirika la Farm Radio Internationali kwa kushirikiana na kituo cha Radio Mwambao ya Tanga.
Mwisho
MKUU wa wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza amesema serikali
wilayani humo itaendelea kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kilimo cha
Muhogo ili kiweza kuwa mkombozi wao katika maendeleo na kuinua kipato chao.
Kauli ya Mkuu huyo wa wilaya ilisomwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Mkinga Zuwani Makame hivi karibuni aliyemuwakilisha katika uzinduzi wa kampeni ya kilimo cha muhogo iliyoanzishwa na shirika la Farm Radio Internationali kwa kushirikiana na kituo cha Radio Mwambao ya Tanga.
Makame alisema Serikali inatambua umuhimu wa elimu kwa
wakulima ikiwemo kuwapatia wakulima elimu stahiki kuhusu kilimo chenye tija
wataweza kunufaika na kilimo chao, hivyo itaendelea kuandaa mazingira mazuri
kwa ajili ya kuwawezesha wakulima kupata elimu ya kilimo bora.
Aidha alisema kuwa kumekuwa na changamoto mbalimbali kwenye
shughuli za kilimo katika maeneo mengi hasa ya wilaya ya Mkinga, na changamoto
kubwa ni ukosefu wa elimu ya njia bora ya kuendesha kilimo chenye tija hivyo
kampeni hizi zimekuja wakati muafaka, naamini zitawanufaisha wakulima na kuweza
kupata mazao mengi katika kilimo chao.
Alieleza kuwa uzinduzi wa kilimo hicho utasaidia wananchi kujiondoa
kwenye umasikini kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo, na ndicho ambacho wenzetu
wa Farm Radio international kupitia mradi huu wanafanya kuelimisha wakulima kwa
njia ya Radio.
Hata hivyo amesema licha ya kuwa na wataalamu wa ugani
wachache na hivyo matumizi ya redio yatasaidia kuwafikia wakulima wengi sana
kwani redio zinafika maeneo mengi ili kuweza kuongeza ujuzi kwa wakulima hao
kabla ya kuanza msimu wa kilimo.
Katibu Tawala huyo amewataka wakulima wote wa vijiji vya
Mzingi Mwagogo, Mapojoni, Mvunde manyinyi na vijiji vyote vya wilaya ya Mkinga
na vijiji jirani vya wilaya za jirani ambapo kampeni hizi zinagusa kupitia
mradi wa njia bora za uvunaji ,usindikaji na uhifadhi wa zao la muhogo , mtumie vema fursa hii
iliyoletwa na wenzetu wa Farm Radio kwa
kushiriki kwenye Kampeni hii kikamilifu.
Ameongeza kuwa kampeni hii itawanufaisha sana kwenye kilimo
na itawasaidia kupata masoko na kujiongezea kipato ikiwa watazingatia vema yale
yatakayokuwa yanafanyika na kuelezwa na wataalamu mbalimbali wa kilimo.
Awali akizungumza katika uzinduzi huo, Mtaalamu wa Mnyororo
wa thamani kwenye mazao ya kilimo kutoka shirika la Farm Radio International
lenye makao yake makuu jijini Arusha, Terevael Aremu Nassary amesem,a shirika
hilo limeona umuhimu wa kushirikiana na radio Mwambao ya Tanga katika kufikisha
elimu yake juu ya njia bora za uvunaji,usindikaji na uhifadhi wa zao la muhogo
ambalo lina soko na linazalishwa kwa wingi mkoani Tanga ikiwemo wilaya ya
Mkinga.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa radio Mwambao FM, Mfaume
Kikwato alisema vipindi vya elimu juu ya njia bora ya uvunaji, usindikaji na
uhifadhi wa zao la Muhogo vitakuwa vikirushwa na kituo hicho kuanzia Julai 5
mwaka huu na kuendelea kila siku za Ijumaa saa moja hadi saa moja na nusu na
marudio yake yatakuwa Jumapili saa moja na nusu mpaka saa mbili usiku.
Mwisho