MADADI
MKURUGENZI MPYA WA UFUNDI TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua
Salum Madadi kuwa Mkurugenzi wake mpya wa Ufundi.
Uteuzi huo umefanya na Kamati ya Utendaji katika
kikao chake cha dharura kilichofanyika jana (Machi 19 mwaka huu) jijini Dar es
Salaam.
Kabla ya uteuzi, Madadi alikuwa akikaimu nafasi
hiyo tangu Januari mwaka huu baada ya Mkurugenzi wa Ufundi aliyekuwepo kumaliza
mkataba wake Desemba 31 mwaka jana.