NAIBU WAZIRI UMMY MWALIMU APOKEA SHLLLINGI MILIONI 100 KWA NIABA YA TAYOA KUTOKA NBC KUSAIDIA VIJANA!!

November 27, 2013

 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto) akipokea mfano wa hundi ya shs milioni 100 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bi. Mizinga Melu kusaidia mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA). Hafla ilifanyika wakati wa tukio la uzinduzi wa mradi huo unaodhaminiwa na NBC jijini Dar es Salaam jana. Katikani ni Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika.
 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Bi. Mizinga Melu (katikati) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Bi. Mwinda Kiula Mfugale wakionyesha vipeperushi kuashiria uzinduzi wa tofuti ya vijanatz.com ikiwa na habari kuhusu ajira (kazitz.com), fedha (fedhatz.com) na ujasiriamali (biasharatz.com). Hafla hiyo ilikwenda sambamba na uzinduzi wa mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana  wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA) unaodhaminiwa na NBC.
3: Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Mizinga Melu akishikana mikono na Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika baada ya kukabidhi  mfano wa hundi ya shs milioni 100 zilitotolewa na benki hiyo kusaidia mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA). Hafla ilifanyika wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi huo unaodhaminiwa na NBC. Kushoto ni Naibu Waziri wa Maendeleo aya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu na kulia ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa NBC, Mwinda Kiula Mfugale.
 Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika (kushoto), Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kulia), na Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa NBC, William Kallaghe wakibadilishana mawazo katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa TAYOA, Peter Masika (kushoto), Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu (kulia), na Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa NBC, William Kallaghe wakibadilishana mawazo katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Mizinga Melu akizungumza na vijana na wageni wengine kuhusu huduma za kibenki na kuhusu mikakati ya benki kusaidia suala la ajira na ujasiriamali kwa vijana katika hafla hiyo.
Wasanii wakitoa burudani kusindikiza uzinduzi wa mradi wa mafunzo ya masuala ya ajira na ujasiriamali kwa vijana wa Shirika la kuelimisha vijana nchini (TAYOA) unaodhaminiwa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jijini Dar es Salaam

UHAMIAJI TANGA WAKABILIWA NA UPUNGUFU WA VIFAA VYA BAHARINI

November 27, 2013


Na  Raisa  Said,Tanga
IDARA ya  Uhamiaji  mkoani  Tanga  inakabiliwa na  changamoto  ya Ukosefu wa  vifaa vya baharini  boti  na  meli  kwa ajili ya doria za baharini dhidi ya wahamaaji haramu wanaongia nchini kwa njia za mwambao wa Pwani.
 
Hayo yamesemwa na Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga  Sixtus Nyaki wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini  kwake   kuhusu hali ya wimbi la uhamiaji haramu katika Mkoa huu kwa sasa, ambapo alisema kwa sasa wanalazimika  kutumia  boti  la  jeshi la  polisi mkoani.
 
“ Tunatumia boti moja la polisi kwa ajili ya doria za mara kwa  mara  za  baharini ,kitu ambacho  wakati mwingine tunashindwa kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu kutoka na boti hiyo kutumika kwa doria nyingine na Jeshi la Polisi”alisema Nyaki.
 
Nyaki alisema ukubwa wa mipaka ya baharini hadi nchi kavu ni mikubwa hivyo kusababisha kushindwa kuithibiti kwa pamoja hali inayosababisha wahamiaji haramu wengi kuvuka na kuingia nchini  kwanjia za panya.
 
Afisa  huyo alisema ushiriki wa wananchi katika biashara ya kusafirisha wahamiaji haramu imekuwa ni chanzo cha tatizo hilo kuwa kubwa kwani wengi wao wanategemea kuishi kwa kusafirisha wahamiaji hao na kuchangia ongezeko la wahamiaji hao.
 
Hata hivyo  aliongelea  juu  ya  kiasi cha wahamiaji   haramu   waliokamatwa katika kipindi cha Octoba  hadi sasa   kuwa  ni kiasi cha wahamjia 68 wamekamatwa sehemu mbalimbali za mkoa  huu.
 
Aliwataja wahamijai hao waliokamatwa  kuwa  wengi ni kutoka katika nchi ya Ethiopia na wengine kutoka nchi  mbalimbali duniani hapa na wengine  wakiishi nchini kinyume cha sharia.
 
Wahamiajia hao na idadai yao ni Waethiopia 48,Wakenya 6,Waganda 5,Wajerumani 3,Wanaijeria 2,Mreno 1,Msomali 1,naraia wa Peru 1.

TANROADS TANGA YAPITISHA MAOMBI YA KUPANDISHWA HADHI BARABARA BUMBULI.

November 27, 2013


   (Meneja wa Tanroads mkoa wa Tanga,Mhandisi Alfred Ndumbaro|}
 
Raisa Said,Tanga.
 
Bodi ya Barabara Mkoani Tanga (TANROADS) imepitisha maombi ya kupandishwa hadhi barabara zenye urefu wa kilometa 130 zinazounganisha vijiji 9 katika Halmashauri mpya ya Bumbuli, mkoani Tanga.
 
Akiwakilisha ombi hilo kwa wajumbe wa Bodi ya barabara iliyokutana hapa mwishoni mwa juma lilipita, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bumbuli, Beatrice Musomisi alisema amewasilisha maombi kwa ajili ya kupandishwa hadhi barabara za halmashauri ya Bumbuli ili ziweze kuhudumiwa na wakala wa barabara Tanzania (TANROADS).
 
Msomisi alisema kwamba barabara hizo ni muhimu kwani zinaunganisha makao makuu ya Bumbuli na halmashauri za wilaya ya Lushoto na Korogwe kupitia kwenye barabara za mkoa za Mombo/Lushoto/Soni/Bumbuli/Dindira na Kwamote pamoja na Mashewa na Bombo Mtoni.
 
Mkurugenzi huyo wa Halmashauri ya Bumbuli alizitaja barabara zitakazounganishwa na vijiji 9 kuwa ni Soni/Mponde/Funta/Tamota/Kerenge ambazo zina urefu wa kilomita 60.
 
Alizitaja barabara nyingine kuwa ni pamoja na Mbelei/Mgwashi/Milingano/Mashewa zenye urefu wa kilomita 70.
 
Hata hivyo, Msomisi alifafanua kuwa kupandishwa hadhi kwa barabara hizo kutasaidia usafirishaji wa mazao ya wakulima katika jitahada za kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na hatimaye kuinua maendeleo ya Halmashauri ya Bumbuli kwa ujumla.
 
Kwa mujibu wa Meneja wa Tanroads Mkoani hapa, Eng. Alfred Ndumbaro maombi hayo ya barabara yamefuata taratibu zote ndani ya Halmashauri ya wilaya na kwamba vikao husika vilikaa na kupitisha maombi hayo.
 
Meneja huyo wa barabara alizitaka halmashauri za wilaya kuzipa umuhimu wa matunzo barabara zote zinazohudumiwa na Wakala wa Barabara (TANROADS) kwa kuwa ni chanzo cha maendeleo.

MAKAMBA :MGOGORO WA KIWANDA CHA MPONDE SIO WA KISIASA.

November 27, 2013
RAISA SAIDI,BUMBULI.
Naibu  Waziri  wa  Mawasiliano  Sayansi na  Teknolojia  January  Makamba  amewataka  baadhi  ya watu  kuondokana  na dhana  ya  kusema  mgogoro  wa  kiwanda cha  chai  cha  Mponde   ni siasa   badala  yake amewataka  kuiacha  serikali  indelee na taratibu zake  za  kulitafutia  ufumbuzi  swala hilo.
Makamba  ambaye pia   ni  Mbunge  wa  jimbo  la  Bumbuli  alisema  yeye kama  mbunge  wa  eneo hilo  lazima  ashirikiane  na  wananchi  wake  na  si kikundi  cha  watu wachache  licha ya kutukanwa  kwa  kuwaunga mkono  wananchi  wake.

Naibu  waziri  huyo  alieleza  kusikitishwa  kwake  na  baadhi ya  watu  kusema  swala  hilo  ni  la  kisiasa na  kwamba  linamaslahi  binafsi  ambapo alisema  ni upambuvu   nakwamba  tangu  2010  wakati  wa  uchaguzi ulishapita  sasa  ni wakati  wa  kuleta  maendeleo  kwa  wananchi  waliomuamini  na  kumtuma  kuwa  muwakilishi wao  bungeni na   si vinginevyo.

“Siamini   kama  kuwaunga  mkono  wananchi  walionichagua yanatokana na tofauti za kisiasa kwani eneo hili linamilikiwa na Chama kimoja ambacho ni Chama cha Mapinduzi na wala sina  maslahi binafsi katika suala hilo” Alisema  Makamba  nakuongeza  kuwa  yeye  anawasimia  wakulima  wa zao la  chai  kupata  haki yao  ya  msingi .


Kiwanda cha Mponde  kimefungwa  takribani  miezi  mitano  sasa kufuatia wakulima kususa kupeleka majani mabichi ya chai kwa madai ya kutaka Uongozi wa Chama cha Wakulima wa Chai Usambara (UTEGA) uitishe Mkutano Mkuu na kuwasomea mapato na matumizi ya chama hicho ikiwa ni pamoja na mapato ya kiwanda ambacho kinamilikiwa na chama hicho.


Hivi  karibuni Makamba, alimwaga machozi hadharani katika kijiji cha Mponde Kweminyasa kutokana na taarifa za watu watano kujeruhiwa kwa risasi za moto kufuatia vurugu zilizotokea  kati ya wakulima wa zao la chai  na Jeshi la polisi.


Vurugu hiyo ilitokea kutokana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu Chiku Gallawa kuamuru kiwanda cha chai cha Mponde kilichokuwa kimefungwa kwa mwezi mmoja na nusu wakati  huo kifunguliwe kwa nguvu chini ya usimamizi wa Polisi jambo  ambalo  zilisababisha  vurugu  kubwa  mpaka  watu  kujeruhiwa  kwa  risasi za  moto.



Makamba alisema kuwa kuna haja kubwa ya kuwepo maridhiano katika kufungua kiwanda hicho badala ya kutumia nguvu. “Unaweza kufungua kiwanda kwa bunduki lakini huwezi kukiendesha kwa bunduki,” alisema na kuwataka wakulima wa Chai wa Mponde kuwa na subira na uvumilivu kwa sababu haki yao haiwezi kupotea kwa sababu kiwanda hicho ni mali yao.

MAKAMU MWENYEKITI UTEGA AONJA JOTO YA JIWE,ATIMULIWA MKUTANONI.

November 27, 2013


   (MBUNGE WA JIMBO LA BUMBULI JANUARI MAKAMBA|}
NA RAISA SAID,BUMBULI.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Chai{UTEGA} katika Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli Richard Mbuguni alipata wakati mgumu baada ya wakulima wa zao la chai kumtaka aondoke  katika mkutano wa hadhara uliofanyika mwishoni mwa juma kwa  kile  kilichoelezwa  kukosa  imani nae.

Uamuzi huo  wa wakulima  ulikuja baada  ya wao kuona hakuna  haja  ya  makamu mwenyekiti  huyo   kuendelea  kushiriki  kikao hicho  huku  wakidai  ni  mmoja  wa wasaliti  wa zao  hilo na ambao  wako upande  wa mwekezaji  ambaye  alikuwa  akiwanyanyasa  wakati wote licha  ya wao kuwaweka  madarakani  viongozi  hao.

Wakizungumza  kwa  nyakati  tofauti  wakulima  hao  wapatao  zaidi  ya 1000  ambao  walionekana  kuwa  na  jazba,  walisema  hawawezi kushirikiana  na  mtu  ambaye  anawanyonya    na  anayesabisha  uchumi  wa  Bumbuli   kushuka  kwa  kuendelea  kumkumbatia  muwekezaji  na  kuwasaliti wao ambao  ndio  wamiliki wa  kiwanda hicho.

Mmoja  wa  wakulima hao  alietambulika  kwa jina  la  Mustafa Soa,  mkazi  wa  kijiji  cha  Kweminyasa   alisema  wao kama  wakulima  hawezi  kujadili  mambo  yao  wakati   viongozi wa Chama  cha Utega  wakiendelea  kuwepo  katika  maeneo  ya mkutano   kwa kuwa  wao  tangu  zamani  hawako  pamoja nao.

Awali  ofisa  Tarafa  wa  Bumbuli  Ismail  Kimweri   katika  kuwatuliza  wakulima  hao  ili  wamuache  makamu  mwenyekiti  ashiriki  mkutano  huo alifikia  hatua  ya  kuwaimbia  wimbo  kwa lugha ya  kisambaa  wenye  maneno  “ Mkazio Kuhembezana wenye  maana  ya  unyumba  ni  mapatano  ambao  uligonga  mwamba.

Akizungumza  katika  mkutano huo wa kujadili uuzaji wa  majani  ya  chai  nje ya kiwanda cha Mponde, ambacho kwa sasa kimefungwa,  Mbunge  wa  Jimbo  la  Bumbuli  January  Makamba  aliwasihi  kuwa  wavumilivu  katika  kipindi  hiki cha mpito na kuwataka  waendelee kutunza zao la chai  na  wauze  majani  ya  chai  kwenye  viwanda  vingine vya  jirani ili waweze kujikimu  kimaisha.

Makamba  ambaye pia ni  Naibu  Waziri  wa  Mawasiliano  Sayansi  na  Teknolojia, alisema  amekwisha zungumza na menejimenti za viwanda hivyo ili viongeze uzalishaji na vifaa vya kusafirishia chai kutoka mashambani hadi kwenye viwanda.

Hata  hivyo  mbunge huyo  aliwataka   wakulima  hao  kuendelea kuwa  na subira  kwa kuwa  ufumbuzi  wa  kufunguliwa  kwa  kiwanda  hicho  unakaribia  kufikia  ukingoni  kwa kuwa  suala  hilo  liko  mikononi  mwa  ngazi  za  juu za  serikali.