WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YENYE TIJA ,ILI KUPATA MAZAO YENYE BORA

January 26, 2017
 mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro,wakati akiofungua Maonyesho ya zana za kilimo  katika viwanja  vya Taasisi ya Utafiti wa kilimo ya Seliani 
 Afisa mauzo wa kampuni ya Irrico Saimoni Manyike   akimuelewesha mkulima jinsi kampuni yao inavyofanya kazi ya kusambaza teknolojia ya umwagiliaji wa Matonye
 Washiriki ambao ni wakulima wakifuatilia kwa makini mada ambazo zilikuwa zikiendelea wakati wa ufunguzi

   Habari picha na Woinde Shizza,Arusha

sekta ya kilimo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo  ufugaji holela , ambao  hupelekea uharibifu wa mazingira,Teknolojia duni pamoja na ugumu wa kupata mitaji ya kuboresha miundombinu ya kilimo.



Hayo yamebainishwa na mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro,wakati akiofungua Maonyesho ya zana za kilimo  katika viwanja  vya Taasisi ya Utafiti wa kilimo ya Seliani  vilivyopo ndani ya jijini Arusha ambapo ni mara ya kwanza kufanyika  .



Alisema kuwa sekta ya kilimo inakabiliwa na changamoto za ufugaji holela ambao unasababishwa na wafugaji ,wakulima kutumia teknolojia duni au zazamani katika ukulima  pamoja na wakulima wengi kukosa mitaji ya kubesha miundo mbinu ya kilimo



Alisema kuwa hii inachangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha maendeleo ya sekta hii kutokana na wananchi wengi kutumia kilimo cha kawaida badala yakutumia kilimo cha kisasa ambacho kinaleta tija .