NAIBU KATIBU MKUU WA CCM BARA NDG: RODRICK MPOGORO AFUNGUA MAFUNZO ELEKEZI KWA MAKATIBU WA UVCCM MIKOA YA TANZANIA BARA NA VISIWANI.

August 27, 2017
Naibu katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi ndg; Rodrick mpogoro akifungua Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaam.
 Mwenyekiti wa umoja wa Vijana na mjumbe wa kamati kuu  ya Chama Cha Mapinduzi Ndg:Sadifa Juma khamisi akizungumza katika Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaam
 Kaimu katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi shaka Hamdu Shaka akizungumza katika Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaam

washiriki wa mafunzo elekezi wakifuatilia mafunzo
Mshiriki Katibu wa umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa kirimanjaro ndg; abdulrahim hamid akiuliza swali wakati wa Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaa.(PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)
FAINALI ZA WATOTO WA COMPASSION MWANZA ZAFANA

FAINALI ZA WATOTO WA COMPASSION MWANZA ZAFANA

August 27, 2017
Fainali za mashindano ya watoto kutoka Vituo vya Huduma ya Mtoto (Compassion) Kanda ya Mwanza zimefana baada ya kufikia tamati hii leo jumamosi Agosti 26,2017 kwenye uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. Mashindano hayo yalianza tangu Mei 20 mwaka huu kwa kuhusisha michezo mbalimbali ikiwemo riadha, mpira wa miguu na mpia wa pete kwa lengo la kuibua na kuendeleza vipaji. Katika mchezo wa mpira wa miguu kwa wachezaji wenye umri kati ya miaka 14 hadi 18, timu ya Anglikana Igoma imeibuka bingwa baada ya kuilaza timu ya Moraviani Kigoto kwa bao 3-1 huku mshindi wa tatu ikiwa ni timu ya PAGT Mabatini iliyoilaza timu ya AICT Bujora kwa mikwaju ya penati 3-1 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika kipindi cha dakika 90. Bingwa kwa upande wa watoto wenye umri kati ya miaka minane hadi 12 ikiwa ni timu ya EAGT Buzuruga iliyoicharaza pia timu ya AICT Buhongwa kwa bao 3-1. Katika mpira wa pete timu ya wasichana wenye umri kati ya miaka 14 hadi 18 ya Anglikana Igoma imeilaza timu ya TAG Nyakato kwa magoli 47-41 na hivyo kuibuka bingwa huku timu ya Moraviani Kigoto ikiibuka mshindi wa tatu baada ya kuilaza timu ya FPCT Pasiansi kwa mabao 62-25. Nayo timu ya pete ya wasichana wenye umri kati ya miaka minane hadi 12 timu ya AICT Buhongwa imeibuka bingwa kwa mabao 14-11 dhidi ya timu yaEAGT Buzuruga. Katika fainali hizo, mgeni rasmi alikuwa Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Ilemela, Sarah Nthangu ambaye amekabidhi zawadi za vikombe na jezi kwa timu zilizoshinda pamoja na washindi wengine kwa upande wa mchezo wa riadha.
Tazama video hapo chini
[embed]https://youtu.be/jevKBgfN9WA[/embed] [caption id="attachment_28152" align="alignleft" width="620"] Nahodha wa timu ya Anglikana Igoma akipokea kombe baada ya timu hiyo kuibuka mshindi kwenye mashindano hayo[/caption] [caption id="attachment_28153" align="alignleft" width="620"] Mgeni rasmi akimkabidhi jezi mshindi wa kukata upepo (riadha)[/caption] [caption id="attachment_28154" align="alignleft" width="620"] Mmoja wa washindi wa riadha akipokea zawadi[/caption] [caption id="attachment_28155" align="alignleft" width="620"] Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Ilemela, Sarah Nthangu ambaye alikuwa mgeni rasmi akizungumza baada ya michuano hiyo[/caption] [caption id="attachment_28156" align="alignleft" width="620"] Berekia Erasto kutoka FPCT Pasiansi akisoma risala kwa mgeni rasmi[/caption] [caption id="attachment_28157" align="alignleft" width="620"] Wachezaji wa Anglikana Igoma (kushoto), Moraviani Kigoto (kulia) pamoja na waamuzi[/caption]       BMG Habari, Pamoja Daima!

TUNAISHUKURU SERIKALI YA CUBA KWA KUTAMBUA MASHUJAA WA AFRIKA-MAJALIWA

August 27, 2017
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameishukuru Serikali ya Cuba kwa kutambua na kuthamini mchango mkubwa uliotolewa na mashujaa wa ukombozi wa Bara la Afrika, akiwemo Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kwa kuwajengea mnara wa kumbukumbu.

Mnara huo umejengwa katika Manispaa ya Playa jijini Havana kwenye eneo maalumu la makumbusho ya mashujaa hao walioshiriki katika ukombozi wa Afrika, ambapo zimewekwa sanamu zao pamoja na maelezo mafupi ya historia zao na nchi wanazotoka.

Waziri Mkuu alifanya ziara katika eneo hilo jana (Ijumaa, Agosti 25, 2017) na  kuweka shada la maua katika mnara huo uliozungukwa na sanamu za mashajuaa wa Bara la Afrika na kuoneshwa sehemu itakayowekwa sanamu ya Mwl. Nyerere.

Akiwa katika eneo hilo, Waziri Mkuu aliishukuru Serikali ya Cuba kwa kujenga makumbusho ya mashujaa hao na kwamba Serikali ya Tanzania itashirikiana na Cuba kuhakikisha kuwa sanamu ya Mwl. Nyerere inawekwa katika sehemu iliyotengwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Instuto Cubano De Amistad Con El Pueblo (Taasisi ya Ushirikiano wa Cuba na Nchi Marafiki), Bw. Jose’ Prieto Cintado alisema mnara huo umejengwa kwa lengo la kutambua thamani na umuhimu wa viongozi hao.

Mkurugenzi huyo alisema Serikali ya Cuba inathamini mchango mkubwa uliotolewa na mashujaa hao katika vita ya ukombozi wa Bara la Afrika, ambapo iliamua kujenga mnara wa kumbukumbu katika nchi yao.

Alisema wananchi wa Cuba pamoja na watu kutoka mataifa mbalimbali ndani na nje ya Bara la Afrika wanakwenda katika eneo hilo la makumbusho na kujifunza historia za viongozi hao. Pia eneo hilo linatumiwa na watafiti wa masuala ya kihistoria.

Mashujaa ambao tayari sanamu zao zimekwishawekwa kwenye eneo la kuzunguka mnara huo ni pamoja na Jomo Kenyatta (Rais wa kwanza wa Kenya), Modibo Keita (Rais wa Mali), Amilcar Cabral (Rais wa kwanza wa Guinea Bissau).

Wengine ni Dkt. Kwame Nkrumah (Rais wa kwanza Ghana), Oliver Thambo (Kiongozi Mwandamizi wa Chama cha Ukombozi cha ANC cha Afrika Kusini), Eduardo Chivambo Mondlane (Kiongozi wa ukombozi nchini Msumbuji).

Wengine ni Samora Moises Machel (Rais wa kwanza wa Msumbuji), Sekou Toure (Rais wa kwanza wa Senegal), Seretse Khama (Rais wa kwanza wa Botswana), Alhaji Aboubakar Tafawa Balewa na Obafemi Jeremiah Awolowo (Mawaziri Wakuu wa zamani wa Nigeria) na Chifu Jeremia Azikiwe (Rais wa zamani wa Nigeria) .
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. kushoto , akiwa na mwenyeji wake kulia ambaye ni Mkurugenzi wa Maswala ya Africa Nnchini Cuba .Balozi Jose Prieta Cintado .August 25/2017 wakiangalia Sanamu ya aliyekuwa Raisi wa Msumbiji Hayati Samora Masheli ambayo ipo katika Makumbusho ya Mashujaa wa Africa yaliopo Havana Cuba Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu .
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa .kulia pamoja na Mama Mary Majaliwa ,kushoto pamoja na mwenyeji wao katikati ambaye ni Mkurugenzi wa Maswala ya Africa Nnchini Cuba .Balozi Jose Prieta Cintado .wakiweka Shada la Maua August 25/2017 katika Makumbusho ya Mashujaa wa Africa yaliyopo Havana Cuba .Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu