March 27, 2014

Timu ya uendeshaji wa huduma za afya wilayani Korogwe, mkoani Tanga

Meneja wa Bima ya Afya – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu (kushoto) akitoa maelezo ya utangulizi wakati wa ufunguzi wa kikao cha Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri (CHMT) kikijadili mchakato wa kubadirisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Kikao hicho cha kwanza kilifanyika jana Machi 25, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga. Pembeni ni mgeni rasmi aliyekaribishwa kufungua kikao hicho, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Lewis Kalinjuna (katikati) na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji Korogwe, Jerry Mwakanyamale (kulia).
 Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, Jerry Mwakanyamale (Kulia) akiongea wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Lewis Kalinjuna (Katikati) katika ufunguzi wa kikao cha Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri (CHMT) kikijadili mchakato wa kubadirisha sheria ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kwenda katika Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA). Kikao hicho cha kwanza kilifanyika leo Machi 25, 2014 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Tanga. Pembeni ni Meneja wa Bima ya Afya – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu (kushoto).
March 27, 2014

NSSF MEDIA CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI MACHI 29

Meneja Kiongozi Idara ya Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume akizungumza wakati swa hafla ya kukabidhi vifaa kwa timu zinazoshiriki mashindano ya NSSF Media Cup yanayotarajiwa kuanza rasmi Machi 29. 
 Meneja Kiongozi Idara ya Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume akizungumza wakati swa hafla ya kukabidhi vifaa kwa timu zinazoshiriki mashindano ya NSSF Media Cup yanayotarajiwa kuanza rasmi Machi 29.
March 27, 2014

*ZIARA YA KINANA TEMEKE, AKUTANA NA VIKUNDI VYA VICOBA VILIVYOASISIWA NA MTEMVU

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Kigamboni Dk. Faustine Ndungulile, alipowasili kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Temeke kwa ajili ya kuanza ziara katika wilaya hiyo leo ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya siku nne mkoani Dar es Salaam. Wapili ni Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu.
 Kinana akivishwa skavu baada ya kuwasili Ofisi ya CCM Temeke
March 27, 2014

MAELFU WAJITOKEZA KUUGA MWILI WA ALIYEKUWA MKUU WA MKOA WA MARA MAREHEMU JOHN GABRIEL TUPA


 
MWILI WA ALIYEKUWA MKUU WA MKOA WA MARA JOHN GABRIEL TUPA UKITOLEWA NJE YA MAKAZI YAKE
 WAOMBOLEZAJI WAKIWA NYUMBANI KWA ALIYEKUWA MKUU WA MKOA
KAMPUNI YA KITAALII YA TANGANYIKA FILM YAKUSUDIA KUIMARISHA SEKTA YA MICHEZO SIHA

KAMPUNI YA KITAALII YA TANGANYIKA FILM YAKUSUDIA KUIMARISHA SEKTA YA MICHEZO SIHA

March 27, 2014
Na Omary Mlekwa Siha
UONGOZI wa kampuni ya Utalii ya Tanganyika Film tawi la Ndarakwai Wilayani Siha mkoani Kilimanjaro umesema kuwa umekusudia kuimarisha sekta ya michezo kwa lengo la kuwawezesha vijana katika  wilaya hiyo katika harakati za kuimarisha michezo.
 

Meneja wa Kampuni hiyo tawi la Ndarakwai, Thomas Olekuya alisema hayo wakati akizungumza na wachezaji wa timu ya Roseline FC na kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya michezo kwa la  kuimarisha michezo katika kata ya Ndumeti wilayani hapo kwenye kikao kilichofanyika kwenye uwanja wa shule ya  msingi Roseline.