PROF.MKENDA ASISITIZA UWEKEZAJI KATIKA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amekitaka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) kuwekeza kwenye Sayansi na Teknolojia ili kuchangia katika kuinuia uchumi..
Prof. Mkenda ametoa rai hiyo Agosti 7, 2023 wakati akizungumza na Viongozi na Wafanyakazi wa Chuo hicho baada ya kutembelea na kujionea Maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na MUST.
Prof. Mkenda ameeleza kuwa kazi ya Chuo Kikuu ni kuzalisha na kusambaza maarifa, kusaka uelewa wa mambo kupitia tafiti, hivyo amesisitiza suala la uwekezaji ili kukiwezesha Chuo hicho kujipambanua vema katika dhana ya kufanya tafiti na gunduzi za Sayansi na kufundisha masomo katika maeneo hayo.
"Tunahitaji kuwekeza lakini katika eneo hili sababu uwezo wetu wa Teknolojia ni duni, nchi yetu na Afrika kwa ujumla zipo nyuma kwenye maeneo ya Sayansi na Teknolojia. Hivyo tunapaswa kuwekeza zaidi ili tuweze kuinua nchi kuwa na teknolohia na zitakazo chochea uchumi" alisema Prof. Mkenda.
Ameongeza kuwa serikali itaendelea kuwasaidia wataalam na watafiti wanaozalisha maarifa katika sayansi na teknolojia na kuchapisha matokeo ya tafiti hizo katika majarida makubwa duniani, ili kuhamasisha na kuleta ushindani katika nyanja hizo muhimu kwa Maendeleo ya kiuchumi.
Nae Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) Prof. Aloys Mvuma amesema kwa kutambua azma ya serikali katika kuboresha Elimu ya Amali, Chuo kimeanzisha Mitaala katika Elimu ya Ufundi, na sasa ina mitaala minne, inayotarajia kutoa Walimu mahiri wenye utaalam wa Uhandisi kwa ajili ya kufundisha Vyuo vya VETA na vile vya Maendeleo ya Wananchi (FDCs).
Aidha ameishukuru serikali na kuipongeza Wizara kupitia Idara ya Sayansi na Teknolojia kwa kuwezesha wabunifu kupata fedha zinazowasaidia kuboresha bunifu zao katika viwango vya juu.
Awali akitoa taarifa kuhusu shughuli mbalimbali za Chuo hicho Prof. Mvuma ameeleza kwamba MUST inajivunia kulea na kuatamia mawazo ya kibunifu yanayovumbuliwa na Wanafunzi, kwani mpaka sasa wanafunzi wanaomaliza hapo wameanzisha kampuni 19 ambazo zimeweza kutoa ajira kwa vijana.
Pia amebainisha kwamba "Moja ya mafanikio makubwa ni Ubunifu na utengenezaji wa mita za maji za kidijitali, zaidi ya mita 38 zimefungwa sehemu mbalimbali kwa majaribio na matokeo yake ni mazuri" alisema Prof. Mvuma.
CRDB yainyamazisha NMB tamasha la Simba Day
WENZA WA VIONGOZI WAZINDUA HUDUMA ZA TAULO ZA KIKE MASHULENI
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akikata utepe kuzindua mradi wa ukarabati wa vyoo vya wasichana na uwekaji wa taulo za kike katika Shule ya Msingi Mtoni wilayani Temeke.
Wenza wa viongozi wakiongozwa na Mama Tunu Pinda (wa kwanza kushoto) na Mama Mary Majaliwa (wa tatu kutoka kushoto mstari wa mbele).
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Mobhare Matinyi, akimshukuru Mama Celina Retala, Afisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha HQ Psds cha taulo za kike kilichopo wilayani Temeke.
Na Khadija Kalili
ASASI ya wenza wa Viiongozi nchini iitwayo Ladies of New Millenium, leo Agosti 7, 2023, imezindua mradi wa choo kwa ajili ya kusaidia watoto wa kike ili waweze kujisitiri na kupata huduma zote wanazozihitaji wakiwa kwenye hedhi.
Uzinduzi huo umefanywa na mlezi wa asasi hiyo, Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa, umefanyika katika Shule ya Msingi Mtoni, Wilayani Temeke, na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mheshimiwa Mobhare Matinyi.
Mheshimiwa Matinyi ametoa shukrani za dhati kwa taasisi hiyo kwa kukikarabati choo cha watoto wa kike na kuwezesha kupata huduma hiyo muhimu.
Mheshimiwa Matinyi amewashukuru pia wadau mbalimbali akiwemo Bi Celina Godfrey Retala, Afisa Mtendaji Mkuu wa HQ Pads kwa kuchangia katoni 100 za taulo za kike kwa ajili ya watoto kujihifadhi wakati wa hedhi.
DC Matinyi ametoa wito kwa watu na wadau wengine kuunga mkono juhudi hizi ili kumuwezesha mtoto wa kike kupata elimu bora bila usumbufu na kuleta mafanikio hapo baadaye kwa jamii.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, ndugu Victor Kangati, ameipongeza asasi hiyo kwa kuleta mradi huo kwani ni miongoni mwa mbinu kubwa zinazosaidia kupunguza utoro kwa watoto wa kike.
Taasisi hiyo yenye lengo la kuwawezesha vijana na watoto kupitia elimu yenye ufanisi na ujumuishwaji katika ngazi zote za maamuzi, imeendesha hafla hiyo na kuhudhuriwa na wake wa viongozi akiwemo mlezi wa taasisi, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa, Mwenyekiti wa taasisi Mama Tunu Pinda na wenza wengine wa viongozi wakiwemo Mama Zakhia Bilal, Mama Asha Bilal, Mama Asina Kawawa na Mama Asha Balozi na Mama Mwantumu Mahiza.
Wadau wa maendeleo Aga Khan Foundation, HQ Pads, na Tosh Cargo .
WASIMAIZI WA UCHAGUZI WATAKIWAKUTEKELEZA MAJUKUMU KWA UFANISI
CCM TANGA YATOA MAELEKEZO KWA MKUU WA WILAYA YA KOROGWE MWEGELO
NA MASHAKA MHANDO, Korogwe
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Tanga, kimetoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya Korogwe Jokate Mwegelo kupitia Katibu Tawala wake (DAS) Mwanaid Rajabu, wahakikishe vituo vya afya vya Kerenge na Mnyuzi vinamalizika haraka ili vianze kutoa matibabu kwa wananchi.
Akizungumza katika siku yake ya kwanza katika mwendelezo wa ziara zake kukagua uhai wa chama na utekelezaji wa ilani ya chama, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajabu Abdallah ambaye alitoa maelekezo hayo baada ya kutofurahishwa na kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Aidha aliiomba Ofisi hiyo ya DC kufuatilia kwa makini taarifa za kibank ili kuweza kujiridhisha na matuminzi ya fedha za miradi hiyo baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Korogwe Vijijini kueleza kwamba kipo kiasi cha fedha kimebaki ingawa mradi huo umesimama kwa sasa.
Rajabu alisema Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa vituo hivyo vya afya kwa lengo la kuwasaidia wananchi wanaoteseka kwa kutembea umbali mrefu zaidi ya km 40 kufuata huduma Korogwe Mjini jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya wananchi hao.
"Mna DC makini sana katika wilaya hii na naomba nitoe maelekezo yafuatayo, DAS hakikasha unamwambia DC mfuatilie majengo haya na yaishe mapema wananchi wetu wapate huduma, lakini pia fatilieni fedha kama ipo kweli kwenye akaunti" alisema na kuongeza,
"Haiwezekani Rais Dkt Samia Suluhu Hassan atafute fedha kwa kuzunguka huko na huko halafu watu washindwe kuzisimamia, watumishi mliopewa dhamana fanyeni kazi kwa weledi wenu na maelekezo haya tunayoyatoa kama hamtayafanyia kazi mtajua chama hiki ni kikubwa kuliko mtu yeyote yule,".
Alisema kinachofanywa na watendaji na Viongozi Wilayani hapo kwa kutokukamilisha ujenzi wa vituo hivyo ni kumchonganisha Rais, Mbunge na hata Diwani dhidi ya wananchi na kuonekana Serikali haiwajali wananchi wake kumbe Korogwe wameletewa fedha nyingi katika miradi mbalimbali lakini watendaji wanashindwa kuzisimamia.
Alisema vipo vituo vya afya vimejengwa kwa gharama hizo hizo za Shs Mil 400 karibu Mkoa mzima wa Tanga na majengo yote yamejengwa tofauti na Korogwe ambapo wamepokea shs Mil 500 kwa kituo kimoja na havijakamilika hali inayoonekana kuna matuminzi mabaya ya fedha.
Aidha alisema pesa nyingi zimeelekezwa Wilayani Korogwe kwa ajili ya miradi ya vituo vya afya jambo la kusikitisha vituo hivyo havijakamilika na ni dalili za wazi zinazoonyesha Wilaya ya korogwe imeonyesha kiasi gani kuna uzembe wa usimamiaji wa miradi ya maendeleo.
Rajabu aliwataka viongozi waliopewa dhama na Rais wafanye kazi kwa weledi na watambue kufanya hivyo kutasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa kama sio kumaliza kero za wananchi hasa katika miradi ya kimaendeleo.
Kwa upande wake Mbunge wa Korogwe Vijijini Timotheo Mzava alisema kwanza wanamshukuru Mh, Rais kwa kutoa Bil 1 kwa ajili ya ujenzi wa vituo viwili vya afya ambapo Kituo cha afya cha Kerenge Shs Mil 500 na kile cha Mnyuzi Shs Mil 500 na kushukuru maelekezo ya Mwenyekiti huyo kwamba yatasaidia wananchi.
Aidha alisema changamoto ya utekekezaji wa miradi hiyo ni ucheleweshwaji na hata majengo yaliyokuwatayari hayakuanza kutumika ingawa uhitaji wa huduma hiyo ni mkubwa kwa wananchi wa maeneo hayo.
Alitumia fursa hiyo kuiomba Serikali ijitoe kwa nguvu zote ili utekelezaji wa vituo hivyo vya afya vikamilike kwa wakati ili kuwaondolea adha wananchi hao kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya.
Akitoa taarifa fupi ya mradi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Korogwe Halfan Magani alisema miradi hiyo imechelewa kutokana na taratibu za kimanunuzi kupitia mfumo wa force Account kupitia kamati ambazo zipo Kijijini.
Alisema mbali ya changamoto hiyo ya mfumo wa kimanunuzi pia mkandarasi alishindwa kuendelea na mradi na Halmashauri ipo kwenye mchakato wa kumtafuta mkandarasi mwengine ili aweze kumalia sehemu iliyobaki.
Mwisho