Usaili wa Maisha Plus Mtwara, funga kazi

June 06, 2016
Ni asubuhi tulivu katika fukwe za bahari ya hindi kusini mwa Tanzania ambapo vijana wengi wamejitokeza kufanya usaili wa mashindano ya Maisha Plus East Africa 2016. Wapo wanaoonekana kujiamini na wengine wamejawa uoga. "Ni siku niliyoisubiri kwa hamu sana" anasema Faustine Komba miongoni mwa washiriki kutoka Mtwara.
678A0009
Safari ya msimu wa tano wa mashindano ya Maisha Plus imeanza rasmi kwa kuanza na usaili uliofanyika katika hotel ya NAF Beach iliyoko Mtwara. Washiriki kutoka mikoa ya jirani nao pia walijitokeza. "Maisha Plus kwangu ni ndoto ya muda mrefu sana, niliposikia mnakuja Mtwara nikasema piga ua lazima nishiriki" Anasema Ismail Likando aliyesafiri kutoka Lindi.
678A0022
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9916
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9925
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
Maswali mengi yalilenga kupima uelewa wa vijana kuhusu mambo mbalimbali ya kijamii ikiwemo mtazamo wao juu ya mwenendo wa kiuchumi. Mengine yalilenga kuwachanganya tu.
678A9961
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9971
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
Mshiriki Grace Pemba anaelezea changamoto mbalimbali alizokutana nazo kutokana na kuolewa akiwa na umri mdogo, anasema hadi sasa ana watoto wawili ambao wanaishi na baba yao. Alipoulizwa maswali zaidi Grace alijawa na simanzi na kujikuta akitoa machozi, "Nimelia kwa sababu mmenikumbusha nyuma nilikotokea" anasema Grace mfanyakazi wa Saloon kutoka mkoani Mtwara.
A video posted by Maisha Plus (@maishaplus2016) on Jun 4, 2016 at 6:47am PDT
678A9980
Mshiriki Grace Pemba akijifuta machozi.
Wakati usaili ukiendelea hali ya kujaa kwa maji baharini ilitokea na kulazimisha timu ya Maisha Plus kubadili utaratibu wa awali wa upigaji picha.
678A0075
Waandaaji wa mashindano ya Maisha Plus wakibadili utaratibu wa awali wa kupiga picha baada ya maji kujaa.
678A0046
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0056
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0281
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0279
Muhitimu wa shahada ya kilimo William Mbaga alibanwa kutoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ikiwemo faida za kilimo cha 'greenhouse' pamoja na namna ambavyo maziwa ya mtindi yanapatikana. William alijieleza kwa ujasiri.
678A0157
William Mbaga akiondoka baada ya kufanya usaili.
Washiriki wenye fani na ujuzi mbalimbali walijitokeza wakiwemo madereva bodaboda, mafundi, waigizaji, waimbaji, wasusi n.k
678A0223
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0083
Waigizaji pia walikuwemo katika usaili wa #MaishaPlusMtwara
678A0167
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0113
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0308
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0328
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.

678A0336
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
Mashindano ya Maisha Plus kwa mwaka huu yanatarajia kuchukua washiriki 30 kutoka nchi za Burundi, Rwanda, Kenya, Tanzania na Uganda ambapo mshindi atajishindia ufadhili wa wazo la biashara lenye thamani ya Tzshs. Milioni 30.
"Mwaka huu washiriki wajipange sana. Maandalizi yaliyofanywa kufanikisha msimu huu hayajawahi kutokea katika historia ya Maisha Plus. Ni kama tunaanza moja" Alisema Masoud Kipanya, miongoni mwa majaji na waanzilishi wa mashindano haya.
678A0145
"Tumewekeza katika teknolojia ya kisasa ili kupata picha za matukio yenye uhalisia zaidi. Watazamaji wategemee burudani safi isiyomithirika kupitia Azam Two." Alisema David Sevuri, miongoni mwa waanzilishi wa Maisha Plus.
Taarifa mbalimbali kuhusu mashindano haya zinapatikana kupitia tovuti rasmi ya www.maishaplus.tv
photo Krantz Mwantepele Founder & CEO , KONCEPT Phone: +255-7125791 02 /+255-767392840 Email: krantzcharles@gmail.com Blog: www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.com Website;www.koncept.co.tz

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI TANZANIA NA AKAUNTI YA MALAIKA LEO

June 06, 2016


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Malaika katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam leo Juni 06,2016.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na watoto waliokua wakiishi katika mazingira magumu wakati uzinduzi wa Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Malaika vilivyozinduliwa leo Juni 06,2016 katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea zawadi ya CD yenye vipindi mbalimbali kutoka kwa watoto waliokua wakiishi katika mazingira magumu kwenye uzinduzi wa Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Malaika vilivyozinduliwa leo Juni 06,2016 katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikabidhi cheti kwa mwakilishi wa kampuni ya simu za mikononi Zantel kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo kuweza kufanikisha uzinduzi wa Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Malaika vilivyozinduliwa leo Juni 06, 2016 katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akikabidhi cheti kwa mwakilishi Mkaazi wa UN Women Bibi Anna Pollins kwa kutambua mchango uliotolewa na Shirika hilo katika kuwezesha kufanikisha uzinduzi wa Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Malaika vilivyozinduliwa leo Juni 06, 2016 katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akibonyeza Laptop kuzindua Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Malaika katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam leo Juni 06,2016. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Malaika katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam leo Juni 06,2016. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na kutoka katika Tasisi mbalimbali walioshiriki katika uzinduzi wa Jukwa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Tanzania na Akaunti ya Mlaika vilivyozinduliwa leo Juni 06,2016 katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam. (Picha na OMR)

RAIS DKT MAGUFULI ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA RAIS WA SAHARAWI, AKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA UBELGIJI, BALOZI WA MAREKANI NA KUAGANA NA BALOZI WA ITALY

June 06, 2016


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa mambo ya Nje wa Ubelgiji Mhe. Didier Reynders aliyemtembelea Ikulu Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italy nchini Mhe. Luigi Scotto aliyemtembelea na kumuaga baada ya kumaliza muda wale wa kazi Ikulu Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitoa pole kwa Balozi wa Jamhuri ya Kiarabu ya kidemokrasia ya Saharawi nchini Mhe. Brahim Buseif alipokwenda ubalozini hapo kutoa pole na kusaini Kitabu cha Maombolezo ya kifo cha Rais wa Saharawi Mhe. Mohamed Abdelaziz Mikocheni jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Mhe. Mark Childress aliyemtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo.PICHA NA IKULU.

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI, (WCF), WAPONGEZWA NA SSRA KWA KUWAFIKIA WADAU MUHIMU

June 06, 2016


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Irene Isaka akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina ya siku tano kwa madaktari wanaotoka mikoa ya kanda ya ziwa kuhusu ajali na magonjwa yanayotokana na kazi Jijini Mwanza. Bi. Isaka alisisitiza umuhimu wa WCF na madaktari kufanya kazi pamoja ili waweze kulipa fidia stahiki kwa wafanyakazi wote kutoka sekta Binafsi na Umma. Wengine pichani kutoka kushoto ni Afisa Utumishi Mkuu, Mkoa wa Mwanza, Bw. Salvatory KyaKyarwenda, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko huo, Bw. Emmanuel Humba.

NA K-VIS MEDIA, MWANZA
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bi Irene Isaka ameipongeza Bodi ya Wadhamini na Mkuurgenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), kwa kuweza kuwafikia wadau wake muhimu kwanza kabla ya kuanza kutoa Fidia kwa Wafanyakazi. 

Bi Isaka aliyasema hayo leo Juni 6, 2016 wakati akifungua mafunzo ya siku tano kwa madaktari 124 kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa kwenye ukumbi wa jengo la PPF Plaza jijini Mwanza.Aidha, amesema kuwa sasa hivi wafanyakazi wasifanye kazi kwa wasiwasi kwani kuna chombo maalumu ambacho ndiyo kinga na msaada wao endapo watapatwa na majanga katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Pia Bi. Isaka ametoa wito kwa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), na madaktari kote nchini kufanya kazi pamoja ili waweze kulipa fidia stahiki kwa wafanyakazi wote kutoka sekta Binafsi na Umma.

Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, ni taasisi ya Serikali iliyoko Ofisi ya Waziri Mkuu, na ulianzishwa kwa sheria ya Fidia Kwa Wafanyakazi namba 20 ya mwaka 2008. Lengo la kuanzishwa kwake ni kuhakikisha Mfanyakazi anapata fidia stahiki kutokana na kuumia kazini au magonjwa yatokanayo na kazi na kwa wanafamilia kupokea fidia kwa niaba ya mwenza wao aliyefariki akiwa kazini.

Mafao yatolewayo na Mfuko huo ambayo kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Masha Mshomba ni pamoja na Fao la matibabu, fidia ya ulemavu wa muda, fidia ya ulemavu wa kudumu, Fidia ya huduma ya marekebisho (Rehabilitation services), Fedha za uangalizi wa mara zote, (Constant attendance care grant), Fedha za mazishi, na fidia kwa wategemezi wa mfanyakazi aliyefariki akiwa kazini au kutokana na maradhi yaliyosababishwa na kazi aliyokuwa akifanya. “Mfuko utaanza kutoa mafao ya kwanza kabisa tangu uanzishwe kuanzia mwaka wa fedha unaoanza Julai, 2016/2017.” Alisema Mkurugenzi Mkuu, Bw. Masha Mshomba.Mafunzo hayo yanatolewa kwa ushirikiano wa WCF na Shirika la Kazi Duniani, ILO. 
Mwenyeketi wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Emmanuel Humba akitoa hotuba yake.
Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, akizungumza mwanzoni mwa mafunzo hayo.
Baadhi ya Madaktari, wakufunzi kutoka ILO wakifuatilia maelezo ya utangulizi
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo
Mkurugenzi Mkuu, Bw. Masha Mshomba, akifafanua baadhi ya mambo kwa waandishi wa habari
Picha ya pamoja
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii, (SSRA), Irene Isaka (kulia), akisalimiana na mtaalamu wa ajali na magonjwa yanayosababishwa na kazi kutoka Shirika la Kazi Duniani, (ILO), Dkt. Jacque Palletier

SERIKALI YA JAPAN YATOA MSAADA WA MAGARI TISA KWA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

June 06, 2016

Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Haji Janabi (katikati) na Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshiba (kushoto) wakikata utepe ikiwa ishara ya makabidhiano ya magari matano yaliyotolewa na Serikali ya Japan kwa ajili ya kusaidia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini. Magari hayo yamekabidhiwa nje ya Jengo la Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam. Kulia anayepiga makofi ni Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali, Thobias Andengenye.
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Haji Janabi akitoa hotuba fupi kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, kuishukuru Serikali ya Japan kwa kuisadia wizara yake kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji magari tisa kwa ajili ya kazi ya kuzima moto na uokoaji nchini. Wa pili kushoto ni Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshiba akifuatiwa na Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali, Thobias Andengenye. Wa pili kulia ni Kamishna wa Operesheni wa Jeshi hilo, Rogatus Kipali na Kamishna Msaidizi, Fikiri Salla. Tukio hilo lilifanyika nje ya Jengo la Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali, Thobias Andengenye akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Haji Janabi ili aweze kuzungumza na baadaye kukabidhiwa magari matano ya kuzima moto na uokoaji. Magari hayo yametolewa na Serikali ya Japan kupitia balozi wake nchini, Masaharu Yoshiba. Tukio hilo la makabidhiano lilifanyika nje ya Jengo la Wizara hiyo.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lilian Mapfa (kushoto) akimkabidhi zawadi Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshiba, mara baada ya Balozi huyo kuikabidhi Wizara hiyo msaada wa magari tisa ya kuzima moto na uokoaji. Tukio la makabidhiano ya magari hayo lilifanyika nje ya Jengo la Wizara, jijini Dar es Salaam leo.
Wakuu wa Idara ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na wageni waalikwa, wakimsikiliza Mkuu wa Jeshi hilo, Thobias Andengenye (hayupo pichani) wakati alipokuwa anatoa hotuba yake kabla ya Serikali ya Japan kutoa msaada wa magari tisa ya kuzima moto na uokoaji. Tukio hilo lilifanyika nje ya Jengo la Wizara, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake, Andengenye aliishukuru Serikali ya Japan kwa msaada mkubwa ambao wameutoa kwa Jeshi lake.
Sehemu ya magari tisa yaliyokabidhiwa na Balozi wa Japan, Masaharu Yoshiba kwa niaba ya Serikali yake yakiwa nje ya Jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Magari hayo yaliyotolewa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji yalipokelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, wa Wizara hiyo, Haji Janabi, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.