Benki Ya CRDB yaendesha Semina Kuwajengea Uwezo Waandishi Wa Habari Kuandaa Taarifa zitakazochochea Ujumuishi Wa Kifedha nchini

February 19, 2024

 

Dar es Salaam 19 February 2024 – Katika jitihada za kuendeleza sekta ya habari nchini, Benki ya CRDB imeendesha semina maalum kwa wadau wa sekta ya habari nchini na uchumi “CRDB Bank Media Day” iliyofanyika katika Makao Makuu ya benki hiyo yaliyopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Akifungua semina hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema “CRDB Bank Media Day” ya mwaka huu imejikita katika kuangazia ripoti ya Finscope 2023 na namna gani vyombo vya habari vinaweza kuchochea ujumuishi nchini.
“Ripoti ya Finscope ya 2023 inaonyesha ujumuishi wa kibenki upande wa huduma za benki ni 22% tu pamoja na jitihada na ubunifu mkubwa katika bidhaa. Hii inaonyesha kuna ombwe kubwa la elimu ya fedha, hivyo leo tumepata kujadili ninamna gani wenzetu wa sekta ya Habari wataweza kusaidia kutoa taarifa na huduma za fedha,” alisema Nsekela.

Katika semina hiyo waandishi wa habari walipata fursa ya kupata mafunzo ya namna ya bora ya kaandaa na kutoa mafunzo ya taarifa za biashara, fedha na uchumi. Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amesema mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kusaidia kujenga waandishi mahiri nchini.
Akizungumza katika semina hiyo, Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuandaa semina hiyo iliyowaleta wadau wa sekta ya habari kujadili namna ya kuongeza mchango wake katika maendeleo hususani katika kuongeza ujumuishi wa kifedha nchini. Matinyi amewahakikishia wadau wa sekta hiyo kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri yatakayosaidia kuboresha sekta ya habari.

Mada mbalimbali zimewasilishwa katika semina hiyo ikiwamo ‘Jukumu la Vyombo vya Habari katika kuchochea Ujumuishi wa Kifedha’ iliyowasilishwa na Mhariri Mstaafu wa Nationa Media Group Kenya, Charles Onyango Obbo, ‘Elimu ya Fedha kupitia Mitandao ya Jamii’ iliyowasilishwa na Fayness Sichwale amshauri wa masuala binafsi ya fedha na Mwanzilishi wa Personal Finance Hub, na Usomaji na Uwasilishaji wa Taarifa za Fedha’ iliyowasilishwa na Dkt. Ndalahwa Masanja, Mhadhiri Mwandamizi Chuo Kikuu cha ESAMI.
Katika Semina hiyo iliyohudhuriwa na waandishi na wahariri kutoka vyombo mbali nchini, Benki ya CRDB pia imezindua shindano maalum la kutafuta waandishi wahabari wachanga wa habari za biashara, fedha, na uchumi. Shindano hilo ambalo litaendeshwa kwa muda wa miezi miwili hadi Aprili 12 2024, litatoa washindi watatu ambao watajishindia zawadi ya Sh. Milioni 1 na nafasi ya kufanya kazi na Benki ya CRDB.
Aidha, katika hafla hiyo Benki ya CRDB imetoa tuzo za kutambua mchango wa waandishi wa habari wawili nguli katika sekta ya habari nchini. Waliokabidhiwa tuzo hizo ni Edda Sanga mwandishi mstaafu wa Shirika la Habari la Tanzania (TBC) na Mwenyekiti wa Umoja wa Waandishi wa Habri Wanawake (TAMWA), na Ndimara Tegambwage mwandishi wa zamani wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, na moja ya waanzilishi wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA). 
Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Mobhare Matinyi, akimkaidhi Tuzo ya Heshima kutoka Benki ya CRDB kwa Mwanahabari wa Habari Mkongwe nchini, Mzee Ndimara Tegambwage , ikiwa sehemu ya kutambua mchango wake katika tasnia ya Habari hapa nchini, wakati wa semina maalum kwa wadau wa sekta ya Habari za uchumi nchini iliyoandaliwa na Benki va CRDB na kutamuliwa kama "CRDB Bank Media Day" ilivofanyika katika Makao Makuu ya benki hive yalivopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaii wa Benki va CRDB, Abdulmajid Nsekela, Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki va CRDB Bruce Mwile pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki va CRDB, Tully Esther Mwambapa.
 Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Mobhare Matinyi, akimkaidhi Tuzo ya Heshima kutoka Benki ya CRDB kwa Mwanahabari wa Habari Mkongwe nchini Mama Eda Sanga, ikiwa sehemu ya kutambua mchango wake katika tasnia ya Habari hapa nchini, wakati wa semina maalum kwa wadau wa sekta ya Habari za uchumi nchini iliyoandaliwa na Benki va CRDB na kutamuliwa kama "CRDB Bank Media Day" ilivofanyika katika Makao Makuu ya benki hive yalivopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaii wa Benki va CRDB, Abdulmajid Nsekela, Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki va CRDB Bruce Mwile pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki va CRDB, Tully Esther Mwambapa. 

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki va CRDB, Tully Esther Mwambapa akizunguma katika semina maalum kwa wadau wa sekta ya Habari za uchumi nchini iliyoandaliwa na Benki va CRDB na kutamuliwa kama "CRDB Bank Media Day" ilivofanyika katika Makao Makuu ya benki hive yalivopo barabara ya Ali Hassan Mwinyi, jijini Dar es salaam.









 



SEMA NA TANGA WAKOSHWA NA UWEKEZAJI KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA-BOMBO WAHAIDI KUWA MABALOZI

February 19, 2024

 


Na Mwandishi Wetu, TANGA

Kundi la Sema na Tanga leo wamefanya ziara ya kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo huku wakifurahishwa na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uwekezaji na kuimarisha huduma za Afya hapa nchini na kuhaidi kuwa mabalozi wa kuisemea vizuri.

Wametembelea na wamejionea uwekezaji mkubwa uliofanyika katika kitengo cha dharura (EMD), kitengo cha uangalizi maalumu (ICU), Kitendo cha radiolojia (CT-scan), Kitengo cha uangalizi maalumu kwa watoto wachanga (NICU), Wodi ya upasuaji, Kitengo cha kusafisha figo (Dialysis Unit)

Akizungumza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt. Japhet Simeo alisema kwamba kundi hilo ambalo ni wadau wa maendeleo walialikwa ili kuweza kuona huduma nzuri ambazo zinatolewa katika Hospitali hiyo na wamethibitisha kuwa uwekezaji ni mkubwa sana na wengi wao walikuwa na picha tofauti na waliyokuwa nayo awali na hawakuamini kama Hospitali hiyo ingeweza kuwa na vifaa kama hivyo na watu wanatibiwa na kupona.

“Ambao waliokuwa na hisia za zamani kwa sasa zitafutika maana wengine wanaamini yale mambo ya miaka 10 iliyopita bado, kwa hiyo Sema na Tanga wanaenda kufuta hayo mambo kwenye fikra za wananchi na tunaamini mtakuwa mabalozi wazuri wa kulisemea hili”Alisema

Hata hivyo alisema hivi sasa wanaendelea kuboresha huduma huku akiishukuru ofisi ya Mkuu wa Mkoa ilivyosimamia kuhakikisha rasimali zinazoletwa zinasimamiwa kikamilifu akianza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba na Katibu Tawala Pili Mnyema namna wanavyompa ushirikiano mkubwa na hivyo kufanya kazi kwa kujiamini

Awali akizungumza Mwenyekiti wa Kundi la Sema na Tanga alisema wana haja ya kuja kukuunga mkono kama wadau wa maendeleo kutembelea kutokana kujionea maboresho ya huduma yaliyosaidia kuondoa makelele yaliyokuwa yakisikika.

Alisema wametembelea wameona maboresho makubwa ,vifaa mbalimbali, nyenzo nzuri za kisasa.“Tuwaheshimu madaktari na wauguzi hapa nchini na tuache kuingiza siasa kwenye mambo ya kitaalamu maana tutakuwa tunawavunja moyo kama kuna mtu atawahujumu sisi tupo tayari kuwasemea na kusimamia na nyie”Alisema

“Tunamshukuru Waziri Ummy kwa kuteletea Mganga Mfawidhi Mpya Dkt Frank Shega na zile kelele zilizokuwepo kwa sasa hazipo zimeondoka ameonyesha waledi mkubwa, tutakutetea kwa kazi yako nzuri unayoifanya bila kupepesa macho”Alisema

QATAR CHARITY YATOA MSAADA TANI 90 KWA WANANCHI WA HANANG

February 19, 2024


div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
Na Mwandishi Wetu.

Ubalozi wa Qatar Tanzania kwa kushirikiana na Tasisi ya Qatar Charity, kwa niaba ya Serikali ya Qatar, imewasilisha misaada muhimu ya kibinadamu kwa waathirika wa Maporomoko ya Udongo yaliyotokea Hanang mkoani Manyara. 

Shehena ya misaada hiyo iliyotolewa leo tarehe 18 Februari 2024 kwa kutumia ndege mbili za mizigo kutoka Qatar inalenga kugusa maisha ya wananchi wa Hanang walioathirika na maafa hayo ambayo madhara yake yalikuwa makubwa. 

Serikali ya Qatar imetoa kwa ukarimu misaada hiyo ya kibinadamu inayojumuisha chakula kikavu katika vifungashio 1,440 (Dry food basket), chakula kilicho tayari kuliwa katika vifungashio 3,024 (Ready to Eat canned food) na vifaa vya usafi wa wanawake jumla 4,200 (women’s dignity kit) na hivyo kufanya jumla ya tani 90 za shehena. 

Naye Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali imepokea kwa moyo wa upendo misaada hiyo itakayoleta faraja kwa Waathirika na kuahidi kufikishwa kwa Walengwa kama ilivyokusudiwa. 

Vilevile Mhe. Nderiananga ameeleza kuwa Serikali inatambua mchango wa wadau wote ikiwemo wananchi, sekta binafsi, asasi za kiraia na kidini, mashirika ya kimataifa na umoja wa mataifa kwa ushiriki wao katika kusaidia wananchi walioathirika na maporomoko ya tope katika wilaya ya Hanang' 

Akipokea Misaada hiyo Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe Queen Cuthbert Sendiga ameishukuru Serikali ya Qatar kupitia Qatar Charity kwa misaada hiyo ya kibinadamu ambayo itakwenda kuwasaidia wananchi wa Hanang kurejea kwenye hali yao ya Kawaida.

Aidha, Mhe Mkuu wa Mkoa amesema kuwa kupatikana kwa Misaada hiyo ni matokeo ya mahusiano mazuri ya nchi ya Tanzania na nchi za jirani ambayo yameimarishwa na serikali ya awamu ya sita Chini Rais  Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ndege ya mizigo iliyosheheni misaada hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Manyara akishuka kwenye ndege hiyo mara baada ya kufanya makabidhiano ya msaada.
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo fupi iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa KIA.