CHUO CHA UONGOZI WA FEDHA KUANZISHA MASOMO YA NGAZI YA CHETI -PEMBA

CHUO CHA UONGOZI WA FEDHA KUANZISHA MASOMO YA NGAZI YA CHETI -PEMBA

August 08, 2015

wat1 
NA RAMADHANI ALI/MAELEZO  
………………………………….. 
CHUO cha Uongozi wa Fedha Zanzibar (ZIFA) kitaanzisha Tawi lake Kisiwani Pemba kuanzia mwaka huu  wa masomo na kitaanza kufundisha  masomo ya   uongozi wa fedha ngazi ya cheti.
Akizungumza na waandishi wa Habari Makao Makauu ya ZIFA Chwaka, Kaimu Mkuu wa Taaluma Dkt. Iddi Salum Haji amesema wameamua kufungua Tawi  Pemba ili kuzipunguzia gharama  familia zenye  kipato cha chini.
Amesema utafiti uliofanywa na Chuo  umegundua  kuna vijana wengi Kisiwani Pemba waliomaliza kidato cha nne na wanazo  sifa za kujiunga na chuo kwa masomo ya cheti  lakini wanashindwa kutokana na familia zao kukosa uwezo wa kuwasomesha.
Ameongeza kuwa chuo kimejipanga  na kukamilisha taratibu zote za kutoa mafunzo hayo  katika Mji wa Wete na wanafikiria kuanzisha Tawi  Mjini Dar es salaam hapo baadae.
Dkt. Iddi  amesema lengo la Chuo hicho ni kujipanua zaidi hasa kufuatia matokeo mazuri ya mitihani ambapo mwaka huu asilimia 98.3 ya wanafunzi   870 waliofanya mitihani kuanzia  ngazi ya cheti mpaka shahada ya kwanza wamefaulu vizuri.
“Wanafunzi waliohitimu fani ya Uhasibu wamepasi asilimia mia,  IT asilimia 97 na  fani ya Ugavi na Ununuzi wamefaulu kwa asilimia 98,” amesema Kaimu Mkuu wa Taaluma.
Amesema mafanikio hayo yamepatikana  kutokana  na wanafunzi kujituma zaidi na walimu  kujitolea  kwa uwezo wao wote na  kuwa  wabunifu  katika kufundisha.
Ameeleza kuwa baadhi ya fani   zinzofundishwa na chuo cha Uongozi wa Fedha  yanaelekeza zaidi  kwa vitendo na yanawasaidia  wahitimu kuweza  kujiajiri wenyewe.
Dkt.  Iddi amewashauri  wazazi kuwa waangalifu  wakati vijana wao wanapotafuta  nafasi za kujiunga na Taasisi za elimu ya juu  na kuwataka wahakikishe wanawapeleka kwenye vyuo vyenye sifa na vilivyosajiliwa na  kutambuliwa na Bodi za elimu ya juu NACTE na  TCU.
“Hivi sasa kumeibuka  msururu wa vyuo vinavyojitangaza vinatoa mafunzo ya Elimu ya juu lakini wanafunzi wanapomaliza na kutafuta ajira ama masomo ya juu inakuwa vigumu kupata kutokana na kuwa havitambuliki,” alisema Dkt. Iddi
Kaimu Mkuu wa Idara ya Masomo ya jumla  ZIFA Maalim Said Mohd amesema chuo hivi sasa kimejipanga kuteremka ndani ya jamii kwa kutoa elimu kwa wajasiriamali  ili waweze  kujiendesha  wenyewe.
“Kwa kuanzia chuo tayari kimeendesha mafunzo ya ujasiriamali  kwa vikundi vya   Wilaya ya Kaskazini A, Wilaya ya Kati  na Wilaya Kusini kwa Unguja na Chake chake na Micheweni  Pemba na lengo ni kumaliza Wilaya zote za Zanzibar,” alisisitiza Maalim Said.
Mmoja wa wanafunzi waliomaliza masomo  mwaka huu Bakar Omar Hamad  ameishauri Wizara ya elimu kufanya mapitio ya Taasisi zinazotoa elimu ya juu nchini ili kuhakikisha  uhalali wa usajili wao,  mitaala inayotumika  inalingana  na masomo na  kuhakikisha walimu  wanazo sifa zinazokubalika.
Amesema wazazi wamekuwa wakiwekeza   fedha nyingi kuwasomesha watoto  wao lakini baadhi  ambao mwamko wa kielimu ni mdogo wanawapeleka vijana wao katika vyuo ambavyo  pamoja  na kupata usajili lakini masomo  yanayotolewa yanakosa ithibati ya kufundishwa.

SIMBA SC YALETA KIPA MBRAZIL ‘HAFUNGIKI’ NA STARIKA ‘MABAO’ DEMBELE WA MALI, MWAKA HUU KAZI IPO LIGI KUU

August 08, 2015


Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
KIPA Mreno mwenye asili ya Brazil, Ricardo Ribeiro de Andrade (pichani) anatarajiwa kutua kesho Dar es Salaam kwa ajili ya kujiunga na Simba SC.
Kaimu Katibu Mkuu wa Simba SC, Collin Frisch ameiambia TANGA RAHA BLOG kwamba mlinda mlango huyo mkongwe wa umri wa miaka 39 atawasili pamoja na mshambuliaji kutoka Mali, Makan Dembele.
Dembele anayetokea JS Kabylie ya Algeria na kipa huyo anayesifika kwa kuokoa hadi michomo ya penalti, watawasili Alfajiri ya kesho.
Aidha, Simba SC leo imempokea mshambuliaji wa Atletico Sport Olympic ya Burundi, Kevin Ndayisenga anayekuja kwa ajili ya majaribio.
Ndayisenga ameletwa ili kuangalia uwezekano wa kuziba pengo la mshambuliaji wa Vital’O ya Burundi pia, Laudit Mavugo, aliyetakiwa na klabu hiyo awali.
Simba SC iliamua kuachana na Mavugo baada ya klabu mbili za nchini humo kupandisha thamani ya mchezaji huyo na kuwa Sh. Milioni 200, badala 110 zilizokubaliwa awali.
Aidha, kuibuka pia kwa mzozo mpya kati ya klabu ya Vital’O FC na Solidarity FC, inayodai kumlea Mavugo, hivyo nayo kudai ina hakimiliki ya mchezaji huyo nako kuliishitua Simba.
Vital’O ikaikoroga zaidi Simba SC baada ya kudai kiwepo kipengele cha wao kupata asilimia 50 kama mchezaji huyo atauzwa na Wekundu hao wa Msimbazi kwenda klabu nyingine.
Mshambuliaji Makan Dembele anatarajiwa kuwasili kesho Simba SC

Pamoja na hayo, Simba SC ilifanikiwa kusajili mchezaji mwingine wa Vital’O, beki wa kushoto na kulia, Emery Nimubona ambaye tayari yupo nchini.
Tayari Simba SC inaye kipa Vincent Angban kutoka Ivory Coast aliyekuja kwa majaribio ambaye amekwishaidakia timu hiyo mechi tatu na kufungwa mabao mawili tu katika mchezo dhidi ya KMKM, Wekundu hao wa Msimbazi wakishinda 3-2. 
Na wakati bado kocha Muingereza, Dylan Kerr hajaamua kuhusu kipa wa zamani wa timu ya vijana ya Chelsea chini ya umri wa miaka 21, Angabn- anakuja Ricardo Ribeiro de Andrade.
Kampuni ya Tigo yafungua Duka jipya la kisasa Sumbawanga Mjini

Kampuni ya Tigo yafungua Duka jipya la kisasa Sumbawanga Mjini

August 08, 2015

X1
Katibu tawala mkoa wa Rukwa,  Bw  Smythies Pangisa (kulia), akikata utepe ikiwa ni ishara rasmi ya  uzinduzi wa duka la Tigo lililopo Sumbawanga mjini, kushoto ni  Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kusini Jackson Kiswaga na katikati ni meneja wa operesheni kwa wateja Tigo kanda ya kusini, Laverty Khana.
X2
Meneja wa operesheni kwa wateja Tigo kanda ya kusini, Laverty Khana(katikati) akitoa maelekezo kwa mgeni rasmi Katibu tawala mkoa wa Rukwa ndugu Smythies Pangisa jinsi watakavyo hudumia wateja, mara  baada ya uzinduzi wa duka la Tigo lililopo mtaa wa Sokomatola ,Sumbawanga mjini.
X3
Wafanyakazi wa duka jipya la Tigo lililopo Sumbawanga mjini wakipozi kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi (mstari wa mbele katikati) ndugu Smythies Pangisa  ambaye ni Katibu tawala mkoa wa Rukwa, muda mfupi baada ya hafla fupi ya uzinduzi wa duka la Tigo Sumbawanga Mjini.
JANET MBENE AKABIDHI VITANDA VAYA KUJIFUNGULIA VYA THAMANI YA MILIONI 30 ILEJE

JANET MBENE AKABIDHI VITANDA VAYA KUJIFUNGULIA VYA THAMANI YA MILIONI 30 ILEJE

August 08, 2015

    5
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mbene akimkabidhi Vitanda vya Kujifungulia Katibu wa CCM wilaya ya Ileje kwa ajili ya Hospitali za wilaya hiyo.
2
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Janet Mbene,akionyesha baadhi ya vifaa vinavyotumika katika hospital ambavyo avimetolewa na Karemjee Foundation kwa ajili ya Hospital ya Ileje.
4
Mganga mkuu wa Wilaya ya ilje, akiangalaia sehemu ya msaada wa vitanda uliotolewa na Janet Mbene.
1
Mafundi wa Hospitala wakiunganisha kitanda cha kujifunguliwa kilicholetwa na Mh Janet Mben kwa ajili ya hospitalai za ieleje.

UTT-PID YASHIRIKI MAONYESHO YA NANE NANE - LINDI

August 08, 2015
Maafisa Masoko wa UTT-PID, Bi Kilave Atenaka (katikati) na  Bi. Mary Minja (kwanza kulia) wakiongea na mteja aliyefika banda lao lililo chini ya wizara ya Fedha katika Maonyesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Afisa Masoko UTT-PID, Bi Kilave Atenaka akihudumia mteja katika banda lao lililo chini ya wizara ya Fedha katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Afisa Masoko UTT-PID, Bi Kilave Atenaka akihudumia mteja katika banda lao lililo chini ya wizara ya Fedha katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
 Muonekano wa viwanja vya Mabano vilivyopimwa na Taasisi ya UTT-PID kwa ushirikiano na Halmashauri vilivyopo Manispaa ya Lindi.
Zaidi ya viwanja 2,500 vilipimwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama vile Makazi, Biashara, Maeneo ya Umma na sehemu za kupumzika.  
 Akielezea Afisa Masoko Bi. Kilave Atenaka alisema kuwa kwa sasa wanaendesha huduma ya uuzwaji wa Fomu kwa ajili ya Viwanja, pia wanatarajia kuanza kuuza kwa umaa na taasisi mbali mbali miradi mipya ikiwemo wa Tundwi Songai – Kigamboni jijini Dar es Salaam na ule wa Kingorwila, Morogoro.
Aidha Bi. Kilave alitumia wito huo kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi ndani ya banda hilo kujipatia elimu mbali mbali zitolewazo na taasisi hiyo hapa nchini.
Toka kuanzishwa kwake Taasisi ya UTT-PID imejikita sana katika upimaji wa maeneno katika mikoa mbalimbali kwa kushirikiana na Halmashauri tofauti nchini. Miradi mikubwa kama ya Bukoba ambapo viwanja zaidi ya 5,000 vilipima kuuzwa, Halmashauri ya Sengerema kwa ushirikiano na Taasisi ilipima zaidi ya viwanja 1,200 na uuzaji pamoja na uwekezaji katika Miundombinu husika unaendelea kwa kasi. Pia Taasisi imewekeza katika miradi binafsi kama vile eneo la Mapinga katika wilaya ya Bagamoyo huku ikatarajia uwekezaji mkubwa zaidi katika mikoa ya Morogoro , Arusha, Dar es Salaam, Maswa, Pwani, Maswa na Ruvuma.
-- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''

JK ALIPOAGWA RASMI NA WASANII WA FANI MBALIMBALI MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM

August 08, 2015
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni  Mhe Paul Makonda alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Mhe. John Pombe Magufuli alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mhe January Makamba  alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Ruge Mutahaba, mratibu mkuu wa hafla  alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na wasanii  alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na msanii na kiongozi wa bendi Mapacha watatu  Jose Mara alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Mona Lisa mmoja wa wasanii  walioratibu hafla alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na msanii JB  alipowasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015. Kushoto kwa JB ni Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Mhe. John Pombe Magufuli
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipewa maelezo ya hafla itavyokuwa baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam ambako Wasani wa fani mbalimbali waliandaa hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na rasmi na  Wasanii wa fani mbalimbali katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
 Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015

  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  Wasanii wa fani mbalimbali wakimkaribisha JK katika  hafla rasmi ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
  JK akipata picha na Mgombea Ubunge Moshi Mjini Davies Mosha na mwendesha talk show Mboni Mashimba kwenye hafla ya Wasanii wa fani mbalimbali ya kumuaga usiku wa Alhamisi Agosti 6, 2015
 JK akisalimiana na msani Cassim Mganga
 Ommy Dimples akipata selfie na JK
 Wasanii wakipata selfie na JK
 Kila msanii aliomba selfie na JK
 selfie
 JK akipata selfie toka kwa
Meza ya Mzee Yusuf na mkewe na wadau wakubwa wa muziki nchini
Meza ya Mzee Walter Bgoya ya familia yake
Meza ya Jose Mara na Kelvin Twissa
Selfie zikiendelea
JK na wakongwe Nyoshi el Sadat na Komando Hamza Kalala
Kila kona selfie
JK akiendelea kusalimiana na wadau wa sanaa 
JK akipeana mikono na Joh Makini
Selfie zimenoga meza ya kina Adam Mchomvu na Joh Makini
Adam Mchomvu akitoa special thanks kwa Prezidaa
JK akimsalimia Nikki wa Pili 
Meza ya Fina Mango
Jose Mara akinogesha shughuli. Huyu jamaa noma
Diamond akitoa shukrani kwa niaba ya wasanii wenzie
Jose Mara jukwaani katika Big Screen
JK na King Majuto
JK akiongea na King Majuto na Mzee Shilo
JK akiwa na Bi Shakila Saidi
Steve Nyerere akiwa kavamia meza kuu
Steve Nyerere akiosha nyota
Diamond akisalimia meza Kuu
Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mwimbaji nyota Patricia Hilary
Mshindi wa Big Brother Africa Idriss Sultan akisalimia meza kuu
Mshindi wa Big Brother Africa Idriss Sultan akisalimiana na Dkt Magufuli
Mshindi wa Big Brother Africa Idriss Sultan akificha uso
Mwanamuziki nyota Ali Kiba akitoa shukrani zake kwa JK
Vanessa Mdee akiwa jukwaani
Meza Kuu
Dkt Magufuli na Nape Nnauye wakifanya mambo jukwaani
JK akifurahi na wasanii
JK akipongezwa na King Majuto kwa kusakata rhumba
JK akipompongeza Dkt Magufuli kwa kupiga tumba kwa ustadi mkubwa
JK akisalimiana na mwigizaji nguli Ray Kigosi
Dkt Magufuli akisalimiana na Bashe
JK na msanii wa Hip Hop mkongwe Fid Q
JK akicheza na Vanessa Mdee
Wasanii wakongwe wakiserebuka
JK akifurahi na wasanii
Furaha na vicheko vilitawala
JK akisalimiana na Bushoke
Dkt Magufuli akisalimiana na Bushoke
MC Richie Mtambalike alinogesha vilivyo hafla hii
Meza kuu wakishangilia baada ya JK kutangazwa Shujaa wa wasanii
Nikki wa pili akionesha  zawadi ya picha waliyoandaa wasanii
Nikki wa pili akionesha meza kuu zawadi ya picha waliyoandaa wasanii
Nikki wa pili akimkabidhi JK  zawadi ya picha waliyoandaa wasanii
Nikki wa pili akimkabidhi JK  zawadi ya picha waliyoandaa wasanii huku Fid Q akimuonesha majina ya wasanii wote yaliyotengeneza mosaic ya picha hiyo
Nikki wa pili akimkabidhi JK  zawadi ya picha waliyoandaa wasanii
Dkt Magufuli akimpongeza Nikki wa Pili
JK akiongea na wasanii
Wasanii wakimsikiliza JK
Wasanii wakimsikiliza JK

Wasanii na wadau wakimsikiliza JK
Wasanii wakimsikiliza JK
Wasanii wakimsikiliza JK
Wasanii wakimpongeza  JK
Wasanii wakimpongeza  JK
Wasanii wakimpongeza  JK
Wasanii wakimpongeza  JK

JK akiendelea kuongea 
Wasanii wakimpongeza  JK