Picha
ikionyesha wa kushoto mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema
akiwa anatulizwa na mchungaji Wilfred Mlayi ,Wa kwanza kushoto ni mkuu
wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa anatulizwa na mfadhili wa Mradi huo
ambaye ni daktari bigwa wa magonjwa ya kina mama na Mtoto Duniani Edru
Broun
Wananchi
waliohudhuria uzinduzi wa ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto ambaye
akupenda kutaja jina lake akiwa anamuomba mmbunge wa jimbo la Arusha
mjini Godbless Lema kutulia na kumuaacha mkuu wa mkoa aendelee kutoa
hutuba.Habari picha na Woinde Shizza,Arusha
VURUGU
kubwa zimeibuka baina ya mkuu wa mkuu wa mkoa Arusha Mringo Gambo na
mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema katika hafla ya uwekaji wa
jiwe la msingi katika hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo ya
buruka nje kidogo ya jiji la Arusha.
Vurugu
hiyo zimeibuka baada ya mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kuvuruga
ratiba iliyokuwa imepagwa na waandaaji wa hafla hiyo ambapo kwa mujibu
wa ratiba iyo ilikuwa imepagwa kuwa hotuba ya mkuu wa mkoa
ingetanguliwa na waandaji wa shughuli hiyo akiwemo waandaji wa hafla
hiyo,wafadhili pamoja na mbunge Lema.
Kabla
ya vurugu hizo mkuu wa Arusha alikaribishwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru
Alexzanda Mnyeti swala ambalo liliibua mzozo mkubwa kwa wananchi
walikuwa wamefika kushuudia tukio hilo la uzinduzi wakiwemo wafadhili
waliofadhili mradi ambao ni shirika la kuhudumia afya ya mama na mtoto
(maternity Afrika ).
Baada
ya kuanza kuhutubia mkuu huyo wa mkoa akielezea historia ya mradi huo
ikiwe upatikanaji wa eneo la kujenga mradi wa hospitali hiyo gafla
mbunge lema alipo simama na kupinga hotuba hiyo hiyo na kudai imejaa
upotoshwaji na siasa ndani kwani yeye ndie aliyetafuta eneo hilo la
ujenzi wa hospitali hiyo kutoka katoka kampuni ya mawala Advocate na sio
kweli eneo hilo limetokana na maono aliyokuwa nayo Marehemu Advocate
Nyaga Mawala ya mda mrefu .
“mkuu
wa mkoa acha kupotosha uma ,mchungaji simamisha hutuba ya mkuu wa mkoa
imejaa siasa anaongea uongo anaongea vitu asivyo vijua,sitakubali huu
uongo uendee siwezi kubali hutuba iendelee kwani anaongea uongo ,akitaka
atumie nguvu ya polisi siogopi kufa ila nataka ukweli ,na aondoe siasa
aseme ukweli hili jamboni lamaendeleo ya wananchi na nikwaifada ya
wananchi haswa mama na mtoto tena wale wasio jiweza kwaiyo naomba mkuu
wa mkoa acha uwongo”alisikika Lema akisema kwa sauti kubwa huku
akimsogelea mkuu huyo wa mkoa.
Jambo
hilo liliwalazimu baadhi ya wageni wa alikwa wakiwemo wakinamama
kumpigia magoti mbunge huyo alionekana akiwa na jazba kubwa huku
akimsogelea mkuu huyo wa mkoa swala ambalo lingeweza kusabisha uvunjifu
wa amani .
Licha
ya Vurugu hizo na kelele za wananchi walionekana nao kupinga hotuba hiyo
ya mkuu wa mkoa,Mkuu wa mkoa wa Arusha aliendelea kuhutubia akiwa
anaeleza kuwa eneo hilo lilitolewa na marehemu Nyaga Mawala kwa serekali
ili liendelezwe kwa kujengwa hospitali na mama na mtoto kitendo ambacho
kiliendeleza kelele za wananchi zikipinga hotuba hiyo wakidai mkuu wa
mkoa anapotosha .“hili jambo sio la siasa tusiingize siasa ,na kama
kunamtu anampango wa kufanya siasa apa anapoteza muda wake mimi ni mkoa
na ninafahamu historia ya eneo hili”alisema Gambo
Kwa
upande wake mfadhili wa maradi huo ambaye ni daktari bigwa wa magonjwa
ya Festula Duniani Dkt.Edru Broun alieza kusikitishwa na tukio
lilijitokeza na kuwataka viongozi waweke pembeni siasa zao na tofauti
zao na wamatangulize mungu ili kutimiza shabaha ya ujenzi wakituo hicho
cha hospitali kitakachoweza kumsaidi mama na mtoto.
Alisema
kuwa ujenzi wa hopitali hiyo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni sita
na kwa awamu ya kwanza kiasi cha shili bilioni tatu kitatumika kujenga
hospitali hiyo fedha ambazo zitatolewa na wafadhili kutoka shirika la
mama na mtoto (martenity Afrika).
Kwa
upande wake mwenyekit wa Tasisi ya maendeleo ya jiji la Arusha (ARDF)
Elifuraha Mtowe Alisema kuwa eneo la kujegwa hospitali hiyo lilitolewa
na marehemu Nyaga Mawala nakwa ARDF kupitia ofisi ya mbunge wa jimbo la
Arusha mjini ndipo taasisi yao ya ARDF ikamamua kutafuta mfadhili ndipo
walipompata MartenityAfrika.
Alisema
kuwa tangu wampate mfadhili waliingia mkataba na wakakubaliana
hospitali iishe ndani ya mika mitano lakaini mfadhili mwenyewe
aliwaakikishia kuwa hospitali hiyo itaisha mapema iwezeka kwani
itakamilika ndani ya mwaka mmoja tu ili mama na mtoto aweze kupata
huduma kwa araka zaidi.
Awali
mbunge Lema aliwaambia waandishi wa habari kuwa mkuu wa mkoa huyo
alikuwa amegoma kuja kuzindua hospitali hiyo hadi pale mbunge huyo
alipoamua kumpiga simu katibu mkuu kiongozi John Kijazi na kumwambia
kuwa mkuu wamkoa kagoma kuja kuzindua hospitali hiyo ndipo katibu mkuu
alipoamua kupiga simu wizara ya tamisema ambapo ndio walimpigia simu
mkuu wamkoa ili aweze kufika kwenye uzinduzi huo.