KUNDI LA MTANDAO WA WHATSAPP LA "SARATANI INFO" LATOA MSAADA WA BIMA ZA AFYA KWA WATOTO 8 WANAPATA MATIBABU YA SARATANI KCMC

May 14, 2017
Mabalozi wa Kundi la Mtandao wa Kijamii wa Whatsaap la Saratani Info wakiwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC tayari kutembelea kitengo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mabalozi wa Kundi la Mtandao wa Kijamii wa Whatsaap la Saratani Info wakiwa wamebeba zawadi mbalimbali kwa ajili ya kutoa kwa wagonjwa wa Saratani katika Hosptali ya Rufaa ya KCMC.
Mkuu wa Kitengo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC,Dkt Furaha Silventi akizungumza na mabalozi wa kundi la Saratani Info lilipotmbelea kitengo hicho.
Mkuu wa Kitengo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC,Dkt Furaha Silventi akizungumza na mabalozi wa kundi la Saratani Info lilipotmbelea kitengo hicho,kulia kwake ni Kiongozi wa Mabalozi hao kanda ya Kaskazini,Veri Njau na kushot ni Mratibu katika kitengo hicho  Everlyn Ndosi.
Kiongozi wa Kundi la Mabalozi wa Saratani la Saratani Info kanda ya Kaskazini,Veri Njau akizungumza na baadhi ya wagonjwa pamoja na mabalozi hao baada ya kuwatembelea katika kituo cha Saratani ,KCMC.
Baadhi ya wagonjwa wa Saratani wanaopatiwa matibabu katika kitengo cha Saratani ,Hospitali ya Rufaa ya KCMC ambao kundi la Mabalozi wa ugonjwaa huo liliwatembelea na kutoa msaada wa gharama za Bima ya Afya kwa watoto nane (8).
Mabalozi wa Ugonjwa wa Saratani wakitembelea katika maeneo mbalimbali ya kitengo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.
Mmoja wa Mabalozi wa Ugonjwa wa Saratani wa kundi la mtandao wa WhatsApp la Saratani Info ,Respicius Baitwa akizungumza kabla ya kukabidhi fedha kwa ajili ya Bima za Afya kwa wagonjwa wa Saratani nane wanaopata matibabu katika kituo hicho.
Mkuu wa Kitengo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC,Dkt Furaha Silventi akitoa neno la shukurani baada ya Mabalozi wa Kundi la WhatsApp la Saratani Info kukabidhi msaada wa fedha kwa ajili ya Bima za Afya kwa watoto nane wanaopata matibabu katika kitengo hicho.
Baadhi ya Mabalozi wa Saratani waliotembelea kitengo cha Saratani katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC kuwaona wagonjwa wa Saratani wanaopata matibabu katika Hospitai hiyo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.


Ziara ya Rais Dk.Shein Maenneo ya Mafuriko leo

Ziara ya Rais Dk.Shein Maenneo ya Mafuriko leo

May 14, 2017
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) alipokuwa akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Idara ya Ujenzi wa Barabara katika Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Nd,Ali Twahir leo wakati alipotembelea Bonde la Kibonde Mzungu kutoka na Mafuriko yalitokea hivi karibuni kutoka na mvua kubwa za Masika zinazoendelea kunyesha,[Picha na Ikulu.]14/05/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa tatu kushoto) alipokuwa akiangalia maji ya Mvua yaliyofurika katika bonde la Mwanakwerekwe nyumba mbili leo kutokana na ujenzi holela wa Nyumba za Wananchi zilizojengwa na kupelekea kutopitisha maji katika njia inayoelekea Ziwa Maboga, kutokana na mvua kubwa za Masika zinazoendelea kunyesha.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) alipokuwa akiangalia maji yanayopita katika barabara ya Mwera gudini – Fuoni meli saba leo wakati alipokuwa katika ziara ya kutembelea maoneo mbali mbali yaliyopatwa na maafa ya Mvua za masika zinazoendelea kunyesha (katikati) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe,Ayoub Mohamed Mahmoud.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ( kushotio) alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Bumbwisudi leo wakati alipofika kuwariji na kuwapa pole kutokana na Nyumba zo kuingiliwa na maji ya mvua wakati alipokuwa katika ziara ya kutembelea maoneo mbali mbali yaliyopatwa na maafa ya Mvua za masika zinazoendelea kunyesha (wa pili kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe,Ayoub Mohamed Mahmoud.

WAZIRI MWAKYEMBE AYAFAGILIA MASHINDANO YA DASANI MARATHON 2017

May 14, 2017
 Mkurugenzi wa Michezo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Yusufu Singo (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa mashindano ya mbio ya Km 21 ya Dasani Marathon 2017  baada ya kuwakabidhi zawadi zao eneo la Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay Dar es Salaam leo. Mshindi wa kwanza, Augustine Sule (aliyesimama juu), Mshindi wa pili Stephano Huche (wa pili kushoto) na mshindi wa tatu Said Makula. Kushoto ni Nalaka Hettierachchi Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Coca Cola Kwanza iliyodhamini mashindano hayo kupitia kinywaji cha maji ya Dasani. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA-KAMANDA WA MATUKIO BLOG)

Na Richard Mwaikenda

WAZIRI wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe ameyafagilia mashindano ya mbio ya Dasani Marathon 2017 yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo imetolewa kupitia kwenye hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Michezo wa wizara hiyo, Yusufu Singo wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi wa mashindano hayo yenye umbali wa Km 10 na  21.

Pia aliipongeza Klabu ya Dar Running Club kwa maandalizi mazuri yaliyofanikisha mashindano hayo yanayodhaminiwa na Kampuni ya Coca Cola Kwanza kupitia maji ya Dasani. Kampuni hiyo imeingia mkataba wa kuyadhamini mashindano hayo kwa miaka mitano.

"Nawapongeza nyote kwa kuchukua jukumu kubwa la kufanikisha maandalizi ya mbio hizi ambayo siyo tu ni nzito bali muhimu katika mchakato mzima wa kujenga utamaduni wa kuzijali afya  zetu na ustawi wa familia zetu, uelewano uliothabiti katika kutekeleza majukumu yetu ya kifamilia na kitaifa". Alisema Mwakyembe.

Awali akizungumza Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Coca Cola Kwanza, Nalaka Hettierachchi alisema wanataka mashindano hayo yawe makubwa ambapo hivi sasa wana mipango ya kuyapeleka pia katika mikoa mingine nchini.

Mashindano hayo yaliyoshirikisha zaidi ya watu 1000 kutoka maeneo mbalimbali nchini, yalianzia na kuishia Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay na kupita barabara mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam ikiwemo ya Ali Hassan Mwinyi.

Aliyeibuka kidedea katika mbio za wanaume za umbali  wa Km 21 ni Augustine Sule, wa pili akiwa Stephano Huche na Said Makula aliyeshika nafasi ya tatu.

Kwa upande wa Wanawake aliyeibuka mshindi ni Jacquline Sakilu, wa pili akiwa  Noela Remmy na nafasi ya tatu ilikwenda kwa Antery John.

Kwa mbio za umbali wa Km 10, mshindi kwa upande wa wanaume alikuwa Sylvester Seleman, wa pili akiwa  Daniel Sinda na Paul Pascal alishika nafasi ya tatu.Mshindi wa kwanza kwa wanawake alikuwa May Naari, wa pili akiwa Sara Hitis na Asia Seleman aliyetwaa nafasi ya tatu.

Kwa upande wa walemavu aliyeshinda ni Shukuru Khalfan, wa pili alikuwa Mathias John na Jonis Stephano alishika nafasi ya tatu.

Mshindi wa kwanza wa mbio za Km 21 kwa upande wa wanaume na wanawake kila mmoja alikabidhiwa sh. mil 1, wa pili sh. 750,000 na wa tatu sh. 600,000.
 Baadhi ya washiriki wakimalizia mbio zao katika Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay
 Washiriki wakivishwa medali baada ya kumaliza kukimbia katika mashindano hayo
 Elizabeth wa NMB Bank akivishwa medali baada ya kumaliza mbio hizo
 ni mbio kwa kwenda mbele
 Mshiriki akiangalia muda alioutumia kukimbia. Kushoto ni Mwanariadha nguli wa zamani Juma Ikangaa
 Juma Ikangaa akiwavisha medali washiriki wa mbio hizo
 Mtoto akiwa miongoni mwa wakimbiaji
 Wakimalizia kukimbia

 Timu ya NMB Bank iliyoshiriki katika mashindano hayo
 Wakifurahia kumaliza mbio
 Wakiendelea na mazoezi baada ya mashindano
 Juma Ikangaa akimkabidhi zawadi mshindi wa kwanza wa mbio za wanawake umbali wa Km 10, Mary Naari
 Mshindi wa kwanza wa mbio za Km 10 wanaume,  Sylvester Simon akikabidhiwa zawadi na Juma Ikangaa

 Dorothy Kipeja wa Dar Running Club waandaji wa mashindano hayo, akimkabidhi zawadi mmoja wa washindi wa Km 21
 Mshindi wa kwanza wa mbio za umbali wa Km 21, Augustine Sule akipongezwa na Juma Ikangaa alipokabidhiwa zawadi na Mkurugenzi wa Michezo, Yusufu Singo (wa pili kulia)
 Mshindi wa kwanza kwa upande wa walemavu  Shukuru Khalfan (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Michezo, Yusufu Singo pamoja na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Coca Cola Kwanza, Nalaka.
 Nahodha wa timu ya riadha ya Radio EFM, Maulidi Kitenge akiwapongeza waandaji wa mashindano hayo baada ya timu hiyo kushiriki ipasavyo.
Mtoto aliyeshiriki na kumaliza vizuri mbio hizo, akizawadiwa soda

Mkazi wa Bunju James Peter azoa milioni za Biko

May 14, 2017
Balozi wa Biko Tanzania Kajala Masanja akifurahia namba ya ushindi ambapo mkazi wa Bunju, jijini Dar es Salaam, James Peter amejinyakulia jumla ya Sh Milioni 10 katika droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Emmanuel Ndaki. Picha na Mpiga picha wetu

MBUNGE WA LUSHOTO ATEMBELEA BARABARA YA MOMBO-SONI KUJIONEA ATHARI ZA BARABARA

May 14, 2017
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia akikagua athari za mafuriko kwenye barabara ya Soni hadi Mombo ambapo imefungwa kutokana na vifusi,mawe kudondoka barabarani na hivyo kusababisha adha hiyo
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia akiangalia athari za barabara ya Mombo hadi Soni ambayo imefungwa kutokana na kushuka kwa mawe makubwa na vifusi
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia akitazama maeneo yaliyoathirika
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia akipita kwenye baadhio ya maeneo yaliyoathirika na udongo kushuka na kusababisha adha kwa wasafiri
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia akisistiza jambo kwa wananchi
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia kulia akisalimiana na wananchi
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia katikati akiwa kwenye picha na wapiga kura wake mara baada ya kukutana nao akiwa njiani kuelekea kwenye kukagua athari za mafuriko
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia kulia akitazama eneo ambalo limetoka jiwe kubwa ambalo lilishuka kwenye barabara ya Mombo- Soni na kusababisha kufungwa
Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi alimaarufu Bosnia kulia akiteta jambo na wataalamu wanaosimamia zoezi la kuondosha kifusi na mawe
Creda likiendelea na kazi yake kama kawaida
Baadhi ya wananchi wakipita kwenye barabara hiyo mara baada ya greda kuondoa kifusi kwenye baadhi ya maeneo yaliyokuwa wameangukiwa na vifusi


Katibu wa CCM wilaya ya Lushoto,Ramadhani Mahanyu akizungumzia suala hilo
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bumbuli akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kadhia ambayo wamekumbana nayo watumiaji wa barabara ya Mombo-Soni kutokana na mawe na vifusi kudondoka


Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM) Shabani Shekilindi  alimaarufu Bosnia akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na athari za barabara ya Mombo hadi Soni kuharibika