KARIBU LEO ESCAPE ONE UCHEZE MZIKI MZURI NA BENDI YAKO YA SKYLIGHT

November 14, 2015



Sony Masamba akichana mistari na mashabiki wa Skylight Band wakiendelea kuzirudi huku Joniko Flower, Sam Mapenzi na Kasongo Junior wakimsikindiza kwa miondoko ya aina yake. Hakika hii sio ya kukosa leo Jumapili.
Kasongo Junior na Suzy wakiwapa raha mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) ndani ya kiota cha Escape One jumapili iliyopita, bila kukosa ya leo itakuwa pale pale.
Kasongo Junior na Suzy wakiendelea wakizirudi kwenye kiota cha Escape One 
Sam Mapenzi akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band Jumapili iliyopita ndani ya kioa cha Escape One Mikocheni ambapo leo pia burudani iko pale pale na ndio kwanza week end imeanza kwa fans wa Skylight Band.
Waimbaji wa bendi ya Skylight, Joniko Flower na Sony Masamba wakiendelea kutoa burudani mbele ya mashabiki wao ndani ya kioata cha Escape One Mikocheni jijini Dar.
Sam Mapenzi na Sony Masamba wakiendelea kuwapa raha mashabiki wa Skylight Band.
Rapa Mkongwe wa muziki wa dansi wa Skylight Band, Joniko Flower akiwasebenesha sehemu ya mashabiki wao Jumapili iliyopita kwenye Skylight Sunday Bonanza‬ kiota cha Escape One Mikocheni jijini Dar es Salaam

Joniko Flower  akizirudi pamoja na Mashabiki wa Bandi ya Skylight pamoja na waimbaji wa bendi hiyo

Suzy akiwapa raha mashabiki wa Skylight Band (hawapo pichani) ndani ya kiota cha Escape One jumapili iliyopita huku akisindikizwa na 
Waimbaji wa Bendi ya Skylight wakiendelea kutoa burudani huku wakiongozwa na Rapa Mkongwe wa muziki wa dansi wa Skylight Band, Joniko Flower
Kifaa kipya cha Bandi ya Skylight, Leah akitoa burudani ya nguvu mbele ya mashabiki wao huku akisindikizwa na Kasongo Junior
Waimbaji wa Bendi ya Skylight pamoja na mashabiki wa bendi hiyo wakiendelea kuzirudi katika kiota cha Escape One Jijini Dar es Salaam

Geofrey Adroph BLOGGER P.O.BOX 24793, Mob: +255 755 274953 /+255 713 363965, Email: pamojapure@gmail.com. Blog: http://www.pamoja.co.tz/ DAR ES SALAAM, TANZANIA
KAMATI KUU YA CCM KUKUTANA KESHO MJINI DODOMA

KAMATI KUU YA CCM KUKUTANA KESHO MJINI DODOMA

November 14, 2015

J1Kamati Kuu ya Taifa ya CCM inatarajiwa kufanya kikao chake cha siku moja mjini Dodoma kesho Novemba 15, 2015 kujadili majina ya wana-CCM walioomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Uspika na Unaibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kamati Kuu itafanya kikao chake kesho saa sita kamili mchana chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Kikao cha Kamati Kuu kitafuatiwa na Kikao cha Kamati ya Wabunge wote wa CCM kitakachofanyika Novemba 16, 2015 saa nne asubuhi katika ofisi za Makao Makuu ya CCM Dodoma. Imetolewa na:- Nape Moses Nnauye KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA, ITIKADI NA UENEZI 14/11/2015
TAIFA STARS YAING’ANG’ANIA VIBAYA ALGERIA YATOKA SARE YA 2-2 UWANJA WA TAIFA.

TAIFA STARS YAING’ANG’ANIA VIBAYA ALGERIA YATOKA SARE YA 2-2 UWANJA WA TAIFA.

November 14, 2015

1
Wachezaji wa timu ya Taifa Stars na Algeria wakichuana vikali kuwania mpira katikati yao wakati wa mchezo wa kufuzu fainali za kombe la dunia  uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam huku timu hizo zikitoshana nguvu kwa kufungana magoli 2-2 na kuifanya Taifa Stars kuwa na kibarua kigumu wakati wa mchezo wa maruduano utakaofanyika Novemba 17 mjini Algers Algeria ili kusonga mbele katika michuano hiyo.Taifa Stars  inahitaji kushinda katika mchezo wake huo ili iweze kusonga mbele.
2
Baadhi ya washangilianji wakishangilia kwa nguvu wakati wa mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
3
Hii ni staili moja wapo iliyotumiwa na washngiliaji wa timu ya Taifa Stars katika mchezo huo.
5
Mdau Muddy, Bariki na  marafiki zao walikuwa ni mmoja wa mashuhuda wa mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa
6
Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars.
7
Kikosi cha timu ya Taifa ya Algeria kikiwa katika picha ya pamoja.

MAANDALIZI YA KIKAO CHA BUNGE YAENDELEA

November 14, 2015

  Mtangaza nia wa uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samweli Sita akiongea na mfanyakazi wa Benki ya CRDB katika viwanja vya Bunge wakati wa maandalizi ya Kikao cha Bunge kinachotarajiwa kuanza hivi kariubuni.

  Mtangaza nia wa uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samweli Sita akiongea na wafanyakazi  wa Benki ya CRDB katika viwanja vya Bunge wakati wa maandalizi ya Kikao cha Bunge kinachotarajiwa kuanza hivi kariubuni.

 Mtangaza nia  wa Uspika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samweli Sita akiongea na baadhi ya waheshimiwa wabunge  kwenye Viwanja vya Bunge wakati wa maandalizi ya Kikao cha Bunge kinachotarajiwa kuanza hivi karibuni.
(PICHA NA BENJAMIN SAWE)

Mtaalamu wa Upasuaji wa Uti wa Mgongo na Magonjwa ya Mfumo wa Fahamu kutoka Hospitali za Apollo kuendesha huduma Dar.

November 14, 2015



Dr Alok Ranjan, mtaalamu wa magonjwa ya mfumo wa fahamu na uti wa mgongo kutoka hospitali ya Apollo akitoa huduma kwa mtoto Zulea akiwa na mama yake Shamila Idd katika kliniki iliyofanyika siku tatu.’

Dr Alok Ranjan, mtaalamu wa magonjwa ya mfumo wa fahamu na uti wa mgongo kutoka hospitali ya Apollo akiongea na waandish wa habari katika cliniki iliyoanza tarehe 11 na kuendelea mpaka tarehe 13 katika hospitali ya hindumandal.



Bwana Hafidhi Rashid Waziri, mmoja wa wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa uti wa mgongo na Dr Alok Ranjan katika hospitali ya Apollo Hyderebad akiongea na waandishi wa habari katika Klinik hiyo.

Shamila Idd mama wa mtoto Zulea mwenye tatizo la uti wa mgongo akiongea na waandishi wa habari katika kliniki iliyoandaliwa na Dr Alok Ranjan, mtaalamu wa magonjwa ya mfumo wa fahamu na uti wa mgongo kutoka hospitali ya Apollo.

Na Mwandishi Wetu,

Tanzania ni moja ya nchi ambazo ina uhaba mkubwa wa madaktari bingwa wa mfumo wa fahamu kitendo kinachopelekea nchi kupoteza fedha nyingi kwa kuwapeleka wagonjwa wa matatizo ya aina hiyo nje ya nchi kupata matibabu na ushauri.
Inakadiriwa kuwa watoto wachanga 1000 kati 4000 wanaozaliwa na tatizo la mfumo wa fahamu hupatiwa matibabu huku wengine 3000 wakishindwa kupatiwa matibabu.
Kutokana na hali hiyo, Hospitali ya Apollo ya nchini India imemleta nchini daktari bingwa wa upasuaji wa uti wa mgongo na mfumo wa fahamu ambaye pia ni Mkuu wa idara ya upasuaji wa magonjwa ya fahamu katika hospitali hiyo DKT ALOK RANJAN ambaye atakuwa akitoa huduma na kuwaona wagonjwa wake aliowafanyia upasuaji siku za nyuma.
Nao baadhi ya wagonjwa waliofika katika kliniki hiyo inayofanyikia katika hospitali ya hindu mandal jijini Dar es Salaam wameiomba serikali kuhakikisha kwamba inasaidia katika gharama za matibabu ya watu wanaosafiri nje ya nchi kufuata matibabu ya magonjwa mbali mbali.
Wamezitaka pia kampuni za bima ya afya kuhudumia wateja wake katika hospitali za kimataifa badala ya kujikita katika hospitali za hapa nchini pekee.
Katika mkutano huo na waandishi wa habari ulofanyika tarehe 12 katika hospitali ya hindumandali Dk. Alok Ranjan kutoka Hospitali za Apollo amewashauri watanzania kubadilisha mtindo wa maisha ili kuepukana na magonjwa ya mfumo wa fahamu na uti wa mgongo. anasema kuwa kwa watu wazima ugonjwa huu mara nying husababishwa na namna mbovu ya ukaaji ambao hudhuru uti wa mgongo, trauma, shinikizo la damu, ajali, kisukari, uzito wa kupitiliza na sababu nyinginezo.
Tanzania kwa sasa inakadiriwa kuwa na madaktari wa mfumo wa fahamu 7 ambao wote kwa sasa ni watendaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam.