WAJUMBE wa CC watakiwa kujenga ushawishi kwa wafanyabiashara-RC Gallawa
Na Oscar Assenga,Tanga.
MKUU wa mkoa wa Tanga Chiku Gallawa amewataka wajumbe wa baraza la watumiaji wa huduma za usafiri wa nchi kavu na majini (Sumatra) kujenga ushawishi kwa wafanyabiashara kutumia usafiri wa majini ili kuweza kupunguza msongamano uliopo barabarani.
Kauli hiyo aliitoa jana wakati akifungua mafunzo ya kamati za mikoa za baraza la watumiaji wa huduma za usafiri wa nchi kavu na majini kilichofanyika katika hotel ya Tanga Beach Resort mkoani hapa na kuhudhuriwa na wajumbe wa baraza hilo kutoka mikoa sita ambayo ni Mwanza, Arusha,Kagera,Tanga,Kigoma na Mtwara.
Gallawa alisema utumiaji huo mbali ya kupunguza msongamano barabarani lakini pia watarahisisha shughuli zao za kila siku na kuweza kufika katika maeneo husika kwa wakati uliopo kuliko kuendelea kutumia usafiri wa nchi kavu ambao huwapotezea muda.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wajumbe wa baraza hilo kutekeleza majukumu yake sanjari na kuwa wazalendo katika kujitolea kwani kwenye maendeleo changamoto zipo hivyo wajumbe wanawajibu wa kuongeza jitihada ili kukabiliana nazo.
Awali akizungumza katika mkutano huyo,Katibu Mtendaji wa Sumatra (CC),Oscar Kikoyo alisema lengo la mkutano huo ambao uliwautanisha wajumbe kutoka mikoa sita ni kuangalia namna ya kuboresha usafiri wa nchi kavu na majini pamoja na kuishauri serikali kwenye baadhi ya mambo ili kuweza kupata maendeleo.
Mwisho.
MKUU wa mkoa wa Tanga Chiku Gallawa amewataka wajumbe wa baraza la watumiaji wa huduma za usafiri wa nchi kavu na majini (Sumatra) kujenga ushawishi kwa wafanyabiashara kutumia usafiri wa majini ili kuweza kupunguza msongamano uliopo barabarani.
Kauli hiyo aliitoa jana wakati akifungua mafunzo ya kamati za mikoa za baraza la watumiaji wa huduma za usafiri wa nchi kavu na majini kilichofanyika katika hotel ya Tanga Beach Resort mkoani hapa na kuhudhuriwa na wajumbe wa baraza hilo kutoka mikoa sita ambayo ni Mwanza, Arusha,Kagera,Tanga,Kigoma na Mtwara.
Gallawa alisema utumiaji huo mbali ya kupunguza msongamano barabarani lakini pia watarahisisha shughuli zao za kila siku na kuweza kufika katika maeneo husika kwa wakati uliopo kuliko kuendelea kutumia usafiri wa nchi kavu ambao huwapotezea muda.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wajumbe wa baraza hilo kutekeleza majukumu yake sanjari na kuwa wazalendo katika kujitolea kwani kwenye maendeleo changamoto zipo hivyo wajumbe wanawajibu wa kuongeza jitihada ili kukabiliana nazo.
Awali akizungumza katika mkutano huyo,Katibu Mtendaji wa Sumatra (CC),Oscar Kikoyo alisema lengo la mkutano huo ambao uliwautanisha wajumbe kutoka mikoa sita ni kuangalia namna ya kuboresha usafiri wa nchi kavu na majini pamoja na kuishauri serikali kwenye baadhi ya mambo ili kuweza kupata maendeleo.
Mwisho.
TIKETI MECHI YA STARS KUANZA KUUZWA KESHO
TIKETI MECHI YA STARS KUANZA KUUZWA KESHO
Wakati
timu ya Ivory Coast inatarajiwa kuwasili leo usiku (Juni 13 mwaka huu)
kwa ndege maalum, tiketi kwa ajili ya mechi kati yake na Taifa Stars
itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa zinaanza kuuzwa kesho
mchana (Juni 14 mwaka huu) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Vituo
vitakavyotumika kwa mauzo hayo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa,
Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom
Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala na BMM Salon iliyoko
Sinza Madukani.
Viingilio
katika mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika katika
kundi C ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani, sh. 7,000 viti vya
rangi ya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C,
sh. 20,000 kwa VIP B wakati VIP A itakuwa sh. 30,000.
Pia
viti 100 vilivyo katika sehemu ya Wageni Maalumu (VVIP) vitauzwa kwa
sh. 50,000 kila kimoja. Tiketi hizo zitauzwa katika ofisi za TFF, na
watakaonunua watapewa kadi maalumu zenye majina yao, majina ambayo pia
watayakuta katika vita watakavyokaa. Kwa maana hiyo hakutakuwa pasi
maalumu (free pass) za kuingia VVIP.
PONGEZI KWA RAIS MPYA WA ZFA
Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga
amempongeza Rais mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), Ravia
Idarous Faina aliyechaguliwa katika uchaguzo mdogo uliofanyika hivi
karibuni.
Amesema
ushindi aliopata Faina unaonyesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ZFA
walivyo na imani naye katika kuhakikisha maendeleo ya mpira wa miguu
visiwani humo.
Rais
Tenga amesema ni imani yake kuwa Rais Faina ataendeleza ushirikiano
uliopo kati ya TFF na ZFA kwa ajili ya ustawi wa mpira wa miguu katika
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kumtakiwa kila kheri katika wadhifa
wake huo mpya.
WAAMUZI WATATU WAFUNGIWA MIEZI MITATU
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefungia miezi mitatu waamuzi watatu
walioshindwa kuchezesha mechi namba 32 ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa
(RCL) kati ya Mpwapwa Stars ya Dodoma na Machava FC ya Kilimanjaro
iliyokuwa ichezwe Juni 2 mwaka huu Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
TFF
kupitia Kamati yake ya Waamuzi iliyokutana katika kikao chake cha Juni
12 mwaka huu kupitia taarifa mbalimbali za waamuzi wa RCL ilibaini
makosa yaliyofanywa na baadhi ya waamuzi na kuyatolea uamuzi.
Waamuzi
hao waliofungiwa ambao wanatoka mkoani Singida ni Jilili Abdallah,
Amani Mwaipaja na Theofil Tegamisho. Wamefungiwa kwa kutoripoti katika
kituo walichopangiwa (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma) na kutoa taarifa ya
uongo kwa kushirikiana na Kamishna wa mechi hiyo.
Kanuni
iliyotumika kuwafungia ni ya 28 kifungu (d) na (g) ya Ligi za TFF, na
adhabu hiyo imeanza Juni 13 mwaka huu. Waamuzi hao pamoja na kamishna
badala ya kwenda Uwanja wa Jamhuri, wao walikwenda kwenye Uwanja wa
Mgambo ulioko Mpwapwa na kuandika ripoti iliyoonesha kuwa timu ya
Machava FC haikufika uwanjani wakati wakijua kuwa mechi hiyo ilitakiwa
kuchezwa katika Uwanja wa Jamhuri.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Subscribe to:
Posts (Atom)