February 03, 2014

MASHINDANO YA NGALAWA YAFANA TANGA

 Ngalawa zikiwa katika mstari kwa ajili ya kuanza mashindano katika pwani ya Kijiji cha Kigombe wilayani Muheza. 
Meneja mauzo wa  ZANTELTanzania  Salum Ngururu, akikamkabidhi zawadi mshindi wa kwanza katika mashindano ya Ngalawa, Juma Mgeni zawadi yake.

WAZIRI MUKANGARA AWAFUNDA MAAFISA MAWASILIANO SERIKALI

February 03, 2014

WAZIRI WA HABARI,VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO,DR.FENELLA MUKANGARA AKIUZNGUMZA JANA KWENYE HOTEL YA TANGA BEACH RESORT WAKATI AKIFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA  HABARI NA MAWASILIANO JANA MKOANI TANGA KULIA KWAKE NI NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA HIYO PROF.ELISANTE OLE GABRIEL.

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI VIJANA,UTAMADUNI NA MICHEZO PROF.ELISANTE OLE GABRIEL AKIZUNGUMZA KWENYE KIKAO HICHO KABLA YA KUMKARIBISHA WAZIRI


 Na Oscar Assenga,Tanga.

WAZIRI wa Habari,Vijana ,Utamaduni na Michezo Dokta Fenella Mukangara ametoa wito
kwa Maafisa Mawasiliano wa Serikali kwenye wizara, Idara na Taasisi za serikali kuendelea kujifunza kwa weledi mambo mbalimbali yatakayosaidia kuleta tija katika kutekeleza majukumu yao ya kusimamia mawasiliano kwenye maeneo yao ya kazi.

Mukangara ametoa wito huo jana wakati wakifungua kikao cha kazi cha maafisa mawasiliano kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini kilichofanyika kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Resort Mkoani Tanga.


Amesema maafisa hao wamepewa jukumu kubwa la kuiwezesha serikali kuipitia ofisi zao kufanya mawasiliano na umma kupitia vyombo vya
habari kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sera na miradi inayotekelezwa na serikali yenye lengo la kustawisha maendeleo kwa watanzania.

WAZIRI MUKANGARA AFUNGUA KIKAO CHA KAZI CHA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO HOTEL YA TANGA BEACH RESORT JANA.

February 03, 2014



WAZIRI WA HABARI,VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO,DR.FENELLA MUKANGARA AKIUZNGUMZA JANA KWENYE HOTEL YA TANGA BEACH RESORT WAKATI AKIFUNGUA KIKAO KAZI CHA MAAFISA  HABARI NA MAWASILIANO JANA MKOANI TANGA KULIA KWAKE NI NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA HIYO PROF.ELISANTE OLE GABRIEL.

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA HABARI VIJANA,UTAMADUNI NA MICHEZO PROF.ELISANTE OLE GABRIEL AKIZUNGUMZA KWENYE KIKAO HICHO KABLA YA KUMKARIBISHA WAZIRI

MKURUGENZI WA IDARA HABARI NA MAELEZO ASSAH MWAMBENE KUSHOTO AKITETE JAMBO NA WAZIRI MUKANGARA BAADA YA KUFUNGUA KIKAO HICHO JANA

BAADHI YA WASHIRIKI KWENYE KIKAO HICHO CHA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO




February 03, 2014

LIVE,MH:MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NAWAFANYABIASHARA TUNDUMA MJINI

Naibu waziri wa Fedha Mh;Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo kwa Wafanyabiashara wa Mji wa Tunduma hii leo alipokutana nao kwenye Mkutano wa ndani kwenye Ukumbi wa High Class One akizungumza nao kuhusu Maendeleo ya Biashara,Ulipaji wa kodi,Changamoto za Mpakani kwenye Ulipaji kodi,matumizi ya Mashine za EFD kwenye makato ya TRA.
 Sehemu ya Mamia ya Wafanyabiashara waliohudhuria Mkutano wa Naibu Waziri wa Fedha Mh;Mwigulu Nchemba wa Kujadiliana na kuelezana namna ya Kuimarisha Ukusanyaji wa mapato nchini.

Naibu Waziri wa Fedha Mh:Mwigulu Lameck Nchemba hii leo ameendelea na Ziara yake ya kikazi ya Kukutana na Wafanyabiashara ndnai ya Mkoa wa Mbeya baada ya Kufanya hivyo kwenye Mkoa wa Njombe na Ruvuma wiki iliyopita.
Hii leo Mh:Mwigulu  amezungumza na mamia ya wafanyabiashara wa Mji wa Tunduma kuhusu nafasi yao ya Kukuza Ukusanyaji wa mapato kwa kaucha kukwepa kulipa kodi,Kuacha kupitisha bidhaa kimagendo kwenye mpaka wa Nchi ya Tanzania na Zambia.
Wafanyabiashara Wakitanzania wasio wazalendo wa Kulipa kodi wamekuwa wakitumia mwanya wa Mpaka kuvuka kufanya biashara Zambia na makazi yao yapo Tanzania kitu kinachopelekea ukusanyaji wa Mapato kuwa Mgumu kwa TRA na taasisi husika. 
Serikali imeamua kufanya maridhiano na Serikali ya Zambia kuhakikisha kunakuwepo na Mpaka uliotenganishwa kwa Mita 50 kila upande wa Nchi hizi mbili ilikudhibiti ukwepaji wa kulipa kodi na biashara ya Magendo.
Naibu waziri pia alitumia nafasi kuwaelimisha Wafanyabiashara umuhimu wa kutumia mashine za EFD kwenye kurahizisha ukusanyaji wa mapato na kukuza biashara zao.
Mbali na hayo wafanyabiashara walipata nafasi ya kutoa mawazo,maoni yao kwa 
Naibu waziri wa Fedha namna ya Kuimarisha Ukusanyaji wa mapato,Uelewa wao kuhusu Mashine za EFD na Ushirikiano watakao onesha kwenye Kudhibiti ukusanyaji mapato mpakani Mwatanzania na Zambia.
Picha na Habari Kwanza Blog
February 03, 2014

SIKU YA SHERIA DUNIANI YAFANYIKA MKOANI DODOMA, WALIA NA UPUNGUFU WA MAJAJI.

 Wakili  wa Serekali Mfawidhi mkoa wa Dodoma, Angaza Mwaipopo akifafanua jambo wakati wa sherehe ya siku ya sheria mjini Dodoma leo.
Jaji Mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Dodoma, Crecensia Makuru akizangumza jambo mbele ya watendaji na wadau wa mahakama wakati sherehe za siku ya Sheria zilizofanyika leo.
 Wakili wa kujitegemea Mary Munissi wa mkoani Dodoma akielezea jambo wakati wa maadhimisho ya siku ya sheria yaliyofanyika leo
 Mahakimu, Mawakili na watendaji wengine wa mahakama wakifuatila jambo walipokuwa kwenye maadhimisho ya siku ya sheria yaliyofanyika leo Dodoma.
 Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu kanda ya Dodoma akizungumza jambo na Kaimu mkuu wa mkoa wa Dodoma ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Singida, Mh. Pasiseko Konne mara baada ya kumalizika shughuli za maadhimisho ya siku ya sheria leo.

Na John Banda, Dodoma


UCHELEWESHWAJI wa kesi nyingi mahakamani katika mahakama ya kanda ya Dodoma kunasababishwa na upungufu mkubwa wa majaji.


Hayo yalisemwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Crecencia Makuru leo mjini humo wakati wa maadhimisho ya siku ya sheria nchini yaliyofanyika katika viwanja vya mahakama kuu.

Alisema kuna upungufu mkubwa wa majaji ambao haulingani na kesi zilizopo hali inayosabisha kuzolotatesha mienendo ya kesi mbalimbali.


Crecencia alisema majaji katika kanda ya Dodoma ni wachache kulingana na kesi zilizopo  ambapo hadi kufikia Desemba 31, 2013 kulikuwa na jumla ya mashauri na 1364 na kuna majaji wawili tu.

Alisema ''idadi ya kesi ni kubwa mno kwa majaji wawili hii inachangia kwa kiwango kikubwa kesi kutosikilizwa na kutolewa maamuzi kwa wakati, upo umuhimu wa kuongeza majaji ili kuwe na uwiano wa masharti yaliyopo'',

Aidha alisema Mahakimu ni wachache huku mahakama nyingi za wilaya zina hakimu mmoja mmoja licha  ya kuwa na mashauri mengi na tatizo linakuwa kubwa pindi mahakimu hao wanapougua, kuuguliwa au kwenda likizo.

Aliongeza kuwa mahakama nyingi za mwanzo hazina mahakimu wa kudumu, mahakama hizo hutembelewa na mahakimu kutoka vituo vingine hali ambayo husababisha ucheleweshaji wa haki kwani mahakimu hulazimika kusafiri umbali mrefu na wakati mwingine miundombinu huwa ni mibovu.

Jaji  huyo alibainisha kuwa sasa posho za washauri wa mahakama zimeboreshwa kutoka Sh.1,500 hadi kufikia 5,000 kwa kila shauri litakalohitimishwa.

Alisema licha ya changamoto mbalimbali zinazoikabili mahakama  kuna mikakati ya kutatua changamoto hizo ikiwemo kuondoa mashauri, kesi zote zenye umri zaidi ya miaka miwili, kuboresha takwimu za mashauri, kesi zilizopo mahakamani, kuboresha na kusimamia masjala pamoja na ukaguzi wa mara kwa mara.

February 03, 2014

*MAMIA WAMZIKA MEJA MSTAAFU SAMWEL ISAAC CHEKINGO KWENYE MAKABURI YA KINONDONI DAR

DSC_0133
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakibeba mwili wa marehemu Meja Mstaafu Samwel Isaac Chekingo mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Kinondoni kwa ajili ya ibada maalum.
DSC_0140
DSC_0143
Marafiki wa karibu wa familia ya marehemu wakiwa wamesimama kuupoke mwili wa marehemu Meja Mstaafu Isaac Chekingo ulipowasili nyumbani kwake Kinondoni jijini Dar mwishoni mwa Juma.
DSC_0047
Mtoto mkubwa wa marehemu (mwenye koti la suti jeusi) akijadiliana jambo na baadhi ya wanakamati wa msiba ulioongozwa na Afande Thomas Ndonde wa JWTZ.
February 03, 2014

RAIS KIKWETE ATEMBELEA KUKAGUA MAJENGO YA BUNGE DODOMA KUELEKEA BUNGE LA KATIBA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua sehemu ya Siti za kukaa ndani ya ukumbi wa Bunge mjijini Dodoma wakati alipotembelea na kukagua kampuni inayokarabati na kufanya marekebisho kwa ajili ya kupokea wajumbe wa Bunge la katiba linalotarajia kuanza baadaye mwezi huu.
 Rais Jakaya Kikwete, akijaribu kipaza sauti katika moja ya siti za ukumbi huo.
 Muonekano wa siti za ukumbini humo baada ya marekebisho...
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembezwa sehemu mbalimbali za majengo ya Bunge mjijini Dodoma alipotembelea kukagua maendeleo ya ukarabati na marekebisho ya ukumbi wa Bunge kujiandaa na Bunge la Katiba marekebisho  tayari kwa kupokea wajumbe wa Bunge la katiba baadaye mwezi huu.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya ujenzi inayokarabati na kufanyia marekebisho ukumbi wa bunge mjini Dodoma tayari kwa kupokea wajumbe wa Bunge la katiba baadaye mwezi huu.

MSHABIKI MBARONI KWA MADAI YA TIKETI FEKI

February 03, 2014
Release No. 018
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 3, 2014

Mshabiki mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi akidaiwa kukutwa na tiketi bandia kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Simba iliyochezwa jana (Februari 2 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Matei Cosmas (28) ambaye ni mkazi wa Buza Njiapanda Kitunda, Dar es Salaam amefunguliwa jalada namba CHA/IR/900/2014 kwenye Kituo cha Polisi Chang’ombe akidaiwa kupatikana na tiketi bandia.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo asubuhi (Februari 3 mwaka huu) limeamkia Kituo cha Polisi Chang’ombe kusaini hati ya maelezo dhidi ya mtuhumiwa.

Ni imani ya Shirikisho kuwa mtuhumiwa atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchini.

Tunatoa mwito kwa washabiki wa mpira wa miguu kuepuka kununua tiketi kutoka mikononi mwa watu, kwani kufanya hivyo ni kosa. Tiketi zinauzwa kwenye sehemu maalumu zenye chapa ya TFF.

RAIS WA TFF ATEMBELEA RUANGWA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametembelea Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.

Katika ziara hiyo aliyoifanya jana (Februari 2 mwaka huu), pia alikuwa mgeni rasmi mechi ya kugombea Kombe la Majaliwa kati ya Hull City na Mbagala City, na kuahidi kuwa TFF itaandaa kozi za awali za ukocha na uamuzi kwa Wilaya ya Ruangwa.

RAMBIRAMBI MSIBA WA OMARI CHANGA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha aliyekuwa mchezaji wa Vijana, Moro United na Yanga, Omari Changa kilichotokea juzi (Februari 1 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.

Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Changa wakati wake uwanjani akichezea timu mbalimbali alitoa mchango mkubwa ambao tutaukumbuka daima.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Changa, klabu ya Moro United na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Katika maziko TFF itawakilishwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Kidao Wilfred, na imetoa rambirambi ya sh. 200,000.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
February 03, 2014
Release No. 017
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 3, 2014

TFF YAADHIMISHA MIAKA 50 FIFA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaadhimisha miaka 50 tangu lipate uanachama wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (TFF) kwa shughuli mbalimbili ikiwemo michezo na makongamano.

Kamati maalumu itaundwa kwa ajili ya kupanga na kuratibu shughuli hiyo ambayo TFF imepanga kuadhimisha nchini nzima kwa kutumia wanachama wake.

TFF wakati huo ikiitwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) ilijiunga na FIFA Oktoba 8, 1964.

PAMBANO LA YANGA, MBEYA CITY LAINGIZA MIL 175
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya wenyeji Yanga na Mbeya City lililofanyika jana (Februari 2 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 175,285,000.

Watazamaji 30,411 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A. Yanga ndiyo iliyoibuka na ushindi wa bao 1-0.

Mgawanyo wa mapato ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 26,738,389.83, gharama za kuchapa tiketi sh. 2,919,200 wakati kila klabu ilipata sh. 42,960,086.50.

Uwanja sh. 21,844,111.53, gharama za mechi sh. 13,106,466.92, Bodi ya Ligi sh. 13,106,466.92, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 6,553,233.46 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 5,096,959.36.

Nayo mechi ya Simba na Oljoro JKT iliyochezwa Februari 1 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 47,705,000 ambapo kila timu imepata sh. 11,254,122 kutokana na watazamaji 8,267.
Mgawanyo mwingine katika mechi hiyo iliyomalizika kwa Simba kushinda mabao 4-0 ni Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 7,277,033.90 na gharama za kuchapa tiketi sh. 2,278,400.

Uwanja sh. 5,722,434.92, gharama za mechi sh. 3,433,460.95, Bodi ya Ligi sh. 3,433,460.95, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,716,730.47 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,335,234.81.

TFF YAPATA HATI YA KIWANJA TANGA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepata hati ya kiwanja chake kilichopo eneo la Mnyanjani katika Jiji la Tanga.

Hati hiyo ya miaka 99 ya kiwanja hicho namba 75 Block D chenye ukubwa wa ekari 7.6 ilikabidhiwa kwa TFF, Januari 13 mwaka huu.

Kiwanja hicho kitaendelezwa kwa matumizi mbalimbali, kubwa ikiwa ni uwanja wa mpira wa miguu.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)