AZAM FC YAIBWAGA MABAO 3-0 RUVU SHOOTING

April 10, 2014
Na Mahmoud Zubeiry, Mlandizi
AZAM FC imeibwaga mabao 3-0 timu ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wake wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni hii.
Ushindi huo unaisogeza karibu kabisa na ubingwa wa Ligi Kuu Azam FC kwa kufikisha pointi 56 baada ya kucheza mechi 24, ikifuatia na mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 52 za mechi 24 pia.
Azam FC ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza mabao 2-0 yaliyotiwa kimiani na Gaudence Mwaikimba dakika ya tisa na Himid Mao dakika ya 36, wote wakimalizia kona za Erasto Nyoni.
Mfungaji wa bao la tatu la Azam FC, Kipre Tchetche akishangilia baada ya kufunga

WAMA YAZUNGUMZIA MAHUSIANO MEMA KATI YAO NA JAMHURI YA WATU WA CHINA

April 10, 2014


 Mkurugenzi wa Uboreshaji Afya Wama ,Dkt.Sarah Maongezi (Kulia) akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu ushirikiano uliopo  baina ya Taasisi ya Wanawake na Maendeleo pamoja na Jamuhuri ya Watu wa China nchini katika kusaidia wananchi ikiwemo ziara wanaoyotarajia kuifanya katika mikoa ya Kanda ya Ziwa kuanzia tarehe 12 hadi 19 Aprili mwaka huu,Katika ni katibu wa Balozi wa China nchini,Ren Zhihong na Meneja Mawasiliano wa Wama Philomema Marijani.
Katibu wa  Balozi wa Jamuhuri ya watu wa China nchini, Ren Zhihong (katika) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa mkutano uliofanyika maelezo leo jijini Dar es salaam kuelezea ushirikiano uliopo baina ya Taasisi ya Wama na Ubalozi wa China katika shughuli za kusaidia jamii.Kulia ni Mkurugenzi wa Uboreshaji Afya Wama ,Dkt.Sarah Maongezi na kushoto ni Meneja Mawasiliano wa Wama Philomema Marijani.

Picha na Lorietha Laurence
******************************************
Na Lorietha Laurence
Taasisi ya Wanawake na Maendeleo  kwa kushirikiana na Balozi wa Jamuhuri  ya watu wa china nchini,  Lu YouQing  itafanya ziara kuitembelea mikoa ya kanda ya ziwa kuanzia tarehe 12 hadi 19 Aprili mwaka huu kwa  shughuli za kusaidia jamii.

SERIKALI YAJIPANGA KUMALIZA AJALI ZA BARABARANI NCHINI

April 10, 2014


Kamanda wa Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani DCP Mohammed Mpinga akiwaonyesha waandishi wa Habari(Hawapo pichani) vipima mwendo vya magari, Kushoto ni Kipima mwendo cha kisasa kinachotumiwa na jeshi hilo na kulia ni kipima mwendo cha zamani, wakati wa mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiangalia Kipima mwendo cha kisasa kinachotumiwa na askari wa usalama barabara, wakati wa mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

*KAMATI ZAANZA KUWASILISHA TAARIFA ZA BUNGE MAALUM LA KATIBA, WENGI WAPENDEKEZA SERIKALI MBILI

April 10, 2014

 Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samuel Sitta akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Bunge hilo leo mjini Dodoma wakati wa uwasilishaji wa Sura ya Kwanza na Sita wa rasimu ya Katiba mpya.

OMOG ANAWEZA KUANZISHA WASHAMBULIAJI WATATU DHIDI YA RUVU SHOOTING LEO!!

April 10, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar Es salaam